Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Diva Afunguka Kwa Uchungu Kinachomfanya Asipate Mtoto

$
0
0
Mtangazaji wa kipindi cha Ala za Roho kutoka Clouds FM, Diva amefungukaa kile ambacho kinapelekea yeye kutobeba ujauzito.

Diva ambaye pia anafanya muziki wa Bongo Fleva ametumia ukurasa wake wa Instagram kueleza changamoto kubwa anayopitia kwa sasa anapohitaji kupata mtoto. 

==>>Tazama hapo chini kusoma alichokiandika Diva.
Nitachokiandika ni kitu ambacho kinaumiza sana Moyo wangu , Naandika Machozi yakiwa yananitoka , Sikutaka kuandika lakini Nahitaji kuandika ili nipate msaada zaidi, Sababu haya ni maisha yangu na naandika toka moyoni sitajali mtu atanifikiria nini au atawaza nini, hii situation is confusing sana na ndio maana nimeshindwa hata kulala yan nashindwa kulala kwa ajili ya hii issue sio tu kulala hata kula vizuri siwezi , Moyo wangu una maumivu mengi sana.

Nimejiuliza maswali sipati, ila nimeamua kuandika hapa, Kwa muda sasa kama mwaka niliamua kutafuta mtoto, Nimekunywa kila aina ya dawa mnayoijua nyinyi, za hospitali ndio nimemeza mpaka ikafika kipindi nikachoka, hizo za kunywa ndio nimemeza mpaka nimechoka, nikaamua kuchukua likizo kwa ajili ya vipimo very deep kujua tatizo ni nini, In my life nishawahi kupata ujauzito lakini haukufika ata Miezi4 and i lost the baby, kiukweli ilivyotokea mimi mwenyewe nilishang'aa, ila kwa ajili ya mambo yaliyokuwa yanaendelea kwenye hio relationship na huyo mwanaume anaitwa Solomoni frank.

Niliona labda Mungu ana Mipango yake, too many lies, so i decided to step out n focus on me ,how i met him Sitaki hata kuandika hapa ila iko siku i will share , Hivyo Basi nikakutana na Madaktari wa TMJ hospital nikafanya kipimo kujua kwanini kupata ujauzito inakuwa mtihani sana. sababu vipimo vyote vilikuwa sawa nikaamua kufanya kipimo cha mirija, ambacho nilifanya 9th july 2018.

Kwa Mtu alieniona hii siku atagundua nilikuwa na maumivu sana , Nililia sana sijawahi lia kama hivyo katika maisha yangu, Nililia sana Nilikuwa na maumivu sina mfano wa kuyafananisha, went to see Dr, Msemo wa Sanitas hosp ambae pia anafanya kazi TMJ ili nijue hasa tatizo , Yeye ni Daktari wangu , Akaniambia majibu yapo umekutwa na Bilateral Cornual Block yaani mirija imeziba, ata kupata mtoto kwa njia ya kawaida inakuwa maajabu sana. alivyokuwa ananielezea.

 Nilijikuta nalia Machozi yana teremka, nilishindwa drive i was in deep pain, nilitamani yule mtoto aliepotea arudi. at some point Sikuwa Pia naamini Mungu ana Exist, historia tu ya maisha yangu ilinifanya nitamani sana mtoto wangu mwenyewe afu the moment nahitaji sana ndio napewa haya majibu.

Basi nilijikuta nalia kupita maelezo ....had to call a friend called @qqtrends4u and gladly she was there for me wakati huu wote alikuwa yeye na @soudybrown ndio walini comfort 😭😭 i was heartbroken , tumeambiwa friends to keep ... hao ndio my friends to keep .. i love them sana sijui hata nieleze vipi hakuna maneno sahihi ya kueleza.

Mungu Mkali sana Nilisema, Mimi Diva ambae natoa misaada , nasaidia, moyo wangu una utu imekuaje haya mambo yanitokee nilijiuliza sana ... sikuweza kulala wala kula mpaka nililazwa kwa kupata Presha, but Nikaanza kuomba kwa Mungu Nikasema hii ni mara ya mwisho naomba.

Nikampigia doctor isaac nikamueleza akaniambia Gods Timing.... mambo yatakuwa sawa, nimeamua kuongea labda kuna wanawake pia wanapitia hii situation , ni situation inaumiza sana na kila ninapokutana na swali utazaa lini nakuwa naumia na hili swali sababu yan mimi Diva hata abortion sifanyi why on earth this imetokea.

wakati wa ukuaji wangu nimeumwa sana na tumbo na naumwa sana na tumbo, nishawahi fanyiwa upasuaji, hivyo solution ilikuwa kuwa na mtoto ili tatizo la maumivu makali ya tumbo kuisha, hivyo naweza sema nimepitia machungu mengi in my life but stil leo usiku huu nimeamka na kuamua kuandika hivi nimemuomba sana Mungu nikasema Im going public with this.

Bila aibu wala uoga na ntasaidia wengine pia wapate msaada ninaohitaji mimi wakati huu sababu najua maumivu yake, naandika hii part 2 chozi au niseme machozi yananitoka. Everything happens for a reason right, i have my best friend called @iammelissa_1 nilikuwa nae kwa simu kwa muda akasema Diva Najua unachopitia, "I know it’s a sensitive subject and sad for you to talk about!

But maybe you should talk about it because you are a great influence in your country and have many fans that are maybe having the same trouble as you So you could help them too talking about it " hivyo nikakaa chini na kuamua kuandika Hivi ninavyoandika .. i believe God is real ... nikaamua kufungua a page ntaweka link on inaitwa Gofundme.com na kuanzisha Kampeni inaitwa ' Dreams , Hopes , Wishes . Nia is to have a donation ya $7000 kwa ajili ya ivf treatment in America. Namshukuru Daktari wangu alisema haya....

Mayai na kizazi chako vyote viko sawa , but unaweza fanya IVF treatment #ivfjourney nikaamua kuwatafuta madaktari wa nje ya nchi kujua nafanyaje, with the amount of money sababu kuna kuishi huko, kula, kwa siku kadhaa pamoja na kupata sperm donor hivyo hio amount inaweza kutosha.

Guys ntaweka link hapo from gofundme , ili kama unaweza uchangie sababu mimi hizo hela sina siwezi danganya, thats alot of money, hivyo link apo juu wil help to support My Campaign called ' Dreams, Hopes, Wishes so that i can have My Miracle Baby baby of my own ....

Nahangaika kupata mtoto sasa hivi sababu ndio umri sahihi, sitaki sema how much nafanya kazi , nalala 2 hours too, nikisikia sauti ya yule daktari kichwani au ndotoni naamka usingizi unaisha unakata, imagine nimebeba all this moyoni mwezi mzima uliopita , Natembea na maumivu ya Majibu ya Daktari, ila nashukuru amenieleza vizuri tu Daktari wangu amesema ' Diva Your stil young , you can have it all done just pray , save for the treatment , keep calm n collected ... have faith ....

Yan wakati wengine wanapata watoto wanatupa, some of us needs alot of money for this treatment , dahhh 😭😭😭😭imagine i even set a baby name , baby room, i so wanted in my life mwaka huu niwe na mtoto 1 tu a baby boy afu mambo yanatokea so fast then huja recover unapata all the news za blockage ..... kumbe zinasumbua sana .. na upasuaji wake nao ni kazi ingine to deal with, kipimo chake tu ni maumivu sijawahi pata ona . ila Nimeandika sababu It is completely sensitive I know but you can imagine the pain i feel everyday.

The Pain ambayo wanawake wengine wanapitia, ni ngumu sana .. moyo ni kiza kinene msione mtu anacheka, wanawake tunapitia majaribu mengi sana i dont kno why!... nacheka, nafanya kazi , spend time with my family n friends ... nafanya mambo mengine lakini Moyo wangu umevunjika ... Sina raha ...

 Niko kwenye huzuni kubwa sana maishani... Naamini Mungu yupo na anasikia kilio changu Maana Nimelia sana mpaka nimechoka nimesali sana 🙏 hivyo Pia naomba Mniombee sana ... thanks💕 love you all 🙏 or you can send the money - Diva Gissele AC/ 3007111473924 Equity Bank, link on bio for Money transfer 🙏

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Jeshi la Polisi Lafafanua Kuhusu Tuhuma za Rushwa

$
0
0
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Barnabas Mwakalukwa, amekanusha kwamba, hakuna mtuhumiwa anayelazimishwa kutoa dhamana ya pesa kama inavyodaiwa na baadhi ya raia pindi wanapotakiwa kufanya hivyo.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa BreakFast kinachorushwa na East Africa Radio, Mwakalukwa amesema, dhamana inayotolewa polisi huwa ni ya maandishi lakini kumekuwa na watu wa daraja la kati wanaowalaghai watu kuwa watoe pesa ili wasaidiwe kutoka chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi.

''Ukitoa rushwa ili ndugu yako atoke polisi wewe ndio unakuwa na tatizo, kwanini utoe rushwa wakati ukifuata utaratibu ndugu yako atapata dhamana tu kama kosa lake linaruhusu'', amehoji Mwakalukwa.

Aidha, amefafanua kuwa, 'Mahabusu sio nyumba ya kuishi hivyo mtuhumiwa akienda atahojiwa kwa muda na huenda akarudi mtaani na ni utaratibu wa kawaida na si kweli kwamba wanatoa rushwa ili watoke mahabusu.

Kwa mujibu wa ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, (TAKUKURU), polisi katika mikoa ya Iringa na Temeke wamenyooshewa kidole kwa kuongoza kwa vitendo vya kuomba na kupokea rushwa.

Katibu Mkuu CCCM Atoa Ongo kwa Wanaohujumu Mali za Chama

$
0
0
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema Chama hicho kinadhibiti mianya ya ubadhilifu wa rasilimali fedha na mali zake ili kijitegemee kiuchumi.

 Alisema endapo rasilimali hizo zitatumika vizuri na kuanzishwa kwa miradi mingine mikubwa ya uzalishaji wa kipato katika ngazi mbali mbali za chama na jumuiya kwa  kuwanufaisha  wanachama wote badala ya watu wachache.

Kauli hiyo aliitoa jana katika mwendelezo wa ziara yake kisiwani Pemba wakati akizungumza na viongozi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi wa Mikoa Miwili katika ukumbi wa Fidel Castro uliopo, Mkoa wa Kusini Pemba.

Dk.Bashiru alieleza kuwa lengo la kusimamia dhana ya ukuaji wa uchumi ndani ya chama kupitia vyanzo vyake vya mali na fedha ni kukiondosha chama katika mazoea ya kutegemea ufadhili wa watu wenye fedha wanaokuwa na malengo ya kujinufaisha wenyewe kisiasa.

Pia aliyataja malengo mengine kuwa ni uimarishaji wa maslahi ya watumishi wa CCM na jumuiya zake kwani bado maslahi yao ni ya kiwango cha chini ambayo hayaendani na hadhi ya taasisi yenyewe.

“ Kwa miaka mingi chama chetu kimeondoka katika misingi ya kujitegemea na badala yake kujitokeza kwa watu wenye fedha kukichangia chama wakati wa uchaguzi na mazoezi mengine ya kitaasisi, sasa katika mageuzi haya ya kimuundo tuna dhamira ya chama chetu kukiondosha uko na tukaweza kutumia mali zetu wenyewe kujiendesha kitaasisi.” Alifafanua Dk.Bashiru.

Alieleza kuwa malengo hayo yakifanikiwa utakuwa ni ushindi mkubwa kwa wanachama wa CCM wote kwani tabia za rushwa na makundi ya kusaka nafasi za uongozi kwa kutumia fedha yatakuwa yamedhibitiwa.

Aliwataka viongozi wote wa taasisi hiyo kuunga mkono malengo hayo kwa kuhakikisha wanapunguza matumizi holela ya fedha na badala yake waanzishe miradi itakayowasaidia kujiendesha ili kulinda heshima na hadhi ya CCM mbele ya jamii.

Pamoja na hayo alizitaka jumuiya zote hasa ya umoja wa vijana (UVCCM) kuhakikisha wanakuwa wabunifu kwa kutumia rasilimia walizonazo kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kilimo, uvuvi na viwanda vidogo vidogo ili vijana wajiajiri wenyewe.

Katibu Mkuu huyo Dk.Bashiru aliweka wazi msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuwa wale wote waliohusika na kutapeli na kujimilikisha mali za taasisi hiyo kinyume na utaratibu wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi alisema wanachama wote wana haki ya kuunga mkono mambo mema yanayotekelezwa na taasisi hiyo kwa nia ya kuongeza ufanisi.

Alisema wakati wa vyama vya ukombozi vya ASP na TANU viongozi wa wakati huo walifanikiwa kupanga mambo ya maendeleo yaliyodumu kwa muda mrefu kutokana na umoja na mshikamano waliokuwa nao hasa katika masuala ya kuvijenga kimaendeleo vyama vyao.

Dk. Mabodi alieleza kuwa suala la uzalendo katika kusimamia maslahi ya kitaifa ni jambo muhimu hasa kwa viongozi wanaoaminiwa na kupewa dhamana za kuongoza jamii.

Akizungumzia ushindi wa CCM visiwani Zanzibar mwaka 2020 alisema mpaka sasa Zanzibar hakuna upinzani bali kuna vikundi vidogo vidogo vya watu wanaojivisha joho la upinzani wakati wao ni madalali wa kisiasa waliofilisika kifikra.

Naibu Katibu Mkuu huyo alisema CCM itashinda kisayansi kutokana na serikali zake kutekeleza mahitaji ya wananchi wa mijini na vijijini kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020.

Serikali Yatoa Ajura kwa Walimu 2160

$
0
0
Serikali imatoa ajira kwa watumishi 2,160 katika shule za sekondari nchini ambapo kati yao waalimu 1900 ni wa masomo ya sayansi na hisabati.

Akizungumza leo jumatatu Agosti 20,2018 Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amesema kati ya watumishi hao walioajiriwa 100 ni waalimu wa lugha na 160 ni fundi sanifu maabara.

Amesema watumishi hao wanatakiwa kuripoti katika ofisi za wakurugenzi wa halmashauri zilipo shule walizopangiwa kuanzia Agosti 23,2018 hadi Septemba 5,2018.

“Watumishi hao wanatakiwa kuripoti kwa muda huo wakiwa na vyeti halisi vya taaluma vya kidato cha nne na kidato cha sita, vyeti halisi vya kitaalam vya mafunzo ya ualimu vya ngazi husika pamoja na cheti cha kuzaliwa, na hatimaye kwenye shule walizopangiwa” amesema Jafo.

Hata hivyo, Jafo amewataka waajiriwa hao kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi na si makao makuu ya halmashauri ili kuomba kuhamishiwa vituo vya kazi.

“Mwajiri yeyote atakayechukua posho ya kujikimu kisha asiripoti kwenye kito chake cha kazi serikali itamchukulia hatua za kinidhamu,” amesema Jafo

Jafo ametumia nafasi hiyo kuwataka wakurugenzi wa halmashauri zenye vituo vya kazi walizopangiwa watumishi hao kuwapokea na kwa kufuata taratibu zote na kanuni za utumishi.

Ndugalile:Ni Marufuku Vifaa vya Kupima UKIMWI Kuuzwa kwa Watu Binafsi

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile amepiga marufuku uuzwaji wa vifaa vya kupimia virusi vya Ukimwi kwa watu binafsi.

Naibu waziri huyo amesema hatua hiyo inatokana na sheria za nchi kutoruhusu mtu kujipima mwenyewe.

Hayo ameyasema leo Agosti 20, 2018 katika hafla ya kukabidhiwa cheti cha ubora wa kimataifa (ISO) kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Ndugulile amesema kwa mujibu wa sheria iliyopo sasa inaruhusu mtu kupimwa virusi vya Ukimwi na mtaalamu au mtoa huduma kutoka kituo cha afya na si vinginevyo.

"Hivi sasa bado tuko katika hatua ya kubadilisha sheria ili tuweze kuruhusu watu kujipima wenyewe lakini hii itakuwa baada ya majaribio yanayofanyika katika baadhi ya maeneo kuonyesha matokeo chanya," amesema Ndugulile

"Kwa hiyo basi naziagiza taasisi zangu kuhakikisha kuwa zinadhibiti uuzwaji holela wa vifaa hivi katika maduka ya dawa kote nchini," ameongeza.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Agosti 21


Watanzania 20 Wapewa Ufadhili Kusomea Masuala Ya Gesi China

$
0
0
Serikali ya China imetoa ufadhili wa masomo  kwa wanafunzi 20 kwenda kusoma masuala ya gesi na mafuta nchini humo.

Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wanafunzi hao, Katibu wa Wizara ya Nishati, Hamis Mwinyimvua amesema lengo la ufadhili huo ni kuhakikisha Watanzania wanajengewa uwezo wa kushiriki katika uendelezaji wa rasilimali ya mafuta na gesi ipasavyo.

Amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, iliingia makubaliano na Serikali ya China kutoa ufadhili wa fani ya mafuta na gesi kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu ambapo kwa mwaka huu wameongeza hadi wale wa shahada ya kwanza ambapo tangu programu hii ianzishwe wanafunzi 100  wamefadhiliwa.

“Niwapongeze Watanzania wenzetu waliopata  ufadhili kwa mwaka huu, haikuwa kazi rahisi na maombi yalikuwa mengi ila wao wamechaguliwa katika nafasi hizo na mjue mnaenda kuwakilisha nchi hatimaye mlete ujuzi nchini.

“Tunaishukuru serikali ya China tumekuwa tukisaidiana katika mambo mengi hasa hili la ufadhili wa masomo ya elimu ya juu, ufadhili huu ni mhimili muhimu katika nchi yetu kuwa na wataalamu wa kutosha katika sekta ya nishati ambayo ni injini ya kufikia katika Tanzania ya Viwanda,” amesema.

Kwa upande wake muwakilishi wa Balozi wa China, XU Chen amesema serikali yake iliamua kutoa ufadhili huo kwa Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano ili kusaidia kupata wataalamu katika sekta ya nishati jambo ambalo litaimarisha ushirikiano wa nchi hizo mbili.

“Tanzania ni nchi yenye utajiri wa mafuta na gesi ila hawana watu wenye taaluma ya kutosha jinsi ya kuvumbua rasilimali hizo na hii ndiyo sababu imetufanya tutoe ufadhili huu na tunafuraha kuona ushirikiano wa nchi hizi mbili unakua,” amesema Chen.

Bei ya Saruji Kushuka......Ni Baada ya Serikali kuiuzia Dangote gesi asilia kwa miaka 20

$
0
0
Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini TPDC, kupitia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wake Mhandisi Kapuulya Musomba, limesaini mkataba wa miaka 20 wa kukipatia kiwanda cha saruji cha Dangote, gesi asilia kama nishati kwa ajili ya kuzalisha saruji.
 
Kufuatia makubaliano hayo yaliyosainiwa jijini Dar es salaam jana, kiwanda cha Dangote kitaacha matumizi ya nishati ya mafuta katika uzalishaji na kwamba mchakato wa kuhama kutoka matumizi ya mafuta kwenda ya gesi utachukua kati ya siku 30 hadi siku 45 kuanzia sasa.

Hivi karibuni kumekuwa na uhaba wa saruji katika soko ambapo kwa mujibu wa Waziri wa Viwanda Mh. Charles Mwijage, moja ya sababu ni kupungua kwa uzalishaji wa kiwanda cha Dangote hivyo kusainiwa kwa makubaliano hayo kutasaidia kupunguza kuadimika kwa bidhaa ya saruji katika siku za usoni ikiwa ni pamoja na bei kushuka.

Mradi wa gesi asilia na iliyosindikwa Tanzania (TGP) ni miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya ujenzi wa miundombinu katika historia ya Tanzania.

Matumizi ya gesi iliyopo nchini yataongeza uwezo wa nchi wa kusafirisha nje rasilimali hiyo na kuboresha miundombinu ya ndani.

Usikilize hapa wimbo MPYA wa HAMISA MOBETTO, Madam Hero

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto anakukaribisha kusikiliza wimbo wake mpya uitwao Madam Hero.

==>>Usikilizew hapo chini

Video: Isikilize Hapa Ngoma mpya ya Harmonize ATARUDI

$
0
0
Msanii chini ya Lebo ya WCB, Harmonize ameachia wimbo wake mwingine ambao kwa sasa unafanya vizuri katika chaneli za YouTube kwa kushika namba 2 kati ya video bora na kutazamwa zaidi katika mtandao huo.

Wimbo huo unaitwa ”Atarudi” akiwa amefanya video yake nchini Nigeria huko Lagos na Afrika Kusini.

Aidha mashabiki wake mbalimbali wametoa komenti zao juu ya ujio wa wimbo huo na kusema wimbo ni mkali na huenda Harmonize akawa mwanamuziki bora mwaka huu na kumpiku bosi wake Diamond Platinumz ambaye naye bado anafanya vizuri na nyimbo wimbo wa jibebe aliyoufanya na wasanii wake Lavalava na Mbosso.

Tazama video ya wimbo huo hapa chini kisha shusha komenti yako.

Bilioni 11 Zatengwa Kuwanufaisha Vijana Wajikwamue Kimaisha

$
0
0
Vijana 30,000 kutoka Mikoa ya Iringa, Mbeya na Mikoa ya Tanzania Visiwani watanufaika na fursa ya mafunzo ya kilimo na ujasiriamali kupitia Program ya Feed the Future inayofadhiliwa na Shirila la Misaada la Marekani (USAID) ambapo watapewa nyenzo na mtaji yenye thamani ya Sh. Bilioni 11.

Hayo yasememwa jana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi,Vijana na Ajira, Anthony  Mavunde akiwa mkoani Iringa wakati akizindua Baraza la Vijana la Ushauri wa Mradi.

Mavunde alisema katika mradi huo vijana watapewa nyenzo na mitaji ya kuanzia shughuli za uzalishaji mali, ambapo amelitaka Baraza hilo kuhakikisha malengo ya mradi yanafikiwa hasa katika kumkomboa kijana wa kitanzania na changamoto za ukosefu wa ajira na kumsaidia kufikia malengo yake.

Naye Kaimu Balozi wa Marekani nchini Dk.Inmi Patterson alisema Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza ujuzi wa Nguvu kazi ya Vijana wa Tanzania na kuhamasisha ushiriki wao katika sekta ya kilimo ili kuongeza pato la Taifa zaidi kupitia sekta ya Kilimo ambayo imeajiri Watanzania wengi.

Kwa upande wa  Kaimu Mkuu Mkoa wa Iringa, Richard Kasesela ameahidi kutoa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo ambao utawanufaisha Vijana wa Iringa kwa kiasi kikubwa.

CHADEMA Walia Rafu Tena....Ni Baada ya Mgombea Wao Kuengeuliwa na wa CCM Kupita Bila Kupingwa Korogwe Vijijini

$
0
0
Mgombea wa ubunge Korogwe Vijijini (CCM), Timotheo Mzava amepita bila kupingwa katika uchaguzi wa mdogo wa marudio.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mzava kujikuta pekee yake muda wa kurudisha fomu ambao mwisho ulikuwa jana  Agosti 20, 2018.

Mkurugenzi Mtendaji wa Korogwe, Dk George Nyaronga ambaye ndio msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo amesema, “mgombea wa CCM amepita bila kupingwa.”

Awali Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, alilalamika 'rafu' iliyochezwa baada ya mgombea wake katika jimbo hilo kuenguliwa kwa kushindwa kurejesha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi huo.

Golugwa, amesema alifika katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo akiwa na mgombe wao, Amani Saguti majira ya saa 5:38 asubuhi kwa lengo la kurudisha fomu.

Amedai kuwa walipofika katika ofisi hiyo, walimkuta msimamizi wa uchaguzi, Samia Guram, lakini alikataa kuzipokea fomu hizo kwa madai kuwa muda wa kurudisha fomu ulikuwa haujafika.

Jana ilikuwa siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa waliotia nia ya kugombea ubunge katika jimbo hilo ambalo limelazimika kufanya uchaguzi kutokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mbunge wake, Steven Ngonyani 'Prof. Maji Marefu' mwezi uliopita.

"Alituambia tusubiri hadi saa 10 jioni ndipo atapokea fomu za mgombea wetu," Golugwa alisema na kueleza zaidi:"Tulihoji kisheria lakini hatukupata majibu sahihi, ndipo tukaamua kwenda kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Korogwe."

Hata hivyo, Golugwa alisema hawakufanikiwa kuonana na Mkurugenzi wa Wilaya ya Korogwe, wakielezwa kuwa alikuwa amekwenda kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo.

Golugwa aliendelea kueleza kuwa kutokana na kushindwa kuonana na kiongozi huyo, waliamua kurejea kwenye ofisi ya msimamizi wa jimbo, lakini walikuta mlango umefungwa na hapakuwapo ofisa yeyote wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

"Tulilazimika kukaa nje ya hiyo ofisi kusubiri. Wakati tunasubiri, CUF (Chama cha Wananchi) walifika kuleta fomu," Golugwa alisema.

"Hata ACT-Wazalendo nao walifika, na ilipofika saa tisa alasiri, CCM (Chama Cha Mapinduzi) nao walifika kurudisha fomu, hivyo wote tukawa nje tunasubiri."Alisema kuwa ilipofika saa 10:30 jioni, mgombea wa CCM na wafuasi wake waliondoka bila ya kuwapo kwa taarifa yoyote kutoka ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.

Hata hivyo, Golugwa alisema ilipofika saa 11:15 jioni, alifika mtu katika eneo hilo na kujitambulisha kuwa ni ofisa utumishi akifuatana na askari polisi wenye silaha, akabandika karatasi iliyoonesha mgombea wa CCM amepita bila kupingwa.

Golugwa alisema kuwa walipojaribu kuhoji hatua hiyo, askari polisi hao waliwazuia na kuwatisha kuwapiga risasi.


Awali, Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, alisema wagombea wao katika majimbo mengine mawili, Yonas Laizer (Monduli) na Asia Msangi (Ukonga) walifanikiwa kurejesha fomu za kuwania ubunge jana. Uchaguzi huo umepanga kufanyika Septemba 16.

Idris Ampa Maneno ya Faraja Hamisa Mobeto

$
0
0
Mchekeshaji Idris Sultan amempongeza Mwanamitindo Hamisa Mobetto kuingia kwenye muziki. Idris amesema yeye anamsapoti Hamisa na anashangazwa na wale wanaomkeli kwa hatua hiyo. 

==>>Kupitia ukurasa wake wa Instagram Idris ameandika;
"Naomba niwe kati ya wale wa kwanza kukusapoti ili ukija kuanza kuchukua matuzo usitusahau maskini wenzio. Mwanzo sio mwepesi ila kama msimamizi wa mpesa vodacom naweza sema yajayo yanafurahisha. Nitashangaa kuona watu wanakukejeli kwenye hii hatua yako katika upiganaji sijui wanataka ukatembee barabarani unauza nanilii sasa.

"Katika hatua za mafanikio jua sana kuchuja maneno. Kama kweli umedhamiria kufanya mziki basi kazaaa na unatoboa tu kwani hao wengine ni kina nani labda. Wengine tulianza hatukubaliki hata tutoe msaada wanguo zetu tutembee watupu ila unakaza tu na baada ya mda unaanza okota fan mmoja mmoja wawili mwishowe una mamilioni #RefuseToStop"

Jana August 20, 2018 Hamisa Mobetto ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jila na Madam Hero. 

Hamisa ni mrembo mwingine Bongo kujaribu bahati yake kwenye Bongo Fleva baada ya wengine kama Wema Sepetu, Jokate Mwegelo Aunt Ezekiel nakadhalika.

Gari la Ikulu ya Rais wa Kenya laibwa na kukamatwa mjini Moshi nchini Tanzania

$
0
0
Jeshi la polisi linawashikilia watu wawili wakazi wa Moshi kwa kukutwa na gari inayosadikiwa kumilikiwa na Ikulu ya Nairobi nchini Kenya ambayo inasadikiwa kuibwa nchini Kenya tarehe 19 Agosti.

Gari aina ya Nissan V8 yenye Namba za Usajili KCP 184 RV. Lakini ilikuwa imebandikwa T954 DEQ ilikamatwa ikiwa njiani ikielekea Kilimanjaro ikitokea nchini Kenya.  Tarehe 19 kulikuwa na taarifa ya gari aina ya V8 kuibiwa Kenya.

==>>Sikiliza kila kitu hapo chini

Harmorapa Mzee wa KIKI Alamba dili NONO la ubalozi wa kampuni ya usafiri

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Harmorapa amepata dili la kuwa balozi wa kampuni ya Moovin inayotoa huduma ya usafiri.

Kampuni hiyo  ya usafiri ya Moovin ilimtangaza rapa Harmorapa pamoja na mtangazaji wa XXL ya Clouds FM jana Jumatatu kuwa mabalozi, tukio ambalo lilifanyika  katika hotel ya Double Tree jijini Dar es salaam

Akiongea baada ya kutangazwa Harmorapa ameishukuru kampuni hiyo kwa kutambua nguvu yake na kuamua kumpatia deal hilo ambalo litamjengea heshima kubwa.

Hapo awali kampuni hiyo ilimtambulisha Madam Ritha wa BSS kuwa balozi wao pia.

Hili ni dili lingine kwa Harmorapa mara baada hapo awali kuwahi kuwa balozi wa kinywaji cha Swala.

Mwanafunzi Ashambuliwa na Kujeruhiwa Vibaya na Fisi

$
0
0
Mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Ibutamisuzi, Kata ya Mbutu wilayani Igunga Mkoa wa Tabora, Nchambi Malunde (9), amenusurika kufa baada ya kujeruhiwa vibaya na fisi wakati akienda shuleni na mwanafunzi mwenzake.

Mama wa mwanafunzi huyo, Masaaka Mwandu, alisema tukio hilo lilitokea Ijumaa majira ya asubuhi wakati mwanaye akiwa na mwanafunzi mwenzake wa darasa la kwanza ambaye hata hivyo, hakumtaja jina wakiwa njiani kwenda shuleni ndipo walipovamiwa na fisi.

Alisema baada ya fisi huyo kuwavamia, alianza kumng'ata mwanae, hivyo kupiga kelele kuomba msaada, hali iliyomfanya mwanafunzi mwenzake kutimua mbio kwenda kutoa taarifa kwenye nyumba ya jirani ambapo wananchi walifika eneo hilo wakiwa na mikuki, mashoka, mapanga na marungu.

Kwa mujibu wa Mwandu, pamoja na wananchi kufika kwenye eneo la tukio na kuanza kumfukuza fisi huyo, aliamua kumuachia mwanafunzi na kuwageukia wananchi akiwatishia kuwashambulia kisha kutoweka na mfuko wa madaftari ya mwanafunzi huyo.

Mama huyo alisema baada ya fisi kutoweka, ndipo wananchi walipomchukua mwanae na kumpeleka nyumbani ili apelekwe Hospitali ya Wilaya ya Igunga kwa matibabu, lakini kabla hawajaondoka fisi huyo alifika nyumbani kwa mwanafunzi huyo huku akiwa na mfuko wa madaftari mdomoni na ndipo wananchi walimfukuza tena.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ibutamisuzi, Ludovick Ngassa, alisema baada ya kumuokoa mwanafunzi huyo waliamua kupiga simu Idara ya Maliasili kuomba msaada na ndipo maofisa wanyamapori walifika kijijini hapo na kuanza kumsaka fisi huyo bila mafanikio.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi, Ibutamisuzi, Alex Simumba, alithibitisha kwamba mwanafunzi huyo anasoma katika shule hiyo na kuiomba Idara ya Maliasili kumsaka fisi huyo hadi apatikane ili kunusuru maisha ya wanafunzi wengine.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Merchades Magongo, alithibitisha kumpokea Nchambi akiwa amejeruhiwa vibaya sehemu za begani, maeneo ya makalio na kusema kuwa amelazwa wodi namba nane na hali yake si nzuri na kwamba majeraha aliyonayo ni makubwa.

Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa Wilaya ya Igunga, Jahulula Edward, alisema baada ya kupewa taarifa na mtendaji wa kijiji hicho juu ya fisi huyo, walikwenda hadi eneo hilo ambapo kwa kushirikiana na wananchi walimtafuta bila mafanikio na kuongeza kuwa wanaendelea kumsaka hadi apatikane.

Kwa mujibu wa Jahulula, pamoja na kumjeruhi mwanafunzi pia fisi huyo alimshambulia ndama hadi kufa, na kutoa wito kwa wananchi kutoa taarifa pindi watakapomuona fisi huyo.

Polisikilimanjaro Yanasa Raia Wa Ethiopia 25 Waliongia Nchini Bila Kufuata Sheria

$
0
0
Na Dixon Busagaga
Jeshi la Polisi linawashikilia raia 25 wa Ethiopia miongoni mwao tisa  ni watoto wenye umri chini ya miaka 18  wakiwa katika kichaka eneo la Himo wakisubiri gari kwa ajili ya kuwavusha kuendelea na safari yao ya Afrika Kusini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Maidizi wa Polisi,Hamis Issah amesema raia hao wa Ethiopia walikamatwa na askari Polisi wakati wa doria wakiwa na kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Baraka itema (25) aliyejitambulisha kama fundi ujenzi .

Raia hao 25 wa Ethiopia wanaendelea kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kwa kusaidiana na jshi la Polisi na kwamba mara baada ya taratibu kukamilika watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili za kuingia nchini bila ya kibali.


Kinachoendelea Mahakamani Katika Kesi ya ‘Ndama mtoto wa Ng’ombe’

$
0
0
Upelelezi wa kesi inayomkabili mfanyabiashara , Ndama Shabani Hussein maarufu kama Pedeshee Ndama Mtoto ya Ng’ombe, umekwama kukamilika kwa sababu Jamhuri inasubiri upelelezi kutoka Australia.

Hayo yalibainika jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde wakati kesi hiyo ilipokuwa inatajwa.

Akiiwakilisha Jamhuri, Wakili wa Serikali, Elia Athanas alidai   upelelezi wa kesi hiyo  haujakamilika,  kwamba kuna taratibu baina ya nchi mbili Tanzania na Australia bado unaendelea ili kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo.

Athanas aliomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa  kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Wakili wa utetezi, Nashon Nkungu alisema anasikitika   upande wa mashtaka haulipi uzito suala hilo na kwamba inashangaza upelelezi  haukamiliki kwa zaidi ya mwaka sasa.

Nkungu aliiomba mahakama kuangalia kesi hiyo kwa jicho la tatu ambalo ni kutenda haki.

Aliiomba upande wa mashtaka uonywe na kutekeleza jukumu lake katika kesi hiyo ikiwa Jamhuri imeshindwa kukamilisha upelelezi suala hilo lifanywe kama sheria inavyotaka ,  hati ya mashtaka iondolewe.

Wakili Athanas baada ya kusikiliza hoja hizo za upande wa utetezi alisisitiza kuwa suala hilo linahusisha nchi mbili tofauti.

“Sisi kwa upande wetu tumekamilisha bado upande huo mwingine kwa kuwa wao wana utaratibu wao na hatuwezi kuwalazimisha watujibu.

“Tunaomba wawe wavumilivu kwa sababu siyo nia ya Jamhuri kuchelewesha shauri hilo,” alidai.

Baada ya kusikiliza hoja zote hizo, Hakimu Kasonde alisema “hakuna ubishi suala la upelelezi linahusisha nchi mbili, tuwape nafasi”  na kuiahirisha kesi hadi Septemba 21, mwaka huu.

Ndama ambaye kwa sasa yupo nje kwa dhamana,  anakabiliwa na shtaka la kwanza hadi la tano baada ya kulikubali shtaka la sita la kutakatisha fedha, kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini ya Sh milioni 200 na kukwepa kesi kifungo cha miaka mitano jela.

Ndama kwa sasa anakabiliwa na mashtaka matano ya  kughushi na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Miongoni mwa mashtaka yanayoendelea kumkabili ni kuwa  Ndama anadaiwa Februari 20, 2014 Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonyesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited.

Pia kampuni hiyo  iliruhusiwa kusafirisha makasha manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images