Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sakata la Picha za Uchi: RC Makonda Amtaka Amber Rutty Ajisalimishe Polisi Kabla ya Saa 12 Jioni

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam amemtaka msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Amber Rutty ajisalimishe polisi mwenyewe baada ya picha zake za utupu kuvuja mtandaoni.
RC Makonda

RC Makonda amemtaka msanii huyo aripoti kwenye kituo chochote cha Polisi kilicho karibu naye kabla ya saa 12 jioni.

“Wakati TCRA wakijipanga kuchukua hatua, mimi namtaka mwenye picha hii kufika kituo chochote Cha Polisi kilichopo karibu na eneo lake kabla ya 12 jioni. Na ukifika waambie umeitwa na RC Makonda watakupatia ujumbe wako.“amesema RC Makonda.

Siku ya jana kwenye mtandao wa Instagram kulisambaa video ya msanii huyo akiwa uchi wa mnyama akifanya mapenzi na jamaa yake, tena kinyume na maumbile.

Tukio hilo la kuvuja video hizo za utupu za Amber Rutty, limekuja masaa machache baada ya Muigizaji Wema Sepetu naye video zake za utupu kuvuja mtandaoni.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Nikki wa Pili Awachana Wasanii wanaotafuta kiki kwa picha za Uchi

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka katika kundi la Weusi Nikki wa Pili amefunguka na kuwashambulia wanaotafuta kiki kupitia mambo ya kijinga. 

Msanii huyo ameongea hayo kwa kuyaandika maneno kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuwachana watu hasa wasanii wanaotafuta kiki kupitia vitu visivyo na maana.

Kauli hiyo ameitoa baada msanii wa Bongo movie na aliyekuwa Miss Tanzania 2006 mwanadada Wema Sepetu  kupost video zisizo na maadili akiliwa denda na mwanaume ambaye hakufahamika jina lake.

==>>Ujumbe wa Nikki wa Pili ni huu hapa:-

Breaking News: Serikali Yamfungia Wema Sepetu Kujihusisha na Filamu kwa Muda Usiojulikana

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu leo baada ya kuitwa kuhojiwa na Bodi ya Filamu Tanzania kuhusu kusambaa kwa picha na video  zake chafu  kwenye mitandao ya kijamii, imeamua kumfungia msanii huyo kujishughulisha na mambo ya filamu.

Bodi hiyo imeamua  kumfungia msanii huyo na kumtaka kutojishughulisha na filamu kwa muda usiojulikana, kufuatia picha zake chafu zilizosambaa mtandaoni.

Ikubukwe kwamba jana  October 25,  msanii huyo aliomba msamaha kutokana na tukio hilo ambalo lilitokea siku kadhaa nyuma ambapo alionekana akiliwa denda na mwanaume anayesemekana ni raia wa Burundi.

Hata hivyo, Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza akizungumzia juu ya msamaha huo amesema kuwa ni unafiki mkubwa kwani sio mara ya kwanza wala ya pili kwake.

“Hii ni kama unafiki fulani, kwa sababu hii sio mara ya kwanza kwa msanii huyu, wala sio mara ya pili, na niseme tu kwamba kwa upande wa Baraza lina mchango wake kufikia hapo alipofikia, ile ni unafiki, haitoshi, mtu mara ya kwanza ya pili unasema hii ni tabia zake, na kwa vile kuna sheria zingine zilizovunjwa, lazima wahusika wachukue hatua zake, hii haitoshi, lazima awe mfano”, amesema

Wema amekuwa akijihusisha mara kwa mara na matukio ya kusambaza picha zisizo na maadili mitandaoni na amekuwa akionywa na vyombo husika lakini mara hii vimeamua kumfungia kabisa kutojihusisha na mambo ya filamu.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Kamishana wa Zamani wa TRA Harry Kitilya na wenzake

$
0
0
Jalada la kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili, aliyekuwa Kamishana wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry  Kitilya na wenzake wawili, linafanyiwa kazi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amedai leo Ijumaa Oktoba 26, 2018, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Huruma Shahidi wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Kishenyi amedai kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba Takukuru wapo katika ukamilishaji wa uchunguzi ili kesi hiyo iweze kuendelea na hatua nyingine.

"Upelelezi bado haujakamilika na vyombo vinavyofanya uchunguzi vipo katika hatua ya ukamilishaji uchunguzi hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama vyombo hivyo vya uchunguzi vimeshakamilika uchunguzi," amedai.

Kishenyi baada ya kueleza hayo, wakili wa utetezi, Oscar Magolosa, alieleza kuwa ni rai yao kuwa upelelezi wa shauri hilo utakamilika haraka ili kesi hiyo iweze kuendelea.

"Ni matumaini yetu upelelezi wa kesi hii utakamilika kwa wakati kama ambavyo, upande wa mashtaka ulivyoiambia Mahakama hapa kuwa vyombo vya uchunguzi vinakamilisha uchunguzi wao," amedai Magolosa.

Baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote, Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 9, 2018 kesi itakapotajwa tena.

Pamoja na Kitilya ambaye ni mwenyekiti wa Kampuni ya Uwekezaji wa Mitaji na Dhamana (Egma), washtakiwa wengine ni waliokuwa maofisa wa Benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.

Washtakiwa hao wanaendelea kusota rumande kwa takribani miaka mitatu sasa kutoka na upelelezi wa kesi hiyo kudaiwa kuwa haujakamilika.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648  au 0656 551 093  au 0746473974

Taasisi Ya Moyo Jakaya Kikwete ( JKCI ) Kutoa Huduma Ya Kliniki Ya Moyo Inayotembea Mkoani Kagera

$
0
0
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera wanatarajia kutoa huduma ya kliniki ya Moyo inayotembea (Cardiac Mobile Clinic) katika Mkoa wa Kagera kuanzia tarehe 5 hadi tarehe 11 Novemba, 2018.

Huduma zitakazotolewa  ni pamoja na upimaji wa vihatarishi vya Magonjwa ya Moyo, ushauri wa kiafya kuhusiana na Magonjwa ya Moyo, na kutoa rufaa kwa wananchi watakaokutwa na matatizo ya Moyo yanayohitajika kupewa rufaa kuja kwenye Taasisi hiyo  kwa uchunguzi wa tiba zaidi.

Hii Hapa Taarifa Rasmi Ya Bodi ya Filamu Kumfungia Wema Sepetu Kujihusisha na Filamu

$
0
0
Serikali  kupitia Bodi ya Filamu Tanzania leo, Oktoba 26, 2018 imemfungia staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu na kumtaka asijihusishe na shughuli za filamu kwa muda usiojulikana, ni baada ya picha zake chafu  akiwa na bwana yake raia wa Burundi kusambaa mitandaoni.

==>>Hapo chini kuna taarifa rasmi toka Bodi ya Filamu nchini 

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 19

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

Kabla sijalijibu swali la muandishi wa habari huyu, nikashuhudia gari la wagonjwa likisimamishwa kwa haraka aneo la mbele la nyumba hii. Wauguzi wakashuka kwa haraka kwenye gari hilo huku wakiwa na kitanda cha kusukuma na kukimbilia ndani ya nyumba hii. Wasiwasi mwingi ukanijaa moyoni mwangu, makamera man wakageuzia kamera zao katika eneo lilipo gari hilo la wagonjwa. Nikaanza kutembea kueleka katika eneo hilo la gari huku nikifwata kwa nyuma na waandishi hao wa habari. Kabla sijalifikia gari hili nikawaona wauguzi wakitoka ndani humu huku juu ya kitanda wakiwa wamemlaza bibi Jane Klopp huku akihemea pumzi ya oksijeni jambo lililo nistusha sana kwani sifahamu ni kitu gani ambacho kimempata mama yangu, bi Jane Klopp.

ENDELEA               
“Daktari ni kitu gani kinacho endelea?”
Niliuliza huku nikiwa na shauku kubwa ya kuhitaji kufahamu.
“Mama yako amepoteza fahamu gafla, tunatakiwa kumwahisha hospitalini sasa hivi”
“Camila kaa na Mery sawa”
“Sawa”
Nikaingia ndani ya gari la wagonjwa huku nikiwa nimekaa pembeni nikimtazama bibi Jane Klopp jinsi anavyo hema kwa kutumia gesi maalumu ya oksijeni. Gari likaanza kuondoka katika eneo la jumba hili, njia nzima madaktari kazi yao ni kuhakikisha kwamba hali ya bibi Jane Klopp haiwi mbaya kabisa. Tukafika hospilini na bibi Jane Klopp akashushwa kwenye gari huku nami nikishuka na tukaanza kutembea kelekea katika chumba cha matibabu. Nikaikunja vizuri mikataba niliyo wasainisha mameneja kisha nikasimama pembeni ya mlango wa chumba hichi.
‘Ethan ni nini kimempta mama?’
‘Ni mstuko’
‘Haliya kae itakaa vizuri?’
‘Ndio usiwe na waasiwasi mkubwa rafiki yangu’
‘Sawa’
Hadi ina inatimia majira ya saa kumi na moja alafajiri bibi Jane Klopp akafanikiwa kupata fahamu zake. Nikakaa naye chini  ya uangalizi mzuri wa madaktari hadi majira ya saa moja asubuhi ndipo nikarudi nyumbani huku daktari mkuu anaye mtibu akiahidi majira ya saa nne asubuhi ataruhuusiwa kurudi nyumbani.
                                                                                                           ***
    Kutokana na kifo cha mzee Klopp utaratibu wa nazishi yake ukatuchukua wiki nzima hadi kukamilika. Hii ni kutokana na umaarufu wake kuanzia kwa wananchi hadi taifa kwa ujumla. Siku ya mazishi ikawadia huku karibia watu wote tukwia tumevalia nguo nyeusi huku wengine wakiwa wamevalia miwani nyeusi ili kuficha huzuni waliyo nayo juu ya kifo cha mzee Klopp. Viongozi mbalimbali kutoka bara hili la Ulaya nao ni miongoni mwa watu ambao wameudhuria mazishi haya.
 
“Mama jikaze”
Nilizungumza huku niiwa nimemuegemeza bibi Jane Klopp kichwa chake kwenye bega langu. Mchunganji akaendelea kuongoza ibada hii fupi, wana familia tukamuaga kwa mara ya mwisho huku tukiwa tumejawa na huzuni kubwa. Baada ya ibada kuisha, tukaondoka eneo hili la makaburini na kuwaachia wazikaji kufanya kazi yao ya kuuweka mwili wa mzee Klopp katika nyumba yake ya milele.
“Ethan”
Bibi Jane Klopp aliniita kwa sauti ya ungonge huku tukiwa katika gari tukirudi nyumbani.
“Ndio mama”
 
“Muangalie dada yako Mery kwa maana siku si nyingi nitamfwata mume wangu kule alipo elekea”
Mimi na Mery tukajawa na mshangao mkubwa sana huku tukimtazama mama usoni mwake.
“Mama huwezi ukafa”
Mery alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Bi Jane Klopp akatabasamu kwa muda.
“Mery mwanangu, mama yako siku zangu za kuishi hapa duniani zina hesabika. Mimi na baba yako tuliweza kudumu sana kwneye ndoa yetu, upendo wetu ulianza toka tulivyo kuwa watoto wadogo na hadi tumekuwa watu wazima.”
Bibi Jane Klopp alizungumza huku akijipangusa machozi usoni mwake kwa kutumia kitambaa chake.
“Yeye ndio alikuwa rafiki yangu wa karibu. Naona kifo kikiwa mbele yangu, nawaomba sana muweze kushikamana, nawaomba sana muweze kupenda na Ethan nakuomba usiweze kusahau asili yako”
“Kivipi mama?”
 
“Ujerumani ni nchi ambayo umekua tu, ila Tanzania ndio nchi ambayo umezaliwa, najua hapo mbeleni utakuwa mchezaji mkubwa sana wa mpira wa miguu. Ila nakuomba ukicheza timu ya taifa, usiichezee Ujerumani, hakikisha unaichezea timu yako ya nchi ya Tanzania. Hata kama ni vikombe basi unailetea sifa nchi yako sawa”
“Sawa mama”
Nilimjibu bibi Jane huku nami machozi yakinimwagika usoni mwangu.
“Mery hakikisha kwamba una chagua mwanaume sahihi kwenye maisha yako, si kila mwanaume anaye kuja kwako ana kupenda, wengi wao wanapenda pesa zako na mali zako, hakikisha kwamba hivyo unaweza kuvihimili kwenye maisha yako ya kila siku.”
“Sawa”
“Ethan kwa upande wako natambua umepata mwnaamke sahihi, ila endapo utamuacha Camila maisha yako yatapoteza muelekeo hata kama utakuwa na pesa nyingi kiasi gani ila maisha yako yatayumba”
 
“Siwezi kumuacha mama nitakuwa naye maisha yangu yote”
“Nashukuru kusikia hivyo”
Bibi Jane Klopp alijibu kwa upole na unyonge wa hali ya juu. Tukafika nyumbani, bibi Jane akatumbo aeleke chumbani kwake kulala kwani anajihisi kuchoka sana.
“Ethan naomba tuzungumze”
Dada Mery alizungumza huku akitangulia nje, tukaa kwenye moja ya benchi la kumpumzikia lililpo katika moja ya bustani.
“Ethan kuna vitu nahitaji kufahamu kuhusu wewe”
“Vitu gani dada yangu?”
“Mama pale alisema kwamba umetokea Tanzania, je unapafahamu kwenu hata tukisema twende tukatembekee huko?”
Nikaka kimya huku nikitafakari maisha yangu ya nyuma.
“Nafahamu mkoa nilio tokea”
“Ni mkoa gani huko Tanzania?”
“Kilimanjaro ndio mkoa nilio tokea, mzee na mama ndiopo walipo nikuta huko”
“Je unaweza kuwakumbuka mama na baba yako au ndugu zako wengine?”
 
Nikajaribu kurudisha kumbukumbu zangu nyuma, ila kitu ninacho kikumbuka ni siku nilipo kuwa nimelala kitandani na kuwasikia mzee Klopp na mke wake wakizungumza.
“Ethan”
“Sikumbuki mtu wa ina yoyote.”
“Hata mama yako humkumbuki?”
“Kwa kweli simkumbuki”
“Mmmm”
“Ila mzee na mama waliniambai kwamba waliniokota pembezoni mwa mto mmoja hivi nahisi huko ndipo nilipo kuwa nimepata matatizo”
“Huo mto walikuambia jina lake?”
“Hawakuniambia na wala siufahamu ni mto gani”
“Inabidi siku moja tupange safari na kwenda nchini Tanzania, natamani sana kuiona hiyo nchi”
“Tuombe Mungu dada yangu mambo yasiwe magumu”
“Ila ushauri wa mama alio kueleza hakikisha kwamba una ufanyia kazi”
“Sawa”
“Poa mimi nipo ndani”
Dada Mery akandoka na kuniacha nikiwa na mawazo mengi sana juu ya kuifikiria nchi yangu ya Tanzania.
                                                                                                                        ***
    Siku zikazidi kusonga mbele huku nami nikizidi kujitahidi kuutenga muda wangu katika masomo na kuongoza mali za mzee Klopp ambazo kwa sasa ni mali zangu. Ethan hakusita kunisaidi kwa kila jambo ambalo ninalifanya kwenye maisha yangu.  Nikiwa mwaka wa mwisho katika masomo yangu ya sekondari, Camila na wanafunzi wezake wakapata safari ya kuelekea barani Afrika kwa ziara ya wiki mbili katika nchi ya Somalia na Tanzania.
 
“Unafurahia safari yako?”
Nilimuuliza Camila huku tukiwa tumekaa kwenye bustani ya shule ninayo isoma mimi.
“Ndio nina furaha”
“Hivi unafahamu kwamba Tanzania ndipo nilipo zaliwa?”
“Weee?”
“Hivi sikuwahi kukuambia hicho kitu?”
“Hapana”
“Mmmm mabona nahisi kwamba nimesha wahi kukuambia?”
“Hapana au kama umeniambia basi nitakuwa nimesahau”
“Tuachane na hayo. Mimi kwetu ni mkoa wa Kilimanjaro”
“Kwenye mlima wa Kilimanjaro?”
“Ndio”
“Ohoo huko ndipo tunapo kwenda”
“Ni mlima mmoja mzuri, naamini utakwenda kufurahia safari ya huko”
“Kweli”
“Camila muda wa kuondoka umefika”
Mmoja wa waalimu aliye kuja na Camila alizungumza huku akitutazama.
 
“Tunakwenda mwalimu”
“Camila hakikisha unakuwa muangalizi huko, kwa nchi ya Somalia huwa sina uhakika nayo katika usalama wake”
“Usijali mume wangu, tumehakikishiwa ulinzi mzuri”
“Sawa, ila vipi baba yako kampeni zake zinaendeleaje?”
“Mmmm vizuri, tuna matumaini anaweza kuchukua kiti cha uraisi”
“Sawa, nenda usije ukamuudhi mwalimu”
Camila taratibu akanibusu mdomoni mwangu kisha akaanza kutembea kueleka kwa mwalimu wake. Hakika Camila ni mzuri kuanzia juu hadi chini. Kiunoni mwake amefungashia makalio makubwa kiasi huku hipsi zake zikiwa zimenona kisawa sawa. Mguu wa bia ndio kabisa umezidi kunichanganya akili yangu.
 
“Una mwanamke mzuri kaka”
Sauti ya rafiki yangu Frenando ikanistua, nikajikuta nikitabasamu huku nikimtazama usoni mwake.
“Yaaa Mungu amenibariki”
“Tukimaliza masomo hakikisha una muoa?”
“Huo ni mpango uliopo mbele yangu, baba yake ameniahidi akipata kiti cha uraisi basi nitamuoa”
“Naamini nitakuwa msimamizi wako”
“Hahaa hilo wala usijali, vipi leo tunaelekea uwanjani?”
“Yaa ndio nilikuja kukustua twende tukaanze mazoezi”
Nikaondoka na Frenando, rafiki yangu kutoka nchini Mexco. Tumekuwa ni marafiki toka kidato cha kwanza hadi muda huu na uwanjani mwezangu anacheza nafasi ya golikipa huku nami nikicheza nafasi ya mshambuliaji. Tukiwa katikati ya mazoezi, tukamuona mwalimu mkuu akifika uwanjani hapa jambo amlao sio kawaida yake.
 
“Ethan na Frenando njooni”
Tukatoka uwanjani na kuwaacha wezetu waendele na michezo.
“Natambua kwamba sasa hivi muna jiandaa na masomo yenu ya mwisho, ila nina jambo moja nina hitaji kuwaomba”
Mwalimu mkuu alizungumza huku akitutazama usoni mwetu, nikatingisha kichwa kidogo ikiwa ni ishara ya kumruhusu mwalimu mkuu aweze kuzungumza kile anacho kihitaji kukizungumza.
“Kuna mashindano ya shule za sekondari za bara la Ulaya. Shule yetu ni moja ya shule zilizo chaguliwa kushiriki kugombani kombe hilo. Kuna shule kutoka, Uingereza, hapa Ujerumani, Hispain na kadhali. Ndio shule yetu ina kikosi kizuri cha wachezaji, ila pasipo nyinyi kuwepo hakuna jambo linalo weza kufanyika na sidhani kama shule yetu inafuzu na kufika mbali”
 
Mwalimu  mkuu alizungumza kwa upole sana na ushawishi mkubwa kwani wachezaji wanao soma kidato chetu wote wametolewa katika kikosi cha timu ya shule ili wapate muda mzuri wa kujiandaa na mitihani ya mwisho. Nikamazama Frenando usoni mwake.
“Mkuu hapo inabidi tusaidiane, kama unavyo jua mitihani ya mwisho inavyo kuwa migumu na inahitaji muda mwisngi wa kujiandaa sasa tukishiriki ina maana kuna asilimia stini ya sisi kufeli”
“Una maanisha nini Frenando?”
“Maana yangu ni kwamba inabidi utuhakikishie juu ya kuvujisha mtiani kwa sisi wawili. Nasi tutajitoa kwa ajili ya shule na utapata sifa timu yako kuchukua ubingwa na pili utapata sifa ya wachezaji wako kufaulu kwa kiwango cha juu”
Mwalimu mkuu macho yakamtoka, akavua miwani yake na kujipangusa macho yake kidogo kisha akaivaa tena.
“Hilo ni kosa la jinani na ikijulikana lazima nifungwe na mutafutiwa matokeo”
“Siri itakuwa ni ya watu watatu, mimi wewe na Ethan?”
“Nipeni muda niwee kulifikiria hilo”
 
“Utakapo kuwa tayari basi nasi tutakuwa tayari”
Mwalimu mkuu akaondoka bila hata ya kuaga na kumfanya Ethan kuangua kicheko cha chini chini.
“Pumbavu, tumemkamata anapenda kujipatia ujiko kupitia sisi na mwisho hatunufaiki na chochote”
Frenando alizungumza huku akiendelea kumsindikiza mwalimu kwa macho.
“Turudi uwanjani”
Nilimuambia Frenando huku nikikimbilia ndani ya uwanja na tukaendelea na mazoezi ya kawaida ambayo tunayafanya kila siku. Baada ya siku tatu mkuu wa shule akatuita ofisini kwake, akatueleza kwamba amekubaliana na makubaliano yetu tuliyo muagiza na atahakikisha kwamba hakuna kati yetu atakaye weza kufeli. 
 
“Kama ni hivyo, anda mashabiki tu”
Frenando alizunugmza huku akinyanyua kwenye kiti alicho kalia na tukatoka ofisini humu. Kitu ninacho mpendea Frenando ni mtu anaye jiamini na huwa hayumbishwi na msimamo wake anao jiwekea. Amekuwa ni msaada mkubwa sana wa kwangu wa kuwakataa wasichana wote wanao mtumia yeye kunisumbua katika swala la mahusiano huku akiamini kwamba Camila ndio mwanamke sahihi kwenye maisha yangu na si hawa wengine wanao nipenda kutokana na pesa pamoja umaarufu wangu.
 
    Wanafunzi wa kidato chetu wakashangaa sana kutuona nasi tumeitwa kwenye kikosi cha timu ya shule. Maswali mengi yakaibuka kwa baadhi ya wachezaji wa darasa letu, ila hatukuweza kuwajibu kitu cha kueleweka huku nasi tukiwaambia hatujui ni kwa nini kocha wa shule ameamua kufanya hivyo. Tukajumuika na wanafunzi wa vidato tofauti tofauti katika kufanya mazoezi na timu ya shule.
“Frenando”
“Mmmm”
“Umepata barua yangu yoyote kutoka kwa shemeji yako?”
“Hapana kwa nini?”
“Aliniahidi kwamba akifika nchini Tanzania atanifahamisha kwamba amefika”
“Labda hajapata simu, si unajua huko alipo kwenda maisha ni tofauti na hapa Ujerumani”
“Ni kweli”
Kocha akatukabidhi ratiba ya nchi tulizo pangwa nzao katika kundi letu hili ambalo ni ‘F’
 
“Nchi ya kuwa nazo makini sana hapo ni Uingereza na Italy, tukifanya makosa hatuto songa mbele na wezetu wamejiandaa kisawa sawa, kwani wachezaji wao wana vipaji na wana uwezo mkubwa. Ethan wewe ni jicho langu, Frenando wewe ni kifua changu na mulio salia nyinyi ni mikono yangu. Nawaomba musiniangushe, nawaomba mufanye kile munacho paswa kufanya kwa miaka yote ya nyuma kwenye mashindano mengine. Haya ni mashindano mapya kabisa kwa timu za sekondari, hapa ndipo kwa kujiuza nyinyi wewenyewe kwani mameneja na makocha kutoka timu kubwa duniani watakuwa wakifwatilia mashindano hayo ambayo yatarushwa moja kwa moja kwenye televishion. Tulinde heshima ya nchi, na heshima na shule pia. Kwa pamoja tutakiwa kishinda sawa”
 
Wachezaji wote tukamuitikia kocha wetu kwani amezungumza maneno hayo hadi machozi yanamwagika usoni mwake, ikiashiria kwamba ana uchu na hamu sana ya kutuona vijana wake tunashinda na kuwa timu bora katika bara zima la Ulaya.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 124 na 125 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA     

“Mr president”   
Nilimuita huku nikimtazama usoni mwake.
“Dany”           
Raisi aliniita huku akiwa amenikazia macho. Hata kabla sijazungumza kitu chochote helicopter sita za kijeshi zikaanza  kutua katika eneo hili, huku zikiwa zimetuweka kati mimi na raisi. Wanajeshi wengi wa kimarekani wakaanza kushuka mmoja baada ya mwingine, huku wakiwa na bunduki zao mikonini na wakaniamrisha kunyoosha mikono juu na kukaa mbali na raisi wao.
   
ENDELEA      
Gafla nikastukia kitu kizito kikinipiga kwa nyuma na kujikuta nikianguka chini na kupoteza fahamu.
                                                                                           ***
Taratibu nikayafungua macho yangu, nikaaza kutazama hili eneo nililopo. Ni ndani ya chumba kilicho pangiliwa vizuri, kitanda nilicho lalia kina ukubwa wa sita kwa sina na nikitanda cha kisasa kabisa. Taratibu nikakaa kitako huku nikijitama mwili wangu, jeraha lililopo begani mwangu, limefungwa vizuri tofauti na bandeji ambayo niliweza kufungwa mara ya kwanza na Hawa. 

Nikashuka kitandani huku nikiwa na boksa tu, nikapiga hatu hadi dirishani, nikafungua pazia na kuchungulia nje. Wingi wa magorofa makubwa kwenda juu, yakaniashiria kwabisa kwamba hapa nilipo ni nchini Marekani. Hata hapa nilipo nipo gorofani, mlango ukafunguliwa na kujikuta nikigeuka na kutazama ni nani anaye ingia.
 
“Habari yako bwana Daniel?”
Mzee mmoja mweusi kiasi alizungumza huku akitabamu sana usonimwake.
“Salama”
“Ninaitwa bwana Alexander Brown ni mshauri mkuu wa raisi wa Marekani”
“Nashukuru kukufahamu bwana Brown”
“Raisi anahitaji kuonana na wewe kuna mambo baadhi anahitaji kujadiliana nawe ikulu”
 
“Ikulu!!?”
Niliuliza huku macho yakinitoka kwa maana kusema kweli sikuwahi kufikiria hata siku moja kwamba ipo siku nitaingia kwenye ikulu tena ya Marekani.
“Ndio, na kwenye hilo kabati hapo kuna nguo unaweza kuzivaa, kisha nikakupeleka hoteli ukapata kifungua kinywa”
“Sawa bwana Brown”
Nilizungumza huku nikiwa na shauku kubwa sana ya kwenda kuingia ikulu ya Marekani, baada ya bwana Brown kutoka katika hichi chumba kwa haraka nikafungua kabati. Nikakuta suti mpya ikiwa kwenye makasha yake, imening’inizwa vizuri huku shati jeupe na tai nyeusi navyo zikiwa vimening’inizwa vizuri sana. 

Kwa furaha kubwa nikajikuta nikianza kuchaza stepu ambazo haya kwenye kwaya hazijawahi kutokea, nikajinyoosha viungo vyangu vya mwili, kisha nikaingia bafuni, nikaoga haraka pasipo kutotesha bandeji niliyo fungwakwenye bega langu. 

Nikajifuta mwili wangu kwa taulo kubwa linalo nukia vizuri, nililipo hakikisha kwamba nipo vizuri. Nikaanza kuvaa kitu kimoja baada ya kingine. Nilipo maliza nikasimama kwenye kioo hichi, huku nikijitazama juu hadi chini.
 
“Viatu”   
Nilizungumza huku nikifungua kabati hili tena, nikavuta droo moja iliyopo chini, nikakuta viatu pamoja na saa ambayo kwa muonekano wa haraka haraka inaonekana ina thamani kubwa sana.
“Asante Mungu”   
Nilijikuta nikitamka maeno hayo kwa furaha kubwa sana. Nilipo maliza kujiandaa, nikapiga hatua hadi mlangoni, nikafungua mlango na kuchungulia nje, nikakuta walinzi wanne pamoja na bwana Brown wakiwa wamesimama wakinisubiria mimi kutoka. 
 
“Twende huku Dany”   
“Sawa”
“Chukua kitambulisho hichi, uvae shingoni mwako kwani mtu haruhusiwi kuingi White House pasipo kuwa na kitambulisho husika”
“Sawa mkuu”
Nikatazama kitambulisho hichi nikakuta kikiwa na picha yangu pamoja na jina langu na la baba yangu, sikutaka kuhoji sana kwa maana nina tambua kwamba wamarekani wana njia nyingi za kuweza kumfahamu mtu kwa undani. Tukaingia kwenye gari moja refu ambalo kwa Tanzania tumezoea kuliita Six door(Milango sita). Mbele yetu zikatangulia pikipiki mbili za polisi huku nyuma yatu kukiwa na gari jeusi likituftwa.
 
“Dany hongera sana”
“Hongera ya nini muheshimiwa?”
“Umeweza kuyaokoa maisha ya raisi wetu””
“Ilikuwa ni jukumu langu kufanya hivyo kwa maana sina roho mbaya”
“Unaonekena”
“Ila ni kwa nini raisi amenileta hapa Marekani?”
“Kusema kweli kwangu mimi sifahamu, ila raisi yeye mwenyewe ndio anaye fahamu. Sisi huwa tunafwata amri yake tu”
“Sawa sawa”
Gari hizi zikasimama kwenye moja ya mgahawa, nikashuka na muheshimiwa Brown.
“Agizia chochote unacho kihitaji?”
“Kwa asubuhi hii sinto kula sana”
“Huwa waafrika sifa yao kubwa ni kwamba wanapenda kula, je ni kweli?”
 
“Hapana, ila wapo baadhi yao wanapenda kula sana, na wapo wanao penda kula kawaida”
Nikaagizia sambusa moja pamoja na chai ya maziwa. Muhudumu akanihudumia kwa haraka sana, nikanywa chai hii kwa haraka ili tu niwahi kwenda kuingia White House.
Tukatoka kwenye mgahawa huu na kuingia kwenye magari, safari ikazidi kusonga mbele huku polisi pikipiki zao zikipiga ving’ora na gari na kila sehemu tunapo pita magari yanatupisha. Kwa mbali nikaliona jengo la White House ambalo kwa mara nyingi huwa ninaliona kwenye baadhi ya filamu za Kimarekani.
 
Ndani ya muda mfupi gari zikaingia kwenye uzio wa ikulu na kusema kweli, nimeingia kwenye ikulu yetu Tanzania ila sijawahi kuona ulinzi mkali kama kwenye hii ikulu. Walinzi walio valia suti nyeusi wana randa randa kila eneo kuhakikisha tu kwamba usalama unakuwa madhubuti.
Moja kwa moja tukaingia ndani, kwenye kordo hizi zimejaa walinzi hadi sasa nikaanza kupatwa na wasiwasi. Tukafika kwenye moja ya mlango, nikatazama juu kidogo nikaona maandishi yaliyo andikwa kwamba hii ndio ofisi ya raisi(President’s Office). Bwana Brown akagonga mlango, baada ya sekunde kadhaa ukafunguliwa kwa ndani na tukaruhusiwa kuingia. Raisi Donald Bush alipo nioana kwa haraka akanyanyuka kwenye kiti alicho kalia na kunifwata, akanipa mkono wa kulia na mimi nikampatia wangu.
“Karibu sana bwana Daniel”
“Shukrani muheshimiwa raisi”
“Karibu ukae”
Nikakaa kwenye sofa nzuri zilizopo ndani ya hii ofisi, bwana Brown naye akaka kwenye sofa jingine kwa ajili ya mazungumzo.
“Dany nashukuru kwa kuweza kuitikia muito wangu, natambua ni mambo mengi yalikuwa yakiendelea nyuma yako”
 
“Ni kweli muheshimiwa”
“Nimeweza kupitia faili lako, hususani maisha yako ya nyuma, ila sijaona kosa lolote ambalo ulilifanya tangu ulivyo kuwa katika kikosi cha NSS”
“Ni kweli”
“Sasa nimekuita hapa kwa ajili ya kazi moja kubwa sana, ninaamini kupitia wewe tunaweza kuifanya Afrika kuwa bara salama na bara lenye amani. Tunahitaji kufuta rushwa, ugaidi ambao unaendeshwa na baadhi ya viongozi walimo kwenye ngazi za juu katika serikali baadhi ya nchi za Afrika”
“Ni kweli muheshimiwa raisi”
“Kitu kimoja nilicho kigundua kutoka kwako, ni kwamba una kipaji kikubwa sana. Tena kipaji chako cha upambanaji ukikitumia vizuri unaweza kufuta giza linalo imulika nchi yako, japo wananchi bado hawaelewi ni kitu gani kinacho endelea katika serikali yao”
“Kweli muheshimiwa raisi”
“Brown naomba faili”
Bwana Brown akasimama na kuchukua faili lilipo juu ya meza ya raisi, akamkabidhi raisi aliye anza kulifunua tartaibu, akalitazama karatasi zake kwa sekunde kadhaa kisha akanikabidhi mimi.
 
“Humo kwenye hilo faili kuna malekezo na mipango yote ambayo tunahitaji wewe kuweza kuifanya. Nchi yangu hususani mimi nitakuwa nyuma yako kuhakikisha kwamba unharibu mifumo yote ya makundi ya kigaidi tukianzia na Al-Shabab, Boko Haramu na Al-Lady”
“Samahani muheshimiwa raisi ninaomba kuuliza”
“Uliza tu”
“Hili kundi la Al-Lady ndio mara yangu  ya kwanza kulisikia”
“Hilo kundi ukifungua nyuma huko utaona maelezo yake. Ila kwa kifupi ni kikundi ambacho kinamilikiwa na kiongozi wa nchi yako, na wafuasi wake ni wanajeshi wa kike ambao anawachukua kuanzi wakiwa watoto hadi kufika ukubwani. Kwa mtazamo unaweza kuona kwamba huyo Livna Livba ndio mkuu wao ila raisi wako ndio yupo nyuma ya hili”
“Kwa nini muheshimiwa raisi musiweze kulichukulia hatua hili jambo?”
“Hatuna ushaidi katika hili, ndio maana mataifa makubwa tunaendelea kuweza mashinikizo kwenye baadhi ya nchi za Afrika ili wamiliki wa hayo makundi waweze kushuka chini, ila kama unavyo jua, nchi kubwa hususani nchi yangu Marekani, hatupatani na nchi nyingi za kiarabu jambo linalo pelekea nchi hizo kuwapa misaada ya kipesa, silaha kwa viongozi hao wa nchi za kiafrika jambo linalo fanya kupata uzito wa kuweza kufwatilia maswala hayo”
Nikashusha pumzi huku nikitazama fiali hili, nikaipna picha ya Livna Livba ikiwa ni moja wapo ya viongozi wa vikundi vya magaidi. Picha nyingine nikamuona baba Hawa akiwa ni kiongozi wa Al-Shabab huku katika kundi la Boko Haramu nikimuona mkuu mmoja anaye itwa Generali Obote Mohamed.
“Hii kazi itaendesha na ofisi yangu ya raisi, ni kazi ya siri sana, utasimama kama mpelelezi wa kiserikali, tutakupa kila aina ya uwezo kuhakikisha kwamba hii kazi inakwenda vizuri”
“Sawa muheshimiwa raisi. Ninaweza kuuliza swali jingine?”
“Uliza tu?”
“Vipi watu kwenye meli waliweza kusalimika?”
Taratibu raisi nikaona furaha yake ikiisha usoni mwake, akamisha chini kichwa chake huku machozi yakimlenga lenga. Tukatazamana na bwana Brown kwa sekunde kadhaa, mguno wa raisi ukatufanya sote kumtazama.
“Mimi na yule kichanga ndio tulifanikiwa kutoka kwenye ile meli, ila wengine wote walifariki dunia katika mlipuko”
“Pole sana muheshimiwa”
 
“Asante , ila rafiki zako ambao walihusika kwenye huu mpango wa kuua maelfu ya watu ndani ya meli, tumeweza kuwakamata na wapo chini ya ulinzi wanaendelea kuhojiwa”
Nikajikuta nikibaki na kigugumizi kikali, nikatamani kuzungumza kitu ila mdomo wangu ukajikuta ukiwa mzito kiasi.
“Una kitu unahitaji kuzungumza juu ya hili?”
“Hapana muheshimiwa raisi, ila nitahitaji kuwaona nao”
“Unaweza kuwaona kwa hilo haina shida”
“Muheshimiwa raisi bila ya kuingilia maamuzi yako ila ninaona hilo jambo sio zuri sana kwa bwana Dany kuweza kulifanya”
“Kwa nini?”
“Tunahitaji kumtumia bwana Dany katika kuendesha hii oparesheni, kuonana na wezake na akiwa katika hali nzuri kama hiyo inaweza kuwafanya wezake kumuona kwamba yeye ni msaliti”
 
“Unashuuri nini bwana Browin”
“Ninacho kushauri muheshimiwa raisi kwa sasa tuhakikishe kwamba tunamuweka mbali bwana Daniel na wezake”
“Samahani kwa kuwaingilia, kwani hadi sasa hivi tangu wahojiwe je kuna jambo lolote ambalo wameweza kuzungumza”
“Hakuna walicho kizungumza”
“Kama hamuta jali ninaomba nionane nao, kwa maana wao watakuwa ni msaada mkubwa sana kwetu”
Muheshimiwa raisi Donald Bush akanitazama usoni mwangu kisha akamtazama bwana Brown, kisha akatingisha kichwa.
“Nimekubaliana na wewe”
Raisi alizungumza kisha akanyanyuka, akachukua mkonga wa simu ya mezani, akaminya moja ya batani na kuiweka sikioni mwake. 
 
“Andaeni magari mawili, bwana Daniel anapelekwa kwenye kikosi cha FBI, nitahitaji aonane na waalifu wote”
Raisi Donald Bush alizungumza na kukata simu.
“Muheshimiwa raisi bwana Daniel hawezi kwenda kuwaona wezake akiwa hivi amependeza, ni lazima watamuona yeye ni msaliti”
“Bwana Browin maamuzi yangu yamesha pita”
“Samahani, ninaweza kupatiwa nguo za wafungwa”
“Ndio”
“Ngingeziomba, nahitaji kufanana na wao”
“Sawa, Brown lishuhulikie hilo swala haraka iwezekanavyo”
“Sawa muheshimiwa raisi”
 
Nikaagana na muheshimiwa raisi, tukatoka ofisini hapa tukiwa tumeongozana na bwana Brown, akanikabidhi kwa mlinzi mmoja wa ikulu. Tukaingia kwenye gari za ikulu na safari ya kueleka kwenye makao makuu ya FBI ikaanza. Safari ikatuchukua muda mrefu kidogo na tukafika katika makao makuu ya FBI, moja kwa moja nikakabidhiwa kwa mkuu wa kikosi hichi cha FBI, nikaingizwa kwenye moja ya chumba, nikakabidhiwa nguo za wafungwa, nikavua nguo zangu na kuvaa vazi hili la kifungwa.
“Nifungeni pingu”
“Sawa”
Nikafungwa pingu za mikonini pamoja na nyororo ndefu miguuni mwangu. Askari wawili wakanipeleka kwenye chumba ambacho nikamkuta Hawa akiwa amechoka kwa kipigo kizito alicho patiwa. Hata kuingia kwangu ndani ya hichi chumba Hawa hajaweza kuniona kutokana na kichwa chake kukiinaminisha chini. Askari hawa wakatoka na kuniacha pake yangu na Hawa, taratibu nikaanza kutembea hadi kwenye kiti alicho kaa Hawa. Nikapiga magoti chini kwa mikono yangu yote miwili nikanyanyua kichwa chake.
 
“Hawa”
Nilimuita kwa sauti ya chini, taratibu Hawa akatafumbua macho yake. Tabasamu pana likaanza kumjaa usoni mwake.
“Dany mume wangu”
“Nipo hapa mke wangu”
Machozi yakaanza kumwagika Hawa taratibu, akusogeza mdomo wake karibu kabisa na mdomo wangu, akausitisha kwa muda kidogo kama mtu anaye tafakari kitu. Gafla nikastulia akinipiga kichwani mwangu kwa kwa nguvu kwa kutumia kichwa chake na kinifanya nianguke chini huku nikihisi kizungu zungu kikali sana.
“Wewe ni muongo msaliti mkubwa wewee”
Hawa alizungumza maneno hayo kwa hasira huku akilia kwa uchungua sana jambo lililo ufanya moyo wangu kuniuma sana.
                                                                           
AISIIIII……….U KILL ME 125

“Baby”       
Niliita taratibu huku nikinyanyuka chini nilipo anguka.
“Mimi sio baby wako, ninakuomba tena usinijue na usinifahamu. Dany nimefanya mambo yote kwa ajili yako leo hii umenifanya nishikiliwe na mikono ya hawa mashetani wa Marekani”
 
Hawa alizungumza huku machozi yakimwagika uso mzima.
“Hawa unazungumza nini mbona hata mimi mwenye nimeshikiliwa kama unavyo niona hapa”
Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Hawa anitazama kuanzia juu hadi chini, kwa mavazi niliyo yavaa dhairi kwamba yanaonyesha kwamba na mimi ni mtuhumiwa katika hii kesi.
“Kwa nini hukuniambia kwamba kwenye ile meli kulikuwa na raisi tena wa Marekani?”
“Raisi?”
“Ndio kitabulisho cha raisi wa marekani nilikikuta chumbani kwetu kikiwa kimeanguka.  Na hicho ndicho kilicho tufanya sisi Wamarekani waweze kutukamata”
 Nikajifanya ninacheka kwa huzuni, huku machozi yakinimwagika usoni mwangu ili kuendelea kulinda uaminifu wangu kwa Hawa.
“Ina maana kwamba mimi ndio nimekileta kitambulisho hicho ndani kwetu?”
 
“Mimi na wewe ndio tulio ingia ndani ya chumba chetu inakuwaje kikwa humo?”
“Unaamini vipi kama mimi ndio niliye kileta wakati tumechukua vitu vingi kwa wale abiria ndani ya meli, iweje wewe uhisi mimi nimekileta na kama ningekuwa ninajua kwamba ndani ya meli kuna raisi basi tungekuwa tumepata mtu wa thamani kubwa kuliko vitu tulivyo vichukua. Kitu kingine kumbuka si kila mtu wako anakupenda lazima kutakuwa na msaliti, laiti na mimi ningekuwa ni msaliti basi nisinge shikiliwa na wala nisinge kuwepo kwenye hili jengo pamoja nanyi”
Maneno yangu yakamfanya Hawa kunitazama machoni mwangu kwa kunichunguza, uzuri ni kwamba ninaweza kuingiza kila hali ambayo ni ya uongo na kuifanya kuwa ya ukweli kwenye maisha yangu.
 
“Dany am sorry mume wangu”
Taratibu nikamkumbatia Hawa huku sote tukimwagikwa na machozi mengi kwenye nyuso zetu. Taratibu Hawa akanibusu mdomoni mwangu, tukajikuta tukinyonyana midomo yetu taratibu sana.
“Dany maisha yetu yote kwa sasa yataishia gerezani, samahani kwa kukuangusha katika harakati za kulipiza kisasi”
“Usiseme hivyo mke wangu, naamini kwamba tuna nafasi ya kuweza kutoka”
“Kivipi Dany, tazama ulinzi ulivyo mkali, hawa watu wana roho mbaya, hapa nilipo wamesha nichoma sindano zaidi tatu za maaumivu ili mradi niweze kuzungumza ukweli”
“Usijali mke wangu nitahakikisha kwamba tunatoka hapa”
“Dany ninakuomba usiyatoe maisha yako kwa ajili yangu, una sa…..”
 
Nikamuwekea Hawa kidole changu mdomoni, kumnyamazisha asizidi kuzungumza sana.
“Kama wewe ulivyo poteza kila kitu kwa ajili yangu, basi na mimi nitapoteza maisha kwa ajili yako sawa”
Hawa akanijibu kwa kutingisha kichwa kwa kunikubalia huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. Taratibu tukakumbatiana tena na kuachiana, nikanyanyuka na kuanza kutembe kuelekea mlangoni.
“Dany?”   
“Ndio”
Niliitika huku nikigeuka na kumtazama Hawa usoni mwake.
“Vyovyote itakavyo kuwa hakikisha kwamba huzungumzi chochote kwao”
“Nimekuelewa mke wangu”
“Kuwa muangalifu”
“Asante”
Nikagonga mpango ukafunguliwa, nikatoka katika chumba chihi, nikafunguliwa pingu pamoja na minyororo iliyo fungwa miguuni mwangu, moja kwa moja nikaelekea katika chumba cha kubadilishina nguo, nikavaa nguo zangu kisha nikamfwata mkuu wa F.B.I.
“Ninahitaji kuzungumza na raisi”
“Twende huku”
 
Nikaingia naye kwenye moja ya ofisi ya vioo. Nikaka kwenye moja ya kiti ambacho mbele yake kuna Tv kubwa. Baada ya sekunde kadhaa nikamuona raisi kwenye Tv hii.
“Muheshimiwa raisi”   
“Ndio Dany”
“Nimemzungumza na Hawa, ila nimeshindwa kumuuliza maswali ambayo nyinyi mulihitaji kutafahamu”
“Kwa nini?”
“Hawa alisha anza kunihisi kwamba mimi ni msaliti kati yao. Ili kujiaminisha kwamba mimi si……”
“Samahani Dany kwa kukukatisha, ila si ulivaa nguo za kifungwa?”
“Ndio muheshimiwa raisi, ila nguo za kifungwa hazikuwa kielelezo kikubwa cha kumfanya Hawa kuweza kunielewa, ninacho kuomba muheshimiwa raisi, inabidi hapa tufanye mchazo ambao utawafunga akili wao”
 
“Mchezo gani Dany, kwa maana wenzako ni magaidi”
“Ndio muheshimiwa raisi, ila ni rahisi sana kumtumia gaidi kumpata gaidi na ni ngumu sana kumtumia mpelelezi kumpata gaidi huwa inahitajika akili ya ziada”
“Ni mchezo gani huo unahitaji mimi niufanye?”
“Ninaomba kwamba tuweze kupatiwa ndege ambayo itatupeleka moja kwa moja hadi Afrika hususani katika nchi ambayo muheshimiwa raisi utahitaji mimi niweze kuianza oparesheni yangu. Tukifika hapo mimi nitajua ni kitu gani cha kufanya kuhakikisha kwamba oparesheni yetu inakwenda vizuri. Cha pili muheshimiwa raisi, ningeomba waandaliwe watu watakao ingiza kujihusisha katika shambulizi la kutuokoa, mimi na wezangu tukiwa tunahamishwa, watu hao ndio watakao tupeleka hadi kwenye ndege itakayo tupeleka Afrika”
 
Nikamuona raisi Donald Bush akifumba macho yake kwa maana jambo nililo lizungumza, ni gumu sana kwenye maamuzi ya raisi kama raisi.
“Muheshimiwa raisi samahani kama nina yaingilia mazungumzo yenu”
Mkuu wa F.B.I alizungumza na kunifanya nimtazame.
“Zungumza Malki”
“Hii oparesheni anayo izungumza bwana Dany, ninaona ni oparesheni ya kijinga ama kipuuzi, itanipotezea watu wangu na pia itatia dosari kitengo changu, ikiwa ina fahamika magaidi walio waua maelfu ya Wamarekani kwenye meli leo hii wapo mikononi F.B.I na leo waambiwe kama wametoroka, hapo kusema kweli muheshimiwa raisi sikubaliani na mawazo ya Dany”
 
“Muheshimiwa raisi, hii ndio nafasi ya pekee kuhakikisha kwamba unaweza kututumia sisi na kuitekeleza kazi yako, kuliko kupelka mamia ya wanajeshi Somalia  wengi wao wanapoteza maisha bila sababu ya msingi. Tafadhali muheshimiwa raisi ninakuomba ulifikiria hili pia”
Ukimya wa raisi ukatufanya mimi na mkuu huyu wa F.B.I mbaye muonekano wake tu, hanipendi hata kuniona sehemu hii.
“Mushimiwa raisi na ukumbuke kwamba sera ya nchi yetu ya Marekani, ni kwamba hatufanyi makubaliano na magaidi na kazi yetu kubwa ni kuhakikisha kwamba tunawaangusha magaidi chini”
 
“Muheshimiwa raisi, kumbuka kwamba nimeyaokoa maisha yako na nilijitahidi kuhakikisha kwamba ninajijeruhi mwenyewe kuyaokoa maisha yako, na laiti kama ningekuwa nina roho mbaya basi hata wewe ningekuua. Muheshimiwa raisi hii ndio nafasi ya pekee kutuaachia sisi Waafrika kujikomboa wenyewe”
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga kwa mbali. Muheshimiwa raisi akakohoa kidogo kisha akatutazama.
“Malki hakikisha unafanya kile ambacho Dany anakihitaji”
“Muheshimiwa raisi….”
“Maamuzi yangu Malki hayapingwi, mimi ndio raisi wa nchi hii ya Marekani fanya kile nilicho kuagiza. Sawa?”
Raisi alizungumza kwa ukali na kumfanya mkuu wa F.B.I kuwa mpole.
 
“Sawa muheshimiwa raisi”   
“Dany nimekuamini na ninakuomba uweze kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba opareheni inakwenda vizuri”
“Sawa muheshimiwa raisi na asante kwa maamuzi yako, sinto kuangusha katika hili na kila gaidi uliye nipa kazi yake nitahakikisha unaishuhudia maiti yake”
“Sawa safari njema”
Mkuu wa F.B. akazima Tv hii huku usoni mwake akionekana kujawa na hasira kali, nikanyanyuka kwenye kiti nilicho kaa na kumsogelea bwana Malki hadi karibu kabisa ya uso wake.
“Utafanya kile nitakacho kuambia ufanye na sinto hitaji kupingwa kwa chochote”
 
Nilizungumza huku nikiwa nimemkazia macho bwana Malik, na yeye akanikazia macho tena kwa msisitizo mkubwa sana.
“Usiombe mtu wangu hata mmoja akapotea ni lazima risasi yangu iingie kwenye kichwa chako, haiwezekani muafrika akanizidi akili”
“Tambua Muafrika ana akili kuliko Mmarekani, tulicho zidiana ni majengo tu basi”
“Ok, sihitaji mabishano na wewe, zungumza unahitaji nini?”
“Mahitaji yangu umeyasikia nilipo zungumza na muheshimiwa riasi, cha kufanya wewe, hakikisha kila kitu ninacho kuhitaji kinakamilika. Muda wa kusafirisha wafungwa ni saa mbili usiku na tukio litokee saa mbili na dakika thelathini usiku. Nimemaliza, fanya hivyo sawa”
“Sawa”
Bwana Malk akatoka kwenye ofisi hii kwa hasira kali sana na kuniacha mimi peke yangu, nikiwa ninatazama tazama wafanyakazi wengine wanao pita pita nje ya hii ofisi. Nikakaa ndani ya hii ofisi huku nikiwa ninafikiria hii kazi itakavyo kwenda, katika masiha yangu hii ndio nafasi yangu ya mwisho kutumia akili kubwa sana kuwaangusaha maadui zangu, huku nikiwa nina msaada wa muheshimiwa raisi wa Marekani bwana Donald Bush.
‘Mungu nisaidie’   
Nilizungumza huku nikimtazama Bwana Malki akija katika ofisi hii akiwa ameongozana na jamaa mmoja mwenye ndevu nyingi usoni mwake.  Wakaingia ndani ya hii ofisi ikabidi kunyanyuka na kusalimana na jamaa huyu.
 
“Asalam alaykum”
Mtu huyu alinisalimia huku akinipatia mkono wa kulia, nikaupokea taratibu huku nikiwa nimejawa na tabasamu pana usoni mwake.
“Walyakum mslam”
“Dewil huyu anaitwa Dany na Dany huyu anaitwa Dewil, ni mkuu wa kitengo cha mawasiliano hapa F.B.I kwa upandw wa Pakistani”
“Ninashukuru kukufahamu bwana Dewil”
“Hata mimi ninashukuru kukufahamu bwana Dany. Nimesikia mpango wako nilio elezewa na mkuu hapa, tayari nimesha andaa vijana wa hiyo kazi na watajipanga pale muda utakapo jitokeza”
“Nashukuru kwa hilo bwana Dewil, vijana wako watakuwa ni wa aina gani?”
“Watakuwa ni Wapakistani, na watakupeleka moja kwa moja hadi kwenye ndege na humo utakuta kila kitu cha kazi yako kuelekea nchini Afrika”
 
“Nashukuru bwana Dewil”
“Unaweza kwenda bwana Dewil”
“Sawa mkuu”
Bwana Dewil akatoka, na kuniacha na bwana Malki.
“Ole wako opareheni hii ifeli au iwe ni njia moja wapo ya wewe kuwatorosha wezako. Nitahakikisha kwamba ninakusaka popote duniani, na nikikukamata nitakuua kwa mkono wangu, kama nyinyi mulivyo muua mke wangu kwenye mlipuko wa hiyo meli”
“Mbaya haito feli na ikufulu…….Mungu mwenyewe ndio atakaye fahamu nini nitakacho kufanya”
Tukatazama na bwana Malki kwa hasira sana, mlango wa hii ofisi ukafunguliwa na akaingia mwanaume msichana mmoja mrefu na mwenye asili ya kiafrika.
 
“Mkuu kuna simu yako kutoka ikulu unaweza kuipokea katika simu yako hiyo hapo mezani”
Bwana Malki akapiga hatua hadi mezani akaichukua simu hii na kuminya batani moja kisha akaiweka sikio la upande wa kushoto.
“Ndio”
“Nimekuelewa mkuu”
“Asante”
Bwana Malki akakata simu hiyo huku akinitazama usoni mwangu.
“Nifwate”
Bwana Malki alizungumza huku akinitazama kwa jazba. Tukatoka katika hii ofisi moja kwa moja tukaelekea hadi kwenye ukumbi ulio jaa viti. Taa za ukumbi huu zikazimwa, na projecta inayo piga mwanga wake ukutani ikawashwa, nikaanza kuona taratibu za oparesheni yangu nitakavyo kwenda barani Afrika ninavyo takiwa kuifanya.
 
“Tutaanzia nchini Somali, kisha Nigeria na kumalizia Tanza”
Mwanaume tuliye mkuta humu ndani alizungumza huku akinionyesha ramani za nchi hizi tatu alizo zitaja.
“Somalia, kundi la Al-Shabab ni kubwa sana, na lina watu wengi sana ambao sio rahisi sana kuweza kuwafahamu kiurahisi. Unacho takiwa kukifanya Dany na watu wako ni kujiweka katika mazingira ya kawaida.”
Mtu huyu akaendelea kunipa maelezo kwa nchi ya Nigeri na Tanza, tulipo maliza majadiliano haya ya nini ninacho takiwa kukifanya katika nchi hizi tatu, tukatoka katika chumba hichi.
“Ninahitaji kitu”
Nilimuambia bwana Malki na kumfanya asimame na kunitazama usoni mwangu.
 
“Nini?”
“Ninahitaji watu wangu wapatiwe chakula kwa maana wana njaa”
“Sawa, kuna kingine”
“Hakuna”
Bwana Malki akanirudisha kwenye ofisini niliyo kuwa. Masaa yakazidi kwenda, huku mara kwa mara nikiwa na kazi ya kuitazama saa yangu ya mkononi. Ilipo timu majira ya saa mbili kasoro robo nipelekwa katika chumba, nikabadilisha nguo zangu na kuvaa nguo za garezani, nikafungwa pingu pamoja nyororo miguuni mwangu, nikavaa raba nyeusi na nikaanza kupelekwa katika chumba amacho nikawakuta Hawa, Mariam, mume wa Mariam, Lusi pamoja na wasichana wengine wawili ambao nao ni walinzi wa Hawa.
Hawa akataka kunyanyuka ili anikumbatie ila akazuiwa na askari wa kike na kumfanya akae hapo hapo alipo kaa. Mariam akanitazama kwa macho makali, sikuzungumza kitu cha aina yoyote na nikajifanya kwamba nimenuna sana.
“Nyanyukeni”
Tuliamrishwa na sote tukanyanyuka, wakaingia wanaume kumi walio jazia miili yao, majaketi yao ya kuzuia risasi yameandikwa kwa maandishi meupe FBI. Wakatushika kwenye mikono yetu maeneo ya makwapa, wakatutoa katika chumba hichi. Tukaingizwa kwenye moja ya gari jeusi aina ya Van. Gari hili ikafungwa kwa nyuma, baada ya sekunde kadhaa. Tukaanza kusikia ving’ora vya magari haya ya wana FBI.
 
“Dany”
Hawa aliniita kwa upole.
“Mmmm”
“Upo salama?”
“Ndio, mke wangu. Jamani tunatakiwa kufanya jambo”
Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikitazama mbele ya gari hili. Tumetendanishwa na nondo ngumu kati yetu sisi na dereva. Kitu ambacho kusema kweli sio rahisi kwa sisi kuweza kumsumbua wala kumgusa dereva.
“Dany hatuna la kufanya na wewe”
Mariam alizungumza kwa sauti iliyo jaa hasira.
“Unazungumza nini Mariam”
“Hakuna mtu ambaye anaweza kushirikiana na wewe, unanuka usaliti”
 
“Hawa waeleze mimi ni msaliti kweli”
Hawa akakaa kimya huku kichwa chake akiwa amekiinamisha chini. Gafla tukastukia gari letu likinyanyuliwa juu, kisha likaangukia kiupande na kutufanya sote kujibamiza bamiza, gari likaanza kuserereka barabarani na kutufanya sote humu ndani kila mmoja kuomba sala yake. Gari likasimama, tukaanza kusikia mirindino ya milio ya risasi, kimoyo moyo nikaanza kujawa na furaha kwa maana mpango wetu unakwenda kama tulivyo pangwa. Mlango wa nyuma ya gari letu ukafunguliwa, wanaume wawili walio funika nyuso zao na kuacha macho yao tu huku mikononi mwao wakiwa na bunduki, wakaanza kuwatoa wezangu mmoja baada ya mwingine ndani ya gari hili na mimi nikawa wa mwisho kutolewa. 

Cha kusangaza Hawa na wezake wote wao wamesimama ila mimi ndio nimelazwa chini huku mitutu ya bundiki ya wanaume hawa wakiwa wamenielekezea mimi.
“Halooo Dany”
Sikuamini macho yangu nilipo muona baba Hawa akisimama pembeni yangu, huku mkononi mwake akiwa ameshika bastola tayari kwa kuniua.

==>>ITAENDELEA KESHO

Alberto Msando: Amber Rutty Anaweza Kufungwa Miaka 30 Jela Kama Itathibitika Amefanya Mapenzi Kinyume na Maumbile

$
0
0
Mwanasheria Alberto Msando ametumia ukurasa wake wa instagram kutoa ufanunuzi kuhusiana na adhabu itakayomkabili mtu endapo atafanya mapenzi kinyume na maumbile na kusema kuwa adhabu yake ni miaka isiopungua 30 jela au kifungo cha maisha.

==>>Hiki ni kipengele cha katiba ya Tanzania kilichowekwa na mwanasheria huyo. 

Mkurugenzi wa Pride mikononi mwa TAKUKURU

$
0
0
Taasisi  ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) imetoa ripoti ya matukio  ambayo ni mkakati wa kitaifa dhidi ya rushwa na mpango wa utekelezaji wa awamu ya tatu  unaoratibiwa na kitengo cha uratibu wa utawala bora ofisi ya Rais Ikulu katika kupiga vita vitendo vya rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Brigedia Jenerali John Mbungo amesema kuwa aliyekuwa mkurugenzi  mtendaji wa taasisi ya PRIDE  inayojihusisha na utoaji wa mikopo kwa wananchi hasa akina mama ili kuwainua kiuchumi Rashid Gergar Malima (60) anatafutwa kwa tuhuma za kughushi nyaraka na ubadhilifu wa fedha za umma.

Amesema kuwa taasisi hiyo iliundwa kwa lengo la kusaidia wananchi wenye kipato kidogo na ilipata mtaji wake wa kwanza wenye thamani ya dola za kimarekani 4,000  kutoka Norway  kupitia NORAD.

Mbungo ameeleza kuwa katika vipindi mbalimbali kati ya mwaka 2015/2017 Malima na wenzake walifanya ubadhilifu wa fedha za kampuni ya PRIDE za kiasi cha shilingi Bilioni moja na milioni nane  na kuandaa malipo hewa kwa watoa huduma mbalimbali yakiwemo Arusha Art, Antelop Safaries, Essence international na paperwork na pia waliandaa malipo ya salary advance ambayo hayakufuata taratibu na baadaye fedha hizo zote walizichukua na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi.

Aidha amesema kuwa mtuhumiwa huyo anadaiwa kutoroka nchini punde tu uchunguzi wa tuhuma hizo ulipoanzishwa mwaka 2018 na taarifa zilizopo ni kwamba alitoroka kupitia eneo la Namanga, na inasemekana kuwa yupo nchini Marekani hivyo amewaomba watanzania nchini na wale wanaoishi Marekani kutoa taarifa za mtuhumiwa huyo ili sheria ifuate mkondo wake.

Watuhumiwa  wengine katika uchunguzi huo wapo na walishahojiwa  na ametoa rai kwa mashirika mengine kuhakikisha kuwa fedha zinazotolewa kwa lengo la maendeleo ya watanzania zinatumika kwa kadri ilivyokusudiwa.

Katika tukio jingine aliyekuwa Afisa Mikopo wa chuo kikuu cha Dar es salaam Ndaki ya Elimu (DUCE) Josephat Museti Machiwa (35) anatafutwa kwa tuhuma za kughushi nyaraka,  wizi na ubadhilifu wa fedha za umma kinyume na sheria.

Imeelezwa kuwa mnamo tarehe 12 Februari 2015 Josephat Machiwa akishirikiana na Mhasibu Lameck Makoye wakiwa watumishi wa Chuo kikuu kishiriki cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es salaam (DUCE) waliandaa hundi  ya malipo yenye thamani kubwa ya fedha  ambazo zilitokana na fedha za mikopo ya wanafunzi kutoka bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) na kuzilipa fedha hizo kwenye akaunti za watu wasiokuwa walengwa na baada ya kufanikisha hilo watuhumiwa hao walizichukua fedha hizo kutoka kwa watu hao kwa njia mbalimbali za udanganyifu.

Aidha katika tukio jingine mamlaka hiyo imefanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa zoezi la ukusanyaji kodi kupitia mfumo wa kieletroniki (matumizi ya EFD  mashine) katika soko la kariakoo na kubaini ukwepaji kodi  unaofanywa na baadhi wa wafanyabiashara   jambo linalopelekea kukosesha mapato kwa serikali.

Akifafanua tuhuma hiyo Mbungo amesema kuwa wafanyabiashara hao hukwepa kodi kwa kuuza bidhaa bila kutoa risiti na kutoa risiti yenye malipo pungufu ikilinganishwa na thamani halisi. Na hadi sasa wafanyabiashara wengi wakubwa na wadogo wamekamatwa kwa tuhuma hizo.

Mbungo amewataka wafanyabiashara hao kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.

BREAKING: Sakata la Korosho Lachukua Sura Mpya....Rais Magufuli Aingilia Kati, Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito

$
0
0
RAIS Dkt. John Magufuli ameitaka Wizara ya Kilimo ijitathmini kutokana na suala la mauzo ya zao la korosho linavyoendelea pamoja na utendaji wa Bodi ya Korosho Tanzania.

Pia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo kumrudisha wizarani Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Prof. Wakuru Magigi baada ya kutoridhishwa na utendaji wake.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Oktoba 26, 2018) katika kikao chake na wakuu wa mkoa ya inayolima korosho kilichofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

“Haturidhishwi na utendaji wa bodi ambao amekiuka maelekezo ya msingi ya Serikali katika kusimamia mfumo mzima wa zao la korosho uliopelekea kuvurugika kwa minada.”

Kutokana na hali hiyo Waziri Mkuu amesema Serikali imesitisha minada yote ya korosho nchini kuanzia leo na kuwataka wakulima wawe watulivu wakati ikishughulikia suala hilo.

Kiongozi huyo wa Bodi ya Korosho analalamikiwa kwa kufanya kazi bila ya kushirikisha ushirika wa zao hilo na kutotambua mamlaka zilizowekwa kisheria kama mkuu wa mkoa.

Mbali na malalamiko hayo pia anadaiwa kuendesha operesheni kwa kutumia silaha na askari  dhidi ya viongozi wa ushirika kinyume cha taratibu za nchi.

Hivyo, Waziri Mkuu amemuagiza Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Lindi na wa  Mtwara wahakikishe gari lenye namba T 814 DDM pamoja na dereva wake linatafutwa popote.

Waziri Mkuu amesema gari hilo ndilo linalodaiwa kutumika katika kuwakamata viongozi wa ushirika waliokuwa wanawasimamia wananchi waliokataa kuuza korosho kwa bei ndogo.

Amesema baada ya dereva wa gari hilo kukamatwa ahojiwe na aeleze askari hao alikuwa anawatoa wapi na nani aliyemtuma. Ameagiza askari wote waliohusika watafutwe.

“Bodi imekuwa ikiwatisha na kuwalazimisha wakulima na viongozi wa ushirika kukubali kuuza korosho kwa bei ya chini jambo ambalo Serikali haiwezi kulikubali.”

Waziri Mkuu amesema Serikali haiwezi kulifumbia macho suala hilo kwa sababu limekuwa likiipaka matope kwani mkurugenzi huyo alikuwa anaingiza askari katika mikoa hiyo bila ya mamlaka kuwa na taarifa.

Kadhalika Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Kilimo kutokaa kimya pindi zinapotokea changamoto kama hizo na badala yake watoe taarifa mapema. “Mambo kama haya yanatokea alafu wizara mmekaa kimya tu.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Magufuli anawapongeza wakulima wa korosho kwa uamuzi wao wa kukataa kuuza kwa bei ndogo na kwamba yuko pamoja nao.

“Rais Dkt. Magufuli ameitaka Wizara ya Kilimo ijitathmini katika suala la mauzo ya zao la korosho linavyoendelea,” amesema Waziri Mkuu.

Pia Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Magufuli anataarifa kwamba kuna baadhi ya watendaji Serikalini wanatumia vibaya jina lake kwamba lazima wahusika wote watachukuliwa hatua.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bw. Gelasius Byakanwa na Mkuu wa mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi walilalamikia kitendo cha Prof. Magigi kuvuruga mfumo wa uuzaji wa korosho.

Pia walisema licha ya kumshauri kiongozi huyo juu ya namna bora ya kuendesha minada ya uuzaji wa korosho hakuwasikiliza na kwamba hakuwa tayari kushirikiana nao na pia alikuwa akidharau mamlaka zao.

Pia alikuwa akiingiza askari na kuwatisha na kukamata viongozi wa ushirika bila ya wao kujua jambo ambalo walisema limezua taharuki kwa watendaji wa ushirika.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, OKTOBA 26, 2018.

Rais Magufuli Kateua Wenyeviti 9 wa Bodi za Serikali

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti 9 watakaoongoza bodi za taasisi za Serikali baada ya wenyeviti waliokuwepo kumaliza muda wao.
  1.  Rais Magufuli amemteua Prof. Joyce L.D Kinabo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (Tanzania Food and Nutrition Centre -TFNC). Prof. Joyce Kinabo ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Idara ya Sayansi na Teknolojia ya Chakula.
  2. Rais Magufuli amemteua Prof. Costa Mahalu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU).
  3.  Rais Magufuli amemteua Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Sauda Mjasiri kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (Public Procurement Appeals Authority – PPAA).
  4.  Rais Magufuli amemteua Mhandisi Leonard Kapongo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (Public Procurement Regulatory Authority – PPRA).
  5.  Rais Magufuli amemteua Prof. Elifas Tozo Bisanda kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO).
  6.  Rais Magufuli amemteua Dkt. Selemani B. Majige kuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania.
  7.  Rais Magufuli amemteua Julius Ndyamukaka kuwa Mwenyekiti wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA).
  8.  Rais Magufuli amemteua Mej. Jen. Mstaafu Hamis R. Semfuko kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Wanyamapori (TAWA).
  9.  Rais Magufuli amemteua Prof. Romanus Cleophace Ishengoma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF).
Uteuzi wa wenyeviti hawa umeanza leo tarehe 26 Oktoba, 2018.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya October 27

Kutana na Shekhe Yassin....Mtabiri wa Nyota, Pete za Bahati, Mimba Kutoshika au Mimba Kuharibika

$
0
0
Whatsap 0743313580....KUTANA NA SHEKHE YASSINI SAIDI
Ni Shekhe aliyejaaliwa karma nyingi kutoka kwa Allah Mwenye uwezo kutatua shida mbali mbali ziwapatazo wanadamu.


Anatibu na kuponya shida mbalimbali zilizo shindikana kwa wanadamu  na kwauwezo wa Allah atakutatulia shida zako inshaalah

Shekhe yassini Saidi anatibu kutumia qur an na rukaiyah pamoja na dawa za kiarabu na za kiafrika


Je? Una Mpenzi,mchumba,mume,mke, aliye kuacha na anaishi na MTU mwingine au anakuahidi ahadi alafu hatekelezi ahadi zake 


SHEKHE YASSINI SAIDI atakusaidia
 @shekhesaidiyasini anatumia picha, au jina la muhusika na kumaliza tatizo lako.

SHEKHE YASSINI SAIDI Anatafsiri ndoto kushinda bahati nasibu, nyota,mvuto wa mwili, Miliki Pete Yabahati Kutoka Falme Kuu bila Masharti Yoyote.

Pia kwa wenye tatizo la uzazi kutoshika mimba au ukishika mimba inaharibika tatizo la nguvu za kiume
Muone @shekhesaidiyasini inshaalla kwa uwezo wake Allah atakusaidia. 


Malipo Nikama Sadaka Na Utalipa Baada Ya Mafanikio.
Wasiliana nami
@shekhesaidiyasini
Whatsapp no +255 743 313 580
Piga no +255 743 313 580
Tigo +255 653 67 1650
Airtel 0683697810

Mwanafunzi Anusurika Kifo Baada ya Choo cha Shule Kutitia.......Tazama Picha

$
0
0
Mwanafunzi  wa darasa kwanza katika Shule ya Msingi Seliani, wilayani Arumeru mkoani Arusha, Emanuel Zakaria (7), amenusurika kufa baada ya kutumbukia ndani ya choo cha 
shimo.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’azi, alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo jana wakati mwanafunzi huyo alipokwenda 
kujisaidia wakati wa mapumziko.

“Tunaangalia chanzo cha kuvunjika kwa shimo hilo ni nini na
ukizingatia sasa hivi ni kipindi cha mvua kubwa zinazoendelea 
kunyesha, tutaangalia pia kama ujenzi haukuwa madhubuti au ni
kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha bado tunafanya uchunguzi wa
tukio hilo,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, alisema tukio hilo lilitokea
 majira ya saa 3: 45 asubuhi muda mfupi kabla ya muda wa mapumziko.


Alisema mwanafunzi huyo, mkazi wa Kijiji cha Olevolosi, baada ya kuopolewa, alipelekwa kwenda kupata matibabu katika Hospitali ya Selian na kwamba hali yake 
inaendelea vizuri.

Muro alisema lilitokana na kutitia kwa ardhi 
kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali ya mkoani
 Arusha.


Mkuu huyo wa wilaya aliwapongeza wananchi wa eneo hilo kwa utayari na kutoa kwa moyohali ambayo ilisaidia kunusuru maisha ya mwanafunzi huyo.


“Niwapongeze wananchi kwa utayari wa moyo wenu wa kujitolea, serikali 
inataka watu wenye moyo wa kujitolea kama walivyofanya leo (jana)
 kuokoa maisha ya mwanafunzi huyu,” alisema.

Hata hivyo, alisema Serikali ipo tayari kuungana na wananchi katika
ujenzi wa choo cha kisasa hadi kitakapokamilika.


“Nimeshatoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha, waanze mchakato wa ujenzi wa choo kipya, Jumatatu, nitakuwa
 shuleni hapo kushirikiana nao ili kuhakikisha ujenzi huo
 unakamilika kwa wakati,” alisema.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Olevolosi, Samweli Mollel, alisema baada ya
kutokea kwa tukio hilo, waliwaita wanafunzi wote madarasani ili
 kuwafanyia uhakiki kwa majina kuangalia watoto kama wapo wote.

Mwalimu Mkuu Atuhumiwa Kuwapapasa Wanafunzi Sehemu za Siri

$
0
0
Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwibara, Bunda mkoani Mara, Betha Sayi, ameingia matatani baada ya kudaiwa kuwadhalilisha wanafunzi wa kike wa shule hiyo.

Sayi anatuhumiwa kuwavua nguo zote wanafunzi hao, zikiwamo za ndani na kuwashika shika katika sehemu za siri kwa madai kuwa anawapima kama wana ujauzito

Tuhuma hizo zilitolewa jana na wanafunzi hao, hali ambayo ilisababisha taharuki kwa wazazi ambao walisema hawawezi kuvumilia kitendo hicho cha udhalilishaji, ukatili wa kijinsia na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Ilidaiwa kuwa, mwalimu huyo alifika shuleni hapo juzi asubuhi na kuwaita wanafunzi hao kila mmoja katika ofisi yake na kuanza kuwavua nguo zote na kisha kuwafanyia kitendo hicho cha udhalilishaji.

Aidha, imeelezwa kuwa, baada ya kuwavua nguo zote na kuwafanyia udhalilishaji huo, alichukua nguo zao za ndani za wanafunzi hao na kuziweka ndani ya boksi.

Hali hiyo iliwafanya baadhi ya wanafunzi hao kukimbilia nyumbani kwao na kutoa taarifa kwa wazazi wao, ambao walitahamaki na kwenda shuleni hapo na kisha wakatoa taarifa katika kituo kidogo cha polisi Kibara.

Akizungumzia sakata hilo, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mwibara, Sylivanus Manyapara, ambaye pia ni Kaimu Mratibu Elimu Kata, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kwamba mwalimu huyo alipelekwa katika kituo cha polisi Kibara, akiwa na nguo za ndani za wanafunzi hao zilizokuwa kwenye boksi.

Mnyapala alisema tayari tukio hilo limeripotiwa katika kituo kidogo cha polisi Kibara na mwalimu huyo alishikiliwa kwa muda kisha akapewa dhamana na nguo hizo ziko kituoni hapo kama kielelezo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kibara B, Mafwili Mnyanga, alisema kitendo hicho kimelaaniwa na wazazi na wananchi wa kijiji hicho.
 
"Kitendo hiki ni kibaya sana na kinaweza hata kusababisha vurugu kwani watoto kufanyiwa hivyo ni unyama. Wamefanyiwa ukatili mkubwa na pia huo ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kwa hiyo sisi wazazi pia tumeathirika kwa kitendo hicho," alisema kwa njia ya simu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images