Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Waziri Lukuvi Aagiza Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi Achukuliwe Hatua Kali za Kisheria

$
0
0
 Na Munir Shemweta
Kilosa, Morogoro: Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amekabidhi taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa kijiji cha Mabwegere na vijiji saba vya wilaya hiyo na mpango wa utekelezaji wake na kuagiza wote waliohusika kupotosha mipaka ya eneo hilo akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi kuchukuliwa hatua za kisheria.

Lukuvi alitoa agizo hilo jana mkoani Morogoro wakati akikabidhi taarifa ya uchunguzi iliyofanywa na Jaji wa Mahakama Kuu ambaye sasa ni jaji wa Mahakama ya Rufaa  Jacob Mwambegele kwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe kuhusiana na mgogoro wa mipaka ya kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani vya Mambegwa,  Mbigiri,  Dumila,  Matongolo na Mfulu vilivyopo Wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro.

"Wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine katika process yote ambayo kwa kiasi fulani imeigharimu serikali fedha nyingi na kuipa maumivu serikali katika suala hilo ni lazima wachukuliwe hatua kali" alisema Lukuvi.

Taarifa ya uchunguzi ilibaini chanzo cha mgogoro ni kukosekana ushirikishwaji wa vijiji jirani katika kuainisha na kuweka mipaka ya kijiji cha Mabwegere jambo lililosababisha kijiji kiwe na eneo la ukubwa wa hekta 10, 234 kuliko hata kijiji mama cha Mfulu chenye hekta 1,717 jambo lililothibitishwa na ukweli kwamba mipaka ya kijiji hicho imeingia ndani ya mipaka ya kata  tatu za Mbigiri,  Msowero,  na Kitete ingawa kiutawala kijiji cha Mabwegere kinaratibiwa na  kata ya Kitete.

Hata hivyo,  Waziri wa Ardhi alisema wizara haijakifuta kijiji cha Mabwegere bali itaanza kutekeleza mapendekezo ya uchunguzi ya kufuta mipaka ya kijiji hicho ambapo sasa TAMISEMI  kwa kushirikiana na wilaya ya Kilosa itatakiwa kuanza mchakato wa kuandaa upya mipaka ya vijiji hivyo kwa njia shirikishi.

Katika taarifa yake,   Jaji Jacob Mwambegere alipendekeza kwa nia ya kuboresha utendaji kazi,  weledi,  maadili na umakini na uwezo wa kulinda na kutunza kumbukumbu katika idara ya Upimaji na Ramani na Ofisi ya Kamishna wa Ardhi hatua za kinidhamu zichukuliwe ili kuzuia migogoro ya ardhi.

Kwa mujibu wa Lukuvi, Wizara ya Ardhi ilikosea katika zoezi la upimaji wa  kijiji cha Mabwegere lakini wilaya ya Kilosa itakuwa na jukumu la kuanza mchakato upya wa uanzishaji wa kijiji hicho.

Alisema,  kwa kuwa serikali inaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani ni jukumu la Tamisemi kwa kushirikiana na wilaya ya Kilosa kuhakikisha mipaka inaandaliwa upya kwa ajili ya kuanzishwa kijiji  upya.

Waziri wa Ardhi alisisitiza kuwa shughuli za binadamu kama vile ufugaji na kilimo hazihusiani na masuala ya mipaka, hivyo wilaya ya Kilosa pamoja na kushughulikia suala la mipaka lazima iandae mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuanza  kupendekeza maeneo ya ufugaji kwa vijiji vyote saba na kusisitiza kuwa ni lazima busara itumike katika kushughulikia jambo hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri Tamisemi Joseph Kakunda alisema uanzishwaji kijiji cha Mabwegere haukufuata sheria na kuwataka wataalamu kuacha kuwa na  nidhamu ya woga na kuzingatia kanuni na sheria katika kutekeleza majukumu yao. 

Aidha, amemuelekeza Katibu Mkuu TAMISEMI kuunda timu itakayochunguza mchakato mzima wa kuanzisha kijiji hicho, na kila atakaebainika kuhusika na uanzishaji wa kijiji hicho kinyume na sheria achukuliwe hatua.

Naye naibu Waziri wa Kilimo Merry Mwanjelwa alisisitiza hatua kuchukuliwa kwa wote waliohusika na kusema katika serikali hii ya awamu ya tano ni lazima kufufua makaburi kwa minajili ya kubaini wote waliohusika kuidanganya serikali.

Taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa mipaka kati ya kijiji cha Mabwegere chenye jumla ya hekta 10,234 na mifugo takriban 24,146 na vijiji jirani katika wilaya ya Kilosa àmbao mara kadhaa ulisababisha vifo vya watu tangu mwaka 2008 lifanyika kwa muda wa siku sitini ambapo uchunguzi wake ulizingatia uanzishwaji,  upimaji,  utolewaji hati miliki kwa kijiji cha Mabwegere,  maeneo yenye mgogoro na hatua zilizokwishachukuliwa juu ya mgogoro huo,  uwiano wa ardhi,   mifugo na mahitaji mengine ya ardhi pamoja na vyanzo vingine tofauti vya mgogoro. 

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiambatana na Manaibu waziri Tamisemi Joseph Kakunda na Kilimo Merry Mwanjelwa amekutana na viongozi wa Halmashauri za vijiji hivyo saba na kuwasomea taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani.

Lukuvi amewaeleza wananchi hao kuwa ameikubali taarifa nzima ya uchunguzi kwa kuwa sheria inampa nafasi ya kuikubali au kuikataa taarifa hiyo, hivyo kuikubali kwake ni mwanzo wa utekelezaji wa mapendekezo ya uchunguzi na ndiyo maana aliamua kwenda kuwaeleza ukweli wa suala hilo.

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi viongozi wa wizara nne za Ardhi,  Tamisemi,  Kilimo pamoja na wizara ya Uvuvi na Mifugo walikaa pamoja na na kupanga mpango wa utekelezaji uchunguzi huo na namna ya kushughulikia mgogoro baina ya kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani.

_---------Mwisho-------------

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Tazama Hapa Binti Emiliana Alivyojishindia 500,000 Kirahisi Kabisa Siku yake ya Kuzaliwa

$
0
0
Baada ya kupata zawadi ya uhai kwenye siku yake ya kuzaliwa, Emiliana Sospeter Kongola amezadiwa zawadi nyingine na siku yake hiyo maalum kwa kushinda Laki Tano kutoka MojaSpesho.

Emiliana (21), mkazi wa Vingunguti, Dar es Salaam alianza kucheza MojaSpesho wiki nne zilizopita na juzi alifanikwa kutoboa ushindi baada ya kucheza namba 3 za bahati ambazo alizitengeneza kutoka katika siku yake ya kuzaliwa.

“Nilivyopigiwa simu sikuamini, nilijua ni matapeli wa mjini. Lakini wakanielezea vizuri na kunambia namna ya kupata pesa yangu niliyoshinda. Na sasa nimeupata ndo nimeamini.” ameeleza Emiliana.

Nawe pia unaweza kuwa mshindi kila siku na jackpot ya kila wiki. Jinsi ya kucheza Mojaspesho ni rahisi
1. Nenda kwenye menu yako ya #Mpesa, #TigoPesa, #AirtelMoney au #Halopesa;
2. Chagua lipia bili
3. Ingiza kampuni namba 123255
4. Ingiza kumbukumbu namba zako 3 za bahati zikifuatiwa na neno SEE mf. 123SEE
5. Weka kiasi kuanzia sh 1000 na utakua umecheza #Mojaspesho.

Wafanyakazi NMB Jela Miaka 28

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu kifungo cha miaka 28 jela kila mmoja wafanyakazi wawili wa Benki ya NMB.

Wafanyakazi hao, Mtoro Midole na Daudi  Kindamba wamehukumiwa jana Jumatatu Oktoba Mosi, 2018 baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka ya wizi, utakatishaji wa fedha na kuisababishia benki hiyo hasara ya Sh1.03 bilioni.

Hukumu hiyo iliandaliwa na hakimu mkazi mwandamizi, Godfrey Mwambapa na kusomwa na hakimu Mkuu, Wanjah Hamza.

Akisoma hukumu hiyo, Wanjah chini ya sheria ya kanuni ya adhabu aliamuru washtakiwa hao mbali na adhabu ya vifungo hivyo pia walipe kiasi cha hicho cha fedha.

John Kikoka aliyekuwa miongoni mwa washtakiwa hao, aliachiwa huru  baada ya mashahidi 21 wa  upande wa mashtaka katika kesi hiyo ya jinai namba 118 ya 2014, kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake.

Hakimu Wanjah akiisoma hukumu hiyo, alisema washtakiwa Midole na Kindamba wamekutwa na hatia katika shtaka la wizi ambapo aliwahukumu kifungo cha miaka mitano jela kila mmoja.

Katika shtaka la kutengeneza miamala ya uongo, ambalo linamkabili mshtakiwa Midole pekee, Hakimu Wanjah alisema atatumikia kifungo cha miaka 10 jela.

Katika mashtaka ya utakatishaji wa fedha, Hakimu Wanjah alisema mshtakiwa Midole na Kindamba wamekutwa na hatia katika shtaka moja moja, kati ya mawili mawili yanayowakabili hivyo kila mshtakiwa atalipa faini katika kosa moja Sh500 milioni hivyo katika mashtaka mawili kila mshtakiwa anapaswa kulipa Sh1 bilioni ama kutumikia kifungo cha miaka mitano jela.

Hakimu Wanjah katika shtaka la kusababisha hasara ya Sh1.03 bilioni kwa benki ya NMB, aliamuru kila mshtakiwa kulipa faini ya Sh5 milioni ama kutumikia kifungo cha miaka mitano jela.

Awali, kabla ya Hakimu Wanjah kusoma hukumu hiyo, wakili wa Serikali mwandamizi Kishenyi Mutalemwa aliieleza  mahakama hiyo kuwa hana kumbukumbu za makosa ya nyuma ya washtakiwa hao.

Wakili  Kishenyi aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu ya kiwango cha juu kwa washtakiwa hao, katika kila kosa walilotiwa hatiani kama Matakwa ya sheria yanavyotaka.

Alibainisha lengo la  kuomba adhabu hiyo ni mshtakiwa wa kwanza ambaye ni mfanyakazi wa benki ya NMB na  amekasimiwa na kuaminika kutunza fedha za wananchi na kwamba kosa la wizi na utakatishaji wa fedha imekuwa ni tishio kwa uchumi nchini hasa ukizingatia kiwango kikubwa cha fedha kilichohusika katika kesi hiyo.

Pia, aliiomba mahakama itoe amri kwa washtakiwa hao kurudisha fedha walizoisababishia hasara benki ya NMB.

Hakimu Wanjah alipowataka washtakiwa hao waongee chochote kabla ya kupewa adhabu hizo, Midole aliiomba Mahakama iwafikirie kwani wamekaa mahabusu kwa miaka minne kwa sababu mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili ni miongoni mwa  mashtaka yasiyo na dhamana kwa mujibu wa sheria.

Pia, aliiomba mahakama impatie nakala ya mwenendo wa shauri hilo na nakala ya hukumu kwa sababu anakusudia kukata rufaa.

Kindamba aliomba mahakama iangalie muda waliokaa mahabusu huku akiomba kupatiwa mwenendo wa shauri hilo na nakala ya hukumu kwa kuwa anakusudia kukata rufaa.

Watoto Wawili Wafariki Dunia Wakiogelea Kisimani

$
0
0
Watoto wawili wa familia moja wakazi wa kijiji cha Tabaruka wilayani Sengerema wamefariki dunia wakati wakiogelea kwenye kisima kilichopo kijijini hapo.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole amewataja watoto hao kuwa ni Given Aloyce (14) na Tekla Aloyce (12) waliokuwa wakisoma shule ya Msingi Tabaruka.

Kipole amesema tukio hilo limetokea Septemba 29, 2018  saa 11:00 jioni kijijini hapo walipokwenda kwenye kisima kufua sare za shule.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna amesema hajapata taarifa hizo lakini anafuatilia.

Mfanyabiashara Jela Miaka 5 Kwa Kosa la Kukutwa na Madini bila Leseni

$
0
0
Mfanyabiashara  Hafidhi Jonggradgorn ametiwa hatiani na madini yake yenye thamani ya Dola za Marekani 105,757.38 kutaifishwa na Serikali baada ya kukiri kosa la kukutwa na madini hayo bila leseni.

Mshtakiwa huyo alihukumiwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.

Mahakama hiyo ilimtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka miwili au kulipa faini Sh milioni mbili kwa kosa la kwanza na kosa la pili jela miaka mitatu au faini Sh milioni tatu.

Kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali, Jackline Nyantori alimkumbusha mshtakiwa mashtaka yanayomkabili ambapo alidai anadaiwa kutenda kosa kati ya Januari 2017 na Juni 3, 2018.

Nyantori alidai shtaka la kwanza mshtakiwa anadaiwa katika maeneo tofauti Tanzania na Falme za Kiarabu na India, akiwa si mtumishi wa umma kwa makusudi alifadhili biashara ya madini kwa lengo la kupata faida.

Nyantori alidai katika shtaka la pili, mshtakiwa katika tarehe hizo maeneo ya Mikocheni A, Mtaa wa Chwaku alikutwa na vito vya thamani aina ya gamestones kilo 62.76 vyenye thamani ya Dola za Marekani 105,757.38.

Mshtakiwa alikiri makosa hayo na kutiwa hatiani na upande wa mashtaka ulitaka apewe adhabu kwa mujibu wa sheria kwa sababu mshtakiwa ameingilia maliasili za taifa.

“Mheshimiwa Hakimu tunaomba madini yataifishwe yakabidhiwe serikalini chini ya Tume ya Madini, bastola arejeshewe mshtakiwa,” alisema Nyantori.

Akijitetea mbele ya hakimu, mshtakiwa huyo aliomba apunguziwe adhabu kwani ana familia na watoto wameshindwa kwenda shule kwa sababu ya kukosa ada, ni mfanyabiashara anayeipa Serikali kipato.

Hakimu Mashauri alisema mshtakiwa mbinu anayotumia inaikosesha Serikali mapato, hivyo alimuhukumu kwa kosa la kwanza faini Sh milioni mbili au kwenda jela miaka miwili.

Alisema kosa la pili faini Sh milioni tatu au jela miaka mitatu.

Hata hivyo mshtakiwa hajalipa faini hivyo amekwenda jela.

Queen Darleen Apangua Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Mbosso

$
0
0
Msanii  Queen Darleen ameeleza ni kwanini watu wamekuwa wakihisi ana mahusiano na Mbosso.

Muimbaji huyo pekee wa kike kutokea WCB amesema ni kwa sababu hajaweka wazi yupo kwenye mahusiano na nani.

"Kwa sababu hawamjui bwana wangu ndio sababu wanaongea lakini wangekuwa wanamjua wasingeongea na hawatamjua hadi niolewe," Darleen ameiambia SnS Tanzania (Simulizi na Sauti).

Kwa upande wake Mbosso alipoulizwa na waandishi kwenye red carpet ya Biko Jibebe Challenge alisema hakuna kitu kama hicho na kuulizwa swali kama hilo ni kuvunjiwa heshima.

Rich Mavoko: Sina Ugomvi Wowote na Diamond

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Rich Mavoko amesema hana tatizo lolote na Diamond Platnumz licha ya kuondoka kwenye lebo ya WCB.

Muimbaji huyo kwenye Mahojiano na The Playlist ya Times FM amesema kilichotokea kati yake na lebo hiyo sio ugomvi bali ulifika mwisho wa biashara yao, hivyo sasa wapo vizuri pamoja na uongozi mzima wa lebo hiyo.

Katika hatua hatua nyingine Rich Mavoko amesema kuwa maneno yanayosikika mwanzoni kwenye video ya wimbo Ndegele hayawahusu WCB kwani walikuwa wanataka tu kuvuta attention ya mashabiki ila kuhusu kuwa ni diss kwa lebo sio kusudio lao kabisa.

Mwaka 2016 Rich Mavoko ndo alijiunga na WCB, wimbo wake wa kwanza kutoa chini ya lebo hiyo unakwenda kwa jina la Ibaki Stori, kisha Kokoro na nyinginezo, pia ameweza kufanya kazi na wasanii wengine nje ya WCB kama Fid Q, Stereo, Nay wa Mitego, Lulu Diva na wengine.

Diamond Platnumz aipendelea Kenya Tamasha Lake la Wasafi Festival

$
0
0
Baada ya kimya kirefu kuhusu ratiba ya tamasha la Wasafi Festival, hatimaye Diamond Platnumz na uongozi wake wameanza kutoa dondoo za tamasha hilo ambapo ratiba inaonesha litahitimishwa nchini Kenya Desemba 31, 2018 .

Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram amedai kuwa, tamasha hilo litahusisha nchi zaidi ya moja na kuahidi kutoa ratiba muda mfupi ujao.

“KENYA!!! KENYA!!!! Jus to let you know that, Ikitokea Tanzania na nchi zitazotajwa tareh 31 DEC #WasafiFestival 2018 itakuwa inahitimishiwa Jijini #NAIROBI 🔥🔥🔥... TANZANIA!!!! najua mnashauku kubwa😊.... kaa hapa hapa na mimi details zenu zaja✋🏻 #SanaaImezaliwaUpya #WCB4LIFE"

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asili

SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Okoa Ndoa Yako Mke,Mume Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
Asilimia kubwa ya binadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wengi wamejaribu kutumia tiba sehemu tofauti bila mafanikio na  kukata tamaa hasa kina baba ambao ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao yapo hatarini kuvunjika kwa sababu Mume hana uwezo wa kumridhisha mpenzi wake 

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MKE AU MPENZI WAKO SABABU ETI UNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME MDOGO: tumia dawa ya NSENWA POWER ;dawa hii hutibu na kuponesha tatizo la  nguvu za kiume .

1 itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
2 itakupa uwezo kuchelewa kukojoa mda wa dakika 15-20 na kumfanya mpenzi wako naye aridhike 
3 huimalisha misuri iliyo legea na kusinyaa 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA : tumia dawa ya MASHESHE NO 2; hii huboresha uume saizi upendayo kuazia urefu wa inch 5,6,7,8 na unene  wa sentumita 2,3,4,5, dawa hizi hazina madhara yeyote kwa mtumiaji hata wazee hutumia na kupona 

MASANZA ni dawa ya vidonda vya tumbo zipo dawa za mvuto wa biashara ,mpenzi,uzazi ngiri,korodani kuvimba miguu. mgongo,kiuno kuuma nk 

MAHALI ILIPO OFISI UNAWEZA UKASHUKIA BUGURUNI MALAPA AU BUGURUNI ROZANA na MWANZA YUPO WAKALA pia unaweza ukaletewa popote ulipo wasiliana nami 0783185060  0752348593 DR AGU

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Kortini kwa Kumchapa Fimbo Mtoto

$
0
0
Mkazi wa Mikocheni A, Pyana Herbo (45), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni, Dar es Salaam kwa tuhuma za kumshambulia kwa mchapa   fimbo mtoto.

Karani wa Mahakama hiyo, Januari Kasekwa alidai  mbele ya Hakimu Marko Mochiwa kuwa Septemba 10 saa 4 asubuhi eneo la Mikocheni A, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimshambulia mtoto Christina Hebron kwa kumpiga na fimbo sehemu mbalimbali za mwili.

Mshtakiwa alikana  shtaka hilona alirudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana hadi Oktoba 5, mwaka huu, kesi itakapotajwa tena.

BREAKING: Necta Yafuta Matokeo Ya Darasa La 7 Kwa Shule Zote Za Chemba Na Baadhi Ya Shule Za Kinondoni, Ubungo, Mwanza Na Kondoa

$
0
0
Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza kuyafuta matokeo ya mitihani ya Darasa la saba kwa shule za msingi zote zilizopo ndani ya Halmashauri ya Chemba, pamoja na baadhi ya shule katika halmashauri ya Kondoa, Kinondoni, Mwanza jiji na Ubungo kwa kosa la kuhusika kwa kuvujisha kwa mitihani ya darasa la saba ikiwa ni kinyume na taratibu na kanuni za mitihani nchini.

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Oktoba 2, 2018 amezitaja shule  zilizofutiwa matokeo ni za halmashauri ya Chemba, Kondoa mkoani Dodoma.

Zingine ni Hazina na New Hazina, Aniny Nndumi na Fountain of Joy za jijini Dar es Salaam na Alliance na New Alliance na Kisiwani zote za Mwanza.

Dk Msonde amesema baada ya uchunguzi shule hizo zimebainika kuvujisha mitihani hiyo iliyofanyika Septemba 5 na 6 wakishirikiana na waratibu wa elimu wa eneo husika.


“Kufuatia kuvunjwa kwa kanuni za mitihani baraza limeamua kufuta matokeo ya kumaliza shule ya msingi ya halmashauri ya Chemba pamoja na shule ya Hazina na Kinondoni, Anyindumina na Fountain of Joy za Ubungo, Alliance na New Alliance ya Mwanza jiji pamoja na Kondoa Integrity ya Kondoa Mjini, na watahiniwa wa mtihani hiyo watairudia tena oktoba 8 na tarehe 9 wiki ijayo" Amesema Charles Msonde.

Aidha baraza hilo limefuta vituo vya mitihani kwa shule nane ambazo zilihusika katika uvujishaji wa mitihani hiyo sambamba na kupendekeza kuondolewa kwenye nafasi za ajira kwa baadhi ya maafisa elimu kata na wilaya waliohusika kwenye udanganyifu huo.

Rais Magufuli Katimiza Ahadi Yake Ya Milioni 20 Aliyoitoa Jana

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 02 Oktoba, 2018 ametekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi Milioni 20 kwa ajili ujenzi wa ofisi ya Wavuvi Wadogo Wadogo (UWAWAKI) waliopo katika eneo la Feri, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli alitoa ahadi hiyo jana alipokutana na wajasiriamali hao wakati akifanya mazoezi ya jioni pamoja na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli ambaye pia ametekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi Milioni 5 kwa akina Mama wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo hasa ya Mamalishe katika eneo hilo.

Fedha hizo zimekabidhiwa na Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike kwa Makamu Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani na kiongozi wa akina Mama wajasiariamali Bi. Ashura Seif Nanjonga, na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sofia Mjema na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bw. Tulusubisya Kamalama.

Kabla ya kukabidhi fedha hizo Bw. Ngusa amesema pamoja na kutoa fedha hizo Mhe. Rais Magufuli ameagiza Manispaa ya Ilala impelekee taarifa ya mapato na matumizi ya soko la samaki la Feri haraka iwezekanavyo na amemuagiza Mkuu wa Wilaya na Manispaa ya Ilala kushughulikia kero za wavuvi na wajasiriamali wa eneo hilo ikiwemo ushuru wenye kero na tatizo la vyoo.

Makamu Mwenyekiti wa UWAWAKI Bw. Amir Amani na kiongozi wa akina mama wajasiriamali wa Feri Bi. Ashura Seif Nanjonga wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwasaidia fedha hizo na kwa kuwajali wao pamoja na Watanzania wengine hasa wanyonge.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sofia Mjema amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutembelea soko la Feri na kuwasaidia wajasiriamali wa soko hilo na amesema yeye na timu yake ya viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala wataanza mara moja kushughulikia kero za wajasiriamali hao.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Oktoba, 2018

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Wapandishwa Kizimbani Kwa Tuhuma Za Kuharibu Noti za Elfu 10

$
0
0
Vijana saba wenye umri kati ya miaka 21 na 24 leo Jumanne Oktoba 2, 2018 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na shtaka la kuharibu noti za Sh70,000.

Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono amewasomea mashtaka yao leo, akieleza kuwa wanakabiliwa na kesi ya jinai namba 299 ya 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Hamza Wanjah.

Kombakono amewataja washtakiwa hao kuwa ni Vicent Kaduma (24), Rogers Swale (23), mwanafunzi Doreen Mwenisongole (22), Kelvin Mgeyekwa (23), Elia Chengula (24), Said Sadiq (21) na Ramadhani Selemani (23) wote wakazi wa Dar es Salaam maeneo ya Bahari Beach na Kunduchi.

Kombakono amedai Septemba 16, 2018 jijini Dar es Salaam, bila ya kuwa na mamlaka washtakiwa hao waliharibu kwa kuzikanyaga noti za Sh 70,000 za Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Baada ya kusomewa shtaka hilo, washtakiwa wote walikana na upande wa mashtaka ulisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Wakili wa upande wa utetezi, Stoki Joackim anayewatetea washtakiwa wote aliiomba mahakama iwapatie dhamana wateja wake kwa sababu shtaka linalowakabili linadhaminika kwa mujibu wa sheria na kwamba dhamana ni haki ya washtakiwa.

Baada ya kusikiliza hoja hiyo, Hakimu Wanjah alitoa masharti ya dhamana kwa washtakiwa kwa kumtaka kila mmoja  kuwa na wadhamini wawili wenye  barua na nakala za kitambulisho na kwamba kila mdhamini asaini bondi ya Sh 2 milioni.

Washtakiwa wote walifanikiwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana na kuachiwa huru.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 2, 2018 itakapotajwa tena.

Kesi Utakatishaji Fedha Dhidi Ya Aliyekuwa Mhasibu Takukuru Yakwama

$
0
0
Kesi  ya utakatishaji fedha na kumiliki mali zisizolingana na kipato chake halali, inayomkabili aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Takukuru, Godfrey Gugai na wenzake wanne, imeshindwa kuendelea kusikilizwa  sababu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina hela ya kuwaleta mashahidi.

Wakili wa Serikali, Pius Hila akisaidiana na wakili kutoka Takukuru, Vitalis Peter ameeleza hayo, leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba,  kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa.

Wakili Hilla amedai walishaita mashihidi  kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam lakini wameshindwa kufika kwa kuwa Mtendaji wa Mahakama hakuwa na fungu la  fedha, kwa  ajili ya kuwalipa.Ameendela kueleza kwa sasa wamepata  kibali kutoka kwa  Mtendaji wa Mahakama ambacho kinawaelezea kuwa malipo yatasubiri fedha zitakapoingia lakini mashahidi wameshindwa kuja kwa  gharama zao wenyewe.

"Mheshimiwa hakimu kutokana na hali hiyo, tunaomba terehe fupi kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji wa kesi hii," ameeleza Hilla.Kutokana na maelezo hayo, Wakili wa Utetezi Alex Mgongolwa aliwasilisha maombi mawili mahakamani hapo.

,"Mheshimwa, tunaomba jitihada za kuwapata mashahidi hao waliopo nje ya mkoa wa Dar rs Salaam ziendelee na pia  ni rai yetu kwa  mahakama upande wa mashtaka walete mashahidi ambao hawahitaji kuombewa kibali na hawatoki nje ya mkoa wa Dar es salaam ili Kesi hii iweze kuendelea," amedai Wakili Mgongolwa.

Kutokana na hayo, Hakimu Simba amesema, mahakama itazungumza na Mtendaji wa Mahakama ili kutafuta fedha sehemu yoyote ili mashahidi hao waweze kuja mahakamani na kutoa ushahidi kwa sababu kesi hiyo ni ya muda mrefu.Kesi imeahirishwa hadi  Oktoba 15 na 16, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa.

Mpaka sasa ni shahidi  mmoja wa upande wa mashtaka, Ayoub Akida(52) ambaye ni Ofisa Utumishi Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ameshatoa ushahidi wake dhidi ya Gugai.Mbali na Gugai, washtakiwa wengine, ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasin Katera.

Katika kesi ya msingi, Gugai na mwenzake, wanakabiliwa na makosa 43, kati ya hayo 19 ni ya kughushi, 23 ni utakatishaji fedha na moja ni kumiliki mali zisizoendana na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbali mbali.Gugai anakabiliwa na kosa la kumiliki mali zisozoendana na kipato chake, analodaiwa kutenda kati ya January 2005 na Decemba 2015.

 Akiwa ofisa wa umma ameajiriwa na TAKUKURU alikutwa akimiliki mali za zaidi ya Sh. bilioni 3.6 ambazo hazilingani na kipato chake cha awali na cha sasa

Mahakama Yagoma Kuifuta Kesi Ya Vigogo Klabu ya Simba

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema haiwezi kifuta kesi ya utakatishaji wa fedha inayomkabili Rais wa Klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange maarufu Kaburu sababu kesi hiyo imeishafikia hatua ya usikilizwaji wa awali.

Badala yake Mahakama kwa mara nyingine, imetoa amri na kuwapa siku 14 upande wa mashtaka kutekeleza amri iliyoitoa ya kuwataka aidha wafute mashtaka dhidi ya Zacharia Hanspoppe na mfanyabiashara, Franklin Lauwo au wabadilishe hati ya mashtaka kwa kuwaondoa washtakiwa hao ili kesi isikilizwe.

Uamuzi huo umetolewa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, kutokana na ombi la mawakili wa washtakiwa hao wakiongozwa na Nehemia Nkoko kuiomba mahakama ifute kesi hiyo kwa sababu upande wa mashtaka wameshindwa kuiendesha.

Akisoma uamuzi huo hakimu Simba amesema amepitia hoja za pande zote mbili na ameona kuwa, huu si muda muafaka wa kufuta kesi hiyo kwa sababu tayari ilikuwa katika hatua ya (PH) na pia ilishatoa amri ambayo bado haijatekelezwa.Hakimu Simba amesema upande wa mashtaka wanatakiwa watekeleze amri iliyotolewa Mei 12 mwaka ,2018, kwa hiyo haiwezi kufuta kesi hiyo, kwa sababu itafuta hadi amri ambayo tayari ilishaitoa na haijatekelezeka.

"Si muda mwafaka wa kufuta kesi hii, natoa siku 14 kuanzia kesho kwa upande wa mashtaka kufanya mabadiliko na kama hawatafanya hivyo, Mahakama inaweza kuamua vingine itakavyoona inafaa, " amesema Hakimu Simba.Aidha Hakimu Simba ametaka amri hiyo itekelezeke kwa sababu hawajulikani ni lini Hansoppe na Lauwo watakamatwa  wakati Aveva na Kaburu wapo mahabusu.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 16 mwaka 2018 kwa ajili ya washtakiwa kusomewa PH.Awali, Wakili wa utetezi, Nkoko aliomba Mahakama hiyo iwafutie mashtaka, washtakiwa hao kwa sababu wameshindwa kuiendesha kesi hiyo.Akijibu hoja hiyo, wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi akisaidia na Wakili kutoka Takukuru, Leonard Swai,  aliiomba mahakama kutupilia mbali maombi hayo kwa sababu bado wanaifanyia kazi amri waliyopewa na mahakama ya kumtafuta Hanspope na Lauwo.

Amedai Septemba 14 mwaka huu, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza kuwa wanawatafuta Hanspope na Lauwo jambo ambalo ni moja ya utekelezaji wa amri iliyotolewa na mahakama.

Katika kesi hiyo washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 10 likiwemo la kula njama, matumizi mabaya na kughushi nyaraka ikionyesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa USD 300,000 kwa Aveva kitu ambacho sio kweli.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images