Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Hamisa Mobetto Atoa Baraka Zote Ndoa Ya Lulu na Majizzo

$
0
0
Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto ameweka wazi kuwa hana kinyongo na kutoa baraka zote kwa ajili ya ndoa ya Lulu na Majizzo.

Hamisa ambaye  amewahi kuwa kwenye Mahusiano na Majizzo siku za nyuma na  kuzaa naye mtoto mmoja ameweka wazi kuwa hivi sasa hana matatizo na Majizzo wala Lulu hivyo kwake ni Poa tu wakifunga ndoa.

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Mobeto alisema kuwa hana kinyongo na Lulu kama ambavyo watu wanasema kwa kuwa mapenzi yake na Majizzo yalishakwisha siku nyingi.

"Mimi na huyo anayetaka kumuoa tulishamalizana, hivyo hakuna tena hata chembe ya mapenzi zaidi ya uhusiano wetu wa kulea mtoto.

"Kwa maana hiyo sina shida kusikia Lulu anaolewa na siku ya sherehe nikipewa kadi nitakwenda“.

Tangu Lulu atoke jela Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa yeye pamoja na mpenzi wake Majizzo wanategemea kufunga ndoa hivi karibuni

Padri anayetumia muziki wa Hip Hop kanisani kushawishi vijana kuhudhuria ibada asimamishwa kazi

$
0
0
 Padri wa Kanisa Katoliki nchini Kenya aliyepata umaarufu kutokana na mtindo wake wa kutumbuiza kwa kutumia muziki wa kufoka amesimamishwa.

Paul Ogalo jina maarufu 'Sweet Paul' amekuwa akitumia muziki wa rap kama njia ya kuwavutia vijana wengi kufika kanisani.

Alikuwa akisema muziki ni njia sahihi si tu kuwavutia vijana bali pia kueneza Injili.

Miongoni mwa nyimbo zake alizokuwa akiimba ni pamoja na "Kujeni church kuna baraka, kujeni church kuna baraka..." au "Father Paul, niki-lock kwenye mic, Nduru (fedha) inafuata, mamanze go tipsy, vijana ruka ruka swag ya kunguru, au sio"

Lakini hatua yake hiyo inaonekana kutowafurahisha viongozi wa Kanisa Katoliki Magharibi mwa Kenya ambao wamemsimamisha kazi kwa mwaka mmoja ili ajitafakari.

Askofu wa jimbo la Kanisa Katoliki la Homa Bay, Philip Anyolo amesema padri huyo ni lazima achague kati ya kuwa rapa na kuwa padri.

Amesema kasisi huyo hataruhusiwa kuongoza ibada ya misa kwa kipindi cha mwaka mmoja ingawa anaruhusiwa kushiriki ibada, na pia anaruhusiwa kufanya ibada ya misa lakini faraghani.

Mavazi ya kasisi huyo yalikuwa ni tofauti na mapadri wengine yeye alipendelea kuvaa fulana ndefu za rangi nyekundu au nyeusi, suruali isiyobana mwili pamoja na kujifunga kitambaa kichwani na kutumbuiza kwa nyimbo kama wafanyavyo wanamuziki wa rap.

Hilo limekuwa likiwafurahisha vijana wengi na hata waumini wengine wa umri mkubwa.

Askofu Anyolo amesema uamuzi wa kumsimamisha kazi ulifikiwa mwezi uliopita.

Hata hivyo amesema kasisi huyo yuko huru kuendelea kutumia muziki wa rap na njia nyingine za kutumbuiza kuwahubiria vijana "lakini hafai kufanya hivyo kwenye altari."

"Mambo ya kidini na ya kidunia hayawezi kuchanganywa. Padri Ogallo ana kipindi cha mwaka mmoja cha kujitafakari na kuamua iwapo amejitolea kufuata maisha kamili ya upadri," amesema askofu huyo.

Padri huyo ameliambia Shirika la Habari la BBC kwamba hado hajapata taarifa za kusimamishwa kazi kwake na wakuu wa kanisa, ila amekuwa akisikia tu taarifa mitandaoni.

"Niligundua ya kwamba vijana wanapenda muziki, ndio maana wanaenda maeneo ya burudani, hivyo nikasema kama wanapenda hivyo basi hiyo ndiyo nitawapatia," alisema awali katika mazungumzo yake na BBC.

"Mimi naimba muziki wa aina yoyote, wa injili, riddims, hip-hop, lingala, raga, reggae pamoja, ili niwape mchanganyiko kamili."

TRCRA Kushirikiana na Polisi Kuwakabili Wezi wa Njia ya Mitandao

$
0
0
Serikali imesema kuwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Polisi watahakikisha wanafanya kazi kwa ukaribu kuhakikisha wote wanaotapeli kwa njia ya mitandao wanakamatwa na kuchukuliwa hatua  kali za kisheria.

Hayo yamebainishwa  kupitia Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, Bungeni Jijini Dodoma Wakati akijibu swali la Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali aliyehoji; “Kumekuwa na wimbi sasa limeibuka la wizi wa kutumia mitandao ya simu wakiwa wanatuma sms kuwa umeshinda ‘Tatu Mzuka’ mara umeshinda Tigo, tuma pesa kwenye namba hii,kumekuwa na desturi hiyo sasa hivi. Nilitaka kupata majibu kutoka kwa Waziri TCRA imechukua juhudi gani wizi wa kutumia simu kwenye mitandao unakomeshwa na kuhakikisha wahusika wanakamatwa?

“Ni kweli kwamba kumekuwa na matukio ya kutumiwa sms Watanzania mbalimbali ambazo zinaonyesha viashiria kwamba kuna utapeli unaoendelea katika huduma za mawasilino lakini kwa kutumia sheria ya 2015 ya wizi wa mitandao TCRA kwa kushirikiana na Polisi wameendelea kufanya kazi kwa karibu kuhakikisha kwamba wote wanaosambaza ujumbe huo wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria,” amesema Nditiye.

Kauli ya Serikali Kuhusu Walimu Waliohamishwa Bila Kulipwa

$
0
0
Serikali imesema walimu wote waliohamishwa kabla ya tamko la Rais John Magufuli aliyeagiza wote wanaohamishwa kupewa kwanza stahiki zao, watalipwa fedha zao kwa kuwa madai yao ni halali.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Juni 25, 2018 bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Joseph Kakunda wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Lyimo.

Katika swali lake Susan alitaka kujua ni lini walimu waliohamishwa watalipwa madai yao ikiwemo waliobadilishiwa vituo vya kazi kutoka ualimu wa sekondari na kuwa walimu wa shule za msingi.

Akijibu swali hilo, Kakunda amesema zoezi la kuwahamisha walimu kabla ya kupewa malipo lilisitishwa baada ya kauli ya Rais hivyo madeni yaliyopo ni waliokuwa wanahamishwa bila malipo na kwamba  baada ya tamko la Rais, hali ni nzuri.

Awali mbunge wa Mbagala (CCM), Issa Mangungu alihoji ni kwa nini Serikali ilifuta posho za kufundishia na lini itazirudisha ili kuwatia moyo walimu waweze kufundisha zaidi.

Naibu Waziri amesema posho hiyo haikufutwa bali iliongezewa katika mishahara ya walimu kwa lengo la kuongeza mishahara na pensheni wakati wa kupata kiinua mgongo.

Ruby afunguka kuhusu picha zilizosambaa kwenye mitandao ya Kijamii Zikimuonesha Amekonda

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Ruby amefunguka kuhusu stori zinazodai kwa sasa mwili wake umepungua (amekonda) ukilinganisha na hapo awali.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Niwaze’ ameiambia FNL ya EATV kuwa picha zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao hajui zimetokea wapi.

Ruby alienda mbali zaidi kwa kueleza kuwa picha hizo zimefanyiwa editing na wale wanaoeneza stori hilo wampe kazi (show) ili anenepe.

"Ile ni picha nasio Rubby halafu mnasema nimekonda kwani mlishawahi kuniona nimenenepa ?, haingii akilini kama vitu ambavyo vya negative wanavyoongea wakati mimi kazi ninafanya, ninaangalia mbele kwenye kazi zangu. Kazi yangu ndio inaongea lakini sio maneno ya watu. Mnaongelea mimi kuonekana mbavu zangu kwanini hamzungumzii kuonekana nina makalio makubwa.

“Halafu kitu kingine basi wawe wanaleta shows, kazi ili tunenepe, hivyo ndio vitu vya kuongea. Kama mnaona tumekonda, mnataka tunenepe, mnaleta shows, kazi,” amesema Ruby.

Ruby alikuwa kimya kwa kipindi kirefu katika muziki mara baada ya kuzinguana na menejimenti yake ya zamani. Wimbo wa kwanza kutoa kwa mwaka huu ni Niwaze aliowashirikisha kundi la The Mafik.

Kesi ya Mbowe Na Vigogo Wengine CHADEMA Yapigwa Kalenda Tena

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kesi inayowakabili Viongozi wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe hadi June 27,2018 kwa sababu Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vicent Mashinji hakufika mahakamani.

Hatua hiyo imefikiwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada wakili wa serikali, Faraja Nchimbi kueleza kuwa kesi hiyo imeitishwa ili washtakiwa wasomewe maelezo ya awali lakini mshtakiwa wa 6, Dk.Vicent Mashinji hayupo mahakamani.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala amedai kuwa Dk. Mashinji ana udhuru yupo katika mahakama ya Songea ana kesi nyingine, hivyo wanaomba ahirisho.

Maombi hayo ya ahirisho yaliibua mvutano wa kisheria baada ya wakili wa serikali Paul Kadushi kutaka kesi iahirishwe hadi kesho, huku wakili Kibatala akitaka iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Kutokana na mvutano huo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi June 27,2018

Mbali ya Mbowe na Mashinji, washtakiwa wengine ni Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika.

Pia mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na mbunge wa bunda, Esther Bulaya na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwemo kula njama, ambapo inadaiwa  February 1 na 16, 2018, Dar es Salaam walikuĺa njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko kutawanyika.

Wanadaiwa kuwa February 16,2018 katika barabara ya Kawawa Kinondoni Mkwajuni washtakiwa hao wakiwa na wenzao 12 ambao hawapo mahakamani walikiuka tamko la kuwataka kutawanyika la Afisa wa polisi SSP, Gerald Ngiichi kwa kugoma kutawanyika na kupelekea uvunjifu wa amani.

Inadaiwa kugoma huko kulipeĺekea hofu na hatimaye kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na majeruhi kwa askari wawili ambao ni  H.7856 PC Fikiri na E.6976 CPL Rahim Msangi.

Sakata la Korosho Lalivuruga Bunge Tena

$
0
0
Wabunge wa CCM, Nape Nnauye (Mtama) na Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini) wamesema hawakubaliani na mapendekezo ya Serikali ya kufuta ushuru wa asilimia 65 wa fedha zinazotokana na mauzo ya korosho nje na kubainisha kuwa kinachofanywa ni kuiua CCM mikoa ya Kusini.

Wakizungumza leo Jumatatu Juni 25, 2018 bungeni mjini Dodoma katika mjadala wa bajeti ya Serikali, wamesema wapo tayari  kudhalilishwa na wabunge wenzao waliopangwa kuitetea Serikali katika suala hilo la Korosho huku mawaziri wawili wakisimama kutetea jambo hilo.

Tayari baadhi ya wabunge wametishia kufanya maandamano iwapo Serikali haitatoa asilimia 65 za ushuru wa mauzo ya korosho nje kwa ajili ya maendeleo ya zao hilo.

Pia, wanapinga mabadiliko ya Sheria ya Korosho yanayokusudiwa kufanywa na Serikali ili ushuru huo upelekwe katika Mfuko Mkuu wa Hazina.

Aliyeanza kuzungumza alikuwa Nape aliyebainisha kuwa ukizungumzia korosho unazungumzia maisha ya watu katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani na mingine inayolima korosho.

“Wakulima wa pamba wakizungumza pamba wanazungmza maisha, sisi hatuna mifugo, almasi na tukizungumza korosho ni maisha na linapozungumzwa hili ushabiki uwekwe pembeni, tunazungumza maisha,” amesema.

“Hili jambo tulilizungumza katika wizara ya Kilimo na mwenyekiti wa Bunge (Mussa Azzan Zungu) ulikuwapo na tulizungumza nje na hatukukubaliana.

Amebainisha kuwa dhana kuwa mapato yote ya korosho yasaidie mikoa ya Kusini si kweli, kwamba yatafanya shughuli nyingine, “badala ya kutuletea fedha unaleta sheria ya kuzifuta kabisa, huku ni kutudharau kwa hali ya juu, mimi nadhani ushauri wangu hebu zungumzieni namna ya kuleta fedha na hii sheria ondoeni kwanza.”

“Dk Mpango mbona unazungumza na korosho na katani peke yake, mbona nia ovu, unapora fedha halafu unaleta sheria hii, maisha haya ni maisha yetu. Tunaopata madhila mabaya zaidi katika gesi, mbaazi imeanguka.”

Huku akizungumza kwa uchungu Nape amesema, “Wanaosema si hela zetu hiki kiatu hamvai nyinyi tunakivaa sisi. Dk Mpango kuweni na huruma na mapendekezo haya yanakwenda kuiua CCM Kusini, yanakwenda kutuweka mahali pagumu sana.”

Kauli hiyo ilimuinua Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, mhandisi Stella Manyanya akimtaka Nape anapochangia kutowashawishi wananchi wa mikoa ya Kusini kupinga mambo mbalimbali yanayoazimiwa kufanywa na Serikali.

Kwa upande wake Ghasia ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti amesema,” kuna wabunge wamekaa vikao, wameandaliwa

waje kutudhalilisha wabunge tunaowatetea wakulima.”

“Wabunge wote tuna haki sawa za kutetea wananchi wetu, anayetoka katika pamba atetee pamba, anayetoka katika madini atatetea madini yake na anayetoka katika korosho atatetea wa korosho.’

“Niwahakikishia wakulima wanaolima korosho wabunge wao tutapambamba na hata haki isipopatikana ila tutawatetea. Tunaambiwa sisi wabinafsi, korosho inalimwa kwa kiwango kikubwa na mikoa miwili au mitatu lakini tulipokaa katika kamati tukakubaliana na kwenda mikoa 17,”

Amesisitiza, “Leo tunaambiwa sisi wabinafsi, kuna watu wanakuja kusimama wanasema wanaijua korosho kuliko sisi. Mimi utafiti wangu wa shahada ya kwanza na ya pili inahusu korosho. Leo mtu anakuja humu anaijua korosho na ninasema kila mtu atetee lake na wananchi mjiandae kuwasikia.”

Baada ya Ghasia kumaliza kuchangia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama alisema Serikali haina nia ovu na suala la korosho na haina nia ya kuwanyanyasa wakulima wa zao hilo.

Katika ufafanuzi wake kuhusu mvutano huo, mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu amesema jambo hilo lisiligawe Bunge na kuwataka wabunge kusubiri hoja zitakazotolewa na Serikali wakati ikijibu jambo hilo.

Credit: Mwananchi

Breaking News : Hiace Yagongana Na Lori La Mchanga Na Kuua Watu 14 Mkuranga

$
0
0
Watu 14 wamefariki dunia na wanne kujeruhiwa baada ya daladala walilokuwa wakisafiria kugongana na lori.

Ajali hiyo imetokea leo Juni 25 saa 10 alfajiri katika eneo la Dundani wilayani Mkuranga Mkoani Pwani.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga Dk Stephen Mwandambo amethibitisha vifo hivyo, amesema maiti za watu 14 zimepokelewa na kuhifadhiwa katika chumba cha maiti hospitalini hapo.

"Ni kweli hili tukio limetokea alfajiri, tumepokea miili 14 na majeruhi wanne," amesema Dk Mwandambo.

Kati ya majeruhi hao, amesema mmoja hali yake ni mbaya na walikuwa wanahangaika kuokoa maisha yake.

Rais Magufuli Awalilia Watu 14,waliokufa Kwa Ajali Ya Hiance Iliyogongana Na Lori La Mchanga Mkuranga

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko taarifa ya vifo vya watu 14 waliopoteza maisha baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori la kubebea mchanga katika eneo la Dundani Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.

Dkt. Magufuli amesema hayo katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo baada ya kupita masaa kadhaa tokea ajali hiyo kutokea leo Juni 25, 2018 wakati basi dogo lililowabeba wanafamilia, ndugu na jamaa waliokuwa wakielekea Msata kuhudhuria sherehe za kumaliza mafunzo ya kijeshi  kwa mtoto wao, kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa linatoka Dar es Salaam kwenda Dundani kuchukua mchanga.

"Naomba unifikishie pole nyingi kwa wanafamilia wote waliopatwa na msiba, waambie naungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi ya kuondokewa na wapendwa wao, na sote tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi", amesema Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine Rais Magufuli pia amewaombea majeruhi wanne wa ajali hiyo wapone haraka ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na majukumu yao ya kila siku.

Serikali Yatoa Taadhari Kwa Wananchi Juu Ya Uwepo Wa Ugonjwa Wa Chikungunya Nchini

$
0
0
Na WAMJW – DSM
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa tahadhari kwa wananchi juu ya kuingia kwa ugonjwa wa Chikungunya nchini baada ya watu wanne waliotokea  nchini Kenya kubainika kuwa na dalili zinazofanana na ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo jijini katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam wakati akiongea na waandishi wa Habari.

“Mnamo tarehe 20, Mwezi Juni, 2018 wasafiri wanne wa familia moja waliotokea tena Mombasa nchini Kenya walishukiwa kuwa na ugonjwa huu baada ya kuwa na dalili zinazofanana na ugonjwa wa homa ya Chikungunya kwenye kutuo cha mpakani cha Holili kilichopo wilayani Rombo mkoani Kiliamanjaro”, alisema Mhe. Ummy

Waziri Ummy aliwatoa hofu wananchi kuwa Ugonjwa huu si mpya katika nchi yetu kwani hapa nchini  uligundulika katika maeneo ya Kusini mwa Tanzania, sehemu za Makonde katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji mnamo mwaka 1952 huku  Jina la ugonjwa likiwa na asili ya Kimakonde lenye maana ya “kilichopinda” yaani hali ya kupinda mwili inayotokana na maumivu makali ya viungo kunakosababishwa na ugonjwa huu.

Kwa upande mwingine Mhe. Ummy alithibitisha juu ya kuwepo kwa ugonjwa wa Dengue nchini hususani katika jiji la Dar es salaam huku idadi ya wagonjwa ambao wamethibishwa kwa kipindi cha Januari hadi Mei ni 226 ambao wanatoka katika mkoa wa Dar es Salaam.

‘Dengue ulithibitishwa kuwepo hapa nchini hususani jijini Dar es Salaam kuanzia mwishoni mwa mwezi wa Januari 2018. Hadi kufikia sasa idadi ya wagonjwa ambao wamethibishwa kuwa na ugonjwa huu kwa kipindi cha Januari hadi Mei ni 226 ambao wanatoka katika mkoa wa Dar es Salaam.  Vilevile ugonjwa huu si mpya hapa nchini kwani umewahi kuripotiwa katika miaka ya 2010, 2013 na 2014” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameeleza dalili za ugonjwa wa Dengue zinashabihiana amabazo ni pamoja na homa ya ghafla, kuumwa kichwa, maumivu ya viungo na uchovu. Dalili hizi huanza kujitokeza siku ya 3 hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa virusi vya magonjwa haya. Wakati mwingine dalili za magonjwa haya yanaweza kufanana sana na dalili za ugonjwa wa malaria. Vilele mara nyingine magonjwa haya yanaambatana na kutokwa na damu sehemu za fizi, mdomoni, puani, kwenye macho na pia kwenye njia ya haja kubwa au ndogo.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amethibitisha kuwa hadi sasa nchini Tanzania hakuna mgonjwa yoyote aliyehisiwa au kuthibitishwa kuwa na virusi vya Ebola, huku kwa tathmini ilifanyika na Shirika la Afya Duniani (Regional Risk Assessment) imesema kuwa Tanzania ipo kwenye uwezekano wa kupata ugonjwa wa Ebola na imewekwa katika kundi la pili miongoni mwa nchi 6 zilizo katika hatari ya kupata maambukizi zaidi, kutokana na kupakana na nchi ya DRC pamoja na mwingiliano mkubwa wa watu wake.

Pia Mhe. Waziri amewatoa hofu Wananchi na kuwataka kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huu kwani mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitishwa kuugua ugonjwa huu hapa nchini, huku akiwaonya wanaosambaza taarifa za uzushi juu ya uwepo wa ugonjwa huu na kuwataka waache haraka.

Aidha, Wizara itaendelea kushirikiana na Sekta mbalimbali katika kuimarisha ufuatiliaji na kuendelea kutekeleza mikakati ya kudhibiti ili ugonjwa huu usiingie nchini na kuendelea kutoa taarifa pamoja na Elimu kwa Jamii kadri itakavyohitajika.

PolePole Awapa Makavu Viongozi Wanaojifanya 'Mungu Mtu"

$
0
0
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kuendelea kuwa watumishi wa watu kwa kufikika kwa haraka pale wanapohitajika ikiwa ni pamoja na kusimamia mali za Umma na Chama hicho kwa kuwa ndio msingi wa ushindi wa CCM katika zama zote.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Bw. Humphrey Polepole wakati akiwa amekutana na Makatibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wa Majimbo, Wilaya na Mikoa yote ya Zanzibar na kuendesha Mafunzo ya Kimkakati ya kuwaongezea maarifa, uweledi na ujuzi katika eneo la Siasa, Itikadi na Uenezi.

Polepole amesema kwamba zile zama za viongozi kujihisi wako juu ya wananchi na hawawezi kupatikana pale wanapohitajika na wananchi zimekwisha, na kwamba Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pi ni rais wa nchi yeye anawapatia fursa wananchi wake pale wanapomuhitaji.

"Zama za viongozi kuwa Mungu watu zimekwisha kwenye chama chetu, ukipigiwa simu pokea. Ukitumiwa meseji jibu hata kama hutaweza kujibu meseji zote.  Mimi najua Mwenyekiti John Pombe Magufuli anapokea simu na anajibu meseji, wewe waziri ni nani au wewe kiongozi wa Chama mkoa hufikiki umekuwa nani? Zama hizo ndani ya CCM hakuna tena nawataka mjirekebishe," Polepole

Pamoja na hayo Katibu Mwenezi huyo amewataka wanaCCM kupitia vikao kuendelea kuifuatilia, kuisimamia na kuitathimini Serikali yao katika namna ambavyo itaendelea kuchochea maendeleo ya wananchi ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015-2020.

Atiwa Mbaroni kwa kuuza sambusa za Paka

$
0
0
Mwanaume mmoja nchini Kenya amenusurika kuuawa na Wananchi wenye hasira kali baada ya Wananchi hao kugundua kuwa Mwanaume huyo amekuwa akiwaauzia sambusa za nyama ya Paka kwa miaka 7.

Mr. James Mukangi anadaiwa kuwauzia wauzaji wa sambusa nyama hiyo ya Paka ikiwa na yeye pia hutengeneza sambusa hizo za nyama ya Paka huku wateja wake wengine akiwauzia nyama hiyo ya paka.

Mwanaume huyo anadaiwa kufanya biashara hiyo haramu kwa kipindi cha miaka 7 na anakadiriwa kuwa ameuza zaidi ya Paka 1000 toka mwaka 2012 huku akipata zaidi ya 11,000 za Kitanzania kwa kila Paka.

Pia Mukangi aliwaeleza Waandishi wa Habari kuwa aliamua kufanya biashara hiyo baada ya kuona kuna pengo sokoni la nyama hiyo.

Kwa mujibu wa sheria za Kenya Paka sio mfugo anayeruhusiwa kutumika kama kitoweo nchini humo.

Aidha jamaa huyo alikamatwa na Wananchi mjini Nakuru nchini Kenya alipokuwa akiwachuna ngozi Paka na ndipo Wananchi hao walipoamua kumshushia kipigo kabla ya Polisi kuja na kumuokoa.

Serikali yaondoa vibali wanaosafirisha samaki wa kitoweo

$
0
0
Serikali imeondoa sharti la wananchi wanaosafirisha samaki kwa ajili ya kitoweo kuwa na vibali.

Uamuzi huo uliotangazwa jana Juni 24, 2018 mjini Sengerema na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina utahusisha wananchi wanaosafirisha samaki wa kitoweo hadi kilo 20 kutoka sehemu moja kwenye nyingine.

Akizungumza wakati wa uteketezaji wa zana haramu za uvuvi zenye thamani ya zaidi ya Sh2.3bilioni, kati yake zikiwemo zana zenye thamani ya Sh1.5 bilioni za mfanyabiashara Josefu Kando (Njiwa Pori), Waziri Mpina amesema uamuzi huo wa Serikali unalenga kutoa fursa kwa wananchi kufaidi na kutumia rasimali za Ziwa Victoria.

Pamoja na kufuta vibali vya kusafirisha kitoweo, Waziri Mpina amesisitiza kuendelea kwa operesheni dhidi ya uvuvi haramu huku akiwaagiza wanaoendelea kumiliki zana haramu za uvuvi kuzisalimisha kabla hawajafikiwa ya mikono mirefu ya dola.

Mkuu wa opereshemi dhidi ya uvuvi haramu wilayani Sengerema, Wenceslaus Luhasile ameahidi kuendeleza vita dhidi ya uvuvi haramu na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano wanapobaini vitendo hivyo katika maeneo yao na kuahidi kutunza siri za wanaotoa taarifa.

Kauli hiyo iliungwa mkono na mkuu wa wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole aliyeongeza kuwa jukumu la kulinda rasilimali za nchi ni la kila Mtanzania kwa ajili ya faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Joshua Nassari Naye Ajilipua Sakata la Korosho...."Huo ni Wizi, Hakuna Lugha Nyingine"

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki ( Chadema),  Joshua Nassari amekifananisha na wizi kitendo cha Serikali kushindwa kutoa Sh 210 bilioni kama asilimia 65 ya fedha za ushuru wa mauzo ya korosho nje ya nchi kwa kuwa jambo hilo lipo kisheria.

Akizungumza katika mjadala wa bajeti ya Serikali mwaka 2018/19 leo Juni 25, 2018 bungeni mjini Dodoma, Nassari amesema asilimia kubwa ya wabunge bungeni wanawawakilisha wakulima, wafugaji na wavuvi.

Amesema hata dhana ya Tanzania ya viwanda inategemea malighafi za kutosha zinazotokana na zao hilo lakini bajeti imekuwa ikipungua mwaka hadi mwaka.

"Leo hii tunaongelea Serikali ya viwanda, sheria ya export levies ilikuwa na lengo la kuongeza uzalishaji wa korosho zetu ndani ya nchi, sasa badala yake Serikali inaiba hela za wananchi, huu ni wizi hakuna lugha nyingine”  -Nassari

Amesema shughuli za kilimo cha korosho sasa zimepanuka na wakulima katika mikoa 17 sasa wanalima zao hilo la biashara lakini Serikali haitaki kutoa fedha hizo ambazo wakulima wamekuwa wakizitegemea.

Amesema kama Serikali ilitunga sheria ya korosho iweje sasa itake kuibadilisha ili fedha hizo ziende katika Mfuko wa Hazina.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 26

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Dkt Tizeba: Wakulima 11,177 Wa Ufuta Wanufaika Na Mradi Wa Farm Afrika

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Dar es salaam
Utekelezaji wa mradi wa Farm Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu umeweza kuwafikia wakulima takribani 11,177 ambapo kati yao wanawake ni 5,474 na wanaume ni 5,703 huku kati ya wakulima hao vijana wakiwa ni takribani 5,821 yaani zaidi ya nusu (52%) kutoka wilaya ya Bahi, Manyoni na Babati.

Hayo yamebainishwa juzi 22 Juni 2018 na Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba wakati akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa zao la ufuta pamoja na mjadala wa mapendekezo juu ya uboreshaji wa masoko ya ufuta, kwenye hafla iliyofanyika Golden Tulip Hoteli Jijini Dar es salaam.

Dkt Tizeba alipongeza jitihada hizo kwani zinachangia kukuza kipato cha wakulima na uchumi wa nchi kwa kuingiza fedha za kigeni huku akiwataka watumishi mbalimbali kuwaunganisha wakulima wadogo wadogo katika masoko rasmi na kujenga uelewa wao juu ya vichocheo na fursa za ushiriki endelevu.

Waziri huyo wa kilimo alilishukuru shirika la Farm Afrika kwa kuona umuhimu na fursa zilizopo katika kilimo cha ufuta katika mikoa ya Dodoma, Singida na Manyara hivyo kuwanufaisha wakulima kupitia mbinu bora za kilimo cha kisasa katika zao hilo.

Alisisitiza kuwa zao la ufuta lina fursa kubwa ya soko ambapo kwa sasa mahitaji ya soko ni zaidi ya mara tatu ya kiasi kinachozalishwa kwa mwaka ambapo hali hiyo inatokana na nafasi kubwa kwa wakulima wa ufuta kujipatia kipato na kuboresha maisha yao.

Alisema kuwa serikali inaweka mkazo mkubwa kwa ajili ya uzalishaji wa mazao ya mbegu za mafuta na juhudi hizo zinajidhihirisha katika hatua ambazo serikali inaendelea kuzichukua kwa kuhakikisha uzalishaji wa mbegu za mafuta ndani ya nchi unaongezeka.

Alisema, kupitia utekelezaji wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili mbegu za mafuta ikiwa ni pamoja na ufuta na alizeti ni miongoni mwa mazao ya kipaumbele ambapo kwa kuanzia msimu wa mavuno ujao zao la ufuta litaingizwa kwenye mfumo wa stakabadhi za ghala na katika kuimarisha upatikanaji wa soko la ziada kwa zao la ufuta na mbegu nyingine za mafuta, Na kuongeza kuwa Bodi ya mazao mchanganyiko kuanza kununua mazao hayo ili kuhakikisha mkulima anapata soko la uhakika zaidi.

Katika hatua nyingine, Mhe Dkt Tizeba aliwasihi wakulima wa ufuta kote nchini kubadilika kuanza kufanya kilimo biashara na kuachana na kilimo cha mazoea cha kujikimu ikiwa ni pamoja na kujua mahitaji ya soko kwa maana ya ubora wa ufuta na kiasi, kutumia teknolojia hususani zana bora, mbegu bora na mbolea sambamba na kujiunga katika vikundi au ushirika na kuuza kwa pamoja na kuwa na nguvu ya pamoja.

MWISHO.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Wabunge CCM wazomeana kisa korosho

$
0
0
Sakata  la malipo ya mauzo ya korosho limeendelea kuteka mjadala wa Bunge, safari hii likisababisha watunga sheria kutoka chama tawala CCM kuzomeana huku Mbunge wa Kilwa Kusini, Seleman Bungara 'Bwege' (CUF) akitolewa ukumbini kwa kuchochea vurugu ndani humo.

Akichangia mjadala huo, Mbunge wa Bukoba Vijijini, na Katibu wa Wabunge wa CCM, Jason Rwekiza, alisema kuwa analazimika kufafanua kauli iliyotolewa na Hawa Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini kuwa kipo kikundi cha wabunge wanaotaka kuwachafua.

Alisema yeye akiwa ni Katibu wa Wabunge wa CCM ndiye anayepanga wachangiaji wa chama hicho bungeni.

"Nalisema hili kwa sababu Mheshimiwa Hawa Ghasia amesema kuna watu wamepangwa na serikali kuwachafua, hii siyo sahihi," Rweikiza alisema. "Orodha ya wachangiaji nimepanga mimi, naomba mnisikilize tulia… tulia... nisikilizeni," alisisitiza mbunge huyo baada ya kuibuka zomeazomea dhidi yake bungeni.

Katika mjadala huo, Ghasia alisema anasikitishwa na maneno yanayosambazwa kwa makusudi dhidi ya wabunge wanaotetea kupelekwa pembejeo kwenye maeneo yao.

"Kuna taarifa kuwa jana (juzi) watu walikaa vikao, wameandaliwa kuja bungeni kuwadhalilisha wabunge hao wanaotetea wananchi, ili wapate pembejeo na kutetea wakulima wapate fedha zao," Ghasia alisema na kueleza zaidi:

"Wabunge wote humu ndani tuna haki sawa za kutetea wananchi wetu. Anayetoka kwenye pamba ataitetea, anayetokea kwenye madini atatetea madini yake na korosho ana haki ya kuitetea korosho yake.

"Na mimi napenda niwahakikishie wananchi kwa ujumla kuwa wabunge wake tupo imara. Tutapambana kuhakikisha haki hii inapatikana na hata isipopatikana, wajibu wetu tutautimiza kama wawakilishi wa wananchi ambao tulichaguliwa kuja kuwatetea bungeni.

"Leo tunaambiwa kuwa eti ni wabinafsi, na ni mbinafsi? Kuna watu wanakuja kusimama wanasema wao ndiyo wanaijua korosho kushinda mtu mwingine humu ndani."

Alisema hata ukifika Chuo Kikuu cha Mzumbe, utakuta ripoti za utafiti wake kuhusu korosho na hata utafiti wake wa shahada yake ya uzamili ulikuwa unahusu namna ya kuifufua korosho na kuitafutia soko.

Kama ilivyokuwa wiki iliyopita wabunge wa pande zote mbili waliendelea kuibana serikali kulipa kiasi hicho cha fedha walipokuwa wanaendelea na mjadala wa mapendekezo ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha na Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017.

Hoja hiyo imeteka mjadala huo kutokana na serikali kuonekana kushindwa kutekeleza matakwa ya Sheria ya Tasnia ya Korosho, inayotaka asilimia 65 ya mauzo ya korosho inatakiwa irudishwe Bodi ya Korosho na asilimia 35 inatakiwa kupelekwa Mfuko Mkuu wa Serikali.

Kabla ya mjadala huo kuanza Jumatatu iliyopita, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Hawa Ghasia, aliwasilisha taarifa ya kamati yake bungeni siku hiyo na kueleza kuwa serikali imeshindwa kupeleka kwenye Bodi ya Korosho Sh. bilioni 201.281.

Kati yake, Sh. bilioni 91.15 ni za mwaka 2015/16 na Sh. bilioni 110.131 ni za mwaka 2016/17.

Ghasia alibainisha kuwa serikali imepeleka Sh. bilioni 10 kwenye mfuko hivyo, bado unaidai Sh. bilioni 81.15 za msimu uliotangulia, hivyo kuathiri zao hilo kwa kiasi kikubwa katika upatikanaji wa pembejeo.

Wakati kamati hiyo ikieleza hayo, jana Mbunge wa Mtama, Nape Nauye (CCM), alisema kuna uwezekano wa kuizika CCM mikoa ya kusini kama serikali haitatoa fedha hizo.

Alisema kuwa aliwahi kutoa hoja bungeni kuhusu suala hilo akitaka kusimamia utekelezaji wa sheria, lakini cha kushangaza anaona serikali inaacha kutekeleza sheria iliyopo huku ikiwasilisha mapendekezo bungeni kufuta ulipaji wa fedha hizo kwa wakulima na badala yake ziende serikali kuu.

Alisema kitendo hicho ni hatua ya serikali kuonyesha dharau kwa wakulima na Bunge, jambo alisisitiza si sawa na haikubaliki.

“Mimi nadhani maoni yangu hebu tuzungumzie namna ya kuleta fedha mlizochukua, hii habari ya kubadilisha sheria iacheni kwanza," Nape alisema.

"Maisha haya ni yetu, tusifike mahali tukafika huku maana ni pabaya sana. Leo mnataka kutupeleka kwenye korosho na hela mliyotarajia kuipata hamtaipata tena maana zao hilo linakufa.

“Mapendekezo yangu tuzungumzie namna ya kupata hela yetu, kueni na huruma kwetu na mapendekezo haya yanaenda kutuweka mahali pagumu sana.

“Nataka kuwaanbia, msipopeleka fedha za korosho kwa wakulima mtakuwa mmeizika CCM kabisa katika mikoa ya kusini maana kutakuwa hakuna namna nyingine ya kuweza kujinasua."

Wakati Nape akichangia, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Stella Manyanya, alisimama kutoa taarifa, akimtaka mbunge huyo kutowatia hofu wakulima wa korosho nchini.

Kutokana na hali ya zomea zomea na vurugu, Mwenyekiti wa Bunge, Azzan Zungu aliyekuwa anaongoza kikao cha jana, alisimama na kuwataka wabunge watulie, akieleza kuwa kila mtu ana uhuru wa kuchangia.

Rwekiza aliendelea kuchangia, akieleza kuwa orodha ya wachangiaji huwa anaipanga yeye na kwamba Ghasia hakupangwa licha ya kuwa kupata nafasi hiyo jana.

Wakati mjadala huo ukiendelea, Zungu alitoa angalizo la mwisho kwa wabunge waliokuwa wanapiga kelele kwa kuzomea na baadaye akaagiza Bwege atoke ndani ya Ukumbi wa Bunge kutokana na kusababisha vurugu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images