Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Amjlia Hali. Dr Hamisi Kigwangala

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amjulia hali.Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla,  leo Agosti 26/2018 .akiwa anaendelea kupatiwa  matibabu katika Wodi aliyo lazwa ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa,  Muhimbili (MOI),

PICHA NA OFISI  YA WAZIRI MKUU

Video Mpya : WCB Wasafi ft. Diamond Platnumz, Mbosso & Lavalava - JIBEBE

$
0
0
Video Mpya : WCB Wasafi ft. Diamond Platnumz, Mbosso & Lavalava - JIBEBE 
==>>Itazame hapo chini

Mikakati Iliyowekwa na Kiwanja cha Ndege cha Kmataifa cha Julius Nyerere (JNIA) Katika Kukabiliana na Ugonjwa wa Ebola

$
0
0
Kitengo cha Afya katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) kimeweka udhibiti madhubuti wa kujikinga na usambazaji wa magonjwa ambukizi ukiwemo ugonjwa wa Ebola. 

Ugonjwa wa Ebola unaosambazwa kwa virusi vya Ebola, husababisha homa kali inayoweza kuambatana na kutokwa damu mdomoni, puani, masikioni, machoni na sehemu nyingine za wazi na unaenea kwa haraka.

Hivi karibuni umetangazwa kutokea nchini Kongo na kusababisha vifo. 

Akizungumzia kuhusiana na mikakati hiyo ya kupambana na magonjwa ambukizi ukiwemo wa Ebola, Afisa Afya Mfawidhi wa JNIA, Dk. George Ndaki amesema wanatoa mafunzo kwa watumishi na wahusika wote wanaotumia kiwanja hicho katika kujikinga na magonjwa hayo.

 “Sisi tumejiandaa vizuri na tumeshafanya jitihada zote tumeshatoa maelekezo, mafunzo na kamati mbalimbali za kiwanja zimejipanga kudhibiti magonjwa yote ya kuambukiza, ikiwemo sisi wenyewe kujikinga na kuwakinga na abiria wote wanaotoka katika nchi hatarishi”, amesema Dkt. Ndaki.

 Aidha akizungumzia kuhusiana na utaratibu ambao Kiwanja kimeweka ili kuhakikisha abiria wenye maambukizi wanapokelewa kwa tahadhari, ambapo wanapowasili na ndege zinazotoka nje ya nchi zinazopakia abiria wanaosafiri kutoka katika nchi zinazoshirikiana na Kongo hutakiwa kusafisha mikono kwa dawa maalum mara waingiapo katika eneo la kuwasili.

 Pia abiria hao wanapoingia katika lango la kuwasili la abiria kutoka nje ya nchi, kumekuwa na mashine maalum inaangalia joto la mwili na likizidi nyuzi joto 38 wanamtaka kutoa maelezo Zaidi ya afya yake.

 “Abiria wote wanapowasili hupita katika eneo maalum ambalo wote hutakiwa kuosha mikono, lakini pia kuna mashine ambazo zimewekwa ili kuweza kuwatambua abiria ambao wanawasili wakiwa na hali ya joto isiyokuwa ya kawaida mfano kuwa na joto la juu sana kuanzia 38oC, ukiachana na hilo kuna fomu maalum ambazo abiria wanapowasili hujaza na pia taarifa kutoka kwa rubani wa ndege kama kuna abiria ana maambukizi kwenye ndege.

Baada ya kumtambua mgonjwa basi atapitishwa katika njia ya tofauti na abiria wengine na kupakiwa katika gari la wagonjwa na kupelekwa Temeke Hospital,” amesema Dk. Ndaki.

 Naye Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha akitoa ufafanuzi juu taarifa za uwepo wa ugonjwa wa Ebola, ameeleza kuwa tayari JNIA wanazo taarifa za mlipuko wa ugonjwa huo na taratibu zote zimeshachukuliwa kwa kuwakagua abiria wanaotoka nje ya nchi.

 “Kwanza kabisa kwa abiria wote ambao wanatokea katika nchi ambazo zinasadikika kuwa na maambukizi wanapowasili wanakuwa sanitized (wanaosha mikono na dawa maalum) ili wasiweze kuleta maambukizi ndani, lakini pia tuna thermo scanners (mashine ambazo zinaangalia hali ya joto la mtu) anapowasili ambapo tunapogundua mgonjwa anamatatizo tunapeleka isolation (Chumba cha wagonjwa wa kipekee) na baada ya hapo anapelekwa katika vyumba vya waonjwa waliotengwa katika hospitali ya Temeke” alibainisha Bw. Rwegasha.

 Katika hatua nyingine Dk. Ndaki amesema mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote ambaye amebainika kuwa na ugonjwa wa Ebola kupitia JNIA. Dk Ndaki ametaja namna ya kujikinga na ugonjwa wa Ebola ni pamoja na kuepuka kugusa damu, machozi, jasho, matapishi, kamasi, mkojo au kinyesi cha mtu mwenye dalili za ugonjwa; pia mtu hatakiwi kugusa, kuosha au kuzika maiti ya aliyekufa kwa Ebola; pia usiguse au kula wanyama kama popo, sokwe au swala wa msituni.

 Dalili za Ebola ni pamoja na homa kali, maumivu ya kichwa na misuli, mwili kulegea, kutapika, kuharisha, vipele ma kutokwa damu

 “Natoa wito tu kwa wananchi kuhakikisha wanafuata taratibu zote tulizoziweka ili kuhakikisha kwamba hatupati mgonjwa yeyote katika nchi yetu.

Kama kila mtu atatekeleza wajibu wake kwa abiria kufuata taratibu, wanaosimamia masuala ya afya wakitimiza wajibu wao, na Kiwanja kikitimiza wajibu wake basi hakika magonjwa ya mlipuko hayataweza kufika katika nchi yetu” alieleza Dkt. Ndaki.

Alichokisema Waziri Mkuu Baada ya Kumtembelea Dkt. Kigwangalla MOI Leo

$
0
0
 Na Andrew Chale
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Kassim Majaliwa leo Agosti 26,2018 amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya mifupa MOI, hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Hii inakuwa ni kwa mara ya pili kwa Waziri Mkuu Majaliwa kumtembelea kumjulia hali ambapo awali alimtembelea Jumapili ya Agosti 5, 2018), wakati Dkt. Kigwangalla akipatiwa matibabu ya awali katika Wodi ya Mwaisela. Akiwa wodini hapo, Waziri Mkuu Majaliwa amemtakia kila lakheri katika kuuguza mkono wake ambapo pia amepata kuzungumza nae juu ya maendeleo ya afya yake.
 
Aidha, Waziri Majaliwa amewashukuru Madaktari wa MOI pamoja na uongozi wake kwa pamoja kutoa huduma bora kwa watanzania na raia wa Nchi za nje ambao wamekuwa kimbilio kuja nchini kupata tiba.

“Nakutakia kila lakheri Kigwangalla. Nimekuja baada ya kusikia umefanyiwa operesheni ya pili. Pia nawashukuru Uongozi na Madaktari wetu wa hapa MOI kwa kutoa tiba nzuri tiba zenu kwa sasa zimezifanya nchi zingine wananchi wake kukimbilia hapa. Viongozi wakuu pia Hospitali hii ndio kimbilio letu kwa sasa na tunawashukuru kwa huduma bora inayofanya Nchi kuwa na heshima kuwbwa,” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
 
Kwa upande wake Dkt. Kigwangalla amemwakikishia Waziri Mkuu kuwa kwa sasa anaendelea vizuri kwani ameweza kufanya mazoezi ya ikiwemo kutembea umbali wa kilometa nne pamoja na mazoezi mepesi kila siku majira ya asubuhi na jioni.
 
“Kwa sasa naendelea vizuri sehemu kubwa ni mkono ndio nauguza. Ila kwa hali ya maendeleo kwa sasa naendelea vizuri pamoja na mazoezi kidogo kidogo naendelea. "Alisema Kigwangalla. 

Aidha, mbali na Waziri Mkuu Majaliwa, jana jioni Agosti 25,2018, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliweza kumtembelea tena na kumjulia hali. 
 
Dkt. Kigwangalla alipata ajali asubuhi ya Jumamosi, Agosti 4, 2018) katikati ya vijiji vya Mdolii na Minjingu wilaya ya Babati mkoani Manyara baada ya gari lake kupinduka na kusababisha kifo cha Afisa Habari wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Hamza Temba na wengine watano akiwemo Dkt. Kigwangalla kujeruhiwa.

BASATA watoa NENO kuhusu afya ya Ommy Dimpoz

$
0
0
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) halijakaa kimya kipindi hiki ambacho msanii wa Bongo Fleva  Ommy Dimpoz anaumwa.

Kupitia ukurasa wao wa mtandao wa Twitter wamemtakia msanii huyo afya njema kipindi hiki anapatiwa matibabu nchini Afrika Kusini. 

"THREAD: Imeripotiwa tena msanii na ndugu yetu @ommydimpoz amerejea hospitalini kwa matibabu zaidi. Tunasimama na wapenda sanaa, wapenzi wake na watanzania wote kwa ujumla katika kumwombea na hatimaye arejee katika afya yake."
 
Tangu mwezi mwaka huu Juni Ommy Dimpoz amekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini ambapo alifanyiwa upasuaji wa koo kisha baadaye alirejea nchini na sasa amerudishwa tena Afrika Kusini. 

Matukio Katika Picha Rais Mstaafu Kikwete Alivyoshuhudia Sherehe Za Kumuapisha Rais Wa Zimbabwe Mhe.mnangagwa

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Zimbabwe Mhe.  Emmerson Dambudzo Mnangagwa zilizofanyika leo Jumapili Agosti 26, 2018. 

Katika safari hiyo Dkt. Kikwete ameambatana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Ndg. Philip Mangula akiwa na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP) Ndg. John  Momose Cheyo

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Agosti 27

Machache Yaliyojiri Weekend Toka Azam Tv

$
0
0
==>>Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania KKKT limetaka tambo zipigwe kujenga siasa za maridhiano zitakazochochea umoja, shikamano na udugu miongoni mwa Watanzania. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kanisa hilo Askofu Dkt. Fredrick Shoo wakati akifungua mkutano wa 35 wa Dayosisi ya kaskazini ya kanisa hilo ambao hufanyika kila baada ya miaka miwili kutathimini utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kanisa. 

==>>Waziri wa mambo ya ndani kangi lugola ametoa muda wa siku nne kwa mkandarasi anayejenga jengo la uhamiaji mkoa wa lindi kuwasilisha taarifa zake za usajili wa kampuni yake pamoja na mkataba uliyomsababishia kushinda tender ya ujenzi wa jengo hilo. 

==>>Uganda wanaibuka mabingwa wa michuano ya Kufuzu Afcon U17 mwakani ambapo wataungana wenyeji Tanzania kutoka ukanda wa CECAFA.

==>Tazama Habari Kamili hapo chini toka Azam Tv

Mwita Waitara Ajitabiria Kushinda Tena Jimbo la Ukonga

$
0
0
Aliyekuwa mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara amesema kwa hali ilivyo ya kisiasa katika jimbo hilo tayari ameshinda.

Waitara anasema anajiandaa kuendelea kuwatumikia wana Ukonga baada ya uchaguzi wa Septemba 16, 2018 kumshinda mgombea wa Chadema, Asia Msangi.

“Mimi ni mbunge ninayeendelea na ninapozungumza na wananchi nasema ninafanya lakini mgombea mwenzangu wa Chadema (Asia Msangi) anasema nitafanya, sasa huoni nimekwisha shinda,”  Waitara amelieleza gazeti la Mwananchi.

Amesema kampeni zake atazizindua rasmi Septemba mosi na kwa sasa anafanya mikutano ya chini kwa chini kwa kukutana na makundi mbalimbali kuzungumza nayo.

Waitara aliyewahi kuwa CCM akahamia Chadema na kurudio tena CCM Julai 28, ameanika mbinu zake sita zitakazomwezesha kumshinda Asia.

Amezitaja mbinu hizo kuwa ni mikutano ya hadhara; kukutana na makundi mbalimbali kama bodaboda; wafanyabiashara; vikoba na kutembea mtaa kwa mtaa.

“Mbinu ya nne ni kutoa mrejesho wa miradi niliyoifanya, tano; kuonyesha kero zilizopo na mwisho namna tutakavyozishughulikia,” amesema Waitara

Lowassa Kuzindua Kampeni za Uchaguzi CHADEMA Monduli

$
0
0
Waziri Mkuu mstaafu ambaye pia in Mjumbe wa Kamati kuu Chadema, Edward Lowassa atazindua kampeni za uchaguzi mdogo wa Monduli, Jumatano Agosti 29, 2018.

Lowassa atazindua kampeni za Chadema eneo la Mtowambu katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Septemba 16.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa Arusha, Aman Golugwa amesema wamejipanga Jumatano Agosti 29 kuzindua kampeni kwa kishindo.

"Tutakuwa na viongozi kadhaa akiwamo Lowassa ambaye ni mbunge mstaafu wa Monduli na tuna uhakika wa ushindi tena Monduli," amesema.

Golugwa amesema chama hicho kinajua michezo michafu ambayo inaendelea kufanywa na CCM, lakini wanataka dunia ijue CCM haikubaliki tena.

"Kuna figisu figisu nyingi hata hizi za wagombea udiwani kupita bila kupingwa lakini wasifikiri Chadema itakufa," amesema.

Katika uchaguzi wa Monduli vyama vinane vinashiriki Chadema wamempitisha kugombea diwani wa Lepurko, Yonas Laizer.

Kata hiyo ndiyo anakotoka Kalanga ambaye pia alikuwa diwani wa kata hiyo hadi mwaka 2015 akiwa CCM na kujiunga na Chadema.

Polisi Wavunja Mkutano wa Vijana Dar Na Waandishi wa Habari........Uliitishwa Kwa Ajili ya Kujadili Demokrasia na Haki za Binadamu

$
0
0
Jeshi la Polisi jana lilivunja mkutano ulioandaliwa na taasisi za vijana kuzungumzia mwenendo mbovu wa haki za binadamu na uvunjwahji wa haki za msingi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Mkutano huo uliotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Landmark, Ubungo kuanzia saa tano asubuhi jana, ulikwama kuendelea baada ya kuvamiwa na polisi huku waandaaji wakitimua mbio kwa hofu ya kutiwa nguvuni.

Wakati waandaaji wa mkutano uliopangwa kuanza saa tano asubuhi  jana Agosti 26, 2018 katika Hoteli ya Landmark, Ubungo jijini Dar es Salaam wakiendelea na maandalizi, ghafla aliingia ofisa mmoja wa polisi aliyekuwa amevalia sareza jeshi hilo na kujitambulisha kwa mlinzi kwamba naye ni mshiriki.

Baada ya kupewa maelezo, ofisa huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana alimweleza mlinzi huyo kuwa hawezi kuingia kutokana na sare zake za kazi na kuita askari wengine waliovalia kiraia ambapo alitoka nje na baada ya muda waliingia askari polisi waliokuwa na silaha za moto kwenye ukumbi wa mkutano.

Hatua hiyo ilizua taharuki miongoni mwa wanahabari na waandaaji wa mkutano huo, baada ya kubaini kuzingirwa na askari kanzu waliovaa kiraia huku askari wenye silaha wakizingira pia eneo hilo na hivyo kuwalazimu waandaaji na wanahabari kila mmoja kuanza kutawanyika ki vyake.

Akizungumzia tukio hilo, Mratibu wa Uhusiano kwa Umma wa Taasisi ya Tanzania Sahrawi Solidarity Committee  (TASSC), Noel Shao alisema walilazimika kusitisha kutoa tamko lao ukumbini hapo baada ya kuhofia usalama kutokana na kuzingirwa na polisi.

“Polisi wenye sare na silaha na askari kanzu wakiwa ndani ya gari zisizo pungua nne za polisi ziliendelea kupiga kambi kwenye Hoteli ya Land Mark kwa zaidi ya saa moja kuhakikisha hatutoi tamko. 

"Hata hivyo, tutaendelea kuwasiliana na umma kupitia njia nyingine za mawasiliano ili kupaza sauti zetu dhidi ya ukandamizwaji wa demokrasia na haki za binadamu,” alisema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Muliro alipotafutwa alisema uwapo wa polisi eneo la hoteli hiyo ni sehemu ya doria ya kawaida.

“Hivi polisi alipo watu wakimbie? Ebu wahoji hao kwa nini walikimbia. Sisi tutaendelea kuwapo na hata sasa ukienda mahotelini utaona polisi, je watu wanakimbia?” alihoji Muliro na kuongeza:

“Wewe si unaona polisi mitaani je watu wanakimbia?  Waulizeni wao kwa nini walikimbia.”

Hata hivyo, muda mfupi baadae, waandaaji hao walitoa taarifa yao  ikiwa imeorozesha waandaaji kuwa ni Taasisi za Umoja wa Kizazi cha Kuhoji Tanzania (UTG), Kamati ya Mshikamano Kati ya Tanzania na Sahara Magharibi (TASSC) na Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP).

Kwa pamoja, mitandao hiyo kupitia kwa mratibu wao, Shao walieleza kuwa wanaharakati wa haki za binadamu, asasi za kiraia na wananchi karibu nchi zote za Afrika Mashariki  wamekuwa wakishughulikiwa ili kuhakikisha baadhi ya tawala  zinatawala bila kikwazo.

Alisema katika kufanikisha hilo, wapinzani wa serikali wanashambuliwa, wanauawa, kubambikiwa kesi, kuozea jela bila hatia, kufilisiwa au kuzuiwa nje ya nchi kwa fimbo ya uraia suala ambalo halipaswi kukaliwa kimya.

Alisema wamefadhaishwa na kushamiri kwa vitendo vya ukandamizwaji wa  haki za binadamu, kusiginwa kwa misingi ya kidemokrasia na utawala bora na kuchipua kwa siasa za mkono wa chuma chini ya mtu mmoja badala ya utawala wa taasisi za umma na vyombo vya uwakilishi wa watu.

Shao alisema kwa Uganda, wameshtushwa na hatua ya hivi karibuni ya Serikali ya Rais Museveni kumkamata, kumshikilia kwenye korokoroni ya kijeshi, kumtesa na kumfungulia mashtaka bandia ya kukutwa na silaha Mwanamuziki na Mbunge wa Jimbo la Kyadondo Mashariki, Robert Kyagulani, maarufu kwa jina la Bobi Wine.

Makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula Kuzindua Kampeni za Chama Hicho Monduli

$
0
0
Makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula atazindua kampeni za uchaguzi mdogo wa Monduli, Jumatano Agosti 29, 2018.

Mangula atazindua kampeni za CCM Monduli mjini  katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Septemba 16.

Katibu mwenezi wa CCM Mkoa Arusha, Shaaban Mdoe amesema tayari maandalizi ya uzinduzi wa kampeni yamekamilika.

"Makamu mwenyekiti wetu (Philip) Mangula ndiye atazindua kampeni na tunaomba wanaCCM kujitokeza ili kuonyesha umoja na mshikamano wetu," amesema.

Mgombea ubunge wa CCM, Julius Kalanga amesema amejiandaa na wana CCM kutetea jimbo hilo ambalo alijiuzulu akiwa mbunge wa Chadema.

"Tutazindua kampeni Jumatano na nina uhakika wa ushindi kwani CCM ni chama imara ambacho kinakubalika sana Monduli," amesema.

Katika uchaguzi wa Monduli vyama vinane vinashiriki Chadema wamempitisha kugombea diwani wa Lepurko, Yonas Laizer.

Kata hiyo ndiyo anakotoka Kalanga ambaye pia alikuwa diwani wa kata hiyo hadi mwaka 2015 akiwa CCM na kujiunga na Chadema.

Wagombea wengine katika jimbo hilo ni Omar Kawanga (DP), Feruzi Juma (NRA), Simon Ngilisho (Demokrasia Makini), Fransis Ringo (Aada-Tadea), Elizabeth Salewa (AAFP) na Wilfred Mlay (ACT-Wazalendo).

RC Makonda Afanya Ibada Kanisani Ili Makontena Yake Yanayouza na TRA Yakose Wateja......Adai Atakayeyanunua Atalaaniwa Na Uzao wake Wote

$
0
0
Siku  moja baada ya makontena 20 yaliyo bandarini kwa jina la Paul Makonda, ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salam kufanyiwa mnada na kukosa wateja, amefanya ibada  akiomba yakose wateja.

Juzi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ilifanya mnada makontena hayo katika eneo la bandari kavu ya Malawi Cargo, lakini yalikosa wanunuzi baada ya waliojitokeza kushindwa kufika bei iliyotakiwa.

Jana Makonda alikwenda katika Kanisa la Anglikana wilayani Ngara, Mkoani Kagera ambako iliendeshwa ibada maalumu ya kuzuia mnada wa makotenda yenye samani za walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Makonda ambaye yupo kwenye msiba wa mama mkubwa wa mkewe, alishiriki ibada hiyo na aliwaambiwa waumini wa kanisa hilo kuwa amesali pamoja nao kwa sababu anaamini Mungu ndiye aliyempa makotenda hayo kwa ajili ya walimu wa Mkoa wake.

Alionya kuwa atakayenunua makontena hayo atalaaniwa yeye na uzao wake wote kwa sababu vya madhabahuni havichezewi.

“Nimekwenda katika ibada ya Jumapili katika Kanisa la Anglikana mjini Ngara, nimefanya ibada maalumu kuhakikisha makontena hayo hayapati wateja kwa kuwa naamini Mungu alinipa kwa ajili ya walimu wa mkoa wangu,” anasema Makonda.

RC Makonda anadai  kupatikana kwa samani hizo ni jitihada zake binafsi za kuboresha mazingira ya kufanyia kazi walimu ikiwa ni kumuunga mkono Rais John Magufuli aliyeamua kutoa elimu bure kwa Watanzania na hasa watoto wa masikini.

“Rais alitambua umuhimu wa elimu ndiyo maana kama msaidizi wake sikuona sababu ya kukaa kimya wakati mazingira ya walimu si rafiki na kusubiri kuwalaumu pale watoto wanapofeli bila kufanyia kazi changamoto zao.
 
“Baada ya kuona jitihada za Rais katika sekta ya elimu, kwa kutoa elimu bure nami nikawaza kama msaidizi wake, nafanya nini kuunga mkono kazi nzuri anayoifanya Rais.”

“Ndipo Mungu aliweka wazo lake ndani ya moyo wangu juu ya ujenzi wa ofisi za walimu kama sehemu ya kuboresha mazingira yao. Kwa utukufu wake Mungu, akaandaa watu wa kuchangia tena kutoka nje na ndani ya nchi,” alisema Makonda.

Akitumia maneno ya vitabu vitakatifu, Makonda alisema utukufu wa Mungu umejidhihirisha kwa Watanzania kuchangia, wakiwemo askari wa Jeshi la Kujenga Taifa waliojitolea kujenga majengo; benki kwa kununua saruji; baadhi ya viwanda kutoa mabati na nondo na wengine kujitolea masinki, mabomba na taa.

Makonda alisema nchi ya China imejenga ofisi, huku Watanzania wanaoishi Marekani wakimpatia samani za walimu ambazo zipo kwenye makontena zaidi ya 20 yaliyokwama bandarini yakidaiwa kodi.

“Wananchi na vyombo vya habari wamejitolea na kuendelea kuhamasisha, huku walimu wakichanga kama sehemu ya kujikomboa.

“Cha kushangaza leo vinapigwa mnada ili kutoza kodi kwa kuwa tu makontena yameandikwa Makonda basi kama jina langu hawalipendi watafakari mzigo alionao mwalimu wa Dar es Salaam anayegombea kiti na mwanafunzi anayekaa chini.

“Inasikitisha sana leo TRA inapiga simu kuomba shule binafsi zikanunue vifaa vilivyoletwa kwa msaada na Watanzania kwa ajili ya Watanzania wenzao.

“Ninachoweza kusema tu waliopewa madaraka wawe na hofu ya Mungu, mimi sikalii viti hivyo hata kama msingi wake ni chuki mchukieni Makonda lakini si walimu,” alisema Makonda.

Makonda alisema, “Nakuhakikishia atakayenunua hivi vifaa vya walimu amelaaniwa yeye na uzao wake na kamwe hatafanikiwa katika maisha yake. Nayasema haya nikiwa na uhakika kwa kuwa vya madhabahuni havichezewi.”

“Hivi ni vifaa kwa ajili ya walimu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mungu hakunipa kwa ajili ya baa wala kumbi za starehe,” alisema Makonda.

Kangi Lugola: Waliovamia Maeneo ya Jeshi Waondolewe Mara Moja

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya wizara yake kuwaondoa mara moja wananchi wote waliovamia katika maeneo ya majeshi nchini.

Ameyasema hayo mara baada ya kukagua Gereza jipya la Wilaya ya Ruangwa linalojengwa ambalo lina ekari 100 lakini ekari 20 zimevamiwa kwa kujengwa kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti, Ufuta na Korosho katika eneo hilo la Jeshi la Magereza.

Akizungumza baada ya kulikagua Gereza hilo mjini Ruangwa, Lugola amesema kuwa kuanzia sasa viongozi wa vyombo vyake wahakikishe hawaruhusu mwananchi yeyote kuingia katika maeneo ya jeshi na atakua mkali kulifuatilia suala hilo.

“Mimi huwa nashangaa sana inakuaje wananchi wanavamia ardhi ya jeshi tena bila woga, halafu jeshi linakaa kimya linabaki kunung’unika, hii haijakaa sawa kabisa na kamwe sikubaliani nalo,” amesema Lugola.

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza mkoani humo, Rajabu Nyange amesema kuwa licha ya ujenzi wa gereza hilo kuendelea kujengwa lakini ekari 20 ilichukuliwa kimakosa na kujengwa kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti na ufuta pamoja na kubangua korosho vinavyomilikiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara,M saniiwa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwawakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu. 
Kutana na Chief MAKATA.Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota zab inadam na bingwa wa tiba za asili Afrikam ashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. chief MAKATA  ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Chief Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi. 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali naU TAJIRI bila masharti na mengine mengi yaS iri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu
+255 676 014 385
+255 767 202 654 Chief MAKATA

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO   0658920640/ 0754372325 / 0620806813
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini, Bunda kwa sasa

Waziri Mkuu Mgeni Rasmi mkutano wa mwaka wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF)

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Mkutano wa 14 wa mwaka wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) utakaofanyika kesho jijini Dar es 
Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye,
maandalizi ya mkutano huo yamekamilika na utatanguliwa na mkutano mwingine wa wajumbe kutoka kongani 14 zinazounda sekta binafsi.

"Mkutano huo ni muhimu sana kwani ndiyo utakaotoa nafasi kufanya uchaguzi wa wajumbe 14 wa bodi ya wakurugenzi ya TPSF wajumbe hao ndiyo
watakaopendekeza majina mawili ya wagombea wa nafasi ya mwenyekiti wa taasisi hiyo," alisema Simbeye.

Simbeye alieleza kuwa wajumbe 14 kutoka kila kongani watakaochagulia na kuidhinishwa kwa
kawaida huwa pia ni wajumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) wakiungana na wajumbe wengine 14 kutoka sekta ya Umma ambapo Rais ndiye mwenyekiti wa Baraza.

Alisema maudhui ya mkutano huo ni ‘Uongozi, biashara unaowajibika katika ushirikiano wa sekta za umma na binafsi kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi’.

Alisema wajumbe watakaochaguliwa kwenye mkutano huo watatangazwa na kuridhiwa na mkutano wa mwaka na kwamba majina mawili yatakayopendekezwa yatachaguliwa kwenye nafasi za mwenyekiti na makamu mwenyekiti.

"Katika bodi inayomaliza muda wake, Mwenyekiti alikuwa Dk. Reginald Mengi na Makamu Mwenyekiti alikuwa Salumu Shamte ambao wamefanya kazi nzuri ya kuiimarisha sekta binafsi nchini," alisema Simbeye.

Simbeye aliongeza kuwa mikutano na vikao mbalimbali ambavyo vimefanywa kati ya sekta za umma na binafsi chini ya bodi inayomaliza muda wake vimekuwa na mafanikio makubwa.

Pia alisema Novemba 20, mwaka huu TPSF itaadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake.

Aliongeza kuwa TPSF ipo mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za Serikali ya Rais John Magufuli.

“Sisi sekta binafsi tumejipanga kutokomeza vitendo vya rushwa miongoni mwa wanachama wetu. Kuimarisha uhusiano wetu na serikali ikiwamo kuhamasisha ulipaji wa kodi miongoni mwa wanachama wetu pia," alisema Simbeye

Jumuiya zinazounda TPSF zinajumuisha Kilimo, Viwanda, Utalii, Benki na Fedha, Madini,Huduma, Wanawake Wajasiriamali, Wafanyabiashara Zanzibar, Ujenzi na Uhandisi, Mafuta na Gesi, Usafirishaji, Makampuni, Biashara na Uchuuzi.

Alichokisema Wema Sepetu Baada ya Kusikia Ommy Dimpoz Kalazwa ICU

$
0
0
Msanii wa filamu za Bongo Movie Wema Sepetu amefunguka na kuweka wazi kuwa hali ya Msanii wa Bongo fleva Ommy Dimpoz imeendelea kuwa vizuri tangu taarifa zake za kuzidiwa kuvuma.

Siku ya Jumamosi taarifa za Ommy Dimpoz kuzidiwa na kulazwa ICU zilisambaa mitandaoni  na kusababisha taharuki kubwa miongoni wa mashabiki zake.

Wema ambaye ana Ukaribu mkubwa na Ommy Dimpoz amefunguka na kuweka wazi baada ya kuwasiliana na Ommy anaamini anaendelea vizuri na hakuna kibaya kitakachotokea:

"To you My Forever Bae… . . . You are Stronger than you Think You are Braver than you Think You are Couragious than you Think You are Bigger than you Think You can overcome whatever thats holding you down right now in the name of Allah… . . . 

"Kama nilikosa nguvu na kuishiwa pose kabisa nilivyosikia u are not ok na uko ICU but after talking to you Im at ease…. We are not ready to hear bad news kabisaa…. No Sir…!!! You will be fine before you know it… That Hospital Bed aint for you… 

"Unajua You mean sooo much to me…. Na nakupenda kwa Kiasi kikubwa sana…. Fanya upone my love… Fanya upone haraka… Ila umekuwa Mcharo sana sasa hivi hadi raha… 😍😍😍 . . . 

"I love you… @ommydimpoz @ommydimpoz @ommydimpoz @ommydimpoz . . . Ila mgonjwa wewe mbea jamani…😂😂😂 You made my nite baby… Missing you sooo much… Cant wait to see you"....Ameandika Wema Sepetu

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images