Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TRA: Wafanyabiashara Msisubiri Tarehe Za Mwisho Kuomba Msamaha Wa Riba Na Adhabu Ya Kodi

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Wafanyabiashara wenye malimbikizo ya madeni ya kodi wametakiwa kutuma maombi ya msamaha maalumu wa riba na adhabu kwenye malimbikizo hayo mapema kabla ya tarehe 30 Novemba, 2018 ili waweze kunufaika na msamaha huo ambao umetolewa kwa lengo la kutoa unafuu kwa kuwapa fursa ya kulipa kodi ya msingi  ndani ya mwaka wa fedha wa 2018/19.


Wito huo umetolewa na Afisa Elimu Mkuu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Rose Mahendeka wakati wa semina elekezi kwa wafanyabiashara, wadau na washauri wa wafanyabiashara kuhusu msamaha huo iliyofanyika leo mkoani Tabora. 


"Nachukua fursa hii kutoa wito kwenu wafanyabiashara kutuma maombi ya msamaha wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya kodi ambapo mwisho wa kutuma maombi ya msamaha huu ni tarehe 30 Novemba, 2018," alisema Mahendeka. 


Mahendeka aliongeza kuwa "Mara nyingi wafanyabiashara huwa mnajitokeza mwishoni kabisa mwa tarehe zinazoonyesha mwisho wa kulipa, kuwasilisha au kutuma maombi fulani suala linalosababisha foleni na msongamano mkubwa katika kutoa huduma katika ofisi zetu. Nachukua fursa hii kuwaomba msisubiri tarehe za mwisho kuleta barua za maombi ya msamaha huu wa riba na adhabu ya madeni ya kodi na naomba mjue kwamba, huu ndio muda muafaka wa kila mwenye malimbikizo ya madeni kutuma maombi Ofisi ya TRA katika mkoa wake kikodi."


Naye, Afisa Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka hiyo Chama Siriwa alisema muombaji wa msamaha wa riba na adhabu ya malimbikizo ya kodi anapaswa kutoa maelezo na vielelezo vya ukweli na uhakika wakati wa uwasilishaji wa maombi yake.

"Kila muombaji anatakiwa kutoa taarifa za ukweli wakati anaomba msamaha huu na endapo itabainika kuwa muombaji ametoa taarifa za udanganyifu, Kamishna Mkuu anayo haki kisheria kubatilisha na hivyo kupelekea muombaji kupoteza sifa za kufaidika na  msamaha huu, " alifafanua Siriwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mihayo iliyopo mkoani hapa inayomilikiwa na Taasisi ya Dini ya Kanisa Katoliki Padri Salvatory Maganga, ameishukuru TRA kwa kutoa Elimu ya msamaha wa riba na adhabu ya madeni ya malimbikizo ya kodi na kuomba elimu hii iendelee kutolewa kwa wafanyabiashara katika maeneo mbalimbali nchini.

Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea kutoa elimu ya msamaha huu hususani kwa wafanyabiashara, wadau na washauri wa wafanyabiashara kwa lengo la kuwahamasisha kutuma maombi ya msamaha huu kabla ya muda uliopangwa haujamalizika ambao ni tarehe 30 Novemba, mwaka huu. 



Mwisho.
 

Benki Ya Standard Charted Kuimwagia Tanzania Sh. Trilioni 3.3 Kujenga Reli Ya Kisasa-SGR

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
BENKI ya Standard Chartered Group imekubali kuipatia Tanzania mkopo nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.46 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 3.3 kwa ajili ya kujenga kipande cha Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) kuanzia Morogoro hadi Makutupora, mkoani Dodoma.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw. Bill Winters, Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa kukubali kugharamia ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa ambayo lengo lake ni kuimarisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo kwenda bara na nchi jirani za Maziwa Makuu na zile ambazo hazipakani na Bahari.

"Tunajenga Reli hiyo ya Kisasa kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Makutupora ambazo ni awamu mbili lakini pia tutajenga reli hiyo kuelekea Isaka mpaka Mwanza na baadaye Rusumo ambapo wenzetu wa nchi ya Rwanda, tutasaidiana, wao watajenga reli hiyo kutoka Rusumo hadi Kigali" Aliongeza Dkt. Mpango

Aidha, Dkt. Mpango amemweleza Kiongozi huyo wa Juu kabisa wa Benki ya Standard Chartered Group anayeongoza Benki hiyo kwenye nchi zaidi ya 60 duniani, kuhusu vipaumbele vikubwa vya nchi ikiwemo kuboresha Shirika la Ndege la Taifa-ATCL, na Ujenzi wa Mradi Mkubwa wa Kufua Umeme wa Mto Rufiji.

"Tunaimarisha Shirika letu la Ndege ili kuimarisha sekta ya utalii kwa sababu tuna vivutio vingi na haipendezi wageni wanao kuja nchini wanafikia nchi jirani, sasa ifike wakati tuwe na uwezo wa kuwasafirisha moja kwa moja kuja nchini kwetu" Alisisitiza Dkt. Mpango.

Alisema Tanzania ni ya pili duniani kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii ikitanguliwa na Brazil lakini inapokea watalii wasiozidi milioni 2 kwa mwaka jambo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi kwa haraka ili sekta hiyo ichangie uchumi wa nchi kwa kiasi kikubwa kupitia fedha za kigeni.

Alisema katika kulifufua Shirika hilo la Ndege, tayari Serikali imenunua ndege nne ikiwemo ndege kubwa aina ya Boeing 787- 8 Dreamliner na kwamba ndege nyingine 3 zitakuwa zimewasili nchini ifikapo mwezi Juni, mwakani, na kulifanya shirika hilo kuwa na ndege 7. 

Alivitaja vipaumbele vingine kuwa ni kuboresha huduma za jamii kama vile elimu, afya, maji na kuendeleza ujuzi kwa wananchi ili waweze kufanyakazi kwenye viwanda na kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa ujumla kwa kuwa maendeleo yanahusu watu.

Akizungumza kwenye mkutano wake na Dkt. Mpango, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Group, Bw. Bill Winters, ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa kiuchumi na kwamba Benki yake itatoa mkopo huo na kuahidi kuwa balozi wa kuelezea mafanikio makubwa ya kiuchumi ya Tanzania kwa wadau wengine.

Aliahidi kuzishawishi taasisi nyingine za fedha ulimwenguni kuangalia uwezekano wa kuunga mkono jitihada hizo ambazo mwisho wake wanufaika wakubwa watakuwa ni wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla.

"Tunaimani kubwa na uwezo wa Tanzania pamoja na fursa nyingi za kiuchumi ilizonazo na kwamba miradi mingi ya kipaumbele iliyoainishwa itafikiwa na tunalo jukumu kama Benki kutoa fedha na kuiweka miradi hiyo pia sokoni ili iweze kupata fedha" Alisisitiza Bw. Bill Winters.

Katika kikao hicho, Bw. Bill Winters aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo nchini Kenya na nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki Bw. Lamin Manjang na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo nchini Tanzania Bw. Sanjay Rughani, ambapo pia Benki hiyo inafanya shughuli zake hapa nchini kwa kipindi cha miaka 101 sasa.

Mwisho

Tundu Lissu Kurejea Nchini Mwakani.....Kaka Yake Asema Risasi Iliyoko Ndani ya Uti wa Mgongo haitaondolewa

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine na ataendelea kubaki na risasi moja kwenye uti wa mgongo.

Hayo yameelezwa leo Agosti 29 na kaka yake Lissu, Wakili Alute Lissu, alipozungumza na wanahabari.

Amesema Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine baada ya kufanyiwa upasuaji zaidi ya mara nne akiwa Ubelgiji ingawa kuna risasi moja ambayo bado imebaki nyuma ya uti wa mgongo.

“Wakijaribu kuitoa huenda ikaathiri uti wa mgogo na hivyo kupata tatizo la kupooza,"amesema.

Lissu alihamishiwa hospitali ya Leuven iliyopo Ulelgiji akitokea hospitali ya Nairobi, baada ya kushambuliwa kwa risasi kadhaa na watu wasiojulikana Septemba 7 mwaka jana.

Alute ambaye amerejea nchini, wiki hii akitokea Ubelgiji kumjulia hali Lissu, amesema huenda mwanasiasa huyo akarejea nchini mwakani, hasa kutokana na mfupa wa mguu wa kulia kuwa bado haujaunga vizuri.

"Hali ya Lissu inaendelea vizuri, lakini napenda kukanusha taarifa kuwa kuna kamati ya mapokezi yake kwani, Lissu kwa hali yake hawezi kurejea nchini hivi karibuni, kutokana na kuendelea na matibabu nje ya hospitali,’’ amesema.

Wakili Mughwai amesema bado Lissu hajapata ruhusa ya moja kwa moja kutoka kwa daktari wake hivyo atakuwa akipatiwa huduma kwenye nyumba aliyopanga jirani na hospitali hiyo ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji.

"Haiwezekani kurudi karibuni, mimi nadhani labda mwakani hasa kutokana na kuhitaji uangalizi wa daktari wake, ingawa yeye binafsi na hata sisi wanafamilia tungependa arudi mapema,"amesema.

Amesema risasi hiyo imeachwa kwa sababu haina athari kwa maisha ya Lissu, kwani si mara ya kwanza, wagonjwa kubaki na risasi mwilini kwani itasababisha madhara makubwa zaidi kama ikitolewa.

Hata hivyo, Wakili Mughwai amesema wanashukuru sana Watanzania wote wakiwepo wanaoishi Ubelgiji kutokana na michango wanayotoa kumsaidia Lissu na kwenda kumjulia hali nchini Ubelgiji.

Chadema kumshtaki Waitara

$
0
0
Chama cha Demokrasia Maendeleo (Chadema) kimempeleka kwenye kamati ya maadili mgombea ubunge wa jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CCM, Mwita Waitara kwa kile walichodai kufanya uchochezi.

Akizungumza leo Agosti 29, mkurugenzi wa oparesheni na mafunzo wa Chadema, Dingo Kigaila kuwa amesema sababu ya kumpeleka kwenye kamati hiyo ni kutokana na madai ya kuhamasisha vurugu kwa kupitia mtandao wa kijamii.

Amesema kwa kutumia simu yake ya kiganjani Agosti 26 mwaka huu aliandika kwamba watu wa kabila lake yaani Wakurya hususani ukoo wa Wairegi wanoe mapanga yao na kumwaga damu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi jimbo la Ukonga.

Amesema Waitara alitumia lugha ya Kiswahili na Kikurya kuandika ujumbe huo, hivyo wameitaka kamati ya maadili, kumuita na kumuhoji mgombea huyo.

Julai 28, 2018 Mwita Mwikwabe Waitara, alitangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge na kujivua nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA na kuhamia CCM.

Waziri Mkuu: Flyover Ya Tazara Imekamilika Kwa Asilimia 98

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesemaujenzi wa barabara ya juu katika eneo la Tazara umekamilika kwa asilimia 98 na itafunguliwa Oktoba mwaka huu na Rais Dkt. John Magufuli.

Mradi wa barabara ya juu (Mfugale flyover) chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani, unalengo la kupunguza msongamano wa magari katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere.
 
Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 29 ,2018) baada ya kukagua ujenzi wa mradi huowa barabara ya juu katika eneo la Tazara jijini Dar Es Salaam.

Waziri Mkuu amesema ameridhishwa kazi ya umaliziaji wa mradi huo inayoendelea kwenye hilo.

“Mradi utapunguza muda wa usafiri katika barabara ya Nyerere hususani  kwa wananchi wanaotoka katikati ya jiji kwenda uwanja wa ndege na wanaotoka Buguruni, Temeke.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi Mkoa wa Dar Es Salaam watafute eneo kwa ajili ya  wafanyabiashara ndogondogo ili waweze kuondoka kandokando ya barabara hizo za juu zinazojengwa.

Waziri Mkuu ameyasema hayo baada ya kukagua ujenzi wa barabara za juu (interchange) eneo la Ubungo, katika makutano ya barabara za Morogoro, Mandela na Sam Nujoma, eneo la Ubungo jijini Dar Es Salaam.

Amesema ni vema wafanyabiashara hao wakaondolewa na kutafutiwa eneo lingine ili kulinda usalama wao kutokana na kazi za ujenzi zinazoendelea kwenye maeneo hayo. Pia amewataka viongozi hao wawaelekeze wananchi maeneo watakapowahamishia wafanyabiashara hao ili waweze kwenda kununua bidhaa.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema mradi huo nao unalengo la kupunguza msongamano wa magari kwa kutenganisha njia za barabara za Morogoro, Mandela na Sam Nujoma ili kuwa na ngazi mbili juu ya barabara za sasa.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema ujenzi wa mradi wa barabara ya juu katika eneo la Tanzara (Mfugale flyover) unagharimu sh. bilioni 100.52 na unajengwa na kampuni  ya Sumitomo Mitsui ya nchini Japan.

Amesema mradi huo umezingatia jinsi ya kuwezesha muunganiko wa mfumo wa usafiri jijini Dar Es Salaam na ule wa mabasi yaendayo haraka awamu ya pili, tatu na ya nne. “Tumeacha eneo la mita 12 katikati ya barabara kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, AGOSTI 28, 2018.

Halima Mdee amuunga mkono Waziri Mpango Sakata la Makonda....."Laana ya KuKu haiwezi mpata Mwewe"

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Halima Mdee ameunga mkono agizo la Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango la kupiga mnada makontena 20 ya mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.

Kupitia mtandao wake wa Twitter ameunga mkono agizo hilo huku akiwataka wananchi kujitokeza kununua samani hizo kama ambavyo Waziri Dkt.Mpango aliwataka watu wenye uwezo wa kununua wajitokeze bila kuogopa chochote.

“Wenye pesa zenu mnada ukipigwa jongeeni kwa wingi, laana ya kuku haiwezi mpata mwewe,” ameandika Mdee kwenye ukurasa wake wa Twitter

Aidha, Dkt. Philip Mpango, Agosti 27, 2018 aliagiza makontena 20 ya samani yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yapigwe mnada ikiwa ni sehemu ya kusimamia sheria na kanuni za kodi zilizopo nchini.

Hata hivyo, tangazo la TRA lililotolewa na Kaimu Kamishna wa Forodha na Ushuru, Ben Asubisye lilikuwa na orodha ya makontena zaidi ya 800, huku jina la Paul Makonda lilijitokeza mara 20 akiwa mpokeaji wa makontena 20 yaliyopo katika bandari kavu ya (DICD).

Waziri Mkuu: Dawa Ya Kuua Viluilui Itumike Kutokomeza Maralia

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa mikoa yote nchini waendeleze kampeni ya kutokomeza ugonjwa malaria kwa kutumia dawa ya kuua viluilui vya mbu.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 29, 2018) alipofanya ziara katika kiwanda cha kutengeneza dawa ya kuua viluilui vya mbu kilichopo katika wilaya ya Kibaha mkoani Pwani.

Amesema nchi inakabiliwa na matatizo makubwa ya ugojwa wa malaria, hivyo ni vema viongozi wa mikoa wakatokomeza viluilui vya mbu kwa kuwa dawa inatengenezwa nchini.

Waziri Mkuu amesema kiwanda hicho cha Labiofam ni cha pekee barani Afrika kwa kuwa na uwezo wa kutengeneza dawa za aina hiyo.”Tutumie fursa hii kutokomeza maralia nchini.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa kiwanda hicho kutumia vyombo vya habari  kwa kuandaa vipindi vya kuelimisha umma kuhusu dawa wanayozitengeneza.

Amesema wananchi wanatakiwa kuelimishwa juu ya umuhimu wa kutumia dawa hiyo kwa ajili ya kuua viluilui katika maeneo ya makazi yao ili kuutokomeza ugonjwa wa maralia nchini.

Naye,Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho, Bw. Aggrey Ndunguru amesema dawa zinazotengenezwa kiwandani hapo zina uwezo wa kuua viluilui vya mbu tu na haina madhara kwa binadamu.

Amesemma dawa hiyo ambayo ipo katika ujazo tofauti tofauti inaweza kuwekwa kwenye makaro ya vyoo, maji yaliyotuama pamoja na katika matanki ya maji ili kuua viluilui.

Katika ziara hiyo Waziri Mkuu alifuatana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo na maafisa wengine wa Serikali.

Mzee Mwinyi Amuombea Dua Na Kumjulia Hali Dkt.kigwangalla MOI

$
0
0
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi leo Agosti 29,2018 amemtembea na kumuombea dua maalum Dkt Hamisi Kigwangalla ambaye anapata matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI akiuguza majeraha ya mkono aliyopata katika ajali iliyotokea Agosti 4, mwaka huu Mkoani Manyara.

Mzee Mwinyi aliambatana na Mkewe Bi. Siti Mwinyi ambapo wamemjulia hali pamoja na kufanya dua hiyo ili aweze kupona haraka kurejea kwenye majukumu yake ya kitaifa.

“Nimefika leo kukujulia hali na upokee dua hii upone haraka. Sisi tunaendelea kukuombea muda wote kwa muumba” alieleza Mzee Mwinyi.

Kwa upande wake Dkt. Hamis Kigwangalla amemshukuru Mzee Mwinyi na Mama Mwinyi kufika kumjulia hali ambapo awali alimuelezea kuwa anaendelea vizuri na muda wowote ataruhusiwa.

“Nashukuru kufika kwenu na sasa naendelea na mzoezi vizuri huku kubwa nikisubiria ruhusa ya Madaktari wanaoendelea kunipatia matibabu” alieleza Dkt. Kigwangalla.

Katika hatua nyingine kwa sasa Dkt. Kigwangalla afya yake imeendelea kuimarika zaidi ambapo jana jioni ya Agosti 28, ameweza kutembea umbali wa zaidi ya Kilometa Nane ambapo hii ni hatua nzuri kwani kila siku amekuwa akiongeza umbali wa kutembea kwa lengo la kufanya mazoezi ya viungo vyake.

Dkt Kigwangalla alihamishiwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI tarehe 12/08/2018 baada ya kupata matibabu ya awali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kwa sasa bado anaendelea na tiba kuuguza mkono wake wa kushoto.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Agosti 30

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE;LUKUBA 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Diwani Kortini Kwa Tuhuma za Wizi

$
0
0
Jeshi la Polisi wilayani Iramba, Mkoa wa Singida, limewafikisha mahakamani watu 19 wakazi wa Kijiji cha Nguvumali, kwa tuhuma ya kuiba vifaa vya ujenzi wa Kituo cha Afya Ndago.

Miongoni mwa waliofikishwa katika Mahakama hiyo ya Wilaya ya Iramba juzi ni Diwani wa Kata ya Ndago, Henry Nkhandi na Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho, Yasin Nyawangele.

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Salumu Nannume, aliiambia mahakama hiyo mbele ya Hakimu Makwaya Charles, kwamba washtakiwa hao walitenda kosa hilo Agosti 3, mwaka huu baada ya kuvunja stoo ya vifaa vya ujenzi na kuiba vifaa hivyo.

Mwendesha Mashtaka Nannume aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Emmanuel Shalua (40), Diwani Nkhandi, Anton Mkumbo (43), Geofrey Selemani (43), Joseph Kitila (50), Shamir Ramadhani (23), Amos Nkana (45) na Rachel John (46).

Wengine ni Jackline Shabani (35), Grace Lyanga (56), Uswili Jackson (54), Elisha Tertlano (52), Maria Yohana (34), Kidyson Kidindima (49), Hawa Swahehe (35), Babu Musa (22), Catherine Songelaeli(35), Emanuel Manase (23) na Yasini Nyawengele ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ndago.

Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka huyo, watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Agosti 3, mwaka huu, majira ya usiku ambapo walivunja stoo na kuiba vifaa vya ujenzi wa Kituo hicho cha Afya Ndago vyenye thamani ya Sh milioni 9.8.

Alivitaja baadhi ya vifaa hivyo kuwa ni saruji, nondo, vigae, mbao na vifaa vingine.

Washtakiwa hao walikana mashtaka na wako nje kwa dhamana hadi Septemba 10, mwaka huu, kesi yao itakapotajwa tena.

Vigogo Benki Ya Posta Watupwa Jela Miaka Mitano.

$
0
0
VIGOGO wawili wa Benki ya Posta Tawi la Tabora na mfanyabiashara mmoja  waliokuwa wanakabiliwa na jumla ya mashitaka saba ikiwemo utakatishaji wa zaidi ya shilingi milioni 700 wametupwa jela miaka mitano au kutakiwa  kulipa faini ya shilingi milioni mia moja (100).

Mbali ya adhabu hiyo Mahakama hiyo baada ya kuwatia hatiani  imewataka  washitakiwa hao kulipa shilingi milioni 710 walizoziibia Benki ya Posta na vinginevyo mali zao zitaifishwe na serikali kufidia kiasi cha fedha zilizoibwa.

Uamuzi wa shauri hilo la jinai namba 154/2015 umetolewa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Tabora Jocktan Rushwela baada ya kuwatia hatiani washitakiwa hao kwa makosa matatu kati ya saba.

Vigogo wa benki ya Posta  Tabora waliopata adhabu hiyo ni Boaz Lunyungu aliyekuwa meneja, George Ngatunga(mhasibu) na mfanyabiashara Umaiya Makiliga.

Katika hukumu hiyo iliyosomwa kwa saa mbili  Hakimu Rushwela aliwatia hatiani watuhumiwa hao kwa makosa matatu kati ya saba waliyokuwa wanashitakiwa nayo ambayo ni kula njma ya kutnda kosa la wizi, kutakatisha fedha na wizi.

Awali upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili mwandamizi wa Serikali Shedrack Kimaro aliiambia Mahakama hiyo kuwa watuhumiwa walitenda makosa hayo kati ya Januari 2014 na julai 2915 katika benki ya posta tawi la Tabora.

Wakili Kimaro alidai  kwenye shitaka la kwanza kuwa katika kipindi hicho washitakiwa kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la wizi.

Ilidaiwa na wakili Kimaro kuwa washitakiwa wote watatu katika tarehe tofauti kati ya mwezi Januari 2014 na mwezi julai 2015 waliiba jumla ya shilingi milioni 710 katika benki ya Posta tawi la Tabora.

Shitaka la tatu ambalo lilikuwa likiwakabili aliyekuwa meneja na Mhasibu wake ilidaiwa kuwa wakiwa ni watumishi wa benki wa Posta walitakatisha fedha shilingi milioni 710 huku wakijua wamezipata kwa njia zisizo halali.

Upande wa jamuhuri wakati wa usikilizwaji wa shauri hilo ulileta jumla ya mashahidi 16 ambao waliweza kutoa ushahidi uliopeleka mahakama kuthibitisha pasipo shaka kwamba watuhumiwa walitenda makosa hayo.

Mahakama imewahukumu kwenda jela miaka mitatu mitatu kwa kosa la kula njama na lile la wizi na miaka mitano kwa kosa utakaktishaji wa fedha, kwa vile adhabu hizo zinakwenda pamoja watutumikia kifungo cha miaka mitano jela.

Washitakiwa hao watatu pamoja na kupata adhabu hiyo ya kifungo bado wanakabiliwa na kesi nyingine ya kuhujumu uchumi wakiwa na watu wengine 13 shauri amabalo bado halijaanza kusikilizwa kwani jalada lake lipo ofisini kwa DPP likisubiri kutolewa uamuzi.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Madiwani Watano wa CHADEMA, CUF Watimkia CCM

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
Madiwani watano wa vyama vya upinzani ikiwemo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA, CUF na ACT Mzalendo na viongozi wengine sita wamevikimbia vyama hivyo na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani.
 
Madiwani hao ni pamoja na Ramadhan Lutambi aliyekuwa diwani wa kata ya Mailmoja kupitia Chadema na Ramadhan Kombe aliyekuwa diwani  kata Mbwawa kupitia ACT. 
 
Wengine ni, Muharami Mkopi Cuf kata ya Ruaruke wilayani Kibiti,Seif Lwambo kupitia Cuf kata ya Beta,Muharami Mketo Cuf Kata ya Lukanga na Mwenyekiti wa Kijiji cha Lukanga.
 
Aidha viongozi waliojiuzulu kwenye vyama hivyo ni Ayubu Chapile ambae alikuwa katibu kata ya Mkuza (CUF) ,Karimu Kasimu katibu tawi chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere (Chadema) ,Selemani Mwinyimkuu mwenyekiti tawi (Cuf),David Mramba Act,Latifa Sangalala mwanachama Chadema Mkoani B na Jumanne Urembo Diwani kivuli ACT kata ya Sofu.
 
Awali Ramadhani Lutambi alisema ,chama kinachofaa kuongoza nchi daima ni CCM kwani vyama vingine havina uwezo,na havijali  viongozi wa ngazi za chini .
 
Alifafanua ,ameamua kuondoka Chadema ili kutekeleza yale yanayofanywa na Rais Dk. Magufuli kwa wananchi wanyonge.
 
Lutambi alikiri kuondoka Chadema kwa hiari yake, kwa akili zake timamu na kudai anajivua vyeo vyote alivyonavyo kuanzia sasa. 
 
Akiwapokea madiwani na viongozi wa vyama hivyo kwenye ofisi za CCM Mkoa, mwenyekiti wa CCM mkoani Pwani, Ramadhani Maneno alisema ,kutokana na utekelezaji mzuri wa ilani wameona hakuna sababu ya kubaki kwenye vyama vyao.
 
Alisema kazi kubwa inayofanywa na chama kupitia Rais Dk .John Magufuli ndio sababu kubwa ya madiwani na viongozi hao kukimbilia CCM. 
 
“Baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha kuwa wabunge,madiwani na viongozi wanaohamia CCM wananunuliwa ,suala hili halipo ,ni kwamba wanarudi kutokana na utendaji kazi wa chama chetu,” alisema Maneno.
 
Maneno alieleza, viongozi hao hawanunuliwi wala kuhongwa bali ni mapenzi yao .
 
“Kuhusu gharama za uchaguzi kuwa ni kubwa hilo ni suala la Tume ya uchaguzi na chama kisilaumiwe kwani kuhama kwao hakuhusiani na kurubuniwa ,” alisema Maneno.

Anna Mghwira Akabidhiwa Rasmi Kadi ya CCM

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemkabidhi rasmi kadi ya uanachama wa chama hicho mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira ambaye alijiunga na chama hicho Desemba 2017.

Mghwira alijiunga na CCM, Desemba 8, 2017  katika mkutano wa Umoja wa Wanawake wa CCM Tanzania (UWT), mjini Dodoma akitokea Chama cha ACT-Wazalendo, mkutano ambao Rais John Magufuli alikuwa mgeni rasmi.

Tangu wakati huo, alikuwa hajakabidhiwa rasmi kadi ya uanachama, hadi jana jioni Jumatano Agosti 29, 2018 alipokabidhiwa kadi ya uanachama na viongozi wa CCM kata ya Kilimanjaro, kata ambayo ndio anaishi.

Viongozi waliomkabidhi kadi hiyo ni Mwenyekiti wa CCM kata ya Kilimanjaro, Ernest Mlembezi, Diwani wa kata hiyo, Priscus Tarimo na Katibu wa tawi la Mawenzi, Joyce Mchome..

Mghwira ambaye alikuwa mwenyekiti wa Taifa wa ACT-Wazalendo, aliwahi kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa 2015, ambapo Rais John Magufuli aliibuka mshindi.

Juni 3, 2017, Rais Magufuli alimteua kuwa mkuu wa mkoa Kilimanjaro, kuchukua nafasi ya Said Meck Sadiki ambaye alitangaza kustaafu.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Asha Baraka Ampigia Magoti Rais Magufuli

$
0
0
Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ inatarajia kuadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake.

Katika maadhimisho hayo bendi hiyo imeandaa tamasha kubwa la muziki wa dansi litakalofanyika 29 Septemba Ukumbi wa Club Legend (zamani Nyumbani Lounge).

Mkurugenzi wa bendi hiyo, Asha Baraka, amewaambia waandishi wa habari kwamba katika maadhimisho hayo bendi ya Twanga Pepeta itafanya shughuli mbalimbali za kijamii kama ishara ya kuwashukuru mashabiki zake.

“Tunakusudia kutembelea Hospitali ya Mwananyamala, tutatoa pia majaketi nakishi (Jacket reflectors) kwa madereva wa pikipiki, hii ni maalum kwa kumuenzi muimbaji wetu, Abdul Semwando aliyefariki kwa ajali ya pikipiki pia tutatembelea vituo kadhaa vya watoto yatima,” amesema Asha.

Mkurugenzi huyo pia ametuma maombi kwa Rais John Magufuli ili aruhusu wanamuziki wa dansi wapige muziki kama zamani zaidi ya saa sita usiku kwa kuwa muziki ndiyo ajira ya vijana wengi.

Naye kiongozi wa bendi, Luiza Mbutu amesema bendi hiyo imezuia baadhi ya waliokuwa wanamuziki wake kurudi katika bendi hiyo kwa kuwa wataua bendi walizopo.

Hata hivyo, Asha Baraka ametoa onyo kwa watu wanaoiba na kuweka nyimbo za bendi ya Twanga Pepeta kwenye mitandao yao bila ridhaa yao huku akionya pia wasanii  wanaocheza nyimbo zao mikoani  kwa kuwa wanakiuka sheria ya haki miliki.

Mangula Azindua Kampeni Za Ubunge Monduli.....Jina la LOWASSA latawala

$
0
0
Makamu mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula jana amezindua kampeni za ubunge wa Monduli jijini Arusha huku, jina la Lowassa likitawala.

Wakizungumza katika mkutano wa kampeni hizo, zilizofanyika uwanja wa soko la Monduli, viongozi wengi wa CCM isipokuwa, Mangula walilazimika kulitaja jina la Lowassa wakati wakieleza sababu za aliyekuwa mbunge wa Chadema wa jimbo hilo kujiunga na CCM.

Viongozi hao walirejea kauli zao kuwa, Lowassa yupo njiani kurudi CCM na waliohama wamemtangulia tu.

Edward Lowassa ni waziri mkuu wa zamani ambaye alihamia Chadema mwaka 2015 na jana alikuwa Mto wa Mbu jimboni humo akizindua kampeni za Ubunge kwa kumnadi Yonas Laiser.

Aliyekuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Monduli na Diwani wa Monduli mjini, Isack Joseph ambaye hivi karibuni alijiuzulu udiwani na kujiunga CCM, alisema kabla ya uamuzi huo alikwenda mara tatu kuonana na Lowassa.

Joseph alisema katika safari zake kwa Lowassa alimweleza ni vigumu kwao kama madiwani wa Monduli kuendeleza maendeleo aliyoacha kwani wapo upinzani. Alisema alichomwambia muda bado wa wao kuondoka Chadema wasubiri hadi mwaka 2019.

"Mimi ndiye nilikuwa rafiki wa karibu wa Lowassa hapa Monduli, nilimwambia, sisi kuendelea kuwa Chadema ni kuwaumiza wananchi kwani hakuna msaada wowote kutoka Chadema," alisema.

Alisema Chadema inapokea ruzuku zaidi ya Sh390 milioni kila mwezi lakini imeshindwa hata kuajiri makatibu wa wilaya ama kujenga hata zahanati.

"Tumeamua kurejea CCM kujali maslahi ya wana Monduli na wala hatujamsaliti Lowassa kwani na yeye yupo njiani anakuja" alisema.

Kwa upande wake, mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kama ambavyo amekuwa akieleza, Lowassa yupo njiani kurudi na watampokea.

Alisema Lowassa anawachezea wananchi wa Monduli kwani anajua yeye bado ni waziri mkuu mstaafu ambaye anatembelea gari la Serikali, analindwa na walinzi wanaolipwa na Serikali.

Alisema yeye kama mkuu wa mkoa ni mjumbe wa kamati ya siasa mkoa hivyo, atawashangaa ambao watashangaa kumuona jukwaani akimnadi mgombea wa CCM.

Naye, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Loota Sanare alisema anawataka wananchi wa Monduli kumchagua Julius Kalanga na kuachana propaganda.

Alisema kama Lowassa angekuwa anawatakia maendeleo wananchi wa Monduli angegombea yeye ama mtoto wake, Fred Lowassa.

Aliwataka wakazi wa Monduli kutorejea makosa kuchagua upinzani kwani sasa wanapaswa kuonyesha wanamuunga mkono Rais John Magufuli kutokana na kazi nzuri anayofanya.

Meneja Kampeni za ubunge Monduli, William Ole Nasha alisema katika kampeni hizo wabunge 16 watashiriki kumnadi mgombea wakiwamo mawaziri.

Alisema Kalanga alikuwa na kila sababu kuhama Chadema kwani mambo mengi ya maendeleo ikiwemo kutatua kero za maji, umeme na migogoro ya ardhi yalikwama.

Akizindua kampeni, Mangula alisema kumekuwepo na maneno ambayo si sahihi  kuwa taratibu za chama zinakiukwa kupitishwa wagombea bila kura za maoni

"Hakuna taratibu zilizokiukwa, kama kunakuwa na mgombea mmoja hakuna haja ya kura za maoni," alisema.

Mangula alisema chama kinatazama mgombea ambaye anaungwa mkono na wengi na kueleza katika uchaguzi uliopita, Kalanga alipata kura 35,000 na kuwashinda wengine.

Mangula aliridhishwa na umati wa wanaccm waliojitokeza kwenye kampeni hizo na mapokezi makubwa waliyompa.

"Mwenyekiti wetu Rais John Magufuli aliniomba nije kuzindua kampeni na alinipa heshima kubwa na nyie nawashukuru kutuunga mkono," alisema.

Alisema katika uchaguzi huo hawashindanishi Ilani za uchaguzi kwani tayari ilani iliyopo ni ya CCM ambayo ndio mipango yake imepitishwa na wabunge.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara akisalimiana na Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Jimbo la Monduli, Bw.Julius Kalanga Laizer akisaimiana na wananchi waliofika katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge jimbo la Monduli uliofanyika jana  jimboni humo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara akimnadi  Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi CCM  Jimbo la Monduli, Bw.Julius Kalanga Laizer akisaimiana na wananchi waliofika katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge jimbo la Monduli uliofanyika jana jimboni humo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni  za Ubunge Jimbo la Monduli, Bw. Julius Kalanga Laizer akisaimiana na wananchi waliofika katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge jimbo la Monduli uliofanyika jana  jimboni humo.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge jimbo la Monduli jana

Lowassa Amnadi Mgombea CHADEMA Monduli...Ampongea Lugola Kuzuia Ma DC, RC Kukamata Watu Hovyo

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kipo imara na kitashinda jimbo la Monduli.

Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema amesema hayo  jana wakati akizindua kampeni za jimbo la Monduli, katika Kata ya Mto wa Mbu, akiwataka wananchi kupuuza propaganda kuwa Chadema itakufa.

Lowassa huku akielezea maendeleo aliyoleta Monduli katika kipindi chake cha ubunge cha miaka 20, alisema aliingia ubunge wa Monduli kukiwa na shida ya maji, barabara, umeme na ardhi lakini alishughulikia na leo kila Mtanzania anajua.

Amesema kumekuwapo na maneno kuwa amerejea Monduli kulinda ngome ya Chadema jambo ambalo siyo sahihi.

"Chadema bado tupo imara na tutashinda," alisema Lowassa huku akishangiliwa

Lowassa alisema kitendo cha kujiuzulu aliyekuwa mbunge wa Monduli, Julius Kalanga kilikuwa cha hovyo na kimemuudhi na kumkasirisha sana.

“Ni aibu kubwa, siku hiyo alipokuwa anahama nilipata taarifa nikampigia simu akasema hapana mzee.

"Kinachoniudhi siyo kuondoka kwake bali sababu alizotoa kuwa eti Monduli hakuna maendeleo aseme alishindwa kuvaa viatu vyangu," alisema.

Alisema ajitokeze Kalanga kutaja wilaya yenye maendeleo kama Monduli, kwa sababu ina barabara na shule kila kata.

"Hivi huyu ana akili kweli, Monduli hatuna hospitali tumejenga hospitali ya kisasa Monduli nzuri sana kuliko pengine." alisema.

Katika mkutano huo, Lowassa ameunga mkono, tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kuzuia polisi kutekeleza maagizo ya wakuu wa wilaya na mikoa kukamata watu bila sababu za msingi.

Alisema kumekuwapo na matukio ya kukamatwa watu bila sababu za msingi, hivyo uamuzi wa Lugola unapaswa kupongezwa.

Lowassa amewataka wakazi wa Monduli, kumchagua mgombea na Chadema, Yonas Laiser kwani ndiye atawaletea maendeleo.

Naye Laiser ameomba wananchi kumchagua kwani anajua kero zao na atashirikiana na Lowassa na madiwani kuzitatua.

Hata hivyo, alisema amekuwa akifuatwa kutakiwa kujiuzulu kugombea ubunge na udiwani na atapewa cheo serikalini lakini amegoma.

Makontena ya Makonda Kupigwa Mnada Tena Jumamosi Hii

$
0
0
Mnada wa pili wa makontena 20 yenye samani zikiwamo   meza na viti, yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, utafanyika Septemba Mosi baada ya ule wa Agosti 25 kutofanikiwa kupata wanunuzi.

Makontena hayo ambayo yamekwama bandarini yanadaiwa kodi ya Sh bilioni 1.2.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa (TRA), Richard Kayombo, amesema mamlaka hiyo imeazimia kufanya mnada wa pili Jumamosi ya wiki hii.

Alisema mnada huo utaanza saa 2:00 asubuhi kwa kufuata taratibu zote za sheria kama mnada wa awali ulivyofanyika, hivyo wananchi wanapaswa kujitokeza kwa ajili ya kununua samani hizo kwa kufuata taratibu na sheria za minada.

Alisema TRA haiwezi kutangaza bei ya mnada huo kabla ya kufanyika kwa sababu ni siri, lakini wateja watakaofika watakuta bei ambayo imepangwa kwa mujibu wa sheria serikali iweze kupata mapato yake.

Aliwaomba wananchi kuondoa hofu kuhusu samani hizo na kuwataka kujitokeza waweze kununua samani hizo.

Baada ya mnada wa Agosti 25 kukwama kwa wateja kushindwa kufikia bei iliyotangazwa, Makonda alijitokeza na kusema mtu atakayenunua makontena hayo aliyosema yana samani za shule za Dar es Salaam, atalaaniwa na Mungu.

Baada ya kauli hiyo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, alimjibu Makonda   akisema makontena hayo yatapigwa mnada mteja atakapopatikana na wala hatishiki na laana zozote.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images