Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Lady Jaydee Afunguka Tetesi Za Kuachana Na Mpenzi Wake

0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ni mkongwe kwenye game Lady Jaydee amefunguka juu ya tuhuma za kuachana na mpenzi wake Spice, ambaye ni msanii kutoka Nigeria Spice.

Akizungumza na kituo cha EATV  amesema kwamba hajaachana na Spice, isipokuwa wawili hao wanafanya kazi ambayo inawalazimu kuwa mbali mbali kwa muda mrefu, ikichangiwa na kuwa raia wa nchi mbili tofauti.

Jaydee ameendelea kwa kusema kwamba licha ya Spice kuwa mbali, amechangia kwa kiasi kikubwa kuweza kufanikisha tamasha la #VocalsNight2018, kwa kuweza kumuunganisha na UTI ambaye  alikuwa MC wa siku ile.

“Unajua sisi ni wanamuziki, na wanamuziki ni watu wa kusafiri, na hatuishi nchi moja, kwa hiyo yeye yuko kwenye kazi zake na mimi nipo kwenye kazi zangu, ni sawa na mume na mke, mume anaenda kazini na mke anaenda kazini kwake, haimaanishi kila siku muwe mnafuatana, leo hayuko hapa lakini ni mtu ambaye nashirikiana naye kwenye mambo mengi, kama kunisaidia kumpata UTI na kuhakikisha amefika hapa Tanzania”, amesema Lady Jaydee.

Hivi karibuni kulikuwa na tetesi za wawili hao kuachana baada ya kuwepo ukimya kati yao na kutoonakana pamoja kwa muda mrefu.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 20

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
         
“Nchi ya kuwa nazo makini sana hapo ni Uingereza na Italy, tukifanya makosa hatuto songa mbele na wezetu wamejiandaa kisawa sawa, kwani wachezaji wao wana vipaji na wana uwezo mkubwa. Ethan wewe ni jicho langu, Frenando wewe ni kifua changu na mulio salia nyinyi ni mikono yangu. Nawaomba musiniangushe, nawaomba mufanye kile munacho paswa kufanya kwa miaka yote ya nyuma kwenye mashindano mengine. Haya ni mashindano mapya kabisa kwa timu za sekondari, hapa ndipo kwa kujiuza nyinyi wewenyewe kwani mameneja na makocha kutoka timu kubwa duniani watakuwa wakifwatilia mashindano hayo ambayo yatarushwa moja kwa moja kwenye televishion. Tulinde heshima ya nchi, na heshima na shule pia. Kwa pamoja tutakiwa kishinda sawa”
 
Wachezaji wote tukamuitikia kocha wetu kwani amezungumza maneno hayo hadi machozi yanamwagika usoni mwake, ikiashiria kwamba ana uchu na hamu sana ya kutuona vijana wake tunashinda na kuwa timu bora katika bara zima la Ulaya.

ENDELEA               
Siku iliyo fwata tukaingia kambini rasmi huku kila mmoja akiwa amesha jiandaa vizuri kwa ajili ya mashindano haya.
“Frenando hembu fanya mpango wa kupata simu ni wasiliane na Camil”
“Poa kaka, ila namba yake unayo?”
“Nitawapigia shuleni kwao, ili waweze kunipatia namba wanayo itumia nchini huko”
 
“Ingekuwa vizuri ukatumia hiyo simu ya chumbani kwetu kuwasiliana nao?”
“Hizi si zimeunganishwa na hapa hapa hotelini, au zinaweza kutoka nje ya hii hoteli?”
“Sijajua ila ngoja tujaribishe tuone itakavyo”
Frenando, akaingiza namba ya mama yake iliyopo nchini Mexco kwenye simu hii, akaisikilizia kwa muda kisha akatingisha akimaanisha kwamba hii simu haina uwezo wa kutoa simu nje ya hoteli hii.
“Badae tutoroke tuende tukatafute simu mjini”
“Hapana hakuna haja ya kutoroka, tumuombe kocha ruhusa kisha tutoke”
“Tatizo lako Ethan wewe ni muoga”
“Sio uwoga Frenando”
“Ila?”
 
“Sura yangu kila sehemu inajulikana, umaarufu muda mwengine ni shida”
“Mmmm, ngoja nina mpango”
“Mpango gani?”
“Nina kuja”
Frenando akatoka chumbani humu na kuniacha mimi peke yangu.
‘Mutakwenda kushinda michezo yote ila fainali sijajua’
Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu huku akiwa amekaa kwenye moja ya sofa humu ndani, nikanyanyuka kitandani na kukaa sofa la mbele yake huku tukitazamana.
“Ina maana fainiali hatushindi?”   
“Sijajua kwa maana timu ambazo mutaingia fainali zote ni ngumu na kuna hati hati ya nyinyi kuto shinda”
Nikakaa kimya kwa muda huku nikimtazama Ethan kwa maana ni jini ambaye ana nitabiria vitu vingi sana vya mbeleni.
 
“Tuachane na maswala ya mpira, vipi mpenzi wangu Camila yupo sehemu salama?”
“Ndio, ukizungumza naye leo usiku hakikisha kwamba unamsisitizia haendi nchini Somali”
“Kwa nini?”
“Somali sio nchi salama kwa wao kwenda, kuna matukio ya kila aina ambayo yanaweza kumkuta. Ukiachilia mbali na matatizo hayo, baba yake anagombania kiti cha uraisi, zinaweza kutumiwa njama za kutekwa kwake, kisha baba yake akashinikizwa kuendelea kugombania uraisi na kama unavyo jua siasa za hapa Ujerumani, watu wana misimamo na niwaelewa wa mambo. Mzuie mpenzi wako kwenda huko na hata ikiwezekana apande ndege mara tu ya kumaliza ziara yao nchi Tanzania.”
Nikashusha pumzi taraibu huku nikimtazama Ethan usoni mwake.
“Naamini huto hitaji kukiona kifo cha mpenzi wako, fanya hivyo nilivyo kuambia”
“Nimekuelewa na ninashukuru sana Ethan”
“Karibu”
“Asante”
“Rafiki yako ana kuja ngoja niondoke”
Ethan akapotea kwenye uepo wa macho yangu. Frenando akaingia huku akiwa ameshika mfuko mweusi.
 
“Ume beba nini?”
“Haya ni makofia ambayo tutavaa tukitoroka”
“Frenando akili yako ipo wapi rafiki yangu. Ninacho taka mimi ni simu na sio makofia”
Nilizungumza kwa kufoka kidogo hadi Frenando mwenyewe akanishangaa kwa maana katika kipindi chote cha urafiki wetu hakunishuhudia siku hata moja nikiwa nimekasirika.
“Ethan kuna jambo lolote baya nililo kufanyia”
“Samahani rafiki yangu. Akili yangu haipo sawa nina hisia mbaya kuhusiana na Camila”
“Hisia mbaya? Hisia gani?”
“Wana ziara ya kwenda nchi Somali wakitoka nchini Tanzania hivyo nahitaji asiende Somali”
“Somali si ndio kule kwenye kundi la Al-Shubabu sijui Al-Shabibi?”
 
“Ndio huko huko”
“Mmmmm hili swala ni muhimu Ethan, sio la kimapenzi tena ni kweli unatakiwa kumzuia kwenda”
“Ndio hivyo nahitaji simu”
“Twende tukamuombe kocha simu yake, kwa maana sisi si wametuzia kuwa na simu”
Nikamtazama Frenando usoni mwake kwa muda kidogo kisha nikaanza kutembea kuelekea nje, akanifwata kwa nyuma na tukaingia kwenye chumba cha kocha bila hata ya kubisha hodi. Tukamkuta kocha akifanya mapenzi na mmoja wa wahudumu wa hoteli hii ambaye alitopokea kwa bashasha sana.
“Ohoo Mungu. Ethan ndio nini hicho”
Kocha alizunguzma huku akijifunika shuka na muhudumu huyo.
 
“Waoooo!!”
Frenando alizungumza huku akijawa na tabasamu pana usoni mwake.
“Simu”
Nilizungumza kwa ufupi tu huku nikimtazma kocha usoni mwake.
“Nini?”
“Nataka simu yako”
Nilimfokea kocha kana kwamba ni kijana mwenzangu. Kocha kwa ishara akanionyesha simu yake ilipo ni ndani ya koti la suti yake aliyo kuwa ameivaa. Nikaingiza kiganja kwenye mfuko wa kushoto, ila sikuikuta, ila katika mfuko wa upande wa kulai nikaikuta. Nikaitoa simu hiyo aina ya Samsung S8.
“Mke wako anapiga”
 
Nilimuambia kocha huku nikimtazama usoni mwake, kwani ni kweli mke wake anapiga simu na ameizima mlio wake ili isisikike pale anapo pigiwa. Kocha akabaki akiwa amenitumbulia macho huku akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana. Nikaipoke simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.
“Ndio mama Philipes”
“Nani mwenzangu”
“Ethan mmoja wa wachezaji wa mume wako”
“Ethan Klopp?”
“Ndio”
“Ohoo nafurahi kusikia hivyo mwanangu habari yako”
“Salama tu mama Philipes”
 
Nilizungumza huku nikiwa nimekazia macho kocha pamoja na muhudumu huyu wa hoteli huko wote wakiwa wamekaa kimya huku miili ikiwatetemeka.
“Yupo wapi kocha wako?”
“Nimetoka na simu yake mara moja na nipo mjini nikirudi nitakufahamisha uzungumze naye”
“Ohoo sawa sawa Ethan, ninafurahi kuzungumza nawe”
“Hata mimi mama nina furahi kuzungumza nawe”
“Sawa nikutakie mchana mwenma”
“Nawe pia”
Nikakata simu na kumtazama kocha na nikamuona jinsia navyo shusha pumzi nyingi. Sikumsemesha kitu chochote zaidi ya kutoka chumbani humu na kurudi chumbani kwetu.
“Ethan umemuachia mzee wa watu hali mbaya”
“Kwa nini?”
 
“Si tazama jinsi vile alivyo pata wasiwasi mwingi jamani.”
“Hahaaa…..umalaya unamsumbua na anatusisitiza sisi tusiwe na wapenzi sijui anatuona sisi sio watu”
“Anatamatatizo”
Nikaingiza namba ya shuleni kwa kina Camila, nikaipiga simu hiyo. Ikaanza kuita na baada ya sekunde kadhaa ikapolewa.
“St Lilian High school. Mery ninazungumza nani mwenzangu”
“Unazungumza na Ethan Klopp”
“Ohoo habari yako”
“Salama, ninaweza kupata mawasiliano ya mpenzi wangu kwa nchi waliyo kwenda?”
“Tanzania?”
“Ndio”
 
“Sawa ngoja nikutumie kwa njia ya meseji”
“Nashukuru sana, je wamefika salama?”
“Ndio wamefika salama”
“Naomba msaada wako Mery”
“Usijali  Ethan”
Nikakata simu kwani sio mara yangu ya kwanza kuzungumza na sekretari wa shule hii. Haikuisha hata dakika moja meseji ikaingia ikiwa na maelezo ya namba ambayo inatumiwa na uongozi walio ongozana nao kwenye safari hiyo nchini Tanzania.
“Duu kumbe nchi ya Tanzania code namba yake ni +225”
Nilizunugmza huku nikimuonyesha Frenando namba hiyo
“Wemechelewa sana kupata huduma za simu”
“Yaaa”
Nikaingiza namba hiyo, ila nikapewa taarifa kwamba simu hii haina salio la kutosha, niongeze tena kisha nipige tena.
“Kocha mzima hana salio kwenye simu yake”
 
“Mmmm sasa tunafanyeje?”
“Inabidi tutoke tukanunue”
“Umeona sasa”
Frenando akanikabidhi moja ya kofia aliyo nunua. Tukatoka chumbani kwetu na kufunga mlango wetu na kuondoka. Tukaanza kuzunguka mitaani huku ni baadhi ya watu wachache sana ambao waliweza kutugundua na wengine walituomba waweze kupiga picha nasi. Tukaingia kwenye moja ya duka la kununu simu, nikatia kadi yangu ya malipo ambayo ina kiasi cha kutosha na sehemu yoyote katika nchi hii ya Ujerumani, nina weza kuitumia kununua kitu cha ina yoyote ile na katika duka lolote.
 
“Tununue simu zetu na tumrudishie yule mwehu simu yake”
Nilizungumza huku tukizunguka katika duka hili ambalo simu zote zilizomo humu ndani ni simu za garama sana. Kila mtu akanunua simu yake, tukasajiliwa laini zetu kama kanunu na taratibu za nchi hii. Tulipo maliza maunuzi yetu tukaingia kwenye moja ya mgahawa, tukanunua vyakula na vinywaji kisha tukarudi hotelini.
“Shika mrudishie simu yake”
Frenando akachukua simu ya kocha na kumpelekea chumbani kwake, nikaipiga namba niliyo kabidhiwa na sekretari. Namba hiyo ikaanza kuita na baada ya muda kidogo ikapokelewa.
 
“Habari yako?”
“Salama, ninaitwa Ethan Klopp ninahitaji kuzungumza na Camila Marco”
“Ohoo hivi sasa ni usiku sana, labda kukipambazuka atakutafuta”
“Sawa sawa mwalimu, ila ana endeleaje?”
“Anaendelea vizuri tu ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kweli”
“Asante basi kukipambazuka utanifahamisha”
“Sawa Ethan”
Nikakata simu huku nikiwa na faraja kuba sana moyoni mwangu, kwani mwalimu huyo aliye pokea simu ni mlenzi wao kwa upande wa wanawake.
 
“Vipi umesha zungumza naye?”
Frenando alizungumza huku akiingia ndani ya chumba hichi
“Ndio ila kule ni usiku amepokea matron wao”
“Ahaa, hivi sasa na huko masaa huwa yana pishana sana ehee?”
“Ndio ila sijajua yanapishana kwa masaa mangapi mangapi”
Tukapata chakula cha mchana. Jioni tukaelekea katika viwanja vya karibu kabisa na hoteli hii kwa ajili ya mazoezi ya hapa na pale.
“Ethan na Frenando nina waomba”
Kocha alituita mara baada ya kumaliza mazoezi, tukasimama mbali kidogo na basi letu la timu.
“Naamini mumeona kilicho tokea mule chumbani”
“Ndio”
“Ninawaomba iwe siri yenu. Ninaomba musiweze kuitoa siri hiyo kwa mtu yoyote”
Kocha alizungumza kwa msisitizo huku akitutazama kwenye nyuso zetu.
 
“Mke wako ana kasoro gani?”
Nilimuuliza kocha kwa upole sana huku nikimtazama usoni mwake.
“Ethan”
“Usiseme Ethan kocha. Tambua nimebeba dhambi kubwa sana ya kumdanganya mke wako. Je dhambi hiyo mimi nina ilipaje eheee?”
“Ethan natambua nyinyi bado ni wadogo, ila muikingia kwenye ndoa mutaweza kujua ni nini kinacho tokea hadi wanaume tunaamua kuwa na wake wa nje”
“Wacha weeee”
Frenando alizungumza kwa kejeli huku akimtazama kocha usoni mwake. Gafla simu yangu ikaanza kuita ikiwa ndani ya kibegi changu mgongoni. Kocha akatoka na macho ya hasira kwani moja ya sheria tukiwa kambini ama shuleni haturuhusiwi kuwa na simu.
“Ethan kwa nini una simu?”
Kocha aliniulza kwa kunifoke sana.
“Acha upuuzi wewe mzee. Muache apokee simu la sivyo tunakwenda kuzungumza uchafu wote kwa mke wako na ushahidi wapicha ninao”
Frenando alizungumza kwa kujiamini na kumfanya kocha kukodolea macho na kukosa jambo la kuzungumza kwa muda huu.

==>>ITAENDELEA KESHO

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648  au 0656 551 093  au 0746473974

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 126 na 127 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
Mlango wa nyuma ya gari letu ukafunguliwa, wanaume wawili walio funika nyuso zao na kuacha macho yao tu huku mikononi mwao wakiwa na bunduki, wakaanza kuwatoa wezangu mmoja baada ya mwingine ndani ya gari hili na mimi nikawa wa mwisho kutolewa. Cha kusangaza Hawa na wezake wote wao wamesimama ila mimi ndio nimelazwa chini huku mitutu ya bundiki ya wanaume hawa wakiwa wamenielekezea mimi.
“Halooo Dany”   
Sikuamini macho yangu nilipo muona baba Hawa akisimama pembeni yangu, huku mkononi mwake akiwa ameshika bastola tayari kwa kuniua.
   
ENDELEA   
Taratibu nikamtazama Hawa machoni mwake, taratibu Hawa akatazama pembeni akimaanisha kwamba haitaji kutazama mauaji yangu. Gafla tukamshuhudia mwanaume mmoja wa baba Hawa akianguka chini jambo lililo wafanya watu kuanza kumzunguka baba hawa huku bunduki zao wakiwa wamezishika vizuri. Baba Hawa na watu wake wakaanza kukimbilia kwenye gari walilo kuja nalo huku wakiwa wameniacha chini nimelala. Nikaona gari gari mbili nyeusi za FBI zikija eneo hili kwa kasi huku wakiendelea kuwashambulia watu wa baba Hawa ambao nao wapo wengi kiasi.
 
Nikachukua bunduki ya mmoja wa watu wa baba Hawa aliye pigwa risasi, nikaanza kubingiria nayo hadi pembezoni mwa barabara, kwa haraka nikanyanyuka na kupiga goti moja chini huku mguu wangu mwengine nikiwa nimeukunja kwa nyuma. Nikafumba jicho langu la upande wa kushoto huku nikimtazama baba Hawa jisi anavyo ingia kwenye gari lake. Hawa akageuka kwa nyuma, akakiona kitendo changu cha kuhitaji kumua baba yake, kwa haraka akasimama mbele yake jambo lilio nifanua nishindwe kabisa kumshambulia baba yake.
“Shiti”       
Nilizungumza kwa hasira huku nikitazama gari la baba Hawa likiondoka kwa kasi huku magari mengini yakiwafwata kwa nyuma. 
 
“Weka silaha yako chini”   
Nilisikia sauti ya ukali ikitokea nyuma yangu, kwa haraka nikaitupa bunduki niliyo ishika pembeni kisha nikalala chini, askari mmoja akanifwata akanifunga mbingu kwa nyuma na kuninyanyua juu.
“Nahitaji kuzungumza na raisi”   
“Una haki ya kukaa kimya siwezi kufanya hivyo pasipo kupata ruhusa yoyote”
“Sawa nalitambua hilo ila ninahitaji kuzungumza na raisi wa nchi yako”
Nilimuambia askari huyu kwa msisitizo, hakulijali hilo zaidi ya kuniingiza ndani ya gari lake. Askari wa vitengo tofauti tofauti wakaanza kufika katika eneo hili la tukio. Askari huyu akanifungulia mlango, akanifungua pingu za mikono yangu.
“Kuna simu yako kutoka kwa muheshimiwa raisi”
 
“Shukrani”
Nilizungumza huku nikiichukua simu hii anayo nipa askari huyu.
“Ndio muheshimiwa raisi”
“Ohooo asate Mungu upoa salama Dany”
“Nashukuru muheshimiwa raisi kwa hilo, ila hii kazi muheshimiwa raisi nahitaji kuiendeleza kabla watu hawa hawajatoka ndani ya Marekani”
“Dany unatakiwa kupumzika kwa sasa, ajali uliyo ipata ni mbaya”
“Nalitambua hilo muheshimiwa raisi, ila sijaumia. Ninakuomba uweze kuniruhusu kuungana na vikosi vya wanausalama wako wanao watafuta magaidi hawa”
 
“Dany”
“Tafadhali muheshimiwa raisi, sihitaji kukuangusha. Ninawajua hawa magaidi nimefanya nao kazi zaidi ya miaka miwili na ninatambua udhaifu wao”
Raisi akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku nikisubiria jibu lake.
“Nimekuruhusu, hakikisha kwamba unawaangusha hao magaidi wote”
“Nashukuru muheshimiwa raisi, ila ninakuomba muheshimiwa raisi ufanye uchunguzi katika kamati yako ya ulinzi kuna msaliti kwa maana watu tuliokuwa tunajua hii oparesheni ni watu wachache sana, sasa kuna mtu atakuwa amevujisha mpango mzima, ndio maana magaidi hawa wameweza kutuvamia kabla hatujafika katika sehemu husika”
 
“Nitalichukualia uangalizi na hilo”
“Asante muheshimiwa raisi”
“Mpatie simu hiyo askari”
Nikairudisha simu kwaaskari huyu, akazungumza na raisi baada ya sekunde kadha akaka simu na kiunitazama usoni.
“Unahitaji nini?”   
“Ninataji mavazi, silaha pamoja na kuweza kujua hawa magaidi hadi kwa sasa wamelekea wapi?”
“Sawa”
Nikaongozaa na askari huyu hadi kwenye moja ya gari kubwa la FBI, nikakabidhiwa nguo ninazo zihitaji ambazo ni mavazi meusi, nikakabidhiwa jaketi la kuzuia risasi pamoja na bastola na magazine nne.
 
“Mumeweza kufahamu ni wapi magaidi hawa wapo?”
“Tumeweza kuwapoteza”
“Kuwapoteza kivipi?”
“Tuliwafwatilia, tukakwakuta magari yao yakiwa yametelekezwa chini ya daraja moja na wao hawapo?””
“Mumeweza kuwafwatilia?”
“Ndio vikosi vinazidi kuwafwatilia”
“Ninaweza kufika katika eneo hilo la tukio?”
“Ndio ila kuna umbali mkubwa kutoka hapa nilipo, inabidi kutumia helicopter kuweza kufika hilo eneo”
“Naomba tufanye hivyo”
Askari huyu akawasiliana na makao makuu yao, na kuomba masaada wa helicopter.
“Itachukua muda gani kufika hapa tulipo?”
“Dakika tano”
“Sawa”
 
Ndani ya dakika tano kama alivyo zungumza  askari huyu, helicopter ya FBI ikatua pembezoni mwa barabara. Mimi na askari huyu moja kwa moja tukakimbilia kwenye helicopter hii na kuingia ndani. Safari ya kueleka katika eneo yalipo telekezwa magari ya magaidi hawa ikaanza. Tukatumia dakika kumi tukiwa hewani, tukafika katika eneo la tukio ambapo napo tukakuta askari wengine wakiwa wamelizunguka eneo hilo likiendelea kufanyiwa uchunuguzi.
“Habari meja Thomsande”
“Salama, meja Barak, huyu anaitwa Dany ni agent anaye fanya kazi chini ya ofisi ya raisi”
“Habari yako agent Dany?”
“Salama tu meja Thomsande”
“Salama tu”
 
“Mumeweza kugundua ni sehemu hani ambayo magaidi wameweza kuelekea?”
“Hadi sasa hivi tumeweza kufanya uchuguzi wote ila hatujaweza kufahamu ni sehemu gani magaidi wamelekea, na hata kamera za hapa hazijachukua tukio lolote na inavyo onekana zimeweza kufutwa matukio yote”
“Je mumeweza kuwafwatilia kwa kutumia satelaiti?”
“Tumejaribu kufanya vyote ila vimeshindikana”
“Je kuna njia za chini?”
“Katika hili eneo hakuna njia za chini ya ardhi kabisa”
Nikalisogelea gari moja ambalo ndio alikuwa amepanda baba Hawa, nikaanza kulikagua kwenye siti za nyuma, katikati ya siti moja na nyingine nikakutana na kipande cha karatasi kidogo sana mbacho si rahisi kwa mtu kuweza kukiona. Nikakifungua na kukuta maandishi yaliyo andikwa kwa damu ya binadamu.
“Somalia”
Niliyasoma huku nikirudi kwa askari niliye kuja naye.
“Umepata nini?”
 
“Wanaelekea Somalia”
“Umejuaje?”
“Kuna hichi kikaratasi kilicho andikwa na damu, kwenye hii gari alipanda baba Hawa pamoja na mwanaye na hii hati ya ya kuandika inafanana kabisa na Hawa.
“Hawa?”   
“Mwanamke ambaye ni mpenzi wake na yeye yupo kinyume na baba yake”
“Basi niwasiliane na wakuu wa viwanja vyote vya ndege, treni pamona na bandari zote ziweze kufungwa ili ulizni uzidi kuimarishwa. “
“Sawa ninaomba kuwasiliana na raisi”
“Sawa”
Raisi akapigiwa simu, nikakabidhiwa simu na kuzungumza naye.
“Dany umepata kitu gani?”
“Wanaelekea Somalia, kwa sasa ningeomba kuweza kupata ndege itakayo nipelekea Somalia moja kwa moja, ili niweze kuwawahi”
“Wewe unahisi watakuwa kweli wanakwenda Somalia?”
“Nina amani hivyo muheshimiwa raisi kwa maana sidhani kama wanaweza kwenda nchi yoyote Duniani, ikiwa wanajua wanataftwa karibia Daunia nzima”
 
“Dany kwa hili inabidi tujirishishe mapema sana kuamini kwamba watakuwa wametoka nje ya nchi hii. Kwani watu wangu wanaendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba wanaimarisha ulinzi wa kuweza kuwatafuta”
“Muheshimiwa raisi, kumbuka muda hautusubiri, na laiti kama wangekuwa wapo ndani ya hii nchi tungeweza kupata muongozo kuanzia hapa tulipo. Ila kumbuka muheshimiwa raisi kwamba hawa watu wanapata ushirikiano na watu waliomo ndani ya serikali yako ndio maana mpango mzima umekwenda tofauti na vile tulivyo kuwa tunafikiria.”
Nilizungumza kwa msisitizo ili kummshawishi raisi Donald Bush kuweza kuamini kwa kile ninacho mueleza.
“Muheshimiwa raisi, nimeianza hii kazi ninakuomba unipe nafasi ya kuifanya hadi iishe tafahali”
“Rudi ikulu”
“Muheshimiwa raisi”
“Dany nimekuambia ninakuhitaji hapa ikulu”
“Sawa muheshimiwa raisi”
 
Sikuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kukata simu, wakanifwata askari wawili wengine wakaniomba tueleke kwenye helicopter kwa safari ya kwenda ikulu. Moyoni mwangu nikajisikia vibaya sana kwa kuona raisi anawaachia magaidi hawa kutoka nje ya nchi yake kirahisi namna hii. Nikaingia kwenye helicopter niliyo kuja nayo na safari ya kuelekea ikulu ikaanza. Tukatumi nusu saa hadi kufika ikulu, nikakabidhi bastola yangu pamoja na magazine kwa walinzi wa ikulu kisha nikapelekwa moja kwa moja hadi ofisi ya raisi niliye mkuta akiwa na mwanaume mmoja mweusi.
“Samahani Dany kwa kuweza kukurudisha katika opareheni yako uliyo kuwa umeianza”
“Hakuna tabu katika hilo”
“Kutana na balozi wa Tanzan bwana Jackson Bongole”
“Habari yako muheshimiw a balozi”
 
“Salama Dany, ni muda mrefu sijakuona”
“Nikumbushe uliniona wapi?”
“Nilikuona katika ziara moja ya raisi aliye toka madarakani, ukiwa mmoja wa walinzi wake”
“Nashukuru katika hilo”
“Dany balozi wako amekuja kuomba kusitishwa kwa wewe kutumiwa na Marekani katika kuendesha oparesheni za kuwasaka magaidi, pasipo nchi ya Tanzan kuweza kutambua”
Raisi alizungumza kwa utaratibu huku akinitazama usoni mwangu, nikamtazama balozi Jackson Bongole kwa macho makali sana yaliyo jaa hasira’
“Dany mimi nimepokea amri kutoka nchini Tzania kutoka kwa raisi na sasa unahitajika kurudi nchini Tannia haraka iwezekanavyo”
 
“Ngoja muheshimiwa raisi pasipo kushusha heshima yako mbele ya raisi, ila hicho kitu unacho kizungumza hakiwezekanai kabisa kwenye maisha yangu. Hivi unatambua ni jambo gani linalo endelea duniani kwa sasa?”
“Mimi nimefwata amri ya raisi wangu, na tambua kwamba Tanzania na Marekani tuna ushirikiano mzuri sana ambao unaweza kuvunjia muda wowote kwa ajili yako”
Nikaka kimya huku nikimtazama balozi, nikamtazama raisi Donald Bush, kisha nikayarudisha macho yangu kwa Balozi Jackson Bongole.
“Muheshimiwa balozi, ninakuomba unisaidie kitu kimoja kama huto jali, ninakuomba niweze kuimaliza hii kazi kisha ndio nitarudi Tanzania”
“Dany ingekuwa ni amri yangu ningeweza kukuruhusu urudi Tanzania, ila sio amri yangu. Mimi mwenyewe ninafwata amri na nimepewa masaa kumi na mbili niwe nimekurudisha nchini Tanzania”
 
“Natambua muheshimwa balozi kwamba unafwata amri, ila tambua huyo ambaye amekupa amri hiyo yeye mwenyewe ni adui yangu namba moja”
“Kivipi?”
“Raisi K2 yeye kwanza ndio amehusika na mauaji ya raisi aliye pita kwa uroho wa madaraka. Raisi K2 yeye ndio anahusika na upotevu wa watoto wa kike unao zidi kuendelea nchini Tanzan, na nchi za jirani. Watoto hao anawakuza na kuwafanya wauaji ambao wanafanya kazi za hatari ambazo kwa wanausalama wa kawaida hawawezi kupambana nao, na hicho kizazi chake amekiandaa kwa miaka mingi sana”
 
“Hayo yote wewe umeyajulia wapi?”
“Kabla ya kujua nimeyajulia wapi, yeye ndio aliye waua wazazi wangu, familia yangu nzima damu yake ipo kwa K2, leo hii unanihitaji kurudi Tanzan ambapo karibi watu wote nchi nzima anajua kwamba mimi ni gaidi, ikiwa gaidi mkubwa ni huyo anaye waongoza. Tafadhali muheshimiwa balozi, hili ninalo lizungumza ni kati yako wewe na mimi, tafadhali ninakuomba uniruhusu kuimaliza hii kazi niliyo inaza”
Mueshimiwa balozi Jackson Bongole akakaka kimya huku akionekana kutafakari jibu la kuweza kunipatia.
“Dany”
“Ndio muheshimiwa Balozi”
“Ukiachilia mbali  tu kwamba kazi yangu ninaweza kuipoteza, ila familia yangu pia ninaweza kuipoteza”
“Kivipi?”
“Muheshimiwa raisi K2 ameniambia kwamba nisipo hakikisha wewe unafika nchini Tanzani basi familia yangu ataingamiza”
“Familia yako ipo wapi muheshimiwa Balozi?”
“Ipo nchini Tanzania, hapa nipo na mtoto wangu wa kiume anaye soma chuo”
 
“Samahani muheshimiwa balozi, una ushahidi wa sauti?”
Raisi aliuliza huku akimtazama balozi usoni mwake.
“Ndio ninao muheshimiwa raisi”
Muheshimiwa balozi Jackson Bongole akatoa simu yake ya mkononi na kutuwekea mazungumzo aliyo kuwa anazungumza na raisi K2.
“Hili swala nitalisimamia mimi kama raisi wa Marekani, nitahakikisha nchi yangu inamshihulikia raisi wako nimemvumilia nimeshindwa. Kabla hajaiteketeza familia yako basi nchi yangu itaanza na familia yake. Dany nakuruhusu kuendelea na oparesheni yako hakikisha kwamba hata raisi K2 unamuweka mikononi mwako na ikiwezekana na yeye unamuanguamiza nitakulinda kwa hali yoyote na hakuna serikali itakayo weza kukukamata sawa”
“Sawa muheshimiwa raisi”
Nilijibu huku nikitabsamu, kwa maana K2 sasa ameingia kwenye sehemu ambazo ni lazima mwisho wake utafika na tena utafika kama ilivyokuwa kwa gaidi wa dunia Osama Bin Laden.

AISIIIII……….U KILL ME 127

“Ndege ya kukupelekea Somalia imesha andaliwa, Dany hakikisha kwamba huniangushi katika hili”
“Mungu anitangulie na nitahakikisha kwamba kila jambo linakwenda bizuri”
“Sawa Dany”
Raisi akanyanyua mkonga wa simu iliyopo mezani mwake
“Njooni mumchukue”
Hazikupita hata dakika mbili, wakaingia wanajeshi wawili walio valia mavazi ya jeshi, wakampigia raisi saluti.
“Mshindikizeni Dany hati katika kiwanja cha ndege cha jeshi”
“Sawa muheshimiwa raisi”
 
Nikamsogelea balozi wa Tanzania bwana Jackson Bongole, nikampa mkono huku nikimtazama machoni mwake.
“Ni wakati wa wewe kuwa jasiri na usiwe nyonge katika hili”
“Sawa kijana, kazi njema”
“Asante”
Nikatoka na wanajeshi hawa, tukatoka nje na kuingia katika gari aina ya HAMMER ambalo hutumiwa na wanajeshi hawa. Safari ya kuelekea katika kambi yao ikaanza huku ndani ya gari hili nikiwaza maneno ya Kk2 jinsi alivyokuwa akimmshinikiza balozi Jackson Bongole kuhakikisha kwamba ananipelekea nchini Tanzaa ambapo moja kwa moja ninatambua kwamba nitakapo fika huko ni lazima tu ataniua.
“Tutachukua muda gani hadi kufika kambini?”
 
“Zimebadki dakika kumi”
“Sawa”
Tukafanikiwa kufika katika kambi ya jeshi, nikakambiziwa kwa mkuu wa anga ambaye moja kwa moja akanipelekea hadi katika kiwanja cha ndege ambacho nimekuta kuna ndege nyingi za kivita zikiwa zimejipanga vizuri.
“Kila kitu unacho kihitaji katika kazi yako kipo ndani ya ndege hii, rubani atakupeleka hadi nchini Somali”
“Sawa”
“Ramani nzima pia ipo humo ndani, chukua hichi kifaa, hakikisha kwamba pale unapokuwa umeshikwa kwenye kazi hii, unakitumia kukiminya hii batani basi sisi huku tutakuwa tumeelewa ni kitu gani kinacho endelea na tutahakikisha kwamba tunakufika katika muda mdogo sana kwa maana ndege zetu hizi zinakwenda kwa mwendo wa kasi sana”
“Shukrani”
Nilijibu huku nikitazama kivaa kidogo lilicho kaa kama rimoti ndogo za magari huku kikiwa na batani moja yenye rangi nyekundu.
 
“Nakutakia kazi njema”
“Asante”
Nikaingia katika ndege hii ndogo ya kijeshi ila inaonekana ina uwezo mkubwa sana katika swala la kwenda kasi. Nikaka kwenye siti, rubani akaniomba nijifunge mkanda pamoja na kuvaa earphone ilizopo pembeni ya siti yangu. Nikafanya hivyo kwa haraka sana, taartibu nikaanza kusikia injini za ndege hii zikianza kunguruma, ndege ikaanza kuondoka katika uwanja huu kwa mwendo wa taratibu, kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo ilivyo zidi kushika kasi na baada ya nusu saa ikaanza kunyanyuka kuelekea juu. Ndani ya dakika moja na sekunde kadhaa ndege ikaka sawa hewani, kwa kupitia earphone nilizo zivaa masikioni mwangu, rubani akaniambia kwamba ninaweza kufungua mkanda na kutazama vifaa vilivyopo kwenye mabegi ndani ya hii ndeg. 
 
    Nikaanza kuchagua bastola ambazo kuseme kweli ni silaha ambayo kwa upande wangu ni rahisi sana kuweza kuitumia na ninapo mlenga mtu huwa ninahakikisha kwamba ninamuangusha. Nikachukua na bunduki mbili kubwa moja ikiwa ni ‘HK M27 IAR’ na nyingine ‘FN SCAR MK 17 ambayo kila mmoja ina uwezo mkubwa sana katika mashumbulizi hususani ya mbali na maadui wangu. Nikachukua mabomu sita ya kurusha kwa mkono. Nikachukua ramani ya inayo onyesha inchi ya Somalia, nikaanza kuiptia taratibu, nikaona ni sehemu gani ambayo kambi ya Al-Shabab ipo, nikachukua peni na kuizungushia dura.
“Dany una simu yak kutoka ikulu”
Rubani alizungumza, nikatazama pembeni ya siti yangu nikaona simu, nikaichukau na kuiwekea sikioni.
“Dany”
“Ndio muheshimiwa raisi”
“Ndani ya hiyo ndege kuna kofia za kijeshi, ningeomba uvae moja, ina kamera ambayo itaonyesha kila unapo kwenda na sisi huku ikulu tutakuwa tunafwatlia hatua baada ya hatua kila unapo pita”
 
“Sawa muheshimiwa raisi”
Nikachukua kofia moja ya rangi nyeusi mama mavazi yangu, nikaitazama vizuri na kuona kamra ndogo iliyopo mbele katika hii kamera, nikaivaa vizuri na kuikaza mikanda yake.
“Hapo tunakupata, pia kuna kinasa sauti naomba ukivae utakuwa unazungumza na mimi moja kwa moja”
“Sawa muheshimiwa raisi”
Nikafungua kijiboksi kidogo sana mithili ya viboksi vinavyo wekea pete za ndoa, nikatoa kifaa cha mwasiliano na kukichomeka katika sikio langu la kushoto.
“Muheshimiwa raisi unaisikia?”
“Ndio ninakusikia Dany”
“Hata mimi ninakusikia”
“Tuambie hadi sasa kwenye hiyo ramani umeweza kugundua kitu gani?”
“Katika hii ramani, sehemu hii ndipo kwene kambi ya Al-Shabab”
Nimuonyesha muheshimiwa raisi, nina imani kwamba anaona kila kitu kutokana na kofia ngumu niliyo ivaa na yenye kamera.
 
“Ndio”
“Haya ndio maeneo yao makuu na si rahisi sana kwa mtu kuweza kufahamu kwamba kuna kambi”
“Ila ni jangwani?”
“Yaa ni jangwani sana na si rahisi kwa mtu kuweza kuiona sehemu”
“Ukifika basi utatusaidia, tumesha andaa wanajeshi mia moja wa Marekani kutokea katika kambi yetu ya jeshi iliyopo hapo Somalia”
“Sawa muheshimiwa raisi, ila ningewaomba waweze kutulia hadi pale nitakapo hakikisha kwamba nimewapa amri ya kuweza kuingia katika kambi, kazi yangu kubwa ni kumkamata mkuu wa Al-Shabab, la sivyo tukicheza vibaya atatutoka mikononi mwetu muheshimiwa raisi”
 
“Sawa, wewe ndio chief kamanda wa hiyo oparesheni”
“Nashukuru muheshimiwa raisi”
Safari ikazidi kwenda mbele huku mara kwa mara nikiandaa silaha zangu, kuhakikisha kwamba hakuna silaha ambayo inaweza kuniletea shida yoyote pale nitakapo kuwa kazini.
“Tuna dakika kumi kufika katika anga la Somalia, unatakiwa uvae parachute”
Rubani alizungumza, nikajikuta nikianza kuingiwa na wasiwasi mkubwa sana kwani kwenye maisha yangu sijawahi kuvaa parachute na wala katika mafunzo niliyo yapata katika chuo cha NSS, wala sikuwahi kuambiwa kwamba kuna swala zima la kuvaa parachute. 
 
Sikuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kuchukua begi la parachute, nikalivaa na kufunga mikanda yake, nikasoma maelezo yake jinsi ya kufanya ninapohitaji kulifungua. Ikanilazimu kichwa changu kuelewa haraka sana kwa kila jambo nililo lisoma kwenye hili parechati.
“Begi langu la silaha vipi?”
“Hilo nalo utalishusha kabla yaw ewe kuruka”
“Nitalipatia wapi?”
“Likifika tu chini begi, kwenye PDA yako hiyo hapo pembeni utaweza kuona ni wapi limeangukia na utalichukua”
“Kama ni mbali”
“Sidhani kama ni mbali”
Nikatazama kivaa changu kidogo(PDA) kilicho kaa muundo wa simu, hichi kinatumika kwa ajili ya kuweza kutazama ramani kwa njia ya mtandao, na hata kutumia picha kadhaa kwa njia ya mtandao.
“Dany una dakika tau kuwa tayari”
“Sawa”
 
“Kuha miwani ya kuzuia upepo hujaivaa, vaa kabla hujaruka”
“Ipo wapi?”
Tazama kwenye begi la kushoto kwako”
Nikatazama begi la kushoto kwangu, nikalifungua kwa haraka na kutoa miwani kubwa, nikaivaa na kuikaza mikanda yake nyuma ya kichwa changu.
“Una dakika moja na nusu kaa tayari mlangoni, hakikisha unatanguliza begi”
“Sawa”
“Kwa sasa Somalia ni saa nane usiku”
“Nimekuelewa”
“Una sekunde thelathini kaa tayari”
Mlango wa ndege taratibu ukaanza kufunguka, kusema kweli jinsi upepo mwingi unavyo ingia ndani ya hii ndege ukanifanya nianze kuchanganyikiwa”
“Tupa begi Dany”
Sikuwa na hata jaja ya kulisikua begi kwani upepe unao ingia wenyewe ukalivuta begi na kulitoa.
“Ruka”
 
Nikaachia sehemu nilizo kuwa nimeshikilia na kujitosa angani. Nikaanza kuzungushwa zungushwa hewani, huku kwa mara kadhaa nikijikuta nikipiga mayowe, ambayo natambu kabisa yanasikika hadi ikulu.
“Dany Dany”
Niliisikia sauti ya muheshimiwa raisi akiniita.
“Ndio, naanguka”
“Tulia, bana pumzi, hakikisha viongo vyako unavikaza, bana miguu yako pamoja na mikono”
Nikafanya kama alivyo niangiza muheshimiwa raisi, taratibu nikajikuta nikianza kuhimili kasi ninayo kwenda nayo chini. Nikajikuta miguu yangu sasa ikiwa ndio inaelekea chini tofauti na nilivyo toka kwenye ndege kwani kicha ndio kilikuwa kimetangulia kwenda chini.
 
“Unaweza kufungua parachute, minya batani katika bega lako la kushoto”
Niliendelea kuyasikilia maelekezo ya raisi, ambaye ameamua kuisimamia hii opareheni yeye mwenyewe japo kuna watu ambao wanapaswa kuisimamia hii oparesheni. Nikaiminya batani iliyopo kwenye mikanda ya hili parachute, fuko kubwa likajitokea kwa juu yangu, sasa hapa nikaanza kupata muhimili mzuri. Nikashika vijikakamba viwili vilivyopo pembeni yangu na kuanza kuliongoza parachute hili, nikaanza kuvuta pumzi taratibu huku nikizidi kwenda chini. 
 
Nikaanza kuikwepa miti ailiyopo katika eneo hili hadi nikafanikiwa kutua chini huku nikikimbia ili kuhimili fuko hili kubwa linalo jikunja lisinifunike. Nilipo hakikisha kwamba nimesimama, nikavua begi la parachuti hili na kuanza kulikusanya kwa haraka, kisha nikalificha kwenye moja moja ya kichaka hata kama ikitokea kwamba nimeshuka katika eneo la maadui basi wasiweze kujua ni kitu gani kinacho endelea. Nikatoa PDA, yangu nikaminya batani ya pembeni, nikaona alama nyekundu inayo onyesha ni wapi bebi langu lilipo, cha kumshukuru Mungu si mbali na eneo hili nilipo.
 
    Nikachomoa bastola yangu na kuanza kutembea kwa umakini katika msitu huhu uku nikifwata maelekezo ya PDA yangu niliyo ishika mkononi mwangu.Nikakaribia eneo ambalo ndipo begi langu limeangukia, nikaona taa za tochi zilizo nifanya nijibanze kwenye moja ya mti.
Mwanga wa mbalamwezi ukanifanya niweze kuwaona watu hawa vizuri, ni wanajeshi walio valia mavazi mavazi ya serikali ya Somalia. Mmoja wao amefungua begi langu na kutoa magazine ya bastola zangu.
“Muheshimiwa raisi kuna wanajeshi wa serikali wanaonekana kulikagua begi langu, na endapo watatoa taarifa kwa wezao inaweza kuwa tataizo kwangu”
 
“Unaweza kujisalimisha mikononi mwao?”
“Nini!!?”
“Nitazungumza na raisi wao na wanaweza kukuachia ndani ya muda mfupi tu na utaendelea na oparesheni yako”
“Hakuna wa kumuamini muheshimiwa raisi katika hili, hawa ndio wanao ogoza kula rushwa kutoka katika kundi la Al-Shabab ndio maana wanashindwa kukabiliana na hili swala”
Nilizungumza huku nikifunga kiwambo cha kuzuia sauti kwenye bastola yangu, nikajisogeza kwenye mti mwingine taratibu pasipo wao kuweza kuniona. Kitendo cha mwanajeshi mmoja kunyanyua simu yake ya upepo na kuhitaji kuwasiliana na wezake ikawa ni kosa kubwa kwangu kwani sikuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kumuua mwajeshi huyu kwa kumpiga risasi ya kichwa jambo lililo mfanya mwenzake kubaki akiwa ameduwaa asijue hata cha kufanya kwani mkononi mwake hana hata silaha ya kujitetea.

==>>ITAENDELEA KESHO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya October 27

Mwanafunzi Anusurika Kifo Baada ya Choo cha Shule Kutitia.......Tazama Picha

0
0
Mwanafunzi  wa darasa kwanza katika Shule ya Msingi Seliani, wilayani Arumeru mkoani Arusha, Emanuel Zakaria (7), amenusurika kufa baada ya kutumbukia ndani ya choo cha 
shimo.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’azi, alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo jana wakati mwanafunzi huyo alipokwenda 
kujisaidia wakati wa mapumziko.

“Tunaangalia chanzo cha kuvunjika kwa shimo hilo ni nini na
ukizingatia sasa hivi ni kipindi cha mvua kubwa zinazoendelea 
kunyesha, tutaangalia pia kama ujenzi haukuwa madhubuti au ni
kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha bado tunafanya uchunguzi wa
tukio hilo,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, alisema tukio hilo lilitokea
 majira ya saa 3: 45 asubuhi muda mfupi kabla ya muda wa mapumziko.


Alisema mwanafunzi huyo, mkazi wa Kijiji cha Olevolosi, baada ya kuopolewa, alipelekwa kwenda kupata matibabu katika Hospitali ya Selian na kwamba hali yake 
inaendelea vizuri.

Muro alisema lilitokana na kutitia kwa ardhi 
kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali ya mkoani
 Arusha.


Mkuu huyo wa wilaya aliwapongeza wananchi wa eneo hilo kwa utayari na kutoa kwa moyohali ambayo ilisaidia kunusuru maisha ya mwanafunzi huyo.


“Niwapongeze wananchi kwa utayari wa moyo wenu wa kujitolea, serikali 
inataka watu wenye moyo wa kujitolea kama walivyofanya leo (jana)
 kuokoa maisha ya mwanafunzi huyu,” alisema.

Hata hivyo, alisema Serikali ipo tayari kuungana na wananchi katika
ujenzi wa choo cha kisasa hadi kitakapokamilika.


“Nimeshatoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha, waanze mchakato wa ujenzi wa choo kipya, Jumatatu, nitakuwa
 shuleni hapo kushirikiana nao ili kuhakikisha ujenzi huo
 unakamilika kwa wakati,” alisema.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Olevolosi, Samweli Mollel, alisema baada ya
kutokea kwa tukio hilo, waliwaita wanafunzi wote madarasani ili
 kuwafanyia uhakiki kwa majina kuangalia watoto kama wapo wote.

Mwalimu Mkuu Atuhumiwa Kuwapapasa Wanafunzi Sehemu za Siri

0
0
Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwibara, Bunda mkoani Mara, Betha Sayi, ameingia matatani baada ya kudaiwa kuwadhalilisha wanafunzi wa kike wa shule hiyo.

Sayi anatuhumiwa kuwavua nguo zote wanafunzi hao, zikiwamo za ndani na kuwashika shika katika sehemu za siri kwa madai kuwa anawapima kama wana ujauzito

Tuhuma hizo zilitolewa jana na wanafunzi hao, hali ambayo ilisababisha taharuki kwa wazazi ambao walisema hawawezi kuvumilia kitendo hicho cha udhalilishaji, ukatili wa kijinsia na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Ilidaiwa kuwa, mwalimu huyo alifika shuleni hapo juzi asubuhi na kuwaita wanafunzi hao kila mmoja katika ofisi yake na kuanza kuwavua nguo zote na kisha kuwafanyia kitendo hicho cha udhalilishaji.

Aidha, imeelezwa kuwa, baada ya kuwavua nguo zote na kuwafanyia udhalilishaji huo, alichukua nguo zao za ndani za wanafunzi hao na kuziweka ndani ya boksi.

Hali hiyo iliwafanya baadhi ya wanafunzi hao kukimbilia nyumbani kwao na kutoa taarifa kwa wazazi wao, ambao walitahamaki na kwenda shuleni hapo na kisha wakatoa taarifa katika kituo kidogo cha polisi Kibara.

Akizungumzia sakata hilo, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mwibara, Sylivanus Manyapara, ambaye pia ni Kaimu Mratibu Elimu Kata, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kwamba mwalimu huyo alipelekwa katika kituo cha polisi Kibara, akiwa na nguo za ndani za wanafunzi hao zilizokuwa kwenye boksi.

Mnyapala alisema tayari tukio hilo limeripotiwa katika kituo kidogo cha polisi Kibara na mwalimu huyo alishikiliwa kwa muda kisha akapewa dhamana na nguo hizo ziko kituoni hapo kama kielelezo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kibara B, Mafwili Mnyanga, alisema kitendo hicho kimelaaniwa na wazazi na wananchi wa kijiji hicho.
 
"Kitendo hiki ni kibaya sana na kinaweza hata kusababisha vurugu kwani watoto kufanyiwa hivyo ni unyama. Wamefanyiwa ukatili mkubwa na pia huo ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kwa hiyo sisi wazazi pia tumeathirika kwa kitendo hicho," alisema kwa njia ya simu.

Serikali Yawataka Watendaji Sekta Ya Ardhi Nchini Kujisahihisha

0
0
Na Munir Shemweta, WANMM Kilimanjaro
Waziri wa Ardhi Nyumba na Mandeleo ya Makazi William Lukuvi amewataka watendaji wa sekta ya ardhi nchini kujisahihisha ili kuepusha mogogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikiwaumuzi wananchi wengi.

Lukuvi alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na wananchi 97 wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na Halmashauri ya Moshi Vijijini katika mkoa wa Kilimanjaro waliojitokeza kwa ajili ya kuwasilisha kero zao za ardhi kupitia program ya Funguka kwa Waziri.

Alisema, ni vyema katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya tano watendaji wa sekta ya ardhi wakaanza kujisahihisha ikiwemo kuweka majalada yote ya ardhi vizuri kabla hajatembelea maeneo yao kinyume chake atawashughulikia wote watakaobainika kukaidi ama kutoweka sawa majalada ya ardhi.

“Mtu yeyote anayetaka kuingusha Serikali katika masuala ya ardhi tutamuangusha yeye na lazima tutekeleze ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa vitendo” alisema Lukuvi.

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Serikali itawanyoosha wale wote wanaoenda kinyume na maadili ya utumishi na kubainisha kuwa hata wale watendaji wa ardhi walioharibu huko nyuma watashughulikiwa.

Akigeukia migogoro ya ardhi, Lukuvi alisema migogoro mingi inayojitokeza sasa ni ile ya miaka ya nyuma ya kuanzia miaka ya themanini na kubainisha kuwa kupungua kwa migogoro mipya kunatokana na Serikali ya sasa kuweka mazingira mazuri ya kushughulikia masuala ya ardhi.

“Leo watendaji wa sekta ya ardhi wamenyooka na kazi ya serikali ya awamu ya tano ni kuwanyoosha wale wanaoenda kinyume na taratibu na sheria katika kushughulikia masuala ya ardhi.

Akigeukia suala la wamiliki wa ardhi kuchukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia, Lukuvi amewahakikishia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa, Serikali inalipa kipaumbele suala la fidia kwa wale ambao maeneo yao yatachukuliwa.

Aliwaeleza kuwa hata ikitokea mtu hakufidiwa kipindi ambacho eneo lake limechukuliwa lakini malipo yake yataanza kuhesebiwa pale eneo lilipochukuliwa na kiwango cha fidia kitakuwa kikiongezeka kadiri malipo yake yanavyochelewa.

Pia aliwaeleza wananchi waliokusanyika katika ukumbi wa ofisi wa mkoa wa Kilimanjaro kuwa wale wote ambao maeneo yao yalishatolewa maamuzi na Mahakama hakuna mtu yoyote mwenye mamlaka ya kubatilisha ikiwemo Serikali.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo October 28

Waziri Mkuu: Tutaendelea Kushirikiana Na Sekta Binafsi

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali inathamini uwepo wa sekta binafsi nchini na kwamba inaendelea kushirikiana nayo katika kuboresha maendeleo ya Taifa.

Ameyasema hayo jana (Jumamosi, Oktoba 27, 2018) wakati alipokutana na bodi mpya ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania kwenye makazi wa Waziri Mkuu, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amempongeza Mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw. Salum Shamte na wajumbe wa bodi hiyo kwa kuchaguliwa kuingoza taasisi hiyo. Bodi hiyo mpya ilikwenda kujitambulisha.

“Serikali inadhamira ya dhati ya kushirikiana na taasisi hii kwa sababu ndio muwezeshaji wa kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo 2025,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw. Shamte amesema sekta binafsi inatambua juhudi za Serikali katika kuboresha mazingira ya biashara nchini Tanzania.

“Sisi tupo tayari kushirikiana na Serikali kwa kuwabana wafanyabiashara ambao wanaenda kinyume na maadili na sheria, ila tunaomba Serikali ishirikiane nasi katika utekelezaji wake.”

Pia, Bw. Shamte ameiomba Serikali iendelee kutoa vivutio kwa biashara zinazoanza ili kuhamasisha uwekezaji kwa kuwa baadhi yake zimeonesha gharama kubwa za uzalishaji.

LIVE: Zitto Kabwe anazungumza na waandishi wa habari

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini ambaye pia ni kiongozi wa ACT Wazalendo,  Zitto Kabwe  anazungumza na waandishi wa habari, unaweza kubonyeza play hapa chini kutazama

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Zitto Kabwe Awataka Wananchi Waendelee Kukemea Matukio ya Utekaji

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amewataka wananchi kutokaa kimya yanapotokea matukio ya utekaji nchini Tanzania, akibainisha kuwa kukemea kunasaidia ukweli kujulikana na hata wahusika kupatikana.

Ametoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 28, 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari unaofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama hicho Kijitonyama, Dar es Salaam.

Amesema Watanzania kupaza sauti baada ya kutekwa na kupatikana kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo’ kumeonyesha jinsi walivyoanza kuchoshwa na vitendo hivyo.

“Haya tumekuwa tukiyasema ndani na nje ya Bunge na tutaendelea kusisitiza kwa sababu tunafahamu umuhimu wa vyombo hivi (vya Serikali). Kama wapo wachache wanaochafua taswira ya vyombo hivi ni lazima tuseme,” amesema Zitto.

“Kama vyombo hivi haviambiwi sisi ni lazima tuseme, hatua zichukuliwe kwa matukio ya awali.”

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Shirika La Ndege (ATCL) Limeondolewa Vikwazo Na Shirikisho la Mashirika ya Ndege Duniani (IATA)

0
0
 Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limeruhusiwa kurejea katika Shirikisho la Mashirika ya Ndege Duniani (IATA), ambapo kuanzia sasa litakuwa na uwezo wa kuuza tiketi zake duniani kote.

ATCL iliondolewa IATA miaka tisa iliyopita baada ya kuelemewa na mzigo wa madeni.

Lakini tangu kufufuliwa upya kwa shirika hilo 2016, limekuwa likipambana kutaka kurejea upya katika uanachama ili kuepuka kukosa malipo ya tiketi zao hususan katika safari za kimataifa.

Taarifa ya ATCL iliyotolewa kwa washirika wake Oktoba 24 na kuthibitishwa na mkurugenzi mkuu wa shirika hilo, Ladislaus Matindi jana  inaeleza kuwa, kurejeshwa kwao kumeanza rasmi mwezi huu.

“Tulipata taarifa kutoka IATA kuwa tumerudishwa kwenye mfumo wa malipo wa pamoja (Airlines Clearing House - ACH)), na sasa Air Tanzania imerejea katika mfumo huo na ni mwanachama halali wa shirikisho hilo,” imeeleza sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na mkurugenzi wa Fedha, Albinus Manambu.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa fomu zote za malipo ambayo hayakufanyiwa kazi au kulipwa wakati ATCL ilipoondolewa katika mfumo, zinapaswa kutumwa upya ACH ili ziweze kushughulikiwa.

Akizungumzia kurejea IATA, mkurugenzi wa Biashara wa ATCL, Patrick Ndekana alisema hatua hiyo inarahishisha uhusiano wao na mashirika pamoja na kampuni zingine za ndege katika biashara kwa kuwa wanapenda kushirikiana na watu waliopo IATA.

“Soko letu katika huduma litapanuka zaidi na tutaweza kushindana na kuifanya Dar es Salaam kuwa njia pana ya kuelekea maeneo mbalimbali, sasa tutafahamika kimataifa na tutaweza kuingia makubaliano na mashirika makubwa ya ndege,” alisema Ndekana.

Aliongeza kuwa hatua hiyo ni muhimu kibiashara hususan wakati huu ambao wamelenga kupanua safari zao nje ya mipaka ya Tanzania.

Alisema kutokana na kurejeshwa IATA, hivi sasa abiria anaweza kukata tiketi za ATCL kokote duniani.

ACT-Wazalendo yaungana na CHADEMA

0
0
Chama cha ACT-Wazalendo kimetangaza kutoshiriki kwenye uchaguzi mdogo wa marudio unaoendelea nchini kwa kile walichodai ni matumizi mabaya ya kodi za wapiga kura.

Akizungumza mbele ya wanahabari, Katibu Mkuu wa chama hicho Doroth Semu amesema kuwa kupitia kikao chao cha kamati kuu kilichokaa mwezi Julai, kiliamua kushiriki katika chaguzi za marudio ambapo wameshiriki kwenye chaguzi tatu lakini baada ya kutafakari wakaona wajiondoe.

Semu amesema kuwa wametafakari namna zoezi la uchaguzi mdogo linavyoendeshwa na kuona kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za wapiga kura kwani wanaojiuzulu ndio wanaoshinda chaguzi za marudio.

"Tumeshiriki chaguzi tatu mfululizo, tumekaa tukatafakari na tumeona kuwa kuendelea kushiriki ni kubariki jambo la viongozi kujiuzulu na kurudi tena kwa namna nyingine, hivyo tumejiondoa kwenye uchaguzi mdogo wa Disemba 2, mwaka huu", amesema Semu.

Kujiondoa kwa ACT-Wazalendo katika uchaguzi wa marudio, chama hicho kinaungana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilichotangaza kujiondoa rasmi kushiriki chaguzi ndogo zote zilizotangazwa kufanyika hivi karibuni na chaguzi zozote zitakazofuata zinazosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa madai kwamba tume hiyo inafanya kazi ya Chama Cha Mapinduzi.

Kauli hiyo ilitolewa Septemba 19, na mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Freeman Mbowe na kuituhumu NEC akidai inafanya kazi ya kuhakikisha chama tawala kinashinda kwa kulazimisha matokeo hivyo hawatashiriki katika chaguzi za marudio kwa kile alichodai kuwa, chama kinapitia maumivu mazingira magumu ya kisiasa.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648  au 0656 551 093  au 0746473974
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images