Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Na Historia Isiyofutika

$
0
0
Na Emmanuel J. Shilatu
Kama ambavyo Watanzania tunavyomkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa kusaidia ukombozi wa upatikanaji wa uhuru ama kama ambavyo Hayati Moringe anavyokumbukwa kwa mapambano ya ubadhirifu wa mali za umma, pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anazidi kujenga historia ya kipindi chote isiyofutika kutokana na utendaji, uchapakazi na uzalendo wake kwa Taifa.

Haya hapa ni baadhi ya Mambo ya kihistoria na yenye heshima kubwa kwa Taifa ambayo Rais Dkt. Magufuli aliyoyafanya;-

*(i) Kuhamia Dodoma*

Wazo la Serikali kuhamia kwenye makao makuu ya nchi mkoani Dodoma liliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mwaka 1973 lakini lilishindwa kutekelezwa katika awamu zote. Si awamu ya kwanza, wala ya pili, ama ya Tatu au ya nne bali limeweza kufanikiwa kwenye utawala wa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli. Leo hii karibia Serikali yote imehamia Dodoma. Wizara, taasisi na idara za Serikali, Waziri Mkuu wameshahamia Dodoma. Mwishoni mwa mwaka huu Rais Magufuli naye atahamia Dodoma. Iliasisiwa na Mwalimu Nyerere, ikahaidiwa kwenye ilani ya uchaguzi, imekuja kutekelezwa vyema na Rais Magufuli. Hii ni historia isiyofutika ya uthubutu, uzalendo alionao Rais Magufuli.

*(ii) Ujenzi wa Miundombinu*

Hili halina ubishi kwa asilimia kubwa kabisa miundombinu ya nchi hii imejengwa chini ya usimamizi wa Dkt. Magufuli toka alipokuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Waziri wa Ujenzi na sasa Rais wa nchi. Hauwezi ukazungumzia uwepo wa mitandao ya barabara nchi nzima pasipo kumtaja Rais Magufuli; hauwezi kuzungumzia uwepo wa madaraja makubwa ya kisasa kama ya Daraja la Nyerere, Daraja la Mkapa pasipo kumtambua mchango wa Rais Magufuli. Leo hii nchini tunajivunia uwepo wa flyovers. Rais Magufuli ameonyesha uwezo na heshima kubwa ya ujenzi wa Miundombinu nchini ambayo imekuwa msaada mkubwa wa kimawasiliano, usafirishaji wa Watu na mizigo, kukuza utalii, kuimarisha shughuli za kibiashara na kuongeza mapato ya nchi.

*(iii) Kulifufua Shirika la Ndege*

Tangu mwaka 1977 nchi yetu ilikuwa na shirika la ndege linalosua sua na linalojiendesha kihasara kubwa. Mara baada ya Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli imefanikiwa kununua ndege mpya 7 na mpaka sasa zimeshawasili ndege mpya 4 ikiwamo ndege kubwa aina ya Boeing 787-8. Wale baadhi wanaosema ndege si kipaumbele wala muhimu kwa Watanzania inabidi watambue Leo hii makusanyo ya mapato ndani ya Shirika la ndege (ATCL) yametoka Tsh. Milioni 700 mpaka kufikia Tsh. Bilioni 4.5. Hii ndio faida ambayo Watanzania tumeipata ya kuwa na kiongozi mwenye maono na mtazamo wa mbali zaidi, Rais Magufuli.

*(iv) Ujenzi wa Stiegler’s Gorge*

Utawala wa awamu ya kwanza uliokuwa ukiongozwa na Mwalimu Nyerere ulikuja na wazo wa kujenga Stiegler’s Gorge mnamo mwaka 1981 lakini umeshindwa kufanyika mpaka awamu hii ya 5 inayoongozwa na Rais Magufuli umeamua kufufua na kuliendeleza wazo hili. Mradi wa Stiegler’s Gorge kupitia Mto Rufiji utafanikiwa kuzalisha Megawattz 2100 utakapo kamilika. Ukamilifu wa mradi huu utajenga uhakika wa umeme nchini, utashusha bei ya umeme nchini na pia utamjengea Rais Magufuli heshima kubwa isiyofutika.

*(v) Mapambano dhidi ya Rushwa na ufisadi nchini.*

Rais Magufuli ameingia kwenye historia ya kiongozi ambaye Serikali anayoiongoza kuwa na mapambano ya dhahiri ya rushwa na ufisadi nchini. Tumeshuhudia Mafisadi Papa ambao walikuwa hawashikiki wala kukamatika wakipandishwa Mahakamani. Katika miaka ya nyuma ilikuwa suala gumu sana kwa Watuhumiwa “Mapapa” kuguswa tu, achilia mbali kupandishwa Mahakamani. Haya ni mapambano ya wazi wazi ya Serikali ya Rais Magufuli ya vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini. Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

*(vi) Uwazi wa taarifa na udhibiti wa rasilimali za nchi*

Tumeshuhudia Serikali ikiweka uwazi kwenye mikataba na uchunguzi wa rasilimali za Taifa na kuweka makubaliano mapya yenye tija Mathalani tumeona uwazi wa sekta ya madini ya dhahabu, almas na Tanzanite ambapo Taifa tumeona namna ambavyo tulivyokuwa tukiibiwa na Serikali kuweka mikakati mipya ya kutokuibiwa tena. Kama haitoshi tumeshuhudia wawekezaji wakibanwa vilivyo juu ya mikataba isiyokuwa na tija kwa Taifa. Ni Serikali ya Rais Magufuli iliweka uthubutu wa kuwabana wawekezaji wa madini wa ACACIA iliyozaa matunda kwa Serikali ya Tanzania kumiliki asilimia 16 ya hisa katika makampuni ya uchimbaji wa madini, Serikali kupata gawio la faida ya madini ya asilimia 50 kwa 50. Yote haya yamewezekana kwa sababu ya uzalendo wake Rais Dk. Magufuli

*(vii) Ujenzi wa Bomba la Mafuta*

Serikali ya Rais Magufuli imefanikisha vilivyo kushirikiana na nchi ya Uganda kujenga Bomba la Mafuta linalotoka nchini Uganda mpaka Tanga nchini Tanzania. Ujenzi huo wa bomba la mafuta utazalisha ajira nchini na utaongeza pato la Taifa. Hayo yote yamefanikiwa kutokana na Serikali ya Rais Magufuli kuzidi kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi nyinginezo.

*Itaendelea …..*
*Shilatu E.J*
0767488622

Gigy Money: Natamani Mwanangu Aige Tabia Zangu na Ntamuunga Mkono

$
0
0
Msanii wa bongo fleva na 'video vixen' nchini, Gigy Money amesema atajisikia furaha na amani endapo mtoto wake wakike aliyempa jina la Mayra,atafata nyayo zake.

Gigy ameiambia Enewz ya EATV kwamba, haiwezi ikatokea mtoto akawa na role model tofauti na mtu ambaye amemzaa.

"Kila mtoto yoyote 'role model' wake ni mama yake mzazi hata iwaje.  Huwezi kusema mwanao atakuwa 'role model' wa mtu mwingine. Hivyo mwanangu atakuwa tu vyovyote atakavyotaka kuwa mimi nitampa ushirikiano. siwezi kumlaumu hata akitaka kuwa kama mimi ila ndio ntazidi kufurahi", amesema Gigy.

Pamoja na hayo, Gigy ameendelea kwa kusema "siwezi kujutia kuzaa halafu kingine ni kwamba kujipanga utajipanga baadae huko wala hupaswi kuwaza kuwa itakuaje nikifanya jambo fulani. Maisha ya siku hizi hayana hiyo kitu, Mungu yupo kila siku anatenda".

Waziri Mkuu Ahimiza Ubobezi Kwenye Sheria

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuibuka kwa sekta za mafuta na gesi hapa nchini kumeleta haja ya kuwa na wabobezi wa masuala hayo katika taaluma ya sheria. 
 
“Taaluma ya sheria kwa sasa inahitaji kuwepo kwa ubobezi. Imekuwa si rahisi tena kwa mwanasheria kuwa na utaalamu wa kutosha katika maeneo yote ya sheria. Hii inatokana na ukweli kuwa taaluma ya sheria imepanuka na masuala mapya kama vile mafuta, gesi, haki bunifu na makosa ya kimtandao yamekuwa yakijitokeza kila kukicha,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumatano, Agosti 15, 2018) wakati akizungumza na wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema uzinduzi wa ofisi hizo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhamishia makao makuu ya nchi Dodoma. “Uzinduzi wa Ofisi unakamilisha uwepo wa mihimili yote mitatu hapa Dodoma. Mahakama Kuu imetengewa ekari 50 na Ofisi za mabalozi zimetengewa ekari 1,800; na wanatakiwa kuanza ujenzi mara moja,” amesema.

Amesema ofisi hizo ni matokeo ya juhudi za makusudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli anazochukua katika kuboresha mfumo wa utoaji haki nchini na kuimarisha ulinzi wa maliasili na utajiri wa Taifa kwa kuunda Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

“Uamuzi huu wa Mheshimiwa Rais unalenga kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanapata haki zao kwa wakati na pia maslahi na heshima ya nchi vinalindwa kikamilifu,” amesema.

Akizungumzia kuhusu kuanzishwa kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Waziri Mkuu amesema ni matarajio ya kila mwananchi kuwa ofisi hiyo itapanua zaidi wigo wa utendaji wake hadi kufikia ngazi ya wilaya.

“Binafsi naamini kuwa, huu ni wakati muafaka wa kuongeza kasi ya kutekeleza dhana ya utenganishaji wa shughuli za mashtaka na upelelezi. Hatua hii, itapunguza kama siyo kuondoa kabisa malalamiko ya wananchi kuhusu vitendo vya kubambikiziwa kesi vinavyodaiwa kufanywa na vyombo vya upelelezi. Ofisi hii inategemewa kuwa mkono wa Serikali katika kuhakikisha kuwa vitendo vya ubambikizaji wa kesi vinakoma na kuhakikisha kuwa kesi zinazofikishwa mahakamani zina ushahidi wa kutosha,” amesisitiza.

Kuhusu Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Waziri Mkuu amesema Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ndiyo mtetezi na mlinzi namba moja wa haki za Serikali na umma wa Watanzania kwa ujumla wake na inapaswa kuhakikisha kuwa maslahi ya nchi yanalindwa katika kesi zote za madai ambazo Serikali inashtaki au kushtakiwa ndani na nje ya nchi.

“Ofisi hii inategemewa kuwa itajizatiti kujenga ubobezi kwenye maeneo ya uendeshaji wa kesi za madai na usuluhishi ili kuhakikisha kuwa inashiriki kikamilifu na tena kwa weledi katika kuendesha kesi za madai ndani na nje ya nchi. Kujengwa kwa ubobezi katika ofisi hii, kutalisaidia Taifa kuokoa fedha nyingi ambazo wakati mwingine Serikali hutumia kuwalipa mawakili wa kigeni hususan katika mashauri ya usuluhishi nje ya nchi,” amesema.

Akizungumza kuhusu ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri Mkuu amesema mabadiliko ya kimuundo yaliyofanywa na Rais Magufuli hayana budi kuwa chachu kwa ofisi hiyo ili iweze kuishauri Serikali katika masuala ya kisheria hususan yale yanayohusu mikataba.

“Kama ilivyo kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali nayo inategemewa kuwa itajenga ubobezi katika maeneo mbalimbali ili kuiwezesha kutoa ushauri mzuri kwa Serikali,” ameongeza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema anaunga mkono uamuzi wa Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi wa kutaka kuwepo na kanzidata ya wanasheria wote waliopo nchini ili waweze kutambulika kwa urahisi.

“Pia endeleeni na mpango wa kuwapangua wanasheria kama mlivyojipanga, hii itasaidia kuleta ubobezi kwenye maeneo yao. Pia sheria zibadilishwe na kuwekwa kwenye Kiswahili ili wananchi wazielewe kwa urahisi,” amesema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, AGOSTI 15, 2018.

Waziri Mkuu: Bado Tunahitaji Wawekezaji Kwenye Sukari

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania bado inawahitaji wawekezaji zaidi katika sekta ya uzalishaji wa sukari ili iweze kukidhi mahitaji.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania mwenye makazi yake Maputo nchini Msumbiji, Mheshimiwa Jean Pierre Jhumun, ofisini kwake jijini Dodoma.

“Mwaka jana nilikiwa nchini Mauritius nilihudhuria Jukwaa la Wafanyabiashara na Wawekezaji kati ya Tanzania na Mauritius, ambapo nilipata fursa ya kuwashawishi wawekezaji wa Mauritius waje kuwekeza kwenye viwanda vya sukari nchini,”.

Ameongeza kuwa Tanzania ina fursa kubwa ya maeneo ya uzalishaji wa sukari ambayo bado hayajaendelezwa, hivyo kama kuna wawekezaji walio tayari na wamekidhi vigezo waendelee na hatua za uzalishaji.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa mbali na kuhitaji wawekezaji kwenye sekta ya sukari, pia amewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Mauritius kuja kuwekeza kwenye sekta ya uvuvi. “Mnaweza kuja kuwekeza kwenye viwanda vya usindikaji wa samaki kwani tuna bahari, mito na maziwa yenye samaki wa aina mbalimbali,”

Kwa upande wake, Balozi Jhumun amesema wawekezaji wa Mauritius  wapo tayari kuwekeza katika uzalishaji wa sukari pamoja na uvuvi na wameshafanya utafiti katika baadhi ya maeneo.

Balozi Jhumun amesema ameambatana na Mwenyekiti wa Mfuko wa Uwekezaji wa Sukari,  Bw. Gansam Boodram kutoka nchini Mauritius kwa ajili ya kufuatilia maeneo ya uwekezaji.

“Tumeitikia wito wa Rais Dkt. John Magufuli wa  kututaka kusaidia katika upatikanaji wa wawekezaji watakaokuja Tanzania kuwekeza kwenye viwanda vya uzalishaji wa sukari,”.

Naye Bw. Boodram amesema tayari wameshatembelea baadhi ya maeneo wanayohitahi kwa ajili ya uwekezaji na wameshafanya utafiti wa udongo pamoja na masoko. Maeneo waliyoyafanyia utafiti ni Kasulu na Kibondo mkoani Kigoma pamoja na Rufiji mkoani Pwani.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, AGOSTI 15, 2018.

Makamu Wa Rais Kumuwakilisha Rais Magufuli Katika Mkutano Wa SADC Nchini Namibia

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anaondoka nchini leo kuelekea Windhoek, Namibia kushiriki kwenye Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (38th Ordinary Summit of SADC Heads of State and Government) unaotarajiwa kufanyika tarehe 17 na 18 Agosti, mwaka huu akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mkutano huo utakaofanyika chini ya Uenyekiti wa Namibia, utatanguliwa na Mikutano mingine mitatu ambayo ni Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali  wa Organ Troika, Mkutano wa Baraza la Mawaziri  na Mkutano wa Makatibu Wakuu.  

Aidha, Mkutano huo utapokea na kujadili agenda mbalimbali ikiwemo Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa SADC, Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama, taarifa ya Mwenyekiti anayeondoka wa SADC Organ, taarifa ya Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, hali ya kiuchumi katika kanda ya SADC na taarifa kuhusu utekelezaji wa Kaulimbiu ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa mwaka 2017.

Vilevile, Mkutano utapokea  Kaulimbiu ya Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali   na kupokea taarifa ya hali ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa SADC. Katika Mkutano huo, Tanzania inategemea kuteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa SADC kwa kipindi cha Agosti 2018 hadi Agosti 2019.

Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam
15/8/2018

Waziri Mkuu Kuanza Ziara Ya Siku 3 Mkoani Tabora Kesho

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Tabora ambapo atawasili mkoani  humo kesho.

Baada ya Waziri Mkuu kuwasili atapokelewa na viongozi wa Serikali na kusomewa taarifa ya Mkoa wa Tabora.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri Waziri Mkuu atatembelea Wilaya ya Igunga, Nzega na Manispaa ya Tabora kwa ajili ya kuzungumza na wananchi, watumishi wa umma na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuwa akiwa wilayani Igunga atazungumza  na wakazi wa Jimbo la Igunga , Manonga na watumishi wa umma na kukagua Kiwanga cha Pamba cha Manonga.

Mwanri aliongeza kuwa baada ya kutoka Igunga Waziri Mkuu atakwenda Nzega na kuzungumza na wananchi wa Jimbo la Bukene, Nzega Mjini na Nzega na watumishi wa umma.

Alisema Waziri Mkuu atakamilisha ziara yake katika Manispaa ya Tabora kwa kuzungumza na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Tabora na Hospitali ya Rufaa Kitete na kukagua maendeleo ya Chuo cha Afya katika Hospitali ya Rufaa Kitete.

Mwanri alisema Waziri Mkuu pia atapata fursa ya kutembelea Kiwanda cha Nyuzi (Tabora Textile) , Kiwanda cha Maziwa na kuongea na wananchi wa Jimbo la Tabora kabla ya kuondoka na kuendelea na majukumu mengine ya ujenzi wa Taifa.

Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kumlaki Waziri Mkuu na kumsikiliza na kuwa tayari kupokea maagizo atakayotoa.

Ubalozi wa Marekani Tanzania watoa ripoti yao juu uchaguzi wa Marudio Uliofanyika Buyungu na Kata Zingine 79

$
0
0
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa taarifa yao kuhusu uchaguzi wa marudio uliomalizika August 12, katika Kata 79 na Jimbo la Buyungu ambapo Mbunge wake alifariki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika website ya US Embassy Tanzania imeeleza kuwa uchaguzi huo uligubikwa na matukio ya fujo na ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi.

Wametoa mfano kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kushindwa kuwasajili baadhi ya wagombea wa upinzani.

Pia umeguswa na vitisho vilivyotolewa na Jeshi la Polisi kwa Wagombea na wanachama wa vyama vya upinzani ikiwemo pamoja na kukamatwa kwa wagombea na kuzuia mikutano ya kampeni.

IGP Sirro Afanya Mabadiliko Ya Makamanda Wa Polisi Mkoa wa Mwanza na Pwani


Fred Lowassa ajiondoa kuwania ubunge Monduli

$
0
0
Kada wa Chadema, Fred Lowassa leo Agosti 15 amejiondoa kwenye kinyang’anyiro cha wanaowania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge jimbo la Monduli.

Baada ya kujiondoa, Chadema kimempitisha diwani wa kata ya Lepurko, Yonas Masiaya Laizer kuwania ubunge wa jimbo hilo.

Fred, ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa alichukua fomu ya kuwania ubunge jimbo hilo wiki iliyopita.

 Aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Julius Kalanga, alijiuzulu uanachama wa Chadema na ubunge na kuhamia CCM. Kalanga ameshateuliwa na CCM kugombea ubunge jimbo hilo.

Akizungumzia uamuzi wa Fred, katibu wa Chadema mkoa wa Arusha, Amani Golugwa alisema baada ya kushauriana, vikao vya uteuzi vilikubali kuondoa jina lake.

"Ni kweli nathibitisha kuwa ameomba kwa sasa si wakati muafaka licha ya kuwa alionesha nia awali na wananchi wengi walimuunga mkono, hivyo chama kimekubali maombi yake na kimempitisha mgombea mwingine,"amesema Golugwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Agosti 16

Alichoandika Msemaji Mkuu wa Serikali Baada ya Ubalozi wa Marekani Kudai Uchaguzi wa Marudio Buyungu Ulikuwa na Kasoro

$
0
0
JANA Ubalozi wa Marekani ulichapisha tamko lao kuhusu uchaguzi wa marudio uliomalizika August 12, katika Kata 79 na Jimbo la Buyungu ambapo Mbunge wake alifariki.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uchaguzi huo uligubikwa na matukio ya fujo na ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi.

Walitoa mfano kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kushindwa kuwasajili baadhi ya wagombea wa upinzani.

Pia wameguswa na vitisho vilivyotolewa na Jeshi la Polisi kwa Wagombea na wanachama wa vyama vya upinzani ikiwemo pamoja na kukamatwa kwa wagombea na kuzuia mikutano ya kampeni.

Muda mfupi baada ya taarifa hiyo kusambaa Msemaji wa Serikali Dr. Hassan Abbas amesema Serikali inajiridhisha juu ya taarifa hiyo na watatoa tamko lao punde.

“Kuna taarifa inasambaa kuhusu kinachodaiwa ni taarifa ya ubalozi mmoja kuhusu masuala ya ndani ya nchi. Tunajiridhisha. Tutatoa tamko punde” Msemaji Mkuu wa Serikali

Serikali Yatahamaki Saruji Kuadimika Sokoni na Kupanda Bei....Yawaita Wadau Kujadiliana

$
0
0
Serikali imekutana na wadau wa sekta ya viwanda kujadili kuadimika kwa saruji, huku inayopatikana ikiuzwa bei ya juu.

Kikao hicho kilichoongozwa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya kilihudhuriwa na wazalishaji wa saruji na wa makaa ya mawe, wasafirishaji na wadhibiti.

Akizungumza katika mkutano huo Manyanya amewataka wazalishaji wa saruji kueleza uwezo wao wa uzalishaji.

Naibu waziri pia amewataka kueleza sababu za kusimamisha uzalishaji ghafla na kwa viwanda vyote.

"Imetushitua kuona saruji imepotea sokoni na kupanda bei ghafla, tena viwanda vyote. Tukasema hapo ni zaidi ya masuala ya kiufundi, kwa hiyo tumewaita kuwasikiliza tujue tatizo ni nini ikiwezekana leo tutoke na uamuzi,” alisema Manyanya.

Alisema sasa kuna fursa nyingi za soko la saruji kupitia miradi inayotekelezwa na Serikali na kwamba  hiki ndicho kipindi cha kuongeza uzalishaji lakini anashangazwa kuona saruji imeadimika na bei imepanda.

RC Songwe Brigedia Jenerali Mwangela Akataa Ombi La Mkandarasi Kuongezewa Muda

$
0
0
Na Grace Gwamagobe -Afisa Habari Songwe
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemas E Mwangela amekataa ombi la Mkandarasi kutoka kampuni ya Mats Engineering Ltd Paulo Philipo Paulo la kuongezewa kipindi cha miezi miwili ili aweze kukamilisha ujezi wa Daraja la Kikamba Wilayani Songwe.

Brigedia Jenerali Mwangela amekataa ombi hilo jana alipokagua ujenzi wa daraja la Kikamba linalounganisha kata za Kapalala na Gua wilayani Songwe kwakuwa sababu alizotoa mkandarasi huyo hazijitosheleji.

Alisema daraja hilo lazima likamilike kwa muda uliopangwa ambao ni Septemba, 2018 huku mkandarasi huyo akitoa sababu kuwa atachelewa kukamilisha ujenzi huo kutokana na mvua nyingi zilizonyesha na mwamba mgumu uliopo eneo la ujenzi.

“Mkandarasi ahakikishe anafanya kazi mchana na usiku ili akamilishe ndani ya muda wa mkataba, vifaa vya kumuwezesha kufanya hivyo anavyo na ombi la kuongezewa muda wa ujenzi mimi siafikiani nalo”, alisema Brigedia Jenerali Mwangela.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia alisema yeye na viongozi wengine wataendelea kusimamia miradi ya maendeleo na katika ujenzi wa daraja hilo watahakikisha wanamsimamia mkandarasi huyo ili amalize ndani ya muda uliopangwa.

Daraja la Kikamba linalolunganisha kata za Kapalala na Gua limeanza kujengwa mwezi Oktoba 2017 na linatarajiwa kukamilia Septemba 2018 likiwa limegharimu shilingi bilioni 1.4.

Profesa Kabudi Atema Cheche Dodoma......Akerwa na maamuzi kufanyika bila Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kuarifiwa

$
0
0
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuanzia sasa mawakili walioko kwenye Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na wanasheria wote katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa na taasisi za Serikali watakuwa ni Mawakili wa Serikali.

Ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumatano, Agosti 15, 2018) kabla hajamkaribisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ahutubie wageni waliohudhuria uzinduzi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Dodoma.

“Kwa miaka mingi kumekuwa na ombwe la usimamizi wa wanasheria walio kwenye utumishi wa umma. Maamuzi mengi yamekuwa yakifanyika pasipo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kuwa na taarifa. Mambo yanapoharibika ndio Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inataarifiwa ili kuokoa jahazi,” alisema.

Alisema hali hiyo kwa miaka mingi imekuwa ikiisababishia Serikali kuingia kwenye migogoro na kuingia hasara. “Baada ya mabadiliko haya, wanasheria wote walioajiriwa katika utumishi wa umma wanakuwa wanafanya kazi na kutumia mamlaka ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndani ya wizara zao, taasisi zinazojitegemea na Mamlaka za Serikali za Mitaa,” alisema.

“Vilevile wanasheria hao watakuwa chini ya uangalizi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Nia ya mabadiliko haya ni kumuwezesha Mwanasheria Mkuu wa Serikali awe na usimamizi juu yao na kuwazuia kufanya kazi bila kufuata maelekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.”

Prof. Kabudi alisema mashirika yote ya kimkakati kama vile Bandari, TANESCO nayo pia yataletwa chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kuepuka kuitia Serikali hasara. “Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye mashirika haya, lakini kuna maamuzi yanafanyika wakati Ofisi ya Mwanasheria Mkuu haina taarifa,” amesema.

“Kutokana na  marekebisho hayo, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itaratibu na kusimamia Mawakili wa Serikali walio katika Ofisi hiyo na wanasheria wote katika Wizara, mamlaka za serikali za mitaa na taasisi za Serikali ambao sasa watakuwa ni Mawakili wa Serikali. Aidha, Mawakili wa Serikali walio katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali watakuwa chini ya uratibu na usimamizi wa Mkurugenzi wa Mashtaka na Wakili Mkuu wa Serikali,” amesema.

Amesema marekebisho hayo yanatokana na marekebisho ya muundo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia matangazo ya Serikali Na. 48, 49 na 50 ya tarehe 13 Februari, 2018.

“Leo tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kufanya marekebisho hayo. Rais alianzisha Ofisi huru ya Taifa ya Mashtaka kuchukua nafasi ya iliyokuwa Divisheni ya Mashtaka chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Vilevile, Rais alianzisha Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya usimamizi na uendeshaji wa mashauri ya madai yakiwemo ya kikatiba ambayo Serikali ni mdaawa ambayo awali yalikuwa yakishughulikiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,” amesema.

Amesema marekebisho hayo yanakusudia kuongeza ufanisi katika uendeshaji wa mashtaka ya jinai nchini hususani utekelezaji wa azma ya Serikali ya kutenganisha shughuli za upelelezi na uendeshaji wa mashtaka. “Kuanzishwa kwa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kunalenga kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa mashauri ya madai na pia kuiwezesha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuimarika katika weledi na ubobezi wa kitaalamu katika kuishauri Serikali na kuandika Miswada ya Sheria kwa kuzingatia mabadiliko makubwa katika tasnia ya sheria kitaifa, kikanda na kimataifa,” ameongeza.

Hata hivyo, Prof. Kabudi alionya kwamba mabadiliko yoyote hayawezi kuleta matokeo yaliyokusudiwa kama watendaji hawatabadili mtizamo wao. Ni kweli muundo uliobadilishwa ulikaa kwa miaka mingi na inawezekana mambo mengi yalikuwa yanafanyika kwa mazoea. “Kutokana na mabadiliko haya, tunakiri kuwa mitizamo yetu na ya watumishi wenzetu lazima ibadilike. Tumejipanga kuhakikisha kuwa watumishi hawafanyi kazi kwa mazoea ili wasiwe na tashwishwi wala ajizi katika kutekeleza majukumu ya umma.”

“In public service, learn to swallow your pride. In public service, learn to learn your limits. In public service, learn to obey the authority above you, and if you don’t, resign and quit,” alisisitiza.

“Tumejipanga kufanya kazi kwa weledi na katika hili tutaweka mikakati ya kuwaongezea watumishi wa ofisi hizi ujuzi katika maeneo mahususi, na katika hilo tutaweka mipango ya kuwafanyia placement ndani na nje ya nchi ili wapate ujuzi mahususi na kuhakikisha wanapata mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika maeneo mbalimbali.

Alisema wameanza mkakati wa kuanzisha umoja wa wanasheria walio katika utumishi wa umma ili kuwawezesha kukutana mara kwa mara na kwamba Agosti 30-31 mwaka huu, wanatarajia kufanya mkutano huo ili kuwaunganisha wanasheria wote wajione wanafanya kazi moja na katika Serikali moja.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Tume Ya Uchaguzi Yaujibu Ubalozi wa Marekani Sakata la Uchaguzi wa Marudio Kuwa na Dosari

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekiri kuona tamko lililotolewa na Ubalozi wa Marekani Tanzania kupitia tovuti yake  linalohusu uchaguzi mdogo uliofanyika  Agosti 12 mwaka huu.

Taarifa hiyo ya Ubalozi ilionesha masikitiko makubwa kuhusu namna mchakato wa uchaguzi katika Kata 36 na Jimbo la Buyungu ulivyofanyika.

NEC imeutaka Ubalozi wa Marekani nchini uthibitishe madai yao kuhusu uchaguzi mdogo wa jimbo la Buyungu na kata 36.

==>>Hili ni tamko la NEC

Meneja wa WCB, Sallam SK adai hakuna bifu kati ya Diamond na Alikiba

$
0
0
Moja ya mameneja kutoka kwa WCB, Sallam SK amefunguka kuhusu bifu la Diamond la Alikiba.

Katika mahojiano na The Playlist ya Times Fm amesema wasanii hao hawana bifu na kama lipo kuna watu wametengeneza.

"Actually hamna ugomvi, hivi vitu vilitengenezwa na actually watu waliotengeneza wanajulikana, haina haja ya kuwataja kuwa airtime sana," amesema.

"Kati ya Ali na Diamond hamna bifu hata siku moja, haijawahi kutokea na uongozi wa Ali na wetu tunakutana tunacheka na kuongea," amesema Sallam.

WCB waeleza bado Rich Mavoko ni wao, na hakuna Mkataba wa Kinyonyaji

$
0
0
Meneja Sallam SK kutokea WCB amesema hadi sasa Rich Mavoko ni msanii wao licha ya yote yanayozungumzwa.

Katika mahojiano na The Playlist ya Times FM amesema bado anashindwa kuelewa malalamiko ya msanii huyo ni yapi kwa sasa,

"Rich Mavoko mpaka sasa ni msanii wa WCB;  Nasema ambapo ni mkataba ulivyo, Rich Mavoko ni msanii wa WCB na pato lake lote linapitia WCB," amesema.

Ameendelea kwa kusema hata channel ya YouTube ya msanii huyo aliyopandisha wimbo wake mpya 'Happy' ipo chini ya WCB.

Pia ameeleza kuwa iwapo ameamua kujitenga na wenzake ni maamuzi yake kwani huwezi kumpangia mtu ila bado wanatambua ni msanii wao na hajawahi kupewa adhabu ya kusimamishwa kama inavyodaiwa.

"Mpaka sasa hivi sijui malalamiko yake ni yapi kwa sababu ukisema sisi tunamnyonya mtu hiki kitu hakiwezekani. Kwanza ukiangalia kwenye mkataba wetu msanii anapata percent kabla hajakatwa kodi, ukiangalia hapo nani ananyonywa?," amesema Sallam SK.

Utakumbuka August 09, 2018 msanii Rich Mavoko alifika ofisi za Baraza la Sanaa Taifa, moja ya vitu vilivyoelezwa ni kuwa alipeleka mkataba wake na WCB katika Baraza hilo kwa kile kinachodaiwa ulikuwa wakinyonyaji.

Mkataba huo inatarajiwa kupitiwa na Tume uliyoundwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ingawa  BASATA walieleza kuwa kutakuwa na kikao kati ya WCB na upande wa Rich Mavoko kwa lengo la kusuluhisha.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Kusinyaa Na Kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kama uume wako  umedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 
 
Ipo dawa  ya ASILI   ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.
 
Ni  dawa  ya  asili  kabisa ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI YA  KUPATA  TIBA  HII : Kupata  tiba  hii  fika  ka6ika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam  ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu  watapelekewa  dawa  mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )  na kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  au  boti  kwa  waliopo  Zanzibar.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :    0693  005 189.

WCB waongoza kuwania AFRIMA, Alikiba, Vanessa Mdee na Nandy Watoswa

$
0
0
Tuzo za All Africa Music Awards (Afrimma) za nchini Nigeria zimetoa list ya wasanii ambao wameingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Wasanii wengi wa Tanzania wameshindwa kufanya vizuri safari hii baada ya wasanii wa WCB   kutawala zaidi kwenye list hiyo.

Katika kipengele cha Best Male Artiste in Eastern Africa, Diamond, Raynanny pamoja na Harmonize wanachuana pamoja.

Kwa upande wa wasanii wa kike, Maua Sama amekuwa nominated kupitia kipengele cha Best Female Artiste in Eastern Africa.

Alikiba na Vanessa Mdee ni kati ya wasanii ambao wamekuwa wakitajwa mara kwa mara lakini mwaka huu wameshindwa kufurukuta kabisa.

Muigizaji wa Bongo Movie, Odama azushiwa kifo

$
0
0
Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Jennifer Kyaka maarufu kama ODAMA amezushiwa kifo na watu kwenye mtandao wa facebook.

Odama akielezea kilichotokea ame-screenshot picha za matangazo na kuyaposti kwenye kurasa zake za mitandao ya kujamii na kuujulisha umma kuwa habari hizo sio za kweli.

Odama kwenye maelezo yake amemshukuru mtu huyo aliyemzushia kifo ambapo amedai kuwa kifo kinapangwa na Mungu na muda wake ukifika basi atakufa ila sio kwa kuzushiwa na binadamu.

“Kifo kipo na hakuna atakaekikwepa, kila binadamu ataonja mauti na kukamilika kwa maisha yetu hapa duniani. Lakini pia hata kama humpendi mtu unamchukia iwe alikutendea ubaya au umeamua tu kumchukia sio vizuri kumuombea kifo tena ukaona haitoshi basi unaweka matangazo mitandandaoni.

‘Nakushukuru wewe ulieamua kufanya hili, najua unaniongezea umri wa kuishi, na nikuambie tu kua mimi ni mzima wa afya na ninaishi kwa kudra za Mungu. Nitakufa tu pale siku yangu itakapofika mungu atakapoamua kunichukua lakini sio kwa kutaka wewe.

“Sijui nilichokukosea mpaka kufikia kunitangazia kifo. Nakuombea maisha marefu ili uendelee kuniona nikivuta pumzi ya mungu. Binadamu sisi laiti tungelijua kua si kitu kabisa tungeacha chuki zisizo na sababu. Asante mungu kwa kila kitu,”
ameandika Odama.

Jambo la kuzushiwa vifo kwa mastaa na viongozi maarufu limekuwa likikithiri siku hadi siku, ikumbukwe kwamba enzi za uhai wake, Mzee Majuto aliwahi kuzushiwa kifo mara kadhaa na yeye kukanusgha, wengine ni Mzee Agustiono Mlema na wengine jambo ambalo si la kiungwana.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images