Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Afikishwa Mahakamani Kwa Kumchoma Moto wa Pasi Kijana Aliyekuwa Anamvizia Binti Yake

$
0
0
Mkazi wa Wilaya ya Hanang mkoani Manyara, Nikodemu Johnson amefikishwa mahakamani kwa kosa la kumpiga na kumchoma kwa pasi ya umeme kijana mmoja mkazi wa Katesh aliyemkuta ndani ya nyumba na binti yake.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo mbele ya Hakimu wa Wilaya Amani Petro Shao.

Ilidaiwa na mwendesha mashtaka kuwa Mei 28 mshtakiwa alimpiga na kumchoma kwa pasi ya umeme Christopher Bayanga (19) baada ya kumkuta kijana huyo kwenye nyumba ya mtuhumiwa.

Alidai kipigo alichomfanyia kijana huyo, hasa kuchomwa kwa pasi ya moto, kimemsababishia maumivu makali na kwamba maisha yake yalikuwa hatarini kwani alifungiwa ndani wakati huo. Johnson yuko nje kwa dhamana hadi Julai 25 wakati kesi hiyo itakaposikilizwa.

Article 8

$
0
0
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendele ya Makazi, imesema ili kurahisisha usimamizi wa wa ardhi na matumizi yake, imenunua vifaa vipya vya kisasa vya kupima ardhi nchi nzima.

Waziri wa Ardhi, William Lukuvi ameyasema hayo leo Jumatatu Julai 9, alipokuwa akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkoa pamoja na Wakuu wa Idara kutoka Ofisi za Ardhi Kanda na Wilaya za Lindi.

Amesema wizara imeamua kufanya usimamizi wa karibu na ofisi zote za kanda kwa kupeleka wataalamu wa fani zote pamoja na kununua vifaa vya kisasa ambovyo vitarahisisha utendaji wao wa kazi.

“Tunataka kama watu wa wilayani wakitaka kupima ardhi, kupanga matumizi bora ya ardhi na kutatua migogoro basi wafike mkoani au kwenye ofisi za kanda wachukue vile vifaa bure wakatumie na kama hawana wataalamu tunao wataalamu wengi kwenye kanda zote wachukuliwe wakafanye kazi,” amesema Lukuvi.

Pamoja na mambo mengine, Lukuvi amesema katika utumiaji wa vifaa hivyo tayari wameandaa mafunzo rasmi kwa ajili ya kuwafundisha maofisa wapimaji wa kanda, mikoa na baadhi ya maofisa wa halmashauri ambayo yatafanyika Dodoma  ili kuwafundisha namna bora ya kutumia vifaa hivyo.

“Tunataka hadi kufikia mwaka 2020 vijiji vyote nchini viwe vimepimwa na kuwa na hati yake pamoja na kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi,” amesema Lukuvi.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

Sumaye Kataja Sababu za Kukubali Mwaliko wa Rais Magufuli Ikulu

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amesema watu waliodhani kwamba angeshindwa kuitikia wito wa Rais John Magufuli kwenda Ikulu wakati viongozi wakuu wastaafu wote walipoalikwa watakuwa hawamjui kwani kwenda kwake ilikuwa nafasi muhimu ya kuzungumza na kiongozi huyo kuhusu masuala yakitaifa.

Sumaye amebainisha hayo wakati akizungumza kwenye kipindi cha Weekend BreakFast kinachorushwa siku ya Jumamosi na East Africa Radio na kusema alifurahi kupata mualiko huo kwani aliona ni fursa muhimu ya yeye kuweza kupata nafasi ya kutoa ushauri wake.

"Nilifurahi sana kupata mualiko wa Ikulu, nilijua nitaweza kupata nafasi ya kusema, niliitumia nafasi ile vizuri sana kumwambia Rais yale ninayoyafikiria wala siyo kumueleza ya kwangu binafsi bali yale ya taifa kwa ujumla. Hivyo waliofikiri tofauti kwamba sitakwenda basi hao ni watu ambao hawanijui vizuri", amesema Sumaye.

Mbali na hayo, Waziri Mkuu huyo Mstaafu amebainisha kwamba sababu kuu iliyomfanya yeye na baadhi ya viongozi wenzake kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) mnamo mwaka 2015 ilikuwa ni kwenda kuongeza nguvu katika  chama cha upinzani.

"Tulitoka CCM kuja CHADEMA ili kuongeza nguvu huku ili mabadiliko yatakapotokea yasitokee upande huu mwingine ukiwa na hasira. Vipo vitu vingi ambavyo tumepandisha sana upinzani mpaka sasa", amesisitiza Sumaye.

Julai 03, 2018 Rais Magufuli aliwaalika viongozi wakuu wastaafu wote na kufanya nao mazungumzo Ikulu Jijini Dar es salaam ambapo waalikwa walikuwa ni Rais wastaafu wa awamu zilizopita, Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu, Maspika na Majaji Wakuu.

Sumaye alikuwa Waziri Mkuu wa awamu ya tatu katika serikali iliyokuwa ikiiongozwa na Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa na alihama CCM mwaka 2015 wakati wa uchaguzi mkuu kwa madai ya kwamba anaunga mkono  mabadiliko yaliyokuwa yakinadiwa na upinzani.

NSSF Watakiwa Kutenga Dirisha La Ukimwi

$
0
0
Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, Sera, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenister Mhagama, ameliagiza Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kuhakikisha linatenga dirisha maalumu la kupima virusi vya Ukimwi ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kutokomeza ugonjwa huo.

Akizungumza katika maonyesho ya 42 ya Sabasaba, Jenista alisema  kufunguliwa kwa dirisha hilo kutasaidia wananchi wengi kujitokeza kupima afya zao.

Alisema ni vyema uongozi wa NSSF ukafanya jitihada za kuwashirikisha wataalamu wa afya ili kufungua dirisha hilo litakalosaidia wananchi wengi kufahamu afya zao.

“Naomba ndugu zangu wa NSSF kuhakikisha mnafungua dirisha la kupima afya katika maonyesho haya ya Sabasaba, tena viongozi wa NSSF muwe wa kwanza,” alisema Jenista.

Alisema kuna utamaduni umejengeka kwa wanaume wengi kukataa kupima afya zao, jambo ambalo limekuwa likichangia kukosekana kwa takwimu za walioathirika na ugonjwa huo.

Alisema kupima afya hasa virusi vya Ukimwi ni uhodari na mwanamume yeyote anayepima kwa hiari anaonyesha umakini wake.

Jenista aliipongeza NSSF kwa kutoa mafao ambayo yamesaidia kuchagiza sekta mbalimbali kujiimarisha.

Pamoja na hali hiyo, aliitaka NSSF kujenga utamaduni wa kulipa mafao kwa wakati ili wananchi wanufaike na mfuko huo.

Alisema utafiti uliofanywa unaonyesha NSSF ina uwezo wa kujiendesha kwa miaka 70, hivyo ni imani ya Serikali kuwa itaweza kufikisha huduma za jamii moja kwa moja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara,  alisema atafungua dirisha la kupima afya na atakuwa wa kwanza kupima.

Alisema NSSF imejipanga kuhakikisha jamii inafikiwa kirahisi na ndio sababu ya kupewa ushindi.

Wizara Ya Madini, Suma JKT Wasaini Mikataba Ya Ujenzi Vituo Vya Umahiri

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Ujenzi ya SUMA JKT, Mhandisi Morgan Nyonyi wamesaini Mikataba Mitatu ya kuanza ujenzi wa Vituo Saba vya Umahiri pamoja na Jengo la Mafunzo kwa Wachimbaji wadogo katika Chuo Cha Madini, Dodoma.

Hafla ya utiaji saini mikataba hiyo imefanyika leo tarehe 9 Julai, 2018, Makao Makuu ya Wizara ya Madini jijini Dodoma na kushuhudiwa na Waziri wa Madini Angellah Kairuki na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo.

Akizungumza baada ya utiaji saini, Waziri  Kairuki amesema kuwa, tukio hilo ni utekelezaji wa  ahadi aliyoitoa wakati akiwasilisha Bungeni Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambapo alieleza kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Madini itaanza ujenzi wa ofisi saba za madini ili zitumike kama vituo vya umahiri vya  masuala ya madini.

Waziri Kairuki amezitaja ofisi hizo kuwa ni Mpanda, Songea, Chunya, Tanga, bariadi, Bukoba na Musoma na kuongeza kuwa, ni pamoja na upanuzi wa miundombinu ya Chuo Cha Madini Dodoma kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa shughuli za madini zinazotekelezwa na Chama Cha Wachimbaji Madini Wanawake.

“ Ujenzi wa Vituo hivyo unatekelezwa kupitia Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) ambapo moja ya malengo mahususi ya mradi huu ni kuboresha Sekta ya madini nchini hususan kuwasaidia wachimbaji wadogo ili kuwaongezea ujuzi katika eneo la uchimbaji wa madini na kukuza uchumi,” amesisitiza Kairuki.

Akizungumzia umuhimu wa vituo hivyo, alisema vimelenga katika kutoa mafunzo ya jiolojia hususan katika utafiti wa madini, mafunzo ya uchenjuaji wa madini kwa kutumia teknolojia rafiki kwa mazingira hususan zisizotumia kemikali ya Zebaki.

Ameongeza kuwa, vituo hivyo pia vitatoa mafunzo ya biashara ya madini kwa wachimbaji wadogo wa madini, mafunzo ya usalama na afya sehemu za kazi na mafunzo ya namna bora za utunzaji wa mazingira kwenye migodi ya wachimbaji wadogo.

Kuhusu gharama za ujenzi wa vituo hivyo amesema kuwa ujenzi wake utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 11.9.

Akizungumzia sababu za kuingia Mkataba na SUMA JKT, Waziri Kairuki amesema kuwa, jeshi hilo limekuwa likijihusisha na kazi mbalimbali  za ujenzi, kujiimarisha kwao nchini, uwezo wao kiufundi katika kutekeleza miradi mikubwa, gharama nafuu, ubora na kuongeza kuwa, mkataba na SUMA JKT utaokoa kiasi cha shilingi milioni 249.3 ikilinganisshwa na wakandarasi wengine.

Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Msanjila amesema kuwa, ujenzi wa vituo hivyo umelenga kuwasaidia wananchi na zaidi ukilenga wachimbaji wadogo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Ujenzi ya SUMA JKT, Mhandisi Morgan Nyonyi amesema kuwa, Jeshi hilo limejipanga kutekeleza mradi huo ndani ya muda uliopangwa wa kipindi cha miezi sita   na utekelezaji wake utafanywa kwa weledi.

Kazi ya ujenzi wa vituo hivyo itasimamiwa na washauri Elekezi  Kampuni ya Y & P Architects ambayo imesanifu majengo ya Chuo Cha Madini Dodoma na Kampuni ya Interconsult Ltd ambayo imesanifu majengo ya Musoma, Bariadi na Bukoba.

Kikwete Awa Kivutio Sabasaba....Asisitiza Ubunifu

$
0
0
RAIS Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, amewataka waandaaji wa maonesho ya biashara ya kimataifa maarufu kama Sabasaba kuendelee kuwa wabunifu zaidi ili kuwezesha wajasiriamali kupata masoko ndani na nje ya nchi.

Kikwete aliyasema hayo jana alipotembelea baadhi ya mabanda ya biashara uwanjani hapo huku akigeuka kuwa kivutio kikubwa katika maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa yanayofanyika jijini Dar es Salaam baada ya wananchi waliofika katika maonesho hayo kufuata msafara wake.

Akizungumza baada ya kutembelea mabanda mbalimbali, Kikwete aliitaka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuwasaidia wafanyabiashara kutafuta masoko ya bidhaa wanazozalisha.

Kikwete alisema ameona bidhaa zote zinazotengenezwa na wafanyabiashara, hivyo kuna haja kubwa ya serikali kuwatafutia masoko wafanyabishara hao katika masoko ya kimataifa.

“Naona kila mwaka bidhaa zinaongezeka ubora wake ni vyema kuwatafutia masoko ili wakue zaidi,” alisema Dk Kikwete.

“Bidhaa nimeziona zinauzika ndani na nje ya nchi kazi kwenu wizara na Tantrade kuwasaidia wajasiriamali hawa ili wakue zaidi,” alisema Kikwete.

Kikwete aliingia katika viwanja hivyo saa 6:00 mchana na kupokewa na Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya.

Baada ya kuingia katika uwanja  wa maonesho wananchi waliokuwapo katika viwanja hivyo waliacha shughuli zao na kumfuatilia nyuma huku wengine wakitaka kumpa mkono kumsalimia.

Katika ziara hiyo ya kutembelea mabanda, Kikwete aliongozana na Manyanya na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (Tantrade), Edwin Rutageluka.

Askari wawili wafikishwa Mahakamani kwa kuhujumu uchumi

$
0
0
Watu watatu wakiwemo polisi jamii wa Mbezi Luis jijini hapa wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi baada ya kukutwa na meno ya tembo ya thamani ya Sh239.5 milioni.

Wakili wa Serikali Faraja Nguka leo Jumatatu Julai 9, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi, Ally Salum amesema washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 45 ya 2018.

Amewataka washtakiwa hao kuwa ni Juma Myali (35), Greyson Muhapa (wote polisi jamii) pamoja na Kefas Mlenzi, dereva na mkazi wa Mbezi Luis.

Amesema washtakiwa hao kwa pamoja Juni 28, 2018 katika eneo la Mbezi Wilaya ya Ubungo walikamatwa wakiwa na vipande 30 vya meno ya tembo vyenye thamani ya dola  105,000 za Marekani sawa na Sh 239,505,000, bila kuwa na kibali cha mkurugenzi wa wanyama pori.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, hawakuruhusiwa kuzungumza chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo.

Upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na hivyo kuahirishwa hadi Julai 23, 2018.

Mahakama Yatupitilia Mbali Ombi la Ruzuku la Chama cha Democratic (DP)

$
0
0
Chama cha Democratic (DP) kimegonga mwamba katika harakati za kutaka kufutwa kwa sheria ya ruzuku kwa vyama vya siasa iliyotolewa kwa ajili maandalizi ya uchaguzi.

DP ilitaka iwapo sheria hiyo haitafutwa, nacho kipewe ruzuku ya Sh100 milioni kwa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Mahakama ya Rufaa imetupilia mbali maombi ya DP ya marejeo ya uamuzi uliotolewa awali na mahakama hiyo katika rufaa ya kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu iliyotupilia mbali kesi ya msingi kuhusu kufutwa sheria hiyo.

Uamuzi wa majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa, Bernard Luanda (kiongozi wa jopo), Augustine Mwarija na Rehema Mkuye ni wa tatu kutolewa kuhusu suala hilo.

Bodi ya wadhamini wa DP, chama kilichoasisiwa na hayati Mchungaji Christopher Mtikila, ilifungua kesi Mahakama Kuu ikiomba kufutwa kwa Sheria ya Ruzuku ya Serikali Namba 11 ya mwaka 1996, ikidai inakiuka Katiba.

Chama hicho kilidai sheria hiyo ni ya kibaguzi kwa kuwa inakinyima ruzuku wakati CCM na CUF vilipewa. Bodi hiyo iliomba DP ipatiwe Sh100 milioni ili kujiandaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, kama ambavyo CCM na CUF vilipewa kujiandaa na uchaguzi huo.

Katika hukumu yake, Mahakama Kuu ilitupilia mbali kesi hiyo kutokana na bodi ya DP kutokuwa na hoja za kisheria zenye mashiko mbele ya jopo la majaji watatu walioisikiliza. Baadaye DP ilikata rufaa Mahakama ya Rufaa kupinga uamuzi huo.

Katika uamuzi dhidi ya rufaa namba 125 ya mwaka 2008 iliyotolewa Agosti 10, 2012 na jopo la majaji-- Eusebia Munuo (kiongozi wa jopo), Bernard Luanda na Sauda Mjasiri-- iliitupilia mbali rufaa hiyo kutokana na kutokuwa na mashiko kisheria. DP ilifungua maombi kutaka Mahakama ya Rufaa hiyo ifanye marejeo ya uamuzi wake.

Akisoma uamuzi wa Mahakama, Naibu Msajili, Amir Msumi alisema wanakubaliana na (wakili wa Serikali kwamba ombi la DP kwa mahakama ni kufungua na kusikiliza upya rufaa yake.

Msajili alisema maombi haya yanafutwa na mwombaji anapaswa kulipa gharama za usikilizwaji.

Mahakama imesema kifungu cha 16 (3) (b) cha Sheria ya Vyama vya Siasa Sura 258 si cha kibaguzi na hakikiuki Katiba ya nchi.

Korti imesema kifungu hicho kinatumika kwa usawa kwa vyama vyote vinavyotimiza masharti ya kupata ruzuku.

Wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo, wakili wa DP, Audax Vedasto aliiomba Mahakama izingatie hoja zao za maandishi akisisitiza kuwa haikutoa uamuzi kwenye hoja za msingi.

Wakili wa Serikali, Mark Mlwambo aliyemwakilisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), aliiomba Mahakama izingatie hoja zake za maandishi akisisitiza kuwa, mwombaji anatafuta kufungua upya rufaa kwa kupitia mlango wa nyuma. Alidai bodi ya DP imeibua hoja mpya, hivyo haijakidhi vigezo vya maombi ya marejeo.

Nisha apost video mtandaoni inayomuonyesha Akibadilishana Ulimi na Mzungu

$
0
0
Msanii wa filamu Salma Jabu aka Nisha amewaacha mdomo wazi mashabiki wake wa filamu baada ya kupost video mtandaoni ambayo inamuonyesha akiliwa denda na mpenzi wake mpya mzungu.

Muigizaji huyo amedai hawezi kukaa kimya bila kumuonyesha mpenzi wake huyo licha ya mashabiki wengi mtandaoni kumdhihaki.

“Ni ngumu sana kuficha hisia zangu kwa mtu nnayempenda, nimeshakuwa na m-black, Mwarabu ila kote niliambulia usaliti na uongo wa mapenzi, niliwahi sikia Wazungu wana mapenzi ya kweli kuliko Waafrica, kujaribu si mbaya.

“Me ni msafiri sijafika bado, na Mwenyezi Mungu anajua kama hapa ndo mwisho wa safari yangu au inaendelea, kikubwa nimeshampata na maneno sijali,’ amesema Nisha.


Katika post nyingine Nisha amesema;“Walimwengu sijui mna nini, nikiibiwa bwana mnanyamaza kimya, nikiwa na wa rika langu ben 10, akinizidi umri kizee, au mlikuwa mnafurahia kujiita bachelor? Sasa nimeshampata bado maneno kedekede. Yeye na mimi kwani tuna kasoro gani? Au mimi nimezaliwa niliye tu na kuibiwa?”
.


CHADEMA Wamtaka Polepole Ajifunze Kupitia Kwa Mwigulu Nchemba

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole kuwa makini na kauli zake anazozitoa kuhusu mikutano ya hadhara lasivyo itakuja kumtokea kama Mwigulu Nchemba alivyofanyiwa.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema baada ya kupita siku kadhaa tokea Polepole alivyotoa kauli yake kuwa 'mikutano ya hadhara haijapigwa marufuku ila imewekewa utaratibu mzuri zaidi wa namna ambavyo wanapaswa kufanya siasa katika nchi huku akidai tatizo kubwa sio mikutano hiyo kutofanyika bali ni viongozi wa upinzani kuishi nje ya majimbo yao'.

"Hicho anachokifanya Polepole ni propaganda nyepesi tu na nimshauri kwamba kwa sasa ajifunze kupitia Mwigulu Nchemba maana naye alikuwa anasema hivyo hivyo kuwa mikutano haijazuiliwa lakini yeye mwenyewe ni juzi tu wamemzuia kufanya mikutano jimboni kwake kabla ya kumruhusu. 

"Anavyosema mikutano haijazuiliwa yeye ndio anakuwa kinara sasa wa kupotosha umma juu ya suala hilo na wala sio sisi", amesema Mrema.

Pamoja na hayo, Mrema ameendelea kwa kusema "hoja yake ambayo anasema Wabunge wetu hawaishi katika majimbo yao ni dhaifu na mufilisi kwasababu Wabunge wetu ndio wanaongoza kukaa katika maeneo yao kuliko wowote wale na pia Wabunge wetu wamezuiliwa kufanya mikutano yao katika baadhi ya maeneo na tuna barua rasmi ya kuzuiliwa".

Saa 24 Baada ya Hierro kuondoka,, Enrique Atangazwa Kocha Hispania

$
0
0
Aliyekuwa kocha wa klabu ya Barcelona ya Hispania, Luis Enrique, ameteuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya Hispania baada ya nchi hiyo kung’olewa katika Kombe la Dunia wakati wa kutafuta 60 bora katika michuano inayoendelea nchini Russia.

Kwa mujibu wa mkataba, Enrique ataishika nafasi hiyo kwa miaka miwili. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 48, anachukua nafasi ya Hierro aliyepewa jukumu hilo saa 48 kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia Hispania ilipocheza na Ureno.

Kocha wa awali, Julen Lopetegui,  alifukuzwa muda mfupi kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia baada ya kukubali kuwa kocha wa klabu ya Real Madrid, na kumwacha aliyekuwa mkurugenzi wa michezo,  Fernando Hierro, kukaimu nafasi hiyo.

Enrique aliondoka Barcelona mwishoni mwa msimu wa 2016/17 baada ya kuitumikia miaka mitatu na baadaye kuzitumikia klabu za Chelsea na Arsena.

Wataalam wa afya 6,180 wapangiwa vituo vya kazi

$
0
0
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imewataka wataalam wa afya 6,180 walioajiriwa kuripoti katika vituo vyao ya kazi ndani ya siku 14.

Wataalam hao wa afya watasambazwa katika vituo vya  afya, hospitali za Wilaya na zahanati nchini.

Akizungumza leo Juni 9, 2019 na Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo amesema atakayeshindwa kuripoti ndani ya muda huo, ajira yake atapewa mwingine.

Mei 10, 2018 Jafo alitangaza nafasi za ajira hizo na kubainisha kuwa watumishi watakaoajiriwa watapangiwa kwa kuzingatia mahitaji, kuwataka wenye sifa za taaluma katika kada ya afya wajitokeze kuomba nafasi kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi.

“Wasijikusanye katika ofisi za mjini kwasababu hatutabadilishia vituo kwa kuwa walipoomba ajira walisema wapo tayari kufanya mahali popote ndani ya Tanzania," amesema Jafo leo.

Jafo amesema upangaji wa watumishi hao umezingatia halmashauri ambazo zina zahanati na vituo vya afya lakini hazina watumishi, vituo vya afya 210 ambavyo vilikarabatiwa na zahanati ambazo zilikuwa zinaongozwa na wahudumu wa afya.

Ametaka wananchi kuwapokea wahudumu wa afya ili wawatumikie na waache kuwafanyia mambo mabaya kama katika baadhi ya maeneo ilivyokuwa ikifanyika.

Amesema majina ya walioajiriwa yanapatikana katika tovuti ya Tamisemi.

Mfumuko wa Bei Wazidi Kupungua

$
0
0
Mfumuko wa bei kwa Juni 2018 umepungua  hadi  asilimia 3.4 ikilinganishwa na asilimia 3.6 ya Mei mwaka huu.

Mkurugenzi wa sensa ya watu na takwimu za jamii, Ephraim Kwesigabo amesema hali hiyo imechangiwa na kupungua kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula.

Akizungumza leo Jumatatu Julai 9, 2018 amesema bidhaa zisizo za chakula zimechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa mfumuko wa bei kati ya Juni 2017 na Juni 2018.

"Bia zilipungua kwa asilimia 1.1, gharama za ukarabati wa vifaa vya umeme na viyoyozi kwa asilimia 1.8, gesi ya kupikia kwa asilimia 5.6 na majiko ya mkaa kwa asilimia 2.0," alisema Kwesigabo.

Kuhusu mfumuko wa bei za vyakula na vinywaji baridi, alisema mpaka Juni uliongezeka hadi asilimia 3.4 kutoka asilimia 2.6 uliokuwapo Mei.

Wakati mfumuko ukipungua nchini, hali imekuwa tofauti kwa nchi za Afrika Mashariki.

Nchini Uganda, amesema kwa mwaka ulioishia Juni mfumuko umeongezeka hadi asilimia 2.2 kutoka asilimia 1.7 uliokuwapo mwaka ulioishia Mei. Hata Kenya, mfumuko huo umeongezeka hadi asilimia 4.28 kutoka asilimia 3.95 za mwaka ulioishia Mei, 2018.

Lugola: Bodaboda dawa yenu inachemka, aja na mwarobaini kupunguza ajali

$
0
0
Kufuatia kuvuliwa cheo kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kutokana na ongezeko kubwa la ajali nchini na kuteuliwa kwa Kangi Lugola ambaye sasa anashika nafasi hiyo, Waziri huyo mpya tayari ameanza kazi kwa kasi hasa katika kutafuta suluhu za ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara.

Ambapo amesema Serikali inajipanga kuja na mbinu mpya ya kudhibiti na kupunguza ajali zinazosababishwa na pikipiki.

Lugola amesema Serikali itaanzisha utaratibu wa kufunga tela katika pikipiki kwamba abiria wataweza kupanda kati ya mmoja hadi wanne na kuketi katika tela hilo.

Kwa kufanya hivyo amesema ajali za pikipiki zitapungua kwa kiasi kikubwa sana kwani pikipiki zikishafungwa tela zitashindwa kutembea kwa mwendokasi mkubwa kutokana na uzito lakini pia zitashindwa kupenya penya barabarani na kufanya vurugu.

”Tutawafungia matela ya kubeba abiria na nyie mkae kwenye foleni kama bajaji na magari mengine. Matela haya yataleta utulivu barabarani lakini pia yatawaongezea tija kwani badala ya kubeba abiria mmoja sasa mtapakia zaidi” amesema Lugola

Ameongezea kuwa ufungwaji huo wa matela utahusisha zaidi pikipiki za biashara na hautazihusu pikipiki binafsi.

”Bodaboda dawa yenu inachemka Serikali inakuja na mpango madhubuti wa kupunguza kama si kumaliza kabisa ajali za barabarani zinazosababishwa na madereva pikipiki,” amesema Lugola.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 10

ACT- Wazalendo Wataja Sababu Chama Chao Kutokukubalika kwa Wanawake

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama cha ACT - Wazalendo, Ndg. Ado Shaibu amedai sababu kubwa ya  chama chao kuonekana hakikubaliki na wanawake wengi ni kutokana na mazingira yasiyo rafiki ya kufanya siasa za upinzani yalivyo nchini na kwamba hayavutii wanawake.

Shaibu amesema kwamba uwezo wa kuvutia wanawake kujiunga na vyama vya upinzani ni changamoto kwa kuwa siasa hizo ni za mikiki mikiki na hiyo imepelekea kuwa tatizo la ki-nchi na siyo la ACT tuu.

Kiongozi huyo ameongeza kwamba licha ya kwamba mazingira kuwa ni magumu, wao ACT wamechukua takwimu hizo za Taasisi ya TWAWEZA kama changamoto na wataangalia mbinu zinazofaa ili kushawishi wanawake wengi kujiunga na vyama vya upinzani.

"Takwimu za TWAWEZA hatupingani nazo japokuwa zina changamoto, kwa hili la kukubalika na wanaume zaidi ya wanawake tumelichukua kama changamoto. 

"Tunatafuta mbinu za kuweza kushawishi wanawake wengi kujiunga. Unajua uwezo wa kuvutia wanawake wakaja kwenye siasa za upinzani ni changamoto sana. 

"Siasa za upinzani ni mikiki mikiki, mabavu, vitisho, mahakamani na kiuhalisia wanawake wana majukumu mengi sana ikiwepo kulea familia hivyo inakuwa changamoto kwao," amesema Shaibu.

"Lakini ukienda hata kwenye vyama vingine huwezi kukuta wanawake wengi kuliko wanaume, hata ukienda Kamati Kuu ya CHADEMA, hii ni kutokana na mazingira ya siasa zetu yalivyo, hii ni changamoto kwetu sote". Aliongeza

Pamoja na hayo Shaibu amevitaka vyama vingine kutopuuza utafiti huo wa TWAWEZA unapotolewa na badala yake waufanyie kazi na hata kama kuna mapungufu wajitahidi kutoa maoni ya maboresho na siyo kubeza.

Katika takwimu zilizotolewa na TWAWEZA wiki iliyopita zinaonyesha kuwa Chama cha ACT- Wazalendo kinakubalika na asilimia 24 ya wanawake huku wanaume wakiwa ni asilimia 40 tu.

Kauli ya Jeshi la Polisi Baada ya Basi la Dar Express Kuteketea Kwa Moto

$
0
0
Baada ya basi la abiria  la Dar Express linalofanya safari zake Arusha - Dar es salaam kuteketea kwa moto  maeneo ya Tegeta,  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Marison Mwakyoma amesema bado wanamsaka dereva wa basi hilo ili kuweza kutoa maelezo ya kina juu ya ajali hiyo.

Kamanda Mwakyoma amesema kwamba ingawa taarifa za awali zinadai kwamba ni kufeli kwa breki ya nyuma, lakini zipo sababu za msingi ambazo zinaweza kutolewa na dereva huyo kwani tukio lililopelekea gari hilo kulipuka halikuwa la ghafla.

Akizungumzia ajali hiyo iliyotokea Tegeta  usiku wa kuamkia jana, Kamanda Mwakyoma amesema kwamba basi hilo lilitokea Arusha likuwa na abiria 42, ambapo 22 walishukia Bagamoyo na wengine waliosalia walifikia maamuzi  ya kushuka baada ya kuona gari linazidi kutoa harufu na ndipo dereva alipoamua kulitelekeza.

Aidha Mwakyoma ameongeza kwamba siyo kila ajali husababishwa na uzembe wa dereva kwani yapo mambo mengi ikiwepo nyaya za umeme kugusana, ku-jam kwa breki ya gari hivyo wamiliki wa magari wanapaswa kuwa makini wanapofanya 'service' ya magari ikiwa ni pamoja na kutazama mfumo mzima wa umeme na siyo kumwaga 'oil'.

Pamoja na hayo Mwakyoma amesema uchunguzi wa kina wa kuhusu ajali hiyo bado unaendelea kufanyika na sasa wanasubiria hati ya ukaguzi wa gari hilo kutokea Arusha kabla ya safari.

Vigogo Watano KNCU , TCCCO Kizimbani kwa Uhujumu Uchumi

$
0
0
Viongozi watano wa Chama cha Ushirika mkoa wa Kilimanjaro(KNCU LTD) na Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha Tanganyika (TCCCO) jana wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ,Moshi na kusomewa Mashtaka tofauti yakiwemo ya uhujumu Uchumi.

Waliofikishwa Mahakamani na kupandishwa Kizimbani ni pamoja na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Kikuu cha Ushirika ,Kilimanjaro (KNCU) Aloisi Kitau (70) Makamu Mwenyekiti mstaafu wa KNCU,Hatibu Mwanga(70) na Meneeja Mkuu wa KNCU ,Honest Temba (38).

Wengine waliofikishwa mahamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi ,Pamela Mazengo ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Kukoboa Kahawa (TCCC0) Maynard Swai (57) na aliyekuwa Meneja Mkuu wa TCCCo ,Andrew Kleruu wanaotajwa kukiuka sheria wakati wa ununuzi wa mtambo wa kukoboa Kahawa.

 
Washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi jana saa nne asubuhi wakiwa chini ya ulinzi polisi.

Washtakiwa hao walisomewa mashtaka na wakili wa Serikali Mwandamizi, Abdallah Chavulla saa 6:25 mchana.

Wakili Chavulla akishirikiana na mawakili wa Serikali, Jackline Nyantori na Shiza Kimera aliiarifu mahakama kuwa upelelezi wa kesi haujakamilika. Hakimu aliiahirisha hadi Julai 24.

Chavulla akiwasomea mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi, Pamela Mazengo alidai kati ya Julai 2014 na Novemba 2017, Kitau, Mwanga na Hatibu walitumia vibaya madaraka wakiwa viongozi wa KNCU.

Alidai katika tarehe tofauti, washtakiwa waliilipa kampuni ya Oceanic Link Shipping Services fidia ya Sh2.9 bilioni kitendo kilichoinyima haki KNCU.

Kampuni hiyo ilikuwa imewekeza katika shamba la Garagagua lenye ukubwa wa ekari 3,429. KNCU ililiuza shamba hilo kwa Sh9.3 bilioni ili kulipa madeni ukiwamo mkopo wa Benki ya CRDB.

Katika shtaka la pili, Chavulla alidai katika kipindi hicho, washtakiwa kwa kukusudia waliilipa kampuni hiyo na kuisababishia KNCU hasara ya Sh2.9 bilioni.

Katika kesi inayowakabili Swai na Kleruu, wanadaiwa kati ya Januari 2014 na Desemba 2015 walitumia vibaya madaraka yao na kununua mtambo wa kukoboa kahawa bila kufuata utaratibu.

Chavulla alidai washtakiwa hao walinunua mtambo wa kukoboa kahawa kutoka kampuni ya Brazafric ya Brazil bila kufuata utaratibu na kuisababishia TCCCo hasara ya Sh1.67 bilioni.

Washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mashtaka yanayowakabili husikilizwa na Mahakama Kuu. Washtakiwa hao walipelekwa rumande kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka kisheria ya kusikiliza shauri hilo na upelelezi wa kesi hizo haujakamilika.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images