Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yajipanga Na Bima Ya Afya Kwa Wote

$
0
0
Serikali  imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuongeza kasi katika kubuni mikakati na maboresho ikiwemo taratibu za kujiunga ambazo zitawawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma zake.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizundua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa NHIF mjini Morogoro ambapo amesema kuwa mwelekeo wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha watu wote wanakuwa na bima ya afya.

“Serikali ya Awamu ya Tano imeweka nguvu kubwa katika utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wananchi hivyo ninawaagiza muongeze kasi katika ubunifu na maboresho mbalimbali ambayo yatakwenda sambamba na matarajio ya Serikali ambayo ni kuwezesha wananchi wengi zaidi kuwa katika mfumo wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya,” amesema Dkt. Ndugulile.

Amewataka watumishi wa Mfuko hususan Mameneja wa Mikoa kutokaa maofisini mwao na badala yake watoke nje kwa ajili ya kuhamasisha wananchi, kuangalia huduma wanazopata katika vituo vya kutolea huduma pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.

Akizungumzia utendaji kazi wa Baraza, amewataka wajumbe wa baraza hilo kutambua wajibu wao ndani ya baraza kwa kuwa ni chombo muhimu katika kubuni na kuweka mipango thabiti ya kuendesha taasisi ambayo ina dhamana kubwa ya kuangalia ama kushughulikia huduma za matibabu kwa wanachama.

Amesema kuwa kwa sasa Serikali iko katika mchakato wa kuwasilisha muswada wa sheria ambao utawezesha wananchi wote kuwa katika utaratibu wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya.

Akitoa salaam za NHIF, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo Bw. Bernard Konga amemhakikishia Naibu Waziri kuwa, Mfuko unaendelea kutekeleza na kuunda mipango ya kuongeza wigo wa wananchi kunufaika na huduma zake.

Amesema kuwa Mwezi Julai, mwaka huu, Mfuko unatarajia kuzindua ‘Ushirika Afya’ ili kuwezesha wakulima katika vyama vyao vya ushirika kunufaika na bima ya afya huku  uundaji wa vifurushi mbalimbali ukiendelea. Mathalan, Mpango wa kulipa michango ya bima kidogo kidogo kwa kudunduliza kwa lengo la kuwawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma za Mfuko.

“Tumejipanga na hivi karibuni tutazindua huduma mbalimbali na hii yote ni mikakati ya kuelekea bima ya afya kwa wote kwa lengo la kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa  huduma za matibabu wakati wowote,” alisema Bw. Konga.

Tanzania Yaieleza UNESCO Umuhimu Wa Utekelezaji Wa Mradi Wa Kufua Umeme Katika Bonde La Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge)

$
0
0
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaeleza umuhimu wa kuendelea na mradi wa kufua umeme katika Bonde la Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) ndani ya Pori la Akiba Selous kwenye Mkutano wa 42 wa Kamati ya Urithi wa Dunia unaoendelea Manama, Bahrain, kuanzia tarehe 24 Juni hadi 4 Julai 2018. 

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huu unajadili hali ya uhifadhi wa maeneo ya Urithi wa Dunia na kutoa mapendekezo kwa nchi wanachama juu ya namna kuboresha uhifadhi wa maeneo hayo.

Kupitia Mkutano huu, Tanzania imeendelea kusisitiza msimamo wake kwenye Kamati ya Urithi wa Dunia juu ya umuhimu wa utekelezaji wa mradi huo. 

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo umesisitiza hayo, kufuatia msimamo uliowasilishwa na Maj. Jen. Gaudence Milanzi, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye Mkutano wa 41 wa Kamati ya Urithi wa Dunia uliofanyika Krakow, Poland, Julai 2017.

Umuhimu wa ujenzi wa mradi huo, uliwasilishwa pia kwenye kikao maalum kati ya wajumbe wa Kituo cha Urithi wa Dunia, Bodi ya Ushauri kwa UNESCO – International Union for Conservation of Nature (IUCN) na Wataalam wa Uhifadhi kutoka Tanzania kilichofanyika tarehe 25 Juni, 2018 Manama, Bahrain. 

Katika kikao hiki, UNESCO imekubali kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha mradi huu hauleti madhara ya kimazingira.

Aidha, wakati wa majadiliano ya ajenda ya hali ya ya uhifadhi ya Selous, Tanzania ilieleza kuwa, kukamilika kwa mradi huo kutaongeza shughuli za kiuchumi kutokana na kiwango kikubwa cha nishati ya umeme cha Megawati 2100 kitakachozalishwa. 

Ujumbe wa Tanzania ulifafanua kuwa tayari tathmini ya athari za kimazingira kwenye mradi wa Stiegler’s Gorge imekamilika na kuwasilishwa UNESCO kwa ajili ya upembuzi na kutumia fursa hiyo kulisisitiza Shirika la UNESCO juu ya umuhimu wa maendeleo endelevu kwenye maeneo ya Urithi wa Dunia.

Kwa nyakati tofauti, Tanzania ilipongezwa na Bodi ya Ushauri ya IUCN, pamoja na Nchi Wanachama wa Kamati ya Urithi wa Dunia kutoka kundi la Afrika ambazo ni; Angola, Zimbabwe na Uganda juu ya hatua kubwa iliyopigwa katika kupiga vita ujangili na kuongezeka kwa idadi ya tembo na faru katika Pori la Akiba la Selous. 

Sambamba na hilo, Serikali za Ujerumani na China zilipewa shukrani kwa kusaidia Tanzania katika kuimarisha ulinzi na uhifadhi katika Pori hilo.

Vilevile, nchi za Afrika ziliunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa mradi huo na kupendekeza ushirikiano baina ya wataaalam wa UNESCO na Serikali ya Tanzania. 

Mwisho, nchi hizo zilitoa mkazo juu ya utekelezaji wa ajenda ya maendeleo endelevu yenye kuzingatia uhifadhi wa maeneo ya Urithi wa Dunia.

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo uliongozwa na Maj. Jen. Gaudence S. Milanzi, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii na kuhudhuriwa na Bw. Joseph Kizitto, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira; Bw. Ali Khalil, Katibu Mkuu Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira – Zanzibar; Dkt. Amina Amir, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utalii na Mambo ya Kale – Zanzibar; Mhe. Samwel W. Shelukindo, Balozi na Mwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Shirika la UNESCO; na Wataalam wa uhifadhi na Urithi wa Dunia kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.  

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
Katika kusherehekea miaka 15 ya kampuni ya NATURAL BEAUTY PROD tunatoa shukrani za dhati sana kwa wateja wetu wote kwa kutuunga mkono miaka yote hiyo.
 
TUNATOA OFFA YA WIKI NZIMA KWA WATEJA WETU UKINUNUA BIDHAA UTAPATA PUNGUZO LA 20%. KWA WATEJA WA MIKOANI UTATUMIWA BURE.

Ni bidhaa salama kabisa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda pia zina matokeo mazuri na kwa haraka zaidi.

🥑🍇🍋🍓🍒🌱🍇🍇
👇👇👇👇
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 7.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @210,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/
7.BOTCHO MULT PLUS_Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza ( Hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/=
8.BOTCHO CREAM HOLOGRAM_ Hii ni yakupaka ya kuongeza (HIPS na MAKALIO) @150,000/=
9.LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu (CHUPA YA BIA) @140,000/=
10.BODY BOOSTER_ Hii ni yakuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @140,000/=
11.YODI PILLS--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza (hips mapaja na makalio) inapatikana kwa @160,000/= N.K

NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ili kuthibitisha ubora wa bidhaa zetu.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no÷

(+255) 659618585
au
0759029968
Follow us instagram-
GOOGLE
YOU TUBE
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod
@natural_beauty_prod < WELCOME ALL>

Tume Ya Madini Yapokea Ripoti Ukaguzi Migodi Ya Madini Ya Vito, Kinywe

$
0
0
Na Samwel Mtuwa – Dodoma
Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Prof. Shukrani Manya leo tarehe 28 Juni, 2018, amepokea ripoti ya Ukaguzi Maalum wa Migodi ya Madini ya Vito na Madini ya Kinywe (Graphite) kutoka kwa Mwenyekiti wa Timu ya Ukaguzi Profesa Justinian Ikingura.

Ripoti hiyo imetokana na Tume Maalum ya Wataalam Sita iliyoundwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Prof. Manya tarehe 17 Juni, 2018 ikilenga kufanya ukaguzi maalum katika maeneo ya uchimbaji wa madini ya Vito na Kinywe katika wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro.

Aidha, ukaguzi huo ulilenga kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko aliyoyatoa hivi karibuni wakati wa ziara yake mkoani Morogoro.

Katika ziara ya Naibu Waziri Biteko mkoani humo, alipokea malalamiko kutoka kwa wachimbaji wadogo wa madini ya vito ambao ni wanakijiji wa kijiji cha Epanko kilichopo katika eneo la mradi wa madini hayo.

Aidha, kufuatia malalamiko hayo Naibu Waziri aliahidi kuunda timu ya watalaam wa madini itakayofanya kazi ya ukaguzi maalum kwa lengo la kutathmin uendeshwaji wa migodi ya madini ya vito na kinywe pamoja na biashara ya madini kulingana na Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 pamoja na marekebisho yake.

Katika ripoti hiyo, timu ya wataalam wa madini imetoa mapendekezo mbalimbali ikiwemo Serikali kupitia Wizara ya Madini na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuweka mkakati wa kufanya Utafiti na tathmin ya madini adimu ya vito katika eneo la Mahenge na maeneo mengine nchini ili kuwepo na takwimu sahihi za kuvutia wawekezaji katika uchimbaji wa madini hayo.

Pendekezo lingine ni Mamlaka husika kuweka mpango wa kutoa huduma ya uthaminishaji wa madini ya vito katika maeneo ya wachimbaji wadogo ili kuwezesha wachimbaji hao kupata bei stahiki ya madini wanayozalisha na hivyo kuongeza kipato chao na kulipa tozo stahiki kwa Serikali.

Wajumbe wa timu hiyo walitoka katika Taasisi ya Jiolojia ya Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Chuo cha Madini Dodoma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Ukaguzi wa Migodi na Afisa Madini Mkazi wa Dodoma.

Rais Magufuli afurahishwa na Tuzo ya Grace

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefurahishwa na ushindi alioupta mjasiriamali Dr. Elizabeth Kilili ambaye amepata tuzo nchini Marekani kupitia bidhaa zake za 'Grace product'.

Rais Magufuli ameeleza furaha yake hiyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter ambapo zaidi amesifu namna ambavyo Dr. Elizabeth alitumia fursa hiyo kukitangaza Kiswahili baada ya kukitumia wakati akishukuru umati wa watu waliokuwepo ukumbini.

Sherehe za utoaji tuzo hizo maarufu kama 'International Quality summit' kwa mwaka 2018 zilifanyika May 27-28 2018, jijini New York nchini Marekani. Tuzo hizo ambazo hutolewa kwa makundi maalum ikiwemo viongozi pamoja na wazalishaji wa bidhaa asili zimefanyika kwa mara ya 32.

''Nimefurahishwa na ushindi wa Grace Products, lakini pia  nimefurahishwa kwa kutumia Kiswahili kukizungumza nchini Marekani, hongereni sana Grace Products''. ameandika Rais.

Kwa upande wake Dr. Elizabeth ameeleza kufurahishwa na pongezi hizo za Mh. Rais, huku akisema zimempa changamoto ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kwenda sambamba na falsafa ya Rais ambayo ni Tanzania ya viwanda.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Rais Magufuli kufanya ziara ya kihistoria nchini Kenya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuzuru nchini Kenya mwezi ujao katika ziara ambayo itakuwa ya kihistoria.

Rais Magufuli kwenye ziara yake ataungana na Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga na kisha kutembelea katika Kaunti ya Nyanza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na gazeti la Nation la nchini Kenya limeeleza kuwa Rais Magufuli anatarajiwa kuwasili nchini Kenya Ijumaa ya wiki lijalo.

Gazeti hilo pia halijaeleza ziara hiyo itakuwa ya siku ngapi na itakuwa na lengo gani katika kipindi hiki ambacho Rais Uhuru Kenyatta na Odinga wameonekana kupatana na kuweka tofauti zao za kisiasa kando.

Hii ni mara ya pili kwa Rais Magufuli kuzuru nchini Kenya ni baada ya kuzuru mwaka jana ambapo alikutana na Rais Uhuru Kenyatta.

Hata hivyo, Rais Magufuli hata kabla ya kukutana na Kenyatta mwaka 2016  kwenye ziara yake nchini Kenya mwaka huo huo alitembelewa na Raila Odinga kijijini kwake Chato..

Ziara hiyo inakuwa ni ya kihistoria na ya kwanza kwa Rais Magufuli kukutana na viongozi hao wawili na wenye nguvu zaidi kwenye siasa za Kenya.

Makamu wa Rais aelekea Mauritania kumuwakilisha Rais kwenye mkutano wa Umoja wa Afrika

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameondoka  jana jioni kuelekea nchini Mauritania ambako atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa 31 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika.

Mkutano huo wa siku 2, utakaoanza tarehe 1-2 Julai 2018, utafanyika kwenye mji mkuu wa nchi hiyo Nouakchott ikiwa ni mara ya kwanza kwa nchi hiyo kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa AU.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni Kushinda Vita Dhidi ya Rushwa chini ya Uenyekiti wa Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame.

Ujumbe wa Makamu wa Rais unajumuisha Mheshimiwa Dkt. Balozi Augustine Mahiga (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na viongozi wengine waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki.

Makamu wa Rais na ujumbe wake wanatarajia kurejea nchini Julai 5, mwaka huu.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais


TRC yahamasisha wafanyabiashara wanaokwenda Uganda kutumia reli

$
0
0
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limewataka wafanyabiashara wanaosafirisha mizigo kwenda Uganda kutumia njia ya reli kwa kuwa ni salama na nafuu.

Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa TRC Focus Makoye amewahakikishia wafanyabiashara kuwa shirika hilo limejipanga vilivyo kutoa huduma hiyo ambayo ilisitishwa miaka 10 iliyopita.

Makoye ameyasema hayo jana  jioni ya Juni 28 ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuanza kusafirisha  mzigo wa  tani 2400 za mafuta mali ya Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) unaopelekwa nchini Uganda.

Amesema kuanza kwa safari hizo ni hatua mojawapo ya kulifufua shirika hilo hivyo wafanyabiashara wachangamkie fursa hiyo.

"Ni furaha kubwa sana kwetu tumeanza safari hii tukiwa tumejipanga kabisa na tunawahakikishia wafanyabiashara kuwa tuko vizuri,

"Wote tunafahamu usafiri wa reli ndio wa gharama nafuu na uhakika, hivyo basi tunawakaribisha watu wengi zaidi ambao wanafanya biashara kati ya Tanzania na Uganda watumie usafiri huu,"amesema

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha lojistiki cha WFP Mahamud Mabuyu amesema wamevutiwa kutumia njia ya reli baada ya kuhakikishiwa usalama wa mzigo.

Kwa mujibu wa Mabuyu usafirishaji kwa njia hiyo pia unasaidia kuokoa dola 40 kwa kila tani ambayo ingesafirishwa kwa kutumia magari.

"Mwaka jana tulishasafirisha tani 16000 kwenda Dodoma na Isaka, mzigo wetu ulifika salama haikupotea hata mfuko mmoja,"

"Hilo limetuvutia na baada ya hizi tani 2400 kuondoka ndani ya muda mfupi tutapeleka tena tani 15,000 hiyo ni kudhihirisha ni kiasi gani tunaridhishwa na TRC,” amesema

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Awajibu Wabunge Waliotaka Ahojiwe na Kamati ya Maadili kwa Kulipotosha Bunge

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dk Adelardus Kilangi amewajibu wabunge waliotaka ahojiwe na Kamati ya Maadili, Kinga na Madaraka ya Bunge kwa madai ya kukidanganya chombo hicho cha Dola kuwa fedha za ushuru wa mauzo ya korosho nje ni za umma.

Wabunge waliomuomba Spika Job Ndugai kuitaka kamati hiyo kumhoji na kumchukulia hatua AG ni Zitto Kabwe (Kigoma Mjini) na Cecil Mwambe (Ndanda).

Akiwajibu wabunge hao AG amesema si kweli kuwa ushuru huo ulianzishwa na Serikali si wakulima, kwamba Bodi ya Korosho ilikuwa ikikusanya kwa niaba ya Serikali.

“Tozo hii haikuanzishwa na wakulima. Bodi ya korosho ilianzishwa kwa sheria ya mwaka 1984 . Lakini mwaka  1998 kulitokea ubadhilifu fedha, Serikali ilitoa maelezo kuwa fedha zisipelekwe mfuko wa Korosho,”amesema.

Amesema  mfuko huo haukuridhika na maelekezo ya Serikali na hivyo ikafungua kesi Mahakama Kuu na kutoa uamuzi kuwa bodi ya korosho inakusanya fedha za Serikali na Serikali ina mamlaka na fedha hizo.

“Mfuko haukuridhika, ukakata rufaa lakini mahakama ya rufaa ilitupilia mbali rufaa hiyo hivyo kisheria uamuzi wa mahakama kuu unabaki ule ule (kwamba fedha hizo ni za umma),”amesema kilangi.

Kuhusu kauli ya kwamba wakulima wa korosho waliingia mkataba na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya kukusanya kodi, mwanasheria huyo amesema hakuna mtu anayeweza kupatana na TRA kukusanya kodi.

“Hatuna mtu yoyote anaweza kukusanyiwa kodi na TRA. Huu ni upotoshaji. Marekebisho ya Sheria ya Korosho ya mwaka 2009 hayatambui mfuko wa kuendeleza korosho.  Haiwezekani kuutambua mfuko kisheria,”amesema.

Amesema kwa mujibu wa Katiba na sheria za fedha, TRA ikishakusanya fedha inatakiwa kupeleka katika mfuko mkuu wa Serikali, hivyo kufanya vingine ni kuvunja Katiba na Sheria.

Kuhusu kufuta Tume ya Mpango, Dk Kilangi amesema kufuta tume hiyo hakuna shida kwasababu majukumu yake yatahamishiwa kwenye wizara na kwamba sheria inaweza kutungwa upya kwasababu hakuna shida katika hilo.

Walichokubaliana Rais Magufuli Na Mnangangwa

$
0
0
Rais wa Zimbabwe, Emerson Mnangagwa aliwasili Tanzania jana na kukubaliana na Rais John Magufuli kushirikiana kibiashara, utalii na kijamii.

Sambamba na hilo, kiongozi huyo alizungumzia shambulio lililofanywa dhidi yake Juni 23, katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika mjini Bulawayo nchi humo akisema lilikuwa dogo na nchi yake iko salama.

Rais Mnangagwa alisema hayo Ikulu mjini hapa, ambapo baadhi ya wasaidizi wake na viongozi wa chama chake cha Zanu –PF walijeruhiwa.

Katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Uingereza, mwanasiasa huyo alilihusisha tukio hilo kufanywa na kundi la G-40 ambalo ni tiifu kwa Grace Mugabe ambaye ni mke wa Rais mstaafu, Robert Mugabe.

Mambo Matatu Waliyokubaliana
Rais Mnangagwa aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), saa 5:30 asubuhi na kupokewa na mwenyeji wake, Rais John Magufuli kisha kukagua gwaride la heshima na kuelekea Ikulu yalikofanyika mazungumzo.

Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu, Rais Magufuli alisema wamezungumza jinsi ya kuimarisha uchumi wa nchi hizi mbili kiuchumi tofauti na uhusiano wa zamani uliokuwa wa kisiasa zaidi.

“Mwaka 2016 biashara kati ya Tanzania na Zimbabwe ilikuwa ni Sh18.3 bilioni sawa na Dola 8.5 milioni. Mwaka 2017 biashara ilikuwa Sh21.1 bilioni sawa na Dola za Marekani 9.5 milioni. Kuna miradi 25 ya Zimbabwe nchini yenye thamani ya Dola 32.02 milioni ,” alisema Rais Magufuli.

Alisema wamekubaliana kupitia Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc) kukuza biashara.

“Ipo mikataba ya kulegeza masharti ya kibiashara katika Sadc. Baada ya uchaguzi ambao naamini atashinda tutaitumia kamati yetu maalumu kuyapitia maeneo hayo,” alisema.

“Tumekubaliana kukuza uwekezaji, nimemwambia kuna hekta 44 milioni za ardhi inayofaa kwa kilimo na kuna hekta 29 milioni zinazofaa kwa umwagiliaji. Vilevile kuna uwekezaji wa mifugo, uvuvi na uchakataji wa madini.”

Katika utalii, Rais Magufuli alisema wamekubaliana kushirikiana wakitumia wingi wa vivutio vilivyopo nchini ili kuwavutia na kutumia mikataba ya mashirika ya ndege likiwamo la Fasjet.

“Mathalan, mtalii akitoka Victoria Falls aende pia Serengeti halafu amalizie safari yake kwenye fukwe nzuri za Zanzibar,” alisema.

Rais Magufuli alisema pia wamekubaliana kuwa na ushirikiano katika huduma za jamii ikiwamo elimu, afya na utamaduni na hasa katika lugha ya Kiswahili ambayo alisema Tanzania ina walimu wa kutosha.

Rais Mnangagwa aliyewahi kuishi nchini aliishukuru Tanzania kwa kuratibu harakati za ukombozi wa Afrika.

“Dar es Salaam tuliyoishi miaka ya 1963 na 1964 ni tofauti kabisa na ya sasa. Tulijenga kambi ya kijeshi kule Bagamoyo ikiwa chini ya chama cha Frelimo tukiwa nchi ya Rhodesia (sasa Zimbabwe), Zambia na Msumbiji,” alisema.

Aliielezea Tanzania kwa Wazimbabwe kama vile mkunga wa ukombozi. Alisema hali si hivyo kwa nchi hiyo pekee bali pia kwa Namibia, Afrika Kusini na Angola, hivyo ni lazima kuishukuru.

Rais Mnangagwa alisema miaka 20 baada ya Zimbabwe kupata uhuru iliingia kwenye anguko la uchumi kutokana na kutekeleza sera ya ugawaji ardhi kwa watu weusi.

“Kwa sasa tunajitambulisha katika uwekezaji wa kimataifa. Hata zile nchi zilizojitenga baada ya kuwekewa vikwazo tunazikaribisha, lakini kwa nchi kama Tanzania ni rafiki yetu tutaendelea kushirikiana,” alisema.

Rais Mnangagwa amepanga kutembelea iliyokuwa kambi yao ya kijeshi ya Frelimo mjini Bagamoyo mkoani Pwani leo.

Ratiba Ya Mechi Zote Kombe La Dunia Hadi Fainali

$
0
0
 Fainali za Kombe la Dunia 2018  zilianza rasmini June 14 nchini Urusi .

Tazama  hapa  ratiba ya mechi zote za michuanpo hiyo kuanzia ile ya ufunguzi hadi fainali yenyewe.

16 Bora Za Kombe La Dunia 2018 Kuanza Jumamosi Hii kwa mchezo mkali kati ya Ufaransa na Argentina

$
0
0
Hatua  ya 16 Bora ya Kombe la Dunia inaanza Jumamosi kwa mchezo mkali kati ya Ufaransa na Argentina mjini Kazan, huku England ikimenyana na Colombia Julai 2.
 
Mechi za nyingine za 16 Bora ni kati ya Uruguay na Ureno Jumamosi pia, Hispania na Urusi, Croatia na Denmark, Jumapili, Brazil na Mexico, Ubelgiji na Japan na Sweden na Uswisi Julai 2 Jumatatu.
 
Hiyo ni baada ya mechi za makundi kukamilishwa jana, bao pekee pa Adnan Januzaj dakika ya 51 likiipa ushindi wa 1-0 Ubelgiji dhidi ya England kwenye mchezo wa Kundi G. 
 
Ubelgiji inamaliza katika nafasi ya kwanza kwenye Kundi G kwa pointi zake tisa, ikifuatiwa na England yenye pointi sita na zote zinafuzu hatua ya 16 Bora huku Tunisia na Panama zikiishia hapa.

Neymar ataiongoza Brazil katika mechi dhidi ya Mexico Jumatatu hatua ya 16 Bora Kombe la Dunia

Hali mbaya kwa Afrika, baada ya timu zake zote kutolewa hatua ya kwanza tu, kufuatia Senegal kuungana na Nigeria, Morocco, Misri na Tunisia kuaga mashindano hayo baada ya kufungwa 1-0  jana na Colombia katika mchezo wa Kundi H, bao pekee la beki, Yerry Mina dakika ya 74 Uwanja wa Samara Arena nchini Urusi. 
 
Timu zinazoaga mashindano haya ni pamoja na mabingwa watetezi, Ujerumani Saudi Arabia, Misri, Iran, Morocco, Peru, Australia, Nigeria, Iceland, Serbia, Costa Rica, Jamhuri ya Korea, Tunisia, Panama, Senegal na Poland.

Baba amuua Mtoto wake kisa Maparachichi

$
0
0
Polisi nchini Kenya linamsaka Mr. Morris Kirema kwa kosa la kumuua Mtoto wake mwenye miaka 12 na kumjeruhi Mtoto wake mwingine mwenye miaka 8 kwa kutumia panga na mateke akiwashutumu Watoto hao kula maparachichi kutoka katika shamba la jirani yao.

Mr. Morris anadaiwa kutumia mateke, ngumi pamoja na panga kuwaadhibu Watoto hao baada ya kula maparachichi kutoka katika shamba la jirani yao na kupelekea Mtoto wake huyo wa kiume mwenye miaka 12 kufa hapohapo.

Kwa upande wa Mtoto wa kike mwenye miaka 8 yeye amejeruhiwa vibaya sana pamoja na Mama yake ambao wanapatiwa matibabu katika hospitali moja nchini humo.

Inadaiwa kuwa mwenye shamba ambalo Watoto hao waliiba maparachichi hayo alidai alipwe kutokana na kitendo walichokifanya Watoto hao na ndipo Mr. Morris alipokasirika na kunuia kuwa lazima atawaua Watoto hao wakirudi kutoka shule.

Aidha duru za kuaminika zinasema kuwa Mwanaume huyo anasumbuliwa na uraibu wa michezo ya bahati nasibu na amekuwa akiwa mchungu akiombwa pesa na Mke wake.

Lori La Mafuta Lalipuka na Kuua Watu 9

$
0
0
Watu 9 wamefariki na magari 54 kuungua baada ya lori moja la mafuta kulipuka na kukamata moto barabarani wakati magari yakiwa kwenye foleni nchini Nigeria June 29.

Lori hilo liligongana na gari moja la abiria na kuanza kuwaka moto barabarani hapo wakati magari yakiwa kwenye foleni majira ya saa 11 jijini Lagos nchini Nigeria.

Inataarifiwa kuwa vifo kutokana na ajali hiyo vinategemewa kuongezeka kutoka Watu 9, huku moto huo ukiyafanya zaidi ya magari 50 yawe nyang'anyang'a.

Duru za kuaminika zinasema kuwa Watu waliofariki ni wale ambao walikuwa karibu na lori hilo ambalo lililipuka na kuwaka moto huku Watu wengine wakikimbia na kuacha magari yao kuokoa uhai wao.

Hata hivyo imeelezwa kuwa ajali za namna hiyo nchini Nigeria sio ngeni kwa maana huwa zinatokea mara kwa mara.

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Mnangwaga Atoa Dola 10,0000 Shule Aliyosoma Huko Bagamoyo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Mnangwaga leo asubuhi ametembelea iliyokuwa shule ya wapigania uhuru wa chama cha FRELIMO ambacho hivi sasa ni Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani.

Rais Mnangwaga akiwa chuoni hapo amesema yeye ni mojawapo ya waanzilishi wa chuo hicho katika miaka ya sitini akiwa pamoja na viongozi wengine wa Chama cha FRELIMO na kwamba alikuwa kiongozi wa ulinzi wa chuo hicho na kwamba hawakuwa na dhumuni la kutafuta madaraka bali ilikuwa ni jitihada zilizosukumwa na uzalendo wa kuzipatia nchi zao uhuru,” Rais Emmerson Mnangwaga.

Rais Mnangwaga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kwa kumpa fursa ya kuitembelea Shule hiyo kwa kuwa ilikuwa ni shauku yake baada ya kuondoka shuleni hapo miaka 58 iliyopita na kuwashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kumtunza katika kipindi chote alichoishi Bagamoyo na kwamba hata sasa anajisikia kuwa ni mmojawapo wa jamii ya watu wa Bagamoyo,” Amesema Rais Mnangwaga.

Pia Rais Mnangwaga ametoa kiasi cha Dola elfu kumi kwa mkuu wa chuo hicho kama shukrani yake ambazo amesema zitasaidia kutatua baadhi ya changamoto chuoni hapo.

TCRA yavipiga faini vituo vya redio kwa kukiuka kanuni

$
0
0
Kamati ya maudhui ya mamlaka ya mawasiliano (TCRA) imevitoza faini ya Sh6 milioni vituo vya redio vya Magic Fm na Rasi Fm kwa kukiuka kanuni za maudhui.

Akisoma hukumu hiyo Juni 29, 2018 Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Joseph Mapunda amesema Magic Fm cha Dar es Salaam, imetozwa faini ya Sh4 milioni kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji kwa kushindwa kuweka mizania wakati wakichambua bajeti ya wizara ya mifugo.

Kupitia kipindi chake cha ‘Morning Magic’ kilichorushwa Mei 18 mwaka huu mtangazaji alieleza kuhusu kufilisika kwa kampuni ya uvuvi ya Taifa (Tafico) na kampuni ya ranchi za taifa (Narco).

Kwa mujibu wa kamati hiyo, watangazaji walitoa taarifa bila kupata maoni ya upande wa serikali na vilevile hawakuwa na uhakika wa taarifa walizozitoa.

Kwa upande wa Rasi Fm cha Dodoma, kilikutwa na hatia ya kukiuka kanuni za utangazaji kwa kurusha maudhui ya ngono katika muda ambao wasikilizaji wake wengi ni watoto.

Mapunda amesema Juni 6 mwaka huu saa tano asubuhi mtangazaji alizungumzia kuhusu ngono na uangaliaji wa filamu za ngono jambo linalowahamasisha vijana na watoto kuwa na tabia mbaya.

Kutokana na hilo kituo hiki kimekutwa na makosa mawili ikiwamo kushindwa kuwalinda watoto na kuweka mada za wakubwa muda ambao wasikilizaji ni watoto.

Kila kosa lilitozwa faini ya Sh1 milioni zinazotakiwa kulipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Rasi Fm Ramadhan Mkotsollah amesema ameridhishwa na uamuzi huo kwa kuwa kweli kosa lilifanyika.

"Ni kweli kulingana na taratibu hilo ni kosa na mie binafsi sikufurahishwa na kitendo hicho ndio sababu tumechukua hatua,"amesema

Hatimaye Muswada kuitangaza Dodoma makao makuu watua bungeni

$
0
0
Miswada mitano ya mwaka 2018 ukiwemo wa Sheria ya kuitangaza Dodoma kuwa makao makuu ya nchi imewasilishwa bungeni leo Ijumaa Juni 29, 2018.

Miswada hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza leo na makatibu wa Bunge ni wa sheria mbalimbali (namba 2), sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali (Namba 3).

Mingine ni wa sheria ya bodi ya kitalaamu ya walimu Tanzania na muswada wa marekebisho ya sheria ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi wa mwaka 2018.

“Kwa mara ya kwanza tumesoma miswada mitano ambayo tutaifanyia kazi Bunge lijalo ikiwamo huu wa Dodoma. Tunawashukuru mawaziri na huu ulikuwa ni muswada ulioahidiwa kipindi kirefu lakini ulikuwa hauji,” amesema Spika Job Ndugai.

“Muswada huu wa mji wa Dodoma kamati ya Serikali za mitaa ndio mtaushughulikia, huu wa namba mbili na tatu tutaupeleka kamati ya katiba na sheria.”

Kuhusu bodi ya kitaalamu wa walimu amesema utapelekwa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii huku ule wa Ubia na Sekta Binafsi na Umma ukipelekwa Kamati ya Bunge ya Bajeti.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Silya: Dawa Bora ya Nguvu za Kiume

$
0
0
SILYA:  Ni dawa ya nguvu za kiume inayoponesha na kuongeza ndani ya dakika 10 tu. Dawa hii inaimarisha misuli ya uume iliyolegea au kusinyaa, ni dakika 3 tu.

Dawa hii inarefusha maumbile mafupi kufikia Inch 6-7, inanenepesha uume mfupi cm 4. Dawa hii inakufanya uchelewe kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa dk 20-30.

Inaongeza uzalishaji wa mbegu za kiume, inakufanya uweze kurudia tendo hata mara 5 bila kujali umri kama nikijana au mzee.

Pia ipo dawa ya kumrudisha mume, mke aliyekuacha au kumpata yeyote umpendaye.. Je umedhulumiwa,au umeibiwa Pesa zako ? Utarudishiwa ndani ya masaa  3.

Tunatibu Presha, Mgongo,Kisukari, Kiuno, Vidonda vya tumbo, kujaa gesi nk. Pata dawa ya mvuto, toa makovu, chunusi mabaka, punguza unene wa mwili, tumbo.

Tupo Dar es Salaam.

Simu: 0784 066 543 /  0653 715 642- Dr Hussein
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images