Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Polepole Awatuhumu CHADEMA kUGAWA Fedha na Sukari

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM), kimesema uchaguzi mdogo wa marudio unaotarajiwa kufanyika Septemba 16, 2018 umekuwa uchaguzi wenye mtihani kwao, kwa madai kukiukwa kwa baadhi ya sheria za uchaguzi ya mwaka 1985 kutoka wapinzani wao wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Katibu wa Itikadi wa Uenezi Humphrey Polepole amesema wapinzani wao wamekuwa wakitumia lugha zisizo na staha pamoja na utoaji wa rushwa kwenye mikutano ya kampeni unaofanywa na baadhi ya viongozi wake.

Polepole amesema; "Wenzetu hawakutaka kuheshimu sheria za vyama vingi, hawakufata maadili ya uchaguzi wenzetu wameyapuuza yote.., kinyume na sheria ya uchaguzi ya mwaka 1985, niwaambie tu TAKUKURU, chama cha CHADEMA wanagawa fedha na sukari kule Monduli na tunalifahamu hilo, tunaomba lifuatiliwe".

Polepole akaongeza; "Kamati ya maadili ya uchaguzi ya jimbo la Ukonga ilitoa adhabu kwa viongozi wa CHADEMA waliotumia lugha chafu kwenye kampeni ikiwemo kumtukania utu wake Mwita Waitara, ikiwataka waombe radhi hadharani lakini wamekaidi mpaka sasa".

Katika hatua nyingine Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema licha ya changamoto hizo wana uhakika kuwa chama chao kitashinda chaguzi hizo.

Uchaguzi wa majimbo ya Monduli  na Ukonga unarudiwa kutokana waliokuwa wabunge wake kwa tiketi ya CHADEMA, Julius Kalanga kwa upande wa Monduli na Mwita Waitara kwa upande wa Ukonga kujiuzulu huku wakiwania tena nafasi hiyo kupitia CCM.

Katika chaguzi hizo Tume ya Uchaguzi ilitangaza marudio ya uchaguzi katika kata 20 pamoja na majimbo matatu ikiwemo jimbo la Korogwe vijijini ambalo mgombea wake Timotheo Mzava wa CCM alipita bila kupingwa na pia katika kata chaguzi za kata 20 chama hicho kilipita bila kupingwa kwa kata 12.

Serikali Yaomba Kuifanyia Marekebisho Sheria ya Adhabu ya Makahaba ambayo kwa sasa Faini yake ni 500 tu

$
0
0
Naibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamadi Masauni ameliomba Bunge kufanya marekebisho ya sheria ya  adhabu ya makosa ya biashara  makahaba ambapo aliitaja kama ni miongoni mwa changamoto zinazopelekea biashara ya ukahaba kuzidi kufanyika licha ya jitihada za serikali kuitokomeza.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Pwani Zainabu Matitu ambaye alihoji "kwanini Jeshi la Polisi linawakamata wauzaji wa biashara hiyo bila kuwakamata wanunuzi pamoja na wapangishaji wa biashara ya madanguro, ambapo alipendekeza kubomolewa kwa eneo la uwanja wa fisi badala yake kujengwe miundombinu ya maendeleo ili wahusika wafanye biashara halali"?

Akijibu swali hilo Naibu Waziri Masauni alisema “..kumekua na changamoto mbalimbali nadhani bunge hili ni wakati muafaka  wa kuzitafakari, moja ni changamoto ya sheria, ukiangalia kwenye kanuni ya adhabu namba 176  (E) sura ya 16 adhabu ni faini isiyozidi shilingi 500 au 1000.., hivyo kuna haja kuangalia na kutafakari ili kazi kubwa inayofanywa ya kuwakamata wahusika na biashara ya ukahaba iwe na tija…”

Aidha Massauni alisema kupitia Wizara ya mambo ya ndani itashirikisha wizara nyingine ikiwemo Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi, katiba na sheria pamoja na wizara afya ili kumaliza tatizo la biashara ya Ukahaba nchini.

“…Tumendaa mkakati wa kushirikisha taasisi nyingine za serikali kama vile wizara ya  Tamisemi, wizara ya katiba na sheria na pamoja na ustawi wa jamii ili kupunguza na kumaliza vitendo hivi ambavyo ni kinyume na utamaduni wetu.” alisema Masauni.

Polisi Mwanza Wamtia Mbaroni Mwanaume Anayebaka Wanawake Baada ya Kuwawekea Dawa za Kulevya Kwenye Vinywaji

$
0
0
Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza linawashikilia watu watatu ambao wamekuwa wakifanya vitendo vya kihalifu katika maeneo mbalimbali mkoani humo, akiwemo mtuhumiwa wa tukio la ubakaji.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa  Mwanza, Jonathan Shanna, amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni  Kennedy Obworo, mwenye umri wa miaka 35, ambaye amekuwa akiwawekea wanawake dawa za kulevya katika vinywaji na kisha kuwabaka na kuwaibia vitu walivyonavyo.

Katika tukio jingine, jeshi hilo linamshikilia Sheshe Mazoya, anayedaiwa kuwa  mganga wa kienyeji mkazi wa Wilaya ya Magu kwa kosa la kukutwa na nyara mbalimbali za serikali ikiwemo mikia miwili ya nyumbu na pembe moja ya swala, kucha za Simba na miiba ya nungunungu ambavyo alikuwa anavimiliki kinyume na sheria.

Aidha, Kamanda Shanna amesema wanamshikilia mwanamke anayefahamika kwa jina la Sonia Fanuel kwa kosa la wizi wa kufungua milango kwa kutumia funguo bandia.

Kamanda Shanna ambaye amechukua nafasi ya Kamanda Ahmed Msangi aliyehamishiwa makao makuu, amesema watuhumiwa wote  wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani Jumatatu ijayo kujibu  tuhuma zinazowakabili.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Dkt Tizeba Awasilisha Taarifa Ya Zao La Kahawa Kwa Katibu Mkuu CCM, Ushirika Waungwa Mkono Kwa Kauli Moja

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Dodoma
Katika vipindi mbalimbali vya historia ya Tanzania masoko ya Kahawa yamekuwa yakiendeshwa kwa mfumo wa ushirika na soko huria, Mfumo wa soko huria uliruhusu makampuni na watu binafsi kununua mazao moja kwa moja kutoka kwa wakulima pasipo udhibiti hali iliyopelekea kuwepo kwa changamoto mbalimbali zikiwemo bei isiyokuwa na tija kwa mkulima, ubora hafifu wa mazao, ukwepaji wa kodi kwa wanunuzi na ukosefu wa takwimu sahihi za uzalishaji na mauzo.

Kutokana na changamoto za mfumo wa soko huria, Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli iliamua kurejesha ununuzi wa mazao matano ya kimkakati (Korosho, Tumbaku, Pamba, Kahawa, na Chai) kupitia vyama vya ushirika tangu mwaka 2016 ili kunufaisha wakulima, wanunuzi/wafanyabiashara na serikali.

Hayo yamebainishwa jana tarehe 14 Septemba 2018 na Mhandisi Mhe Dkt Charles Tizeba, Waziri wa kilimo wakati akiwasilisha taarifa ya mwenendo wa soko la kahawa nchini kwa Dkt Bashiru Ali Kakurwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi katika ukumbi wa mikutano wa CCM Makao makuu maarufu kama White House, Mkutano uliohudhuriwa na wabunge kutoka maeneo yote yanayozalisha kahawa, Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga, Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (NEC) Makongoro Nyerere, Naibu waziri wa Kilimo, Mhe Omary Mgumba, wataalamu kutoka wizara ya kilimo akiwemo Naibu katibu mkuu Prof Sizya Tumbo, Mrajis wa vyama vya ushirika,vyama vya ushirika na wawakilishi wa wakulima kutoka maeneo yanayolima kahawa.

Katika taarifa hiyo Dkt Tizeba alieleza kuwa kamwe hawezi kuruhusu mtu mmoja mmoja au kundi la watu kuvunja ushirika ambao hivi karibuni umeanza kuimarika mahususi kwa ajili ya kumkomboa mkulima uamuzi ambao umebainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 katika sura ya pili ibara ya 22 ikisisitiza kuviimarisha na kuviwezesha vyama vya ushirika kuwa na uwezo wa kutafuta masoko ya mazao ya wakulima ya ndani na nje kwa kuweka mfumo madhubuti wa ukusanyaji, uchambuzi na uenezaji wa taarifa za masoko na kutoa elimu juu ya uongezaji wa thamani na biashara.

Alieleza kuwa zipo faida nyingi kwa mkulima anapouza kupitia ushirika na hasa vyama vya msingi ambazo ni pamoja na wakulima kuwa na nguvu ya pamoja ya kushauriana ili kupata bei nzuri na kunufaika na kilimo, wakulima kupata nguvu ya kuanzisha na kuendesha maghala na viwanda vya kuongeza thamani ya mazao yao, kuwawezesha wakulima kutunza ubora wa mazao kwa mujibu wa sheria, kanuni na miongozo ya mazao husika.

Faida zingine ni kuwawezesha wakulima kupunguza gharama za uzalishaji kwa kuagiza pembejeo kwa pamoja, kuwezesha upatikanaji mazao ya uhakika na yenye ubora kwa wanunuzi, kuwezesha serikali za mitaa na serikali kuu kupata mapato yake stahiki kulingana na uzalishaji halisi, kuwezesha upatikanaji wa takwimu sahihi za idara ya wakulima na uzalishaji; na kuwawezesha wanunuzi kufanya malipo ya mazao kwa kuzingatia makubaliano yaliyofikiwa katika minada.

Aidha, Dkt Tizeba alisema kuwa mwenendo wa mauzo ya kahawa kwa msimu wa mwaka 2016/2019 ni mzuri ukilinganisha na misimu miwili iliyopita ya mwaka 2016 na 2017. Mauzo ya kahawa kwa mwezi Agosti 2018 ni mara mbili ya mauzo ya msimu wa mwaka 2017 ni mara nne ya msimu wa mwaka 2016. “Mauzo ya kahawa mwezi Septemba 2018 kwa mnada mmoja uliofanyika ni zaidi ya mauzo yote ya mwezi Septemba 2017 na ni sawa na mauzo yote ya kahawa kwa mwezi Septemba msimu wa mwaka 2016” Alisisitiza Dkt Tizeba

Kwa upande wake Dkt Bashiru Ali Kakurwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi akizungumza mara baada ya mjadala huo kutuama kwa masaa 8 kujadili namna ya kupata masoko ya mazao ya kilimo, urahisi wa upatikanaji wa mitaji, siasa ya kilimo kupitia ushirika na maandalizi ya miundombinu rafiki katika kilimo, alisema kuwa nchi ya Tanzania ipo katika mageuzi makubwa ya kimfumo na kimuundo hivyo mgogoro wa kiuchumi ni lazima ujitokeze kutokana na watu kulazimisha mazoea na haramu kuwa halali.

Alisema kuwa viongozi wote wa chama na serikali wanapaswa kuunga mkono jitihada za serikali kumkomboa mkulima kupitia ushirika, kujenga uchumi kupitia mshikamano lakini ushirika unaotakiwa ni ule wa Demokrasia wenye mizizi imara ili kuimarisha usalama wa nchi katika kilimo ambao unategemea wakulima wadogo.

Dkt Bashiru aliongeza kuwa ni lazima CCM kiwe chama kinachoingoza na kuisimamia serikali kwa kujenga utamaduni wa kujadiliana mambo muhimu ya kitaifa ili kukifanya chama hicho kuongeza imani maradufu kwa wananchi waliokiamini chama hicho na kukipa dhamana ya kuongoza Dola kupitia ilani ya ushindi ya mwaka 2015-2020.

Katika hatua nyingine ameitaka Wizara ya kilimo na Wizara zingine zote sambamba na taasisi za umma kutoa taarifa za mara kwa mara kwenye vyombo vya habari kuhusu yale yanayofanywa na serikali, kueleza mikakati ya serikali katika kuimarisha uchumi, sambamba na kutaja mafanikio yanayofanywa na serikali ili kuongeza uelewa kwa wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakipotoshwa.
 
MWISHO.

Jeshi La Polisi Jijini Arusha Lawahakikishia Usalama Wananchi Siku ya Kupiga Kura Kesho

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limesema litaendelea kuimarisha ulinzi katika uchaguzi mdogo wa marudio wa kugombea kiti cha ubunge unaotarajiwa kufanyika kesho Jumapili wilayani Monduli kama jinsi ilivyokuwa kwenye kampeni.

Akitoa taarifa hiyo leo asubuhi, Kamanda wa Polisi mkoani hapa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi, alisema wananchi wenye sifa za kupiga kura wajitokeze kwa wingi katika vituo vya kupigia kura kwani Jeshi hilo limezidi kuimarisha ulinzi ili uchaguzi huo ufanyike kwa amani na utulivu.

“Kama ilivyo kwenye kampeni hali ilikuwa tulivu na wakati wa uchaguzi tutahakikisha kwamba hali hii inaendelea kuwa shwari, askari toka vikosi mbalimbali watakuwepo wilayani hapo kwa ajili ya kuhakikisha uchaguzi unafanyika katika hali ya usalama.” Alilisitiza Kamanda Ng’anzi.

Aidha aliwataka wananchi wa jimbo la Monduli mara baada ya kutimiza haki yao msingi ya kupiga kura wasikae kwenye vituo kwani hali hiyo inaweza kusababisha vurugu.

Kamanda Ng’anzi aliwaonya baadhi ya watu wanaopanga kufanya fujo wakati wa uchaguzi au mara baada ya uchaguzi kumalizika watakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria na kusisitiza kuwa yeye mwenyewe atakuwepo wilayani humo kwa ajili ya kujionea na kusimamia kwa karibu shughuli za Usalama katika kipindi chote cha kupiga kura hadi kutangaza matokeo.

“Ole wao watakaopanga kufanya vurugu, Jeshi la Polisi lipo imara na halitashindwa kumkamata yeyote atakayeshawishi au kufanya fujo katika uchaguzi huo ambao tunategemea utakuwa wa amani na utulivu”. Alimalizia kwa kuonya Kamanda Ng’anzi.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Atiwa Mbaroni Kwa Kumnyonga Mjomba Wake

$
0
0
Mkazi wa Kijiji cha Mwai, Kata ya Mtenga wilayani Nkasi, mkoani Rukwa, Said Matenga (50), ameuawa kwa kunyongwa kwa kamba na mpwa wake baada ya kumfukuza nyumbani kwake kutokana na tabia za wizi.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 2:30 usiku katika kijiji hicho, wakati marehemu akitoka kunywa pombe katika kilabu kilichopo kijijini hapo.

Alisema siku moja kabla ya tukio hilo, Matenga alimfukuza nyumbani kwake mpwa wake huyo aitwaye Singu George (35) kutokana na tuhuma za kuiba vitu vya nyumbani kwake na kwenda kuviuza ili apate fedha ya kununulia pombe.

Baada ya mpwa wake huyo kufukuzwa nyumbani kwa babu yake, kitendo hicho kilimkasirisha na kuwahusisha rafiki zake waliofahamika kwa majina ya Mathias Said (28) pamoja na Luleka Luhende (28) ambao walimvizia mzee Matenga na kisha kumuua kwa kumnyonga na kamba shingoni.

Kamanda Kyando alisema baada ya watuhumiwa hao kufanya mauaji hayo waliutupa mwili wa marehemu kwenye majani karibu na Mto Lita uliopo kijijini hapo.

Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya uchunguzi zaidi na watuhumiwa hao wanashikiliwa na polisi na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika, ili wakajibu tuhuma zinazowakabili.

Spika Nduai: Hakuna Bunge Lolote Katika Historia ya Nchi Yetu Lililowahi Kuwa na Wasomi Wengi Kulizidi Hili la 11

$
0
0
Spika  wa Bunge, Job Ndugai, amewasilisha bungeni takwimu za umri na kiwango cha elimu cha wabunge wote ambapo wenye Shahada za Uzamivu na Uzamili ni 161 kwa Bunge zima.

Ndugai alisema hayo jana, baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kutoa hoja ya kuahirisha Bunge, ambapo alisema katika takwimu hizo, Chama cha Wananchi (CUF) wanazo 14, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) 31 na Chama Cha Mapinduzi (CCM) 114.

Aidha, Spika Ndugai pamoja na mambo mengine, alisema hakuna Bunge limewahi kuwa na wasomi wengi kuzidi hili la 11 tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961.

Katika takwimu zake hizo, amemtaja Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Bulembo (CCM), kuwa ndiye mbunge mwenye umri mdogo kuliko wote, akiwa na miaka 27, huku mbunge mwenye umri mkubwa kuliko wote akiwa na miaka 74, lakini hata hivyo, hakumtaja ila alisema; “ila leo hayupo.”

“Jana niliwaambia nitafanya zoezi kidogo la takwimu za wasomi ya kuona bunge letu likoje kiusomi, nimefanya ‘homework’ yangu, nitataja wachache, maana baadhi ya watu wanapenda kuliita bunge hili bunge la vijana, lakini baada ya takwimu hizi wabunge wenye umri wa miaka 40 kwenda mbele ni asilimia 80 ya wabunge wote.

“Kwa hiyo haya maneno ya kusema hili bunge la vijana siyo kweli, wakati mwingine ujana wakati mwingine ni ya ujumla sana, mtu anaweza akafikiri bado kumbe umri umeshaenda,” alisema Spika.

Alisema kwa upande wa kundi la Viti Maalumu, kwa kuanzia ameangalia takwimu za elimu ya sekondari kwenda mbele na kwamba elimu ya msingi ameiacha hadi siku nyingine.

“Elimu ya sekondari kwa Viti Maalumu wote ni 24, katika hao 24 CUF wako watano, Chadema watano, CCM 14, wenye cheti na stashahada CUF wanne, Chadema wanane na CCM 16,” alisema.

Spika Ndugai alisema wenye Shahada na kuendelea, Viti Maalumu CUF mmoja, Chadema 23, CCM 32, upande wa Shahada ya Uzamivu jumla 11, CCM 10 na mmoja Chadema, na kuongeza kuwa takwimu hizo zinasaidia wale wanaosema CCM haina wabunge wasomi, kwani bado CCM inatamba.

“Maprofesa tunao saba na wote saba ni wa CCM, PhD kwa wabunge wote humu ni 29, moja CUF, moja Chadema na 27 CCM, maana yake watu kwenye mitandao ooh CCM imejaza vihiyo mara eeh ehh, sasa takwimu hizo,” alisema Ndugai.

“Kwa ujumla wake wako baadhi wanasema Bunge hili ndiyo Bunge ambalo tangu historia halijawahi kutokea la namna hii kwa aina hii ya elimu niliyoieleza hili ni bunge la 11 tangu tupate uhuru, hakuna bunge limewahi kuwa na wasomi wengi kuzidi hili bunge la 11, huo ndio ukweli wenyewe na ndiyo hali halisi.

“Nilikuwa naangalia kule Buyungu kwa Mheshimiwa Chiza (Mbunge wa Buyungu, Christopher Chiza) wagombea wale wa CCM walikuwa kama 22, waligombea kwa CCM wote ni wahitimu wa vyuo vikuu, hiyo inakupa picha ya nchi sasa na inakoelekea, yaani kama Buyungu hali ni hiyo kwa vyovyote vile na kwingine nako kutakuwa kumechangamka,” alisema Spika Ndugai.

VIDEO: Kitu anachotamani Kukifanya Jackline Wolper kwa Rihanna na Nick Minaj

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Jackline Wolper amesema ndoto yake kubwa ni kumvisha msanii wa Marekani, Rihanna.

Wolper ambaye ni Mbunifu wa Mavazi pia ametaja wasanii wengine kuwa ni Cardi B na Nicki Minaj.

"Mimi hapa Jackline Wolper siku isiyo na jina nitawavalisha Rihanna, Cardi B au Nicki Minaj maana wale ndio wana swag zangu.

"Nitaanza na Rihanna kwa sababu ndio mchizi wangu, mambo yake ndio yangu, yaani mimi ndio Rihanna wa Bongo. She don't care anafanya maisha yake, anavaa kile anachojisikia akiona yeye amependeza basi amependeza, ndio mimi," Wolper ameiambia Wasafi TV.

Jackiline Wolper ni Mbunifu wa Mavazi kupitia duka lake linalokwenda kwa jina la House of Stylish

==>>Msikilize hapo chini akifunguka

Makontena ya Makonda Yakosa Wateja Tena

$
0
0
Makontena  ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam leo Jumamosi Septemba 15, 2018 yamekosa tena wateja.

Makontena hayo yameshindikana kuuzwa katika mnada uliofanyika jijini Dar es Salaam. Hii inakuwa ni mara ya nne makontena hayo kushindwa kuuzika.

Akizungumza kwenye mnada huo, mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya udalali ya Yono, Scolastica Kevela amesema mnada huo umeendeshwa lakini mnunuzi hajapatikana.

Kevela amesema hadi sasa bei zinazofikiwa na wateja hazijafikia malengo waliyowekewa. Amesema wao kama madalali wataendelea kufanya utafiti wa kuwapata wateja.

Wateja wachache waliokuwa kwenye mnada huo walionekana kutaja bei lakini hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kufikia kiwango kilichowekwa.

NEC Yavitaka Vyama Na Wagombea Kuzingatia Na Kuheshimu Sheria Siku Ya Kupiga Kura

$
0
0
Na Mwandishi wetu
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa, wagombea, wananchi na watendaji wa uchaguzi kuzingatia na kuheshimu matakwa na masharti ya Sheria za Uchaguzi, Sheria za Nchi na Maadili ya Uchaguzi wakati wa upigaji kura, kuhesabu, kujumlisha kura, na kutangaza matokeo katika uchaguzi mdogo utakaofanyika kesho Jumapili kwenye majimbo ya Ukonga na Monduli na kata 9 za Tanzania Bara.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage katika risala yake kuelekea uchaguzi huo mdogo unaofanyika kufuatia sababu mbalimbali ikiwamo wabunge na madiwani kujizulu, kufariki, kutohudhuria vikao na kufutwa uanachama.

Jaji Kaijage aliwataka wadau hao wa uchaguzi kushirikiana na Tume kuhakikisha kuwa viashiria vya kuvunjika kwa amani na utulivu vinaepukwa ili uchaguzi utakaofanyika uwe huru, wazi na wa haki.

Mbali na wito huo, Mwenyekiti huyo aliwasihi wapiga kura wote waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na wanaoishi kwenye maeneo yanayofanya uchaguzi mdogo, kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka wawaongoze kwa kipindi cha takribani miaka miwili ijayo.

“Wananchi wafanye na kutekeleza zoezi la kuwachagua wawakilishi wao bila hofu, woga, wasiwasi au ushawishi kwani chini ya Kanuni ya 3.1 (b) ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, Serikali imepewa wajibu wa kuhakikisha kuwa kuna hali ya usalama, amani na utulivu katika kipindi chote cha Uchaguzi.”, aliongeza Jaji Kaijage na kusisitiza kuwa:

“Ni matumaini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa, hali ya amani na utulivu kwenye maeneo ya Uchaguzi ambayo imekuwepo hadi hivi sasa, itaendelea kudumishwa ili kuhakikisha uchaguzi huu mdogo unafanyika na kumalizika salama kwa ustawi wa Taifa letu.”

Alivikumbusha vyama vya siasa na wagombea kuwa mwisho wa mikutano ya kampeni ni leo saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni na baada ya muda huo, vyama, wagombea na mashabiki wasifanye kampeni za aina yoyote, kama vile kutumia alama za vyama zinazoashiria kampeni, vipeperushi, bendera, mavazi na vingine kwa kuwa kesho ni siku ya uchaguzi.

“Pale panapokuwa na malalamiko yoyote ya ukiukwaji wa Sheria na Taratibu za Uchaguzi, malalamiko hayo yafikishwe kwenye mamlaka inayohusika kwa utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria. Vivyo hivyo, viongozi wa vyama vya siasa, wagombea au wafuasi wao na wananchi kwa ujumla wajiepushe na vitendo vinavyoweza kusababisha fujo au vurugu katika vituo vya kupigia, kuhesabia na kujumlishia kura”, alisema.

Jaji Kaijage aliwataka wapiga kura kuondoka kituoni na kwenye maeneo ya kituo cha kupigia kura mara baada ya kupiga kura yake kwa kuzingatia tafsiri sahihi ya Kifungu cha 104 (1) kikisomwa pamoja na Kifungu cha 72(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania kwenye Shauri la Madai Anuai (Misc. Civil Cause No. 37 la mwaka 2015) mpiga kura.

Aliongeza kuwa mbali ya wale ambao Sheria za Uchaguzi zinawaruhusu kuingia na kuwepo kwenye vituo vya kupigia kura, wananchi wanatakiwa kujiepusha na mikusanyiko au mikutano katika maeneo ya vituo vya kupigia kura na vyama vya siasa vimeweka mawakala vituoni ambao watalinda maslahi ya vyama husika na wagombea wao.

Alikumbusha kuwa wanaoruhusiwa kuingia kwenye Vituo vya kupigia, kuhesabia na kujumlishia kura ni wale tu walioainishwa kwenye kifungu cha 72(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na kifungu cha 63(2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Alivitaka vyama siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi huo kuweka mawakala katika vituo vyote vya kupigia na kujumlishia kura kwa utaratibu ambao vilikubaliana na Tume tarehe 10/07/2018 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Alivikumbusha kuwa mawakala hao wanaruhusiwa kuwepo katika vituo vya kupigia kura na wanatakiwa kufuata na kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazoongoza Uchaguzi katika kipindi chote cha kupiga, kuhesabu, kujumlisha kura na kutangaza matokeo.

Jumapili ya tarehe 16 Septemba, 2018, ni Siku ya kupiga kura katika uchaguzi mdogo wa Ubunge wa Majimbo ya Ukonga katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam, Monduli katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli mkoani Arusha na uchaguzi mdogo wa Udiwani katika Kata Tisa (9) zilizopo katika Halmashauri 5, za mikoa 4 ya Tanzania Bara.

“Uchaguzi huu Mdogo wa Ubunge na Udiwani Tanzania Bara, utahusisha jumla ya wapiga kura 470,936 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kutakuwa na Vituo vya Kupigia Kura 1,143.

Jaji Kaijage aliwakumbusha wapiga kura wa Majimbo ya Ukonga, Monduli na kata zote kuzingatia kuwa upigaji kura utafanyika katika vituo vile vile vilivyotumika wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambavyo vitafunguliwa saa moja kamili (1:00) asubuhi na kufungwa saa kumi kamili (10:00) jioni.

Alisema iwapo, wakati wa kufunga kituo watakuwepo wapiga kura katika mstari ambao wamefika kabla ya saa kumi jioni na hawajapiga kura, wataruhusiwa kupiga kura.  Mtu yeyote hataruhusiwa kujiunga katika mstari wa wapiga kura baada ya saa kumi kamili (10:00) jioni.

Alisisitiza kuwa watakaoruhusiwa kupiga kura ni wale tu ambao wamo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye Jimbo au Kata husika na wana kadi ya mpiga kura na wale waliopoteza kadi zao za kupigia kura au zimeharibika au zimechakaa watumie Pasi ya Kusafiria, Leseni ya Udereva au Kitambulisho cha Uraia kinachotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Hata hivyo, alisema mpigakura ataruhusiwa kutumia vitambulisho hivyo mbadala, iwapo tu; atakuwa aliandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mwaka 2015, jina lake liwe katika orodha ya wapiga Kura katika kituo anachokwenda kupiga Kura na majina yake yaliyopo katika Daftari la Mpiga Kura yafanane kwa herufi, maneno na tarakimu na majina yaliyopo katika kitambulisho mbadala.

Atiwa Mbaroni Kwa Kumkata Panga na Kumuua Mtoto wa Mkewe Walie Achana Naye

$
0
0
Jeshi la polisi mkoani Mtwara linamshikilia mkazi wa Mkalapa wilayani Masasi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto Clara Thomas (2) ambaye ni mtoto wa aliyewahi kuwa mke wake kwa kumkata  panga shingoni.

Akizungumza leo Jumamosi Septemba 15 mwaka huu, kamanda wa polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya amesema tukio hilo lilitokea jana(Ijumaa) katika Kijiji cha Chibwini baada ya mama mzazi wa marehemu kwenda kumtembelea mama wa mtuhumiwa ili kuwasalimia watoto aliowaacha kwa mwanaume huyo.

“Mtuhumiwa amezaa na mama wa marehemu watoto wawili na baada ya hapo wakaachana, lakini huyu mwanamke, alikwenda Msumbiji na kuolewa kisha kumzaa Clara (marehemu),”amesema Mkondya.

Kamanda Mkondya amesema baada ya mama kukaa muda mrefu Msumbiji  alifunga safari kuja Masasi kwa ajili ya kuwasalimia watoto nyumbani kwa mkwewe wa zamani.

“Wakati mama wa marehemu anafika nyumbani hapo, (mtuhumiwa)  alikuwa shambani lakini alirudi nyumbani baada ya kupata taarifa  kuwa mzazi mwenzake amefika kuwasalimu watoto,” amesema Kamanda.

Kamanda Mkondya ameeleza kuwa, wakati Clara anakwenda nyuma ya nyumba kujisaidia, mtuhumiwa  alimfuata nyuma na kumkata panga shingoni.

Amesema polisi wanakamilisha upelelezi na utakapokamilika watamfikisha mahakamni.

Magari Yaanza Kupita Katika Barabara Ya Juu (Flyover) Eneo La Tazara Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Baada ya hivi karibuni Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa kutembelea na kukagua ujenzi wa barabara za juu (flyover), eneo la Tazara Dar es salam na kusema umekamilika kwa asilimia 98, hatimaye leo barabara hizo zimeanza kutumika.

Msemaji mkuu wa serikali Dkt. Abbas Hassan, amethibitisha kuwa kuanzia leo serikali imeruhusu rasmi matumizi ya barabara hizo hadi pale uzinduzi utakapofanyika mwezi ujao.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitembelea barabara hizo za juu tarehe 29/8/2018, katika makutano ya Barabara ya Mandela na Nyerere (Tazara) na kusema mradi huo umekamilika kwa asilimia 98.

Katika ziara yake hiyo Majaliwa aliweka wazi kuwa wakati wowote kuanzia Oktoba, 2018, Rais John Magufuli atazindua barabara hiyo ambayo imepewa jina la Mhandisi Patrick Mfugale.

Serikali ya Tanzania ilisaini mkataba wa ujenzi wa barabara hizo na Kampuni ya Sumitomo Mitsui Construction ya Japan mwaka 2015 na kueleza kuwa mradi huo utagharimu zaidi ya Sh87 bilioni.



Dongo Janja Asherehekea Siku Yake Akiwa Kalazwa Hospitali

$
0
0
Ikiwa leo September 15, 2018 ni siku ya kuzaliwa Dogo Janja, siku hiyo muhumu haijamuendea vizuri msanii huyo.

Dogo Janja amezidiwa kiasi cha kulazwa katika kituo cha Afya cha AAR Sinza, Dar es Salaam kwa matibabu kutokana na kusumbuliwa na kifua kutoka siku ya jana

Kwa sasa Dogo Janja anaendelea vizuri na matibabu kwenye kitu hicho cha afya ambapo amelazwa kwa ajili ya uangalizi zaidi wa kimatibabu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Septemba 16

IGP Aonya Vurugu Chaguzi Jimbo La Ukonga Na Monduli

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro ameonya wale wote watakaojaribu kufanya fujo wakati wa Chaguzi ndogo katika Majimbo ya Ukonga na Monduli kuwa watachukuliwa hatua kali kwa kuwa Jeshi hilo limejipanga kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafanyika kwa amani na utulivu.

IGP Sirro ameyasema hayo jana Jijini Dar es Salaam baada ya  kuzungumza na Askari watakaosimamia zoezi hilo  leo katika Jimbo la Ukonga ambapo amesisitiza kila mmoja kuwa makini katika kusimamia zoezi hilo.

Aidha IGP Sirro amewataka Wananchi kutambua wajibu na mara wamalizapo kupiga kura kurudi nyumbani ili kusubiria matokeo.

Ajinyonga Baada ya Kuwaua Kwa Mapanga Watoto Wake Wawili

$
0
0
Mkazi wa Chanika jijini Dar es salaam, Dotusi Isaya anadaiwa kuwaua watoto wake wawili, kumjeruhi kwa panga mkewe pamoja na mama mkwe, kisha kujiua baada ya kukataliwa kuwachukua wanae.

Akizungumzia tukio hilo, kamanda wa polisi Mkoa wa Lindi, Pudensiana Protas amesema Isaya alifanya mauaji hayo usiku wa kuamkia jana huko Nachingwea mkoani humo ambapo mtuhumiwa alikwenda Nachingwea anakoishi mkewe Mariam Lucas na kujificha pembeni mwa nyumba ambayo haijamaliza kujengwa (pagala) akimvizia kisha kumkata panga eneo la kisogo na begani.

“Baada ya kumkata mkewe aliingia ndani ya nyumba (katika) chumba wanacholala watoto na kukuta wanawe wawili wamelala na watoto wengine, lakini yeye aliwaua wanawe kwa kuwakatakata”, amesema Kamanda.

Kamanda amesema kuwa Isaya ameamua kufanya tukio hilo baada ya mkewe kumkatalia asiende na watoto wake Bukoba baada ya kuondoka jijini Dar es salaam walikokuwa wakiishi awali, ambapo mke wake alimwambia mume wake kuwa watoto wakiwa wakubwa atawachukua, lakini kwa sasa ataendelea kuishi nao kwa kuwa bado ni wadogo.

Kamanda ameongeza kuwa kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, wamesema walianza kusikia vilio saa sita usiku na walipofika eneo la tukio waliwakuta majeruhi wawili (Amanda na Mariam) pamoja na maiti za watoto wawili pamoja na mtuhumiwa akiwa amejinyonga.

Hilo si tukio la kwanza la mzazi kuua watoto wake kwani Aprili 2017, mkazi wa Bukoba, Respicius Deogratius aliwaua wanaye mapacha waitwao Nyakato na Nyangoma kwa kuwakata vichwa.

Tukio jingine ni la Aprili mwaka huu ambapo Pius Salum, mkazi wa Matai, Kalambo mkoani Rukwa alimuua mtoto wake, Benedicto Salum (13) kwa kumpiga ngumi na mateke tumboni akidai si wake.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Wimbo Mpya wa Mbosso- Hodari

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images