Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Kubenea adai Hana Mpango wa Kuhamia CCM, Posti yake instagram yajadiliwa kila kona

$
0
0
Na Magdalena Kashindye
MBUNGE wa Ubungo, Saed Kubenea amesema hana mpango wa kuhamia Chama cha mapinduzi CCM kwa sasa.

Kubenea amekuwa akihusishwa kikihama chama chake  cha CHADEMA  tangu mwaka jana, wimbi la viongozi, wabunge na madiwani wa upinzani kujiuzulu nafasi zao na kujiunga na kujiunga na CCM.

Juzi aliandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram akitetea uamuzi wa viongozi wa upinzani kujiuzulu nafasi zao na kujiunga na CCM.

Ujumbe huo wa mbunge Saed ulisambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii na kuibua mjadala kutokana na kuhusishwa kwake kwa muda mrefu kujiunga na chama tawala.

"Si wote wanaohama wamenunuliwa, ingawa ni kweli kuwa wapo baadhi ya waliohama wamenunuliwa. Kuna wengine wamehama kutokana na kuwapo migogoro, chuki na ubaguzi katika maeneo waliyokuwapo." ilisomeka hivyo posti ya Kubenea

Alipotafutwa na Gazeti la Nipashe, kutaka  kujua juu ya ujumbe wake  alioposti Kubenea alikiri kuuandika na kueleza kuwa kuhamia CCM kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, kulimsukuma kuandika ujumbe huo.

"Ujumbe huo ni kweli ni wa kwangu," Kubenea alisema, "niliandika baada ya Julius Mtatiro kutangaza kuhama CUF na kujiunga na CCM.

"Inawezekana hakunuliwa, lakini inawezekana njaa ndiyo imempeleka huko kwa sababu kwanza ukumbuke chama chake kina mgogoro mkubwa, pia upande aliokuwa yeye, hakuna ruzuku. Kwa hiyo, hawakuwa na pesa ya kujiendesha na ndiyo maana akaona ahame tu.

"Nasema hivyo kwa sababu kuna baadhi ya watu ambao mimi nawafahamu, walihama na hawakununuliwa isipokuwa walishindwa kuvumilia baada ya kukutana na watu ambao walitofautiana nao kimawazo, yaani mawazo yao yalikinzana, wao badala ya kuvumilia walishindwa."

Alipoulizwa kuhamia CCM  kama naye ni miongoni mwa wanaodaiwa wako kwenye njiani  kujiunga na CCM, Kubenea alisema hana mpango wa kukihama chama chake kwa sasa.

Hii ni mara ya pili kwa Kubenea kukana taarifa za kukihana chama chake kwani wiki chache zilizopita alisema hawezi kahama na kama kunamapungufu watayarekebisha ndani na akishindwa ataendelea na shughuli zake za uandishi wa Habari.

Habarika Masaa 24......Pakua Upya Application Yetu Tukuhabarishe Usiku na Mchana

$
0
0
==>Pakua Upya Application yetu tukuhabarishe masaa 24 usiku na mchana.

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia;

IGP Ampandisha Cheo Mwanariadha Kwa Kuvunja Rekodi.

$
0
0
Na. Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amempandisha Cheo Mwanariadha wa Polisi Fabian Nelson kutoka Konstebo hadi Koplo baada ya kuchukua medali ya dhahabu  na kuvunja rekodi ya mbio za mita 5000 katika Michezo ya Shirikisho la Wakuu wa Majeshi ya Polisi Ukanda wa Afrika Mashariki (EAPCCO)  iliyomalizika mwishoni mwa wiki Jijini Dar es Salaam.

Mwanariadha huyo alikimbia dakika 13: 45: 99 na kuwashinda Wanariadha wa Jeshi la Polisi la Kenya na Uganda ambapo Tanzania  ilishika nafasi ya pili katika ushindi wa jumla ambapo nafasi ya kwanza ilienda Kenya na  ya tatu Uganda.

IGP Sirro alimpandisha Cheo hicho katika hafla ya kuwapongeza Wanamichezo walioshiriki Michezo hiyo katika bwalo la Maafisa wa Polisi Oystabya IGP Sirro alisema mwanariadha huyo amekuwa akionyesha juhudi katika mbio ndefu jambo ambalo limekuwa likileta sifa kwa Jeshi la Polisi na nchi kwa Ujumla.

 “ KIla mmoja anastahili pongezi kutokana na kutuwakilisha vizuri katika michezo hii, hivyo tunathamini mchango wa kila mmoja kwa nafasi yake katika kuitangaza nchi yetu na nawaahidi tutaendelea kutambua mchango wa kila mmoja” Alisema Sirro

Aidha, Alisema maandalizi ya michezo ijayo yanaanza sasa ili kuhakikisha kuwa wanaendelea kufanya vizuri zaidi na kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika michezo ya mwaka huu ikiwemo kuingia kambini mapema na kuajiri wanamichezo pindi nafasi zitakapopatikana.

Kwa upande wake Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa alisema kazi iliyofanyika ni kubwa na kila mshiriki alijituma kuhakikisha kuwa Vikombe na medali zinabaki hapa nchini.

Michezo inayoshindaniwa ni pamoja na soka ,mpira wa mikono, mpira wa wavu, mpira wa pete, Ngumi, Taekwondo, Judo na Riadha ambapo nchi zilizoshiriki ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudani, Sudani Kusini na Tanzania.

Mbowe Na Vigogo Wengine CHADEMA Waiomba Mahakama ya Kisutu Isitishe Kusikila Kesi Yao

$
0
0
Viongozi 9 wa Chadema akiwemo mwenyekiti wao, Freeman Mbowe wamewasilisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu maombi ya kuomba kesi yao ya jinai namba 112/2018 kuahirishwa hadi rufaa yao itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Pia, wameomba kesi hiyo iahirishwe hadi maombi yao ya kutaka kesi iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu isitishwe usikilizwaji wake hadi hapo rufaa yao itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi na Mahakama ya Rufani.

Maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo leo Jumatatu Agosti 13, 2018 mbele ya mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na mawakili wa upande wa utetezi. Jeremiah Mtobesya na Peter Kibatala.

Wakili wa Serikali Mkuu, Dk Zainabu Mango ameieleza mahakama kuwa wamepewa hati ya maombi hayo namba10/2018 na kwamba wapo tayari kuwasilisha majibu kinzani kesho na kuwapatia upande wa utetezi.

Wakili wa utetezi Mtobesya naye aliomba wapewe siku mbili ili waweze kufaili majibu ya nyongeza kama watakuwa nayo.

Baada ya kusikiliza pande zote, Hakimu Mashauri aliamuru upande wa mashtaka kuwasilisha majibu kinzani Agosti 14, 2018  na iwapo upande wa utetezi  utakuwa na majibu ya nyongeza wayawasilishe Agosti 16,  2018.

Hakimu Mashauri amesema maombi hayo yatasikilizwa Agosti 21, 2018 na kwa upande wa kesi ya msingi nayo pia itatajwa mahakamani hapo Agosti 21, 2018.

Wakati hayo yakiendelea washtakiwa wote walikuwepo mahakamani.

Washtakiwa hao wamekata rufaa Mahakama ya Rufani wakipinga uamuzi wa Mahakama Kuu kutupilia mbali maombi yao ya marejeo dhidi ya maamuzi madogo yaliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari 1 na 16, 2018 jijini Dar es Salaam.

Twaweza Yakanusha Habari Ya Gazeti La Tanzanite Iliyodai Mkurugenzi Wake Ni Mwanachama Wa Chadema

$
0
0
Taasisi ya Twaweza imekanusha taarifa zilizoandikwa na gazeti la Tanzanite  kuwa Mkurugenzi wake, Aidan Eyakuze ni mwanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Aidan Eyakuze si mwanachama wa Chadema na hajawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini.

Hata hivyo, Wameongeza kuwa Twaweza ni taasisi huru isiyofungamana na chama chochote cha kisiasa hivyo taarifa iliyoandikwa na gazeti hilo ni ya uongo

==>>Isome taarifa yao hapo chini
 Twaweza imeona taarifa za uongo kwenye gazeti mojawapo la Agosti 13, 2018. Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza sio mwanachama na hajawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini Tanzania.

Twaweza ni taasisi huru isiyofungamana na chama chochote cha siasa. Tunaamini katika uhuru na haki za msingi ikiwemo uhuru wa kujumuika na uhuru wa kutoa maoni. 

Hizi ni haki za msingi za binadamu ambazo zimeainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Mitazamo ya kisiasa au uanachama wa kisiasa wa mfanyakazi yeyote wa Twaweza haushawishi maudhui ya kazi zetu na tafiti tunazochapisha.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Agosti 14

Magereza Yaandaa Mkakati Wa Kujitosheleza Kwa Chakula

$
0
0
Na Deodatus Kazinja
Watendaji wote ndani ya Jeshi la Magereza wametakiwa kujiandaa kisaikolojia kupokea mkakati maalum wa uzalishaji wa  chakula unaolenga kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa na ziada kuuzwa katika sehemu nyingine.

Hayo yamesemwa  na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Phaustine Kasike jana Agosti 13, 2018 alipokuwa akizungumza na maafisa, askari na watumishi raia wa jeshi hilo  alipofanya ziara yake ya kwanza mkoani Dodoma tangu ateuliwe kushika wadhifa huo Julai 13 mwaka huu.

Kamishna Jenerali Kasike amesema maandalizi ya mkakati huo yanaendelea vizuri makao makuu ya jeshi hilo na katika kipindi kifupi kijacho maelekezo ya utekelezaji wake yatatolewa na kushushwa katika vituo vyote vya magereza kwa ngazi ya mikoa na wilaya.

Amesema mkakati huu utakapokuwa umekamilika itakuwa ndiyo dira ya utekelezaji ndani ya jeshi  na utamtaka kila kiongozi kuwa na mpango kazi katika eneo lake unaokwenda sambamba na malengo mapana ya jeshi hilo.

“Ninaamini jambo hili linawezekana na kwa kuanza na raslimali chache zilizopo kwakuwa wataalam wapo, ardhi ipo na nyenzo za kuanzia zipo tukijipanga vizuri tunaweza kupata mahala pazuri pa kuanzia” Amebainisha Jenerali Kasike

Na kuongeza “ miongoni mwa taasisi zenye wasomi  wazuri katika maeneo mengi ni pamoja na jeshi letu la Magereza, sasa umefika wakati wa kuona wataalam hawa wanatumika kwa kushirikikshwa ipasavyo ili kuona wanaleta tija jeshini na taifa kwa ujumla”

Sanjari na hayo Kamishna Kasike amewataka watumishi wa jeshi hilo kote nchini kubadili mtazamo wa namna wanavyofanya kazi kwa kusoma alama za nyakati na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Kamishna Kasike amesema ifike mahala kila mmoja ajisikie aibu na fedheha kuona jeshi letu linasemwa vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo hata katika mambo ambayo yako ndani ya uwezo wa watendaji wenyewe.

Akitolea mfano wa uingizwaji wa vitu visivyoruhusiwa magereza kama vile simu, bangi, pesa nakadhalika kutohitaji bajeti kuviondoa ni kiasi cha watendaji  kubadilika tu.

“ Hapa kuna tatizo kubwa la kimaadili, badilikeni. Nitakuwa mkali sana. Nimeanza kwa kuwaeleza ili nieleweke vizuri kwa hatua nitakazozichukua kwa askari asiyetaka kubadilika. Adhabu zitakuwa kali kwelikweli. Amesisitiza Jenerali Kasike.

Amewakumbusha askari wote nchini kutambua dhamana waliyonayo, thamani ya kazi yao na dhamana walizonazo kwa familia zao ili kuachana na tamaa zisizokuwa na msingi ambazo mwisho huwaingiza katika matatizo makubwa.

Aidha, Kamishna Kasike amewaambia kuwa anatambua uwepo wa changamoto kadhaa kama vile ukosefu wa nyumba na zilizopo kuchakata, ukosefu mkubwa wa vyombo vya usafiri, malimbikizo ya madeni, kutopandishwa vyeo kwa wakati, uhaba wa sare na mengine.

Amewahakikishia kuwa serikali iliyoko madarakani inayatambua yote na tayari imeanza kuchukua hatua katika baadhi ya mambo na kuwaomba ushirikiano wakati yeye akiwa mtendaji mkuu anafanya ufuatiliaji.

Ziara ya Kamishna Kasike mkoani Dodoma imemfikisha pia gereza Msalato ambapo ametembelea mradi wa upigaji kokoto na kuzungumza na maafisa na askari wa gereza hilo. Awali alimtembelea Katibu Mkuu Utumishi Dr.Laurean Ndumbaro ofisini kwake na kubadilisha taarifa mbalimbali za kiutendaji.

VIDEO | Barnaba - Tuachane Mdogo Mdogo

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Barnaba ameachia video ya wimbo wake uitwao Tuachane Mdogo Mdogo.

<<DOWNLOAD HAPA>>   Au isikilize hapo chini


Ndoa ya Young Dee Yaota Mbawa

$
0
0
Baada ya kusambaa picha katika mitandao na ikaelezwa kuwa huenda msanii Young Dee ameona, imekuja kubainika haikuwa kweli bali ni wimbo wake mpya.

Young Dee alichanganya mashabiki wake hasa pale alipokuwa akipatiwa pongeza za ndoa na yeye kuzipokea kwa mikono miwili.

Siku moja baada ya hayo yote  Young Dee ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Naoa, wimbo huo umekuja kuondoa stori zote za Young Dee kufunga ndoa. 

==>>Usikilize wimbo huo hapa chini.

Kamati Ya Bunge Yaitaka Serikali Kukutana Na Wenye Viwanda

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imeitaka serikali kukaa na wamiliki wa viwanda nchini na kuhakiki gharama za uzalishaji ambazo zimekuwa zikisababisha bidhaa za wazalishaji wa ndani kushindwa kushindana na zinazoingizwa nchini.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Sadick Murad ametoa kauli hiyo  jana Agosti 13, wakati kamati hiyo ilipotembelea kiwanda cha uzalishaji wa mabati na vifaa vingine Alaf.

Murad amesema gharama za uzalisha zimekuwa kikwazo kwa viwanda vya ndani ambazo vinazalisha bidhaa kwa bei ghali ilihali zinazoingizwa nchini zinauzwa kwa bei rahisi.

“Gharama za uzalisha zikiwa fair na wazalishaji wa ndani kupunguziwa kodi za umeme na tozo nyingine, gharama za uzalishaji zitashuka,” amesema ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero (CCM).

Aidha, alitoa wito kwa wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji, kuisimamia vema Shirika la Viwango (TBS) na Mamlaka ya Mapato (TRA) ili ziendelee kutoa huduma rafiki kwa wazalishaji wa ndani ambao wamekuwa chachu katika uzalishaji wa ajira na ukuzajia uchumi.

Hata hivyo, Katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Joseph Buchweshaija amesema tayari imeandaa mpango maalumu wa kwa kushirikiana na TBS kuondoa bidhaa hafifu sokoni. Tayari tumeanza kuisafisha suala hilo na ninawaahidi kuendelea kutekeleza yote mliyoagiza,” amesema.

Aidha,  Meneja Mkuu wa kiwanda hicho cha Alaf, Dipti Mohanty aliieleza kamati hiyo kuwa umeme umeendelea kuwa mojawapo ya kikwazo kikubwa katika uzalishaji wa bidhaa zao.

Kingwalla Kaweza kusimama mwenyewe baada ya Ajali....Tazama picha

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utali Dr Hamisi Kigwangalla anaendelea kuimarika vizuri baada ya kupata ajali ya gari alipokuwa akitokea mkoani Arusha kuelekea Dodoma baada ya gari lake kupinduka na kusababisha kifo cha Afisa habari wa wizara hiyo Hamza Temba. 

==>>Hapa kuna picha mbili akiwa ameweza kusimama mwenyewe nje ya Hospitali.

MUSIC AUDIO: Diamond Platnumz X Lava Lava X Mbosso – Jibebe

$
0
0
WCB wamekuja pamoja kwa mara nyingine tena, ni baada ya Diamond Platnumz kuachia ngoma mpya 'Jibebe' ambayo amemshirikiana na Lava Lava pamoja na Mbosso. Isikilize hapa.

Mbosso Amjibu Rich Mavoko kuhusu WCB kuwanyonya wasanii

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Mbosso amesema haamini iwapo WCB inawanyonya wasanii.

Muimbaji huyo akipiga stori na SnS Tanzania (Simulizi na Sauti) amesema kwa upande wake anaamini fedha iliyowekezwa kwake haijarudi, hivyo hawezi kuona iwapo ananyonywa.

"Nilipoingia WCB hadi kufikia leo nahisi bado sijarudisha  pesa ambayo wamewekza kwangu, kwa hiyo nikiambiwa nanyonywa binafsi nitapiga kwa sababu naona mimi ndio nawanyonya hadi leo kuna baadhi ya hela imetumika kwangu haijarudi.

"Na ukifanya masihara kuna wasanii wengine wamo mule mule hela ambayo imetumika kuwafanyia brand haijarudi, kwa hiyo ikija ukaniambia Mbosso unanyonywa WCB toka uje na vigezo, uje na ushahidi wa kutosha kwamba nanyonywaje," amesema Mbosso.

Kauli ya Mbosso inakuja mara baada ya hivi karibuni kuripotiwa kuwa msanii Rich Mavoko amepeleka mkataba wake na WCB kwenda kupitiwa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) kwa kile kinachodaiwa kuwa ulikuwa wa kinyonyaji.

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Star Media Yawaomba Radhi Wateja Wake Kwa Kutopata Chaneli Za Bure

$
0
0
STAR Media (T) Ltd, imewaomba radhi wateja wake pendwa na umma kwa ujumla kwa kutopata chaneli za bure kwa muda sasa.

Taarifa iliyotolewa  na Mkurugenzi Mtendaji Star Media(T)Wang Xiaobo amesema leo kuwa hiyo imesababishwa na kukosekana kwa elimu na mawasiliano mazuri kuhusu aina ya tofauti za dikoda (ving’amuzi) tulizonazo, ambayo yamesababisha kwa wateja wao kuendelea kulipia chaneli za bure.

"Tunapenda kuwafahamisha wateja wetu kuwa ziko aina mbili za dikoda, ya kwanza ni ile ya Chaneli za bure (FTA) ambayo mteja halazimiki kila mwezi ili kutazama chaneli za bure.

"Na nyingine ni ya chaneli za kulipia, ambayo mteja atatakiwa kulipia kifurushi chake kila mwezi," amesema

Ameongeza kwa wateja wapya, dikoda (ving’amuzi) hizo zinapatikana kwenye maduka yao pamoja na mawakala wao, lakini kwa wateja ambao tayari wameshanunua dikoda (ving’amuzi) za kulipia wanaweza kubadilisha dikoda (ving’amuzi) zao kuwa FTA kwa kutembelea katika ofisi zetu na kupata utaratibu.

 Amesisitiza Star Media (T) Ltd, itaendelea kuzingatia masharti yote ya leseni, pia inaufahamisha umma kwamba imekubali kufuata na kutekeleza maagizo ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwamo kulipa faini ambayo tayari imeshaanza.

Pia wanawafahamisha umma wa watanzania kwamba sasa wanaweza kuendelea kufurahia chaneli za bure na huduma zetu kwa ujumla.

Mwenyekiti Wa CCM Taifa, Dkt. John Magufuli Aendesha Kikao Cha Kamati Kuu Ya Hlmashauri Kuu Ya CCM Taifa

$
0
0
Rais John Magufuli akisalimiana na mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM alipowasili katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam.

Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba kwa ajili ya kuendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.
Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa katika ukumbi wa mikutano katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba kwa ajili ya kuendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

Viwanja Villvyopimwa Kwa Makazi.

$
0
0
Viwanja Salama vilivyopimwa Kwa ajili ya makazi, vipo Vikubwa sqm 3200 Bunju masait pembeni ya Bagamoyo road Bei million 95 ,kina fence na geti pande mbili hati mkononi view nzuri ya Bahar..... Kwa umbali ,jirani mita 200 kutoka Bunju bus stand na soko la Bunju pia jirani na kituo kipya cha mafuta na mall mpya, nyumba ya mlinzi ipo,price negotiable,(2) sqm 3018 kipo level njia ya Baobab km 2 tu kutoka Bagamoyo road .

Jiran block street na kiwanda kipya cha matunda umeme maji vipo na majirani wamejenga vizuri,(3) sqm 500 hadi 1200 hapa Kerege jiran na kanisa la Roma na mahakama,mita 600 kutoka Bagamoyo road ardhi ipo level,(4) sqm 400 hakijapimwa 

Kipo mjini jiran na block street majirani wamepiga fence km 2kutoka Baobab secondary mita 200kutoka barabara ya vikawe na mita 50 kutoka tank la maji hapa umeme maji na kanisa vipo Bei Tsh million 4.5 ...Maongezi yapo.

 Kwa mawasiliano piga 0677705808. Karibuni sana

Viwanja vya Karege

Mbunge wa CHADEMA Anthony Komu Akanusha Taarifa za Kutaka Kuhamia CCM

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini (CHADEMA), Anthony Komu amekanusha kauli iliyotolewa na aliyekuwa Mbunge wa Ukonga (CHADEMA) kuwa mbunge huyo yuko mbioni kutimkia CCM.

Komu amesema kuwa hawezi kuondoka CHADEMA na hajawahi kufanya mazungumzo na Waitara kuhusu suala hilo kwani yeye ndio muasisi wa upinzani na anajivunia historia hiyo .

“Mimi sio sehemu ya mpango huo na sielewi Waitara katoa wapi taarifa hiyo naomba wananchi wangu watambue kuwa mimi sio mpinzani wa kuunga unga mimi ni miongoni mwa waasisi wa upinzani”, amesema Komu.

Jumamosi ya Agosti 11, 2018 wakati akiongea na kituo cha EATV,  Waitara aliwataja wabunge watano kutoka CHADEMA wanaotaraji kujiunga na CCM akiwemo Anthony Komu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images