Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Balozi wa Syria aiomba radhi Serikali ya Tanzania

$
0
0
Balozi wa Syira nchini Abdulmonem Annan ameiomba radhi serikali ya Tanzania baada ya kusambaa kwa video iliyomuonyesha akisema atahamasisha raia wa Syria, wasiwekeze nchini kwa kile alichodai polisi hawalifanyii kazi suala la kuporwa fedha kwa Ofisa Ubalozi wa Syria. 

 Machi 20, Ofisa Ubalozi huyo, Hassan Alfaouri alishambuliwa na watu wasiojulikana na kuporwa zaidi ya euro 9300(zaidi ya Sh 25 milioni).

Baada ya tukio hilo, Balozi huyo alisema  alitoa taarifa kwenye mitandao ya kijamii  kwa njia ya video akisema kuna ufuatiliaji hafifu wa suala hilo na hivyo atahamasisha raia wa Syria wasije kuwekeza nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Suleman Salehe alisema maneno aliyosema balozi Annam yalikuwa ni ya uchochezi hivyo waliamua kufanya nae mikutano minne.

Alisema wao kama Wizara walifanya jitihada na kuhakikisha jeshi la polisi linafanya uchunguzi na kuhusiana na tukio hilo na kuwakamata watu wawili ambao ni dereva na katibu wake.

“Wizara inamshukuru Balozi kufunguka na kutoa taarifa muhimu kuwa ametaarifiwa na jeshi la polisi kuwa watuhumiwa wawili wamekamatwa na sehemu ya kiasii cha fedha kimepatikana”amesema Salehe

Amesema kwa kuwa balozi amebakiza miezi michache  amalize muda wake hapa nchini, Wizara itaanda taarifa ili aweze kukutana na Mkuu wa jeshi la polisi na washughulikie suala hilo.

Mnyeti Afungua Kiwanda Kilichofungwa na Mkea Mkuu wa Serikali, Ataka Akamatwe Yeye Badala ya Mmiliki

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amekifungua kiwanda cha pombe kali cha Mati Super Brand cha mjini Babati kilichofungwa na Mkemia Mkuu wa Serikali huku akitaka akamatwe yeye, badala ya wamiliki wa kiwanda hicho.

Mnyeti ameyasema hayo juzi wakati akichukua uamuzi huo ambapo amefafanua kwamba hakubaliani na sababu zilizotolewa mpaka kiwanda hicho kufungwa

Akitoa maelezo Mnyeti amesema mwekezaji huyo amefunga mitambo yake na kutoa ajira kwa wananchi, badala ya kupewa ushirikiano watendaji wanaohusika, wao ndiyo  wanamkwamisha kwa kukifunga kiwanda, ikiwa ni takribani miezi mitatu sasa.

"Bado kuna watu wanaandaa mazingira ya rushwa, yaani badala watumie hata siku tatu za kumshauri kitaalamu wanakimbilia kufunga kiwanda. Kuna baadhi ya watumishi wa Serikali wana ukiritimba mno, sasa mimi nakifungua kiwanda hiki halafu wakija wanikamate mimi," alisema.

Mkemia Mkuu wa Serikali alikifunga kiwanda hicho kwa maelezo kuwa kimekosa kibali cha kuidhinisha matumizi ya kemikali za kuzalisha pombe hizo Machi, 2018

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Waziri Mkuu ashauri wajenzi wakope trilioni 1/- NEEC

$
0
0
WAJENZI wametakiwa kutumia fursa ya uwepo mifuko 19 yenye ukwasi wa zaidi ya Sh trilioni 1.3 katika Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kitaifa (NEEC) kukopa ili kuimarisha, kuboresha, kuongeza bidhaa na kupanua huduma zao.

Akizindua Maonesho ya Wajenzi Dodoma kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Kazi, Vijana na Ajira), Anthony Mavunde alisema fursa hiyo ni muhimu kwao waitumie kwa kuinua mitaji na kuboresha bidhaa na huduma zao.

Maonesho hayo ya Wajenzi Dodoma ya siku mbili yenye kaulimbiu 'Tunajenga Jiji la Dodoma,' Majaliwa alisema wanatakiwa kutoogopa kutumia fursa hiyo ya uwepo wa mifuko hiyo katika kukopa na kupata fedha za mitaji katika kuzalisha bidhaa ambazo zitachangia kuboresha bidhaa za ujenzi wa Dodoma kuwa mji wa kisasa zaidi.

“Serikali ipo pamoja na kampuni za wazawa ambazo zinazalisha bidhaa na zinazoa huduma mbalimbali, hivyo nazo zinatakiwa kutengeneza bidhaa zenye viwango ili kuleta mchango katika uchumi nchini,” alisema.

Alisema kampuni hizo zikipata mikopo zitasaidia vijana ambao ni nguvukazi muhimu kupata kazi na kutoa mchango mkubwa katika kuzalisha bidhaa na kukuza uchumi na kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo 2025.

“Wajenzi watakuwa wamechangia kwenye mkakati wa serikali ambao unataka ifikapo 2021, vijana asilimia 40 wana kwenye shughuli za viwanda,” alisema Waziri Mkuu.

Alisema katika kufikia azma hiyo ya kuwa katika uchumi wa kati mwaka 2025, lazima kuwa na namba maalumu za vijana wenye ujuzi mkubwa ili kushiriki katika uzalishaji viwandani.

Alisema kwa sasa takwimu zinaonesha kwamba nchi ina nguvu kazi ya watu milioni 23.3 na vijana wenye umri wa kati ya miaka 14 hadi 34 ni milioni 14.4 ambao wanatakiwa ndio wanatakiwa kuwa kuwa na ujuzi ujuzi wa juu.

“Kwa sasa ni vigumu nchi kufikia katika uchumi wa kati kama vijana wengi wenye ujuzi wa juu, kati na chini ni wachache, hivyo inatakiwa kuongezeka ili kufikia malengo hayo.

Alisema kati ya nguvukazi hiyo ya vijana milioni 22.3, wenye ujuzi wa juu ni asilimia 3.6 tu, ujuzi wa kati ni asilimia 16.5 na ujuzi wa chini ni asilimia 79.9, kiwango ambacho ni kidogo.

“Ili kufikia uchumi wa kati inatakiwa kuwa vijana wenye ujuzi wa juu asilimia 12, wa kati asilimia 34 na wa chini asilimia 54," alisema.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga alisema lengo la maonesho hayo ni kuhakikisha watu wanapata fursa ya kwenda kuona maonesho ili kupata bidhaa zenye ubora kwa ajili ya ujenzi wa Dodoma.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa alisema wajenzi wanatakiwa kuhakikisha wanazalisha bidhaa bora ambazo zitashindana katika soko la nje ya ndani ya nchni.

Majaliwa alisifia waandaaji wa maonesho hayo yanayoshirikisha kampuni 40, ambao ni Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) pamoja na AFM, akisema ndio yameanza, lakini baadaye yatakuwa makubwa na kushirikisha kampuni za nje ili kupata taaluma, mang'amuzi na ujuzi wao.

Waziri Ummy: Nitakuwa Mkali Kwa Yeyote Atakayekwamisha Huduma za Afya Nchini

$
0
0
SERIKALI imesema itaongeza nguvu kuhakikisha wagonjwa wa figo, moyo na saratani wanapata huduma za kibingwa katika hospitali za hapa nchini.

Pia imesema haitamvumilia mtu yeyote ambaye atasababisha kudorora kwa mkakati huo wa serikali wa kuwezesha huduma za magonjwa yasiyoambukiza nchini ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wadhamini wa Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini hapa. Bodi hiyo inaongozwa na Dk Deodatus Mtasiwa.

“Mimi nitaendelea kuwa mkali sana kwa mtumishi yeyote atakayesababisha kudorora au kukwama kwa huduma za afya katika hospitali zetu,” alisema Ummy na kuitaka bodi hiyo kuwa makini na kuhakikisha hakuna uzembe unaofanyika katika uendeshaji wa hospitali hiyo nyeti.

Alisisitiza kuwa usimamizi makini utawezesha lengo la kuanzishwa kwa hospitali hiyo la kutoa huduma za afya maalumu za kibingwa, huduma za uchunguzi na tiba kwa magonjwa yote huku ikijikita zaidi kwenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama figo, moyo, macho, damu na saratani kufikiwa kwa ufanisi uliotarajiwa.

Huduma nyingine zilizopangwa kutolewa ni pamoja na kutoa huduma za endoscope, kufundisha wataalamu wa kada za afya na kufanya tafiti mbalimbali ili kuboresha afya ya jamii ya Watanzania na hivyo kuipunguzia serikali mzigo wa gharama za matibabu nje ya nchi.

Akizungumzia umuhimu wa hospitali hiyo, alisema kuna ongezeko kubwa la magonjwa yasiyo ya kuambukiza duniani kwani Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema wagonjwa 100, kati ya hao, 47 huugua magonjwa yasiyo ya kuambukiza, na vifo 100, kati yake, 60 hutokana na magonjwa hayo.

“Kama tusipochukua hatua za kudhibiti takwimu hizo zitaongezeka mara mbili zaidi na serikali itaongeza nguvu kusaidia magonjwa ya figo, moyo na saratani,” alisema Ummy.

Alisema kwa mwaka 2013 hadi 2016, serikali ilipeleka wagonjwa 590 kwenda kutibiwa nje ya nchi, ambao wagonjwa 430 kati yao, walikuwa wa moyo na 160 wa kupandikizwa figo.

“Kwa takwimu za kuanzia Julai 2013 hadi Juni 2016, magonjwa ya moyo na figo ndiyo yalikuwa yakiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa kutibiwa nje ya nchi na kuigharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 36.6,” aliongeza waziri.

Alisema, kati ya wagonjwa 590 waliosafirishwa na serikali, 430 walienda kutibiwa moyo na 160 walienda kupandikizwa figo.

Alisisitiza kuwa kwa kuanzishwa huduma hizo katika hospitali mbalimbali nchini ikiwemo ya Benjamin Mkapa, kutaokoa kiasi kikubwa cha fedha na kuipunguzia serikali mzigo wa gharama.

Aliiagiza Bodi ya Hospitali ya Benjamin Mkapa kuwa kwa kuwa imeanza upandikizaji wa figo kuhakikisha inaweka malengo ya kupandikiza idadi maalumu ya wagonjwa itakayosaidia kukuza uwezo na taaluma.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo iliyopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Alphonce Chandika alimweleza waziri kwamba baada ya mafanikio ya upandikizaji wa figo wakisaidiana na wadau wa Tokushukai kutoka Japan, Machi 22, mwaka huu, wagonjwa wengine watafanyiwa upandikizaji huo Agosti mwaka huu.

Alisema mwezi ujao wataanzisha upasuaji wa kutumia matundu madogo kwa kushirikiana na wadau kutoka Marekani baada ya madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, koo, pua na masikio kurejea nyumbani wakitokea India walikonoa bongo zao kuhusu tiba hiyo.

Pamoja na kutaka usimamizi makini ili kuokoa maisha ya Watanzania na fedha zinazotumika kupeleka wagonjwa nje, Ummy alitaka bodi kuhakikisha fedha za mkopo Sh bilioni 119 kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) zilizokopwa kujenga hospitali zinalipwa.

Akizungumzia masuala ya utafiti, pamoja na kulazwa kwa wagonjwa, alisema ndani ya mwezi moja wagonjwa wataanza kulazwa katika hospitali hiyo na anatarajia watakaofika kulazwa ni wale wanaohitaji huduma za kibingwa.

“Ndugu Mwenyekiti wa Bodi, tafiti ni eneo nyeti na muhimu sana katika kukuza na kuendeleza weledi, ujuzi na maarifa katika taaluma mbalimbali, hivyo ni lazima hospitali ijikite katika kufanya tafiti mbalimbali ili kugundua matatizo/changamoto na kuyapatia majawabu kwa maendeleo ya hospitali na Taifa kwa ujumla,” alisema Ummy.

Aliongeza kuwa ni matumaini yake bodi hiyo kwa kushirikiana na uongozi wa hospitali itahakikisha shughuli za utafiti zinaendelea kufanyika kikamilifu na matokeo ya utafiti yatumike kubaini na kutatua changamoto ili kuboresha utoaji wa huduma ya matibabu nchini.

Alisema uanzishwaji wa hospitali hiyo ya kibingwa ni utekelezaji wa mikakati ya serikali ya kupambana na magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza.

Polycarp Pengo awataka maaskofu kuhubiri umoja wa Taifa

$
0
0
 Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amewataka maaskofu kuhubiri umoja kwa waumini wao.

Pengo amesisitiza hilo leo Jumapili Juni 24, 2018 katika misa ya kumuweka wakfu Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga, Beatus Urassa inayofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania mjini humo na kurushwa moja kwa moja na Redio Tumaini.

“Katika kuliongoza Tanzania ni muhimu sisi maaskofu tusisitize juu ya umoja wa waamini waliokombolewa kwa damu moja ya Kristu. Kwa mazingira ya Tanzania, wewe na mimi na maaskofu wote tusisitize umoja wa Watanzania na Tanzania,” amesema Pengo.

“Tusikubali  kuziruhusu damu mbalimbali zinazotufanya kuwa wenye kabila hili au lile zikatawala na kuvunja umoja  wa Taifa letu. Tuombeane katika kazi hii. Tutunze umoja wa waumini na wa Taifa letu.”

Amesisitiza, “Wewe umezaliwa mkoani Kilimanjaro ni mchaga unayetoka Rombo. Katika utandawazi wa Tanzania siku hizi ni muhimu kuzingatia yafuatayo, unayo damu ya kichaga ndani ya mwili wako, nakuomba wala usikatae na usijaribu kuificha damu hii.”

“Hakuna sababu wala uhalali kwako wa kujaribu kuficha ukweli huu. Neno moja lazima ulikumbuke ni kuwa wewe na mimi na kundi lote hatujakombolewa kwa damu ya kichaga wala ya kifipa na kinyakyusa, sote tumekombolewa kwa damu ya Kristo.”

Askofu Urassa anachukua nafasi ya Mhashamu Damian Kyaruzi ambaye amestaafu.

Waziri Mwakyembe Amtembelea Kumjulia Hali Mzee Majuto

$
0
0
Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) jana  tarehe 23 Juni, 2018 amemtembelea msanii nguli wa filamu Bw. Amri Athumani (Mzee Majuto) ambaye amefikia katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam akitokea India alipopelekwa na Serikali kwa ajili ya kupata matibabu.

 "Serikali inafuatilia matibabu yako kwa ukaribu, hivyo usiwe na wasiwasi", alisisitiza Dkt. Mwakyembe akiongoea na Mzee Majuto. 

Akizungumza Mzee Majuto ameishukuru Serikali kwa kumhudimia na kumpeleka India kupata matibabu.

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Lapata Rais Mpya

$
0
0
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) leo Jumapili Juni 24, 2018 limemchagua Askofu wa Jimbo Katoliki la Mpanda, Gervas Nyaisonga kuwa rais wa baraza hilo.

Askofu Nyaisonga aliyetangazwa leo katika misa  ya kumuweka wakfu Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga, Beatus Urassa iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania mjini humo, amechukua nafasi ya Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa aliyemaliza muda wake.

Ngalalekumtwa amemtangaza Askofu Nyaisonga na kusema atatumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu.

England Yaifungashia Virago Panama Kombe La Dunia Kwa Kipigo Cha Mbwa Koko

$
0
0
Timu ya England imeibuka na ushindi mnono wa mabao 6-1 baada ya kuisambaratisha Panama bila huruma kwenye fainali za Kombe la Dunia mchezo uliopigwa leo Jumapili  katika Uwanja wa Nizhny Novgorod, Russia
 
Ushindi huo unaipandisha England kileleni kwenye msimamo wa Kundi G ikiwa pointi 6 sawa na Ubelgiji lakini wakiwa na tofauti ya mabao ya kufunga.
 
Kwenye kundi hilo, Panama na Tunisia zimejikuta zikianza kufungasha virago baada ya kupoteza michezo yake miwili  kila timu.
 
Katika michezo miwili, Panama imezalisha mabao 9 baada ya kupoteza mchezo mbele ya Ubelgiji iliyoibuka na ushindi wa mabao 3-0 na kupokea kipigo cha mabao 6 leo.
 
Mabao ya England yaliwekwa wavuni na Harry Kane aliyefunga ‘hat trick’, John Stones (2) huku bao la tatu likiwekwa wavuni na Jesse Lingard.
 
Panama itakamilisha mchezo wake wa mwisho dhidi ya Tunisia Juni 28 wakati England itakamilisha mechi yake dhidi ya Ubelgiji tarehe hiyohiyo.
 
Mchezo wa jana usiku, Ubelgiji iliiadhibu Tunisia mabao 5-2 na kukata tiketi yake mapema ya kucheza hatua ya 16 bora.

CUF waichambua bajeti ya Serikali 2018/2019

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) kimeishauri Serikali kutenga zaidi ya asilimia 10 ya bajeti yake kwa ajili ya sekta ya kilimo ili kufikia azma ya Tanzania kuwa nchi yenye uchumi wa kati.

Kauli hiyo imetolewa leo Juni 24, 2018 na Julius Mtatiro, mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya chama hicho upande unaomuunga mkono Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.

Akichambua bajeti ya Serikali iliyowasilishwa Alhamisi iliyopita bungeni mjini Dodoma, Mtatiro amesema bajeti hiyo haijatoa mikakati ya kuinua sekta jumuishi ambazo zinaajiri watu wengi kama kilimo, ufugaji, uvuvi, biashara na utalii.

Amesema kilimo ambacho kinaajiri zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania kila mwaka kinapangiwa bajeti chini ya asilimia mbili, fedha zinazopitishwa na Bunge hazitolewi zote.

Mtatiro amesema uchumi hauwezi kukua kama Serikali haitaweka mikakati ya kuchochea sekta zinazoajiri watu wengi.

"CUF tulitarajia kwamba bajeti itaweka mipango ya kusimamia sekta jumuifu zenye kuajiri watu wengi, lakini hamna kitu. Hakuna usimamizi kwenye mazao muhimu ya biashara, hata korosho iliyoingiza zaidi ya Sh1 trilioni haijawekewa mikakati ya kuiinua zaidi," amesema Mtatiro.

Amebainisha kwamba mwaka 2017 sekta ya uvuvi haikupangiwa kabisa fedha za maendeleo lakini mwaka huu imetengewa Sh56 bilioni ambazo nazo anasema hazitoshi kuinua sekta hiyo.

"Kila mwaka vijana milioni moja wanaingia kwenye soko la ajira wakati Serikali na sekta binafsi zikiajiri watu wasiozidi 100,000. Hapa kuna tatizo na bajeti kuu haijaliangazia hili,” amesema.

Senegal yabeba matumaini kutinga 16 bora

$
0
0
Timu za Senegal na Japan zimegawana pointi baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 huku sare hiyo ikiziweka kwenye matumaini ya kufuzu hatua ya 16 bora baada ya kufikisha pointi nne kila moja.

Senegal na Japan ili kuwa na uhakika wa kufuzu hatua ya 16 bora zitasubiri matokeo ya mechi baiana ya Poland na Colombia mchezo unaotarajiwa kupigwa usiku huu leo Jumapili.

Sare yoyote ya Poland na Colombia itakuwa imezipa nafuu Japan na Senegal na kuzipa nafasi ya kubwa ya kusonga mbele.

Kundi H ambalo lina timu za Japan, Senegal, Poland na Colombia zitakamilisha mchezo wa tatu kila moja Juni 28 ambapo Colombia itakutana na Senegal huku Japan wakiwavaa Poland.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 25

Ratiba Ya Mechi Zote Kombe La Dunia Hadi Fainali

$
0
0
 Fainali za Kombe la Dunia 2018  zilianza rasmini June 14 nchini Urusi .

Tazama  hapa  ratiba ya mechi zote za michuanpo hiyo kuanzia ile ya ufunguzi hadi fainali yenyewe.

Poland Yaaga Kombe La Dunia Urusi Kwa Kichapo Cha Bao 3-0 Dhidi Ya Colombia

$
0
0
Poland imeyaaga mashindano ya Kombe la Dunia Urusi kwa kukubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Colombia.

Matokeo ya mchezo huo yamewekwa kimiani na Yerry Mina (40'), Radamel Falcao (70') na Juan Cuadrado dakika ya 75.

Poland inaondoka rasmi kwenye michuano kufuatia kupoteza mchezo wa pili mfululizo baada ya ule kwanza dhidi ya Senegal kuruhusu nyavu zao kufungwa mabao 2-1.

Msimamo wa kundi H unaonesha Colombia wapo nafasi ya tatu wakiwa na alama 3 huku Senegal wakishika nafasi ya pili, wakati Japan wakiwa wa kwanza.

Tanzania Yaweka Msimamo Mkali Kwenye Itifaki Ya Utalii Na Usimamizi Wa Wanyamapori Ya EAC

$
0
0
Na Hamza Temba-Arusha
……………………………………………………..
Itifaki ya Utalii na Usimamizi wa Wanyamapori katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) imezua mjadala mzito na mabishano makali katika Mkutano wa Nane wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa jumuiya hiyo uliofanyika Jijini Arusha juzi.

Mvutano huo ulisababishwa na hoja iliyowasilishwa na Tanzania ambayo ilitaka kuboreshwa kwa kifungu cha nne cha itifaki hiyo ambacho kinazitaka nchi wanachama kutangaza eneo lote la jumuiya ya Afrika ya Mashariki kama kituo kimoja cha safari za utalii duniani.

Tanzania ikiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, ilipinga vikali na hatimaye ikagoma kusaini itifaki hiyo ambayo imejadiliwa kwa zaidi ya miaka saba mpaka pale mapendekezo yake yalipoingizwa kwenye kifungu hicho.

Kifungu hicho kilikuwa kinasema, “Every Partner State shall market and promote the Community as a single tourist destination”, (Kila nchi mwanachama itatangaza jumuiya kama kituo kimoja cha safari za utalii (duniani)).

Tanzania ikapendekeza kwenye kifungu hicho uongezwe mstari unaosema, “while maintaining country identites” (huku kila nchi mwanachama ikibaki na utambulisho wake halisi).

Mapendekezo hayo ya Tanzania yaliungwa mkono na Burundi na kupingwa vikali na nchi za Kenya, Uganda na Rwanda ambazo zilisema hakuna madhara yeyote ya kutobadilisha kifungu  hicho. Nchi ya Sudan Kusini haikuweza kushiriki mkuatano huo.

Licha ya majadiliano makali yaliyosababisha mkutano huo  kumalizika majira ya saa nne za usiku badala ya saa 12 jioni kwa mujibu wa ratiba ilivyopangwa, wajumbe hao walikubali mapendekezo ya Tanzania na hatimaye itifaki hiyo ikasainiwa.

Awali itifaki hiyo ilijadiliwa kwenye vikao vya wataalam wa jumuiya hiyo na Makatibu Wakuu, siku tatu kabla ya kuwasilishwa kwenye Baraza hilo la Mawaziri.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla alisema Tanzania ililazimika kuweka msimamo huo ili kuepuka madhara ya nchi nyingine kutangaza vivutio vyake kuwa viko nchini kwao kama ambavyo nchi ya Kenya imewahi kutangaza mlima Kilimanjaro upo kwao.

Aidha, alisema msimamo huo pia ulilenga kulinda maslahi ya Tanzania kwakuwa ni nchi pekee yenye vivutio vingi na ambayo imehifadhi ardhi yake kwa zaidi ya asilimia 32 ukilinganisha na nchi nyingine wanachama, mfano Kenya ambayo imehifadhi asilimia 7 tu ya ardhi yake.

Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Ibara ya 115 (1-3) na Ibara ya 116 unaeleza kuwa jumuiya inaweza kuanzisha sera, mikakati na mbinu mbalimbali za kufanya shughuli za utalii na usimamizi wa wanyamapori kwa pamoja, huku kila nchi ikiruhusiwa kubaki na usimamizi, mikakati na sera zake kadri inavyoona inafaa.

BAWACHA wasema katazo la mikutano ya hadhara Ni Pigo Kwa Wanawake

$
0
0
Baraza la Wanawake  Chadema (Bawacha) limesema uamuzi wa Serikali kupiga marufuku mikutano ya hadhara unarudisha nyuma juhudi za wanawake kufikia usawa wa asilimia 50 kwa wanawake kwa wanaume.

Kauli hiyo imetolewa jana Jumapili Juni 24, 2018 na makamu mwenyekiti wa baraza hilo, Hawa Mwaifunga wakati akizungumza na wanahabari katika mkutano wa kamati ya utendaji ya baraza hilo uliofanyika mjini hapa.

Mkutano huo wa siku mbili pamoja na mambo mengine unalenga kuwapa mafunzo, mbinu na ujasiri viongozi wa mikoa wa chama hicho.

Mwaifunga alisema wanawake wengi wamekuwa na hofu kutokana na uamuzi wa kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara, jambo ambalo linawafanya wanawake washindwe kujitosa katika siasa.

Alisema uamuzi huo umewanyima fursa Watanzania kuwasikiliza wanasiasa ili baadaye waje wafanye uamuzi wa kuwachagua wagombea wa chama kinachofaa.

“Kwa sasa ni kutishana na kukamatwa na kuwekwa ndani. Kipindi cha nyuma watu walifanya siasa za kistaarabu sana, ndiyo maana tuliwapata akina Halima Mdee (mwenyekiti Bawacha), Paulin Gekul (Babati Mjini (Chadema). Walipatikana baada ya kuonekana majukwaani,” alisema.

Katibu wa Bawacha,  Grace Tendega alisema wataendelea kupambana  licha ya kuwa wanaoonekana kufanya siasa majukwaani wanakamatwa.

Alisema baraza hilo limejipanga kuhakikisha majimbo sita yanayoongozwa na wabunge wanawake wa Chadema yanalindwa.

Steve Nyererre Akerwa na Picha za Nusu Uchi Irene Uwoya

$
0
0
Msanii wa bongo movies Steve Nyerere ameonyesha kukerwa kwake na tabia ya baadhi ya wasanii kutumia miili yao kama kiki katika sanaa hasa kwa kukaa uchi jambo ambalo limekuwa likifanywa sana na wakina dada katika tasnia ya sanaa.

Steve Nyerere anasema kuwa haamini hata kidogo kama msanii mkubwa kama Irene Uwoya anaweza kutumia mwili wake kuweka wazi kwa ajili ya kupata kiki katika mtandao ilihali swala hili linadhalilisha sana hadhi yake  na watu wake wa karibu.
 
Katika ukurasa wake wa instagram , steve nyerere aliandika “Sitaki kuamini kuwa kiki inapatikana kwa kukaa uchi au ili uwe star  lazima ufanye kitu ambacho jamii na familia yako itakuona  wewe kama kituko na kitu cha ajabu basi wewe hapo ukajiona star , hapana hapo hata waliokuzunguka watakuona kituko.”

"Sifa ya msanii ni moja tu , msanii ni kioo cha jamii,kuburudisha na kuelimisha kupitia sanaa ama kipaji chake,  inapotokea mtu anafanya kinyume na katiba yetu huyo anatuchafua wote, hata wenye maadili wanaonekana walewale."

Wikiend iliyopita, mwana dada Irene Uwoya aliweka picha katika ukurasa wake wa instagram na Kuacha watu mdomo wazi baada ya picha hiyo kumuonyesha akiwa mtupu na sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa wazi ilhali heshima yake katika jamii ni tofauti na yale anayoyafanya.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images