Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Hotuba Kamili Ya Rais Magufuli Akiwa Sibiti 10/09/2018

$
0
0
Rais Magufuli jana tarehe 10 Septemba, 2018 amemaliza ziara yake ndani ya mkoa wa Simiyu na ametaka mkandarasi anayejenga daraja la Sigiti kuhakikisha kufikia Machi mwakani ujenzi huo uwe umakamilika.

==>>Hotuba nzima iko hapo chini
 

Rais Magufuli Atoa Salamu Za Pole Kwa Majeruhi Sita Wa Ajali Simiyu, Wakiwemo Waandishi Watano

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa pole kwa waandishi wa habari watano wa Mkoa wa Simiyu na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani waliopata ajali katika wilayani Meatu, wakati akiwa ziarani wilayani humo, salamu ambazo zimewasilishwa kwa niaba yake  na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, ambaye aliwatembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu walikokuwa wakipatiwa matibabu.

Akiwasilisha salamu za Mhe.Rais,  jana jioni Mhe. Mtaka amesema magari matano ya Simiyu ya Serikali na gari binafsi yaligongana na watu sita wakajeruhiwa wakiwemo waandishi watano na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani  na kusisitiza kuwa Mhe. Rais ameguswa na jambo hilo, hivyo ametoa shilingi laki tano kwa kila majeruhi ili iwasaidie katika matibabu.

“...magari ya waandishi wa habari lakini kulikuwa na gari binafsi, baada ya msafara wa Rais kwa sababu ya vumbi,  dereva mmoja katika yale magari alisimama kutaka kuona njia vizuri, magari yaliyokuwa yakifuatana  matano yakagongana kwa nyuma, watu sita wakapata majeraha miongoni mwao walikuwepo waandishi wetu watano na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani”

“Mhe. Rais anatoa salamu zake za pole kwa majeruhi wote,  ameguswa sana na jambo hili hasa pale aliposikia kuwa sehemu ya majeruhi ni waandishi ambao tumekuwa nao pamoja katika ziara hii, wakafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha Watanzania,  akaomba mimi kama Mkuu wa Mkoa nifikishe salamu zake za pole kwa niaba  yake kwa watu hawa sita” alisema.

Ameongeza kuwa Mkoa utaendelea kuchukua tahadhari kupitia jeshi la polisi hasa katika misafara ya viongozi na kuhakikisha kuwa wanajenga uelewa wa pamoja kwa madereva wakati wa maandalizi ya safari juu ya namna ya kuchukua tahadhari.

.Rehema Evance ambaye ni mwandishi wa Azam TV amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwatambua na kuona awape mkono wa pole ambao amebainisha kuwa fedha hizo zitawasaidia katika kugharamia matibabu.

“ Kwanza namshukuru Mungu kwa kutujalia tukapona,  lakini kipekee napenda kumshukuru Mhe. Rais kwa kuona kuna haja ya kutusaidia katika hili, kwa hiki alichotoa Mungu ambariki sana kitatusaidia kwenye matibabu, tunaahidi kuendelea kuwahabarisha Watanzania na kuhakikisha yale yote yanayotendeka ndani ya nchi yanawafikia” alisema.

Ajali hii iliyotokea wilayani Meatu Septemba 09, 2018 imesababisha majeruhi sita ambao ni waandishi watano Rehema Evance (AZAM TV), Belensi China(ITV), Aidan Mhando(Channel Ten), Phaustine Fabian(Mwananchi), Mpiga Picha Samson Masunga pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani na hakuna kifo kilichotokea..

Majeruhi wote walipatiwa matibabu katika Hospitaliya Wilaya ya Meatu ambapo waandishi wa habari Rehema Evance (AZAM TV), Phaustine Fabian(Mwananchi), Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani waliruhusiwa na Belensi China(ITV), Aidan Mhando(Channel Ten), na Mpiga Picha Samson Masunga walipewa Rufaa kwenda Bugando kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Kwa mujibu wa majeruhi hao waliopelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando wote wamefanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu na  Septemba 10, 2018  wameruhusiwa.   

MWISHO

Ajali ya Gari la Kubeba Mbao Yaua Watu Wanne Rombo

$
0
0
Na Dixon Busagaga,Rombo.
Watu  wanne wakiwemo wawili wa familia moja wamefariki dunia papo hapo baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Isuzu kuacha njia na kwenda kugonga gema katika eneo la Kikelelwa wilayani Hai.

Waliofariki dunia wametambulika kwa majina ya Emanual Josephat Silayo (28) ,Viviano silayo (35) wakazi wa Mbomai Juu,Juma Idd (20) maarufu kama mwarabu na mwingine aliyefahamika kwa jina moja la Deolla .

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Hamis Issah aliyefika eneo la tukio amethibitisha kutokea kwa ajalo hiyo na kwamba dereva wa Loli hilo lililokuwa limebeba mbao alikimbia kusiko julikana baada ya ajali..

"Jitihada za kumtafuta dereva zinafanyika na chanzo cha ajali ni kupoteza muelekeo kwa Lori hilo na baadae kugonga Gema ndipo watu waliokuwa wanmekaa mbele walichomoka na kwenda kupigiza vichwa katika Gema na kupasuka"alisema Kamanda Issah.

Kamanda Issah amesema gari hilo likiwa na shehena ya mbao lilikuwa likitokea eneo la West Kilimanjaro ,eneo maarufu kwa uchanaji wa mbao na kwamba lilikiwa likielekea Rombo kupitia njia ya Rongai.

"Ni gari la kubeba mbao lilikua linatoka West Kilimanjaro kupitia njia ya Kikelelwa wilayani Rombo ,Gari aina ya Isuzu likiwa na namba za usajili T 889 ACN lilimshinda dereva na kuacha njia na baadae kugonga ngema iliyosababisha watu wanne waliokuwemo katika gari hilo kufa papo hapo." alisema Kamanda Issah.

Miili ya marehemu wote imehifadhiwa katika hosptali ya wilaya ya Rombo kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Taarifa ya hali ya Mfumuko wa Bei nchini kwa mwezi Agosti, 2018

$
0
0
Maana ya Fahirisi za Bei za Taifa 
Fahirisi za Bei za Taifa ni kipimo kinachotumika kupima mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma mbalimbali zinazotumiwa na sampuli wakilishi ya kaya binafsi nchini Tanzania. Bei za bidhaa na huduma 278 zikiwa ni pamoja na bidhaa 97 za Vyakula na Vinywaji Baridi na 181 zisizo za Vyakula hukusanywa kila mwezi katika kila mkoa.    

Mizania Mpya za Bidhaa na Huduma na Jamii na Kizio cha Bei 
Mizania ya Fahirisi za bei za Taifa zimetokana na matumizi ya kaya binafsi kutoka mikoa 25 ya Tanzania Bara. Mizania inajumuisha matumizi ya kaya zote binafsi kutoka mijini na vijijini yaliyotokana na Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya binafsi wa mwaka 2011/12. Kizio cha bei kinachotumika kukokotoa Fahirisi za Bei za Taifa ni cha mwezi Desemba, 2015.  

Makundi ya Bidhaa na Huduma za Jamii
Fahirisi za Bei za Taifa hufuata makundi yaliyokubalika Kimataifa yanayoitwa mchanganuo wa matumizi binafsi “Classification of Individual Consumption by Purpose (COICOP)”. Fahirisi za Bei zinajumuisha makundi 12 ya mfumo wa COICOP pamoja na fahirisi za bei kwa makundi maalumu. Makundi hayo maalumu ni; 1) Vyakula na vinywaji baridi-vikijumuisha vyakula vinavyoliwa majumbani na mahotelini; 2) Nishati na Mafuta - kundi hili linajumuisha umeme na aina nyingine za nishati zinazotumika majumbani pamoja na petroli na dizeli; 3) Fahirisi za bidhaa na huduma zote za jamii isipokuwa vyakula na vinywaji baridi; 4) Fahirisi za Bidhaa na huduma zote za jamii isipokuwa vyakula, vinywaji baridi, nishati na mafuta.

Namna ya Kukokotoa Fahirisi za Bei za Taifa
Fahirisi za Bei za Taifa katika ngazi za mwanzo hukokotolewa kwa kutumia wastani wa jiometria “geometric mean of Price Relatives” na kanuni ya Lowe Index Formula ambayo ni aina ya “Laspeyres Index Formula” hutumika kukokotoa Fahirisi za Bei za Taifa katika ngazi ya makundi makubwa.

Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi. Jedwali Namba 1 hapo juu linaonesha kuwa, Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2018 umebaki kuwa asilimia 3.3 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018. Hii inamaanisha kuwa, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2018 imebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018. Fahirisi za Bei zimeongezeka hadi 112.01 mwezi Agosti, 2018 kutoka 108.46 mwezi Agosti, 2017. Mfumuko wa Bei wa bidhaa za Vyakula na Vinywaji Baridi kwa mwezi Agosti, 2018 umepungua hadi asilimia 2.2 kutoka asilimia 2.8 ilivyokuwa mwezi Julai, 2018.  

Mfumuko wa Bei kwa Bidhaa za Vyakula na Bidhaa Zisizo za Vyakula
Mfumuko wa Bei kwa kipimo cha mwaka kwa bidhaa za vyakula vinavyoliwa nyumbani na migahawani kwa mwezi Agosti, 2018 umeongezeka kidogo hadi asilimia 3.2 kutoka asilimia 3.0 mwezi Julai, 2018. Aidha, badiliko la Fahirisi za Bei kwa bidhaa zisizo za vyakula kwa mwezi Agosti, 2018 limeongezeka hadi asilimia 4.6 kutoka asilimia 4.2 mwezi Julai, 2018. 


Mfumuko wa Bei wa Bidhaa na Huduma zote isipokuwa Bidhaa za Vyakula na Nishati 
Mfumuko wa Bei ambao haujumuishi vyakula na nishati kwa mwezi Agosti, 2018 umeongezeka hadi asilimia 2.0 kutoka asilimia 1.6 mwezi Julai, 2018.  

Fahirisi inayotumika kukokotoa aina hii ya Mfumuko wa Bei, haijumuishi vyakula vinavyoliwa nyumbani na migahawani, vinywaji baridi, petroli, dizeli, gesi ya kupikia, mafuta ya taa, mkaa, kuni na umeme. Vyakula na bidhaa za nishati vina sifa ya kuwa na bei ambazo hubadilika mara kwa mara, hivyo vikiondolewa kwenye fahirisi ya bidhaa na huduma zote hubakia fahirisi ambayo ina mwelekeo imara kwa Watunga Sera.  



Kielelezo Namba 1 hapo juu kinaonesha kuwa, Fahirisi za Bei zimekuwa na mwenendo imara kutoka mwezi Agosti, 2017 hadi mwezi Agosti, 2018. Katika kipindi hicho, Mfumuko wa Bei umepungua kutoka asilimia 5.0 mwezi Agosti, 2017 hadi asilimia 3.3 mwezi Agosti, 2018.  
  
MABADILIKO YA FAHIRISI ZA BEI KATI YA MWEZI JULAI, 2018 NA MWEZI AGOSTI, 2018. 
Fahirisi za Bei kati ya mwezi Julai, 2018 na mwezi Agosti, 2018 zimepungua kwa asilimia 0.4 ikilinganishwa na kupungua kwa asilimia 0.3 mwezi Julai, 2018 kutoka mwezi Juni, 2018. Fahirisi za Bei zimepungua hadi 112.01 mwezi Agosti, 2018 kutoka 112.44 mwezi Julai, 2018. 


Kupungua kwa Fahirisi za Bei kumechangiwa hasa na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula. Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa fahirisi ni pamoja na; mchele kwa asilimia 1.7, mahindi kwa asilimia 3.6, unga wa mahindi kwa asilimia 3.5, unga wa ngano kwa asilimia 1.2, unga wa mtama kwa asilimia 2.0, mbogamboga kwa asilimia 2.8, mihogo kwa asilimia 1.6 na magimbi kwa asilimia 3.6. 



 

Mgambo wa Makonda Waingiza Milioni 346 Kwa Mwezi

$
0
0
Baada ya kuendesha kampeni ya usafi kwa mwezi mmoja, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda ametoa taarifa ya kampeni hiyo.

Akizungumza jana katika kikao hicho Makonda alisema kuwa tangu kuanza kwa kampeni hiyo zaidi ya watu 10000 wamekamatwa, watu 4443 waliachiwa huru, 376 walipata dhamana na takribani watu 6577 walilipa faini iliyofikia shilingi milioni 346 na laki 6 ambapo nusu ya fedha hizo ilikuwa ni malipo kwa mgambo wanaosimamia usafi na hadi sasa watu 6 bado wapo mahakamani.

Aidha amesema kuwa yeye na wakuu wa Wilaya wamelaani kitendo cha mgambo wa kusimamia usafi kumpiga raia katika eneo la Bunju na wamefatilia na hadi sasa watuhumiwa wapo katika gereza la Segerea na amewataka mgambo hao kufanya kazi kwa kufuata na kusimamia sheria kwani hakuna sheria inayorusu kupiga raia.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Bashe Ataka Mgombea Chadema Apewe Ulinzi Yasijirudie Ya Kinondoni

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe, amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kutoa ulinzi wa kutosha kwa mgombea ubunge wa Jimbo la Ukonga kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Asia Msangi ili kuondoa uzushi kuwa mgombea huyo anataka kutekwa.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni za jimbo hilo uliofanyika Mziga Mwanagati, jijini Dar es Salaam  jana Jumatatu Septemba 10, Bashe alisema kuna taarifa zimetolewa na watu wa Chadema wakidai wamepata taarifa kuwa mgombea wao atatekwa, hivyo ni vyema vyombo vya ulinzi na usalama vikahakikisha vinamlinda.

Bashe alisema si vema kupuuza maneno hayo kwani wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni walipuuza yakatokea maafa.

“Nimesikia wakitoa hoja kuwa CCM wanataka kumteka mgombea wao, vyombo vya ulinzi naomba mtoe ulinzi huyu dada alindwe kuanzia nyumbani kwake, kwenye gari na kwenye kampeni ili isije ikafika mahali wakaanza kusema ametekwa,” alisema Bashe.

Pamoja na mambo mengine, Bashe amesema chama chao kimejipanga hivyo ni vyema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakatenda haki.

“Naiomba NEC itende haki ili ikifika siku ya uchaguzi Septemba 16 upinzani wasipate sababu ya kufanya vurugu,” alisema.

Aidha, Bashe amewataka viongozi wa upinzani kuacha kusema kuwa wanaohamia CCM wamenunuliwa kwani kuna wengi wamehama chama tawala na kwenda upinzani lakini lakini hakuna aliyesema amenunuliwa.

“Kati ya waliowahi kuhama upinzani ni pamoja na Mgombea wa CCM wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara, Mgombea wao wa Monduli, Julius Kalanga na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Naomba wapinzani watuambie waliwapa Sh ngapi hawa?

“Vyama vya siasa ni sawa na gari unapanda likupeleke mahali, ukiona halikufikishi unashuka, ndivyo alivyofanya Waitara,” alisema Bashe.

Alisema kwa sasa CCM ndiyo chama pekee chenye demokrasia ambapo kinaruhusu kukosoana, kuzungumza na Waziri Mkuu yupo, jambo ambalo Chadema hawawezi.

“Huko kwao hakuna hayo mambo, ni zidumu fikra za mwenyekiti kwa hiyo naomba waangalie nyumba yao waache haya mambo ya kusema watu wamenunuliwa,” alisema Bashe.

Credit:Mtanzania

Gigy Money Afunguka Baada ya Video Kusambaa Wakipapasana Gizani na Msani Lavalava

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Gigy Money amefunguka kuhusu ukaribu wake na Lava Lava kutokea WCB.

Hii ni baada ya hivi karibuni kuwepo kwa video inayowaonyesha wawili hao wakishikana sehemu ambayo ilkuwa na giza kiasi. Hata hivyo Gigy Money ameeleza kuwa hapo walikuwa club na hakuna chochote kati yao.

"Mshikaji tu kwani kulambana ni nini, ni club pale na inategemea na mlivyozoeana," amesema Gigy Money.

Pia ameongeza kuwa, 'Sina mume wala sina mpango wa kuolewa, am single, i mean i have no boy friend'.

Spika Ndugai Awataka Wabunge CCM, Mawaziri Waitumie Mitandao ya Kijamii Kupangua Hoja za Wapinzani

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai  amekerwa na wabunge wa CCM na Mawaziri kutotumia mitandao ya kijamii kupeleka majibu na ufafanuzi wa Serikali kwa wananchi kama wafanyavyo wapinzani.

Ndugai alieleza hisia zake  jana Septemba 10, 2018 akisema wabunge wa upinzani wamekuwa wajanja katika kutumia mitandao ya kijamii ambayo inasomwa dunia nzima na hivyo kuwaaminisha watu.

Alitoa kauli hiyo wakati Bunge likipitisha muswada wa sheria wa marekebisho ya sheria mbalimbali namba 3 wa 2018.

"Kuna katabia kamezuka humu, wabunge wanaishambulia Serikali lakini inapokuja muda wa kujibu wanakuwa hawapo, lakini wanakuwa wameshashinda maana wanakuwa wametuma kwenye YouTube na watu dunia nzima wanasoma lakini ninyi (wabunge wa CCM) hakuna, utakuta hata ufafanuzi wa mawaziri hakuna," alisema Ndugai.

Alisema ni wakati sasa wabunge wa CCM na mawaziri kujipanga na kutumia mitandao ipasavyo ili dunia ijue mambo mazuri ya Bunge la Tanzania na hapo ndipo watu watapata ufafanuzi kwa maswali ya upande wa pili.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Alichokisema Makamu wa Rais Kuhusu Ahadi ya Milioni 50 kwa Kila Kijiji

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, amesema wananchi wasitegemee kupelekewa fedha Sh. milioni 50 walizoahidi mwaka 2015 katika kipindi cha uchaguzi kwa kila kijiji.

Ameyasema hayo jana Septemba 10, 2018, katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kazuramimba wilayani hapa mkoani Kigoma, kwamba hawatapelekewa fedha hizo na badala yake zitapelekwa kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuliko kuwapa fedha hizo kwa kila kijiji Serikali imeamua kuwekeza katika elimu, afya, barabara pamoja na maji lengo ni kupeleka maendeleo katika nchi.

"Serikali ya awamu ya tano imeamua kujitegemea katika kujitegemea lazima tujiwekee mikakati kuleta maendeleo katika nchi yetu.”

“Tumeanza kuwekeza katika maswala ya usafiri wa anga na nyie ni mashahidi mmeshuhudia tukinunua ndege zetu," alisema Samia Suluhu

Alisema Serikali imeamua kujitegemea lakini sio kujitegemea asilimia miamoja, kwani wataendelea kuhitaji misaada lakini kuna changamoto au vipaumbele vya kitaifa katika vipaumbele hivyo pesa itakayo patikana itashuka hadi kwa mwananchi wa chini.

"Tumeamua kujenga reli itakavyokuwa inaenda haraka na kubeba mizigo mingi zaidi na ikifanya kazi faida yake itafika mpaka kwa wananchi wa chini,” alisema

Alisema Serikali imeamua kuweka umeme mkubwa utakaowaka nchini nzima bila kuzimika ambao utatumika kwenye viwanda vitakavyojengwa Tanzania na faida yake itawafikia wananchi wote.

"Fedha hizo ambazo tumesema tutawapa katika kila kijiji tungeweza (kugawa) kwa kila mtu tusingeweza kuona faida yake.”

“Kwa hiyo sisemi tunaifuta ahadi yetu ipo kwenye ilani ya uchaguzi chama kimetuagiza ni wajibu wetu Serikali kutekeleza, lakini maendeleo kuna kupanga na kuchagua katika mipango yetu ya sasa hivi, hilo tumeliweka pembeni kwanza," alisema makamu huyo.

Alisema wasikae na kudanganya watu kwamba kuna fedha hizo zinatoka serikalini zinakuja zitaingizwa katika miradi muhimu kuliko kuwapa fedha mkononi na ukizingatia serikali inatoa fedha nyingi katika kuhudumia sekta ya elimu.

Irene Uwoya Azungumzia Ukaribu Wake na Diamond Platnumz

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Irene Uwoya amefunguka mara baada ya Diamond Platnumz kumposti hivi karibuni na kitoandika chochote.

Muingizaji huyo akipiga stori na SnS Tanzania (Simulizi na Sauti) amesema kuwa alichukulia kitu hicho kawaida ingawa watu walitafsiri vibaya.

"Sioni kama ni tatizo kwa sababu aliposti tu picha ambayo mtu mwingine anaweza akaposti. Watanzania wanapenda tu kufikiria vitu, ku-judge wanavyoweza wao, haikuwa tatizo kwangu," amesema Irene Uwoya.

Hapo jana kwenye Biko Jibebe Challenge  Irene Uwoya ndiye alikuwa host wa tukio hilo. Shindano hilo lilianzishwa na Diamond baada ya kutoa wimbo wake unaokwenda kwa jina la Jibebe ambao ameshirikiana na Mbosso na Lava Lava.

Toka Bungeni: Serikali Yasema Kuwa Sekta Binafsi Zinaruhusiwa Kulipa Mshahara Zaidi Ya Kima Cha Chini

$
0
0
Serikali imesema sekta binafsi wanaruhusiwa kuwalipa watumishi wake zaidi ya kiwango cha kima cha chini cha mshahara pale ambapo wanaona kufanya hivyo itaongeza motisha kwa wafanyakazi wao.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Anthony Mavunde, amesema bungeni jijini Dodoma leo Jumanne Septemba 11, akijibu swali la Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), aliyeuliza katika kipindi cha na maswali na majibu bungeni endapo serikali haioni haja ya kuboresha mishahara yake na kuzielekeza sekta binafsi kulipa mishahara inayoendana na hali ya maisha.

Akijibu hilo Mavunde amesema, serikali imeweka utaratibu kwa waajiri na wafanyakazi katika sekta binafsi, kujadiliana na kufunga mikataba ya hali bora mahali pa kazi kwa lengo la kuboresha maslahi yao ikiwamo mshahara na stahiki nyingine.

“Kupitia utaratibu huu, sekta binafsi wanaruhusiwa kulipa zaidi ya kima cha chini ili kuwafanya wafanye kazi kwa bidii na kujituma kwa lengo la kuzalisha mali au katika ktoa huduma.

“Hata hivyo, pia Sheria ya Taasisi za Kazi Na. 7, ya mwaka 2004 kama ilivyorekebishwa mwaka 2015, imeanzisha Bodi ya Mishahara ya sekta binafsi ambayo ina jukumu la kufanya utafiti kwa kuzingatia hali halisi ya gharama za maisha na masuala mengine ya kiuchumi na kupendekeza kiwango cha kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Mavunde amesema serikali iko katika hatua za mwisho za kuiwezesha bodi hiyo kufanya utafiti kuhakikisha utafiti huo unakidhi matakwa ya Sheria, Kanuni na Taratibu zinazokubalika nchini na viwango vya kimataifa.

==>>Tazama hapo chini

VIDEO: Halima mdee aibua upya sakata la Tanganyika Packers Bungeni

$
0
0
Halima mdee ameibua upya sakata la Tanganyika Packers na kuibana serikali itoe majibu juu ya mradi wa ujenzi wa nyumba zaidi ya 50,000 za kisasa katika eneo hilo. 

Tazama hapo chini majibu ya Serikali

Bungeni: Mbunge Aitaka Serikali Itoe Sababu za Kumtunza Faru Fausta Kwa Gharama Kubwa Kuliko Hata Wazee Wasiojiweza

$
0
0
Faru maarufu anayejulikana kwa jina la Fausta amezua gumzo bungeni baada ya Mbunge wa Viti Maalumu, Suzana Mgonokulima, kuhoji ni kwa nini serikali inamhudumia faru huyo kwa gharama kubwa wakati hazalishi kutokana na kuwa mzee.

“Serikali inamhudumia Faru Fausta kwa gharama ya Sh milioni 64 kwa mwezi, lakini serikali haiwezi kuhudumia mwananchi aliyezeeka ambaye hawezi kufanya shughuli yoyote ya kujikimu na maisha na hana mtu wa kumsaidia, je ni kipi muhimu zaidi kati ya Faru Fausta au mwananchi mzee asiyeweza kufanya lolote na hana wa kumsaidia,” amehoji mbunge huyo.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amesema faru huyo amekuwapo katika Hifadhi ya Ngorobgoro tangu mwaka 1965 ambapo kwa sasa ndiye faru mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani.

“Kutokana na uzee, Faru Fausta alijeruhiwa na fisi Septemba mwaka juzi, hivyo kulazimu atunzwe kwenye kizimba kwa ajili ya uangalizi maalumu ambao unahusisha matibabu na chakula, hivyo gharama iliyokuwapo kipindi hicho ilitokana na hali ya dharura iliyohitajika ikiwamo miundombinu, ulinzi, matibabu na malisho ambayo matumizi yote hayo kwa mwezi yalikuwa Sh milioni 1.4 kwa sasa hali yake inazidi kuimarika na gharama imepungua hadi Sh 285,000 kwa mwezi.

“Hata hivyo, faru huyo si kwamba ni muhimu kuliko wazee bali uamuzi wa kumtunza kwenye kizimba ulifanyika kwa lengo la kunusuru maisha yake ili aendelee kuwa kivutio cha utalii na kuingiza fedha za kigeni nchini,” amesema.

Hata hivyo, majibu hayo hayakumridhisha mbunge suzana ambaye katika swali lake la nyongeza alihoji tena umuhimu wa faru huyo ambaye hata hivyo amefungiwa watalii watamuonaje na kwamba umuhimu wake ni zaidi ya wazee waliopigania nchi na kuleta amani lakini hawatunzwi na serikali.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Hasunga amesema faru huyo anahifadhiwa kutokana na umuhimu wake na jinsi alivyoliingizia taifa fedha nyingi za kigeni na wengi wanataka kujua ataishi miaka mingapi ambapo sasa hivi ana miaka 53.

Hata hivyo, hali hiyo ilimuibua Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndungulile ambaye amesema kwa mujibu wa sera ya afya serikali inatambua wazee ambapo imeweka utaratibu wazee zaidi ya miaka 60 wanapata matibabu na wanapata kipaumbele kwenye huduma ya afya ambapo mapato yanayopatikana katika Sekta ya Utalii ndiyo hayo hayo yanakwenda kuhudumia wazee hao.

Mbunge Ahoji Uhalali Raia Wa Msumbiji Kupiga Kura Nchini

$
0
0
Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali, amehoji bungeni uhalali wa raia kutoka nchini Msumbiji na Tanzania ambao wamekuwa kushiriki katika uchaguzi katika nchi zote mbili.

“Kumekuwa na raia wengi kutoka Msumbiji katika Jimbo la Mchinga hasa vijiji vya Kilangala B, Butamba na Mvuleni Kilombwani, wamekuwa wakishiriki uchaguzi katika nchi zote mbili, je, raia hao ni Watanzania au wa Msumbiji, na je, Serikali imepitisha utaratibu wa raia pacha na kuwapa watu maalumu,” amehoji Bobali.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Anthony Mavunde, amesema sheria hazijaruhusu uraia wa nchi pacha wala hakuna watu maalumu waliopewa uraia wa aina hiyo.

“Ibara ya 5 (2) (a) ya katiba hairuhusu mtu mwenye uraia wa nchi nyingine kushiriki shughuli za uchaguzi ikiwamo kupiga kura, hata hivyo, ili mtu aweze kupiga kura lazima awe ameandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura lililoanzishwa chini ya Ibara ya 5 (3) (a) ya Katiba,” amesema Mavunde.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Manara akerwa na TFF kutumia neno hujuma kifungo cha meneja wa Simba

$
0
0
Mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano ndani ya klabu ya Simba, Haji Manara ameonyesha kutofurahishwa na kitendo cha Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF kutumia neno hujuma katika kumpatia adhabu ya kumfungia mwaka mmoja kutojihusisha na mpira meneja wa timu hiyo, Richard Robert.

Kupitia mahojiano na EFM radio, Manara amesema kuwa lugha ya hujuma iliyotumiwa na TFF siyo nzuri na wanapaswa kuangalia maneno ya kutumia.

”Tunangojea kupokea barua alafu tutalitolea tamko kwa sababu Simba hatuwezi kulikalia kimya hili jambo tutasema ama kukata rufaa ama tutasema lakini kwanza tunasubiri barua,” amesema Haji Manara

Manara ameongeza ”Unajua neno hujuma sijui maana yake, hujuma ni jambo kubwa sana, hujuma ni dhambi kuu sijui, hujuma adhabu yake ni kifo, jeshini kule ukiujumu adhabu yake ni kupigwa risasi sasa hii kwa kutumia neno hujuma peke yake hiyo imetustua watu wote Simba nadhani TFF wataangalia namna sahihi ya kutumia lugha.”

”Lugha za hujuma hazikutufurahisha sana lakini yote kwa yote wacha leo nione barua ikija tutazungumza.”

Kesi Ya Halima Mdee Yapigwa Kalenda....Shahidi Kadai Anaumwa

$
0
0
Ushahidi wa kesi inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee haukusikilizwa leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya mshtakiwa (Mdee) katika kesi hiyo kudaiwa anaumwa.

Hayo yameelezwa leo Septemba 11 na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Akizungumza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, Mutalemwa amesema kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa leo Septemba 11 kwa mashahidi wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi lakini mshtakiwa hayupo akidaiwa kuumwa

Baada ya Kishenyi kueleza hayo, mdhamini wa Halima Mdee, Fares Robinson aliieleza mahakama kuwa anaumwa.

Hakimu Simba baada ya kusikiliza Maelezo ya upande hizo zote aliipanga kesi hiyo kusikilizwa tena Oktoba 8, mwaka huu ambapo mashahidi wa upande wa mashtaka wataendelea kutoa ushahidi wao.

Katika kesi hiyo mashahidi wawili wa upande wa mashtaka tayari wamekwishatoa ushahidi wao ambao ni Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ilala(RCO),  Davis Msangi na Mkuu wa Kituo cha polisi cha Urafiki,Mrakibu wa Polisi Batseba  Kasanga.

Mdee alifikishwa mahakamani hapo kwa Mara ya kwanza Julai 10, mwaka huu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images