Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Idriss Sultan Amuombea Msamaha Maua Sama

$
0
0
Mchekeshaji wa filamu na muigizaji wa bongo 'movie' nchini, Idris Sultan amemuombea msamaha mwanamuziki Maua Sama kutokana na yaliyomkuta na kushauri mamlaka husika kutoa elimu kupitia mwanadada huyo kwa madai adhabu aliyoipata hadi sasa inamtosha.

"Binafsi ningependa kumuombea msamaha Maua kwa kuwa lengo sio kuivunjia heshima fedha yetu na Benki Kuu kwa ujumla. 

"Katika harakati za kujitafutia ugali makosa yatafanyika tu ila muhimu ni tukae tukumbuke lengo, na sio kukomoana, au kuonyeshana nani anajua zaidi, kuwekeana mabavu. Bali lengo ni kuelimisha jinsi ya kutunza vyetu wenyewe", ameandika Idriss.

Pamoja na hayo, Idriss ameendelea kwa kusema kuwa "ningependa ku-propose mumtumie Maua kuelimisha wengine kupitia 'influence' yake na adhabu aliyopata mpaka sasa tufanye imetosha. Hakuna aliye juu ya sheria ila tuvae tu uhusika wa lengo".

Msanii Maua Sama ambaye taarifa ya kukamatwa kwake ilitolewa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam, Lazaro Mambosasa hadi sasa bado anashikiliwa  katika kituo cha kati jijini Dar es salaam ambapo inadaiwa zoezi la uchunguzi linaendelea ili kusudi aweze kupandishwa mahakamani kujua tuhuma zake.

Tokea kukamatwa kwa Maua Sama kumeibuka mijadala mingi kwenye mitandao ya kijamii, ambayo kila mmoja anaongea jambo lake kuhusu  suala hilo bila ya kufahamu sheria zaidi zinasemaje.

Benki kuu ya Tanzania (BoT)  Jumanne Septemba 18, ilitoa  onyo kwa wananchi kuheshimu fedha ya Tanzania kwa kuwa ni moja ya alama ya taifa na kuonya kwamba kudhihaki na kukejeli noti na sarafu ni kosa la jinai.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Viwanja (vimepimwa) vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Kwa Mapinga viko Viwanja vya size na bei zifuatazo: 20/20 (sqm 400 ) kwa sh 4 milion, 20/30 (sqm 600 ) kwa sh 6 milion, 20/40 (sqm 800 ) kwa sh 8 milion, 20/35 (sqm 700 ) kwa sh 9 milion, sqm 1400 kwa sh 18 milion, sqm 1500 kwa sh 20 milion, sqm 2000 kwa sh 31 milion, sqm 3000 kwa sh 40 milion, 1 acre kwa sh 55 milion.

Pia iko plot 1 ya sqm 1000 (25/40) upande wa kiharaka (kiembeni beach) jirani na Ndoto polepole, plot inauzwa kwa sh 18 milion. Plots ziko umbali wa km 3 kutoka main road

Kwa Bunju ziko plot 2 zimepakana na kila moja ina ukubwa wa sqm 1700 kwa bei ya sh 45 milion sawa na tsh 90 milion (ukiziunganisha zote mbili).

Hint: Hakuna dalali.

For more information, call 0758603077, whatsap 0757489709, email: menejadar@yahoo.com

Madereva wanaosafirisha mizigo nje ya nchi watakiwa kuomba Pasipoti Mpya za Kielektroniki

Msajili wa Vyama Awataka Viongozi wa Vyama Kuimarisha Demokrasia Ndani ya Vyama Vyao

$
0
0
 Vyama vya siasa hapa Nchini vimetakiwa kudumisha na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama vyao ili viweze kutekeleza majukumu yao kama taasisi imara tofauti na mawazo ya walio wengi kuwa vyama hivyo sio imara kiasi cha kufananishwa na vikundi vidogo vidogo katika Jamii kama vile Saccos.

Hayo yalisemwa na Msajili wa vyama vya siasa hapa Nchini Jaji Francis Mutungi wakati wa ufunguzi wa kikao kazi na Viongozi wa Kitaifa wa vyama vya siasa jana  jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuvijengea vyama uwezo wa masuala ya rasimali fedha na rejista ya chama ili viweze kujiendesha kama taasisi.

Jaji Mtungi aliviambia vyama vya siasa kuwa ni muhimu kujenga vyama kama taasisi imara kwani mtu yeyote kutoka nje anayeitaji kuwekeza katika vyama hawezi kuwekeza katika chama ikiwa chama husika kitakuwa na hati chafu kutoka Ofisi yaMdhibiti na  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

‘’Mafunzo ya rasimali fedha na regista ya vyama kama vile mali za vyama ni muhimu kwasababu pamoja na vyama kupatiwa mafunzo haya ni vyema mkatambua kuwa vianawajibika kwa wananchi katika suala zima la utendaji wa ndio maana msajili analazimika kufanya ukaguzi katika vyama’’Alisema Jaji Mtungi.

Aidha Jaji Mtungi aliwaambia wawakilishi wa vyama vya siasa kuwa elimu ya fedha na regista ya chama ni muhimu kwasababu pia zoezi hili linasaidia sana kupunguza migogoro ndani ya vyama vya siasa.

Wakati huo huo Makamu Mkuu Mstaafu wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mkandala ambaye aliwasilisha mada ya Jinsi ya Kuendesha chama kama taasisi,alisema lengo la chama cha siasa chochote ni kujiandaa kushika madaraka au kuwa wapinzani wa serikali hivyo lazima kuhakikisha vinajijenga kama taasisi inayoaminika kwa wananchi.

Profesa Mkandala alisema siasa vyama vingi hapa Nchini ni matokeo ya ukoloni mamboleo ambao ulianza kushamiri hapa nchini kwa miaka 1990 ambapo nchi ya Tanzania kama zilivyo nchi nyingine Barani Afrika zilikumbwa na mabadiliko ya kiuchumi ya soko huria ikiwemo nchi zilizokuwa za ujamaa kuanza kufuata m asharti ya Shirika la Fedha Duniani IMF.

Aidha Profesa Mkandala alitaja vigezo vinavyofanya chama kuwa Taasisi muhimu kuwa ni Itikadi, Uongozi bora, Wanachama, Sera na programu za chama, Rasilimali

Lugola: Marufuku Watumishi wa Wizara Yangu Kunyanyaswa

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka viongozi na watumishi mbalimbali wa wizara yake wafanye kazi kwa kushirikiana na kuacha tabia ya kunyanyasana wakati wanatekeleza majukumu yao ya kikazi.

Lugola pia amesema kila mtumishi wa wizara yake ana umuhimu mkubwa kwa kufanikisha mafanikio ya wizara hiyo kwakuwa watumishi hao wanafanya kazi kwa kutegemeana. 

Akizungumza na watumishi wa makao makuu wa wizara hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Veta, jijini Dodoma jana, Lugola alisema kikao hicho alikiitisha kwa lengo la kujuana na watumishi hao pamoja na kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi.

“Mambo muhimu ambayo yatatuletea mafanikio ndani ya wizara yetu ni kufanya kazi kwa bidii, kufanya kazi kwa kushirikiana na tukifanya hivyo hakika tutapendana na kuzidi kufanikiwa,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, hapendi kuona mtumishi yeyote ananyanyaswa kwa kutopewa haki zake au kucheleweshewa pasipo kuwa na sababu za msingi ikiwemo malipo mbalimbali ya watumishi wanayodai, na endapo yatatokea hayo watumishi hao wamletee kero zinazowakabili ofisini kwake na kwa kushirikiana na katibu mkuu wa wizara hiyo watazitatua.

“Utumishi wa umma naujua, na pia nimepitia manyanyaso kadhaa mpaka leo nimefikia hapa kutokana na historia yangu, kwanini tusipendane?, kwanini tunyanyasane?, kwanini tusishirikiane?, ni tabia mbaya na inatakiwa kulaaniwa kwa baadhi ya wakuu wa idara na vitengo pamoja na wengineo ambao wanatabia ya kunyanyasa watumishi waliochini yao,” alisema Lugola.

Mkutano huo ambao ni wa kwanza kwa Waziri Lugola, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali, Jacob Kingu pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Ramadhan Kailima, kuzungumza na watumishi wa Wizara hiyo tangu walipoteuliwa miezi kadhaa iliyopita, walitaka kujuana zaidi na watumishi wa wizara hiyo pamoja na kujua changamoto zao zinazowakabili. Toggle screen reader support

Aliyekuwa Akitapeli Watu Kwa Kutumia Majina Ya Jakaya Kikwete, Salma Kikwete, Ridhiwan Viccoba Afikishwa Mahakamani

$
0
0
Mfanyabiashara, Masse Uledi (41), amekiri kumiliki simu tisa na laini nane zilizotumika kujipatia pesa kwa udanganyifu Sh. milioni 3.6 kama dhamana ya mkopo kutoka Focus Vikoba-na kutumia majina ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Salma Kikwete, Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi na Mchungaji Getruda Rwakatare.

Uledi alikiri madai hayo jana aliposomewa maelezo ya awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.Maelezo hayo yalisomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita, alidai 2017, mshtakiwa alifungua kurasa katika mtandao wa kijamii wa Facebook kwa majina manne tofauti akidanganya yanatoa mkopo kupitia Focus Vikoba.

Ilidaiwa katika kurasa hizo mshtakiwa alitangaza wanaohitaji mkopo kupitia taasisi hiyo, wawasiliane kwa namba za simu, 0759142712, 0714230840 na 0657076983 ili kupata mkopo.

Ilidaiwa kuwa Joyce Chitumbi alipiga simu kuomba mkopo wa Sh. milioni 10, na Septemba 9, 2017, alitakiwa kutoa Sh. 840,000 kama dhamana ya mkopo huo.

Upande wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa Daniel Dangi alitoa dhamana ya Sh. 600,000 na Sh. 200,000 kwa nyakati mbili tofauti kama dhamana ya mkopo wa Sh. milioni mbili.

Mwingine anayedaiwa kutapeliwa ni Lucas Kiula, ambaye alitoa ya Sh. 2,160,000 kama dhamana ya mkopo wa Sh. milioni 10, baada ya kudanganya taasisi hiyo iko chini ya Mchungaji Rwakatare wakati akijua si kweli.

Jamhuri ilidai mshtakiwa baada ya kujipatia fedha hizo alizima simu na namba nyingine alipopigiwa hakupokea.

Taarifa zilifikishwa Kituo Kikuu cha Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam na walifanya uchunguzi wa kimtandao na kubaini mshtakiwa anaishi Kitunda.

Ilidaiwa baada ya uchunguzi, Polisi walifanikiwa kufika nyumbani kwake na baada ya upekuzi walifanikiwa kumkamata na simu za mkononi nane na laini za simu tisa zilizotumika kwenye kurasa za facebook kwa majina ya Rais Kikwete, Mama Salma, Mengi na Mchungaji Rwakatare.

Mshtakiwa aliposomewa maelezo ya awali, alikiri majina na anuani yake, alikiri kumiliki simu na laini hizo kwamba ni mali ya marehemu mumewe.

Katika kesi ya msingi ilidaiwa kati ya Septemba 28 na Novemba, 2017 mshtakiwa alijipatia Sh. 3,600,000 kama dhamana ya kutoa mkopo wa jumla ya Sh. milioni 22 kutoka kwa watu tofauti huku akijua si kweli.

Awali, aliposomewa mashtaka hayo alikana na yuko nje kwa dhamana. Kesi itaendelea kwa kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri Oktoba 11, mwaka huu.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Steve Nyerere Ajitosa Sakata la Soudy Brown, Maua Sama....Ataka Waachiwe, Wapewe Nafasi ya Kuomba Radhi

$
0
0
Wakati msanii wa muziki, Maua Sama pamoja na mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu, Soudy Brown wakiendelea kusota rumande huku wasanii wengi wakionekana kuwa kimya, muigizaji Steve Nyerere ameibuka na kuamua kulizungumzia sakata hilo.

Steve ameomba wadau hao wa sanaa kuachiwa halafu waje kuomba msamaha kwa wananchi kwa kosa ambalo wamelitenda.

==>>Tazama alichokiandika hapo chini

"Morning .Yapita siku 5 Leo rafiki zetu wapo ndani ,Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kuwapa pole sana tena sana,Hili jambo kila kila Mmoja wetu amekuwa analiongelea anavyo JUA yeye wangine kisiasa na wangine wanalisema kama jambo jepesi hivi,MSANII NI KIOO CHA JAMII ,jambo lolote analo fanya basi linaweza kuwa na FAIDA kwa TAIFA letu ama hasara kwa TAIFA letu,.

"Sidhani kama MTU mwenye akiri kabisa kabisa akasimama na KUSEMA kukanyaga NOTI ya TAIFA lako na kumwaga mihela chini ni JAMBO zuri kama yupo huyo MTU huyo basi atakuwa na mapungufu naye.

"Tumefundishwa kulinda na KUHESHIMU chochote kile chenye Alama ya TAIFA,Sasa Naimani kupitia wenzetu na JAMII nyingine kuna la kujifunza hapa TENA kubwa sana,ILA NAJUA MTOTO akinyea mkono wa kulia huukati .Na mkubwa akikosea huchutama kwa kosa.

"Kwanza kabisa hakuna MTU aliye juu ya sheria maana sheria ni msumeno ,Kwa niaba ya wenzetu hawa tunaomba radhi sana tena sana kwa vyombo vyote husika.Imani yangu bado VIJANA hawa KAZI ya kuelimisha JAMII kupitia vipaji vyao inaitajika sana

"MIMI kama KIJANA mwenzao naomba kuchukua nafasi hii kuwaombea radhi naamini hawata rudia na si wao TU hata kwa sisi wangine,Nitafurahi nikisikia wamepewa dhamana ,Nitafurahi nikiona wapo huru na kuja kuomba radhi kwa WATANZANIA ,ambao hawakufurahishwa na tendo hilo ,Maana wakati wewe unakanyaga pesa kuna MTANZANIA anatafuta pesa kwa matibabu TU, mwingine kwa milo 3 TU ,mwingine kwa Ada ya mwanae shule TU, ILA ameikosa. 

"BASI KWA HILI NAAMINI TUTAKUWA TUMEJIFUNZA KITU. Kwa Niaba ya wenzangu TUNAOMBA RADHI. TUNAOMBA KAMA WENZETU WATAPATA DHAMANA BASI LITAKUWA JAMBO JEMA.

"TUNAIMANI MAOMBI YETU YA DHAMANA KWA WENZETU YATAFANYIWA KAZI.NAIMANI HATA WAO WALIVO FANYA IVO HAWAKUJUA KAMA NI KOSA. TUNAOMBA WAPEWE DHAMANA.

Atiwa Mbaroni Kwa Kumpa Mimba Binti Yake

$
0
0
Polisi katika Mkoa wa Mjini Magharibi wanamshikilia Muhammed Juma Muhammed kwa tuhuma za kumtia mimba binti yake wa kambo mwenye umri wa chini ya miaka 18.

Hata hivyo, kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Thobias Sedeyoka alisema jana kuwa kwa sasa yupo likizo, lakini amesikia uwepo wa taarifa za binti aliyetiwa mimba na baba yake.

Taarifa za kitendo kilichofanywa na mtuhumiwa huyo zilijulikana baada ya polisi kupatiwa taarifa na sheha wa Shehia ya Kijichi, Simba Ally Makame ambaye alipewa taarifa hizo na vijana wanaoshiriki ulinzi shirikishi. Binti huyo kwa sasa ameshajifungua.

Baada ya kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi katika Kituo cha Polisi Bububu, baba huyo alikiri kufanya kitendo hicho huku akidai kuwa “shetani alimpitia”.

Msako Wa Polisi Jijini Arusha Wafanikisha Kupata Gari Lililoibiwa, Bastola

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limefanikiwa kupata gari lililoibiwa aina ya Toyota Surf lenye namba za usajili T.996 AGK pamoja na Bastola aina ya Browning iliyokuwa na risasi Nane ndani ya Magazine.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana mchana  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi alisema kwamba tukio la kuibiwa kwa gari hilo lililokuwa linaendeshwa na Bi. Sarah Cornel (40) Mwalimu wa Sekondari na ni mkazi wa Olasiti jijini hapa lilitokea Septemba 17 muda wa saa 9:50 Alasiri katika maeneo ya Stand Ndogo.

“Mara baada ya kuegesha gari lake maeneo ya Stendi Ndogo alienda madukani kwa ajili ya kufanya manunuzi aliporudi hakulikuta ndipo alipoelekea kituo Kikuu cha Polisi kwa ajili ya kutoa taarifa ambayo ilifanyiwa kazi kwa kuanza kuweka vizuizi maeneo ya barabara kuu na kufanya msako mkali”.

Alisema wahalifu hao baada ya kuona njia zote zimedhibitiwa waliamua kulitelekeza gari hilo katika kituo cha Afya Kaloleni kilichopo jijini hapa ambapo siku ya pili muda saa 05:30 Asubuhi lilipatikana huku watuhumiwa wakiwa wametoweka na Jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi wa Kisayansi ili kuweza kuwabaini.

Mbali na tukio hilo Polisi mkoani hapa wameweza kupata silaha aina ya bastola ambayo ilikuwa na risasi nane ndani ya Magazine, Kamanda Ng’anzi alisema lilitokea Septemba 15 mwaka huu katika kijiji cha Kimyaki kilichopo tarafa ya Enaboishu wilayani Arumeru.

Alisema Jeshi hilo lilipata taarifa hiyo toka kwa raia wema ambapo waliwadokeza kuwapo kwa silaha hiyo ndani ya chumba cha mtu waliyekuwa wanamdhania mhalifu ndipo askari walikwenda katika eneo hilo na kufanikikwa kupata silaha hiyo ambayo wanakiri ilikuwa inamilikiwa isivyo halali na Jeshi hilo linaendelea na msako mkali kumtafuta mtuhumiwa huyo.

Mbali na mafanikio hayo msako wa Jeshi hilo umeweza kufanikisha kupata mali mbalimbali zikiwemo TV mbili “flat Screen”, Laptop, Jenereta na vitu vingine ambavyo vinasadikiwa kuibiwa katika mitaa mbalimbali ya jiji la Arusha siku za nyuma.

Kwa upamde wa Usalama barabarani Jeshi hilo limepanga kuanzisha kikosi maalum kwa ajili ya kuwadhibiti waendesha boda boda wanaovunja sheria hasa za kubeba abiria zaidi ya mmoja maarufu kama “Mishikashi” na wale wanaovuka mataa bila kuruhusiwa.

Kamanda Ng’anzi alisema kikosi hicho kitakuwa na askari ambao watakuwa wanavaa kiraia na watasambazwa katika maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha hali ambayo anaamini itakomesha tabia ya madereva wa boda boda wanaovunja sheria kwa makusudi.

Mkebe Spesho Wa Dawa Ya Mitishamba Yenye Uwezo Mkubwa Wa Kumsaidia Mtu Aliyeathirika Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

$
0
0
Je, Unamatatizo haya na yamekusumbua kwa muda mrefu bila kupata tiba?

Wanaume wengi wanaupungufu wa nguvu za kiume. na kuwa na maumbile madogo ya kiume. 

Magonjwa kama. kisukari. presha, ngiri, kolodani kuvimba busha tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri , punyeto nk huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume 

Tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 ,    inatibu na kuponyesha matatizo haya yote         

 SUPER SHAFT;  ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume mara dufu na maumbile madogo ya uume                                    
 (1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa                                        
 (2) inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka.                           
 (3) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 na kuimalika uume zaidi                                  
(4) pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa 
    
NYATI POWER; inarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia 1_8 unene  sm 2_4 
(1) inaimalisha mirija ya uume iliyo legea ama kusinyaa                                                                       
(2) inasaidia kusafisha mirija ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume                        
(3) Husaidi kuurudisha nje uume uliyoigia ndani      
(4) inasaidia kuongeza manii nyingi ambazo zina viini vya uzazi                                                              
(5) Husaidia kutibu madhara ya punyeto matumizi makari ya madawa ya kizungu mirungi bangi na sigara

Tunatibu Magonjwa Yote Sugu Ngiri Kolodani Kuvimba Busha Bila Kufanyiwa Opresheni Tezi Dume Kisukari Presha Aina Zote Ugonjwa Wa Moyo Kwikwi Kichomi Miguu Kufa Ngazi Nk

Tunapatikana Magomeni Mikumi Karibu Na Kanisa Katoriki La Roma

Tumaini Tradition Clinc Ndiyo Sululisho La Matatizo Tote 

PIGA SIMU 0745_495181 AU  0682_ 644040                               
WOTE MNAKARIBISHWA TUMAINI TRADITION CLINC 
 

Rais Magufuli Amteua Balozi Mstaafu Ali Siwa Kuwa Mwenyekiti Wa Bodi Ya Wadhamini Ya NSSF

$
0
0
Rais Magufuli Amteua Balozi Mstaafu Ali Siwa Kuwa Mwenyekiti Wa Bodi Ya Wadhamini Ya Nssf


Serikali Yafuta Baadhi Ya Tozo Za Kikanuni Zilizokuwa Zikitozwa Na OSHA Kuvutia Wawekezaji

$
0
0
Serikali imefuta tozo tano zilizokuwa zikitozwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (Osha) lengo likiwa ni kuwapunguzia mzigo waajiri.

Tozo zilizofutwa ni ada ya fomu Sh2,000, ada ya ukubwa wa eneo la kazi ambayo ilikuwa ni kati ya Sh 50,000 hadi Sh1.8 milioni.

Nyingine ni ada ya leseni na ada ya ukaguzi Sh200,000, ada ya vifaa vya kuzimia moto Sh500,000 na siku ya usalama kazini ambayo ilikuwa ikitozwa Sh450,000.

Akizungumza leo Alhamisi Septemba 20, 2018 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama amesema kuondolewa kwa tozo hizo ni agizo la Rais John Magufuli.

Mhagama amesema Osha imepitia mambo mengi ikiwemo kupunguza ratiba za ukaguzi ambazo zimekuwa zikifanyika mara kwa mara hasa katika sekta binafsi.

"Kwa mfano katika sekta binafsi kulikuwa na maumivu makubwa zaidi, yaani huyu anakagua hili, kesho mwingine, keshokutwa tena, sasa haipo hiyo na badala yake vyote vitakaguliwa kwa wakati mmoja, kwani tuna mfumo wa taasisi zote kwenda pamoja," amesema Mhagama.

Akizungumzia ajali zilizotokea mwaka jana, amesema jumla ya ajali 755 ziliripotiwa na kati ya hizo vifo vilikuwa 6 na 749 ni majeruhi.

Sekta ya uzalishaji iliongoza kwa asilimia 87, madini asilimia 7, ujenzi asilimia 4 na sekta nyingine asilimia 2.

Amesema utekelezaji wa punguzo la tozo hizo umeanza mara moja kuanzia yalipoanza mabadiliko ya fedha mwaka wa fedha hivyo akatoa onyo kwa watumishi watakaojihusisha na utozaji.

Tido aiambia mahakama mchakato wa kuitoa TBC analogia yalikuwa maelekezo ya Kikwete

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando amedai mchakato wa kulitoa shirika hilo analogia kuingia kwenye digitali ulitokana na maelekezo ya Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete.

Amedai hatua hiyo ilitokana na uamuzi wake wa kumtaka alibadilishe shirika lifikie katika hadhi inayostahili ambapo pia mchakato huo ulifanywa na Bodi ya shirika hilo na kupata baraka za Bodi ya Zabuni.


Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Tido ameyaeleza hayo leo Septemba 20, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi wakati akiongozwa na wakili Martine Matunda na Ramadhani Maleta kutoa ushahidi wake wa utetezi katika kesi inayomkabili.

Akitoa utetezi wake mahakamani hapo amedai tuhuma anazotuhumiwa nazo zimemuumiza sana kwa sababu alikuwa na ndoto ya kuifikisha TBC mbali ili iweze kutoa gawio kwa Serikali na si Serikali kutoa fedha kwa TBC.

Kuhusu kuisababishia Serikali hasara ya Sh 887.1 milioni, Tido amedai hakushirikishwa kwa namna yoyote katika malipo hayo na kwamba angeshirikishwa angeweza kunusuru pesa hiyo isilipwe.

Amedai mwaka 2012 aliitwa Takukuru kutoa maelezo na kwamba malipo yanaonyesha kufanyika mwaka 2015 yeye akiwa tayari ni mtuhumiwa na hakuwahi kuitwa popote kuulizwa kuhusu mchakato mzima wa mradi kabla malipo hayo hayajafanyika kwani angeweza kushauri.

Tido aliyeanza kujitetea leo Septemba 20 kuanzia saa tatu asubuhi amemaliza utetezi wake saa sita mchana.

Makonda Awapa Miezi Minne Waajiri Kuhakikisha Wanawaajiri Watu Wenye Ulemavu Kama Sheria Inavyowataka

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametoa miezi minne kwa waajiri wa Makampuni na Mashirika kuhakikisha wanawaajiri watu wenye ulemavu Kama Sheria ya Walemavu ya 2010 na Mikataba ya kimataifa ya mwaka 2006 iliyoridhiwa na Tanzania mwaka 2009 sura ya 27 unavyowaaagiza kufanya hivyo.

RC Makonda amesema ifikapo Mwezi January mwakani ataanza ziara ya kutembelea kwenye kila kampuni na taasisi jijini humo kukagua Kama wametekeleza sheria na agizo hilo ambapo watakaobainika kukaidi watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Aidha RC Makonda amesema kitendo cha kuwaajiri walemavu itapunguza ongezeko la ombaomba,ukatili, utupwaji wa watoto wenye ulemavu, kuhamasisha walemavu kusoma pamoja na kuwawezesha walemavu kuhudumia familia zao.

“Hatuwezi kuwa na ndugu zetu wamesoma na wanasifa za kupata Kazi lakini tunawanyima matokeo yake wengine wanaishia kujinyonga, kinamama wanatupa Watoto wenye ulemavu, mila potovu zinaendelea kupoteza haki na mwisho wanabaki wakiwa Masikini na kushindwa hata kumudu gharama za Matibabu, Jambo hili sio la kufumbia macho” alisema Makonda

Kwa mujibu wa Sheria ya ajira kwa watu wenye ulemavu No. 9 ya mwaka 2010 kifungu cha 31 inamtaka kila mwajiri mwenye wafanyakazi zaidi ya 20 kuhakikisha 3% ya wafanyakazi ni watu wenye ulemavu.

CRDB Yamtangaza atakayechukua nafasi ya Dr. Charles Kimei

$
0
0
Bodi ya CRDB imemtangaza Abdulmajid Musa Nsekela kurithi kiti cha mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo, Dk Charles Kimei, kuanzaia Juni, 2018.

Nsekela anarudi kujiunga na Benki ya CRDB baada ya kuondoka kwa takriban muongo mmoja uliopita alipoihama benki hiyo na kujiunga na Benki ya NMB.

Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa CRDB, Ally Laay leo Alhamisi Septemba 20, 2018  inasema mteule huyo ana ufahamu wa kutosha kusimamia na kuongoza taasisi za fedha na amekuwa mbunifu wa bidhaa na huduma tofauti kwa kipindi alichohudumu kwenye sekta hiyo.

“Nsekela ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 kwenye sekta ya benki; biashara na udhibiti,” inasomeka sehemu ya taarifa ya mwenyekiti huyo.

Mabadiliko hayo ya uongozi wa juu wa benki hiyo kubwa zaidi nchini yanafanyika kumruhusu Dk Kimei kupumzika baada ya kuingoza kwa takriban miaka 21.

Ndani ya uongozi wa mkurugenzi huyo, Nsekela alikuwa miongoni mwa waliochangia mafanikio ya taasisi hiyo kabla hajaondoka na kujiunga na NMB, wapinzani wa kibiashara kwenye sekta ya benki na fedha.

Taarifa ya Laay inabainisha kuwa Nsekela alijiunga na CRDB mwaka 1997 kama ofisa wa benki na miaka mitatu (2000) baadaye akapandishwa cheo na kuwa meneja uhusiano.

Kutokana na utendaji mzuri, miaka mitatu mbele (2003) aliongezewa majukumu na kuwa meneja uhusiano mwandamizi, nafasi aliyodumu nayo mpaka anaondoka na kujiunga na NMB mwaka 2008.

Fedha ya Zambia kuanza kutumika Tanzania

$
0
0
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga na mwenzake wa Benki Kuu ya Zambia, Dk. Denny Kalyalya, wanatarajia kutia saini makubaliano ya kuruhusu matumizi ya fedha za nchi mbili shilingi ya Tanzania na Kwacha ya Zambia ziweze kutumika katika nchi hizo mbili hasa katika eneo la mpakani la Tunduma na Nakonde.

Hatua hiyo sasa inakwenda kutoa fursa ya kiuchumi kwa kufanya biashara na uwekezaji katika miji ya mpakani ya Tunduma (Tanzania) na Nakonde (Zambia).

Makubaliano hayo yanatarajiwa kusainiwa kesho mkoani Songwe mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa huo, Brigedia Jenerali Nicodemas Mwangela na baada ya tukio hilo utafanyika mkutano wa hadhara katika eneo la Tunduma ambapo magavana hao watazunguza na wananchi wa pande zote mbili.

Taarifa iliyotolewa  na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ilieleza kwamba lengo la makubaliano hayo ni kuwezesha kupokelewa sarafu za nchi hizo mbili na taasisi rasmi za fedha ikiwa ni pamoja na mabenki ya biashara ya pande zote mbili bila kikwazo chochote.

“Nia ya hatua hii ni kurahisisha biashara kati ya nchi hizi mbili, kuondoa biashara holela ya fedha za kigeni mpakani na kuziwezesha serikali za Tanzania na Zambia kujipatia mapato stahiki ya kodi na tozo kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazofanyika katika miji hiyo.

“Benki Kuu za mataifa haya mawili rafiki, zimefikia hatua ya kusaini makubaliano hayo baada ya utafiti na majadiliano yaliyoanza tangu mwaka jana ambayo yalikuwa na lengo la kupambana na biashara holela ya fedha za kigeni na kuwawezesha wananchi wa pande zote kunufaika na shughuli za kiuchumi za mpakani,” ilieleza taarifa hiyo.



Kivuko Cha Mv. Nyerere Kinachotoa Huduma Kati Ya Ukara Na Bugolora Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza Kimezama Leo Majira Ya Mchana

$
0
0
Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari kati Bugorora katika Kisiwa cha Ukerewe na Kisiwa cha Ukara katika Ziwa Victoria mkoani Mwanza kimezama leo Alhamisi Septemba 20, 2018.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana amesema kivuko hicho kimezama wakati kikielekea katika Kisiwa cha Ukara.

Kamanda Shana amesema kuwa kivuko hicho kimezama leo mchana  baada ya kupinduka.

“Kiliondoka saa 6 mchana na ilipofika saa nane kamili mchana kilipinduka,” amesema.

Amesema kuwa watu watatu wameokolewa na shughuli ya uokoaji inaendelea ikiongozwa na mkuu wa mkoa huo, John Mongella.

Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Hassan Karonda amekiri kuzama kwa kivuko hicho

Waziri Mkuu Aagiza Watafiti Wa Zao La Ufuta Wapelekwe Makutupora

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba apeleke wataalamu kwenye kituo cha utafiti kilichopo Makutupora, Dodoma ili wazalishe mbegu bora za ufuta kwa ajili ya mikoa ya kanda ya kati.

Ametoa agizo hilo leo mchana (Alhamisi, Septemba 20, 2018) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mauno, wilayani Kondoa ambako alienda kukagua ujenzi wa kituo cha afya. Waziri Mkuu leo ameanza ziara ya kikazi ya siku saba katika mkoa wa Dodoma.

Alikuwa akijibu ombi la mbunge wa viti maalum, Bi. Mariam Ditopile ambaye alisema mkoa wa Dodoma ni wa pili kwa uzalishaji wa ufuta hapa nchini lakini aina ya ufuta inayozalishwa ni ya daraja la chini kwa sababu hawana mbegu za ufuta mweupe.

“Ili mradi mikoa ya kanda ya kati inazalisha ufuta, ninamuagiza Waziri wa Kilimo ahamishe watumishi kutoka kokote ili wakae Makutupora na kuwasaidia wakulima wawe na mbegu bora zenye kutoa mafuta mengi,” alisema.

Amesema kila mwaka Serikali inatumia zaidi ya dola za Marekani milioni 267 kuagiza mafuta ya kula kutoa nje ya nchi na kwamba hivi sasa imeamua kufufua mazao ya mbegu za mafuta ili mafuta ya kula yazalishwe kwa wingi hapa nchini.

 “Sasa hivi tumeanza kufufua mazao ya mbegu za mafuta ni nilianza mkoa wa Kigoma kwa kuhimiza kilimo cha michikichi. Sasa hivi niko Dodoma nahimiza ufuta na alizeti na nitaenda Singida kwa ajili ya zao hilo la alizeti,” amesema.

Kuhusu bei ya zao hilo, Waziri Mkuu amemtaka Mkuu wa Mkoa huo, Dk. Binilith Mahenge awasiliane na wakuu wa mikoa ya Lindi na Mtwara ili kubaini mbinu walizotumia kuhimiza zao hilo lakini pia amemtaka asimamie kwa karibu na ahakikishe kuwa katika msimu ujao, uuzaji wa zao hilo unafanyika kwa njia ya minada ili wakulima waweze kupata bei nzuri.

“Acheni kuuza ufuta nyumbani. Tabia ya mnunuzi kumfuata mkulima nyumbani ni wizi mtupu. Uzeni ufuta kwa minada, uzeni ufuta kwa minada. Kama mnataka hela, uzeni ufuta kwa minada,” amesisitizia wananchi hao.

“Ni kazi ya maafisa kilimo na maafisa ushirika wa wilaya kusimamia zao hili ka karibu. Wabainishe maghala ya kuhifadhia mazao huko huko wilayani ili wakulima wakishavuna, mnarekodi mavuno yao, mnapanga tarehe ya mnada mapema ili wananchi wawepo na wanunuzi wawepo pia,” amesema.

Amewataka wananchi hao walime kwa wingi zao la alizeti kwa sababu lina bei nzuri na halina gharama kubwa za maandalizi. “Nimeambiwa kulima ekari moja hapa Mauno ni sh. 30,000; kila ekari inatumia kilo tano na kila kilo moja ya mbegu ni sh. 500/- ukiweka na palizi kama sh. 30,000/- gharama zote ni sh.62,500/-,” amesema.

“Ukivuna ekari moja unapata magunia 20, na kila gunia linatoa dumu moja la lita 20. Kwa magunia yote utapata madumu 20, na kila dumu linauzwa sh. 60,000/- kwa hiyo una uwezo wa kupata sh. milioni 1.2 kwa ekari moja. Ukitoa gharama zako, bado unabakia na sh. 1,137,500/-. Sasa ukilima ekari mbili au tatu hali itakuwaje?” alihoji Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake wilayani Kondoa ambako atazungumza na wananchi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images