Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

UTEUZI: Pancras Bujulu ateuliwa kuwa Mkurugezi Mkuu VETA


Navy Kenzo Wazungumzia Kujiunga na Lebo ya WCB Ya Diamond

0
0
Kundi la Navy Kenzo ambalo kwa sasa linafanya vizuri na wimbo wao mpya 'Katika' ambao wamemshirikisha Diamond Platnumz limeeleza ilivyokuwa hadi kumshirikisha muimbaji huyo na ishu ya kusaini WCB.

Navy Kenzo wakizunguza na Waandishi kwenye red carpet ya Biko Jibebe Challenge, wamesema wimbo huo walimtumia Diamond wakijua fika angeupenda na kwa sasa wanafanya kazi na Meneja Sallam SK na sio lebo ya WCB.

"Huu wimbo ambao tunatakiwa tumuweke, tukamtumia nadhani alikuwa kwenye tour yake ya Marekani, yeye mwenyewe aliipokea kwa shangwe sana kwa sababu mimi mwenyewe nilijua ni wimbo ambao ataupenda, akarudi tukaifanya then we have Katika today," amesema Nahreel.

Kuhusu suala la kusaini kwenye lebo ya WCB, Nahreel amesema bado hilo ila kwa sasa wanafanya kazi na Sallam SK kutokea kwenye labo hiyo pia.

Tangu Navy Kenzo kuwa chini ya Meneja Sallam SK wametoa nyimbo mbili ambazo ni Fella na Katika.

Bodi Ya Nafaka Na Mazao Mchanganyiko Kiungo Cha Wakulima Nchini

0
0
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inatekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) ili kuhakikisha kuwa Kilimo kinakua kwa asilimia 6 kwa mwaka kuendana na malengo ya Programu Kabambe ya Maendeleo ya Kilimo Barani Afrika (CAADP).

ASDP Awamu ya pili inatekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2027/28 imekijikita katika kuleta mageuzi ya  mtazamo uliopo wa kilimo cha kujikimu kufikia uendeshaji wa kilimo kwa mfumo wa kibiashara.

Aidha ASDP awamu ya pili imeweka kipaumbele kuendeleza mazao ya kilimo yakiwemo mazao makuu matano ya biashara (pamba, tumbaku, korosho, kahawa na chai) kwa kushirikisha wadau mbalimbali, hatu inayolenga kutimiza malengo ya Tanzania kufikia uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025.

Wakulima nchini wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo ukosefu wa miundombinu mizuri na umbali wa masoko, hivyo hukwaza wakulima kusafirisha mazao yao hadi mahali pa kuyauzia na wengi wao kujikuta wakiuza mazao yao kwa walanguzi na wasafirishaji kwa bei ya chini.

Mara nyingi wakulima hupunjwa kwa sababu ya kukosa taarifa sahihi za soko, au kutoelewa vipimo halali vya uzito na ujazo na wafanyabiashara wasio waaminifu hunufaika isivyo halali kwa kufanya udanganyifu katika vipimo.

Kutokana na hali hiyo, Serikali ilianzisha Bodi ya Mazao Mchanganyiko ili kujikita katika biashara ya mazao ya nafaka na mengine yasiyo na chombo cha usimamizi ili kumpa unafuu wa maisha mkulima.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19, Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba anasema kutokana na usimamizi imara wa Serikali kupitia Bodi za mazao, uzalishaji wa mazao mbalimbali umeendelea kuimarika hususani mazao ya asili ya biashara.

Anasema kuwa katika mwaka 2017/18 Bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko imenunua tani 2,504.09 za mahindi kutoka kwa wakulima wa mikoa ya Iringa na Ruvuma yenye thamani ya Tsh Bilioni 1.25.

Dkt. Tizeba anasema hadi kufikia mwezi Desemba mwaka hadi kufikia mwezi Desemba 2017 Bodi imesagisha tani 146.5 ambapo zimepatikana tani 112.7 za unga wa mahindi na tani 33.8 za pumba, ambapo usagishaji unaendelea na mauzo yanaendelea katika mikoa ya Iringa, Dodoma, Dar es Salaam na Mwanza.

Anaongeza kuwa katika kuongeza uwezo, Bodi imepokea mkopo wa Tsh Bil 3.66 kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kununua mashine yenye uwezo wa kusagisha tani 60 za mahindi kwa siku na mashine yenye uwezo wa kukamua tani 20 za mbegu za alizeti kwa siku zitakazofungwa katika eneo la Kizota mjini Dodoma.

“Aidha, Mashine hizo zitakapoanza kufanya kazi Bodi itaweza kununua tani 17,000 za mahindi na tani 6,000 za mbegu za alizeti kutoka kwa wakulima kwa mwaka na mzabuni wa kufunga mashine hizo kampuni ya UGUR ya Uturuki inatarajia kukamilisha ufungaji wa mashine kabla mwezi Julai, 2018” anasema Waziri Tizeba.

Dkt. Tizeba anasema katika mwaka 2018/19 Serikali itaendelea na uhamasishaji wa uanzishwaji wa kilimo cha mkataba na kibishara kwa zao la muhogo katika kanda za Mashariki na Kusini kwa kushirikisha Halmashauri za Wilaya ya Mikoa ya Lindi, Mtwara, Manyara, Singida na Morogoro.

Kwa mujibu wa Dkt. Tizeba anasema kilimo cha mkataba, Serikali itahamasisha wakulima kulinda mazao ya mikunde, bustani na mafuta kibiashara kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.

Ununuzi wa mazao ya wakulima kupitia Bodi ya Mazao utasaidia kuokoa uharibifu wa mazao mengi ya nafaka yanayokaridiwa kabla ya kuvunwa yakiwa shamba kutokana na tekonojia duni ya utunzaji na uhifadhi.

Kuandaliwa kwa mfumo wa ukusanyaji wa takwimu za mazao ya chakula na mazao yanayosindikwa viwandani, utasaidia kubaini wa mazao hayo upotevu katika mnyororo wa thamani na kutengeneza mikakati ya kuboresha viwanda, na hatimaye kutengeneza ajira na kipato.

Kubenea: Naweza Kuhama CHADEMA Muda Wowote Nikiamua

0
0
Mbunge wa jimbo la Ubungo (CHADEMA), Saed Kubenea amefunguka kuwa yeye kutohudhuria kwenye zoezi la uzinduzi wa kitabu cha sera za Chama hicho haimaanishi kuwa anataka kundoka kwani kuondoka ni maamuzi na anaweza tekeleza muda wowote.

Kubenea amesema kuwa katika uzinduzi wa sera halikuwa jambo la lazima, na alikuwa katika utekelezaji wa majukumu mengine hivyo wanaohoji kutoshiriki kwake ni watu waliopo kwaajili ya kumchafua.

Kubenea amesema kuwa ukumbi ulikuwa mdogo na walitakiwa kuthibitisha ushiriki, hivyo ukumbi usingeweza kujaza wabunge wote wa CHADEMA na Dar es salaam hayuko yeye peke yake.

“Naweza shiriki uzinduzi saa nne asubuhi na mchana nikahama, kwahiyo nisihukumiwe kwa kutoshiriki kwangu, kwakuwa haikuwa lazima na hakuna uhusiano wowote baina ya sera na kuhama, na sikuwa peke yangu Dar es salaam tuko zaidi ya saba”, amesema Kubenea.

Septemba 25, 2018 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilizindua kitabu cha sera za chama hicho toleo la mwaka 2018 kikiwa na sera 12 ambazo zimezungumzia namna ambavyo chama hicho kimejipanga kuinua maisha ya mtanzania, suala lililoibua maswali ni kwanini Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea hajaonekana katika eneo la tukio bila kuwa na taarifa kwa Umma.

Mbali na hilo Kubenea pia amekuwa nyuma katika majukwaa ya CHADEMA ikiwemo kutoonekana ushiriki wake katika kampeni za uchaguzi mdogo wa majimbo ya Ukonga na Monduli, baada ya kudaiwa kuwa miongoni mwa wabunge walioko mbioni kutimkia CCM kutokana na kutokuwa na maelewano na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe, tuhuma ambazo yeye amekuwa akizikataa na kudai hakuna wa kumuondoa.

Rais Mstaafu Mwinyi Atoa RambiRambi ya Milioni Mbili Ajali ya MV Nyerere

0
0
Rais Mstaafu wa awamu wa pili, Ali Hassan Mwinyi, ametoa rambirambi ya Sh milioni mbili kwa familia za waliopoteza ndugu zao katika ajali ya kivuko cha Mv Nyerere.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika kitaifa jijini hapa leo Jumatatu Oktoba Mosi, Rais huyo mstaafu aliwaomba wazee na makundi mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo kusimama kwa dakika moja kwa ajili ya kuwakumbuka waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea hivi karibuni na kuua watu zaidi ya 200.

“Tunakutana hapa baada ya janga kubwa lililotokea Ziwa Victoria, waswahili wanasema mkaa na maiti haachi kulia lia nami naanza kwa kutoa milioni mbili kama rambirambi,” amesema Mwinyi.

Lugola Awataka Wakuu Wa Idara Kushirikiana Na Vyombo Vya Ulinzi Na Usalama

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka wakuu wa idara kushirikiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Katavi.

Amesema hayo leo Oktoba mosi akiwa na kamati ya ulinzi na usalama pamoja na wakuu wa idara wa mkoa wa Katavi, alipowasili mjini Mpanda akitokea Kigoma.

Waziri huyo amefanya ziara ofisi za mkoa huo kwa ajili ya kujua ushirikiano wa watendaji wakuu wa mkoa huo pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoani humo.

Waziri Lugola amepolekewa na kaimu mkuu wa mkoa wa Katavi, Lilian Matinga na baadhi ya maofisa mbalimbali wa polisi mkoani humo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimsikiliza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, ACP Damas Nyanda alipokua anafafanua jambo katika Kikao cha Wakuu wa Idara wa Mkoa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoani humo. Watatu kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa huo, Abdallah Malela. 

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Watu 1,300 kuzikwa kaburi moja Indonesia

0
0
Maandalizi  ya kuizika miili ya takribani watu 832 waliofariki baada ya nchi ya Indonesia kukumbwa na tetemeko la ardhi pamoja na Tsunami yameanza.

Hapo awali kikosi maalumu kilielekezwa kuandaa kaburi la miili 300 lakini maelekezo mapya yametaka kaburi hilo liwe kwa ajili ya watu 1,300

Aidha serikali imesema kuwa idadi ya waliofariki na kujeruhiwa huenda ikaongezeka kutokana na kutoonekana kwa watu wengi huku juhudi za kufukua vifusi zikiendelea.

Uduni wa vifaa vya uokoaji unaelezwa kuchangia kuchelewesha kutoa miili ya watu 60 iliyokwama kwenye vifusi vya jengo moja la hoteli iliyoanguka katika Jiji la Palu lenye watu wapatao 300,000 ambapo watu wengi zaidi wamepatikana wakiwa wamekufa.

Rais wa Indonesia, Widodo, amekubali kupokea misaada kutoka nje baada ya kutembelea eneo hilo Jumapili ambapo ametaka zifanywe juhudi za usiku na mchana kukabili madhara ya tetemeko hilo lililokuwa na ukubwa wa ‘magnitude’ 7.5.

Video Mpya: Harmorapa ft. Amber Lulu - DUDE

0
0
Msanii Harmorapa anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya 'Dude' ambao amemshirikisha Amber Lulu. Itazame hapa.

Spika Ndugai Aindikia Barua Tume Ya Uchaguzi Kuhusu Kujiuzulu Kwa Mbunge Wa Jimbo La Serengeti.

Waziri Mkuu Mgeni Rasmi Kongomano la Wakulima

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la siku tatu la wakulima takribani 2,400 kutoka mikoa yote nchini.

Kongamano hilo ambalo ni la maadhimisho ya  miaka 25 tangu kuanzishwa kwa taasisi ya Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (Mviwata) litafanyika katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro Oktoba 3, 2018.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 1, 2018 juu ya ujio wa Majaliwa pamoja na kuadhimisha miaka hiyo 25 ya Mviwata, mkurugenzi mtendaji wa Mviwata, Stephen Ruvuga amesema waziri mkuu atafungua maadhimisho hayo pamoja na kuzungumza na wakulima hao.

Ruvuga amesema kongamano hilo pia litaambatana na  kongamano la kitaifa la wakulima kuhusu Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda nini nafasi ya wakulima wadogo, pamoja na mkutano mkuu wa 23 wa Mviwata.

Amesema watu wa kada mbalimbali  na mashuhuri wakiwemo mawaziri, wabunge, viongozi na watendaji waandamizi wa Serikali, wawakilishi wa balozi, washirika wenza, marafiki wa Mviwata na wadau toka ndani na nje ya nchi wanategemewa kuhudhuria akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally ambaye atakuwa mtoa mada mkuu katika kongamano hilo.

Ruvuga amesema kongamano hilo litajadili jinsi gani wakulima wanaweza kujipanga na kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda na kuangalia viwezeshi muhimu vya kufanikisha ushiriki wa wakulima wadogo katika mfumo wa uchumi wa viwanda ambao ndio mkakati wa Serikali ya awamu ya tano.

Wengine watakaoshiriki ni kamishna wa ardhi, mkurugenzi wa NDC, Profesa Damian Gabagambi pamoja na Profesa Issa Shivji.

Naye Ofisa Sera na Utetezi wa Mviwata, Thomas Laiser amesema mustakabali wa wakulima upo kwa wakulima wenyewe hivyo ujio wa waziri mkuu wa kuzungumza na wakulima utainua ari mpya na kuona namna Serikali inavyoendelea kuwathamini.

Laiser amevipongeza vyombo vya habari kwa namna ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wakulima wanapata manufaa kutoka kwa Serikali yao, huku akiviomba kutochoka kuhabarisha wananchi.

Wazee Nchini Wataka Uwakilishi Bungeni Na Mabaraza Ya Madiwani

0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
WAZEE wameiomba serikali kuhakikisha wanapata uwakilishi wa viti maalumu bungeni na mabaraza ya maidwani nchini ili kuweza kupaaza sauti zao sanjari na kutungiwa sheria kama yalivyo makundi mengine.

Akizungumza kwenye kilele cha siku ya wazee duniani Rais wa awamu ya pili Alhaji Ally Hassan Mwinyi amesema kuwa serikali ipo teyari na inaendelea kuhakikisha wazee wanapata huduma bora ikiwemo sheria hiyo.

Amewataka wazee hao kuwa na subira wakati mchakato wa kupata sheria ukiendelea sambamba na mapitio ya sheria hiyo kwani walipotoka na wanapoelekea na pazuri sana kuliko awali.

“Nawasihi sana muwe na subira wakati serikali ya awamu ya tano ikiendelea na mchakato huu wa wazee kupata sheria pamoja na suala la pensheni mliloomba kwenye risala yenu”alisema mwinyi.

Kwa upande wake waziri wa Afya wazee jinsia na watoto Ummy Mwalim alisema kuwa mchakato wa sheria umefikia mahali pazuri hivyo wanajipanga kuhakikisha mapitio ya sera ya wazee ya mwaka 2013 yanafanyiwa kazi kabla ya kuwa sheria.

Amesema kuwa masuala yote hayo yahitaji kufikiwa na kufanyiwa kazi na serikali ya wamu ya tano itahakikisha inaondoa kero zote wanazokumbana nazo wazee ikiwemo suala la matibabu.

“Nawasihi wazee wangu pindi mnapoenda kupata matibabu msiwahukumu wahudumu wa Afya wote bali msome jina la mhudumu huyo ili tuweze kudili nae na wataka wahudumu wote kuacha kutoa lugha zisizo na staha kwa wazee watakayefanya hivyo tutadili nae”alisema Ummy

Nae Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema kuwa mkoa huo umejipanga kuhakikisha wazee wote zaidi wanapata huduma bora za afya na yeyote atakaye enda kinyume hatua mbali mbali za kisheria zitachukuliwa juu yake.

Amesema kuwa mkoa huo una jumla ya wazee zadi ya 90 elfu na kati yao 16 elfu wanapata huduma za afya na vitambulisho na mkoa umejipanga kuhakikisha wote wanafikiwa.
 
Mwisho……………………..

Tanzania Yaongoza Duniani Kwa Kuwa Na Utajili Wa Urithi Wa Asili Baada Ya Brazil

0
0
Tanzania ni ya pili kwa Urithi wa Maliasili baada ya Taifa la Brazil la Bara la Amerika ya Kusini kwa kuwa na vivutio vingi vya Asili.

Hayo yameelezwa leo wakati wa ufunguzi rasmi wa Tamasha la Urithi Wetu (Urithi Festival)  linalofanyika katika viunga vya Kijiji cha Makumbusho Jijini  Dar-es –Salaam na Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wadau wa Utalii Tanzania,  Bwana  Abdukadir Luta Mohamed.

Amesema kuna vivutio vingi vya  urithi wa utamaduni, ukiweka pamoja vivutio vya utalii wa asili na utamaduni, Tanzania inaweza kuongoza kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii  duniani.

Bwana Mohamed  amevitaja baadhi ya vivutio hivyo  kuwa pamoja na tamaduni, makabila, mila, desturi, vyakula na Malikale.

Awali akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Urithi Kitaifa, Profesa Audax Mabula ameeleza kuwa Tanzania inajivunia kuwa na lugha kuu nne zilizopo Barani Afrika.

Amezitaja lugha hizo kuwa ni Wabantu ambao inawajumuisha makabila kama vile Wasukuma, Wajita na Wanyamwezi, Wanailotiki inawajumuisha Wamaasai, Wakushitiki-inayojumuisha  Wairaq,Wambulu, Wakhoisan –inayowajumuisha Wahadzabe na Wasandawe.

Profesa Mabula ameeleza kuwa, Kabila la Wasandawe limeanza kupotea lakini ni imani kuwa kabila hilo litaendelezwa kupitia tamasha la Urithi Wetu.

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Urithi Kitaifa amesema "Utalii wa Utamaduni utainuliwa kupitia Urithi festival.

Amewaomba Watanzania kushiriki vema kwenye Tamasha hili na kuvaa mavazi ya Kitanzania kama vitenge, ngozi, batiki, shuka na mavazi mengine ya asili katika maadhimisho haya na ya kila  Mwezi wa tamasha la Urithi.

"Urithi festival inatoa fursa kwa watu wote. Tunapenda waje hapa waone ubunifu, vitu muhimu na mambo ya ubunifu wa kila aina” Amesema Profesa Mabula.

Ameongeza kuwa, Watu tuheshimu Urithi wetu wa Utamaduni ili kuchochea Utalii wa ndani na nje ya Nchi.

Tamasha hilo limepambwa na  vikundi mbalimbali vya ngoma za kiasili, sarakasi, nyimbo, Wajasiriamali, vyakula vya kiasili ikiwemo nyama choma za porini  kama swala na nyati zilnazouzwa kwa shilingi elfu Nane kwa kilo.

Naye Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Bw. Richard Mayongela  katika kuunga mkono Tamasha la Urithi Wetu, imekabidhi fulana 100 katika hafla hiyo.

Tamasha hilo ambalo litakuwa likifanyika kila mwaka, linaandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, na lilizinduliwa rasmi Septemba 15 mwaka huu jijini Dodoma na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan likiwa na lengo la kuongeza idadi ya watalii nchini.

Imeelezwa kuwa, baada ya Tamasha hilo kufungwa rasmi jijini Dar-es-Salaam litaendelea kufanyika Jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheikh  Amri  Abeida Karatu, ambako ni njia kuu ya kuingilia katika Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro na Serengeti kuanzia Oktoba 8  hadi  13.

 MWISHO.

Baraza la Wazee CHADEMA Lasema Lina Ushahidi wa Wabunge na Madiwani Wao Kununuliwa na CCM

0
0
Baraza la Wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) limesema hatua ya baadhi ya viongozi na wanachama wa vyama vya siasa kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kunatokana na shinikizo kutoka katika chama hicho tawala.

Wakizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wazee Kimataifa, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema, Hashim Juma Issa, na katibu wake  Roderick Lutembeka  wamesema baadhi ya viongozi huzushiwa kesi kwa lengo la kuwatishia ili wahamie chama tawala.

Katibu wa baraza hilo  Roderick Lutembeka amesema Chadema inaposema wabunge na madiwani wao wanaoamia CCM wananunuliwa inao ushahidi.

"Suala la ushahidi wa wabunge na madiwani kununuliwa tunao na tuliwahi kutoa ushahidi wa mkuu mmoja wa wilaya akizungumza na kupanga mipango yote. Ushahidi huo tuliupeleka Takukuru lakini ukafunikwa funikwa," amesema Lutembeka na kuongeza;

"Kuna mtu kahamia juzi tu hapa, kafika huko kaanza kufanya mambo ya ajabu, kuna kijana mmoja alichukua mkopo alikuwa rafiki wa huyo mtu, alikuwa akimlazimisha ahamie huko ushahidi wa ushawishi huo tunao"


Katika hatua nyingine, baraza hilo limetoa maazimio ya sera mpya ya Chadema na kudai linaunga mkono sera hiyo ambayo pia imewagusa wazee.

"Leo ni siku ya wazee tunaona tuitumie siku hii pia kutoa maazimio yetu juu ya sera mpya ya Chadema tunaona sera imeelezea namna itakavyotatua changamoto za wazee" amesema Lutembeka.

Lutembeka amesema miongoni mwa maazimio ya wazee ni kuunga mkono sera hiyo katika kutatua changamoto za wazee ikiwamo huduma za afya kwa wazee.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya October 2


Mbunge Bwege Atiwa Mbaroni

0
0
Mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Seleman Bungara 'Bwege' anashikiliwa na polisi akidaiwa kutaka kufanya mkutano wa hadhara bila kuwa na kibali.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Christopher Ngubiagai , Bwege alikamatwa jana saa 10 jioni eneo la Maalim Seif  lililopo Kilwa Kivinje.

Ngubiagi amesema mbali na Bwege wengine wanaoshikiliwa na polisi ni madiwani wanne akiwemo diwani wa Kilwa Masoko na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Abuu Mjaka.

Rais Magufuli Ameahidi Kutoa Milioni 20 Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Ofisi Ya Wajasiriamali Wa Eneo La Feri Jijini Dar

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 1 Oktoba, 2018 ameahidi kutoa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa ofisi ya wajasiriamali wa eneo la Feri Kivukoni Wilayani Ilala Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli amekutana na Wajasiriamali hao ambao wanajumuisha Wavuvi wadogo na Mamalishe wakati akiwa katika mazoezi ya jioni pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli ambaye pia amewachangia wajasiriamali wanawake shilingi Milioni 5.

Pamoja na kumshukuru Mhe. Rais Magufuli, wajasiriamali hao wameomba awasaidie wasifukuzwe na Manispaa ya Ilala katika eneo hilo, na badala yake wawekewe utaratibu mzuri wa kufanya biashara zao.

Pia wameomba waondolewe ushuru unaotozwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA), kwa mitumbwi ya wavuvi wadogo wa samaki, kama ambavyo Serikali imewaondolea ushuru wakulima wanaopeleka sokoni mazao yasiyozidi tani moja.

Aidha, Wajasiriamali hao wamempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi nzuri ya kuiongoza nchi na kushughulikia kero za Watanzania ikiwa ni pamoja na kuwatembelea na kuwasikiliza kwa mara ya pili.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli ameahidi kufanyia kazi maombi ya Wajasiriamali hao na amewapongeza kwa juhudi zao za kujitafutia kipato.


Bosi Mpya TAKUKURU Atema Cheche...."Someni Alama za Nyakati, Nchi Hii Sio Salama kwa Wala Rushwa"

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Kamishna wa Polisi Diwani Athumani ameongea na Vyombo vya habari akiwataka wananchi kuongeza kasi kusoma alama za nyakati maana serikali ya awamu hii sio salama kwa wala Rushwa.

Akiwa Mkoani Kagera jana October 1,  CP Diwani alisema kuwa TAKUKURU inayoongozwa na yeye itatekeleza wajibu wake kwa kuzingatia Sheria haitaangalia itikadi, hadhi au cheo ulichonacho, atakayejihusisha na vitendo vya Rushwa hatabaki salama.

Diwani alisema atahakikisha anawaburuza mahakamani watuhumiwa wote wa vitendo vya rushwa mapema sheria ichukue mkondo wake. 

Pia aliwahadharisha watumishi wa umma kuwa makini na uadilifu wao katika maeneo ya kazi kwa vile sasa nyakati zimebadilika Serikalini.

Alisema kutokana na Rais Magufuli kueleza kutoridhishwa na namna washukiwa wa vitendo vya rushwa wanavyoshughulikiwa, jukumu lake kubwa la haraka ni kuwafikisha mahakamani watu wote waliotajwa au kuripotiwa Takukuru. 


Alisema watumishi wanapaswa kubadilika na kufanya kazi kwa weledi na kutumia muda wa kazi vizuri kwani Serikali hii haina mzaha.

“Huu si wakati wa mtumishi wa umma kujilimbikizia mali kiujanja ujanja. Kila mtumishi wa umma aridhike na anachokipata na afanye kazi kwa bidii ili kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli katika kuhakikisha fedha za umma zinatumika kwa shughuli za maendeleo. 


“Katika uongozi wangu nitahakikisha natumia juhudi zangu zote kwa ushirikiano na viongozi wenzangu wanaopiga vita rushwa kuhakikisha Tanzania bila rushwa inawezekana,” alisema.

Alisema rushwa ni adui mkubwa wa haki ambaye hapaswi kufumbiwa macho kwani imekuwa inarudisha nyuma maendeleo ya wananchi na kuwaathiri wananchi wanyonge.


“Niko tayari kupambana na nina imani hii vita nitaishinda. Wanaojipanga kuchukua rushwa au kutoa rushwa wajipange upya,” Diwani alionya.

Alisema Takukuru imejiwekea malengo kuona miradi yote inatekelezwa haraka na kwa ufanisi na kukamilisha utafiti wao kuhusu mazingira ya rushwa na kuomba ushirikiano wa wananchi.


“Takukuru peke yetu hatuwezi kufanya kazi peke yetu. Tunahitaji ushirikiano wa wananchi wote. Mfano nimeona kuna mianya mikubwa ya rushwa kwa wafanyabiashara wanaotumia mashine za EFDs.

Kiwango wanachoandika kwenye risiti hakiendani na bidhaa wanazouza.


 “Hawa inabidi tule naosahani moja. Nakemea wale wote wanaochukua asilimia fulani kabla ya mkandarasi hata hajatekeleza mradi,” alisema. 

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco G aguti alimpongeza Diwani kwa kuteuliwa akisema hana shaka na uwezo wake kusimamia masuala makubwa ya kitaifa.

NFRA Washikilia Msimamo Wao Kuhusu Ununuzi wa nafaka ya mahindi kwa ajili ya akiba ya Taifa ya Chakula

0
0
Na Mathias Canal, NFRA
Zoezi la kununua nafaka ya mahindi kwa ajili ya akiba ya Taifa ya Chakula unaendelea katika maeneo mbalimbali kote nchini ambapo wakulima kwa kiasi kikubwa wameitikia wito uliotolewa na Wakala wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) wa kutonunua mahindi yasiyokuwa na ubora.

Pamoja na Ubora wa mahindi kuwa changamoto katika maeneo mengi nchini kutokana na hali ya msimu wa mwaka Jana kuwa na jua Kali na mvua za msimu jambo lilolopelekea Mazao kuharibika yakiwa shambani.

Katika hatua nyingine Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. zikankuba ameendelea na ziara ya kikazi ya kutembelea vituo mbalimbali vya ununuzi ambapo hivi tarehe 1 Octoba 2018 alitembelea kituo cha ununuzi cha Kigonsela kilichopo Mkoani Ruvuma kukagua mwenendo wa zoezi la ununuzi katika kituo hicho.

Katika ziara hiyo ya Mtendaji Mkuu wa NFRA mkoani Ruvuma, Meneja wa Kanda ya Songea Ndg Amos Mtafya alieleza kuwa Kanda ya Songea pekee imepangiwa kununua jumla ya tani 7, 000 kwa awamu ya kwanza ya ununuzi na hadi kufikia leo tarehe 1 Oktoba 2018 Kanda hiyo imeshanunua zaidi ya tani 6000.

Ili kuimarisha dhana ya Ushirika, Wakala umenunua kwa kiasi kikubwa mahindi kupitia vyama ya Ushirika na vikundi vya wakulima yaani SACCOS na AMCOS ambazo jumla yake zinakuwa 23 ambazo ndizo zilizobainishwa na uongozi wa Mkoa wa Ruvuma.

Vikundi hivyo vya wakulima ni kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Songea vijijini, Mbinga mji, Mbinga vijijini,  Namtumbo na Wilaya ya Nyasa.

Vumilia alionyesha kuridhishwa na hali ya ubora wa nafaka iliyonunuliwa na kuwahimiza watumishi wa NFRA kuendekea kusisitiza na kununua mahindi yenye vigezo vya ubora unaokubalika kwa ajili ya Hifadhi ya Taifa ya Chakula.

Katika hatua nyingine Bi Vumilia amewapongeza watumishi wa NFRA kwa kazi nzuri ya kiuweledi wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao na wakala kwa ujumla.

MWISHO.

Mkebe Spesho Wa Dawa Ya Mitishamba Yenye Uwezo Mkubwa Wa Kumsaidia Mtu Aliyeathirika Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

0
0
Je, Unamatatizo haya na yamekusumbua kwa muda mrefu bila kupata tiba?

Wanaume wengi wanaupungufu wa nguvu za kiume. na kuwa na maumbile madogo ya kiume. 

Magonjwa kama. kisukari. presha, ngiri, kolodani kuvimba busha tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri , punyeto nk huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume 

Tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 ,    inatibu na kuponyesha matatizo haya yote         

 SUPER SHAFT;  ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume mara dufu na maumbile madogo ya uume                                    
 (1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa                                        
 (2) inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka.                           
 (3) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 na kuimalika uume zaidi                                  
(4) pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa 
    
NYATI POWER; inarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia 1_8 unene  sm 2_4 
(1) inaimalisha mirija ya uume iliyo legea ama kusinyaa                                                                       
(2) inasaidia kusafisha mirija ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume                        
(3) Husaidi kuurudisha nje uume uliyoigia ndani      
(4) inasaidia kuongeza manii nyingi ambazo zina viini vya uzazi                                                              
(5) Husaidia kutibu madhara ya punyeto matumizi makari ya madawa ya kizungu mirungi bangi na sigara

Tunatibu Magonjwa Yote Sugu Ngiri Kolodani Kuvimba Busha Bila Kufanyiwa Opresheni Tezi Dume Kisukari Presha Aina Zote Ugonjwa Wa Moyo Kwikwi Kichomi Miguu Kufa Ngazi Nk

Tunapatikana Magomeni Mikumi Karibu Na Kanisa Katoriki La Roma

Tumaini Tradition Clinc Ndiyo Sululisho La Matatizo Tote 

PIGA SIMU 0745_495181 AU  0682_ 644040                               
WOTE MNAKARIBISHWA TUMAINI TRADITION CLINC 
 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images