Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sababu ya Muna Love kuacha mwili wa Marehemu Mtoto Wake Airport

$
0
0
Baba mdogo wa marehemu, Patrick Peter, Bazo Komu amefafanua sababu ya mama mzazi wa mtoto huyo Rose Alphonce 'Muna Love' kuondoka uwanja wa ndege akiwa na dokumenti zitakazosaidia mwili wa mtoto wake kuchukuliwa katika uwanja wa ndege ni kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo.

Akizungumza katika uwanja wa ndege wa Mwl. Julius Nyerere, Bw. Bazo amesema hilo limetokea baada ya mwanamama huyo kupoteza nguvu baada ya kushuka uwanjani hapo na wao kumuingiza kwenye gari pasipo kukumbuka kuchukua dokumenti hizo.

Bazo ameweka wazi kwamba hakuna tatizo lingine ambalo lingesababaisha wao kushindwa kuuchukua mwili wa mtoto kwa kuwa mambo yote yalishapangwa na hakuna tafrani yoyote inayoendelea kuhusiana na mtoto wapi akazikwe.

"Hakuna tatizo lolote, wala hapakuwa na makubaliano ya mtoto azikwe wapi kwa sababu tunajua mama ni nani na baba ni yupi. Kitu kilichotokea ni kwa sababu wote tumemuona Muna hali yake ilivyo. Ameshuka hajiwezi, imebidi ashikiliwe ili aweze kutembea. Tumejisahahu kuzichukua hizo dokumenti baada ya kumuingiza kwenye gari. Na kwa hali ya kawaida huwezi kuingia kwenye pochi ya mwanamke kukagua" amefafanu Bazo.

Ameongeza, "Kwa sasa tunafanya utaratibu wa kujua jinsi gani hizo dokumenti zitafika hapa ili tuweze kuuchukua mwili wa mtoto tuweze kuendelea na taratibu zingine"

Waziri Tizeba afanya ziara ya kushtukiza katika Maduka makubwa ya Sukari na Mchele

$
0
0
Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba jana usiku amefanya ziara ya kushtukiza katika maduka makubwa ya kuuza sukari na mchele jijini Dar es salaam,na kubaini kuna uingizwaji wa bidhaa hiyo kimagendo na kutoa agizo kwa Jeshi la Polisi kuwakamata wahusika.

Waziri wa Kilimo akiambatana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Miraji Kipande amesema kuwa uuzwaji wa bidhaa hizo unahitaji mfanyabishara kufuata na kukamilisha utaratibu , hivyo wafanyabiashara wanaouza sukari na mchele kinyume cha sheria, Kanuni na taratibu za nchi wawajibishwe mara moja.

Katika ziara hiyo Waziri amekuta Sukari na mchele uliokuwa ukiuzwa na wafanyabiashara hao kinyume na taratibu za nchi, Sukari iliyokutwa ilikuwa  imefungashwa katika ujazo wa kilo moja moja na zilisomeka kuwa zimetoka nchini Mauritius na Uingereza ambazo ziliingizwa nchini bila ya kuwa na kibali cha Waziri Mkuu au Bodi ya Sukari Tanzania ambayo ipo chini ya Wizara ya Kilimo.

Kwa sasa wafanyabiashara hao wametiwa nguvuni na suala hilo limefikishwa Polisi kwa ajili ya uchunguzi na taratibu zingine za kisheria pindi uchunguzi utakapokamilika watuhumiwa hao watapandishwa kizimbani.

Hatimaye mwili wa Patrick wawasili Dar es salaam

$
0
0
Mwili wa mtoto wa muigizaji wa filamu nchini, Muna love, Patrick Peter, umewasili nchini leo saa 11:45 jioni na kupelekwa hospitali ya Aga Khan kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Taarifa zilizotolewa na Baba Mdogo wa Marehemu, Patrick ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi amesema kwamba Mwili huo uliondoka Kenya saa 9:40 jioni.

"Ratiba ya mazishi iko vilevile, kesho mwili utakuja nyumbani kwa baba wa mtoto Mwananyamala kwa ajili ya kuagwa na baadae utaagwa viwanja vya Leaders na utazikwa makaburi ya kinondoni. "Tunashukuru mwili umeshawasili, na tayari tumeshaupeleka Aga Khan kwa ajili ya kuhifadhiwa. "amesema Bazo.

Bazo amesema, baada mwili huo kuwasili ratiba zitaendelea kama zilivyopangwa hapo awali.

Waziri Jafoo Atoa Agizo Kwa Wakuu Wa Mikoa Wote Nchini

$
0
0
Na  Stella Kalinga, Simiyu
Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) Mhe.Selemani  Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa nchini kuweka mpango mkakati wa kuwahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ulioboreshwa kama alivyofanya  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka, ili kuwapunguzia wananchi gharama za matibabu.

Mhe. Jafo alitoa agizo hilo wilayani Busega mkoani Simiyu katika hafla ya kupokea Majengo ya wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji  katika Kituo cha Afya NASA, ikiwa ni moja ya vituo vya Afya 38 mkoani Simiyu, pamoja na magari tisa yakiwepo magari matatu ya kubebea wagonjwa (Ambulance) na magari Sita kwa ajili ya uratibu wa huduma za Afya  yaliyopatikana chini ya ufadhili wa  UNFPA/KOICA , msaada uliogharimu jumla ya shilingi bilioni 5.52.

 “Agenda yako Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ya kuhakikisha wananchi wote wanajiunga na Bima ya Afya, wewe utakuwa Mkuu wa Mkoa Kinara ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia mkutano huu niwaagize wakuu wa mikoa wote wahakikishe wanakuja na mpango wa kuwasaidia wananchi wao kupitia mikakati  watakayoibuni, kuwa kila mwananchi anakuwa na bima ya afya kupitia CHF iliyoboreshwa” alisema Jafo.

Awali akikagua  jengo la wodi ya wazazi na jengo la upasuaji katika kituo cha Nasa Waziri Jafo amepongeza viongozi wa Wilaya ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa kusimamia na kuhakikisha majengo hayo yanajengwa katika viwango bora kwa kutumia “Force Account” na kuwataka wananchi kuyalinda na kuyatunza majengo hayo.

Mhe. Jafo amewataka Waganga  Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanatoa huduma za afya vizuri katika maeneo yao kwa kuhakikisha kuwa wanakagua vituo vyao mara kwa mara badala ya kukaa ofisini.

Aidha, amewataka kuboresha mazingira ya vituo vyote vya afya nchini kuhakikisha vinakuwa visafi, huku akisisitiza  kusimamia kufungwa kwa mfumo wa Kielektroniki wa Kukusanya Mapato,   ili kuhakikisha kuwa mapato hayapotei.

Mhe. Jafo, amewataka wataalamu wa afya kuhakikisha wanakusanya na kuwa na takwimu sahihi za watoto wanaozaliwa na kufariki ili kuwezesha Serikali kuwa na takwimu sahihi zitakazowezesha kupambanana tatizo  la vifo vya akina mama na watoto.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Anthony Mtaka amewashukuru wafadhili Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA), kwa namna walivyoshirikiana na Serikali katika kuchangia kuboresha huduma za afya mkoani humo, ikiwa ni pamoja na kujenga vituo vya kutolea huduma za afya.

Kuhusu mkakati wa Mkoa juu ya Bima ya Afya, Mtaka amesema “Tungehitaji kuwa ni mkoa ambao kila mwananchi atafaidika na huduma zinazotolewa na  Hospitali na vituo vingine vya kutolea huduma za afya kwa kuwa na bima ya afya ili waweze kupata matibabu yao vizuri” .

Naye, Mkuu wa Idara ya Afya KOICA Tanzania  Kira Thomas amesema pamoja na kufadhili ujenzi wa vituo vya afya mkoani Simiyu, mkakati wao ni kuhakikisha Zahanati 31 mkoani Simiyu zinapatiwa vifaa vya dharura kwa ajili ya kutoa  huduma za dharura na kuongeza  damu kwa mama wajamzito wakati wa kujifungua.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Busega Mbunge wa Jimbo la Busega Dkt. Raphael Chegeni amesema uwepo wa wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji utatatua changamoto ya huduma za afya ya muda ya wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma na akaishukuru Serikali kwa kutenga shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya.

Waziri wa Kilimo: Serikali Kupambana Na Wabadhirifu Kwenye Vyama Vya Ushirika

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Mwanza
Serikali imetangaza Kiama kwa viongozi na baadhi ya watendaji wa vyama vya ushirika waofanya ubadhilifu wa Mali za ushirika kwa manufaa yao pekee pasina kuwanufaisha wanachama wote.

Imeelezwa kuwa ubadhilifu wa rasilimali za ushirika unaofanywa na baadhi ya viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika umekuwa ni tatizo sugu na hata kuwakatisha tamaa baadhi ya wananchi kujiunga na vyama hivyo.

Kalipio kwa wabadhilifu hao limetolewa na Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba Leo 6 Julai 2018 wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la wanaushirika Tanzania linalofanyika katika uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza.

Kongamano hilo la Siku mbili litaambatana na maonesho ya bidhaa na shughuli zinazofanywa na vyama hivyo vya ushirika kote nchini ambapo wanachama watapata fursa ya kubadilishana uzoefu, na kujadili mafanikio na changamoto wanazokabiliana nazo katika uendeshaji wa sekta ya ushirika nchini.

Dkt Tizeba aliwasisitiza washiriki wa kongamano hilo kutumia vizuri siku hizo mbili za kongamano hilo kwa ajili ya ustawi wa Maendeleo ya vyama vya ushirika na kujadili kwa kina namna bora ya uendeshaji na usimamizi wa vyama hivyo.

Alisema kuwa kauli mbiu ya siku ya ushirika Duniani kwa mwaka 2018 isemayo "Ushirika kwa ulaji na uzalishaji endelevu wa bidhaa na huduma" inakumbusha kwamba vyama vya ushirika sharti vihakikishe vinajitangaza na kutafuta Masoko ya bidhaa na huduma zake kwa jamii nzima.

Mhe Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba aliongeza kuwa serikali inatambua kuwa ushirika ni nyenzo muhimu ya kuwasaidia wananchi katika upatikanaji wa mtaji na kuwawezesha kuunganisha nguvu zao za kiuchumi katika kujiendeleza kiuchumi.

Alisema kuwa zipo juhudi kubwa zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanahamasishwa na hatimae kujiunga kwenye vyama vya ushirika kulingana na shughuli zao za kiuchumi ili kuondoa dhana kuwa vyama vya ushirika ni kwa ajili ya Kilimo cha Mazao ya biashara ya nchi za nje.

Sambamba na hayo Mhe Tizeba ameitaka Tume ya Maendeleo ya ushirika na shirikisho la vyama vya ushirika kuendelea kuwahamasisha wananchi kuendelea kutambua umuhimu wa kujiunga katika vyama vya ushirika kulingana na shughuli za wananchi mfano ushirika wa Viwanda, Madini, Ufugaji, Usafirishaji, Uvuvi na Kilimo.

Aliongeza kuwa serikali inatambua na kuthamini mchango wa ushirika wa Taifa katika kuyafikia malengo ya milenia na malengo mbalimbali ya nchi kama uimarishwaji wa sekta ya viwanda, Kilimo, uvuvi na biashara na kuchangia katika ongezeko la kipato kwa wananchi na hatimaye kuchangia katika ukuaji wa pato la Taifa

Kigwangallah: Mifugo Itakayokamatwa Kwenye Maeneo Ya Hifadhi Itataifishwa Bila Ya Huruma

$
0
0
Na Hamza Temba, Nkasi Rukwa
...............................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametangaza zoezi rasmi la kuanza kutaifishwa mifugo itakayokutwa kwenye maeneo ya hifadhi nchini kinyume cha sheria ili kukomesha vitendo hivyo.

Dk. Kigwangalla ametoa tamko hilo jana alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kizi kinachopakana na Pori la Akiba Lwafi lililopo wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja wilayani humo .

Amesema Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009, Kifungu cha 111 kinaruhusu kutaifisha mifugo na mali itakayokamatwa hifadhini.

Amesema kwa kipindi cha miezi tisa tangu ateuliwe kuiongoza wizara hiyo amekuwa akitoa msamaha kwa wnanchi wanaakamatwa na mifugo hifadhini jambo ambalo kwa sasa hatofanya tena kwakuwa elimu imeshatolewa vya kutosha.

"Maeneo ya hifadhi sio shamba la bibi lisilokuwa na mwenyewe, ni lazima watu waheshimu sheria za uhifadhi, nawahakikishia tukiwakuta kwenye maeneo ya hifadhi, tutawakamata na kutaifisha mifugo yenu, hakutakuwa na huruma wala msalia mtume" alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo Dk. Kigwangalla ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kuwasilisha ahadi iliyotolewa na Waziri aliyemtangulia ya shilingi milioni 3 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Kizi. Pia ameiagiza mamlaka hiyo kuchangia mabati kwa ajili ya darasa moja katika kijiji hicho ili wananchi wanufaike na faida inayopatikana kwenye uhifadhi.

Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji Mwingine Tena

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kesho Julai 7, 2018  atafanyiwa upasuaji wa mwisho utakaomwezesha kutembea bila msaada wa magongo.

Ujumbe wa Lissu alioutoa leo Julai 6, 2018 kutoka nchini Ubelgiji anakoendelea na matibabu,  ameeleza safari ya matibabu yake inavyoendelea hadi sasa.

Lissu, aliyeko nchini Ubelgiji kwa matibabu anafanyiwa upasuaji huo ikiwa ni mwendelezo wa matibabu anayopatiwa tangu aliposhambuliwa kwa risasi  zaidi ya 30 Septemba 7, 2017 akiwa katika makazi yake mjini Dodoma.

“Operesheni ya mwezi uliopita imepona, angalau kwenye muscles (misuli). Mfupa bado una kazi kubwa kidogo na utachukua muda kupona,” amesema Lissu.

“Licha ya maendeleo haya mazuri, bado kuna operesheni moja zaidi inahitajika. Madaktari wangu walipaswa kuniwekea ‘metal frame’ ya kusapoti mfupa uliofanyiwa operesheni mwezi uliopita.”

Mwasheria huyu mkuu wa Chadema amesema, “hata hivyo, hiyo ilishindikana kwa sababu operesheni yenyewe ilichukua saa saba na nilipoteza damu nyingi sana.”

Amesema mguu huo wa kulia uliumizwa sana kwa risasi, “ulivunjwa sehemu mbili na mfupa wa juu ya goti uliharibiwa. Kazi ya kuurekebisha ni ngumu sana kwa sababu hiyo.”

“Madaktari  wa Nairobi (Kenya) na wa hapa (Ubelgiji) wamefanya kazi kubwa kuhakikisha wanautibu vizuri mpaka sasa naweza kusimama na kutembea, hata kama ni kwa kuchechemea kwa magongo.”

Amesema upasuaji huo atafanyiwa kesho asubuhi ili kukamilisha tiba ya mguu huo na kwamba akipona ataweza kutembea bila msaada wa mgongo.

 “Madaktari wangu wameniambia kwamba hiyo ‘metal frame’ itakaa mguuni kati ya miezi sita hadi nane. Hata hivyo, haina maana kwamba nitakaa hospitalini kwa muda wote huo,” amesema.

“Haina maana kwamba sitaweza kufanya kazi yoyote ile katika kipindi hicho. Kwa kushauriana nao, pamoja na nyie ndugu, familia na jamaa zangu na viongozi wenzangu, tutaangalia mambo ninayoweza kuyafanya wakati nikiwa kwenye safari ya full recovery.”

Varane,Griezman Waipeleka Ufaransa Nusu Fainali Kombe La Dunia Baada Ya Kuwachapa Uruguay 2-0

$
0
0
Timu ya taifa ya Ufaransa imeondolewa katika michuano ya Kombe la Dunia kwa kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Ufaransa.

Mchezo huo wa kwanza wa hatua ya robo fainali umemalizika kwa Ufaransa kujipatia mabao hayo kupitia kwa Raphale Varane na Antoine Griezman.

Matokeo hayo yanaifanya Ufansa kuipa tiketi Uruguay kuyaaga mashindano hayo ambayo ilitinga hatua hiyo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ureno.

Baada ya mchezo huo, baadaye kutakuwa na mechi nyingine baina ya Brazil na Ujerumani kuanzia saa 3 kamili usiku huu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya July 7

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Brazili Yafungasha Virago Kombe la Dunia....Ni Baada ya Kutandikwa 2-1 na Ubelgiji

$
0
0
 Kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kimeyaaga mashindano ya Kombe la Dunia kwa kukubali kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Ubelgiji.

Walikuwa ni Ubelgiji walioanza kutikisa nyavu za Brazil mnamo dakika ya 13 tu ya mchezo kupitia kwa Fernadinho ambaye alijifunga kwa mpira wa kichwa.

Ubelgiji walikuja tena kambani na kuweka bao la pili kwa mkwaju mkali ulioenda moja kwa moja nyavuni kupitia kwa Kevn De Bruyne kwenye dakika ya 31 kipindi cha kwanza.

Licha ya kuamka kwa kasi kipindi cha pili huku wakiutawala mchezo kuliko Ubegiji, Brazil walikosa nafasi nyingi ambazo kama wangezitumia vema wangeweza kupindua matokeo.

Mnamo dakika ya 76, Renato Agusto aliweza kuipatia Brazil bao la kufutia machozi na kuufanya ubao wa matokeo kuwa 2-1.

Baada ya kufunga bao hilo Brazil walionekana kupigana kufa na kupona ili kusawazisha lakini mpaka dakika 90 zinaisha walikuwa nyuma kwa mabao hayo mawili kwa moja.

 Ubelgiji sasa itacheza na Ufaransa kwenye nusu fainali.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Maelfu Ya Vijana Wa Jkt Na Mgambo Wafurika Ofisini Kwa Rc Makonda Kuchangamkia Fursa Ya Ajira

$
0
0
Maelfu ya Vijana waliohitimu mafunzo ya JKT na Mgambo na hawana kazi jana walifurika kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kwaajili ya kupatiwa ajira ya kusimamia kikamilifu suala la usafi na kuwatoza faini wanaochafua mazingira.
 
Akizungumza na Vijana hao RC Makonda ametangaza Rasmi kutengua kipengele kilichokuwa kikiwataka Wafanyabiashara kufunga maduka yao siku ya Jumamosi hadi Saa nne asubuhi kwaajili ya usafi na badala yake amewakabidhi jukumu hilo vijana wa JKT na Mgambo ambapo watakuwa wakiwakamata wafanyabiashara watakaokaidi kufanya usafi.

Aidha RC Makonda amesema vijana hao watakuwa na jukumu la Kusimamia kampuni zilizopewa kazi ya Usafi kwenye maeneo husika, Kuwakamata, kuwatoza faini watupaji wa taka pamoja na kufuatilia kujua kila nyumba inapeleka wapi taka wanazozalisha ambapo ifikapo Jumanne ya Julai 10 itakuwa ndio mwisho wa usajili wa vijana hao.

Hata hivyo RC Makonda amewataka vijana hao kutotumia nguvu kuwaadhibi watu watakaotii Sheria huku akiwahimiza pia kuwakamata vibaka wanaopora Mali za watu.

Kabla ya vijana hao hawajaanza kazi watapatiwa mafunzo ya sheria ya mazingira ili waweze kutekeleza majukumu yao pasipo kumuonea mtu.

TCRA yaagizwa kuzishughulikia kampuni za ving’amuzi

$
0
0
Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) imetakiwa kuzichukulia hatua kampuni za ving'amuzi ambazo zinakiuka leseni kwa kuzuia matangazo ya chaneli za bure.

Agizo hilo limetolewa jana Julai 6 na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi   Mhandisi Atashasta Nditiye wakati kamati ya bunge ya miundombinu ilipotembelea (TCRA).

Mhandisi Nditiye amesema serikali haitazifumbia macho kampuni zinazoleta michezo ya kijanja wakati zinafahamu fika maelekezo ya leseni zao.

"Hakuna kufumbia macho, kama kuna mtu nyumbani kwake hajalipia king'amuzi halafu amekatiwa chaneli za bure asisite atoe taarifa na hatua zichukuliwe haraka,"

Amesema kampuni za Star times, Digitek, Ting na Continental zinatakiwa kurusha bure chaneli tano za hapa nchini ili kuwapa fursa wananchi kupata taarifa. Chaneli hizo ni TBC, ITV, Channel ten, EATV na Star TV.

Nditiye pia ameziagiza kampuni za simu kuzingatia usajili wa laini kwa kutumia teknolojia ya biometriki ambayo inahusisha uchukuaji wa alama za vidole na picha ya mtumiaji wa namba husika.

Amesema mfumo huo wa usajili una lengo la kuhakikisha namba moja ya simu inatumiwa na mtu mmoja hivyo itasaidia kukabiliana na vitendo vya matumizi mabaya ya mawasiliano.

"Niwaambie watanzania kuwa changamoto ya watu kutumia vibaya laini za simu limeshapatiwa ufumbuzi na linakwenda kumalizika kabisa muda si mrefu kutokana na mfumo huu,”

“Sasa mtu akisajili namba lazima zichukuliwe alama za vidole na picha apigwe ili tujue kabisa namba fulani inatumiwa na nani,”

Kuhusu utapeli unaofanywa na wanaotuma meseji za kuelekeza fedha itumwe amesema tatizo hilo limeshatatuliwa.

Tiba Bora ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume

$
0
0
OFA! Je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? Sasa utapona kwa sh 15000 tu .Ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku .Ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hela yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu, huwezi kuamini Ila wengi wameiamini,inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja 

Dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume 

Dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia 

Ni dawa ya asilia, haina madhara yoyote,watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi

Pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini s kwa bei ya ofa, ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote 

Imesaidia watu zaidi ya 148 ndani ya mwaka mmoja tangu igunduliwe  na Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia 

Pia tunatibu magonjwa mbalimbali, kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, nk 

Maelezo zaidi ; Dr kiboko-  0679923297

IGP Sirro akemea uhalifu wa majini

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro ametangaza kiama kwa maharamia na wahalifu wanaofanya uhalifu ndani ya Ziwa Victoria, maziwa mengine na bahari ndani ya mipaka ya Tanzania akisema siku zao zinahesabika.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya mwezi mmoja kwa askari polisi 30 wa kikosi cha maji jijini, IGP Sirro alitaja matukio yatakayokomeshwa ndani kipindi kifupi kijacho kuwa ni pamoja na yale ya kuvamiwa na kuporwa kwa wavuvi ndani ya ziwa hilo linalochangiwa na nchi tatu za Kenya, Uganda na Tanzania.

“Serikali imejipanga kukomesha uhalifu ndani ya maji yote ndani ya mipaka ya Tanzania; siku za maharamia ndani ya Ziwa Victoria na maeneo mengine nchini zinahesabika,” amesema IGP Sirro

Amesema askari waliofuzu mafunzo hayo pamoja na wengine ambao tayari wamenolewa kukabiliana na maharamia ndani ya maji watatumika kufanya doria ziwani kudhibiti uhalifu wa aina zote ikiwemo wizi na biashara haramu.

Katika mikakati hiyo, Serikali kwa mujibu wa IGP itanunua boti na zana za kisasa kwa ajili ya doria ziwani.

Mkuu wa Chuo cha Wanamaji kilichopo jijini Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi Mboje Kanga alisema pamoja na mafunzo ya nadharia darasani, askari hao pia wamepata mafunzo kwa vitendo ndani ya ziwa na kufuzo kwa viwango vya juu katika mapambano dhidi ya vitendo vya ujangili, uharamia, ugaidi na aina zote za uhalifu ndani ya maji.

“Asakari wanaohitimu mafunzo katika chuo hiki kilichoanzishwa mwaka 2011 wana uwezo, ujuzi na ujasiri wa kupambana na uhalifu na vitendo vyovyote haramu ndani ya mito, maziwa na bahari,” amesema Kanga

Uteuzi Mwingine Uliofanywa na Rais Magufuli

Waziri wa Afya: “TFDA isiwe chanzo cha vikwazo katika juhudi za Tanzania ya Viwanda"

$
0
0
Na  WAMJW, Dar as Salaam
Mamlaka ya chakula na dawa TFDA imetakiwa kuwa chachu ya uchumi wa viwanda hususani katika kuzalisha dawa hapa nchini ili kupata matokeo chanya katika hatua ya kuinua uchumi wa viwanda.

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa kukabidhi vyeti vya ithibaki kwa kiwango cha kimataifa ISO 17025 kwa maabara ya chakula na maikrobailojia za TFDA.

“TFDA isiwe kikwazo kwa wawekezaji nchini hususan Viwanda vya kuzalisha dawa ili kuunga mkono juhudi za Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli ya kuelekea uchumi wa viwanda”

Aidha,Waziri Ummy amesema TFDA wanawajibu wa kuwawezesha wafanyabiashara kutoa bidhaa zao wanazozileta nchini mapema zaidi Mara wanapokuwa wamejiridhisha na ubora unaokidhi afya za watanzania na kuwapa vibali mapema.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA )Agnes’s kijo amesema wanawajibu wa kuimarisha afya za watanzania na kuimarisha maabara zao kwa viwango vinavyokubalika kitaifa.

Kijo amesema vyeti hivyo vya kimataifa ni ishara kubwa inayoonyesha Kuwa TFDA inafanya kazi katika kudhibiti ubora wa bidhaa hususan vyakula na dawa ili kujenga afya za wananchi.

TFDA imepokea vyeti vya uthibiti kwa kiwango cha kimataifa kwa maabara ya chakula na daea ambapo wamefanya vizuri katika upimaji wa vyakula na dawa vinavyoingia na kutoka nchini.

Mkuu wa Majeshi Mstaafu Davis Mwamunyange Kateuliwa na Rais Maguful

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Jen. Mstaafu Davis Mwamunyange kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya  Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

Jen. Mstaafu Mwamunyange ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ) Mstaafu. Uteuzi wa Jen. Mwamunyange unaanza July 7, 2018.

Wamarekani Watatu Watiwa Mbaroni Uwanja wa Ndege Wakiwa na Madawa ya Kulevya

$
0
0
Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), imemkamata raia wa Marekani, Loniel Royford (63) kwa tuhuma za dawa za kulevya kilo 2.18 aina ya heroin.

Kamishna wa operesheni, Frederick Milanzi amesema Royford alifika Juni 29 akijitambulisha kama mtalii lakini alitiliwa shaka wakati anaondoka nchini Julai 4. “Tulimtilia shaka, mtalii amekuja na kukaa siku chache, yaani Juni 29 na akataka kuondoka Julai 4, tukampekua akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA),” alisema Milanzi.

Milanzi alisema licha ya mashine za X-Ray kukagua bila kuona dawa sehemu hizo mwilini na kwenye mizigo yake, polisi hawakumruhusu kuondoka.

“Hawa watu wanatumia mbinu za hali ya juu, baada ya kumkagua kwa kina tulibaini amefumua begi na kuweka kitambaa kingine maalumu ambacho si rahisi x-ray kubaini kama kuna dawa za kulevya,” alisema.

Alisema hata walipopekua mabegi yake na kutoa mizigo yote lakini hawakuona dawa na kwamba baada ya kufumua begi hilo, walikuta kilo 2.18 za dawa aina ya heroin.

“Tulizipeleka kwa mkemia mkuu wa Serikali na akathibitisha ni heroin,” alisema. Pamoja na huyu, raia wengine wawili wa Marekani, wenye asili ya India mtu na mkewe, walikamatwa Juni 28 wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) kwa tuhuma za kukutwa na kilo 8.9 za heroin.

Milanzi aliwataja raia hao kuwa ni Imtiaz Hussein Sheikh (53) na mke wake, Miranda Sheikh (61).

“Taarifa zilitoka hapa kwetu makao makuu lakini tulituma ofisa wetu ambaye alikwenda Kia na akashirikiana na polisi wa kule hadi kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images