Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

ATCL Yazindua Safari Yake Ya Kwanza Ya Dar es Salaam Kwenda Bujumbura

$
0
0
Shirika la ndege Tanzania (ATCL),  jana Agosti 30, 2018 limeanza safari yake ya pili ya nje ya nchi ikielekea Bujumbura, Burundi.

Safari hiyo ilianza jana asubuhi saa 3 kamili ambapo ndege aina ya Bombadier Q400, iling’oa nanga uwanja wa ndege wa Julius Nyerere, Dar es Saalam.

Taarifa iliyotolewa  Agosti 30 na Kitengo cha Habari na Maelezo cha Waziri Mkuu, imeeleza kuwa hiyo inakuwa ni safari ya pili ya nje ya nchi baada ya ile ya Agosti 26  ambapo ndege hiyo ilielekea  Entebe, Uganda.

“Kuanza kwa safari hiyo mpya ya Bujumbura kutafungua milango ya kibiashara na kitalii baina ya Tanzania na Burundi, pia kutaongeza wigo wa safari za ndege za shirika hilo linalofufuliwa,” imesema taarifa hiyo

Akipokea ndege kubwa aina ya Boeing 787-8 Dreaamliner, Julai mwaka huu, Rais John Magufuli alisema nchi   inang’aa na imefunguka kimataifa kwani uwezo upo na nia ya kuona shirika la ndege la Tanzania linaimairika, nayo ipo.

Alilitaka shirika hilo  kubuni mikakati ya kibiashara ambayo itawawezesha kudumu kwenye ushindani lakini pia kupata faida ya kutosha na hatimaye kutoa gawio kwa serikali.

Bob Wine akamatwa tena

$
0
0
Mbunge wa Upinzani nchini Uganda ambaye pia ni mwanamuziki, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine ambaye anadaiwa kupigwa na kuteswa baada ya kukamatwa mapema mwezi huu, inasemekana amezuiwa kuondoka kwa ajili ya kwenda kupata matibabu nje ya nchi.

Kwa mujibu wa BBC akizungumzia kukamatwa kwa mteja wake, Mwanasheria wa Mbunge huyo,Robert Amsterdam amesema Bobi Wine alizuiliwa kuingia katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Uganda na kuchukuliwa na polisi ambao wanadaiwa kumpeleka katika hospital ya serikali.

”licha ya kwamba Jaji alitaka apewe pasi yake ya kusafiria kwa sababu anahitaji kuondoka nchini humo kwa sababu ya kwenda kupata matibabu nje, kufuatia mateso makali ambapo yeye na wabunge wengine 33 wa upinzani waliyapata, amechukuliwa kikatili na gari la wagonjwa la polisi, Mawakili hawajui wapi alipopelekwa na tumepatwa na mshtuko..” Alisema wakili wa Bobi Wine

Kabla ya Kuzuiliwa kwa Bobi Wine, mbunge mwingine tena wa upinzani Francis Zake pia alizuia Uwanja wa ndege kwa ajili ya kwenda kupata matibabu nje ya nchi.

Bob Wine anakabiliwa na makosa ya uhaini, kufuatia tukio la kushambuliwa kwa mawe gari la Rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni. Aliachiliwa kwa dhamana kutoka kizuizini alikokuwa akishikiliwa siku ya Jumatatu, akiwa katika hali mbaya.

Mwanasheria wake Robert Amsterdam ameongeza kuwa kipaumbele cha Bobi Wine ni kupata matibabu na si kuitoroka nchi.

”Watoto wake watabaki nchini Uganda, ni safari ya muda mfupi, kwa ajili tu ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu. Anakabiliwa na maumivu makali.”

“Anamajeraha makubwa yaliyosababishwa na kuteswa kwake na vitu vya chuma na vifaa vingine vilivyotumika kumtesea na anahitaji msaada.”

”Tuseme kuwa hakuna kiungo chake chochote cha mwili kisichouma na ana matatizo makubwa katika figo lake.”

Siku ya Jumatano Spika wa Bunge la Uganda alitaka kukamatwa kwa maafisa usalama walioshiriki kumpiga mbunge huyo.

Hata hivyo serikali ya Uganda imekataa madai kuwa Bobi Wine alitendewa vibaya wakati alipokuwa kizuizini.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na Serikali nchini China

$
0
0
Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC) utafanyika Beijing kuanzia tarehe 01 hadi 04 Septemba, 2018.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utaongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa. 

Viongozi wengine watakaoshiriki Mkutano huo ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga; Mhe. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mhe. Rashid Ali Juma, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na Viongozi wengine Waandamizi.

Mkutano huo utafunguliwa na Rais wa China, Mhe. Xi Jinping ambaye pia ni Mwenyekiti wa jukwaa hilo, kwa kushirikiana na Mwenyekiti Mwenza, Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Matamela Cyril Ramaphosa, utahudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ambaye pia ni Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Antonio Guterres na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Afrika ambaye pia ni Rais wa Chad, Mhe. Moussa Faki Mahamat. Mkutano huo pia utashuhudia uchaguzi wa Mwenyekiti Mwenza mpya kutoka Afrika.

Kaulimbiu ya Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika kwa mwaka 2018 ni “China na Afrika: Kuelekea Jumuiya Imara kwa mustakabali wa wote kupitia ushirikiano kwa manufaa ya wote” (China and Africa: Toward an Even Stronger Community with a Shared Future through Win-Win Co-operation).

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utatanguliwa na kikao cha Makatibu Wakuu kitakachofanyika tarehe 01 Septemba, 2018. Kikao hicho pamoja na mambo mengine kitapitia agenda za mkutano huo na kuziwasilisha kwenye kikao cha Mawaziri kitakachofanyika tarehe 02 Septemba, 2018.

Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati Afrika na China pamoja na mambo mengine utajadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na China na kufanya mapitio ya mikakati ya pamoja ya maendeleo iliyopo kati ya Afrika na China. 

Jukwaa hilo ambalo lilianzishwa mwaka 2000 huwaleta pamoja viongozi wa Afrika na China kujadili masuala ya ushirikiano na maendeleo na kutathmini utekelezaji wa makubaliano mbalimbali yanayofikiwa kati yao.

Aidha, masuala ya ushirikiano katika uendelezaji Miundombinu kama Barabara, Reli, Bandari na upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Bara la Afrika yatajadiliwa kwa kina. 

Agenda nyingine itahusu kilimo cha kisasa ambapo China itatoa uzoefu wake katika kutumia sayansi na ubunifu wa kiteknolojia katika kufikia uzalishaji wenye tija na kuongeza thamani kwa mazao ili kuwa na soko la uhakika.

FOCAC 2018 pia itajadili masuala ya biashara na uwekezaji ambapo kwa kuona umuhimu huo, Mhe. Xi Jinping, Rais wa China atafungua rasmi Mkutano wa Jukwaa la Biashara kati ya China na Afrika utakaofanyika tarehe 03 Septemba, 2018.

Mkutano wa kwanza wa Wakuu wa Nchi wa Jukwaa hili ulifanyika Beijing mwaka 2006 na Mkutano wa Pili ulifanyika nchini nchini Afrika Kusini mwaka 2015.

Wakati wa Mkutano wa pili, China ilitangaza mpango kabambe wa kuhamasisha mapinduzi ya viwanda na kilimo cha kisasa kwa Afrika wenye gharama ya Dola za Marekani bilioni 60 katika utekelezaji wake. 

Kufuatia ushirikiano kupitia Jukwaa hilo biashara kati ya China na Afrika imeongezeka pamoja na ongezeko la ushirikiano wa kiutamaduni na biashara baina ya watu wa China na Afrika.

Pembezoni mwa Mkutano huo, Tanzania na China zimeandaa Kongamano la Biashara ambalo litafunguliwa rasmi na Mhe. Waziri Mkuu tarehe 02 Septemba, 2018. Kongamano hilo ambalo litajadili kwa kina masuala ya uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na China litashirikisha takribani makampuni 80 kutoka nchi hizi mbili.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dodoma.
30 Agosti 2018

Harmonize Aimwagia Sifa JIBEBE Ya Diamond....Awashukuru Mashabiki kwa Sapati yao WCB

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Hamonize amefunguka kuhusu wimbo wa Diamond Platnumz 'Jibebe' alioshirikiana na Mbosso na Lava Lava kukutana na ule wake, Atarudi.

Muimbaji huyo kutokea WCB amesesema nyimbo hizo zinafanya vizuri kutokana  na ukweli kwamba mashabiki wameamua kuwa nao na si kwamba wanajua sana.

"Kabisa siumeona mwenye balaa la Jibebe lakini nashukuru watu wanatusapoti sana sio kwa sababu sisi tunajua sana, watu wamemua tu kutusapoti WCB fo life," Harmonize ameiambia Wasafi TV.

Katika hatua nyingine Harmonize amefunguka kuhusu kuanzisha Band yake na sababu ya kufanya hivyo pia.

"Konde Music Band itakuwa na bei zake, ukisikia Harmonzie anatumbuiza kwa Band lazima hela itakuwa ni tofauti, so tutegemee vitu vizuri tu nachukua muda mwingi kufanya mazoezi kuzipitia nyimbo zangu vizuri, ikifikia siku nikatumbuiza mtu asiboreke apate ladha zaidi," amesema Harmonize.

Harmonize ni miongoni mwa wasanii walioshiriki kwenye Listening Party ya Albamu ya Barnaba inayokwenda kwa jina la Gold. 

==>>Msikilize hapo chini akifunguka

Rich Mavoko Kaachia Video ya wimbo Wake Ndegele....Ndani ni Kama Kamchokonoa Diamond na WCB

$
0
0
Msanii wa muziki, Rich Mavoko ameachia video ya wimbo wake ‘Ndegele’ ikiwa ni video yake ya kwanza toka aingie kwenye mgogoro na WCB  ya Diamond, label ambayo amefanya nayo kazi kwa miaka 2.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya kazi akiwa katika kampuni yake ya Billionea kid,  kupitia video hii ni kama katupa jiwe gizani ambapo  mashilawadu wanadai linawalenga moja kwa moja WCB ambao hapatani nao.

==>>Itazame hapo chini

Sumaye: CCM Imepoteza Mwelekeo, Wananchi Wameichoka

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema moja ya dalili za chama cha siasa kilichochokwa na wananchi ni  kutumia nguvu.

Sumaye ambaye ni mwenyekiti wa Chadema kanda ya Pwani ametoa kauli hiyo jana Alhamisi Agosti 30, 2018  wakati akimnadi mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Ukonga, Asia Msangi katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Gulu Kwalala.

Alisema CCM imechokwa na wananchi na kwa saa inachokifanya ni kung’ang’ania madarakani kwa kutumia nguvu.

“Kama unajiamini na wananchi wanakukubali kwa nini uwaonee wananchi, uwatishe kwa kila aina ya vitisho. Huko ni  kujilazimisha kuwa wananchi wanakukubali  wakati unawaziba midomo. Unawalazimisha kukubali unachokitaka,” alisema.

Amesema wanaopenda  mabadiliko ndani ya  Chadema, CUF na hata CCM,  huu ndio wakati wao wa kujipambanua na kuonyesha uwezo wao katika siasa kwa kufanya uamuzi sahihi.

“Hivi kweli hatuna akili kiasi hiki? Mtu tulimpa kura hapa hapa na ametutukana hadharani na bado tunampa tena” alihoji  Sumaye akimlenga mgombea wa CCM katika jimbo hilo, Mwita Waitara , ambaye awali alikuwa mbunge wa Ukonga kwa tiketi ya Chadema.

Gigy Money Amtolea Povu Zito Zari.......“Ulitoka chini, usiniongelee vibaya tena wewe ni rika la mamaangu na Nikimtaka Diamond Nampata"

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo na video vixen, Gigy Money amejibu kile alichoanzisha Zari The Bosslady.

Utakumbuka kwenye moja ya post za Zari kwenye mtandao wa Instagram alikuwa anazindua chuo, sasa kuna shabiki alim-tag Gigy kwenye post hiyo na Zari akajibu asihusishwe na masuala ya Gigy.

Sasa Gigy Money amejibu hilo, kwenye mahojiano na BongoStarsExclusive ameeleza kushangazwa na kauli hiyo.

"Dada Zari mimi ni type yako? usihusishwe na mimi kwa hiyo mimi mdudu au? kweli ukiwa na hela unabadilika kiboko yake Hamisa. Hata ukisema huyo Diamond nikimtaka nampata, kwa kitu gani ambacho sina na mwenzangu anacho, mimi mzee vile? akaah!!.

“I know ni mama yangu. Mama, mgeni, nchi jirani tumekupa kiki usiniongelee vibaya tena. Nakuomba yani sector ya mapenzi isikufanye ukatuchukie Tanzania nzima. Aliyekuchifua ni Chibu sio Gigy, do not talk shit about anybody. So my dear Zari i don’t know you, i appreciate you and even if we are not on the same level am growing, am gonna be there so watch me madam,”  amesema Gigy Money. 

==>>Hapo chini kuna Video 3, Msikilize Gigy Money akitema Povu zito

==>>Video ya Kwanza:

==>>Video ya Pili


==>>Video ya Tatu

LIVE | Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu wakizungumza na wanahabari

$
0
0
Tume ya Haki za Binadamu inatoa ripoti yake ya haki za binadamu Tanzania kwa nusu ya kwanza mwaka 2018  kupitia kwa waandishi wa habari.
 
==>>Wasikilize hapo chini

Jeshi La Polisi Mkoani Mbeya Lamtia Mbaroni Baba Aliyemuua Mwanae Kwa Kumnywesha Sumu

$
0
0
JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mwanaume mmoja mkazi wa Kijijicha Isitu Wilayani Mbarali ambaye amefahamika kwa jina la GEOFREY EMILIO  MWANGANGA [21] kutokana na kumuua mtoto wake aitwaye PRINCE GEOFREY EMILIO mwenye umri wa miezi 5.

Mwili wa marehemu ulipatikana mnamo tarehe 30.08.2018 majira ya saa 17:30 jioni huko katika Kijiji cha Isitu porini, Kata ya Chimala, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alimuua mtoto huyo kwa kumnywesha sumu ambayo bado haijafahamika aina yake na kisha kwenda porini kumfukia. 

Inadaiwa kuwa awali mnamo tarehe 28.08.2018, baba mzazi wa marehemu bwana GEOFREY EMILIO alikwenda nyumbani kwa mke wake ambapo alikuwa anaishi baada ya kuwa wametengana na kumchukua mtoto huyo kwa nguvu bila kibali cha mama mzazi wa mtoto.

Mtuhumiwa baada ya kukamatwa alidai kuwa mtoto alikuwa amempeleka kwa ndugu zake huko Makete Mkoani Njombe lakini baadae alikiri kuwa mtoto huyo amemuua na kumtupa porini na katika ufuatiliaji aliwapeleka Polisi eneo alipokuwa amemfukia marehemu.

Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi kwani mtuhumiwa alikuwa anahisi mtoto huyo sio wake amebambikiwa ni wa mwanaume mwingine. 

Mwili wa marehemu umefukuliwa na kuhifadhiwa katika Hospitali ya Misheni Chimala kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kitabibu.

Katika Tukio Jingine:
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawasaka watu wanaodaiwa kufukua kaburi na kisha kuchukua mifupa ya mwili wa marehemu ambaye alikuwa na ulemavu wa ngozi [Albinism].

Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 30.08.2018 majira ya saa 03:00 usiku huko katika Kijiji cha Ngonga kilichopo Kata ya Ngonga, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa mbeya ambapo kaburi la mtu mmoja aliyekuwa anajulikana kwa jina la ANDUSAMILE MWALWEBE @ KANJANJA [65] Mkazi wa kijiji cha Ngonga ambaye aliyefariki dunia mwaka 2012 kwa maradhi ya kawaida na ambaye aliyekua na ulemavu wa ngozi (Albinism) kukutwa limefukuliwa na mtu/watu wasiojulikana na kisha watu hao kuchukua mifupa ya mwili wa mtu huyo ( skeleton).

Kiini cha tukio hilo ni imani za kishirikina. Aidha inadaiwa kuwa kabla ya

kuchukua mifupa ya marehemu, watu hao walichimba shimo kubwa pembeni mwa kariburi hilo lililojengwa kwa tofali za saruji kisha wakabomoa upande mmoja wa jeneza (sanduku) na kuchukua mifupa hiyo na kutoweka nayo. Upelelezi unaendelea ikiwa ni pamoja na msako ili kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa hao.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na misako na operesheni

mbalimbali katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya ili kuzuia na kudhibiti matukio ya uhalifu pamoja na ajali za barabarani

Imesainiwa na.
[MODESTUS CHAMBU – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
KAIMU KAMANDA: 0658 376 052

Mgonjwa Afariki Dunia Baada Ya Ambulance Mali Ya JWTZ Kupata Ajali

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
ELINIKUNDA Mushi (50) ,amefariki dunia baada ya gari la kubebea wagonjwa (ambulance) mali ya jeshi la wananchi wa Tanzania  (JWTZ) , lililokuwa likimuwahisha hospital ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu kupata ajali eneo la Kibiki, kata ya Bwilingu, Chalinze mkoani Pwani.
 
Katika ajali hiyo watu wengine wanne walijeruhiwa baada ya dereva wa ambulance kudaiwa kuligonga gari nyingine kwa nyuma,lililokuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara kwa ajili ya matengenezo .
 
Akitoa taarifa kuhusu tukio hilo, kamanda wa polisi mkoani Pwani, (ACP) Wankyo Nyigesa ,alisema ajali hiyo imetokea alfajiri agost 31 mwaka huu.
 
Alieleza, gari namba 3489 JW 12 aina ya Ashok Leyland inayomilikiwa na kikosi cha jeshi 911 KJ cha Ihumwa Dodoma, mali ya JWTZ, lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Dar es salaam aliligonga gari lingine lenye namba za usajili T. 764 ACK aina ya Toyota canter na kusababisha kifo cha mtu mmoja .
 
Nyigesa alisema, aliyepoteza maisha ni Elinikunda ambae alikuwa mgonjwa akipelekwa kwenye matibabu katika hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi. 
 
“Watu wanne walijeruhiwa ambao ni pamoja na Beatrice Shidodolo (56)muuguzi wa hospital ya Dodoma, Ufo Swai (48) mkazi wa Ngerengere yeye alikuwa akimhudumia mgonjwa akiwa Dodoma “alisema Nyigesa. 
 
Nyigesa aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Justine Patrick (28)ambae alikuwa dereva wa gari namba T. 764 ACK iliyokuwa imeegeshwa kwa matengenezo na Rashid Rais (35) alikuwa fundi wa gari hilo wakazi wa Chalinze. 
 
Uchunguzi wa awali umebaini katika ambulance hiyo ilikuwa imepakia watu wengine wanne ambao hawakuweza kupata majeraha yoyote ambao ni MT. 3480 SGT Elimasa Mushi (40) askari wa JWTZ makao makuu ya Jeshi (MMJ). 
 
Nyigesa aliwataja wengine kuwa ni MT 95881 PTE Taulin Kaira (30) askari wa  911 KJ aliyekuwa msindikizaji wa gari hilo la wagonjwa, Eveline Stanley (25) alipewa msaada wa usafiri na mtoto wake wa miezi 11 anaitwa Nicholous Petro na dereva wa gari hilo MT. 67451 SGT Shaban Mpwate. 
 
Kamanda huyo alifafanua, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospital ya Jeshi ya Lugalo na majeruhi wamepelekwa katika hospital hiyo. 
 
Dereva wa ambulance Shaban Mpwate,anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi. 
 
Nyigesa aliwaasa madereva wa magari ya dharura kama magari ya wagonjwa kuhakikisha wanachukua tahadhari kubwa wanapokuwa wamepewa kipaombele na watumiaji wengine wa barabara ili kuweza kuepuka ajali zembe.

CCM Yawatosa Wasanii....Yasema Hakuna Bajeti Yao, Itabaki na TOT

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Dk Bashiru Ally amesema chama hicho hakitakuwa na bajeti kwa ajili ya wasanii na badala yake watabaki na vikundi vilivyopo ndani ya chama.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Agosti 31, 2018 wakati akifungua  mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) jijini Dodoma.

Dk Bashiru amesema kwa sasa wasanii watakaoshiriki shughuli za chama hicho, watapewa huduma muhimu pekee ikiwemo malazi, chakula na usafiri.

Akifungua mkutano huo, amesema msanii wa Afrika ni mwana mapinduzi, mpambanaji na kwamba mashairi ya wimbo wake ni lazima yawe na hisia zinazowakera na kuwazomea wanyonyaji.

“Yakowapi mashahiri hayo, ziko wapi nyimbo hizo, ziko wapi ngoma hizo za kusifu bara letu na kuwakumbusha vijana bara hili liliwahi kutawaliwa,” amesema.

“Ndio maana nimesema ndani ya CCM hatutakuwa na bajeti ya wasanii tena, hakuna tutabaki na TOT tutaimarisha chombo chetu kile kama alama na Vijana Jazz basi. Tukienda Arusha tutawakuta wasanii kule wataimba mashairi, watacheza ngoma.”

Amesema alipopokelewa makao makuu ya chama hicho aliburudishwa na vikundi vya ngoma, kubainisha kuwa si kwamba wasanii wa nyimbo alizoziita za kurukaruka ni wabaya, bali kibaya kwa mtazamo wake ni ujumbe uliomo ndani ya sanaa hiyo.

Msanii ROSA REE Aachia Wimbo Mpya ...One Way, Utazame Hapa

$
0
0
Msanii Rapper wa kike Rosa Ree Siku ya Leo ameachia wimbo wake mpya Unaoitwa One Way

==>>Nimekuwekea Video ya Wimbo huo Hapa Chini: Bonyeza Play

Polisi Kinondoni inawashikilia mgambo watatu kwa kumshambulia na kumjeruhi Mwananchi

$
0
0
Polisi Kinondoni inawashikilia mgambo watatu, kwa kumshambulia na kumjeruhi Robson Orotho, mkazi wa Bunju Dar kwa kutolipa faini ya usafi Sh50, 000.



Mufti Mkuu, Sheikh Abubakar Zuberi amtembelea na kumfanyia dua Dkt. Kigwangalla MOI

$
0
0
Na Andrew Chale
Mufti Mkuu wa Tanzania Shekh, Abu Bakari Zuberi  leo Agosti 31,2018 amemtembea na kumuombea dua maalum Dkt Hamisi Kigwangalla ambaye anapata matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI akiuguza majeraha ya mkono aliyopata katika ajali iliyotokea Agosti 4, mwaka huu Mkoani Manyara.

Mufti, Sheikh Zuberi  aliambata na Mjumbe wa Halmashauri Kuu BAKWATA, Sheikh  Yusuph Hassan Tonge ambapo kwa pamoja wameweza kuendesha dua maalum ili kupona haraka majeraha yake.

“Nimetoka Makka kwenye hijja tumekuombea dua. Nimerejea nikaona nije kukuona na pia kukuombea dua ili upone haraka.”  Alisema Mufti, Sheikh Zuberi.

Mbali na dua, pia Mufti, Sheikh Zuberi ameweza kumpongeza Dkt. Kigwangalla kwa juhudi zake za kazi katika Wizara yake hiyo.

Aidha, Dkt. Hamisi Kigwangalla amemshukuru Mufti Mkuu, Sheikh Zuberi  pamoja na BAKWATA kwa kuendelea kumuombea dua ambapo pia aliwaeleza kuwa kwa sasa hali yake inazidi kuimarika huku akisubiria ripoti za Madaktari.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi wa Taasisi ya MOI, Fiderisi Minja ambaye aliwapokea wageni hao, amesema kuwa Madaktari Bingwa na Wauguzi wanaendelea kutoa tiba bora  kwa wagonjwa wote wanaofika kufanyiwa tiba katika taasisi hiyo.

Dkt. Kigwangalla alihamishiwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI tarehe 12/08/2018 baada ya kupata matibabu ya awali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kwa sasa bado anaendelea na tiba kuuguza mkono wake wa kushoto.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 1

Dk. Bashiru asema mikataba uwekezaji CCM ya kifisadi

$
0
0
Katibu  Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally, amesema mikataba ya uwekezaji katika chama hicho na jumuiya zake, inatarajiwa kupitiwa upya kwa kuwa baadhi ni ya kifisadi na kitapeli.

Dk,. Bashiru alisema hayo jana jijini hapa wakati akifungua Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), huku akibainisha kuwa umoja huo ndio unaoongoza kuwa na mikataba mingi mibovu.

Alisema lengo la kuipitia upya mikataba hiyo ni kujadiliana kwa misingi ya usawa na hakutakuwa na mkataba ambao chama au jumuiya inapoteza umiliki wake.

Aidha, alisema limeshaundwa baraza la wadhamini wa chama ambalo kwa mujibu wa Katiba ya CCM, lina mamlaka ya kusimamia mali zote za chama na jumuiya zake.

“Yale yote mabaraza ya Jumuiya yaliyokuwapo yalikuwa uchochoro wa wizi na uporaji wa mali za jumuiya na yamefutwa kikatiba,”alisema.

Dk. Bashiru alisema wakati wa uhakiki wa mali za chama kuna mambo yalionyesha kuwa jumuiya hiyo imeanza kupoteza misingi ya nidhamu.

“Mali zenu nyingi zimekuwa hazitumiki vizuri. Ni jumuiya ambayo ina mikataba mibovu na hasa mkataba wa mradi wenu mkubwa pale Dar es Salaam, ni mkataba wa wizi, wa kitapeli,” alisema.

Alibainisha kuwa, chama kimedhamiria kuchukua taratibu za kisheria kurejea mikataba hadi ifike mahali ambapo mwekezaji na umoja huo wanakuwa sawa.

“Hatutaki mikataba ambayo chama au jumuiya inapoteza umiliki wake kama yaliyopo pale kwenye miradi yenu jijini Dar es Salaam. Mikataba ile pamoja na mambo mengine mmepoteza haki ya kumiliki wa ardhi yenu,” alisema.

Alifafanua kuwa, katika moja ya mikataba mwekezaji ametumia hati kukopa na kwamba mkataba huo UVCCM inapata asilimia 25 huku mwekezaji asilimia 75.

“Sasa kwa nini msifanye kama Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wao wameenda kukopa halafu wanajenga halafu watalipa kutokana na uwekezaji waliopata,” alisema huku akisisitiza kuwa: “Mikataba ya aina hiyo imefika mwisho na haitatokea mikataba tena kama hiyo.”

Katika hatua nyingine, Dk. Bashiru aliwataka vijana kuendesha mijadala inayohusu demokrasia katika mitandao ya kijamii ili kuimarisha uhuru wa kujitawala, amani na utulivu.

Aidha, aliwataka viongozi wa UVCCM kuhakikisha wanafanyia kazi suala la ukomo wa madaraka ndani ya jumuiya hiyo kwa kuondoa viongozi au kutochagua viongozi ambao umri wao kikanuni hauruhusiwi.

Akimkaribisha Katibu Mkuu, Mwenyekiti wa Umoja huo, Kheri James, aliwataka wajumbe wa kikao hicho kuchagua watu wenye sifa na uzalendo ndani ya chama na si kuchagua watu ambao ni vibaraka.

Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Raymond Mwangwala, alisema tangu Katibu Mkuu wa chama aanze kazi sasa ni siku 100 na kwamba amefanya mapinduzi na mabadiliko makubwa ndani ya chama.

Aliwataka vijana hao kuhakikisha wanatetea maslahi ya chama na taifa kwa ujumla badala ya kujikita kwenye mitandao ya kijamii na kwamba wawe mstari wa mbele kumtetea Rais John Magufuli kutokana na utendaji anaofanya.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Makontena ya Makonda kupigwa tena mnada leo

$
0
0
Makontena 20  yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ‘kwa ajili ya ofisi za walimu’, yanapigwa mnada kwa mara ya pili leo na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Jumamosi iliyopita, makontena hayo yalipigwa mnada lakini yalikosa wateja kutokana na wengi kushindwa kufikia bei iliyokuwa ikiuzwa ya Sh. milioni 60 kwa kontena moja.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Udalali Yono Action Mart, inayosimamia mnada huo, Scollarstika Kevela jana alisema mnada huo unaorudiwa kwa mara ya pili utafanyika kuanzia saa 3:00 bandarini eneo la Kurasini.

“Mnada huu utafanyika tena kesho (leo) na makontena yale yale 20 tutayanadi kwa wateja ingawa sijui kama yameongezeka kwa sababu TRA ndio wasimamizi wa mnada huu,” alisema Kevela.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images