Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Sakata la Korosho Laendelea Kutikisa Bungeni

0
0
Sakata la kutaka Serikali kutoa asilimia 65 ya ushuru wa mauzo ya korosho nje ya nchi limeendelea kutikisa Bunge baada ya mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali kusema iwapo Serikali haitatoa fedha hizo utakuwa mwanzo wa kufa kwa chama tawala katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

“Waziri Mpango (Dk Philip-Waziri wa Fedha na Mipango) wewe ni mchumi. Watu wa Lindi na Mtwara tulikuwa maskini na zao la korosho ndilo lilikuwa mkombozi wetu, hatutakubali kukaa bungeni kama zao la korosho linakufa, tunakwenda kuandamana, mnaleta mabadiliko ya sheria, kwa kweli hili hatutakubali,” alisema Bobali.

Tayari baadhi ya wabunge wametishia kufanya maandamano iwapo Serikali haitatoa asilimia 65 ya ushuru wa mauzo ya korosho nje kwa ajili ya maendeleo ya zao hilo.

Pia, wamepinga mabadiliko ya sheria ya korosho yanayokusudiwa kufanywa na Serikali ili ushuru huo upelekwe katika Mfuko Mkuu wa Hazina.

Bobali ametoa kauli hiyo jana Ijumaa Juni 22, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Serikali bungeni mjini Dodoma.

“Kuna Sh200 bilioni zinazodaiwa na wakulima, Waziri Mpango (Philip-Waziri wa Fedha na Uchumi) peleka hizi fedha wakulima wa korosho hatutakubali na habari hii si ndogo, hili jambo ni zito nawambieni CCM inakwenda kufa,” alisema.

Bobali aliungwa mkono na mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Tuza Malapo aliyesema kuwa haiwezekani kuzungumzia uchumi wa mikoa ya Kusini bila kuzungumzia zao la korosho na kusisitiza Sh200 bilioni ni lazima zipelekwe  kwa wakulima.

“Mimi nimezaliwa Mtwara, nimesoma Mtwara kwa hiyo najua hili suala la korosho naomba kupata majibu ya hizi fedha. Waziri Mpango semeni hizi fedha mnazipeleka lini na ziko wapi. Tumekuita katika kikao mara kadhaa hukuja, na hii sheria mliyoileta najua itapita maana kila jambo likija humu ndani linapita,” alisema.

Tumekurahisishia....Fuatilia HAPA LIVE Kila Kitu Kinachoendelea Kombe la Dunia Nchini Urusi

0
0
Tumekurahisishia....Fuatilia HAPA  LIVE  Kila Kitu Kinachoendelea Kombe la Dunia Nchini Urusi 

  Keyword:
MP=Matches Played
W=Matches Won
D=Draws
L=Matches Lost
P=Points

Inasemekana Infinix Kushirikiana Na Google Katika Uzinduzi Wa Simu Mpya Barani Afrika.

0
0
inasemekana kampuni ya simu ya Infinix kuzindua simu mpya ikiwa ni muendelezo wa Infinix NOTE 4 kwa kushirikiana na GOOGLE. Uzinduzi huo unategemewa kufanyika mnamo mwezi wa sita barani Afrika nchini Dubai katika jengo la Burj Khalifa.
 
Kwa pamoja ikishirikiana na GOOGLE kampuni ya simu ya Infinix imeweka nia ya kuzindua simu iliyo na ubora zaidi ya matarajio ya wengi na inasemekana kupitia ushirika wake na GOOGLE ujio wa simu zote za NOTE kutumia mfumo wa Android 1 (A1) wenye ufanisi zaidi ya Android Oreo.
 
Zaidi ya watu 200 mpaka sasa wameshapata mwaliko kutoka katika kampuni hizo mbili kwenda kushuhudia uzinduzi huo pamoja na kushuhudia namna Android 1 (A1) inavyofanya kazi kupitia GOOGLE Assistant na GOOGLE Lens.
 
 Akiongelea mafanikio ya kampuni, muongeaji wa kampuni ya Infinix Bwana Erick Mkomoye alisema kwamba, “tangu kutambulishwa kwa kampuni ya Infinix mwaka 2013, kampuni imeweza kudhihirisha ubora wake na kuweza kupenya katika masoko ya Afrika na tuko mbioni kuwaletea teknolojia mpya kupitia simu mpya itakayozinduliwa wiki ijayo.

Zitto Kabwe Afunguka Mazito...." Ni makosa makubwa tunakwenda kuyafanya"

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), amesema hali mbaya ya uchumi iliyoko nchini na matatizo ya kibajeti ni matokeo ya makosa yaliyofanyika katika bajeti ya mwaka 2016/17 baada ya serikali kuongeza kodi kwenye maeneo mbalimbali, hususan utalii.

Vile vile, amesema endapo sekta ya utalii, zao la korosho na Bandari ya Dar es Salaam vitaendelea kuchezewa, kiwango cha kubadilishia fedha kitafika Sh. 5,000 hadi 6,000 kwa Dola moja.

Zitto alitoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma jana alipokuwa anachangia mapendekezo ya bajeti ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha na Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017.

“Matatizo yote ya kibajeti na ukwasi wa fedha tulio nao hivi sasa ni kutokana na makosa yaliyofanyika mwaka 2016/17 baada ya serikali kuongeza kodi kwenye huduma za utalii," Zitto alisema na kueleza zaidi:

“Ndiyo maana bajeti hii na ya mwaka jana imepanda kwa asilimia mbili tu. Serikali irekebishe makosa haya kwa sababu tangu kodi imepandishwa kwenye utalii, kasi yetu ya kuongeza utalii imezidi kushuka.

“Huko nyuma utalii ulikua kwa asilimia 12 lakini sasa hivi ni asilimia tatu. Nataka niwaambie sasa hivi ukicheza na utalii, ukicheza na Bandari ya Dar es Salaam, ukicheza na zao la korosho, 'exchange rate' (kiwango cha kubadilisha fedha) kitafika mpaka Sh. 5,000 na 6,000.

“Hii ni kwa sababu sekta hizi zinatuingizia fedha za kigeni. Napendekeza ile VAT (Kodi ya Ongezeko la Thamani) kwenye utalii iondolewe."

Akizungumzia kuhusu mfumo mpya wa stempu za kielektroniki (ETS), Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo alisema utaongeza gharama kwa wananchi kwa sababu bei ya vinywaji kama vile maji na soda itaongezeka, lakini akasisitiza kuwa ukisimamiwa vizuri mapato ya nchi yataongezeka.

Kuhusu kusudio la marekebisho ya Sheria ya Mfuko wa Korosho ili asilimia 65 ya mauzo ghafi yapelekwe kwenye Hazina, Zitto alisema ni makosa makubwa kwa serikali kutaka kuchukua fedha hizo za wakulima.

“Fedha ambayo imetengwa kisheria mmechukua hamjarudisha halafu hapo hapo mnataka kubadilisha sheria ili fedha hizo ziende kwenye Mfuko wa Hazina, hili haliwezekani kabisa,” Zitto alisema.

Katika mjadala huo, Mbunge wa Muleba Kusini, Prof. Anna Tibaijuka (CCM), alisema kwa sasa serikali inatumia fedha nyingi kulipa Deni la Taifa, jambo ambalo anaamini litakwamisha maendeleo.

“Waziri wa Fedha na Mipango, (Dk. Philip Mpango) tunakuomba utakapokuja hapa kufanya majumuisho, utuletee majibu kwamba tumejisahau wapi," alisema Prof. Tibaijuka.

Naye Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe (Chadema) aliitaka serikali kukamilisha mradi mmoja baada ya mwingine na kuachana na utaratibu wake wa kuanzisha miradi mipya wakati ya nyuma haijakamilika.

“Tulianza gesi ya Mtwara ambayo ingewanufaisha wananchi lakini serikali imeruka, imeachana na gesi wamekimbilia kwenye mradi wa Stiegler’s Gorge. Hatuna nia ya kupinga huu mradi lakini kwanini tusikamilishe kwanza miradi iliyopo?" Mwambe alihoji.

“Kuhusu zile Sh. bilioni 81 za wakulima wa korosho, nitaongoza wananchi wangu wa Ndanda katika maandamano mpaka serikali itoe hizo fedha kama alivyosema juzi Bwege (Mbunge wa Kilwa Kusini, Selemani Bungara -CUF).

“Fedha zetu hawajatupa halafu wanataka kubadilisha sheria ili fedha zote ziende kwao, hatutakubali na wanataka kuwaingiza Watanzania mkenge, hili jambo watuachie sisi wamakonde."

Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF), aliunga mkono hoja hiyo akieleza kuwa Dk. Mpango asipotoa Sh. bilioni 81 za Mfuko wa Korosho, wananchi wa kusini hawatamwelewa.

“Mnataka kubadilisha sheria ili fedha mchukue, huu uchumi wa aina gani huu Dk. Mpango? Naomba upeleke fedha za korosho vinginevyo hatutakuelewa maisha yote. Hii habari si ndogo hata kidogo. Hicho chama chenu lazima mjue mnakizika huko kusini," Bobali alisema.

Katika mjadaka huo, Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga (Chadema), aliitaka serikali kupandisha mishahara ya watumishi wa umma kwa kuwa ni muda mrefu haijafanya hivyo ilhali ni matakwa ya kisheria.

Mbunge wa Geita Mjini, Costantine Kanyasu (CCM) aliipongeza serikali kwa jitihada zake kukuza uchumi wa Tanzania lakini akakosoa operesheni dhidi ya uvuvi haramu inayofanywa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, akieleza kuwa inapunguza mapato yatokanayo na sekta ya uvuvi.

Neema kwa Vijana: Tazama Hapa Tangazo la Nafasi za Kazi Toka Jeshi la Polisi

0
0
TANGAZO LA AJIRA.

Jeshi la Polisi Tanzania linatangaza nafasi za ajira kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa vijana wa JKT wa Operesheni Kikwete waliopo nje ya kambi za JKT (waliomaliza mkataba wenye elimu ya kidato cha nne, sita, stashahada, stashahada ya juu na shahada.

Waombaji watatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:

1.Awe nje ya kambi ya JKT. 
2. Awe Mtanzania kwa kuzaliwa. 
3. Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 25 kwa wenye elimu ya kidato cha nne, sita na stashahada.
4.Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi 28 kwa wenye elimu ya Stashahada ya juu na Shahada. 
5. Awe na elimu ya kidato cha nne aliyemaliza mwaka 2014, 2015 na 2016 mwenye ufaulu ufuatao:-
  • . Aliyemaliza mwaka 2014 awe na ufaulu wa GPA usiopungua 0.6
  •   Aliyemaliza mwaka 2015 na 2016 awe na ufaulu usiozidi alama (Points) 30.
6. Awe na elimu ya kidato cha sita aliyemaliza mwaka 2014, 2015 na 2016 na kufaulu. 
7. Awe na Stashahada aliyehitimu mwaka 2014, 2015 na 2016. 
8. Awe na Shahada aliyehitimu mwaka 2014, 2015 na 2016. 9. Awe na cheti halisi cha kuzaliwa, vyeti vya taaluma (Academic Certificates) pamoja na vyeti vya kuhitimu elimu aliyonayo (Leaving Certificate/Transcript). 
10. Awe na picha 3 za rangi (passport size). 
11. Asiwe na kumbukumbu za uhalifu. 
12. Awe na afya njema (kimwili na kiakili) iliyothibitishwa na daktari wa serikali. 
13. Awe hajaoa/hajaolewa au kuwa na mtoto. 
14. Asiwe na alama za kuchora mwilini (Tattoo). 
15. Awe tayari kufanya kazi za Polisi mahali popote Tanzania. 
16. Awe na urefu usiopungua futi tano inchi tano (5.5″) kwa wanaume na futi tano na inchi tatu (5.3) kwa wanawake. 
17. Waombaji watakaofaulu usaili ndio watakaochaguliwa. 18. Awe hajawahi kutumia madawa ya kulevya.
19. Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya Polisi. 
20. Awe hajaajiriwa na Taasisi nyingine. 

21. Waombaji wote waandike barua za maombi wao wenyewe kwa mkono (hand written) wakiambatanisha nakala za vivuli vya vyeti kwa anuani ifuatayo:- 

Inspekta Jenerali wa Polisi, 
Makao Makuu ya Polisi,
S.L.P 9141
 Dar es Salaam.

NB: Barua za maombi ziwasilishwe kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa ambapo mwombaji yupo. 

22. Waombaji wenye masomo/taaluma za Sayansi na Ufundi watapewa kipaumbele. 
23. Usaili utafanyika kwenye Ofisi ya Kamanda wa Mkoa husika. 
24. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 01/07/2018.

Kwa maelezo/ufafanuzi zaidi kuhusu nafasi, sifa na vigezo pamoja na tarehe ya kuanza usaili tembelea tovuti ya Polisi kwa anuani ifuatayo www.policeforce.go.tz au fika Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa uliopo.

Swing Asli

IMUSSA A. TAIBU – ACP] 
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Mzee Majuto asimulia jinsi India ilivyonusuru maisha yake

0
0
Mchekeshaji maarufu nchini Amri Athumani maarufu kama Mzee Majuto, amerejea nchini kutoka India alikokuwa akifanyiwa matibabu ya tezi dume.

Ambapo amefunguka kuwa sasa anaendelea vizuri mara baada ya kupatiwa matibabu ya hali ya juu .Amesema kuwa endapo asingefanyiwa matibabu hayo huenda angepoteza maisha.

”Mimi sijambo nashukuru, Hospitali ni Hospitali isipokuwa wenzetu wapo mbali zaidi, nimefanyiwa mambo mengi sana ambayo kama nisingefanyiwa ningeondoka mapema sana namshukuru Mungu” amesema Majuto.

Mzee Majuto ameongeza kuwa baada ya kumaliza matibabu hayo anataka kutenga muda mwingi kwaajili ya kupumzika zaidi na kuacha kujihusisha na masuala ya sanaa ya uchekeshaji na kudai kuwa Tanzania bado kunawachekeshaji wengi ambao wataweza kuendeleza sanaa hiyo.

Muigizaji huyo wa vichekesho kwasasa amepokelewa na yupo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Mei 4, 2018 Mzee Majuto alisafirishwa kwa gharama za serikali, kwenda nchini India kwa matibabu ya tezi dume baada ya kusumbuliwa na ugonjwa huo kwa kipindi cha muda mrefu.

Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yaongezeka nchini

0
0
Na.WAMJW-Dodoma
Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa kama moyo,figo na mengineyo yanaongezeka kwa kasi duniani kote na hapa nchini yamekua yakigharimu Serikali  kiasi cha shilingi Bilioni 36.6 kwa mwaka.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa jana Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema hapa nchini kwa takwimu za Julai 2013 hadi Juni 2016 magonjwa ya Moyo na Figo ndiyo yalikuwa yakiongoza kwa idadi kubwa ya wagonjwa   kutibiwa nje ya nchi na kugharimu Serikali kiasi hicho cha fedha.

“Kati ya wagonjwa 560 waliosafirishwa na Serikali  wagonjwa 430 walienda kutibiwa moyo na wagonjwa 160 walienda kupandikizwa figo ”alisema Mhe.Ummy.

Aidha, Waziri Ummy alisema kuwa kwa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) magonjwa yasiyoambukiza yanachangia vifo kati ya watu mia moja  watu sitini hufa kwa magonjwa hayo na kati ya wagonjwa 100 watu 47 wanaugua magonjwa yasiyoambukiza

Waziri Ummy aliongeza kuwa kwa kuanzishwa hospitali ya Benjamin Mkapa kutaokoa kiasi kikubwa cha fedha na kuipunguzia Serikali mzigo mkubwa  wa gharama na badala yake fedha hizo zitatumika kuimarisha miundombinu ya hospitali za hapa nchini.

Hata hivyo aliitaka bodi hiyo ya wadhamini kuongeza kasi  ya utekelezaji wa mikakati ya kuboresha huduma za afya ili kuvutia wagonjwa wengi zaidi kutibiwa hospitalini hapo na kupunguza rufaa za wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kwa matibabu.

“Nawaomba mkachape kazi  bila kuchoka ili hospitali hii ikawe na tija katika kuwahudumia watanzania na hata ndugu zetu wa nchi jirani hasa za  Jumuiya ya Afrika Mashariki katika huduma za matibabu ya Kibingwa”,Alisisitiza Waziri Ummy.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Dkt. Alponce Chandika alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa hospitali hiyo ni kutoa huduma za afya maalum za Kibingwa ikiwemo uchunguzi wa magonjwa ya Moyo,Figo,Macho,Damu, Saratani pamoja na kutoa  huduma za upasuaji kwa kutumia matundu madogo(endoscope).

“Mbali na huduma hizo hospitali yetu inatumika kwa ajili ya kufundisha wataalamu wa kada za afya,kufanya tafiti na huduma za kliniki tembezi” alisema Dkt.Chandika.

Dkt.Chandika alisema kuwa wanatarajia mwezi Agosti kufanya tena upandikizaji  wa figo kwa wagonjwa watatu pia wanatarajia kufanya upasuaji wa matundu madogo kuanzia mwezi Julai mwaka huu

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt.Deodatus Mtasiwa alisema kuwa Serikali na wananchi wanatarajia huduma nzuri katika hospitali hiyo hivyo hawanabudi kushirikiana na hospitali mbalimbali zinazotoa huduma za Kibingwa ili kutoa huduma stahili hapa nchini.

Sambamba na uzinduzi wa bodi hiyo yenye wajumbe sita Waziri Ummy  alizindua kitengo cha kuchuja damu katika hospitali ya Benjamin Mkapa.

Shirika la Reli Tanzania laanza kusafirisha mizigo Uganda

0
0
Shirika la Reli Tanzania {TRC} limeanza kusafirisha mizigo kwenda Kampala nchini Uganda ikiwa ni miaka takribani 10 tangu usafiri wa mizigo kwenda Uganda kupitia reli usitishwe.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa .Amesema kuwa Treni hiyo huvuka ziwa Victoria kwa kutumia MV Umoja.

“Shirika la Reli Tanzania {TRC} laanza kusafirisha mizigo kwenda Kampala Uganda ikiwa ni miaka takribani 10 tangu usafiri wa mizigo kwenda Uganda kupitia reli usitishwe. Treni hii huvuka ziwa Victoria kwa kutumia MV Umoja.Hongera Serikali ya Awamu ya Tano,” ameandika Msigwa kupitia ukurasa wake wa Twitter.

 Msigwa ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Katibu Mkuu CCM: Ni Ruksa wabunge wa CCM kuikosoa Serikali

0
0
Katibu mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema ni ruksa kwa wabunge wao kuikosoa Serikali, lakini akatoa angalizo; wasitumie lugha kali, wasizushe wala kutia chumvi mambo wasiyo na uhakika nayo.

Dr Bashiru ameyasema hayo  katika mahojiano a gazeti la Mwananchi.

Alisema mbunge atakayeitetea Serikali ya CCM ambayo imewekwa madarakani na wananchi, pia hatakuwa amefanya kosa.

“(Wabunge wa CCM) Waisimamie Serikali na waikosoe kwa ushahidi na kwa hoja, ama hadharani katika Bunge,” alisema Dk Bashiru.

“Lakini kwa kufuata taratibu za kibunge au ndani ya kamati ya wabunge wa CCM.”

Alisema hiyo ni kwa sababu kamati ya wabunge ina uongozi na taratibu zake na kwamba katika kamati hiyo wabunge hukosoana waziwazi na kuambiana ukweli kuliko hata wanavyofanya hadharani.

“Kwa sababu mbunge wa CCM ana chama chake, ana wapigakura wake, ana haiba yake mwenyewe na msimamo wake na ana Taifa lake, maeneo haya manne anahitaji kuyawekea uwiano,” alisema mhadhiri huyo wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

“Maeneo haya yana masharti. Huwezi ukawa mbunge unaisifu Serikali inayoelekeza mambo ambayo yanaharibu uchumi, huo sio utaifa. Ndio maana hata mwalimu alifikia mahali akasema ‘CCM sio mama yangu. Kama CCM inaweza kuwa na mambo ya ovyo naweza kuachana nayo’.”

Alisema ndio maana kuna wakati Mwalimu Nyerere alimuunga mkono mgombea wa upinzani.

Alisema alifanya hivyo kwa sababu alidhani mgombea aliyeteuliwa na CCM hakuwa anafaa na yule aliyeteuliwa na upinzani alikuwa anafaa.

“Kwa hiyo mwalimu hapo alikuwa hasaliti chama chake, alikuwa anasimamia nchi. Huwezi kukubali mtu wa ovyo ashinde kwa sababu ni CCM. Kazi yetu ndani ya chama ni kuhakikisha tunachuja wagombea wetu ili wale tunaowatoa wawe wanakubalika,” alisema.

“Na (wabunge wa CCM) wakishashinda, wanakwenda kujiwakilisha wao wenyewe kwa nafsi zao kama Watanzania, kukiwakilisha chama, wapigakura ambao ni wana CCM na wasio wanaCCM na nchi yao,” alisema Dk Bashiru.

Hata hivyo, Bashiru alisema kwa bahati mbaya wabunge wa pande zote mbili wameshindwa kuweka uwiano wa maeneo hayo.

“Wengine ukiwasikiliza ni porojo zao. Wamedandia hoja fulani lakini wengine ukiwasikiliza wameegemea kwenye chama zaidi. Lakini msimamo ule una madhara kwa wapiga kura wake ambao wengine si wanachama wa chama chochote,” alisema.

Alisema ukisikiliza wabunge wengine, unaona hawana mtazamo wa kitaifa na wanakuwa wanavuta sehemu moja.

“Kwa hiyo ni kazi ya kuelimishana na tunafanya hivyo kwenye vikao na kwenye kamati kuhakikisha kuwa wabunge wanatoa michango yao kwa nguvu zao zote, vipaji vyao vyote, kusimamia maslahi ya nchi yao, maslahi ya chama wapiga kura wao na taifa,” alisema.

Dk Bashiru alisema wakipatikana wabunge wa aina hiyo, wanaoangalia maslahi ya kila upande bila kujali wanatoka kambi gani, Tanzania itakuwa na Bunge imara la kuisimamia Serikali.

Kuhusu kuingiliwa uhuru kwa wabunge wa CCM wanapochangia mijadala, Dk Bashiru alisema wamekubaliana na uongozi wao na wanafanya mpango katika Baraza la Wawakilishi kuhakikisha kuwa sekretarieti ya chama inafuatilia mwenendo wa utendaji wa wabunge wa chama hicho katika vikao vya maamuzi.

Alisema mbunge anayelalamika kuminywa kwa uhuru wake akihisi kamati ya uongozi wa chama hicho imemnyima uhuru wa kuzungumza katika chombo cha maamuzi, aende kumueleza.

“Juzijuzi nimezungumza naye vizuri (mmoja wa wabunge wa CCM) na tutakuja kukutana naye. Ni kijana ambaye ana mawazo ya kujenga na ana misimamo lakini tukubaliane kuwa si kila unachokiamini lazima kikubalike katika mjadala,” alisema Bashiru na kuongeza.

“Kama mtu mvumilivu lazima ifike mahali ujue kuwa mawazo yatakayotawala maamuzi, ama yanaweza kuwa sehemu ya mawazo yako au yakatofautiana na mawazo yako. Kwa hiyo sitarajii kabisa vyombo hivi vikawa na mawazo yanayofanana.”

Alisema iwapo kuna taratibu ambazo zinawanyima nafasi ya kuzungumza wabunge wa CCM, utaratibu huo hautaruhusiwa.

“Tunahitaji kamati za wabunge ziwe imara ziwe na mazingira huru ya kukijenga chama ndani ya Bunge sio kuwaingilia wabunge uhuru wao, lakini ukishakuwa mwanachama ukubali umeugawa uhuru wako,” alisema.

“Ni suala la kugawagawa tu. Ni sawa na ndoa, unagawa kidogokidogo. Kama nilivyosema ni makundi manne hapo. Ni kweli uhuru wa wabunge umegawanyika na hakuna Bunge duniani ambako utakuta ubunge wao uko kamili na ukikuta hivyo, hilo halitakuwa Bunge bali ni kundi fulani,” alisema.

Alisema Bunge ni lazima litakuwa na utaratibu ambao unamnyang’anya uhuru mbunge lakini uhuru huo lazima uwe na maslahi kwa Taifa au kwa wapigakura, mbunge mwenyewe au chama.

“Labda kama (mbunge) anasema chama kimechukua kipande kikubwa kuliko vingine, hilo linajadilika. Mimi ningetaka chama kiweke utaratibu wa kuwapa uhuru wabunge kutumia vyombo hivyo kama kamati za Bunge na kamati ya wabunge wa CCM kuwa vyombo vya majadiliano na mashauriano,” alisema.

Hata hivyo, alisema majadiliano yawe ni ya kukosoana lakini wasitumie lugha kali, wasizushe mambo, wasiweke chumvi kwa jambo ambalo si la kweli na waibue mambo mapya ya maslahi ya wananchi.

Dk Bashiru pia alisema si kila kitu kinachozungumzwa kina maslahi na wananchi na kwamba Afrika haijafikia kiwango cha Bunge linazungumza masuala ya wananchi wakati wote.

“Sauti ya wananchi haiwezi kusikika kwenye Bunge la kitaifa tu,” alisema.

“Tungeimarisha vyombo vya vijiji na kuheshimu maamuzi ya vyombo vya serikali za kijiji na wilaya, matatizo mengi yangesemwa na kutatuliwa na vyombo hivyo. Wabunge wasisahau tunapoimarisha nguvu ya Bunge lazima tuimarishe vyombo vingine vya maamuzi vya chini.”

Alisema demokrasia ya kweli katika nchi masikini kama ya Tanzania ni kuwa vyombo imara vya maamuzi vya chini ambako ni karibu na wananchi.

“Nenda kule vijijini ni mikutano mingapi ya vijiji inafanyika? Hakuna anayeratibu na anayejali lakini ipo kikatiba. Akishachaguliwa, anasubiri uchaguzi mwingine hakuna anayejali. Tunataka wabunge wetu wasibebe demokrasia ya kibunge pekee kama ndio demokrasia pekee.”

Pia alisema demokrasia katika ngazi ya vijiji inatakiwa ipate nguvu kwa kuwa ndiko matatizo makubwa.

“Nani anaratibu maoni kwenye mikutano inayofanyika chini ya miti vijijimi na ni nani anasikiliza?” alihoji.

Alisema CCM inataka kuona vyombo vyote vya maamuzi vinapata nguvu na sauti zake zisikilizwe, lakini bahati mbaya Bunge ndilo linaonekana ndio chombo pekee cha uwakilishi.

Alisema asilimia 70 ya serikali za vijiji na asilimia 65 za serikali za mitaa na halmashauri zipo chini ya CCM na ndivyo atakavyoshughulika nazo.

Credit: Mwananchi

LHRC yalia na katiba mpya, Bisimba afunguka

0
0
Timu maalumu ya wataalamu iliyoundwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kufuatilia mkwamo wa mchakato wa Katiba Mpya imependekeza njia tatu za kupatikana kwa Katiba Mpya.

Njia zilizopendekezwa ni Mosi, kuendelea na mchakato kuanzia pale ulipoishia, kwa wananchi kupigia kura Katiba Inayopendekezwa.

Pili, kuundwa kwa timu ya wataalamu watakaoandaa rasimu nyingine ya Katiba ambayo itapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya Ndiyo au Hapana.

Tatu, ni kujenga mwafaka wa kitaifa ili makundi yatakayoingia kwenye Bunge Maalumu la Katiba yawe na dhamira moja ya kuandaa katiba bora kwa maslahi ya Taifa.

Akizungumzia mkwamo wa mchakato wa Katiba mpya jana Ijumaa Juni 22, 2018 kiongozi wa timu hiyo, mhadhiri wa sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Dk James Jesse alisema mchakako wa Katiba Mpya ulisababishwa na kukosekana kwa mwafaka wa kitaifa.

Alisema makundi mbalimbali yalikuwa na malengo tofauti katika katiba, jambo lililosababisha wapinzani kususia mchakato huo na kufanya Bunge liwe la upande mmoja.

Alibainisha sababu nyingine kuwa ni uchaguzi wa mwaka 2015 ulisababisha kusimama kwa mchakato huo.

Alibainisha kuwa Serikali na vyama vya siasa vilielekeza nguvu zao kwenye uchaguzi huo na kuacha Katiba.

"Mwafaka wa kitaifa unaonekana ungekuwa suluhisho na kupatikana kwa Katiba lakini haukuwepo ndiyo maana tunaikumbusha Serikali kuhuisha mchakato huo," alisema.

Dk Jesse amlibainisha sababu nyingine ya mkwamo huo ni Serikali ya Awamu ya Tano kusisitiza kwamba Katiba Mpya si kipaumbele chake bali maendeleo ya Taifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema Katiba Mpya ni moja kati ya ajenda tatu za kituo hicho na wataendelea kuhamasisha kupatikana kwake.

Alisema kuna mambo mengi ya muhimu yameondolewa kwenye Katiba Inayopendekezwa kama vile mgawanyo wa madaraka, ukomo wa ubunge na tunu za Taifa.

"Tuendelee na mchakato wa katiba Mpya, haijalishi tutaanzia wapi lakini tunataka iwe na mambo muhimu ambayo yaliondolewa kwenye rasimu ya pili ya katiba kama vile tunu za taifa, ukomo wa ubunge, usawa wa kijinsia na mgawanyo wa madaraka," alisema Dk Kijo-Bisimba.

Bomu Lalipuka Waziri mkuu mpya wa Ethiopia akihutubia

0
0
Mlipuko mkubwa umetokea katika mkutano wa waziri mkuu mpya wa Ethiopia, Abiy Ahmed.Inaarifiwa kwamba watu 83 wamejeruhiwa huku 6 wakiwa katika hali mahututi.

Kiongozi huyo ameondolewa eneo hilo haraka na kwa muda mfupi baada ya kutoa hotuba yake katika mkutano alioandaliwa kuiunga mkono serikali yake.

Maelfu walikuwa wamekusanyika katika bustani kuu ya Meskel mjini Addis Ababa.

Abiy amelitaja shambulio hilo kama "Jaribio ambalo halikufanikiwa la vikosi visivyotaka kuiona Ethiopia imeungana".

Vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa na wamepelekwa katika kituo cha afya kilicho karibu na bustani hiyo kupokea matibabu.

Abiy aliichukua nafasi ya waziri mkuu Ethiopia baada ya kiongozi aliyekuwepo Hailemariam Desalegn aliopjiuzulu ghafla mnamo Februari

Yeye ni kiongozi wa kwanza kutoka jamii ya Wa Oromo ambayo imekuwa ikiandamana dhidi ya serikali kwa takriban miaka mitatu ambapo mamia ya watu walifariki.

Inaaminika Abiy anaungwa mkono pakubwa miongoni mwa vijana wa Oromo pamoja na makabila mengine.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 42 alizaliwa katika mji wa Agaro huko Oromia na anatoka katika familia iliyochanganyika waislamu na wakristo.

Trump asema Korea kaskazini bado ni 'tishio kubwa'

0
0
Rais wa Marekani Donald Trump ameidhinisha upya vikwazo dhidi ya Korea kaskazini akitaja taifa hilo kuwa 'tishio lisilo la kawaida' kutokana na silaha zake za nyuklia - siku 10 tu baada ya kutamka kwamba hakuna hatari yoyote kutoka kwa Pyongyang.

"Hakuna tena tishio kutoka Korea kaskazini," alituma ujumbe mnamo Juni 13, siku moja baada ya kukutana na kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un huko Singapore.

Hatua hiyo imekuja wakati Marekani na Korea kusini zimefutilia mbali mazoezi mawili ya pamoja ya kijeshi.Wizara ya ulinzi Marekani Pentagon imesema lengo ni kuunga mkono majadiliano ya kidiplomasia.

Marekani imekuwa na 'hali ya dharura kitaifa' iliyoidhinishwa kuhusiana na Korea kaskazini tangu 2008.

Tangu hapo marais wamekuwa wakiidhinisha hali hiyo kuendelea mtawalia na vikwazo dhidi ya Pyongyang.

Rais Trump aliendeleza hali hiyo ya dharura jana Ijumaa kutokana na 'uwepo wa hatari ya kuongezeka kwa silaha katika rasi ya Korea na hatua na sera za serikali ya Korea kaskazini'.
 
Haya "yanaendelea kuzusha tishio lisilo la kawaida kwa usalama wa kitaifa, sera ya nchi za nje na uchumi wa Marekani", alisema katika taarifa kwa bunge.

Wanachama wa Democratic wanasema tamko la sasa kutoka ikulu ya White House linakwenda kinyume na majigambo ya awali ya rais Trump kuhusu ufanisi wa mkutano wa Singapore.
 
Katika mkutano huo wa kihistoria kati ya rais wa sasa wa Marekani na kiongozi wa Korea kaskazini Viongozi hao walisaini taarifa ambapo Marekani iliahidi usalama kwa Korea kaskazini na mwenzake akaahidi "kushughulika kusitisha mipango ya nyuklia katika rasi ya Korea" - pasi kufafanua maana ya ndani ya makubaliano hayo.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amesema kuwa vikwazo dhidi ya Korea kaskazini vitasalia wakati majadiliano yanaendelea kuhusu silaha zake za nyuklia.

Hatahivyo, vyombo vya habari Korea kaskazini vimeripoti kuwa Trump alikubali 'kuondosha vikwazo' wakati uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ukiendelea.

Credit:BBC

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 24

Mexico Yaitandika Korea Kusini 2-1

0
0
Mchezo wa kundi F katika michuano ya Kombe la Dunia Urusi, umemalizika kwa Korea Kusini kufungwa mabao 2-1 na Mexico.

Mabao ya mchezo huo yaliwekwa kimiani na Carlos Vela dakika ya 26 kwa njia ya penati pamoja na Xavier Hernandez kwenye dakika ya 66.

Bao pekee la Korea liliwekwa kimiani na Song Heung mnamo dakika ya 90 zikiwa zimeongezwa tatu mpira kumalizika.

Waziri Mkuu: Mitandao Isitumike Kukwamisha Shughuli Za Serikali

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza mifumo ya utoaji huduma Serikali kwa njia ya mitandao isitumike kukwamisha shughuli za Serikali au mipango ya utoaji huduma kwa wananchi.

Amesema watakaobainika kuhujumu mifumo hiyo wachukuliwe hatua za kinidhamu na amesisitiza kwamba Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli haitawavumilia watumishi wasio waadilifu.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Jumamosi, Juni 23, 2018) mara baada ya kuzindua mifumo tisa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwenye kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, jijini Dodoma.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka 2018 iliyotolewa na Umoja wa Afrika (AU) ni  “Mapambano dhidi ya Rushwa kwa kushirikisha wadau na kujenga uongozi bora ili kufikia Malengo ya Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na Malengo ya Maendeleo Endelevu”.

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa Watumishi wa Umma wote nchini, wananchi, Sekta Binafsi, Sekta ya Umma, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Kisiasa na Wadau mbalimbali,  kuunga mkono jitihada za Serikali katika mapambano dhidi ya rushwa.

“Hii ni sehemu ya kutekeleza kwa vitendo Malengo ya Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika (AU) na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya 2030 ya Umoja wa Mataifa  ambayo yamehimizwa na Kaulimbiu ya mwaka huu,”.

Pia Waziri Mkuu amewaagiza Watendaji  Wakuu wa Taasisi zinazosimamia mifumo hiyo pamoja na maafisa  waliopewa dhamana ya kuwahudumia wananchi kupitia mifumo hiyo, wahakikisha wanailinda na kuitumia vema ili iweze kuwa na tija na manufaa yaliyokusudiwa.

Mifumo hiyo aliyoizundua inahusu utoaji Huduma Serikalini ambayo ni Mfumo wa Usajili wa Vizazi  na Vifo, Mfumo wa Taarifa za Kitabibu, Mfumo wa Taarifa za Ununuzi, Mfumo wa Kumbukumbu za Kielektroniki na Mfumo wa Ofisi Mtandao.

Mingine ni Mfumo wa Ankara Pepe na Ulipaji wa Serikali, Mfumo wa Utoaji Huduma za Serikali Kupitia Simu za Mikononi, Mfumo wa Barua Pepe wa Serikali na Mfumo wa Vibali vya Kusafiri.

Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali la kutumia mifumo ya TEHAMA ni kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika utendaji kazi wa shughuli za Serikali za kila siku.

“Hivyo basi, mtakubaliana nami kuwa, Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika kutengeneza mifumo ya TEHAMA ili kutekeleza kwa vitendo azma ya kuwapatia wananchi hususani wa vijijini huduma bora na kwa wakati,” amesema.

Kwa upande wa wananchi,Waziri Mkuu amewataka  waendelee kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imejipambanua kwa vitendo pamoja na kuwa na dhamira ya dhati ya kutoa huduma bora kwa wananchi wake.

Uzinduzi huo umehudhuliwa na waziri wa nchi, ofisi ya raisi menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Bw. George Mkuchika, waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji Charles Mwijage, naibu waziri Ujenzi, Uchukuzi na mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye, na naibu waziri wa nchi OR-TAMISEMI Josephat Kakunda, wabunge, muwakilishi wa benki ya dunia, makatibu wakuu, watendaji na viongozi wa taasisi za umma.

Tunisia Maumivu Tena....Ni Baada ya Kupewa Kichapo cha Mbwa Koko na Ubelgiji

0
0
Tunisia imepokea msiba mwingine katika michuano ya Kombe la Dunia baada ya kukumbana na kipigo cha mbwa koko cha mabao 5-2 kutoka kwa Ubelgiji.

Katika mchezo huo wa Kundi G uliopigwa Uwanja wa Spartak, Ubelgiji wamejipatia mabao yao kupitia kwa Romelu Lukaku aliyefunga mawili.

Mabao mengine ya Ubelgiji yaliwekwa kimiani na Eden Hazard aliyefunga mawili pia moja likiwa la penati, pamoja na Michy Batshuayi katika dakika ya 90.

Mabao ya Tunisia yaliwekwa kimiani na Dylan Bronn katika dakika ya 18 ya kipindi cha kwanza na Khaziri dakika ya 90+3.

Msimamo wa kundi hilo unaonesha Ubelgiji ipo kileleni ikiwa na alama 6 kisha ikifuatiwa na England yenye 3 huku Panama na Tunisia zikiwa hazijapata alama yoyote.

Ujerumani waendeleza ubabe....Ni Baada ya Kuitandika Sweden 2-1

0
0
Mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia timu ya taifa ya Ujerumani, imefufua matumaini ya kusonga mbele baada ya kushinda kwa mabao 2-1 dhidi ya timu ya taifa ya Sweden ambayo haijawahi kuwafunga kwa miaka 40.
 
Ujerumani sasa wameamka kuonekana kutaka kulinda ubingwa wao waliochukua mwaka 2014 nchini Brazil baada ya mechi ya kwanza kupoteza dhidi ya Mexico.

Ujerumani wapo kwenye hatari ya kufuata nyayo za Mabingwa wa 2010 nchi ya Hispania ambao waliondolewa hatua ya makundi nchini Brazil mwaka 2014. Ufaransa pia nao waliondolewa hatua ya makundi mwaka 2002 baada ya kushinda mwaka 1998.

Sweden ambayo ilitangulia kwa bao la mapema ilishindwa kulinda bao lake ambalo lingefuta rekodi  yao ya kutoifunga Ujerumani tangu walipoifunga 3-1 mwaka 1978. Bao la Sweden lilifungwa na Ole Ola Toivonen dakika ya 32 na marco Reus kusawazisha dakika ya 48 na Toni Kroos kuongeza dakika ya 90.

Baada ya mwaka 1978 timu hizo zimekutana mara 12 ambapo Ujerumani imeshinda mara 6 na kutoka sare mara 6.  Katika Kundi F sasa Ujerumani ina alama 3, Sweden 3 na Mexico 6 huku Korea ya Kusini wakiwa hawana alama.

Diamond anusurika katika ajali nchini Marekani

0
0
Msanii wa Bongo Flava, Diamond Platnumz amenusurika katika ajali ya gari nchini Marekani ambapo yupo kwa ajili ya tour ya albamu yake ‘A Boy From Tandale’

Muimbaji huyo amepata ajali hiyo wakati akitokea kwenye show. Kupitia mtandao wa Instagram ameandika;

"Dah Tumepata ajali na kunusurika kufa usiku wa leo wakati tunatoka kwenye show….ila Mwenyez Mungu ametupa nafasi nyingine tena ya kuishi na kuendelea kushikana mkono na vijana wenzangu mtaani kwa pamoja tuziokoe familia zetu duni🙏🏻…."

Diamond ndiye mwanzilishi na mmiliki wa label ya WCB ambayo inasimamia wasanii kama Harmonize, Rayvanny, Rich Mavoko, Queen Darleen, Lava Lava na Mbosso.

Godbless Lema Aguswa Na Hali za Vigogo wa Escrow Wanaosota Mahabusu

0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekiri kuwaone huruma watuhumiwa wa makosa ya uhujumu uchumi, wafanyabiashara Harbinder Seth  pamoja na James Rugemalila kwa kuitaka serikali ikamilishe upelelezi kwani watu hao wanapitia mateso kwa kukaa mahabusu.

Lema ameonyesha kuguswa na watu hao baada ya picha zao kusambaa siku ya Jumatano hii walipokuwa wamekwenda kusikiliza kesi yao huku upande wa mashtaka wakidai kuwa bado upelelezi haujakamilika.

"Ninaona huruma juu yenu. Serikali kamilisheni upelelezi juu ya watu hawa kama wanastahili adhabu walipe walichopanda, kuwa mahabusu bila kesi yako kusikilizwa ni mateso kuliko mnavyoweza kufikiri".

Ameongeza Pengine wanastahili adhabu lakini ni vyema Mahakama ifanye maamuzi.

Seth na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu, kughushi na kutoa nyaraka za kughushi.

Pia, wanadaiwa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Dola 22 milioni za Marekani na Sh309.46 bilioni
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images