Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Full on: Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
Full on: Ni dawa bora ya nguvu za kiume, hukufanya ufurahie tendo la ndoa kwa asilimia mia (100%) bila kuchoka 

Itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara 4  bila kuchoka, itakufanya pia uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30 kwa tendo la kwanza pia huchochea hormone za ashki,pia kuzalishwa kwa wingi kwenye mfumo wa uzazi

Gembe: huboresha maumbile madogo ya kiume na kuyafanya yawe kwenye umbo sahihi na litakalomtosheleza mke/mpenzi kwa asilimia 100% kwa kuwa matatizo haya huwa na vyanzo vyake kama vile kufanya punyeto,masturbation)diabetes) kisukari,matatizo ya neuron)yaani mishipa ya fahamu,mgoro,ngiri,tumbo kuunguruma,magonjwa ya mfumo wa mkojo mfano U.T.I.gono, miguu kuwaka moto na kufa ganzi.

Pia tunatibu kutokwa na nyama sehemu ya haja kubwa kwa siku3,pia kutibu busha bila kupasua,mvuto wa mapenzi
 
Kama huna muda wa kufika ofisini kwetu utaletewa popote. Mikoani unatumiwa bus 

Tupo Mbagala Rangi tatu

Simu;  0762606571 / 0787575969- Dr Mijingo

ACT Wazalendo Yawataka Nape, Bashe na Hawa Ghasia Wahame CCM, Wajiunge ACT- Wazalendo

$
0
0
Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi ACT Wazalendo, Ado Shaibu amefunguka kuwa hakuna mwanaharakati anayeweza kulitetea Taifa akiwa chini ya Chama tawala.

Shaibu amefunguka hayo katika mkutano wa wake na wanahabari jan, katika ofisi za Chama hicho ambapo alisema kuwa endapo wabunge, Nape, Bashe na Hawa Ghasia wana nia ya dhati ya kuwatetea wanyonge wahamie ACT-Wazalendo.

“Wabunge wanaotetea haki za wanyonge, wakina Nape, Bashe na Hawa Ghasia haiwezekani kufanya harakati za kuwatetea wanyonge huku mkiwa CCM, sana sana mtaonekana waasi katika chama chenu njooni kwetu”, alisema Shaibu.

Hayo yamejiri ikiwa ni siku chache kabla ya kuahirishwa kwa vikao vya Bunge, liliibuka sakata la korosho lililokuwa likiendelea katika vikao vya Bunge, ambapo Wabunge wa CCM ambao waliokuwa wakilipigia kelele suala hilo ni Hussein Bashe, Nape Nnauye pamoja na Hawa Ghasia.

Rais Magufuli: Ni Marufuku Kuwahudumia Wafungwa Bura, Wafanye Kazi

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli ametoa agizo kwa Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi, aliyeapishwaa jana Kangi Lugola kuwa anapaswa kuanzisha mpango madhubuti wa kusimamia na kuwatumia wafungwa katika mpango kazi wa kilimo, na sio kuwalea magerezani.

Akizungumza jana katika hafla ya kuwaapisha viongozi walioteuliwa,alimwagiza Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kuhakikisha wafungwa wote nchini wanafanyakazi katika mashamba ya kilimo ili kuzalisha chakula kwa faida ya nchi.

“Haiwezekani Tanzania ikawa ni nchi ya kupoteza fedha nyingi kuwahudumia wafungwa na kupata hasara wakati Nchi za wenzetu wanatumia wafunga katika shughuli za uzalishaji”, alisema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli aliongeza kuwa suala la muda upi wa wafungwa kufanya kazi, atajua mwenyewe iwe usiku au mchana, anachotaka yeye ni kazi tu.

Kiwanda Kikubwa Cha Dawa Kujengwa Nchini

$
0
0
Kiwanda kikubwa cha kutengeneza dawa kinatarajiwa kujengwa nchini ili kupunguza adha na gharama zinazoikumba nchi wakati wa kuagiza dawa nje ya nchi.

Hayo yamesemwa leo Julai 3 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu wakati wa kujadili uwekezaji wa kiwanda cha dawa hapa nchini.

"Leo tumekutana kujadili jinsi ya kuwekeza na kiwanda cha kutengeneza dawa cha FOSUN PHARMA hapa nchini ili kupunguza changamoto za kuagiza dawa nje ya nchi na kutokomeza tatizo la upatikanaji wa dawa nchini,” amesema Waziri Ummy.

Amesema kujengwa kiwanda hicho kitapunguza asilimia kubwa ya fedha inayokwenda nje kwa ajili ya manunuzi ya dawa kwani mpaka sasa asilimia 94 ya fedha zinakwenda kununua dawa nje na asilimia 6 ndiyo inanunua dawa ndani ya nchi.

Waziri Ummy amesema uwekezaji huo utapunguza muda wa kuagiza dawa kwani muda mwingine huchukua miezi tisa mpaka 11 kupata dawa kutoka nje ya nchi hivyo kuifanya Serikali kuagiza mzigo mkubwa zaidi ili kukimbizana na mahitaji ya Watanzania.

"Tunatumia muda mrefu kupata dawa tangu tunapoagiza na wakati mwingine tunaweza kupata dawa zisizo na ubora kutokana na dawa hizo kukaguliwa na mdhibiti wa nje hivyo zinaweza zikaruhusiwa tu na zikija kukaguliwa na mdhibiti wa ndani unaweza kukuta hazina ubora,” amesema Waziri Ummy.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa kampuni hiyo inayotengeneza sindano za kutibu malaria kali ya ATESUNAT itaweza kutengeneza sindano nyingi zaidi na kuweza kuwahudumia nchi jirani ikiwemo Kenya, Uganda na Burundi.

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema kuwa hakuna kikwazo kwa kampuni hiyo kuanzisha ujenzi wa kiwanda cha dawa hapa nchini kwani kitasaidia upatikanaji wa dawa kwa urahisi na kukua kwa uchumi kupitia viwanda.

"Tumejadili na kuwakubalia bila ya kuweka kikwazo kwani tumeridhishwa na ubora wao katika utengenezaji wa dawa na mafuta nchini kwao hivyo tunawakaribisha kuja kufanya uwekezaji huo," amesema Waziri Mwijage.

Naye Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji Nchini, Geofrey Mwambe amesema kuwa wameupokea uwekezaji huo na wanaufanyia kazi haraka iwezekanavyo ili kuipeleka Tanzania kuelekea uchumi wa Viwanda.

"Kutokana na ahadi ya Rais Dk John Pombe Magufuli la kuipeleka nchi kwenye uchumi wa viwanda na kutokomeza kabisa tatizo la uhaba wa dawa hatuna budi kushirikiana na wawekezaji hao kutimiza lengo hilo," amesema Mwambe.

Mbali na mawaziri Mwalimu na Mwijage, kikao hicho cha kujadili uwekezaji wa kiwanda hicho cha kutengeneza dawa pia kimehudhuriwa na wawakilishi kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA, Bohari Kuu ya Dawa (MSD),  Kituo cha Uwekezaji nchini TIC na wadau mbalimbali.

Mbunge Profesa Majimarefu Kuagwa Kesho July 4

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Steven Ngonyani maarufu kama Profesa Maji Marefu, ataagwa kesho na baadaye mwili kusafirishwa kuelekea jimboni kwake Korogwe kwaajili ya maziko.

Kaka wa marehemu, Hilary Ngonyani amesema kuwa taratibu za kuaga mwili wa marehemu zitatangazwa baadae, ikiwemo mahali itapaofanyika ibaada ya kuaga mwili wa marehemu Maji Marefu, pindi watakapokamilisha mawasiliano na ofisi ya Bunge.

“Mwili utabaki Muhimbili leo, hadi hapo kesho tutakapoaga katika viwanja ambavyo taarifa itatolewa badae baadaya ya kukamilisha mawasiliano na Ofisi ya Bunge, ambapo ataagwa na wakazi wa Jijini Dar es salaam pamoja na wabunge wenzake na baadaye tutaanza safari ya kuelekea Korogwe kwaajili ya shughuli ya Mazishi”, amesema Hilary Ngonyani.

Taarifa za kifo cha mbunge huyo ziliripotiwa usiku wa Julai 2, majira ya saa 3:20 na Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha.

June 6, 2018 mbunge huyo alifiwa na mkewe, Mariam aliyekuwa akipatiwa matibabu hospitali ya taifa pia.

IGP Sirro Kafanya mabadiliko kwa makamanda wa polisi kwa baadhi ya mikoa....RPC Wa Mbeya Kaondolewa

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi kwa baadhi ya mikoa.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 3, 2018  iliyosainiwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa, inasema mabadiliko hayo yanalenga kuongeza juhudi za kuzuia ajali zilizotokea mara kwa mara katika baadhi ya mikoa.

Katika mabadiliko hayo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Deusdedit Nsimeki aliyekuwa makao makuu ya upelelezi Dar es Salaam anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) Mkoa wa Simiyu.

Aliyekuwa RPC Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei anakwenda kuwa RPC Mkoa wa Mbeya.

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kaimu RPC Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Mussa Taibu amehamishiwa makao makuu ya polisi Dar es Salaam.

Aliyekuwa RPC Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Wilbroad Mutafungwa anakwenda kuwa RPC Mkoa wa Morogoro, nafasi yake ikichukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Emmanuel Nley kutoka makao makuu ya polisi Dar es Salaam.

Wengine waliohusika na mabadiliko hayo ni aliyekuwa Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Geita Kamishna Msaidizi wa Polisi, Stanley Kulyamo anayekwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara.

IGP Sirro amewataka makamanda wa polisi wa mikoa nchini, kuendelea kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha ajali hazitokei katika maeneo yao na kuwachukulia hatua kali madereva watakaosababisha ajali kwa uzembe.

Rais Magufuli Akutana Na Baadhi Ya Viongozi Wakuu Na Viongozi Wastaafu Ikulu Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam ili kukutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wakuu na viongozi wastaafu ambao anakutana nao kwa mara ya kwanza wote kwa pamoja.
Viongozi Wakuu wastaafu wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam tayari kukutana na kuzungumza na mwenyeji wao Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyewaalika.
Viongozi Wakuu wastaafu wakimsikiliza Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza nao leo.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Gharib Bilali.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mtaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, John Samuel Malecela.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Spika Mstaafu, Pius Msekwa.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Spika Mstaafu, Anne Makinda.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Jaji Mkuu Mstaafu, Jaji Barnabas Samatta.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Jaji Mkuu Mstaafu, Jaji Augustino Ramadhan.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Waziri Mkuu Mstaafu, Salim Ahmed Salim.

Rais Magufuli ajadiliana na Viongozi wastaafu Kuhusu hali ya nchi

$
0
0
Rais John Magufuli amewakaribisha viongozi wakuu wastaafu Ikulu huku akisema anajisikia mwenye baraka na heshima kubwa kukutana na viongozi hao.

Akizungumza leo Julai 3 katika hafla hiyo maalum, Rais Magufuli amesema amewakaribisha Ikulu ili ajadiliane nao kuhusu hali ya nchi na wamweleze bayana yale waliyoona ametekeleza vizuri na kumshauri pale alipoteleza.

Akiwakaribisha viongozi hao, Rais Magufuli aliyekuwa ameambatana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi, John Kijazi amewataka viongozi hao wajisikie wapo nyumbani na wasiwe na hofu kuzungumza chochote wanachofikiria.

“Kwangu ni heshima kubwa kukutana nanyi leo, mmenipa heshima kubwa kuitika wito wangu na kuja hapa wengi wenu mmeacha kazi zenu. Naona furaha kwani viongozi wengi sijawahi kuonana nao tangu wastaafu au niingie madarakani. Namwona Jaji Samatta ...sijawahi kuonana naye tangu astaafu. Wengi sijawahi kuona nao baadhi yao nimekuwa nikiwateua tu nasaini kwenye makaratasi nikiamini ninawajua lakini sijawahi kuwaona. Mzee Lowassa amewahi kuja hapa Ikulu tulikutana naye,” alisema.

Amesema amewaita kujadiliana nao kwa vile wao ni viongozi muhimu na kwa nyakati tofauti walitoa mchango mkubwa katika taifa hivyo kwake ni jambo jema kuonana nao ili kujadiliana kuhusu mambo ya nchi.

“Nina bahati kuwa kuwa kiongozi wakati viongozi wengi wakiwa bado hai, ni sehemu chache duniani kuwa kiongozi halafu wale waliokutangulia wakiwa bado wapo, nashukuru sana,” alisema.

Viongozi anaokutana nao ni pamoja marais waastafu, akiwamo Benjamin Mkapa na Aman Karume. Pia yupo makamu wa rais mstaafu Mohammed Gharib Bilal. Wengine ni mawaziri wakuu wastaafu, Dk Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, Cleopa Msuya, John Malecela, Edward Lowassa, Frederick Sumaye na Mizengo Pinda.

Pia, wamo maspika wastaafu, majaji wakuu wastaafu na viongozi wengine waandamizi waliomaliza muda wao.

Mahakama yatengua amri kukamatwa Babu Tale

$
0
0
 Mahakama Kuu imetengua na kufuta amri ya kuwakamata na kuwafunga gerezani wakurugenzi wa Tip Top Connection Company Limited, Hamis Shaban Taletale maarufu Babu Tale na ndugu yake Idd.

Uamuzi wa kufuta amri hiyo ulitolewa juzi na Jaji Edson Mkasimongwa baada ya kujiridhisha kuwa haikuwa halali kutokana na mamlaka iliyoitoa kutokuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Februari 16 naibu msajili wa mahakama hiyo, Wilbard Mashauri aliamuru Babu Tale na nduguye Idd wakamatwe na kupelekwa kifungoni katika Gereza la Ukonga kwa kushindwa kutekeleza hukumu ya mahakama na Aprili 4 alitoa na kusaini hati ya kuwakamata.

Katika hukumu iliyotolewa na Jaji Agustine Shangwa Februari 18, 2016 ndugu hao waliamriwa kumlipa fidia ya Sh250 milioni, mhadhiri wa dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde kutokana na makosa ya kutumia mahubiri yake kibiashara bila ridhaa yake.

Madereva wawili wa mabasi ya Mbunge Msukuma watiwa mbaroni

$
0
0
Jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia madereva wawili wa kampuni ya mabasi ya King Msukuma kwa makosa ya kuendesha magari yakiwa mabovu na kuhatarisha usalama wa abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Mwanza kwenda Kagera na jingine likitokea Kagera kwenda Mwanza.

Ubovu wa magari hayo ulisababisha abiria 120 kulazimika kulala kwenye kituo kikuu cha polisi Geita hadi walipoletewa usafiri mwingine jana asubuhi na kuendelea na safari zao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 3, Kamanda wa polisi mkoani hapa Mponjoli Mwabulambo amesema magari hayo yalikamatwa jana saa 11 jioni katika operesheni ya ukaguzi wa magari inayoendelea mkoani hapa.

Mponjoli amesema katika operesheni waliyoifanya walikagua magari 59 na 47 yalikutwa na makosa madogomadogo na kutozwa faini, mawili yalikuwa na matatizo makubwa na kuzuiwa kuondoka huku mengine yakiruhusiwa kuendelea na safari baada ya kuonekana hayana tatizo.

Amesema madereva wa mabasi ya kampuni ya King Msukuma wanaoshikiliwa ni Kini Daud (50) na Omary Oloyce.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Jumatano ya July 4

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
Katika kusherehekea miaka 15 ya kampuni ya NATURAL BEAUTY PROD tunatoa shukrani za dhati sana kwa wateja wetu wote kwa kutuunga mkono miaka yote hiyo.
 
TUNATOA OFFA YA WIKI NZIMA KWA WATEJA WETU UKINUNUA BIDHAA UTAPATA PUNGUZO LA 20%. KWA WATEJA WA MIKOANI UTATUMIWA BURE.

Ni bidhaa salama kabisa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda pia zina matokeo mazuri na kwa haraka zaidi.

🥑🍇🍋🍓🍒🌱🍇🍇
👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @210,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @140,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/=
11.YODI PILLS--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza (hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
GOOGLE
YOU TUBE
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod < WELCOME ALL>

Taarifa Kuhusu Taratibu Za Mazishi Ya Aliyekuwa Mbunge Wa Jimbo La Korogwe Vijijini, Marehemu Stephen Hillary Ngonyani

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ameongoza kikao cha pamoja baina ya uongozi wa Bunge na familia ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Korogwe Stephen Ngonyani maarufu kama Profesa Maji Marefu.

Kupitia taarifa iliyotolewa na kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano Ofisi Ndogo ya Bunge, imesema kuwa ibaada ya kuaga mwili wa marehemu Ngonyani, itafanyika katika viwanja vya Karimjee kuanzia saa 3:00 asubuhi na baada ya hapo mwili utasafirishwa kwenda wilayani Korogwe mkoani Tanga kwaajili ya mazishi.

“Jumatano tarehe 4 Julai, mwili wa marehemu utaagwa kwa heshima zote za Kibunge katika viwanja vya Karimjee vilivyopo jijini Dar es salaam, kuanzia saa 3:00 asubuhi na baadaye safari ya kuelekea jimboni kwake Korogwe kwaajili ya mazishi itaanza”, imesema taarifa.

Mheshimiwa Ngonyani amefariki usiku wa Jumatatu tarehe 2 mwezi Julai, katika hospitali ya taifa ya muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu, na atazikwa siku ya Alhamis ya tarehe 5, jimboni kwake Korogwe katika makaburi ya Kwa-Mndolwa.

Sweden Yatinga Robo Fainali Kombe La Dunia

$
0
0
Timu ya taifa ya Sweden imeibuka na ushindi wa bao 1-0, kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora Kombe la Dunia dhidi ya Switzerland iliyomalizika jana  usiku  huko Saint Petersburg huko Urusi.

Ushindi huo wa Sweden umeichukua historia ya Kombe la Dunia na kuirudisha nyuma hadi mwaka 1958, ambapo Sweden walikuwa wenyeji na walishinda mechi mbili mfululizo kwa mara ya kwanza robo fainali na nusu fainali na kutinga fainali.

Kabla ya kushinda dhidi ya Switzerland jana, Sweden ilitoka kushinda 3-0 mechi ya mwisho hatua ya makundi kwenye kundi F dhidi ya Mexico, hivyo mechi ya jana imekuwa ya pili mfululizo kwa Sweden kushinda.

Bao la Sweden limefungwa na kiungo Emil Forsberg  ambaye jana ripoti zilieleza kuwa kocha wa Manchester United Jose Mourinho, alitarajiwa kuwepo uwanjani kwaajili ya kumfuatilia nyota huyo ambaye ameibuka kiungo bora wa Sweden katika miaka ya 2014, 2016 na 2017.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Rais Magufuli akumbushia mbio zake za urais na Lowassa

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli amemsifia Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kuwa ni mtu mwema sana kwa kile alichokieleza kwamba hakuwahi kumtukana kipindi walichokuwa wanagombea pamoja katika Uchaguzi Mkuu wa Rais wa mwaka 2015.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo jana Julai 03, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na viongozi wakuu wastaafu aliowaalika kukutana nao katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Ikulu Jijini Dar es salaam.

"Nilifanya kazi katika kipindi chenu, mzee Mkapa aliniteua kuanzia Naibu Waziri kule ambapo Waziri Mkuu wetu alikuwa mzee Sumaye kwa kipindi chote cha miaka 10. Ikaja awamu ya nne, Waziri Mkuu wetu alikuwa mzee Edward Lowassa na bahati nzuri, uzuri wa Mh. Lowassa wakati wa kampeni tulipokuwa tunagombea wala hakunitukana hata kidogo ni mtu mwema sana huyu", alisema Dkt. Magufuli.

Mbali na hilo, Rais Magufuli amesema kuwa lengo kubwa ya yeye kuwaita wazee hao Ikulu kukaa ni kutaka kuwasalimia kwa kuwa inamuwia vigumu kwenda kwa mmoja mmoja.

"Nimeamua kuwaita hapa ili tukae, tufahamiane, tuzungumze na kama kuna mambo yoyote yale kuzungumza tufanye hivyo na mimi nahitaji busara za wazee ndio sababu kubwa ya kuwaita sina sababu nyingine yoyote lakini pia nimekuwa nimewakumbuka",  alisisitiza Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amesema na yeye anatamani siku moja akiistafu awe miongoni mwa wazee hao.

TRA Yakanusha Watanzania Kulipia WhatsApp

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Maneno ya Huzuni ya Rais Magufuli akimlilia Profesa Majimarefu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Yustino Ndugai kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mkoani Tanga Steven Hillary Ngonyani maarufu “Profesa Majimarefu”.

Profesa Majimarefu amefariki dunia usiku July 2, 2018 katika katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu hizo Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa na kifo cha Profesa Majimarefu ambaye alikuwa Mbunge hodari na aliyewapenda na kuwapigania wananchi wa Jimbo lake la Korogwe.

“Spika Ndugai nimehuzunishwa sana na kifo cha Profesa Majimarefu, tumempoteza mtu aliyejitoa kuwahudumia wananchi kwa juhudi zake zote, aliyependa maendeleo na aliyekuwa rafiki wa watu, nakupa pole sana wewe Spika, Wabunge wote, familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na wote walioguswa na kifo hiki” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufulli amemuombea Profesa Majimarefu apumzishwe mahali pema peponi.

England Yatika Robo Fainali Kombe La Dunia Ikiimaliza Colombia Kwa Penalyi 4-3

$
0
0
Timu ya taifa ya England maarufu kama 'Simba watatu', imetinga hatua ya robo fainali baada ya kuibuka na ushindi wa jumla ya penati 4-3 baada ya dakika 120 kuisha kwa sare ya 1-1 dhidi ya Colombia kwenye mchezo wa 16 bora uliomalizika jana usiku .

England ambayo iliongoza kwa bao 1-0 kutoka dakika ya 57 ilijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kusawazishiwa bao hilo katika dakika ya 90, hivyo kulazimu mchezo kwenda katika dakika za nyongeza kabla ya penati kuamua.

Katika mchezo huo mshambuliaji na nahodha wa England Harry Kane alifunga bao la England hivyo kufikisha mabao 6 na kuifikia idadi sawa ya mabao kama aliyofunga James Rodriguez wa Colombia kwenye fainali za mwaka 2014 nchini Brazil ambapo aliibuka mfungaji bora.

Jordan Pickford amekuwa golikipa wa kwanza wa England kupangua penati kwenye mechi ya mashindano tangu alipofanya hivyo kipa wa zamani wa England David Seaman dhidi ya Argentina mwaka 1998.

Penati za England zimefungwa na Harry Kane, Marcus Rashford, Kieran Trippier na Eric Dier huku Jordan Henderson akikosa. 

Kwa upande wa Colombia waliofunga ni Radamel Falcao, Juan Cuadrado na Luis Muriel huku Mateus Uribe na Carlos Bacca wakikosa. 

England sasa itakutana na Sweden kwenye mechi ya robo fainali siku ya Jumamosi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images