Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Kusinyaa Na Kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume

0
0
Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  ya  uume na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA  KIUME YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kama uume wako  umedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 
 
Ipo dawa  ya ASILI   ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.
 
Ni  dawa  ya  asili  kabisa ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  uume  ndani ya siku thelathini.

JINSI YA  KUPATA  TIBA  HII : Kupata  tiba  hii  fika  ka6ika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam  ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu  watapelekewa  dawa  mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY )  na kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabus  au  boti  kwa  waliopo  Zanzibar.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :    0693  005 189.

Waziri Lugola Aapa Kupambana Na Polisi Wanaobambikizia Kesi Wananchi

0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameapa atapambana na baadhi ya polisi nchini ambao wanatabia ya kubambikizia kesi wananchi kwa kuwa wanaichafua Wizara yake pamoja na nchi kwa ujumla.

Katika kulifanikisha hilo, Lugola amesema atafanya ziara ya kushtukiza katika vituo vya polisi  mbalimbali nchini ili kupambana na polisi wenye tabia hiyo mbaya na endapo akiwakamata hata waonea huruma.

Waziri Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, aliyasema hayo wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Kenkombyo, Kata ya Neruma, jimboni kwake, wilayani Bunda, alisema tabia hiyo ya baadhi ya polisi wanayoiendeleza katika vituo vya polisi yapaswa kulaani na atakua mkali zaidi katika kulifuatilia hilo.

“Nilishawaambia polisi na leo nawaaambia tena, nitakua nafanya ziara ya kushtukiza mara kwa mara katika vituo vya polisi, na hamjui saa wala siku lini nitakuja, hili nilisemalo sitanii kabisa, lazima nitapambana nanyi, hii ni serikali ya awamo ya tano inataka wananchi waishi kwa amani zaidi bila kua na hofu ya aina yoyote,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kua, yeye ni mtetezi wa polisi na anajua kazi nzuri ambayo inafanywa na idadi kubwa ya polisi, lakini wale polisi wachache wenye tabia hiyo hata waonea huruma kamwe wakati analitelekeza hilo.

 “Nitatetea wafanyakazi wa Magereza, Zimamoto, Uhamiaji, Polisi na wengineo wanaofanya kazi vizuri kwa kuzingatia sheria, lakini kwa wale wanaokula rushwa na kubambikiza kesi hao watapata tabu sana na hili nalisisitiza kuwa hawatapona,” alisema Lugola.

Pia aliwataka wananchi waache tabia ya kwenda kufungua kesi polisi ili kumkomoa mtu fulani kwa kua anachuki nae, na hilo likibainika huyo mwananchi mwenye tabia hiyo ambaye anashirikiana na polisi ili tu kumkomoa mtu fulani, hakika polisi na huyo mwaanchi atapambana nao.

Aliongeza kua, anataarifa baadhi ya askari wa usalama barabarani sehemu mbalimbali nchini sio tu katika Jimbo lake la Mwibara, baadhi ya askari hao wanachukua rushwa kwa wananchi ambao hawajafanya kosa lolote ila uwalazimisha ili tuu waweze kupata rushwa, hilo nalo atapambana nalo.

“Hao askari wa barabarani wakati mwingine wanawasumbua wenye magari, wakati mwingine unakuta mtu kaegesha pikipiki yake wanaichukua wanaipeleka kituoni, ukiuliza unaambiwa utaikuta kituoni, na ukienda kituoni wanakuweka ndani, na ukitoka unaombwa rushwa, mimi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sitarajii hilo kutokea,” alisema Lugola.

Aidha, Lugola alizungumzia kuhusu maendeleo ya jimbo lake akiwataka wananchi wa jimboni humo, licha ya kuwa wanapata fedha za maendeleo lakini wananchi hao wanapaswa  kuweka nguvu katika miradi ya maendeleo katika katika sekta ya elimu, afya, kilimo pamoja na zinginezo.

Pia alisema wanatarajia kujenga kituo kikubwa cha polisi eneo la Kibara hivyo watahitaji nguvu ya wananchi katika kulifanikisha hilo kwa eneo hilo ili maendeleo yazidi kupatikana wananchi wakifanya kazi kwa amani na utulivu.

Lugola ambaye yupo ziarani jimboni kwake, licha ya kuzungumzia masuala hayo ya maendeleo, pia anafuatilia mechi za mpira wa miguu katika kata mbalimbali ndani ya jimbo hilo baada ya kuanzisha mashindano ya michezo ya Kangi Bonanza, ambapo timu mbalimbali ushiriki nawashindi upewa fedha na wachezaji bora wanasafirishwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchujwa  katika timu ndogo ya Klabu ya Simba, jijini humo, akiwa na lengo ya kukuza vipaji vya wananchi wake ndani ya Jimbo lake.

Hukumu ya Mbunge wa Mbozi, Pascal (CHADEMA) Haonga Kusomwa Leo

0
0
Katibu Mkuu Chadema Dk Vicent Mashinji, mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa na katibu wake, Emmanuel Masonga wamewasili katika mahakama ya wilaya ya Mbozi, Songwe kusikiliza hukumu ya Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga.

Haonga na wenzake, Wilfredy Mwalusamba (katibu wake) na Mashaka Mwampashi wanakabiliwa na makosa matatu ya kufanya fujo na kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo,  kosa la pili na tatu ni kuwazuia  askari kutekeleza majukumu yao.

Wanadaiwa kutenda kosa hilo Agosti 28, 2017, na leo Ijumaa Agosti 10, 2018 mahakama hiyo inatarajia kutoa hukumu ya kesi hiyo.

Mbali na viongozi hao, pia wananchi na wafuasi wa Chadema wameanza kumiminika katika mahakama hiyo huku ulinzi ukizidi kuimarishwa kutokana na askari kutanda kila kona wakiwa na silaha za moto.

Ufafanuzi wa TCRA kuhusu kuondoa chaneli za runinga zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka ving'amuzi vya Azam, Multichoice na Zuku

0
0
Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imefafanua kuhusu kuondoa Channel za Televisheni za ndani zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka Ving’amuzi vya Azam, Multichoice na Zuku.

Jukwaa la wahariri (TEF) Lalaani Polisi Kuwapiga Waandishi wa Habari

0
0
Jukwaa la wahariri nchini limelaani vitendo vya kupigwa kwa waandishi wa habari vinavyofanywa na Jeshi la Polisi pindi wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kauli hiyo imekuja kufuatia kupigwa kwa waandishi wawili siku ya Jumatano tarehe  8, Agosti ambapo mwandishi kutoka wilayani Tarime mkoani Sita Tuma aliyekuwa akitekeleza majukumu yake wakati jeshi hilo lilipowatanya kwa silaha za moto wafuasi wa CHADEMA waliokuwa katika mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani.

Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Dodatus Balile amesema kuwa kitendo hicho cha kukamatwa kwa mwandishi na kushikiliwa wakati akiwa kazini si sahihi na taratibu za mamlaka haziruhusu vitendo dhidi ya wanahabari.

“Mwandishi amekamatwa akiwa kwenye eneo la kazi wala hakufika pale kwaajili ya kuandamana kama walivyodai wao, kama wao walivyokuwa kazini hata sisi tunakuwa kazini”, amesema Balile.

Tarehe 8, Agosti Jeshi la polisi , wilayani Tarime mkoani Mara, liliwashikilia Mbunge wa Tarime Mjini Esther Matiko, mwandishi wa habari, pamoja na mara baada ya kuamuru wanachama wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), kusitisha kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea nchini.

Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) Lalaani Mwandishi wa Habari Kupigwa na Polisi

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Picha: Maelfu ya Wananchi Wajitokea Kumsindikiza Mzee Majuto Tanga

0
0
Maelfu wamejitokeza kuusindikiza Mwili wa msanii Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto kuelekea Msikitini kabla ya kwenda eneo alilochagua kuzikwa.

Mzee Majuto alifariki usiku wa Jumatano, Agosti 8, 2018 katika Hospitali ya Muhimbili, ambapo kesho yake, Agosti 9, 2018 mwili wake ulipelekwa katika Msikiti wa Maamur, Upanga, jijini Dar es Salaam, kuswaliwa kabla ya kupelekwa viwanja vya ukumbi wa Karimjee kuagwa. Baadaye mwili huo ulisafirishwa kuelekea jijini Tanga kwa maziko.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Mahakama Yamwachia Huru Mbunge CHADEMA

0
0
Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, Songwe imemuachia huru mbunge wa Mbozi (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wawili baada ya kukutwa hawana hatia katika kesi iliyokuwa ikiwakabili.

Haonga na wenzake, Wilfredy Mwalusamba (katibu wake) na Mashaka Mwampashi wameachiwa huru leo mchana Ijumaa Agosti 10, 2018.

Walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matatu ya  kufanya fujo na kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo,  kosa la pili na tatu ni kuwazuia  askari kutekeleza majukumu yao.

Akisoma huku hiyo leo hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Nemes Chami amesema katika mashtaka yote matatu, upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha makosa.

 "Katika ushihidi wa mashahidi sita wa upande wa Jamhuri hakuna mahali walipothibitisha kwamba washtakiwa walikataa kukamatwa,” amesema.

“Hakuna mahali walipoonesha kwamba washtakiwa hawa waliwazuia askari kutekeleza majukumu yao na hakuna mahali walipothibitisha kwamba washtakiwa walilazimisha kurudi ukumbini baada ya kutolewa nje.”

Amesema kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha ushahidi wa mashtaka waliyoyawasilisha mahakamani hapo, mahakama inawaachiria huru washtakiwa wote.

Amesema kama kuna upande unaona haujaridhika na hukumu hiyo una haki ya kukataa rufaa ndani ya muda wa kisheria.

PICHA: Rais Dkt. Magufuli akutana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt aliyemtembelea akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuonesha albamu ya picha Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt inayoonesha Shule ya Sekondari ya Ihungo iliyobomolewa kabisa na Tetemeko la Ardhi mkoani Kagera lililotokea Septemba 10, 2016  ambayo imejengwa upya na serikali ya Uingereza kupitia mpango wake wa maendelo ya elimu kupitia UKAid/DFID. Picha hizo zinaonesha shule hiyo baada ya tetemeko, wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi siku ya mwaka mpya wa 2017 na inavyoonekana sasa baada ya kujengwa upya. Mhe. Mordaunt, ambaye yuko nchini kwa ziara ya kikazi, alimtembelea  Rais Dkt. Magufuli akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa zawadi ya kinyago cha "Umoja"  Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt aliyemtembelea akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke aliyeongozana na , Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt aliyemtembelea akiwa ameongozana pia na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy aliyeongozana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke,  walipomtembelea  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018  Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wanahabari kuishukur serikali ya Uingereza  kwa misaada yake mbalimbali ikiwemo Shilingi Bilioni 307 kwa kuunga mkono juhudi zake za kuopambana na rushwa pamoja na kuboresha sekta za afya na elimubaada ya kukutana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza (Department of International Development - DFID - ) Mhe. Penny Mordaunt aliyemtembelea akiwa ameongozana na Balozi wa Uingereza nchini Mhe. Sarah Cooke, na Mkuu wa ofisi ya DIFD nchini Mama Beth Arthy Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 10, 2018.

Picha na IKULU

Uingereza yatoa msaada wa Tsh. Bilioni 307.5 kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli

0
0
Uingereza imetoa msaada wa Sh bilioni 307.5 kwa Tanzania kwa ajili ya kuunga mkono juhudi Rais John Magufuli katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya.

Akitangaza msaada huo Ikulu jijini Dar es Salaam leo Ijumaa agosti 10, baada ya kukutana na Rais Magufulu, Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Penny Mordaunt amesema fedha hizo zinatolewa kwa ajili ya kuunga mkono vipaumbele vya Rais Magufuli ambapo kati yake Sh bilioni 124.5 zitaelekezwa katika kuinua ubora wa elimu hususani kutoa fursa ya elimu kwa watoto wa kike na wenye ulemavu.

Aidha, Sh bilioni 23.5 zitaelekezwa katika kuunga mkono juhudi za kupambana na rushwa na Sh bilioni 160 zitaelekezwa katika kuboresha huduma za afya.

“Tunafanya hivi ili kudhihirisha dhamira yetu ya kuimarisha na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wetu, tunataka kujielekeza katika kuhakikisha Rais Magufuli anafanikisha ahadi zake kwa Watanzania na tunafurahi kuwa wadau muhimu wa hilo,” amesema Mordaunt.

Kwa upande wake Rais Magufuli amemshukuru Mordaunt kwa msaada huo na amemuomba kufikisha shukrani zake kwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May kwa mchango mkubwa ambao Uingereza hutoa kuchangia bajeti ya Serikali na kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Namshukuru sana Waziri Penny Mordaunt kwa kutambua juhudi zetu za kuinua elimu, kupambana na rushwa na ufisadi na kuboresha huduma za afya, msaada huu utatusaidia kuongeza nguvu kwa sababu watoto wakipata elimu bora, tukikomesha rushwa na watu wetu wakiwa na afya njema tutaweza kujenga viwanda na kukuza uchumi wetu kwa kasi zaidi” amesema Rais Magufuli.

Hata hivyo, Rais Magufuli amemuahidi Mordaunt kuwa fedha zilizotolewa zitatumika vizuri na kwamba Serikali itahakikisha uhusiano wa Tanzania na Uingereza unazidi kuimarishwa kwa kuwa inatambua kuwa Uingereza ndiyo mwekezaji mkubwa hapa nchini na imekuwa ikitoa misaada mikubwa ya fedha za walipa kodi wa Uingereza kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania.

Kauli ya Mambosasa Kuhusu Polisi Kumshambulia kwa Kipigo Mwandishi wa Habari

0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema polisi imeanza uchunguzi wa tukio la kupigwa kwa mwandishi wa habari wa Wapo Redio, Sillas Mbise.

Mbise anadaiwa kushambuliwa na polisi juzi Agosti 8, 2018 wakati wa mchezo kati ya Simba na Asante Kotoko ya Ghana.

Video za tukio hilo zimesambaa katika mitandao ya kijamii, zikimuonyesha Mbise akishushiwa kipigo na polisi.

Akizungumza leo Ijumaa Agosti 10, 2018 Mambosasa amesema polisi wameanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kufungua jalada la uchunguzi wa picha hizo za video.

Amesema hiyo inakwenda sambamba na kumtaka mtendewa wa kosa hilo la kupigwa kutoa taarifa kituo cha polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Amesema mtu yeyote anatakiwa kutoa malalamiko yake pale anapoona ametendewa vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya leo Jumamosi ya Agosti 11

Tamko la Serikali Kuhusu Ugonjwa Wa Ebola Uliotokea Katika Nchi Jirani Ya Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo

0
0
Utangulizi
Ndugu wanahabari,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kutoa taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Nchi hiyo ya DRC imetangaza tena kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mnamo tarehe 1 mwezi Agosti, 2018, ambapo jumla ya wagonjwa 26 na vifo 10 vilitolewa taarifa na wagonjwa 4 kati yao walithibitishwa kimaabara kuwa na ugonjwa wa Ebola. Wagonjwa hawa wametokea katika vijiji/Maeneo ya Mangina ikiwa ni kama km 30 tu magharibi mwa mji wa Beni kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi ya Uganda ikiwa ni kama km 100 tu, na pia likiwa karibu sana na nchi ya Rwanda.

Huu ni mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola kutokea nchini DRC, na umetokea wiki moja baada ya nchi hiyo kutangaza kuisha kwa mlipuko mwingine uliotokea mwezi Mei mwaka huu ambao ulikuwa katika jimbo la Equator, Magharibi mwa DRC, umbali wa zaidi ya km 2,000 kutoka eneo la huu mlipuko mpya uliotokea.

Ndugu wanahabari,
HADI SASA HAPA NCHINI TANZANIA HAKUNA MGONJWA YOYOTE ALIYEHISIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA NA VIRUSI VYA EBOLA. Hata hivyo, kugunduliwa kwa ugonjwa huu kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi za Uganda na Rwanda ni jambo la kutuweka kwenye wasi wasi kwani eneo hili liko karibu sana na nchi yetu kuliko eneo lingine lolote ambako ugonjwa huu umeshawahi kutokea kwenye nchi ya DRC. Hivyo nchi yetu ipo hatarini kuambukizwa ugonjwa huu kutokana na ukaribu na muingiliano wa watu, hasa kuhusiana na wasafiri wanaotoka na kuingia hapa nchini.

Kwa sababu hizi, watanzania hatuna budi kuchukua tahadhari ya hali ya juu ili kujikinga na kudhibiti na ugonjwa wa Ebola.  Hivyo Wizara inapenda kutoa tahadhari ya ugonjwa huu kwa wananchi wote katika Mikoa yote ya Tanzania, lakini hasa ile inayopakana na nchi jirani za DRC, Uganda na Rwanda. Mikoa hiyo ni pamoja na Mwanza, Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe. Aidha tahadhari na hatua stahiki zichukuliwe katika maeneo yote ya mipakani ambapo abiria wanaingia nchini kutoka nchi jirani.

Ugonjwa wa Ebola

Ugonjwa wa Ebola husababishwa na virusi vya Ebola ambavyo huambukiza kwa njia zifuatazo;
  1.  Kugusa Damu au majimaji kutoka kwa mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo,
  2.   Kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa ugonjwa huo,
  3.  Kugusa wanyama (Mizoga na wanyama wazima) walioambukizwa kama vile Sokwe na Swala wa msituni.
Dalili za Ugonjwa
Dalili za Ugonjwa huanza kuonekana kwa mtu aliyeambukizwa baada ya siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi. Dalili hizo ni pamoja na;
  1.     Homa kali ya ghafla,
  2.     Kulegea kwa mwili,
  3.     Maumivu ya misuli,
  4.     Kuumwa kichwa na vidonda kooni.
  5.   Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha, vipele vya ngozi na pia figo na Ini kushindwa kufanya kazi.
  6.   Kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa na damu ndani na nje ya mwili.
Namna ya Kujikinga na ugonjwa wa Ebola:

Ugonjwa wa Ebola unaweza kuzuilika. Njia kuu za kujikinga na ugonjwa huu ni:-
  1. Kuepuka kugusa au kuingiwa na mate, damu, mkojo, jasho, kinyesi, machozi na majimaji mengine yanayotoka mwilini mwa mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa  wa Ebola
  2.     Kuepuka kushughulikia maiti ya mtu aliyefariki akiwa na dalili za Ebola; badala yake watoe taarifa kwa uongozi wa kituo cha huduma za Afya kwa ushauri.
  3.   Kuepuka kula nyama za Wanyama wa porini kama sokwe, swala na popo na pia kugusa mizoga ya Wanyama hao
  4.   Kuepuke mila na desturi zinazoweza kuchelewesha kupata huduma muhimu na kuzidi kueneza ugonjwa wa Ebola.
  5.   Kuzingatia usafi wa mwili
  6.   Kutoa taarifa mapema kwa viongozi wa Serikali na wa huduma za Afya katika ngazi zote pale anapotokea mtu mwenye dalili za Ebola.
  7.  Kuwahi katika vituo vya huduma za Afya pale mtu anapoona dalili za ugonjwa huu.

Hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara kufuatia kupatikana kwa taarifa ya Ugonjwa huu huko DRC

Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizi tangu mwezi Mei 2018, hatua zifuatazo zinaendelea/zimechukuliwa na Wizara ili kujiandaa kukabiliana na mlipuko huo:
  1. Kufanya tathmini ya utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini (Operational readiness assessment) kwa nchi nzima kwa kushirikiana na WHO na kuainisha mapungufu ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi. Mapungufu hayo yanaendelea kuyafanyiwa kazi ili kujenga uwezo na utayari katika nchi yetu.
  2.  Tumetengeneza mpango mkakati wa kujiandaa na kupambana na mlipuko wa Ebola endapo utatokea nchini (Costed Ebola Contingency Plan). Mpango huu umeandaliwa kwa kushirikiana na WHO. Mpango umeainisha maeneo ya kujenga uwezo kwa wakati huu wa kujiandaa, pamoja na hatua za kuchukua endapo ugonjwa utaingia ikiwa ni pamoja na gharama zake.
  3. Tumefanya mafunzo ya Timu za dharura (Rapid Response Teams) ngazi ya Taifa na katika Mikoa ya Dar es Salaam, Songwe, Rukwa, Katavi, Kigoma na Kagera
  4. Tumeimarisha ufuatiliaji wa wasafiri mipakani (travellers entry screening) kwa kutumia vifaa vya kupima joto la mwili (thermo scanners) na fomu maalum za wasafiri
  5.  Wizara imepokea vifaa vya kukabiliana na Ebola kutoka WHO vikiwemo; Thermo scanners, Vifaa Kinga, au PPE, kama vile gloves, body bags, vifaa vya ufungashaji wa sampuli nk. Vifaa hivyo vimeanza kusambazwa mikoani kupitia MSD
  6.  Uelimishaji wa umma umefanyika na unaendelea kufanyika kwa kupitia vyombo vya habari vya kitaifa na kijamii, na mitandao ya kijamii. Vile vile vipeperushi na mabango vinaendelea kuandaliwa
  7. Vikao vya uratibu vimefanyika katika ngazi ya taifa na mikoa ambayo ipo katika hatari zaidi. Pia ufuatiliaji wa karibu unaendelea kupitia Kituo cha ufuatiliaji wa magonjwa ya dharura cha Wizara (Public Health Emergency Operation Centre is on “High Alert”)
  8. Wataalam kutoka ngazi ya Taifa kwa sasa wako katika mikoa ya Kigoma Katavi Rukwa Kagera Kilimanjaro Mwanza Songwe na Mbeya kufanya tathmini ya utayari katika ngazi ya mikoa na Wilaya (Readiness Assessment)
  9.  Maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kutekeleza kazi nyingine kama ifuatavyo:
  •  Kufanya mafunzo katika mikoa iliyo salia ikiwemo Mwanza, Kilimanjaro na Mbeya ambayo imesalia katika ile mikoa nane iliyo katika hatari zaidi
  •  Mafunzo ya waandishi wa habari 30 (media orientation)
  • Zoezi la udhibiti wa matukio ya dharura (simulation exercise) katika ngazi ya Taifa
  •  Mafunzo kwa wasfirishaji wa sampuli kwenda katika maabara



Hitimisho
Nawaomba Wakuu wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri wote nchini kuchukua Tahadhari na kuendelea kuelimisha wananchi wote juu ya ugonjwa huu na kuwataka kutokuwa na hofu ila kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huu kwani mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitishwa kuugua ugonjwa huu hapa nchini.

Aidha Wizara itaendelea kushirikiana na sekta mbalimbali katika kuimarisha ufuatiliaji na kuendelea kutekeleza mikakati ya kudhibiti ili ugonjwa huu usiingie nchini. Vilevile Wizara itaendelea kutoa taarifa pamoja na Elimu kwa Jamii kadri itakavyohitajika.

Imetolewa na
Ummy A. Mwalimu (Mb)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto
10/08/2018

Oparesheni Jokate yakutana Na VISIKI......Ni Baada ya Waziri wa Mifugo Kupiga Marufuku Ukamataji Holela wa Mifugo

0
0
Siku chache baada ya mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani, Mh. Jokate Mwegelo kufanya oparesheni ya kukata mifugo katika maeneo ya hifadhi zilizopo wilayani humo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina amepiga marufuku tabia ya ukamataji mifugo kiholela.

Mpina ametoa marufuku hiyo wakati akifunga maonesho ya 25 ya Nane nane Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani na Morogoro katika viwanja vya Mwalimu JK Nyerere mjini Morogoro.

Mpina amesema katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali kuendesha operesheni za kukamata mifugo na kuifungia bila kuipatia huduma muhimu ikiwemo maji, malisho na matibabu na matokeo yake mifugo mingi hufa na kusisitiza kuwa operesheni hizo zinapofanyika ni lazima zihusishe pia maofisa wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuwa na uelewa wa pamoja wa jambo hilo.

Aidha Mpina alisema utaratibu unaofanyika hivi sasa wa kukamata hovyo mifugo ni ukiukwaji wa sheria namba 17 ya Magonjwa ya Wanyama ya mwaka 2003 na, Sheria ya Ustawi wa Wanyama Namba 19 ya Mwaka 2008 ambazo zinataka mifugo inapokamatwa kuzingatia masuala ya magonjwa na ustawi wa mifugo katika kipindi chote inapokuwa imeshikiliwa.

Katika hatua nyingine, Mpina pia alielezea kutoridhishwa na utoaji wa mikopo wa Benki ya Kilimo (TADB) ambapo kwa taarifa iliyotolewa sekta ya uvuvi hakuna mkopo wowote uliotolewa katika mwaka wa fedha uliopita huku upande wa sekta ya mifugo wakiambulia wajasiamali wanne tu .

Aidha kiasi cha jumla ya mikopo iliyotolewa ya Sh. Bilioni 39 kwa mwaka mzima ni kidogo sana ikilinganishwa na mahitaji wa mikopo katika sekta za kilimo,mifugo na uvuvi, huku akipongeza kazi nzuri inayofanywa na Taasisi ya PASS na SAGGOT-CTF katika kuwadhamini wakulima , wafugaji na wavuvi katika kupata mikopo.

Kutokana na changamoto hizo, Waziri Mpina ameitaka benki hiyo kurekebisha kasoro zilizopo na kujipanga vizuri kuhudumia sekta hizo, vile vile amewaagiza makatibu wakuu wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuitambua na kupitia miradi yote ya wajasiriamali katika sekta zao ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo kwa wakati.

Sambamba na hilo amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kupitia idara ya maendeleo ya jamii na idara ya ushirika kuwaandaa na kuwaunganisha wananchi katika kukidhi vigezo vya kupata mikopo katika taasisi za fedha.

Pia aliagiza Halmashauri zote nchini kuwatambua vijana wanaohitimu mafunzo katika vyuo vya ugani vya SUA, FETA, LITA na ATI na kuwatumia katika safari ya kuleta mageuzi ya uvuvi,mifugo na kilimo katika maeneo yao na kwamba hata mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa wanawake,vijana na walemavu kundi hili la wagani liangaliwe kwa jicho la pekee.

Mbali na hilo Waziri Mpina alisema pamoja na Serikali kuwekeza fedha nyingi katika ujenzi wa mialo na masoko ya samaki baadhi ya halmashauri zimetelekeza miundombinu hiyo na kuendelea kutoa huduma katika maeneo yasiyo rasmi, pia baadhi ya mialo na masoko haifanyiwi matengenezo wala ukarabati kiasi cha kukosa huduma muhimu kama maji, vyoo, umeme na majokofu ya kuhifadhia samaki hali inayosababisha usumbufu na hasara kwa wananchi licha ya kutozwa ushuru kila uchao.

Kufuatia hali hiyo Waziri Mpina ametoa miezi mitano kwa Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinakarabati na kuweka huduma muhimu na kwamba wataoshindwa kufanya hivyo mialo na masoko hayo yatarejeshwa chini ya usimamizi wa Wizara na halmashauri hizo hazitaruhusiwa tena kukusanya mapato yatokanayo na sekta hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alimhakikishia Waziri Mpina kuwa maagizo yote aliyotoa watayafuatilia na kuyasimamia ili kuona utekelezaji wake kwani Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuleta mageuzi ya kweli katika sekta za Kilimo,Mifugo na Uvuvi.

Pia Ndikilo alisema ni jambo la kusikitisha kuona licha ya fursa kubwa za mifugo na uvuvi zilizoko katika mikoa ya Kanda ya Pwani lakini hadi sasa hakuna kiwanda hata kimoja cha kuchakata samaki wala nyama na kumuomba Waziri Mpina kuandaa kongamano ya mikoa hiyo ili kujadili kwa pamoja namna ya kuwekeza katika viwanda vya kuchakata bidhaa hizo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Kebwe Stephen Kebwe alisema maonesho hayo ya mwaka huu yamekuwa na mafanikio makubwa kwani wakulima,wafugaji na wavuvi na makundi mengine yamejitokeza kwa wingi na wamepata fursa ya kujifunza teknolojia mpya zitakazoboresha uzalishaji.

Maonesho hayo yalihudhuriwa na wakuu wa mikoa, wilaya, mameya, wakurugenzi wa halmashauri,madiwani pamoja na sekta binafsi.

Risala Ya Mwenyekiti Wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC ) Kuhusu Upigaji Kura Katika Uchaguzi Mdogo Utakaofanyika Kesho Agosti 12

0
0
RISALA YA MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MHE. JAJI (R) SEMISTOCLES S. KAIJAGE KUHUSU UPIGAJI KURA KATIKA UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE KATIKA JIMBO LA BUYUNGU NA UDIWANI KATIKA KATA THELATHINI NA SITA (36) TANZANIA BARA TAREHE 12 AGOSTI, 2018

Ndugu Wananchi;

Awali ya yote, kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi nachukua fursa hii kuvipongeza Vyama vya Siasa vilivyojitokeza kushiriki uchaguzi huu mdogo kwa kuwadhamini Wagombea waliochukuwa fomu na hatimaye kuteuliwa kuwania nafasi hizo zilizo wazi za Ubunge na Udiwani.
 
Nitumie nafasi hii pia kuwapongeza wananchi wote katika Jimbo la Buyungu na Kata Thelathini na Sita (36) zinazohusika na uchaguzi huu, kwa utulivu mliouonyesha wakati wote wa kipindi cha Kampeni. 

Ndugu Wananchi;
Kesho Jumapili tarehe 12 Agosti, 2018, ni Siku ya kupiga kura katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge wa Jimbo la Buyungu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma.  Vile vile, Uchaguzi mdogo wa Madiwani katika Kata Thelathini na Sita (36) zilizopo katika Halmashauri 29, za mikoa 19, ya Tanzania Bara. Uchaguzi huu Mdogo wa Ubunge na Udiwani Tanzania Bara, utahusisha jumla ya Wapiga Kura 485,203 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kutakuwa na Vituo vya Kupigia Kura 1,314.

Ndugu Wananchi;
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kutumia nafasi hii kuwakumbusha wapiga kura wa Jimbo la Buyungu na kata zote zitakazoshiriki Uchaguzi huu kuzingatia mambo muhimu yafuatayo:-
 
i)    Mosi, Upigaji kura utafanyika katika vituo vile vile vilivyotumika wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na vitafunguliwa saa moja kamili (1:00) asubuhi na kufungwa saa kumi kamili (10:00) jioni.  Iwapo, wakati wa kufunga kituo watakuwepo wapiga kura katika mstari ambao wamefika kabla ya saa kumi jioni na hawajapiga kura, wataruhusiwa kupiga kura.  Mtu yeyote hataruhusiwa kujiunga katika mstari wa wapiga kura baada ya saa kumi kamili (10:00) jioni.

ii)    Pili, watakaoruhusiwa kupiga kura ni wale tu ambao wamo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye Jimbo au Kata husika na wana kadi ya mpiga kura. Hata hivyo, Tume kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 61(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, pamoja na kifungu cha 62(1) cha Sheria  ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, imeruhusu wapiga kura ambao ama kwa bahati mbaya wamepoteza kadi zao za kupigia kura au zimeharibika au zimechakaa watumie mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo; wanaweza kutumia Pasi ya Kusafiria, Leseni ya Udereva au Kitambulisho cha Uraia kinachotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

iii)    Tatu, mpiga kura aliyepoteza kadi yake ya kupigia kura au kadi hiyo kuharibika au kuchakaa ataweza kuruhusiwa kutumia Vitambulisho hivyo mbadala, iwapo tu; atakuwa aliandikishwa kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mwaka 2015, jina lake liwe katika orodha ya Wapiga Kura katika kituo anachokwenda kupiga Kura na majina yake yaliyopo katika Daftari la Mpiga Kura yafanane kwa herufi, maneno na tarakimu na majina yaliyopo katika kitambulisho mbadala.

iv)    Nne, katika zoezi la upigaji kura, na kwa kadri itakavyowezekana kipaumbele kitatolewa kwa wagonjwa, watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali, wanawake wajawazito au wenye watoto wachanga, na wazee. 
 
v)    Tano, mpiga Kura mwenye ulemavu wa kutoona, ataruhusiwa kwenda kituoni na mtu atakayemchagua mwenyewe kwa ajili ya kumsaidia  kupiga kura yake.

vi)    Sita, ni wajibu wa Vyama vya Siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi kuweka Mawakala katika vituo vyote vya Kupigia na Kujumlishia Kura kwa utaratibu ambao tulikubaliana wakati wa Mkutano wa Tume na Vyama vya Siasa tarehe 10/07/2018 uliofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam, na nakala ya utaratibu huo kutumwa kwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

vii)    Saba, mawakala hao wanaruhusiwa kuwepo katika Vituo vya Kupigia Kura na wanatakiwa kufuata na kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazoongoza Uchaguzi katika kipindi chote cha kupiga, kuhesabu na kujumlisha kura na kutangaza matokeo.

Ndugu Wananchi;
Pamoja na kuwakumbusha mambo machache yanayopaswa kufanywa na kufuatwa siku ya Uchaguzi, Tume pia inapenda kusisitiza mambo yafuatayo:-
 
Kwanza, mwisho wa mikutano ya kampeni ni leo saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni. Baada ya muda huo, Vyama, wagombea na mashabiki wasifanye kampeni za aina yoyote, kama vile kutumia alama za Vyama zinazoashiria kampeni, vipeperushi, bendera, mavazi n.k kwa kuwa kesho ni siku ya Uchaguzi.  Aidha, wananchi waheshimu Sheria za Nchi wakati wote wa upigaji, kuhesabu, kujumlisha kura na kutangaza matokeo. 
 
Pili, pale panapokuwa na malalamiko yoyote ya ukiukwaji wa Sheria na Taratibu za Uchaguzi, malalamiko hayo yafikishwe kwenye mamlaka inayohusika kwa utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria. Vivyo hivyo, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wagombea au wafuasi wao na wananchi kwa ujumla wajiepushe na vitendo vinavyoweza kusababisha fujo au vurugu katika vituo vya Kupigia, Kuhesabia na Kujumlishia Kura.
 
Tatu, kwa kuzingatia tafsiri sahihi ya Kifungu cha 104 (1) kikisomwa pamoja na Kifungu cha 72(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania kwenye Shauri la Madai Anuai (Misc. Civil Cause No. 37 la mwaka 2015) mpiga kura anatakiwa kuondoka kituoni na kwenye maeneo ya kituo cha kupigia kura mara baada ya kupiga kura yake. Aidha, mbali ya wale ambao Sheria za Uchaguzi zinawaruhusu kuingia na kuwepo kwenye Vituo vya kupigia kura, wananchi wanatakiwa kujiepusha na mikusanyiko au mikutano katika maeneo ya Vituo vya kupigia kura. Vyama vya Siasa vimeweka mawakala vituoni ambao watalinda maslahi ya vyama husika na wagombea wao. 
 
Nne, wanaoruhusiwa kuingia kwenye Vituo vya kupigia, kuhesabia na kujumlishia kura ni wale tu walioainishwa kwenye kifungu cha 72(1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na kifungu cha 63(2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
 
Tano, Vyama vya Siasa, Wagombea, Wananchi na Watendaji wa Uchaguzi kwa ujumla wanakumbushwa kuzingatia na kuheshimu matakwa na masharti ya Sheria za Uchaguzi, Sheria za Nchi na Maadili ya Uchaguzi wakati wa Upigaji Kura, Kuhesabu, Kujumlisha hesabu za Kura, na Kutangaza matokeo.

Ndugu Wananchi;
Kwa kumalizia, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inawasihi tena Wapiga Kura wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na wanaoishi kwenye maeneo yanayofanya Uchaguzi Mdogo, kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuwachagua Viongozi wanaowataka wawaongoze kwa kipindi cha takribani miaka miwili ijayo.  Wananchi wafanye na kutekeleza zoezi la kuwachagua wawakilishi wao bila hofu, woga, wasiwasi au ushawishi kwani chini ya Kanuni ya 3.1 (b) ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, Serikali imepewa wajibu wa kuhakikisha kuwa kuna hali ya usalama, amani na utulivu katika kipindi chote cha Uchaguzi.

Ni matumaini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa, hali ya Amani na Utulivu kwenye maeneo ya Uchaguzi ambayo imekuwepo hadi hivi sasa, itaendelea kudumishwa ili kuhakikisha Uchaguzi huu mdogo unafanyika na kumalizika salama kwa Ustawi wa Taifa letu. 
 
Aidha, kila Mwananchi, Vyama vya Siasa na wadau wote wa uchaguzi tushirikiane, ili kuhakikisha kuwa viashiria vya kuvunjika kwa amani na utulivu vinaepukwa ili uchaguzi utakaofanyika uwe huru, wazi na wa haki.

KUMBUKA, KUPIGA KURA NI HAKI YAKO YA MSINGI KWA MUSTAKABALI WAKO NA WA NCHI YAKO, NENDA UKAPIGE KURA.
 
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.

Wizara Ya Mambo Ya Ndani Yatoa Tamko Kuhusu Akaunti Feki Ya Instagram Inayodaiwa Kuwa Ya Waziri Kangi Lugola

0
0
TAARIFA KWA UMMA
Kumekuwepo na akaunti feki ya mitandao ya kijamii ya instagram ambayo imesajiliwa kwa jina la ‘‘kangilugola’’ na imekuwa ikitoa taarifa mbalimbali kwa jamii kuhusu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara hii kwa ujumla.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi  inapenda kuujulisha Umma wa Watanzania kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Kangi A. Lugola hana akaunti yoyote kwenye mitandao ya Kijamii  hivyo akaunti yoyote  iliyosajiliwa kwa jina la kangilugola ni feki.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inatoa onyo kali kwa mtu yeyote anayejihusisha na kutumia jina la Kangi Lugola kusajili akaunti hiyo feki sambamba na kutoa taarifa za Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara kwa ujumla kupitia akaunti hiyo feki, na yeyote atakayebainika kujihusisha na jambo hili hatua za kishera zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha taarifa zote za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi zitatolewa kupitia tovuti ya wizara kwa anuani ya www.moha.go.tz na twitter ya  Wizara kwa akaunti ya MsemajiMamboyaNdani. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Vigogo Chama cha Ushirika Kilimanjaro Kuendelea Kusota Rumande

0
0
Vigogo watano wa ushirika mkoani Kilimanjaro wanaokabiliwa na kesi mbili za uhujumu uchumi na kudaiwa kusababisha hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 4.9, wamegonga mwamba katika maombi ya dhamana Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi, baada ya Jaji Winfrida Koroso kutupa maombi hayo.

Jaji Koroso aliyesikiliza maombi hayo, anatoka Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, Kitengo cha Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa maarufu kama Mahakama ya Mafisadi.

Mahakama hiyo iliketi kwa siku mbili na kutoa uamuzi wake jana, baada ya mawakili wa upande wa utetezi ambao wanawawakilisha washtakiwa hao kuweka pingamizi, wakidai kwamba kuna udhaifu katika hati iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP).

Wanaokabiliwa na kesi hizo ni Mwenyekiti wa zamani wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoani humo (KNCU 1984 Ltd), Aloyce Kitau, makamu wake, Hatibu Mwanga na Katibu Mkuu, Honest Temba. Wote kwa pamoja wanatuhumiwa kuusababishia ushirika huo hasara ya Sh. bilioni 2.9

Wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha Tanganyika Coffee Curing Co. Ltd (TCCCo), Meynard Swai na Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Andrew Kleruu, ambao wanadaiwa kukisababishia hasara ya Sh. bilioni 1.6

Akisoma uamuzi huo jana, Jaji Koroso alisema mahakama hiyo imepima kwa umakini maombi ya dhamana hiyo na imeona hayana msingi, kwa kuwa suala hilo linagusa maslahi ya wanachama wa KNCU.

Jaji huyo alisema katika hati za viapo vya dhamana zilizowasilishwa katika mahakama hiyo, ni dhahiri kwamba si halali kisheria kwa sababu zimewasilishwa zikiwa zimedurufiwa na si halisi.

Katika shtaka la kwanza, Kitau (70), Mwanga (70) na Temba (38) wanatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi kinyume cha kifungu cha 96 (1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya Sheria iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002.

Ilidaiwa katika tarehe tofauti, kati ya Julai, 2014 na Novemba, 2017 wakiwa katika Manispaa ya Moshi, Kilimanjaro, walitumia vibaya mamlaka ya ofisi yao na bila kufuata sheria, kuilipa fidia Kampuni ya Ocean Link Shipping Services Ltd.

Shitaka la pili ambalo pia linawakabili washtakiwa wote watatu, ni la kuisababishia hasara KNCU, kinyume cha Aya ya 10 (1) cha Jedwali, na vifungu vya 57 na 60 (2) vya Sheria ya Uhujumu Uchumi, Sura ya 200 ya Sheria iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002.

Swai (57) na Kleruu (56) kwa upande wao, kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya matumizi mabaya ya ofisi, kinyume na kifungu cha 96 (1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002 na la pili ni la kukisababishia hasara kiwanda hicho.

Hakimu aionya Jamhuri kesi ya vigogo wa Simba

0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa siku saba  hadi Agosti 7 kwa upande wa Jamhuri kukamilisha mchakato wa kubadilisha hati ya mashtaka ili kuwaondoa washtakiwa wawili katika kesi inayomkabili aliyekua Rais wa  klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake, Godfrey Nyange (Kaburu).

Washtakiwa wanaotakiwa kuondolewa katika kesi hiyo ni Zacharia Hanspope na Frank Lauwo ambao hawajawahi kufika mahakamani hapo.

Mapema, mahakama hiyo ilikubali upande wa Jamhuri kubadilisha hati ya mashtaka kutoka washtakiwa wawili na kuwaunganisha Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe na mfanyabiashara Franklin Lauwo.

Hati hiyo, ilisomwa katika mahakama hiyo iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi umekamilika.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali Leonard Swai alidai kesi hiyo haiwezi kuanza kusikilizwa kwa sababu washtakiwa wawili bado hawajakamatwa.

Upande wa utetezi, ulipinga na uliomba hati ya mashtaka kufanyiwa mabadiliko kwa kuwaondoa washtakiwa ambao hawajakamatwa ili Aveva na Kaburu wajue hatima yao na mahakama iliamuru hati kubadilishwa.

Jana, Jamhuri ulidai kuwa wanasubiri kibali cha DPP cha kuwaondoa washtakiwa wawili ili kuwasomea maelezo ya awali marais hao.

"Mheshimiwa hakimu DPP bado yuko nje ya Dar es Salaam tunaahidi kwamba hata kama yuko Dodoma tutamfuata au hapa hapa Dar es Salaam ili akamilishe hatua ya kuruhusu kesi hii kuendelea," alidai Swai.

Mara baada ya kudai hayo, mshtakiwa wa kwanza, Aveva  aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe za karibu ili waweze kusikiliza kesi hiyo kwa madai kuwa imechukua muda mrefu huku wakili wa Jamhuri, Shadrack Kimaro na wa Takukuru, Swai wamekuwa wakirushiana mpira.

Mshtakiwa wa pili, Kaburu amedai kuwa ni zaidi ya mwaka mmoja sasa umepita wapo mahabusu tangu kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani hapo huku mawakili hao wakidai faili lipo kwa DPP.

Alidai mshtakiwa wa kwanza, Aveva ana matatizo ya kiafya na kwamba kila wiki anaenda kliniki kwa ajili ya matibabu hivyo kuendelea kurushiana mpira ni kuwaumiza.

Alidai hadhani kwamba si DPP ameshindwa kushughulikia kesi yao, bali ni ucheweshaji wa makusudi unaofanywa na mawakili hao katika kesi hiyo kutoka kwa DPP na Takukuru.

Alidai upelelezi umeshakamilika kilichobaki ni kubadilisha hati hiyo ili kesi ianze kusikilizwa, hivyo aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe za karibuni ili waweze kuwaona na kuwaonea huruma kuliko kupanga tarehe za mbali.

Wakili Swai alidai kuwa hoja zilizotolewa na washtakiwa hao zina mashiko na kuahidi kushughulikia suala hilo.

Hata hivyo, Hakimu Simba alitoa siku saba kwa upande wa Jamhuri kukamilisha mchakato wa kubadilisha hati ya mashtaka ili kesi hiyo iweze kusikilizwa.

“Ukiangalia afya ya Aveva unaona kabisa ni mgonjwa, anatakiwa kwenda kliniki kwa wiki mara mbili, hivyo basi tunalazimika kuangalia ratiba ya matibabu yake ili tupange kesi,” alisema Hakimu Simba.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images