Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dr Hindu: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR HINDU popote ulipo . Muone  DR HINDU,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

CHADEMA Wapangua Tuhuma Za Mbunge Wao Aliyejiuzulu Leo na Kuhamia CCM

$
0
0
Baada ya Mbunge wa Jimbo la Ukerewe mkoani Mwanza kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Michael Mkundi kutangaza  kujiuzulu na kuomba kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) usiku wa jana Oktoba 10, CHADEMA wamekanusha tuhuma alizozitoa dhidi ya chama hicho.

Kupitia barua aliyomwandikia Spika wa Bunge Job Ndugai, Mkundi amesema kuwa amechukua uamuzi huo baadaya kutopatiwa ushirikiano na chama chake katika maafa ya kuzama kwa kivuko cha Mv. Nyerere kilichopelekea vifo vya watu zaidi ya 230.

Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema amesema kuwa Mbunge huyo alipatiwa ushirikiano ikiwemo wabunge kuchanga michango na kufika kisiwani Ukara.

"Wabunge walitoa rambirambi zao pamoja na kufika kwenye eneo la tukio pamoja na baadhi ya viongozi labda yeye aseme kama alitaka nani na nani wafike huenda kuna watu alitaka wafike na hawakufanya hivyo", amesema Mrema.

Mrema ameongeza kuwa chama kimeshangazwa na tuhuma hizo na wamejaribu kumtafuta lakini hakupokea simu na baadae hakupatikana tena, na kusema kuwa wanamtakia kila la heri katika maisha yake mapya anayokwenda kuanza huko aendako.

Katika barua yake kwa Spika wa bunge ya kujiuzulu uwanachama wa chama chake cha zamani (CHADEMA) na kujiuzulu nafasi yake ya Udiwani na Ubunge, amedai kuwa Chama chake cha zamani (CHADEMA) kimepoteza heshima na utu baada ya kumtelekeza katika kipindi ambacho alihitaji msaada na ushirikiano kutoka kwenye chama hicho na uongozi wake katika kipindi cha msiba wa ajali ya Kivuko cha MV Nyerere, iliyotokea Septemba 20, 2018.

Uteuzi Mpya Uliofanywa Leo Octoba 11 na Rais Magufuli

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Msemaji wa Simba Haji Manara Afunguka Sakata la Mo Dewji Kutekwa

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Simba umewaomba mashabiki na wanachama wake kuwa watulivu  wakati Jeshi la Polisi likiendelea kumtafuta mwekezaji wa timu hiyo,  Mohammed Dewji “Mo Dewji” ambaye ametekwa leo alfajili.

Wito huo umetolewa baada ya mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kukumbwa na taharuki kuhusiana na tukio la kutekwaji bilionea huyo ambaye mpaka sasa ameifanyia mambo makubwa klabu ya Simba.

Msemaji wa klabu ya Simba, Hajji Manara amesema kwamba familia yake imemuahidi kuwa watulivu na kuwataka mashabiki wa Simba na wapenzi wa soka wote kutulia katika kipindi hiki ambacho vyombo vya usalama vinafanya kazi yake.

"Tumestuka sana, wengine tulipata taarifa mapema, nashukuru Jeshi la Polisi na kamati ya ulinzi na usalama chini ya RC Makonda, tunalowaomba wapenzi wanachama wa Simba watulie, familia yake wameniahidi kuwa watulivu, nimezungumza na mzee wake na familia yake katika hali ya utulivu, kwa hiyo tuwaombe watu watulie tuwaachie vyombo vifanye kazi yake, tunaloamini Mo atapatikana akiwa mzima Inshallah kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na watekaji watakamatwa", amesema Haji Manara.

Sambamba na hilo Haji Manara amewataka watu kutoa taarifa zozote kwa Jeshi la Polisi na sio kuzungumza kiholela, ili kulisaidia jeshi hilo kufanya kazi ya kumtafuta mfanyabiashara huyo.

Mo Dewji ambaye ni mmwekezaji na shabiki mkubwa wa timu ya Simba, ametekwa na watu ambao wametajwa kuwa ni wazungu asubuhi ya leo alipokuwa akienda gym.

Waziri Mkuu Abaini Madudu Fedha Za Dawa Mpwapwa ....Amuagiza Mkuu Wa Wilaya Afanye Uchunguzi Kubaini Zinapokwenda

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Bw. Jabir Shekimweri afanye uchunguzi kuhusu matumizi ya sh. milioni 70 zinazotelewa kila mwezi na Serikali kwa ajili ya kununulia dawa kwenye wilaya hiyo.

"Kilichokuwa kinasemwa na wabunge bungeni nilidhani sicho, nikasema nakuja niyasikie mwenyewe. Kweli wananchi hawaridhiki nimeona. Sasa mkuu wa wilaya shughulikia hili jambo ili kubaini fedha za dawa zinakwenda wapi.”

Alitoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Oktoba 10, 2018) wakati akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule msingi Mpwapwa, ambapo alipokea malalamiko ya wananchi juu ya ukosefu wa dawa. Dawa pekee wanazopewa ni za kutuliza maumivu tu.

Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali kutoa fedha hizo kila mwezi ni kuhakikisha kwamba wananchi wote wanapata huduma za afya popote walipo badala ya kusafiri umbali mrefu kwenda makao makuu ya wilaya.

"Kila mwezi Serikali inatoa zaidi ya sh milioni 70 kwa ajili ya kununulia dawa kwenye wilaya hii ya Mpwapwa. Pia kuna fedha za mfuko wa afya sh. milioni 60 pamoja na fedha za matokeo mazuri ya afya sh. milioni 300 kwa mwaka, shida ya dawa haitakiwi kuwepo hapa.”

Waziri Mkuu alibainisha kuwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwatumikia wananchi ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuwapatia mahitaji muhimu kama huduma bora za afya na ndiyo sababu ya kutoa fedha hizo za dawa.

Awali, kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwawa, Bw. Paul Swea kuwahamishia vijijini baadhi ya watumishi waliopo kwenye idara ya kilimo. Hatua imekuja baada ya kubaini idara hiyo ina watumishi saba ambao wote wapo ofisini badala ya kuwepo vijijini na kuwasaidia wananchi kwenye shughuli za kilimo.

Alimtaka mkurugenzi huyo kuandika barua za uhamisho kwa watumishi hao kwenda vijijini kisha nakala za barua hizo akabidhiwe kabla hajaondoka wilayani Mpwapwa, ambapo alisisitiza kuwa watumishi hao wanapaswa kwenda kufanyakazi na wakulima kwa karibu na kuhakikisha wanawapa elimu ya kutosha itakayowawezesha kulima kwa kisasa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 05

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

‘Wewe…..wewe…..’
Nilijitahidi kumuita ila hakuitika. Nikamaliza kula na nikaacha chombo changu hapa hapa juu ya meza kama utaratibu wa kawaida, kwani kuna wafanyakazia maalumu hushuhulika katika swala la kuosha vyombo, nikarudi bwenini, nikavua nguo zangu, nikajifunga taulo na kueleka katika bafu ambalo tunatumia wanafunzi wa darasa la kwanza kwenye bweni hili. Nikavua taulo langu na kulitundika kwenye msumari, nikajifunga taulo langu kisha taratibu nikaanza kuoga, nikiwa nimejipaka mapovu mwili mzima, akaingia bonge na kundi lake na wakaanza kunicheka huku wakizunguka jambo lililo sababisha nijawe na woga mwingi sana.

ENDELEA
“Wewe sokwe unajifanya hodari kupendwa na wasichana wetu si ndio?”
Bonge alizungumza huku akinisukuma sukuma, kwa woga nilio nao nikajikuta nikishindwa kufanya jambo lolote zaidi ya kushika sabuni yangu walio nikuta nayo.
“Mshikeni”
Bonge aliwaamuru wezake, ambao kwa haraka wakanishika mikono yangu, jambo lililo nifanya nianze kulia hata kabla sijapigwa.
 
“Hehehee, linalia jinga hili”
Bonge alizungumza hukua kicheka na kuwafanya wezake wote walio nishika kuanza kucheka kwa dharau, bonge akaanza kunipiga vibao vya mashavuni huku akiendelea kunicheke. Nikajitahidi kwa nguvu zangu ili mrdi nijitetea kwa vijana hawa ila sikuweza kufanya chochote zaidi ya kuendelea kupigwa vibao vya unyanyasaji na bonge huyu. Akanipokonya sabuni yangu na kuanza kunipakaza nayo kichwani kwa nguvu hadi nikaanza kunishi maumivu.
“Nataka hii rangi yako nyeusi itokea mwilini mwako”
 
Bonge alizungumza huku akiendelea kunisugua sabuni hii mwilini mwangu huku akihamia mgongoni mwangu. Kusema kweli machozi ya hasiri yalizidi kunimwagika. Baaada ya bonge kunifanyia vitendo hivi vya unyanyasaji, akaniamshirisha wezake kuniachia na nikaanguka chini huku nikilia kwa uchungu sana. Wakaongeza nguvu ya bomba hili la maji kisha wakatoka bafuni humu huku wakicheka sana. Taratibu nikanyanyuka huku moyoni mwangu nikijiapiaza kulipiza kisasi kwa bonge na wezake. Nikajitahidi kuoga huku nikiendelea kububujikwa na mchozi, nikamaliza na kurudi chumbani kwangu. Nikabadilisha nguo na kuvaa nguo za michezo huku nikiendelea kuwa na hasira yangu. Nikachukua viatu vyangu vya kuchezea mpira na kueleka uwanjani. Nikawakuta wanafunzi wa darasa la kwanza wakipangwa nani aanze kucheza kwenye mechi ya darasa la pili. Bonge na wezake nao ni miongoni mwa wachezaji walio jitolea katika kucheza mechi hii.
 
“Ethan”
Mwalimu wa michezo wa darasa langu aliniita huku akinitazama.
“Naam”
“Mbona macho yako ni mekundu, vipi una umwa?”
“Hapana mwalimu”
Nilijibu huku nikitazama chni, mwalimu kwa ishara akaniita na kuniwekea kiganja cha mkono wake wa kulia shingoni mwangu ili kunipima joto la mwilini mwangu.
“Joto lako lipo vizuri”
Aliniambia huku akiendelea kunishika shika kwenye shingo yangu.
 
“Ben”
Mwalimu na Bonge akaitika, hapa ndipo nikafahamu jina halisi la bonge.
“Unacheza namba gani?”
“Mfungaji mwalimu”
Nikatamani kucheka kwa kweli, kwa maana huyo anaye sema anaweza kucheza nafasi ya ufungaji ni kibonge hata kutembea kwake ni shuhuli, kinacho mpa uhodari kidogo ni wezake anao tembea nao. Mwalimu wa darasa letu akapanga kikosi chake cha kwanza na mimi na wezangu wengine tukabaki nje. Wachezaji wakapewa jeshi na wakaingia kiwanjani. 
 
“Mbona wewe hujachaguliwa?”
Sauti ya kike ikanistua na kugeuka nyuma, nikamuona binti aliye nisaidia muda wa machana nilipo kuwa nina nyanyaswa na kina bonge akiwa amesimama nyuma yangu huku na yeye akiwa amevalia nguo za mazoezi na walinzi wake wakiwa pembeni yake.
“Nitacheza tu”
“Nawewe kukaa”
Aliniuliza huku akionyesha sehemu ya pembeni yangu ambayo haina mtu katika benchi hili.
“Sawa unaweza kukaa”
 
Taratibu akakaa huku akiwa na tabasamu pana sana.
“Kwa nini wewe hujaenda kucheza na wezako”
“Mimi sipendelei sana michezo ya kike, ninapenda sana mpira”
“Mmmm….sasa huku wanacheza wanafunzi tu wa kiume?”
“Yaa ila nikipata nafasi na mimi nitacheza”
“Hahaaa..unapenda kucheza nafasi gani?”
“Golikipa”
“Weeee huoni ni nafasi ambayo ni hatari”
Msicha huyu hakunijibu chochote zaidi ya macho yetu kuyapeleka golini kwetu na tukashuhudia goli likiingia kwneye nyavu ya goli letu. Mpira ukaanza tena, mwanafunzi mwenzetu akampatia pasi bonge, ila bonge badala ya kupiga pira akapiga hewa na kuanguka chini kama kifurushi cha chumvi. Nikamuona mwalimu akifumba macho yake kwani yeye ndio kama kocha.
 
“Hhahaa ujanja wa bure nje, kumbe uwanjani ni mpuuzi”
Nikatamani kusema kitu ila nikaishia kukaa kimya tu.
“Wamekuone tena baada ya pale holini?”
“Hapana”
“Una uhakika?”
“Ndio”
“Hili bonge linakivunia nafasi ya baba yake kuwa mkuu wa shule nzima, ndio maana linakuwa jeuri”
“Ahaaa kumbe baba yake ni mkuu wa shule”
“Ndio, ila mimi ndio niyamkomesha kwa maana baba yake hata kwangu hazungumzi chochote”
 
“Unaitwa nani?”
“Mim?”
“Ndio”
“Naitwa Camila”
“Aha una jina zuri”
“Asante na wewe ulisema unaitwa nani vile?”
“Ethan”
“Sawa sawa”
Tukashuhudia goli la pili likiingia, hazikupita hata dakika mbili tukafungwa goli la tatu, na mpira ukaenda dakika za mapumziko. Bonge akwa na kazi ya kuwafokea wezake huku akitoka uwanjani akiwa amenunua sana. Wachezaji wakaka chini huku tukiwa tumemzunguka mwalimu wetu wa darasa. Mwalimu akaanza kupanga kikosi wachezaji nilio kuwa nao nje, wakaambia watacheza kipindi cha pili huku mimi peke yangu nikiwa ndio nimeachwa.
“Mwalimu mbona Ethan haujamuingiza”
 
“Hatuta……”
Bonge akaanza kuzungumza, ila Camila akamuonyeshea ngumi na kumfanya bonge kukaa kimya.
“Atacheza ngoja tuwajaribu na hawa wezake”
“Sawa”
Camila akanitazama huku akitabasamu na kunifanya kidogo nijawe na amani kubwa sana moyoni mwangu, kumpata rafiki ambaye kusema kweli ameanza kuwa mtetezi wangu mkubwa kutoka kwa kina bonge na kundi lake. Bonge na wachezaji wengine wakaingia katika kipindi cha pili cha mchezo huku bonge akiwa amefungw akitambaa cha uongozi wa timu. Kusema kweli mwalimu ana mpendelea bonge ila hajumudu kwa lolote uwanjani, zaidi ya kupiga piga tu kelele. Kuingia na kuingia tukafungwa goli la nne lililo mfanya mwalimu kukasirika sana.
 
“Mwalimu kwani Bonge ana msaada gani uwanjani?”
Camila alizungumza kwa hasira huku akimtazama mwalimu. Mwalimu akameza tu mate na kukaa kimya.
“Unamuogopa kwa sababu baba yake ni mkuu wa shule. Sasa mtoe na mimi babu yangu ni raisi”
Camila alizungumza kwa msisitozo nikamuona mwalimu akizidi kuwa mnyonge sana na akapata kigugumizi cha kufanya maamuzi. Mwalimu akamuita refa msaidizi na kumuambia kwamba anahitaji kufanya mabadiliko ya timu.
“Ila wewe unaweza au naingiza ugonjwa zaidi?”
Mwalimu aliniuliza kwa jazba kidogo jambo ambalo likaufanya moyo wangu kufedheheka kidogo.
“Nitaweza”
 
Nilibu kinyonge huku nikimtazama mwalimu usoni mwake. Mpira ulipo toka bonge akaambiwa kwamba anatakiwa kutoka jambo lililo mfanya bonge kukasirika sana. Nikakabidhiwa jezi yenye namba tisini na tisa mgongoni mwangu, yaani namba ya mwisho kwenye mpira.
“Jitahidi Ethan sawa”
Camila alizungumza kwa kuninong’oneza
“Sawa”
Bonge akanitazama kwa macho makali, akashindwa kunifanya chochote kwa maana amemuona Camila akiwa amesimama pembeni yangu. Alipo fika nje ya uwanja akavua kitambaa cha mkononi mwake na kukitupa chini, nikakiokota, nikataka kukivaa ila mwalimu akakataa na kuniambia nikamkabidhi kipa wetu. Nikakimbia huku nikielekea golini, nikamkabidhi golikipa kitambaa na akajifunga mkononi mwake.
 
‘Nicheze wapi Mungu wangu’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiuona uwanjani ni mkubwa sana. Nikawaona washambuliaji wa darasa la kwanza wakija kwa kasi, nikajaribu kumzuia mwenye mpira, ila nikastukia kuona mpira ukipita katikati ya miguu yangu kisha akakimbilia mbele kidogo na kufunga goli la tano. Nikamtazama Camila huku mapigo ya moyo yakinienda kasi sana, woga ukanijaa. Nikimtazama mwalimu, sura yake imejaa hasira, nikiyahamishia macho yangu kwa bonge, yeye ndio usisema, naona hata pale alipo ananitukana matusi mengi sema tu siyasikii kutokana nipo mbali naye.
“Usiogope”
Mchezaji mmoja wa darasa la pili aliye nipitishia mpira wangu katikati ya miguu alizungumza huku akinipiga begani mwangu. 

Wezangu wawili wakachukua mpira na kuuweka katikati ya kiwanja huku mimi nikiwa nje ya dura hili kubwa. Wakanza mpira, na cha kushangaza wakanipatia mpira na wakatawanyika kuniachia kizaa zaa hichi. Nikatazama goli la wapinzani wangu, nikashusha pumzi kidogo kisha nikapiga mpira huu kwa mguu wangu wa kushoto, mpira kwa kasi huku ukielea elea hewani, ukafika golini, na golikipa wa darasa la pili akashindwa kuudaka na ukaingia nyavuni.
 
Nikabaki nikiwa nimeshikwa na butwaa, wanafunzi wenzangu wakaanza kunirukia huku wakishangilia, ila nikashindwa hata nifanye nini kwani sijui imekuwaje hadi mpira huo kufika golini. Nikamtazama Camila nje ya uwanja, nikamuona akininyooshea dole gumba huku akitabasamu.
“Ethan unaweza, unaweza”
 
Wezangu walinipa moyo huku wakitawanyika. Wachezaji wa darasa la pili wakaanza mpira, mchezaji wetu mmoja akafanikiwa kuwapokonya mpira huu na kunipasia, nikautuliaza huku nikiwaangalia wachezaji wa darasa la pili wanavyo nifwata, nikaanza kuichezesha miguu yangu kwa kuizungusha juu ya mpira, wakajaribu kuuchukua, ila nikaugusa kidogo na wakaukosa, nikaanza kukimbia kuelekea golini mwao, kila mchezaji wa darasa la pili alipo jaribu kunifwata, nilijikuta nikimtoka na akaukosa mpira huu, nilipo fika golini nikamtisha kipa kama ninapiga mpira huu kulia, jambo lililo mfanya kipa kuruka kulia, ila kwa mguu wangu wa kushoto nikaupeleka mpira huo upande wa kushoto na kuzifanya nyavu za goli la darasa la pili kutingishika. Goli hili kusema kweli, likanifanya niruke kwa furaha. 
 
Nikakumbatiana na wachezaji wezangu kwani tuna matumaini ya kukomboa magoli matatu yaliyo salia.
‘Hii ndio nafasi ya wewe kuwa na nguvu hapa shule’
Nilimsikia rafiki yangu akiniongelesha katika ufahamu wangu wa akili.
‘Kweli’
‘Ndio, hakisha kwamba watu wanakujua wewe ni nani?’
‘Sawa’
Mpira ukaandelea, nikafanikiwa kuuchukua mpira huu na kama kawaida, nikawachenga wachezaji wa darasa la pili, nilipo fika golini, nikampatia mchezaji mwenzangu, akapiga shuti zito na tukafunga goli la tatu. Uwanja ukaanza kujaa, wanafunzi na waalimu walio kuwa wakiendelea na michezo mengine, wakaanza kuhamia kwenye huu uwanja. 
 
“Tumebakisha goli mbili, tunaweza kujitahidi sawa”
Niliwahimiza wezangu mara baada ya kumaliza kushangilia goli letu hili. Wachezaji wa darasa la pili wakazidi kuchanganyikiwa, kwani mashambulizi yalizidi kuwaelemea, hatukumaliza hata dakika mbili, mchezaji wetu mwengine akapiga kichwa mpiwa nilio piga nikiwa pembeni ya uwanja na kufunga goli la pili.Shangwe zikazidi kurindima uwanjani hapa, watu wakasahau kama tunao cheza hapa ni watoto, ila burudani tunayo itoa kwa kweli ni ya kukata na shoka.
 
“Ethan, Ethan”
Mwalimu aliniita, kwa haraka nikamkibilia hadi alipo na kumshikiliza.
“Tuna dakika tano, jitahidini mukomboe”
“Tano?”
Nilimuliza huku nikimwagikwa na jasho mwili mzima.
“Ndio”
“Sawa mwalimu”
“Ethan”
Camila aliniita, akanionyeshea vidole viwili, nikamnyooshea dole ngumba kwa mkono wangu wa kulia kisha nikarudi kiwanjani. Mpira ukaanza, kutokana nimesha ujua udhaifu wa wachezaji hawa wa darasa la pili, nilicho kifanya ni kuumiliki mpira, kasi na nguvu alizo nijalia Mungu kusema kweli, zinanisaidia kuweza kuminyana nao wanafunzi hawa. Wachezaji wote wa darasa la pili wakawa wananikaba mimi na kuwasahau wezangu, nilipo fika golini kwao kwa bahati mbaya wakanichezea rafu na refa akaweka ipigwe penati. 

Wezangu wakaniomba nipige penati hiyo ila nikakataa, akapiga golikipa wetu, na kwa bahati nzuri akafanikiwa kufunga, ubao wa magoli ukaonyesha goli ni tano kwa tano. Nikamuona mwalimu wetu akikenua meno yote thelathini na mbili yanaonekana, akanionyeshea kwamba zimebaki dakika mbili kabla ya mpira kuisha, mpira katika kuchezwa kwa bahati mbaya ukatoka katika upande wa darasa la pili na refa akaamuru ipigwe kona. 

Tukakusanyika golini mwa darasa la pili, mchezaji wetu mmoja akapiga kona moja maridhwa, bila ya kuhofia kwamba nitaumia au kuvunjika, nikaruka juu na kupiga tikitaka moja nzuri na mripa ukaingia golini, na kuufanya uwanja mzima kujawa na rufaha, wezangu wakanilalia hapa chini nilipo anguka huku machozi ya furaha yakinimwagika usoni mwangu. 
 
“ETHAN….ETHAN…..ETHA…..N”
Uwanja mzima uliimba jina langu, wezangu wakanisaidia kunyanyuka na tukarudi upande wetu. Kitendo cha darasa la pili kuanza mpira, refarii akapiga kipinga cha mwisho akishiaria kwamba mpira umekwisha. Nikamuona Camila akiingia kwa kasi uwanjani, breki ya kwanza akanirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku akiliwa kwa furaha. Mechi tu ya kirafiki imeonekana kama mechi ya mashindano makubwa ya kugombania kombe. 
 
“Nakupenda Ethan, nakupenda sana Ethan”
Camila alizungumza huku akiendela kunikumbatia kwa nguvu na machozi yakizidi kumiminika usoni mwake, nikajikuta nikishindwa hata kuzungumza kwani hara rafiki zake bonge walio nipiga leo bafuni, wote wakanifwata na kunikumbatia, kasoro Bonge tu yeye mwenyewe ndio amebaki nje ya uwanja huku akiwa amenuna sana na dhairi anaonyesha kwamba bado ana kinyongo na mimi.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 97 na 98 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
Huyo dada ambaye ananieleza huyu dereva bodaboda, hafananii kabisa na Linda, kwa maana Linda ni mweusi japo ni mrefu kiasi.
“Alitoka katika mazingira ya aina gani?”   
“Alitoka anakimbia, tena kama picha nilimpiga kwenye simu yangu, yaani ni bonge la totozi”
Dereva bodaboda alizungumza huku akinipatia simu yake, nikaichukua na kuitazama picha hiyo. Sikuamini macho yangu baada ya kumuona Yudia kwenye hii picha akiingia kwenye gari la Linda, jambo  lililo nifanya nijikute nikianza kufura kwa hasira kwa maanaYudia na mwenzake na K2 bado wananiandama sana kwenye maisha yangu.

ENDELEA       
Nikiwa katika hali ya mshangao, nikaona kitanda cha wagojwa, kikiingizwa kwenye gari la wagojwa, kwa haraka nikakimbia hadi kwenye gari, madaktari wakajaribu kunizuia ila nikawazidi nguvu kwa maana nimemuona Linda akiwa yupo hoi maututi.
 
“Ni mke wangu”   
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga, daktari alipo niona ninamaanisha kwa kile ninacho kizungumza akaniruhusu  ili niweze kumuona Linda, ambaye niliweza kumfahamu mkono wake alio  vaa saa, ambao  ulikuwa unaning’inia kwenye kitanda.
“Linda, Linda”   
Nilimuita huku nikiwa ninamtazama uso wake ambao umechakaa kwa kuungua kwa moto na mwili wake una majeraha mengi ya moto.
“Da….dy Dany”
Linda aliniita kwa sauti ya chini sana iliyo zidi kunitisha.
“Ndio nipo hapa nipo hapa mpenzi wangu”
“Ch….chuk….”
Linda alizungumza maneno huku akifumbua kiganja cha mkono wake wa kulio japo umeungua sana, ila akajikaza sana. Nikaona kadi ndogo ya kuhifadhia kumbukumbu, nikaichukua taratibu huku nikiendelea kumtazama usoni mwake.
 
“N….ili…pi…zie kisasi”
Linda aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kukata kata huku hali yake ikiwa mbaya
“Kaka tunakuomba utoke tumuhudumie mgonjwa”
“Dany…..ni…ni…nakupendaa……”
Linda baada ya kuzungumza maeneno hayo akatulia tuli, kwa haraka madaktari wawili wakaanza kuhangaika naye huku wakinihitaji niweze kusogea pembeni kwa maana gari lilisha anza kutembea. 

Machozi yakaendelea kunimwagika usoni mwangu, sikuamini kwamba Linda anakufa kirahisi namna hii, ikiwa ni msichana ambaye alikuwa na malengo makubwa sana kwenye maisha yake. Kila madaktari walivyo jitahidi kuhakikisha kwamba wanajaribu kuyaokoa maisha ya Linda wakawa wamechelewa, hadi tunafika hospitali ya Bombo, Linda, akashushwa kwenye gari, akapakizwa kwenye kitanda ambacho hakupelekwa tena kwenye wodi ya kuhudumiwa, ila moja kwa moja akapelekwa kwenye jengo la kuhifadhia maiti jambo lililo zidi kuumiza moyo wangu.
“Dokta nitahitaji maiti yangu kuifadhiwa hadi niweze kurudi”
“Hapa maiti ikikaa kwa muda mrefu huwa manispaa inachukua jukumu la kumzika”
 
“Hata kama, ila hakikisha kwamba maiti yangu inakaa kwa kipindi chote hadi pale nitakapo rejea, akizikwa kabla  ya mimi kurudi, basi utachukua nafasi yake”
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na hasira sana, hadi daktari akabaki akiwa amenitumbulia macho nikatazama namba ya droo ambayoa ameingizwa Linda, nilipo hakikisha nimeihifadhi vizuri kichwani mwangu nikatoka katika jengo hili la kuhifadhia maiti, huku kichwa changu kikiwa kinamfikiria ni kitu gani ambacho ninaweza kumfanya Yudaia ambaye tayari alisha futika kwenye kichwa changu, ila kwa hili nitahakikisha kwamba nilazima ninamuua tena kwa mateso ambayo hajawahi kuyafikiria kwenye maisha yake kwamba yatatokea kwenye maisha yake.
 
Kitendo cha kutoka nje ya geti la hospitali, nikakumbuka namba niliyo pewa na binti wa kiarabu kwenye duka la kubadilishia pesa, nikakitoa kikaratasi kwenye mfuko wangu nikaitazama namba ya simu ambayo ameiandika. Nikatazama huku na kule, kwenye mabenchi ya kusubiria wagonjwa, nikawaona baadhi ya vijana wakiwa wamekaa wakichezea chezea simu zao. Nikapiga hatua hadi walipo.
“Madogo niaje?”
“Poa poa bro”
“Oya dogo simu yako ina vocha hapo, kuna mtu nahitaji kumpigia”
“Yaaa ina bando la kutosha”
“Ninakuomba uniazime”
“Poa ila pigia hapa hapa si unajua mjini hapa”
“Usijali dogo”
Dogo akanipatia simu yake, nikaanza kuingiza namba ya simu ya binti wa kiarabu. Kwa bahati nzuri namba yake ikaanza kuita, haikuchukua hata sekunde nyingi ikapokelewa.
“Mambo vipi?”
“Safi nani?
“Dany, ni muda mchache nilitoka hapo dukani kwako, nilikuja kubadili pesa za kikenya”
“Ahaa Dany mambo vipi, upo wapi?”
“Nipo Bombo hapa hospitalini, kuna mgonjwa nilikuja kumuona”
 
“Sawa, ninaweza kuja kukuchukua?”
“Ndio maana nikakupigia, ila namba sio ya kwangu, mimi nimekaa kwenye hizi benchi ukija hapa utanikuta nimekaa”
“Sawa nipe dakika kumi na tano nitakuwa nimesha fika hapo”
“Sawa”
Nikakata simu, nikamkabidhi dogo simu  yake huku nikimpatia noti ya shilingi elfu kumi kama asante.
“Asante sana kaka”
“Usijali dogo”
Nikakaa benchi hizi huku nikiendelea kufikiria ni wapi ambapo ninaweza kumpata Yudia. Nikatazama memory card hii ambayo nimepatiwa na Linda. Sifahamu ndani imehifadhiwa vitu gani ila nina hamu sana ya kuweza kufahamu ni kitu gani ambacho kipo humu ndani. Gari nyeusi iana ya Toyota Harrier ikasimama pembeni ya benchi hizi, honi ya gari hilo likamfanya kila mtu aliye kaa katika hii sehemu kulitazama gari hili, kioo kikashushwa nikamuona binti wa kiarabu akiniita, nikanyanyuka na kumfwata sehemu alipo.
 
“Ingia”
Alizungumza, nikafungua mlango wa mbele wa gari, nikaingia nikatzama siti ya nyuma hakuna mtu. Binti huyu akafunga kioo cha gari, akageuza gari na kuondoka eneo hil la hospitalini.
“Za muda Dany?”
“Safi tu”
“Ulikuja kumuona nani?”
“Ahaa kuna rafiki yangu nilikuja kumuona, kidogo malaria inamsumbu”
Nilimdanganya binti huyu na wala sikuhitaji aweze kunifahamu kwamba mimi ni nani.
“Ila anaendeleaje?”
“Yupo vizuri kiasi, siku mbili hizi watakwenda kumruhusu”
“Pole yake, ehee vipi unaelekea wapi kwa sasa?”
“Kusema ukweli kwa sasa sina pa kuelekea, ndio maana nikaona nikupigie ili kuweza kuonana na wewe tuzungumze”
“Kweli huna pa kuelekea Dany?”
 
“Yaa sina pa kuelekea, labda upange wewe”
“Okay, mmmmm…….tuelekee Tanga beach resort”
“Hakuna shaka katika hilo”
Binti huyu akaonyesha furaha kubwa aliyo kuwa nayo, sikujua lengo lake kubwa haswa ni nini, japo akili zangu zinanipekeka kwamba amenipenda kimapenzi japo sina uhakika sana katika hilo.
“Hivi unaitwa nani  vile?”
“Radhia, ila mara nyingi sana huwa wananiita Cajol”
“Basi na mimi nitakuita Cajol”
“Sawa upendavyo wewe”
Tukafika kwenye hoteli hii iliyopo pembezoni mwa bahari. Tukatafuta sehemu iliyo tulia kisha tukaketi. Kila mmoja akakaa kimya kwa dakika kadhaa akisubiria mwenzake aweze kuzungumza. Cajol akabaki akiwa anatabsamu tu, muhudumu akafika sehemu tulipo.
 
“Msikilize kaka hapo”
Cajol alizungumza huku akinitzama usoni mwangu, muhudumu akanitazama.
“Muna chakula gani?”
Akanipatia kkitabu kilicho andikwa idadi ya chakula kilichopo katika hii hoteli, nikakisoma taratibu kisha nikamuonyesha ni chakula gani ninacho kihitaji. Nikamuagizia na kinywaji ambacho ni kilevi hadi Cajol akanitazama.
“Unatumia kilevi?”
“Mara moja moja tu”
“Okay na mimi niletee kinywaji kama alicho agiza yeye”
“Je chakula”
“Hicho hicho kama chake”
Muhudumu akaondoka na kutuacha tukiwa tunatazamana, nikayatazama mandhari ya hili eneo, yananikumbusha kipindi nilipo kuwa na mama alipokuwa anatafutwa na majambazi wa meya wa jiji.
 
“Mbona unalishangaa lile eneo pale?”
“Ahaa…linanikumbusha mbali sana”
“Ulisha wahi kuja na mpenzi wako hapa nini?”
“Hapana, nilikuja na mama yangu, ambaye kwa sasa ni marehemu”
“Ohoo pole sana Dany, hata mimi mama yangu kwa sasa ni marehemu”
“Pole na wewe”
“Asante. Dany kusema kweli siamini kwenye maisha yanagu kama leo hii nipo na wewe, kwa maana ni kwa kipindi kirefu sana nilikutafuta ila sikuweza kukuona”
“Ni mihangaiko ya hapa na pele ndio ilinifanya niwe bize sana”
“Pole sana, Dany nahisi kwamba unaweza kunishangaa kwa kile ambacho nitakwenda kukizungumza”
Muhudumu akafika kwenye meza yetu na kutufanya tukatishe mazungumzo yetu, akatuwekea vinywaji tulivyo muagiza.
 
“Karibuni, chakula kinakuja muda si mrefu”
“Asante”
Muhudumu baada ya kuondoka, Cajoli akaendelea kuzungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Dany ni aibu kwa mtoto wa kike kuweza kuweka hisia zake za mapenzi mbele ya mwanaume, ila kwangu ninaomba niweze kuweka hivyo kwa maana kuseme kweli ninakupenda kutoka moyoni mwangu, na hilo jambo hadi baba yangu analifahamu, na nilikataa wanaume kadhaa ambao walipanga kunioa.”
Nikajikuta nikishusha pumzi huku nikimtazama Cajoli usoni mwake.
‘Masikini weee, laiti angejua moyo wangu kwa sasa hauna mapenzi ya kweli kwa mwanamke, wala asinge zungumza hichi anacho kizungumza’
 
Nilijisemea kimoyo moyo, huku nikimtazama Cajoli, sikuhitaji kuyakwepesha macho yangu usoni mwake, kwa maana ninahitaji kufahamu kama ni mkweli au ni muongo. Machozi yakaanza kumlenga lenga Cajoli hadi nikabaki nikkiwa ninamshangaa.
“Dany nilijipangia kukaa kwa miaka kumi ndio nije kukubali kuwa kimapenzi na mwanaume tofauti na wewe, kwa maana ningefahamu kwamba umekufa au upo mbali na sehemu nilipo mimi na ingebaki kuwa kama ndoto tu kwamba nimekutana na mwanaume ambaye nilimpenda ila sikuweza kumueleza kile ambacho nipo nacho moyoni”
“Cajol”
 
“Mmmmm”
“Unaniamini kitu gani hadi unanikabidhi moyo wako kwangu, ikiwa hunijui kama ni mkweli kwenye mahusiano au nimuongo”
“Danya kulifahamu au kuto kulifahamu hilo swala ni jambo ambalo wala halite niumiza moyo wangu, kikubwa ni kuweza kufahamu kwamba nimekupata wewe. Tazama sasa ni mwaka wa nne huu nimekuwa nikikusubiria wewe huoni ni…….”
Cajoli akanyamaza baada ya muhudumu kufika katika hili eneo. Akakiweka chakula mezani, akatukaribisha na kuondoka.
“Cajoli utakubali kuwa na mimi katika hii halia mbayo nipo nayo”
“Dany hali yako mimi sinto ijali, sinto jail kama ulikuwa unatafutwa na askari au laaa”
 
Nikastuka kidogo baada ya kugundua kwamba mimi nilikuwa nikisakwa na askari Tanza nzima, ila ni miaka michache iliyo pita nyuma.
“Nilikuwa nikikuombea kila siku, nilikuwa nikihakikisha kwamba haipiti siku ninakuombea mwenyezi Mungu kuweza kukulinda na mikasa yote hiyo ambayo unapitia na wala sikuwahi kumuambia mtu yoyote kwamba mwanaume ambaye ninampenda ni gaidi ambaye anatafutwa na serikali, japo nilijaribu kutembea kwenye mikoa ambayo nilihisi ninaweza kukupata ila sikufanikiwa”
Maneno ya Cajoli yakanifanya nizidi kuwa mpole, kati ya wanawake ambao nilisha wahi kuwa nao sikuwahi kusikia mwanamke hata mmoja ambaye anasema kwamba aniombea ili niwe wake.
 
Nikiwa katika kutazama tazama watu wanao ingia katika eneo hili, nikamuona Yudia akikatiza kwenye moja ya bustani ya hii hoteli akiwa ameongozana na jamaa wawili walio valia suti nyeusi, nikataka kunyanyuka kumfwata ila Cajoli akaniwahi kunishika mkono, akanyanyuka na kunikumbatia kwa haraka na kuanza kuninyonya denda, na kuniziba sura yangu kwa kupitia jicho langu la upande wa kushoto, nikamuona Yudia akisimama na kunitazama kwa macho makali sana jambo lililo nifanya nizidi kumnyonya denda Cajoli huku nikiiziba sura yangu kwenye uso wa Cajoli ili Yudia na watu wake wasije kuanzisha varangati nikiwa na huyu binti wa watu ambaye sihitaji matatizo yangu niliyo nayo yamkumbe yeye kama yaliyo mkuta Linda ambaye kwa sasa yupo mochwari.
                                                                           
AISIIIII……….U KILL ME 98                                                                                                

Yudia na watu wake wakaondoka, na kunifanya nimuachie Cajoli ambaye tayari alisha anza kulainika kwa jinsi ninavyo mnyonya denda.
“Nisubirie mara moja”   
“Unakwenda wapi Dany?”
“Ninakuja mara moja usiondoke”
“Sawa”
Nikaanza kutembea kwa mwendo wa haraka kuelekea sehemu alipo kwenda Yudia. Nikatoka hadi nje ya hoteli na kuona gari aina ya Toyota VX V8 likiondoka katika eneo hili la hoteli, nikazitazama namba zake za usajili na kuzikremisha.
“Samahani dada hili gari lililo toka wamepanda watu wangapi?”
Nilimuuliza muhudumu wa hii hoteli ambaye nimemkuta kipindi ninatoka nje.
“Wamepanda watatu, mdada mmoja na wengine ni wanaume”
“Shukrani sana, huwa wanapendaga kuja hapa?”
“Hapana ndio kwanza ninawaona leo”
Asante dada yangu”
Nikarudi sehemu nilipo muacha Cajoli, nikavuta kiti na kukaa.
“Mwenzio nimesha anza kula”
“Hakuna tabu, ehee niambie”
“Safi, natamani tukitoka hapa twende kwangu”
“Hilo halina tatizo kabisa”
“Kweli Dany”
“Yaa”
 
“Yaani sitamani hata kula hichi chakula naomba twende sasa hivi nyumbani kwangu”
“Tumalizie kula kwanza”
Tukaendelea kula haraka haraka, hadi tukamaliza kula. Tukamuita muhudumu aliye tuhudumia, Cajol akamlipa kiasi cha garama zote wanazo tudai, kisha tukaondoka eneo hili la hoteli.
“Mimi ninaishi maeneo haya haya ya hapa Sahare”
“Ahaa”
“Yaa kwangu sio mbali sana na hapa”
Cajol aliendelea kuzungumza huku akiendesha gari lake. Tukafika kwenye moja ya nyumba yenye geti kubwa, akapiga honi, geti likafunguliwa na mlinzi. Taratibu akaingiza gari lake ndani na kulisimamisha kwenye maegesho yaliyomo ndani ya hii nyumba yake.
“Dany karibu sana hapa ndio kwangu”
“Asante”
Cajol akatoa funguo kwenye pochi yake na kufungua mlango wa kuingilia ndani.
“Dany karibu jisikie upo kwako kabisa, na kuwa na amani”
“Asante”
 
Kitendo cha Cajil kufunga mlango wake wa mbele, akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kunionya midomo yangu. Sikuwa na hiyana kabisa zaidi ya kuanza kumburudisha Cajoli binti kiarabu. Ndani ya muda mchache tukajikuta tukiwa tumezama kwenye dimbwi moja kubwa sana la mapenzi. Kila mmoja akajitahidi kwa uwezo wake kuhakikisha kwamba anamburudisha mwenzake.
“Dany nakupenda sana mwanaume wa ndoto zangu”
“Ninakupenda pia”
“Kweli Dany?”
“Ndio”
Majibu yangu yote hayana ukweli kwa maana kwa maisha yangu ya sasa sina upendo wowote moyoni mwangu, kwa maana nipo katika kipindi kikubwa sana cha kuweza kuwakabili maadui zangu ambao ndio kwanza nao ninahisi kwamba wanaaza kuniwinda. Cajoli akanikumbatiwa kwa nguvu huku machozi yakimwagika.
“Dany nakupenda sana, sihitaji kuwa mbali na wewe kwenye haya maisha yangu”
“Usijali kwa hapa nilipo fikia nitahakikisha kwamba ninakulinda na kukuheshimu, sinto hitaji adui yoyote kuweza kukushika wala kukudhuru”
 
Nilizungumza maneno ambayo sikufahamu hata yametokea wapi, machozi taratibu yakanza kunimwagika, si kwamba ninampenda Cajoli ika nikutokana na kuikumbuka familia yangu. Taratibu nikamuachia Cajoli na kujipangusa machozi yangu usoni.
“Una laptop?”
“Yaa ninayo”
“Unaweza kunisaidia pamoja na adapter, nikaweka memory card?”
“Ndio ninavyo njoo huku”
Tukaingia chumbani kwa Cajoli, nikiwa nimeishika shuruali yangu mkononi. Nikaitoa memory card ambayo nilikabidhiwa na Linda. Cajoli akaniwashia laptop yake na kunikabiza adapter ya kuwekea memory card. Nikaiweka, hazikupita sekunde nyingi, adapter ikasoma nikakutana na faili moja lililo andikwa kwa maandishi makubwa yanayo someka ‘SIRI’. Cajoli akanitazama usoni mwangu.
 
“Ngoja nikupishe ufanye kazi yako”
“Sawa”
Cajoli akaingia bafuani na kuniacha chumbani, nikafungua faili hili na kukuta video tatu pamoja na faili moja ambalo limeifadhiwa maandishi kadhaa. Nikafungua faili hilo na kuanza kulisoma taratibu.
‘Hii ni siri ambayo ni kubwa katika maisha yangu, kwa jina ninaitwa Linda Jonson, mimi ndio mtu ambaye nimehusika na kumficha mke wa makamu  wa raisi Eddy Godwin. Nilipewa kazi ya kumuua Phidaya na K2 kwa ajili ya wivu wake wa kimapenzi kwa kiongozi huyu.’
 
Nikajikuta nikimeza mate huku nikikaa vizuri kwenye kitanda nakuendelea kuisoma story hii.
‘Sikuwa ni mwanamke mwenye roho mbaya kwa maana niiye agizwa kumuua ni mwanamke mwenzangu. Kazi hii nilipewa na mwenzangu kwa jina anaye itwa Mariam. Mariam alipewa kazi ya kumua aliyekuwa mkuu wa mkoa Bi Joyce pamoja na familia yake.’
Nilijikuta nikistuka huku nikikaa vizuri kuendelea kuisoma stori hii ambayo sasa ninaanza kuupata ukweli kwa nani ni muhusika wa mauaji ya familia yangu.
‘Mariam aliweza kutekeleza azimio lake ambalo aliweza kuwepea, alifanya hayo yote kwa shinikizo la kuyalinda maisha ya mama yake. 
 
Wahusika wakuu katika kuwateka na kuwatumikisha mabinti wadogo katika meli kubwa iliyopo katikati ya bahari ni K2, ambaye kwa sasa yupo mbioni katika kinyang’anyiro cha kuwa raisi. Msaidizi wake mkuu ni Yudia, ambaye ni adui yangu mkubwa sana. Wa tatu ni Livna Livba huyu ni mkuu wa kikosi cha kuongoza wasichana wote wanao patikana kwenye gereza hilo’
Mapigo  ya moyo kwa mbali nikaanza kuyasikia yakinienda kasi. Sikutaka kuendelea kusoma maelekezo mengine, nikafungua video moja na kuanza kuona mandhari ya ndani ya meli hiyo ambayo ndipo walipo kusanywa wasichana wengi kutoka mataifa mbali mbali.
Nikafungua video nyingine, video hii inaonyesha jisni mama yangu aliyo kuwa akijitahidi kupambana na Mariam katika nyumba ambayo wala sielewi ni nyumba ya wapi. Mariam akafanikiwa kumtuliza mama yangu na kumchinja kabisa shingo yake. 
 
Machozi yakaanza kunimwagika usoni mwangu, yaliyo changanyikana na hasira kali. Mauaji hayo hayakuishia kwa mama yangu yakendelea hadi kwa Asma, Diana na mwanangu wa kike. Matukio yote haya yamerekodiwa na kamera za ulinzi zilizopo kwenye eneo hilo la mauaji.
“Dany”
Nilisikia sauti ya Cajol akiniita pembeni yangu, nikamtazama huku machozi yakiendelea kunimwagika usoni mwangu. Taratibu akanisogelea na kukaa pembeni yangu.
“Hawa ni kina nani?”
“Hii ni familia yangu, yote imesha uwawa”
“Mungu wangu, ndio wameuwawa kikatili kiasi hichi?”
“Yaa. Cajoli mwanaume ambaye upo naye sidhani kwamba ni sahihi kwenye maisha yako”
 
“Noo Dany, mimi nimerdhika na wewe, sijalishi kwamba wewe ni gaidi, au laa. Mimi ninakupenda na ninakuhitaji kwenye maisha yangu. Nitakusaidia kwa chochote kila ambacho utasema nikusaidie”
“Cajoli wakati nilio kuwa nao kwa hivi sasa ni mgumu sana, ni wakati ambao ninaweza kukuingiza wewe kwenye matatizo, sihitaji kukupoteza na wewe, sihitaji kukuona damu yako inamwagika pasipo kuwa na kosa lolo……”
Cajoli akaniziba mdomo wangu kwa kutumia kidole chake.
“Dany sijalishi nitamwagikwa na damu, sijali hilo, ninacho kihitaji ni kuhakikisha kwamba unashinda, unakuwa na furaha. Mimi nina pesa, mimi ninajuana na watu wengi, ninaweza kufanya chochote kupitia pesa yangu”
“Cajoli pesa katika hili aihitajiki, kwa maana watu wote ambao ninakwenda kukabiliana nao ni watu wenye nguvu kubwa sana hapa nchini, mmoja wao akiwa ni raisi huyu mpya wa hii nchi”
 
“Haijalishi Dany, mimi najua kitu cha kufanya, wewe niambie ni nini ambacho unakihitaji kwa sasa hivi”
“Ninacho hitaji ni kuanza kumsaka mtu mmoja baada ya mwengine nikiwa peke yangu, kama ni kunisaidia sihitaji ujulikane kama unanisaidia, kwa maana wakirudi kwako ni lazima watakuua”
“Sijali hilo Dany nitahakikisha kwamba kila jambo linakwenda vizuri mpenzi wangu”
“Sasa hivi ni saa ngapi?”
“Saa nne kasoro usiku”
“Ninaweza kupata wapi silaha”
“Silaha ya aina gani?”
“Bastola”
“Ninayo bastola yangu ambayo ninaitumia kwenye ulinzI binafsi”
“Unaweza kunipatia”
“Yaa”
Cajol akafungua kabati lake la nguo na kutoa bastola yake. Akanikabidhi, nikaikagua bastola yake na kukuta ina risasi za kutosha.
“Kwenye laptop yako ninaweza kuangali ni wapi ninapo weza kupata gari fulani”
 
“Yaa ninaweza kukufanyia hivyo”
Cajol akachukua  laptop yake, nikamtajia namba ambazo nilizikremisha kwenye gari alilo ondoka nalo Yudia na watu wake.
“Ina search”
“Nimelipata, kwa sasa lipo maeneo ya Mkonge hoteli”
“Nahitaji kwenda sasa hivi”
“Muda huu?”
“Ndio, kuna kazi ninahitaji kwenda kuifanya, nikitoka hakikisha unafunga milango na usifungue hadi pale nitakopo rudi”
“Sawa”
Nikaingia bafuni na kuoga kwa haraka kwa ajili ya kutoa jasho la mapenzi, nikarudi chumbani na kumkuta Cajoli  akiwa ameniandalia nguo zangu  ambazo nilikuwa nimezivaa, ila akaniongezea na sweta mbalo lina kofia yake kwa juu. Nikavaa nguo kwa haraka haraka, nikavaa na sweta hili, baada ya kuhakikisha kwamba nipo vizuri, nikaagana na Cajoli.
 
“Dany chukua simu hii nitakuwa ninakupa maelekezo kama gari hilo linaweza kuondoka katika hoteli hiyo”
“Sawa”
Nikachukua simu nyingine ya Cajoli, akanikabidhi na funguo za gari lake kisha nikaondoka. Safari ya kuelekea katika hoteli ya Mkonge hoteli haikuchukua muda mrefu nikafika, nikasimamisha gari kwenye maegesho, simu ya mfukoni mwangu ikaita ikanibidi kuitoa simu na kuipokea huku nikiwa nimesimama pembeni ya gari langu.
“Dany umefika”
Niliisikia sauti ya Cajoli akizungumza kwenye simu, ila kabla sijajibu nikahisi kitu kizito kikinigandamiza kichwani mwangu huku nikisikia sauti nzito ya mwanaume ikiniamrisha kwamba nisigeuke nyuma la sivyo atanichangua ubongo wangu.

==>>ITAENDELEA KESHO

Updates za Mchana: Polisi Yasema Mo Dewji Bado Hajapatikana, Oparesheni Kali ya Kumtafuta Bado Inaendelea

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amezungumza mchana huu kuhusiana na tukio la kutekwa mfanyabiashara maarufu nchini, Mo Dewji ambapo amesema hadi mchana huu taarifa rasmi ni kwamba Mo bado hajapatikana na watekaji bado hawajakamatwa.

Mambosasa amewataka wananchi kuzipuuza taarifa zinazosambaa mitaani kwamba Mo kapatika akiwa Coco beach kwa kuwa ni za uongo na wala hazijatolewa na ofisi yake.

Amesema jeshi la polisi linaendelea na Opareshen kali kwa kushirikisha mikoa mitatu kuhakikisha Mo Dewji anapatikana na watekaji wanatiwa Mbaroni

Waziri Mkuu: Atakayedokoa Mali Ya Umma Hatovumiliwa....Awasisitiza Watumishi Wa Umma Wawe Waadilifu Na Waaminifu

$
0
0


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema vitendo vya udokozi wa mali ya umma havitavumiliwa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, hivyo amewataka watumishi wawe waadilifu na waaminifu wanapotekeleza majukumu yao.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Oktoba 11, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo akiwa katika ziara mkoani Dodoma.

Waziri Mkuu amesema Serikali haitamvumilia watumishi wa umma ambaye si muadilifu, mvivu na wala rushwa hawana nafasi, hivyo ni lazima wajibike na ambao watashindwa kutekeleza majukumu yao watapa shida kwenye Serikali hii. “Hakuna mchezo kwenye Serikali hii, watumishi wa umma wanapaswa kulitambua hili.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewataka watumishi hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kufuata maelekezo yaliyotolewa kwenye Ilani ya uchaguzi Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2015/2020.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka watumishi hao wahakikishe wanapanga ratiba ya kwenda kuwatembelea wananchi hususani waishio vijijini na kushirikiana nao katika kutatua kero zinazowakabili si kukaa ofisni.

Waziri Mkuu amesema kila mtumishi kwenye idara yake anapaswa kwenda kwa wananchi, kama ana siku tano za kufanyakazi kwa wiki basi siku tatu azitumie kwenda kwa wananchi kutatua changamoto zao na kama ana siku sita, siku nne azitumike kuwafikia wananchi.

Akizungumzia kuhusu idara ya kilimo, Waziri Mkuu amesema Maafisa Kilimo wote wanatakiwa kwenda vijijini kufanyakazi na si kubaki ofisini na alishatoa agizo hilo alipokutana nao jijini Dodoma. “Wakulima huko vijijini wanahangaika peke yao huku maafisa kilimo wamekaa ofisini.”

Waziri Mkuu amewataka watumishi wa umma wazingatie itifaki, mipaka ya madaraka yao pamoja na kuheshimu viongozi. Amesema hata kama ni mkuu wa idara pia anapaswa kumheshimu mtumishi aliyekuwa chini yake.

Awali,Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kongwa, aliishukuru Serikali kwa kutatua kero mbalimbali ikiwemo changamoto ya ukosefu wa maji pamoja na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mbande hadi Kongwa ambapo aliomba ujenzi huo uendelee hadi Mpwapwa.

Aidha, aliiomba serikali kugawa kwa vipande eneo la Rachi ya Taifa lililopo wilayani hapo kwa wafungaji kwa kuwa limekuwa halitumiki. “Napendekeza wananchi wapewe vitalu kisha wafuge kwa njia ya kisasa kwa kupatwa mbegu bora. Hii itasadia kuzalisha bidhaa bora za nyama na maziwa pamoja na wananchi kupata ajira.”

NayeMkuu wa  Wilaya ya Kongwa, Deo Ndejembi aliishukuru Serikali kwa kuwapatia fedha za kutekeleza miradi mbalimbali wilayani humo, hadi sasa wameshapokea zaidi ya sh. bilioni tatu kwa ajili ya miradi ya maji.

Kuhusu upatikanaji wa dawa kwenye wilaya hiyo alisema umefikia zaidi ya asilimia 90 na  wananchi wanapata huduma ya matibabu kwa ubora.

“Pia Kongwa hakuna njaa. Tumeweza kuhamasisha kilimo cha mtama kwenye vijiji 89 ambapo Mbunge (Ndugai) alitoa sh. milioni saba kwa ajili ya mbegu ambapo sasa tumeweza kufikia ziada ya tani laki mbili.”

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alisema mafanikio ya Kongwa ni matokeo ya uwepo wa amani na utulivu kwenye eneo hilo.

Hata hivyo, alimuomba Waziri Mkuu baada ya rais kusaini sheria ya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi ni muhimu ikapewa kipaumbele pamoja na miji mingine midogo inayozunguka jiji la Dodoma kupata fedha za kupima maeneo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya October 12

TAKUKURU Yawafikisha Mahakama Vigogo ACACIA Kwa Rushwa ya Bilioni 13.5/-

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoani Mara, imewafikisha mahakamani watuhumiwa saba akiwamo raia wa kigeni wa mgodi wa North Mara Gold Mine ulio chini ya kampuni ya Acacia kwa kosa la rushwa ya Sh. bilioni 13.5.

Fedha hizo Sh. 11,348,781,535 na Dola za Marekani 925,222 (sawa na Sh. 2,116,850,177), zinadaiwa kutolewa kwa lengo la kuwezesha upendeleo katika uthamini na maamuzi mbalimbali ya vijiji dhidi ya mgodi.

Watuhumiwa hao walifikishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi, Veronika Mgendi, wakikabiliwa na kesi tano tofauti zinazohusu makosa ya kuomba na kupokea rushwa kutoka kwenye mgodi huo, kinyume na kifungu 15 (1) na (2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.

Waliofikishwa mahakamani ni watumishi wa umma ngazi ya uthamini, Adam Yusufu, Peter Mrema na Joseph Kleruu.

Wengine ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Kewanja, Tanzania Omtima, Diwani kata ya Kemambo, Bogomba Chichake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyakunguru, Abel Nyakibaru na raia wa kigeni ambaye ni Mhasibu wa mgodi huo, Marten Vande Walt.

Akisoma hati ya mashtaka, Mwanasheria wa Takukuru, Leonard Swai, alidai kuwa watuhumiwa hao walikula njama za kutenda makosa hayo kati ya Januari 2016 hadi Mei 2018, kwa nyakati na siku tofauti.

Alidai kuwa Diwani Rashid kwa kipindi hicho alijipatia zabuni mbalimbali kwenye mgodi huo kwa njia ya rushwa iliyomwezesha kupata Sh. 7,709,575,914.19.

Swai alidai kuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kewanja, Tanzania O’mtima alijipatia Sh. 1,102,880,803 alizopokea kutoka mgodi wa North Mara kama kishawishi ili shule ya Nyabigina isihamishwe kutoka Mrwambe kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na badala yake ijengwe Mrwambe kwa unafuu wa gharama kwa mgodi wa North Mara.

Kwa mujibu wa mwanasheria huyo, Mwenyekiti wa kijiji cha Nyakunguru, Nyakibari alipokea rushwa ya Sh. 966,687,343 iliyolipwa kwake kama fidia kutoka mgodi wa North Mara ili kumshawishi kusaidia mgodi huo kutowalipa baadhi ya wanakijiji fidia.

Alidai mahakamani kuwa, Mthamini Mkuu na Mshauri wa serikali kwa mambo yanayohusu uthamini, Kleruu katika kipindi cha mwezi Mei na Juni 2013, alipokea rushwa ya Dola za Marekani 243,650.75 (Sh. bilioni 2.1) kutoka North Mara kama kishawishi cha kuwapa upendeleo mgodi huo katika uthamini wa mazao na mali za wananchi na hivyo kuwakandamiza wananchi wanaozunguka mgodi.

Alidai, kutokana na hali hiyo mtuhumiwa aliwapa ahueni isiyo halali wamiliki wa mgodi huo.

Swai alidai kuwa mtuhumiwa huyo akiwa kama Mthamini Mkuu wa Serikali, alijipatia kiasi cha Dola za Marekani, 681,572 (sawa na Sh. bilioni 1.5) kutoka kweye mgodi huo kama kishawishi cha kampuni yake binafsi kupewa kazi ya upimaji na uthamini wa mali na mazao ya wananchi kupisha mgodi huo kuendelea na uchimbaji.

Aidha, alidai O’mtima akiwa Mwenyekiti wa kijiji cha Kewanja, alipokea rushwa Sh. 90,251,475 kutoka katika mgodi wa North Mara, kama kishawishi cha kusaidia mgodi kupata upendeleo katika maamuzi mbalimbali ambayo yatatolewa na serikali ya kijiji.

Aidha, ilidaiwa Welf, ambaye ni raia wa kigeni wa Afrika Kusini, akiwa Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Meneja wa Ardhi wa North Mara Gold Mine, akishirikiana na Johaness Jansen Van Vuuren, ambaye alikuwa meneja kwa pamoja walitoa Sh. 93,896,000 kwa Adam Yususu Adam, aliyekuwa Mthamini Mkuu katika kikosi kazi kama kishawishi cha kutoa upendeleo wa mgodi katika uthamini ambao ungefanywa na kikosi kazi.

Mwanasheria huyo alidai kuwa, Yusumu ambaye ni mthamini mkuu anashtakiwa kwa kosa la kupokea rushwa ya Sh. 93,896,000 kutoka mgodini humo, kinyume cha sheria.

Aidha, Mrema akiwa Mthamini Mkuu katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, anadaiwa kupokea Sh. 30,000,000 kutoka kwa Johaneness Jansen Van Vuuren, aliyekuwa Meneja wa mgodi kama kishawishi cha kumwezesha awasaidie North Mara kuwapa upendeleo katika uthamini ambao ungeendelea.

Viwanja Vinauzwa: Low, Medium and High Density plots for sale: Bunju & Mapinga

$
0
0
Low, Medium and High Density plots for sale: Bunju & Mapinga

Wenye uhitaji wa viwanja vikubwa kwa bei nafuu mnakaribishwa.


Kwa Mapinga Kimele, vipo viwanja vya ukubwa 10/20 bei milion 2, 20/20 bei milion 4, 20/30 bei milion 6, 20/40 bei milion 8, na 35/40 bei milion 18.


Bei hizi ni kwa wateja wanaolipa kwa awamu. Endapo mteja atalipa pesa yote (kwa mkupuo mmoja) bei itapungua kwa tsh 500,000 kila kiwanja. Umbali kutoka main road ni kilometa 3.

Pia vipo viwanja vikubwa sana (low density plots) eneo la Baobab sec (Mapinga to Kibaha Road) vyenye ukubwa sqm 1500 kwa tsh 20 mil, sqm 1900 kwa tsh 25 mil, sqm 2300 kwa tsh 30 mil, na sqm 3000 kwa tsh 39 mil.

Kwa Bunju (dsm) vipo viwanja kuanzia milion 50 kwa sqm 1700 mpaka milion 100 kwa sqm 3000.

Karibu Mapinga (mji wa baridi na hewa safi). Ujanja ni kununua/kuongeza akiba ya viwanja (assets) kwa ajili yako na kizazi chako. Wachumi wanasema "Money Is What It Does"
Ukipata taarifa hii mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Hakuna dalali, mpigie mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709

Waziri Wa Kilimo Dkt Tizeba Ashuhudia Utiaji Saini Hati Ya Maridhiano Ukopeshaji Wa Matrekta

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Morogoro
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba  jana  tarehe 11 Octoba 2018 ameshuhudia utiaji saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta kwa vyama vya ushirika vya msingi.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika Ukumbi mdogo wa Mikutano katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo (SUA) Mjini Morogoro Waziri Tizeba amesisitiza matrekta hayo kutumika ipasavyo kwenye sekta ya kilimo ili kuongeza tija kwenye uzalishaji wa kilimo nchini jambo litakalokuwa na manufaa kwa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Taasisi ambazo zimeshirikiana kufanikisha utiaji saini huo ni Bodi ya Pamba ambayo ipo chini ya wizara ya kilimo, Benki ya Maendeleo ya kilimo-TADB, Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Tume ya Maendeleo ya ushirika.

Dkt Tizeba alisema kuwa Vyama vya ushirika vya msingi vinapaswa kuongeza juhudi katika kilimo ili kuakisi kulipa gharama za mkopo ambao ni asilimia 20 ya mkopo wote katika kipindi cha miaka mitatu huku asilimia zingine 80 zikilipwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo-TADB.

Utiaji huo wa saini hati ya makabidhiano ya ukopeshaji wa matrekta 300 kwa vyama vya msingi vya ushirika unajili wakati ambapo hivi karibuni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwaalimkabidhi Waziri wa kilimo Dkt Charles Tizeba jumla ya matrekta 500 ya Ursus kwa ajili ya kukopeshwa kwenye  vyama vya ushirika vya msingi ili wakulima kunufaika na tija katika kilimo hususani zao la Pamba.

Akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini Dkt Tizeba alisema kuwa sekta ya kilimo nchini bado inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo tija ndogo inayosababishwa na matumizi madogo ya pembejeo, huduma duni za ugani na matumizi ya zana duni za kilimo ambapo wakulima wengi wanatumia majembe ya mkono au kutumia maksai wakati wa kulima.

“Katika kilimo cha Pamba msimu wa mwaka 2017/2018 ushahidi unaonyesha wakulima walichelewa kuanza kuandaa mashamba kwa sababu Maksai wakati wa kiangazi wanadhoofu sana,” Alikaririwa Dkt Tizeba na kuongeza kuwa

“Mara mvua inaponyesha hawawezi kulima mpaka majani yawe mengi ndio wapate nguvu za kuanza kulima, hali hii inaondoa uwezekano wa wakulima kutumia teknolojia mpya katika kilimo kama vile kilimo hifadhi ambacho kimedhihirika kuongeza tija zaidi ya mara mbili”

Tizeba alisema mtazamo wa mpango huo ni kuunganisha nguvu za mkulima mmoja mmoja ili kuharakisha kuleta maendeleo yao ambapo utatekelezwa kwa kutumia sehemu ya fedha zinazolipwa AMCOS kama kamisheni ya kusimamia ununuzi wa pamba ambapo matarajio ni kukusanya Bilioni 6 kama uzalishaji wa pamba utafika kilo milioni 400 kwa mwaka.

Alisisitiza kuwa Bodi ya Pamba pamoja na Tume ya Maendeleo ya ushirika zinapaswa kufuatilia kwa karibu hatua zote mwenendo wa ufanyaji kazi wa matrekta hayo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa punde yanapoanza kufanya kazi yawe yanafanyiwa marekebisho ya mara kwa mara.

MWISHO.

African Export Import kuipatia Tanzania Zaidi ya Shilingi Trilioni moja Kugharamia Ujenzi Wa Reli Na Vituo Vya Biashara

$
0
0
Na: WFM,  Mjini Bali Indonesia
African Export Import Bank (Afreximbank) ya Misri, imeonyesha nia ya kuipatia Tanzania mkopo wa zaidi ya Shilingi trilioni moja (dola za Marekani zaidi ya milioni 500) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kipaumbele hasa ya miundombinu ya reli na kujenga vituo vya biashara (SEZ and Industrial parks).

Hayo yalibainishwa mjini Bali Indonesia, na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango baada ya Mkutano na Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel,  uliofanyika  wakati wa mikutano ya mwaka  ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ikiendelea.

Waziri Mpango, alisema kuwa Afreximbank imethibitisha kuwa ipo tayari kutoa mkopo wa  dola za Marekani milioni 125  (takribani Shilingi bilioni 285.9) kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Kimataifa  (SGR),  kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Dodoma.

“Afreximbank wanania pia ya kutoa  dola milioni 400 (takribani Sh. Bilioni 914.9) ambazo wanaweza kutukopesha kwa ajili ya kugharamia miradi ya miundombinu itakayorahisisha biashara kati ya Tanzania na nchi jirani na Bara la Afrika kwa ujumla,  ili kuchochea kasi ya ukuaji wa biashara katika nchi hizo kwa lengo la kuondoa umasikini”, aliongeza Dkt. Mpango.

Alisema kuwa kwa kuwa tayari Tanzania ilikuwa na mkakati wa kufungua vituo vya biashara katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara na mikoa mingine, suala la mkopo huo ni fursa kubwa kwa  maendeleo ya nchi, hivyo jambo hilo litafanyiwa kazi kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji  na Sekta Binafsi, ili Taifa liweze kunufaika na fedha ambazo benki hiyo ipo tayari kuzitoa.

Aidha, amesema kuwa  katika majadiliano na benki hiyo kuna umuhimu wa kuangalia namna ya rasilimali fedha ambazo Benki Kuu za nchi mbalimbali za Afrika zimekuwa zikiwekeza nje ya Bara hilo, ili ziweze kuwekezwa kwenye benki za Afrika kama Afreximbank ili kuleta maendeleo kwa haraka katika Bara hilo.

Vile vile benki hiyo imeikaribisha Tanzania kushiriki mkutano wa biashara utakaofanyika mwezi Desemba mwaka huu mjini Cairo Misri, ambapo kwa upande wa Tanzania ni fursa kwa Makampuni ya umma na binafsi kutangaza bidhaa mbalimbali zinazozalishwa kwa lengo la kukuza biashara ndani ya Bara la Afrika.

Makamu wa Rais wa Afreximbank Bw. Amr Kamel, alisema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi za kimkakati kwa kuwa ina mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi jirani, hivyo Afreximbank imeamua kusaidia miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu ili kuharakisha maendeleo ya nchi ya Tanzania na nyingine.

Waziri Dkt. Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa kuisaidia Tanzania katika mkakati wa kufikia uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo mwaka 2025, hivyo kuwa Taasisi yenye tija si tu kwa maendeleo ya Tanzania lakini pia kwa Bara la Afrika.

Upelelezi kesi ya Sethi, Rugemalira Bado haujakamilika

$
0
0
Upelelezi wa kesi inayomkabili Harbinder Sethi na James Rugemalira katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Iman Nitume ameeleza hayo jana Oktoba 11, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilipotajwa, akidai upelelezi bado haujakamilika.

Baada ya wakili huyo wa Serikali kueleza hayo, wakili wa utetezi, Dora Mallaba ameomba upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo ili kesi ianze kusikilizwa.

Hakimu Shaidi baada ya kusikiliza hoja hizo ameiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Sethi na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Washtakiwa hao wapo rumande tangu Juni mwaka jana kutokana na kukabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo kwa mujibu wa sheria hayana dhamana.

Kutana Na Shekhe Massory kutoka Pemba.....Anasafisha Nyota, Mvuto wa Biashara, Tatizo la Kutoshika Mimba, Miguu Kuwaka Moto

$
0
0
✨Je umekuwa ukihangaika na kusumbuliwa na Maisha ,Matatizo Mengi ya Kimaisha pasipo Mafanikio???

✨Bado haujachelewa....Kutana Na Shekhe Massory kutoka Pemba  Bingwa wa kutatua Matatizo Yote Yanayo husu Maisha na kukupa Dawa zitakazo kusaidia  Katika Maisha Yako kama vile;

✨Mvuto Wa Biashara 

Kuwa Na Wateja Wengi Katika Bishara YakoKumvuta Mpenzi Awe Mume Au Mkee aje Karibu Yako
Mtu Mwenye Tatizo La Kutoshika Mimba Au Akishika Inatoka...Tiba Hiyo Ipo 
Kumzuia Mume Au Mke Asitoke Nje Ya Ndoa Au Kwenye Mahusiano Yenu
✨kutibu Chango La Uzazi 
✨ Miguu Kuwaka Moto
 ✨ Kuweka Kinga  shambani Nyumbani na hata Dukani Au Sehemu Yako Ya BiasharaKusafisha Nyota 
Kurudiswa Kazini
✨Pia Kuna Pete Za Bahati

✨ Kwa Mawasiliano
+255 718 826768 -Tgo
+255 692 610596 -Airtel
+255 620 144631 -Halotel

Whatssap Namba
+255 620 144631


✨Wote Mnakaribiswa Mpate Dua Kutoka Pemba Kwa Shekhe Mansoory✨

✨Malipo Ni Baada Ya Mafanikio Inshaalah✨

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum✨

Alichosema Lulu Diva kuhusu muziki wa Hamisa Mobetto

$
0
0
Muimbaji Lulu Diva amesema Mwanamitindo Hamisa Mobetto ni mtu ambaye amekuwa akimvutia zaidi kutokana na kazi zake za kila siku na hasa alipoingia kwenye muziki.

Kwenye Mahojiano na The Playlist ya Times FM amesema licha ya Hamisa kuwa mwanamke mrembo na maarufu bado anajitahidi kufanya kazi zake na sio kutegemea kupewa tu.

"Hamisa ananivutia anapokuwa anajituma,  msichana ambaye anapigana kwa kile ambacho anakihitaji, unajua wasichana wengi wanafikiri ukishakuwa mzuri basi unaweza ukapata chochote kwa kutumia uzuri lakini mimi naona kwa Hamisa ni tofauti kidogo pamoja ni mama wa watoto wawili, kwa hiyo naona anajitihadi," amesema Lulu Diva.

Licha ya Hamisa kuwa Mwanamitindo kwa sasa ameingia kwenye muziki ambapo ameachia wimbo wake wa kwanza uitwao Madam Hero, huku Lulu Diva akifanya vizuri na wimbo  wake mpya unaokwenda kwa jina la Alewa ambao amemshirikisha Producer S2kizzy.

Alikiba aeleza ni kwanini MoFaya haijaingia sokoni

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Alikiba amefunguka kwanini hadi sasa kinywaji chake cha MoFaya hakijaingia sokoni.

Muimbaji huyo amesema kila hatua imekamilika ingawa kuna kitu kilikwambisha ila ana imani siku sio nyingi kitaingia sikoni.

"Ok, tayari tumemaliza kila process nadhani kuna delay kidogo imetokea ambayo imefanya hadi sasa watu hawaioni katika soko ila bila shaka Mwenyenzi Mungu akijali hivi karibuni itakuwa tayari na ninaomba Watanzania waipokee," Alikiba ameiambia The Playlist ya Times FM.

Utakumbuka kinywaji cha MoFaya kilitambulishwa kwa mara ya kwanza April 29, 2018 ambayo ilikuwa siku ya harusi ya Alikiba.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images