Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Ahukumiwa Miaka 60 Jela Kwa Kumbaka na Kumpa Mimba Mwanafunzi

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro imemhukumu kifungo cha miaka 60 jela Abrahamu Kaaya (23) mkazi  wa kijiji cha Karansi wilayani Siha kwa makosa mawili ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Karansi.

Hukumu hiyo imetolewa leo Jumatatu Oktoba 22, 2018 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Jasmine Abdul baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi watano.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Simoni Feo amedai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa  alitenda kosa hilo Oktoba 11, 2017 katika kijiji hicho.

TFF Imemthibitisha, Ammy Ninje Kuwa Mkurugenzi Wa Ufundi

$
0
0
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemtangaza kocha wa zamani wa Serengeti Boys, Ammy Ninje kuwa Mkurugenzi wa ufundi wa Shirikisho hilo akichukua nafasi ya Salum Madadi.

Madadi aliondolewa katika nafasi hiyo mapema mwaka huu na kukaimiwa na Oscar Milambo ambaye baada ya uamuzi huu atarudi katika majukumu yake ya ukocha.

Ofisa habari wa TFF, Mario Ndimbo alisema kikao cha kamati tendaji ya TFF kilichokutana Jumamosi ya Oktoba 20 kilipitisha uamuzi wa kumteua Ninje.

"Ninje ndio atakuwa Mkurugenzi wa Ufundi kwa sasa na anatakiwa kuanza kazi mara moja kwani TFF inatambua anaishi Uingereza, lakini kuanzia sasa atarudi hapa nchini katika kituo chake cha kazi, " alisema.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 15

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
“Hata kama, ila nahitaji wale vijana nao niwafanye kitu kibaya”
“Kweli?”
“Ndio”
“Twende”
“Wapi?”
“Si sehemu walipo ukawafanyie kitu kibaya”
“Si unaona kabisa nina jeraha”
“Huniamini au?”
Nikamtazama Ethan kwa muda kidogo, kisha nikachomoa sindano inayo ingiza maji kwenye mishipa yangu. Nikashuka kitandani, Ethan akanikumbatia kwa kasi ya ajabu tukatoka katika eneo hili la hapo hospitalini na kuanza safari ya kwend aeneo walipo vijana ambao walinipiga na kunichoma kisu changu katika mbavu zangu.

ENDELEA
 Kwa uwezo wa Ethan, ndani ya muda mchache tukafika katika moja ya jumba bovubovu ambalo kidogo lipo nje ya mji.
 
“Hapa ndipo wanapo ishi?”
“Ndio”
Ethan alizungumza huku tukisimama nje ya mlango wa kuingilia. Taratibu Ethan akaanza kugonga mlango huu.
“Sasa kwa nini tunagonga”
“Unahisi tukiingia kwa staili tulio ijia unahisi watakutambuaje, kesho si watasema wewe ni jini, ikiwa jini ni mimi”
“Mmmh”
“Yaa, tena ninaingia ndani ya mwili wako”
Ethan akapotea kwenye uwepo wa macho yangu. Mwili mzima ukanisisimka na kujihisi ni mtu mwenye nguvu sana. Mlango ukafunguliwa, akasimama kijana ambaye kwa haraka niliweza kumtambua kwani yeye ndio aliye anza kunisemesha siku walipo nivamia.
 
“Hei wewe mtu mweusi umekuja kufanya nini hapa?”
Jamaa alizungumza kwa dharua. Nikamsukumia ndani, nikashangaa kumuona jamaa akipaishwa kimo cha mbuzi na akatua kwenye moja ya meza na kuiangukia hadi ikavunjika vunjika jambo ambalo liliwastua wezake wengine.
“Ni useng** gani huuu”   
Mwenzao mmoja alizungumza huku wakiacha kucheza game ya mpira kwenye tv iliyopo hapo sebleni na kunifwata. Woga na wasiwasi kama nilio kuwa nao kwa siku ya kwanza wote umeniondoka, maumivu kwenye jeraha langu sikuweza kuyahisi kabisa mwilini mwangu. Kuna kijana humu ndani akaokota kitu chake kuhakikisha kwamba ana nivamia.
 
Wakaanza kunishambulia ila kila walivyo jaribu niliweza kuwadhibiti kisawa sawa na kila niliye mpiga ngumi aliambulia ngumi au teke lililo wapelekea kuvunjika katika sehemu hiyo ambayo nitampiga. Ndani ya muda mfupi vijana wote nane nikafanikiwa kuwadhibiti na kila mmoja ana ugulia maumivu huku wengine wamepoteza fahamu.
“Unatakiwa kuwaua ili siri yako isitoke”
Niliisikia vizuri sauti ya Ethan  masikioni mwangu.
“Ethan kuua ni dhambi”
“Watakuua wewe siku, waue wote”
Ethan alizungumza kwa ukali, nikawatazama vijana hawa jinsi wanavyo pata shida ya maumivu. Roho ya kuwaua ikaanza kunijaa. Huruma ya kibinadamu ikafutika kabisa, nikaanza kuwavunja shingo mmoja baada ya mwengine. Zoezi la kuwaua halikumaliza dakika hata tano.
“Kazi nzuri”
 
Ethan alizungumza huku akitoka mwilini mwangu.
“Ngoja nifute ushahidi wote”
Ethan alizungumza huku akizikusanya maiti hizi na kuziweka eneo moja. Akanyoosha mkono wake wa kushoto, nikastuka sana mara baada ya kuona ukitoa moto mwingi ulio sababisha maiti za vijana hawa kuanza kuwaka. Tukatoka nje na Ethan kwa uwezo wake wa kijini akaendelea kuichoma nyumba hii na kuwaka moto mkubwa sana. Kama tulivyo kuja hapa ndivyo tulivyo rudi hospitalini na hakuna nesi aliye weza kugundua.  
 
‘Ninaondoka ila hakikisha kwamba siri ya mauaji humuambii mtu wa aina yoyote hata Camila mwenyewe sawa’
“Sawa”
Ethan akaondoka katika eneo hili. Kupitia tv iliyomo humu ndani kwangu, nikaona taarifa juu ya kuungua kwa jumba moja lililopo nje ya mji huku ikisadikika kuna watu wemeungulia ndani ya nyumba hiyo. Taarifa hii kidogo ikanipa wasiwasi kwa maana watendaji wa tukio hilo ni mimi na Ethan.
 
    Asubuhi taratibu zikaendelea kama kawaida, madaktari wakanitembelea na kunichoma sindano za kukausha kidonda. Baada ya wiki moja nikaruhusiwa kutoka hospitalini hapa nikiwa na afya yangu nzuri kabisa. Nikakaa siku chache nyumbani kisha nikarudi shule kuendelea na masomo yangu ya darasa la pili. Kurudi kwangu shule imekuwa ni furaha kwa waalimu na wanafunzi wezangu. Maasomo yakazidi kusonga mbele huku ushiriki wangu kwenye michezo ukizidi kuinyanyua shule kwenye mashindano mbali mbali ndani na nje ya nchi ya Ujerumani. Ufauliji wangu katika masomo nao ukazidi kunifanya niwe kipenzi cha wanafunzi wengi sana, huku Camila kadri ya siku zinavyozidi kwenda ndivyo jinsi tulivyo jikuta tukizama kwenye penzi letu.
                                                                                                                 ***   
    Nikiwa na umri wa miaka kumi na mbili nikamaliza elimu ya msingi na nikachaguliwa kwenda shule ya vipaji maalumu huku Camila akichaguliwa kwenda katika shule nyingine ya jinsia moja ya kike ila ni karibu sana na shule yetu hii ya kiume. Nikiwa kidato cha pili, nikaletewa maombi mengine ya kujiunga na timu nne kubwa za mpira ambazo ni Liverpool, Real Madrid, Bacelona na Beyurn Munich.
“Ethan unaitwa”
 
Mwenzangu mmoja aliniita nikiwa bwenini nikipitia pitia baadhi ya mikataba niliyo tumiwa kwa njia ya barua pepe na mameneja wa timu hizo kwani kipaji changu cha mpira kimekuwa kikubwa kwa hali ya juu.
“Na nani?”
“Mkuu wa shule”
Nikarudisha mikataba hii ndani ya kabati langu, nikalifunga kisha nikaanza kuongozana na kijana huyu kuelekea kwa mkuu wa shule. Nikaingia ofisini kwake na kumkuta akiwa peke yake. Nikamsalimia na akaniomba niweze kukaa kwenye kiti kilichopo pembeni ya meza yake.
“Samahani kwa kukutoa kwenye mapumziko yako”
“Hakuna tabu mwalimu”
“Kuna taarifa imekuja hapa sio njema kidogo kwako na wala kwetu”
 
Nikajiweka vizuri kwenye kiti huku nikimtazama mwalimu mkuu usoni mwake.
“Nimepokea simu kutoka nyumbani kwenu na dada yako ndio alinipigia”
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi huku nikimtazama mkuu wa shule.
“Unatakiwa kwenda nyumbani sasa hivi kwa maana hali ya mzee wako haipo vizuri sana. Tumekuandalia helicopter ya shule na itakuepeleka hadi nyumbani kwenu”
Nikashikwa na kigugumizi na nikashindwa hata kujua ni kitu gani ninaweza kukizungumza, kwani mzee Klopp ni zaidi ya baba kwangu, kwa maana amekuwa ni mpiganaji na ni mtu ambaye amenifunza mambo mengi sana hususani kwenye maisha ya mpira. Nikiwa katika hali ya bumbuwazi,  akaingia sekretari wa shule.
 
“Mkuu helicopter ipo tayari kwa kuondoka”
“Sawa, nenda na Ethan hakikisha kwamba humuachi peke yake hadi pale atakapo fika nyumbani kwao”
“Sawa mkuu”
Tukatoka ofisini humu na moja kwa moja tukaelekea katika kiwanja cha helicopter. Tukaingia ndani ya helicopter hii na taratibu tukaanza safari ya kuelekea nyumbani huku akili yangu ikijaribu kutengeneza picha ya hali ya nyumbani nitakavyo ikuta. Akili yangu moja inaniambia kwamba mzee Klopp amefariki huku akili yangu nyingine inaniambia kwamba mzee Klopp yupo hai.
 
‘Ethan upo wapi rafiki yangu’
Nilimuita Ethan kimoyo moyo pasipo hata sekretari wa shule kuweza kusikia kitu chochote. Ndani ya dakika kumi na tano tukafika katika jumba la mzee Klopp ambapo napo kuna uwanja wa helicopter, nikafunguliwa mlango na mmoja wa walinzi wa jumba hili la mzee Klopp, nikashuka na nikaanza kukimbia kuelekea ndani ya jumba hili.
Ukimya nilio ukuta sebleni ukanistua sana, kwa haraka nikapandisha ngazi kuelekea gorofani, nikakutana na madaktra wawili kwenye kordo wakizungumza na dada Mery. 
“Ethan”
Dada Mery aliniita huku kwa haraka akinifwata na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa sauti ya chini sana
“Baba yupo wapi?”
“Yupo chumbani”
 
Sikutaka hata kuulizia hali yake ipo vipi kwa haraka nikaingia ndani ya chumba cha mzee Klopp, nikamkuta akiwa amewekewa mashine za kupumulia huku pembeni yake akiwa amekaa bibi Jane Klopp. Bibi Jane Klopp taratibu akanyanyuka huku akinitazama usoni mwangu. Macho yake yamebadilika rangi na kuwa mekundu sana, anaonekana ni mtu ambaye alikuwa akilia kwa muda mrefu sana. Bibi Jane Klopp akanikumbatia kwa muda huku akilia. Mzee Klopp akanitazama kwa muda huku akihema kwa shida sana, kwa ishara ya mkono wake wa kulia akaniita. Nikamuachia bibi Jane Klopp na kumfwata mzee Klopp kitandani alipo lala.
“Eth…a….”
 
Mzee Klopp aliniita kwa shida sana, machozi yakaanza kunimwagika usoni mwangu.
“Ndio baba”
“M…ua…an..ngalie mama yak….o na dada yako”
“Mimi…..ni….nakufaa, ila hakikisha kwamba unatimiza ndoto zako sawa mwanangu?”
“Sawa baba”
“Makampuni yote yapo chini yako, wewe ndio mmiliki na nilisha weka kila kitu kwa mwana sheria hakikisha kwamba unayaongoza katika msingi na msimamo mzuri. Hakikisha kwamba huyumbishwi na umri wa mtu yoyote sawa”
Mzee Klopp alizunugmza kwa kujikaza sana
“Sawa baba”
 
Mzee Klopp akanitazama kwa muda kidogo, kisha akaniomba niweze kumkumbatia. Taratibu nikamuinamia na kumkumbatia. Kwa ishara mzee Klopp akamuita mke wake naye akamuomba amkumbatie, nikatoka nje na kumuita dada Mery akaingia chumbani humu tukawakuta bibi Jane Klopp na mume wake wakiwa wamekumbatiana huku wote wakiwa wanalia kwa uchungu sana. Dada Mery naye akajumuika mama yake katika kumkumbatia baba yake.
Mlio wa mashine ya kumsaidia kupumua, ikaanza kutoa mlio mithili ya alarm. Jambo lililo tufanya tushtuke sana na kuogopa kwa haraka wakaingia madaktari na wakamuomba bibi Jane Klopp na mwanaye wamuachie mzee huyo. Madaktari kwa kutumia mashine maalumu wakaanza kumstua kifuani mzee Klopp. Mashine hizo hazikuweza kufanya kazi kwani bado kijimstari cha rangi nyekundu kinaonekana kwenye mashine hiyo.
 
Madaktari wakajitahidi kulifanya zoezi hilo ndani ya dakika tano, kisha wakatugeukia huku wakiwa na sura za masikitiko sana. Daktari mmoja akatingisha kichwa akiashiria kwamba mzee Klopp hatupo naye tena duniani. Nikamshuhudia bibi Jane Klopp akianguka chini na kupoteza fahamu. Dada Mery akajitahidi kwa uwezo wake kuhakikisha kwamba hapati mstuko, ila bumbuwazi lililo mpata hakika limemfanya abaki amekaa pembeni ya mwili wa marehemu pasipo kufanya jambo lolote. 
 
Kwa kusaidiana na madaktari hawa wawili tukasaidiana kumnyanyua bibi Jane Klopp na kumlaza kwenye moja ya sofa na akaanza kumpatia huduma ya kwanza. Hali ambayo inayo endelea ndani humu hakika imenifanya nami niwe nimekaa njia panda, hakika sijui nianzie wapi, kwani kila linalo endelea ninahisi ni kama muujiza ambao natamani siku zirudi nyuma ila ninashindwa.
“Ethan”
Daktari mmoja aliniita kwa ishara tukatoka nje ya chumba hichi.
“Mzee ameondoka duniani, wewe kama mwanaume hivi sasa tunakutegemea kuweza kutoa kauli ya familia kama mwanaume. Dada yako ndio kama vile unavyo muona alivyo. Mama naye ndio kama vile, tunakusikiliza”
Maneno ya daktari huyu yakanifanya nimkodolee tu macho na kushindwa hata kumjibu jambo la aina yoyote.
“Ethan”
“Naam”
“Umenielewa kitu ninacho hitaji kukizungumza”
“Ndio nimekuelewa”
“Jiandae katika hilo na tunahitaji mwili wa mzee kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kabla haujaanza kuharibika”
 
“Ngoja kwanza kwani mzee alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa gani?”
“Saratani ya damu ndio ilikuwa inamsumbua”
“Kwa nini sikuweza kuambiwa hadi leo amefariki ndio ninaambiwa hili jambo?”
“Mzee mwenyewe alihitaji usiambiwe”
“Kwa nini?”
 
“Kwanza ni kutokana na umri wako, pili ni kutokana na masomo.”
Nikafumba macho yangu taratibu kisha nikayafumbua.
“Hakikisheni kwamba habari ya kufa kwa baba haivuji hadi pale nitakapo wambia sawa”
“Sawa Ethan”
Nikarudi ndani ya chumba hichi na kumshika mkono dada Mery na kutoka naye ndani humu. Tukaingia chumbani kwangu, Mery akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kulia kwa uchungu sana, nikaanza jukumu la kubembeleza taratibu.
 
“Ethan kweli baba amekufa”
“Yaa amekufa, ila nakuomba ujikaze sasa”
“Eheee”
“Nahitaji ujikaze nitazame nitazame”
Nilizungumza huku nikimshika dada Mery mashavuni mwake. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa.
“Sisi ndio tulio baki sasa, tujikaze na tushirikiane katika hili, ukiniacha mimi mwenyewe katika hili nitashindwa sawa dada yangu”
“Ehee”
“Sasa sikia kitu kimoja, nahitaji niweze kupata kitabu cha orodha ya mameneja wote wa kampuni za mzee na wale wanasheria wake wawili. Si unafahamu kitabu kilipo?”
“Ndio”
 
“Twende ukanipatie”
Tukatoka katika chumba changu na kuelekea katika ofisi ya mzee Klopp. Dada Mery akafungua moja ya kabati, tukaona shelf ya chumba akaingiza namba za siri ambazo niliweza kuziona. Akafungua mlango na akatoa kitabu hicho chenye majina na namba za simu za watu wote ambao ni wasimamizi wa makampuni ya mzee Klopp ambayo ni zaidi ya kumi na mbili. Nikaanza kazi ya kumpigia kila mmoja na kumuomba aweze kufika katika nyumba ya mzee Klopp haraka iwezekanavyo kwani kuna kikao cha dharura. Ndani ya lisaa moja mameneja kumi na mbili pamoja na wanasheria wawili wakafika nyumbani humu, huku kila mmoja akishangazwa na wito wangu, kwani haukuwa ni wito wa kubembeleza zaidi ya kuwa wito wa kuamrisha.
 
“Kijana mdogo inakuwaje unatuita kwa kutuamrisha?”
Mzee mmojaa alizungumza kwa kufoka huku wakiwa wamekaa sebleni hapa.
“Mzee kabla sijamaliza kuzungumza nilicho waitia kuanzia hivi sasa huna kazi”
Maneno yangu yakawafanya watu wote kustuka sana, hata dada Mery mwenyewe akaonekana kustushwa kwani maamuzi yangu hakuna hata mmoja aliye yataarajia kwamba nitayatoa hivyo.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 116 na 117 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA     
 “Yudia, mbona una hatari sana?”   
“Kwa nini?”
“Yudia analindwa sana kuliko hata Hawa, na Yudia kwa sasa ana cheo kikubwa kuliko Hawa”
“Kisa ni nini cha Hawa kushushwa cheo ikiwa yeye ni mtoto wa mkuu”
“Kisa cha yeye kushushwa cheo na kupokonywa madaraka yote ni wewe Dany”
Nikabaki nikiwa nimekodolea macho mwalimu kwa maana nina kipindi kirefu sana tangu mimi kuondoka katika hii kambi na sijafahamu ni kitu gani Hawa amekifanya na kinacho nihusu mimi hadi kupokonywa madaraka yake na kukabidhiwa Yudia.
   
ENDELEA   
“Kisa mimi?”   
“Yaa, Hawa tangu ulivyo pata mateso na kufikia hatua ya baba yake kukuuza kwa watu ambao hawajulikani, ilimsikitisha sana Hawa. Akawa hafwati sheri inayo wekwa na baba yake, akawa ni msichana wa pombe. Ilifika hadi hatua baba yake akaamua kumuweka mahabusu”
“Nini?”
“Yaa huo ndio ukweli, hawa yule ambaye tulikua hatuifahamu sura yake, sasa hivi tunaiona kama kawaida”
Hapa ndipo nikaanza kupata picha kwenye video ambayo K2 alitumiwa na magaidi, nilimuona Hawa na baba yake, japo sikutilia maanani ni kwa nini aliruhusu sura yake kuonekana katika mkanda huo wa vidoe.
 
“Sasa hawa kwa sasa yupo wapi?”
“Yupo kwenye chumba chake, katika ile nyumba ndogo”
“Kwa hiyo ametolewa kwenye lile jumba kubwa”
“Yaa, yaani nikikuambia amepokonywa kila kitu ujue hana chochote, mipango yote kwa sasa anaiendesha huyo Yudia, hapa watu hatukaliki, kama ninasikia amefanya mashambulizi juzi Tanzania, na hadi hapo hakuna hata shambulizi moja lililo fanikiwa”
“Ticha unaweza kunisaidia jambo moja”
“Jambo gani Dany”
“Ninahitaji kwenda kumuona Hawa usiku huu”
Mwalimu akaka kimya kwa muda huku akitafakari ombi langu ambalo mimempatia
“Sawa twende, ila funga hicho kitambaa chako usoni”
“Sawa”
 
Nikafunga kitambaa changu na kubakisha sehemu ya macho yangu. Tukaanza kutembea kwa kasi kuelekea katika nyumba ndogo inayo sadikika kwamba ndipo alipo Hawa. Walinzi hawakuweza kunistukia kwa maana nipo kwanza na mwalimu wa hii kambi pili ninafahamu nyendo na mienendo ambayo Wasomali wengi huwa wanatembeaa, kwa hiyo hata tembea yangu ilinilazimu kuibadilisha kwa muda ili nisijulikane. Tukakutana na walinzi wawili wa kike nje la mlango wa nyumba hii
“Ninawaomba nionane na mkuu”
Mwalimu alizungumza huku akiwatazama walinzi hawa kwenye nyuso zao.
“Mkuu kwa sasa amelala”   
“Ninawaomba mumuamshe, muelezeni kwamba ni dharura. Tafadhali”
Walinzi hawa wakatazamana, kisha mmoja akamkonyeza mwenzake, akafungua mlango na kuingia ndani. Baada ya dakika moja akarudi.
 
“Amekuomba uingie”
“Nisubiri hapa”
Mwalimu alizungumza, nikatingisha kichwa, akaingia ndani na kuniacha na walinzi hawa huku nikitazama tazama mazingira ya eneo hili ambalo ninalifahamu vizuri sana na hakuna kitu chochote ambacho kimeweza kubadilika.
“Unaitwa ndani”
Mlimzi mwengine wa kike aliye toka ndani, alizungumza na mimi kwa lugha ya kiarabu ambayo ninaifahamu vizuri. Nikaingia ndani nikiwa na bunduki yangu, Hawa aliye kaa kwenye sofa baada ya kuniona kwa haraka akanyanyuka na kunikimbilia kwa harakana na kunikumbatia kwa nguvu.
“Ohoo asante Mungu, Dany upo salama”
 
“Hata mimi pia ninamshukuru Mungu kukuona upo salama”
Nikavua kitambaa changu huku tukiachiana na Hawa, akawatazama walinzi wake wengine wawili walipo humu ndani pamoja na mwalimu. Kisha akanishika mkono na tukaingia kwenye chumba chake cha kulala. Kitu cha kwanza tu baada ya Hawa kuufunga mlango, akanikumbatia kwa nguvu huku akiangua kilio  kikubwa sana japo ni cha chini chini, ila inaashiria kabisa kwamba analia kwa uchungu pamoja na maumivu ya muda mrefu yaliyo kuwa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu.
 
“Shiiii usilie Hawa”   
“Dany hujui ni mateso ya kiasi gani ambayo nimepitia kwenye maisha yangu tangu kuondoka kwako katika hii kambi”
“Hawa sikuondoka kwa kupenda”   
“Yaa ninafahamu hilo Dany, samahani kwa kushindwa kukusaidia kipindi ulivyo pata matatizo”
“Yamaesha pita hayo”
Hawa akaniachia na kunitazama mwili wangu, machozi yakendelea kumwagika usoni mwake, ikabidi nimkumbatie tena na kukirudisha kichwa chake kifuani mwangu.
“Usilie Hawa nipo karibu nawe sasa”   
“Kweli Dany?”
“Yaaa, nimekuja kwa kazi moja tu”
“Kazi gani?”
“Nahitaji kumuua Yudia”
“Kwa nini?”
Swali la Hawa likanifanya nikae kimya huku nikimtazama usoni mwake kwa maana ninazielewa vizuri hisia za Hawa juu yangu na nikimumbia kwamba nilikuwa nina mke ninaweza kumjengea hali ambayo sihitaji kumjengea kwa muda huu. Pia Yudia amehusika katika mauaji ya Linda msichana aliye nisaidia kutoka katika hospitali niliyo kuwa nimepelekwa na John .
 
“Dany”   
“Yaaa”
“Yudia amekufanyia nini?”
“Yudia amefanya mambo mengi sana kwenye maisha yangu, nilimfahamu Yudia hata kabla hajakuja kwenye hii kambi. Yudia alikuwa mfanyakazi wa ndani nyumbani kwetu miaka mitatu nyuma”
“Mfanyakazi wa ndani?”
“Yaa alikuwa ni mfanyakazi wa ndan, ila pale nyumbani alikuja kwa kazi maalumu na baada ya muda niligundu ya kwamba ametoka katika kundi hili”
“Sijawahi kuisikia stori ya Yudia kuwa mfanyakazi wa ndani, ila hilo lisiniumize kichwa sana, kabla ya kufanya lililo kuleta ninakuomba unisaidie kitu Dany wangu”
“Kitu gani?”
 
“Ninahitaji kurudi kwenye madaraka yangu, ila sina mtu wa kunipa njia za mimi kuweza kurudi katika madaraka yangu niliyo pokonywa na Yudia”
“Kwani wewe na Yudia muna mahusiano gani kati yenu?”
“Ni ndugu, ila kwa sasa baba ametokea kumthamini sana Yudia kama vile ni mtoto wake wa kumzaa wakati ni baba mdogo kwa baba mkubwa”
“Hawa kama utahitaji msaada wangu, basi hakuna njia nyingine ya kufanya zaidi ya kuua?”
Hawa akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu akiwa kama haamini kwa kile ambacho nimekizungumza.
“Hawa baba yako, Yudia hao wote kwangu ni maadui, pasipo kufanya mauaji hakuna kitu ambacho kinaweza kukurudisha wewe kwenye nguvu. Utaendelea kuwa chini na utaendelea kuwatumikia wao na watakuweka kwenye kifungo hichi cha ndani hadi mwisho wa maisha yako”
“Dany ninaogopa”
 
“Katika hili hakuna kuogopa, baba yako kama angekuwa anakupenda na kuheshimu mawazo yako, kwanza asinge fanya ukatili kama huu ambao amenifanyia, ilifikia hadi hatua akataka kukata uume wangu, so alihitaji kunihanisi?”
Nilizungumza kwa hasira ila kwa sauti ya chini huku nikimtazama Hawa usoni mwake. Hawa machozi yakaendelea kumwagika kwa maana kila kitu ninacho kizungumza ndicho kilicho jitokeza kwenye maisha yangu.
“Hawa wewe unahitaji nguvu, kwa nini tusitumie umoja wetu kuchukua madaraka kwenye hili kundi. Sihitaji kuwa muongo wala mnafki kwako, nikimua baba yako na Yudia, roho yangu itatulia”
 
“Noo Dany baba yangu hana la hatia katika mikono yako?”
“Unahitaji msaada wangu au auhitaji msaada wangu?”
Nilizungumza kwa sauti nzito huku nikimtazama Hawa usoni mwake, taratibu akakaa kwenye kitanda chake huku machozi yakimwagika, nikamsogelea na kusimama mbele yake, taratibu nikachuchumaa na kukinyanyua kichwa chake alicho inamisha uso wake chini.
“Hawa natambua ni jinsi gani unavyo mpenda baba yako, ila unatakiwa kuhakikisha kwamba tunafanya liwezekanalo kuhakikisha kwamba baba yako na Yudia wanaondoka kwenye uso huu wa dunia”
 
Hawa akaendelea kukaa kimya huku akimwagikwa na machozi, nikaupitisha mkono wangu wa kushoto na kuishika shingo yake kwa nyuma, taratibu nikamsogeza karibu na uso wangu, tukatazamana kwa sekunde kadhaa. Uvumilivu ukatushinda na kutufanya tuanze kunyonyana midomo yetu kwa kasi sana huku kila mmoja akiwa anatoa mihemo mizito ya mahaba. Galf tukasikia king’ora cha tahadhari kilichotufanya mimi na Hawa kuachia, na soto tukasimama. Hawa akakimbilia dirishani kwake na kuchungulia nje.
“Kuna nini kinacho endelea?”
“Nahisi kuna uvamizi”
Moja kwa moja nikatambua atakuwa David pamoja na kundi la Zero wamekuja kunisaidia katika mpango wa kuvamia ngome hii.
 
“Mkuu tumevamiwa tunatakiwa kukutoa katika nyumba hii”
Mlinzi wa Hawa aliingia chumba pasipo kubisha hodi na kuzungumza maneno hayo huku akiwa amesimama kikakamavu akimtazama Hawa usoni mwake na wala hakuwa na muda wa kuzungumza na mimi wala kunitazama.
“Siwezi kuondoka humu ndani”
“Mkuu geti kuu tumevamiwa na kundi la Zero, wanaendelea kupambana na wanajeshi wetu, kukaa hapa itakuwa ni hatari kwa maisha yako”
“Bite nielewe basi, nimekuambia sihitaji kuondoka hapa, hakikisheni kwamba ulinzi nje unakuwa mzuri, na waambie kikosi changu chote kwamba wajiweke mbali na hiyo vita na wanatakiwa kuja kuzunguka nyumba sawa”
“Sawa mkuu”
Mlinzi wa Hawa akatoka na kutuacha tukiwa tunasikilizia milio ya risasi jinsi inavyo rindika huko nje.
“Kwa nini hutaki kutoka humu ndani?”   
“Nipo na wewe naamini kwamba kila jambo linakwenda vizuri”
 
“Hawa nisikilize u…..”
“Dany sihitaji kwenda mbali na wewe, pia si yupo Yudia na baba, wataongoza jeshi na watahakikisha kwamba wanawazuia hao watu wa Zero kwa maana ni kundi dogo sana”
Nikamtazama Hawa usoni mwake, nikasikilizia nje jinsi milio ya risasi inavyo zidi kuendelea kusikika. Nikataka kumbuambia Hawa kwamba watu wa Zero wamekuja kunisaidia mimi ila nikashindwa kuzungumza hivyo kwa maana hadi sasa hivi sijajua akili yake inafikiria nini kwenye mpango ambao upo kati yetu kwa maana swala la kumuangamiza baba yake limekuwa gumu sana kwa upande wake. 
“Dany”
“Mmmmm”
“Ninakupenda sana, niliamua kwenda kinyume na baba yangu kwa kukutafuta wewe kwa kupindi kirefu kwa ajili ya upendo wangu kwako. Natambua ya kwamba baba yangu ni mkosaji mkubwa sana kwenye maisha yako ila ninakuomba uweze kumsamehe”
Kabla sijazungumza kitu chochote mlango ukafunguliwa, akaingia mlinzi wa Hawa aliye toka muda machache ulio pita.
“Mkuu nina habari nzuri”
“Habari gani?”
“Watu wa Zero wameweza kudhibitiwa, huku Ziro na Stive wamekamatwa”
“Stive, Stive gani?”
“Yule aliyekuwa mshauri wa Yudia na injinia wa mabomu ya nyuklia”
 
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kusikia kwamba Stive amekamatwa.
“Imekuwaje amekuwa msaliti?”
“Bado sijagundua mkuu, labda nifanye uchunguzi”
“Sawa hakikisha kwamba unaniletea habari zote utakazo zifahamu”
“Samahani kwa kuwaingilia”
Mlinzi wa Hawa akanitazama usoni mwangu.
“Unaweza kuniletea taarifa ya wapi atakapo hifadhiwa?”
Mlinzi wa Hawa akamtazama mkuu wake, Hawa akatingisha kichwa kumruhusu kuleta taarifa hiyo ya sehemu ambayo Stive atafungikiwa kisha mlinzi huyu akatoka.
“Walinzi wako una waamini?”
“Yaa hadi kufa kwangu ninawaamini, na wote sidhani kama kuna msaliti kwa maana wamekunywa damu yangu na wameapa kunipigania na kunitunzia siri zangu za ndani hadi dakika ya mwisho ya pumzi zao”
“Wamekunywa damu yako?”
“Ni kiapo ambacho niliwafanyia tangu nikiwa binti mdogo na wengi wao unao waona hapa nimekua nao tangu nilipo kuwa nao watoto”
 
“Sawa”
“Ila huyu Stive sijui ni kwa nini ameamua kumsaliti Yudia na baba kwa maana kinacho kwenda kufwata hapo ni yeye kuuwawa kikatili sana”
“Una muda gani tangu umfahamu Stive”
“Ni mwaka wa nne sasa, kipindi unakuha hapa yeye alikuwa na kazi za nje, na alikwenda kuongoze ujuzi huko Pakistani”
“Ujuzi wa nini?”
“Ujuzi wa kuunda silaha pamoja na mabomu makubwa yakiwemo ya nyuklia”
“Ahaa”
“Ila kwa nini unamuulizia ulizia huyo Stive una mfahamu?”
Nikaka kimya kwa dakika kadhaa huku nikiwa nimetazama chini, taratibu nikakinyanyua kichwa changu na kumtazama Hawa mwenye shauku ya kuhitaji kufahamu jibu la swali lake.
“Yaa nina mfahamu. Stive ni kaka yangu kwa damu moja”
Hawa akashangaa huku macho yakimtoka, ninaamini kwamba hakutarajia kuweza kusikia kwamba mimi na Stive ni mtu na ndugu yake.

AISIIIII……….U KILL ME 117  

“Hahaa, Dany acha kunitania”       
“Niamini mimi, Stive ni kaka yangu”
“Ila mbona hamfanani kabisa”
 
“Undugu sio kufanana ila ni kufaana”
“Hapana Dany kwa hili siwezi kukuami kwa asilimia mia moja”
“Ila kuna ushahidi ambao  yeye anao, unao dhibitisha kwamba mimi na yeye ni mtu na ndugu yake”
“Ushaidi wa kitu gani?”
“Ni video ya marehemu baba yangu”
“Marehemu baba yako!!?”
“Yaaa amenieleza kwamba baba yangu alimuachia video hiyo”
Hawa akaka kimya huku akionekana kutafakari kitu fulani, akapiga hatua hadi kwenye meza iliyomo humu chumbani, akawasha computure iliyopo juu ya meza.
“Unafanyaje?”   
“Huwa kila histori ya mtu kwenye hili ngome huwa inaandikwa na kuhifadhiwa, kwaa ajili ya kutuwezesha kumuamini mtu na kumchukua kiurahisi”
“Unataka kuniambia kwamba nilicho kizungumza kuhusiana na Stive huwezi kukiamini?”
“Yaa asilimia mia moja”
“Mmmm”
 
Hawa akaanza kuminya batani za keyboard ya hii computure, akatafuta jina la Stive, haikuchukua muda sana likaonekena. Taratibu nikayakaza macho yangu kwenye kioo cha computure hii na kunza kusoma historia ya Stive na anaonekena na picha yake pembeni.
“Anaitwa Stivine Kundasemi, uraia wake ni Rwand, amezaliwa mwaka 1983”
Hawa alizungumza huku akinitazama usoni mwangu, sikumjibu kitu chochote zaidi ya kuendelea kusoma historia ya Stive. Stive amezaliwa katika familia ya watoto wanne huku yeye akiwa nimtoto wa tatu, kaka zake walisha uwawa kwenye vita vya Rwanda mwaka 1994”
“Sasa hapo Dany ninashindwa kuelewa unapo niambia kwamba Stive ni kaka yako”
“Una picha zake za nyuma?”
“Ndio hizi hapa”
Hawa akaminya batani kadhaa, akanionyesha picha za Stive tangu alipo kuwa mdogo hadi kufikia ukubwa, kipindi anajiunga na kundi hili la Al-Shabab. Pia nikaona picha za wazazi wa Stive ambao wanafana naye sana uzuri ni kwamba sura zao hazifanani sana na Warwanda.
 
“Tena Stive kabila lake ni Muhutu, na wewe ni Mtanzania halisi, sasa hapa undugu unatokea wapi?”
“Imekuwaje baba yangu ameweza kukiri kwamba Stive ni kaka yangu?”
“Dany kuna mbinu nyingi za mtu kuweza kukiri kwamba nyinyi ni ndugu, na njia ambayo ninaona ilitumika hapo ni kwamba baba yako aliwekewa shinikizo nyuma ya kamera, huwezi jua labda alishikiwa bunduki, au akafanyiwa hila yoyote ya kukufanya kwamba wewe kuweza kumuamini”
Maneno ya Hawa yakazidi kuniingia akilini mwangu na kujikuta nikijilaumu kwa nini ninakuwa na kichwa chepesi ambacho kinanifanya kumuamini kila mtu kirahisi.
“Sijui ni kwa nini Stive alinisaidia”
“Alikusaidia wapi?”
“Nilipo kuwa nimekamatwa na Yudia mapangoni, Stive ndio mtu aliye nitorosha kwa njia za panya hadi tukatokea nchini Kenya”
“Stive ni mpelelezi mzuri sana, alifanya hivyo ninaamini kutakuwa na mbinu ambayo ipo nyumba ya msaada wake, labda bado anafanya kazi chini ya Yudia, na ili kuweza kukupambaza akaona amtumie Stive ili kukupata wewe kirahisi”
“Ninaweza kuipata histori ya baba yangu?”
“Ninaweza kuitafuta kwenye mitandao mingine”
Nikamtajia Hawa jila la baba yangu na kunza kulitafuta.
“Jina la baba yako sio ngeni sana masikioni mwangu”
“Uliwahi kulisikia wapi?”
“Kuna siku nilisikia baba akilizungumza akiwa na K2 kabla hajawa raisi”
 
“Ulisikia wakizungumzia kuhusiana na nini?”
“Kusema kweli sikuweza kufwatilia sana kwa maana mimi na K2 picha haziendi kabisa. Yap nimeipata”
Hawa alizungumza huku akinionyesha histori ya baba yangu, sote tukajikuta tukiwa kimya baada ya kuona picha za mauji ya kutisha ya baba yangu. Japo ninatambua kwamba baba yangu amefariki ila kusema kweli sikuweza kujua amefariki kwa kitu gani. Picha hizi zinaonyesha baba yangu alikufa kwa mateso makubwa sana huko nchini Japan. Baba alimwagikwa tindikali mwilini mwake, kisha akachomwa moto. Sura ya baba ikaanza kunijia kichwani mwangu, nikaanza kukumbuka ucheshi wake na ukarimu alio nionyesha kwangu. Machozi yakaanza kunitiririka taratibu usoni mwangu. Mlango ukafunguliwa kwa haraka nikajikuta nikijifuta machozi na kumtazama mtu aliye ingia humu ndani.
“Mkuu kuna upepelezi unao fanyika kwa kila nyumba humu ndani ya kambi”
“Upelelezi wa nini?”
“Wanamtafuta Dany”
Tukatazama na Hawa sote tukionekana kushangaa.
“Nani aliye sema kwamba Dany yumo humu ndani?”
“Ni Stive, amepewa ruhusa ya kufanya hivyo na Yudia”
“Stive si ulisema amekamatwa na kupelekwa kwenye chumba cha mateso?”
“Stive sio msaliti, amefanya hivyo kwa kutumwa”
“Dany unaona, nilikuambia. Sasa hakikisha kwamba hakuna mpelelezi anaye ingia nyumbani kwangu”
“Sawa mkuu”
Binti huyu akatoka na kunifanya nikae kitandani taratibu huku nikiwa na mawazo mengi kichwani mwangu.
“Walisha kuingiza kwenye mtego Dany, na wakikushika nina uhakika watakua kikatili sana”
Hasira dhidi ya Stive ikaanza kunipanda, nikatamani hata kutoka nje na kwenda kumkamua kwa kadri nitakavyo weza ila nikajikuta nikishindwa kabisa kutokana hata nguvu za mwili wangu zimenipungua tangu niweze kuiona picha ya baba akiwa ameuwawa kikatili.
“Dany, Dany”
“Mmmm”
 
“Nitahitaji nikufiche kwenye chumba changu cha ardhini”
“Kuna chumba cha ardhini?”
“Yaa”
Hawa akatembea hadi kwenye kabati lake la nguo, akafungua milango miwaili ya kabati hili kisha akasogeza nguo, nikaona mlango mwengine ulipo nyuma ya kabati hili lililo jengewa ukutani. Sote tukaingia, na kushuka chini ya ardhi, akawasha taa.
“Kuna kitanda, Tv, bafu na choo vipo hapa. Utakaa huku chini na nitakuwa ninakupa habari kwa kila kitu ambacho kitakuwa kinaendelea huko nje”
“Sawa”
Hawa akanisogelea na kunibusu mdomoni mwangu, kisha akapandisha ngazi kwa haraka, akafunga mlango wa kuingilia ndani ya hichi chumba na kuniacha nikitazama mazingira ya hichi chumba. Nikajilaza kitandani huku nikiwa nimetawaliwa na mawazo na kujiuliza imekuwaje hadi Stive aamue kunidanganya kwamba mimi ni ndugu yake, na hata kama walimshinikiza baba yangu kuweza kukiri kwamba Stive ni kaka yangu, inaonekana kuna mtandao mkubwa sana ambao uliuiangamiza famili yangu, na mtandao huo unasimamiwa na watu wengi wenye nguvu ya kipesa hadi majeshi.
 
“Pesa yangu ingekuwepo, ningeweza kufanikisha kila hambo”
Nilizungumza huku nikiitazama Tv kubwa iliyomo humu ndani ya hichi chumba.
“Siwezi kuliacha jasho la Cajoli limwagike kirahisi namna hii, lazima pesa iweze kurudi”
Nikajilaza kitandani, wala sikuweza kupata usingizi kabisa, masaa yakazidi kwenda kasi. Sikuweza kufahamu ni saa ngapi kutokana sina saa yoyote. Mlango ukafunguliwa kwa haraka nikanyanyuka kitandani huku nikiwa nimeishika bunduki yangu. Nikamuona Hawa akishuka kwenye ngazi huku mkononi mwake akiwa ameshika sahani pamoja na chupa ya chai, ikanibidi kuishusha bunduki yangu chini.
“Habari yako Dany”   
“Salama”
Hawa akaviweka vitu alivyo vishika mezani kisha akanikumbatia, mikono yangu nikipitisha kiunoni mwake, taratibu tukaikutanisha midomo yetu na kunza kunyonyana. Hisia za mapenzi zikazidi kutawala miili yetu, taratibu tukajikuta tukianza kuvuana nguo moja baada ya nyingine. Tukabakiwa na nguo za ndani nikataka kumvua Hawa chupi yake ila akakataa na kuniachia huku akisimama mita chache kutoka sehemu nilipo simama.
 
“Vipi?”   
“Dany siwezi kufanya hivi”
“Kwa nini?”
Nilimuuliza Hawa huku nikimsogelea, akaanza kurudi nyuma na mwisho akajikuta akifika ukutani na mimi nikawa nimesha mkaribia.
“Dany mimi bado ni bikra na nilisha weka kiapo kwa Mungu, nitafanya hivi kwa mwanaume ambaye atanioa tu”
“Hawa umesha kua, hupaswi kuogopa”
Nilizungumza huku nikiushika mkono wa kulia wa Hawa, nikamshikisha jogoo wangu aliyopo ndani ya bokta, akataka kuutoa mkono wake, ila nikamzua na kuendelea kumshikisha jogoo wangu.
“Tazama jinsi ninavyo umia Hawa, mmmmm kwa nini lakini?”
Nilizungumza kwa sauti ya chini sana na yenye msisimko wa mapenzi, Hawa akabaki kimya huku akiwa ananitazama kwa bumbuazi usoni mwake.
“Da….aa”   
“Shii”
Nilizungumza huku nikianza kuzinyonya lipsi zake, Hawa akaanza kulegae tena, nikambeba na kumpeleka kitandani, nikamlaza taratibu na kuendelea kumnyonya midomo yake. Mlio wa simu ukatufanya sote kusitisha zoezi ambalo tunahitaji kulifanya.
 
“Ngoja nipokee simu”
Nikamtazama Hawa usoni mwake kwa sekunde kadhaa kisha nikamuachia, akashuka chini ya kitanda, akatoa simu yake kwenye mfuko wa suruali ambayo alikuwa ameivaa.
“Ni mlinzi wangu”
Hawa alizungumza kabla hajapokeza, nikatingisha kichwa na kumruhusu aweze kupokea simu yake.
“Haloo”
“Baba…..!!?”
“Ninakuja sasa hivi”
Hawa akakata simu na kuanza kuivaa suruali yake.
“Vipi?”   
“Baba anakuja kunitembela huku inabidi niende”
“Sawa”
“Kwani sasa hivi ni saa ngapi?”
“Saa kumi na mbili asubuhi”
Hawa akamaliza kuvaa nguo zake, kwa haraka akapandisha ngazi na kutoka humu chumbani na kufunga kila kitu na nina amini kwamba atakuwa amerudi chumbani kwake. Nikavaa suruali yangu na kuanza kupandisha ngazi kwa utaratibu hadi mlangoni, nikalitega sikio langu kwenye mlango kusikia kitu kinacho endelea. Sikuweza kusikia kitu chochote, nikaa hapa mlangoni kwa dakika kumi, nilipo ona hakuna jambo linalo endelea nikashuka chini, nikafungua chupa ya chai nikamimina chai kiasi kwenye kikombe kilicho kuwa kimefunikia chupa hii ya chai. 
 
‘Kweli nitaweza kupambana na watu hawa wengi nama hii?’
‘Lazima niweze, sitakiwa kuwa mnyonge, waliniulia wazazi wangu, kwa nini na wao niwaache wakiwa hai’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikinywa chai taratibu taratibu. Mlango ukafunguliwa tena, Hawa akashuka kwa haraka na kunifwata kitandani nilipo kaa.
“Kuna lipi jipya?”
“Baba alikuwa ananiuliza kama nimeweza kuona wewe?”
“Kwa nini akuulize wewe?”
“Nahisi kwamba wamenitilia mashaka kwa maana jana sikumruhusu mtu kuingia chumbani kwangu, kwa hiyo nahisi hapo ndipo walipo zidi kupata mashaka kwamba wewe upo chumbani kwangu”
“Umemuona Stive?”
“Yaa ameongozana na baba kuja hapa”
“Nikuombe kitu?”
“Niombe tu kitu”
“Leo ninaomba nianze kufanya kazi yangu kimya kimya kwa maana siwezi kuendelea kukaa humu ndani ikiwa maadui zangu wanazidi kunitafuta kwa ajili ya kuniangamiza”
“Ila Dany bado sijaweka mambo sawa?”
“Hapana wewe niachie tu hiyo kazi, hii ngome ninaijua vizuri sana, so ninakuomba niweze kushuhulikia matatizo yangu yaliyo nileta hapa”
 
“Sawa mimi sina kipingamizi katika hilo. Je kuna vitu vyovyote ambavyo utavihitaji?”
“Ndio, nitahitaji nguo nyeusi tu, sime, bastola mbili, magazine za kutosha”
“Umepata, kitu kingine je?”
“Labda jaketi la kuzuia risasi”
“Poa, nitakoungezee na saa”
“Nitashukuru sana”
“Mbona huli viazi vyangu, ua hupendi kula viazi vitamu?”
“Hapana, ninakula mbona”
Taratibu tukaanza kula viazi hivi pamoja na chai, huku tukisimuliana mambo mengi ya nyuma. Hawa akaniaga na kuondoka, baada ya masaa sita mbele akarudi akiwa na vitu vyote nilivyo muagiza pamoja na ramani inayo onyesha majengo yote ya humu ndani.
“Dany hii kazi ninakuomba uifanye pasipo mtu yoyote kuweza kugundua chochote, kwa njia hii ninaamini kwamba nitaweza kurudi kwenye madaraka yangu”
 
“Sawa sinto kuangusha, ila kama unataka kurudi kwenye madaraka yako ninakusisitizia hawa watu watatu wanatakiwa kuondoka duniani?”
“Nani na nani?”
“Wa ni Stivie, wapili ni Yudia na wa tatu ni…….”
Nikaka kimya huku nikimtazama Hawa usoni mwake, kwa ishara akaniomba nizungumze.
“Wa tatu ni baba yako, nikiimaliza kazi hiyo watu wote ndani ya hii kambi watakusikiliza wewe na kuifwata amri yako na nilazima niweze kuwaua na vibaraka wao kwa maana tukiwaacha hawa vibaraka wanaweza kuja kukudondosha tena madarakani.”
Hawa taratibu akanisogelea hadi karibu na uso wangu, akanitazama kwa macho makavu yaliyo jaa ukakamavu, akavuta pumzi taratibu kisha akaishusha kwa nguvu na kukifanya kifua chake nione jinsi kinavyo shuka.
“Nakuruhusu kumuua baba yangu, ila nitaomba uwe mume wangu hadi kufa kwangu”
Sikutegemea Hawa anaweza kuzungumza maneno kama haya, jambo lililo nifanya nijawe na furaha na taratibu nikampiga busu la mdomo kumuhakikishia kwamba haya matatizo yakiisha nitakuwa mume wake wa maisha yake yote hadi pale kifo kitakapo tutenganisha.

==>>ITAENDELEA KESHO

Rais Magufuli Amjulia Hali Mbunge Wa Makete Profesa Norman Sigala Ambaye Amelazwa Katika Hospitali Ya Muhimbili Dar

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Mbunge wa Makete Profesa Norman Sigala King ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Mbunge wa Makete Profesa Norman Sigala King ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam akizungumza mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kumjulia hali leo tarehe 22/10/2018.

Alichokisema Godbless Lema Baada ya Kuhojiwa na Jeshi la Polisi Kwa Masaa Matatu

$
0
0
Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Isaya Mungure  amesema mbunge wa chama hicho Arusha Mjini, Godbless Lema ameitwa polisi kufafanua kauli zake kuhusu tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo’.

Mungure ambaye alikuwepo katika mahojiano ya awali kati ya Lema na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi amesema mbunge huyo ametakiwa kueleza ni kwa nini alitoa kauli kutaka wapelelezi wa nje ya nchi kuchunguza kutekwa kwa mfanyabiashara huyo.

Kwa upande wake, Lema amesema mara baada ya kufika hapo jeshi hilo lilimuhoji kuhusiana na masuala ya kutekwa kwa mfanyabiashara Mohamed Dewji.

Kwa mujibu wa Godbless Lema ametoa maelezo kwa jeshi hilo ambapo amesema alishauri kuongeza nguvu juu ya namna ya kupambana na matukio ya kiuhalifu.

“Nimeandika kile ambacho nakijua na ni kile nilichokizungumza kwenye press, nimesema sitoacha kulikemea jeshi hilo na kulionya pale nitakapoona panafaa kama Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani. 


"Kuna mashaka ambayo wanayo watu wengi kuhusu yaliyojitokeza kwenye hili suala, huwezi kuondoa mashaka hayo kwa kutisha watu bali kwa kuleta majibu, hivyo wasiyapuuze.

“Nipo tayari popote na kwa yeyote ku-defend kile nilichokisema kuhusu utekaji. Wakisoma wataona hiyo wanayosema kuisaidia polisi na nimewasaidia kwelikweli, hivyo.

“Wasione watu tunazungumza wakadhani kwamba tutatumiwa na mabeberu, hatutumiki Ila tunatafakari miaka 50 inayokuja jeshi la polisi litakuaje”.
amesema Lema.

Akizungumzia kuhusu Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kuzuia wananchi wasifanye mijadala ya tukio la utekani, Lema amesema waziri huyo hawezi kuzuia wananchi kuzungumza.

“Nimemwambia RPC wakinihitaji hakuna haja ya kufanya sinema za zamani za kuruka ukuta na kukata fensi, wanipigie tu nitakwenda mwenyewe kwa nauli yangu wala sitatumia mafuta yao,” alimaliza lema.


RC Makonda Atangaza Ajira Kwa Vijana wenye Taaluma ya IT

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, anawaalika wote wenye utaalam wa Teknolojia ya Habari yaani (Information Technology – IT specialists) kufika ofisini kwake Novemba 1, 2018, asubuhi kwa ajili ya kuunda Mfumo wa Kuratibu Uwajibikaji wa Watendaji wa Umma ili kuhakikisha malalamiko ya wananchi yanashughulikiwa kwa uharaka.

Mfumo huo utakuwa ukipokea malalamiko ya watendaji wasiowajibika kuanzia ngazi ya mitaa, kata, wilaya, mikoa na viongozi wakuu akiwemo mkuu wa mkoa, katibu tawala mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi, makatibu tawala wilaya na wakuu wa idara, ambapo watakuwa wakiona ni mtendaji gani asiyewajibika kutatua kero za wananchi.

Makonda amesema hataki kuona wananchi wanafika kwenye ofisi za umma na kuambiwa “Njoo kesho” kila siku pasipokujua kuwa wanatumia nauli na kupoteza muda.

Mfumo huo utampa mwananchi uwezo wa kueleza malalamiko yake endapo amefika ofisi ya umma na watendaji kushindwa kushughulikia kero zake kwa uzembe.

Mo Dewji: Namshukumu Mungu kwa kuokoa maisha yangu

$
0
0
Mfanyabishara Mo Dewji amerudi mtandaoni kwa mara kwanza toka atekwe na watu wasiojulikana na baadae kuachiwa na watekaji hao akiwa salama.

Bilionea huyo alitekwa alfajiri ya Oktoba 11 na kumuachia huru usiku wa manane wa Oktoba 20 baada ya msako mkali wa jeshi la polisi.

Jumatatu hii Mo ambaye pia ni mwekezaji wa klabu ya Simba, ametweet kwa mara ya kwanza kuwashukuru watanzania ambao walikuwa wanamuombea katika kipindi chote kigumu alichopitia.

“Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yangu. Pamoja na kupitia kipindi kigumu lakini daima amesimama upande wangu. Marafiki zangu, napenda kuwashukuru wote kwa maombi yenu na kunitakia kheri. Mungu awazidishie kwa wema wenu. Baraka za Mungu ziwe nanyi leo na daima,” alitweet Mo jioni ya leo.

IGP Simon Sirro ameapa kuwatia nguvuni wakiwa wapo hai ama wamefariki, watu ambao wamtemka mfanyabishara huyo lakini leo ni siku ya tatu toka wamuachie bado hawajapatikana.

Hawa wa Diamond Akutwa na ugonjwa mwingine, sio Ini kama ilivyoelezwa Hapo Awali

$
0
0
Baada ya kuwasili nchini India kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa unaomsumbua, msanii wa Bongo Fleva, Hawa Mayoka ‘Hawa wa Nitarejea’,  amefanyiwa vipimo na kubainika hana tatizo la ini bali ana tatizo la moyo ambalo limekuwa likifanya tumbo lake kujaa maji kila wakati.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Meneja wa Diamond Platnumz, Hamis Taletale ‘Babu Tale’,  ambaye ndiye amempeleka Hawa nchini India ameandika:

“Asante Mungu tumefika salama India na tumefanya vipimo vyote upya salama na jibu lililotoka kwa wataalamu kwa asilimia 95% hawajaona tatizo linalohusiana na ini kwa mgonjwa ila ni moyo ndiyo uliyokuwa unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini.

“Hivyo basi kutahitajika kufanyika upasuaji mkubwa ambao utakuwa na uangalizi mkubwa wa wataalamu, then wametuhakikishia baada ya hapo mgonjwa atapata nafuu na inawezekana hizo 5% zilizobaki itakuqa poa na tatizo la ini halitokuwepo.

“Kikubwa tunaomba mtuombee dua na msiache kumuombea pia @diamondplatnumz apate nguvu ya kuendela kumsaidia kwa maana kutoa ni moyo. Kikubwa sana naomba tumuombee Hawa sababu anaingia kwenye upasuaji mkubwa na hii ni hatua ya yeye kuqa salama. Mungu tusimamie.”

Hivi karibuni Diamond alijitolea kumsaidia Hawa matibabu nchini India ambayo yatagharimu shilingi milioni 50 ikiwa ni baada ya kuugua kwa muda mrefu na kudaiwa kusumbuliwa na ugonjwa wa inim jambo ambalo imeonekana ni moyo.

Serikali Yawataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri Zote Nchini Kuhakikisha Wanatokomeza Malaria

$
0
0
Na, Paschal Dotto- MAELEZO
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya  Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imezitaka Halmashauri nchini kupambana na kudhibiti maambukizi  ya malaria ili taifa kuondokana na tatizo hilo na hivyo badala ya kuhangaika – muda na gharama – na matibabu, kutoa nafasi kwa wananchi kuendelea na ujenzi wa taifa wakiwa na afya njema .

Akizungumza katika uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa viashiria vya malaria nchini, wa mwaka 2017, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka watendaji hao wakuu; wakuu wa wilaya na wakuu wa halmashauri zote nchini kupambana na maambukizi ya malaria ili kutokomeza tatizo hilo nchini

“… mwezi Mei, 2015 Kasulu, Kigoma, kwenye maadhimisho ya siku ya malaria duniani tulizindua takwimu za awali ambazo zilionesha kiwango cha malaria kimeshuka toka asilimia 14 hadi asilimia 7 huku mikoa ya Kigoma asilimia 24.4, Geita asilimia ni 17.3, Mkoa wa Kagera asilimia 13.4 na Mtwara asilimia 14.8 … malaria bado ni kubwa, kwa hiyo Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi katika halmashauri hizo, wafanye kazi ya kusimamia kazi ya kutokomeza malaria”, Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy alisema kuwa katika utafiti huo unaonesha kuwa kila Halmashauri zina asilimia kadhaa za kiwango cha malaria, kwa maana viwango hivyo havikatishi tamaa kwa watendaji wa halmashauri kuchukua dhamira madhubuti ya kupambana na maambukizi ya malaria katika maeneo yao ili kutokomeza kabisa tatizo hilo, kama mpango wa Serikali wa kupambana na malaria unavyobainisha.

Aidha, Waziri aliongeza kuwa, katika hali ya kudhibiti kiango cha malaria, Serikali ina mpango wa kushusha kiwango hicho hadi kufika chini ya asilimia moja ifikapo 2020, kadhalika kutokomeza kabisa malaria ifikapo 2030, ili kuwawezesha wananchi kufanya kazi wakiwa na afya njema.

“tumeweka malengo kwamba kufikia 2020 tunataka kiwango cha malaria kifikie chini ya asilimia moja, na ifikapo 2030 tuwe tumetokomeza kabisa malaria nchni.” Amesisitiza Waziri.

Akaongezea kwa mfano, kwa Mkoa wa Kigoma ambapo halmashauri zake kiwango ni kikubwa zaidi, zikwemo Halmashauru za Kakonko (asilimia 30.8), Kasulu (asilimia 27.9), Kibondo (asilimia 25.8),  Uvinza (asilimia 25.4), Kigoma (asilimia 25.1), Buhigwe (asilimia 24) na Kigoma (asilimia 25.1), halmashauri hizi na nyinginezo, Wakurugenzi pamoja na watendaji wengine eneo la afya na jamii, wanapaswa kufanya kazi na wananchi ili kuweza kuondoa tatizo hili.

Kwa upande mwingine, wananchi wametakiwa kushirikiana na watendaji wa Halmashauri kutunza mazingira yao kwa kufukia madimbwi, kujenga vyoo bora, kukata nyasi na kuzoa taka katika maeneo yao,na kwamba itapunguza vifo vinavyosababishwa na malaria, kwani takwimu nchini zaashiria vifo vya watoto ni 33 kati ya watoto 1000, wakati Serikali imelenga, kama si kutokomeza vifo, basi vifikie hadi watoto 9 kati ya watoto 1000.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya October 23

Uteuzi wa Viongozi Watano Uliofanywa na Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jana, Oktoba 22, 2018 amefanya uteuzi wa Wenyeviti wa Bodi mbalimbali.


Taarifa ya ya Ikulu imeeleza kuwa Rais magufuli ameteua Wenyeviti watano kuchukua nafasi pamoja na kuziba nafasi za Wenyeviti wawili ambao wamekuwa wabunge.

Miongoni mwa walioteuliwa ni Dkt. Mwanza Kamata kuwa Mwenyekiti wa Mamlaka ya Biashara Tanznia (TANTRADE), akichukua nafasi ya Christopher Chiza ambaye amechaguliwa kuwa mbunge wa jiombo la Buyungu hivi karibuni.

Mwingine ni Dkt. Maria Mashingo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Maendeleo (TIB), akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Palamagamba Kabudi ambaye aliteuliwa kuwa mbunge na baadaye Waziri wa Katiba na Sheria.

Taarifa kamili kama ilivyoambatanishwa hapo chini.

Waziri Mkuu: Ushirikiano Wa Taasisi Za Dini Na Serikali Ni Muhimu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ushirikiano mzuri baina ya taasisi mbalimbali za dini nchini na Serikali ni jambo la muhimu katika kuboresha na kuimarisha amani.

Ameyasema hayo jana (Jumatatu, Oktoba 22, 2018) alipowasili jijini Mwanza akiwa njiani kwenda mkoani Simiyu ambako leo  anatarajia kufungua maonesho ya wajasiriamali.

Alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, Waziri Mkuu alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella na viongozi mbalimbali wa mkoa huo wakiwemo wa Serikali na wa dini mbalimbali.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua mkakati wa viongozi wa dini wa kuunda kamati za amani nchini ambapo walianzia kwenye ngazi ya mkoa na sasa wamefikia katika kata.

“Viongozi wa dini mnadhamana kubwa katika kulifanya  Taifa liendelee kudumisha amani, utulivu na mshikamano, hivyo ushirikiano wenu na   Serikali ni muhimu.”

Alisema viongozi wa Serikali wakati wote wamekuwa tayari kufanyakazi na viongozi pamoja na taasisi mbalimbali za dini, lengo ni kuimarisha amani na utulivu uliopo nchini.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mwanza inawajibu wa kuhakikisha kwamba maeneo ya mkoa huu yanaendelea kuwa salama.

Pia, Waziri Mkuu amempongeza Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Sheikh Hassan Bin Mussa Kabeke kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo.

“Nakupongeza kaimu sheikh wa mkoa kwa kuteuliwa na ninakutakia kila la heri katika kazi yako na kwamba dhamana yako kubwa ni kuwaunganisha waislamu na waumini wa dini zote.”

TFDA Yatoa Elimu Ya Madhara Ya Sumukuvu Kwa Wasindikaji

$
0
0
Na.Alex Sonna,Dodoma
Mamlaka ya chakula na Dawa TFDA kanda ya Kati Dodoma imeanza kutoa elimu kwa wasindikaji wa mazao ya Nafaka baada ya kubaini baadhi ya bidhaa wanazozalisha hususani unga wa mahindi na siagi ya karanga kuwa na vimelea vya ugonjwa wa sumukuvu ambao ni hatari kwa afya ya watumiaji na wakati mwingine husababisha vifo.

Mafunzo hayo yanatokana na ripoti ya ufuatiliaji wa usalama na ubora wa bidhaa zitokanazo na unga mchanganyiko na siagi ya karanga uliofanywa na mamlaka hiyo ya mwaka 2015-2018 na kubaini mazo hayo huzalishwa kwa wingi mkoani humo yana dalili ya uwepo wa fangasi na sumukuvu.

Akizungumza na washiriki Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw.Maduka Kessy  amesema kuwa wasindikaji wa chakula wanahitajika kuwa wasafi na weledi mkubwa kwa kuwa kinyume na hapo athari yake ya kupata sumukuvu ni hatari kwa walaji.

“Katika ufuatiliji huo ilibainika kuwa bidhaa hizi zilikuwa na dalili ya uwepo wa sumukuvu,hususani katika bidhaa zitokanazo na mahindi na karanga hizi ndizo wajasiliamali wengi wanauza”amesema Bw.Kessy

Kwa upande wake Meneja wa kanda ya kati Dodoma wa Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) Dkt Engelbart Bilashoboka,amewataka wasindikaji kubaini vyanzo vya uchafunzi wa chakula kutokana na sumukuvu ili waweze kuizuia.

Dk.Bilashoboka amesema kuwa wasindikaji wakibaini watakuwa wamewalinda walaji wa bidhaa hizo zinazotengenezwa kwa kuepusha maradhi kama vile ya kuumwa tumbo,kutapika,kuharisha na hali ya umanjano machoni na viganjani na hata kusababisha ba vifo pia.

Aidha amesema kuwa malengo ya  mamlaka hii  kuanzishwa kwake ni kuhakikisha kuwa chakula,dawa,vipodozi,vifaa tiba na votendanishi vitakavyotumika hapa nchini na vinakidhi ubora na usalama kwa watumiaji.

Kwa upande wa baadhi ya Wasindikizaji wamekiri kutokuwa na uelewa juu ya sumukuvu kwani awali walikuwa wakisindika Nafaka Kienyeji bila kuchagua mazao ambayo mengine yana  dalili za uwepo wa vimelea vya ugonjwa huo.


Video Mpya: Wahu- Nifanane Nawe

$
0
0
Msanii wa muziki kutokea nchini Kenya, Wahu anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Nifanane Nawe. 

Itazame hapo chini

Video Mpya: ChindoMan Ft. Memo – Cha Ukucha

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Chindo Man anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya uitwao  Cha Ukucha akishirikiana na Memo. Itazame hapa.

Wimbo wa Navy Kenzo na Diamond watamba chati za BBC Radio 1Xtra

$
0
0
Wimbo wa kundi la Navy Kenzo, Katika umefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwenye chati za BBC Radio 1Xtra.

Wimbo huo ambao wamemshirikisha Diamond Platnumz hapo Jumapili October 22  uliweza kufikisha views milioni 4 kwenye mtandao wa YouTube.

May mwaka huu msanii Harmonize alifanikiwa kuingiza ngoma yake ya Kwangwaru kwenye Top 5 za Afro Boss Airline DNA za kipindi cha Destination Africa kinachoendeshwa na DJ Edu kupitia BBC Radio One Xtra

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Kusinyaa Na Kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kama uume wako  umedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 
 
Ipo dawa  ya ASILI   ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.
 
Ni  dawa  ya  asili  kabisa ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI YA  KUPATA  TIBA  HII : Kupata  tiba  hii  fika  ka6ika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam  ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu  watapelekewa  dawa  mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )  na kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  au  boti  kwa  waliopo  Zanzibar.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :    0693  005 189.

Waziri Jafo Aimwagia SIFA Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Kwa Kutekeleza Miradi Kwa Ufanisi

$
0
0
Waziri wa nchi OR-TAMISEMI Mhe.Seleman Jafo  ameipongeza Manispaa ya Ilemela kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo inayozingatia thamani ya fedha.

Pongezi hizo amezitoa akiwa kwenye ziara ya kikazi katika  Manispaa ya Ilemela kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo alikagua jengo la utawala la Halmashauri, jengo la hospitali ya Wilaya, ujenzi wa barabara ya Sabasaba-Kiseke-Buswelu pamoja na ujenzi wa miundombinu katika kituo cha Afya Buzuruga.

Sanjari na ukaguzi wa miradi hiyo aliongea na watumishi wa Manispaa na kuwasisitiza kufanya kazi kwa ueledi na  kujiamini huku akisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato na kumtaka Mstahiki Meya wa Manispaa kuhakikisha anasimamia ipasavyo ukusanyaji wa mapato hasa katika soko la samaki la Mwaloni kwani ndio chanzo kikuu cha mapato cha Halmahauri.

“Mna kila sababu ya kusimamia mapato katika soko la samaki,hakikisheni mapato yote ya soko    yanaingia vizuri na yanasimamiwa vizuri, sitaki kusikia soko la mwaloni linaharibiwa kuwa sio chanzo muhimu cha mapato ya Manispaa ya Ilemela”, Alisisitiza

Aidha amemtaka afisa mapato kuhakikisha anasimamia mapato na kama kuna wizi unaendelea basi ahakikishe anafunga mianya yote hasa katika soko la samaki na kuongeza kuwa anataka kuona mapato yanaongezeka na halmashauri inasonga mbele

Pia amewapongeza waheshimiwa madiwani kwa usimamizi wao mzuri na kuwataka kuendelea  kupambana katika kuisimamia manispaa pamoja na miradi  ya maendeleo ili Manispaa iweze kusonga mbele

Akiwa katika kituo cha Afya Buzuruga, ambapo alipata wasaa wa kuongea na wagonjwa waliofika kutibiwa, Mhe. Jafo amesema kuwa amefarijika kuona kuwa  Manispaa ya Ilemela  imefunga mifumo ya kielektroniki (GOTHOMIS) katika vituo vyote vya afya na zahanati na kuifanya  Halmashauri  hii kuwa ya kwanza ya mfano na hivyo ameziagiza Halmashauri zote  kukamilisha uwekaji wa mifumo ya hii.

Pamoja na hayo ameitaka Halmashauri kuhakikisha wanaitumia mifumo hiyo kwa lengo lililokusudiwa la ukusanyaji wa mapato kwa maslahi mapana ya Halmashauri na vituo vya afya huku akiwasisitiza watumishi kufanya kazi kwa ueledi.

Akihitimisha ziara yake ameahidi kuwa atahakikisha fedha za umaliziaji wa miradi zinaletwa ili kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati uliokusudiwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images