Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Aagiza Mhasibu Aliyehamishwa Arudishwe

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Manispaa ya Tabora kumrejesha kwenye nafasi yake ya Uhasibu Halima Temihaga ambaye alihamishiwa Ofisi ya masoko baada ya kuwalalmikia  viongozi wa Idara yake.

Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo mjini hapa wakati akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, wa Manispaa , Madiwani na viongozi mbalimbali ikiwa ni siku ya mwisho ya ziara yake mkoani Tabora.

Aliutaka uongozi wa Manispaa ya Tabora kumrejesha kwenye nafasi yake na  kutombugudhi mtumishi huyo.

Katika kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo Msalika Makungu kufuatilia kwa karibu Ofisi ya Idara ya Fedha ya Manispaa hiyo kuona utendaji kazi wake.

Waziri Mkuu alisema kuwa Halima alipewa uhamisho na Mkuu wake wa Idara baada ya kulalamikia kitendo cha kutumia namba yake ya siri kuidhinisha malipo bila ya kumshirikisha yeye mwenyewe kama Mhasibu.

Mhe. Majaliwa aliongeza kuwa katika tukio hilo hati ya malipo namba hati iliyotumika kutoa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni tano ambazo ilidaiwa ni malipo ya kazi za ziada kwa ajili ya Wahasibu wa Manispaa hiyo ( PV  namba 2018 002321 ) ya tarehe 13 Aprili mwaka huu.

Aliongeza kuwa fedha nyingine kiasi cha shilingi  milioni 8.4 zilizotolewa kwa PV namba 2018 0001492 haijulikana matumizi yake.

Kutokana na kasoro hizo Waziri Mkuu alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Manispa hiyo kuwa makini na kazi yake huku akiwaagiza Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa kuisimamia kwa karibu Ofisi hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Agosti 19

Spika Job Ndugai amjulia hali Dkt. Kigwangallah

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ameambatana na Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai na baadhi wa Waheshimiwa Wabunge wamemtembelea Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Khamis Kigwangalla kwa lengo la kumjulia hali katika Hospitali ya Taifa ya Muhumbili alikolazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu baada ya kupata ajali ya gari.

Wanakijiji 68 Watiwa Mbaroni kwa Kuharibu Miundo Mbinu......Ni Wale Ambao RC Mbeya Aliagiza Wakamatwe

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu 68 kati yao 62 ni wanaume na 06 ni wanawake kwa tuhuma za kufanya uharibifu wa miundombinu ya maji huko katika Kijiji cha Ngole kilichopo Kata ya Ilungu, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Katika msako mkali uliofanywa mnamo tarehe 17.08.2018 kuanzia majira ya saa 10:00 asubuhi hadi saa 18:00 jioni huko katika Kijiji cha Ngole jumla ya watuhumiwa 68 walikamatwa.

Awali mnamo tarehe 14.08.2018 kuanzia majira ya saa 10:00 asubuhi huko katika Kijiji cha Ngole, Kata ya Ilungu, Tarafa ya Tembela watuhumiwa hao kwa makusudi na bila halali waliharibu mabomba na vyanzo vya maji kwa kutumia silaha za jadi na kusababisha hasara ya takribani Shilingi Milioni 14 mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni michango ya baadhi ya wanakijiji na wafadhili.

Watuhumiwa hao watafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Aidha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishina Msaidizi Mwanadamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa msisitizo kwa watanzania na wana Mbeya wote kuhakikisha wanalinda rasilimali zetu zikiwemo miundombinu ya afya, elimu, barabara, maji na nishati ili kufikia malengo tarajiwa ya uchumi wa viwanda. 

Pia Kamanda MATEI anatoa rai yeyote atakayeharibu miundombinu hiyo Polisi tutamkamata na kumfungulia shitaka la kuhujumu uchumi [Sabotage] na kuhakikisha wanafikishwa Mahakamani.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na Operesheni mbalimbali, doria katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha hali ya Mkoa inakuwa shwari ikiwa ni pamoja na kufanya ukaguzi wa magari, kuwapima kilevi madereva pamoja na kuendelea kutoa elimu ya matumizi salama ya barabara kwa makundi mbalimbali ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

               Imetolewa na:              
 [ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

Waziri Azuia Umeme Kuruka Nyumba za Tembe

$
0
0
WAZIRI wa Nishati, Dk. Merdad Kalemani, amewataka wakandarasi wote nchini wanaotekeleza mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kuhakikisha wanaweka umeme katika nyumba zote zikiwamo za tembe huku akipiga marufuku kurukwa.

Akizungumza wakati akiwasha umeme katika vijiji vya Lukungu, Nyakaboja na Bukabile vilivyoko Wilaya ya Busega, Simiyu, alisema wamekuwa wakipata taarifa za wakandarasi waliopewa kazi ya kutekeleza mradi huo kuwa wamekuwa wakiziruka nyumba hizo kwa madai hazifai kupata huduma hiyo.

Aliwataka wakandarasi hao kuhakikisha wanapeleka umeme katika kila kijiji na kila kitongoji ili wananchi waweze kuondokana na adha kubwa wanayokumbana nayo ya kukosa nishati ya umeme.

“Nimepata taarifa kuwa wananchi wenye nyumba za tembe wanarukwa, maagizo yangu ni marufuku kuruka nyumba ya tembe, tena nyumba hizo zipewe kipaumbele cha kwanza kupata umeme na hakuna kuruka kijiji, kitongoji au nyumba yoyote,” alisema Kalemani.

Alisema Serikali haitaongeza muda, siku wala saa kwa mkandarasi yeyote atakayeshindwa kutekeleza mradi huo kwa muda mwafaka waliopewa na Tanesco na aliwataka kutekeleza mradi huo hadi kukamilika kwake kwa muda mwafaka.

Alisema mkandarasi White City anayetekeleza mradi huo Simiyu kasi yake ni ndogo na alimtaka kuongeza kasi zaidi ili kuhakikisha vijiji 152 mkoani humo vinapata umeme.

Alisema katika Wilaya ya Busega kupitia mradi huo vijiji vyote 54 vilivyoko wilayani humo vitapata umeme na aliwataka wananchi kuhakikisha wanalipia gharama ya Sh 27,000 ili kupatiwa huduma hiyo.

Pia alizitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha wanafunga mfumo wa umeme katika taasisi za umma zikiwemo shule na vituo vya kutolea huduma za afya.

“Wakati sisi tukihangaika kuleta umeme kwa kila mwananchi, niwatake wakurugenzi wa halmashauri pamoja na madiwani kupitia vikao vyao, watenge bajeti kuhakikisha taasisi zote za umma zinafungiwa mfumo mzima wa umeme kwa ndani,” alisema Kalemani.

Awali, Mbunge wa Busega, Dk. Rafel Chegeni, alisema bado kuna baadhi ya vitongoji na vijiji vimerukwa na mkandarasi anayetekeleza mradi huo.

Dk. Chegeni alisema kilio kikubwa cha wananchi wa jimbo hilo ni ukosefu wa umeme na alimwomba Kalemani kutatua changamoto hiyo iliyodumu kwa muda mrefu.

Harmonize na Professor Jay waingia Location Kupika "Atarudi"

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Harmonize tayari ameingia location kwa ajili ya kufanya video ya wimbo aliofanya na Professor Jay.
Muimbaji huyo kutokea lebo ya WCB ame-share video kupitia Insta Stori wakiwa locationi maeneo ya Kariakoo Dar es Salaam, director wa video hiyo ni Kenny ambaye pia amehusika katika video ya wimbo Kwangwaru ambayo Harmonize amemshirikisha Diamond.

Wimbo wa Harmonize na Professor Jay unakwenda kwa jina la Atarudi akiwa umetengenezwa na producer Bonga. Tayari Harmonize ameweka wazi kuwa wimbo huo utatoka August 28, 2018.

Amber Lulu Afunguka kwa Sasa Ameacha Umalaya, Ameamua Kufanya Muziki

$
0
0
Msanii wa muziki, Amber Lulu amefunguka kwa kudai kwamba kuna wakati anaamua kufanya umalaya lakini kwa sasa ameachana na mambo hayo. 

Muimbaji huyo ambaye alikuwa ni mmoja kati ya wasanii waliopamba tamasha la Komaa Concert la EFM, amedai kwa sasa ameamua kufanya muziki na kuacha mambo mengine.

"....Nafanya muziki kwa sasa, sifanyi mambo mengine na nikiamua kufanya umala nafanya kweli". Anakaririwa Amber Lulu

RC Makonda afunguka kuhusu Harusi ya Lulu Michael

$
0
0
Kwa kipindi kirefu kumekuwa na stori za hapa na pale kuwa muigizaji wa filamu Bongo, Elizabeth Machael 'Lulu' anaolewa na Majey.

Sasa basi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana  August  18, 2018 akiongea na waandishi wa habari alipohudhuria Komaa Concert aliulizwa kuhusu uwepo wa harusi hiyo.

RC Makonda amesema Harusi ya Lulu na Majey ni miongoni mwa harusi tatu ambazo ni lazima azisimamie.

"Majizo tayari yupo kwenye mipango na binti yangu Lulu na wameshakuja nyumbani na wameshafanya vikao vingi vya kupanga kwa ajili ya Harusi," alisema RC Makonda.

RC Makonda ametaja harusi nyingine mbili ambazo lazima azisimamie ni ile ya Meya wa Kinondoni, na ya Lemutuz.

==>>Msikilize hapo chini

Lugola Aonya Polisi Kutumiwa Na Mafisadi Kupora Ardhi Za Wananchi

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaonya Polisi nchini ambao wanatumiwa na mafisadi kuwanyanyasa wananchi maskini kwa kupora ardhi zao na kukimbilia kufungua kesi vituoni wakilazimisha ardhi hiyo iwe mali yao.

Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Ragati, Kata ya Kasuguti, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, Lugola alisema amepata malalamiko mengi kutoka sehemu mbalimbali nchini, kuwa mafisadi uonea wananchi maskini  kwa kupora kwa nguvu ardhi wakidai wanamiliki wao na wanatumia badhi ya polisi wasiokua waaminifu ili kuwakandamiza wananchi hao.

Kutokana na hatua hiyo, Lugola amepiga marufuku kwa mwananchi yeyote ambaye anakurupuka kukimbilia kituo cha polisi kufungua kesi za ardhi ambazo hazina uthibitisho wa jinai yoyote, badala yake kesi au malalamiko yake kwanza ayapeleke katika mabaraza ya ardhi katika eneo husika ili ziweze kutatuliwa.

Lugola ameongeza kuwa, mafisadi hao ambao wanafedha baada ya kuona mmiliki halali wa ardhi hiyo anagoma kuondoka katika sehemu husika, basi utumia fedha zake kwa kukimbilia polisi kufungua kesi bila ya kuwa na uthitisho wowote huku baadhi ya polisi wasiokua waaminifu wakitumiwa katika kufanikisha ardhi hiyo ananyang’anywa mwananchi huyo.

“Kuanzia leo mwananchi yeyote atakaeenda kufungua kesi kituo cha polisi inayohusu masuala ya ardhi na endapo kiwanja hicho kimepimwa lazima awe na hati inayoonyesha yeye ni mmiliki halali, ili iwasaidie polisi wajue wewe ndio mmiliki halali, na kwa upande wa ardhi ambayo haijapimwa lazima mwananchi huyo aende polisi akiwa na uthibitisho kutoka kijijini au katika mtaa  unaosema kwamba eneo hilo ni la kwako na polisi wathibitishe hilo,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, na endapo kesi ya mlalamikaji yeyote ipo mahakamani anapaswa kuheshimu makahama na si kuendeleza kufanya usumbufu katika jamii pamoja na kwenda polisi na kuanza kutafuta njia ya kumsumbua mwananchi ambaye ni maskini katika eneo hilo.

Katika hilo, Lugola alifafanua kuwa, endapo mwananchi ana hukumu ya mahakamani inayoonyesha ameshinda kesi hiyo, mwananchi huyo anapaswa kwenda polisi na nakala ya hukumu yake ili polisi waweze kushuhudia kwamba pande zote mbili ziliwahi kugombana kuhusu ardhi na kufikishana mahakamani lakini mmojawapo alishinda.

“Rais Magufuli alianzisha Mahakama ya mafisadi hapa nchini, kwa taarifa niliokua nayo, mahakama hii ina uhaba wa mafisadi, sasa mimi nitaitafutia wateja kwa kuhakikisha wale mafisadi ambao uonea wananchi, utesa wananchi, uiba fedha za serikali au taasisi yoyote nitawafikisha katika mahakama hiyo, hatutakubaliana na manyanyaso ya aina yoyote katika Serikali hii ya awamu ya tano” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kua, hataki kusikia  mwananchi anaonewa, na pia aliapa hatacheka na mafisadi, atapambana nao sehemu yoyote nchini na pia yupo tayari kwalolote na  ameanza kupambana na mafisadi ndani ya wizara yake na tayari wameanza kurudisha fedha za Serikali.

Aidha, Lugola katika hotuba yake alipiga marufuku kwa waendesha bodaboda wenye tabia ya kubeba abiria zaidi ya mmoja kuiacha tabia hiyo ili kuepusha ajali, lakini aliwataka polisi kutorudi nyuma, wahakikishe wanawakamata waendesha bodaboda wasiofuata sheria za usalama barabarani.

Waziri Lugola yupo katika ziara jimboni kwake kwa kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuwaunganisha wananchi kupitia Bonanza lake la michezo ya mpira wa miguu ambalo linashirikisha kila kata wakitoa washindi mbalimbali ambao anawapa zawadi pamoja na kuingia moja kwa moja katika mashindano ya kugombea Kombe la Kangi.

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Awapiga Marufuku Wakuu wa Wilaya Kuweka Watumishi wa Umma Mahabusu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema hataki kusikia wakuu wa wilaya zilizopo katika Mkoa wake wakiwaweka ndani watumishi wa umma.

Mtaka ametoa kauli hiyo  Ijumaa Agosti 17, 2018 wakati akifunga kikao cha madaktari wa mikoa na wilaya zote nchi nzima uliofanyika mjini Dodoma.

“Sisi viongozi tuwalinde watumishi wetu, mimi nilipoenda kuwa mkuu wa mkoa wa Simiyu niliwaambia wakuu wangu wa wilaya kuwa sitaki kusikia mtumishi wa umma kuwekwa mahabusu,” amesema Mtaka.

“Wakati mwingine ukiona matamko ya wanasiasa kwenye maeneo ya kazi unajiuliza hivi RM0 (mganga mkuu wa mkoa) anakaa kwenye kikao kushauri haya yatokee? Kwenye mkoa wangu hutaona huu upuuzi.”

Agosti 14, 2018 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo alikemea tabia ya baadhi ya wakuu wa wilaya kutumia vibaya mamlaka waliyonayo kuwaweka watu ndani.

Aliwataka wakuu hao kuhakikisha wanasoma na kuzielewa sheria zinazowaongoza ili kufanya kazi kwa weledi.

Katika siku za hivi karibuni, wakuu wa wilaya wamekuwa wakitumia ‘sheria ya saa 48’ kutoa adhabu kwa kuwaweka baadhi ya watu mahabusu.

Mamlaka hiyo wamepewa kupitia Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 na hutakiwa kutumia amri ya kumweka ndani-kwa muda usiozidi saa 48-mtu au kundi la watu ambao kubaki kwao nje kunaweza kusababisha madhara  makubwa katika jamii.

Baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakitumia sheria hiyo kama adhabu au hukumu, badala ya malengo yaliyowekwa ya kulinda usalama wa watu wengine.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Viongozi Na Watumishi Nchini Wakumbushwa Kutekelza Majukumu Yao Kwa Kutanguliza Mbele Moyo Wa Uzalendo Na Masilahi Ya Taifa

$
0
0
Viongozi na Watumishi nchini wamekumbushwa kutanguliza mbele moyo wa uzalendo na masilahi mapana ya taifa wanapotekeleza majukumu yao ili kupeleka maendeleo ya taifa mbele na kuimarisha usalama wa taifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt (Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati akifunga kozi fupi ya tano kwa viongozi iliyofanyika Chuo cha cha Taifa cha Ulinzi – Tanzania (NDC) jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mkuchika amesema, ni matumaini kuwa washiriki waliohudhuria kozi hiyo, utendaji wao wa kazi utabadilika kwa kuwa na tija kwani sasa mbinu zote zinazohusu namna ya kufikiri kimkakati, kufanya tathmini katika mambo mbalimbali ili kufikia maamuzi wamezipata.

“Sasa mnatambua dhana ya usalama wa Taifa vema na kwa mapana zaidi, si kulinda mipaka na mali za wanajamii tu, bali pia inahusisha kutunza mazingira, kuwa na chakula cha kutosha, kupiga vita rushwa na madawa ya kulevya na mengine mengi ambayo ninyi mnayafahamu zaidi,” Mhe. Mkuchika amesema na kuongeza kuwa usalama wa watu ni muhimu kuliko jambo jingine lolote, hivyo masuala ya usalama yawe ni sehemu ya kuzingatia katika utendaji wa kila siku na hasa pale maamuzi yanayogusa masilahi ya nchi na jamii yanapotolewa.

Aidha, Mhe. Mkuchika amesema, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kuipeleka nchi katika Uchumi wa Viwanda, lakini suala la rushwa limekuwa kikwazo kikubwa kufikia lengo hilo, hivyo ni jukumu la viongozi wote kutoa majawabu ya namna gani malengo yatafikiwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi -Tanzania, Luteni Jenerali Paul Massao ameishukuru Serikali kwa kuhakikisha viongozi na watumishi wengine wanahudhuria kozi hiyo muhimu kwa masilahi ya taifa.

Jumla ya wahitimu 24 walikabidhiwa vyeti, baadhi yao wakiwa ni Waheshimiwa Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Viongozi Waandamizi wa Taasisi za Serikali.

Mtaala wa kozi hiyo ulilenga katika masuala yanayohusu masilahi, uzalendo na dhana nzima ya usalama wa taifa.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
TAREHE 18 AGOSTI, 2018

Magari Matano Ya Mizigo Yatekeketea Kwa Moto Boda Ya Rusumo Mkoani Kagera

$
0
0
Magari matano ya mizigo yameteketea kwa moto katika kituo cha forodha Rusumo Wilaya ya Ngara mkoani Kagera mpakani mwa Tanzania na Rwanda baada ya gari la mafuta ya petrol kuligonga gari jingine na kupoteza mfumo wa breki.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Augustino Olomi amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa yuko njiani akielekea eneo la tukio na taarifa zaidi itatolewa kuhusiana na kiasi cha mali iliyoungua.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Ngara, Luteni Kanali Michael amesema ukosefu wa zimamoto ni changamoto kubwa wilayani Ngara kutokana na matukio ya ajali ya moto kuongezeka na ombi lilishatumwa serikalini lakini utekelezaji wake haujafiki.

Ikumbukwe Julai 6, katika mkutano wake na waandishi wa habari Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola aliwashusha vyeo makamanda wawili kwakushindwa kudhibiti ajali, ambao ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya pamoja na Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto Mkoa wa Kagera ambapo alidai kuwa wameshindwa kutekeleza majukumu yao.

Julai 24, 2018 akiwa jijini Arusha Waziri Lugola alitoa onyo kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuacha mara moja tabia ya kutokwenda kwenye matukio ya moto kwa kisingizio cha kutokuwa na vifaa vya kutosha.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Waziri Mkuu: Kero Za Ardhi Tabora Zitatatuliwa Na Waziri Wa Ardhi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atakwenda katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ili kutatua kero kubwa za ardhi.

Ameyasema hayo jana jioni (Jumamosi, Agosti 18 ,2018) wakati akizungumza na wananchi wa Manispaa hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chipukizi.

Waziri Mkuu aliyasema hayo baada ya wabunge na wananchi kueleza changamoto kubwa zinazowakabili ikiwe ya migogoro ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu.

“Waziri wa Ardhi atakuja hapa na ramani zake, atakutana na watendaji na kumaliza matatizo yote makubwa ya ardhi na yale madogo madogo yatashughulikiwa na Mkuu wa Wilaya,”.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu alisema wilaya zote zinatakiwa zihakikishe zinakuwa na shule moja ya kidato cha tano na sita kwenye kila tarafa nchini na Serikali itapeleka walimu.

Alisema uwepo wa shule hizo utaamsha ari ya wanafunzi kusoma kwa bidii, jambo litakaloongeza idadi ya wanaoendelea na masomo ya kidato cha tano na sita.

Kadhalika Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji wote kuanzia ngazi ya halmashauri hadi vijiji wawasimamie wanafunzi wa kike na wahakikishe wanamaliza masomo bila ya kukatishwa.

“Huu ni mkakati wa Taifa tunataka watoto wa kike wote walindwe ili waweze kumaliza shule na marufuku kukatisha elimu yao, iwe kwa kuwapa ujauzito au kuwaoa, adhabu yake ni kali,”.

Waziri Mkuu jana jioni alimaliza ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tabora baada ya kuwa amefanya ziara katika wilaya za Igunga, Nzega na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, AGOSTI 19, 2018.

Nandy Afunguka Jinsi Familia Yake Itavyokuwa Pindi Akiamua Kuolewa

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Faustina Charles ‘Nandy’, amesema anatamani kuja kuwa na familia ya mfano wa kuigwa huku akitaja vigezo vitatu atakavyovizingatia.

Nandy anasema miongoni mwa sifa kubwa anazotamani ndani ya familia yake ni pamoja na ile ya kumcha Mungu, kutafuta pesa pamoja na kuwa na watoto wasiopungua watatu.

“Kila mmoja anatamani familia jinsi alivyojipanga mwenyewe, kwa upande wangu natamani sana familia iliyo bora, yenye hofu ya Mungu na ikipendeza nipate watoto wengi,” anasema Nady

Alisema anaamini wakati wake ukifika naye ataingia kwenye maisha ya ndoa na kutimiza malengo yake.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>