Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

CHADEMA Kuteua Wagombea Agosti 15......Kalanga Mgombea Pekee CCM, Waitara Naye Kujitosa tena Jimbo la Ukonga kupita CCM

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kitafanya uteuzi wa wagombea ubunge katika majimbo ya Monduli, Korogwe na Ukonga Agosti 15 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema amesema hayo leo Alhamisi Agosti 9.

“Wameanza kuchukua fomu za uteuzi ila sisi uteuzi ni Agosti 15, ndiyo vikao vitakaa na kuteua,” amesema Mrema.

Wakati chama hicho kikijipanga kufanya uteuzi huo, tayari Chama cha Mapinduzi (CCM), katika Jimbo la Monduli kimempitisha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo aliyejiuzulu wiki iliyopita, Julius Kalanga kuwa mgombea pekee licha ya wanaCCM Kuandamana kumpinga.

Kadhalika hali ikiwa hivyo katika Jimbo la Monduli, tayari aliyekuwa Mbunge wa Ukonga aliyejiuzulu na kuhamia CCM, Mwita Waitara anadaiwa kuchukua fomu kupitia chama hicho akiomba kuteuliwa kugombea tena jimbo hilo huku katika Jimbo la Korogwe wakitarajia kufanya uchaguzi leo.

Wiki iliyopita, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilitangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo matatu na wa udiwani katika kata mbili za Tanzania Bara utakaofanyika Septemba 16, mwaka huu ambapo fomu za uteuzi wa wagombea wa majimbo hayo zitatolewa kuanzia Agosti 13 hadi 20, mwaka huu.

Rais Magufuli Asisitiza Ushirikiano Imara kati ya Tanzania na Uganda

$
0
0
Rais John Magufuli amesema Tanzania na Uganda zitaendelea kufanya biashara kwa pamoja ili kuimarisha uchumi wa nchi zote mbili na kudumisha mshikamano kati yao.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Agosti 9, Ikulu jijini Dar es Salaam wakati Rais Magufuli akizungumza baada ya mazungumzo yake na  Rais Yoweri Museven ambaye aliambatana na viongozi mbalimbali kutoka nchini Uganda.

“Nimefurahia sana ziara ya mzee wetu Museven pamoja na ujumbe aliokuja nao hivyo ningependa Tanzania na Uganda tufanye biashara kwa pamoja na tuwe kama ndugu,” amesema Magufuli

Aidha rais Magufuli amesema wamekaa na Rais Museven na kukubaliana kutafuta namna ya kuzuia watu wenye lengo la kuharibu viwanda vya Uganda kutokana na hali hiyo kuwahi kutokea kipindi cha nyuma

“Kuna sukari iliwahi kuingizwa hapa nchini kumbe ilikuwa haijatengenezwa na viwanda vya Uganda bali ilikua na lengo la kuharibu viwanda vyao hivyo tumezungumza na rais Museven ili suala hilo lisijitokeze tena,” amesema Rais Magufuli

Rais Museven yupo nchini kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuimarisha ushirikiano na ujirani mwema uliopo kati ya Tanzania na Uganda.

Safari ya Mwisho ya Mzee Mjuto, Mamia wajitokeza kutoa heshima za Mwisho viunga vya Karimjee Hall.

$
0
0
Mamia  ya waombolezaji wamejitokeza katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kuaga mwili wa aliyekuwa muigizaji nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ leo Agost 9, 2018.

Mzee King Majuto alifariki dunia jana majira ya saa 2:00 usiku Agosti 8, 2018 katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa siku kadhaa.

Baada ya kuaga mwili utasafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga kwa maziko ambayo yatafanyika kesho Ijumaa.

==>>Tazama Video hapo chini

Rais Magufuli Ashindwa Kujizuia na Kumwaga Machozi Akimuaga Mzee Majuto

$
0
0
Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ameshindwa kujizuia na kujikuta akimwaga machozi wakati alipokuwa akiaga mwili wa aliyekuwa msanii nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Agosti 9, 2018.

Rais Magufuli alifika Karimjee na kujumuika na viongozi mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete na waombolezaji wengine katika kuaga mwili wa nguli huyo aliyefariki dunia jana Jumatano, majira ya saa 2 usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbuili alipokuwa akitibiwa.

Mwili wa Mzee Majuto umesafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga ambako atazikwa kesho Ijumaa, Agosti 10, 2018 mchana.

Mbunge Ester Matiko, Mwandishi wa Tanzania Daima na Wafuasi wa CHADEMA Waachiwa Baada ya Kukamatwa jana na Polisi

$
0
0
Mbunge wa Tarime Mjini,  Ester Matiko, mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima Sitta Tuma na wafuasi wengine 14 wa Chadema waliokuwa wamekamatwa na polisi kwa tuhuma za kufanya mkutano usio halali wameachiwa. Hata hivyo, wametakiwa kuripoti polisi kesho.

Matiko, Tuma na wafuasi hao walikamatwa na polisi jana wakati wa kampeni za kumnadi mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Turwa.

Akizungumza na wanahabari leo Agosti 9 Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime /Rorya Henry Mwaibambe amesema polisi iliwataka wafuasi hao na viongozi watawanyike kwa kuwa mkutano huo siyo halali.

Pia, amesema baadhi ya wananchi waliondoka lakini wengine walikaidi, ndipo polisi ikalazimika kuwatawanya kwa mabomu lakini watuhumiwa hao walikaidi kuondoka jambo lililolazimu polisi kuwakamata.

“Nilipokea barua jana kutoka kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Turwa ya kusitishwa kwa kampeni za chaguzi za Chadema lakini chama hicho kilikaidi licha ya kupewa barua ya kusitisha mkutano.

“Polisi tulipewa barua ya zuio la mkutano ikionyesha kuwa Chadema wamekiuka kifungu cha 124 A cha Sheria ya Taifa ya uchaguzi,kamati ya maadili ya uchaguzi Kata ya Turwa kupitia kikao kilichoketi Agosti 8,2018 kilichowashirikisha na viongozi wa siasa kilisitisha kampeni za Chadema,” ameongeza.

Amesema Chadema waliambiwa wasifanye mkutano tangu saa sita mchana jana lakini saa kumi jioni kundi la watu zaidi ya 300 walionekana ofisi ya Chadema wakiwa kwenye mkusanyiko.

Mwaibambe amedai mbunge Matiko alitakiwa kuondoka eneo hilo lakini aligoma na kuanza kutukana polisi na hakuna yeyote aliyepigwa wakati wanakamatwa na kupandishwa kwenye gari.

“Kama wamepigwa wakiwa ndani ya kituo hiyo ni ishu,” amesema.

Akizungumzia kukamatwa kwa mwandishi wa habari Mwaibambe amesema;

“Nimepigiwa simu nyingi na media nyingi, waandishi wa habari wakiwamo wa Tarime wakiomba nimwachie Mwandishi mwenzao lakini polisi tumekataa, huyu amekamatwa akiwa kwenye mkusanyiko uliozuiwa. Waandishi wenzake waliondoka yeye akabaki.”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Agosti 10

Mfumuko Wa Bei Wa Taifa Umepungua Kufikia Asilimia 3.3

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Julai, 2018 umepungua hadi kufikia asilimia 3.3 ikilinganishwa na asilimia 3.4  mwezi Juni, 2018.

Hayo yameelezwa  jana na Jijini Dodoma na  Mkurugenzi wa sensa na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ephraim Kwesigabo alipokuwa akitoa taarifa  ya mfumuko wa bei kwa mwezi Julai mwaka huu.

Kwesigabo alisema, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 imepungua ikilinganishwa na kasi ilivyokuwa kwa  mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 kumechangiwa hasa na kupungua kwa mfumuko wa bei wa baadhi ya bidhaa za vyakula, ambapo bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei kati ya Julai, 2017 na Julai 2018 ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 9.5, mtama kwa asilimia 17.8, unga wa mihogo kwa asilimia 14.1, matunda jamii ya machungwa kwa asilimia 22.2, maharagwe kwa asilimia 5.8 na mihogo mibichi kwa asilimia 12.5,” alifafanua Kwesigabo.

Aliendelea kusema kuwa ni zaidi ya miaka 15 tangu itokee tarakimu kama hiyo ya mfumuko wa bei ambayo iko vizuri kwa uchumi wa nchi.

Aidha alitaja hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya  nchi za Afrika Mashariki kama ifuatavyo; Uganda mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 3.1 kutoka asilimia 2.2 kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018. Kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 4.35 kutoka asilimia kutoka asilimia 4.28 kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

Mfumuko wa bei wa Taifa unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome.

Waziri Ndalichako Azindua Baraza La Uongozi La NACTE

$
0
0
Na Regina Mkonde
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  leo tarehe 9 Agosti, 2018 amelizindua Baraza jipya la Uongozi la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika jana tarehe 9 Agosti, 2018 katika ukumbi wa mikutano wa NACTE ulioko jijini Dar es Salaam, Prof. Ndalichako alilipongeza baraza lililomaliza muda wake, na kutoa maagizo kwa baraza jipya.

Prof. Ndalichako amelitaka baraza hilo kuendelea kusimamia pamoja na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa na vyuo hapa nchini.

Vile vile, Prof. Ndalichako amelitaka baraza hilo kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika vyuo vilivyosajiliwa na vitakavyosajiliwa hapa nchini, ili kuhakikisha elimu inayotolewa kwa wahitimu inakidhi soko la ajira.

Katika hatua nyingine, Prof. Ndalichako amelitaka baraza jipya la NACTE kuongeza juhudi katika kufanya utafiti wa soko la ajira ili liweze kuwashauri wawekezaji wanaotaka kuanzisha vyuo, kutoa mafunzo yanayokidhi soko la ajira.

Hali kadhalika, Prof. Ndalichako amelitaka baraza la NACTE kusimamia vyema vyanzo vya mapato hasa vya ndani ili liweze kujiendesha kwa ufanisi zaidi.

Sambamba na hilo, ameishauri NACTE kutoa ushauri kwa wanaotaka kuanzisha vyuo, kutoa mafunzo kuhusu sekta zinazotoa ajira kwa sasa, hususani sekta ya kilimo, viwanda, madini na gesi.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi NACTE, Profesa John Kandoro amemhakikishia Prof. Ndalichako kwamba watatekeleza maagizo yake, akisema kuwa, baraza lake litaendelea kufanya tathimini ya ubora wa vyuo pamoja na kuendeleza elimu ya ufundi ili kufanikisha adhma ya serikali ya uchumi wa viwanda. 

Baba Aua Mtoto kwa Kipigo Jijini Mwanza

$
0
0
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Sumbugu wilayani Misungwi  jijini Mwanza, Mariamu Tabu (18)amefariki dunia kwa kile kilichodaiwa ni kupigwa na baba yake mzazi baada ya kutohudhuria shuleni.

Akizungumza na wanahabari jana Agosti 9, Kamanda wa Polisi jijini humo Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kituo cha Misungwi na atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Kamanda Msangi amesema kuwa mama mzazi wa Mariam, Kija Mashauri amelieleza Jeshi la Polisi kuwa Agosti 6, mwanaye alikwenda shule lakini hakurudi nyumbani badala yake alirudi Agosti 7 jioni, ndipo baba yake aliuliza alipokuwa na kuanza kumpiga.

“Baba tayari tumemkamata kwa ushirikiano na wananchi, mara baada ya kutekeleza tukio la kumpiga mwanae alitaka kukimbia akazuiwa na wanakijiji, ambapo walimuwahisha mtoto katika zahanati ya kijiji kwakuwa alikuwa katika hali mbaya alifariki akiwa mapokezi”, amesema Msangi.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Gari la Mbunge CHADEMA Lapata Ajali....Dereva Afariki

$
0
0
Na Magdalena Kashindye
Gari la Mbunge wa CHADEMA Lucy Magereri lenye namba za usajili T l348 CSR limepata ajali eneo la Issuna wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambapo Dereva aliyefahamika kwa jina la Thomas Maro amepoteza maisha papo hapo.

Ajali hiyo imetoka jana Agosti 9 ambapo ndani ya gari hiyo alikuwepo dereva mwenyewe kwani alikuwa analitoa gari hilo Dodoma kulipeleka Shinyanga ndipo lilipogongana na Fuso lililokuwa linatoka Singida kwenda Dar es Salaam.

Dereva wa Fuso amepata majeraha madogo madogo huku mwili wa marehemu ukihifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Sweetbert Njewike amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa Fuso kuendesha gari upande ambao sio wake, na sasa amekamatwa yupo kituo cha Polisi kwa ajili ya mahojiano.

Waziri Mkuu Ataka Wanafunzi Walioanza Shule Kumaliza Pamoja

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha wanafunzi wote wanaoingia kidato wanahitimu masomo yao ya kidato cha nne.

Majaliwa ameyasema hayo jana Alhamisi Agosti 9, alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mnacho iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi akiwa katika ziara yake ya kutembelea jimboni kwake.

“Serikali haitaki kusikia mwanafunzi anaacha shule kwa utoro wala akiacha shule kwa kupata mimba akiwa shuleni badala yake inataka wanafunzi wote wamalize masomo yao salama kwani tumefanikiwa kupunguza baadhi ya changamoto zikiwamo kuajiri walimu wapya ambao wamesambazwa katika shule zao nchi nzima,” alisema.

Hata hivyo, Majaliwa alisema licha ya kuajiri walimu pia serikali imemaliza changamoto ya vitabu kwa kupeleka vitabu vya sayansi ya sanaa katika shule zote za sekondari nchini kwa kupunguza uwiano wa wanafunzi wanaotumia vitabu hivyo ambapo awali kitabu kimoja kilikuwa kinatumika na wanafunzi 10  na kwa sasa kitabu kimoja kinatumika kwa wanafunzi watatu hadi watano.

Alisema mkakati wa serikali kwa siku za usoni ni kuhakikisha kila mwanafunzi anakuwa na kitabu chake cha kujisomea  ili kuwafanya wanafunzi hao kusoma wakiwa huru.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi alisema kuwa Mkoa wa Lindi umekuwa ukifanya vibaya katika mitihani yake ya kitaifa ya darasa la saba na mtihani wa kidato cha nne.

“Katika miaka miwili mfululizo kuanzia mwaka 2015  na 2016  mkoa ulikuwa ukishika nafasi ya mwisho katika mitihani ya kidato cha nne kwa nchi mzima, ambapo kwa  mitihani wa shule ya msingi darasa la saba kwa mwaka jana mkoa ulishika nafasi ya nne kutoka nafasi ya 19 mwaka juzi,” alisema.

Fredy Lowassa kurithi mikoba ya baba yake Monduli kwa Tiketi ya CHADEMA

$
0
0
Baada ya kuwepo kwa mashinikizo mbalimbali yakimtaka mtoto wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa awamu ya nne, Edward Lowassa kugombea Ubunge jimbo la Monduli Fred Lowassa, hatimaye ameweza kutimiza maagizo hayo kwa kuchukua fomu rasmi jana Agosti 09, 2018.

Fred Lowassa amechukua maamuzi hayo baada ya jimbo hilo kuwepo wazi kutokana na aliyekuwa Mbunge wa eneo hilo Julius Kalanga kujiuzulu mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.

Mbali na Fred kuchukua fomu hiyo kutoka CHADEMA pia wamejitokeza wanachama wengine ndani ya chama hicho kuonesha nia ya kuomba ridhaa ya Jimbo hilo ambapo ni pamoja na Mwenyekiti Baraza la Wanawake wa CHADEMA mkoa Cecilia Ndosi, diwani viti maalum, Yona Laizer, Lobulu Kivuyo aliwahi kuwa mgombea katika uchaguzi mdogo uliopita Kata ya Muhita na Eric Ngwijo.

Katibu wa CHADEMA kanda ya Kaskazini ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Arusha, Aman Golugwa amesema wagombea hao wanatarajiwa kupigwa kura za maoni katika kikao kitakachofanyika Agosti 12, 2018 siku ya Jumamosi.

"Kwa jimbo la Monduli hadi kufikia majira ya saa 10 jioni ambapo ndio ilikuwa mwisho wa kurudisha fomu, tulipata watia nia wanne. Kuhusu Fred Lowassa tutatoa taarifa rasmi maana kuna vitu, tumekubaliana tuvifanye kidogo lakini naye ni miongoni mwa waliochukua na kurudisha fomu", alisema Golugwa.

Jimbo la Monduli limekuwa wazi kuanzia usiku wa Julai 30, 2018 baada ya Mbunge aliyechaguliwa 2015 (CHADEMA), Julius Kalanga kujiunga na CCM kwa kile alichoeleza kuwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli na kudai kuwa ameondoka CHADEMA kwasababu ya siasa za chuki na uhasama.

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Mbeya Agoma Kujiuzulu Uenyekiti wa CCM Iringa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema hatajiuzulu nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa licha ya kushinikizwa na baadhi ya wanachama kuachia nafasi hiyo.

Chalamila alitoa msimamo huo jana alipokuwa anazungumza na viongozi wa dini na kueleza baadhi ya wanachama wa CCM Mkoa wa Iringa wanamshinikiza ajiuzulu, ili kukidhi matakwa ya utaratibu mpya wa chama unaotaka mtu mmoja kuwa na cheo kimoja.

Alisema ataendelea kuwa mwenyekiti mpaka Rais Dk. John Magufuli ambaye ndiye aliyemteua, atakapotoa maelekezo mengine.

“Baada ya kuteuliwa kuna baadhi ya watu walinifuata wakinitaka nijiuzulu nafasi ya uenyekiti, sasa ninachokijua ni kwamba Rais aliniteua kuwa Mkuu wa Mkoa akiwa anajua kuwa mimi ni mwenyekiti, hivyo naendelea kushika nyadhifa zote mpaka nitakapopata maelekezo mengine,” alisema Chalamila.

Katika hatua nyingine, Chalamila alisema kwa muda mrefu Jiji la Mbeya limekuwa halipati maendeleo kutokana na mwendelezo wa siasa chafu zinazoifanya serikali ishindwe kutekeleza baadhi ya miradi ya maendeleo.

Aliwataka viongozi wa dini kuisaidia serikali katika kuhubiri amani na kuwaelimisha vijana kufanya kazi kwa bidii badala ya kuendekeza vijiwe vya siasa zisizokuwa na manufaa katika maisha yao ikiwamo kukashifu vyama wasivyoviunga mkono.

Alisema katikati ya Jiji la Mbeya barabara ilitakiwa iwe ya njia nne na barabara ya mchepuko kutoka Uyole mpaka Songwe kwa ajili ya magari makubwa ya mizigo ilitakiwa iwe imejengwa, lakini siasa zimekuwa zikikwamisha.

“Hili ni jiji, lakini siku zote huwa najiuliza kuwa ni kweli serikali imeshindwa kujenga barabara ya njia nne, ni kweli serikali imeshindwa kujenga kilomita 40 barabara ya mchepuko na je, serikali imeshindwa kuukamilisha uwanja wa ndege wa Songwe na kuupa hadhi yake ya kimataifa?” Alihoji Chalamila.

“Ninachokiona hapa ni kwamba siasa ndiyo ‘zinatucost’ (zinatugharimu), mtu anaamua kurudisha nyuma mikono na kuacha aone tunavyofanya, lakini kwa sasa naona hali imeanza kuwa tulivu, mimi na katibu tawala tutamwandikia rais atusaidie baadhi ya miundombinu hii muhimu iboreshwe haraka,” alisisitiza.

Aliwaomba viongozi wa dini mkoani humo, kuendelea kuisaidia serikali kuwaelimisha vijana kuhusu mambo mbalimbali ya maendeleo na kuachana na siasa chafu ambazo hazina manufaa kwa sasa.

Aliwataka kuanzisha madarasa maalumu ya kuwafundisha vijana ujasiriamali kwenye maeneo yao ya kuabudia, ili wajikite kwenye shughuli hizo na kujiletea maendeleo.

Credit:Nipashe

Wawili Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kuwatorosha Wanafunzi na Kuwapeka Dar Wakafanye Kazi za Ndani

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Iringa linawashikilia watu wawili waliokuwa wakiwasafirisha wanafunzi watano wa shule ya sekondari ya Mlafu kwenda Dar es Salaam kufanya kazi za nyumbani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi (ACP),  Juma Bwire, alisema  tukio lilitokea Julai 31, mwaka huu, katika mji mdogo wa Ilula, Kilolo mkoani Iringa.

Bwire alisema watuhumiwa hao walikuwa wakihangaika kuwasafirisha kwa ajili ya kuwatumikisha kazi za ndani, baada ya wanafunzi hao kutoweka kwa wazazi wao tangu Julai 29 mwaka huu na walisafirishwa kwa bodaboda kutoka Mlafu hadi Ilula.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Tulizo Mtega (19) na Rosemary Msasalage (18) wote wakazi wa Ilula na kwamba mbinu iliyotumika kuwarubuni wanafunzi hao ni kuwa wamepata kazi mbalimbali za kuuza maduka Morogoro na Dar es Salaam.

Snura na mpenzi wake wapata ajali

$
0
0
Msanii wa Bongo, Snura Mushi amenusurika katika ajali ya gari. Muimbaji huyo alikuwa ameongozana na madensa wake, aliyetoa taarifa ya ajili hiyo iliyotokea majira ya saa nne usiku ni Minu Calypto ambaye anatajwa kuwa mpenzi wa Snura. 

Kupitia Instagram ameandika; "Jana mida ya saa nne usiku tulipata ajali mimi na Snura Mushi na ma-dancer wetu wawili pamoja na dereva.. Gari ilipinduka ila tunashkuru Mungu tuko salama.. #WeGood"


Mzee Majuto Kuzikwa Leo Katika kijiji cha Kiruku yalipo mashamba yake Huko Tanga

$
0
0
Mwili wa muigizaji wa vichekesho Amri Athumani 'Mzee Majuto' umewasili Donge nyumbani kwake  jana 7.05 usiku . Safari ya kwenda Tanga kwaajili ya mazishi ilianza saa 10.15 jioni baada ya kumuaga katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.

Leo  Agosti 10, kuanzia saa 5.45 mchana, ibada ya mazishi itafanyika katika msikiti wa Nuruguda uliopo karibu na nyumbani kwake na kuzikwa kijiji cha Kiruku yalipo mashamba yake nje kidogo cha jiji la Tanga.

Mzee Majuto alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya Tezi Dume ambapo Januari mwaka huu,alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam na kisha baadaye kupelekwa India kwa Matibabu zaidi . June 23, mwaka huu  alirejea nchini na kupelekwa moja kwa moja  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Habarika Masaa 24......Pakua Upya Application Yetu Tukuhabarishe Usiku na Mchana

$
0
0
==>Pakua Upya Application yetu tukuhabarishe masaa 24 usiku na mchana.

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia;

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images