Magari yakwama Daraja la Ruvu kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.....
↧
↧
Daraja la Mbagala ---Kongowe nalo lakatika kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Dar
↧
Morogoro nayo yakumbwa na Mafuriko kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.....
Mvua za masika zinazoendelea kunyesha nchini zimesababisha mafuriko pia
katika mkoa wa Morogoro kama picha (juu na hapo chini) zilizopigwa
katika maeneo ya Nane Nane, Mwembesongo na Mji Mpya zinavyoonyesha.
Vijana wa Kichangani, Manispaa ya Morogoro wakipita eneo la maji ya mafuriko
Wakazi
wakishikana mikono kupita eneo la mafuriko ya maji ya mvua eneo
barabara inayounganisha
↧
Mvua yaua watu 10 jijini Dar, madaraja sita yabomoka.....Wakazi Jangwani wazikimbia nyumba zao
Mvua
kubwa ziliyonyesha mfululizo kuanzia juzi maeneo mbalimbali jijini Dar
es Salaam zimesababisha vifo vya watu kumi na kuharibu miundombinu ya
barabara ikiwamo madaraja sita kubomoka.
Aidha, mradi wa mabasi yaendayo kasi (Dart) umelazimika kusimamisha
shughuli zake, baada ya ofisi zake za Jangwani kukumbwa na mafuriko na
kusababisha hasara ya zaidi ya Dola za Kimarekani 30,000.
↧
Video Mpya : Lady Jaydee aachia rasmi video ya single yake mpya ...."NASIMAMA"
↧
↧
Athari ya Mvua jijini Dar : Walikubaliana ambebe mgongoni ili amnusuru asilowe....Bahati mbaya jamaa aliteleza, dada kalowa mwili mzima
↧
Rais Kikwete atembelea maeneo yaliyokumbwa na mafuriko mkoa wa Pwani
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mmoja wa baadhi ya abiria waliokwama baada ya barabara ya Chalinze-Dar es Salaam kuharibiwa vibaya na mafuriko
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Mkewe Mama Salma Kikwete
na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza wakikagua athari za mafuriko
zilizoharibu vibaya barabara ya Chalinze- Dar es Salaam eneo la Ruvu
Darajani
↧
Mzee Gurumo afariki dunia.....
Mkongwe wa
Dansi nchini, Maalim Muhidin Gurumo aliyekuwa akitumikia Bendi ya Msondo
Ngoma ‘Baba ya Muziki’ kabla ya kustaafu mwaka jana, amefariki dunia.
Mwanamuziki huyo amefariki leo
alasiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa
matibabu.
Mzee Gurumo amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu, hali iliyomfanya
↧
Magazeti ya leo Jumatatu ya tarehe 14 April 2014
↧
↧
Wanaswa kwa tuhuma ya kuwa na heroin kwenye kondomu
VIJANA wawili wenye asili ya kiasia, wakazi wa jiji la Arusha, wametiwa mbaroni na polisi mkoani hapa kwa tuhuma ya kukutwa na kete 170 za dawa za kulevya aina ya heroin na bangi kete 300.
Walihifadhi dawa hizo kwenye mfuko mweusi aina ya sandarusi na zingine kete 170 zikiwekwa kwenye mpira wa kiume (kondomu) ndani ya gari.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas aliwataja
↧
Rose Muhando roho mkononi....Anusurika kutekwa, akimbilia Dar.....Ajali ya Msama yahusishwa
Mwanamuziki wa Injili daraja la kwanza nchini, Rose Muhando anaishi
roho mkononi kufuatia madai kwamba kuna watu wanaomsaka wakisemekana
wametumwa kuichukua roho yake.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Rose anaishi kwa machale jijini Dar
akikimbia Dodoma baada ya taarifa kwamba mtu mmoja aliyetajwa kwa jina
moja la Nasani na wenzake wanataka kumdhuru kama si kumtoa roho kabisa.
“
↧
Alex Msama anaendelea vizuri na matibabu baada ya kupata ajali mkoani Dodoma
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dares salaam inayoandaa matamasha ya Pasaka na Krismwass Bw. Alex Msama anaendelea
vizuri baada ya kupata ajali mkoani Dodoma kisha kupelekwa katika
hospitali ya mkoa wa Dodoma na baadaye kuhamishiwa katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili katika wodi Kibasila namba 16.
Msama anaendelea
vizuri na matibabu na amesema hali yake
↧
Bomu lajeruhi watu 15 mkoani Arusha waliokuwa kwenye baa moja iitwayo Arusha Night Park wakitazama mpira
Watu 15 wamejeruhiwa kutokana na mlipuko
wa bomu katika baa maarufu ya Arusha Night Park katika eneo la Mianzini
katika jiji la Arusha.
Tukio hilo lilitokea jana saa mbili usiku wakati
mamia ya watu wakiwa katika baa hiyo wakiangalia mechi ya soka ya Ligi
Kuu ya England kati ya Chelsea na Swansea. Chelsea ilishinda 1-0.
Mmoja wa wamiliki wa baa hiyo, Angelo Mwoleka pia
↧
↧
Mr Nice apata ajali akiwa kwenye Bajaji ....Abiria mwenzake afariki dunia papo hapo
Msanii mkongwe Mr Nice amepata ajali juzi ndani ya bajaji akiwa na
abiria mwenzake jijini Dar.
Ajali hiyo ilitokea baada ya gari moja "kuwachomekea ", hali iliyomfanya dereva wa Bajaji hiyo kuikwepesha na
kugonga mti.
Hali ya Mr Nice sio nzuri sana,kwani amevimba kichwa na
kuumia sana sehemu za usoni na abiria mwenzake ambaye hajafahamika jina
alifariki papo hapo
<!--
↧
Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Kahama agonga watu watatu kwa gari....Alianza na dereva bodaboda, watu wakamzingira, akaondoa gari kwa kasi na kumfumua tumbo mtu mwingine
Majeruhi wa awali Joseph Malugu akiwa hospitali ya wilaya ya Kahama baada ya kuumia vibaya mguu wake na sehemu nyingine za mwili.
***
via gazeti la MAJIRA -- Watu watatu wamejeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Bw. Elia Haway.
Majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ambapo
↧
Rais Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara kufuatia kifo cha mwanamuziki Muhidini Maalim Gurumo.
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara kufuatia kifo cha mwanamuziki maarufu na wa
siku nyingi, Muhidini Maalim Gurumo kilichotokea tarehe 14 Aprili, 2014 katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)
↧
Gari Dogo laangukiwa na lori lililokuwa limebeba mchanga....Juhudi za JWTZ, kikosi cha zimamoto na uokoaji zafanikiwa kumnasua dereva wake
Picha za ajali iliyotokea asubuhi ya leo huko Makongo jijini Dar es
Salaam ambapo lori lililokuwa limebeba mchanga lililiangukia gari dogo.
Juhudi za Askari wa Jeshi la Wananchi wakishirikiana na kikosi cha
zimamoto na uokoaji zilifanikisha kumnasua kutoka kwenye mchanga dereva
wa gari dogo mwendo wa saa moja u nusu hivi asubuhi baada ya kuwemo ndani ya gari hilo tangu saa 11 afajiri.
↧
↧
Picha mbalimbali toka jijini Arusha baada ya mlipuko wa bomu la jana
↧
Ratiba ya mazishi ya msanii Maalim Gurumo aliyefariki jana.....
Leo saa 10 jioni kutakuwa na kisomo nyumbani kwa marehemu Tabata-Kisukulu jijini Dar es Salaam.
Kesho saa 3 asubuhi mwili wa marehemu utawasili nyumbani kwake kwa ajili ya sala.Saa 4 asubuhi safari ya kuelekea kijiji cha Masaki wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kwa maziko itaanza.
Ndugu wa marehemu Gurumo
wakiwa katika picha ya pamoja, kuanzia kushoto ni mtoto wake Mwalimu
Muhidin,
↧
Profesa Mwandosya atoa taarifa rasmi kuhusu ajali ya helicopter iliyotokea jana na kuwahusisha makamu wa rais, Kova na Magufuli.....Aomba wajumbe watoe posho ya siku kuchangia wahanga wa mafuriko
Waziri wa nchi ofisi ya rais, Profesa Mark Mwandosya ametoa
taarifa rasmi kufuatia ajali ya helicopter iliyotokea jana na
kuwahusisha makamu wa rais , Dr. Gharibu Bilali, Kamanda wa polisi kanda
maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,
Said Mecky Sadick.
Prefesa Mwandosya ametoa taarifa hiyo leo katika bunge maalum la
katiba mjini Dodoma ambapo
↧
More Pages to Explore .....