Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yatangaza Kiama kwa Wamiliki wa Leseni za Uchimbaji Madini na Vitalu Ambavyo Haviendelezwi

0
0
Serikali imetangaza kunyanganya leseni za uchimbaji madini ambazo hazitumiki kwa muda mrefu pamoja na vitalu ambavyo vimehodhiwa na wachimbaji bila kuendelezwa wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Pia imewataka wachimbaji wote wa madini ya dhahabu wanaofanya shughuli zao kwenye vyanzo vya maji na kuharibu mazingira kuondoka mara moja.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo jana Jumatatu Julai 30 wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Chunya ikiwa ni siku yake ya siku kufanya ziara kutembelea wilaya zote za Mkoa wa Mbeya.

“Ndugu zangu tumesikia hapa kwamba kulikuwa na shughuli za uchimbaji madini kwenye vyanzo vya maji na kama mnavyojua uchimbaji madini unatumia madawa kadhaa ambayo wakisafisha yanaingia ndani ya mto.

“Sasa vile vimelea vikiingia kwenye maji yale sio rahisi kusafishwa vikaondolewa  na Chunya vyanzo vya maji ni vichache na ndio maana tumefunga migodi yote ambayo imekuwa ikifanya shughuli zake kwenye vyanzo vile. Nasisitiza tena shughuli zozote zinazofanyika kule mtoni za kuharibu maji, za kuharibu vyanzo vya maji zisimame mara moja na waondoke, hatutawavumilia hawa watu,” alisema Samia.

Awali, Waziri wa Madini, Angela Kairuki  amesema  kuna watu wamepewa leseni za uchimbaji wa madini lakini hawaziendelezi wala vitalu walivyopewa pia hawaviendelezi watazinyang’anya leseni hizo na kuwapatia wengine wenye uhajitaji.

Alisema hilo linakuja baada ya malalamiko ya wachimbaji wadogo ambao hawana maeneo ya kuchimba madini lakini maeneo makubwa yamehidhiwa na wachimbaji wakubwa ambao hawayaendelezi.

“Mheshimiwa Makamu wa Rais, wapo watu wamepewa leseni za uchimbaji madini lakini lakini hawazitumii leseni hizo, hawajaendeleza maeneo ya uchimbaji ambayo wamepewa na kwa kuwa wilaya hii (Chunya) imejikita zaidi kwenye uchimbaji madini niseme katika hadhara hii tunawapa onyo la mwisho wale wote tuliowapa leseni lakini hawaziendelezi tutazifuta na kuwapa watu wengine wenye nia ya kuwekeza.”

Breaking News: Pigo Tena CHADEMA.....Mbunge wake wa Monduli Ajiuzulu na Kuhamia CCM

0
0
Julius Kalanga aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli kupitia Chadema amejiuzulu nafasi zake zote ikiwemo Ubunge na kuhamia CCM usiku wa kuamkia leo.

Katika sababu mojawapo ya kujiuzulu aliyoieleza,amesema ni Kuunga mkono juhudi kubwa za kuleta maendeleo zinazofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli.

"Siwezi kuwa sehemu ya kukwamisha maendeleo ya wananchi wa Monduli kwa kupinga kila kitu. Ubunge si tatizo kwangu naweza kuwa mkulima au mfugaji ila si kuwa kikwazo," amesema Kalanga

Hapo pichani alikuwa akitambulishwa rasmi usiku na Msemaji wa chama cha CCM,Ndugu Pole.

Kufuatia uamuzi huo jimbo la Monduli liko wazi

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Serikali Yasema Haina Taarifa ya Gazeti la Mwanahalisi Kushinda Kesi Mahakamani

0
0
Wakati mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya HaliHalisi, Saed Kubenea amesema Jumatano ijayo atachapisha nakala ya kwanza ya gazeti la Mwanahalisi baada ya kushinda kesi katika Mahakama Kuu, Serikali imesema haina taarifa na ujio huo.

Kubenea aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba, gazeti hilo limeshinda kesi iliyofunguliwa mwaka 2017 katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na uamuzi umefanyika hukumu ilitolewa Jumanne ya wiki iliyopita.

“Kama kampuni Jumatano ya wiki ijayo, tutachapisha nakala ya gazeti hilo kwa mara ya kwanza tangu lifungiwe,” alisema.

Alisema taratibu za kuomba leseni zinaendelea lakini gazeti kwa mujibu wa sheria halihitaji kusajiliwa tena badala yake, Mahakama imeamuru lifunguliwe na liendelee kuchapishwa.

Kubenea ambaye pia ni mbunge wa Ubungo (Chadema), alisema Mahakama imesema mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) hana mamlaka yoyote siyo tu kuomba watoe maelezo ni kwa nini walichapisha habari hiyo, bali hata kuwaomba wapeleke utetezi wao.

Wakili wa Kampuni hiyo, Nashoni Nkungu, alisema uamuzi huo ulitolewa Julai 24, mwaka huu na Jaji Beatrice Mutungi.

“Mahakama katika uamuzi wake ilisema amri zilizotolewa wakati wa kulifungia gazeti ni batili, hazikufuata misingi ya kisheria na hakukuwa na haki ya usikilizwaji kwa upande wa mlalamikaji.

“Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo hana mamlaka yoyote, si tu ya kuwaomba watoe maelezo juu ya habari husika, hata ya kuwaomba walete utetezi wao.

“Na mahakama ilisema hilo si jukumu mojawapo katika yale majukumu ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo kama yalivyoainishwa kwenye Sheria ya Huduma za Habari,” alisema Nkungu.

Alisema hata waziri hana mamlaka ya kulifungia gazeti kama alivyofanya kwa kupitia kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo.

“Mamlaka pekee ambayo anayo ni kuondoa ‘content’ ya habari ambayo inaonekana inahatarisha usalama wa taifa, kimsingi hata waziri hana mamlaka ya kufungia gazeti.

“Mahakama ilisikitishwa na kutotiliwa mkazo kwa amri ambazo zilitolewa mahakamani, kwani kulikuwa na amri zingine zilizotolewa, lakini mkurugenzi aliendelea kufanya kinyume, amekanywa kutoendelea kwenda kinyume na amri ambazo mahakama imekwishazitoa.

“Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo hana mamlaka yoyote si tu ya kuwaomba kama alivyofanya katika kesi hii, hana mamlaka yoyote ya kuandika barua kwa chombo cha habari na kukiambia kijieleze,” alisema.

Hata hivyo, mkurugenzi wa Maelezo ambaye pia ni msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas alisema wao kama Serikali hawana taarifa ya hukumu hiyo.

Alisema mbali na kutokuwa na taarifa ya kushinda kesi hiyo, kuna taratibu chini ya sheria ya huduma za habari zinazotakiwa kufuatwa kabla gazeti halijachapishwa.

 “Sheria hiyo imeanza kutumika Desemba 31 mwaka 2016 ambayo inaeleza kwa namna yoyote ile hakuna gazeti litakaloruhusiwa kuchapishwa bila kuwa na leseni period (basi), ”alisema Dk Abbas.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Uchapishaji ya Hali Halisi, Saed Kubenea, alisema wanakusudia kuwashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura, kwa madai kuwa wameisababishia hasara kampuni hiyo ya Sh bilioni 2.2.

Alisema uamuzi huo wa mahakama umewasaidia kuonekana mbele ya jamii kwamba hawakuwa na makosa na kudai kuna watu wana hila na gazeti lao lisionekane mtaani.

“Mahakama imethibitisha hatukuwa na hatia, hivyo tunapanga kudai fidia kwa sababu tumepata hasara zaidi ya Sh bilioni 2, tumepoteza wafanyakazi, matangazo na wadau mbalimbali tuliokuwa tukishirikiana nao.

“Tutamshtaki AG na aliyekuwa Naibu Waziri (Wambura) tutamshtaki binafsi ili iwe onyo kwa viongozi wengine wanaotumia madaraka yao vibaya,” alisema Kubenea.

Mkurugenzi huyo alisema wanatarajia gazeti hilo litaanza kuchapishwa wiki ijayo na kuwataka waandishi wa habari na vyombo vya habari wasiogope kudai haki kwani mahakama bado ziko huru na zinatenda haki.

“Mwaka 2012 tulifungiwa kwa muda usiojulikana tukaenda mahakamani gazeti likarejeshwa Septemba 2015, twendeni mahakamani tukajenge hoja.

“Tunaamini mahakama zetu bado ziko huru na zinaweza zikatenda haki, isipokuwa kuna baadhi ya watu ndani ya Serikali wana kiburi cha kutotii maamuzi ya mahakama, pengine kwa masilahi yao binafsi ama kwa kutumwa,” alisema Kubenea.

Kauli ya Mbowe Baada yaabunge wake CHADEMA Kuzidi Kuhamia CCM

0
0
Joto la kisiasa likiwa limepamba moto kwa wanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kukihama chama chao na kukimbilia CCM, Mwenyekiti Freeman Mbowe amesema hatishiki juu ya hilo bali anaona kama wanazidi kukiimarisha na kuwa na nguvu zaidi.

Kauli hiyo ya Mbowe imekuja kufuatia matukio ya Wabunge wa ndani ya CHADEMA pamoja na madiwani kujivua nyadhifa zao katika nyakati tofauti tofauti huku baadhi yao wakidai wanaelekea chama tawala (CCM) kwa lengo la kumuunga mkono Rais Magufuli katika utendaji wake wa kazi na wengine wakisema hawaridhishwi na utendaji wa chama hicho kwa madai kuna sera ya ubaguzi na kutokuwepo suala la uchaguzi la viongozi ndani ya chama hicho.

"Wale wanaokimbilia vyama vingine wanakiimarisha zaidi chama chetu kwa sababu kina tupa fursa ya kubaki na viongozi na wanachama wenye uchungu na nia ya dhati ya kukijenga chama chao. Wanaofika bei kwa ahadi ya fedha au vyeo waondoke mapema na nina wahakikishia CHADEMA itaendelea kuwa taasisi imara zaidi kuliko ilivyo sasa", amesema Mbowe.

Ndani ya siku tatu, Wabunge wawili wamejiuzulu kutoka CHADEMA wakielekea CCM ambapo jana Julai 30, 2018 aliyekuwa Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga alitangaza kurudi CCM alipokuwa awali, Julai 28, 2018 naye aliyekuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara alitangaza kukihama chama hicho.

Kalanga anakuwa Mbunge wa tatu CHADEMA, kujivua ubunge ambapo Mbunge wa kwanza alikuwa Dkt. Godwin Oloyce Mollel ambaye Disemba 14, 2017 alijivua ubunge wake kwa kile alichokieleza ni kuenda kuunga mkono kazi za Rais Magufuli.

Kwa kipindi cha takribani miaka mitatu tayari wabunge watano wameshajivua nyadhifa zao, ambapo dimba lilifunguliwa na Lazaro Nyalandu kutoka CCM kwenda CHADEMA, Maulid Mtulia CUF kuelekea CCM, Godwin Mollel CHADEMA kwenda CCM, Waitara kutoka CHADEMA kurudi CCM na sasa Julius Kalanga kutoka CHADEMA kurudi CCM.

Rais Magufuli Ataka Nchi zenye Uhaba wa Chakula Zije Zinunue Nchini

0
0
Rais John Magufuli ametoa wito kwa mabalozi ambao nchi zao zina uhaba wa chakula kuja kununua nchini ili wakulima wapate masoko.

Amesema hakuna haja ya kwenda kununua chakula cha wakimbizi Ulaya wakati kinapatikana Tanzania.

Rais alisema Serikali inatafuta soko la chakula ili kutowavunja moyo wakulima ambao katika msimu huu wamezalisha ziada huku nchi ikiwa na chakula cha kutosha.

Alisema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi hati za utambulisho za viwanja kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yenye makazi yake nchini kwa ajili ya kujenga ofisi na makazi jijini Dodoma.

Jumla ya hati za utambuzi 67 zilikabidhiwa, kati ya hizo 62 ni za balozi za nchi na tano ni za mashirika ya kimataifa.

“Kama Somalia wanahitaji chakula waje wanunue hapa, kama South Sudan (Sudan Kusini) wanahitaji waje wanunue hapa, kama DRC wanahitaji waje kununua hapa,” alisema.

Rais alisema, “Kama kuna chakula kinatakiwa kupelekwa kwa refugees (wakimbizi), kwa nini mkanunue chakula kutoka nje huko Ulaya na kukisafirisha kwa gharama kubwa, si chukua hapa tu Songea.”

Rais Magufuli alisema alikutana na mkurugenzi mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), David Beasley ambaye alijionea ziada ya chakula iliyopo nchini.

Lugumi Ajisalimisha Kwa Kangi Lugola

0
0
Mfanyabiashara Said Lugumi na mmiliki wa Kampuni ya Lugumi Enterpreises Limited, amejisalimisha polisi kuitikia wito wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola aliyemtaka kujisalimisha kwake ndani ya siku 10.

Lugumi aliwasili katika Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi leo asubuhi Julai 31, ikiwa ni siku 10 tangu Waziri Lugola atoe agizo hilo Julai 21, mwaka huu.

Mfanyabiashara huyo aliongozwa na Ofisa wa Polisi kuelekea ofisini kwa Waziri Lugola baada ya kutoka Makao Makao Makuu ya Polisi Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai.

Julai 21, mwaka huu Lugola alitoa agizo akimtaka mfanyabiashara huyo kujisalimisha ili azungumze naye kuhusu kazi aliyopewa lakini hata hivyo hakuimaliza.

Kampuni ya Lugumi ilitekeleza mradi wa kufunga mfumo wa utambuzi wa alama za vidole katika vituo vya polisi uliogharimu Sh bilioni 37.

LIVE: Rais wa TLS Bi. Fatma Karume Anaongea na Waandishi wa Habari Muda Huu....Msikilize Hapo

0
0
Bi. Fatma Karume Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) anazungumza na Waandishi wa habari katika Ofisi za TLS, Dar es salaam...Msikilize Hapo chini

Kauli ya Lowassa Baada ya Mbunge wa CHADEMA Jimboni Kwake Kujiuzulu na Kuhamia CCM

0
0
Muda mchache baada ya Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga (Chadema), kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amewataka wananchi jimboni humo wasife moyo na kuwa na utulivu.

Lowassa ambaye pia amewahi kuwa Mbunge wa Monduli kabla ya Kalanga, amesema amesikia taarifa za kujiuzulu kwa mbunge huyo na kwamba kwa sababu zozote ambazo amezitoa ni haki yake kikatiba.

“Najua Wana-Monduli wote nikiwamo mimi uamuzi huo umetuhuzunisha na kutuumiza, lakini nawaomba msife moyo hata dakika moja zaidi kitendo hicho kizidi kutupa nguvu, ari, hamasa na mori zaidi ya kuendeleza mapambano ya kuitafuta demokrasia na mabadiliko ya kweli.

“Hakuna jipya katika hili, ni kawaida kwa wanasiasa duniani kuhama vyama vyao na kubadilishana vijiti. Monduli imetupa heshima kwenye harakati za mabadiliko, naomba msife moyo,” amenukuliwa Lowassa ambaye pia ni Mjumbe Kamati Kuu ya Chadema.

Alichokisema Lowassa Kuhusu Tetesi za Mtoto Wake Kukugombea Umbunge Jimbo la Monduli

0
0
Baada ya kuwepo kwa mashinikizo mbalimbali yakimtaka Freddy Lowassa kijana wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Edward Lowassa, kugombea nafasi ya Ubunge kwenye jimbo la Monduli. Mh. Lowassa amesema bado hajawa na maoni juu ya mashinikizo hayo kwani hayajamfikia.

Mh. Lowassa ameyasema hayo wakati  alipohojiwa kama yupo tayari kumruhusu kijana wake Freddy Lowassa kuchukua dhamana ya kuiongoza Monduli baada ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Julius Kalanga kujiuzulu nafasi yake .

Mh. Lowassa amesema; "Mimi bado taarifa hizo za kumhusu Freddy sina, sijazipata. Ngoja kwanza nizifuatilie na baada ya hapo ninaweza kutoa tamko. Siwezi kuzungumzia kitu kwa sababu bado mimi hazijanifikia,".

Tangu kusambaa kwa taarifa za Mbunge Kalanga kujiuzulu nafasi yake na kuhamia CCM jana usiku, mitandaoni kumekuwa na mashinikizo mbalimbali ambayo yakimtaka Freddy Lowassa  kuwa mwakilishi wa wanaMonduli huku wakidai kwamba Kalanga amewaambisha wamasai.

Mmmojawapo ya watu hao ni Mbunge wa Sombetini Arusha, Ally Binamu Bananga yeye amedai kwamba yeye atakishawishi chama kimpitishe Freddy kugombea.

"Huyu ndio wa kwenda kuzima kiherehere cha Kalanga, uchaguzi mdogo ukiitishwa nitakishawishi chama changu twende na FREDDY LOWASSA, kampeni meneja nakamata ungo mwenyewe mzee baba, mkuu wa ngome Godbless Lema, huku mzee Lowassa, kule mama Lowassa" , ameandika Bananga  ujumbe huo.

Jimbo la Monduli limekuwa wazi kuanzia jana usiku baada ya Mbunge aliyechaguliwa 2015 (CHADEMA), Julius Kalanga kujiunga na CCM kwa kile alichoeleza kuwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli na kudai kuwa ameondoka CHADEMA kwasababu ya siasa za chuki na uhasama.

Lugola Amtaka Zitto Kabwe Ajisalimishe Polisi Haraka Sana

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amemtaka mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kujisalimisha kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi kwa maelezo kuwa ametoa kauli za uchochezi.

Lugola ametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 31, 2018 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Amesema Zitto ametoa kauli za uchochezi na kuwatukana viongozi wa Serikali wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika jimbo la Kilwa Kusini.

Katika mkutano huo Zitto alialikwa na mbunge wa jimbo hilo, Seleman Bungara maarufu Bwege.

“Kosa jingine la Zitto ni kwenda kufanya mkutano eneo ambalo sio la kwake kwa mujibu wa taratibu. Nampa siku mbili ajisalimishe kwa RPC (Kamanda wa polisi mkoa wa Lindi),” amesema Lugola.

“Akikaidi nitamuagiza IGP (Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini-Simon Sirro) amkamate popote alipo. Nilishasema na nitaendelea kusema katika uchaguzi huu na zijazo watu wanaotukana  viongozi hawatabaki salama.”

Mbowe Kapigwa Onyo la Mwisho na Mahakama.....Akirudia Dhamana Yake Itafutwa

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema itamfutia dhamana Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe endapo akishindwa kufika mahakamani bila sababu za msingi.

Hayo yamesemwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya Wakili wa serikali, Faraja Nchimbi kuhoji kwanini Mbowe hajafika mahakamani hapo mara mbili mfululizo.

Nchimbi ameeleza kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali lakini mshtakiwa wa kwanza Mbowe hayupo.

“Tunaomba mahakama itoe onyo kwa washtakiwa kuhusu kutofika mahakamani,”.

Baada ya kueleza hayo alisimama mdhamini wa Mbowe na kueleza kuwa amekwama kwenye foleni wakati akija mahakamani.

Naye wakili wa utetezi, Hekima Mwesipu amedai kuwa Mbowe amekwama katika foleni kwa sababu ya msafara wa kiongozi aliyekuwa akipita.

“Mdhamini amesema Mbowe amekwama katika foleni, hivyo angepata dharura nyingine angesema, “ Mwesipu.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mashauri amesema anatoa onyo la mwisho kwa Mbowe na endapo akirudia atamfutia dhamana.

“Mdhamini ukamwambie kuwa tutamfutia dhamana, asikutumie wewe kama chambo,” amesema Hakimu Mashauri

Baada ya kueleza hayo, ameahirisha kesi hiyo hadi August 2,2018 kwa ajili ya usikilizwaji wa awali.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk.Vincent Mashinji na Manaibu wake, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Wengine ni Mchungaji Peter Msigwa ambaye ni mbunge wa Iringa Mjini, Esther Matiko (mweka hazina wa BAWACHA), Halima Mdee (mbunge, Kawe), John Heche (mbunge, Tarime Vijijini), Ester Bulaya (mbunge, Bunda).Kwa pamoja, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 13, yakiwamo ya kufanya mikusanyiko na maandamano yasiyo halali.

Wanadaiwa kutenda makosa hayo February 16, 2018 katika Barabara ya Kawawa, eneo la Kinondoni Mkwajuni na kusababisha vurugu zilizosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.

Waziri wa Afya: ‘likizo Ya Uzazi Kwa Wanaume Si Ya Kunywa Pombe’

0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka wanaume kutoitumia likizo ya siku tano ya uzazi kwa wanaume kwenda kunywa pombe.

Aidha, amesema ataifuta likizo hiyo kwa wanaume endapo atajiridhisha haina manufaa na inatumika ndivyo sivyo.

Akizungumza kuhusu Wiki ya Unyonyeshaji itakayoanza kesho hadi Agosti 8, mwaka huu, Waziri Ummy amesema likizo hiyo ni kwa ajili ya kumsaidia mama anapokuwa amejifungua na si vinginevyo.

“Likizo ya uzazi kwa wanaume si ya kwenda kunywa pombe, lakini wapo wanaume wanachukua likizo na nyumbani hawaonekani, nitafanya utafiti kuangalia iwapo ina manufaa kama hakuna tutaifuta,” amesema.

Serikali Kukuza Utalii Kupitia Mchezo Wa Golf

0
0
Na Hamza Temba-WMU
........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amesema Serikali itatumia fursa ya ujio wa Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus kutoka nchini Marekeni kubuni viwanja vya mchezo huo karibu na maeneo ya vivutio vya utalii nchini ili kuvutia watalii wengi wa kimataifa na hivyo kukuza pato la sekta hiyo.

Dk. Kigwangalla amesema hayo jana mara baada ya kumuaga mchezaji huyo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam alipokuwa akirudi nchini kwao baada ya kumaliza ziara yake ya siku kumi yeye na familia yake katika vivutio mbali mbali vya utalii hapa nchini.

“Tutatumia utaalamu na uzoefu wake kwenye mchezo wa Golf kwa kumtaka aje na kampuni yake atusaidie kutengeneza plan (mpango) ya kujenga viwanja vya golf.

“Amedesign viwanja zaidi ya 300 kwenye nchi zaidi ya 50 duniani na nchi hizo zimefaidika, amesema katika project zake zaidi ya asilimia 90 zinafanya vizuri pamoja na kwamba ni uwekezaji wa gharama kubwa bado imelipa kwa kiasi kikubwa na hakuna hata kiwanja kimoja kimepata hasara na vimekuwa vinasaidia kukuza utalii katika nchi hizo.

“Lengo letu ni kutengeneza ukanda maalum wa viwanja vya golf ambao utakuwa na viwango vya kimataifa na utavutia wacheza Golf kutoka nchi mbalimbali duniani, kwahiyo hii ni aina nyingine ya utalii wa watu wenye uwezo ambao wataleta pesa nyingi kwa wakati mmoja.

 “Tutaendelea kuwa na mawasiliano nae na kampuni yake ili tuweze kuona anawezaje kutusaidia na sisi walau tuwe na hiyo plan (mpango) lakini pia tukapata wawekezaji wakaja kuwekeza kwenye viwanja vya golf vitakavyojengwa karibu na fukwe, karibu na mito au hifadhi za Taifa ambapo tutavutia sio tu watalii ambao wanaokuja  kufanya utalii wa wanyamapori au beach lakini tutavutia watalii wanaokuja mahsusi kwa kwa ajili ya utalii wa golf” alisema Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo Dk. Kigwangalla amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kujali maslahi ya wageni mashuhuri wanaokuja nchini ikiwemo ya usiri wa safari zao na kwamba atakayetaka aje kimya kimya na aondoke kimya kimya atapata heshma hiyo na atakayekubali kuwa wazi naye pia atapata heshma hiyo.

Kwa upande wake Jack Nicklaus alisema amefurahishwa sana na vivutio mbalimbali vya utalii alivyovishuhudia katika safari yake hapa nchini pamoja na ushirikiano na ukarimu mzuri kutoka kwa watanzania na ameahidi kuwa balozi wa utalii wa Tanzania huo aendako.

Jack Nicklaus ndiye mchezaji mwenye tuzo nyingi kuliko wachezaji wengine wa mchezo huo hapa duniani kwa sasa, ameweka rekodi ya kushinda mashindano ya kulipwa 117 na mashindano makubwa 18 (major champions).

Serikali kumnyang’anya Mohammed Enterprises mashamba.

0
0
Na. Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula amesema serikali imekusudia kuchukua baadhi ya mashamba yanayomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises na kuwapa wananchi kwa kuwa wameshindwa kutimiza masharti ya endelezaji wake.

Mhe. Mabulla amesema hayo baada ya kufanya ziara ya ukaguzi wa mashamba katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amegundua kampuni ya Mohammed Enterprises inamiliki maeneo makubwa sana kwa zaidi ya hekta 9,418 sawa na hekari 20,779 ambayo wamechukulia mkopo kwa ajili ya kupanda mkonge, kitu ambacho hakijafanyika kwa asilimia kubwa.

“Hii kampuni ya Mohammed Enterprises imetupa taarifa ambazo si za kweli kwamba wameendeleza maeneo yao wanayoyamiliki kwa asilimia 83, mimi nimefika katika mashamba yote 14 wanayoyamiliki na nimeona ni eneo kubwa sana ambalo limebaki pori na halijapandwa mkonge tangu wakabidhiwe mwaka 2000 takribani miaka 17 sasa wakati wananchi wa Korogwe wanakosa maeneo ya kulima, kuishi na kufugia” amesema Mhe. Mabula.

“Kwa sasa Wizara yangu imejiridhisha kwamba kuna haja ya kugawa maeneo yanayomilikiwa na Mohammed Enterprises ambayo hayajendelezwa kwa kupandwa mkonge ili wapewe wananchi wa Korogwe ambao wana uhaba wa ardhi kwa muda mrefu kutokana na maeneo makubwa kumilikiwa na watu wachache”. Mhe. Mabula ameongeza.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabulla amefanya ziara ya ukaguzi wa mashamba yote 14 yanayomilikiwa na Kampuni ya Mohammed Enterprises na kugundua kuwa amepanda mkonge eneo dogo sana na sehemu kubwa ni mapori tofauti na taarifa aliyopewa na kampuni hiyo.

Waziri pia amesema mashamba hayo yametumika kuchukua mikopo benki lakini mikopo hiyo haijatumika kuendeleza mashamba hayo kitu ambacho kinafanya wananchi wayahitaji maeneo hayo lakini wanashindwa kuyatumia kwa kuwa yanamilikiwa na kampuni ya Mohammed Enterprises.

Akijatetea mbele ya Naibu Waziri wa Ardhi Meneja anayesimamia Mashamba yote ya mkonge ya kampuni ya Mohammed Enterprises ndugu Newalo Nyari mesema kwamba si kweli kwamba hawajaendeleza maeneo hayo bali wameendeleza na wamepanda mkonge baadhi ya maeneo na mengine wameyaacha mapori ili kuhifadhi misitu na mengine wanawaachia wananchi waweze kupanda mazao yao ikiwa ni ushirikiano wa kijirani.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Handeni aliyekuwa akikaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Godwine Gondwe ambaye ameonesha kukasirishwa na maneno ya meneja huyo kwamba wameendeleza mashamba hayo wakati yeye mwenyewe ameshuhudia kwa macho yake mashamba yote 14 na kuona hali halisi ya mapori ambayo hayaendelezwa.

Baadhi ya wananchi wa Korogwe wameonesha kufurahishwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuipunguzia umiliki wa baadhi ya maeneo yanayomilikiwa na kampuni ya Mohammed Enterprises ambayo watapewa wananchi hao ili waweze kufanya shughuli zao za maendeleo.

Hata hivyo kwa mujibu wa sheria ya ubatilishaji umiliki wa mashamba ni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiye mwenye dhamana ya kumyanga’anya mmiliki wa ardhi au mashamba baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri wa Ardhi.

Alichokisema Zitto Kabwe Baada ya Lugola Kumtaka Ajisalimishe Polisi Pamoja na Video ya Utani ya Wazee wa Kigoma Wakiseti Mitambo yao kwa Kimbunga

0
0
Leo  Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amemtaka Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ajisalimishe kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi kwa kufanya Mkutano katika Jimbo lisilo lake.

Muda mfupi baada ya agizo hilo Zitto Kabwe amejibu kupitia ukurasa wake wa Twitter ;“Waziri hana hayo mamlaka. Kama polisi wananitaka watoe wito wa kisheria nitakwenda. Naendelea na kampeni za Mbunge wa Buyungu ambapo tunamwunga Mgombea wa CHADEMA na madiwani wa ACT Wazalendo kwenye kata kadhaa. Nashauri Waziri ampate kwanza yule Mbwa wa Polisi Bandari”

==>>Baadae akaweka na video ya utani kuonesha wazee wa kigoma wakitesti mitambo yao kwa kimbunga.Itazame hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Agosti 1

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

Serikali Yawalilia Wanafunzi Wanne Waliofariki Wakiogelea Bahari ya Hindi

0
0
SERIKALI  imesikitishwa na vifo vya wanafunzi wanne ambao ni wasichana wa kidato cha nne kutoka shule ya sekondari Kimbiji iliyopo Kigamboni jijini Dar es salaam waliofariki kwa ajali ya maji walipokuwa wakiogelea katika bahari ya Hindi.

Vifo vya wanafunzi hao vilitokana na sherehe iliyoratibiwa na shule husika ili kuwapongeza wanafunzi hao wa kidato cha nne baada ya kufanya vyema mitihani yao ya kujipima.

Akizungumza kwa majonzi shuleni hapo,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amesema serikali imepokea kwa masikitiko vifo hivyo na kutoa pole kwa wanafunzi, wazazi, na walimu wa shule hiyo kwa msiba huo mzito.

 Waziri Jafo amewataka walimu wote nchini kujiepusha na ufanyaji wa sherehe za wanafunzi katika mazingira hatarishi. Aidha, Waziri Jafo aliwasilisha rambirambi kwa familia nne za wafiwa.

Wanafunzi waliofariki dunia ni Secilia Ernest Paulo, Selestina Vitus Malipesa, Agnetha Philipo Mlaki na Queen Leonard Mandala.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images