LIVE: Kardinali Pengo anazungumza na Waandishi wa Habari
↧
↧
Hatima ya Kubenea, Komu kujulikana leo
Hatima ya Mbunge wa Ubungo Saed Kubenia na yule wa Moshi vijini, Anthony Komu, itajulikana leo baada ya kikao cha dharura cha Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Jana, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari kutangaza kikao hicho.
Alisema kitafanyika Dar es Salaam leo na ajenda kuu ni masuala yanayoendelea ndani na nje ya Chama hicho.
“Tutatoa taarifa rasmi juu ya maazimio ya kikao hiki kitakapomalizika,” ilisema taarifa ya Mrema.
Taarifa hiyo imetolewa siku chache baada ya sauti zinazoaminika kuwa ni za Kubenea na Komu, kusambaa kwenye mitandao ya jamii wakijadili kuwashughulikia baadhi ya viongozi wa chama hicho.
Kwa mujibu wa sauti hizo, Kubenea na Komu walikuwa wakipanga kumshughulikia Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob.
Awali inasikika sauti ikisema; “Boni hana msaada wowote kwenye haya mambo”.
Kisha inasikika sauti nyingine ikisema; “Anao msaada mkubwa sana kwa sababu Boni…ujue ndiyo wamemsambaratisha Waitara.
“Boni ni mjumbe wa kamati kuu, ni msema ovyo, ni mtu ambaye ana misimamo ya vuguvugu lakini anaheshimika.
“Kuna watu wanamchukulia kama ni mpiganaji, ni mtu mwenye msimamo ambao ndiyo hao wanampa uhalali Mbowe. Ukimuondoa Boni umempiga sana Mbowe, sana yaani.
“Unajua viko vitu vya msingi vya kufanya, ku – deal na Mbowe ni kwenye mambo ambayo ni halali”.
Hata hivyo baadhi ya watu wa karibu na Komu walidai mbunge huyo alituma kwa makosa sauti hiyo katika kundi la WhatsApp la Kaskazini bila kujua.
Hata hivyo wabunge hao walipoulizwa walikana kuhusika na sauti hizo na kudai kuwa zimetengenezwa kwa lengo la kuwachafua.
↧
Wakili wa TAKUKURU Akwamisha Kesi ya Tido Muhando
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando ameshindwa kuulizwa maswali na upande wa mashtaka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana baada ya Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kutokuwepo mahakamani hapo.
Wakili Swai ambaye anaiwakilisha Serikali kwenye kesi hiyo, ilielezwa mahakamani hapo yupo safarini Musoma mkoani Mara kwa shughuli nyingine ya kikazi.
Wakili wa Takukuru, Dismas Muganyizi, alieleza mahakamani mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa Wakili Swai yupo nje ya Mkoa wa Dar es Salaam na amekwenda Musoma kwenye majukumu mengine na kuiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi hiyo.
Hata hivyo, Tido alitakiwa kuulizwa maswali dhidi ya utetezi alioutoa mahakamani hapo Septemba 20, mwaka huu huku akiongozwa na mawakili wake, Dk. Ramadhani Maleta na Martin Matunda.
Hakimu Shahidi aliridhia ombi la upande wa mashtaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 30, ambapo Tido ataanza kuulizwa maswali na upande wa mashtaka dhidi ya utetezi wake.
Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulileta mashahidi ambao ni pamoja na aliyekua Mkurugenzi wa Shirika hill, Clement Mshana, Ofisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya na Mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa.
Tido alisomewa mashtaka manne likiwamo la kutumia madaraka vibaya na kuisababishia Serikali hasara ya Sh milioni 887.1.
↧
Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...
Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku kupitia simu yako ya mkononi.
Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku kupitia simu yako ya mkononi.
Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu tukuhabarishe masaa 24.
Ni rahisi tu << BOFYA HAPA KUPAKUA APP YETU>>
↧
Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo.
Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.
Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.
Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa
MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni
Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto
Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648 au 0656 551 093 au 0746473974
↧
↧
Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake
KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la nguvu za kiume .
1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa
JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona
MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk
MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060 0752348593 DR AGU
↧
Tanzania yajipanga kuteka soko la muhogo China
Serikali imewataka wazalishaji wa zao la muhogo nchini kuongeza uzalishaji ili kuwawezesha kupata soko la uhakika nchini China.
Hatua hiyo itaifanya Tanzania kuongeza wigo wa kusafirisha zao hilo nchini humo ambapo kwa mwaka 2017 inakadiriwa kupeleka bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani laki tatu sawa na Sh.milioni 687, huku China ikiingiza bidhaa zake hapa nchini zenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 3.1.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Profesa Siza Tumbo katika mkutano wa wadau wa wa zao la Muhogo kitaifa ambao umeandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI), Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo cha Kitropiki(IITA) na Wizara ya Kilimo, kitengo cha Mpango wa Maendeleo ya sekta ya kilimo awamu ya pili(ASDP II).
Mkutano huo unalenga kuandaa mipango ya kuendeleza zao hilo kuwa kibiashara na kuchangia katika maendeleo ya nchi.
Alisema kama Taifa kunatakiwa kuwapo na msimamo wa kuchangamkia soko la zao hilo nchini China kutokana na fursa ya kibiashara iliyopo.
“Uzalishaji upo chini kitakwimu lakini kuuhalisia haipo hivyo, sasa tunatakiwa tuwe ma champion kwenye uzalishaji wa zao hili ni zuri sana ili tuweze kuleta mageuzi kwenye zao hili,”alisema.
Alibainisha kuwa zao hilo nchini ni la pili kwa umuhimu zaidi katika mazao ya chakula baada ya mahindi na asilimia 84 ya jumla ya uzalishaji nchini ni kwa matumizi ya chakula cha binadamu, lakini uzalishaji huo bado uko chini na zao hilo halijatumika kikamilifu.
Aidha aliwataka Watanzania kula vyakula vya asili ili kulinda afya zao kwa kuwa kumekuwapo na mtazamo hasi kwa jamii kuwa kuna baadhi ya mazao ikiwamo muhogo na mtama kwamba hayafai kwa chakula jambo ambalo ni upotoshaji.
Aliwataka wakulima wa muhogo kutokatishwa tamaa na kauli hizo badala yake waongeze nguvu katika uzalishaji ili waweze kushindana na masoko makubwa ikiwamo nchi ya China.
Tanzania ni nchi ya 12 kwenye uzalishaji mkubwa wa muhogo duniani na ya sita barani Afrika baada ya Nigeria, Kongo DRC, Ghana, Angola na Msumbiji ambapo kila mwaka unachangia asilimia 5.5 ya jumla ya uzalishaji wake duniani na asilimia 14 kwa Afrika.
Mahitaji ya baadaye ya zao la muhogo nchini Tanzania unalengwa kuongezeka na kuwa kati ya tani 530,000 na 630,000 na kwamba hali hiyo inatokana na kuongeza thamani ya muhogo kwa kutengenezea unga, wanga na kuwa malighafi katika viwanda vya bia, pipi na vitafunio, viwanda vya nguo, karatasi, rangi na dawa.
↧
Mahakama yapokea hati ya kifo mshtakiwa kesi ya uhujumu uchumi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imepokea hati ya kifo ya mshtakiwa wa tatu Benjamin Mwakatumbula aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na kusababishia serikali hasara ya Sh.bilioni 1.16, pamoja na wenzake akiwamo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA) wa zamani, Dickson Maimu.
Mwakatumbula wakati wa uhai wake alikuwa Kaimu Mhasibu Mkuu wa Nida, hati ya kifo chake iliwasilishwa na upande wa utetezi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa jana.
Wakili Serikali Imani Mitumizizi alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na ilipangwa kwa ajili ya kutajwa.
Hata hivyo, mshtakiwa Maimu aliwakabidhi Wakili wa utetezi Faisal Ali bahasha ya kaki na ilipofunguliwa ilikuwa na hati ya kifo na kuikabidhi mahakama.
Hakimu Mashauri alisema mahakama imepokea hati ya kifo cha Mwakatumbula na mwenendo wa kesi dhidi yake umefutwa.Alisema kesi hiyo itatajwa tena Novemba 15,mwaka huu dhamana ya washtakiwa inaendelea.
Mbali ya Maimu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Biashara wa NIDA, Avelin Momburi na Mkurugenzi wa TEHEMA, Joseph Makani.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers, Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond na Xavery Kayombo.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kutumia madaraka vibaya, kula njama, kutumia nyaraka za uongo kumdanganya mwajiri na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh. 1,169,352,931.
↧
Mbunge Aliyeitosa CHADEMA na Kuhamia CCM Apangua Tuhuma za Kuandikiwa Barua
Aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul amejibu madai ya baadhi ya makada wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wanaomshutumu kuandikiwa barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kutokana na barua hiyo kuwa na kasoro na kufanana na barua zingine za wabunge waliojiuzulu kabla yake.
Gekul amesema kuwa wanadamu wakiamua kukutaftia kosa hawawezi kukosa cha kuongea hivyo amewataka Chadema wahangaike kujibu hoja zake na si kuanza kuangalia vitu binafsi.
“Wanadamu wakiamua kutafuta makosa kwako hawayakosi, utakuwa mtu wa ajabu unayeangalia zaidi maandishi badala ya ujumbe wa barua, uandishi wa barua mimi siangalii, kwangu sikuona kama ni hoja.”amesema Gekul
Amesema kuwa makosa ya kiuandishi hutokea popote, hivyo kukosewa kuandikwa kwa barua yake ya kujiuzulu sio tatizo lakini chamsingi ni ujumbe umefika sehemu husika na wala sio lugha iliyotumika, hivyo amewataka wahangaike na kujibu hoja zake.
Hivi karibuni katika mtandao wa Twitter afisa habari wa CHADEMA, Tumaini Makene alikosoa uandishi wa barua za wabunge waliojiuzulu kwa madai kuwa ni za aina moja.
Pauline Gekul ametimiza idadi ya wabunge 8 kutoka vyama vya upinzani waliotangaza kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa madai mbalimbali ikiwemo kumuunga mkono Rais Magufuli.
↧
↧
Vigogo Wawili wa ACACIA Wakamatwa na TAKUKURU
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imewakamata aliyekuwa Makamu wa Rais wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Acacia, Deo Mwanyika na Mshauri wa Serikali ndani ya kampuni hiyo, Alex Lugendo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo alisema wanawashikilia watu hao tangu juzi, na kwamba leo wanaweza kufikisha mahakamani kufunguiwa mashtaka kwa tuhuma zinazowakabili.
“Mwanyika na Alex tuliwakamata kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi katika nyanja ya madini. Wakiwa viongozi waandamizi walishindwa kusimamia nchi ipate mapato kama ilivyotakiwa kwa mujibu wa sheria.
Deo Mwanyika alijiunga na Acacia mwaka 2001 akiwa ameitumikia kwa miaka 17, alitangazwa kujiuzulu Agosti 24 kwa barua ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Acacia, Peter Galeta kwenda kwa wafanyakazi wote wa kampuni hiyo.
↧
Radi Yaua Wanafunzi 6 na Kujeruhi Wengine 25
Wanafunzi sita wa shule ya msingi, Emaco Vision iliyopo mjini Geita wamefariki dunia baada ya kupigwa na radi wakiwa darasani huku wengine wakijeruhiwa wakiwamo walimu wawili.
Tukio hilo limetokea leo Jumatano Oktoba 17, 2018 saa 3:30 asubuhi. Wakati mvua ikinyesha na radi kubwa kupiga.
Ofisa elimu msingi, Yese Kanyuma amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kusema hadi sasa majeruhi ambao bado wako hospitali ni 25.
↧
Jibu la Gigy Money Kuhusu Kujiunga lebo ya WCB
Msanii wa Bongo Fleva, Gift Starnford maarufu Gigy Money, amesema hajawahi kufikiria kujiunga na lebo ya WCB na kama ingemlazimu kufanya hivyo angeenda kuwa Diamond wa kike.
Gigy anasema anaamini kila msanii ana nafasi ndani ya kazi zake na hajawahi kufikiria kujiunga na kundi hilo kwa kuwa uwezo wake ni wa kipekee.
“Si kwamba WCB kusingetimiza ndoto zangu, nina malengo ya mbali sana na kama ungenilazimisha nijiunge pale basi labda ningeenda kuwa Diamond wa kike, yaani nifanye zile kazi anazofanya yeye na kitakachotutofautisha na jinsia pekee,” amesema Gigy Money.
Ameongeza kuwa kitendo cha kuwa karibu na Diamond kimezidi kumpa uthubutu na kuona ana deni kubwa mbele ya mashabiki zake huku akidai amekuwa akipata msaada mkubwa wa jinsi ya kuongeza ufanisi wake kutoka kwa staa huyo.
↧
Sponsored Post: Kwanini Wanawaume Wenye Pesa Za Kichawi Huwa Wanatumia Pesa Nyingi Sana Kuwahonga Wanawake Zao?
DOKTA MUNGWA KABILI : 0744 000 473.
Je Mwanaume Mwenye Pesa Za Kichawi Anaweza Kutumia Uchawi Huo Huo Kumroga Mwanamke Kimapenzi ?
Kama Jibu Ni Ndio Kwanini Basi Wanawaume Wenye Pesa Za Kichawi Huwa Wanatumia Pesa Nyingi Sana Kuwahonga Wanawake Zao ?, Kwanini Wasitumie Tu Uchawi Wa Mapenzi Ili Kujiepusha Na Gharama Za Kutumia Pesa Nyingi Kwa Kitu Ambacho Uchawi Unaweza Kufanya.?Hili ni swali nililo ulizwa na kijana mmoja ambae amejitambulisha kama msomaji mzuri wa makala zangu.
YAFUATAYO NDIO MAJIBU YANGU :
Kwanza kabla ya yote unatakiwa ujue mwanaume huyo ambae unasema ana pesa za kichawi amezipata kwa kutumia tambiko la aina gani.
Na hii ni kwa sababu matambiko ya biashara na mali yamegawanyika katika aina kuu mbili.
Aina ya kwanza ni matambiko yanayo julikana kama MATAMBIKO BARIDI na aina ya pili ni matambiko yanayo julikana kama MATAMBIKO YA MOTO.
Linapokuja suala la matumizi ya pesa kwa wanawake, ni vigumu sana kwa mtu asie na jicho la tatu kutofautisha baina ya mwanaume anae tumia matambiko baridi katika biashara zake na mwanaume anae tumia matambiko ya moto katika biashara zake kwa sababu wote huwa wanatoa pesa nyingi sana kwa wanawake.
TOFAUTI NI HII HAPA CHINI
MWANAUME ANAE FANYA BIASHARA ZAKE KWA KUTUMIA MATAMBIKO BARIDI.
Mwanaume ambae anafanya biashara zake kwa kutumia matambiko baridi hutoa pesa nyingi kwa mwanamke kwa lengo la kuitumia nyota ya mwanamke huyo katika biashara na shughuli zake zote za kumuingizia riziki na kipato.
Ni hivi katika ulimwengu usio onekana, ukitaka kuchukua nyota ya mtu kwa njia rahisi kabisa, ni kumfanya mtu huyo akutegemee wewe kwa kila kitu hususani katika masuala yote yanayo husu pesa na rizki kwa ujumla.
Ukifanikiwa kumfanya mtu yoyote Yule akutegemee wewe kwa kila kitu, kuanzia kula chakula, kuvaa, na mambo yote muhimu katika maisha hasa hasa yale yanayo husu rizki basi unakuwa umeichukua nyota yake na matokeo yake milango yake yote ya kuingiza rizki inahamia kwako.
Riziki yake inakuwa inapitia kwako. Mlango wake wa kuingizia riziki unahamia kwako. Mtu huyo anakuwa hawezi kupata pesa yoyote ile bila pesa hiyo kupitia kwenye mikono yako.
Ili mtu huyo apate rizki yoyote ni lazima rizki hiyo ipitie kwanza kwako.
Kwa hiyo mwanaume huyu anapokuwa anakupa wewe mwanamke pesa nyingi maana yake ni kwamba anakupa pesa zako mwenyewe.
Kama nilivyo dokeza hapo juu kwamba njia hii ni njia ya halali kabisa kwa sababu wote mnafaidika .
Anaeitumia nyota yako anafaidika na wewe ambae nyota yako inatumika unafaidika pia.
Kwa lugha nyepesi mwanaume huyo anakuwa anasafiria nyota yako.
Ndio maana sharti kuu la kutumia njia hii ni lazima umtunze vizuri mtu ambae anakutegemea wewe kwa kila kitu.
Kadri unavyo mtunza vizuri na kumpa mahitaji yake muhimu ndivyo mambo yako katika biashara na shughuli zako yatakavyo kuwa yanakunyookea.
Hii ni njia ya asili na ya halali kabisa, hata wewe unaesoma makala haya unaweza kuwa unasafiria nyota za watu wengine bila wewe mwenyewe kujua wala bila wao wenyewe kujua.
Kwa mfano kama una watu wanao kutegemea wewe kwa kila kitu kama vile mke, watoto, au wazazi na wewe unajitahidi kuwatunza na kuwapa mahitaji yao ya muhimu basi milango yao ya rizki inahmia kwako na rizki yako inakuwa kubwa na wala unakuwa hauwezi kuishiwa kabisa.
Ni rahisi kwa mwanaume ambae hana kabisa watu wanao mtegemea kuishiwa na kukosa hata hela ya kula lakini mwanaume mwenye wategemezi kama vile watoto. Ndio maana hata kwenye mabar na sehemu za starehe wanaume walio kwenye ndoa ndio wanao ongoza kwa kutoa ofa za pombe kuliko ambao hawana wategemezi.
Kama una nafasi unashauriwa usiishie kuwatunza watoto, mke na wazazi wako tu , jaribu kutafuta na watu wengine ambao unaamini wana mahitaji maalumu katika maisha lakini hawana watu wa kuwasaidia.
Kwa mfano watoto yatima. Unaweza kwenda kwenye kituo cha watoto yatima ukachukua mtoto mmoja au wawili kwa kadri Mwenyezi Mungu alivyo kujaalia na kwenda kuishi nao nyumbani kwako au kama nyumbani kwako hauna nafasi ya kuwaweka basi uwe unawapelekea mahitaji yao hapo hapo kituoni kwao.
Hii ni njia rahisi sana na ya uhakika ya kufungua na kuongeza milango ya rizki.
Ni njia mujarab sana na watu walio tumia njia hii wamepata mafanikio makubwa sana katika shughuli zao zinazo husisha vipato vyao.
MWANAUME ANAE FANYA BIASHARA ZAKE KWA KUTUMIA MATAMBIKO YA MOTO
Mwanaume huyu anakupa pesa nyingi sana wewe mwanamke kwa sababu pesa zake ni pesa za kichawi ambazo hazina thamani.Chenye thamani ni nyota yako.
Kwanza kabla ya kuanza kukupa pesa zake, anaanza kwanza kwa kuimiliki nyota yako kichawi.
Na anapata uhalali wa kiroho wa kumiliki nyota yako baada ya kutoa sadaka maalumu kwa ajili ya kumiliki nyota yako.
Mwanaume huyu anakuwa anaitumia nyota yako katika shughuli zake na anakuwa anapata pesa nyingi sana kupitia nyota yako.
Pesa anazo kupa wewe ni pesa za kichawi ambazo anakuwa amezipata kwa kufanya matambiko ya moto.
Ni pesa ambazo zina thamani tu katika ulimwengu wa rohoni lakini hazina thamani katika ulimwengu wa nyama.
Ili pesa hizo ziwe na thamani ni lazima atafute mtu mwenye pesa zenye thamani katika ulimwengu wa nyama kwa ajili ya kubadilishana nae.
Mtu huyo ni wewe kwa sababu nyota yako ina utajiri mkubwa.
Kwa hiyo anacho kifanya hapo anakuwa anakupa pesa zake za kichawi ambazo hazina thamani kwa kubadilishana na nyota yako ambayo thamani yake ni mara elfu zaidi ya pesa anazo kupa.
Hii haina tofauti na uchawi wa chuma ulete. Wachawi wanao chukua pesa za watu kwa chuma ulete huwa wanakuwaga na pesa za kichawi pia ambazo hazina thamani katika ulimwengu wa nyama.
Ili pesa ziwe na thamani ni lazima wazibadilishe na mtu mwenye pesa zenye thamani katika ulimwengu wa nyama.
Ndio maana mtu wa chuma ulete akikupa pesa yake ukamrudishia chenji. Hiyo chenji uliyo mrudishia ndio yenye thamani na sio ile aliyo kupa.
KUHUSU WANAUME WENYE PESA ZA KICHAWI KUWAROGA KIMAPENZI WANAWAKE.
Kwa kawaida mwanaume mwenye pesa haitaji kutumia uchawi kumroga mapenzi mwanamke.Uchawi wanao weza kuutumia wanaume hawa ni kumfunga mwanamke asiende kwa mtu mwingine kwa sababu za kinyota.
Hataki nyota ya mwanamke wake ichafuliwe kwa sababu tendo la kujamiiana ni moja kati ya mambo makuu yanayo chafua nyota za watu kwa kiasi kikubwa sana.
Kwa hivyo mwanaume huyu hatumii uchawi wa jamii ya limbwata katika kumroga mapenzi mwanamke isipikuwa atamfunga tu kichawi mwanamke huyo asiwe na mwanaume mwingine kwa sababu za kinyota.
Hata hivyo yapo mazingira yanayo walazimisha wanaume hawa kuwaroga mapenzi wanawake wanao wataka .Hasa hasa pale anapo gundua mwanamke Fulani ana nyota kali ya biashara, mali na utajiri.
Mwanaume anae fanya biashara zake kwa kutumia uchawi akigundua kuna mwanamke ana nyota kali ya biashara, mali na utajiri basi atafanya juu chini kumpata mwanamke huyo hata kama ni mke wa mtu.
Hata kama mwanamke huyo yupo kwenye ndoa na mumewe na wana watoto zaidi ya mmoja, mwanaume mwenye kutafuta pesa kichawi atafanya juu chini ampate mwanamke huyo.
Na hii ni moja kati ya sababu ya ndoa nyingi sana kuvunjika siku hizi licha ya kuwa wanandoa mmepata watoto na watoto wenyewe bado wadogo.
Kinacho tokea mwanaume huyu akigundua kuwa mwanamke Fulani ana nyota kubwa ataanza kwa kutumia njia zake zote za kawaida ili kumnasa kimapenzi mwanamke huyo kama vile kutoa pesa, zawadi kubwa kubwa na kadhalika.
Mwanamke huyu akiweka ngumu licha ya jamaa kutumia njia zake zote ikiwemo pesa kushindikana, basi ndipo mwanaume huyu huamua kutumia uchawi sasa.
Hii ni njia inayo fanywa hata na wachawi katika shughuli zao za kichawi.
Wachawi wakitaka kufanya misheni yao ya kichawi huwa wanaanza kwanza kwa kutumia njia za kawaida. Njia za kawaida zikishindwa ndipo sasa hutumia uchawi.
Kwa mfano A na B ni mke na mume wanao pendana sana na wanafanya shughuli zao na zinawaendea vizuri. Wachawi hawapendi kuwaona A na B wakiwa pamoja kwa upendo .
Watakacho kifanya wachawi hao ni kuanza kupeleka maneno ya umbea kwa A na B ili kuwagombanisha.
Maneno ya umbea yakigonga mwamba sasa ndio wachawi hao huamua KUPELEKA MAJESHI. Kupeleka majeshi maana yake ni kufanya uamuzi wa kutumia silaha za kichawi kukamilisha misheni yao na uamuzi huu ukishafikiwaga huwa haubatilishwi.
Vivyo hivyo mwanaume huyu anapokutana na mwanamke mwenye nyota ya mali huanza kumtongoza kwa kutumia njia za kawaida na njia za kawaida zikishindikana basi ndio hutumia uchawi.
Wakati mwingine mwanamke huyu kwa sababu anakua anampenda mume wake na ndoa yake na hataki kuwasumbua watoto wake anaweza kumkubalia mwanaume huyo kama mchepuko, lakini lengo la mwanaume huwa ni mwanamke huyo awe wake peke yake.
Kwa hiyo hata baada ya kuwa katika mahusiano na mwanamke huyo, mwanaume huyo ataendelea kumshawishi mwanamke huyo aachane na mume wake.
Juhudi za kumshawishi mwanamke huyo kwa njia ya kawaida zikishindikana basi ndipo mwanaume huyo huamua kutumia uchawi wa kuwatenganisha mwanamke huyo na mume wake na yeye mwanaume kumchukua mke na kwenda kuishi nae.
Mwanaume aliye kimbiwa na mkewe katika mazingira haya anaweza kujiona hana thamani na kwa kudhani labda ana kasoro kumbe kilicho tokea ni kitu kingine kabisa ambacho hata mke wake akijui.
Ushauri wangu ukiwa na mkeo hakikisha unamtunza na kumuhudumia kwa kila kitu bila kujali na yeye ana kazi au lah.
Wazee wetu walikuwaga na msemo wao mzuri sana ambao vijana wa siku hizi wanautumia vibaya. Wazee walikuwa na msemo usemao “ Mwanamke ni kama mtoto “ sasa bahati mbaya vijana wa siku hizi msemo huu wanauchukulia kumaanisha kwamba mwanamke ana akili kama za mtoto.
Watu wenye mtazamo huu wanakosea sana . Wazee waliposema wanawake ni kama watoto walimaanisha kitu kimoja tu, nacho ni MATUNZO.
Mtoto wako hatakiwi kuwaza atakula nini au atavaa nini, mtoto wako akiumwa atakacho kiwaza ni uchungu wa dawa au maumivu ya sindano na sio kwamba atapata dawa au la.
Vivyo hivyo mke wako au mwanamke wako hatakiwi kuwaza atakula nini au atavaa nini nakadhalika.
Wewe unatakiwa kuwaza kwa ajili yake na ni lazima uwaze kwa ajili yake kwa sababu usipo waza kwa ajili yake watatokea wanaume wengine ambao watawaza kwa ajili yake na kuchukua nafasi yako.
Asili ya wanawake ni kuishi kwenye utajiri kwa sababu nyota zao ni nyota za utajiri. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu alivyo waumba. Hakuwaumba wateseke.
Ndio maana HAWA alimkuta ADAMU akiwa tayari kwenye bustani ya Edeni ambayo ndani yake kulikuwa na kila kitu. Katika ulimwengu usio onekana EDEN maana yake ni utajiri.
Simaanishi kwamba kama wewe sio tajiri usioe au usiwe na mwanamke, hapana namaanisha unapokuwa na mwanamke au mke jitume fanya kazi kwa bidii na umtunze mkeo kwa kila kitu, ukifanya hivyo basi utachukua nyota yake na wewe pamoja na yeye mtapata mafanikio makubwa sana kwa sababu wanawake karibu wote wana nyota za mali na utajiri na wasio kuwa na nyota za mali na utajiri ni wale ambao nyota zao zimechafuliwa. Katika ulimwengu usio onekana, hapa ndipo unapokuja ule msemo “nyuma ya mafanikio ya kila mwanaume kuna mwanamke”.
Sura ya saba ya kitabu changu “ MAMBO TISA YANAYO UNDA NYOTA YA MWANADAMU: UHUSIANO KATI YA NYOTA YA MTU NA MAFANIKIO YAKE KATIKA MAISHA ina itwa “ NAFASI YA NYOTA YA MWANAMKE KATIKA MAFANIKIO YA MUME WAKE “.
Watu wengi walio pata bahati ya kusoma kitabu changu hicho wameniomba sura hiyo niitolee kitabu chake yenyewe na nina wa ahidi kuyafanyia kazi maombi yenu.
Nitakapo kamilisha kuandika kitabu hicho basi nitawatangazia ili mpate kujifunza zaidi.
Kwa ambao hawakubahatika kupata nakala za kitabu changu mnaweza walau kusoma maelezo kuhusu kitabu hicho kupitia : http://mungwakabhili.blogspot.com/2018/06/mambo-tisa-yanayo-unda-nyota-ya.html
MAKALA HAYA YAMESIMULIWA NA DOKTA MUNGWA KABILI. DOKTA MUNGWA KABILI ANAPATIKANA KUPITIA SIMU NAMBA : 0744 000 473.
↧
↧
AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 106 na 107 )
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
Tukaondoka na raisi na kuelekea kwenye hospitali iliyomo humu ndani ya Ikulu. Tukaingia kwenye moja ya chumba, tukamkuta mtoto wa K2 akiwa hoi bin taabani.
“Huyu ni mwangu, huu ugonjwa ulimpata masaa matatu nyuma. Ujio wenu ninaimani mutamsaidia, hapa ninazunguma kama mama na si raisi. Dokta Lameck ninakuomba na timu yako kama kuna uwezekano wa mwangu kupona nitawaongezea mara mbili ya kiasi cha pesa ambacho mulikihitaji kutoka katika serikali yangu”
K2 alizungumza huku machozi yakimlenga lenga, nikatzamana na Cajoli, mwili mzima ukanisisimka baada ya kusikia maneno ya K2, hasira ya mauji ya mwangu pamoja na familia yangu ikaanza kunipanda mawazo ya kumuu mtoto wa K2 yakaanza kunijia kichwani mwangu taratibu na nikadhamiria kuhakikisha kwamba leo ninaondoa maisha ya mtoto wa K2.
ENDELEA
“Nimekuelewa muheshimiwa raisi, tafadhali tungeomba nafasi ili kuweza kumtibu mwano”
“Hakuna shida mimi nipo tayari kukaa hata hapo nje ili mradi mwanangu aweze kupata matibabu na kupona”
“Sawa ila muheshimiwa raisi ninahitaji uweze kuitunza ahadi yako katika hili ulilo lizungumza”
“Usijali dokta Lameck”
“Okay”
K2 akatoka nje na walinzi wake. Nikautazama mlango baada ya kufungwa, nikataka kwenda kuufunga ila Cajoli akaniwahi kunishika mkono.
“Unataka kufanya nini?”
“Nahitaji kuufunga mlango”
“Dokta Lameck”
Cajoli alizungumza kwa sauti ya chini huku akinisogelea karibu yangu
“Natambua kwamba una hasira kali na unakisasi cha kikali dhidi ya K2. Tafadhali ninakuomba utulie”
“Shem ni kitu gani kinacho endelea”
“Nipo sawa shem tuanzeni kazi”
Kila mmoja akachukua gloves nyeupe na kuzivaa viganjani mwake.
“Hapa hakuna kazi kubwa inatubidi kumchoma sindano huyu kijana”
Cajoli alitoa maelekezo huku mimi nikifungua brufcase na kutoa kichupa cha dawa. Nikamkabidhi Cajoli akaisingiza sindano na kuvuta dawa kidogo na kumchoma kijana huyu kwenye mkono wake.
“Itachukua dakika thelathini kwa virusi wote kufa mwilini mwake.”
“Una uhakika na unalo lizungumza?”
“Yaa nina uhakika honey, tukae humu ndani ya hichi chumba hadi dakika hizo zitakapo kwisha”
“Sawa”
Kazi iliyo bakia kwentu ikawa ni kutazama saa ya ukutani jinsi inavyo zungusha mishale yake taratibu, kila nilipo jaribu kumtazama mtoto wa K2 roho ya kishetani na ya mauji inanikaba kooni mwangu huku moyoni mwangu nikisikia sauti mbili zikipingana, moja ikinihitaji nimuue mtoto wa K2 iwe njia moja ya kulipiza kisasi, huku roho nyingine ikinihitaji kuwa mvumilivu nichukue kiachi cha pesa alicho kizungumza K2 na niondoke zangu.
“Dokta”
Shem Cajoli aliniita na kunifanya nigeule, nikamkuta akiwa amesimama pembeni ya kitanda cha mtoto wa K2. Mapunye punye yote yoliyo kuwa mwilini mwake yote yametoweka. Amerudi katika hali yake kama kawaida.
“Mambo kijana”
Cajoli alizungumza huku akimtazama mtoto huyu usoni mwake.
“Safi”
“Unajisikiaje?”
“Vizuri tu”
“Unaweza kushuka kitandani?”
“Ehee”
“Shuka”
Kijana huyu akashuka kitandani, Cajoli akamshika mkono na kumsimamisha mbele ya kioo kilichomo kwenye hichi chumba kijana, huyu akaanza kujishangaa mwili wake jinsi ulivyo rudi katika hali yake ya kawaida.
“It’s me real”
“Yaa ni wewe”
“Mom”
Mtoto huyu akaita kwa nguvu na kuwafanya walinzi wa K2 kuingia kwa haraka ndani ya chumba hichi. K2 akaingia, alipo muona kijana wake amerudi katika hali ya kawaida, akamkimbilia na kumkumbatia kwa nguvu huku akimpiga mabusu mfululizo mashavuni mwake. Machozi ya asira yakaanza kunilenga lenga, upendo anao uonyesha K2 kwa mwanaye kusema kweli roho yangu ina niuma sana.
“Dokta Lameck asante sana”
K2 alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Nikabaki kutabasamu tu kwa maana sihitaji kuzungumza, isije kinywa changu kikateleza na kuvuruga hali ya hewa bure.
“Mom nimepona”
“Yaa I see my son”
K2 akatuomba tutoke katika chumba chumba hichi. Moja kwa moja tukalekea katika ukumbi wa mikutano ambapo hapo tukakutana na madaktari wengine ambao wameshindwa kutengeneza dawa ambayo inaweza kuwaua virusi hawa wanao tesa mamilioni ya Watanzania.
“Munaweza kukaa”
K2 alizungumza huku akielekea kwenye kiti kilichipo mbele ya meza hii kubwa na ndefu yenye viti zaidi zaidi ya kumi kwa kila upande. Muhudumu katika ukumbi huu wa mkutano, akatonyesha viti vya kukaa katika hii meza. Taratibu tukaketi huku macho yangu nikiyapitisha pitisha kwa madaktari hawa ambao hakuna hata mmoja ambaye ninamtambua.
“Mabibi na mabwana, ninawatangazia kwamba dawa ya Virusi hivi vilivyo sambaa kwa maji, imepatikana kutana na dokta Lemeck David pamoja na timu yake”
Ikatubidi sote watatu kusimama ili watu waweze kutuona.
“Dokta Lameck David pamoja na timu yake, wameweza kugundua dawa ambayo. Nilijitolea kufanyiwa majaribio katika mwili wa mwanangu na kama munavyo weza kumuona, mwangu yupo salama kabisa na ana afya nzuri na amerudi katika hali yake ya kawaida.”
Madaktari wpte waliomo ndani ya ukumbi huu wakaanza kupiga makofi wakifurahia jambo kupatikana kwa dawa ambayo inaweza kuua virusi vinavyo endelea kuwatesa mamilioni ya Watu
“Kusema kweli ninayo furaha kutoka moyoni. Nikiwa kama mama ninaumia kuona watan wanateseka, watanzania wanasitisha kazi zao. Leo nimepokea taarifa juu ya ajali nyingi barabarani. Utakuta dereva anakunywa maji na kupata ugonjwa huu, mwisho wa siku anashindwa kabisa kuhimili gari kwa kuchanganyikiwa na anajikuta akipata ajali. Kwa uvumbuzi wa dokta Lameck David, ningeomba sasa atupatie ufafanuzi wa hii dawa yake, pamoja na matumizi yake. Dokta Lameck David karibu sana”
K2 alizungumza akiwa na furaha sana, nikashusha pumzi taratibu huku nikiwa na tabasamu pana usoni mwangu ila laiti kama mioyo yetu inge kuwa inaonekana kwa nje, basi K2 asinge niruhusu hata nimkaribie karibu yake. Taratibu nikasimama huku nikiwawazama madaktari katika chumba hichi.
“Habari za usiku”
Watu wote wakaitikia, nikaliweka vizuri koti langu la suti kisha nikajikoholesha kidogo na kuiweka miwani yangu sawa ili mradi yote ni madoido ya kulisoma eneo la humu ndani.
“Kama muheshimiwa riasi alivyo weza kutanguliza utambulisho wetu, basi si vyema nikalisema jina langu kamili. Ninaitwa dokta Lameck David Alimeida, ni mtanzania halisi ila nimeweza kusoma inchini India, na nimesomea maswala ya udaktari na ugunduzi wa madawa. Wiki moja iliyo pita niliweza kuingia nchini Tanzania, nikitokea India, nikiwa nimemaliza miaka tisa ya kusomea maswala ya ugunduzi wa dawa za magonjwa sugu kama HIV, EBOLA, na kadhalika.”
Nikanyamaza kidogo na kuiweka sawa miwani yangu, kwani kitu ninacho kizungumza vyote ni uongo mtupu na laiti wangejua kwamba sisi ndio chanzo cha virusi hawa wasinge kubali hata kukaa meza moja na mimi.
“Leo asubihi nilipo weza kuona ugonjwa huu wa kutisha, ikanilazimu mimi na timu yangu kuweza kuanza harakati za kutengeneza dawa ambayo itaweza kuokoa maisha ya mamilioni ya Watanzania. Tulipo hakikisha kwamba tumefanikiwa kutengeneza dawa hii kwa haraka iwezekanavyo, niliweza kuchukua jukumu la kumpigia raisi simu, huku nikiwa tayari nimesha fanya jaribio kwa mgonjwa mmoja ambaye ni jirani kabisa na sehemu ninayo ishi.”
“Ninamshukuru mama hapa, muheshimiwa raisi kwa kuweza kuwa msikivu, Mungu aliweza kumuongoza, na kutukubalia vijana wake kuja kufanya hichi ambacho tayari tumesha kifanya. Nilikaa na timu yangu nikaona kwamba dawa hii tuipe jina la K2, jina la raisi wetu, kwa maana ni mama shupavu na ni mama ambaye ninaimani atalifikisha mbali taifa letu”
Ukumbi mzima ukalipuka kwa makofi, laiti kama watu wengeruhusiwa kupiga vigelele gele basi wangepiga kwa shangwe sana. Yote niliyo yazungumza yanatoka kinywani mwangu na si moyoni mwangu, nimeyazungumza kuhakikisha kwamba ninazidi kuiteka akili ya K2 pamoja na watu wake.
“Ohoo this is real suprize, sikutarajia kama dokta Lameck unaweza kuipa dawa yako jina langu”
“Yaa ninakuomba ulipokee kwa mikono yote muheshimiwa raisi”
“Sawa, mimi sina kipingamizi katika hilo. Dokta Lameck nafani ni yako sasa, kuunda timu yako itakayo fanya kazi chini yako kuhakikisha kwamba untengeneza dawa nyingi nyingi za kuwaponya wagonjwa”
“Nashukuru muheshimiwa raisi kwa cheo hicho. Ila ninawazo moja kubwa, ambalo linaweza kuifanya Tanzania kupona kwa wakati mmoja na kama si wakati mmoja basi watapishana kwa dakika kadhaa tu”
“Zungumza tu dokta Lameck”
“Kutokana ugonjwa huu umeenea kwa maji,basi tunataka maji hayo kuweza kuyaweka dawa yetu, na itakwenda kuua virusi wote ambao wapo kwenye hayo maji na hii itakuwa ni njia raisi kwako muheshimiwa raisi kuwatangazia wananchi kwamba maji wanayo yatumia ni salama na ni dawa kwao”
“Your so real genius. Sijui siku zote ulikuwa wpai kijana mwenye akili kama wewe?”
“Nilikuwa India”
Jibu langu likawafanya watu wote ndani ya ukumbi kucheka,hata K2 mwenyewe akacheka sana.
“I real like you dokta Lameck. Okay, madaktari wote sasa hivi mutakuwa chini ya dokta Lameck, mutahakikisha kwamba munafanya naye kazi kwa usihirikiano kuhakikisha kwamba hadi inatimu saa moja asubihi basi kila jambo lipo kwenye mstari na huu ungonjwa, utakuwa ni historia kwenye nchi yetu”
“Sawa muheshimiwa”
“Dokta Lameck na timu yako ninawaomba tuongozane”
Kikao kikaishia hapo, huku moyoni mwangu nikiwa nimejawa na matumaini makubwa sana ya ushindi katika ulipizaji wa kisasi. Tukaingia na raisi ofisini kwake.
“Nimeona niwatangulizie nusu ya pesa, ili muweze kupata nguvu ya kufanya kazi”
“Sawa, muheshimiwa tutashukuru sana”
K2 akachukua mkonga wa simu iliyopo mezani mwake, akaminya minya namba kadhaa kisha akapiga simu.
“Habari yako mkurugenzi”
“Ninahitaji muweze kuingiza pesa katika akauti nitakayo kutumia dakika chache kuanzia hivi sasa. Na nitahitaji muingizi dola za kimarekani bilioni kumi”
“Sihitaji msawali fanya kama nilivyo kuagiza”
K2 akakata simu na kuirudisha sehemu alipo itoa.
“Watanzania bwana, mtu umemueleza kitu cha kueleweka, ila bado anahoji msawali”
K2 alizungumza huku akitutazama kwenye nyuso zetu.
“Ndio nchi yetu muheshimiwa raisi”
Cajoli alijibu.
“Kweli Cajoli si ndio?”
“Ndio”
“Ninaomba munipatie namba ya akaunti yenu”
Cajoli akataja namba yake ya akaunti, K2 akaituma kwa mkurugenzi wa benki. Ndani dakika tano meseji ikaingia kwenye simu ya Cajoli akatuonyesha sote. Nilihisi kuchanganyikiwa kwa furaha kwa maana kwenye maisha yangu sikufikiria kumiliki kiasi kikubwa cha pesa kama hichi.
“Mukiifanya hii kazi, ninawahakikishia hiyo pesa nyingine ninawaongezea kutoka mfukoni mwangu mimi mwenywe”
“Sawa muheshimiwa raisi”
“Ngoja sasa niwapeleke maabara”
Tukatoka katika ofisi ya raisi akatupeleka kwenye maabara. Akatuacha ndani ya maabara kwa ajli ya kuanza kuifanya kazi yetu.
“Shem jamani nina ushauri”
“Ushauri gani?”
“Ninakuomba Cajoli hiyo pesa uweze kuihamishia kwenye akaunti nyingine, isije ikatokea ikarudishwa, tukawa tumefanya kazi bure”
“Kweli, ngoja niiweke kwenye akaunti yangu ya Dubai”
“Sawa”
Cajoli akaanza kuminya minya simu yake. Baada ya dakika tano akanyanyua uso wake ulio jaa tabasamu pana sana.
“Dubai wamekubali kuipokea pesa yangu na kuiingiza kwenye akaunti yangu”
“Kumbe huwa wanasumbua sana?”
“Sana, mara nyingi wanahofia kuingiziwa pesa za ufisadi na kuchafua jina la nchi yao”
“Hapo kweli, sasa nitahitaji tuandae chupa za maji ishirini na nne. Kila chupa tuweze kuweka dawa, baada ya hapo chupa zote nitahiji tumuombe muheshimiwa raisi aweze kuzisambazo chupa hici kwenye vyonzo vyote vya maji”
“Sawa dokta”
Kabla hatujaanza kufanya jambo lolote, mlango wa maabara ukafunguliwa. Wakaingia wanaume wawili walio jazia miili yao kwa mazoezi huku wakiwa wamevalia sare za jeshi. Wakaniangalia kisha mmoja akazungumza kwa sauti nzito.
“Dokta Lameck David Almeida ongozana na mimi”
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi, nikamtazama Cajoli, ninamuona kabisa amejawa na wasiwasi unao pelekea hadi kuanza kulengwa lengwa na machozi.
AISIIIII……….U KILL ME 107
“Usijali, honey ninakuja. Endeleeni na kazi ambayo nimewaachia”
“Sawa doktar”
Shem Cajoli alinijibu, nikatoka ndani ya maabara na kuongozana na wanajeshi hawa ambao mmoja ametangulia mbele huku mmoja akiwa nyuma yangu. Sikuhitaji kufahamu kwamba ninapelekwa wapi pia sikuhitaji kuonyesha wasiwa wangu usoni. Tukaingia kwenye moja ya ofisi, nikakuta wakuu wa jeshi wapatao sita wakiwa na vyeo vya juu kabisa.
“Kaa pale”
Mwanajeshi mmoja niliye kuja naye alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu nikatembea hadi kwenye kiti walicho niomba nikae kisha wanajeshi hawa wawili wakatoka ndani ya ofisi na kuniacha na walinzi hawa.
“Habari yako dokta Lameck David?”
“Salama tu”
“Tunatambua machango wako katika katifaa, muda mchache tumeweza kuangalia kikao chako ulicho kuwa unazungumza na raisi pamoja madaktari, ila tunakuomba kukuhoji maswali mawili matatu kama huto jail”
Mzee mmoja mweusi alizungumza huku akiwa amenikazia macho usoni mwangu. Kwa kujiamini nikaanza kutazama kila sura ya kiongozi hawa wa jeshi waliomo humu ndani, kisha nikashusha pumzi kimya kimya pasipo mtu yoyote kuweza kugundua kwamba ninaouondoa wasiwasi wangu moyoni mwangu.
“Kabla hujaniuliza swali lolote muheshimiwa. Ningependa kufahamu kwamba kikao hichi raisi anakifahamu?”
Wakuu hawa wajeshi wakatazamana kisha mzee ambaye ndio muongeaji tangu nifike humu ndani akanijibu.
“Ndio raisi anakitambua hichi kikao”
“Ningeomba nizungumze naye kwenye simu ili niweze kukubaliana nanyi kwa kile munacho kizungumza”
“Kwa nini unahitaji kuzungumza na raisi?”
Mzee mwengine alizungumza baada ya kuona ukimya ulianza kuchukua nafasi yake.
“Nimekuja hapa kwa mamlaka ya raisi, nilizungumza naye kwenye kikao na amenipa majukumu ya kufanya. Mmekuja kunichukua nikiwa katikati ya kazi ambayo nimekabidhiwa na raisi, ndio maana nikahitaji kuzungumza na raisi”
“Dokta Lameck tulikuita hapa kwa dakika japo tano, tulihitaji kuhoji maswali mawili matatu”
“Siwezi kujibu maswali yenu pasipo idhini ya muheshimiwa raisi kwa hiyo ninawaomba munirudishe kule mulipo nitoa nikaendelee na kazi yangu kwa maana timu yangu haiwezi kufanmya kazi pasipo mimi”
Wazee hawa wakaka kimya kwa maana akili zao nilisha zisoma kwa haraka sana ndio maana nikaamua kuwakatisha kwa kigezo cha kuhitaji kupata jibu kutoka kwa raisi, kutokana na kikao hichi kuto kuwa na uhalali wowote.
“Munaweza kuingia”
Mzee ambaye alikuwa ni mzungumzaji alizungumza kwa sauti ya msisitizo huku akiwa ameminya batani kwenye simu iliyopo juu meza. Wakaingia wanajeshi ambao walinileta humu ndani.
“Mrudisheni maabara”
“Sawa mkuu”
Nikanyanyuka kwenye kiti nilicho kalia, moja kwa moja nikaongozana na wanajeshi hawa nilio kuja nao. Moja kwa moja tukarudi maabara na kuwakuta Cajoli wakinisubiria. Wanajeshi hawa walipo funga mlango na kuondoka, Cajoli akanifwata kwa haraka na kunikumbatia kwa nguvu huku akiwa amejawa na furaha.
“Wamekuambiaje?”
“Nilikutana na viongozi wa jeshi walihitaji kunihoji maswali ila nikakataa kuhojiwa”
“Umekataa!!?”
“Ndio nimekataa kutokana sio kikao rasmi”
“Kivipi shem?”
“Ni kikao ambacho kimeitishwa na viongozi hao wa jeshi, ila raisi alikuwa hakifahamu”
“Hapo umefanya jambo la muhimu sana mume wangu. Sasa tumesha weka dawa katika chupa zote ambazo ulihitaji tuziweke maji. Zipo tayari kwa kutumika”
“Tunahitaji kuzungumza na raisi sasa, tumuambia kwamba kazi imekwisha kilicho baki ni dawa hii kusambazwa kwenye vyanzo vyote vya maji mikoani mwote”
“Sawa”
“Ngoja nikazungumze naye”
“Sawa”
Nikafungua mlango wa maabara na kutoka, nikamuuliza mlinzi mmoja sehemu ambayo ninaweza kumuona raisi. Akaniomba niongozane naye hadi kwenye ofisi, akazungumza na walinzi wa raisi, mmoja akaingia ndani ya hii ofisi iliyo tengenezwa kuta zake kwa vioo. Idadi ya viongozi waliomo ndani ya ofisi hii ninao waona kwa nje wanafika kumi na tisa, wengi wao wamevalia mavazi ya jeshi, huku ni wachache sawa ndio wamevalia suti. Nikamuona mlizi wa raisi akimnong’oneza K2 masikioni. K2 akanitazama kisha taratibu akanyanyuka kwenye kiti na kutoka nje na mlinzi wake.
“Ndio dokta Lameck”
“Kazi imakamilika muheshimiwa raisi”
“Dawa mumetengeneza katika muundo gani?”
“Muundo wa maji, ambayo yatamwagwa katika vyanzo vyote vya maji kwa kila mkoa, na maji hayo yatakapo samba, yataua kila kirusi kinacho patikana kwenye maji na wananchi wakitumia baada ya nusu saa watapona”
“Safi sana daktari basi itabidi chupa hizo zikabidhiwe kwa wakuu wa mikoa na kazi ianze kufanyika usiku huu huu”
“Ni kweli muheshimiwa”
“Ninashindwa kuongozana na wewe kwa maana nina kikao muhimu sana, nchi ipo katika kushambuliwa?”
“Kushambuliwa?”
“Ahaa wewe ni daktari haya ni mambo ya ulinzi zaidi, kwa hiyo sio vyema nikakuelezea”
“Sawa ila kama kutakuwa na mbinu yoyoyote ya kuwasidia ninaweza kuwasaidia”
“Hakuna tatizo. Anjelina ongozana na daktari Lameck hadi maabara atakupa kazi ya kufanya. Ukimalizia hakikisha munawapeleka yeye na timu yake katika chumba cha kupumzikia”
“Sawa muheshimiwa raisi”
Nikaongozana na mmoja wa walinzi wa raisi moja kwa moja tukaelekea hadi kwenye maabara, nikampa maelekezo ya kitu gani kifanyike akatii.
“Raisi ameniambia kwamba nchi ipo katika kushambuliwa”
“Ipo katika kushambuliwa, kivipi?”
“Hakuniambia kwa undani sana, ila kutokana tumeshapata mkwanja wetu ambao tuliukusudia kilicho baki ni kurocha rocha”
“Ndio nini shem?”
“Kuondoka”
“Hahaa haki ya Mungu kumbe shem una maneno ya kihuni namna hiyo?”
“Furaha tu”
“Tunaweza kwenda chumba cha mapumziko”
Mlinzi wa K2 alizungumza, tukatoka naye na kuongozana naye kweneye kordo zilizopo humu ndani ya ikulu. Kitu ambacho kinanishangaza ni hekaheka za wafanyakazi wa ikulu. Kila mmoja anaonekana kuwa bize sana usiku wa siku ya leo.
“Kuna kitu gani kinacho endelea dada?”
“Hakuna kitu dokta”
“Kweli dada?”
“Ndio daktari, nilicho agizwa ni kuwapeleka katika chumba cha kupumzikia na hapo munaweza kumsubiri raisi”
Angelina alizungumza kwa sauti ya msisitizo na kutufungulia katika chumba ambacho amegizawa tuweze kuwepo. Chumba hichi telvishion kubwa, masofa pamoja na friji kubwa.
“Tunashukuru”
“Karibuni sana”
Angelina alizungumza na kuondoka, shem Cajoli akajitupa kwenye kitanda huku akiwa na amechoka.
“Tumesha kuwa mabilionea jamani. Huu siamini”
Shem Cajoli alizungumza huku akijilaza vizuri kwenye sofa alilopo.
“Mungu ni mwema, ninaamini mimi na mume wangu hapa tunakwenda kufunga bong…………”
Cajoli hakumalizia sentensi yake, soite tukajikuta tukistushwa na mtetemesho mzito wa ardhi.
“Ni nini hicho mume wangu”
Cajoli alizungumza huku akinikimbilia na kunikumbatia.
“Lala kwenye sofa”
Nilizungumza huku nikimlaza Cajoli kwenye sofa.
“Ninawaomba munisubirie hapa hapa ninakuja”
“Dany”
Cajoli aliniita jina ambalo hatukukubaliana kuniita, sikumjibu kitu chochote zaidi ya kuufunga mlago kwa nje. Kila mtumishi wa ikulu, anakimbia kuelekea anapo pafahamu yeye. Walinzi wa raisi nao wapo bize katika kukatiza kila kona ya hii ikulu, ikiashiria kwamba hali kwa sasa ipo mbaya.
“Dada, dada, dada kuna nini huko nje?”
Nilimuita dada mmoja huku nikimshika mkono kwa maana yupo katika harakati za kuyaokoa maisha yake.
“Magaidi, magaidi”
“Wapo wapi?”
“Waneivamia ikulu”
“Mungu wangu!!”
Nilijikuita macho yakinitoka, kwa haraka nikarudi ndani ya chumba ambacho nimewaacha Cajoli na shemeji.
“Tunatakiwa kuondoka hili eneo sasa hivi”
“Kuna nni huko nje Dany?”
“Ikulu imevamiwa na magaidi”
“Imevamiwa na magaidi?”
“Ndio, hatuna muda wa kuzungumza, tutafute njia ya kuondokea hapa ikulu haraka iwezekanavyo”
Nilizungumza huku jasho likinimwagika usoni mwangu. Taratibu nikaanza kutembea kwa mwendo wa tahadhari hadi mlangoni. Nikaufungua mlango na kuchungulia nje, nikaona watu walio valia nguo nyeusi wakipambana na kikosi cha walinzi wa raisi.
“Jificheni nyuma ya masofa hakikisheni munanisubiria hapo”
“Shemeji ninakuomba twende wote”
“Hapana baki na Cajoli”
“Shemeji mimi nipo vizuri sana kwenye maswala ya upambanaji kwenda peke yako inaweza kuwa hatari sana kwako”
“Ok Cajoli baki hapo sawa?”
“Sawa”
Cajoli alinijibu huku machozi yakimwagika usoni mwake. Kitu nilicho kigundua kwa mke wangu, ni mwepesi sana kwenye swala la kumwagikwa na machozi. Tukatoka na shem Cajoli na kuanza kutembea kwa tahadhari kwenye kordo hii, huku macho yetu yakiangaza huku na kule kutafuta bunduki kwa maiti yoyote ambayo imepigwa risasi. Nikabahatika kupata bastola mbili, kutoka kwa mlinzi mmoja wa raisi niliye mkuta ameuwawa.
“Chukua hii”
Nilizungumza huku nikimkabidhi shem Cajoli bastola mmoja, taratibu tukaanza kutembea kwa kunyata na kwa umakini katika hii kordo.
“Shem tunakwenda wapi?”
“Kumtafuta K2”
“Shem ngoja kwanza, K2 ni wa kazi g
ani kwa sasa. Kwa nini tusitafute njia ya kuondokea humu ndani”
“Cajoli huu ndio muda wangu wa kuhakikisha kwamba ninaiondoa roho ya K2, sina nafasi nyingne nitakayo ipata kwenye maisha yangu zaidi ya hii”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwa nimekazia macho shem Cajoli, usoni mwake, hakuwa na cha kubisha zaidi ya kutingisha kichwa kukubali kwa kile nilicho kizungumza mimi.
==>>ITAENDELEA KESHO
↧
Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 10
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
“Bora na wewe umeona, wezako hapa wana shangaa. Sasa tuzungumzeni biashara, munamsajili au niondoke na kijana wangu akawe zao la timu nyingine”
“Weee tukikataa nahisi tutakuwa wendawazimu, mtu unaona kwamba tumeletewa Mess alafu tumkatae. Klopp mimi nipo tayari mkusajili”
“Kiwango cha chini ni paund milioni kumi kama munapesa tuingie mezani, ila kama hamuna kesho nina panda naye ndege ninaelekea naye Hispani na huko munafahamu kuna mapapa wakubwa R. Madrid na Bacelona”
“Klopp kumbuka wewe hapa una heshima, usitufanyie hivyo bwana?”
“Nina heshima, ila huku anakwenda kuvunja rekodi na heshima yangu, siwezi kumuachia bure kwa maana ni zao langu hili na si lenu”
Mzee Klopp aliendelea kushikilia msimamo wake wa kuhitaji kuniuza katika timu hii jambo ambalo ni jema sana kwenye maisha yangu ya mpira nikiwa bado ni kijana mdogo wa miaka saba.
ENDELEA
Viongozi hawa wa hii timu ya Dotmund wakaa kimya huku wakitutazama mimi na mzee Klopp.
“Basi tutalizungumza mzee Klopp”
“Sawa, munamruhusu kijana wangu akaendelee na mazoezi yenu au tuondoke?”
“Muache tu aendelee na mazoezi hakuna tabu”
Kocha wa timu ya vijana alizungumza huku akiwa na tabasamu sana. Nikarudi uwanjani na nikaendelea kuonyesha uwezo wangu mara mbili hata na mara ya kwanza nilipo kuwa nikicheza kwa maana nimesikia kiwango cha pesa kilicho tajwa kwa ajili ya mimi kununuliwa. Hadi tunamaliza mazoezi tayari nimefunga goli nane peke yangu huku nikitoa mchango wa goli mbili. Kila mchezaji akatokea kunipenda huku wachezaji wengine wakubwa wakiomba kupiga nami picha. Hapa ndipo nilipoa anza kuigundua nguvu niliyo nayo kwa maana wachezaji vijana wao ndio huwaomba wachezaji wakubwa kupiga nao picha, ila kwangu imekuwa tofauti ya hivyo. Nikapiga picha na wachezaji karibia wote huku wengine wakinionyesha video za magoli ambayo nimeyafunga.
“Hei Ethan”
Mchezaji mmoja mkubwa aliniita na akasogea na mimi pembeni.
“Unajua nini juu ya hii Club?”
“Hii Club alicheza baba yangu mzee Klopp yule pale”
“Hilo ndio unalo lijua?”
“Ndio”
“Una kipaji kikubwa sana, tena sana mdogo wangu. Ninacho kushauri usikubali kusajiliwa katika timu hii, ligi yetu ya hapa Ujerumani bado haijapata nguvu kama ligi ya nchini Uingereza na Hispania. Mshauri baba yako akupeleke ukafanye tena majaribio kwenye timu kubwa kama Liverpool, Man City, Man United, Arsenal, Madrid au Bacelona. Nakuhakikishia baada ya miaka mitano mbeleni utakuwa bilionea sawa”
“Sawa kaka”
“Liweke hilo akilini na usimuambie mtu mwengine zaidi ya baba yako”
“Sawa”
Mchezaji huyu akanikunjia ngumi mkono wake wa kulia, nami nikakunja nguni na kuzigonganisha, kisha kaniruhusu kuelekea kwa baba yangu mzee Klopp.
“Ethan”
“Ndio baba”
“Una kipaji sana leo umenitoa kifua mbele kwenye hii club”
“Asante sana baba”
“Mazoezi mengi, kujituma na heshima hilo ndio jambo kubwa na la muhimu sana kwenye mpira wa miguu. Zingatia hayo pasipo kumuangalia mtu wala pasipo kupenda umaarufu. Si unaona watu wanakufwata wenyewe?”
“Ndio baba”
“Ukijitahidi katika hayo, kila jambo litakwenda kufanikiwa kwa upande wako sawa”
“Sawa baba”
“Sanamu ambayo nilikuwa ninaizungumzia muda ule ndio hii hapa”
Mzee Klopp akanionyesha sanamu moja kubwa sana inayo fanana na yeye, ila hii inamuonyesha enzi zake akiwa mchezaji.
“Aliye ichonga hii sanamu ni nani?”
“Ni mmoja anaitwa Karius, ila kwa sasa ni marehemu, yeye ndio aliitengeneza hii sanamu na kuiuza kwenye hii Club, ni heshima kubwa sana kwangu kuwekwa kama hivi. Naamini kwamba na wewe siku moja ukiwa mtu mwenye makamu kama yangu basi nawe utawekwa kama hivi”
“Nitahakikisha baba, sanamu langu linakuwa kubwaaaa kupiga hata hili la kwako”
“Hahaaa hilo ndio jambo ninalo hitaji kulisikia nahitaji uvunje rekodi ya mchezaji mmoja hapa duniani ambaye hadi sasa hivi haijawahi kuvunjwa”
“Mchezaji gani baba?”
“Anaitwa Edson Arantes do Nascimento”
“Heee ndio nani huyo!?”
Niliuliza huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana.
“Jina lake maarufu anaitwa Pele. Ni mchezaji maarufu duniani kwa kipindi chote toka karne ya ishirini hadi sasa. Hakuna mchezaji ambaye aliweza kuivunja rekodi yake ya magoli”
“Kwani amefunga magoli mangapi?”
“Magoli elfu moja na sabini na nne”
“Mmmmm”
“Ndio kwa umri wako unaweza kuyafikia. Hakikisha kwamba una yafikia na kuyapita”
“Baba ila magoli elfu ni mengi sana”
“Nalitambua ila kila mechi ukiweka wastani wa kufunga magoli matatu. Ukicheza mechi mia tatu hamsini na nane utakuwa umeyafikisha hayo magoli.”
“Duu”
“Yaa unajua mpira ni kama familia. Jinsi unavyo panga idadi ya watoto wako unao wataka kuzaa na kuwalea ndivyo jinsi utakavyo panga jinsi ya kufunga. Hakikisha kwamba kila unapo ingia uwanjani unaweka nia na kunuwia kwamba ni magoli mangapi ambayo una yahitaji, kufunga kwa siku hiyo. Endapo una pata nafasi funga kama leo ulivyo funga magoli nane sawa”
“Sawa baba”
“Nakuambia mambo haya, sikuwahi kumuambia mchezaji wangu yoyote hata pale nilipo kuwa kocha. Fanyia kazi haya maneno yangu, utaona jinsi dunia itakavyo kuheshimu sawa”
“Sawa baba”
Mzee Klopp akaendelea kunitembeza katika maeneo tofauti tofauti ya uwanja huu mkubwa wa mpira. Baada ya kumaliza matembezi haya, akanipeleka kwenye mabafu nikaoga na kuvaa nguo zangu. Safari ya kurudi nyumbani ikaanza taratibu.
“Baba nina weza kukuuliza sawali?”
“Ndio unaweza kuwa huru”
“Hivi ni club gani ambayo kwa mtazamo wako unaweza ona nitafanikiwa kufikisha kiwango hicho cha magoli hapa duniani?”
Mzee Klopp akaka kimya kidogo huku akionekana kulifikiria swali nililo muuliza.
“Club kubwa?”
“Ndio baba”
“Kusema ukweli, ukicheza nje ya hapa Ujerumani, hilo linawezekana kwa maana ligi ya huku, moja ni ngumu sana, pili ina wendawazimu wengi sana ambao, wao hawato ona huruma kukuvunja wewe miguu na wao wakapewa kadi nyekundu zitakazo waweka nje ya uwanja kwa baadhi ya mechi tu kisha wao wakarudi, ila wewe utaendelea kuuguza majeraha”
Mzee Klopp alizungumza kwa upole sana na umakini wa hali ya juu.
“Ligi ya Uhispania, kule kwa sasa kuna wafalme wawili tu wanao onekana kuliko wachezaji wengine. Wao ni Ronaldo na Messi. Hadi ukiwa mkubwa wewe hawa watu watakuwa wamesha stafu kucheza, ila kwa ligi ya Hispani siipendi sana japo ina pesa nyingi”
“Je ligi ya Uingereza?”
“Uingereza ligi yake haieleweki, haina mbabe, timu inaweza kupanda daraja na ikachukua ubingwa. Niligi yenye ushindani mkubwa sana naamini kwa wewe itakufaa kama kweli utakuwa unaipenda sana ligi hiyo”
“Ninaweza kukuomba kitu?”
“Ndio niombe mwanangu”
“Unaonaje ukanipeleka Uingereza nikafanya mazoezi japo kwenye timu moja wapo kubwa ili uangalie wapi wataweka kiasi kikubwa waninunue?”
“Hilo ni wazo moja zuri sana. Hakika wewe una akili sana, sikukaa na kulifikiria hilo, moyo wangu na mapenzi yangu niliyaelekezea Dotmund. Ila kutokana kwa sasa mpira ni biashara na fursa ya kutengeneza historia yako binafsi nitakupelekea jijini Liverpool ukajiunge na majogoo hao wa London kwa kufana mazoezi, ukipita hakuna shaka kwa maana utakuwa upo katika timu salama”
“Sawa baba”
Tukafika nyumbani na kumkuta Merry na mama wakiwa na furaha sana ambayo kwa haraka haraka wanaonekana kuna jambo wameliona.
“Yaani Ethan kwenda tu huko leo, ona ulivyo zagaa kwenye mitando ya kijamii, tazama jinsi wachezaji wakubwa walivyo weka picha zako Instergram”
Mery alizungumza huku akionionyesha picha hizo kwenye simu yake.
“Tena honey kuna habari nyingine nzuri sana”
Bibi Jane Klopp alizungumza.
“Kuna simu mbili moja imetoka nchini Hispania, raisi wa Real Madrid anahitaji kuzungumza na wewe na simu nyingine imetoka Uingereza, tajiri wa Chelsea Roman Abramovich wote wanahitaji kuzungumza juu ya Ethan”
Mzee Klopp akanitazama huku akiwa ametabasamu kwa furaha sana.
“Tena wamesema ikiwezekana wakutumie hata private jet uende na Ethan katika hizo timu”
Nikamuona mzee Klopp akiwa kama amewehuka kwa furaha, mara azunguke huku mara achukue simu ya hapa sebleni mara airudishe.
“Wametumia simu ile ya nyumbani”
“Niletee”
Bibi Jane Klopp akaanza kutembea kuelekea ndani huku akiwa katika mwendo wa haraka haraka. Kusema kweli furaha imenijaa sana moyoni mwangu. Bibi Klopp alirudi hapa sebleni haraka haraka huku simu hiyo ikiwa inaita.
“Ni namba kutoka Uingereza”
“Uingereza?”
“Ndio mume wangu?”
Mzee Klopp akaichukua simu hiyo, akaipokea na kuiweka sikioni mwake.
“Ndio”
“Sawa”
“Tutakuja”
“Basi nitawapa maelezo yapi ya kufwata”
“Sawa sawa”
“Haya”
Mzee Klopp akakata simu na kuanza kushangilia seble nzima hadi sote tukaanza kumcheka.
“Ethan ndoto yako imekuwa kweli”
Mzee Klopp alizungumza huku akininyanyua na kunikumbatia.
“Unakwenda Liverpool”
“Kweli baba”
“Niamini, acha kwanza tukazungumze na timu ya Liverpool”
Mzee Klopp aliendela kuzungumza huku akiwa amenibeba.
“Muweka mwenzako chini usije ukamuangusha”
“Siwezi kumuangusha kabisa, sasa inabidi muanze kumuandalia nguo, leo nina panga utaratibu wa ndege yao wanayo ituma kisha kesho tunaanza safari kuelekea Uingereza sawa”
“Sawa baba”
Niliitikia nikiwa na furaha sana. Mery akaniita na kuninong’oneza.
“Usiondoke pasipo kumuambia chochote Camila”
“Ninaweza kuwasiliana naye kupitia simu yako?”
“Ndio”
Mery akanipatia simu yake na nikakimbilia chumbani kwangu. Nikampigia Camila kupitia simu ya mama yake, akapokea, nikamsalimia mama yake na kwa bahati nzuri hakuwa mbali na Camila.
“Ethan mbona leo una furaha sana?”
“Nimeitwa katika kikosi cha watoto cha timu ya Liverpool jijini London”
“Ethan acha utani?”
“Haki ya Mungu vile baba ametoka kupigiwa simu sasa hivi”
Camila hakunijibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya.
“Halooo”
“Ethan?”
“Ndio mpenzi wangu”
“Huto niacha kweli ukienda huko?”
Camila alizungumza kwa unyonge sana hadi furaha yangu ikaanza kunipotea.
“Mpenzi wangu, siwezi kufanya chochote kibaya juu ya penzi letu”
“Ethan najua ni jinsi gani ninavyo kupenda, ukienda huko ni lazima wahitaji ubaki huko huko, na mimi sitaki mpenzi wangu iwe hivyo”
“Nakuapia Camila kwa jina la Mungu, siwezi kukusaliti. Najua unapenda kuniona ninafanikisha ndoto zangu, nakuomba unipe nafasi yenye baraka niweze kufanikisha ndoto zangu mpenzi wangu sawa”
“Sawa Ethan, ukienda kesho munarudi lini?”
“Sijajua kwa maana ninakwenda kufanyiwa majaribio ya kwanza, nikiwanikiwa basi tutajua ni lini nitatakiwa kurudi tena Uingereza”
“Ila Ethan kuwa makini, sasa hivi utanipoteza kabisa duniani kwa maana nina kupenda sana”
“Siwezi kukupoteza wewe ni wangu tu”
“Kweli?”
“Ndio mpenzi wangu”
“Sawa tutazungumza usiku sasa hivi tunajiandaa na mama tunataka kwenda mjini kwenye maduka”
“Poa nina kupenda Camila”
“Ninakupenda Ethana wangu mwaaaa”
“Asante mpenzi wangu”
Camila akaka simu na kunifanya nijawe na furaha sana moyoni mwangu, ndoto za kuwa mchezaji mkubwa duniana zinaanza kutimia taratibu.
‘Ethan”
Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu, ikiniita nyuma yangu ambaye uhalisia wake ni jini.
“Shitii umenistua sana”
‘Nisikilize sina muda mwingi sana. Kesho usiende hiyo safari kwa maana mukifika nchini Uingereza mmoja wenu kati ya baba yako au wewe atapigwa risasi na kufa hivyo musiendeee”
Maneno ya Ethan yakanistua sana moyo wangu, hakuhitaji hata nimuulize swali, akapotea mbele ya upeo wa macho yangu na kunifanya niwe katika wakati mgumu sana ulio iyeyusha furaya yangu mithili ya barafu katika jua kali.
==>>ITAENDELEA KESHO
↧
Shirika La Marie Stopes Tanzania Laruhusiwa Kuendelea Kutoa Huduma Zake Hapa Nchini
↧
PICHA: CHADEMA Wanunua Magari Mapya Ambayo Wameyaonesha Rasmi Leo
Chama cha Demokrasia na Maendeleo,Chadema, leo Jumatano October 17 kimeonyesha magari yake aina ya Ford Ranger ambayo yatatumika katika shughuli za kukiimarisha chama hicho na kukirejesha kwa wananchi.
Msemaji wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Tumaini Makene ameseama magari hayo yatatumika katika chaguzi na utekelezaji programu ya Chadema msingi..
Msemaji wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Tumaini Makene ameseama magari hayo yatatumika katika chaguzi na utekelezaji programu ya Chadema msingi..
↧
↧
Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.
Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa
MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )
YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,
SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.
LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.
WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0759208637 / 0622344969
↧
Alichokiongea Leo Kardinali Pengo Wakati Akiongea na Waandishi wa Habari
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo amesema injili peke yake haitoshi kuhubiri amani bali kuna taasisi nyingine ikiwemo serikali na dini nyingine ambazo zinapaswa kusimamia suala hilo.
Kardinali Pengo ametoa kauli hiyo leo Ofisini kwake St.Joseph, jijini Dar es salaam wakati akiongea na wanahabari ikiwa ni kuelekea sherehe ya miaka 150 ya usambazaji wa injili nchini ambayo ilianzia mjini Bagamoyo.
“Shughuli za kuinjilisha zinaendelea katika mfumo wa kibinadamu, kwanza injili haiko peke yake kwenye sehemu yetu ya Tanzania bara na maeneo mengine, kama wadau wa amani na maelewano, tuna sababu za kutokuwa na maelezo kwenye vitu vingine mnavyovisema kama chokochoko ”, amesema.
“Huwezi ukasema ni failure (kushindwa) ya uinjilishaji peke yake kwa sababu wadau wa amani ni pamoja na serikali watu wa dini na madhehebu mbalimbali, wote tunagombania amani, wote tunategemea watu kupiga hatua.”Ameongeza Kardinali Pengo.
Aidha, Kardinali Pengo amesema mbali na changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwenye jamii ni vyema watu wakatambua umuhimu wakutunza misingi ya umoja na amani iliyopo ili kuweka kizazi kijacho katika mazingira bora ya upendo na mshikamano huku akionesha kusikitishwa na vitendo vya baadhi ya Makanisa kuwa na migogoro ambayo inapunguza imani ya waumini kwenye makanisa yao
Kardinali Pengo amesema wanakwenda kuadhimishia Bagamoyo mkoani Pwani kwa sababu Injili ndiko ilianzia.
↧
Wanafunzi 25,532 Wapangiwa Mikopo Katika Awamu Ya Kwanza
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwafahamisha waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kuwa imetoa orodha ya Awamu ya Kwanza yenye jumla ya waombaji wa mwaka wa kwanza 25,532 waliopangiwa mikopo yenye thamani ya TZS 88.36 bilioni.
Akitangaza orodha hiyo leo (Jumatano, Oktoba 17, 2018) jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru amesema kati ya wanafunzi hao, wanaume ni 16,085 na wanawake ni 9,447.
Bw. Badru ameongeza kuwa katika awamu hiyo ya kwanza HESLB pia imetoa mikopo yenye thamani ya TZS 850.35 milioni kwa watanzania wanafunzi 69 wanaoendelea na masomo nje ya nchi chini ya makubaliano maalum na nchi rafiki zipatazo saba ambazo ni Msumbiji, Algeria, Cuba, Urusi, Serbia, Urusi na Ujerumani.
Bajeti ya TZS 427.5 bilioni zimetengwa kwa mikopo ya elimu ya juu 2018/2019
Katika mkutano huo, Bw. Badru ameeleza kuwa bajeti ya fedha za mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2018/2019 ni TZS 427.5 bilioni na tayari Serikali imeshatoa TZS 137.06 bilioni zinazohitajika wakati vyuo vinafunguliwa mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba na mwezi Novemba (2018). Kwa ajili ya kuwakopesha wanafunzi wapya na wanaoendelea na masomo wapatao 123,285.
“Fedha nyingine tutazipokea baadaye katika robo ya pili ya mwaka wa fedha kwa ajili ya malipo ya wanafunzi watakaopangiwa mikopo … kwa hiyo kwa sasa, tuna fedha tunazohitaji kwa waombaji wote wenye sifa,” amesema Bw. Badru katika mkutano uliohudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Uchambuzi na Upangaji Mikopo wa HESLB Dkt. Veronica Nyahende.
Kuhusu kutangaza Awamu ya Pili
Bw. Badru amesema kuwa HESLB itaendelea kutoa awamu nyingine za orodha za wanaopangiwa mikopo kadri itakavyokamilisha uchambuzi wa orodha za wanafunzi walioomba mikopo na ambao pia wamepata na kuthibitisha udahili wao katika chuo kimoja ili kuhakikisha fedha za mikopo zinawafikia wanafunzi wahitaji katika vyuo walivyothibitisha.
Upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wa mwaka wa pili na kuendelea
Aidha, Bw. Badru amesema kuwa wanafunzi wenye mikopo na wanaoendelea na masomo wataendelea kupata mikopo ikiwa wamefaulu mitihani yao na matokeo yao kuwasilishwa HESLB na vyuo husika.
“Tunatoa mikopo ili mwanafunzi asome, kwa hiyo tutaendelea kuwapa mikopo wanafunzi wenye mikopo na wanaendelea na masomo ikiwa tumepokea uthibitisho kuwa ana sifa za kuendelea na masomo katika mwaka unaoanza hivi punde,” amesema Bw. Badru.
Upatikanaji wa orodha kamili ya waliopangiwa mikopo
Majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo katika awamu hii ya kwanza yataanza kupatikana baadae leo katika mtandao wa HESLB wa uombaji mkopo (https://olas.heslb.go.tz) na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha ya majina hayo pia zinatumwa vyuoni kwa ajili ya kurahisisha taratibu za usajili wa wanafunzi hao.
Lengo la Bodi ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wenye sifa ya kupata mikopo katika mwaka wa masomo 2018/2019, wanapangiwa mikopo kabla vyuo kufunguliwa mwishoni mwa mwezi Oktoba, mwaka huu (2018).
Aidha, Bodi inapenda kuwasihi waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa kwa awamu inayofuata ukiendelea.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano,
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Jumatano, Oktoba 17, 2018
↧
More Pages to Explore .....