Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Polisi Wafungua Jalada la Uchunguzi Dhidi ya Zitto Kabwe

$
0
0
Jeshi la Polisi limefungua jalada la uchunguzi dhidi ya kauli zilizotolewa na mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe.

Akizungumza leo Jumatano Agosti Mosi, 2018 msemaji wa polisi, Barnabas Mwakalukwa amesema kwa sasa uchunguzi unafanyika kuhusiana na tuhuma zinazomkabili mbunge huyo ambaye pia ni kiongozi wa ACT.

Mwakalukwa ameeleza hayo ikiwa imepita siku moja tangu Waziri wa Mambo ya Ndani,  Kangi Lugola kumtaka kiongozi huyo kujisalimisha polisi  kwa maelezo kuwa ametoa kauli za uchochezi.

Lugola amesema Zitto ametoa kauli za uchochezi na kuwatukana viongozi wa Serikali wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika jimbo la Kilwa Kusini, mkoani Lindi.

Katika mkutano huo Zitto alialikwa na mbunge wa jimbo hilo, Seleman Bungara maarufu Bwege.

Mwakalukwa amesema kufuatia agizo hilo la Lugola tayari wamefungua jadala kuchunguza jambo hilo, kwamba uchunguzi ukikamilika na iwapo itaonekana mbunge huyo anahitajika, watamuita polisi.

Amesema polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria, kwamba Zitto akihitajika ataripoti kwa kamanda wa polisi mkoani Lindi.

Jana, Zitto alijibu kauli ya Lugola ya kumtaka aripoti polisi akibainisha kuwa atakwenda ikiwa atapewa wito wa kisheria.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter Zitto amesema, “waziri hana hayo mamlaka. Kama polisi wananitaka watoe wito wa kisheria nitakwenda.”

“Naendelea na kampeni za ubunge wa Buyungu ambapo tunamuunga mgombea wa Chadema na madiwani wa ACT- Wazalendo kwenye kata kadhaa. Nashauri waziri ampate kwanza yule mbwa wa polisi bandari.“

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Alhamisi ya Agosti 2

Watu Wawili Watiwa Mbaroni Jijini Mbeya Kwa Kosa la Kumchoma Moto Mtoto

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wawili Judith Amoni Mwansansu (39)  Mkazi wa Mwanjelwa na Aive Alex Swalo  (17) Mkazi wa Mwanjelwa Mtaa wa Soko kwa kosa la  kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto aitwaye Daines Kefas Mwansasu (06) Mwanafunzi wa Shule ya Awali – Mlimani na Mkazi wa Mtaa wa Soko hapa Jijini humo.

Taarifa ya tukio hilo imetolewa jana tarehe 1 Agosti, 2018 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Ulrich Matei.

Akielezea kuhusu tukio hilo kwa wanahabari, Kamanda Matei amesema tukio hilo lilifanyika Jumanne  majira ya saa tatu usiku ambapo jeshi la polisi lilipokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa raia wema, ya kwamba mtoto huyo amejeruhiwa sehemu mbalimbali kwa moto.

“Inadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio mhanga alikuwa ameenda kucheza na rafiki zake na aliporudi nyumbani majira ya jioni ndipo shangazi yake alimuadhibu kwa kumchapa na waya wa umeme sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha na maumivu makali mwilini. Inadaiwa kuwa tarehe 01.08.2018 majira ya asubuhi, watuhumiwa waliendelea kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto huyo kwa kumuunguza kwa moto sehemu za miguuni na kwenye makalio,” ameeleza Kanada Matei.

Kamanda Matei amesema kuwa “Mtoto amejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake baada ya kufanyiwa vitendo vya ukatili na shangazi yake akishirikiana na mtoto wake. Watuhumiwa wote wawili wamekamatwa kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo. Mhanga amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu zaidi ya kitabibu.”

Katika hatua nyingine, amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kukabiliana na vitendo vya uhalifu na ajali za barabarani ili kuhakikisha kuwa wageni na wakazi wa Mkoa huu wanaendelea kuwa salama na mali zao.

“Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa usalama hali inayopelekea kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu pamoja na ajali za barabarani,” amesema.

Kamanda Matei ameendelea kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahalifu. Pamoja na kwa wazazi/walezi kujiepusha na vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto wao kwani ni kinyume cha sheria.

Wajawazito Wanatakiwa Kupata Huduma Za Uzazi Bure-dk. Ndugulile

$
0
0
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesisitiza kuwa huduma za uzazi kwa wajawazito zinatolewa bila ya malipo katima Hospitali na vituo vya afya vya Serikali.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa ziara yake ya kujua hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Rufaa Temeke, Amana na Mwananyamala leo jijini Dar es salaam.

“Nimesikia pale wajawazito wameniambia wamekuja na vifaa vya kujifungulia kutoka majumbani mwao sitaki kusikia mwanamke mjamzito analipishwa wala kuja vifaa vya kujifungulia kwani sera yetu inasema huduma za uzazi ni bure” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile alisema kuwa wanawake wajawazito , watoto chini ya miaka 5 na wazee wasio na uwezo wanapata matibabu bure kulingana na sera ya Afya inavyosema. Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa kila mtoa huduma anapaswa kuandika taarifa ya mgonjwa kabla na baada ya kumpa huduma katika kituo chake cha kazi.Aidha Dkt. Ndugulile aliwataka watoa dawa katika hospitali na vituo vya afya kuandika majina asilia ya dawa na siyo yale ya kampuni pamoja na kufuata muongozo wa dawa uliyowekwa na Serikali.

“Marufuku watoa dawa kuwaandikia wagonjwa dawa na kwenda kununua nje ya kituo cha afya na badala yake dawa zote zitolewe katika hospitali au kituo cha afya kama zimeisha zinatakiwa kuagizwa kwa haraka na nauagiza uongozi wa Hospitali ya Amana kuwarudishia wagonjwa wa wodi ya watoto waliokwenda kununua dawa nje leo hii ” alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Temeke Dkt. Amaan Malima amesema kuwa changamoto kubwa inayowakumba ni upungufu wa watumishi .

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Hospitali ya Rufaa ya Amana Dkt. Meshack Shimwela amesema kuwa anaomba radhi kwa tatizo hilo lililojitokeza kwani hakuna tabia kama hiyo hospitalini hapo na amehaidi kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo.

Halima Mdee na Wengine 13 Watiwa Mbaroni

$
0
0
Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Halima Mdee (Mb) pamoja na viongozi wengine, wanachama na wapenzi wa CHADEMA Jimbo la Kawe takribani 13, jana walikamatwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Polisi Kawe kwa kosa la kufanya mkusanyiko usio na kibali.

Mdee amesema alipigiwa simu na vijana wanaofanya biashara ya kutengeneza bustani wa eneo la Mzimuni, Kawe kwamba wamepewa notisi ya kuondoka.

Amesema wakati anapigiwa simu, alikuwa Kunduchi katika ziara hivyo ikamlazimu kwenda kuwasikiliza wananchi wake.

“Nilipofika, nilizungumza nao na kuwaeleza suala hili nalishughulikia, kwani nimewasiliana na wizara ya ardhi, mipango miji na Tarura (wakaka la wabarabara za vijijini na mijini).”

“Ni kweli wale vijana wako eneo la barabara na wamenieleza hawana tatizo la kuondoka, lakini wanahitaji kuelekezwa wapi watakwenda kuendelea na shughuli zao.” amesema.

Amesema baada ya kumaliza kuzungumza nao, aliondoka lakini alipofika mbele akaelezwa kuna watu wamekamatwa huko alipotoka.

“Nikaona nirudi, nilipofika nikakuta baadhi ya wafanyabiashara na wanachama wanarushwa kichura chura, nikahoji kuna nini sikupata majibu yanayoeleweka.”amesema.

Mdee amesema baada ya hapo, watuhumiwa hao waliokuwa chini ya ulinzi, wakapelekwa kituo cha polisi Kawe  na yeye akatangulia kituoni.

“Nilipokuwa nakwenda, kama mita 20 nikaambia na mheshimiwa rudi, niliporudi nikaambiwa niko chini ya ulinzi, na kuniweka katika gari yao, tukaenda hadi kituoni na kuhojiwa kwa kufanya mkusanyiko usiokuwa na kibali,” amesema Mdee

Hata hivyo, baada ya kuhojiwa wale wafanyabiashara na wanachama wa Chadema  waliachiwa  huru.

Mmoja Atiwa Mbaroni Kwa Kujifanya Katekwa na Wasiojulikana

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia mtu mmoja, aliyejulikana kwa jina la Prosper Lema, aliyedai kutekwa na watu wasiojulikana na kuanza kutumia uongo kuomba fedha kwa ndugu zake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, amesema, taarifa hizo za Bw. Lema zilipatikana baada ya ndugu zake mtuhumiwa huyo kwenda katika kituo cha polisi kirumba jijini humo kutoa taarifa ya ndugu yao kutekwa na watu wasiojulikana Julai 18, mwaka huu baada ya kuwatumia ujumbe akiomba fedha.

Kamanda Msangi amesema kwamba mtuhumiwa Lema aliomba fedha zaidi ya shilingi milioni tano kwa familia yake kwa kutuma ujumbe kwenye simu ili aweze kuachiwa huru na watu waliomteka.

Aidha ameongeza kwamba mtuhumiwa Lema atafikishwa Mahakamani pindi uchunguzi wa tukio hilo utakapokamilika.

Mbali na hayo, Kamanda Msangi amewatahadharisha wananchi kuwa makini na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapobaini kuwepo kwa dalili zinazofanana na hizo.

Taarifa kwa Umma Kuhusu Kujiuzulu kwa Mbunge Julius Kalanga Laizer

NaneNane Simiyu: Naibu Waziri Wa Kilimo Atao Wito Kwa Wakulima Kutumia Zana Bora Za Kilimo, Kulima Kilimo Chenye Tija

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt. Mwanjelwa ametoa wito kwa wakulima kote nchini kulima kilimo chenye tija kwa kutumia zana bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kupata mavuno mengi na bora.

Dkt. Mwanjelwa ameyasema hayo Agosti Mosi, mara baada ya kukagua mabanda ya maonesho ya Kilimo katika Uwanja wa Nanenane wa Kanda ya Ziwa Mashariki uliopo Nyakabindi Bariadi, katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu.

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali kupitia Mfuko wa pembejeo unatoa mkopo wa pembejeo kwa riba ndogo sana, hivyo akatoa wito kwa wakulima wote nchini kwenda katika Halmashuri zao na kupata utaratibu wa kuomba mikopo hiyo ili waweze kupata mikopo itakayowawezesha kununua zana bora za kilimo.

“ Nitoe wito kwa wakulima wote nchini wajitahidi sana kwenda kwenye  kulima kilimo cha kisasa kilimo chenye tija, sisi kama Serikali tuna mfuko wetu wa pembejeo unaotoa mikopo kwa riba ndogo sana, hivyo wakulima wanaweza kuomba mikopo hiyo na kwenda kununua pembejeo bora za Kilimo” alisema Dkt. Mwanjelwa.

Katika hatua nyingine Dkt. Mwanjelwa amewataka maafisa ugani kuwafuata wakulima shambani badala ya kukaa ofisini, ili kuwapa elimu ya kilimo bora na kuwawezesha wakulima  kufikia lengo la kulima kilimo chenye tija.

Naye Baraka Itemu mkulima wa Mpunga kutoka Geita  ametoa wito kwa wakulima wenzake kote nchini kuachana na matumizi ya jembe la mkono na jembe la kukokotwa na ng’ombe kwa kuwa ni teknolojia iliyopitwa na wakati na haina tija katika uzalishaji.

“ Mimi ni mkulima wa mpunga binafsi matrekta yamenisaidia sana maana  naweza kulima eneo kubwa kwa muda mfupi na nikapata mazao mengi, natoa wito kwa wenzangu wanaotumia majembe ya mkono na ya kukokotwa na ng’ombe waache waende kwenye makampuni ya matrekta wakakope,  ili waweze kuzalisha mazao kwa wingi” alisema Baraka.

Nao wauzaji wa zana bora za kilimo waliofika katika maonesho ya Nanenane Bariadi mkoani Simiyu wamesema wako tayari kushirikiana na wakulima ili kuhakikisha wanapata zana hizo, huku wakibainisha kuwa wakulima wasiokuwa na uwezo wa kununua zana hizo kwa fedha taslimu wako tayari kuwakopesha.

Maonesho ya Nananane mwaka 2018 yanafanyika Kitaifa Mkoani Simiyu, ambapo yameanza leo na yatahitimishwa Agosti 08, 2018.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Naibu Waziri wa Áfya: Marufuku Kupiga Muziki Mahospitalini na Vituo Vya Afya

$
0
0
Na WAMJW - KAGERA
Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile amepiga marufuku kwa hospitali na vituo vyote vya kutolea huduma za Afya nchini kuonesha miziki katika maeneo yote yakutolea huduma na kuwataka kuweka jumbe zinazohusu Elimu Afya kwa umma pindi wanapongoja kupata huduma.

Ameyasema hayo jana wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika ukumbi wa halmashauri ya Muleba katika Mkoa wa Kagera.

"Ni marufuku kwa hospital zote kuonesha miziki katika maeneo yote ya utoaji huduma za afya" alisema Dkt Ndugulile.

Pia Dkt. Ndugulile amemwagiza Mganga mkuu wa Wilaya ya Ngara DKt. Revokatus Ndyekobora kuhamasisha wananchi Juu ya umuhimu wa kuudhuria kliniki kwa mama mjamzito walau mara nne ndani ya kipindi chá ujauzito wake na kuhakikisha wanajifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

"Tuongeze kasi katika kuhamasisha wakina mama wajawazito kuhudhuria kliniki, na kwenda kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya" alisema Dkt Ndugulile. 

Pia alisema kuwa Serikali inaendelea kuboresha sekta ya Áfya nchini kwa kutoa pesa ya ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za Afya na kuhamasisha ushirikishwaji wa wananchi katika ujenzi wa vituo hivyo (Forced account)

"Miundombinu tunaendelea kuboresha, Mkoa mzima tumeleta shilingi Bilion 5.9 kwaajili ya kuboresha vituo vya Áfya, viwili vikiwa katika Wilaya ya Ngara "alisema Dkt Ndugulile .

Kwa upande mwingine Dkt Ndugulile aliendelea kusema kuwa katika kuelekea kuboresha huduma za afya Serikali imeanzasha utaratibu wa kituo nyota kwa vituo vya Áfya, hospitali na Zahanati, na kutoa maagizo kwa Halmashauri zote nchini kuhakikisha Asilimia 80 ya vituo vyake vyote vya kutolea huduma za Afya havishuki chini ya nyota tatu (3)

"Serikali imeanzisha utaratibu wa kutoa madaraja ya Ubora kwa vituo vyote vya kutolea huduma za Afya , tunaanzia nyota sifuri kwa maana Kwamba kiwango chako chá Ubora ni chá chini sana Mpaka nyota 5 ambacho kiwango chako ni chá juu sana, tunataka Asilimia 80 ya Vituo vyao vyote katika kila halmashauri visipungue nyota tatu" Alisema Dkt Ndugulile.

Mbali na hayo Dkt Ndugulile amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Ngara. Luten.... Kuimarisha usimamizi katika ngazi zote za Wilaya ili kuweza kufikia Ubora wa huduma za afya kwa Asilimia 80 katika vituo vyake vyote.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ngara Dkt Revokatus Ndyekobora amesema kuwa lishe duni kwa watoto hasa walio chini ya Miaka 5 bado imekuwa tatizo na kusema kuwa wameweka mikakati thabiti yakuweza kupambana dhidi ya tatizo lá lishe duni. 

"Hali ya Lishe bado ni shida, ambapo tunaendelea kupambana nayo na tayari tumeweka mikakati thabiti yakuweza kupambana dhidi ya lishe duni " alisema

DKt. Revokatus Ndyekobora aliendelea kusema kuwa Wilaya ya Ngara ináupungufu wa watumishi kwa Asilimia 59.2 jambo linaloleta changamoto katika utoaji wa huduma za afya.

"Tuna upungufu wa watumishi kwa Asilimia 59.2 , Kwaiyo tunafanya kazi katika hali ya upungufu, tunamshukuru tumepata watumishi 36, lakini waliripoti 33, na juzi TAMISEMI waliondoa watumishi 2" alisema Dkt Revokatus Ndyekobora

Picha ya Gadner na Mwanae Yazua Gumzo Mitandaoni

$
0
0
Kuna picha  aliweka Gadner akiwa amerepost kutoka katika akaunti ya binti yake Karen ikiwa inaonyesha akiwa amemkumbatia mtoto wake  huku wakiwa wamelala kwenye kochi, na kwa jinsi wao walivyochukulia ilikuwa ni kama mapenzi ya baba na mtoto.

Lakini baada ya picha hiyo kwenda katika mitandao ya kijamii ilileta gumzo na kusemewa maneno mengi sana huku wadau na baadhi ya mashabiki wakisema kuwa hayo sio maadili ya kitanzania hasa kwa baba na binti yake.

Huku wengine wakimtuhumu sana gadner na kusema kuwa hawamuamini sana kutokana na ukweli kwamba amekuwa akitoka kimapezni na wasichana wenye umri kama wa binti yake , hivyo hiyo inaleta picha mbaya kwa mashabiki wanaomuona akiwa anafanya hivyo.

==>>Tazama baadhi ya maoni hapo chini

Wanaotorosha Madini ya Tanzanite Kukiona cha Moto

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Simanjiro
Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesema Serikali itaaendelea kusimamia  ulinzi  na kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite na watakaokwenda  kinyume na matakwa ya Sheria, kiama chao  kinakuja.

Waziri Kairuki aliyasema hayo tarehe 1 Agosti wakati wa ziara yake mkoani Manyara wakati alipotembelea migodi mbalimbali ya madini  ya tanzanite ndani ya ukuta wa Mirerani.

Alisema ziara hiyo ililenga kuangalia suala zima la ulinzi katika ukuta unaozunguka migodi  ya tanzanite, shughuli za uchimbaji madini  mengine zinavyofanyika na kuangalia namna uzalishaji wa madini ya tanzanite  unavyoendelea katika migodi husika.

Kairuki aliongeza kuwa, ziara hiyo ililenga  kuangalia namna Sheria ya Madini inavyotekelezwa, masuala ya Mikataba ya watumishi katika migodi  na namna migodi husika inavyolipa  kodi  mbalimbali za Serikali  yakiwemo masuala ya usalama sehemu za kazi na  wafanyakazi kwa ujumla.

“Utoroshaji madini hausaidii, fedha ni za haraka lakini zinawaadhibu watanzania walio wengi kwa kuwa, fedha hizo hizo zingeweza kutumika katika miradi mingine ya maendeleo. Hivyo, kila mtanzania awe mlizi wa mwenzake,” alisema Kairuki.

Awali, akizungumza  katika eneo Lemshuku kunakofanyika shughuli za uchimbaji wa madini ya Green Garnet, waziri Kairuki alisema kuwa, serikali inatambua mchango wa wachimbaji wadogo katika kuchangia pato la taifa kupitia shughuli za uchimbaji, hivyo akawaasa wachimbaji nchini kufuata Sheria, kanuni na taratibu ili kufanya shughuli halali ikiwemo kulipa kodi stahiki.

Akizungmzia suala la ruzuku kwa wachimbaji wadogo, waziri Kairuki alisema hivi sasa serikali imesitisha kwa muda utoaji rukuzu kwa kuwa inaandaa utaratibu wa wazi na endelevu ambao utawezesha wachimbaji  na serikali kunufaika kupitia rasilimali madini.

Aliongeza kuwa, serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa shughuli za uchimbaji mdogo wa madini ikiwemo kuhakikisha kuwa inawawezesha wachimbaji kutoka uchimbaji mdogo kwenda katika uchimbaji wa kati na kuongeza, “ tayari tumetenga maeneo zaidi ya 44 kwa ajili ya wachimbaji wadogo.

Akitolea ufafanuzi suala la vibarua katika migodi ya madini, aliwataka wale wote wanaofanya vibarua katika maeneo hayo kuhakikisha kuwa, wanapata mikataba yao kabla ya kuanza kazi.

Kuhusu masuala ya utoaji leseni za uchimbaji madini, Waziri Kairuki  alisema   ndani ya kipindi cha wiki 2 Tume ya Madini itaanza kutoa leseni kwa waombaji waliokidhi vigezo na kuongeza kuwa, kwa wanaomiliki leseni bila kuziendeleza watanyang’nywa na hivyo akawaasa wamiliki wasiokuwa na uwezo wa kuendeleza maeneo yao kutoa tarifa ili waweze kuunganishwa na wenye uwezo wa kuwekeza waweze kushirikiana.

Pia, waziri Kairuki alihamasisha kuhusu uwekezaji katika mashine za kukata na kunga’risha madini ili kuwezesha shughuli hizo kufanyika nchini na kuongeza kuwa, kupitia Sheria Mpya ya Madini  hairuhusu yoyote kusafirisha madini ghafi nje ya nchi.

Kwa upande wake,  Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mlabwa, alisema  ni lazima Sheria, Kanuni na taratibu zizingatiwe wakati wa utekelezaji shughuli za uchimbaji madini na kuongeza kuwa, serikali inatambua mchango wa kila aina ya madini yanayopatikana nchini.

Naye, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Tumaini Magesa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto alisema kuwa, shughuli za uchimbaji katika eneo la Mirerani zinaendelea na hivyo serikali itaendelea kuboresha ulinzi na kuhakikisha kwamba unaimalika.

Rais Magufuli Mgeni Rasmi mkutano wa 34 wa Jumuiya ya Serikali ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat)

$
0
0
Rais John Magufuli anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa 34 wa Jumuiya ya Serikali ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat). Mkutano huo utafanyika Septemba 24 hadi 28 mwaka huu na kushirikisha wajumbe 500 wakiwemo wataalam na wageni waalikwa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat) ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam amesema hayo mjini Dodoma.

Kaulimbiu ya mkutano huo ni Umuhimu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kutoa Huduma na Ushiriki wa wananchi kupitia fursa na vikwazo kuelekea uchumi wa viwanda.

Amesema mkutano huo unalenga kubainisha mamlaka za serikali za mitaa zipo karibu zaidi na wananchi na zinatoa huduma na kubainisha umuhimu wa wananchi katika kubuni na kusimamia miradi ya maendeleo na kuibua fursa za uwekezaji viwanda kufikia uchumi wa kati.

Amesema agenda zitakazojadiliwa pamoja na mambo mengine kujadili taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa shughuli za jumuiya, taarifa za fedha na kupitisha bajeti ya mwaka 2018/2019.

Makamu Mwenyekiti wa Alat na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa, Steven Mhapa aliitaka Alat Mkoa kufanya mikutano yao mwishoni mwa mwezi huu na taarifa za vikao hivyo kupelekwa kwa Katibu wa Alat ili zijumuishwe kwenye taarifa ya Jumuiya.

Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe alisema mkutano huo utakuwa na usalama akitaka wananchi kutumia fursa hiyo. Mukadam alisema michango ya wanachama haikuwa  vizuri kwa sasa uongozi wake umejipanga kuhakikisha wanachama wake wanalipa madeni.

" Tumepanga kuweka mazingira ya kuhakikisha wanachama wanatoa michango na hii si kwa ajili ya mkutano huo pekee bali kuhakikisha wanajenga jengo la kitega uchumi jijini Dodoma kwa ajili ya wana Alat," amesema na kuongeza mkutano huo utagharimu sh milioni 300.

Breaking News: Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania anazungumza na waandishi wa Habari

$
0
0
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania anazungumza na waandishi wa Habari 

==>>Msikilize hapo chini

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

$
0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Maandalizi Ya Kupumzisha Mwili Wa Marehemu Shadrack Sagati - Afisa Habari Mwandamizi

Benki Wa Wanawake (TWB) na Benki ya TPB Zaunganishwa baada ya TWB kushindwa kutimiza masharti ya kuwa na mtaji wa kutosha

$
0
0
Benki ya Wanawake (TWB) imeungana na Benki ya TPB baada ya benki hiyo kushindwa kutimiza masharti ya kuwa na mtaji wa kutosha kujiendesha.

Kutokana na hatua hiyo, wateja, wafanyakazi, mali na madeni yote ya TWB yataunganishwa na Benki ya TPB kuanzia leo.

Hayo yamesemwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Agosti 2, kuhusu hatua mbalimbali benki hiyo ilizochukua kwa baadhi ya benki ambazo zimekiuka masharti ya Sheria ya mabenki na taasisi za fedha.

Amesema Januari 4, mwaka huu iliziongezea  muda wa miezi sita benki nne za Tandahimba Community Bank (Tacoba), Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) na Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) hadi Juni 30, mwaka huu ili kufanikisha kiwango cha mtaji kinachohitajika na sheria za mabenki  na kanuni zake cha kiwango cha chini cha mtaji wa Sh bilioni mbili kwa benki.

Aidha, amesema hata baada ya muda huo kuisha na kuongezewa mwezi mmoja hadi Julai 31, mwaka huu ili kukamilisha benki mtaji, benki mbili zilifanikiwa huku TWB ikishindwa.

Ameanisha Benki ya Tacoba na KCBL kwa sasa zimeongeza mtaji na kukidhi kiwango knachohitajika kisheria na zitendelea na shughuli zake kwa mujibu wa sheria kama kawaida.

“Kutokana na hali hiyo, Wanahisa wa TWB na TPB Bank PLC, wameamua kuunganisha benki hizo ili kuboresha ufanisi na utendaji wa benki hizo, hivyo kutokana na muungano huo kutakuwa na benki moja ambayo itaendelea kuitwa benki ya TPB Bank PLC.

“Benki Kuu imeridhia uuganishaji wa benki hizo kuanzia Agosti 3, mwaka huu ambapo itaendelea kuwa na mtaji wa kutosha kama sheria ya mabenki inayotaka.

“Hivyo wateja, wafanyakazi, mali na madeni yote ya TWB yataunganishwa na TPB, muungano huo utaifanya muungano mpya kuwa imara zaidi na kuwa na mtaji wa kutosha kama inavyotakiwa kisheria, chini ya kifungu cha 17, cha sheria ya mabenki na taasisi za kifedha ya mwaka 2006.

“BoT inawaomba wateja wa TWB kuwa watulivu katika kipindi hiki cha mpito cha uunganishaji wa benki hizi,” amesema Profesa Luoga.

Breaking News: Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Yachukua Usimamizi wa Benki M Baada ya Kufulia na Kushindwa Kujiendesha

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesimamisha Bodi ya Wakurugenzi na uongozi wa Bank M na kuchukua usimamizi wa benki hiyo kukosa fedha za kujiendesha.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Agosti 2, Gavana wa BoT, Profesa Florens Luoga amesema BoT imechukua hatua hiyo kulinda maslahi ya wateja wakopeshaji wote wanaohusika na shughulia ambazo azilikuwa zikiendeshwa na Benki M.

“Kwa mamlaka iliyopewa BoT chini ya sheria namba 56, (1) (g,) (3) cha sheria ya benki ya mwaka 2006, BoT imeamua kuchukua usimamizi wa Benki M kuanzia leo.

“Uamuzi huu umechululiwa baada ya kubainika benki hiyo ina upungufu mkubwa wa ukwasi kinyume na matakwa ya sheria ya kibenki na kanuni zake unaohatarisha usalama wa sekta za kifedha ambao kuendelea kutoa huduma kwa benki hiyo utahatarisha usalama wa amana za wateja wake.

“Kutokana na uamuzi huo, BoT imesimaisha bodi ya wakurugenzi na uongozi wa Banki M kuanzia leo, hivyo kutokana na uamuzi huo imemteua Meneja Msimamzi ambaye atakuwa na shughuli ya kusimamia benki hiyo kwa kipindi ambacho itakuwa chini usimamizi wa BoT,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Profesa Luoga amesema katika muda usiozidi siku 90 kuanzia sasa shuguli za utoaji wa huduma za kibenki katika benki hiyo, zitasimama kuipa nafasi BoT kutathimini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa suala hilo.

Jenerali wa Magereza nchini Phaustine Kasike Awaasa Maofisa wa Jeshi la Magereza Kuzingatia Maadili ya Kazi

$
0
0
Na Lucas Mboje, Magereza;
KAMISHNA Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike amewataka Maofisa na askari wa Jeshi hilo kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume na maadili ya kazi yao, badala yake wazingatie kanuni, miiko na maadili ya uendeshaji wa Jeshi la Magereza.
 
Kamishna Jenerali Kasike ametoa rai hiyo jana Agosti 1, 2018 wakati akiongea na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Arusha alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo.
 
Alisema kuna upungufu katika uzingatiaji wa maadili kwa baadhi ya Maofisa na askari hususani mahusiano mabaya ya askari na wafungwa ikiwemo tabia za askari kuingiza simu magerezani.
 
Amesema hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa kwa maofisa na askari watakaobainika kufanya vitendo hivyo ikiwemo kuwajibishwa na kufukuzwa kazi.
 
“Mnajua kabsaa gharama za kujihusisha na tabia hizi za mahusiano mabaya na wafungwa nawaasa mzingatie maadili mnapotekeleza majukumu yenu ya kazi”. Alisisitiza Kamishna Jenerali Kasike.
 
Kuhusu agizo la Rais Dkt.  John Pombe Magufuli kuhusu kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa Kamishna Jenerali Kasike amesena kwa sasa Jeshi hilo linakamilisha mpango kazi wake utakaowezesha utekelezaji wa agizo hilo.
 
Amewataka askari wote nchini kujiandaa kisaikolojia kutekeleza agizo hilo bila kisingizio chochote kwani Jeshi la Magereza linazo rasilimali za kutosha kutekeleza agizo hilo.
 
“Tunayo ardhi yakutosha, nguvu kazi ya wafungwa ipo hivyo agizo la Rais na Amiri Jeshi Mkuu lazima litekelezwe bila kisingizio chochote”. Alisema Jenerali Kasike.
 
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Arusha ambapo lengo la ziara hiyo ni kukagua utendaji kazi pamoja na kuzungumza na Maofisa na askari wa Jeshi hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images