Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waliokutwa na madini kinyume na sheria Wahukumiwa Miaka mitatu Jela au faini milioni 24

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu miaka mitatu jela ama kulipa faini ya Sh. 24 milioni wafanyabiashara wawili wa madini baada ya kukiri kosa la kukutwa na madini ya Coloured Gemstones yenye thamani ya Dola za Kimarekani 1.8 milioni.

Pia mahakama hiyo imeamuru madini hayo yataifishwe. Hata hivyo, washtakiwa hao wameweza kuepuka kutumikia kifungo hicho baada ya kulipa faini hiyo.

Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwizire baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande kuwasomea mashtaka mawili washtakiwa hao ambapo walikiri makosa yao.

Baada ya kukiri makosa yao, Mahakama iliradhimika kuhamia maeneo ya Msasani Kinondoni Dar es Salaam ambapo vielelezo vya kesi hiyo vilikuwepo, ambapo kesi iliendeshwa na washtakiwa kutiwa hatiani. Washitakiwa hao ni Aazam Nazim (Raia wa India) na Ango Mbossa raia wa Tanzania.

Hakimu Rwizire hivyo alimtaka kila mshtakiwa kulipa faini ya Sh. 6 milioni kwa kila kosa ama kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela katika kila kosa.

Kwa kuwa kila mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili hivyo kila mshtakiwa atapaswa kutoa faini ya Sh. 12 milioni iwapo atashindwa atatumikia kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuwa vifungo hivyo vinaenda sambamba.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda makosa yao kati ya January 2017 na June 2018 katika maeneo ya Misisiri A eneo la Mwananyamala.

Wanadaiwa kukutwa na madini aina ya Coloured Gemstones kilogramu 75,920.04 yenye thamani ya Dola za Kimarekani 1,795,687.87.

Mwita Waitara: Nilikataa Kuwa Kenge Ndo Maana Nikahamia CCM

$
0
0
Mgombea ubunge Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara amesema amekataa kuwa kenge kwenye safari ya mamba ya Chadema.

Waitara alisema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Bombambili eneo la Kivule kwenye kampeni ya kuomba ridhaa ya kuongoza tena Jimbo la Ukonga.

Alisema baadhi ya viongozi wa Chadema akiwamo Freeman Mbowe, kwenye majimbo yao kuna huduma muhimu ilihali yeye kwake kuna shida ya maji, umeme, barabara ndiyo maana hawaoni shida kuwakataza wenye majimbo yenye hali mbaya kama lake kuonana na mawaziri wenye dhamana.

“Mbowe jimboni kwake Hai kuna umeme hadi migombani, Mbeya kwa Sugu kuna halikadhalika, nikitaka kuonana na mawaziri ambao nitashirikiana nao nakatazwa.

“Waswahili wanasema kwenye safari ya mamba na kenge wamo, nimekataa kuwa kenge kwenye safari ya Chadema kwa sababu mimi najua Bombambili kuna shida ya barabara, maji na umeme. Naonekana ni mbunge nisiyefanya kazi, jimbo langu lina changamoto nyingi nimejiongeza,” alisisiza Witara.

Kwa mujibu wa Waitara, amefuata mafunzo ya wahenga yasemayo akili za kuambiwa changanya na zako, hivyo ameamua kuzichanganya na kuamua kuhama.

Alifafanua kuwa amejiridhisha bila shaka kuwa kwa siku za hivi karibuni kwa uongozi wa Mbowe hadhani kama atashika dola.

Alisema kwa mchezaji wa mpira siku zote ana mawazo ya kucheza timu itakayokuwa bingwa; “kwa upinzani huu utasubiri sana, nimeamua nijiunge na timu inayocheza ligi kuu nimeachana na wale wa mchangani,” alisema Waitara.

Waitara alidai kuwa hata aliposhinda jimbo hilo ni juhudi zake binafsi na wananchi wa Ukonga na siyo Chadema.

Alisema aligombea akiwa kama yatima alikusanya michango mwenyewe, kampeni meneja mwenyewe na hakuna hata mmoja kutoka Chadema aliyemsaidia.

“Tumalizeni hili la ubunge halafu tutakuja kuzungumza la udiwani, kwani tunataka kuwang’oa wote waliobaki ili tuongee lugha moja kwa ajili ya maendeleo ya wana-Ukonga, ” alisema Waitara.

Alisema hataki kujibizana na Chadema kwa mambo wanayosema kwenye mikutano yao, lakini kama yupo anayetaka kuona vyeti vyake yupo tayari kuvionyesha hadharani na kwamba viongozi wa chama hicho wameamua kusema uongo.

TANZIA: John Guninita wa CCM afariki dunia

$
0
0
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), mkoa wa Dar es Salaam John Guninita amefariki dunia.

Taarifa zinabainisha kuwa Guninita ambaye ameshawahi kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM), alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mdogo wake na marehemu, Gerald Guninita ambaye naye aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo wakati wa Uongozi wa Awamu ya Nne.

Miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015, Guninita alikuwa miongoni mwa makada wa CCM waliojiunga Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kupewa cheo cha meneja wa kampeni.

Hata hivyo, mapema mwaka huu, marehemu Guninita aliripotiwa kurudi CCM huku akiomba radhi kwa hatua yake ya kukihama chama alichokitumikia kwa muda mrefu.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Barua ya Saed Kubenea Kujiuzulu CHADEMA Yaibua Mjadala

$
0
0
Barua  ya Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), kuomba kujiuzulu imezua mjadala mzito ndani ya chama hicho.

Kubenea anadaiwa kuandika barua kuomba kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, jambo ambalo linaonekana kuleta mgongano na kurushiana mpira.

Wakati mjadala huo ukishika kasi hadi sasa mbunge huyo hajakubali wala kukataa kuhusu barua hiyo aliyomwandikia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vicent Mashinji ambaye anasema pindi itakapomfikia ataifanyia kazi haraka.

Barua hiyo ya Agosti 28 mwaka huu ilianza kusambaa mitandaoni juzi, ambapo Kubenea alikuwa akitoa utetezi wake kutokana na kuandikiwa barua na na Katibu Mkuu wa chama hicho akitakiwa kujieleza kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kusababisha migogoro kupitia mitandao ya kijamii.

Katika barua hiyo yenye kumbukumbu MB/U/CDM/018/1  kwenda Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Kubenea alitakiwa kujibu tuhuma tano dhidi yake.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Dk. Mashinji alikiri kuona barua ya mbunge huyo kupitia mitandao ya kijamii, huku akiweka wazi kwamba pindi itakapomfikia ataifanyia kazi kwa haraka.

“Barua hiyo kama ambavyo umesema mwandishi ipo mitandaoni mimi bado sijaiona na kama nikiiona nitaifanyia kazi,’’alisema Dk. Mashinji.

Katika kile kinachooneka kuwa ni kukosekana kwa ufafanuzi wa kina Kubenea alikiri kupokea barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa chama hicho ikimtaka kujieleza  kutokana na kikao cha Kamati Kuu (CC) iliyokutana Julai 7 na 8 mwaka huu.

Katika sehemu ya majibu ya Kubenea kwa Katibu Mkuu alieleza kukiri kupokea barua iliyoelekezwa kwake  Julai 19  mwaka huu 2018 yenye Kumb. Na. C/HQ/K/PWN/MG/30/8, kuhusu “KUJIELEZA KWA KATIBU MKUU”

Sekta ya mifugo Kuchangia Asilimia 9 ya Pato la Taifa

$
0
0
Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza mpango mkakati wa kuendeleza sekta ya mifugo unaotarajiwa kuongeza mchango wa sekta hiyo kwenye pato la Taifa kutoka asilimia 6.9 hadi 9%.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Abdallah Ulega amesema bungeni jijini Dodoma kuwa, utekelezaji wa mkakati huo pia unatarajiwa kukuza sekta ya mifugo kutoka asilimia 2.8 hadi 5.2%.

Wakati anajibu swali la Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvester Koka, Ulega amesema, mkakati huo una lengo la kupunguza na kuboresha mazingira rafiki na endelevu katika uzalishaji mifugo yenye tija kwa kuzalisha mitamba milioni moja kwa mwaka.

Wabunge wameelezwa kuwa mitamba hiyo itapatikana kutoka makundi ya ng'ombe wa asili kwa kufanya uhimilishaji. Koka alitaka kufahamu Serikali ina mpango gani kuboresha bidhaa za nyama nchini pamoja na mazao mengine yatokanayo na mifugo.

Ulega amesema, mkakati wa kuendeleza sekta ya mifugo utaimarisha upatikanaji wa uhakika wa maji, malisho na vyakula bora vya mifugo, utahamasisha matumizi ya teknolojia za ufugaji wa kisasa, utaboresha afya, masoko, biashara na kuongeza thamani ya mazao ya mifugo.

Amesema, mkakati huo utaongeza uzalishaji mazao ya mifugo ikiwemo idadi ya ng'ombe wa maziwa kutoka 789,000 hadi milioni tatu, utaongeza uzalishaji maziwa kutoka lita bilioni 2.4 hadi lita bilioni 3.8 kwa mwaka.

Kwa mujibu wa Ulega, mkakati huo pia utaongeza uzalishaji wa nyama kutoka tani 679,992 hadi tani 882,100, utaongeza uzalishaji ngozi za ng'ombe, mbuzi na kondoo kutoka futi za mraba milioni 89 hadi futi za mraba milioni 98.9 na utaongeza uzalishaji mayai kutoka mayai bilioni 3.2 hadi mayai bilioni 6.4.

"Pia, mkakati unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa huduma za ugani, kuongeza uzalishaji wa chanjo za mifugo zinazozalishwa hapa nchini, kuongeza usindikaji wa mazao ya mifugo, pamoja na kuongeza usambazaji wa teknolojia za ufugaji bora ili kufikia wafugaji wengi zaidi"amesema Ulega.

Kangi Lugola Ashangaa Wananchi Kuchoma Moto Kituo Cha Polisi Mtu Akifia Humo Lakini Hawachomi Kitanda Mtu Akifa Anafanya Mapenzi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema, si watu wote wanaopoteza maisha katika vituo vya polisi wanakuwa wameteswa.

Waziri Lugola pia amehoji, kwani nini mtu akipoteza maisha akiwa kituo cha polisi wananchi wanavamia kituo lakini hawachomi nyumba na kitanda mwananchi anapoaga dunia wakati anafanya mapenzi.

Ameyasema hayo bungeni wakati anajibu maswali ya nyongeza  ya wabunge kwenye kikao cha nane cha Mkutano wa 12 wa Bunge unaoendelea jijini Dodoma. 

Lugola amesema, mwananchi anaweza kupoteza maisha wakati wowote na mahalali popote na ndiyo maana kwenye Biblia imeandikwa kifo ni mtego, humnasa mtu wakati wowote na mahali popote.

"Kwa hiyo mwananchi anaweza akafa akiwa polisi, anaweza akafa akiwa anafanya mapenzi, anaweza akafa akiwa kwenye gari anasafiri, anaweza akafia hata humu ndani ya Bunge humu. Kwa hiyo isije ikachukuliwa kwamba anayekufia kwenye kituo cha polisi ni kwamba ameteswa" amesema.

Hata hivyo Waziri Lugola amekiri kuwepo kwa matukio ya wananchi kufia mikononi mwa Polisi.

"Na pale ambapo matukio hayo yanajitokeza tumekuwa tukifanya uchunguzi. Na pale inapobainika kwamba Polisi wamehusika tumekuwa tukichukua hatua. Na ndiyo maana Mheshimiwa Spika tunazuia wananchi wasichukue sheria mikononi za kuanza kuvamia vituo kwa sababu mtu amefia mikononi mwa polisi...

"Na ndiyo maana nimekuwa nikihoji, huyu anayekufa akifanya mapenzi mbona hawaendi kuchoma kitanda na nyumba kwamba amefia mikoni mwa kitanda"amesema Lugola.

Wakati anajibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mlimba, Suzan Kiwanga, Waziri Lugola amesema, Jeshi la Polisi halina nia ya kuwatesa wananchi wanapokamatwa na kuwekwa mahabusu.

Mbunge huyo alitaka kufahamu kauli ya Waziri Lugola kuhusu mahabusu kukosa chakula.

"Mahabusu wote wanapata chakula na wapo watu ambao wanapewa tenda hizi za kuleta vyakula kwa mahabusu"amesema na kuongeza kuwa, kuna wananchi wanaoruhusiwa kupeleka vyakula kwa mahabusu.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Makamu wa Rais Kumwakilisha Rais Magufuli tamasha la urithi Dodoma

$
0
0
Makamu wa Rais Samia Suluhu atakuwa mgeni rasmi katika uzunduzi wa tamasha la urithi litakalofanyika kati ya Septemba 15 hadi 22 mwaka huu jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 13 2018, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk Binilith Mahenge amesema kuwa Samia atamwakilisha Rais John Magufuli ambaye ndiye awali alikuwa awe mgeni rasmi.

Amesema maonyesho lengo la tamasha hilo ni kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini hususani kwa kuendeleza mazao ya utalii, utamaduni na malikale.

“Kauli mbiu ya maonyesho haya ni ‘Urithi wetu Fahari yetu’ na yatahusisha wadau kuonyesha mambo ya burudani, maigizo, utalii na tamaduni, malikale na kazi mbalimbali za mikoa,”amesema.

Amesema kutakuwa na maandamano yenye shamrashamra za ngoma, machifu, watalii, washahiri, maigizo, wasanii mbalimbali wa ndani na nje ya nchi akiwemo Mrisho Mpoto na Wanne Star.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Serikali Kuwezesha Vituo Vya Utafiti Ili Kuongeza Uzalishaji Wa Aina Mpya Wa Mbegu Bora

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Arusha
Serikali imeahidi kuendelea kuwezesha vituo vyake vya utafiti kote nchini kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa aina mpya za mbegu bora za mazao mbali mbali.

Kauli hiyo imetolewa na Mhe Dkt Charles Tizeba Waziri wa Kilimo, wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau wa mbegu ambapo ni mjumuiko wa Jumuiya ya Wafanyabiashara ya Mbegu (TASTA), TOSCI, USAID East Africa Trade Investment Hub, AGRA-MIRA Project, AATF, ASA na TPRI kwa kushirikiana na wizara ya Kilimo na wadau wengine wa maendeleo unaofanyika katika Ukumbi wa Mount Meru Hotel Jijini Arusha.

Alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa Wizara ya kilimo inafikia hatua ya kuwa na uzalishaji Wa aina mpya za mbegu bora za Mazao mbalimbali tayari serikali imechukua hatua ya kuanzisha Taasisi ya Utafiti Wa kilimo - TARI kwa lengo la kuboresha utendaji wa kitafiti ili kuleta tija katika ugunduzi wa aina mpya za mbegu.

Alisema kuwa TARI itasaidia kuongeza uzalishaji wa mbegu bora hapa nchini na hivyo kuwa na matokeo chanya ya uhakika wa chakula katika ngazi ya kaya na Taifa kwa ujumla pia kuongeza kipato kutokana na ziada.

Dkt Tizeba alisema kuwa Mpango wa Kuendeleza sekta ya Kilimo awamu ya pili – ASDP II ambao Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ameuzindua hivi karibuni unasisitiza masuala ya uendelezaji wa kilimo chenye tija, Kilimo biashara chenye kuboresha mapato ya mkulima na kilimo  kinachomhakikishia mkulima usalama wa chakula na lishe.

"Haiwezi kuwa rahisi kuongeza uzalishaji wa kilimo hapa nchini kama msingi wa kilimo ambao ni uzalishaji wa mbegu bado tutakuwa tumeuacha nyuma pasina kuweka msisitizo hapo, hivyo tunapaswa kutazama upya namna bora ya kupunguza gharama ya mbegu" Alikaririwa Mhe Dkt Tizeba na kuongeza kuwa

"Baada ya serikali kujitoa katika uendeshaji wa biashara mbalimbali na kuruhusu sekta binafsi kufanya biashara, hii ilitoa fursa kwa sekta binafsi kushiriki katika tasnia mbalimbali ikiwemo hii ya mbegu, lengo kuu la dhana hii ya ushirikishaji wa sekta binafsi na ile ya umma (PPP) ni kuwezesha na kuhakikisha kwamba maslahi mapana ya wakulima yanalindwa na mazingira ya biashara yanaboreshwa ili wakulima na sekta binafsi wote wafaidike na jitihada wanazozifanya"

Waziri Tizeba aliongeza kuwa Ili kutekeleza lengo la kuongeza tija na uzalishaji katika sekta ya mbegu, Wizara ya Kilimo kupitia Sheria ya Mbegu ya Mwaka 2003, imeweka mifumo mbalimbali ya namna ya kutoa na kufikisha huduma kwa wakulima kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa lengo la kuboresha huduma hizo ili kuongeza kasi ya ukuaji wa maendeleo ya wakulima.

Alizitaja jitihada hizo kuwa ni katika kutekeleza majukumu ya pamoja katika ubia baina ya sekta ya umma na ile ya binafsi. "Lakini kwa bahati mbaya juhudi hizi hazijazaa matunda yaliyotarajiwa na ndiyo maana mpaka sasa bado tunakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uzalishaji mdogo wa mbegu, uwepo wa mbegu zisizokidhi viwango vya ubora sokoni na kutegemea mbegu za kuagizwa kutoka nje. Hali hii tunatakiwa kuondokana nayo na kuhakikisha tunazalisha mbegu za kutosha mahitaji ya ndani na ziada kuuza nje" Alisistiza Dkt Tizeba

Aidha, alidema juhudi mbalimbali zinaendelea kufanyika kati ya Serikali na Sekta binafsi katika kupambana na uwepo wa mbegu zisizokidhi viwango vya ubora sokoni. Miongoni mwa juhudi hizo ni kuweka karatasi yenye maelezo na utambulisho ‘label’’ katika vifungashio vya mbegu. "Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria ya Mbegu ya mwaka 2003 ambapo utekelezaji wake umekuwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na malalamiko ya wafanyabiashara kudai kuwa hizo ‘lebel’ zinaongeza gharama. Hivyo napenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha wadau wote wa sekta ya mbegu kuwa hilo ni takwa la kisheria hivyo ni budi sote tulizingatie" Alisema

MWISHO.

Mgombea CHADEMA Ukonga ahofia kutekwa

$
0
0
Mgombea ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam Asia Msangi amesema miongoni mwa changamoto anazokutana nazo kuelekea uchaguzi wa marudio jimbo hilo utakaofanyika siku ya jumapili ya  septemba 16, ni hofu ya kutekwa na watu wasiojulikana.

Akizungumza katika kituo cha EATV leo, mgombea huyo wa CHADEMA amesema kupitia viongozi wa juu wa chama chake wamepokea taarifa juu ya uvumi wa kutaka kutekwa siku moja kabla ya zoezi la kupiga kura.

“…Baadhi ya changamoto kwenye uchaguzi huu wa marudio ninazokutana nazo .., kuna baadhi ya watu wetu wanatishiwa kutekwa na kuna mwingine alitekwa ila kwa ushirikiano na mwenyekiti jana amepatikana.., lakini pia kupitia viongozi wa juu wa chama tumepokea taarifa ya mimi kutaka kutekwa kabla ya jumamosi na hili jambo tutalifikisha polisi. ” Amesema Asia Msangi

Aidha Asia Msangi amesema licha ya  miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia seikali ya awamu ya tano ikiwemo reli ya kisasa (SGR), ununuaji wa ndege pamoja na Shirika la ndege la Tanzania ATCL anaamini miradi hiyo haiwezi kuwa kikwazo cha kutoshinda uchaguzi wa jimbo hilo.

“ Licha ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Rais Magufuli bado maisha ya mwananchi mmoja mmoja wa jimbo la ukonga ni magumu.., hiyo miradi haiakisi chochote.., wananchi wa ukonga hawawezi kunufaika..”Ameongeza Asia Msangi

Uchaguzi wa jimbo la Ukonga unarudiwa kufuatia aliyekua Mbunge wa jimbo hilo kupitia CHADEMA Mwita Waitara kutangaza kujivua nafasi hiyo Julai 28 mwaka huu kwa madai ya kuwa na mgogoro na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe.

Taratibu Mpya za Kusimamia Uagizaji wa Sukari Kukamilika Oktoba

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Serikali imepanga kukamilisha utaratibu mpya wa kuagiza sukari nchini ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu. Utaratibu huo mpya unatagemewa kuwa mwarobaini wa kukomesha mrundikano wa sukari kwenye viwanda vya sukari nchini.

Hakikisho hilo limetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mheshimiwa Charles Mwijage wakati akiwasilisha taarifa ya hali ya sukari nchini.

Waziri Mwijage ameliambia bunge kuwa sukari inayozalishwa nchini haikidhi mahitaji na kwa mwaka 2018/19 uzalishaji unakadiriwa kufikia tani 353,651 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na hakuna kiwanda kinachozalisha sukari kwa ajili ya matumizi ya viwandani.

Upungufu huo wa sukari inayozalishwa nchini umesababisha nakisi ya sukari takribani tani 316,349,  tani 161,349 zikiwa za matumizi ya kawaida na tani 155,000 kwa ajili ya matumizi ya viwandani.

“Hadi kufikia Septemba 5, 2018, viwanda vyetu vilizalisha jumla ya tani 119,671.19 ambazo ni sawa na asilimia 33.84 ya malengo ya uzalishaji wa sukari kwa mwaka huu hivyo kiasi cha sukari kilichopo nchini kinatosheleza mahitaji ya sukari kwa kipindi cha miezi mitatu mbali na uzalishaji unaoendelea” alisema Mhe. Mwijage.

kulipatia ufumbuzi tatizo hilo Waziri Mwijage amesema Serikali imeshatoa maelekezo kwa wamiliki wa viwanda vya sukari nchini kuwasilisha mapendekezo kuboresha mfumo wa usambazaji ili kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa hiyo muhimu unakuwa wa uhakika na bei nafuu.

Akiongea kuhusu bei na upatikanaji wa sukari, Waziri Mwijage amesema tathmini ya miezi sita  kuanzia mwezi Machi hadi Agosti, 2018 inaonyesha hali ya upatikanaji wa bidhaa hiyo ni mzuri na bei yake imekuwa ikitengemaa. Kwenye tathmini hiyo ongezeko  la bei limekuwa kati ya shilingi 50 hadi shilingi 150.

Mahitaji ya sukari nchini kwa mwaka yanakadiriwa kuwa tani 670,000 ambapo tani 515,000 ni matumizi ya kawaida na tani 155,000 ni kwa mtumizi ya viwandani.

Waziri Mkuu Kuwa Mgeni Rasmi mkutanowa Wakuu wa Vyombo vinavyopambana na dawa za kulevya kutoka nchi 54

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi  katika mkutano wa 28  wa Wakuu wa Vyombo vinavyopambana na dawa za kulevya kutoka nchi 54 za Afrika ujulikanao kama (28 th HONLEA- Afrika).

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar e salaam Kamishna wa Huduma za Mamlaka kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Vallite Green Mwashusa alisema kuwa Waziri Mkuu Majaliwa anatarajiwa kuwa  mgeni rasmi katika mkutano, huo wa 28  wa Wakuu wa Vyombo vinavyopambana na dawa za kulevya kutoka nchi 54 za Afrika unaojulikana  kama (28 th HONLEA- Afrika).

 Kamishna huyo wa Huduma za Mamlaka alisema kuwa “lengo la mkutano huu ni kubadilishana uzoefu na kupanga mikakati ya pamoja kuhusu udhibiti na mapambano dhidi ya dawa za kulevya katika nchi  hizi 54 za Afrika”

Aliongeza kuwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Dawa za Kulevya na Vitendo vya Uhalifu (UNODC) Kanda ya Afrika   imeipa heshima Serikali ya Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa 28.

Mkutano huo ambao unaoratibiwa na Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Dawa za Kulevya na Vitendo vya Uhalifu (UNODC) unatarajiwa kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kuanzia Septemba 17 hadi 21 mwaka huu.

Shilingi Bilion tano zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Studio za redio na luninga za TBC ijini Dodoma

$
0
0
Na Shamimu Nyaki –WHUSM
Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni tano kwa ajili  ya ujenzi wa studio za Redio na Runinga  za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)  katika makao makuu ya nchi Dodoma.

Hayo yamesemwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Sera,Bunge,  Kazi ,Ajira, Vijana na wenye ulemavu Mhe. Antony Mavunde alipokua akijibu swali la Mhe. Anna Richard Lupembe (Viti Maalum) kwa niaba ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe aliyeuliza ni lini Redio Tanzania (TBC Taifa) itasikika katika kata za Ilela na Ilunde Wilayani Mlele.

Akijibu swali hilo Mhe. Mavunde amesema kuwa Serikali inaendelea na jitihada za kupanua usikivu wa TBC katika  Mikoa na Wilaya ambazo  hazina usikivu au kuwa na usikivu hafifu  ambapo katika bajeti ya mwaka 2016/2017 kiasi cha shilingi Bilioni moja zilitengwa kwa ajili ya kupanua usikivu katika wilaya tano za mpakani mwa nchi.

“Mkakati wa Serikali ni  kujenga mitambo ya redio katika mikoa ya Songwe,Katavi,Njombe na Simiyu katika bajeti ya mwaka 2019/20  na katika bajeti ya mwaka 2018/19 TBC imetengewa kiasi cha shilingi Bilioni tano kwa ajili ya kujenga studio za redio na luninga makao makuu ya nchi Dodoma”.Alisema Mhe. Mavunde.

Aidha Mhe. Mavunde ameeleza maeneo ambayo mitambo imefungwa na tayari  matangazo ya redio yamewashwa ni Rombo,Nyasa (Mbambabay), Tarime,Kibondo/Kakonko na Namanga kwa ajili ya kuongeza usikivu wa TBC.

Serikali yasitisha uagizwaji wa mchele nje ya nchi

$
0
0
Serikali imesitisha uagizwaji wa mchele kutoka nje ya nchi kutokana na uliopo nchini kutosheleza mahitaji.

Mchele uliopo nchini kwa sasa ni zaidi ya tani milioni 2.2, kiwango kilichotokana na wakulima wa mpunga kupatiwa mbinu bora za kitaalamu.

Katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mathew Mtigumwe alisema jana kuwa mahitaji ya mchele yanatosheleza kwa sasa.

Mtigumwe alisema hayo wakati akizungumza na wakulima wa mpunga kutoka mikoa mbalimbali nchini katika mafunzo yaliyofanyika mjini Moshi yaliyofadhiliwa na Shirika la Misaada la Japan (Jica).

Alisema mahitaji ya mchele nchini ni tani 900,000 na kwamba uzalishaji kwa sasa umeongezeka na nchi ina ziada ya zaidi ya tani milioni 1.2.

“Serikali mwaka huu haina haja ya kuagiza mchele kutoka nje ya nchi, ” alisema Mtigumwe

Alisema wanatambua mchango wa kuwasaidia wakulima unaofanywa na Jica ambapo wale wadogo wa mpunga wamefanikiwa kuongeza kiwango cha uzalishaji tofauti na siku za nyuma.

“Kutokana na uzalishaji huu umeifanya Tanzania kuwa nchi ya tano Kusini mwa Jangwa la Sahara katika uzalishaji wa mpunga baada ya nchi ya Nigeria, Madagascar, Mali na Guinea.”

Mwakilishi mkuu wa Jica nchini, Toshio Nagase alisema zaidi ya wakulima 15,000 wamenufaika na mradi huo na kuweza kujikwamua na umaskini.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yatangaza Uchaguzi Mdogo Wa Udiwani Katika Kata 37

$
0
0
Mwandishi wetu
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 37 za Tanzania Bara zilizopo katika Halmashauri 27 na mikoa 13 ya Tanzania Bara,  utakaofanyika tarehe 13 Oktoba mwaka huu.

Akitangaza uchaguzi huo, Mwenyekiti wa NEC Jaji wa Mahakama ya Rufaa Semistocles Kaijage, alisema fomu za uteuzi wa wagombea katika uchaguzi huo zitatolewa kati ya tarehe 15 hadi 21 Septemba, mwaka huu.

Alisema uteuzi wa wagombea utafanyika tarehe 21 Septemba, mwaka huu wakati kampeni za Uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 22 Septemba hadi tarehe 12 Oktoba mwaka huu.

Jaji Kaijage alifafanua kuwa uchaguzi huo unafuatia Tume kupokea taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za udiwani kwenye kata hizo kutoka kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa kwa kutumia kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa.

“Baada ya kupokea taarifa hiyo na kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(3) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa; Tume ina utaarifu umma kuhusu kuwepo kwa Uchaguzi mdogo katika Kata hizo thelathini na saba (37).”, alisema Jaji Kaijage.

Kufuatia uchaguzi huo, Mwenyekiti huyo wa NEC alivialika Vyama vya Siasa, Wadau wote wa Uchaguzi na Wananchi kwa ujumla kushiriki katika Uchaguzi huo.

Aliongeza kwa kuviasa Vyama vya Siasa na Wadau wa Uchaguzi kuzingatia matakwa ya Katiba, Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Madiwani), 2015, Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015 na maelekezo yote yaliyotolewa au yatakayotolewa na Tume wakati wote wa Uchaguzi huo.

Wakati huo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewateua Madiwani watatu Wanawake wa Viti Maalum kujaza nafasi wazi za madiwani katika Halmashauri tatu za Tanzania Bara.

Akitangaza uteuzi huo, Mwenyekiti wa NEC Jaji wa Mahakama ya Rufaa Semistocles Kaijage, aliwataja madiwani hao kuwa ni Halima Salum Kisenga (CCM) wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni.

Wengine walioteuliwa ni Emmy Anania Shemweta kupitia CCM katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Nuru Mwalimu Chuma kupitia Chama cha Wananchi (CUF) katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Jaji Kaijage alisema uteuzi huo umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa, ambaye aliitarifu Tume kuwepo kwa nafasi wazi kupitia vyama hivyo baada ya walioteuliwa kufariki dunia na kujiuzulu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 14

Lugola Atoa Ufafanuzi Mahabusu Kukaa Masaa 24 Polisi bila KJufikishwa Mahakamani

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema suala la mtuhumiwa kukaa mahabusu saa 24 linazingatia suala la upelelezi wa awali hivyo mtu akitolewa humo kusaidia kupeleleza muda huanza kuhesabiwa upya anaporudishwa ndani.

Amesema, kwenye Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai mtuhumiwa anapokamatwa kwa mara ya kwanza na kuwekwa mahabusu anaweza kutolewa kabla ya kufika saa 24 kwa ajili ya upelelezi au kwenda kuonesha silaha au kuonesha ushahidi kutokana na maelezo yake.

"Mnapomtoa atakaporudi mahabusu huyo mtuhumiwa anaanza kuhesabiwa masaa yake upya. Sasa kwa bahati mbaya wananchi wanahesabu tangu tangu alipokamatwa lakini kisheria tunahesabu tofauti"alisema  jana Waziri Lugola wakati anajibu swali la Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche.

Heche alitaka Waziri Lugola atoe tamko kwamba polisi wazingatie sheria na iwezo marufuku kwa mtuhumiwa kuwekwa mahabusu zaidi ya saa 24 bila kufikishwa mahakamani.

Lugola alisema, si nia ya Serikali kutesa wananchi hivyo askari watakaokiuka sheria hiyo ya mahabusu saa 24 watachukuliwa hatua.

"Hakuna yeyote ambaye sisi tunamfumbia macho. Kwa hiyo Mheshimiwa Heche uwe na amani. Huyo mtu unayemsema huyo tumeshatoa maelekezo, na tunajua concern yako"alisema Lugola.

 Alikiri kuwepo kwa malalamiko ya wananchi kuwekwa nani na baadhi ya polisi wasio waaminifu na waadilifu kwa makosa yasiyostahili.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images