Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Vyama vya msingi (AMCOS) Viajiri Watumishi Wenye Sifa

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) waajiri mameneja wenye sifa ili kuepuka ubadhirifu ndani ya vyama hivyo.

Ametoa rai hiyo jana (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.

Amesema watumishi ambao wamepata nafasi za juu katika AMCOS ni lazima wawe na elimu ya ushirika kutoka Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU). "Utumishi katika hivi vyama mara nyingi unaenda na uaminifu. Kama Chama kikiona kina mtu wanayemwamini, ni lazima kimpeleke chuoni ili apate sifa stahiki," alisema.

Alisema anataka kuona huduma za ushirika kwa wananchi zikiwianishwa na kile wanachofundishwa wataalamu kwenye vyuo vya elimu ya juu.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amemwagiza Makamu Mkuu wa Chuo cha Ushirika Moshi ahakikishe wanafunzi wanaopangiwa kufanya mafunzo kwa vitendo (field training) wanasambazwa kwenye AMCOS mbalimbali nchini.

"Wanafunzi wanaoenda field training kutoka kwenye Chuo chako, wapangiwe kwenda katika AMCOS. Hapa nchini tuna zaidi ya AMCOS 4,000 na wanafunzi wako 1,000 kwa hiyo kila mmoja akisimamia AMCOS nne, nne, watakuwa wamesaidia sana kupeleka elimu ya ushirika huko vijijini.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria sherehe hizo ni pamoja na Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba na Naibu wake Dkt. Mary Mwanjelwa. Wengine ni Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Ilemela, Angelina Mabula, Wakuu wa Mikoa ya Kagera, Mara, Simiyu, Wakuu wa Wilaya na viongozi wa CCM.

Siku ya Ushirika Duniani huadhimishwa Jumamosi ya kwanza ya Julai kila mwaka. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni: “Ushirika kwa ulaji wa uzalishaji endelevu wa bidhaa na huduma.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, JULAI 8, 2018.

Waziri Mkuu: Himizeni Wakulima Wakulima Kufungua Akaunti Benki

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka maafisa ushirika wawahimize wakulima wafungue akaunti benki ili kuepuka wizi wa fedha za vyamma vya msingi (AMCOS).

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.
 
Amesema kumekuwa na wizi wa kupanga unaofanywa na watu wachache wasio waaminifu. "Kuna AMCOS walienda kuchukua sh. milioni 50 benki, wakaja nazo kwenye pikipiki, wakati wanafungua mlango na boksi la hela liko hapo chini, ikaja pikipiki nyingine na watu wawili wakabeba boksi na kupotea nalo."

"Sasa ujiulize hao waliokuja na pikipiki ya pili walijuaje kama wale wa mbele walikuwa na fedha? Mtu anaporwa hela yote hiyo hata mchubuko hana, hiyo siyo sahihi, hizo ni hela za Chama cha msingi tunapaswa kuzilinda," alisisitiza.

Aliwataka maafisa ushirika wakasimamie jukumu hilo ili fedha ikilipwa na mnunuzi baada ya mnada, meneja wa AMCOS anaenda benki anaingiza hela kwenye akaunti za wanachama wake mara moja.

"Hii itaondoa shaka ya wanachama kuibiwa fedha zao, itaondoa hatari ya maafisa wa vyama vya msingi kutembea na fedha nyingi za Chama, na kuepusha wizi usio wa lazima. Hivi sasa wakulima wengi wana simu za mkononi. Ni rahisi kwao kupata ujumbe mfupi wa maandishi kwamba kuna fedha imetumwa katika akaunti yako," alisema.

Alisema Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwepo wa mfumo jumuishi wa huduma za kifedha (financial inclusion) ambao umesaidia kuwepo kwa mawakala wa kibenki hadi vijijini.

"Mkulima akitaka kuichukua fedha yake hana haja ya kusafiri hadi wilayani, sasa hivi anapata huduma hizo pale alipo kupitia kwa mawakala au kwenye mtandao wa simu," alisema.

Siku ya Ushirika Duniani huadhimishwa Jumamosi ya kwanza ya Julai kila mwaka. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni: “Ushirika kwa ulaji wa uzalishaji endelevu wa bidhaa na huduma.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Akemea Maafisa Ushirika Wenye Visingizio

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekemea tabia ya kutowajibika miongoni mwa watumishi kwa kisingizio cha mgawanyo wa madaraka.

Ametoa onyo hilo jana (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.

Amesema kuna maafisa ushirika ambao hawataki kuwajibika kwa sababu wameajiriwa TAMISEMI na wengine wako chini ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika.

"Afisa Ushirika wa Wilaya yuko mkoani ambako ni chini ya TAMISEMI, Mrajis Msaidizi wa Mkoa yuko Wizarani. Serikali ni moja, kwa hiyo wote bado mnawajibika kwa Mrajis Msaidizi wa Mkoa," alisema.

Aliwataka Wakurugenzi wa Halmashauri (DED) wasiwapangie kazi nyingine zilizo nje na taaluma yao maafisa ushirika wa wilaya na wahakikishe wanatoa taarifa kwenye vikao vya Halmashauri zao.

"Msimpe kazi ya kufundisha Afisa Ushirika kwa sababu hakuna mtu mwingine. Afisa Ushirika aachwe afanye kazi ya ushirika na atoe taarifa kwenye vikao vyenu. Madiwani mnapokutana kwenye Baraza, mpeni nafasi Afisa Ushirika aeleze maendeleo ya ushirika yakoje katika wilaya yenu."

Alisema changamoto nyingine zinazoikabili sekta ya ushirika ni wizi na ubadhirifu miongoni mwa watendaji wa vyama vya ushirika waliopewa dhamana ya kuvisimamia na kuviendesha vyama hivyo.

Alisema changamoto nyingine ni ukosefu wa elimu ya kutosha ya ushirika miongoni mwa wanachama, viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika; kuporomoka kwa imani ya ushirika miongoni mwa jamii na kwa baadhi ya wanachama kutokana na vyama vya ushirika kushindwa kukidhi mahitaji ya wanachama wake.

Nyingine ni uwepo wa madeni makubwa katika baadhi ya vyama vya ushirika nchini na baadhi ya viongozi wa kisiasa na wafanyabiashara kuwa na mtazamo hasi kwenye ushirika kwa malengo ya upotoshaji kwa maslahi yao binafsi.

Ili kukabiliana na changamoto hizo, Waziri Mkuu aliitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika ihakikishe kwamba usimamizi, udhibiti, uhamasishaji wa vyama vya ushirika unafanyika kikamilifu na kwa wakati kwa kuzingatia Sheria ya Ushirika namba 6 ya mwaka 2013 na kanuni zake za mwaka 2015.

Pia aliiagiza Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika iwasaidie wanaushirika katika mchakato wa urasimishaji wa mali zao na utoaji wa hati miliki za kimila za kumiliki ardhi kwa wakulima wadogo wadogo vijijini ili waweze kuzitumia kama dhamana ya kukopa mikopo katika taasisi za kifedha kwa ajili ya kilimo na shughuli nyingine za kiuchumi.

Aidha alizitaka mamlaka zote zinazohusika na maendeleo ya sekta ya ushirika nchini zijiwekee malengo yanayotekelezeka ya kusukuma gurudumu la maendeleo ya ushirika na kujipima kila inapohitajika.

Siku ya Ushirika Duniani huadhimishwa Jumamosi ya kwanza ya Julai kila mwaka. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni: “Ushirika kwa ulaji wa uzalishaji endelevu wa bidhaa na huduma.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Askofu Mkuu mwandamizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Yuda Thadeus Ruwa’ichi Kupokelewa Septemba 7

$
0
0
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam wa Kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amesema jimbo hilo linatarajia kumpokea Askofu Mkuu mwandamizi, Yuda Thadeus Ruwa’ichi, Septemba 7.

Kardinali Pengo alisema hayo jana wakati akiwapangia vituo vya kazi mapadri wapya na kuwabadilisha wale wa zamani baada ya sherehe za upadirisho, zilizofanyika katika viwanja vya Msimbazi Centre, jijini Dar es Salaam.

Juni mwaka huu, Papa Francis wa 16 alimtangaza Ruwa’ichi kuwa askofu mkuu mwandamizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Kardinali Pengo alisema mapokezi hayo yatategemea ujio wa hati yake kutoka kwa Papa Mtakatifu Francis wa 16, pamoja na yeye mwenyewe kuweka tayari vitu vyake.

“Kwa hiyo tarehe hiyo inaweza kubadilishwa kwa sababu hizo mbili,” alisema.

Kadhalika aliwataka vijana wa kanisa hilo kukimbilia upadri kwa sababu huko kuna uhakika wa ajira.

“Vijana kimbilieni huku kuna uhakika wa ajira, huku siyo kama huko kwingine kwa hiyo ni wakati wenu. Ninyi mapadri wapya nawapa likizo ya siku 28 ili muende huko mkamshukuru Mungu,” alisema Kardinali Pengo.

Aliwataka mapadri wapya kuwa tayari kufanya kazi mahali popote watakapotumwa ili waendelee kutenda kazi ya Mungu.

Live Video: Tazama Ndege mpya ya Tanzania Boeing 787-8 Dreamliner Ilivyowasili Nchini

$
0
0
Tazama hapa moja kwa kutoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, ndege mpya ya Tanzania aina ya Boeing 787-8 Dreamliner ikiwasili ikitokea, Seattle nchini Marekani.

Ndege hiyo ni ya nne kuwasili kati ya saba zilizonunuliwa na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuliwezesha shirika la ndege la Tanzania (ATCL) ili kuimarsha huduma zake

Dkt.Meru Ateuliwa Kuwa Mwenyekiti Wa Bodi Ya Wakala Wa Vipimo Na Mizani (Wma)

Rais Magufuli Awaongoza Watanzania Kupokea Boeing 787-8 Dreamliner

$
0
0
RAIS Dk.John Magufuli amewaongoza viongozi wa ngazi mbalimbali pamoja na Watanzania kupokea ndege mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 262 aina ya Boeing 787-8 Dreamliner ambayo imetua katika ardhi ya Tanzania saa 11.25 jioni.

Ndege hiyo kabla ya kutua ilichukua dakika kadhaa ikionekana katika anga la Tanzania huku Rais Magufuli  na Watanzania kwa ujumla wakiishangilia wakati inashuka.

Mbali na Rais Magufuli pia alikuwepo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan , Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali.

Baada ya ndege hiyo kutua ilipata heshima ya kumwagiwa maji kama ishara ya kuipokea rasmi.

Ndege hiyo ambayo ni kubwa na ya kisasa baada ya kupata heshima ya kumwagiwa maji kama ishara ya kuikaribisha ilikwenda eneo maalumu ambalo Rais amewaongoza Watanzania wengine kuipokea.

Baada ya ndege hiyo kusimama rasmi ulifunguliwa mlango ili waliokuja nayo washuke ambapo mlango ulifunguliwa saa 11:38 ambapo marubani walioleta ndege walikuwa wa kwanza kushuka huku wakipunga mkono.

Rais Magufuli aliipokea ndege hiyo kwa kukata maalumu kama kiashirio cha kuipokea rasmi ndege hiyo.

Hivyo waliokuja na ndege hiyo waliikabidhi kwa Rais ambapo alikatata utepe huo kushiaria kuipokea.

Rais Magufuli baada ya kuipokea aliingia ndani ya ndege hiyo.

Rais Magufuli amesema kuwa ujio ndege ni heshima na ni mali ya Watanzania na kuwataka wananchi watangulize maslahi ya Tanzania na kwamba tabia ya wizi, dhuluma haina nafasi na wengi.

Amesema hapo zamani katika shirika hilo kulikuwa na mambo ambayo hayakuwa na maana na ndio maana ndege hizo ni mali ya Serikali na ATCL wamekodishiwa.

“Tumeona mkono wa Serikali uingie ili kila kinachoingia tukione.Watanzania wengi wanaunga mkono na wale wachache ambao hawaungi mkono Mungu atawaumbua,”amesema Rais Magufuli.

Kwa upande wa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa ndani ya ndege hiyo amesema ni fahari kubwa kwani ni mali ya Watanzania.

Amesema wakati Rais anahimiza watu kubana matumizi wengi walikuwa hawamuelewi lakini sasa wanaona yanayofanyika.

Wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa ndani ya ndege hiyo amesema Rais anayo nia ya dhati ya kuleta maendeleo na kwamba kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu imesababisha ujio wa ndege hiyo.

“Rais anahimiza watu kufanya kazi na matoke yake watu wanafanya kazi na kulipa kodi ambayo ndio imesababisha kununulwa kwa ndege hiyo na nyingine,”ameema.

Mrema Aipongeza Serikali Kwa Kununua Ndege Mpya

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha United Democratic (UDP), John Cheyo ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kununua ndege pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa reli ya kisasa.

Wakati Cheyo akisema utekelezaji wa miradi hiyo unadhihirisha kuwa fedha ipo serikalini, mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema amesema ununuzi huo wa ndege umeitoa Tanzania aibu ya kutokuwa na ndege licha ya wingi wa rasilimali.

Wametoa kauli hizo leo Jumapili Julai 8, 2018 katika hafla fupi ya mapokezi ya ndege mpya ya Serikali aina ya Boeing 787-8 Dreamliner inayowasili leo nchini.

“Rais ametuvisha nguo tulikuwa uchi. Tulikuwa hatuna ndege kubwa wakati tuna rasilimali nyingi. Sasa jina la Tanzania litatukuka dunia nzima," amesema.

Mrema ambaye aliwania urais mwaka 1995 kwa tiketi ya chama hicho na kushika nafasi ya pili, amewataka wananchi kuacha kumsema vibaya Rais Magufuli ili aweze kuchapa kazi.

Rais Magufuli asema wasiofurahia Serikali Kununua Ndege ya Dreamliner Watapata Tabu Sana

$
0
0
Rais John Magufuli amebainisha sababu za kununua ndege ikiwa ni pamoja na kujenga heshima na kulinda hadhi ya Taifa.

Amesema ilikuwa aibu kwa Tanzania, nchi yenye idadi ya watu zaidi milioni 50 kutokuwa na ndege.

Pia, amesema Watanzania wengi wamefurahia ujio wa ndege hiyo na kwamba, kama wapo ambao hawajafurahia basi watapata tabu sana.

Dk Magufuli amesema hayo leo Julai 8, 2018 akipokea ndege aina ya Boeing 787- 8 Dreamliner iliyowasili saa 11:15 jioni.

Amesema ununuzi wa ndege hiyo ni jitihada za Watanzania wote ambao wanalipa kodi.

Rais ametaja sababu nyingine kuwa ni kuboresha huduma ya usafiri wa ndege nchini kwa sababu Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) lilikuwa na ndege moja pekee yenye uwezo wa kubeba abiria 51.

Amesema Watanzania wengi hawatumii usafiri wa ndege lakini haimaanishi kwamba hawapendi kutumia aina hiyo ya usafiri.

“Hawatumii kwa sababu ndege zilikuwa zinakwenda miji mitatu pekee, lakini sasa wanatua kwenye miji 12," amesema Rais Magufuli.

Amesema pia gharama zilikuwa kubwa, hivyo ujio wa ndege hiyo utapunguza gharama za usafiri na wananchi wa kawaida wataweza kusafiri.

Rais Magufuli amesema sababu nyingine ni kukuza sekta ya utalii nchini.

"Tunataka tuwe tunafanya safari za kimataifa. Ninaamini tukianza na ndege hii na ile nyingine ikija, ni wazi kwamba idadi ya watalii nchini itaongezeka," amesema.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi amesema ununuzi wa ndege una manufaa makubwa ambayo ni pamoja na kuimarisha mtandao wa usafiri nchini.

"Ndege hizi zitaimarisha biashara, uwekezaji na utalii nchi. ATCL zitunzeni ndege na muweke mipango mizuri ya biashara na kuilipa serikali fedha za ukodishaji kwa mujibu wa mkataba," amesema Balozi Kijazi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Leonard Chamliho amesema ndege ya Dreamliner itaanza safari katika miji ya Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mwanza ili kuwapa uzoefu marubani.

Amesema Septemba, 2018 ndege hiyo itaanza kwenda Bombay (India), Bangkok (Thailand) na Guangzhou (China).

Pia, amesema wameanza mchakato ili ndege hiyo iwe inatua Uingereza.

Rais Magufuli Kampa Ujumbe Mzito Balozi wa Marekani....." Wambie Boeing Wakamilishe Haraka Ndege Yetu ya Pili, Pesa Ipo"

$
0
0
Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemtaka Balozi wa Marekani afikishe salamu zake kwenye Kampuni ya ndege ya Boeing kuwa wakamilishe haraka ndege ya pili inayotakiwa kufika Tanzania kwa kuwa hela za kulipia zipo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo  katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, wakati wa sherehe za kupokea ndege mpya ya Boeing 787-8 Dreamliner  iliyowasili leo kutokea Seattle nchini Marekani.

"Ndege hizi ni matokeo ya Watanzania kulipa kodi na kuchapakazi. Nawapongeza wote walioshiriki kikamilifu. Ndege zote hizi tumenunua kwa fedha zetu wenyewe, hatujakopa kwa mtu. Tunataka Balozi wa Marekani utufikishie salam Boeing kuwa ile Dreamliner ya pili waikamilishe haraka, hela tunazo" - Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kwamba "Madai kuwa Watanzania wengi  hawafaidiki na ndege hayana msingi. Wapo wengi wanaohitaji ndege bei ilikuwa juu. Ndege hii imewafurahisha wengi na kama yupo mtu hajafurahia tukio hili basi huyo atapata tabu sana!-Rais Magufuli

Pamoja na hayo Rais amefafanua kuwa ndege hiyo imeletwa ili iweze kuimarisha na kuongeza mapato ya utalii nchini kwa kuwa 70% ya watalii wanatumia ndege.

Mh. Rais amesisitiza kwamba "Ukiongeza ndege wasafiri wanaongezeka. ATCL imeongeza wasafiri kutoka 4000 kwa mwezi mpaka 21,000 kwa mwezi. Tunaboresha usafiri wa reli, majini na barabara. Waliodhani kuwa maboresho ya Bandari hayana tija sasa wameaibika".

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya July 9

Kauli ya Mwigulu Nchemba Baada ya Ndege Mpya ya Dreamliner Kutua Nchini

$
0
0
Rais Dr. John Pombe Magufuli jana  ameipokea ndege mpya aina Boeing 787-8 Dreamliner ambayo imenunuliwa na Serikali mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini DSM.

Baada ya mapokezi hayo baadhi ya watu wamekua wakitoa pongezi zao akiwemo aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba ambapo ameandika katika ukurasa wake Twitter  kuwa; 

“Historia nyingine imeandikwa, tunakila sababu ya kujivunia maendeleo haya, Asante serikali yetu chini ya Rais J.Magufuli kwa hatua hii nyingine kubwa ya kuipeleka nchi yetu mbele katika usafiri wa anga.”

Waziri Kigwangalla Awasimamisha Kazi Maofisa Na Askari Wote 27 Wa Tawa Katika Pori La Akiba Uwanda

$
0
0
Na Hamza Temba, Rukwa
.......................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amewasimamisha kazi Maofisa na Askari Wanyamapori wote 27 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA katika Pori la Akiba Uwanda akiwemo Kaimu Meneja, Lackson Mwamezi kwa kushindwa kusimamia vizuri pori hilo na kutuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kuomba na kupokea rushwa.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku tatu tangu amsimamishe kazi meneja wa Pori hilo, Mark Chuwa kwa tuhuma kama hizo pamoja na tuhuma nyingine ikiwemo kushindwa kuondoa ngo'mbe zaidi ya 12,000 ambao wamedaiwa kuwepo ndani ya pori hilo.

Pori la Akiba Uwanda lipo katika bonde la ziwa Rukwa katika wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa na linasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Dk. Kigwangalla amefanya uamuzi huo jana alipotembelea pori hilo sambamba na kufanya mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kilyamatundu ambapo alipokea taarifa ya malalamiko kuhusu askari hao kupokea rushwa kutoka kwa watu wenye uwezo na kuwaruhusu kuchunga hifadhini huku wakiwanyanyasa masikini kwa kukamata mifugo yao.

Alifafanua tuhuma hizo kuwa ni pamoja na kudaiwa kujihusisha na vitendo vya kuomba na kupokea rushwa kutoka kwa wavuvi wanaovua samaki Ziwa Rukwa kwa kuwatozwa kila mmoja Sh. 100,000/- kwa mwezi na kuruhusu mifugo kuchungwa hifadhini kwa kipindi cha  miezi mitatu ambapo  kila mfugaji hutozwa  kati ya Shilingi milioni sita hadi saba.

Dk. Kigwangalla pia ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru kuchunguza mali  na tuhuma za rushwa walizopewa askari wote wa pori hilo wakiwemo watano waliotuhumiwa kwenye mkutano wa hadhara kwa kuomba rushwa ya shilingi milioni 6 kwa ndugu Shija Imeli ili wamruhusu kulisha mifugo yake hifadhini kwa muda wa miezi mitano.

Shija alisema mnamo tarehe 05 Januari mwaka huu akiwa nyumbani kwake na Ndugu Shemen Kuzenza, askari watano wa pori hilo walifika nyumbani kwake na kumtishia kuwa endapo atalisha mifugo hifadhini wangemkamata huku wakijua hana sehemu nyingine ya malisho hivyo wakamtaka kutoa rushwa ya shilingi milioni 6 ili aruhusiwe kulisha mifugo yake hifadhini kwa muda wa miezi mitano.

Alisema walifanikiwa kuwapa askari hao jumla ya shilingi mil. 5.8 kwa nyakati tofauti na kwamba walivyoshindwa kumalizia laki 2 zilizobakia askari hao walikamata mifugo yao nje ya eneo la hifadhi.

Kufuatia malalamiko na tuhuma hizo, Dk. Kigwangalla aliitisha gwaride la utambuzi lililohusisha askari wa Jeshi la Wananachi wa Tanzania (JWTZ), askari  wa usalama barabarani na maofisa na askari wanyamapori wa TAWA waliokuwepo katika mkutano huo wa hadhara.

Shija na mwenzake Kusenza waliweza kuwatambua askari watano wa TAWA waliowatuhumu kuwaomba rushwa na hapo hapo Waziri Kigwangalla akawaamuru kukabidhi silaha zao na kumuagiza  Mkuu wa Polisi wa  Wilaya ya Kipolisi  ya Laela, Aloyce Nyatola kuwakamata mara moja na TAKUKURU ianze uchunguzi wa tuhuma hizo ili sheria ichukue mkondo wake na iwe fundisho kwa wengine.

Hata hivyo, baada ya mkutano wa hadhara, Dk. Kigwangalla aliamua kukagua baadhi ya maeneo ndani ya pori hilo na kubaini uharibifu mkubwa uliofanywa na mifugo huku dalili zikiwa ni kinyesi cha ng'ombe kilichokuwa kimezagaa kila mahali.

Hapo hapo alimuagiza Mkurugenzi Mkuu TAWA, Dk. James Wakaibara ambaye aliwakilishwa na Mkurugenzi wa Biashara na Huduma za Utalii wa mamlaka hiyo, Imani Nkuwi kuwasimamisha kazi wafanyakazi wote wa pori hilo na kuleta wengine wapya wasimamie pori hilo ili kupisha uchunguzi.

"Hawa wote wasimamishwe kazi na uchunguzi ufanyike kitu gani kilikua kinaendelea hapa, kwanza ifanyike parade kuhusu suala la kumuomba rushwa yule mfugaji, wabainike moja kwa moja wafunguliwe mashtaka, na hawa wote nataka wachungunguzwe na mali walizonazo kama ambavyo imeelezwa kuwa hawa wametumia hili pori kama kitega uchumi chao binafsi, huu ni uhujumu uchumi" aliagiza Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo, Dk. Kigwangalla ametoa siku 30 kwa wananchi wote  wenye mifugo ndani ya pori hilo kuitoa kwa hiari yao wenyewe kabla ya operesheni maalum itakayowaondoa kwa nguvu. Alisema kama walijua pori hilo ni shamba la bibi sasa wasahau na wajipange namna ya kutafuta malisho au kupunguza idadi ya mifugo yao na kuanzisha miradi mingine ya maendeleo.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

Kangi Lugola afunguka tena kuhusu watu wanaopotea Akiwemo Azory Gwanda na Ben Saanane.

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amezungumzia tena suala la baadhi ya watu kutoweka akiwemo mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda na msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Ben Saanane.

Lugola ameeleza kuwa jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini uhalisia wa kutoonekana kwa watu hao na kwamba litatoa kauli yake baada ya kuthibitisha pasipo na shaka kuhusu kilichotokea.

Aliwataka Watanzania kuachana na uvumi usio na uthibitisho kuwa watu wanaotoweka wakiwa nyumbani kwao, kama ilivyokuwa kwa Azory wametekwa au kuuawa kwani Jeshi la Polisi ndilo lenye mamlaka kisheria kuthibisha hilo.

“Sio kila anayetoweka nyumbani kwake huwa ametekwa au kuuawa kama inavyovumishwa. Dhana hii inaniumiza na napenda watu waachane nayo,” anakaririwa na gazeti la Mwananchi.

“Tunaendelea kuchunguza kubaini sababu za kutoonekana kwao. Hauwezi kusema mtu amekufa bila kuwa na uthibitisho, na utathibitisha kwa kuuona mwili wake,” aliongeza.

Wazir Lugola aliongeza kuwa uchunguzi wa jeshi hilo ni kama jicho ambalo lina mwisho wa kuona, hivyo utakapofika mwisho wataeleza walichokibaini na mwisho kufanyia kazi jarada hilo ikiwa ni pamoja na kulifunga.

Ufafanuzi wa kauli ya Waziri Lugola umekuja ikiwa ni siku chache baada ya kuzua mijadala alipoeleza kuwa Serikali haiwezi kuingilia uhuru binafsi wa mtu kutoweka nyumbani kwake na kwenda anapotaka yeye.

Alisema watu wengi hufanya maamuzi yao wanapoona maisha yanawaendea visivyo, na huamua kwenda kuishi kokote watakapo na uamuzi wao huo unalindwa na Katiba ya nchi.

Gigy Money Azimikia Umbo la Vanessa Mdee

$
0
0
Msanii wa Bongo fleva Gigy Money amefunguka na kuweka wazi kuwa anavutiwa sana na umbo la msanii mwenzake Vanessa Mdee.

Moja kati ya vitu ambavyo vilitengeneza headlines kuhusu Gigy Money ni kupungua ghafla kwa mwili wake na kuzua tetesi kuwa anaumwa na maneno mengine mengine.
 
Lakini Kwenye mahojiano na Clouds Fm, Gigy Money amesema hivi sasa anajithidi kupunguza mwili wake ili aweze kutumbuiza vizuri jukwaani kama anavyofanya Vanessa Mdee.

"Kuna muonekano wa show tofauti na picha za Instagram mimi sasa hivi ni performer, huwezi kwenda jukwaani una limwili lako tu. Kwa hiyo mtu unatakiwa na mwili fulani hivi”.

"Do you look Vanessa akiwa ana-perform, how do you feel unaoana kabisa machachari, anaweza kuwa na bendi, anaweza kuinua mguu, unafurahi, sio mtu shabiki anasubiri utikise makalio tu”.

Siku chache zilizopita Gigy Money alikiri kuwa sababu pekee iliyomfanya mpaka apungue mwili ni mapenzi ambapo alikuwa anaumizwa na penzi la Baba watoto wake Mo J.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images