Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ujerumani Ya KWANZA Kufungua Ofisi ya Ubalozi Dodoma

0
0
Ujerumani  imekuwa nchi ya kwanza kufungua ofi si ndogo mjini Dodoma, iliyozinduliwa mjini hapa jana. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa ofisi hiyo ya mawasiliano, ambayo itafanya pia shughuli za kibalozi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga alisema hatua hiyo ni ishara chanya kwa nchi nyingine kufungua ofisi zao jijini Dodoma. 

“Tunajua Umoja wa Mataifa umefungua ofisi yake ya mawasiliano hapa jijini Dodoma, lakini kwa upande diplomasia ninyi (Ujerumani) mmekuwa wa kwanza kufungua ofisi ndogo na huu ni mwelekeo mzuri wa kuhamia kabisa jijini hapa na pia ni ishara chanya kwa mataifa mengine kuhamia Dodoma,” alisema.

Mahiga aliongeza, mara nyingi historia inajirudia, wakati leo (jana) tunasherehekea uzinduzi wa ofisi ndogo ya ubalozi wa Ujerumani, takribani miaka 100 iliyopita Ujerumani walikuwa wakisherehekea kufikia nusu ya ujenzi wa Reli ya Kati.” 

Alisema Ujerumani imekuwa na uhusiano wa miaka mingi na kuwa nchi ya kwanza kuiingiza Tanzania kwenye uchumi wa dunia.

Mahiga aliiomba Ujerumani kuwa mstari wa mbele na mbia wa kuisemea Tanzania katika mashirika ya kimataifa kama Umoja ya Ulaya (EU), na Baraza la Umoja wa Mataifa la Ulinzi na Usalama na kuongeza kuwa ajenda zote za nchi, zitakuwa zikijadiliwa hapa nchini.

 Balozi wa Ujerumani nchini, Dk Detlef Waechter alisema ofisi yake imefungua ofisi ndogo ya Wakala wa Ujerumani wa Maendeleo (GIZ) na (KFW) pamoja na Ubalozi wa Ujerumani uliopo Dar es Salaam baada ya kuwapo kwa ongezeko la uhitaji.

 “Karibu serikai yote ya Tanzania imeshahamia katika mji mkuu, tumeona ongezeko la uhitaji wa kutafuta njia ya kuendeleza ushirikiano katika nyanja zote kwa kiwango kile kile, ukaribu na urafiki wetu,” alisema.

Aliongeza: “Hii ndio sababu watendaji watatu wa Ujerumani katika nchi hii wameungana na kusema tufanye mpango wa kufungua uwakilishi Dodoma”. 

Dk Waechter alisema Ujerumani inajua kuwa nchi kuhamisha makao yake makuu huchukua muda mrefu na kupitia changamoto kadhaa. Alitoa mfano hatua ya nchi yake iliyohamisha makao makuu yake kutoka mji wa Bonn kwenda Berlin.

“Tukiwa katika mwaka wa 30 tangu kuanza kuhamisha Makao Makuu ya nchi, asilimia 50 ya watumishi wa serikali bado wanafanya kazi zao si katika mji mkuu mpya wa Berlin, ila bado wako Bonn.” 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge aliwahakikisha ulinzi na usalama kwa Mkoa wa Dodoma na kuongeza kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada za kuboresha miundombinu na huduma ili kuhakikisha watu wa mataifa yote wanaishi wa usalama.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Agizo la Rais Magufuli Laanza Kutekelezwa....Nemc, Mkemia Mkuu wa Serikali wachukua sampuli maji yenye Sumu

0
0
Wataalamu  kutoka Baraza la Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, wamechukua sampuli zaidi ya kumi ya maji kutoka katika vyanzo mbalimbali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi, ili kuona kama maji hayo yana kemikali zenye madhara kwa viumbe hai.

Sampuli ya maji hayo yanayodhaniwa kuwa na kemikali yanayotiririka kutoka katika mgodi wa Acacia North Mara mpaka kwenye makazi ya watu.

Uchukuaji wa sampuli hizo ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli alilolitoa hivi karibuni alipokuwa ziarani mkoani Mara.

Akizungumza wakati zoezi hilo likiendelea, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dk. Vedast Makota, alisema kuwa NEMC imeanza kutekeleza agizo hilo kwa kuchukua sampuli katika maeneo yote ili kubaini kama zina madhara kwa viumbe hai au la.

“ NEMC kwa kushirikiana na ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali watafika kila mahala ikiwamo kupitia vibali vyote vya awali ili kubaini kama utolewaji wa vibali hivyo ulikidhi vigezo vinavyotakiwa na kuona kama wamiliki wa mgodi huo wanazingatia masharti yaliyoagizwa katika vibali hivyo,” Dk. Makota alisisitiza.

Alisema utafiti wao utaenda sambamba na uchukuaji sampuli mbalimbali yakiwamo maji, mimea na mchanga ambapo watahakikisha wanashirikiana na jamii inayozunguka mgodi huo ili kufanikisha zoezi zima kuona kama kuna viashiria vinavyoshukiwa kuwa na chembe chembe zenye kemikali.

“Tupo katika hatua za awali za utekelezaji wa agizo hilo ambapo wataalamu wametembelea maeneo ya Mto Tigite, ambao kwa kiasi kikubwa maji yake ndiyo yanatumika sana kwa wakazi wa eneo hilo katika shughuli mbalimbali za kijamii,” alisema.

Alisema wameshatembelea mabwawa mbalimbali yanayotumika kuhifadhia tope sumu (TFS) zinazotokana na shughuli za mgodi huo, ikiwamo wataalamu kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kuchukua sampuli mbalimbali ambazo zitapelekwa maabara kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya kitaalamu.

“Baada ya kukamilisha zoezi la utafiti na uchukuaji sampuli hizo na kubaini ukiukwaji wa sheria za mazingira ni wazi kuwa NEMC haitosita kuchukua hatua kali za kisheria kwa mmiliki ili iwe fundisho kwa wengine,” alisema.

Naye Meneja wa Kanda Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Venkya Masambu, alisema kwa kutambua uharibifu mkubwa unajitokeza katika maeneo ya migodini, ofisi yake kwa kushirikiana na NEMC waliamua kuchukua sampuli hizo upya ambazo watazipeleka katika maabara ya serikali yenye wataalamu waliobobea.

“Endapo sampuli zitakazopelekwa kwa Mkemia Mkuu zitabainika kuwa na madhara kwa binadamu hawatasita kutoa ushauri kwa wamiliki wa mgodi, ili kuona namna gani ya kutatua dosari zinazoweza kujitokeza,” alisema.

Mratibu wa Uendeshaji Idara ya Uchenjuaji Dhahabu wa Acacia North Mara, Patice Kabazimu, alisema wamewapokea wataalamu hao na watahakikisha wanawapatia ushirikiano wa kutosha kufanikisha kazi yao.

“Sisi kama Acacia tunatambua umuhimu wa zoezi linalofanywa na wataalamu hawa ili kuleta ustawi na maendeleo kwa jamii yetu,” alisema.

Kamati ya Bunge Yaitaka Serikali Kuzifanyia Marekebisho Sheria Ndogo Zinazokinzana na Katiba ya Nchi

0
0
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, inayoongozwa na mwanasheria mkongwe na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, imeitaka Serikali kubadilisha na kuzifanyia marekebisho baadhi ya sheria ndogo ili ziendane na sheria mama za nchi kwani nyingi zinakinzana.

Chenge akiwasilisha bungeni jana taarifa ya uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa kwenye mkutano wa 10 na 12 wa Bunge, alisema kamati yake ilibaini baadhi ya kanuni zilizotungwa na wizara zinakwenda kinyume na masharti yaliyowekwa na sheria mama au sheria nyingine za nchi.

Alitaja baadhi ya mapungufu ya kanuni hizo kuwa ni pamoja na kuweka mikokoteni.

Alisema kifungu cha 36 (1) cha Sheria ya Tafsiri ya Sheria kinasema sheria ndogo yoyote inapaswa kutokiuka masharti ya Sheria ya Bunge inayotoa mamlaka ya kutungwa kwake au sheria nyingine yoyote.

Sheria alizosema zinakinzana na sheria mama ni Sheria ya Mafuta na Gesi, Sheria ya Madini, Kanuni ya Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) na Sheria ya Mipango Miji.
 
Mipango Miji

Akizungumzia sheria hiyo, Chenge alisema ina masharti yanayokinzana na sheria mama ambapo katika kanuni ya 3 inayotoa tafsiri ya neno ‘vehicle’ ikihusisha vitu kama mkokoteni wa kuvutwa na ng’ombe, baiskeli ya matairi mawili na baiskeli ya matairi matatu (guta) ambapo tafsiri hiyo ni kinyume na ile inayotolewa na Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 168.

Alisema sheria hiyo haijabainisha vifaa hivyo kuwa ni sehemu ya vyombo vya moto ambapo masuala hayo kwa namna yoyote ile hayahusiani na maudhui ya kanuni hiyo inayohusu masuala ya mipango miji.

“Kamati ilifanya uchambuzi na kubaini kanuni ya 3 inatoa tafsiri ya neno jengo kuwa inahusisha pia mabango ya matangazo na minara ya simu kinyume na tafsiri inayotolewa na sheria mama chini ya kifungu cha 2 ambayo pamoja na masuala mengine haijafafanua masuala ya mabango ya matangazo na minara ya simu,” alisema.

Mafuta
Akizungumzia sheria hiyo, Chenge alisema uchambuzi ulibaini Kanuni ya 4 (2) (b) ya kanuni hizi inampa Waziri wa Fedha jukumu la kushiriki katika majadiliano ya mikataba ya kugawana mapato katika sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia nchini.

“Kamati inaona kanuni hii imemuongezea Waziri wa Fedha majukumu mapya ambayo hayatajwi katika kifungu cha 4 cha Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi, sura ya 328.

“ Kwa mujibu wa kifungu cha 5 na 47 vya Sheria ya Petroli ya mwaka 2015, majukumu ya yanayoainishwa na kanuni husika yanapaswa kutekelezwa na Waziri wa Nishati, TPDC na PURA kwa niaba ya Serikali ambapo majukumu haya hayaingiliani na yale ya Waziri wa Fedha chini ya Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi,” alisema.

Madini
Kuhusu Sheria ya Madini, Chenge alisema kamati imebaini dosari katika kanuni ya 3 inayotoa tafsiri ya neno Kampuni ya Mzawa/Wazawa kuwa ni ile inayomilikiwa kwa asilimia 51 na Mtanzania/Watanzania na ina asilimia 80 ya Watanzania katika nafasi za watendaji wa juu.

“Tafsiri inayotolewa katika kanuni hii haipo katika Sheria ya Makampuni Sura ya 212 ambayo ndiyo sheria mama inayosimamia masuala yote ya kampuni nchini.

“Utaratibu wa kuanzisha tafsiri mpya ya maneno ni vema ukaanzia katika Sheria Mama au Sheria nyingine ya nchi ambayo ni mahsusi kwa jambo fulani, hii itasaidia kuondoa uwezekano wa kuwa na mkanganyiko wa tafsiri za maneno mbalimbali,” alisema Chenge.

Alisema katika kanuni ya sheria hiyo pia tafsiri ya neno Kampuni ya mzawa/wazawa na Benki ya Watanzania wazawa iliyotumika katika kanuni hiyo ina ukakasi.

“Pamoja na nia njema ya wizara ya Madini ya kuweka tafsiri hizo, utekelezaji wake una changamoto na unaweza ukawa na matokeo hasi kwa kampuni kama Puma Energy ambapo Serikali inamiliki asilimia 50 ya hisa zote na kwa Benki ya NBC Ltd, ambapo Serikali inamiliki asilimia 15 ya hisa zote.

“Sheria ndogo hiyo haitambui umiliki wa Serikali wa hisa katika benki ya NBC na katika Kampuni ya Puma kuwa ni umiliki wa Watanzania na hivyo kuzikosesha kampuni hizo fursa ya kushiriki kiuchumi katika sekta ya madini.

“Halikadhalika benki na taasisi za fedha nyingi zilizosajiliwa hapa nchini ambazo hazimilikiiwi na Watanzania kwa asilimia 100 au kwa hisa nyingi zitakosa fursa ya kushiriki kwenye sekta ya madini, kamati haiamini kwamba haya ndiyo yalikuwa madhumuni ya kutungwa kwa sheria hiyo,” alisema Chenge.

VIDEO: Esma Platnumz Avunja Ukimya.....Niliachana na Petit kabla ya ishu za kuchepuka na Mnyarwanda

0
0
Mdogo wake na Diamond Platnumz, Esma Platnumz amefunguka kwa kudai kwamba ameachana na aliyekuwa mume wake wa ndoa, Petit ambaye alifanikiwa kuzaa naye mtoto mmoja.

Mapema wiki hii Petit Man ambaye alizaa mtoto mmoja na Esma, aliingia kwenye kashfa nzito baada ya kusambaa mtandaoni audio ambayo anasikika akizungumza kimahaba na mwanamke anayedaiwa kuwa wakinyarwanda.

Baada ya sakata hilo, Esma amefanya interview na Wasafi TV na kueleza mengi kuhusu mahusiano yake na Petit Man.

“Kingine ambacho hawakijui mimi na Petit tuliachana muda mrefu hata zile voice note nilivyokuja kuzisikia nilicheka sana halafu akinipigia simu,” alisema Esma Platnumz.

==>>Msikilize hapo chini

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Mkurugenzi Halmashauri ya Msalala Apata Ajali

0
0
Mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala,  Simon Belege na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mibako Mabubu wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wamepanda kugonga ng’ombe katika mteremko wa Mlima Sakenke.

Viongozi hao walikuwa wakitokea mkoani Dodoma kuelekea Igunga, Tabora kuwahi kikao cha utekelezaji wa ilani ya CCM kitakachofanyika kesho Jumamosi Septemba 15, 2018.

Katika gari hilo, Mkurugenzi huyo  alikuwa pamoja na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, mweka hazina, Masatu Mnyoro na mwanasheria wake, Mashaka Mabula.

Majeruhi wa ajli hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Igunga mkani Tabora wakiendelea kupatiwa matibabu.
 
Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Bonaventura Kalumbete amesema  Belege na Mabula ndiyo waliokuwa wamelazwa lakini baada ya kuwapatia matibabu hali zao zinaendelea vizuri na wakati wowote wataruhusiwa.

Sakata la Tundu Lissu Laibuka Tena Bungeni....Serikali Yawatupia Lawama CHADEMA

0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndio wanachelewesha kukamilika kwa ripoti ya uchunguzi dhidi ya shambulio la mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.
 
Waziri Masauni ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali laMbunge wa Ubungo (CHADEMA) Saed Kubenea bungeni leo Septemba 14, ambalo lilihoji kuwa kumekuwa na matukio mengi ya kihalifu yanatokea ikiwemo kupotea na kutekwa watu, lakini serikali imekuwa ikionesha kuwalinda zaidi watu wao wa karibu na sio wanaharakati wanaoipinga serikali na kuhoji ni lini ripoti ya serikali itakamilika kuhusiana na tukio la kushambuliwa kwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Masauni amemtaka Kubenea kufuta kauli yake aliyodai kuwa ni upotoshaji kwa jamii kwani hakuna matabaka katika ulinzi wa raia na mali zao na kusema kuwa;  “Napenda kujibu swali la Kubenea lakini ningependa kumpinga na kumkosoa vikali kwa kauli yake, kwani hakuna matabaka katika kulinda na kusimamia usalama wa raia na mali zao wote na hakuna matabaka, kuhusu shambulio la Tundu Lissu chama chao hakitoi ushirikiano ikiwemo kumficha dereva ambaye ndiye shuhuda namba moja”.

Aidha Masauni ameongeza kuwa masuala ya kigaidi yanahitaji muda zaidi kukamilisha uchunguzi wake kwakuwa huhusisha taasisi nyingine za nje zaidi ya Jeshi la polisi hivyo unahitaji muda na umakini wa hali ya juu.

Suala la watu wasiojulikana limekuwa likiibua mvutano bungeni kila ifikapo zamu ya kuchangia kwa wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kuibuka kwa matukio ya utekaji na kupotea kwa watu maarufu kuanzia mwaka 2017 wakiwemo wanahabari na wasanii wa muziki.

#Tanzania ya Viwanda: Bilioni 216 Zatumika Kukamilisha Miradi ya Umeme Kanda ya Kusini

0
0
Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma
Serikali  imetumia kiasi cha shilingi bilioni 216 kukamilisha mradi wa Umeme  wa Makambako hadi Songea ikiwa ni moja ya miradi ya kimkakati yenye lengo ya kufanikisha sera ya Tanzania ya viwanda.

Akizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amesema kuwa ifikapo mwisho wa mwezi Septemba mitambo ya mradi huo itawashwa na wananchi wa mikoa ya Njombe na Ruvuma wataanza kufurahia umeme wa uhakika kutoka gridi ya taifa.

“Mradi  huu utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi kwani wataunganishiwa umeme kwa  bei nafuu ya mradi wa REA  ambayo ni  elfu 27 tu  na kuwanufaisha wateja  22,700 hali itakayowawezesha wananchi  kutumia umeme huo kwa ujenzi wa viwanda na shughuli za maendeleo katika maeneo yao” Alisisitiza Dkt. Kalemani

Akifafanua zaidi Dkt. Kalemani  amesema kuwa  kukamilika kwa mradi huo kutaokoa fedha kiasi cha Shilingi bilioni 9.1 ambazo zinatumika kununua mafuta mazito yanayotumika kwenye mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Madaba, Ludewa, Mbinga, Namtumbo na Songea Mjini.

Akielezea ujenzi wa mradi huo uliotekelezwa na Serikali ya Tanznaia kwa kuhsirikiana na Serikali ya Sweden, Waziri Kalemani amesema mradi huo umetekelezwa kwa awamu mbili. “Sehemu  ya kwanza ya mradi huu imehusisha  ujenzi wa vituo vitatu vya kupooza na kusambaza umeme mkubwa wa msongo wa KV 220 vilivyojengwa Makambako, Madaba na Songea na sehemu ya pili ilihusisha ujenzi wa miundo mbinu ya kusafirisha umeme”.

Akizungumzia mradi wa REA awamu ya tatu ambao unatarajiwa kuunganisha vijiji 5100 kwenye mtandao wa umeme Dkt. Kalemani amesema vijiji 818 tayari vimeshaunganishwa tokea kuanza kwa mradi huo mwezi Julai mwaka huu.

Aliongeza kuwa lengo la Serikali kufikisha umeme katika Vijiji 12,268  ni kutekeleza azma ya kufikisha umeme kwa kila mwananchi bila kujali anaishi mjini au kijijini ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Kwa upande wa mradi wa Kinyerezi Dkt. Kalemani amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na megawati 218 tayari zimeshaingizwa kwenye gridi ya Taifa. Megawati za umeme zilizobaki zinatarajiwa kuingizwa kwenye gridi ya taifa kabla ya mwanzo wa mwezi Oktoba.

Mbowe, Lowassa Wawasha Moto Monduli.....Awasema Baada ya Uchaguzi Mdogo Kuisha Wataibuka na Ajenda ya Katiba Mpya

0
0
Na Ahmed Mahmoud ,Arusha
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa wamesema baada ya kumalizika kwa chaguzi ndogo nchini wataibuka na ajenda ya kudai haki na uhuru sanjari na mabadiliko ya katiba mpya ambayo italinda Amani na uhuru wa watanzania.

Wamesema uhuru na haki unavunjwa licha ya Katiba ya nchi kufafanua kwa kina kuhusu mambo hayo kwani ukiona katiba inavunjwa haki haipo hivyo wanaona jambo la msingi ni katiba mpya ambayo itakuwa ajenda yao kuu kuanzia sasa..

Wametoa kauli hiyo jana Alhamisi Septemba 13, 2018 katika mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Monduli, Yonas Laizer ambapo walisema kuwa ili nchi iwe na amani ya kweli lazima Haki na Uhuru viwepo kinyume chake ni kuwepo na uvunjwaji wa wazi wa katiba.

Akizungumza katika mkutano huo Lowassa alisema mambo yanayoendelea Monduli anatamani angekuwa na nafasi na uwezo wa kugombea tena ubunge ili kusimama kupinga vitendo vya uvunjaji wa katiba.
 
“Wana Monduli  mambo yanayoendelea kwa sasa nchini  yanahitaji Katiba Mpya tena itakayotoa adhabu kwa yeyote atakayekiuka au kwenda kinyume chake ikiwemo haya ya kuwanyima wapinzani kugombea, kuongoza au kufanya siasa kwa kuwatisha, kuwateka na kuwalaghai,” alisema Lowassa.

“Natamani ningegombea tena mngeona kama haya ningeruhusu ila kwa sababu siwezi basi naombeni mpeni kura  Laizer. Nitakuwa nampa mbinu za kufanya na msikubali kuibiwa siku hiyo mkiletewa fujo wamama naombeni pigeni ukunga wa mwizi nasi tutawasaidia.”

Kwa upande wake Mbowe alisema kuzuiwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya Bunge, mikutano ya hadhara huku viongozi wa vyama vya siasa wakitishiwa ni uvunjwaji wa sheria, kwamba kwa sasa wanavuta kasi ya kuanzisha ajenda ya kutaka Katiba ya nchi kufuatwa.

“Rais anapoingia madarakani mbali na kuapa kwa kutumia kitabu cha dini yake lakini pia anaapa kulinda, kupigania na kutetea katiba ya nchi,” alisema Mbowe.

“Cha kushangaza ndio kwanza katiba inavunjwa ikiwa ni pamoja na kuzuiwa kuonyeshwa kwa vipindi vya Bunge.”

Alisema kwa sasa hata wapinzani waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu uliopita wanatishiwa, kutekwa huku wenye mioyo miepesi wakilaghaiwa kwa fedha na madaraka.

“Wananchi tunapaswa kufahamu kuwa hakuna aliye juu ya sheria, si kiongozi wala mtawala. Haki na wajibu vinapaswa kufuatwa ikiwa ni pamoja na na wananchi kugombea na kuchaguliwa bila kujali wanawakilisha chama gani wala wao ni dini gani,” alisema.

Alisema anashangazwa na kitendo cha wagombea wa CCM katika chaguzi ndogo kutumia viongozi wa Serikali kuwapigia kampeni sambamba na kutumia magari ya Serikali.

“Baada ya uchaguzi huu tutaanzisha hoja ya kupata maelezo ya chaguzi hizi ni za kisheria au za kihuni hasa mawaziri na viongozi wa Serikali kupigia kampeni wagombea wa CCM,” alisema.

“Pia wagombea wenyewe kutumia magari ya Serikali ikiwemo analotumia mgombea ubunge wa CCM Monduli (Julius Kalanga). Gari hilo ni la mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha vijijini (kutaja aina na namba zake).”

Mbunge wa Chadema Arusha Mjini, Godbless Lema amewataka wananchi kumchagua Laizer ili afichue maovu ya Kalanga ambaye alikuwa mbunge wa Monduli kwa tiketi ya Chadema kabla ya kutimkia CCM na kupitishwa kuwania tena ubunge.

Kwa upande wake Laizer amewataka wananchi wa Monduli kumchagua ili kurejesha huduma za maji za uhakika  kama ilivyokuwa miaka ya nyuma Lowassa alipokuwa mbunge wa jimbo hilo.

“Nichagueni jamani nihakikishe namuumbua  Kalanga juu ya kuwagawia wananchi wasio wa Monduli ardhi ya Monduli,” alisema Laizer.
 
Mwisho

TAKUKURU Yatangaza Zawadi Kwa Atakayesaidia Kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hanspope

0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) imewataka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Klabu ya Simba, Zacharia Hans Pope na Frankline Lauwo kujisalimisha katika ofisi zake au kituo cha polisi kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa Septemba 14, 2018 na naibu mkurugenzi mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali, John Mbungo katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amedai kuwa Hanspope alitoa taarifa za uongo kuhusu malipo ya kodi.

Amesema Zacharia kwa kushirikiana na washtakiwa wengine Evans Aveva, Geofrey Nyange 'Kaburu' walitoa maelezo ya uongo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba klabu ya Simba imenunua nyasi bandia kutoka Kampuni ya Ninah Guangzhou Trading zenye thamani ya Dola 40,577  za Marekani, maelezo ambayo yalikuwa ya uongo kwani nyasi hizo zilinunuliwa kwa dola 109,499.

Kuhusu Lauwo, Mbungo amesema alifanya kazi ya ukandarasi wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa Simba uliopo Bunju, Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa Sh249, 929,704 wakati akiwa hajasajiliwa katika Bodi ya Makandarasi Tanzania.

"Tumewatafuta kwa njia za siri na uwazi bila mafanikio. Tunawataka kuripoti kituo cha Takukuru au polisi,"amesema Mbungo.

"Mwananchi atakayefanikisha kupatikana kwa watu hawa atapatiwa zawadi.”

Uzalishaji wa Mazao ya Chakula Waimarika Nchini

0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula na upatikanaji wake nchini umeendelea kuimarika.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo mjini Dodoma alipokuwa akitoa hoja ya kuahirisha Mkutano wa 12 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutangaza kuanza kwa mkutano ujao mnamo Novemba 6 mwaka huu.

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa tathmini iliyofanyika mnamo mwezi Juni, 2018 imeonyesha kwamba uzalishaji wa mazao ya chakula katika msimu wa mwaka 2017/18 ni tani milioni 16.9 ambapo kati ya hizo tani milioni 9.5 ni mazao ya nafaka na tani milioni 7.4 ni mazao yasiyo ya nafaka.

“Kutokana na uzalishaji huo na kwa kuzingatia mahitaji ya chakula nchini ambayo ni tani milioni 13.6, kutakuwa na ziada ya tani milioni 3.3 hivyo nchi itajitosheleza kwa chakula kwa asilimia 124,”alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuwasihi wananchi kutumia akiba hiyo ya chakula kwa uangalifu kwani zipo nchi jirani ambazo zina uhaba mkubwa.

Vile vile ameziagiza taasisi zote zinazosimamia elimu ya lishe na afya kuongeza nguvu zaidi katika kutafuta mbinu bora na kutoa elimu kwa wananchi ili kupunguza kiwango udumavu na utapiamlo hususan kwa watoto wadogo.

Akizungumza kuhusu upatikanaji wa pembejeo za kilimo nchini, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa pembejeo muhimu za kilimo kwa wakati ambapo katika msimu wa kilimo wa mwaka 2018/19 upatikanaji wa mbolea aina zote umefikia kiasi cha tani 215,207 wakati matarajio ya matumizi ya mbolea hiyo ni tani 485,000.

Aidha, Serikali itahakikisha upatikanaji na matumizi sahihi ya viuatilifu kwa mazao mbalimbali na kwamba kwa msimu wa mwaka 2018/19 Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 10  kwa ajili ya kupambana na wanyama pamoja na wadudu waharibifu.

Waziri Mkuu Ampongeza Mwakinyo Kwa Kumchapa Muingereza

0
0
WAZIRI MKUUKassim Majaliwa amempongeza mwanamasumbwi wa Kitanzania Bw. Hassan Mwakinyo (23) kwa kumchapa bkondia Mwingereza Bw. Sam Egginton.

Bw. Mwakinyo alimchapa Bw Egginton kwenye raundi ya pili ya pambano lao la masumbwi lililofanyika Jumapili, Septemba 9, 2018, huko  Birmingham nchini Uingereza.

Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo leo (Ijumaa, Septemba 14, 2018) wakati akiahirisha mkutano wa 12 wa Bunge, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Novemba 6, 2018.

Amesema bondia huyo amelipa Taifa heshima kubwa kwa kulitangaza kimataifa katika Nyanja ya michezo, hivyo amewataka wanamichezo wengine nchini waige mfano wake.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu  ameipongeza timu ya Taifa ya Wanawake (Kilimanjaro Queens) kwa kutwaa kombe la Afrika Mashariki.

Pia ameipongeza timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kwa kuwa washindi wa tatu kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kwenye mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). 

“Hongereni sana wanamichezo wetu na endelezeni moyo huo wa kizalendo mliouonesha katika kulitangaza Taifa letu.

Pia Waziri Mkuu amesema mwaka 2019 Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano ya mpira wa miguu kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON-U17) yanayoandaliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika.

Amesema hiyo ni fursa nyingine ya kipekee ya kulitangaza Taifa letu katika nyanja za Kimataifa, hivyo Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea na maandalizi, ambayo yatahusisha ukarabati wa viwanja vitakavyotumika katika mashindano hayo.

Waziri Mkuu ametoa wito kwa wananchi watumie vizuri uwepo wa mashindano hayo kujiongezea kipato hususan kupitia biashara ya bidhaa na huduma kwa wageni, pia amewataka wawe wazalendo kwa kuunga mkono timu zinazoshiriki mashindano ya Kimataifa ili zipate mafanikio.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri : Uwekezaji Wa Mshahara Ni Jukumu La Mfanyakazi

0
0
Serikali imeeleza kuwa uwekezaji wa mishahara kwa wafanyakazi nchini ni jukumu la mfanyakazi mwenyewe kwa kuwa mshahara ni mali ya mfanyakazi hivyo anaweza kuutumia kwa kuwekeza au kuto kuwekeza.

Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu maswali ya Mbunge wa Viti maalum Mhe. Mwantum Dau Haji, aliyetaka kujua Serikali inasema nini kuhusu uwekezaji wa mishahara kwa watumishi wa umma na kuwepo kwa ucheleweshaji wa mishahara kwa Watumishi wa Umma..

Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali kwa upande wake inawalipa mishahara wafanyakazi wake kwa wakati kwa kuzingatia waraka wa Hazina namba 12 wa mwaka 2004 ambao unaitaka Serikali kulipa mishahara kabla ya tarehe 25 ya kila mwezi.

“Kumbukumbu za malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma zinaonesha kuwa, kuanzia Julai 2017 hadi Agosti 2018, watumishi walilipwa mishahara yao kati ya tarehe 20 na 24 ya kila mwezi hivyo napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu na umma kwa ujumla kuwa hakuna ucheleweshaji wa malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma” alieleza Dkt. Kijaji.

Aidha Serikali imekuwa ikiwatendea haki wafanyakazi wake katika upandishaji wa madaraja na kila mwaka wafanyakazi hupandishwa madaraja.

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango.

Waziri Mkuu: Miaka Mitatu Ya Rais Magufuli Imeongeza Ari Ya Kufanya Kazi

0
0
*Ameimarisha nidhamu, uadilifu kwenye utumishi wa umma

*Ameboresha miundombinu ya reli, barabara, nishati, elimu na afya

WAZIRI MKUUKassim Majaliwa amesema Rais Dkt. John Magufuli katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake, amefanikiwa kuimarisha nidhamu, uadilifu na uwajibikaji ndani ya utumishi wa umma pamoja, kukemea uzembe na kujenga ari ya kufanya kazi.
 
Mafanikio mengine ni ununuzi wa meli katika ziwa Nyasa, Tanganyika na Victoria pamoja na kufufua Shirika la Ndege la Tanzania ili kuimarisha usafiri wa anga na kukuza sekta mtambuka zikiwemo za utalii, afya, kilimo na kujenga reli ya kiwango cha kimataifa (SGR).

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Septemba 14, 2018) wakati akiahirisha mkutano wa 12 wa Bunge, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Novema 6, 2018.

Amesema mafanikio mengine yaliyofikiwa katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dkt. Magufuli ni kuendesha vita dhidi ya rushwa na ufisadi kwenye taasisi za umma sambamba na kuanzisha Mahakama ya Mafisadi na kuimarisha ulinzi wa rasilimali za nchi ikiwemo madini na maliasili.

“Kujenga vyanzo vipya vya umeme kama vile mradi wa kuzalisha umeme wa maji megawati 2,100 katika bonde la mto Rufiji (Stiegler’s Gorge), kusambaza umeme hadi vijijini sambamba na kuongeza kasi ya utekelezaji wa  miradi ya awamu ya tatu ya mpango wa REA ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania).”

Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Magufuli ameimarisha huduma za afya hususan upatikanaji wa dawa, vifaatiba katika vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya na utoaji Elimumsingi Bila Malipo kwa watoto wa Kitanzania.

Pia amehakikisha miradi yote ya maji inayotekelezwa inakuwa bora, yenye uwiano na thamani halisi ya fedha pamoja na kukamilishwa kwa wakati na kuimarisha kilimo, ushirika na bei za mazao ya biashara.

Waziri Mkuu amesema juhudi zote hizo zinafanywa kwa lengo la kuiwezesha nchi kufikia malengo ya dira ya Taifa ya kuwa na uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025. “Niwaombe Watanzania wenzangu tuendelee kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais katika kuleta maendeleo.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wawekezaji kutumia fursa ya uwepo wa mazingira mazuri ya uwekezaji nchini, biashara na upatikanaji wa malighafi kwa kuja kujenga viwanda mbalimbali hususan vya kuchakata mazao ya kilimo.

 IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

John Guninita kuzikwa Jumatano Septemba 19

0
0
Mwili wa Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita unatarajiwa kuzikwa Jumatano Septemba 19, 2018 kijijini kwao Kibaoni, Ifakara mkoani Morogoro.

Guninita ambaye jina lake linabaki katika orodha ya wanasiasa wenye uwezo wa kutenda kile wanachoamini alifariki dunia jana Septemba 13, 2018 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mdogo wa marehemu,  Gerald Guninita amesema mwili wa kaka yake utachukuliwa MNH Jumanne  asubuhi, misa ya mazishi itakayofanyika nyumbani kwake Tabata Kimanga.

Amesema, awali Guninita alikuwa anasumbuliwa na kwiwi, kiungulia na baada ya vipimo alibainika kuwa na uvimbe tumboni.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Septemba 15

Msigwa amshukuru Rais Magufuli

0
0
Baada ya shirika la Umeme nchini (TANESCO),  kuwasha kituo kipya cha kupoza na kusambaza umeme cha Madaba mkoani Ruvuma,  Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa amemshukuru Rais Dk. John Magufuli.

Msigwa ametoa shukrani hizo kwa niaba ya wana Ruvuma ambao ameeleza ni wazee wake kwa sababu ni mkwe wao, akibainisha kuwa adha waliyokuwa wanaipata sasa imebaki historia, kutokana na kuwa na umeme wa uhakika tofauti na zamani ilivyokuwa ambapo walikuwa wanategemea umeme wa jenereta.

"USENGWILI SANA LIDODA" Kwa tunaojua adha ambayo Songea na Mkoa mzima wa Ruvuma umepata kwa miaka mingi kutokana na tatizo la umeme, kuna kila sababu ya kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuhakikisha mradi wa kujenga njia ya umeme ya 220KV uliogharimu shilingi Bilioni 216 unakamilika. Sasa Songea imeunganishwa na gridi ya Taifa na inapata umeme wa uhakika kuliko enzi ya majenereta ambayo yalikuwa yanaelemewa mpaka yanapasuka kama ukuta wa nyumba. Kwa niaba ya Wazee wangu wa Songea, Wakwe zangu na Shemeji zangu nasema USENGWILI SANA LIDODA (Mhe. Rais), NA CHILAU MEWAWA. @ikulu_mawasiliano" Ameandika Msigwa

TANESCO ilifanikiwa kuwasha mitambo ya kituo hicho cha Madaba iliyoanza kujengwa mwaka 2017 usiku wa Septemba 13, 2018. Kituo hicho kitasambaza umeme wa kilovolti 220/33kv.

Baada ya kukamilika kwa mradi huo inakadiliwa wakazi wa maeneo hayo hususani yale ya vijiji vya karibu, wataunganishiwa huduma ya umeme kwa gharama nafuu sana kwa kiasi kisichozidi shilingi 27,000.

Mambosasa Atoa Onyo Kwa Waliojipanga Kulinda Kura Kesho

0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya  Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, amevitahadharisha vikundi vya vijana ambavyo vinatumika kisiasa kutaka kuvunja amani kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo la Ukonga kwa kisingizio cha kulinda kura.

Akiongea jana kwenye mkutano na wanahabari, Mambosasa alisema, jeshi lake limejipanga vyema kuhakikisha uchaguzi huo unaanza na kumalizika salama huku mshindi akitarajiwa kupatikana kwa ushindi wa kura na si vinginevyo.

''Kuna vitendo vimekuwa vikijitokeza kwenye chaguzi, ambapo vikundi vya vijana vinajiita walinda kura, kitu ambacho ni kinyume na sheria hivyo watakaofanya hivyo kwenye uchaguzi wa Ukonga wataishia kwenye mikono ya dola'', alisema.

Mambosasa alisema watahakikisha usalama wa zoezi zima kuanzia kusambazwa kwa vifaa vya kupigia kura katika vituo vyote hadi kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi huo unaofanyika Jumapili Septemba 16, 2018.

Katika uchaguzi huo wagombea wa vyama vya CHADEMA na CCM, wanachuana vikali ambapo CCM inawakilishwa na Mwita Waitara huku CHADEMA wakiwakilishwa na Asia Msangi.

Mbali na hilo Mambosasa ameibanisha jeshi hilo limefanikiwa kukamata watuhumiwa 8 akiwemo mwanamke mmoja, wanaodaiwa kuendesha vitendo vya uporaji wa Bajaj katika eneo la Mvuti Gongo la mboto jijini Dar es salaam.

Waziri Mkuu: Serikali Kuachana Na Uagizaji Mafuta Ya Kula

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuimarisha kilimo cha mbegu za mafuta iliTanzania iachane na uagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje.

Amesema malengo ya kampeni hiyo ni kuhakikisha kuwa mkoa wa Kigoma na maeneo mengine yenye fursa ya kulima zao la chikichi yanaimarisha kilimo hicho. “Hivi sasa, nchi yetu inatumia takribani Dola za Marekani milioni 294 kila mwaka kwa ajili ya kuagiza mafuta hayo.”

Ametoa kauli hiyo jana (Ijumaa, Septemba 14, 2018) katika hotuba yake aliyoitoa wakati wa kuahirisha Mkutano wa 12 wa Bunge jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Novemba 6, mwaka huu.

Amesema sambamba na azma ya Serikali ya kuweka mkazo katika kusimamia uzalishaji na masoko ya mazao makuu matano ya biashara ambayo ni pamba, kahawa, korosho, chai na tumbaku, Serikali imedhamiria pia kupanua wigo kwenye mazao mengine muhimu ikiwemo chikichi, alizeti na ufuta ili kukidhi uzalishaji wa mbegu za mafuta nchini.

 “Katika kutekeleza azma ya Serikali, kuhusu kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula nchini, tarehe 28 Agosti, 2018 nikiwa mkoani Kigoma nilizindua kampeni maalumu ya kuendeleza zao la chikichi ambalo kwa sasa linatambulika kama zao kuu la sita la kipaumbele,” amesema.

Amesema ili kuhakikisha nchi inajitosheleza kwa mahitaji ya mafuta ya kula, Serikali imeweka mikakati ya kuendeleza zao la chikichi kwa kuanzisha kituo cha utafiti wa zao la chikichi katika eneo la Kihinga, mkoani Kigoma.

“Serikali imeandaa mpango mkakati wa uzalishaji wa miche bora ya chikichi milioni 20 ifikapo mwaka 2021. Kwa kuanzia, mwaka 2018/2019, Serikali inakusudia kuzalisha miche bora ya chikichi milioni 10 ambayo itasambazwa kwa wakulima,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali pia imeandaa mpango mkakati wa miaka mitano wa utafiti wa mbegu bora ili kuongeza tija kutoka tani 1.6 hadi kufikia tani 4.0 za matunda ya chikichi kwa hekta kwa mwaka.

Amesema Serikali imeweka mazingira mazuri ya kuvutia uwekezaji na matumizi ya teknolojia ya kisasa kwa ajili ya uchakataji zao la chikichi na imepanga kusimamia vituo vikuu vya uzalishaji vya gereza la Kwitanga, Ilagala na JKT Bulombora.

Amewataka Watanzania wachangamkie fursa ya kilimo cha zao la chikichi ili nchi iweze kujitosheleza kwa mafuta ya kula na ziada kuuza nje. “Nitoe rai pia kwa wawekezaji, waje  kuanzisha viwanda vya kuchakata chikichi na mazao yake,” amesisitiza.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali kwa upande wake, inaimarisha taratibu za uingizaji wa sukari na mafuta ya kula kwa kuweka madaraja na usimamizi makini.

Ameitaka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo wakamilisha jukumu hilo kwa wakati.

“Pia, naagiza vyombo vya dola viongeze ushirikiano na mamlaka husika ambazo ni TRA, TFDA, Bodi ya Sukari na TBS ili kudhibiti uingizaji holela wa sukari na mafuta ya kula ikiwa ni pamoja na kuziba mianya ya magendo,” amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images