Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

OMBI LANGU; kwanza naomba radhi kwa watu wanaofika kwenye ofisi yangu na kuchelewa kupata huduma kutokana na foleni ya watu wengi kuja pia pongezi nyingi nimepata kutokana na mafanikio makubwa wanayoyapata baada ya kutumia hii dawa ombi langu naomba upige cm nikuelekeze hii dawa hapohapo kuepuka usumbufu na kuokoa mda wako asante

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Serikali Kutovivumilia Vyuo Vitakavyotoa Mafunzo Kinyume Na Utaratibu

$
0
0
Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), kutovibembeleza vyuo visivyo na sifa, badala yake ivichukulie hatua kali ikiwamo kuvifungia.

Pia ameitaka kuhakiki kwa makini vyuo vikuu vyote na kuvichukulia hatua vitakavyobainika kukiuka utaratibu wa utoaji wa elimu.
 
Hata hivyo, wadau wa elimu waliozungumzia hatua hiyo wamesema imechelewa kuchukuliwa kwani tayari kuna wahitimu kutoka vyuo hivyo wasio na sifa.
 
Profesa Ndalichako alitoa maagizo hayo jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini hapo, alipozindua maonyesho ya 13 ya elimu ya juu, sayansi na teknolojia yenye kaulimbiu “Elimu ya Juu Bora kwa Mapinduzi ya Viwanda.”
 
Alisema, “Katika awamu hii watu wanaofanya kazi kwa mazoea hawana nafasi, lazima muwe wabunifu na mpitie upya zana mnazotumia kuhakiki ubora wa vyuo, inawezekana zina matobo.”
 
Alisema Serikali itaendelea kuimarisha mfumo wa ithibati na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ili kuhakikisha asilimia kubwa ya wahitimu wa shahada wanachangia ukuaji wa uchumi kulingana na elimu waliyopata.  
 
 “Katika ubora wa elimu hatutakuwa na mzaha, naomba hilo lieleweke vizuri kwa wadau wote, ili kuimarisha elimu tunapaswa kufanya kazi kwa pamoja,” alisema.
 
Alisema Serikali na wadau wengine wa elimu ya juu kila mmoja atimize wajibu wake. “Tuwe na uzalendo, elimu isiwe ni biashara, bali fursa ya kuendelea.”
 
Profesa Ndalichako alisema Chuo Kikuu cha Kenyatta kiliamua kufunga tawi la Arusha baada ya matokeo ya uhakiki kuonyesha udhaifu, huku tawi la Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira Mbeya likifungwa Julai 5.
 
“Natoa wito kwa taasisi zote za elimu ya juu ambazo matokeo ya uhakiki yalibainisha zina upungufu zifanyie marekebisho kasoro hizo haraka iwezekanavyo kama walivyoelekezwa na mamlaka za ithibati. Vinginevyo hatua stahiki zitachukuliwa, ikiwa ni pamoja na kufuta usajili wa vyuo hivyo,” alisema.
 
Mwakilishi wa kamati ya vyuo vikuu, Profesa Yonica Ngaga alisema hatua ya kuvidhibiti vyuo visivyo na sifa imechelewa kuchukuliwa kwa sababu tayari vimetoa wahitimu walio kwenye kampuni na taasisi kadhaa.
 
“Hatua hii ilipaswa kuchukuliwa mapema. Hata hivyo, si vibaya kwa sababu tayari TCU inachukua hatua, itasaidia kudhibiti uzalishaji wa wasomi wasio na sifa,” alisema.
 
Alisema baadhi ya vyuo vilianzishwa kwa sababu ya uwapo wa Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa kuwa wengi watakuwa na uwezo wa kulipa ada.
 
“Vipo vinavyoshindana kwa wingi wa wanafunzi na hawajishughulishi kuangilia wahitimu wao ni mahiri kiasi gani kwenye masoko ya ajira, matokeo yake wahitimu wao wengine ni mabomu wakipewa kazi wanaharibu kwa kuwa hawana uwezo,” alisema.
 
Katibu mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa alisema maonyesho hayo yameshirikisha taasisi 68 za elimu ya juu zikiwamo nne kutoka nje ya nchi.

Lugola Ambana Tena IGP Sirro.....Ataka Majibu Ifikapo Saa 12 Jioni

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema ifikapo saa 12 jioni leo atahitaji maelezo kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro kuhusu alipo mbwa maalumu wa polisi wa kikosi cha Bandari ambaye hajulikani alipo.

Lugola ametoa kauli hiyo leo, Alhamisi Julai 19, 2018 wakati alipofanya ziara Bandari ya Dar es Salaam, kwa ajili ya kuona utendaji kazi wa jeshi la polisi bandarini hapo.

Amesema kikosi kina jumla ya mbwa sita maalumu, wawili wapo mafunzoni na wanabaki wanne ambapo kati yao mmoja aitwaye Hobby hajulikani alipo.

Alisema ameulizia alipo mbwa huyo lakini haijulikani alipopelekwa wala alipolala tangu alivyoondolewa jana asubuhi.

Hivyo amesema akimaliza ziara yake leo, saa 12 jioni IGP Sirro yeye mwenyewe ampigie simu akiwa na huyo mbwa  pale polisi Bandari ili ajiridhishe  alikuwa wapi na alikwenda kufanya nini

Ester Matiko; Dkt. Wilbrod Slaa ni kiongozi aliyeniumiza sana

$
0
0
 Mbunge wa Tarime Mjini , Esther Matiko (CHADEMA) amefunguka kuwa katika vitu vilivyowahi kumuumiza tangu aingie kwenye siasa ni pamoja na kuondoka kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbrod Slaa.

Matiko amefunguka hayo kupitia Kikaangoni ya EATV ambapo amesema kuwa amewahi kuumizwa na siasa pindi kiongozi huyo alipoondoka wakati chama kikimhitaji.

“Dkt. Wilbrod Slaa ni kiongozi aliyeniumiza sana wakati alipoondoka ndani ya chama kwa kuwa aliondoka kipindi ambacho kila mtu hakutegemea, ni kama mwanajeshi mko vitani kisha akaamua kuwageuka njiani”, amesema Matiko.

Aidha ameongeza kuwa, “Zitto ni kiongozi ambaye ana nafasi yake kwa vijana wa taifa hili. alipoondoka CHADEMA niliumia lakini nilimtakia kila la kheri kwa huko alipochagua kwenda”.

Septemba 1, 2015 Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Wilbrod Slaa, ambaye kwa sasa ni balozi wa Tanzania nchini Sweden, alitagaza rasmi kuondoka katika chama hicho na kustaafu mambo ya siasa.

Waziri Mbarawa: Sitamvulimia Mtu Yeyote

$
0
0
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa amesema katika uongozi wake ndani ya wizara hiyo hatowavumilia watendaji wanaoshindwa kusimamia kwa ufanisi miradi ya maji.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Julai 19, 2018 wakati akifungua kongamano la kuhamasisha sekta binafsi kushiriki katika maendeleo ya sekta ya maji nchini.

Mbarawa amesema amebaini kuna watu wamepewa dhamana ya kusimamia miradi lakini wanashindwa kufanya kazi hiyo kama inavyotakiwa.

Amesema katika muda mfupi alioingia kwenye wizara hiyo amekutana na miradi mingi ambayo imeshindwa kukamilika ndani ya muda uliopangwa kutokana na uzembe.

"Miradi mingi ya maji ni ya muda mrefu, tatizo sio pesa kuna uzembe unafanyika huenda ni kwa maslahi binafsi. Maeneo mengine mkandarasi yupo eneo la mradi lakini kazi imesimama,"amesema.

"Hili ni tatizo hatuwezi kwenda hivi  lazima tubadilike kama  wizara, hatuwezi kumpa kazi mkandarasi kwa sababu tunamfahamu au anazunguka koridoni. Tutawapa kazi wakandarasi wenye uwezo na viwango na tutawasimamia wafanye kazi kwa ubora unaostahili.”

Profesa Mbarawa pia amewataka wakandarasi watakaopewa kazi za miradi ya maji kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa uaminifu bila kujali utaifa wao.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mhandisi Stella Manyanya amesema kongamano hilo  ni muhimu kwa kuwa  linatoa fursa kwa sekta binafsi na Serikali kushirikiana katika kuhakikisha maji yanapatikana kwa urahisi.

Amesema kupitia kongamano hilo, Serikali na sekta binafsi watakuwa na  mwelekeo mmoja wa kuleta matokeo makubwa katika sekta ya maji na viwanda.

Irene Uwoya na Hamissa Mobetto Waomba radhi Kwa Picha za Nusu Uchi Kama Walivyoagizwa na TCRA

$
0
0
Wasanii Hamisa Mobeto na Irene Uwoya wameomba radhi kwa kosa la kuweka picha za utupu katika mitandao ya kijamii. Wamechukua uamuzi huo saa chache baada ya kutakiwa kufanya hivyo na kamati ya maudhui ya mamlaka ya mawasiliano (TCRA).

Uamuzi wa TCRA umetolewa leo asubuhi Alhamisi Julai 19, 2018 baada ya wasanii hao kukiri kosa katika mkutano uliowahusisha waandishi wa habari.

Kupitia kurasa zao za mtandao wa kijamii wa Instagram, Uwoya ndio alikuwa wa kwanza kuomba radhi kwa kuweka picha anayoonekana amejilaza huku sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa wazi.

“Wapenzi wangu, ndugu zangu, wakubwa zangu na wadogo zangu naomba radhi kwa picha niliyopost ...,najua nimekwaza, sikujua nitawakwaza sababu ya role mode wangu Beyonce, nimejifunza sasa …,nawapenda,"

Naye Hamissa ameandika….

NAOMBA RADHI KWA UMMA:

Husika Na Kichwa Cha Habari Hapo Juu.

Mimi Hamisa Mobetto
Ambaye ni Mfanya Biashara Wa Mitindo (Fashion Entrepreneur) Apa Nchini Tanzania Na Pia Ni Raia Wa Tanzania 🇹🇿 Naomba Kutumia Fursa Hii Kuomba Radhi Kwa Watanzania na Wengine Wote Ambao Ni Watumiaji Wa Mitandao .
Kuhusiana Na Kitendo Cha Mimi Na Washabiki Zangu (Fans) Wangu Kutuma Picha Zangu Zinazoonyesha Nusu Utupu Kwenye Page Zao Za Instagram.
.
Pia Natumia Fursa Hii Kuwashukuru Kamati Ya Maudhui Kwa Jinsi Walivyonita Kwenye Kamati Yao Na Kunipa Nafasi Ya Kujitetea Na Mwisho Kufanya Uamuzi Wenye Haki Kwangu Na Kwa Wapenzi (fans) Wangu Wote . Ninawashukuru Sana.🙏🏾
.
Mwisho Kabisa Niwahusie Vijana Wenzangu Kuepuka Kutumia Mitandao Ya Kijamii vibaya Kwani Kwa Sasa Kuna Sheria Kali Zinazokataza Picha Mbaya kutumwa Kwenye Mitandao .Naomba Pia Wapenzi (fans)Wangu Kuanzia Sasa Kutuma Picha Zangu Zenye Staha Au Kutumia Biashara Zangu Kunisapoti.
.
Nawashakuru Sana Na Mbarikiwe Sana.❤️🙏🏾

Serikali Imewataka Wadhibiti Ubora Wa Elimu Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Weledi

$
0
0
Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma
Serikali imewataka Wadhibiti Ubora wa Elimu katika ngazi zote kutekeleleza majukumu yao kwa weledi ili kukuza kiwango cha elimu hapa nchini.

Akizungumza leo Jijini Dodoma wakati wa hafla ya kukabidhi magari 47 kwa wadhibiti Ubora wa Elimu na Baraza la Mitihani (NECTA), Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amesema ku ni utekelezaji wa sehemu ya mikakakti ya kukuza elimu hapa nchini hasa kipindi hiki Taifa linapoelekea katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Kati ya hayo, 45 yamekabidhiwa kwa wadhibiti ubora wa elimu ngazi ya Kanda na Wilaya na 2 kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) .

“Imani yangu ni kuwa magari haya yatatunzwa vizuri na yatatumika kufanya kazi na malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo hivyo yatasaidia kuboresha elimu hapa nchini ” Alisisitiza Prof. Ndalichako

Akifafanua, Prof. Ndalichako  amesema kuwa magari hayo yanalenga kusaidia Taifa kuzalisha wataalamu wenye weledi, mahiri na wabunifu hasa katika kipindi hiki Taifa linapoelekea katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Aliongeza kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wale wote watakaotumia magari hayo kwa maslahi binafsi na wale watakaoshindwa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya elimu.

Katika kuimarisha elimu, Prof. Ndalichako amesema kuwa Serikali imefungua ofisi mpya 5 za udhibiti ubora wa shule katika Halmashuri za Songwe, Kigambaoni, Ubungo, Chalinze na Ushetu kwa lengo la kuimarisha shughuli za udhibiti ubora katika Halmashuri.

Jambo jingine ni kuandaliwa kwa mkakati wa Taifa wa Elimu jumuishi (2018-2021) ili kushughulikia masuala ya elimu kwa watoto wote wakiwemo wenye mahitaji maalum na kutoa fursa kwa wadau wengine wa maendeleo kupata maeneo ya kuchangia utekelezaji  wa elimu jumuishi.

Hivi karibuni Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilikabidhi pikipiki 2,894 ambazo zimesambazwa katika halmashuri 156 katika mikoa 25, pikipiki hizo zitasaidia waratibu elimu kata katika kutekeleza majukumu yao ili kuhakikisha kuwa elimu bora inatolewa shuleni katika maeneo yao.

Magari 45 yaliyotolewa kwa Wadhibiti ubora wa elimu ngazi ya kanda na wilaya na 2 kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) ni chachu katika kuimarisha sekta ya elimu  hapa nchini na kuongeza ari kwa watendaji katika sekta ya elimu.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Ziara Ya Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Korea

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea, Mhe. Lee Nak-yon atafanya ziara ya kikazi nchini kwa mwaliko wa mwenyeji wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), kuanzia tarehe 21 hadi 23 Julai 2018. Ziara hiyo itakuwa ya kwanza kufanywa na kiongozi wa ngazi ya juu kutoka Jamhuri ya Korea tangu nchi zetu mbili zianzishe mahusiano ya kidiplomasia mwaka 1992. 

Madhumuni ya ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili na kufungua zaidi fursa za ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi katika ngazi na sekta mbalimbali. Mhe. Waziri Mkuu Lee atafuatana na ujumbe mzito wa maafisa wa Serikali, wabunge na wafanyabiashara wakubwa. Ujumbe wa wafanyabiashara utakaoongozana na Mhe. Lee unatarajiwa kukutana na wenzao wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Wafanyabiashara uliopangwa kufanyika jijini Dar es Salaam tarehe 23 Julai 2018. Mkutano wa kwanza ambao ulikuwa na mafanikio makubwa ulifanyika Seoul mwezi Februari 2018.

Mhe. Lee Nak-yon atawasili nchini saa kumi na mbili na nusu jioni (12:30) ya tarehe 21 Julai 2018 na atapokelewa na mwenyeji wake Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku inayofuata, Waziri Mkuu Lee na mwenyeji wake Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), watafanya mazungumzo rasmi jijini Dar es Salaam na baadaye watashuhudia uwekaji saini wa mkataba wa kuondoa hitaji la visa kwa wenye hati za kusafiria za kidiplomasia na za utumishi (diplomatic and official/service passport). Aidha, Mhe. Lee atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa ajili ya kusalimiana.

Jamhuri ya Korea ni mshirika mkubwa wa maendeleo wa Tanzania ambapo kupitia  Shirika la Kimataifa la Maendeleo (KOICA) na Mfuko wa Ushirikiano wa Uchumi na Maendeleo (EDCF) yamekuwa yakitoa misaada na mikopo mingi ya masharti nafuu kwa Tanzania ikiwemo misaada ya fedha katika bajeti, ujenzi wa miundombinu ya jamii, mafunzo ya muda mfupi na mrefu, wataalamu mbalimbali wa kujitolea, vifaa na mashine kwa ajili ya sekta mbalimbali ikiwemo ya afya.

Baadhi ya miradi ambayo imegharamiwa na Serikali ya Korea ni pamoja na Mradi wa kuboresha Huduma ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Chanika, Mradi wa Mfumo wa Usajili wa Meli na Mabaharia kwa Njia ya Mtandao Zanzibar, Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Taifa ya Taaluma na Tiba (MUHAS) kampasi ya Mloganzila na ujenzi wa daraja katika mto Malagarasi.

Vile vile, Korea ni mshirika mkubwa katika kusaidia maendeleo ya Bara la Afrika ambapo hivi karibuni katika mkutano wa Sita wa Jukwaa la Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na Africa (KOAFEC VI) uliofanyika mwezi Mei 2018, Busan, Korea ambapo Serikali ya Korea ilitangaza msaada wa Dola za Marekani bilioni 5 kwa ajili ya Bara la Afrika kwa kipindi cha mwaka 2018/2020. Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazonufaika na msaada huo.

Waziri Mkuu Ateta Na Balozi Mbelwa Kairuki

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Tanzania nchini China, Balozi Mbelwa Kairuki na amempongeza kwa kazi nzuri anayoifanya tangu aende huko.

Amekutana na Balozi Kairuki leo (Alhamisi, Julai 19, 2018) katika makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam, na amemtaka Balozi huyo ahakikishe anaboresha mahusiano kati ya Tanzania na China.

“Ni lazima nikupongeze kwa namna unavyoendelea kufanya kazi na unavyojitahidi kudumisha mahusiano na China. Tunashukuru kwamba wageni wanaokuja hapa nchini kutoka China wanatoa taarifa nzuri na jinsi unavyosaidia kuitangaza nchi yetu huko nje.”

“Umefanya kazi nzuri ya kuwaelekeza wawekezaji wa huko kwamba wakati tunaunda Serikali na kutengeneza mfumo wa utawala, tuliamua kujenga kwanza mifumo imara na kutambua fursa zetu tulizonazo ili baadaye Watanzania waweze kunufaika na hizo fursa.”

Amesema kupitia utaratibu huo, Serikali ilitaka Watanzania wamiliki ardhi ndipo mgeni apate, na kama kuna uzalishaji wowote unafanyika basi Mtanzania awe wa kwanza kunufaika, Serikali inufaike na mwekezaji naye anufaike.

“Tunakushukuru kwamba umesaidia kuwaambia wachina watulie wakati Serikali ikirekebisha mifumo yake. Na wao wameyaona mabadiliko hayo, kwani tumesimamia vita dhidi ya rushwa, na wao walikuwa ni waathirika wakubwa, lakini pia tumeongeza uwajibikaji. Watu wetu sasa wanawajibika kwenye viwanda na makampuni yao na Watanzania kwa ujumla, wametambua umuhimu wa kufanya kazi ili waweze kuishi,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Serikali hivi sasa iko kwenye programu ya kutangaza utalii uliopo nchini hasa kwa kuamua kuagiza ndege kubwa zitakazobeba watalii na kuwaleta moja kwa moja hapa nchini.

“Sasa hivi tumepata wageni maarufu kutoka nje ya nchi akiwemo Rais mstaafu wa Marekani, Mheshimiwa Barack Obama na wachezaji maarufu duniani, kwa hiyo tunaendelea na mikakati yetu ya kutangaza utalii huko nje.”

Aliyekuwa Miss Gerezani Ahukumiwa Kifo

$
0
0
Mlimbwende wa taji la urembo katika gereza kuu la wanawake la Lang'ata (Miss Lang’ata Prison 2016)  Jijini Nairobi amehukumiwa kifo baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake aliyefamika kwa jina la Farid Mohamed mwaka 2015.

Mrembo huyo mwenye jina la Ruth Wanjiku Kamande amepatikana na kosa la kumuua mpenzi wake huyo katika mtaa wa Buruburu, Nairobi mnamo tarehe 20 Septemba, 2015 baada ya kuwa na mvutano kati yao.

Jaji Jessie Lessit amesema upande wa mashtaka ulithibitisha kumkuta mshatikiwa na hatia pasipo kuwa na shaka yoyote ambapo amedai kwamba  vitendo vya Kamande vilionyesha aliua kwa kukusudia. 

Kwa mujibu wa vyombo vya habari kutoka Kenya vimeripoti kwamba mrembo huyo alijitetea kwamba mzozo kati yake na mpenzi wake ulikuja pale alipoiona kadi ya hospitali iliyoashiria kwamba Mohammed alikuwa akipokea matibabu ya Ukimwi.

Aidha ameeleza kwamba mpenzi wake huyo (marehemu Mohamed) alimwambia wakati huo ni heri wafe wote kuliko hali yake ya Ukimwi ifahamike hadharani ambapo wakati mzozo ukiendelea ulimpelekea kumchoma na kisu kilichokuwa kinachotumiwa jikoni.

Pamoja na hayo mahakama imekataa utetezi wa Bi Wanjiku wa kwamba marehemu alijaribu kumbaka ambapo ilielezwa kuwa uchunguzi wa madaktari ulionyesha hakukuwa na ukweli kuhusu madai hayo.

Wanjiku kwa sasa ambaye ana umri wa miaka 25 wakati anakamatwa ndiyo alikuwa amejiunga na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kusomea masuala ya biashara, kwa mujibu wa wakili wake.

Wanjiku amekuwa mahabusu tangu mwaka 2015 katika gereza la Lang'ata  akisubiri maamuzi ya mahakama dhidi ya shtaka lake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya July 20

Familia ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete yapatwa na msiba mzito

$
0
0
Baba mzazi wa mke wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Bi. Salma Kikwete,   mzee Rashid Mkwachu  amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Taarifa iliyotolewa jana Alhamisi Julai 19, 2018 na mbunge Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete kwa niaba ya familia,  imesema shughuli za mazishi zitakuwa Msasani nyumbani kwa familia ya Kikwete, huku akieleza ratiba ya mazishi.


Mbunge wa Zamani CUF Ajiunga CCM

$
0
0
Mbunge wa zamani wa viti maalumu (CUF), Amina Mwidau amejivua uanachama wa chama hicho na kutangaza kujiunga na CCM.

Amina katika taarifa aliyoisambaza kwenye vyombo vya habari jana, alisema sababu ya kuhama CUF ni kutaka kujipanga kivingine katika safari ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Alisema baada ya miaka miwili na nusu ya kutafakari mwenendo wa kisiasa ndani ya CUF na vyama vingine vya upinzani, pamoja na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano ameamua kujivua uanachama wa chama hicho.

“Nimeridhika sasa ni wakati muafaka wa kujipanga kivingine katika safari ya kushiriki kuleta maendeleo na ustawi wa wananchi wote,” alisema.

Amina aliyekuwa mbunge mwaka 2010 hadi 2015 na aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alisema ameamua kujiunga na CCM kwa sababu ana ndoto ya kuendelea kushirikiana na wananchi katika kuleta ustawi na maendeleo, hivyo hayupo tayari kuishia njiani.

Breaking News: Wema Sepetu ahukumiwa jela mwaka mmoja kwa Madawa ya Kulevya

$
0
0
Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya milioni 2 baada ya kukutwa na makosa mawili ya kutumia na kuhifadhi dawa za kulevya aina ya Bangi nyumbani kwake.

Akisomewa hukumu hiyo leo Julai 20, 2018 katika Makahama ya Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, Wema Sepetu ametakiwa kulipa faini hiyo na kama akishindwa basi atapelekwa jela kutumikia adhabu hiyo.

Katika hukumu nyingine wafanyakazi wawili wa ndani wa msanii huyo ambao nao walitajwa kwenye kesi hiyo wameachiwa huru na mahakama hiyo kwa kukutwa bila hatia.

Trump amualika Putin Washington

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump anakusudia kumwalika Washington, Rais wa Urusi Vladmir Putin baadaye mwaka huu, licha ya kuendelea kuwepo ukosoaji juu ya mkutano wao uliofanyika Jumatatu wiki hii katika mji mkuu wa Finland Helsinki.

Msemaji wa Ikulu ya Marekani Sara Sanders amesema majadiliano kuhusiana na ziara hiyo tayari yameanza.

Hata hivyo, Kiongozi wa maseneta kupitia chama cha Democrat nchini humo Chuck Schumer ameupinga mualiko huo mara moja kwa kusema kuwa Rais Trump hapaswi tena kukutana ana kwa ana na Rais Putin mpaka pale Wamarekani watakapojua nini kilitokea katika mkutano wa Helsinki.

Awali katika mkutano wake na kituo cha televisheni cha CNBC Rais Trump alitetea tena msimamo wake wa kuimarisha mahusiano na Urusi, lakini amesema kama jambo hilo halitafanikiwa, atakuwa adui na Rais huyo wa Urusi kushinda ilivyokuwa awali.

Wakati huohuo taarifa hizo za mualiko wa Rais Putin, zimeonekana kumshangaza Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa Marekani Dan Coats, ambaye aliambiwa jambo hilo katika mahojiano ya moja kwa moja wakati wa mkutano wa usalama uliofanika katika jimbo la Colorado.

Alijibu kwa kucheka na kusema kuwa ''..hilo litakuwa la namana ya pekee''

Ameongeza kusema kuwa bado hajafahamu nini walichojadili Rais Putin na Trump katika mkutano wao, ambao ulihudhuriwa tu na watafsiri wao.

Wema Sepetu Kafanikiwa Kulipa Faini na Kukwepa Kifungo

$
0
0
Msanii na mlimbwende wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu  amelipa faini ya Sh2milioni na kuepuka kifungo cha mwaka mmoja jela. 

Wema amelipa faini hiyo leo Ijumaa Julai 20, 2018 baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumhukumu kulipa faini ya Sh1milioni kwa kila kosa au kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kukutwa na kutumia dawa za kulevya aina ya bangi.

Wakati Wema akikutwa na hatia, washatakiwa wenzake ambao ni wafanyakazi wake wa ndani, Angelina Msigwa na Matrida Abbas wameachiwa huru baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Akisoma hukumu hiyo iliyochukua zaidi ya dakika 45,  Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba amesema upande wa mashtaka umeleta mashahidi watano, ambao walithibitisha mashtaka hayo.

Amesema baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wake, washtakiwa wote walikutwa na kesi ya kujibu  na walijitetea wakiongozwa na wakili wao,  Albert Msando.

"Nawaachia huru mshtakiwa wa pili na wa tatu kwa kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao lakini kwa upande wa Wema hakuna shaka lolote kwamba alipatikana na dawa za kulevya,” amesema hakimu.

Magereza Na JKT Kushirikiana Katika Miradi Ya Uzalishaji Mali

$
0
0
Jeshi la Magereza na Jeshi la Kujenga Taifa wameahidi kushirikiana katika miradi mbalimbali ya uzalishaji mali kupitia mashirika yake ya Magereza Corporation Sole na SUMA-JKT.

Hayo yamejiri wakati wa ziara ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike  alipomtembelea Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Matin Busungu ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake  za kujitambulisha kwa viongozi mbalimbali wa kitaifa tangu ateulie kuwa mkuu wa Jeshi hilo Julai13, 2018.

Katika mazungumzo yao, wakuu hao wa taasisi hizo muhimu nchini wameonesha utayari wa ushirikiano katika miradi ya ujenzi pale taasisi moja inapokuwa na miradi mikubwa inayoweza kuhitaji utaalam au nguvu ya kuweza kushirikiana.

Aidha, Meja Jenerali Busungu amesema kuwa JKT  lipo tayari kulikopesha matrekta Jeshi la Magereza wakati litakapokuwa limekamilisha  mpango wake kilimo cha kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa kama ilivyoelekezwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

“Namshukuru sana  Meja Jenerali Busungu kwa kuonesha utayari wa kushirikiana na Jeshi la Magereza, kilichobaki ni kujipanga na kuanza utekelezaji mara moja”. Amesema Jenerali Kasike.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images