Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Katibu Mkuu CCM Dk Bashiru Ally aonya mzaha matukio ya watu kutekwa

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amewaomba wananchi wanaozungumza kimzaha juu ya matukio ya watu kutekwa na watu wasiojulikana kutofanya hivyo.

Pia, ametoa ushauri kwa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (Tantrade) kuwa na siku maalumu ya kudumisha amani na umoja katika maonyesho inayoandaa.

Dk Bashiru alisema hayo jana alipotembelea Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika viwanja vya maonyesho vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Alisema jitihada zinazofanywa na Serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli ya kupambana na ufisadi na rushwa zinajenga vitisho jambo ambalo linawafanya watu wasioitakia mema nchi kutofurahia.

“Vitisho vingi sana duniani vya kiusalama, kuna watu nasikia wanafanya mzaha wa kiusalama, wanazungumza watu wanaopotea. Wanazungumza kimzaha, kulikuwa na matatizo pale Kibiti ukienda Rufiji (mkoani Pwani), hayajatatulika lakini tunashukuru vyombo vya ulinzi na usalama wamekabiliana nao,” alisema Dk Bashiru.

Alisema, “Kuna vitisho vingi sana, bahati mbaya kijiografia eneo letu hili limekaa vibaya, ukanda wote wa Bahari ya Hindi ni eneo hatari. Eneo hatari kwa ugaidi, eneo hatari kwa maharamia, eneo hatari kwa kila vitisho vya kiusalama.”

Dk Bashiru alisema, “Vita ya rushwa si ya CCM au ya Rais Magufuli, ni vita ya Watanzania wote, rushwa ni adui wa haki, rushwa ni adui wa maendeleo na yote tunayoyafanya hatuwezi kuendelea kama tumefungwa minyororo na mafisadi.”

Alisema Taifa lilipofikia halipaswi kurudi nyuma au kukubali kuyumbishwa bali kuungana katika kuipigania nchi.

Katibu mkuu huyo alisema ni muhimu katika maonyesho hayo kuwapo na siku maalumu ya kutangaza amani na kudumisha umoja.

Dk Bashiru alitoa wito kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kutowaumiza wananchi wanaoishi jirani na hifadhi za Taifa na hasa wanapokuwa wakiwahamisha.

“Mnapokuwa mnataka kuwatoa wananchi msitumie nguvu, bali waelimisheni, msiwachomee nyumba na kuwapiga. Kwa kufanya hivyo mnachonganisha wananchi na chama, chama kipo kwa ajili ya kuwasaidia wananchi na si kuwachomea nyumba,” alisema Dk Bashiru.

Alisema, “Chama hakipendi kuona ng’ombe wa watu wanaswagwa, wananchi wanaharibiwa mali zao au wanapiga mayowe.”

Pia, alishauri Tantrade kuwa na siku maalumu ya kudumu ya kupambana na rushwa ambayo ni adui wa haki.

Jalada la Mke wa Bilionea Msuya Lakwama Kwa DPP

$
0
0
Upande  wa Jamhuri umedai katika kesi inayomkabili mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake dhidi ya kesi ya mauaji ya dada wa bilionea huyo, Aneth Msuya kwamba jalada la kesi hiyo liko kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa hatua za kikazi.

Kesi hiyo ilipangwa kutajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kwamba jalada liko kwa DPP likifanyiwa kazi.

Hakimu Simba aliilekeza Jamhuri itoe taarifa za jalada hilo tarehe ijayo. Mbali ya Miriam, mshtakiwa mwingine ni mfanyabiashara Revocatus Muyela.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Mei 25, 2016 walimuua kwa makusudi dada wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya.

Nusu Fainali Ya Kwanza Ya Kombe la Dunia 2018 ni Leo Kati ya Ufaransa na Ubelgiji

$
0
0
Nusu ya fainali ya kwanza ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi inaanza leo kwa mchezo mmoja kupigwa katika Uwanja wa Saint Petersburg baina ya Ufaransa na Ubelgiji.

Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na asilimia kubwa ya wadau wengi soka duniani itaanza majira ya saa 3 kamili usiku wa leo.

Mpaka sasa Ufaransa waliowahi kutinga hatua ya fainali mwaka 2006 dhidi ya Italia, wamepewa asilimia kubwa ya ushindi kuliko wapinzani wao Ubelgiji.

Ufaransa na Ubelgiji zimekutana mara 73 katika mashindano yote huku Ubelgiji wakishinda mara 30 na Ufaransa wakishinda mara 24 pamoja na kwenda sare mechi 19, leo watakuwa wanakutana mara ya 74.

Vilevile timu hizi kukutana mara ya mwisho katika michuano hii ilikuwa ni mwaka 1986 ambapo Ufaransa iliweza kushinda mabao 4-2 katika hatua ya kusaka mshindi wa tatu.

Na katika mchezo wa mwisho ambao ulikuwa wa kirafiki, Ubelgiji waliibuka na ushindi wa mabao 4-3 jijini Paris, mwaka 2015.

Kesho kutakuwa na mchezo mwingine wa pili ambapo England iliyokuwa haipewi nafasi kubwa kufanya vizuri, itakuwa inacheza na Croatia.

Kamati Kuu Ya CCM Kukutana Leo Dar es Salaam

$
0
0
Kamati  Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inatarajiwa kukaa leo Dar es Salaam ambako pamoja na mambo mengine, inatarajiwa kujadili wabunge wa chama hicho ambao hawakuwapo bungeni wakati wa kupiga kura ya kupitisha bajeti kuu ya Serikali ya mwaka 2018/19.

Kikao cha Kamati Kuu kitafanyika baada ya kile cha sekretarieti kilichofanyika jana chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Dk. Bashiru Ally, ambaye leo atawasilisha taarifa ya kikao hicho mbele ya wajumbe wa Kamati Kuu chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli.

Katika kikao cha sekretarieti masuala kadhaa yalijadiliwa, ikiwamo suala la utekelezaji wa ripoti ya Tume ya Uhakiki wa Mali za Chama iliyoongozwa na Dk. Bashiru.

Pia kilijadili utekelezaji wa ripoti hiyo na hatua za kuchukua baada ya Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli, kuagiza Katibu Mkuu kupitia sekretarieti afanyie kazi na kuchukua hatua haraka.

Pamoja na taarifa hiyo, pia kikao hicho cha Kamati Kuu kitajadili na kupitia jina la mgombea ubunge wa Buyungu katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12 na mgombea wa nafasi ya uwakilishi Jimbo la Jang’ombe kisiwani Unguja baada ya aliyekuwa mwakilishi wake kuvuliwa uanachama wa CCM.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa baada ya kuwasilishwa taarifa ya Tume ya Uchunguzi wa Mali za Chama, Mei 21, mwaka huu, baadhi ya vigogo waliotajwa kwenye ripoti hiyo wameanza kurejesha magari na nyumba ambazo wanadaiwa kujimilikisha.

Pamoja na hali hiyo, inaelezwa kuna uwezekano mkubwa wa kufanyika kwa mabadiliko ya makatibu wa mikoa na wilaya wa CCM, hasa wale ambao ripoti ya uchunguzi imewagusa moja kwa moja.

Kwa wale ambao wameshindwa kurejesha mali hizo, sasa wamepewa barua za kutakiwa kuzirejesha na watakaposhindwa wapo hatarini kuburuzwa mahakamani.

Wakati hayo yakiendelea, kwa upande wa Zanzibar, jana Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, aliongoza kikao cha Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar mjini Unguja.

Kikao hicho kilikuwa na ajenda mbili, ambazo ni mapendekezo ya kupiga kura za maoni katika Uchaguzi wa Jimbo la Jang’ombe na mapendekezo ya wanachama wa CCM wanaoomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Uwakilishi katika jimbo hilo.

Wajumbe walimchagua Samia kuwa mwenyekiti wa muda na kuongoza kikao hicho kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM, Dk. Ali Mohammed Shein ambaye yupo safarini nje ya nchi.

Hatma ya dhamana ya mfanyabiashara , Peter Zakaria Kujulikana Leo

$
0
0
Hatma ya dhamana ya mfanyabiashara maarufu Kanda ya Ziwa, Peter Zakaria inatarajiwa kujulikana leo wakati Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma itakapotoa uamuzi kuhusu zuio la dhamana yake iliyowasilishwa na upande wa Jamhuri wiki iliyopita.

Mfanyabiashara huyo anayemiliki kampuni ya mabasi ya Zakaria yanayosafiri kati ya mikoa ya Mwanza, Simiyu na Mara alifikishwa mahakamani Julai 5 akikabiliwa na mashtaka mawili ya kujaribu kuua kwa kutumia silaha baada kwa kuwajeruhi kwa risasi Ahmed Segule na Issac Bwire.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Rahimu Mushi, wakili wa Jamhuri, Lukelo Samuel aliiomba Mahakama kuzuia dhamana ya mshtakiwa akidai hali za majeruhi wa tukio hilo lililotokea Juni 29 si nzuri na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu.

Mawakili wa utetezi Kassim Gila na Onyango Otieno walipinga ombi hilo wakisema hakuna nyaraka wala uthibitisho uliowasilishwa mahakamani kuthibitisha kuwa hali za majeruhi ni mbaya na wamelazwa hospitalini.

Baada ya kusikiliza hoja za zote mbili, Hakimu Mushi aliahirisha shauri hilo hadi leo Julai 10 ambapo anatarajiiwa kutoa uamuzi wa kuhusu dhamana.

Mtoto wa miaka 2 ajiua kwa risasi ya baba yake

$
0
0
Nchini Marekani huko, Houston, Texas mtoto wa miaka miwili, Christopher Williams Jr amefariki dunia mara baada ya kujipiga risasi kichwani kwa bunduki ambayo imekuwa ikihifadhiwa na wazazi wake nyumbani kwao.

Tukio hilo limetokea pindi wazazi wa mtoto huyo wakiwa nyumbani, hivyo bado haijafahamika iwapo wazazi wa mtoto huyo watashtakiwa kwa kuhusika na tukio hilo.

Hata hivyo Polisi wa Houston wamesema wanajaribu kubaini ni vipi mtoto huyo aliyepewa jina la utani “Junior” aliweza kuifikia bunduki hiyo.

Polisi wanasema bunduki hiyo ambayo hutumia risasi za ukubwa wa 9mm ilipatikana eneo la tukio na kwamba ilikuwa inamilikiwa na babake.

Aidha kumekuwa na matukio kama hayo yanayokea mara kwa mara kwa watoto kujipiga risasi na kujiua kimakosa nchini Marekani miaka ya karibuni.

Mkuu wa kitengo cha waathiriwa maalum katika idara ya polisi ya Houston David Angelo ametoa wito kwa wazazi walio na bunduki kuchukua tahadhari zaidi.

“Ni lazima uweke salama silaha, iwe ni kwa kuhakikisha kifaa cha kufyatulia risasi kimewekwa salama au kuiweka salama silaha kwa njia nyingine kuhakikisha matukio kama haya hayatokei tena siku za usoni,” alisema.

Walimbwende 16 wasusia shindano la Miss Burundi 2018

$
0
0
Warembo 16, waliokuwa wanashiriki shindano la kumtafuta Miss Burundi wamejiondoa katika hatua ya fainali iliyopangwa kufanyika Julai 21, 2018 na kupelekea shindano hilo kuhairishwa mpaka Julai 28, mwaka huu.

Hali iliyopelekea nchi ya Burundi kuingiwa na hofu kubwa ya kupatikana kwa mlimbwende atakaye iwakalisha nchi hiyo kimataifa kwa mwaka 2018 katika mashindano yenye mlengo wa kuonyesha utamaduni, uweledi na urembo wa mwanamke wa Burundi.

Hata hivyo warembo hao wamefikia maamuzi hayo ya kususia shindano hilo kufuatia madai kuwa shindano la mwaka huu kumefanyika udanganyifu mkubwa upande wa zawadi itakayozawadiwa kwa mshindi wa kwanza na mshindi wa pili.

Ambapo waandaaji wa shindano hilo, Burundi Event hapo awali walitangaza washindi hao kujinyakulia gari, kiwanja chenye mita mraba 400 pamoja na hundi ya pesa taslimum, cha kushangaza ni kwamba walimbwende hao wanadai kuwa hakuna maandalizi yeyote ya zawadi hizo.

Aidha kufuatia mzozo huo wanakamati watano wa shindano hilo waliamua kuchukua uamuzi wa kujiudhulu.

Taasisi ya Mo Dewji yatoa Milioni 125 kugharamia matibabu ya watoto wenye saratani

$
0
0
Taasisi ya Mo Dewji imetoa msaada wa Tsh. 125 Milioni kwa kituo cha Tumaini la Maisha kilichopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ili kusaida kugharamia matibabu ya magonjwa ya saratani kwa watoto wanaopatiwa huduma katika kituo hicho.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Rachel Chengula alisema msaada huo ni mwendelezo wa misaada ambayo imekuwa ikitolewa na taasisi kwa kituo hicho.

Alisema wanatambua hali ngumu ambayo wanapitia watoto hao wanapouguza magonjwa ya saratani, hivyo wanaamini msaada huo utasaidia kuboresha huduma kwa watoto waliopo kituoni hapo na kuwezesha watoto waliopo mikoani kusafirishwa ili kufikishwa hospitalini na wao wapatiwe matibabu.

“Kama upo hai na mwanao anapumua, mshukuru Mungu kuwa ana makusudi na wewe na ana makusudi na mtoto wako. Usikatishwe tamaa na magonjwa, tunaamini kwamba watoto hawa watapona na kurudi nyumbani, watasoma na watalitumikia Taifa letu,

“Kama mnavyofahamu Mohammed Dewji amekuwa akifanya kazi na Tumaini la Maisha tangu mwaka 2012 ili kusaidia watoto kupatiwa matibabu, na kupitia taasisi yake tutaendelea kushirikiana ili kusaidia watoto wetu wapatiwe matibabu,” alisema Chengula.

Naye Meneja wa Wafadhili wa kituo cha Tumaini la Maisha, Alex Kaijage aliishukuru Taasisi ya Mo Dewji kwa msaada ambao wamekuwa wakiwapatia na kuwaomba kuendelea kuwa na moyo huo wa kusaidia matibabu ya watoto wenye saratani ili warejee katika hali ya kawaida na kuendelea na shughuli zingine ikiwepo kusoma.

“Tunajua kwamba tunahitaji sana sana hizi fedha kufanikisha matibabu ya hawa watoto, sio tu usafiri wa kutoka huko wanakotoka na kuja bali hata dawa ambazo tunazipata kwa sababu ya huu mchango ambao Mohammed Dewji ametuwezesha. Kwa sababu yenu watoto hawa wanapata matibabu, kwa sababu yenu wanapona kwahiyo tunawashukuru sana,” alisema Kaijage.

Kwa upande wa mmoja wa wazazi ambao mtoto wake anapatiwa matibabu katika hicho, Hamisi Samweli aliwataka wadau wengine wenye uwezo wa kifedha kuwa na moyo wa kusaidia kama anavyofanya Mohammed Dewji ili watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa kifedha wapatiwe matibabu.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo dawa na PETE za bahati zenye uwezo mkubwa wakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.
 
Kutana na Sharif Al_noor. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. -SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA- Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi.
 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
 
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudisha  alipotea(MSUKULE), kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET) Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa nambari ya simu
 
+255 746 426 604

Wakuu wa Mashirika ya Umma Wasiotoa Gawio Serikalini Watakiwa Kujitathimi Kama Wanatosha

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amewataka wakuu wa mashirika ya umma yaliyoshindwa kutoa gawiwo kwa Serikali kujitathimini kama wanastahili kuendelea kuyaongoza.

Dk Mpango amesema hayo leo Julai 10, 2018 jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongomano la kujadili jukumu la taasisi za umma katika utekelezaji wa sera ya viwanda lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi.

Akisoma hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyemtuma kumwakilisha, Dk Mpango alisema kuna jumla ya mashirika ya umma 270.

"Mimi katika nafasi ya waziri wa fedha na mipango, siridhiki na mashirika ambayo hayatoi gawio kwa Serikali," amesema Dk Mpango

“Wakuu wa mashirika husika na bodi wajitathimimi na nimekwisha muagiza Msajili wa Hazina, achambue na kufuatilia kwa karibu mienendo wa biashara na uongozi wa mashirika yote ili yale yasiyoenda vizuri tuondokane nayo lakini wahusika wawajibishwe,hatutaki kurudia makosa ya zamani," ameongeza

Amesema mashirika 232 yanamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100, mawili asilimia 50, manne zaidi ya asilimia 50 na mashirika madogo 32 kwa ubia ambayo nayo huenda yakabadilika kwa kuyaunganisha.

Dk Mpango amesema kati ya mashirika ya biashara 34 yanayomilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali, mashirika 30 hayajatoa gawiwo ka mwaka 2016/17   .

Kati ya mashirika 36 yanayomilikiwa kwa ubia na wawekezaji,mashirika 20 hayajatoa gawio Serikalini.

Naye Msajili wa Hazina, Dk Athuman Mbuttuka amesema kongamano hilo ni muhimu katika kujadili namna ya kutekeleza sera ya viwanda.

Awali, Kadari Singo wa Taasisi ya Uongozi amesema kongamano hilo litajadili kwa kina adhima hiyo ya sera ya viwanda na jinsi inavyoweza kutekelezwa na kuchangia ukuaji wa maendeleo.

Mfanyabiashara Peter Zakaria asomewa mashtaka mapya, anyimwa dhamana

$
0
0
Matumaini ya Mfanyabiashara maarufu Kanda ya Ziwa, Peter Zakaria kupata dhamana na kuungana na familia yake yameyeyuka baada ya kurejeshwa rumande kwa kukosa dhamana katika moja ya mashtaka mapya mawili aliyosomewa leo.

Wakati akisubiri uamuzi wa Mahakama kuhusu dhamana yake katika kesi ya kujaribu kuua kwa kuwapiga risasi Ahmed Segule na Isaac Bwire, leo Julai 10, Zakaria amejikuta akisomewa shtaka jipya la kumiliki bunduki aina ya shortgun na risasi tano kinyume cha sheria.

Licha ya kuachiwa kwa dhamana  katika shtaka la kujaribu kuua, mfanyabiashara huyo amejikuta akirejeshwa mahabusu baada ya Wakili wa Serikali, Samuel Lukelo kupinga dhamana yake katika kesi ya kumiliki silaha na risasi kinyume cha sheria.

Juhudi za mawakili  wa Zakaria, Kassim Gila na Onyango Otieno kuishawishi Mahakama mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi, Rahim Mushi kumpa dhamana mteja wao leo hazikuzaa matunda baada ya shauri hilo kuahirishwa hadi Julai 12 uamuzi kuhusu dhamana hiyo utakapotolewa.

Katika shtaka la kwanza, Zakaria anayemiliki kampuni ya mabasi ya Zakaria yanayosafiri kati ya mikoa ya Mwanza, Simiyu na Mara anadaiwa kujaribu kuwaua kwa kuwapiga risasi Segule na Bwire wanaodaiwa kuwa ni maofisa usalama wa taifa katika tukio lililotokea Juni 25 eneo la kituo cha mafuta kinachomilikiwa na Zakaria mjini Tarime.

Mahakama imemuachia kwa dhamana katika shauri hilo baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini watatu, wawili wakiwa watumishi wa Serikali waliosaini hati ya dhamana ya Sh10 milioni.

Awali mshtakiwa alifikishwa mahakamani Julai 5 na kusomewa mashtaka hayo ambapo leo mahakama ilipanga kutoa uamuzi kuhusu dhamana.

Katika shtaka la pili, mshtakiwa anadaiwa kumiliki bunduki aina ya shortgun na risasi tano kinyume cha sheria. Kosa hili halikuwa na dhamana na amerudishwa rumande hadi Julai 12.

CUF Yawavua Uanachama Madiwani Watatu Tanga

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF), jijini Tanga kimewavua uanachama madiwani watatu wakiwamo wawili wa Viti Maalumu na mmoja wa Kata ya Mwanzange.

Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Daudi Mayeji, ametangaza hatua hiyo jana jioni baada ya kupokea barua kutoka kwa uongozi wa chama hicho.

“Nimepokea barua kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF Taifa, Magdalena Sakaya ikeleza kuwafuta uanachama kwa madiwani wawili wa Viti Maalumu, Halima Juma na Fatuma Hamza na Diwani wa Kata ya Mwanzange, Rashid Jumbe,” amesema Mayeji.

Amezitaja sababu tatu zilizoainishwa katika barua hiyo kukivuruga chama, kukataa wito wa kamati ya maadili ya chama hicho na kukaidi kufika katika kikao cha Baraza la Uongozi Taifa la chama hicho.

Akizungumza baada ya uamuzi huo kutangazwa, Jumbe ambaye pia wa Mwenyekiti wa CUF wilaya, amesema hatambui waliomfuta uanachama kwa sababu si viongozi wala wanachama wa chama hicho.

Wakati huo huo, madiwani hao wa Viti Maalumu nao waliungana na Jumbe wakidai hawatambui uamuzi huo kwa sababu hawamtambui Sakaya wala Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba kwa sababu alishafukuzwa uanachama.

“Walioandika barua za kutufukuza sisi hatuwatambui, kiongozi tunayemtambua ni Katibu Mkuu wetu Maalim Seif Sharrif Hamad hao wengine hatuwajui,” wamesema.


Hakimu Kesi Ya Vigogo CHADEMA Agoma Kujitoa..... Asema Hajawahi Kukataliwa Kwa Sababu Za Ajabu Ajabu

$
0
0
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri anayesikiliza kesi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema akiwamo Mwenyekiti, Freeman Mbowe amegoma kujitoa.

Hakimu Mashauri ametoa uamuzi huo leo Jumanne Julai 10,  baada ya kuombwa na washtakiwa hao kujitoa wakidai hawana imani naye.

“Ilitolewa sababu kwamba kwa mwonekano wa hakimu hawezi kutenda haki, niko katika benchi hili kwa miaka 22 sasa sijawahi kuombwa kujitoa kwa sababu za ajabu ajabu kama hizi, sababu hiyo sikuitilia maanani.

“Nimepitia sababu zote za kutaka nijitoe lakini maombi hayo hayana mashiko ya kutosha kunikataa,” amesema Hakimu Mashauri.

Aidha, Hakimu Mashauri amesema aliziona sababu zote zaidi ya 10 hazina msingi ikiwamo kwamba anapendelea upande wa Jamhuri na kwamba ana nia ovu ya kutaka kuzika haki.

Washtakiwa katika kesi hiyo wanatuhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali, kufanya uchochezi wakiwa katika mkutano wa kampeni za Jimbo la Kinondoni, Viwanja vya Buibui Februari mwaka huu.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

NEC yatangaza tarehe rasmi ya uchaguzi

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza tarehe rasmi ya uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo la Buyungu pamoja na udiwani katika kata 79 za Tanzania Bara ambapo siku ya uchaguzi huo imepangwa kuwa Agosti 12 mwaka huu.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage wakati alipokuwa akizungumza katika mkutano na wajumbe wa tume hiyo mbele ya waandishi wa habari leo Julai 10, 2018 na kusema kwamba wamefikia maamuzi hayo baada ya tume hiyo kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai kuhusiana na uwazi wa jimbo hilo.

"Tumeshaandaa ratiba ya uchaguzi huu, tunatarajia fomu zianze kuchukuliwa Julai 8 hadi 14, uteuzi wa wagombea utafanyika Julai 14. Kampeni tunatarajia zianze kufanyika kuanzia Julai 15 hadi Agosti 11 na uchaguzi utakuwa Agosti 12", amesema Jaji Kaijage.

Pamoja na hayo, Jaji Kaijage ameendelea kwa kusema "uchaguzi huu mdogo wa Ubunge na Udiwani utahusisha jimbo la Buyungu, halmashauri ya Kakonko mkoani Kigoma na Udiwani katika kata 79 zilizopo katika halmashauri 43 kwenye mikoa 24 ya Tanzania Bara. Katika uchaguzi huu vituo vya kupigia kura vitakuwa vile vile vilivyotumika katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015".

Jimbo la Buyungu limekuwa wazi kutokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Kasuku Samson Bilago aliyefariki Mei 26 mwaka huu na kupelekea jimbo hilo kuwa wazi hadi sasa.

Picha: Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli aongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndg John Pombe Joseph Magufuli aongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi kinachofanyika katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es salaam, leo tarehe 10th July, 2018.

Tarimba Ajitoa Kamati Ya Kuisaidia Yanga, Afunguka Mazito

$
0
0
Aliyekuwa  Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Mpito ya kuivusha Yanga, Abbas Tarimba ametangaza kuachia ngazi kwenye wadhifa huo kwa madai kuwa hakuna maelewano baina yake na Makamu Mwenyikiti wa Yanga, Clement Sanga, ambaye ameivunja kimyakimya kamati hiyo ambayo ilipitishwa katika mkutano mkuu.

Kufuatia tukio la kuvunjwa kwa kamati, Tarimba amesema hawezi akawa na muda wa kuonana na Sanga kwa sababu ameivunja kamati, na hata kama asingefanya hivyo asingekuwa tayari kutekeleza majukumu ya kamati hiyo.

“Waachane na mimi, mimi sina muda wa kuonana na Sanga waachane na mimi, yeye kwanza kamati kaisha ivunja na hata kama wasinge vunja mimi nisingeweza kufanya kazi nao” alisema Tarimba.

Mbali na kauli hiyo, Tarimba amekanusha uwepo wa taarifa zilizokuwa zimeripotiwa kuwa kamati yake imelipa madeni ya fedha zote zilizokuwa ni malimbikizo ya madeni kwa wachezaji. Tarimba ameeleza kuwa hakuna ukweli kuhusiana na hilo akiwahusisha viongozi wa Yanga kuwa wamekuwa waongo hivyo na kuwaomba waache masuala ya usanii kwa kuwa klabu hiyo ni taasisi kubwa.

“Wanayanga mnadanganywa Yaani wanayanga mnadanganywa mchana kweupe, Yanga tuna tamaduni zetu sio hizi, viongozi ni waongo, nawaomba watulize akili zao wasaidie timu, wengine ni wakubwa wanaongoza mpaka bodi ya ligi, sasa watumie ukubwa huo kuipeleka Yanga mbele waache uongo uongo,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images