Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Naibu Waziri wa Afya Dr Ndugulile Azitahadharisha NGOs kufuata vipaumbele vya Serikali

$
0
0
Na WAMJW Shinyanga
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile ameyataka Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kufuata vipaumbele vya Serikali katika maeneo wanayofanya kazi na kutoa huduma .

Ameyasema hayo mkoani Shinyanga wakati akizungumza na wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga wakuu wa Wilaya na Maafisa Maendeleo ya Ustawi wa Jamii katika hitimisho la ziara yake mkoani humo.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini ni wadau muhimu katika Maendeleo ya taifa ila wanapaswa kufuata vipaumbele vinavyotolewa na Mikoa na Halmashauri wanazoenda kufanya kazi na kutoa huduma.

Ameongeza kuwa katika Mikoa mingi kumekuwa na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayofanya kazi za aina moja kwa watu wa aina moja hivyo kufanya maeneno mengine kukosa nguvu.

Ametolea mfano changamoto iliyopo ya mimba na ndoa za utotoni katika baadhi ya Mikoa ukiwemo mkoa wa Shinyanga hivyo wadau wanapaswa kuelekeza nguvu katika kupambana na masuala muhimu ya eneo husika.

“Niwapongeze wadau wetu ila pia niwaase tu tuzingatie vipaumbele vya Mikoa na Halmashauri ili kusaidiana na Serikali katika Maendeleo” alisisitiza Dkt. Ndugulile

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Josephine Matiro amemuhakikishia Naibu Waziri  kuwa watasimamia kwa kuratibu kwa  karibu kazi zote zinazofanywa na wadau.

“Nikuhakikishie Mhe. Naibu Waziri tulisimamia agizo lako kwa ukamilifi” alisema Mhe. Josephine.

Nyumba Mbili Zachomwa Moto Jijini Mwanza Na Wananchi Wenye Hasira Kali....RPC Msangi Atoa Onyo

$
0
0
Kwamba tarehe 25.07.2018 majira ya saa 03:00hrs usiku katika mtaa wa Nyakabungo “A” kata ya Isamilo wilaya ya Nyamgana jiji na mkoa wa Mwanza, nyumba mbili mali ya Selina Francis, @ mama Mkapa, miaka 50, mkazi wa mtaa Nyakabungo na Abdalah Mwita @ Machela, zimechomwa moto na kundi la wananchi waliojichukulia sheria mkononi baada ya kuona watoto wa wahanga tajwa hapo juu wakijihusisha na uhalifu hapo mtaani mara kwa mara  kwani watoto hao wamekuwa wakikamatwa na kufikishwa mahakamani lakini wamekua wakiachiliwa kwa dhamana kisha kurudia tena kutenda uhalifu kitendo ambacho kimekuwa kero kubwa kwa wananchi wa eneo hilo.

Vilevile nyumba moja mali ya Manka Francis James @Mushi, iliharibiwa vibaya na kundi hilo la wananchi kwa kuvunjwa milango na madirisha na kuharibiwa vitu mbalimbali vilivyokuwemo ndani kwa kumtuhumu mwanamke huyo kuwa anashiriki katika kuficha wezi na vibaka pamoja na kujihusisha na utapeli kwa wananchi wa mtaani hapo na Mwanza kwa ujumla kwa kuwauzia dhahabu bandia, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Inadaiwa kuwa wananchi wa mtaa tajwa hapo juu wamekuwa wakimlalamikia na kumtuhumu mtoto wa Mama Selina Francis aitwaye Mkapa Mwabe pamoja na mtoto wa mzee Abdalah Mwita aitwaye Emmanuel Mwita @ Mwita  kuwa ni wezi/vibaka mtaani hapo. 

Vilevile wakimtuhumu Manka Fransis James @ Mushi kwa kushiriki kuwaficha wezi na vibaka nyumbani kwake pindi wanapotenda uhalifu mtaani na kuwatapeli wananchi kwa kuwauzia dhahabu feki.

Inasemekana kuwa kutokana na tuhuma hizo ndipo tarehe na majira tajwa hapo juu kundi la wananchi waliojawa na hasira kutokana na vitendo vya waanga walikwenda na kuvamia nyumba ya bwana Abdalah Mwita pamoja na nyumba ya mama Selina Francis ambapo waliwakuta watoto wadogo, wenye nyumba hawakuwepo kisha waliwatoa watoto nje na kuchoma nyumba hizo moto. 

Aidha inadaiwa kuwa baada ya hapo kundi hilo la wananchi lilikwenda kwenye nyumba ya Manka Francis pia walikuta watoto mwenye nyumba hakuwepo kisha waliwatoa  watoto nje na walivunja madirisha na milango na kuharibu vitu mbalimbali vilivyokuwepo katika nyumba hiyo wakiwa wanataka……

Baada ya hapo raia wema walitoa taarifa kituo cha polisi ambapo askari waliokuwa doria walifika haraka eneo la tukio na kukuta tayari wahalifu hao wamekimbia. 

Msako mkali wa kuwatafuta wale wote wanaotuhumiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika uhalifu huo bado unaendelea. 

Pia msako na ufuatiliaji wa vijana wanaotuhumiwa kufanya uhalifu mtaani hapo pamoja na wazazi wao bado unaendelea. 

Pia hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa au kupoteza maisha katika tukio hilo, aidha thamani halisi ya vitu vyote vilivyoharibiwa katika uhalifu huo bado haujafahamika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishina wa polisi Ahmed Msangi anatoa onyo kwa watu wote wenye tabia za kujichukulia sheria mkononi kuacha mara moja kwani ni kosa kisheria na wale wote waliohusika endapo watabainika hatua kali za kisheria zitachuliwa dhidi yao. 

Sambamba na hilo pia anawataka wananchi watambue kwamba dhamana ni haki ya mtuhumiwa endapo tu kama kesi anayohumiwa nayo inadhaminika hivyo wananchi waache tabia ya kujichukulia sheria mkoni pindi watuhumiwa wanapofikishwa mahakamani na kuachiliwa kwa dhamana kwani ni hitaji la kisheria wakati shauri linaendelea mahakamani. 

Aidha anawaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa mapema za wahalifu ili waweze kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

IMETOLEWA NA:
DCP: AHMED MSANGI
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA.

Lugola Amtaka IGP Sirro Ampelekee Ripoti ya Miaka Mitano ya Mauaji na Utekaji Bodaboda

$
0
0
Siku chache baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola, kumwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro kuhusu mbwa na ujambazi, jana amemtaka ampelekee orodha ya miaka mitano ya matukio ya utekaji wa bodaboda na kuuawa kwa madereva wake.

Waziri Lugola alitoa agizo hilo jana akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha katika Kituo cha Polisi cha Muriet.

Akiwa ziarani humo alipata fursa ya kusikiliza kero za wananchi ndipo waendesha bodaboda hao walipotoa malalamiko yao kuhusu kutekwa na kuuawa wakiwa kazini.

Mwenyekiti wa Waendesha Bodaboda Kata ya Muriet iliyopo mjini humo, Akili Mbaga, akizungumza kwa niaba ya wenzake, alimweleza Waziri Lugola kuwa, wamekuwa wakiuawa na wezi wa bodaboda na kesi zimejaa polisi bila kufuatiliwa.

Mbaga alimuomba Waziri Lugola awasaidie ili matukio hayo yakomeshwe.

Kutokana na ombi hilo, Waziri Lugola alisema anajua baadhi ya maeneo madereva wa bodaboda wamekuwa wakitekwa na wakati mwingine wakizuiliwa barabarani na magogo kisha kunyang’anywa vyombo vyao vya usafiri na kuuawa.

“Ninamwelekeza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) aniletee orodha ya miaka mitano iliyopita mpaka sasa ikiwa na takwimu kwa maeneo, kiwilaya na kimkoa na nchi kwa ujumla, niweze kuona matatizo haya yamekithiri hasa maeneo gani ili tuwe na mikakati ya kujipanga kwa kuongeza nguvu kuhakikisha matatizo haya yanamalizika,” alisema.

Alisema hatua hiyo ya kumtaka IGP kumpelekea orodha hiyo, ina lengo la kutafuta mwarobaini wa kuyamaliza matukio hayo.

Polisi Waua Mmoja kwa Kipigo Akidaiwa ni Mvuvi Haramu

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoani Geita, Mponjoli Mwabulambo 
**
Mtu mmoja kati ya wanne waliokamatwa katika operesheni ya kudhibiti uvuvi haramu Ziwa Victoria, amefariki dunia kutokana na kile kinachodaiwa kuwa alipata kipigo kutoka kwa askari wanaosimamia operesheni hiyo.

Aliyefariki dunia ni Paschal Kanyembe (40), mkazi wa Kitongoji cha Mlila, Kijiji cha Rubambangwe wilayani Chato mkoani Geita.

Mbali na Kanyembe, watuhumiwa wengine waliokamatwa na kudaiwa kujeruhiwa katika operesheni hiyo ni Busu James, Emmanuel Luchagula na Rusato Magesa.

Akizungumzia tukio hilo, mke wa marehemu, Ester Justine (39), alisema  juzi kuwa majira ya saa saba usiku wa kuamkia Jumanne, askari wa doria ya kudhibiti uvuvi haramu walifika nyumbani kwake na kutoa amri kwa wanandoa hao kufungua mlango.

Alisema walilazimika kuomba dakika chache ili wavae na askari hao walikubali na kuwapatia dakika mbili za kufanya hivyo na baadaye wanandoa hao walifungua mlango wa nyumba yao.

Ester aliendelea kueleza kuwa, pasi na kujua kinachoendelea, askari wawili kati ya kundi kubwa lililokuwa nyumbani kwake, waliingia ndani na kumweka chini ya ulinzi mume wake huku wakimtaka kusalimisha nyavu haramu walizodai amezificha.

"Baada ya mume wangu kuwaambia kuwa hausiki na uvuvi wa aina yoyote ile, walianza kumshambulia kwa marungu na mateke huku wakimvuta kwenda nje," Ester alieleza.

"Hata walipomfikisha nje waliendelea kumpiga sana hadi akashindwa hata kukaa chini, akabaki amelala chali.

"Nikiwa mlangoni, nilishuhudia kipigo hicho, lakini baadaye askari waliniamuru kurudi ndani kulala huku wakiondoka na mume pamoja na vijana wengine watatu ambao tayari walikuwa wameshawekwa chini ya ulinzi.

"Majira ya saa mbili asubuhi leo (Jumanne) nilipiga simu ya mume wangu ili kujua kama ameachiwa lakini ilipokelewa na mmoja wa askari hao ambaye alianza kuniuliza kama mume wangu huwa ana ugonjwa wa kifafa, kisukari au shinikizo la damu.

"Nilipowajibu kuwa hajawahi kuugua magonjwa hayo, wakaniambia 'tafuta usafiri uje kwa mume wako yupo huku Kituo cha Afya cha Nyabugera Muganza'. Ikabidi niende huko."

Ester aliongeza kuwa mume wake alipelekwa katika kituo hicho na askari hao.Rafiki wa marehemu, Didas Emmanuel, alisema  juzi kuwa baada ya kufika Kituo cha Afya Muganza akiwa na Ester, alishuhudia rafiki yake akiwa hajiwezi huku akiwa anaongezwa maji mwilini kwa sindano.

Alisema kuwa matabibu waliokuwa wanampa kituoni hapo, walimshauri kwenda kituo cha polisi kuchukua fomu ya polisi ya kuruhusu mtu aliyejeruhiwa kutibiwa (PF3) kabla ya mgonjwa wao kuhamishiwa Hospitali ya Wilaya ya Chato kwa ajili ya matibabu zaidi.

"Tukiwa njiani kwenda hospitali ya wilaya kumwahisha mgonjwa wetu ili apatiwe matibabu, majira ya saa 5:30 asubuhi, ndugu yetu alikata roho," alisema.

Wakazi wengine wa eneo hilo, Daud Kingu na Enos Petro, walidai vitendo vya askari wa doria ya uvuvi haramu kupiga wananchi ovyo, kuvamia nyumba za watu usiku, kupora simu na fedha za wananchi vimekuwa vikitokea mara kwa mara kwenye maeneo yao.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Chato, Dk. Eligobeth Kalisa, alikiri kupokea maiti ya mtu huyo pamoja na wagonjwa wengine watatu waliopelekwa na Idara ya Maliasili ambao walitibiwa na baadhi yao kuruhusiwa kuondoka baada ya afya zao kuimarika.

"Itoshe tu kusema kuwa taarifa za uchunguzi (Kanyembe) tumeshawapatia polisi. Na unajua mambo haya yakishakuwa kwenye jinai, sisi haturuhusiwi kuyazungumzia. Kwa hiyo, mambo mengine watafute polisi," alisema Dk. Kalisa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa kifo hicho kilitokea kwa bahati mbaya kwa kuwa lengo la askari hao ni kudhibiti uvuvi haramu na siyo vingine.

"Ni kweli tukio hilo lipo na umauti ulimkuta kijana huyo jana (juzi) majira ya saa sita mchana akiwa amefikishwa kwenye Kijiji cha Mkuyuni wakati akiwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi baada ya kumpatia rufani kutoka Kituo cha Afya cha Nyabugera. Kijana huyo alipungukiwa nguvu na umauti kumkumba," alisema Mwabulambo.

Chanzo: Nipashe



Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Adaiwa Kumnasa Vibao Ofisa Ardhi, CCM Walaani

$
0
0
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi
**
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma Mjini kimelaani kitendo cha Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi kumpiga vibao mtumishi wa ofisi yake, Damas Mwakindingo ndani ya ofisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Julai 25, 2018, Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Robert Mwinje alisema kitendo alichokifanya Kunambi hakikubaliki kwa kuwa hakuna sheria  inayoruhusu mtumishi kupigwa.

“Sisi kama Chama, kazi yetu ni kushauri lakini pia kushauri kuna mwisho wake,” alisema Mwinje.

Katika mkutano huo na waandishi wa habari, Mwinje alimbatana na madiwani wa CCM wa Jiji la Dodoma.

Hata hivyo, baadaye alipohojiwa kuhusu tuhuma hizo, Kunambi alisema hawezi kuongea chochote kuhusuiana na tuhuma hizo na badala yake akamtaka anayedai kupigwa ndiyo azungumza na waandishi wa habari.

“Mimi sina cha kuongea na badala yake ongeeni na huyo wanayesema nimempiga, ila mie nitakutana na huyo mwenyekiti (Mwinje) mahakamani,” alisema Kunambi.

Damas Mwakindingo ambaye ni ofisa ardhi wa Jiji anayedaiwa kupigwa na Mkurugenzi wa Jiji alikanusha vikali tuhuma hizo na kusema hajapigwa na Mkurugenzi wa Jiji.

“Ni watu tu wamezusha, kwani hata hivyo tulikaa na tukayamaliza, hivyo yamekwisha,” alisema Mwakindingo

Tenga Awataka TFF Wasikurupuke....Ataka Sheria ya Wachezaji 10 wa Kigeni Ifanyiwe Tathimini Kwanza

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Leodegar Tenga ameliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)  liache kukurupuka na badala yake lipitie kwa kina sheria ya wachezaji 10 wa kigeni katika timu za Ligi Kuu.

Sheria hiyo iliyopitishwa hivi karibuni na TFF, inaruhusu timu zinazoshiriki Ligi Kuu nchini kusajili wachezaji wa kigeni 10 kutoka idadi ya awali iliyoruhusu timu inayoshiriki ligi kuu kuwa na wachezaji wakigeni saba.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana  Jumatano Julai 25, Tenga alisema sheria hii ikiwezekana ipitiwe tena kwa kina ili ionekane kama inaweza kusaidia ligi hiyo.

“Kuwe na tathimini ya kina juu ya sheria hii tujiulize kama kweli inaweza kusaidia timu zetu na wachezaji wa hapa nyumbani pia tutafakari kama tunaweza kufika tunapokwenda kwa sheria hii.

“Wakati mwingine kuwa na ushirikishwaji mzuri ili watu watoe maoni yao juu ya hili jambo na hata tunaposajili wachezaji hawa tuhakikishe tunasajili wachezaji wenye viwango vizuri,” alisema Tenga.

Aidha, katika mkutano huo mwenyekiti huyo amesisitiza vyama vya michezo kitaifa kuhakikisha vinafuata sheria za kimichezo vizuri na kuhakikisha kunakua hakuna migogoro ya muda mrefu  kwenye vyama.

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

$
0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

Maradhi Ya Kichawi Na Tiba Zake

$
0
0
Wachawi  wana  uwezo  wa  kumsababishia  mtu maradhi  kwa  kutumia  uchawi.

Mtu  aliye tupiwa  maradhi  ya  kichawi  huanza kuonyesha  dalili  zote  za  mgonjwa  wa  maradhi  husika. 

Kama  mhusika  ametupiwa  maradhi  ya  kiharusi  basi  ataonyesha  dalili  zote  za  mgonjwa  wa  kiharusi, kama  ametupiwa  maradhi  ya  kifafa  basi  ataonyesha  dalili  zote  za  mtu mwenye  kusumbuliwa  na  maradhi  ya  kifafa  na kama  atakuwa  ametupiwa  ukichaa  basi  mtu huyo  ataonyesha  dalili  zote  za  mtu  mwenye  kichaa.

DALILI   ZA  MAGONJWA  YA  KICHAWI
Kila maradhi  ya  kichawi  yana  sifa na dalili zake     za  kipekee.

Kwa  maana  ya  kwamba  kifafa  cha  kichawi  kina  dalili  zake, kichaa  cha  kichawi  kina  dalili  zake, kiharusi  cha  kichawi  kina  dalili zake  nakadhalika  nakadhalika.

Lakini  maradhi   yote  ya  kichawi  huwa  na  sifa  moja  ya  kipekee  ambayo  kila  mwenye  kusumbuliwa  na  maradhi  ya  kichawi  huwa  nayo.

Nayo  ni  kutumia  tiba  nyingi  kwa  muda  mrefu  bila  kupata  nafuu  yoyote  ya  kudumu  pamoja  na  ugonjwa  kuto onekana  kwenye  vipimo  vya   hospitalini.

                  AINA   YA  MARADHI  YA  KICHAWI
Maradhi ya  kichawi  yamegawanyika  katika   aina  kuu  mbili  kama  ifuatavyo :

1.    AINA YA  KWANZA : MARADHI  YA  KICHAWI  YATOKANAYO NA  KULISHWA  SUMU  ZA  KICHAWI

2.    AINA  YA  PILI  :  MARADHI  YA  KUTUMWA  KWA  KUTUMIA  MAJINI  WA  KISHEITWANI

MARADHI   YATOKANAYO   NA  KULISHWA  SUMU  ZA  KICHAWI.

Wachawi  wana  elimu  na  maarifa  mapana  sana  kuhusu  miti  mbalimbali  ya  porini  ambayo inapotumiwa na  wanadamu  au  wanyama  hutengeneza  sumu  yenye  kusababisha  maradhi  mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  au mnyama  husika.

Mfano  kuna  mti  mmoja  wa  porini. Ni mti  mrefu wenye  kutoa  majani  yenye  kunukia. Mafuta  ya  mti  huu  hutumiwa  na  wachawi  katika  kuwasababishia  watu  maradhi  ya  ini.

Mafuta  ya  mti  huo  husababisha  kufeli  kwa  ini.  Kinacho  fanyika  mtu  aliekusudiwa  anakuwa  anawekewa  kijiko  kimoja  kidogo cha  mafuta  hayo kwenye  chakula  anacho  tumia  kwa  muda  wa  siku  saba  mfululizo.

Sumu hiyo  hufanya  kazi  kwa  taratibu  sana  na  inaweza  kuchukua  hata  miezi  sita  kuanza  kuonyesha  dalili.

 Mwisho  wa  siku  mhusika  alielishwa  sumu  hiyo  ndio  anakuwa  tayari amekuwa  ameshapewa  maradhi  ya  ini.

 Mara  nyingi  uchawi  huu  hufanywa  na  mtu  wa  karibu.

Kuna mti mmoja  wa  porini  ambao wachawi  wanau  tumia  kuwasababishia  wanawake  wajawazito  tatizo  la  kuchoropoka  kwa  mimba.

Majani  ya  mti  huu  hupondwa  pondwa  na  kuchemshwa  na kisha  kuchanganywa  kwenye  chakula  atakacho  kula  mwanamke  mwenye  ujauzito  mchanga.

Mwanamke  huyo  akisha  kula  dawa  hizo  za  kichawi  basi  hazitapita  siku  tatu  huo  ujauzito  utachoropoka.

Hali  hii  itakuwa  inajirudia  kila  mwanamke  huyo  anapokuwa  amebeba  ujauzito  kwa  sababu  wanao kuwa  wanasimamia  zoezi  hilo  ni  watu  wake  wa  karibu.

Ndio  maana  unakuta  wanawake  wengine  amebeba  mimba  Zaidi ya  nne  na  zote  zinachoropoka  na  kumsababishia  maisha  magumu  katika  ndoa  yake.

Hayo  ni  baadhi  ya  maradhi  lakini  karibu  kila  maradhi  unayo yafahamu  wewe  wachawi  wanaijua  miti ya  porini  ambayo  wakimlisha  mtu  basi  moja  kwa  moja  inakwenda  kuathiri  sehemu husika  katika  mwili  wa  mkusudiwa  na  kumsababishia  maradhi  yaliyo  kusudiwa.  Ipo  miti  inasababisha  uziwi, upofu, ugumba,  ukhanithi, pumu,mtoto kuchelewa kuongea, kutembea  nakadhalika.

MARADHI   YA   KUTUMWA   KWA   KUTUMIA   MAJINI   WA  KICHAWI.
Haya  ni  maradhi  yanayo  tumwa  moja  kwa  moja  kwa  mkusudiwa  kwa  kutumia  majini  wa  kisheitwani.

Hapa  jinni  wa  kisheitwani  huamriwa  kwenda  kukaa  ndani  ya  nafsi  ya  mtu  Fulani  na  kumsababishia  maradhi  Fulani.

Mtu  aliye  tumiwa  jinni huyu wa  kisheitwani  huanza  kuonyesha  dalili  zote  za  mtu  mwenye  maradhi  yaliyo  kusudiwa.

Atakaa  na  maradhi  hayo  kwa  muda  mrefu  na  atatumia  tiba  za  kuondosha  maradhi  hayo bila  kupata  nafuu  yoyote  ya  kudumu na  mwisho  wa  siku  atakata  tamaa  kabisa  akisubiri  kifo  kimchukue .

TIBA ZA   MAGONJWA   YA   KICHAWI
Maradhi  ya  kichawi  yanaweza kutibiwa  kwa  kutumia  dua, kafara, na  miti  ya  aina  mbalimbali  kulingana  na  aina  ya  maradhi  yanayo  msumbua  mhusika.

Lakini  kabla  ya  mhusika  kutibiwa  ni  lazima ijulikane  kwanza  kama  maradhi  yanayo  msumbua  ni  ya  kawaida  ( ya kibinadamu ) ama  ya  kisheitwani  ( maradhi  ya  kichawi )

Zipo  njia  mbalimbali zinazo  tumika  kujua  kama  mgonjwa  husika  maradhi  yake  ni  ya  kibinaadamu  au  ya  kisheitwani.

 Nitazielezea  kwa  ufupi  njia  hizo.

(  Utajuaje  kama  maradhi  yanayo  kusumbua  ni maradhi  ya  kichawi )

1.    Kusoma  dalili  za mgonjwa. ( Kila  maradhi  ya  kichawi  yana  dalili  zake  maalumu  ambazo  huweza  kutumika  kama  viashiria  vya  kujua  kama  mhusika  ana sumbuliwa  na  maradhi  ya kibinadamu  au  ya  kichawi.

2.    Kusoma nyota  ya  mgonjwa  ili kujua  kama imetiwa  kiza cha maradhi

3.    Kufanya  dua  maalumu  ya  kuomba  kujua  kama  maradhi  yanayo  msumbua  mhusika  ni ya  kibinadamu  au  ya  kisheitwani. Kama  ni  maradhi  ya  kibinadamu  basi  mgonjwa huyo  atapewa  tiba  za  kawaida  ambazo  hutibu  magonjwa  ya  kibinaadamu  na  kama  ni  itajulikana  ni  maradhi  ya  kisheitwani  basi  atapewa  tiba  sahihi  kulingana  na  maradhi  yanayo  msumbua.

4.    Kumtibu  mgonjwa  kwa  kutumia tiba  maalumu  za  asili  ambazo  hutibu  na  kuondosha  kabisa  maradhi  husika.

 Katika  ulimwengu  wa  kitabibu  zipo  tiba  maalumu  za  asili  ambazo zina sifa ya  kutibu  na  kuondosha  kabisa aina  Fulani  ya  maradhi  yanayo  wasumbua  wanadamu.

 Ikitokea  tiba  hiyo  imeshindwa  kumtibu  mgonjwa  huyo basi  ni ishara  ya  moja  kwa  moja  kwamba  maradhi  yanayo  msumbua  mtu  huyo  ni  maradhi  kisheitwani.

Mfano  wa  tiba  hiyo  ni  ile  itokanayo  na  mti  wa  Mgude.

Kwa  wenyeji  wa mikoa  ya  Tanga, Pwani  na  kusini  ( Lindi  na  Mtwara ) mtakuwa  mnaujua  mti  huu  vizuri.

 Unajulikana  kwa  wengi  katika  utabibu  kama  mti  wenye  kukaliwa  na  majini  wakubwa  wa  kisheitwani  wenye  sifa  tofauti  tofauti.

Ni mti  wenye  maajabu  sana  na  unao  tumika  kufanyia kafara  nyingi  kubwa  kubwa.

Kwa  kifupi  ni  mti  unaopendwa  sana  na  majini  wabaya.  Kama  unataka  kufanya  ushirika  ama  agano  na  majini  wabaya  basi  mti  wa  mgude  utakufaa  sana.

Ukiwa  unataka  kuwa  unaona  mauza  uza  nyumbani  kwako  basi  panda  mti  huu  wa  mgude.     Mti wa Mgude unaingia  pia  katika  nyungu  ya  miti  saba  mikubwa  ya  porini na  huweza  kutumika  pia  kuwafukuza  baadhi  ya  majini  wabaya  ambao  ni  wadogo  kimamlaka  kwa  majini  wanao  kaa ndani  ya  mti  huu.

Sasa  basi  mti  huu  wa  Mgude  mbali  na  kuwa  na sifa  hizo  nilizo  zitaja  hapo  juu, lakini  pia  mti  huu  unatoa  tiba  mujarabu kabisa . Mti  wa  mgude  unatumika  katika  kutibu  na  kuondosha  kabisa  maradhi  yafuatayo :

1.    KIHARUSI  :   Magamba  na  majani  ya  mti  wa  mgude  huanikwa  juani  na  kukauka  kisha  husagwa  halafu  unga  unga  wake  huchemshwa  na  maji  na  kisha  kimiminika  kupewa  mtu  mwenye  maradhi  ya  kiharusi . Mgonjwa  atapona  kabisa  kiharusi  ndani  ya  siku  21.  ( KIHARUSI  KINACHO  TIBIWA  NA  TIBA  HII  YA  MTI  WA  MGUDE  NI  KIHARUSI  CHA  KAWAIDA  NA  SIO  CHA  KUROGWA.  KATIKA  ULIMWENGU  WA  KITABIBU, MGONJWA  WA  KIHARUSI  AKITUMIA  TIBA HII  HALAFU  ASIPONE  BASI  NI  ISHARA  KWAMBA  MARADHI  ALIYO  NAYO  YAMETOKANA  NA  KUROGWA.

2.    UKHANITHI :  Hapa   namzungumzia  mwanaume  ambae  hawezi  kabisa  kusimamisha  uume wake na  sio  yule  shida  ya  udhaifu  tu wa  nguvu  za  kiume. Namaanisha  asie w eza  kabisa  kusimamisha  uume  wake . Magamba  ya  mgude  huanikwa  juani  na  kusagwa  ama  kupondwa  pondwa  hadi yawe  unga  na  kisha kuchemshwa  na  mgonjwa  kupewa  kimiminika  anywe   mara  tatu  kwa  siku  asubuhi mchana  na  usiku  kwa  muda  wa  siku  saba. Asipopona  maradhi  yake  basi  hicho  kiashiria kwamba  maradhi  ya  mhusika  yanatokana  na  kurogwa kwa  hivyo  hutafutwa  tiba  ya  kubatilisha  uchawi  ulio  msababishia  mhusika  maradhi  ya  ukhanithi.

3.    MALARIA  YA  UBONGO (  ambayo  huchukuliwa  kama  ukichaa ).   Mti  wa  mgude  hutibu  na  kuondosha  kabisa  maradhi  ya  malaria  iliyo  panda  kichwani  au  malaria  ya  Ubongo. Majani  ya  mgude  huchukuliwa  na  kuanikwa  juani  kisha  kusagwa  halafu  kuchemshwa  na  maji  halafu mgonjwa  anakuwa  anapewa  kunywa  kwa  muda  wa  siku  kumi  na  nne.  Kama  maradhi  yake  ni  ya  kawaida  basi  ndani  ya  hizo  siku  kumi  na  nne  atakuwa  amepona  maradhi  yake  na  ikiwa  vinginevyo  basi  ni ishara  kwamba  maradhi yake  ni  ya  kutengenezwa  kichawi.

4.    TATIZO  LA  KUCHOROPOKA  KWA  MIMBA : Mizizi  ya  mgude  hutumika  kutibu  na  kuondosha  kabisa  tatizo  la  kuchoropoka  kwa  mimba  hata  kama  limedumu  kwa  muda  mrefu  kiasi  gani.  Mwanamke  mwenye  tatizo  la  kuchoropoa mimba  akitumia  mizizi  ya  mgude  halafu  tatizo  lake  likaendelea  kujirudia  basi  ni  ishara  ya  moja  kwa  moja  kwamba  tatizo  lake  hilo  linasababishwa  na  majini  wa  kisheitwani.

5.    Maradhi  mengine  yatibiwayo  na  mti  wa  Mgude  ni pamoja  na kichocho  na  kuhara.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA. MUNGWA  KABILI. ANAPATIKANA  KWA  SIMU  NAMBA  0744  000  473.

Makala  haya  yanapatikana  kwa  undani  Zaidi  katika  kitabu “ MAMBO TISA  YANAYO  UNDA  NYOTA  YA  MWANADAMU : UHUSIANO  KATI  YA   NYOTA  YA  MTU  NA  MAFANIKIO  YAKE  KATIKA  MAISHA ambacho  kimeandikwa  na  Dokta. Mungwa  Kabili.


Katika  Makala  zijazo  nitakuwa  nikielezea  magonjwa  yote  ya  kichawi  kwa  kuangalia  ugonjwa  mmoja  baada  ya  mwingine. Jinsi  yanavyo  tengenezwa  na  wachawi, lengo  la  kuyatengeneza, jinsi ya  kujiikinga  nayo  na  jinsi  ya  kujitibu   kwa  mtu  ambae  tayari  ametupiwa  maradhi  hayo  ya  kichawi.

Pia  kufuatia maombi  ya  watu  wengi  ambao  wameshindwa  kupata  nakala  za kitabu  changu  MAMBO TISA  YANAYO  UNDA  NYOTA  YA  MWANADAMU…  Siku  chachae  zijazo   nitayaelezea  mambo  hayo  moja  baada  ya  jingine.

MTI  WA  MGUDE  NI  HUO  AMBAO  PICHA  YAKE  INAONEKANA  HAPO  JUU.

Ray C Aguswa na staili ya maisha ya sasa ya Lulu Michael

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki nchini Tanzania, Ray C amejikuta akilengwa na machozi baada ya kuangalia video iliyosambaa mtandaoni ikimuonesha Muigizaji wa Bongo Movie, Elizabeth Michael ‘Lulu’ akicheza kwaya kanisani.

Ray C amedai kuwa video hiyo imemfanya akumbuke kipindi cha nyuma wakati alipopitia kwenye matatizo ya kuugua kwani kipindi hicho alikuwa ni mcha Mungu na alikuwa hakosi kanisani tofauti na sasa.

“Lulu nimeangalia hii video zaid ya mara kumi nahisi!mpaka machozi yamenilenga kwakweli!Sikumbuki lini nimeingia kanisani!“ameandika Ray C kwa kujutia kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusisitiza kuwa amejifunza jambo kutoka kwenye video hiyo.

“Najiona mzima sasa na nasahau kuwa Mungu ni mkali! nimejifunza kitu kutoka kwako my dear! kikubwa sana. You Inspire Me..“amemaliza hivyo Ray C.

Picha na video ya Lulu ikimuonesha mwenye afya nzuri akiwa Kanisani akicheza na waumini wenzake ilisambaa Jumatatu ya wiki hii. 

Tazama video yenyewe hapa chini ikimuonesha Lulu akicheza kanisani

Harmorapa Adai Moyo Wake Upo Kwa Wema Sepetu , Achora Tattoo Ya Jina Lake

$
0
0
Msanii wa hip hop Harmorapa ambaye anajizolea umaarufu kwa vituko vyake amefunguka na kudai anampenda Wema na amechora Tattoo mpya ya Jina lake.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Harmorapa amefunguka na kudai mwanamke ambaye anajitangaza kuwa ataolewa na Harmorapa ni muongo kwa sababu hana Mahusiano naye.

Harmorapa amefunguka na kudai hana mpango wa kumuoa mwanamke aliyetoka Mwanza kwa ajili yake aliyejitambulisha kwa jina la Khadijah na kudai anataka kumuoa Wema.

Harmorapa amedai kwamba zile picha zinazosambaa Kwenye mitandao ya kijamii zilikuwa ni clip za Kwenye Movie mpya ambayo amecheza naye lakini sio wapenzi.

Lakini pia Harmorapa amefungukia mapenzi yake kwa Wema Sepetu na kudai anampenda kupita kiasi na Yupo Tayari kumuoa muda wowote na hata kukiri kuchora Tattoo ya Jina na lake Kwenye shingo.

Siku za nyuma Wema ameshawahi kumtolea povu Harmorapa na kumtaka aache kujitangaza Kwenye vyombo vya habari kuwa anampenda kwani alikuwa anamkera.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Mwanafunzi Afariki Dunia Bweni likiteketea kwa moto

$
0
0
Mabweni ya shule ya msingi St. Joseph Rutabo iliyopo Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera yameungua moto usiku wa kuamkia leo.

Bweni hilo limeteketea leo Alhamisi Julai 26, 2018 huku mashuhuda wa tukio hilo wakisema viongozi wa wilaya hiyo wapo katika kikao na walimu kujadili tukio hilo.

Kwa mjibu wa Afisa elimu mkoa wa Kagera Aloyce Kamamba amesema mwanafunzi wa darasa la tano ameungua na kufariki hapohapo lakini wengine wanaendelea kupatiwa huduma,

Wema Sepetu asema atajaribu kuwa na roho mbaya ili afanikiwe

$
0
0
Msanii wa filamu Wema Sepetu amedai kwa sasa anajaribu kujifunza kuwa na roho mbaya kwa kuwa kuna baadhi ya vitu vyake vingi vimekwama kutokana na kuwa na roho ya huruma. 

Muigizaji huyo amedai watu wengi wenye roho mbaya wamefanikiwa zaidi kuliko wale wenye wema ambao hutumia maisha yao kusaidia marafiki zao.
 
Hata hivyo wema anasema kuwa kwa upande wake yeye inakuwa ngumu kuwa na roho mbaya kwa sababu mungu anakuwa tayari amekuumba hivyo hivyo huwezi kubadilika hata kidogo katika hilo.

Lakini amesema kuwa na yeye atajitahidi kuwa na roho mbaya ili aone kama inawezekana kufanikiwa kama wengine.

"Wanasemaga watu wenye roho mbaya wanafanikiwa sana, na mimi roho hiyo sina kwa sababu ninachoamini ni kwamba kama umejariwa roho nzuri basi hiyo ni roho yako tu huna haja ya kuwa na roho nyingine, sometimes roho yangu nzuri inaniponza sana.ila nitajitahidi kujifunza roho mbaya.

Akiongelea kuhusu kesi yake iliyoisha hivi karibuni wema ansema hana la kusema zaidi ya kumshukuru mungu kwa kuwa kipindi icho alikuwa katika wakati mgumu wa kufanya mambo mengi kwa kusua sua.

Mwalimu Mkuu Adaiwa Kutoweka Baada Ya Kumpa Mimba Mwanafunzi wake wa Darasa la 7

$
0
0
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kilambo cha Mkolechi, kata ya Kala wilayani Nkasi mkoani Rukwa, Eradi Kapyela ametoweka katika na kwenda kusikojulikana baada ya kudaiwa kumpa mimba mwanafunzi wake wa darasa la saba.

Taarifa hiyo ilibainishwa jana kwenye kikao cha Baraza la Madiwani baada ya Mbunge wa Nkasi Kusini, Desderius Mipata kualalamika ndani ya kikao hicho kuwa ameshangazwa na kitendo cha serikali kutomchukulia hatua  mwalimu huyo kwa kitendo hicho.

Amesema mimba kwa wanafunzi wilayani humo bado ni tatizo hivyo jitihada za makusudi za mapambano ni lazima ziendelee na kuwa mwalimu huyo ni lazima achukuliwe hatua za kisheria.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo, Missana Kwangulah amesema  taarifa za mwalimu huyo wanazo na juhudi za kumsaka zinaendelea kwani muda wa siku tano umepita tangu mwalimu huyo atoweke katika kituo chake cha kazi bila taarifa na kwaamba amefanya hivyo kukwepa mkono wa sheria.

Ndege Mbili Mpya za Bomberdiar Kutua Novemba Mwaka Huu......

$
0
0
Serikali imeahidi kuleta ndege nyingine mbili za C Series ifikapo Novemba mwaka huu na Boeing nyingine Januari 2020, ikiwa na lengo la kutimiza ndoto yake ya kuhakikisha inafufua Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Ndege hizo zitakazowasili zitakuwa ni mwendelezo wa ndege zilizofika nchini awamu ya kwanza aina ya Bomberdiar na hivi karibuni kushuhudia kuwasili kwa ndege nyingine Boeing 878 Dreamliner.

Akizungumza  na waandishi wa habari jana, Msemaji wa Serikali, Dk. Hassan Abbasi, alisema   manufaa ya ndege hizo yameanza kuonekana na zinasaidia wananchi wengi kusafiri na kufanya biashara zao kwa haraka.

“Tangu tulete ndege hizi abiria wa ATCL waliongezeka hadi kufikia 107.207 katika mwaka 2016/17 wakati mwaka 2015/16 walikuwa 49,173 ikiwa ni ongezeko la asilimia 118,”  alisema Dk. Abbasi.

Akizungumzia gawio la mashirika ya umma kwa serikali, alisema yemekuwapo  maneno  ya kupotosha kutoka kwa wanasiasa kuhusiana na gawio la Sh bilioni 700 lililotolewa hivi karibuni kwa Serikali na mashirika hayo   kuwa sio sahihi, jambo ambalo ni uongo.

Mbunge Ester Mahawe Awashangaa Wapinzani

$
0
0
Na John Walter Babati
Mbunge wa viti maalum Ccm mkoa wa Manyara mheshimiwa Ester Mahawe amesema anashaangazwa na upinzani kusimama majukwaani na kusema serikali haifanyi kazi.

Ameyasema hayo wakati akimnadi mgombea udiwani wa chama hicho katika kata ya Bagara Nikodemus Bonifasi [Nyeusi] katika mtaa wa Osterbay mjini Babati leo.

Amesema serikali iliyopo madarakani imefanya mengi na itaendelea kufanya,akitolea mfano ndege saba ambazo serikali imenunua kwa pesa za ndani ili kuinua shirika la ndege [ATCL] na kuongeza kasi ya uchumi wa nchi pamoja na barabara za lami zinazoendelea kujengwa mjini Babati kilomita kumi.

Mgombea udiwani wa Chama cha Mapinduzi [CCM] Nikodemus Bonifasi amesema kuwa kwake yeye udiwani si kitu,bali anaangalia wananchi wanataka nini.

Akizungumzia mambo ambayo atayafanya endapo wananchi wa kata ya Bagara watampatia nafasi amesema tayari chama chake kimeshaorodhesha katika ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015,’Kwa hiyo mimi nitakachokifanya ni kusimamia utekelezaji” alisema Nyeusi.

Akieleza kwanini aliondoka Chadema alisema  ameondoka kwa sababu Chadema wanapinga kila jambo linalofanywa na serikali na kwamba yeye chama hicho hakina mkataba na wananchi bali CCM ndio kina mkataba na wananchi wake.

Kwa upande wa mgombea wa Chadema Mathias Zebedayo amewaambi wakazi wa kata ya Bagara kuwa akipata nafasi ya kuwa diwani atahangaika kuhakikisha Mbaazi na Mahindi yanapanda bei pamoja na kusimamia upimaji wa maeneo ambayo hayajapimwa katika kata hiyo.

Mnyeti Awapa Siku Tisini Idara Ya Ardhi Kutoa Hati Miliki Babati

$
0
0
Na John Walter Babati
Mkuu wa mkoa wa MANYARA Alexender Pastory Mnyeti ameiagiza idara ya ardhi mjini Babati kutoa hati miliki  kwa wote wenye viwanja Maisaka A Babati Mjini ndani ya siku tisini.

Agizo hilo amelitoa kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika Julai 25 katika shule ya msingi Sinai kusikiliza malalamiko ya wakazi wa Maisaka.

Kwa mujibu wa Mnyeti,agizo hilo ni la Rais Magufuli baada ya kusoma na kutazama taarifa ya Habari baada ya nyumba zilizokuwa zimejengwa kiholela katika eneo la Maisaka A kuwekewa alama ya X iliyosababishwa na uzembe wa idara ya ardhi na mipango miji.

Mnyeti amesema kuwa hati hizo atakabidhi mwenyewe kwa wananchi  tarehe 25 Oktoba mwaka huu na kuwataka wananchi wote ambao bado nyumba zao zina X wakazifute waishi kwa uhuru.

"Kwa Tanzania ukitaka kubomoa waliojenga Kiholela ni asilima 75% serikali imeona iwaache ambao tayari wameshajenga kwa sababu serikali kupitia idara ya Ardhi na Mipango miji  ilishakosea kuwaachia  watu hao kujenga bila kufuata utaratibu” alisema Mnyeti.

Hata hivyo ametoa onyo kwa wanaoendelea kujenga katika maeneo ambayo sio rasmi  huku akitoa onyo kwa waliojenga kwenye milima.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Mkurugenzi Mkuu Wa Shirika La Mpango Wa Chakula Duniani (WFP) Ikulu Jijini

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images