Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Benki Ya Dunia Yaahidi Kutoa Fedha Kukuza Matumizi Ya Sayansi Na Teknolojia Tanzania

$
0
0
Na.WFM Mjini Bali- Indonesia
Benki ya Dunia imeahidi kuwekeza zaidi nchini Tanzania katika Sayansi na  Teknolojia ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi  kwa lengo la kuisaidia Tanzania kukuza uchumi wa viwanda na kuondoa umasikini  kwa wananchi wa wake.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, alipofanya mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Bw. Hafez Ghanem, katika mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Mjini Bali Indonesia.                    

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki ya Dunia imeamua kuwekeza katika teknolojia kwa kuwa ni eneo sahihi linaloweza kukuza uchumi wa Taifa kwa zaidi ya mara mbili kutokana na tafiti zilizofanywa na Benki ya Dunia.

“Kimsingi Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia amefurahia ajenda za maendeleo za Tanzania kuhusu kujenga uwezo wa rasilimali watu katika kukuza uchumi wa viwanda na ameahidi kuanza kwa kuwekeza zaidi kwa watoto wenye umri mdogo ili mipango ya maendeleo ya nchi iwe endelevu”, alieleza Dkt. Mpango.

Aidha Waziri Mpango alimueleza Makamu wa Rais wa Benki hiyo kuwa Tanzania imeweka  mikakati  mbalimbali ya kujenga uchumi wa viwanda utakaotumia malighafi za ndani ili kuongeza ajira kwa wananchi walio wengi.

Kuhusu umuhimu wa Sekta Binafsi katika maendeleo ya nchi Waziri Mpango alisema Makamu wa Rais Bw. Ghanem, ameahidi kuwekeza zaidi katika miradi ya pamoja kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), kwa kuiwezesha Serikali ya Tanzania na wadau wengine kwenda kupata mafunzo yatakayoongeza ujuzi wa utekelezaji wa miradi hiyo katika nchi zilizofanya vizuri katika eneo hilo ili kuongeza ufanisi wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Kwa upande wake Kamishna na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere, amesema kuwa mfumo wa dunia ya sasa unazitaka nchi kujitegemea kimapato hivyo TRA itaendelea kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa  kuwa Benki ya Dunia imeahidi kuboresha miundomibnu ya ukusanyaji mapato kwa nchi ya Tanzania.

Waziri Mpango ameiomba Benki ya Dunia iendelee kuisaidia Tanzania kwa kutoa rasilimali fedha katika kuwezesha miundombinu ya kukuza uchumi ikiwemo ya miradi ya nishati ya umeme, ujenzi wa reli kwa kiwango cha Kimataifa (SGR), na miradi ya maji.

Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia ameahidi kutembelea Tanzania mwanzoni mwa mwaka ujao ikiwa ni juhudi za kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo kati ya benki hiyo na Tanzania.

Mikutano ya mwaka ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), inaendelea mjini Bali Indonesia ambapo imewakutanisha wadau wa masuala ya fedha wakiwemo Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu kutoka nchi mbalimbali Dunia kujadili Sera na misaada inayotolewa na Taasisisi hizo.

Imetolewa na:-
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Raia Wakigeni Wakamatwa JNIA Kwa Kutorosha Mamilion

$
0
0
Abiria wawili Raia wa Sudan Kusini na Syria jana wamekamatwa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wakisafirisha fedha taslim dola 70,000 za Kimarekani sawa na shilingi milioni 156 za Kitanzania na paundi 3410 za Sudan bila kufuata taratibu.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria la JNIA, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi, Barnabas Mwakalukwa alimtaja Raia wa Sudan Kusini Bi. Nada Zaelnoon Ahamed (38) mwenye hati ya kusafiria namba P01563534 amekamatwa saa 10:00 jioni akiwa eneo la ukaguzi wakati akiingia ndani tayari kusafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ 485) akielekea Nairobi.
 
Hatahivyo, Afande Mwakalukwa amesema abiria huyo amekamatwa na dola 60,000 za Kimarekani na paundi za Sudan 3410, ambazo zote kwa pamoja alishindwa kutoa taarifa ya fedha alizokutwa nazo kwa mujibu wa sheria ya utakatishaji fedha ya mwaka 2006 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012.
 
Pia alimtaja Bw. Mohamed Belal (31), Raia wa Syria mwenye hati ya kusafiria namba 003-16L096876 aliyekuwa akisafiri kwa ndege ya Shirika la ndege la Ethiopia (ET 864) kuelekea Syria kupitia Addis Ababa amekamatwa na dola za kimarekani 10,000 sawa na Tsh. milioni 20 za Kitanzania, ambazo naye alishindwa kuzitolea taarifa.
 
“Watuhumiwa wote wawili wamezuiwa na hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya uchunguzi zaidi na hatua za kisheria zilizopo,” amesema Afande Mwakalukwa.
 
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela amewapongeza maafisa usalama wa JNIA kwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha wasafiri, wadau na maeneo yote ya viwanja vya ndege yanabaki salama na vitendo vya kiuhalifu havina nafasi katika viwanja hivyo.
 
Bw. Mayongela amesema pamoja na watumishi hao kufanya kazi katika wakati mgumu kutokana na baadhi ya abiria kuwa watata kila wanapotaka kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kanuni.
 
Ametoa wito kwa wadau, wasafiri na wafanyakazi wote kushirikiana na maafisa usalama, vyombo vya ulinzi na usalama katika kutoa taarifa stahiki ili vitendo vya kiuhalifu kama hivi visipate nafasi kwenye viwanja vya ndege kwani ndio vinatoa taswira ya nchi.
 

MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa nchi zote 16 za SADC

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Laurean Rugambwa Bwanakunu wamesaini mkataba wa makubaliano ya MSD kuwa mnunuzi Mkuu wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kwa ajili ya nchi 16 wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Hatua hii inafuatia uteuzi wa serikali ya Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) ulifanywa wakati wa mkutano wa SADC wa mawaziri wa Afya wa nchi wanachama, uliofanyika mwezi Novemba, 2017 nchini Afrika Kusini.

 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Bw. Laurean Bwanakunu amesema tangu wakati huo hadi sasa wamekuwa wakishirikiana na na Sekretarieti ya (SADC) kuandaa rasimu ya mpango wa utekelezaji wa manunuzi ya pamoja yaani SADC Pooled Procurement Services (SPPS).

 Amesema kulingana na mpango huo, uratibu wa manunuzi umeanza rasmi tarehe jana, tarehe 9/10/2018, kupitia mkataba wa makubaliano yaani Memorandum of Understanding (MoU) kati ya MSD na Sekretarieti ya SADC.

 Bwanakunu ameongeza kuwa MSD itakuwa na majukumu ya kupokea mahitaji ya manunuzi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kutoka kwa nchi hizo 16 za Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kununua dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara, kusimamia takwimu na taarifa za dawa pamoja na kusimamia Kanzidata (Database) ya dawa za nchi hizo.

 Ameongeza kuwa MSD itasimamia bei elekezi ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara, kusimamia mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao kwa nchi zote wanachama, kutoa huduma za kitaalam na kupanga bei elekezi. MSD pia itaanzisha kitengo maalumu ndani ya kurugenzi ya manunuzi kwa ajili ya kazi hii ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba ba vitendanishi vya maabara kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya SADC tu.

 Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Sekretariet ya SADC Dkt. Stergomena L. Tax ameeleza kuwa Tanzania kuwa mnunuzi mkuu wa dawa kwa nchi za Ukanda wa SADC ni heshima kubwa kwa Taifa, kuaminiwa kwa huduma bora, uwezo na kukidhi vigezo vya kitaalamu katika mnyororo wa ugavi.

 Makubaliano hayo yameshuhudiwa na Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye amesema kwamba SADC imeipa Tanzania heshima kubwa na kuichagiza MSD kuhakikisha inatekeleza majukumu yake vizuri ili isionekane kuwa SADC ilifanya makosa kuichagua Tanzania.

NECTA: Wanafunzi waliojitokeza kufanya mitihani ni zaidi ya tuliotarajia

$
0
0
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limesema idadi ya wanafunzi waliojitokeza kurudia mtihani wa darasa la saba kwa tarehe 8 na 9 mwezi huu ni zaidi ya idadi iliyotarajiwa na baraza hilo na usimamizi wa sasa uliimarishwa zaidi.

==>>Msikilize Katibu mkuu NECTA akiongea hapo chini

Waziri Mkuu Awataka Viongozi Wa Wilaya Ya Kyerwa Wajipime.....Ni kutokana na biashara za magendo zinazoendelea wilayani humo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amechukizwa na biashara za magendo zinazoendelea katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera, hivyo amewataka viongozi wa wilaya hiyo wajipime wenyewe.

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Kagera Bw. Adam Ntogha kumsimamisha kazi Afisa wa Forodha katika mpaka wa Mulongo  Bw. Peter Mtei kwa tuhuma za kujihusisha na biashara za magendo.

Ametoa agizo hilo jana (Jumanne, Oktoba 9, 2018) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa wa Kagera katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani hapa kilichofanyika mjini Bukoba.

“Biashara za magendo zinafanyika bila ya wao kuchukua hatua, mnatia aibu yaani hakuna kazi inayofanyika. Viongozi wa wilaya ya Kyerwa mjipime wenyewe, mialo mingi katika wilaya yenu inatumika kwa biashara ya magendo na butura.”

Waziri Mkuu aliongeza kuwa katika mwalo wa Mulongo ulipo kwenye eneo ambalo  Tanzania inapakana na nchi za Uganda na Rwanda, biashara za magendo na butura zinafanyika na hakuna kiongozi wanaochukua hatua.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimtaka Meneja wa TRA asiwahamishe watumishi wabovu kutoka kituo kimoja cha forodha na kuwapeleka kingine kwa kuwa huko wanakowapeleka wanakwenda kuendeleza biashara za magendo na kuikosesha Serikali mapato.

Alitolea mfano mtumishi wa mamlaka hiyo Bw. Mtei ambaye alihamishiwa kituo cha Mulongo akitokea kwenye kituo cha Mtukura kilichopo katika mpaka wa Tanzania na Uganda kwa tuhuma za kuchukua rushwa na kushirikiana na wafanyabiashara wa burura.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema mtumishi huyo tayari alishapewa barua ya uhamisho kwenda katika kituo cha forodha cha Rusumo miezi minne iliyopita hadi sasa hajahama na anaendelea na biashara za magendo ambapo Agosti 5, mwaka huu anadaiwa kupitisha mzigo wa magendo uliobebwa kwenye gari aina ya fuso yenye namba za usajili T 957 AXF mali ya Erasto Muga.

“Meneja TRA msimamishe kazi Bw. Mtei leo (jana) hatuwezi kuwa na watumishi wabovu alafu nyie mnawahamisha vituo ili wakaendelee kuharibu eneo lingine. Mnajua mkakati wa Serikali hii ni kudhibiti rushwa hivyo hatuwezi kuvumilia suala hili.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alimuagiza Meneja wa TRA wa mkoa wa Kagera Bw. Ntogha afanye ukaguzi kwenye vituo vyote vya forodha katika mkoa huo pamoja na kuongeza idadi ya watumishi na kudhibiti vitendo vya rushwa.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

IGP Sirro afanya mabadiliko kwa Makamanda wa Polisi nchini

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Polisi nchini.


==>>Taarifa kamili iko hapo chini


Video Mpya: Jux ft. Joh Makini - Tell Me

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Jux anakukaribisha kutazama video ya wimbo mpya uitwao Tell Me. Itazame hapa.

Serikali yapiga marufuku madaktari kuandika dawa kwa majina ya kampuni

$
0
0
Serikali imepiga marufuku madaktari kuwaandikia wagonjwa dawa kwa kutumia majina ya kampuni badala yake watumie majina ya kitaalamu.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Oktoba 10, na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto Dk. Faustine Ndugulile, katika kuangalia mfumo wa upatikanaji dawa na vifaa tiba nchini.

Amesema tabia ya madaktari kuandika dawa kwa kutumia majina hayo ya kampuni kumesababisha wagonjwa kukosa dawa na licha ya kuwapo kwa dawa nyingine zenye uwezo wa kutibu sawa na hizo.

“Dawa zinazotumika hapa nchini ni sawa na zile zinazotumika katika nchi nyingine duniani, kwa hiyo kutoa dawa China, India, Marekani au Ulaya ni utofauti wa gharama.

“Kwa mfano mimi ni daktari nikikuandikia ukanunue soda ukikuta soda yoyote utapona ila nikikwambia ukanunue Cocacola lazima uipate hiyo.

“Kwa hiyo wawaAndikie wagonjwa dawa kwa majina ya asili kwa sababu ukimwandikia mgonjwa panadol ni kumtaka lazima anunue dawa hiyo hata kama kuna dawa nyingine hawezi kupewa,” amesema Dk. Ndugulile.

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Kwanini Ushindwe Kumkizi Mwenzi Wako Kwa Tatizo La Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Suluhisho La Matatizo Hayo Muone Dr Masele Atamaliza Matatizo Yako

$
0
0
Mbepe; ni dawa ya nguvu za kiume,kurefusha na kunenepesha maumbile madogo kwa muda mfupi.

MHOLA; ni dawa inayotibu kisukari,presha,degedege,kifafa,mwili kupooza, Kipanda uso,kiuno,mgongo,kuzuia mimba isotoke, Kuuma tumbo chini ya kitovu.

NDAGULA; ni dawa ya kuunga mifupa kwa mda mfupi kwa aliye pata ajali na kuvunjika,ataanza kupata nafuu ndani ya siku 14 na kufanya mazoezi

Inhondi; ni kwa wale wenye busha,kuota nyama sehemu ya Siri, Miguu kuwaka moto.

Lukomolo;  Ni dawa ya mvuto wa mapenzi Kumvuta mme, Mke, Mchumba hawala atakutafuta mwenyewe

Tupo mbagala rangi 3, kwa dar huduma utaletewa popote ulipo kwa tiba na ushauli piga no. 0742215230/0787131395/0712757594 dr MASELE

CRDB yaeleza sababu kumpumzisha Dk. Charles Kimei kabla ya muda Kuisha

$
0
0
Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, imeeleza sababu za kumpumzisha aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Dk. Charles Kimei kabla ya muda wake kumalizika kuwa ni vigumu kwa benki hiyo kuwa na wakurugenzi wawili kwa wakati mmoja.

Awali, bodi hiyo ilieleza kuwapo kwa kipindi cha mpito cha takribani miezi minane ambacho Mkurugenzi Mtendaji mpya aliyetambulishwa leo, Abdulmajid Nsekela, angefanya kazi na Dk. Kimei aliyemaliza muda wake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Jumatano Oktoba 10, wakati wa kumtambulisha Mkurugenzi mpya wa benki hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Ally Laay, amesema katika kikao walichokaa Oktoba 2 mwaka huu, walitafakari upya uamuzi wake huo na kupitisha maamuzi kuwa Dk. Kimei apumzike.

“Tuliamua Dk. Kimei apumzike na kumpisha Mkurugenzi Mtendaji mpya kwa kutilia maanani misingi ya utawala bora na maadili yetu ya kazi ingeleta ugumu kwa benki kuwa na wakurugenzi watendaji wawili kwa pamoja kwa kipindi kirefu,” amesema Laay.

Aidha, amesema Nsekela ni mbobevu na ana weledi wa kutosha katika masuala ya uongozi wa mabenki hivyo kutohitaji kushikwa mkono kwa muda mrefu kama ilivyoamuliwa hapo awali.

Kwa upande wake Nsekela, ameishukuru bodi hiyo kwa kujenga imani kubwa kwake na kuona anastahili kuchukua kijiti cha Dk. Kimei.

“Benki ya CRDB ni kubwa sana na inafanya vizuri kwa muda mrefu lakini ukubwa si tija kwa sababu huku mbele tuendako mkubwa na mdogo mnaweza kuwa sawa,” amesema Nsekela.

LHRC yampongeza Rais Magufuli kutotekeleza adhabu ya kifo

$
0
0
Wakati watu 472 nchini Tanzania wakiwa wamehukumiwa adhabu ya kifo, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kinatambua mchango wa Rais John Magufuli katika kutetea haki za binadamu.

Akizungumza leo Oktoba 10, 2018 katika maadhimisho ya 16 ya siku ya kupinga adhabu ya kifo duniani, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Felista Mauya amesema kituo hicho kinatambua mchango wa Rais wa Awamu ya Tano.

“Tunampongeza Rais John Magufuli, alisema hadharani kwamba hatatekeleza hukumu ya kifo katika kipindi chake na kutoa msamaha kwa wafungwa 62 waliohukumiwa kunyongwa tukio ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Tanzania,” amesema Mauya.

Katika hatua nyingine Mauya amesema Tanzania kwa sasa ipo katika hatua isiyo rasmi ya kupinga na kutotekeleza adhabu ya kifo japo hakuna jitihada za lazima zilizochukuliwa kuonyesha nia ya kuifanya hali hiyo kutambulika kisheria.

“Kama sehemu ya maadhimisho Oktoba 9, mwaka huu kituo kimefungua kesi ya kikatiba namba 22 ya mwaka 2018 kupinga uwepo wa adhabu ya lazima ya kifo kwa kuzingatia mifano ya nchi jirani kama Kenya, Uganda na Malawi ambapo adhabu ya lazima ya kifo imefutwa kabisa,” amesema.

Mwanasheria ambaye pia ni Mkurugenzi wa utetezi na maboresho, Flugence Massawe amesema sheria hizo zinatakiwa zirekebishwe ili zitoe nafasi zaidi kwa mahakama na wale wanaoshtakiwa.

Waziri Ndalichako Amfananisha Rais Magufuli na Mwalimu Nyerere

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemfananisha Rais John Magufuli na Hayati Mwalimu Julius Nyerere akisema amekuwa mstari wa mbele kupigania masilahi ya Taifa na kupambana na viongozi wanaokwenda kinyume na matarajio ya Watanzania.

Akizungumza leo Oktoba 10, 2018 katika kongamano la kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere linalofanyika katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni Dar es Salaam, Profesa Ndalichako aliyekuwa mgeni rasmi amesema Mwalimu alijali masilahi ya Taifa na ndiyo maana hakuwa na mali nyingi hadi alipostaafu.

 “Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi wa mfano ambaye katika maisha yake aliweka mbele masilahi ya Taifa kuliko masilahi yake binafsi.”

“Tumeona hata wakati anastaafu ukiangalia mali alizokuwa nazo zilikuwa haziakisi nafasi ya uongozi katika Taifa aliyokuwa nayo katika miaka mingi ya uongozi,” amesema Profesa Ndalichako.

Amesema Mwalimu Nyerere hakuwa kiongozi aliyejinufaisha mwenyewe binafsi, bali alikuwa ni utumishi wa kuwatumikia Watanzania na alifanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa na kwa unyenyekevu.

“Leo miaka 19 hatunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere sote tunapaswa kumuenzi kwa kuiga mambo aliyofanya kwa Taifa,” amesema.

“Pia, tunashuhudia Rais wetu wa Awamu ya Tano, John Magufuli anavyoweka mbele masilahi ya Taifa na amekuwa mstari wa mbele katika kupigania rasilimali za Taifa na hana mchezo kabisa na yeyote anayekwenda kinyume na maadili ya Kitanzania.”

Profesa Ndalichako amewataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuwa ni mwepesi kuchukua hatua pale anapoona viongozi wa umma hawaendani na matarajio ya wananchi waliompa ridhaa ya uongozi.

Kongamano hilo lenye kauli ya ‘Falsafa ya Mwalimu Nyerere katika kujitegemea na maendeleo ya viwanda Tanzania, limehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally.

Wengine ni; Balozi Ibrahim Kaduma, aliyewahi kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, Jaji Mkuu mstaafu, Augustino Ramadhani na mwanasiasa mkongwe, Paul Kimiti na wengineo.

Akizungumzia utendaji wa Serikali, Profesa Ndalichako amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na utoaji elimu bure, ujenzi wa viwanda na miundombinu ya uchukuzi kama kuimarisha shirika la ndege na ujenzi wa reli ya kisasa.

Ameendelea kusema Serikali imekuwa ikitekeleza mradi wa umeme wa Stieglier’s Gorge huku usambazaji wa umeme ukiendelea kwa kasi.

Waziri Ndalichako Amfananisha Rais Magufuli na Mwalimu Nyerere

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemfananisha Rais John Magufuli na Hayati Mwalimu Julius Nyerere akisema amekuwa mstari wa mbele kupigania masilahi ya Taifa na kupambana na viongozi wanaokwenda kinyume na matarajio ya Watanzania.

Akizungumza leo Oktoba 10, 2018 katika kongamano la kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere linalofanyika katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni Dar es Salaam, Profesa Ndalichako aliyekuwa mgeni rasmi amesema Mwalimu alijali masilahi ya Taifa na ndiyo maana hakuwa na mali nyingi hadi alipostaafu.

 “Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi wa mfano ambaye katika maisha yake aliweka mbele masilahi ya Taifa kuliko masilahi yake binafsi.”

“Tumeona hata wakati anastaafu ukiangalia mali alizokuwa nazo zilikuwa haziakisi nafasi ya uongozi katika Taifa aliyokuwa nayo katika miaka mingi ya uongozi,” amesema Profesa Ndalichako.

Amesema Mwalimu Nyerere hakuwa kiongozi aliyejinufaisha mwenyewe binafsi, bali alikuwa ni utumishi wa kuwatumikia Watanzania na alifanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa na kwa unyenyekevu.

“Leo miaka 19 hatunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere sote tunapaswa kumuenzi kwa kuiga mambo aliyofanya kwa Taifa,” amesema.

“Pia, tunashuhudia Rais wetu wa Awamu ya Tano, John Magufuli anavyoweka mbele masilahi ya Taifa na amekuwa mstari wa mbele katika kupigania rasilimali za Taifa na hana mchezo kabisa na yeyote anayekwenda kinyume na maadili ya Kitanzania.”

Profesa Ndalichako amewataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuwa ni mwepesi kuchukua hatua pale anapoona viongozi wa umma hawaendani na matarajio ya wananchi waliompa ridhaa ya uongozi.

Kongamano hilo lenye kauli ya ‘Falsafa ya Mwalimu Nyerere katika kujitegemea na maendeleo ya viwanda Tanzania, limehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally.

Wengine ni; Balozi Ibrahim Kaduma, aliyewahi kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, Jaji Mkuu mstaafu, Augustino Ramadhani na mwanasiasa mkongwe, Paul Kimiti na wengineo.

Akizungumzia utendaji wa Serikali, Profesa Ndalichako amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na utoaji elimu bure, ujenzi wa viwanda na miundombinu ya uchukuzi kama kuimarisha shirika la ndege na ujenzi wa reli ya kisasa.

Ameendelea kusema Serikali imekuwa ikitekeleza mradi wa umeme wa Stieglier’s Gorge huku usambazaji wa umeme ukiendelea kwa kasi.

Katibu Mkuu Kilimo Mhandisi Mtigumwe Akabidhiwa Rasmi Tume Ya Taifa Ya Umwagiliaji

$
0
0
Na Mathias Canal, WK-Dodoma
Katika kuongeza ufanisi kwenye matumizi ya umwagiliaji katika kilimo kama sehemu ya utekelezaji wa Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (Agricultural Sector Development Programme -Phase Two -ASDP II) rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe amekabidhiwa Tume ya Umwagiliaji na katibu Mkuu wa wizara ya maji Prof Kitila Mkumbo.

Uamuzi huo wa Tume ya umwagiliaji kuhamishiwa wizara ya
kilimo unalenga kuiwezesha wizara yenye dhamana ya sekta ya maji kudhibiti matumizi ya maji katika umwagiliaji bila kuwa na mgongano wa kimajukumu.

Imeelezwa kuwa sekta ya umwagiliaji ndiyo inayoongoza kwa
matumizi ya maji hapa nchini  ambapo kwa sasa kiwango cha matumizi ya maji kwa ajili ya umwagiliaji kinakadiriwa kuwa mita za ujazo milioni 10,309 kwa mwaka ambacho ni sawa na asilimia 83.6 ya matumizi ya maji yote hapa nchini.

Kufuatia uamuzi huu wa serikali Tume ya umwagiliaji sasa
itawajibika kiutawala kwa katibu Mkuu wa wizara ya kilimo na hivyo jina la wizara ya maji kubadilika na kuwa wizara ya Maji.

Katika kutekeleza maamuzi ya serikali ya kuhamishia wizara ya kilimo jukumu la umwagiliaji, leo tarehe 10 Octoba 2018 Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe na Katibu Mkuu wa wizara ya maji Prof Kitila Mkumbo wamefanya makabidhiano ya nyaraka muhimu kuhusu Tume ya Umwagiliaji zikiwemo sera ya umwagiliaji, Sheria ya umwagiliaji, na mpango kabambe wa Umwagiliaji (Revised National Irrigation Master Plan).

Utekelezaji wa maamuzi ya serikali kuhamishia jukumu la
umwagiliaji kwenda wizara ya kilimo utaendelea kutekelezwa hatua kwa hatua katika mwaka wote huu wa fedha 2018/2019 na utakamilika kwa marekebisho ya Hati ya mgawanyo wa majukumu ya wizara ya Maji na Wizara ya kilimo.
 

Kada wa CCM mahakamani kwa kuishi nchini bila kibali

$
0
0
Idara ya Uhamiaji, imemfikisha mahakamani Kada maarufu wa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Iringa, Michael Mlowe kwa tuhuma za kuishi nchini bila kibali na kutoa taarifa za uongo kuhusu uraia wake.

Mlowe ambaye kwa jina maarufu Mayko Namlowe (44) ni raia wa Uingereza, alifikishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando.

Akisoma mashtaka, Wakili wa Serikali kutoka Idara ya Uhamiaji, Novatus Mlay alidai mshtakiwa huyo ni mfanyabiashara na Mkazi wa Lugalo Kihesa Iringa.

Mshtakiwa anadaiwa kwamba Mei 31, mwaka huu katika Makao Makuu ya Ofisi ya Uhamiaji iliyopo Wilaya ya Temeke akiwa raia wa Uingereza aliishi nchini akiwa hana Visa wala nyaraka yoyote inayomwezesha kufanya hivyo.

Mlay alidai katika shtaka la pili, Mlowe anadaiwa kutoa taarifa za uongo, inadaiwa Mei 31, mwaka huu katika ofisi hizo za uhamiaji akiwa raia wa Uingereza alitoa taarifa ya uongo inayohusiana na uraia wake.

Kwa kufanya hivyo mshtakiwa alijipatia kitambulisho cha kitanzania namba 19741219_51108_00001_24 ambacho kina jina la Michael Juma Mlowe wakati akijua alichokifanya ni kosa.

Mshtakiwa alikana mashtaka, yuko nje kwa dhamana hadi Novemba 11 kesi itakapotajwa.

Madereva wa wa Mabasi mwendokasi Dar wakimbia na funguo

$
0
0
Kampuni inayotoa huduma ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es salaam (UDART) hatimaye imetoa ufafanuzi kuhusiana na vurugu zilizotokea leo katika kituo cha mabasi hayo cha Kimara jijini Dar es salaam, baada ya kukosekana kwa usafiri huo kwa takribani masaa 3.

Msemaji wa UDART Bw. Deus Bugaywa amesema chanzo cha tukio hilo ni hujuma zilizofanywa na baadhi ya madereva mishale ya saa 9 alfajiri, baada ya kuziba lango kuu la kutokea magari upande wa mbele pamoja ya hali kadharika wa nyuma kwa kuegesha mabasi yenye urefu wa mita18 na kusababisha usumbufu uliojitokeza.

"Baada ya mabasi matano ya kwanza kutoka ndani dereva mmoja alichukua basi na lenye urefu wa mita 18 9articulated bus na kuliegesha eneo la ndani ya lango kuu la kutokea upande wa mbele hivyo kuziba njia na wakati huo huo dereva mwengine aliziba lango la mbele la nyuma kwa basi lenye ukubwa huo huo."amesema Bw. Bugaywa.

"Baada ya kufanya tukio hilo madereva hao walikimbia na funguo za mabasi hayo kusikojulikana na walinzi walijaribu kuwafatilia lakini hawakufanikiwa kuwapata" ameongeza.

Aidha Bw. Bugaywa ameomba radhi wananchi kwa usumbufu uliojitokeza kituoni hapo huku akikanusha taarifa za ucheleweshaji wa mishahara ya wafanyakazi hao kutohusishwa na tatizo hilo.

"Tunapenda kufafanua kuwa mishahara ya wafanyakazi ya mwezi Septemba imeanza kulipwa tokea Oktoba 9, 2018 na hatuoni sababu ya kuunganisha suala hilo na mishahara; tayari tumepeleka suala hilo mbele ya Jeshi la polisi na hatua za kiuchunguzi zinaendelea ili kuwabaini waliofanya uhalifu huo"
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images