Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wezi dawa za serikali Wabanwa

$
0
0
Serikali imeanzisha mfumo mpya wa kuweka nembo kwenye dawa zinazosambazwa na Bohari ya Dawa (MSD), ili kudhibiti wizi wa dawa za serikali unaofanywa na watumishi wake katika zahanati, vituo vya afya na hospitali.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndungulile, alibainisha hayo katika ziara yake mkoani Mwanza, alipokuwa akikagua bohari za dawa na wodi za wagonjwa katika Hospitali ya DDH wilayani Sengerema.

Serikali tumeanzisha mfumo mpya wa kuweka nembo kwenye dawa zetu ambayo ni (GOT), ili kudhibiti wizi wa dawa za wagonjwa kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali unaofanywa na watumishi wake,” alisema Dk. Ndungulile.

“Serikali tumeanzisha mfumo huo mpya wa kuweka nembo kwenye dawa za tembe na makopo ili kuzuia kuibiwa na kuuzwa katika maduka ya dawa yakiwamo ya watumishi,” alisema zaidi Dk. Ndungulile.

Alisema kama mtu yeyote atabainika akiuza dawa zenye nembo hiyo awe mtumishi wa serikali au binafsi, atakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Akiwa Wilaya ya Sengerema, Naibu Waziri huyo alikagua zahanati ya kijiji cha Nyamizeze na kutoa zawadi ya cheti kutokana ubora wa huduma kwa kuwa na nyota nne.

Zahanati hiyo ilianzishwa mwaka 1964 na ina watumishi sita. Inahudumia vijiji vitatu vyenye wakazi 8,000 wanaotegemea kupata huduma kwenye zahanati hiyo.

LHRC yakosoa wagombea wa upinzani kuenguliwa.....yampinga waziri Lugola suala la kulaza madereva mahabusu

$
0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekosoa utaratibu wa kuengua wagombea udiwani 30 wa vyama vya upinzani katika uchaguzi wa marudio.

Juzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza kuwa wagombea wa udiwani 30 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamepitishwa bila kupingwa baada ya wagombea wa vyama vya upinzani kuenguliwa kwa madai ya kutokidhi vigezo.

Katika taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga, alieleza kuwa kuenguliwa kwa wagombea hao kumewanyima haki ya kushiriki uchaguzi mdogo, huku akidai kuwa hoja zilizotumika kuwaengua hazina mashiko.

"Baadhi ya wagombea hususan wa vyama vya upinzani wameenguliwa katika mchakato wa uteuzi wa wagombea kwa sababu mbalimbali zikiwamo tuhuma za kutokidhi vigezo vya kiufundi, kisheria kwa kutokujua kusoma na kuandika pamoja na vigezo vya kutokuwa raia," Henga alieleza katika taarifa hiyo.

Mkurugenzi huyo alisema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria au utekelezaji wa kazi au shughuli ya mamlaka ya nchi.

“Ikumbukwe nchi yetu ni ya kidemokrasia na inafuata misingi ya mfumo wa nyama vingi tangu mwaka 1992, Sheria ya Vyama vya Siasa imeweka mfumo wa vyama vingi, ni vyema usawa ukazingatiwa pasipo ubaguzi wa aina yoyote ili kuweka mazingira ya uchaguzi kuwa huru na yenye uwazi,” alisema.

Aliongeza kuwa kituo kinaisihi NEC kuzingatia misingi ya demokrasia na kutenda haki katika kusimamia uchaguzi nchini, ikiwa ni pamoja na wananchi na mamlaka za serikali kuheshimu misingi ya kikatiba na kisheria katika kutekeleza majukumu yake.

Henga pia alisema LHRC inapinga vikali kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ya kuagiza askari kuwalaza mahabusu madereva watakaosababisha ajali kutokana na ubovu wa gari.

"Kauli hii inakiuka miongozo ya kikatiba inayoweka misingi ya dhamana pamoja na dhana ya kutokuwa na hatia mpaka pale itakapothibitika kama ilivyoainishwa katika Ibara ya 13(6)(b) ya Katiba," Henga alisema.

Mkurugenzi huyo alisema kitendo hicho kinaweka mazingira magumu kwa mtuhumiwa kufikia haki ya kupata dhamana kama haki ya kikatiba na kusababisha kuchelewa kwa haki au kukosa kabisa haki ya dhamana kwa kuwa haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.

Alisema Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai inaweka bayana taratibu za kuchukua dhidi ya watu wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali na kwamba kwenda kinyume cha utaratibu wa kisheria ni kupuuza utawala wa sheria.

“Kituo hakitosita kumfikisha kiongozi yeyote mahakamani atakayetoa maagizo yanayokiuka misingi ya mikataba ya kimataifa inayolinda haki za binadamu, katiba na sheria za nchi,” alisema.

Henga alisema kituo hicho pia kimeshtushwa na mfululizo wa vitendo na kauli zinazotolewa na viongozi wa serikali zinazokiuka katiba na sheria za nchi.

Alisema kuwa kupitia barua ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mji wa Tunduma mkoani Songwe yenye kumbukumbu namba TTC/01/89/49 kwenda kwa watendaji wa kata wote kuwazuia kutoa barua za kuwawekea dhamana wanaokabiliwa na mashauri ya polisi na mahakamani, inakinzana na haki za binadamu.

Baada Ya Mkwasa Na Sanga Kuachia Ngazi, Uongozi Yanga Watoa Tamko Juu Ya Watakaorithi Nafasi Zao

$
0
0
Baada ya viongozi wa Yanga kuzidi kuachia ngazi akiwemo Kaimu Mwenyekiti wa klabu hiyo jana, Clement Sanga kutangaza kujiuzulu wadhifa wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika, ameitisha kikao na wahabari leo.

Nyika ameitisha kikao hicho kuzungumzia mustakabali mzima wa Yanga juu ya kujaza nafasi za viongozi wake walioachia ngazi namna utakavyokuwa.

Ikumbukwe Yanga imekuwa haina Mwenyekiti kwa muda mrefu tangu kujiuzulu kwa Yusuf Manji akidai anahitaji kupumzika kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi binafsi.

Baada ya Manji, wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji akiwemo Salum Mkemi na Khalfan Hamis nao wameachia ngazi kutokana na kutokuwa na maelewano mazuri baina yao na uongozi wa juu wa klabu.

Kutokana na kujizulu kwao, uongozi wa Yanga kupitia kwa Nyika utaeleza kiunagaubaga leo hatma ya nafasi zao ikiwemo suala la uchaguzi wa kujaza nafasi ya Mwenyikiti pamoja na ile ya Katibu Mkuu.

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
Katika kusherehekea miaka 15 ya kampuni ya NATURAL BEAUTY PROD tunatoa shukrani za dhati sana kwa wateja wetu wote kwa kutuunga mkono miaka yote hiyo.
 
TUNATOA OFFA YA WIKI NZIMA KWA WATEJA WETU UKINUNUA BIDHAA UTAPATA PUNGUZO LA 20%. KWA WATEJA WA MIKOANI UTATUMIWA BURE.

Ni bidhaa salama kabisa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda pia zina matokeo mazuri na kwa haraka zaidi.

🥑🍇🍋🍓🍒🌱🍇🍇
👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @210,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @140,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/=
11.YODI PILLS--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza (hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
GOOGLE
YOU TUBE
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod < WELCOME ALL>

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0



 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 

---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Mashabiki Washangilia Sanga Kujiuzulu Yanga

$
0
0
Kufuatia Kaimu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga kuachia ngazi jana, baadhi ya wadau na wachama wa Yanga wengi wamepongeza uamuzi huo.

Wanachama hao wamekubaliana na maamuzi ya Sanga huku wengi wakieleza ni sahihi kwake kufanya hivyo kutokana na mwenendo mzima wa klabu ulivyo sasa.

Mbali na mwenendo wa klabu, wachama hao wamesema Sanga alikuwa amechelewa wakieleza alipaswa kufanya hivyo mapema ili kuwapa nafasi wengine.

Wengi wao wamefunguka na kueleza Sanga alikuwa haiendeshi Yanga kwa ueledi na kupelekea kuleta kutokuelewana baina yake na viongozi wengine haswa wa kamati ya utendaji waliojiuzulu akiwemo Khalfan Hamis.

Kitendo cha Sanga kuachia ngazi kimewakonga nyonyo wachama hao pamoja na baadhi ya mashabiki kwa maamuzi yake na sasa itabidi ikiwezekana uchaguzi ufanyike ili mbadala wa Mwenyekiti apatikane.

Sanga ameeleza sababu mojawapo iliyompelekea kuachia ngazi ni kushutumiwa na baadhi ya watu akisema walipanga kwenda kuvamia kwake wakiwa na mapanga jambo ambalo ameona linaweza kuhatarisha maisha yake.

Edo Kumwembe Awachana Yanga: “Pesa sio makalio, tujifunze kuheshimu wenye pesa”

$
0
0
Kinacho Trend katika mitandao ya kijamii kwa sasa ni suala la viongozi wa club ya Yanga kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya Yanga na kuiacha timu katika kipindi kigumu, hivyo sintofahamu inazidi kutanda nini itakuwa hatma ya timu hiyo kuelekea msimu wa 2018/19.
 
Kutokana na matatizo na changamoto zinazoendelea katika club hiyo mchambuzi wa masuala ya soka Edo Kumwembe ameandika maneno au ushauri katika ukurasa wake wa instagram ikilenga kuwakosoa wale mashabiki wa soka ambao wanapenda kuwakwaza wafadhili wa timu hizo.
 
“Pesa sio makalio kwamba kila mtu anayo……tujifunze kuheshimu watu wenye pesa..zile kelele za nyakati zile za watu fulani dhidi ya Manji..wakimpinga sana…wengine wakasema “Atuachie Yanga yetu”
 
“Leo ndo muda wao wa kuichukua Yanga yao, wakalipe Kambi, wawalipe akina Yondan na Kessy, washushe akina Kagere wao pale Jangwani Yaani Manji hayupo na hakuna atakayewakataza…yuko wapi yule Mzee? Yuko wapi yule kijana machachari?”
 
“Iliwahi kutokea pale Tanga..watu walimwambia Nassor Binslum awaachie timu yako..wakaishia kushuka na kupoteza dira…Simba iko Uturuki na kuna watu hawamtaki Mo..waambie wamsajili mchezaji mmoja tu kwa shilingi milioni kumi”
 
“Baada ya dakika tano ukiwapigia simu utasikia ‘Namba unayopiga haipatikani’…Pesa sio makalio kwamba kila mtu anayo…nadhani baada ya Yale yanayotokea Jangwani tutaanza kuheshimu wenye pesa…huu sio mpira wa nyakati za Ujamaa kwamba unamnunua Makumbi Juma kwa kumpa feni ya ukutani…tuheshimu wenye pesa!!! Asanteni”

Ali Kiba Asajiliwa Rasmi Kuichezea Coastal Union....Kilichobaki ni Saini Yake Tu

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Coastal Union ya jijini Tanga umethibitisha kutarajia kumsajili msanii wa muziki wa Bongo, Alikiba kwaajili kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Alikiba anayetamba na kibao chake cha Mvumo wa Radi huenda akaanza kuonekana kwenye mechi mbalimbali za ligi kuu kupitia na timu yake ya Coastal Union endapo usajili huo utakamilika.

Kupitia kipindi cha Esports kinacho ruka kwenye radio ya E FM, Mwenyekiti wa klabu ya Coastal Union, Steven Mguto amethibitisha kuwa kwenye mazungumzo na msanii huyo ili kupata huduma yake ya kukipiga katika kikosi cha wagosi hao wa kaya.

"Kiukweli siku zimebaki kidogo lakini na sisi kama zoezi letu limefikia ukingoni nafikiri mpaka kesho tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kueleza nani na nani tumemsajili.

"Kwa sababu kwa sasa ndiyo tunamalizia watu wengine maswala ya mikataba sasa sirahisi kuweza kumtaja mkataba bado haja saini mwisho wasiku anaweza akageuza nia na ikawa kitu kingine.

"Kwa kiasi kidogo kuna ukweli wa kutaka kumsaini Alikiba lakini pia mambo haya jakaa sana sawa lakini wenyewe mnamuona naye ni mchezaji ingawaje si wa kiwango cha juu kwasababu hana mazoezi ya mara kwa mara ya kucheza mpira hivyo kuwa katika mazungumzo ni kweli.

Alikiba ataweza kuisaidia Coastal Union licha ya uchezaji ndani ya uwanja lakini pia ataweza kuibeba klabu hiyo kupitia umaarufu wa staa huyo wa muziki nchini na bara zima la Afrika.

Klabu ya Coastal Union imepanda rasmi ligi kuu mwaka huu baada ya kuiyaga michuano hiyo msimu wa mwaka 2015/16.

Lulu Diva Azungumzia Wimbo wake Mpya wa ONA Ulivyobadili Maisha Yake

$
0
0
Mwanadada Lulu Diva amefunguka na kuelezea mafanikio yake ya muziki tangu alipoanza mpaka alipofikia sasa na kusema kuwa kwa sasa na yeye amekuwa akijiona kuwa ni msanii mkubwa sana kutokana na wimbo wake huu mpya wa sasa hivi.

Lulu diva anasema kuwa wimbo wa ona ambao amemshirikisha Rich Mavoko ambao kwa sasa umekuwa ukifanya vizuri katika vituo mbalimbali vya radio na tv umekuwa moja ya mafanikio yake makubwa na anaona kabisa kuwa kwa sasa amepiga hatua kubwa kutokana na hilo.
 
"Wimbo wa ona umenipeleka kwenye levo nyingine kabisa, kwa sasa mimi ni miongoni mwa wasanii wakubwa ambao kila siku shoo zinazidi kuongezeka tu  na hata hadhi yangu pia."- Anasema Lulu Diva

Diamond Awajia Juu Wanaodai kuwa yeye ni Shoga

$
0
0
Staa wa Muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemwaga povu zito na kuwajia juu watu wote wanaomkosoa na kumuita shoga baada ya kuonekana akiwa amevaa kikuku.

Wiki iliyopita Kuna picha zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii zilizomuonyesha Msanii huyo akiwa amevaa Kikuu Kwenye miguu yake, skendo ambayo ilikamata vilivyo hasa kwenye mitandao ya kijamii na kumjengea picha tofauti kwa  mashabiki wake.
 
Baadhi ya mashabiki hao kwenye mitandao hiyo walikasirishwa na kitendo hicho hivyo kummwagia matusi ya nguoni kutokana na kuchukizwa na kitendo hicho. 

Hoja kuu kutoka kwa mashabiki hao ilikuwa kwamba, jambo hilo haliendani na utamaduni wa Kitanzania na kwamba wanaofanya hivyo ni mashoga na lengo lake ni kuharibu vijana wadogo wa Kitanzania.

Baada ya povu hilo la mashabiki, Global Publishers walimsaka Diamond ili kusikia anajiteteaje juu ya skendo hiyo ya ushoga:

"Kwanza sijui kama kile ni kikuku, nilivaa kama ninavyovaa mikufu au cheni. Niliona ni urembo kama urembo mwingine na kwamba haiwezi kuwa ishu kubwa kama ilivyotokea”.

Diamond aliwakemea wanaomuita Shoga na kuwataka waache mara moja kwani yeye mwenyewe anachukizwa na tabia za mashoga:

"Ninawaomba chondechonde waache kunihusisha na jambo hilo baya, ujue nyuma yangu kuna watu wengi mno wanatamani kuwa kama mimi hasa vijana wadogo.

“Sasa wakiona ninahusishwa na jambo ambalo linapigwa vita nchini mwetu, wataacha kunifuatilia kama mtu wanayetamani kuwa kamawao," alisema Diamond na kuongeza: "Lakini unajua imekuwa ni kasumba kwa watu maarufu kuhusishwa na jambo hilo ili kuwajengea picha fulani kwa mashabikia”.

Faiza Ally Amtolea Povu Zito Sugu.....Acha Dharau, Siwezi kufuata hela ya matumizi ya Mtoto Mlimani City

$
0
0
Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Faiza Ally amemjia juu mzazi mwenzake ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini na msanii mkongwe wa Bongo fleva Sugu.

Sugu na Faiza wamezaa mtoto mmoja anayeitwa Sasha lakini wamekuwa kwenye mgogoro wa kifamilia kwa muda mrefu sana ambapo Faiza amekuwa akidai kuwa Sugu anagoma kumlea mtoto.
 
Wawili hao walionekana kumaliza tofauti zao mwezi uliopita baada ya Sugu kutoka jela ambapo Faiza aliandika Kwenye mitandao ya kijamii kuwa yeye na Sugu wamemaliza tofauti zao.

Lakini Faiza amemtolea povu Tena Sugu jana ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika:

“Natuma barua kwako kwa sababu sehemu pekee ya kukufikishia ujumbe ukaupata ni hapa ni hivi toka tumeachana sasha ana mwaka na miezi 6 mpaka leo hujatafuta namna sahihi ya kumtunza mwanao sasa tafuta njia sahihi na yenye heshima mimi sio wa kufanyia shopping na happy eti nikachukue mlimani 😂😂😂”

“Hiyo ni zarau sana baba kama ulikosa muda ungetuma hela ! Lazima uweke heshima kwa baby mama wako na mwanao! sasa ni hivi siwezi kwenda kuchukua sukari na maziwa mlimani ni DHARAU!!!!!!” 

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Madini Ya Tanzanite Yakamatwa Kwenye Unga

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa  Manyara, limewatia mbaroni watu watatu wakazi wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro kwa tuhuma za kukutwa na kilo 7.53 za madini ya Tanzanite waliyokuwa wameyaficha chini ya unga uliokuwa kwenye ndoo.

Akizungumzia na waandishi wa habari jana kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Zephania Chaula alisema tukio hilo lilitokea juzi jioni wakati wa upekuzi uliokuwa ukifanywa na maofisa madini, usalama wa taifa na polisi katika lango la kuingilia ndani ya ukuta unaozungumka migodi ya Tanzania.

Chaula alisema wakati wa upekuzi watu hao watatu walibainika kuficha madini hayo kwenye ndoo iliyokuwa na unga.

Alisema mwanamke aliyekamatwa akiwa na ndoo hiyo mkononi anajishughulisha na kazi ya kuchekecha mchanga na udalali wa madini.

“Madini waliyaficha kwenye ndoo iliyokuwa imewekwa unga wa mahindi,” alisema Chaula

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Judith Paulo, Midumbi Ojijo na Joshua Aguta.

Alipoulizwa kuhusu thamani ya madini hayo alisema bado haijajulikana na watuhumiwa wanashikiliwa na polisi katika kituo cha Mirerani kwa mahojiano zaidi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Augustino Senga jana alithibitisha  kukamatwa kwa wahumiwa hao  na kwamba bado wanashikiliwa na polisi kwa uchunguzi.

Viwanja Vinauzwa..............Surveyed plots for sale: Mapinga (Baobab Sec, km 5 kutoka Bunju-DSM)

$
0
0
Surveyed plots for sale: Mapinga (Baobab Sec, km 5 kutoka Bunju-DSM).
 
Viwanja ni vikubwa sana (low density plots). Viwanja viko umbali wa km 2 kutoka main road (Bagamoyo Road).
Ziko plots za sqm 1400, sqm 2100, na sqm 2700.
Bei ya kila sqm ni sh 13,000 (negotiable)
 
Huduma za kijamii (maji, umeme) zipo na miundombinu yote iko vizuri (mradi wa kusogeza lami mpaka nyumbani umeanza). Ramani zote (Town plan & Deed plan) zipo tayari. Hati ya miaka 99 itapatikana ndani ya miezi 2 tu.
 
Hakuna dalali, contact mhusika: 0758603077
Pia, vipo viwanja vya bei nafuu sana ambavyo taratibu za upimaji zimeanza lakini bado hazijakamilika (on-process). Hivi viko Kimele, ni kilometa 3 kutoka main road (Bagamoyo Road). Viwanja viko planned (kwa mpangilio mzuri) na ukinunua unapimiwa ili upate hati kwa gharama ya sh 300,000 tu.
 
Bei ya viwanja inabadilika kuendana na size ya kiwanja ulichochagua.
Bei ni: milion 2 for 10/20, mil 3 for 15/20, mil 4 for 20/20, mil 5 for 25/20, mil 6 for 20/30, mil 8 for 20/40, mil 11 for 25/45, mil 12 for 30/40 na mil 16 for 40/40, mil 20 for 0.5acre, mil 38 for 1 acre. 

Ruksa kulipa kwa awamu ndani ya miezi 3-4.
 
Hakuna dalali, mpigie mhusika,0758603077

Mahakama, TLS Wakubaliana Kushirikiana

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Fatma Karume na viongozi wengine wamekutana na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Profesa Ibrahimu Juma na kuelezwa mpango mkakati ambao ndiyo dira ya mahakama.

Uongozi huo wa TLS umekutana na Jaji Mkuu na wadau wengine wa mahakama leo Jumanne Julai 24, ambapo Msajili Mkuu wa Mahakama, Catherine Revocati pamoja na mambo mengine amesema hiyo ni fursa ya kuanza kushirikiana.

“Mpango mkakati ndiyo dira ya mahakama, tunaomba ushirikiano katika eneo la Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama),  lazima tubadilike, twende dunia inavyokwenda, tuachane na matumizi ya karatasi.

“Mawakili ni wadau wetu muhimu, bila wao sisi hatuwezi kufanya kazi, na wao bila sisi hawawezi kufanya kazi, tulianza nao, wameanza kujiandikisha katika mfumo mpya, tunaomba muendelee kutupigia debe waendelee kujiandikisha,” amesema Revocati.

Kwa upande wake Rais wa TLS, Fatma amesema mahakama haiwezi kuboresha mazingira ya utoaji haki katika maamuzi kama hawatazungumza na TLS.

Leseni FEKI 878 Za Madereva Zakamatwa

$
0
0
Jumla ya leseni 878 kati ya 73,904 za magari mbalimbali madereva wake wamebainika kuzitumia daraja lisilostahiki.

Leseni hizo ni zile zilizokaguliwa kuanzia Julai 4 hadi 15, mwaka huu katika ukaguzi maalumu uliofanywa wa kukagua leseni hizo.

Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Musilimu amesema hayo jijini Dar es Salaam leo Jumanne Julai 24.

“Kwa madereva wote watakaobainika kuendesha magari bila leseni stahiki kulingana na magari wanayoendesha, watakamatwa na kufikishwa mahakamani na leseni zao zitafungiwa kwa kigezo cha kukosa sifa ya kuendesha magari hayo,” amesema.

Aidha, Kamanda Musilimu ametoa muda wa wiki moja kwa madereva wanaodaiwa na mfumo wa Usimamizi wa Trafiki kulipa madeni yao yote.

Amesema baada ya muda huo uliotolewa kupita wataanza msako nchi nzima kukamata madereva wanaodaiwa na kuwapeleka mahakamani na gari zao zitazuiliwa. 

Kamanda Musilimu pia amesisitiza kuwachukulia hatua abiria wanaowashawishi madereva kuongeza mwendo wa gari wawapo safarini.

“Abiria watakaochochea ajali za barabarani kwa kuwaambia madereva waongeze mwendo watachukuliwa hatua, inapaswa abiria kutoa taarifa waonapo uvunjwaji wa sheria,” amesema. 

Pamoja na mambo mengine, amesema Agosti Mosi mwaka huu, askari wa usalama barabarani watafanya uhakiki wa kina wa leseni za madereva kwa madereva wa magari ya abiria, mizigo, magari binafsi, pikipiki na magari ya serikali nchi nzima.

“Tutakuwa na fomu husika kwa ajili ya uhakiki wa leseni za madereva fomu hizi zitakaa katika vituo vya daladala (stendi) na katika vituo vya mizani hii itapunguza kurudia rudia ukaguzi wa leseni kwa madereva,” amesema.

Je Umepungukiwa Nguvu Za Kiume Na Umetumia Dawa Nyingi Bila Mafanikio?

$
0
0
Hakika nawashukuru wote mliotumia hii dawa na kunipa pongezi nyingi Sana sasa offa imeisha maana nilitoa ya wiki 2 tu     na watu wengi walioitumia wamepona kabisa 

Dawa hii ni dawa ya maajabu kabisa na huwezi kuamini ila wengi walioitumia wameiamini maana kati ya watu 89 walioitumia ndani ya wiki 2 watu76 wamepona kabisa na watu 9 hawajapona na watu 4 hawajatoa majibu! 

Dawa hii ni dawa inayotibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na unapona kabisa, dawa hii ni dawa ya asili,(mitishamba) utaitumia mara moja tu na hautatumia dawa ya nguvu za kiume tena 

Dawa hii inawafaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70, zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ....watafiti wa dawa asilia pamoja na waganga  wameikubali pia dawa hii inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi 

Ukitumia hii dawa unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha, inauwezo wa ajabu na tiba bora kabisa

 SOMA DALILI HIZI;  kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa 2 .kushindwa kurudia tendo la ndoa 3. kuwahi kufika kileleni 

Dawa hii imesaidia watu wengi sana dawa hii imegunduliwa na dr kiboko mganga wa tiba za jadi kutoka mafia pia tunatibu matatizo mbalimbali kama mambo ya biashara, nyota, kesi, mapenzi, nk, pia tunahitaji WAKALA wa kupokea dawa zetu katka nchi ya KENYA, ZAMBIA, UGANDA, mikoani tunatuma kwanjia ya mabasi au fika ofisini kwangu  Mafia kisiwani  

maelezo zaidi wasiliana na DR KIBOKO 0679923297

Salamu za Pongezi za Mhe. Rais Magufuli kwa Rais Filipe Nyusi na Wananchi wa Msumbiji.

$
0
0
Rais John Magufuli ametuma salamu za pongezi kwa Rais wa Msumbiji, Filipe Nyusi  wanachama wa Frelimo na wananchi  wa nchi hiyo ambao kesho Jumatano Julai 25, 3018 wanaadhimisha miaka 50 ya mkutano wa pili wa chama hicho.

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne Julai 24, 2018 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa inasema katika sherehe hizo zitakazofanyika Matchedje katika jimbo la Niassa, Rais Magufuli atawakilishwa na Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na makamu mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula.

Katika salamu zake, Magufuli amewatakia heri wananchi wote wa Msumbiji na kuwapongeza kwa mafanikio waliyoyapata ikiwemo kudumisha uhuru wao.

Amesema Tanzania inajivunia uhusiano, historia na ujirani mwema na nchi hiyo.

“Kwa niaba ya Serikali, CCM na watanzania wote naungana nawe (Nyusi) na wananchi wote wa Msumbiji katika kusherehekea siku hii muhimu,” amesema Rais Magufuli.

“Siku hii inatukumbusha jukumu muhimu tulilonalo la kuulinda na kuutetea uhuru ambao waasisi wa mataifa yetu Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania na Samora Machel wa Msumbiji waliupigania.”

Rais Magufuli amemhakikishia Nyusi kuwa Tanzania  itaendelea kudumisha na kukuza uhusiano wake na Msumbiji katika ngazi ya Serikali na vyama vya CCM na Frelimo, kuimarisha ushirikiano hasa katika masuala ya uchumi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images