Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Full on: Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume

0
0
Full on: Ni dawa bora ya nguvu za kiume, hukufanya ufurahie tendo la ndoa kwa asilimia mia (100%) bila kuchoka 

Itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara 4  bila kuchoka, itakufanya pia uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30 kwa tendo la kwanza pia huchochea hormone za ashki,pia kuzalishwa kwa wingi kwenye mfumo wa uzazi

Gembe: huboresha maumbile madogo ya kiume na kuyafanya yawe kwenye umbo sahihi na litakalomtosheleza mke/mpenzi kwa asilimia 100% kwa kuwa matatizo haya huwa na vyanzo vyake kama vile kufanya punyeto,masturbation)diabetes) kisukari,matatizo ya neuron)yaani mishipa ya fahamu,mgoro,ngiri,tumbo kuunguruma,magonjwa ya mfumo wa mkojo mfano U.T.I.gono, miguu kuwaka moto na kufa ganzi.

Pia tunatibu kutokwa na nyama sehemu ya haja kubwa kwa siku3,pia kutibu busha bila kupasua,mvuto wa mapenzi
 
Kama huna muda wa kufika ofisini kwetu utaletewa popote. Mikoani unatumiwa bus 

Tupo Mbagala Rangi tatu

Simu;  0762606571 / 0787575969- Dr Mijingo

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Tatizo La Nguvu Za Kiume Kuboresha Uume Mdogo Tunatibu Busha Na Vidond Vya Tumbo

0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME KUBORESHA UUME MDOGO TUNATIBU BUSHA NA VIDOND VYA TUMBO :acha kujiona mpweka pale ukutanapo na mke au mpenzi wako kwa sababu kutokuwa na uwezo wa kumridhisha na ni chazo kikubwa cha ndoa nyingi kuvunjika au kusababida mke au mpenzi kusalitiana

 NI NINI TIBA YA NGUVU ZA KIUME 
Mapro power no 2 ndio tiba tosha kwa sasa kwani hutibu matatizo yafutayo;
 1 kuwai kufika kileleni kabla mwenzi wako hajakojoa, dawa hii itakufanya uchelewa kwa mda wa dakika 15 -20 
2 dawa hii itakufanya urudie tendo La ndoa zaidi ya Mara tatu 3, dawa hii hutibu tatizo La uume kuwa legelege 

4 dawa hii huondoa uchovu, miungurumo ya tumbo pale umalizapo kufanya tendo La ndoa.

Unasubili nini sasa... OKOA NDOA YAKO NA MAISHA YAKO SASA 

Makakanua;hii ni dawa ya kuboresha uume mdogo na mwembamba na kurudi kwenye hali yake ya awali kwani dawa hii husaidia kuitanua misuli ya uume haswa kwa wanaume waliofanyiwa tohara wakiwa watu wazima, kumbuka hakuna dawa ya kuongeza maumbile endapo umezaliwa ukiwa na uume mdago

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUWA MDOGO 1 kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima
 2 unene kupita kiasi 
3 kuvaa nguo za kubana sana
 4 kulala na nguo hasa zile za kubana kwa wale wanaoishi maeneo ya joto

TUNATOA DAWA YA KISUKALI,PRESHA, MIGUU KUUMA, KUPUNGUZA KITAMBI, MATITI MAKUBWA, PIA ZIPO DAWA ZA MVUTO WA MPENZI, MVUTO WA WATEJA KWENYE BIASHARA NK

Fika Mbagara Zakhemu barabara iendayo Kibonde maji utaona ofisi imeandikwa Mabura Crinic au piga simu no 0752348593 DR MABULA 

Kwa wateja wa Mwanza na mikoa ya jirani yupo wakala wetu hapo Mwanza. DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMI WOTE MNAKALIBISHWA

Bunge lahairishwa rasmi hadi Septemba

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa hoja ya kuahirishwa kwa mkutano wa 11 wa Bunge la Bajeti ulioanza Aprili 3 na kumalizika leo Ijumaa Juni 29, 2018.

Akiwasilisha hoja hiyo leo bungeni, Majaliwa amesema maswali 530 ya msingi na 1705 ya nyongeza yameulizwa na wabunge.

Pamoja na mambo mengine, Majaliwa amezungumzia masuala mbalimbali, zikiwemo halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mikopo kwa ajili ya vijana, wanawake na wenye ulemavu na zisaidie uundaji wa Saccos shirikishi za makundi.

Kuhusu uchangiaji damu, amewaomba wananchi kujenga utamaduni wa kuchangia damu ili kuwezesha upatikanaji wa damu kwa wingi kwa wenye uhitaji.

Akizungumzia Virusi vya Ukimwi na kampeni ya upimaji Ukimwi ya Furaha Yangu, amesema hadi kufikia Machi, 2018 watu wanaoishi na VVU walikuwa milioni 1.02, kati yao watu milioni 1.0 walikuwa wanatumia dawa za kufubaza virusi hivyo.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge Job Ndugai amesema, “tumemaliza Bunge hili maarufu la korosho na kuliwaka kweli kweli, Serikali imetuambia tuiamini na nafikiri mambo yatakwenda muswano.”

Serikali Yatenga 4.3bn/- Kujenga Vituo Vya Kuhifadhi Damu Salama

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga sh. bilioni 4.3 ili kujenga vituo vya kuhifadhi damu (satellite blood banks) kwenye mikoa 12.

Ameitaja mikoa hiyo kuwa ni Manyara, Katavi, Rukwa, Ruvuma na Njombe. Mingine ni Tanga, Arusha, Pwani, Singida, Songwe, Geita na Simiyu.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Juni 29, 2018) bungeni jijini Dodoma katika hotuba yake aliyoitoa wakati wa kuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge. Bunge limeahirishwa hadi Septemba 4, mwaka huu.

Amesema lengo la mpango huo ni kuboresha upatikanaji wa damu hasa kwa akinamama wanaopoteza damu nyingi wakati wa kujifungua. “Serikali imedhamiria kupunguza vifo vya akinamama na watoto vitokanavyo na uzazi. Katika kutekeleza azma hiyo, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo inaendelea kufanya ukarabati na ujenzi wa majengo ya upasuaji, maabara, wodi za wazazi, nyumba za watumishi na wodi za watoto,” amesema.

Amesema kukamilika kwa majengo hayo, kutaboresha huduma za uzazi kwa akinamama na watoto wachanga. “Hatua hii itawezesha upatikanaji wa huduma kamili za uzazi na kupunguza vifo vya mama na watoto. Katika mwaka 2018/2019, eneo litakalopewa kipaumbele ni kuimarisha upatikanaji vifaa na watumishi katika vituo 208 vinavyoendelea kuboreshwa,” amesema.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi watumishi wa afya, waongeze juhudi ya kuhamasisha wananchi wajitolee damu na pia akawaomba wananchi nao wawe na utamaduni wa kuchangia damu ili kuwezesha upatikanaji wa damu salama itakayohifadhiwa kwenye benki hizo.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kuimarisha huduma za kibingwa nchini kwa kutenga shilingi bilioni 14 ili kuanzisha huduma ya kuchunguza mwili bila upasuaji (PET Scan) katika taasisi ya Saratani ya Ocean Road.

Amesema kuanza kwa huduma hiyo kutapunguza asilimia 80 ya wagonjwa wa saratani waliokuwa wanapelekwa nje ya nchi kwa ajili ya kipimo hicho na kwamba Serikali itaweza takribani shilingi bilioni 5 kwa mwaka zilizokuwa zinatumika kwa ajili ya kulipia wagonjwa waliokuwa wakienda nje ya nchi kwa ajili ya kipimo hiki.

Amesema Serikali itasogeza huduma ya tiba ya saratani katika ngazi ya Hospitali za Kanda ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Bugando Mwanza, Hospitali ya Kanda ya Kaskazini KCMC na Hospitali ya Rufaa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini, jijini Mbeya.

“Vilevile, katika mwaka 2018/2019, Serikali itaimarisha upatikanaji wa huduma za kibingwa katika hospitali za rufaa za mikoa kwa kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya ikiwa ni pamoja na majengo, vifaa tiba na madaktari bingwa. Jumla ya shilingi bilioni 40 zimetengwa kwa ajili ya kuimarisha hospitali hizi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo kupitia Mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (Education Performance for Results – EP4R) itaimarisha miundombinu kwenye shule zenye uhitaji mkubwa.

“Katika mwaka 2018/2019, Serikali itatumia shilingi bilioni 155.58 kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe 25, ununuzi wa vifaa vya maabara, ujenzi wa mabwalo 85, vyumba vya madarasa 2,000 na motisha kwa Halmashauri kutokana na ufanisi katika utekelezaji wa vigezo vya EP4R,” amesema.

Amesema kwa sasa, Serikali inatarajia kuajiri walimu 4,785 wa shule za msingi zenye uhitaji mkubwa na kwamba tayari imeshatangaza nafasi za ajira kwa walimu 2,000 wa masomo ya sayansi, hisabati na lugha ambao watapangwa kwenye shule za sekondari zenye uhitaji mkubwa.

Amesema kuwa Serikali imetangaza nafasi za ajira kwa mafundi sanifu maabara 160 ambao nao pia watapangwa kwenye shule zenye uhaba wa wataalamu hao.

Tanzania Yaongoza Kwa Wanyama Pori Afrika......Ni baada ya Serikali na wananchi kulinda rasilimali za nchi

0
0
IMEELEZWA kuwa jitihada za Serikali za kulinda rasilimali za nchi na ushirikiano kutoka kwa wananchi zimesababisha ongezeko kubwa la idadi ya wanyama pori, hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye wanyama wengi barani Afrika.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 29, 2018) katika hotuba yake aliyoitoa bungeni wakati wakuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge jijini Dodoma.

Amesema ili kuitumia vema fursa ya kuwa na vivutio vingi ikiwemo wanyamapori wengi na kuleta tija kwa nchi, Serikali imeendelea kuandaa utambulisho wa Tanzania Kimataifa (Destination Branding), lengo likiwa ni kuitambulisha Tanzania kama kituo mahsusi cha utalii duniani.

“Tunalenga kuvutia wageni wa kimataifa waje kuitembelea Tanzania, kuongeza wigo wa kutangaza vivutio na kufanya vivutio vya utalii vifahamike duniani. Pia, Serikali inakamilisha mchakato wa kuanzisha Channelmaalum katika Television ya Taifa (TBC1) kwa ajili ya kutangaza utalii,” amesema.

Waziri Mkuu amesema maandalizi ya kuanzisha studio ya kutangaza utalii kwa njia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yanaendelea vizuri, ambapo studio hiyo itawezesha kutambua, kufuatilia na kuwasiliana moja kwa moja na watu wanaofuatilia Tanzania na vivutio vyake.

Pia, Serikali inakusudia kuanzisha chombo kitakacho simamia fukwe za bahari, mito na maziwa lengo la hatua hiyo ni kuimarisha utalii wa fukwe Bara na Visiwani kwa kujenga hoteli, maeneo ya mapumziko na michezo mbalimbali.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amezungumzia jitihada zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na changamoto ya migogoro ya matumizi ya ardhi miongoni mwa watumiaji kwa kuunda timu ya kisekta ikijumuisha watendaji wa sekta mbalimbali zinazohusika kwenye masuala hayo.

Sambamba na hilo, Waziri Mkuu amesema Serikali imeandaa mipango ya matumizi ya ardhi, kupima mipaka ya vijiji, kutunga na kurekebisha sera, sheria na kuandaa mipango mbalimbali ya kuboresha matumizi na utawala wa ardhi.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Serikali imeandaa mipango ya kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi nchini. “Ni matumaini yangu kwamba programu hii ikitekelezwa, ardhi itatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii na pia kudhibiti migogoro ya ardhi,”.

Waziri Mkuu amesema katika mwaka wa fedha 2018/19, Serikali itaendelea kutatua migogoro inayojitokeza na pia kutoa elimu kwa umma ili watumiaji wote wa ardhi waweze kuzingatia mipango ya matumizi ya ardhi inayoandaliwa katika vijiji.

Amesema katika juhudi za kudhibiti migogoro kwenye maeneo mbalimbali ya utawala, jumla ya vijiji 11,256 kati ya vijiji 12,545 vilivyopo nchini vimepimwa, hiyo ni sawa na asilimia 90 ya vijiji vyote, huku lengo likiwa ni kupima mipaka ya vijiji vyote na kuvipatia vyeti vya kijiji kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

“Hatua hii itasaidia kwa kiwango kikubwa kutatua migogoro ya mipaka kati ya vijiji. Ili kuharakisha kasi ya upimaji nchini, Serikali itaendelea kutumia makampuni binafsi ya upimaji na upangaji makazi kwa vibali maalum,”.

Akizungumzia kuhusu hifadhi ya mazingira, Waziri Mkuu amesema misitu inaendelea kukatwa hovyo kwa sababu mbalimbali ikiwemo matumizi ya nishati ya mkaa na kuni, ili kukabiliana na tatizo hilo Serikali itaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kote nchini.

Amesema Serikali itashirikiana na sekta binafsi kuweka utaratibu mahsusi wa kuwawezesha na kuwaratibu wajasiramali wanaojishughulisha na nishati mbadala ili kuwa na uzalishaji wa kutosha wa nishati hiyo na iweze kusambazwa katika maeneo yote nchini.

Aidha, Serikali itaendelea kuboresha na kukamilisha Mkakati wa Tungamotaka (National Biomass Energy Strategy) na kusambaza kwa wadau nchini ili kuratibu vyema upatikanaji na matumizi ya nishati hiyo.

Serikali Yawataka Watendaji Kuwajibika....Ni katika ukusanyaji wa mapato na nidhamu ya matumizi

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watendaji wa Serikali katika ngazi zote wawajibike ipasavyo kwenye ukusanyaji wa mapato na kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha na rasilimali za Taifa.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali itaimarisha ukaguzi katika ngazi zote na ufuatiliaji wa karibu wa miradi ya maendeleo na kufanya tathmini za mara kwa mara ili kuhakikisha kwamba miradi na kazi zitakazofanyika zinawiana na thamani ya fedha (Value for money) za umma zinazotolewa na Serikali. 

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Juni 29, 2018) katika hotuba yake aliyoitoa bungeni wakati wa kuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge jijini Dodoma.

Vilevile, Waziri Mkuu amesema taasisi zote za Serikali zinasisitizwa kutumia mifumo ya kieletroniki kukusanya mapato na wafanyabiashara wote wanahimizwa kutumia mashine za EFD na kulipa kodi kwa hiari.

Amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha kwamba malengo ya ukusanyaji wa mapato na matumizi yanazingatia bajeti iliyoidhinishwa na Bunge. “Viongozi na watendaji wote wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za matumizi ya fedha za umma katika eneo la ukusanyaji wa mapato,”.

Waziri Mkuu amesema Serikali itasimamia ipasavyo utekelezaji wa bajeti sambamba na kuongeza uwajibikaji na nidhamu ya matumizi ya fedha zilizoelekezwa katika vipaumbele mbalimbali kama ilivyoidhinishwa na Bunge.

Amesema katika utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya mwaka 2018/2019, Serikali itashirikiana na sekta binafsi, wadau wa maendeleo na wananchi wote kwa ujumla ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa katika mwaka 2018/2019, Serikali imepanga kutumia jumla ya sh. trilioni 32.48. Kati ya fedha hizo, sh. trilioni 20.47 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida sawa na asilimia 63 ya Bajeti na sh. trilioni 12.01, sawa na asilimia 37 ya bajeti yote zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wadau wa kilimo, mifugo, uvuvi na sekta nyingine watumie fursa mbalimbali zinazopatikana katika utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mpango ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDPII),ili kutimiza ndoto ya Taifa kufikia uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025.

Aidha, Waziri Mkuu ameziagiza taasisi zote zinazohusika na utekelezaji wa  ASDP II, ziimarishe usimamizi na ufuatiliaji ili utekelezaji wa mpango huo uwe na mafanikio makubwa.

Amesema mpango huo unaweka mkazo katika maeneo makuu manne, ambayo ni usimamizi endelevu wa matumizi ya ardhi na maji katika kilimo; kuongeza tija na faida katika kilimo, mifugo na uvuvi; kukifanya kilimo kiwe cha kibiashara na kuongeza thamani ya mazao na kuwajengea uwezo wadau wa sekta katika uratibu, ufuatiliaji na tathmini.

Juni 4, 2018, Rais Dkt. John Magufuli alizindua Awamu ya Pili ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini (ASDP II), ikiwa na lengo la kuongeza tija na uzalishaji katika mnyororo wote wa thamani ili kuvipatia malighafi viwanda vitakavyoanzishwa na kupata ziada ya  kuuza katika masoko ya nje ya nchi na kupata faida kubwa.

Muhogo Sasa Rasmi Kwenye Mazao Ya Biashara.....Ni baada ya kupata soko kubwa nchini China

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya China imetoa fursa ya kufungua soko la muhogo mkavu kutoka Tanzania, tukio ambalo  linafungua ukurasa mpya wa zao la muhogo kuwa miongoni mwa mazao ya biashara.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 29, 2018) bungeni jijini Dodomakatika hotuba yake aliyoitoa wakati wakuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge.

Amesema ili kuwezesha wakulima na wafanyabiashara wa Tanzania kunufaika na fursa hiyo, Mei, 2018 ulisainiwa mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya China kuruhusu bidhaa za muhogo mkavu kutoka Tanzania kuingia katika soko la China. 

Amesema kufuatia hatua hiyo, mwezi huu wa Juni 2018, tani 74 za muhogo mkavu kutoka Tanzania zimeingia China kupitia Bandari ya Qingdao iliyopo katika jimbo la Shandong.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema kiasi cha muhogo kilichofanikiwa kuingizwa katika soko la China bado ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji ambayo yanazidi tani 150,000 kwa mwaka.

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa Watanzania wachangamkie fursa ya kilimo cha muhogo ambacho kimeonesha kuwa na tija kubwa, pia amevitaka vituo vya utafiti wa kilimo viwawezeshe wakulima kupata mbegu bora na mbinu za kisasa ili waongeze uzalishaji na kukidhi mahitaji ya soko hilo.

Waziri Mkuu amesema kutokana na zao la muhogo kuonekana kuwa na matumizi menginezaidi ya chakula, Serikali inaendelea kuvutia uwekezaji wa viwanda vya kuchakata muhogo na kuzalisha bidhaa mbalimbali.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwamba umekuwa na mafanikio katika maeneo mengi nchini kwa sababu wakulima wadogo na wa kati wapo kwenye ushirika, hivyo kuwa na nguvu ya soko na bei nzuri ya mazao yao.

“Mathalani, kwa kutumia mfumo huo, mwezi huu bei ya ufuta imeongezeka kutoka shilingi1,500 hadi shilingi 2,800 kwa kilo na kuua mfumo usio rasmi wa uuzaji wa zao hilo ujulikanao kama ‘chomachoma’ ambao  ulimpunja mkulima kwa ujazo na bei,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema mfumo huo unasaidia kuzuia upotevu wa mazao unaotokana na uhifadhi dhaifu, pia unasaidia kuhifadhi mazao ili kusubiri kuuza wakati muafaka na kuyaongezea thamani mazao kabla ya kuyauza.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa mfumo huo unatekelezwa kikamilifu na kuleta tija kwa wakulima.

Amesema hatua hizo ni pamoja na ushirikishwaji wa wadau, kuimarisha ushirika, kuweka miundombinu ya masoko na kuboresha muundo wa taasisi na vitendeakazi vya Bodi ya Stakabadhi za Ghala.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa watendaji Serikalini kuhakikisha kuwa mazao mengi zaidi yanaingizwa katika stakabadhi za ghala ili kuwe na tija kwa wakulima.

Tundu Lissu Afunguka Mazito Kuhusu Dereva wake na Mwenyekiti Freeman Mbowe

0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameamua kuondoa utata kutokana na kile ambacho kimekuwa kikihojiwa na baadhi ya watu kuhusu shambulio alilopitia Septemba 7, 2017 Area D huko mkoani Dodoma.
 
Mbunge huyo amesema kwamba mara nyingi hapendi kujibizana na watu wanaohisi kwamba maswali kuhusu shambulio lake yanaweza kukosa majibu kutoka kwa viongozi wa chama chake ambapo amesema yeye kama muathirika na kiongozi wa CHADEMA atatoa ufafanuzi.

Lissu amewajibu wanaotaka kumvisha dereva wake uhusika wa shambulio lake hasa baada ya kutofika kituo cha polisi kuhojiwa, amesema kuwa utaratibu wa kisheria haukufuatwa na baada ya shambulio hakukuwa na wito wa kumtaka yeye (dereva) afike kituo cha polisi mpaka alipofika Nairobi.

"Dereva wangu aliondokea Dodoma kuja Nairobi na aliletwa na Mheshimiwa Goddie Lema. Hakukuwa na wito wowote kutoka polisi ambao hakuutii. Polisi walipoanza kuulizia habari zake tuliwaambie wamfuate Nairobi alikokuwa. Tuliwaambia wafuate utaratibu wa Sheria ya Kusaidiana Katika Masuala ya Jinai ili dereva wangu na mimi mwenyewe tuhojiwe kuhusiana na shambulio dhidi yangu.  Waliahidi kuja Nairobi. Tuliwasubiri, hawakuonekana mpaka tuliposafiri kuja Ubelgiji" Lissu.

Ameongeza kuwa dereva wake alisafiri kwenda Ubelgiji kwa pesa zile zile za msaada wa Wasamaria wema.

Akifafanua kuhusu kuumia mguu wa kulia zaidi wakati gari lake limeonekana kupigwa risasi upande wa kulia Lissu anasema kwamba "Sio kweli kwamba ni mguu wa kulia tu ndio ulioathirika, maeneo mengine yaliyopigwa na kuumizwa vibaya ni mguu wa kushoto ulipigwa mara mbili ijapokuwa hakuna mfupa uliovunjika, mkono wa kushoto ulipigwa na kuvunjwa vibaya chini ya kiwiko".

Aidha, "kipande cha risasi kilitolewa kwenye kiwiko chenyewe, mkono wa kulia ulipigwa na kuvunjwa vibaya chini ya kiwiko. Risasi sita zilitolewa tumboni na nyingine imebaki karibu na uti wa mgongo".

Pamoja na hayo Lissu ameondoa utata ulikuwa ukihoji kwa nini Mwenyekiti wa Chama chake Freeman Mbowe alikuwa wa kwanza kufika hospitali  "Mbowe hakuwepo kwenye eneo la shambulizi lakini watu wengine walikuwepo.Mfanyakazi wangu wa nyumbani alikuwepo. Mke wa Waziri wa Madini Medard Kalemani ambaye tunaishi jengo moja alikuwepo. Kwenye jengo jirani anakoishi Naibu Spika Tulia, mfanyakazi wake wa nyumbani alikuwepo na ndiye aliyenikimbiza hospitalini".

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe pamoja na Dereva wa Lissu (aliyebeba nguo Mkononi) mara baada ya kumfikisha  Mbunge Lissu hospitali ya General Dodoma siku aliyopigwa risasi.

"Baada ya kushambuliwa na wakati nakimbizwa hospitali, mimi ndiye niliyemwambia dereva wangu ampigie simu Mwenyekiti Mbowe na wabunge wengine kuwapa taarifa. Walifika hospitalini more or less muda huo huo niliofika mimi. Nilikuwa na fahamu muda wote mpaka nilipoingizwa theatre ndio nikapoteza fahamu" .

Mwenyekiti Mbowe anaishi upande wa pili wa Area D. Site 3 (ninakokaa mimi) na Sengia (anakoishi Mwenyekiti) zinatenganishwa na ukuta mmoja. Yote ni majengo ya TBA na njia yetu ya kwenda au kutoka bungeni na mjini ni moja.

Pamoja na hayo Lissu amefafanua sababu iliyompelekea yeye mida ile kuleke nnyumbani kwake ambapo mesema kwamba "Mimi na dereva wangu tulitoka bungeni saa saba mchana tukaelekea nyumbani kwangu Area D kula chakula cha mchana. Hatukukutana na mtu yeyote njiani na wala hatukusimama mahali popote mpaka tulipofika nyumbani. Tulianza safari ya kwenda Area D takribani saa saba mchana. Bunge lilikuwa limeahirishwa kwa ajili ya chakula cha mchana".

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 30

Maamuzi ya Rais Magufuli kuhusu sherehe ya mashujaa July 25, 2018

0
0
Rais Dkt. John Magufuli ameagiza shilingi milioni 308 zilizotengwa kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, zitumike kuboresha miundombinu ya barabara Jijini Dodoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri Mkuu jana Juni 29, 2018, wakati akizindua kituo cha Polisi kinachohamishika katika hafla iliyofanyika eneo la Kisasa, Jijini Dodoma na kusema Rais Magufuli ametoa agizo hilo ili fedha hizo ziende kukarabati miundombinu ya barabara pamoja na taa za kuongezea magari katika barabara ya kisasa na taa za barabarani kwenye barabara mpya ya Emmaus-African Dream yenye urefu wa kilomita 1.4, ambayo kwa sasa inajengwa kwa kiwango cha lami.

"Kutokana na msongamano uliopo ambao unaweza kusababisha ajali. Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Magufuli ameamua fedha zote zilizoandaliwa kwa ajili ya maadhimisho hayo zitumike kuboresha barabara. Pia ameawataka watanzania wote waadhimishe siku hiyo ya kumbukumbu ya mashujaa kwa kufanya usafi katika maeneo yaliyo jirani na makazi yao pamoja na yale ambayo wamezikwa mashujaa ikiwa ni njia ya kuwaenzi", amesema Waziri Mkuu.

Kufuatia uamuzi huo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mkoa waratibu zoezi hilo kwenye maeneo yao.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameliagiza Jeshi la Polisi lianze kujikita kwenye matumizi ya mifumo ya kiulinzi ya kielektroniki yaani 'City Surveillance Sytems' ili limudu kudhibiti hali ya sasa ya uhalifu.

Kila ifikapo Julai 25 ya kila mwaka Tanzania huadhimisha siku ya mashujaa kama sehemu ya kuwaenzi mashujaa hao ambao waliipigania nchi hii kwa namna moja ama nyingine.

Diwani Chadema anayedaiwa kumbaka mwanafunzi aendelea kusota rumande

0
0
Diwani wa Kata ya Kia (Chadema), Yohana Laizer ameendelea kusota rumande baada ya hakimu anayesilikiza kesi yake kutokuwepo mahakamani, ikielezwa kuwa yupo likizo.

Diwani huyo anatuhumiwa kwa makosa mawili ya kumbaka na kumpatia ujauzito mwanafunzi wa shule ya msingi Obrieni iliyopo Kata ya Kia Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.

Jana Juni 29, 2018 kesi hiyo namba 152 ya 2018 ilipangwa kusikilizwa katika mahakama ya Wilaya ya Hai, lakini imeahirishwa kwa mara ya tatu kutokana na hakimu kutokuwepo mahakamani.

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Hai,  Regina Mushi  ambaye kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilitajwa mbele yake, alisema  hakimu mwenye mamlaka ya kusikilia kesi hiyo  yupo likizo,  kwamba yeye hana mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo mpaka pale hakimu huyo atakaporejea.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 5, 2018 kwa ajili ya  usikilizwaji wa awali.

Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ilala (RCO) Atoa Ushahidi Kesi ya Halima Mdee Dhidi ya Rais Magufuli

0
0
Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ilala (RCO), Davis Msangi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa alibaini maneno yaliyotamkwa na mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee ni ya jinai wakati akiangalia mtandao wa kijamii wa you tube kupitia simu yake.

Msangi ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka aliyaeleza hayo jana Ijumaa Juni 29, 2018 wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kutoa lugha ya matusi inayomkabili Mdee.

Katika kesi hiyo Mdee anadaiwa kuwa alifanya kosa hilo Julai 3, 2017 katika ofisi za makao makuu ya Chadema yaliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni.

Anadaiwa kumtukana Rais John Magufuli kuwa “anaongea ovyo ovyo, anatakiwa afungwe breki” kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Halima alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Julai 10, 2017.

Akiongozwa na wakili wa Serikali, Patrick Mwita kutoa ushahidi, Msangi amedai kuwa Aprili 2017 hadi Januari 2018 alikuwa mkuu wa upelelezi wilaya ya Kinondoni.

Shahidi huyo wa kwanza wa upande wa mashtaka amedai kuwa Julai 4, 2017 alikuwa ofisini kwake na kupitia simu yake katika mtandao wa you tube aliona kichwa cha taarifa iliyoandikwa Magufuli afungwe breki.

Msangi amedai aliifungua na kuisikiliza maudhui ya ndani na kwamba yeye kama mlinzi wa amani aliona kuna jinai, kwamba alimuona Mdee akizungumza maneno hayo na alifuatilia na kutambua kuwa alikuwa katika mkutano na waandishi wa habari.

Alibainisha kuwa maudhui yalikuwa ni maneno kuongewa kwa sauti na kwamba kilichomfanya aone kuna jinai ni maneno yaliyoongelewa kuwa rais ana mambo ya ovyo ovyo anatakiwa afungwe breki.

Amebainisha kuwa baada ya kupata kipande cha video ya Mdee katika mkutano huo kutoka kwa Abdul, akatambua kuwa alichokiona you tube hakikuwa cha kutengeneza, hivyo kufungua jalada la uchunguzi.

Alidai kuwa baada ya kuipata video hiyo, aliituma kwa mtaalam wa matukio kutoka maabara ya kisayansi polisi makao makuu.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 11, 2018 siku ambayo mashahidi wa upande wa mashtaka wataendelea kutoa ushahidi katika kesi hiyo.

Wauguzi 6 watiwa hatiani kwa kusababisha Mama kukosa Mtoto kwa Uzembe

0
0
Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) limewataka  Wauguzi wanaojijua kuwa wanatumia vyeti feki  popote walipo nchini kujisalimisha mara moja kabla halijaamua kuwafuata huko waliko.

Hayo yamesemwa na Msajili wa TNMC Bi. Agnes Mtawa ambapo amebainisha kwamba katika kikao cha 193 kilichofanywa na Baraza hilo limewabaini watu 15 wanaojitambulisha kuwa ni wauguzi lakini kanzi data ya Baraza hilo imeonesha kuwa vyeti hivyo siyo halali na leseni wanazotumia ni za kugushi.

Amesema kuwa  Baraza limejadili suala la baadhi ya watu wanaogushi vyeti na leseni za taaluma ya uuguzi na ukunga ambapo limebaini kuwa katika robo mwaka Aprili - Juni, 2018 watu watano walitambuliwa kugushi vyeti na leseni hivyo wamepelekwa kwenye vyombo vya dola ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Pamoja na Baraza limewapa onyo kali Wauguzi Wakunga sita katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa kushindwa kutimiza majukumu yao ya kitaaluma wakati wakitoa huduma kwa mgonjwa hali ambayo ilipelekea mama mjamzito kupoteza mtoto kwa sababu ya uzembe.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

0
0
Katika kusherehekea miaka 15 ya kampuni ya NATURAL BEAUTY PROD tunatoa shukrani za dhati sana kwa wateja wetu wote kwa kutuunga mkono miaka yote hiyo.
 
TUNATOA OFFA YA WIKI NZIMA KWA WATEJA WETU UKINUNUA BIDHAA UTAPATA PUNGUZO LA 20%. KWA WATEJA WA MIKOANI UTATUMIWA BURE.

Ni bidhaa salama kabisa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda pia zina matokeo mazuri na kwa haraka zaidi.

🥑🍇🍋🍓🍒🌱🍇🍇
👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @210,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @140,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/=
11.YODI PILLS--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza (hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
GOOGLE
YOU TUBE
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod < WELCOME ALL>

Profesor Jay Asema "Tumechoka kuzika nguo", Serikali Yamjibu

0
0
Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule (Proffesor Jay) jana  alisema kuwa zaidi wananchi 40 wa  kata ya Luhembe, Jimbo la Mikumi wamepotea na hawapatikani.

Mbunge huyo alihoji Serikali ina sema nini juu ya wananchi hao wanaopotea na hawaonekani na tabia ya watumishi wa TANAPA kuwachukua wakazi wa Mikumi na kuwatesa.?

Akijibu swali hilo
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga alimuagiza ‘Prof. Jay’, kupeleka ushahidi wa madai yake ili serikali iyafanyie kazi.

Hasunga alisema; "Mheshimiwa Mbunge naomba ulete ushahidi wa kupotea kwa wananchi ili kutanabaisha taarifa hizo na serikali itashughulikia suala hilo maana serikali ipo kwa kulinda usalama wa wananchi”.

Naibu Waziri aliongeza kuwa serikali tayari imetatua mgogoro wa mpaka kati ya wakazi wa Mikumi na maeneo ya hifadhi.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Kampuni ya Asas Dairies Ltd yaahidi kufunga mitambo ya kuchakata maziwa Busokelo mkoani Mbeya

0
0
SERIKALI imesema Mwekezaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd ameahidi kufunga mitambo ya kuchakata maziwa kama kiasi cha maziwa kitaongezeka kwenye wilaya ya Busokelo.

Aidha, kwa sasa mwekezaji anakusanya jumla ya lita 3600 za maziwa kwa siku.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Busokelo(CCM) Fredy Mwakibete.

Mwakibete katika swali lake, alihoji serikali ina mpango gani wa kusaidia kumalizia kiwanda cha maziwa kinachojengwa kata ya Isange hasa ikizingatiwa maziwa mengi yanaharibika kwa kukosa soko.

Alisema Busokelo ni miongoni mwa Halmashauri zinazozalisha maziwa ya ng’ombe kwa wingi ambayo kwa mwaka inazalisha zaidi ya lita milioni 50.

Akijibu swali hilo, Ulega alisema kiwanda hicho kilianza kujengwa na serikali mnamo mwaka 2012 chini ya program ya kuendeleza sekta ya kilimo ya awamu ya kwanza.

“Kupitia program hiyo Sh.Milioni 140 zilitolewa na kutumika kujenga jengo la kiwanda, kuingiza umeme, maji na ununuzi wa tenki la kupoza maziwa lenye ujazo wa lita 2030,”alisema.

Aidha alisema uibuaji wa ujenzi wa kiwanda cha Maziwa cha Isange ulitokana na ukosefu wa soko la maziwa na hivyo kufanya maziwa mengi kuharibika.

Hata hivyo alisema ujenzi wa kiwanda ilikwama baada ya kumalizika kwa Programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo awamu ya kwanza(ASDP I) ambayo ilikuwa ikifadhili Mradi wa kiwanda hicho.

“Halmashauri ya wilaya ya Busokelo ilitangaza fursa ya uwepo wa jengo la kiwanda cha maziwa kwa ajili ya wawekezaji ambapo mwekezaji wa Asas Dairies Ltd alijitokeza na kuomba kuwekeza katika jengo la kiwanda cha maziwa,”alisema.

Kadhalika, alisema Mwekezaji baada ya kuingia mkataba na Halmashauri ameanza kutumia jengo hilo kama Kituo kikubwa cha kukusanyia maziwa yanayonunuliwa kutoka kwa wafugaji kupitia ushirika wa wafugaji wa maziwa na Utambuzi na sasa mwekezaji anakusanya jumla ya lita 3600 za maziwa kwa siku.

ATCL: Watanzania Kaeni Mkao Wa Kukalia Kiti Cha ndege mpya ya Dreamliner 787

0
0
WATANZANIA nchini wametakiwa kukaa mkao wa kukalia kiti cha ndege mpya ya Dreamliner 787 itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria 262 ambayo inatarajiwa kuwasili nchini hivi karibuni.

Hayo yamesemwa jana na Ofisa wa Idara ya Biashara wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) Lily Fungamtama wakati anazungumza na wananchi waliofika kwenye banda la ATCL  lililopo kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea Sabasaba jijini Dar es Salaam.

“Watanzania wakae mkao wa kukakilia kiti cha ndege mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 262 .Ndege ambayo inauwezo wa kukaa angani muda mrefu,”alisema Fungamtama.

Aliongeza kuwa watanzania wana kila sababu ya kumuunga mkono Rais Dk.John Magufuli kwa kuhakikisha wanapanda ndege hiyo yenye uwezo wa kusafiri masafa marefu.

Amewahakikishia wananchi wote kuwa ATCL imejipanga kutoa huduma bora na za kisasa na kufafanua kuwa wafanyakazi  wa ndege zao wamepikwa katika kutoa hduma bora na kuzingatia heshima na maadili ya mtanzania.

Aliongeza kuwa wafanyakazi wa ndege wameandaliwa vema kupitia chuo cha ATCL Training Institute ambacho jukumu lake ni kuandaa wafanyakazi wenye viwango bora vya kutoa huduma katika ndege za shirika hilo.

“ATCL tunatoa huduma katika kiwango cha juu kwa kuzingatia misingi ya maadili ya mtanzania.Tumejipanga vema kuwahudumia Watanzania wote na kwa sasa tunasubiri ujuo wa ndege mpya ya Dreamliner,”alisema.

Mmoja ya wananchi waliofika kwenye banda la ATCL ambaye jina halikupatikana alisikika akisema hajapanda ndege ya Bombardier lakini atahakikisha Dreamliner 787 anaipanda.

“Hii Dreamliner lazima nitaipanda tu maana kutoka Tanzania hadi Mumbai nchini India tunasafiri angani bila kuchimba dawa.Lazima niipande tu na ni vema nikamuunga mkono Rais wangu kwa vitendo,’amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images