Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

BREAKING NEWS | Waziri Kangi Lugola akizungumza na waandishi wa habari

0
0

BREAKING NEWS | Waziri Kangi Lugola akizungumza na waandishi wa habari


Nchi Iko Salama, Polisi Wanaendelea Kumtafuta Mo Dewji

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola,  leo amesema nchi ipo salama na Watanzania waendelee na shughuli zao za kijamii, kiuchumi na kisiasa kwani serikali imejipanga vizuri katika kushughulikia matukio yote ya uhalifu yanapojitokeza.

 Lugola, amesema Jeshi la polisi linaendelea na mchakato wa kumtafuta mfanyabiashara maarufu Mohammed Dewji "Mo Dewji" aliyetekwa siku ya Alhamis Oktoba 11,2018 jijini Dar es slaam.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo, Kangi amesema takribani watu 20 wanashikiliwa na jeshi la polisi ili kusaidia kutoa ushirikiano wakati wakiendelea kuwasaka watu wote waliohusika na tukio la utekaji ikiwemo kumpata Dewji mwenyewe.

''Niwahakikishie watanzania, jeshi la polisi linaendelea kushughulikia tukio la kutekwa kwa Mohamedi Dewji, likiwasaka waliomteka na tutahakikisha wanapatikana, ambapo hadi sasa navyozungumza takribani watu 20 wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano'', amesema.

Mh. Lugola pia amemtaka IGP Simon Sirro kutoa maelekezo kwa askari wake, kuwaachia ndani ya saa 24 watu wanaowashikilia kwa uchunguzi kuhusiana na kutekwa kwa Mohammed Dewji mara baada ya kuwahoji na kubaini hawana taarifa kamili.

Aidha akisoma taarifa ya matukio ya uharifu yaliyotokea nchini tangu mwaka 2016, Kangi amesema jeshi la polisi linaendelea kuwashikilia watuhumiwa wa matukio ya kiharifu na kuwataka wananchi kuacha minong'ono kwamba serikali na vyombo vya usalama havifanyi kazi ipasavyo.

Mwaka 2016 Watu 5 kati ya 9 waliokuwa wametekwa walipatikana wakiwa hai, huku watu 27 waliotekwa  mwaka 2017, 22 wamepatikana huku watatu wakiwa hawajapatikana.

Aidha takwimu za watoto walioripotiwa kupotea kuanzia Januari hadi Oktoba mwaka huu ni 21, ambapo watoto 17 wamepatikana wakiwa hai na watoto 4 hawajapatikana hadi sasa.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 99 na 100 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588 
ILIPOISHIA     
Nikachukua simu nyingine ya Cajoli, akanikabidhi na funguo za gari lake kisha nikaondoka. Safari ya kuelekea katika hoteli ya Mkonge hoteli haikuchukua muda mrefu nikafika, nikasimamisha gari kwenye maegesho, simu ya mfukoni mwangu ikaita ikanibidi kuitoa simu na kuipokea huku nikiwa nimesimama pembeni ya gari langu.
“Dany umefika”   
Niliisikia sauti ya Cajoli akizungumza kwenye simu, ila kabla sijajibu nikahisi kitu kizito kikinigandamiza kichwani mwangu huku nikisikia sauti nzito ya mwanaume ikiniamrisha kwamba nisigeuke nyuma la sivyo atanichangua ubongo wangu.

ENDELEA
“Dany”   
Sauti ya Cajoli ikaendelea kusikia kwenye simu ikiniita jina langu, sikuweza kumjibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya na kusikiliza amri ya mtu huyu aliye simama nyuma yangu.
“Rudi nyuma”
Alizungumza tena, nikafanya kama anavyo hitaji, taratibu nikaanza kurudi nyuma kwa hatua ndogo ndogo.
“Ingia kwenye gari”
 
Mtu huyo alizungumza na kunifanya niingie kwenye gari jengine ambalo lipo pembeni ya gari ambalo nimekuja nalo na ninahisi huyu mtu aliweza kuniona kipindi ninashuka kwenye hili gari  langu.
Nikautazama mlango wa gari hili ulio funguliwa, taratibu nikaingia, jamaa wa nje akafunga mlango na taa iliyopo ndani ya gari hili ikawashwa. Pembeni ya siti ambayo nimekaa nikamkuta John akiwa anatabasamu.
“Vipi DANY?”
John alizungumza akiwa amejawa na furaha nyingi usoni mwake. Jambo ninalo jiuliza ni jinsi gani ambavyo Jonh amweza kufahamu sehemu mimi nilipo wakati nilitoroka hospitali nchini Kenya pasipo kuweza kumuambia mtu yoyote.
 
“Safi tu”
“Naona hospitalini uliondoka kinyume na makubaliano yetu?”
“Nikuulize swali?”
“Yaa kuwa huru tu”
“Huwa sipendi kuishi kwa kufwata amri ya mtu yoyote kwenye maisha yangu. Ndio maana mipango yote ninayo kwenda kuifanya ninahitaji kuifanya mimi peke yangu”
“Hhaaaa Dany unanihitaji mimi, unahitaji msaada wangu pasipo mimi utaumia kwa maana watu unao kwenda kupambana nao sio wadogo, ni watu ambao wameishika hii nchi”
 
“Sikia broo ninajiamini kwa kile ninacho kwenda kukifanya so ninakuomba usiingilie mipango yangu sawa”
Nilizungumza kwa kufoka, cha ajabu John hakuonyesha kukasirishwa na maneno yangu, akabaki akiwa anatabasamu tu.
“Dany wewe bado ni mdogo sana, usihitaji kuumia peke yako. Tupo kaka zako tuna uwezo wa kukusaidia, tupe nafasi ya kukusaidia”
 
“Jibu ni hapana, wewe ufahamu ni machungu gani ambayo ninayo kwa mauaji ya familia yangu”
“Dany kila jambo halihitaji kutumia hasira. Kila jambo linahitaji utulivu, jambo la muhimu kwa hivi sasa ni kuhakikisha kwamba unatumia akili kubwa kuliko kutumia hasira. Wewe ni professional training agent so huwezi kutumia hasira kwenye mission ambazo unataka kuzifanya”
“Ninajua ni nini ninacho kifanya, ninakoomba uniache niondoke”
 
“Ok sihitaji kukubana ila ukihitaji msaada wangu, chukua hii kadi yangu ina namba zangu za simu”
Nikaangalia bussines card ambayo ananipatia John, nikaichukua kisha nikashuka kwenye gari. Mlinzi wa John akaingia kwenye gari na kuondoka eneo hili na kuniacha nikiwa nimesimama nikilisindikiza gari hilo kwa macho jinsi linavyo ondoka katika eneo hili. Simu yangu ambayo bado ipo mkononi mwangu ikaita tena wala sikufahamu ni muda gani ambao Cajoli alikata simu.
“Ndio”
“Dany upo Salama mume wangu?”
“Yaa nipo salama, kuna mambo nilikuwa ninayafanya”
“Lile gari limeosha ondoka hapo hotelini na lipo katika barabara ya kuelekea Raskazoni”
 
“Nimekupata, ila sio mbali kutoka hapa”
“Yaa sio mbali, ukilifukuzia unaweza kuliwahi”
“Sawa”
Kwa haraka nikaingia kwenye gari, nikaliwasha. Nikarudi nyuma kwa haraka, nikaliweka sawa na kuondoka eneo la hoteli kwa mwendo wa kasi. Nikatazama pande zote za barabara kuhakikisha hakuna gari linalo tokea upande wowote wa barabara nikaingiza gari langi barabarani na kuanza kuelekea barabara ya raskazoni walipo elekea Yudia na watu wake. 

Kwa mwendo wangu wa kasi, nikafanikiwa kuliona gari hilo, taratibu nikachomoa bastola yangu tayari kwa mashambulizi ninayo kwenda kuyafanya. Nikazidi kuongeza mwendo hadi nikalikaribia gari lao, nikalipia kwa kasi kisha nikafunga breki za gafla huku gari langu nikihakikisha linaziba barabara. Dereva wa gari la Yudia akafunga bereki na kusimamisha gari lake mita chache kutoka lilipo gari langu. 

Kwa haraka nikashuka huku bastola nikiwa nimeishika kwa mikono yangu  yote miwili kwa ukakamavu. Nikapiga rasiai moja kwenye tairi la mbele la gari lao na kulifanya lishuke chini kwa upande huo wa tairi. Nikaanza kutembea kwa kunyata huku nikiwa ninajiamini sana, kitu kilicho anza kunipa mashaka ni pale nilipo ona mashambulizi yangu hayajibiwi. Nikiwa nimelikaribia gari mlango wa upande wa dereva ukafunguliwa, akashuka bibi wa kizungu, huku akitetemeka mwili mzima. 
 
“Lala chini”
Nilimuamrisha huku nikiendelea kutembea kwa mwendo wa tahadhari, nikaufungua mlango  wa siti za nyuma, sikuona mtu yoyote kwenye gari. Siti ya mbele kuna mtoto mdogo wa kiafrika akiwa ameinama kwenye siti huku amejikausha kimya akiogopa kitu kinacho endelea.
Nikazunguka nyuma ya gari, namba za usajili za gari ni zile zile nilizo zikremisha.
“Fu**kkkkkkk”
Nilizungumza kwa hasira huku nikirudi kwenye gari langu. Nikaingia kwenye gari na kumpigia simu Cajoli
“Vipi umefanikiwa?”
“Hapana gari ni lenyewe ila wahusika sio”
Nilizungumza huku nikuliweka sawa gari langu, nikaondoka eneo la ktukio na kumuacha bibi kizee wa kizungu akiwa amelala chini kifudi fudi.
 
“Imekuwaje?”
“Hata mimi sielewi imekuwaje, ngoja nirudi nyumbani tu”
“Sawa”
Nikakata simu na kuiweka pembeni, nikiwa maeneo ya Bombo darajani, nikapishana na gari mbili za polisi zikielekea kwa kasi katika eneo ambalo ninahisi ndipo kulipo tokea mlio wa risani. Moja kwa moja nikaeleka nyumbani kwa Cajoli, nikapiga honi mlinzi akafungua geti nikaingiza gari na kulisimamisha sehemu nilipo litoa. Cajoli aliye simama mlangoni kwa haraka akanifwata na kunikumbatia kwa nguvu, tukaingia ndani huku tukiwa tumeshikana mikono.
 
“Mbona muda ule nilisikia sauti ya kiume tofauti na yako kwenye simu?”
“Kuna watu ambao wanahitaji mimi kufanya kazi nao”
“Kivipi?”
“Nina historia ndefu sana kwenye maisha yangu, kadri muda unavyo zidi kwenda ndivyo jinsi nitakavyo kuwa nikikuambia mambo kadhaa kuhusiana na mimi”
“Sawa Dany ila walikuteka?”
Cajoli aliuliza huku machozi yakimlenga lenga.
“Hapana hawakuniteka, ila ni mazungumzo ya hapa na pale. Hivi unafahamu raisi anakuja lini Tanga?”
“Raisi anakuja kesho kutwa, ana ziara ila sijajua  anazifanyia wapi?”
 
“Inatosha siku moja”
“Kivipi?”
“Kumuua raisi”
Cajoli akakaa kimya huku akifikiria kitu cha kunishauri.
“Dany ila kitu unacho taka kukifanya ni cha hatari sana”
“Natambua ila nahitaji kufanya hichi, hii ndio nafasi yangu mimi ya pekee katika kutimia adhima yangu. Natambua Cajoli unanipenda, ila ninakuomba usinizuie katika hili ambalo ninahitaji kulifanya”
“Sawa Dany mimi ninakuruhusu kwa moyo mmoja, japo hujaniadisia mengi ila kwa mauaji yale niliyo yaona kwenye familia yako ni vyema ukalipiza kisasa ila niahidi kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Naomba uhakikishe unabaki salama salimini”
 
“Kwa hilo Mungu yu pamoja nami”
“Kuna rafiki yangu, anamiliki ghala la silaha, asubihi nitawasiliana naye na tunakwenda kwake, utachagua silaha yoyote utalayo ihitaji katika kazi yako”
“Sawa nitashukuru sana katika hilo”
Cajoli taratibu akaanza uchokozi wa mapenzi ambao mwanaume yoyote atakaye fanyiwa ni lazima atasisimka hususani jogoo wake. Taratibu tukajikuta tukizama kwenye dibwi kubwa la mapenzi. Nikamuinamisha Cajoli kwenye sofa la hapa sebleni, nikakishika kiono chake vizuri na kuanza kula kitumbua chake, safari hii nikahakikisha ninampa haki kubwa ambayo sidhanikama nitampa tena, kwa maana kazi ambayo ninaiendea sidhani kama nitarudi hai. 
 
Kelele za Cajoli  zikaendelea kusambaa hapa sebleni, sikulijali hilo nilicho kijali ninampa heshima madhubuti. Waarabu weupe taratibu nikaanza kuwasikia wakitoka kwa mbali, sikutaka kuwamgwaga nje kama nilivyo fanya kwenye mtanange wa mwanzo. Wote nikawamwagia ndani
“Ohooooo”
Cajoli akatoa mguno ulio endana na pumzi nyingi, kila mmoja jasho jingi linamwagika usoni mwake kwa maana shuhuli sio ndogo.
“Asante sana Dany, s** zako ni tamu, yaani ninazisikia zinavyo tembea mwilini mwangu”
“Kweli?”
 
“Yaa na nipo kwenye danger zone, Mungu akitujali tukipata mtoto, itazidi kuwa furaha kwenye maisha yangu”
“Kama ikiwa hivyo ninaomba umtunze mwangu na kumfundisha maadili yaliyo mema”
“Kwa nini unazungumza hivyo, sema tutamtunza na kumlea katika maadili yaliyo mema. Dany ukimaliza hiyo kazi ninakuomba tuondoke Tanzania, twende tukaishi Dubai”
“Dubai?”
“Yaaa Dubai ndio nyumbani kwetu, japo nimezaliwa Tanzania, ila asili ya wazizi wangu ni Dubai”
“Mungu abariki katika hili”
“Nibebe”
Cajoli alizungumza kwa sauti ya kudeka, nikanyanyuka kwenye sofa nililo kalia. Nikainama kidogo akanipandia mgongoni mwangu. Nikambeba kama mtoto mdogo na kuingia naye chumbani. 

Tukaoga kwa pamoja na kurudi chumbani. Usiku huu, ninaweza kusema ni usiku ambao ninalala kwa amani kwenye maisha yangu, hisia zangu zinawaza mambo mengi juu ya kazi ambayo ninayo kwenda kuifanya. Cajoli kwa uchovu wa shuhuli niliyo mpatia, usingizi uliwahi kumpitia akiwa amekilaza kichwa chake kifuani mwangu. Taratibu nikamsogeza na kichwa chake na kililaza kwenye mto. Nikashuka kitandani na kuchukua Laptop  yake aliyo iweka kwenye meza ya kioo iliyopo humu ndani. Nikaiwasha kwa bahati nzuri haina namba za siri, wazo likanijia kichwani mwangu, nikaingia kwenye mtandao wa N.S.S ambao ndio ofisi nilizokuwa ninafanyia kazi.
Ili niweze kupata habari za ndani kabisa katika huu mtando unao husika na kikosi cha ulinzi wa taifa, inabidi kuingiza namba za siri ambazo siku zote huwa wafanyakazi wa kitengo hichi wao ndio wanafahamu. 
 
‘Nikiingiza namba yangu itakuwa ni shida kwangu’
Niliwaza akilini mwangu, nikijaribu kutuliza kichwa kuhakikisha ninakumbuka namba za K2, japo inaniwia ugumu  katika kukumbuka namba zake ila nikazidi kuumiza kichwa na kukituliza kuhakikisha ubongo wangu unakumbuka namba za siri za K2.
Kwa bahati nzuri nikafanikiwa kukumbuka namba zake za siri, kwa haraka nikaziingiza kwenye sehemu mbayo inamuhitaji mfanyakazi kuweza kuingiza namba hizo za siri. Akaunti ya K2 ikafunguka, jambo lililo nifanya nishushe pumzi nyingi, kwa maana nilihisi nimekosea kile nilicho kiingiza.
 
Nikaanza kusoma taarifa zilizopo kwenye mtandao wao, nikaona pia ziara ya K2 kuja mkoa wa Tanga. Atafanya mkutano wa hadhara wa kuwahutubia wananchi wa mkoa huu wa Tanga katika kiwanja cha Tangamano. Nikaona mabadiliko ambayo yamefanyika kwenye kitengo hichi huku mkuu wao kwa sasa akiwa ni Babyanka. Nikaendelea kusoma taarifa za kutafutwa kwangu, japo sasa hivi sitangazwi kwenye vyombo vya habari ila kwenye mtandao wao nipo na wananitafuta kimya kimya kwa maana hadi sasa hivi hawana taarifa kwamba nipo hai au nimekufa.
Hadi inafika alifajiri, bado ninaendelea kusoma taarifa zao. Cajoli akaamka na kunikuta nikiwa nipo kwenye sofa.
“Umeamka mapema mume wangu?”
“Yaaa umelalaje?”
“Leo nimelala vizuri sana, sijawahi kulala usingizi mtamu kama huu kwenye maisha yangu”
“Kweli?”
“Ndio mume wangu”
 
Cajoli akashuka kitandani taratibu na kunifwata hadi sehemu nilipo kaa. Akanikalia kwenye paja la mguu wa kulia huku akinikumbatia.
“Nakupenda sana Dany wangu”
“Nakupenda pia, tujiandae twende kwa rafiki yako”
“Sawa, ila ngoja nikuandalie kifungua kinywa, tule ndio twende sawa mume wangu?”
“Poa mke wangu”
Cajoli akatoka chumbani, nikaendelea kusoma taarifa katika mtandao wetu, kuna baadhi ya wafanyakazi wamefariki dunia na wengi wao ninawafahamu. Cajoli akarudi chumbani akiwa na sahani aliyo weka kifungua kinywa pamoja na glasi iliyo jaa juisi. Tukapata kifungua kinywa, kisha tukaingia bafuni na kuoga haraka haraka. Tukajiandaa na kuondoka nyumbani.
“Rafiki yako anaishi wapi?”
 
“Maeneo ya Kange kule”
“Sawa”
Hatukuchukua muda mwingi tukafika maeneo ya Kange, tukasimama nje ya geti. Cajoli akapiga honi na geti likafunguliwa, tukaingia ndani ya nyumba hii ambayo inaonekana ni ya kawaida sana. Tukakaribishwa na rafiki yake huyo ambaye ni msichana wa kike.
“Huyu ndio boyfriend wangu niliye kuwa ninakuambi kwenye meseji”
“Ohoo Dany karibu sana kwangu”
“Asante sana”
“Dany huyu ni wajina wangu anaitwa Cajoi naye”
“Yaa tumefanana majina tangu utotoni tulikuwa tunafanya kazi kwa pamoja”
“Nashukuru kukufahamu”
“Alafu shem kama sura yako sio ngeni sana kwangu”
“Yaa najua hilo, utakuwa umeniona sehemu”
Tulizungumza huku tukiingia ndani.
“Twendeni huku”
 
Tukaingia kwenye moja ya chumba ambacho kina ngazi za kushuka chini, tukaingia kwenye chumba kilichopo chini ya ardhi. Cajoli akasukuma mlango huu mzito ambao umetengenezwa kwa chuma tu. Tukaingia kwenye chumba ambacho nikikubwa, na kimejaa silaha za kila aina.
“Dany jisikie huru kuna silaha na mabomu ya kila aina, hata ukihitaji bomu la nyuklia ninaweza kukupatia”
“Nyuklia?”
“Yaaa njoo ulione”
Cajoli huyu akafunua moja ya turubai lililo funika moja ya meza, nikaona bomu la nyukila ambalo endapolitalipuka sehemu yoyote linaweza kuua mamilioni ya watu na wengi wao hawana hatia kwenye maisha yao.

AISIIIII……….U KILL ME 100                                                                                               

“Hili bomu si zuri sana kwa kazi ambayo unahitaji kwenda kuifanya shemeji yangu”
“Yaa sio zuri, ila nitahitaji silaha kadha ambazo ninaweza kukamilisha hii kazi yangu”
“Chumba chote sasa ni mali yako kuwa huru”
“Shukrani”
Nikiaanza kuzunguka ndani ya chumba hichi huku nikichagua bunduki ambazo ninaona zinaweza kwenda kunisaidia kwa kazi iliyopo mbele yangu. Kwenye moja ya kabati nikaona nguo nyeusi zikiwa zimening’inizwa vizuri.
“Hizi nguo ni vipi?”
”Hizo ni nguo ambazo huwa nina shonesha mwenyewe. Kwa watu ambao wanahitaji nguo za kufanyia kazi basi inakuwa ni rahisi kwa wao kuchukua nguo kutoka kwangu”
“Ninaweza kuzijaribisha?”
 
“Ndio unaweza shemeji yangu”
Nikazitoa kwenye kabati na kuziweka kwenye meza iliyopo humu ndani. Taratibu nikaanza kuvua nguo zangu, ikambidi shemeji kugeuka na kunipa mgongo. Nikazijaribisha nguo hizi, unaweza ukasema kwamba ziliandaliwa kwa ajili yangu kwa maana zimenikaa vizuri mwilini mwangu.
“Shem hizi nguo uliandaa kwa ajili yangu nini?”
Shemeji Cajoli akanigeukia na kunitazama, akaachia tabasamu pana huku akinitazama usoni mwangu. “Wajina umemtoa wapi huyu mwanaume?”
“Kwa nini?”
“Mzuri sana”
“Utani sasa huo wajina”
“Shosti ninakuambia, unatakiwa kuwa makini kumlinda mumeo si unajua wanawake wenyewe wa sasa shida tu, wanajitongozesha wenyewe”
“Hilo nalo neon wajina”
“Shem kuna bullet proof jakets zipo kwenye hilo kabati la pili unaweza kuwa na hata mmoja”
“Asante shemeji yangu”
Nikafungua kabati la pili na kukuta majaketi ya kuzuia riasai yakiwa yamepangwa vizuri. Nikachukua moja nikalijaribisha. Likanikaa vizuri mwilini mwangu.
“Kila kitu kipo vizuri, nipatieni begi ninaloweza kuweka zana zangu”
 
“Usijali katika hilo”
Cajoli akatoka na nikabaki na mpenzi wangu.
“Dany unauhakika na hichi unachokwenda kukifanya?”
Cajoli aliniuliza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu.
“Yaa am sure kwa kile ninacho kwenda kukifanya”
“Ila nimeanza kupata hisia mbaya katika hili”
“Hisia gani?”
“Sifahamu ni hisia gani, ila sipo vizuri katika hili ambalo umeamua kwenda kulifanya”
“Baby nisikilize, najua nilazima utakuwa na wasiwasi mwingi katika hili, ila tambua ya kwamba ninafanya hivi kwa ajili ya familia yangu. Ninafanya hivi kwa ajili ya kutengeza amani ya maisha yangu. Amani ya familia yangu ambayo ninakwenda kuitengenza mimi na wewe. Unahitaji niendelee kuishi kwa kukosa amani na kuandamwa na wabaya wangu hadi kwa wanangu ambao nitapata kutoka kwako?”
 
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga, hadi Cajol naye akaanza kumwagikwa na machozi usoni mwake.
“Nafanya haya yote kwa ajili yako na wanangu. Nilipo fikia panatosha kabisa, sihitaji kukupoteza wewe. Sina mama, sijui ni wapi alipo baba yangu, sifahamu kama yupo hai au laa. Nimebaki mnyonge kwenye dibwi ambalo sidhani kama ninaweza kutoka. Kwa nini na mimi nisilipize kisasi nikiwa na nguvu zangu, au una hitaji waje walipize watoto wetu?”
“No Dany”
Cajoli alizungumza na kunikumbatia kwa nguvu, taratibu tukajikuta tukianza kunyonyana midomo yetu kwa hisia kali sana huku machozi yakiendelea kutiririka kwenye nyuso zetu.
“Mmmghgg”
Tulisikia sauti ya Cajoli nyuma yetu, tukaachiana na kumtazama.
 
“Shem begi hili hapa”   
Shem Cajoli akanikabidhi begi kubwa jeusi, wote watatu tukaanza kusaidia kuingiza silaha ambazo nimezichagua, huku bunduki moja ikiwa ina uwezo wa kupiga risasi kwa umbali mrefu sana. Kazi haikuwa ngumu sana, baada ya muda mfupi tukawa tumemaliza kuingiza silaha zote kwenye begi huku nyingi zikiwa ni bastola na magazine zake.
“Jamani tupateni hata chakula cha mchana hapa kwangu?”
“Shem inabidi nikafanye maandalizi mapema kuhakikisha kwamba kazi yangu haiendi vibaya”
“Ila shem, kazi ambayo unakwenda kuifanya mbona kama ni kubwa sana huoni kama inaweza kuleta matatizo kwako”
“Bora wajina umenisaidia kuzungumza”
Cajoli alizungumza kwa sauti ya unyonge sana huku akinitazama usoni mwangu.
“Mimi ninawaomba muwe wapole na watulivu, kikubwa ni kuniombea kwa mwenyezi Mungu, ili kazi yangu iweze kutimia”
“Sawa shem, ila ukihitaji msaada wangu ninaomba unijulishe”
 
“Hapana shemeji, kazi hii sihitaji iweze kuingia kwenye maisha ya mtu mwengine. Nyinyi kikubwa mbacho munatakiwa kuweza kukifanya, ninawaomba muweze kuniombea kwa mwenyezi Mungu aweze kunifanikisha katika hili”
Maneno yangu yakawafanya Cajoli na mwenzake kukaa kimya, hapakuwa na mtu aliye weka kipingamizi kutokana na msimamo wangu nilio uamua kwa jambo hili. Tukaagaana na shem Cajoli na kuondoka nyumbani kwake huku begi la silaha  nikiwa nimeliweka siti ya nyuma. Njia nzima wote tupo kimya, akili yangu ina kazi ya kuwaza ni kitu gani ambacho ninaweza kukifanya kuhakikisha kwamba ninaweza kumuua K2 na watu wake.
“Dany”
Cajoli aliniita kwa sauti ya upole na kunifanya nitoke kwenye dimbwi la mawazo, nikamtazama, kwa ishara ya macho akanionyesha mbele yetu. Nikaona askri barabarani wakiwa wanasimamisha magari yanayo ingia jiji la Tanga huku kizuizi chao wakiwa wamekiweka maeneo ya majani mapana, maeneo ya kiwanja cha ndege cha mkoa wa Tanga.
 
“Tulia usiwe na wasiwasi”
“Sasa wakikagua hili begi huku siti ya nyuma”
“Usiwe na wasiwasi Cajoli wewe tulia tena jifanye unazungumza kiarabu mimi nitakuwa mtafsiri wako, hao polisi ukizungumza nao kiarabu basi hawato elewa”
“No Danu hiyo hilo halitokuwa wazo zuri kwetu wanaweza kunisumbua na kuanza kuhitaji maswala ya passport”
“Ok wewe tulia wala usionyeshe wasiwasi wowote”
“Sawa”
Taratibu Cajoli akasimamisha gari pembeni kama polisi wa usalama barabarani alivyo hitaji afanye hiyo. Polisi akatembea hadi sehemu gari lilipo na kumfanya Cajoli kushusha kioo cha upande wake taratibu,
“Habri zenu wakuu”
“Salama tu kaka”
“Naomba driving leseni”
Cajoli akafungua kipochi chake kidogo na kutoa leseni yake na kukabidhi askari, akaisoma kwa dakika moja kasha akamrudishia. Akasoma kazi kadhaa zilizo bandikwa kwenye kioo cha mbele, alipo jiridhisha akarudi kwenye kioo.
 
“Safari njema waheshimiwa”
“Shukrani na wewe kaka”
Cajoli akafunga kioo cha gari na tukaendelea na safari yetu. Tukafika nyumbani, nikafungua mlango nyuma wa gari nikatoa begi lenye silaha. Moja kwa moja nikaingia ndani huku nikimfwata Cajoli kwa nyuma.
“Njoo chumba hichi”
Cajoli alizungumza, tukaingia kwenye chumba ambacho kina vitu vichache ikiwemo meza kubwa.
“Nenda kaandae chakula, leo ninahitaji kula chakula chako mke wangu”
“Sawa, ila upo sawa Dany?”
“Yaa am, fine “
Sure”
 
“Yaa nina uhakika, kuwa na amani mke wangu, wewe ndenda kaandae chakula”
“Sawa  honey”
Cajoli akanisogelea na kunibusu mdomoni mwangu akaondoka ndani ya chumba hichi. Nikaanza kupanga sila zangu, huku nyingine nikizifuita vumbi kuhakikisha kwamba utendaji wake wa kazi unakuwa sawaia. Kazi hii ikanigarimu zaidi ya lisaa limoja, nilipo hakikisha kwamba silaha zimekamilika kuwa sawa. Nikaanza kupanga ni ipi nianze nayo katika kuifanya kazi yangu. Nianyanyuka na kutoka katika chumba hichi, nikaingia jikoni na kumkuta Cajoli akiendelea kupika chakula.
“Bado hujamaliza?”
“Yaa bado sijamaliza, vipi wewe umesha maliza?”
“Kwa kiasi fulani, laptop ipo wapi?”
“Pale ulipo iacha asubuhi”
 
Nikatoka jikoni na kuingia katika chumba cha kulala, nikaichukua laptop na kuridi nayo kwenye chumba chenye silaza zangu za maangamiuzi. Nikaingia kwenye mtandao wa NSS, kuangalia kama kuna habari yoyote mpya. Sikukuta habari yoyote mpya tofauti na zile nilizo zikuta jana usiku.
Niafungua video ambayo sikuifungua kati ya video tatu zilizopo kwenye memory card aliyo nipatia Linda. Maandishi ya rangi nyekundu yakaonekana kwenye video hii ynayo someka kwa kusema.
 
‘Magaidi wakubwa Afrika na mitandao yao’
Picha ya kwanza ikaonekana K2, huku pembeni kukiwa na malezo yake, umiliki wa kundi kubwa la wasichana ambao kazi yao ni kuua pale wanapo tumwa kufanya kazi hiyo. Wakaonyeshwa watumishi wake wakuu ambao wa kwanza ni Livna Liva wa pili ni mama yangu mzazi, jambo lililo nifanya nibaki nimekodolea macho video hii,  hadi ikanilazimu kuisimamisha na kuyasoma maelezo ya mama.
 
Mama yangu anaonyesha ni gaidi aliye ingia kwenye mfarakano na bosi wake ambaye ni K2. Chanzo kikubwa cha K2 na mama kuingia katika mgogoro mkubwa ni swala zima la kugombania madaraka huku kila mmoja akijona yeye ndio mwenye nguvu kubwa zaidi ya mwenzake.
K2 na mama walikuwa marafiki wa muda mrefu tangu walipokuwa jeshini, ila mama aliacha jeshi na kuingia kwenye maswala ya uongozi huku K2 akifanikiwa kuingia katika kitengo cha NSS. Hawa wote wawili wamehusika sana kwenye kifo cha raisi wa kwanza wa kike Tanza ambaye ni bi Rahab na nafasi hiyo ikachukuliwa na kaka wa K2.
 
Historia hii kidogo ikaanza kunipa mwanga wa mambo ambayo nyuma yalikuwa yanatokea pasipo mimi kuweza kuelewa ni kitu gani ambacho kinaendelea.
‘Nahitaji uniletee kichwa cha K2 hapa’
Maneno haya ya mama yakajirudia kichwani mwangu, kwa hapo awali nilihisi mama anazungumza hivyo kutokana na ukatili ambao K2 alinifanyia kwa kunifunga kwenye gereza la giza pasipo kosa la aina yoyote. Nilihisi labda ni wivu wa mapenzi juu yangu kumbe kuna jambo ambalo linaendelea nyuma yake.
Historia kwa ufupi kati ya mama na K2 ikaishia hapo, nikaendelea kutazama magaidi wengine ambao wanafanya kazi na K2 jambo linalo nishangaza watu wote walipo chini ya K2 hakuna mwanaume hata mmoja, wengi wao ni wamama ambao sijawahi kuwaona hata siku moja kwenye maisha yangu.
 
“Dany chakula tayari honey”
“Sawa”
“Tuje kula huku au nikiandae mezani?”
“Twende tu tukalie mezani”
Nikazima laptop na kuelekea mezani kwa ajili ya chakula. Cajoli akaninawisha mikono kisha na yeye akanawa. Taratibu tukaanza kula ndizi nyama alizopika.
“Dany”
“Mmmm”
“Ninakuomba unapo kwenda huko uhakikishe unarudi salama mume wangu.”
“Usijali, ila kuna kazi ambayo ninahitaji kuifanya tofauti na hii ambayo nilipanga kuifanya”
“Kazi gani tena!!?”
“Kuudondosha mtandao wa K2, kwa maana hata nisikisema kwamba nimuue yeye, bado nitakuwa suijaipata amani ambayo ninaitafuta”
 
“Huo mtando wewe una ufahamu?”
“Ndio nina ufahamu, kupitia hawa watu wake, ndivyo jinsi nitakavyo kuwa nikimdhohofisha hadi itafikia kipindi atakosa nguvu, na akikosa nguvu ya madaraka basi kwangu itakuwa ni rahisi sana kumuangamiza”
Cajoli akashusha pumzi nyingihuku akinitazama usoni mwangu. Akaonekana ni mtu mwenye furaha ambayoa anaizuia kuionyesha usoni mwake.
“Ila kesho nitakwenda kwenye viwanja hivyo kusoma mazingira, nahitaji kumuona K2 jinsi alivyo livyo kwenye sura ya uraisi”
 
“Utakwenda na silaha”
“Yaa ni lazima kwenda na silaha kuhakikisha ninajilinda”
Siku nzima ikapita nikiwa ninapanga mipango yangu ya kimya kimya wala sikuhitaji kumshirikisha Cajili kwa kila kitu. Asubuhi ikawadia, huku moyo wangu ukiwa imejawa na shauku kubwa ya kuhakikisha kwamba ninahakikisha kwamba leo ninaondoka na roho ya K2. Nikachukua bastola zangu mbili nikazificha kwenye soksi za miguuni mwangu. Nikavaa jaketi la kuzuai risasi kisha juu yake nikavaa na sweta lenye kofia.
“Cajoli ninakuhitaji ubaki ndani, tazama Tv kuangalia kinacho tokea sawa baby”
“Ila Dany nakuomba usifanye kinyume na kile ambacho umekipanga”
“Usijali katika hilo nitahakikisha kwamba sifanyi ujinga”
“Sawa mume wangu, ninakupenda”
“Ninakupenda pia”
“Utatumia gari?”
“Hapana, nitapanda pikipiki”
“Una pesa ya kutosha?”
“Ndio”
 
Tukakumbatiana na Cajoli kisha nikatoka nje. Nikatoka nje ya geti nikatembea hadi mtaa wa pili, nikamkodisha dereva bodaboda, nikampa maelekezo kueleka hadi katika viwanja vya Tangamano ambapo hapo K2 atakuwepo. Dereva akafanya kama nilivyo muagiza, nikafika katika viwanja hivi viliyo jaa watu wengi pamoja na askari huku walinzi wa raisi wakiwa wamezagaa kila mahala. Nikaingia kwenye gorofa moja linalo tazamana na uwanja huu wa Tangamamo. Nikaanza kupandisha kwenye ngazi kueleka juu, huku nikiwa makini sana, kwa naana huuwa ninajua walinzi wengine kwa mara nyingi huwa wanakaa juu ya magorofa wakiwa na bunduki zao maalimu za kupiga risasi masafa marefu yote hiyo ni katika kuimarisha ulinzi wa raisi.
 
Nikaingia kwenye mlango wa juu kabisa katika goroa hili
ambao niliukuta ukiwa umerudishiwa tu. Nikamuona askari mmoja wa kikosi cha NSS, akiwa amejificha shemu na bunduki yake ya aina kama hiyo.
 
Kwa mwendo wa kunyata na kwa uamakini sana nikamsogelea, nikachomoa bastola yangu kwenye soks ya mguu wa kulia. Kwa kutumia kitako cha bastola nikampiga nacho kwa nyuma na kumfanya adondokee pembeni.
Nikachukua mawasiliano yake aliyo yavaa sikioni, nikayavaa mimi vizuri, kila kitu ambacho wanapeana taarifa askari wote wa NSS katika eneo hili ninayasikia. Nikalala katika sehemua mbayo alikuwa amelala akikagua maeneo ya chini ya gorofa kwa kutumia darubini yake ambayo imefungwa kwenye bunduki hii.
 
“Zimebaki dakia mbili raisi kufika kiwanjani”
Nilisikia taarifa hiyo kutoka kwa sauti ya kike ambayo nina ifahamu sana, kwani ni Babyanka. Nikashusha pumzi nyingi huku bunduki nikiwa nimeinyooshea barabarani sehemu ambayo gari za raisi zitasimama. Gari nyeusi tatu zinazo fanana zikazimama kwenye sehemu maalumu zilipo andaliwa raisi kushuka. 

Walinzi wa rais anao tembea nao kwenye gari wakashuka kwa wingi huku wakiwa makini kuhakikisha raisi akishuka kwenye gari anakuwa salama. Mlizi mmoja akafungua mlango wa nyuma wa gari ya katikati. Nikamuona raisi akishuka taratibu kwenye gari huku akiwapungia mikono wananchi wake walio anza kumshangilia kwa furaha sana.
 
Nikamvuta taratibu K2 kwa kutumia darubini ya hii bunduki. Nilipo hakikisha msalaba mwekundu ninao uona kwenye hii darubini umekaa vizuri kichwani mwake, taratibu nikaikoki bunduki, huku nikishusha pumzi nyingi. 

Nikamuangalia K2 jinsi anavyo furahi na wananchi huku akiwapa mikono ya hongera. Gafla mwili mzima ukaanza kunitetemeka huku jasho jingi likinimwahika mwili mzima. Nikajaribu kuhakikisha kwamba ninajikaza kumuweka K2 katika tageti yangu, ila ninashindwa kabisa. 

Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi, taratibu nikajaribu kunyanyuka ila nikashindwa kabisa na kujikuta nikiiangusha bunduki pembeni na kulala chali, huku nikitazama juu na kuona jinsi dunia inavyo zunguka kwa kasi jambo ambalo kwenye maisha yangu sikuwahi kuliona hata siku moja.

==>>ITAENDELEA KESHO

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya October 14

Waziri Mkuu Afunga Tamasha La Urithi Festival .....Atoa Miezi Miwili Wizara Ya Habari Ikamilishe Mchakato Wa Vazi La Taifa

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa muda wa miezi miwili na nusu kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezoiwe imekamilisha mchakato wa Tanzania kuwa na vazi la Taifa.

Amesema Watanzania bado hawajaunganishwa kwa kuwa na vazi la Taifa, ambalo mchakato wake  umeendeshwa kwa miaka mingi na wizara hiyo bila ya kujulikana wamefikia wapi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Oktoba 13, 2018) wakati akifunga tamasha za Urithi Festival, lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini  Arusha.

“Ifikapo Desemba 30,2018 tuwe tumeanza kupata sura ya vazi la Taifa ili wadau walijadili na waamue ni vazi gani la Mtanzania ambalo litawakilisha Taifa kama nchi nyingine walivyomudu kuwa na vazi la Taifa.”

Aliongeza kuwa ili kufikia azma  Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezoiandae tamasha maalumu kwa ajili ya kuonesha aina tofauti za nguo ili kupata vazi la Taifa.

Kadhalika, Waziri Mkuu aliwaagiza waandaaji wa tamasha la Uridhi Festival wahakikishe kuanzia  mwakani kuwe na uratibu wa pamoja baina ya Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara ili tamasha lifunguliwe upande mmoja na kufungwa upande mwingine wa Muungano.

Amesema kwa kufanya hivyo watakuwa wametoa  fursa kwa walio Zanzibar kujifunza na kuona utamaduni wa bara na wa bara kujifunza ya Zanzibar, hivyo itasaidia kudumisha  umoja wa kitaifa. “Hakikisheni ikiwa tamasha litafunguliwa Tanzania Bara basi lifungwe Zanzibar ili liweze kuwa na tija’’.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amesema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020, inaitaka Serikali kuongeza msukumo katika kukuza utalii na kutangaza vivutio vyetu vya utalii vikiwemo utamaduni na malikale.

“Mtakubaliana nami kwamba tunapaswa kuendeleza mila, tamaduni na desturi zetu kwani ndizo kichocheo muhimu cha uzalendo tulionao hususan katika suala zima la maadili. Vilevile, utamaduni ni zao la uhakika kwenye sekta ya utalii na ukarimu.”

Amesema thamani ya utamaduni mara nyingi imekuwa ikionekana kwenye sekta nyingine kama elimu, afya, michezo, kilimo, viwanda na maendeleo ya jamii, ambapo alitoa rai kwaWizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, wadau wote wa utalii hususani Sekta binafsi na wananchi kwa ujumla washirikiane katika kulinda, kutunza, kutangaza na kuendeleza vivutio vya utalii nchini.

“Lengo la Serikali ni kuongeza idadi ya watalii kutoka 1,102,026 mwaka 2015 hadi 2,000,000 ifikapo mwaka 2020. Lengo hili linatekelezwa kwa kuwezesha sekta binafsi kuwekeza kwenye huduma ya miundombinu ya utalii na kuendelea kutangaza utalii ili kuwafikia watalii wengi zaidi.” 

Amesema Urithi Festival ni chachu ya kukuza, kulinda, kuimarisha nakutangaza utamaduni na malikale zetu na kuvigeuza kuwa zao la utalii. Tamasha hili litatuweka pamoja zaidi na kudumisha umoja, utaifa na uzalendo kwa nchi yetu.

Aidha, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuikumbusha Wizara ya Maliasili na Utalii kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mkoa wa Dodoma kuanza maandalizi mara moja ya kutekeleza agizo la Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan la kutenga eneo mahususi ambalo litatumika kwa ajili ya Tamasha la Urithi kila mwaka kitaifa Mkoani Dodoma.

“Napenda kutumia fursa hii na hasa nikizingatia maagizo ya Makamu wa Rais kuwapa changamoto Wizara ya Maliasili na Utalii na wadau wa utalii kuhakikisha kuwa kuanzia mwaka kesho (2019) tamasha hili linatambulika Kimataifa na kuwa moja ya kichocheo kikuu cha kukuza pato la Taifa litokanalo na utalii“

Amesema wakati wa uzinduzi wa tamasha hilo Septemba 15, 2018 jijini Dodoma, Makamu wa Rais, Mama Samia aliagiza kila Mkoa kutenga bajeti kwa ajili ya Tamasha la Urithi. “Napenda kutumia fursa hii kuwakumbusha tena Wakuu wa Mikoa kuanza maandalizi mapema.“

“Tamasha la Urithi sio tu linaenzi utamaduni na mila zetu, lakini ndio njia bora zaidi ya kurithisha vizazi vijavyo mila, desturi, tamaduni na historia yetu. Kwani yeyote yule ambaye haenzi utamaduni wake basi huyo ni mtumwa.“

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Safari ya matibabu ya Hawa wa Diamond kwenda India yakwama

0
0
Msanii Hawa Said maarufu Hawa wa Diamond, amejikuta akirudishwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam (JNIA) baada ya kutotimiza vibali vya kusafiri vya kimatibabu kwenda India.

Akizungumza na Gazeti la Mwananchi  baada ya kukwama jana Oktoba 13, 2018 meneja wa Diamond Platinumz ambao ndiyo wamechukua jukumu la kugharamia matibabu hayo, Babu Tale amesema hali hiyo imewakuta wakiwa tayari wameingia ndani ya uwanja wa ndege na kuanza kukaguliwa nyaraka zao mbalimbali.

Babu Tale amesema nyaraka iliyowakwamisha kusafiri ni kibali cha daktari kuelezea hali ya mgonjwa ili wahudumu ndani ya ndege wajue namna watakavyomhudumia.

“Kuna mgonjwa anaweza akawa katika hali ya kuzimia, kutapika anatakiwa ahudumiwe tofauti, hivyo Hawa imeshindikana kwa kuwa hakuna hizo nyaraka inayoonyesha hivyo kutoka kwa daktari na wametwambia turudi itakapokamilika,” amesema.

Hawa, Babu Tale na mama yake, Ndagina Hassan ilikuwa waondoke jana saa 10:45 na ndege ya Shirika la Emirates.

Hawa na mama yake, Ndagina, walifika uwanjani hapo tangu saa 7:00 mchana huku Babu Tale akiwasili saa 9:00 alasiri.

Naye Hawa amewaomba Watanzania kumuombea dua katika matibabu hayo.

Mbunge wa Babati Mjini kwa kupitia Chadema Pauline Gekul, ajiuzulu na Kujiunga CCM

0
0
Mbunge wa Babati Mjini (Chadema), Pauline Gekul ametangaza kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na CCM.

Barua inayosambaa  mitandaoni kuanzia  saa 4.20 usiku wa kuamkia leo ikionyesha kwenda kwa Spika wa Bunge Job Ndugai ikiwa imesainiwa na Gekul anasema amejiuzulu uanachama na ubunge wake.

Miongoni mwa sababu za uamuzi huo ni baadhi ya viongozi wa CHADEMA kuhujumu kwa makusudi jitihada zake za kupelekea wananchi maendeleo.

Mwanamke amwagiwa tindikali na mumewe

0
0
Jeshi la Polisi mkoani Simiyu linamshikilia mwalimu wa shule ya sekondari Kanazi ya mkoani Kagera, Deogratias Bankana kwa kumwagia tindikali mkewe, Angel Francis kutokana na wivu wa mapenzi. 

Muathirika na mumewe wanaeleza kilichotokea hapo chini

Credit: Azam Tv

Kutana Na Shekhe Massory kutoka Pemba.....Anasafisha Nyota, Mvuto wa Biashara, Tatizo la Kutoshika Mimba, Miguu Kuwaka Moto

0
0
✨Je umekuwa ukihangaika na kusumbuliwa na Maisha ,Matatizo Mengi ya Kimaisha pasipo Mafanikio???

✨Bado haujachelewa....Kutana Na Shekhe Massory kutoka Pemba  Bingwa wa kutatua Matatizo Yote Yanayo husu Maisha na kukupa Dawa zitakazo kusaidia  Katika Maisha Yako kama vile;

✨Mvuto Wa Biashara 

Kuwa Na Wateja Wengi Katika Bishara YakoKumvuta Mpenzi Awe Mume Au Mkee aje Karibu Yako
Mtu Mwenye Tatizo La Kutoshika Mimba Au Akishika Inatoka...Tiba Hiyo Ipo 
Kumzuia Mume Au Mke Asitoke Nje Ya Ndoa Au Kwenye Mahusiano Yenu
✨kutibu Chango La Uzazi 
✨ Miguu Kuwaka Moto
 ✨ Kuweka Kinga  shambani Nyumbani na hata Dukani Au Sehemu Yako Ya BiasharaKusafisha Nyota 
Kurudiswa Kazini
✨Pia Kuna Pete Za Bahati

✨ Kwa Mawasiliano
+255 718 826768 -Tgo
+255 692 610596 -Airtel
+255 620 144631 -Halotel

Whatssap Namba
+255 620 144631


✨Wote Mnakaribiswa Mpate Dua Kutoka Pemba Kwa Shekhe Mansoory✨

✨Malipo Ni Baada Ya Mafanikio Inshaalah✨

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum✨

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Rais Magufuli Ashiriki Ibada Maalumu Kumuombea Baba Wa Taifa, Amtembelea Mama Maria Nyerere

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mjane wa Baba Taifa, Mama Maria Nyerere, aliyemtembelea nyumbani kwake Msasani baada ya kutoka katika Ibada Maalumu ya kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Oktoba 14, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli wakiwa na Mama Maria Nyerere walipomtembelea nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam baada yakuhudhuria Misa Maalumu kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Oktoba 14, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli wakisindikizwa  na Mama Maria Nyerere pamoja na mwanae Makongoro Nyerere na wajukuu wake walipomtembelea nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam baada yakuhudhuria Misa Maalumu kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Oktoba 14, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli wakiungana na waumini wengine katika Ibada Maalumu ya kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Oktoba 14, 2018. PICHA NA IKULU

Kumbukumbu Ya Miaka 19 Ya Kifo Cha Hayati Baba Wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

0
0
KUMBUKUMBU YA  MIAKA 19  YA KIFO CHA HAYATI BABA WA TAIFA MWL. JULIUS KAMBARAGE  NYERERE.

✍🏻Taifa letu Tanzania leo tunamkumbuka Shujaa wetu na Kiongozi wetu Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Mwl. Julius Nyerere alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania ambaye alizaliwa Mwaka 1922 na baada ya Kulitumikia Taifa lake alitwaliwa na Mwenyezi Mungu tar. Oktoba 14, 1999 Huko Uingereza Katika Hospitali ya St. Thomas. Ameishi Miaka Takribani 77.

✍🏻Tunamkumbuka Baba wa Taifa kwa Mengi aliyoifanyia Nchi yake na Taifa lake Tanzania. Amekuwa Kiongozi Mzalendo wa Kweli Katika Taifa lake, Mchapa Kazi.

✍🏻 Baba wa Taifa aliacha Kazi yake ya Ualimu na Kuchagua Siasa kama njia Sahihi ya Kulikomboa Taifa lake Tanganyika. Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere aliongoza Mapambano dhidi ya Wakoloni ili Kudai Uhuru Wetu. Wakati wote alikuwa ni Adui wa Rushwa, Maradhi, Ujinga, Ufisadi na mambo Mengine mengi aliyoamini ni Adui wa Maendeleo ya Taifa letu.
✍🏻Ijapokuwa Tuna Makabila Mengi Tanzania, Baba wa Taifa alifanikiwa Kuwaunganisha Watanganyika na kuwafanya kuwa wamoja na kuishi kwa Upendo na Kuongea Lugha Moja.

✍🏻Leo tunapoadhimisha hii Siku Muhimu ya Kumkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwl. JK Nyerere, ni vyema tukakumbuka Mambo Muhimu ambayo Baba wa Taifa aliyakataa na kuona ni Mambo ambayo yanaweza Kutugawa Watanzania; Tukatae Kubaguana Kwa Udini, Ukabila, Kutoheshimu Utu wa Watu. Isitokee Mtu ama Kiongozi yeyote akatubagua kwa Nyanja hizo huyo atakuwa ni Adui namba moja wa Taifa letu. Mwl. Nyerere alikuwa Kiongozi nambari Moja Kulinda Rasilimali za Taifa letu ambazo ni Urithi Kwetu na Vizazi Vyetu Vijavyo.  Mwl. Nyerere Baba wa Taifa alihimiza Watu Wafanye Kazi kwa Bidii ili Kujikomboa na Umasikini lakini pia Kufanya Kazi kwa Bidii ni Chachu ya Maendeleo ya Taifa letu.

✍🏻Nichukue nafasi tena kuwaomba Watanzania Wote kuungana  na Mzalendo Mwingine Nambari Moja wa Taifa letu Mwl. Dkt .  John Pombe Magufuli, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Katika Kufanya Kazi kwa Bidii Kama ambavyo husisitiza Mara kwa Mara Kwamba Serikali yake  Ifanye Kazi kwelikweli na WanaNchi tufanye Kazi kwelikweli na Kwa Bidii, Kulinda Raslimali za Nchi yetu kama ambavyo alionyesha Kupitia Sakata la Makinikia, Kuendeleza Mapambano dhidi Rushwa, Maradhi, Umasikini, Ufisadi, Udini, Ukabila na Kwamba Juhudi hizi za Rais wetu Mpendwa John Pombe Magufuli ni za Kuungwa Mkono na Watanzania Wote wenye Mapenzi Mema na Taifa letu huku Tukitambua Hakuna Mtu wa nje  atakayekuja Kutujengea Nchi yetu isipokuwa ni Sisi Watanzania wenyewe ndiyo tutakaoweza kusimama imara na Kuijenga Tanzania tunayoitaka.

✍🏻Nimalizie kwa Kumpongeza sana Rais Wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli Kwa Kuchapa Kazi na Kutuletea Maendeleo Watanzania.  Ni hakika ya Kwamba anatembea ndani ya dira ya Hayati Baba wa Taifa Mwl. J.K Nyerere na Dira &  Muelekeo wa Serikali yake atakayoiunda kuwatumikia Watanzania  aliyoitoa Mwaka 2015 wakati wa Ufunguzi wa Bunge baada ya Kuapishwa kuwa Rais wa Hawamu ya Tano.

✍🏻MUNGU Ibariki Tanganyika, MUNGU Ibariki Zanzibar, MUNGU Ibariki Tanzania na MUNGU mmbariki Rais wetu Mpendwa Mwl. John Pombe Magufuli pamoja na Viongozi wengine Chini yake akiwemo Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ali  Mohammed Shein.

Robert PJN Kaseko
Mjumbe Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha.
Oktoba 14, 2018

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Rais Magufuli: Serikali itaendelea kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa Vitendo

0
0
Rais John Magufuli amesema Serikali itaendelea kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuhakikisha fikra na mipango mizuri aliyoiweka inatekelezwa kwa manufaa ya Watanzania wote.

Ametoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 14, 2018 wakati akizungumza na mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam alikokwenda kumtembelea muda mfupi baada ya kushiriki Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay.

Taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu imemnukuu Rais Magufuli akisema Mwalimu Nyerere alifanya kazi kubwa ya kujenga misingi imara ya nchi kuwa na amani, umoja na mshikamano na pia kujenga misingi ya uchumi wa kujitegemea kupitia Azimio la Arusha.

Rais Magufuli ametoa wito kwa Watanzania wote hasa vijana kuungana na Serikali katika kuyaenzi yaliyofanywa na Baba wa Taifa na pia kuliombea Taifa.

Naye Mama Maria Nyerere amemshukuru Rais Magufuli kwa kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa na amemhakikishia yeye na wana maombi wenzake pamoja na Watanzania wote wanamuombea heri yeye, viongozi wote na Taifa kwa ujumla.

Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth amekutana na mtoto wa Baba wa Taifa, Makongoro Nyerere na wajukuu wa Baba wa Taifa.

Waumini hao kwa pamoja wamemuombea Baba wa Taifa, aliyefariki dunia Oktoba, 14  1999 ambako katika mahubiri yake, Paroko Msaidizi Padre Barthlomeo Bachoo amesema katika uhai wake Hayati Baba wa Taifa aliongoza Taifa kwa hekima kubwa, alipenda amani, haki, alipiga vita ukoloni, udini, ukabila, rushwa, uonevu na alikuwa mcha Mungu aliyekuwa akisali katika kanisa hilo.

“Tunapomkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere kila Mtanzania ana wajibu wa kuliombea Taifa, kuwa balozi wa amani, upendo, umoja na mshikamano na pia tuwaombee viongozi wetu waishi falsafa ya Mwalimu Nyerere, tusimtafute Mwalimu Nyerere makaburini bali tumtafute katika mambo aliyotufundisha” amesema Padre Bachoo.

Mazingira Bora Ya Miradi Kuipatia Mikopo Sekta Binafsi Tokaka Katika Mashirika Ya Kimataifa

0
0
Na. WFM, Bali Indonesia
Mazingira bora yakutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Sekta Binafsi kutaiwezesha sekta hiyo kupata fedha katika Mashirika ya Kimataifa ambayo yametenga bajeti kwa ajili ya kuimarisha sekta hiyo.

Hayo yameelezwa mjini Bali Indonesia na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, baada ya kumalizika kwa  mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) iliyowakutanisha Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu wa nchi mbalimbali.

Dkt. Mpango alisema kuwa, yapo Mashirika ambayo yapotayari kutoa fedha iwapo kuna uhakika wakurudishwa kwa fedha hizo kama zitatolewa kwa mfumo wa  mikopo, hivyo ni vizuri mazingira ya utekelezaji miradi ya Sekta Binafsi yakaboreshwa ili kuwe na urahisi wa upatikanaji wa fedha hizo.

Alisema kuwa, nchi za Afrika ikiwemo Tanzania zinahitaji pia fedha za kuwekeza kwenye miundombinu ya kiteknolojia ili kuweza kuchochea ukuaji wa uchumi

“Kama nchi inatakiwa kuhakikisha  inaongeza mapato ya ndani ya kodi  na yasiyo ya kodi kwa kuwa jambo hilo ni moja ya kigezo chakuweza kupata fedha zaidi kutoka Mashirika ya Kimataifa”, alieleza Dkt. Mpango.

Naye Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Yamungu Kayandabila, alisema kuwa katika mikutano ya mwaka ya WB na IMF, imesisitiza kuondoa vikwazo vya kibiashara kati ya nchi na nchi  kwa kuwa biashara imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza pato na uchumi wa nchi unategemea mahusiano mazuri kati ya taifa moja na lingine.

Dkt. Kayandabila alisema kuwa, Mataifa makubwa ikiwemo China na Marekani yanatakiwa kupunguza mvutano unaosababishwa na vikwazo vya kodi baina yao ili kutoathiri nchi ndogo ikiwemo Tanzania inayofanya biashara na nchi hizo.

Mikutano ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa imemalizika mjini Bali Indonesia kwa Mkurugenzi Mtendaji wa IMF Bi. Christine Lagarde na Rais wa Benki ya Dunia Bw. Jim Yong Kim, kukutana na Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu ambapo waliangazia mwenendo wa uchumi wa ulimwengu hasa Afrika ambayo uchumi wa baadhi ya nchi unaenda vizuri na nyingine kutofanya vizuri na kusababisha Bara hilo kuonekana uchumi wake kuonekana kukua kwa kasi ndogo.

Serikali kufunga CCTV Camera katika Majiji Yote Nchini Ili Kukabiliana na Matukio ya Utekaji

0
0
Serikali inatarajia kusambaza kamera maalum za CCTV katika miji mikubwa na mikoa iliyoko karibu na mipaka ya nchi kwa lengo la kuimarisha ulinzi, na kukomesha matukio ya kihalifu ikiwemo matukio ya utekaji.

Hayo yamesemwa leo Oktoba 14, 2018 jijini Arusha na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni kwenye ziara ya kutembelea vitengo vya wizara yake vilivyoko jijini humo, ambapo amesema mazingira ya utendaji kazi wa polisi yamekuwa na changamoto nyingi ambazo baadhi yake zinakwaza utekelezaji wa majukumu yao hivyo Serikali imeamua kuwaongeza nguvu ili kurahisisha majukumu yao.

“Tunampango wakufunga CCTV Camera hasa katika miji mikuu ili kupunguza matukio mbalimbali ikiwemo suala la utekaji, hata ukiangusha sindano lazima ionekane, na ninawaonya wanasiasa uchwara wasitumie tukio hili kujipatia umaarufu”, amesema Masauni.

Masauni ameongeza kuwa , “Matukio ya utekaji ni sifa mbaya sana ila sitaki kulielezea sana maana jana (juzi) Waziri wa Mambo ya Ndani amezungumza mengi ikiwemo mafanikio ya jeshi la polisi, ila hili la mfanyabiashara Mohamed Dewji limechukua sura kubwa hadi duniani kutokana na umaarufu wake na linatisha hata watalii lakini niseme serikali ina mikakati ya kutokomeza hili”.

Taarifa za kutekwa kwa mfanyabiashara huyo anayekadiriwa kuwa na utajiri wa Sh3.5 trilioni zilianza kusambaa Alhamisi ya Oktoba 11, saa 1:00 asubuhi katika mitandao ya kijamii, kabla ya polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam kuthibitisha saa mbili asubuhi.

Watu 26 wanashikiliwa, kutekwa kwa Mo Dewji

0
0
Watu 26 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam akiwemo, Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘Mo’ ambaye pia ni mwekezaji wa klabu hiyo.

Taarifa za kutekwa kwa mfanyabiashara huyo anayekadiriwa kuwa na utajiri wa Sh3.5 trilioni zilianza kusambaa Alhamisi ya Oktoba 11, saa 1:00 asubuhi katika mitandao ya kijamii, kabla ya polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam kuthibitisha saa mbili asubuhi.

Akithibitisha kukamatwa kwa idadi ya watu hadi Jumapili Oktoba 14 ,Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa idadi imeongezeka na kufikia 26 na uchunguzi bado unaendelea.

"Mpaka sasa wanashikiliwa watu 26, na bado uchunguzi unaendelea endapo idadi ikiongezeka au kupungua tutawajuza", amesema Mambosasa.

Kuhusu idadi ya walioachiwa huru na majina yao, Mambosasa amekataa kutoa taarifa hiyo akidai inaweza kuathiri sehemu ya uchunguzi.

VIDEO | Joel Lwaga Ft. Chris Shalom – Umejua Kunifurahisha | Download

0
0
Sikiliza hapa video mpya ya Joel Lwaga Ft. Chris Shalom – Umejua Kunifurahisha . Unaweza kuiDownload pia hapo chini

Wimbo Mpya | Engine – Sakata

CHADEMA Hapakaliki.....Wabunge Wake Saed Kubenea, Antony Komu na Meya Bonifasi Jacob Ndani ya Vita Kali

0
0
Meya wa Ubungo, Boniface Jacob na wabunge wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Anthony Komu, (Moshi Vijijini) na Saed Kubenea (Ubungo), wameingia kwenye vita ya maneno baada ya Meya huyo kudai wabunge hao wanataka kumpoteza kwa kumdhuru.

Sakata hilo limechagizwa baada ya kusambaa kwa ujumbe wa sauti (voice note) zinazodaiwa kuwa za wabunge hao kuanzia jana Jumamosi Oktoba 13, iliyoambatana na ujumbe wa Jacob, akidai wabunge hao wanapanga kumpoteza hadi kuomba msaada wa serikali ili kumuumiza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye wabunge hao wanataka aangushwe lakini Bony amekuwa mwiba katika mpango wao huo.

Katika sauti hizo, wabunge hao wanasikika wakizungumza namna Meya huyo alivyo na nguvu na msaada mkubwa kwa Mbowe, kiasi kwamba ukimuondoa yeye utakuwa umemuumiza Mbowe. 

Hata hivyo, wabunge hao kwa nyakati wamekana sauti hizo si zao, ambapo Kubenea amedai ni mpango wa watu ambao inaonekana  wako kazini kuendeleza mchezo wao kuchafua watu na anaamini imekuja wakati huu kwa sababu ya uchaguzi.

“Ni kwa sababu kuna uchaguzi ndani ya chama na watu wanajipanga kwa ajili ya 2020 na kuna makundi, kwa hiyo watu wanahitaji ubunge, urais, uongozi kwenye chama, sisi tunaamini ni makundi tu ndani ya chama,” amesema Kubenea.

Kwa upande wake Komu, amesema sauti inayosikika si yake, ni sauti zilizochezewa na watu ambao hajui nini malengo yao lakini amepuuza na hatajibu kwenye mitandao kwani si tabia yake.

“Bony mimi natoka naye wapi? Yaani Bony ni kijana mdogo sana, yeye ni Meya wa Ubungo na mimi Mbunge wa Moshi Vijijini, nakutana naye wapi? Yaani tuna maslahi gani tunayopigania mimi na Bony, sina nia na jimbo lake sijui udiwani wake au umeya wake.

Akizungumzia suala hilo, Meya Jacob amesema amesikia sauti hizo na tayari amechukua hatua kwa kukitaarifu chama na mamlaka nyingine husika.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images