Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bucha bubu za mbuzi Zaitesa Halmashauri ya Mji wa Kahama

$
0
0
Na Magdalena Kashindye
Kuwepo kwa bucha bubu za mbuzi katika halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga imekuwa  ikiisababishia hasara katika halmashauri hiyo kutokana na baadhi ya watu kuchinja  mbuzi mtaani na nyumbani kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Mifugo wa halmashauri ya mji wa Kahama Costantine Lugendo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake.

Lugendo amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa uchinjwaji wa mbuzi  umekuwa ukidorora kutoka mbuzi 60 na kufikia mbuzi 20 pekee kwa siku katika machinjio rasmi lakini upatikanaji wa nyama hiyo umekuwa ukiongezeka mtaani.

 Afisa mifugo huyo amekili  kuwa kuna tabia kwa baadhi ya watu wamekuwa wakichinja mbuzi  mtaani au nyumbani na kupeleka kwenye migahawa kuuza nyama  kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.

Bwana Lugendo amesema kuwa idara Ya mifugo inafanya mkakati wa kuweka askari watakaofanya doria ya kuwakamata watu wanaochinja mifugo  mtaani kwa ajili ya nyama ya kuuza  ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Hata hivyo Lugendo amesema kuwa uchinjaji  na  uuzaji wa nyama  ovyo bila kukaguliwa na maafisa mifugo  ni hatari kwa afya ya Mlaji kwani haijulikani imechinjwa katika mazingira gani huku pia halmashauri kushindwa kupata mapato ya mifugo.

Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania imefanya utaratibu maalum wa uchinjaji wa mifugo katika machinjio  maalum yaliyorasimishwa na serikali  ili kulinda afya ya mlaji.


Waziri wa Kilimo Dk Charles Tizeba Awavaa Watafiti wa Kilimo

$
0
0
Waziri wa Kilimo Dk Charles Tizeba amewataka watafiti wa Kilimo kupeleka matokeo ya utafiti wanaoufanya kwa wakulima wanaowazunguka.

Ametoa kauli hiyo jana Ijumaa Julai 20, 2018 katika maonyesho ya Kilimo cha biashara jijini Arusha.

Amesema kwa muda mrefu watafiti wa kilimo wanajifungia na tafiti zao huku jamii iliyowazunguka ikzalisha mazao machache.

"Bahati mbaya hakuna uhusiano kati ya watafiti na wakulima. Watafiti wanafanya kivyao na wakulima kivyao," alisema Dk Tizeba.

“Kuna kituo cha utafiti cha Seliani lakini ukienda King'ori tu hapo, hoi. Utakuta kuna mkulima yuko nje ya wigo wa taasisi miaka 30, anacholima ni tofauti kabisa. Kuna kituo cha utafiti wa kahawa (Tacri) lakini wakulima wa kahawa wanalia.”

Amewataka watafiti kubadilisha mtazamo na kuacha kujifungia na tafiti zao.

"Kuna mahindi lishe hapa, yapo miaka tisa nani anajua? Msipobadilisha mtazamo tutabaki na maprofesa wenye vyeti tu," alisema.

Amevitaka vituo vya utafiti kufanya biashara ya mazao wanayozalisha badala ya kusubiri kupata fedha za Serikali kujiendesha.

Habarika Masaa 24......Pakua Upya Application Yetu Tukuhabarishe Usiku na Mchana

$
0
0
==>Pakua Upya Application yetu tukuhabarishe masaa 24 usiku na mchana.

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia;

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Rais Magufulu Atoa Pole Kwa Rais Mstaafu Kikwete Kwa Kufiwa Na Baba Mzazi Wa Mkewe Mama Salma Kikwete

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018

 Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama salma Kikwete, kwa kufiwa na baba yake mzazi Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete na wanafamilia wakiomba dua walipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mama Janeth Magufuli wakiagana na mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Mama Salma Kikwete baada da ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na ndugu wa  Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete baada da ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  wa Mama Salma, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mama Janeth Magufuli wakisindikizwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete baada ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  Mama Salma, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018. Picha na IKULU

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yateua madiwani wanane viti maalum

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeteua madiwani wanane wa Viti maalum wa CCM na Chadema kujaza nafasi zilizoachwa wazi.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Julai 21, 2018  na mwenyekiti wa NEC  Jaji Semistocles Kaijage inaeleza kuwa uteuzi huo umefanyika katika kikao cha tume hiyo cha Julai 19, 2018.

Walioteuliwa ni Rajabu Kalinga (CCM-Songea), Mary Mbilinyi (CCM-Makete), Zainab  Mabrouk (CCM-Kongwa).

Restuta Gardian (CCM-Muleba), Siglinda Ngwega (CCM-Morogoro), Zena Luzwilo (CCM-mji Kahama), Neema Massawe (Chadema-Monduli) na Teodola Kalungwana (Chadema-Iringa).

 “Uteuzi huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya Serikali za mitaa ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa,” imesema taarifa hiyo.

Imesema nafasi hizo za madiwani ni za Chadema na CCM, baada ya walioteuliwa awali kufariki dunia na kujiuzulu.

Mbowe na Wenzake Wakwama Mahakama Kuu....Wakili Wao Kukata Rufaa

$
0
0
Mahakama  Kuu  ya Tanzania imetupilia mbali maombi yaliyowasilishwa na viongozi tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ya  kupitia, kuitisha na  kuchunguza kumbukumbu za mwenendo wa kesi namba 112, iliyofunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ili kujiridhisha na usahihi na uhalali wa amri zilizotolewa.

Shauri hilo lilisikilizwa na Jaji Rehema Sameji, huku upande wa waleta maombi (Chadema) ukiwakilishwa na mawakili Peter Kibatala, huku upande wa wajibu maombi (serikali) ukisimamiwa na mawakili, Paul Kadushi, Faraja Nchimbi na Wankyo Simon.

Viongozi waliofungua shauri hilo ni Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk. Vincent Mashinji na Manaibu wake, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Wengine ni Mchungaji Peter Msigwa, ambaye ni Mbunge wa Iringa Mjini, Esther Matiko (Mweka Hazina wa Bawacha), Halima Mdee (Mbunge, Kawe), John Heche (Mbunge, Tarime Vijijini) na Ester Bulaya (Mbunge, Bunda).

Akisoma uamuzi huo mahakamani hapo jana, Jaji Sameji alisema, amepitia hoja zilizowasilishwa na waleta maombi (Chadema) na kubaini kuwa, kifungu namba 372 kilichowasilishwa mahakamani hapo kina utata, hali iliyosababisha mahakama kujikuta kwenye wakati mgumu.

Alisema kwa kuwa shauri la msingi bado linaendelea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kwamba sheria inakataza maombi madogo kuombewa marejeo kwenye mahakama hiyo, jambo hilo limewafanya wasiwe na mamlaka ya kusikiliza maombi hayo.

Alisema kutokana na hali hiyo, ameamua kutupilia mbali maombi hayo na kuwataka waleta maombi (Chadema) kufungua rufaa ikiwa hawajaridhika na uamuzi huo.

“Mahakama imeamua kutupilia mbali maombi yaliyowasilishwa na viongozi wa Chadema, wakiiomba Mahakama Kuu kupitia, kuitisha na kuchunguza kumbukumbu za mwenendo wa kesi namba 112, iliyofunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa sababu haina mamlaka ya kisheria kufanya hivyo wakati shauri bado linaendelea Mahakama ya Kisutu,” alisema Jaji Sameji.

Hata hivyo, mawakili wa waleta maombi (Chadema) tayari wamewasilisha notisi ya kukata rufaa Mahakama ya Rufaa, wakipinga uamuzi huo.

Katika shauri hilo, viongozi wa Chadema, walifungua maombi Mahakama Kuu ya kuiomba mahakama hiyo kupitia mwenendo wa kesi ya jinai inayowakabili viongozi hao, iliyopo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Katika kesi ya msingi namba 112 ya mwaka 2018, viongozi hao walisomewa mashtaka 13, yakiwamo kufanya mikusanyiko, vurugu na maandamano yasiyo halali na kusababisha kifo cha aliyekuwa Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.

Viongozi hao wanadaiwa kutenda makosa hayo Februari 16, mwaka huu, katika Barabara ya Kawawa, eneo la Kinondoni Mkwajuni.

Madiwani Watatu CHADEMA Wavuliwa Uanachama

$
0
0
Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Mbeya umependekeza kuvuliwa uanachama kwa madiwani watatu wa chama hicho mkoani humo kutokana na utovu wa nidhamu waliouonyesha.

Madiwani hao na kata zao katika mabano ni Geofrey Kajigili (Sisimba), Newton Mwatuboje (Manga)na Hamphrey Ngalawa (Iwambi).

Mwenyekiti wa Chadema Mbeya Mjini, Obadia Mwaipalu ametangaza uamuzi huo leo Jumamosi  Julai 21, 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari na kubainisha kuwa  vikao halali vya chama vilivyoketi mara kadhaa kujadili hatua stahiki dhidi ya madiwani vimefikia uamuzi huo.

Amesema kutokana na utovu wa nidhamu, kukiuka katiba ya Chadema na kukaidi utekelezaji wa maazimio ya uongozi wamepeleka mapendekezo yao kwa uongozi wa chama hicho Kanda ya Nyasa ili  hatua zichukuliwe.

Lugola Ampa Maagizo Mazito IGP Sirro Kuhusu Sakata la Lugumi.......Pia Kamtaka Kaimu Mkurugenzi Mkuu NIDA Kufika Ofisini Kwake July 25

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Simon Sirro kumpeleka ofisini kwake mmiliki wa kampuni ya Lugumi, Said Lugumi.

Amesema Lugumi anatakiwa kufika katika ofisi yake iliyopo mjini Dodoma Julai 31, 2018 saa 2 asubuhi.

“Waliopita hawakuwa maninja sasa ameingia ninja namtaka Lugumi aje muda ukifika tutawaambia Watanzania,” amesema.

Waziri Lugola ametoa kauli hiyo leo  mbele ya waandishi wa habari alipokuwa akitoa tathmini ya ziara aliyoifanya kuanzia Julai 11, 2018  kwenye taasisi mbalimbali zilizo chini ya wizara yake.

Pia amemuagiza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida),  Andrew Massawe kufika ofisini kwake Julai 25, 2018 mjini Dodoma akiwa na mtambo wa kutengeneza vitambulisho vyaTaifa au kampuni ikiwa na fedha hizo.

Amesema kuna kampuni iliyopewa jukumu la kuleta mtambo kwa ajili ya vitambulisho hivyo  na muda umeisha bila mtambo huo kuonekana.

“Afike ofisini kwangu mjini Dodoma pamoja na watu waliopewa tenda hiyo waje na mtambo au fedha hizo kiasi cha Sh32 bilioni,”amesema Lugola.

Amesema watu hao kama hawana fedha  au mtambo basi wawe na maelezo yatakayojitosheleza kwa nini mtambo huo haujawasili hadi leo.

Zahanati Yateketea Kwa Moto....Mtendaji wa Kijiji Mbaroni Kwa Mahojiano

$
0
0
Watu watano akiwamo ofisa mtendaji wa kijiji cha Ulaya, wilayani Igunga mkoani hapa,  Zablon Hussin wanashikiliwa polisi kwa mahojiano wakihusishwa na tukio la jengo la zahanati ya kijiji hicho kuungua moto.

Jengo hilo liliungua moto usiku wa Julai 14, 2018 na kusababisha hasara ya zaidi ya Sh85 milioni.

Akizungumza na wanahabari leo Jumamosi Julai 21, 2018  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema majina ya watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa yanahifadhiwa kuepuka kuharibu upelelezi.

"Wakati moto huo unazuka, zahanati ile haikuwa na mlinzi na tayari tumetoa maelekezo kwa viongozi wa Serikali za mitaani kuhakikisha maeneo yote ya umma yanakuwa na ulinzi," amesema Kamanda Nley.

Kaimu Mganga Mkuu wilaya ya Igunga, Dk Bonaventura Kalumbete amesema moto huo pia umeteketeza dawa na vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Sh25 milioni.

Dk Kalumbete amesema juhudi zinaendelea kutafuta jengo jingine ili litumike kwa ajili ya huduma wakati mchakato wa ukarabati zahanati iliyoungua ukiendelea.

Makamu Wa Rais Awasili Mkoani Songwe Leo

Lugola Awataka Wakimbizi Kurejea Kwao......Pia Katoa Maagizo Kuhusu Wafungwa Kujilisha, Simu Gerezani na Swala la Ajali Nchini

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ametoa maagizo kadhaa kwa idara mbalimba zilizopo chini yake kuhakikisha wanayatekeleza kwa maslahi ya nchi.

Ametoa maagizo hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anatoa tathimini ya ziara yake aliyoifanya katika vyombo vya vyote vya ulinzi na usalama na idara zote za wizara hiyo.

Amefafanua katika ziara yake aliyoianza Julai 11 mwaka huu yako mambo ambayo ameyabaini na hivyo ameona haja ya kuyaeleza kwa mustakabali wa ustawi wa Taifa kwa ujumla.

“Miongoni mwa mambo ambayo nimeelekezwa na Rais Dk.John Magufuli ni kuhakikisha anasimamia suala la Magereza kujitosheleza kwa chakula.

“Hivyo nimeagiza Jeshi la Magereza nchini kuwasilisha mkakati madhubuti na unaotekelezeka wa kujitosheleza kwa chakula ili kuipunguzia Serikali mzigo wa kulisha wafungwa,”amesema.

Akifafanua katika hilo amesema kuwa kama mkakati huo kutakuwa na kipengele kinachoweka vikwazo kwa wafungwa kutofanya kazi za kuzalisha basi katika Bunge la Septemba wataanza kwa kuweka kipengele ambacho kinaelekeza wafungwa kufanya shughuli za uzalishaji chakula.

“Mbona walioko majumbani wanalima kwa ajili ya kupata chakula kwanini waliko magerezani wasilime chakula kwa ajili yao na ikiwezekana kupata na ziada kwa ajili ya kulisha maeneo mengine,”amesema.

Wakati huo huo Lugola amesema ili kukomesha vitendo vya kuingiza vitu hatarishi magerezani ikiwemo simu za mkononi tayari ametoa maagizo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza kusimamia kikamilifu nidhamu ya askari wake wenye wajibu mkubwa katika kukomesha vitendo hivyo vya kihalifu.

“Katika kikao changu na maofisa wa Magereza , nimezungumza na CGP kuwa gereza lolote ambalo linapatikana na matukio hayo Mkuu wa Gereza awatajibika.

Pia Waziri Lugola amesema katika utatuzi wa ajali za barabarani ambazo zimekuwa tatizo kubwa kwa kupoteza maisha ya Watanzania na kuacha majeruhi amesema tayari amevunja baraza la Taifa la Usalama barabarani na kamati zake za mikoa na wilaya ili kuanza upya.

“Kabla ya mwisho wa mwezi huu nitakuwa nimeshaunda baraza jipya.Aidha nimeagiza Jeshi la Polisi nchini kuongeza juhudi katika usimamizi wa Sheria ya usalama barabarani na ukaguzi wa magari ili kudhibiti ajali.

“Hatua kali zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kutotii sheria za usalama barabarani na kuendesha magari mabovu yanayosababisha ajali na kusababisha vifo,”amesema.

Aidha amesema amesema kumekuwepo na kero ya muda mrefu ya askari na watumishi raia kutobalishiwa mishahara baada ya kupandishwa vyeo.

“Nimewaagiza wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama na idara zote ndani ya Wizara hii ifikapo mwisho wa Agosti kero zote ziwe zimetatuliwa na asiwepo askari wala raia ambaye analipwa mshahara tofauti na cheo chake au kutolipwa mashahara kabisa,”amesema.

Wakati huohuo Waziri Lugola amesema ametoa maagizo kwa Idara ya Huduma za Wakimbizi kuongeza kasi ya kurejesha wakimbizi wa Burundi kwani hali ya amani kwenye nchi hiyo imerejea.

Pia ametoa maagizo kuhakikisha wakimbizi wote wasioishi kambini warejeshwe kambini mara moja

Pia Waziri Lugola amesema kwa suala la usalama wa raia na mali zao ni jambo muhimu kwa Watanzania ambao wanahitaji kufanya kazi saa 24 ili kuendana na azma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati.

Amesema tayari ametoa maelekezo kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini kuwalisha mkakati wa kuimarisha usalam ili watanzania waweze kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii kwa saa 24 wakiwa na uhakika na usalama wao na mali zao.

“Hatuwezi kupewa amri , maelekezo na ratiba za kazi zetu na wahalifu.Gari inatoka Kagera  na kasha inapita Mwanza eti ikifika Morogoro inaambiwa haitakiwi kusafiri usiku kwasababu ya kufohia usalama.Hii haiwezekani.Tutakaa na wadau wa usafiri ili nao utapate maoni yao na kasha tutaamua,”amesema.

Viwanja Salama Kwa Makazi Vinauzwa kwa Bei Nzuri....Changamkia Fursa

$
0
0
Tunauza Viwanja Ukuni Bagamoyo kituo kimoja kabla ya Bagamoyo town..... sqm 1200 Tsh million 15 umbali meters 400 kutoka Bagamoyo road,M Mapinga sqm 700,800 hadi 1000 Tsh Bei Tsh 1300 per sqm.

Buyuni chanika sqm 997 block 10 plot 81 Tsh million 12,k Ina hati tayari,M Mwasonga Kigamboni vipo kuanzia sqm 500 hadi 1000 Bei Tsh 700 Kwa sqm

Mapinga sqm 2197 Bei Tsh 14000 per sqm na sqm 2723 Bei Tsh 14000 per sqm, unaingilia njia ya Baobab Maongezi yapo, karibu na mtaa wa block Street,uliojengwa kisasa,.

Pia km tatu kutoka Bunju sokoni kuna 20/40 million 9, na 20 / 25 mil 6 na 20 / 45 Bei million 10 .5 , kuna view nzuri ya Bunju masait na Mabwe pande
 
Pia Kijiji kizuri cha Amani upepo mwingi km 5 kutoka baharini kuna 20/40 Bei Tsh million 8 njia unaingilia Mapinga kuelekea baharini yan kulia.

Mawasiliano: 0677705808

Lugola: Achaneni na Mbwa Aliyepotea, Tuliachie Jeshi la Polisi Lifanye Uchunguzi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ameitaka jamii ya kitanzania hususani waandishi wa habari kuacha kufuatilia tukio la kupotea mbwa wa Jeshi la Polisi anayejulikana kwa jina la Hobby, kwa kuwa jambo hilo kwa sasa lipo chini ya uchunguzi.

Waziri Lugola ametoa kauli hiyo leo Julai 21, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara yake katika vyombo vya Ulinzi ambavyo vipo chini ya Wizara  yake na kubaini changamoto na madudu mbalimbali yaliyokuwa yakifanywa na askari hao kwenye maeneo yao ya kazi.

“Nimekubaliana na Ispekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro jana Julai 20, 2018 kwamba waingie kwa undani sana kufanya uchunguzi wa nini kimetokea kwenye kikosi hicho halafu baadae wanipe taarifa. Kwa hiyo jambo hili sasa linaenda kufanyiwa kazi na Inspekta Jenerali wa Polisi”,amesema Waziri Lugola.

Pamoja na hayo, Waziri Lugola ameendelea kwa kusema “na nyinyi wanahabari kwa kuwa jambo hili linaenda kufanyiwa uchunguzi naomba sasa tuache kufuatilia jambo hili ili chombo husika kiweze kuchunguza halafu tuone nini cha kufanya”.

Julai 19, 2018, Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola alibaini upotevu wa mbwa huyo wakati alipokuwa kwenye ziara yake katika Kikosi cha Farasi na Mbwa kilichopo eneo la Bandari Jijini Dar es Salaam na kumuagiza IGP Sirro kutoa maelezo ya upotevu wa mbwa.

Mbali na hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewaonya wananchi kuacha tabia ya kupotosha taarifa na matamko yake ambayo anayatoa kwenda sehemu husika.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya July 22

Waziri Mkuu Majaliwa Ampokea Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Korea

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amempokea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Lee Nak-yon ambaye amewasili nchini jana  saa 12:30 jioni (Jumamosi, Julai 21, 2018) kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.

Kwenye uwanja wa ndege, Waziri Mkuu huyo wa Jamhuri ya Korea alipokelewa pia na Waziri wa Mambo ya Nje, Dk. Augustine Mahiga, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Isack Kamwele, Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Eng. Stella Manyanya na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Waziri Mkuu Lee Nak-yon anatembelea Tanzania ikiwa ni hatua ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili. Hii ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa ngazi ya juu wa nchi hiyo kufanya ziara ya kiserikali tangu nchi hizo zianzishe mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1992.

Pia ameambatana na ujumbe wa maafisa wa Serikali, wabunge na wafanyabiashara wakubwa ambao watashiriki Kongamano la Kibiashara baina ya Korea na Tanzania (Korea-Tanzania Business Forum) lililopangwa kufanyika kesho  (Jumatatu, Julai 23, 2018) kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Leo, Jumapili, Julai 22, 2018, Waziri Mkuu Lee Nak Yon atakuwa na mazungumzo rasmi ya kiserikali na mwenyeji wake pamoja na viongozi kadhaa wa Serikali na pia kwa pamoja watashuhudia uwekaji saini mkataba wa kuondoa hitaji la viza kwa watu wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na za utumishi (diplomatic and service  passports).

Pia ataenda Ikulu kumsalimia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, atatembelea Makumbusho ya Taifa, Hospitali ya Mnazi Mmoja na kituo cha utunzaji taarifa cha NIDA kilichopo Kibaha.

Anatarajiwa kuondoka nchini Jumatatu jioni, Julai 23, 2018.

Uteuzi Mwingine Uliofanywa na Rais Magufuli

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Kamuagiza RPC kuwachukulia hatua mkuu wa kituo Kwa Rushwa

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amemtaka Kamanda wa Polisi mkoani humo kumchukulia hatua za kinidhamu Mkuu wa Kituo cha Polisi Mwanga na askari wa kituo kidogo cha polisi  Nyumba ya Mungu na Lang'ata wilayani kutokana na tuhuma za rushwa dhidi yao.

Mghwira ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,ametoa agizo hilo jana  Julai 21,wakati akizungumza kwenye mkutano wa Hadhara katika Kata ya Lang'ata,Wilaya ya Mwanga.

Katika Mkutano huo ambao, uliohudhuriwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,  Humphrey Polepole, na viongozi wengine wa chama na serikali,Mghwira alisema Askari hao wamekiuka taratibu na kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa,hatua ambayo imekuwa kikwazo kikubwa katika jitihada za kudhibiti uvuvi haramu katika Bwawa la Nyumba ya Mungu.

Alisema Askari hao wamejianzishia vituo vyao vya ushuru na kuanza kukusanya mapato yatokanayo na uvuvi haramu katika Bwawa la Nyumba ya Mungu,ambalo lilifungwa baada ya kukithiri kwa uvuvi haramu na samaki kupotea.

"Naomba niseme Askari wa Lang'ata na Nyumba ya Mungu mmenikwaza,kwani kituo chenu kipo juu na mtu hata awe mfupi kunizidi anaweza kuona mazingira yote ya Bwawa na kuona wavuvi haramu,lakini wao huwa hawawaoni,  hii ni hatari sana,naomba RPC uwaondoe mara moja na kuwachukulia hatua,"alisema Mghwira.

Mkuu huyo ambaye alitangaza kulifunga Bwawa la Nyumba ya Mungu kwa Muda,alisema serikali ilikuwa na nia njema kulifunga Bwawa hilo,lakini Askari wamepoteza malengo ya serikali na kukwamisha mpango  wa kuacha samaki wawe wakubwa.

Akizungumza katika kikao hicho, Polepole alisema serikali haitawavumilia askari au watendaji watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na kuchafua utendaji mzuri wa Serikali ya awamu ya Tano.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images