Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Kusinyaa Na Kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kama uume wako  umedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 
 
Ipo dawa  ya ASILI   ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.
 
Ni  dawa  ya  asili  kabisa ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI YA  KUPATA  TIBA  HII : Kupata  tiba  hii  fika  ka6ika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam  ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu  watapelekewa  dawa  mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )  na kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  au  boti  kwa  waliopo  Zanzibar.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :    0693  005 189.

Wimbo Mpya: Dully Sykes Kaachia Kaachia Wimbo Mpya Akiwa na Harmonize Unaitwa Kadamshi

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Dully Sykes ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao Kadamshi ambao amemshirikisha Harmonize, wimbo huu umefanyika na Producer Bonga ndani studio za Beta Sound. 

==>>Usikilize hapa.

Rais Magufuli Kushudia Utiaji Saini Wa Mkataba Wa Ujenzi Wa Meli Leo

$
0
0
Rais Dkt John Magufuli leo Septemba 03, 2018 atashuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa meli mpya na chelezo katika Ziwa Victoria, tukio hili linafanyika Jiji Mwanza na litarushwa moja kwa moja na TBC1, Azam Tv, ikulu.go.tz

Mikataba hiyo itahusisha ujenzi wa meli moja mpya, chelezo ya kujenga meli hiyo, ukarabati wa meli ya Mv Victoria na Butiama katika Bandari ya Mwanza Kusini jijini hapa.

Meli hiyo mpya itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo pamoja na magari madogo 20 na itafanya safari zake kati ya Mwanza na Bukoba kupitia bandari ya Kemondo, Mwanza na Musoma na pia, Mwanza na bandari za nchi jirani za Kenya na Uganda.

Imeelezwa kuwa mkataba mwingine ni wa ukarabati mkubwa wa meli ya Mv Victoria yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 200 za mizigo, iliyokuwa ikifanya safari zake kati ya Mwanza na Bukoba kabla ya kusitisha mwaka 2014 kutokana na kuharibika kwa mitambo yake. Ukarabati huo unatarajiwa kuchukua miezi 12.

Meli nyingine itakayofanyiwa ukarabati ni MV Butiama yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 100 za mizigo, meli ambayo ilikuwa ikifanya safari zake kati ya Mwanza na Nansio Ukerewe kabla ya kuharibika mwaka 2010.

Kukamilika kwa meli hiyo kutarahisisha usafiri kwa wananchi waishio kwenye visiwa vya Ukerewe.

Nisha Awatolea Povu Zito Wanaomsema Anasura Mbaya

$
0
0
Msanii wa filamu Bongo, Nisha amewatolea povu zito  wale wanaokuwa wakikosoa muonekano wake.

Muingizaji huyo amesema kuwa kujisifia una muonekano mzuri wakati hauna bahati haina maana yoyote.

==>>Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

"Halafu nyie mnaosema nina shepu mbaya hivi mshawahi kuhongwa hata Mil. 5 cash nyie? maana msije kujisifu shepu nzuri bahati 0. Nguvu yenu ya vocha achilia masuala ya kuzisaka wenyewe huko ndo usithubutu,wanawake wabaya tunajua kuzisaka chapaa hatari.

"Uzuri wangu kama bungo uko ndani kwa ndani babu weee ukiona picha lazma mate yakutoke na uzuri akili,tabia na mipango ndo maana NAJIKUBALI. 📸 @mubast." Ameeleza Nisha.

Licha ya kufanya vizuri katika filamu, pia Nisha ameingia kwenye muziki wa Bongo Fleva ambapo hadi sasa ametoa nyimbo mbili, Bachela na Yeye.

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Godbless Lema Ampingia Kampeni Mgombea Wa CHADEMA Ukonga....Awataka Wananchi Wajitoke Kwa Wingi Kupiga na Kulinda Kura

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema kitendo cha Asia Msangi kujitokeza kugombea ubunge Ukonga ni ujasiri ambao unatakiwa kuungwa mkono kabla hata hajasema atafanya.

Lema ameyasema hayo jana Septemba 2, 2018 kwenye kampeni za Chadema zilizofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Chanika, jijini Dar es Salaam.

Alisema wanaume wa Dar es Salaam wamekuwa ni waoga na wanarubuniwa na fedha au kuahidiwa vyeo.

Alisema yeye ataendelea kupigania haki za wanyonge licha ya vitisho vingi dhidi ya wapinzani.

Lema ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema amewataka wakazi wa Chanika kumchagua mgombea huyo ili akaungane naye kwenye harakati za kujenga demokrasia.

Alisema Chadema imeibiwa kura kwenye chaguzi za Kinondoni na Siha, hivyo amewataka siku ya uchaguzi kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kulinda kura zao.

"Hamna dhambi kubwa kama uoga, msitishwe na hawa polisi, ninyi mna nguvu kubwa kuliko wao. Uchaguzi huu si kati ya Asia na Mwita bali ni kati ya nuru na giza," alisema Lema.

Mbunge huyo amesema vita inayoendelea ni ya demokrasia dhidi ya watu wanaotumia nguvu kubwa kuua demokrasia ya Tanzania.

LIVE: Matangazo ya Moja Kwa Moja Rais Magufuli Akishuhudia uwekaji saini mikataba ya ujenzi wa meli mpya Mwanza

$
0
0
Fuatilia hapa moja kwa moja kutoka Mwanza muda huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli katika hafla fupi ya uwekaji saini mikataba ya ujenzi wa meli mpya, MV. Victoria na MV.Butiama katika ziwa Victoria.

Profesa Mwandosya Avunja Ukimya Sakata la Makontena Ya Makonda

$
0
0
Sakata  la makontena 20 yaliyoko Bandari ya Dar es Salaam kwa jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda limemwibua waziri wa zamani katika Serikali ya awamu ya nne, Profesa Mark Mwandosya akikumbushia misingi ya utawala bora.

Makontena hayo yaliyokwama bandarini baada ya Makonda kushindwa kulipa kodi ya Sh bilioni 1.2, kwa mara ya pili juzi yalishindwa kuuzwa kwa mnada baada ya wanunuaji kushindwa kufikia bei.

Juzi, Profesa Mwandosya aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, akisema alivyofundishwa misingi ya utawala bora, mkuu wa nchi akimkosoa mtumishi hadharani, anapaswa kuandika barua ya kujiuzulu.

Ingawa hakumtaja Makonda moja moja, lakini ni wazi kuwa alimlenga mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaam, kwa kuwa ni siku chache tu baada ya Rais Magufuli kumkosoa Makonda hadharani na kumtaka alipe kodi hiyo.

“Nilifundishwa misingi ya utawala, mkuu wa nchi akimkosoa mtumishi hadharani, unapeleka barua ya kujiuzulu ili kulinda heshima yake na kwa kufanya hivyo unajijengea heshima mbele ya umma. Nikiri kwamba huenda misingi hiyo imepitwa na wakati,”aliandika Profesa Mwandosya.

Jumapili ya Agosti 26 mwaka huu, Makonda alifanya ibada maalumu ya kumwomba Mungu ili wanaofanya mnada wasipate wateja.

“Amelaaniwa mtu yule atakayenunua furniture (samani) za walimu. Nimefanya ibada maalumu ya kuhakikisha makontena hayo hayapati wateja kwa sababu naamini Mungu alinipa kwa ajili ya walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, wanaofanya kazi katika mazingira magumu ikiwa ni jitihada zangu binafsi." Alisema Makonda

Kauli hiyo ya Makonda ilimwibua Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango siku moja baadaye, aliyeapa kusimamia sheria na kuhakikisha makontena hayo yanapigwa mnada

Alhamisi ya wiki iliyopita, Rais Dk. John Magufuli aliingilia kati mzozo kuhusu makontena hayo ambao ulianza tangu Machi mwaka huu, akimtaka Makonda alipe kodi.

Walimu Wanaotuhumiwa Kumuua Mwanafunzi Kwa Viboko Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Walimu  wawili wa Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba  wamefikishwa Mahakamani leo asubuhi Septemba 3, 2018   wakikabiliwea na kesi ya mauaji ya Mwanafunzi Sperius Eradius (13) wa darasa la 5.

Walimu hao waliofikishwa mahakama ya wilaya ya Bukoba kusomewa mashtaka yanayowakabili  ni Mwalimu Respicious aliyetoa adhabu ya vibobo na Mwalimu aliyedai kupotelewa na mkoba Elieth Gerald.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba  17, 2018  na watuhumiwa wote  wamerudishwa rumande.

Watanzania Waishio Nje Watakiwa Kushawishi Wawekezaji

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewatakaWatanzania waishio nje ya nchi  wahakikishe wanashiriki kikamilifu kujenga uchumi wa nchi yao  kwa kushawishi wawekezaji wenye mitaji mikubwa waje kuwekeza nchini na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John Magufuli inaamini kuwa Tanzania itapata maendeleo makubwa ya kiuchumi endapo wananchi wake watatekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya “Hapa Kazi tu”.

Aliyasema hayo jana jioni (Jumapili, Septemba 02 ,2018) wakatiakizungumza na Watanzania waishio nchini China kwenye ofisi za Ubalozi wa Tanzani uliopo jijini Beijing.

Alisema nchi zote zilizoendelea  zilihakikisha kuwa wananchi wake wanaelewa na kutekeleza matamko yanayowahamasisha kufanya kazi, hivyo alitumia fursa hiyo kuwahamasisha Watanzania popote walipo kutekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu.’

Waziri Mkuu alisema China ambayo imefanikiwa kuwa moja kati ya nchi zenye nguvu  kubwa ya kiuchumi duniani, imefika hapo kutokana na mchango mkubwa uliotolewa na wananchi wake, ambao waliamua kuunga  mkono juhudi za Serikali yao kwa kufanya kazi kwa bidii na weledi wakiwa ndani au nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwataka Watanzania waishio nje ya nchi wajiepushe na vitendo vya uhalifu hasa biashara ya dawa za kulevya  ambayo inachafua jina na heshima ya nchi yao kimataifa.

“Tanzania ni nchi nzuri na inaheshimika duniani, nawasihi wote mnaoishi nje muachane kabisa na biashara haramu ya dawa za kulevya kwa sababu inalitia doa Taifa na adhabu yake katika baadhi ya nchi ni kifo,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Awali, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga alisema mwelekeo  wa Diplomasia ya Tanzania Kimataifa hivi sasa ni kiuchumi (economic diplomacy), hivyo Watanzania waishio nje wanapaswa kuwa wabunifu, makini katika kutafuta fursa zenye manufaa kwa nchi yao.

Alisema Diplomasia ya Uchimi si kupeleka Tanzania wawekezaji tu bali wawekezaji katika viwanda ambavyo kila vinapojengwa vinachangia kuinua uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake,Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki aliwaasa vijana kuitumia teknolojia ya mawasiliano na mitando ya jamii kutafuta habari na taarifa muhimu hasa nafasi za masomo ili kujiendeleza kielimu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, SEPTEMBA 03, 2018.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Polisi.

Mwonekano mpya wa Diamond Platnumz baada ya kusuka

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul a.k.a Diamond Plutnumz ameibuka na mwonekano mpya wa nywele baada ya kusuka.

Hii imekuwa ni mara ya tatu ya msanii huyo kuonekana na mwonekano mpya kichwanii baada ya mwonekano wa kwanza uolikuwa kwenye nyimbo yake na Rayvan ya Salome.
 
Katika nyimbo Rockonolo aliyoshirikishwa na Lumina alionekana pia na mwonekano mwingine wa nywele akiwa amesuka,lakini huu ni mwanekano mwingine kichwani wa Diamond Platnumz...

China Kutoa Dola Bil. 60 Kwa Maendeleo Ya Afrika

$
0
0
RAIS wa China, Xi Jinpingamesema China itatoa jumla ya dola bilioni 60 za Marekani kwenye mpango wake wa miaka mitatu ya ushirikiano na Afrika katika shughuli za maendeleo.

Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Septemba 03 ,2018) wakati akifungua Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaofanyika jijini Beijing nchini China.

Rais Jinping ameahidi kuwa nchi yake itatoa ushirikiano ili kuhakikisha kwamba amani ya kudumu inapatikana Barani Afrika, hatua ambayo ni muhimu kwa ustawi wa nchi za Afrika.

Maeneo mengine ambayo Rais huyo ameahidi kuwa China italisaidia Bara la Afrika ni pamoja na ujenzi wa miundombinu, ushirikiano katika sekta ya biashara  na huduma za afya.

Kadhalika, Rais Jinping amesema China itatoa nafasi za mafunzo ya kilimo bora na mafunzo ya ufundi kwa watalaam kutoka nchi za  Afrika ili kuchangia katika maendeleo ya uchumi.

Amesema hivi sasa anaamini kwamba China na nchi za Bara la Afrika wako karibu zaidi na wanashirikiana vizuri sana katika shughuli za kimaendeleo ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Mkutano huo  ulianza kwa sherehe ya ukaribisho na baadae viongozi  kutoka nchi mbalimbali barani Afrika na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antyonio Geterres walipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na mwenyeji wao Rais wa China.

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa ambaye anamuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika mkutano huo alisalimiana na Rais Jinping baada ya ufunguzi. Mkutano huo utaendelea kesho ambapo viongozi wengi kutoka Bara la Afrika watapata nafasi ya kuzungumza.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, SEPTEMBA 03, 2018.

Apandishwa cheo na Rais Magufuli kwa masharti yakutolewa Sifa

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli amempandisha cheo Kaimu meneja wa Kampuni ya huduma za Meli (MSCL) Erick Hamis kuwa Meneja mkuu kwa kile alichodai kuwa amependezwa na mikakati yake inayoonesha dhahiri nia yake ya kulifufua shirika hilo na kumpa sharti la kutolewa sifa na kuliua tena shirika.

Rais amefanya uamuzi huo wakati akihutubia wananchi na wafanyakazi wa kampuni hiyo jijini Mwanza baada ya kushuhudia makubaliano rasmi ya mkataba wa ujenzi wa Meli mpya Chelezo, na ukarabati wa Meli za MV Victoria na MV Butiama katika ziwa Victoria na kampuni nne kutoka Korea Kusini, mkataba ambao una thamani ya Shilingi bilioni 152.

Rais Magufuli amesema kuwa kampuni hiyo ilikuwa ikielekea mwisho na alikuwa mbioni kuifuta kama sio jitihada za kiongozi huyo kuonesha nia katika kupambana na rushwa ambayo ndio kikwazo alichokitaja kuua vyanzo vya mapato, hivyo kumuagiza meneja huyo kuhakikisha hakuna kitakachopotea kuanzia leo anapokabidhiwa majukumu rasmi.

"Enzi zile kulikuwa na wizi, wafanyakazi walikuwa wakiiba mafuta. Mapato yalipokuwa yakipatikana yalikuwa yakipelekwa Dar es Salaam na wafanyakazi wanafahamu". Rais Dkt. Magufuli.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji mradi wa ujenzi wa meli hiyo mpya na ukarabati wa meli nyingine za MV Viktoria na Mv Butiama na ujenzi wa Chelezo, Meneja huyo amesema ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 yenye tani 400 utatoa ajira 250.

Ratiba ya Bunge ambalo linatarajia kuanza kesho September 4 - 14. ‬

$
0
0
Mkutano wa Kumi na Mbili wa Bunge unatarajiwa kuanza siku ya Jumanne tarehe 4 Septemba, 2018 na kumalizika tarehe 14 Septemba, 2018 Jijini Dodoma. Shughuli zitakazofanyika katika Mkutano huu ni kama ifuatavyo:-

1.0 KIAPO CHA UAMINIFU
Kutakuwa na Kiapo cha Uaminifu kwa Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chizza Mbunge wa Jimbo la Buyungu aliyechaguliwa kwenye Uchaguzi Mdogo tarehe 12 Agosti, 2018.

2.0  MASWALI
Katika Mkutano huu wa Kumi na Mbili, wastani wa maswali 125 ya Kawaida yanatarajiwa kuulizwa na Wabunge. Aidha, wastani wa Maswali 16 ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yanatarajiwa kuulizwa kwa siku ya Alhamisi tarehe 6 na 13 Septemba, 2018.

3.0 MISWADA YA SERIKALI
Bunge pia linatarajia kupitisha kwa hatua zilizobaki Miswada mitano (5) ya Sheria ambayo ilisomwa Mara ya Kwanza katika Mkutano wa Kumi na Moja (11) wa Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 91. Miswada hiyo ni :-
  1.  Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018 [The Dodoma Capital City (Declaration) Bill, 2018];
  2.  Muswada wa Sheria ya Bodi ya Kitaalam ya Walimu Tanzania wa Mwaka 2018 [The Teacher’s Professional Board Bill, 2018];
  3.  Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.2) wa Mwaka 2018 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.2) Bill, 2018];
  4.  Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.3) wa Mwaka 2018 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No.3) Bill, 2018] na
  5.   Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi wa Mwaka 2018 [The Public Private Partnership (Amendment) Bill, 2018].

4.0 TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE
Kamati ya Sheria Ndogo itawasilisha taarifa zake Bungeni zinazohusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na Bunge.

Ratiba yote ya Mkutano wa Bunge inapatikana katika Tovuti ya Bunge ambayo ni www.parliament.go.tz.

Imetolewa na:-       Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mawasiliano,
Ofisi ya Bunge,
DODOMA.
3 Septemba, 2018.

Watano Wafungua Kesi Mahakama Kuu Kupinga Channel za Ndani Kuondolewa Dstv, Azam, Zuku

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Iringa imeahirisha kupokea maombi ya kesi ya kupinga kuondolewa kwa chaneli za ndani kwenye ving’amuzi vya Azam, Dstv, Zuku na Star times iliyofunguliwa mahakamani hapo na watu watano hadi kesho.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania anayesikiliza kesi hiyo, Penterine Kente leo Septemba 3, 2018 amelazimika kuahirisha shauri hilo kwa dakika 20.

Uamuzi huo aliufanya baada ya kutokea ubishani wa kisheria baina ya mawakili wa upande wa waleta maombi na wakili wa Serikali aliyetaka mahakama kutoa muda mpaka walalamikiwa wengine watakapokuwepo mahakamani jambo lililopingwa na mawakili wa upande wa waleta maombi.

Baada ya mabishano hayo Jaji Kente aliamua kutoa muda wa dakika 20 ili kila upande ukaweke vizuri hoja zao na waliporejea baada ya muda huo Jaji aliamua kuahirisha kesi hiyo mpaka kesho.

Katika kesi hiyo waleta maombi Silvanus Kigomba, Jesca Msambatavangu, Oliver Motto, Sebastian Emmanuel Atilio na Hamdun Abdallah wanaiomba mahakama kubatilisha amri ya kuondolewa chaneli za ndani kwenye ving’amuzi vya kampuni hizo.

Wanasema ving’amuzi hivyo ambavyo wamekwishavitumia kwa muda mrefu na wananchi wamevinunua baada ya kuamini watapata huduma ya kutazama maudhui yanayorushwa na chaneli za ndani kupitia ving’amuzi hivyo.

Katika kesi hiyo namba moja ya mwaka 2018 waleta maombi wanawakilishwa na mawakili wawili Chance Luwoga na Edmond Mkwata.

Edmond amewataja walalamikiwa ni pamoja Multichoice (T) Limited, Simba net (T) Limited, Azam Televison, Starmedia (T) LTD, Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Mwanasheria MKuu wa Serikali.

Akizungumza kwa niaba ya walalalamikaji hao, Msambatavangu amesema kimsingi wao ni walaji wa habari na walikuwa wanapata habari kupitia chaneli za Tanzania za ndani ya nchi kwa hiyo kutokana na malumbano ya watoa huduma na serikali kwa sasa hawapati huduma hizo.

Msukuma Asema Lowassa Anampango wa Kurudi CCM

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Kasheku maarufu Musukuma (CCM), amesema viongozi wengi wa vyama vya upinzani wanataka kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Musukuma ameyasema hayo jana kwenye uzinduzi wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani Kata Machame Uroki wilayani Hai, uliofanyika katika Viwanja vya Kurasinde na ambapo pia amesema ifikapo Septemba 10 mwaka huu, nguzo za umeme italetwa katika kata hiyo ili wananchi waondokane na tatizo la umeme huku akiwataka kumchagua mgombea udiwani wa jimbo hilo kupitia CCM, Robson Kimaro.

“Viongozi wengi wanaitaka CCM, sasa nawasihi wananchi mliopo katika vyama vya upinzani kujitafakari kama mko sehemu salama,” amesema.

Aidha, akizungumzia kuhusu umeme katika wilaya hiyo amesema: “Sisi tutakwenda kumwagiza waziri mwenye dhamana na sasa tunapozungumza Meneja wa Tanesco (Shirika la Umeme nchini), Mkoa wa Kilimanjaro amesema nguzo zipo tayari kwa hiyo ndani ya siku 10 tatizo lenu la umeme litakuwa limekwisha katika  vijiji hivyo viwili vya Kurasinde na Bwera, ninachokizungumza nina uhakika nacho kwa sababu nipo ndani ya chama chenye serikali na kama nazungumza uongo nifukuzwe bungeni.”

Naye Mbunge wa Jimbo la Mbinga, Sixtus Mapunda amesema, Robson alikuwa Diwani mzuri na mwenye nia ya kuwatumikia wananchi lakini tatizo alikuwa katika chama kisichojali maendeleo ya wananchi.

“Wananchi wa Machame Uroki mnahitaji maendeleo na si maneno, Robson baada ya kutambua hilo na kutambua dhamira yake ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo alitambua hawezi kutimiza lengo hilo ndani ya Chadema na kuamua kujiunga ndani ya CCM ili kuwaletea maendeleo hivyo naombeni mumuunge mkono kwa kumpa kura za kishindo,” amesema Mapunda.

Awali, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Patrick Boisafi alisema kuwa, katika maneno ya mkoa huo ambayo wananchi wamewachagua viongozi wa vyama vya upinzani maendeleo yake yamekuwa yakirudi nyuma na kuwataka wananchi kutorudia makosa.

Kwa upande wake, Mgombea Udiwani Robson Kimaro amesema, kata hiyo ina changamoto ya uchakavu wa majengo ya Shule ya Msingi Mkwasaringe hali ambayo ni hatarishi kutokana na nyufa katika kuta hali ambayo imesababisha wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la nne kutumia darasa moja kusoma kwa kupokezana ambapo ameahidi kutaitatua changamoto hiyo.

Rais Magufuli Ahadili Kulipa Deni la Wafanyakazi Ambalo ni Bilioni 3.7 Ndani ya Wiki Mbili

$
0
0
Rais Dk. John Magufuli ameahidi kulipa madeni ya mishahara ya wafanyakazi wa 'Marine Service' jijini Mwanza ambao wanadai shilingi bilioni 3.7 na atawalipa ndani ya wiki huku akiwaonya kufanya kazi kwa juhudi na  ipasavyo.

 Rais Magufuli ametoa ahadi hiyo  leo akiwa jijini Mwanza kushuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa Meli mpya na Chelezo katika Ziwa Victoria, ambapo  ujenzi huo utagharimu shilingi Bilioni 88. 76.

''Mimi nitawapa hizo bilioni 3.7 ndani ya wiki mbili, sasa ole wenu msifanyekazi tena mtazitapika, nawaambia kabisa huu sio muda wa kubembelezana lazima tubanane kwa sababu tumechelewa'', ameonya Rais Magufuli.

Wafanyakazi hao wanadai malimbikizo ya mishahara ya takribani miezi 27 ambapo  Rais Magufuli ameeleza kuridhishwa na mwenendo wa uendeshaji wa sasa wa Marine Service chini ya Kaimu Mkurugenzi Erick Hamis.

Rais yupo ziarani katika mikoa mitatu ya Mwanza, Simiyu na Mara ambapo atazindua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Jambazi Lanaswa na Jeneza Songwe

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Songwe, linamshikilia mtu mmoja ambaye amekuwa akijihusisha na matukio mbalimbali ikiwemo, ujambazi, utapeli kwa kutumia nembo za freemason, akiwa na silaha aina ya  Air Gun  pamoja na risasi 135.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Kamanda wa Polisi Mkoani Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi Mathias Nyange amesema, mtuhumiwa huyo aliyejulikana kwa jina la Jerico Chifunda Msukuma, ni mkazi Nazareti Mjini Tunduma.

Mbali na kukutwa na vitu hivyo pia amekutwa na vitambulisho vinavyoonesha uraia wa nchi mbili Tanzania na Zambia ambapo anadaiwa kufanya matukio ya uhalifu kisha kukimbilia nchini Zambia.

Vitu vingine ambavyo amekutwa navyo Msukuma ni pamoja na jeneza dogo, pingu,  pasi inayotumika kutapeli watu kupata fedha, mashine ya kunakilisha  noti bandia, na karatasi zinazolingana ukubwa na noti ya shilingi 10,000.

Katika Hatua nyingine jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu 12 wakiwa na vitu mbalimbali kama runinga na radio, ambavyo vimeibwa katika matukio mbalimbali  na kwamba tayari vimetambuliwa na wamiliki.

Swala la Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye miradi ya ujenzi Lamkera Rais Magufuli...Atoa Wiki Moja kwa Waziri wa Fedha

$
0
0
Rais John Magufuli ametoa muda wa wiki moja kwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango na mwenzake wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Isack Kamwelwe kumaliza tatizo la Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kwenye  miradi ya ujenzi akisema inachelewesha na kukwamisha miradi.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo jijini Mwanza leo Septemba 3, 2018 wakati akihutubia wananchi baada ya kushuhudia utiaji saini mikataba ya kujenga meli mpya, Chelezo na ukarabati wa meli mbili za Mv Butiama na Mv Victoria.

"Suala la msamaha wa VAT ni kikwazo kwa miradi ya maendeleo. Unakuta miradi iko tayari kutekelezwa lakini linakuja suala la VAT linakwamisha," amesema nakuongeza: "Waziri (wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi), kaeni na Waziri wa Fedha mlimalize hili na limalizike ndani ya wiki moja."

Rais Magufuli yuko kwenye ziara ya kikazi katika mikoa mitatu ya Kanda ya Ziwa ya Mwanza, Mara na Simiyu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images