Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bunge laiweka kitimoto serikali....Ni Baada ya Maofisa Wake Kukaguia Samaki Wakiwa Jikoni

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeitaka serikali kutoa maelezo ya kina kuhusu watumishi wa Wizara ya Uvuvi na Mifugo kuvamia Mgahawa wa Bunge na kisha kuwapima samaki waliokuwa wakiuzwa, kitu ambacho kinadaiwa haikuwa sahihi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson baada ya wabunge kuomba muongozo wa kiti ili suala hilo lijadiliwe bungeni.

Akiomba muongozo wa spika, mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba kwa kutumia kanuni ya 47  alitaka bunge lisimamishe shughuli zake ili kujadili jambo hilo.

Serukamba alisema kuwa maofisa uvuvi walivamia Mgahawa wa Bunge bila kutoa taarifa kwa Katibu wa Bunge, Spika wa Bunge wala Naibu Spika wa Bunge.

Aidha, maofisa hao waliingia jikoni bila kufuata utaratibu wowote na kuvaa vifaa mikononi na kuanza kupekua chakula ambacho tayari kilishapikwa, jambo ambalo linatishia usalama wa wabunge.

Hata hivyo, kutokana na hoja hiyo Naibu Spika wa Buge Dkt. Tulia Ackson alikuabaliana na hoja ya mbunge huyo na kuitaka serikali leo itoe majibu ya swala hilo.

WCB: "Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu.....Kwa Kuwa Walitukataa na Sisi Tunawakataa"

$
0
0
Wasanii wa  kundi la  WCB wamezungumza kuhusu baadhi ya vyombo vya habari kutopiga nyimbo za wasanii wao.

Miongoni mwa mameneja wa WCB, Babu Tale  katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam  jana alisema kwa vile vyombo hivyo viliwakataa mwanzo na sasa waendelee hivyo hivyo.

‘Tunaendelea kuwaomba waendelee kushinikiza wafanyakazi wao wasipige nyimbo zetu..

“Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu kwa sababu wao walitukataa mwanzo, tunawakataa kwa sababu wao walitukataa,” alisema Babu Tale kwa msisitizo.

Hapo awali Diamond Platnumz alisema siku zote katika tasnia mbalimbali michezo ya kubaniana ipo ila hawezi kulaumu.

Diamond  alisema kufuatia hatua hiyo iliyochukuliwa na vyombo hivyo  iliwapa nguvu timu nzima ya Wasafi kufanya kazi kwa bidii ili waweze kuwasaidia wasanii wengine ambao wanakutana na changamoto hiyo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Irene Uwoya Awatolea Uvivu Wanaomponda Kwa Mavazi Aliyovaa

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya na mke halali wa mwanamuziki Dogo Janja amewatolea uvivu mashabiki zake kwenye mtandaoo wa kijamii kuwa sio wa kwanza yeye kuvaa nguo za ufukweni hivyo wasimpangie chakufanya kwa madai vazi hilo mume wake amelipenda nasio vinginevyo.

Uwoya ametoa kauli hiyo asubuhi ya leo kupitia mtandao wake wa kijamii baada ya kupita siku moja tokea alipo-post picha aliyokuwa amevalia vazi jeupe lililokuwa linaonesha maumbile yake ya mwili na kusababisha mashabiki zake kumtolea maneno makali kuwa haheshimu ndoa yake wala mume wake kwa kuwa anachokifanya sasa hakipendezi na wadhfa wake aliokuwa nao.

"Ukivaa nguo kawaida ana kigodoro, nikim-post mume oonh mdogo na nisipo post kwanini hum-post mara humpendi. Nikivaa nguo za ufukweni nipo uchi mke wa mtu, sasa nasema hivi kwa wale iliyowauma poleni sana siku nyingine ntawashirikisha nikitaka ku-post. Hivi kwani mimi ni wa kwanza bongo kuvaa hivi maeneo ya ufukweni. Mume wangu kaipenda balaah yani", ameandika Uwoya.

Kwa tamaduni za kiafrika na kitanzania mara zote watu wanaamini endapo mwanamke atakapokuwa ameolewa basi kuna mavazi huwa anaepuka kuyavaa hata kama akiwa kwenye fukwe za bahari na hicho ndicho mashabiki zake walichokiamini lakini kwa bahati mbaya leo wamekutana na jambo la utofauti.

Kupima samaki kwamponza Waziri....Spika Ndugai Adai Hiyo ni Dharau Kubwa

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameliomba radhi Bunge na wabunge kwa kile kilichotokea jana Juni 19, 2018 kwa maofisa wa wizara yake kuingia bungeni bila ridhaa.

Akitoa taarifa ya Serikali bungeni leo Juni 20 kuhusu kilichotokea jana, Mpina amesema sehemu ya utekelezaji wa shughuli za wizara ikiwamo operesheni sangara ambayo jana ilitendeka bungeni, itaendelea lakini kwa bahati mbaya utekelezaji huo haukuzingatia tararibu za Bunge.

Amesema Juni 19 akiwa katika mgawaha wa Bunge aliona samaki wa sato akahisi wapo chini ya sentimita 25.

“Nikamuagiza katibu wangu, kwamba wakaguzi wakajiridhishe na samaki hao na wakaguzi walimuhoji muuzaji mgahawa ambaye alikiri ni wachanga walikuwa chini ya sentimita 25,” amesema.

Ameongeza: “Napenda kukiri kwamba watumishi katika kutekeleza kazi hiyo waliingia bila kibali, kupima chakula kilichopikwa na kwa taratibu hizo, wizara inaliomba radhi Bunge lako tukufu na wewe mwenyewe.”

Mara baada ya kauli hiyo, Spika Job Ndugai amesema anamshukuru Mpina kwa maelezo yake lakini akaongeza kuwa, kilichofanywa na maofisa hao ni dharau ya juu.

“Tumshukuru waziri kwa maelezo aliyoyatoa, lakini kwa waziri mkuu tunasikitishwa sana na kilichotokea, sisi si Bunge pekee duniani, sisi ni jumuiya ya kimataifa, wenzetu wakisikia kuna waziri na maofisa walichofanya ni dharau ya juu sana,”amesema.

Amesema linapotokea kosa la jinai katika eneo la Bunge, kamanda wa polisi ana wajibu wa kumjuluisha Spika kwani Bunge halilindi Spika.

 “Wapimaji wa wizara wanapima samaki mikono haina hata gloves, mikono wazi, wanashika shika, si wao peke yao, wamealika na waandishi wa habari, yaani ni kama mpango fulani wa kuliweka Bunge kusipostahili, kwa hiyo aaaaaaaa, kwa kawaida naomba tukubaliane nami, ukiwa umekasirika sana unapaswa kusamehe,”amesema.

Hata hivyo, baada ya kauli hiyo Bunge lilikaa kimya ghafla na wabunge kadhaa wa CCM na upinzani wakasimama kuomba mwongozo lakini hawakupewa fursa hiyo.

SUGU: Nitawaburuza BASATA Mahakamani

$
0
0
Mwanamuziki Joseph Mbilinyi maarufu Sugu ambaye ametoka jela hivi karibuni amelieleza Bunge leo Jumatano Juni 20, 2018 kwamba atatumia mawakili sita kulifungulia mashtaka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kupinga kufungiwa wimbo wake wa #219.

Akizungumza katika mjadala wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 bungeni leo Juni 20,  2018, Mbilinyi amesema kila taasisi imegeuka kuwa polisi ikiwemo Basata walioufungia wimbo huo uliovuja, kabla ya kuutoa rasmi.

Amebainisha kuwa Basata limetoa taarifa ya kuufungia wimbo huo wakati hawajui gharama alizotumia kuutengeneza.

“Wimbo umevuja wao  wanatoa statement (taarifa) ya kuufungia. Hawajawahi hata kuingia studio,  hawajui hata gharama. Wanataka wote tuimbe nyimbo za mapenzi,” amehoji.

Wakati akieleza hayo, Sugu alikatishwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Juliana Shonza na kubainisha kuwa anachozungumza mbunge huyo wa Mbeya Mjini si sahihi.

“Wimbo unavuja vipi wakati uko kwenye mitandao. Hata mashairi yake ninayo hapa. Nyie wenyewe mlisema Basata wanafungia nyimbo bila taarifa,”amesema.

Amesema utaratibu unataka mtunzi kupeleka mashairi ya wimbo wake Basata kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuutoa katika redio, televisheni, mitandao ya kijamii na maeneo mengine.

Akijibu taarifa hiyo, Sugu amesema hawezi kumjibu naibu waziri huyo kwa sababu ni mdogo wake lakini anachofahamu ni kwamba yeye si  kama kama wanamuziki wengine  waliofungiwa nyimbo zao na baraza hilo.

“Sitampinga mheshimiwa Spika. Lakini  mimi sio kama Roma. Naiburuza mahakamani Basata  wimbo umevuja mimi sijautoa bado. Nina mawakili sita nitawaburuza mahakamani ndio watakoma,”amesema.

Taarifa ya Basata inasema imefikia hatua hiyo kwa kuwa una maneno ya uchochezi na kuhatarisha amani na utangamano miongoni mwa jamii.

Mbali na kuufungia Basata pia imetoa onyo kwa msanii huyo kuutangaza na kuusambaza kwa watu wengine.

Katika wimbo huo wenye beti tatu, mbunge huyo anazungumzia harakati zake za kisiasa zilizosababisha afungwe gerezani akiwa mfungwa namba 219.

“Muziki sikuuchagua, bali ulinichagua, nikafanya kweli na dunia ikanijua, nilichofanya kwa hili gemu mnakijua. Mbeya ndiyo inanitesa (wanaitaka Mbeya), najua Mbeya ndiyo inanitesa. Lakini bado napenda Mbeya inavyonitesa,” inasema sehemu ya kibao hicho.

Msukuma Ampa MAKAVU Waziri Sakata la Kupima Samaki 'jikoni'

$
0
0
Mbunge wa Geita (CCM), Joseph Kasheku Musukuma amemtaka Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhanga Mpina kujitafakari na kung’atuka kufuatia maofisa wa wizara hiyo kuingia bungeni bila ridhaa katika mgahawa wa Bunge na kupima samaki wanaodaiwa kuvuliwa haramu.

Musukuma ametoa kauli hiyo leo Jumatano Juni 20, 2018 bungeni mjini Dodoma katika mjadala wa bajeti ya Serikali mwaka 2018/19.

“Nilikamatwa na samaki katika basi langu, tukaombwa rula…, waziri ajitafakari,” amesema Musukuma na kuongeza;

“Wizara hii  tumekuwa na mawaziri watano madaktari lakini leo tumeleta mgambo sijui shule ya aina gani? ni vizuri tukakaguliwa vyeti, mtu ana elimu ya kuunga uunga, yeye amekiri sijui hajui kwamba anakosea.

"Huu urais utakuja kututokea puani hasa sisi wasukuma, tumeamua kunyamaza na kumwachia Mungu apambane nae.”

Akitoa taarifa ya Serikali bungeni leo kuhusu kilichotokea jana, Mpina amesema ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za wizara ikiwamo operesheni sangara ambayo jana ilitendeka bungeni, itaendelea lakini kwa bahati mbaya utekelezaji huo haukuzingatia tararibu za Bunge.

Amesema Juni 19 akiwa katika mgawaha wa Bunge aliona samaki wa sato akahisi wapo chini ya sentimita 25 na kuagiza wachunguzwe.

Mbunge BWEGE Kuitisha Maandamano Makubwa Ya Wakulima wa Korosho

$
0
0
Mbunge wa Kilwa Kusini (CUF) Selemani Bungara maarufu kama Bwege amesema endapo Serikali haitatoa asilimia 65 ya mauzo ya korosho nje ya nchi kwa wakulima wa mikoa ya Kusini hadi Juni 30 mwaka huu wakulima na wabunge wataandamana.

Akichangia bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 bungeni leo juni 20 2018, Bungara amemuomba Spika wa Bunge Job Ndugai kuyapokea maandamano hayo.

Amesema yeye akiwa mwenyekiti wa wabunge wa mkoa wa Lindi wamekuwa wakikaa pamoja na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuzungumzia mambo yanayowahusu na ndio maana hivi sasa mambo ndani ya mkoa huo yanakwenda vizuri.

“Hii ni kwa sababu tuko wabunge wanne wa upinzani na nyie mko wanne, ngoma droo. Lakini kuna njama ya makusudi inayofanywa na Serikali ya CCM ya kuturudisha nyuma kwa makusudi na sisi hatukubali,”amesema.

Amesema kuwa wanapata ushuru wa huduma kutoka katika miradi ya gesi lakini Waziri wa Fedha na Mpango, Dk Philip Mpango anataka kupeleka mabadiliko ya sheria ili kuwanyang’anya ili mikoa hiyo ya Kusini irudi nyuma kiuchumi.

Amesema kuna suala la fedha za korosho ambazo Serikali inatakiwa kurudisha asilimia 65 ya mauzo ya korosho nje ya nchi na kwamba mwaka wa fedha 2017/18 walikuwa wanatakiwa kuwarudishia wakulima hao Sh 81 bilioni lakini hadi leo haijafanya hivyo.

“Mheshimiwa Spika ikifika Juni 30 kama hela haijatoka uje (Ndugai) upokee maandamano yetu maana Serikali ya CCM inafanya kazi kama patasi ambayo haifanyi kazi mpaka igongwe. Wabunge wa mkoa wa Lindi tutaandamana hadi asubuhi ili mtoe fedha zetu,”amesema.

Amesema endapo Serikali haitatoa fedha hizo hadi kufikia muda huo varangati kama lililokuwa wakati wa miradi ya gesi inaanzishwa litaanza upya katika mikoa hiyo.

“Wabunge wa mikoa ya Kusini tuungane tupambane huyu Mpango (Dk Mpango) ana matatizo sana,”amesema.

Ameshauri bajeti iongozewe katika mifugo, kilimo na maji na kwamba kama wakiongeza bajeti katika maeneo hayo kwa mara ya kwanza ataiunga mkono bajeti hiyo.

Amesema anajua kuwa wataongeza mishahara na fedha za kilimo mwaka 2019 ikiwa ni mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu ili wachaguliwe katika nafasi zao.

“Mwaka 2019 ndio mtaongeza bajeti kwa wakulima na mishahara kwa wafanyakazi ili wawapigie. Nyie wajanja mnatuua mwishoni. Miaka mitano mnawaacha wapate tabu,”amesema.

Jeshi La Polisi Shinyanga Linachunguza Mauwaji Ya Wanaume Wawili.

$
0
0
Na, magdalena kashindye
Jeshi la polisi mkoani shinyanga linafanya uchunguzi wa vifo vya kutatanisha vya wanaume wawili vilivyotokea Ngogwa wilayani kahama mkoani humo.

Taarifa ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari iliyotolewa juni 20 /2018 na kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga ACP Saimon H. Haule  miili ya wanaume wawili ambao hawajafahamika majina yao, kabila na mkazi wanaokadiliwa kuwa na umri wa miaka 25_30 ilikutwa katika eneo la soko la Ngogwa wilayani kahama juni 19 /2018 saa 3:00 asubuhi .

Haule alisema mwili wa mwanaume mmoja ulikutwa na jeraha kichwani linaloashiria alikatwa na kitu chenye ncha kali huku mtu wapili akiwa hana jeraha wala mchubuko.

"Tunaendelea kufanya uchunguzi wa vifo vya wanaume wawili vyenye utata   vilivyo bainika juni 19/2018 huko Ngogwa kahama ili kibaini chanzo cha vifo hivyo "alisema Haule.

ACP Haule alisema miili ya marehemu imehifadhiwa katika  chumba cha kuhifadhia maiti  hospital ya halmashauri ya mji wa kahama kwa utambuzi na ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na Jeshi hilo kuwabaini waharifa wa tukio hilo.

Waziri Lukuvi atengua uteuzi wa Mkurugenzi NHC

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ametengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemia Mchechu.

Kupitia Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Dorothy Mwanyika imesema kuwa kwa mamlaka aliyonayo waziri Lukuvi chini ya kifungu cha 18(1) cha sheria ya Shirika la Nyumba la taifa amesitisha uteuzi huo kuanzia leo Juni 20, 2018.

“Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kwa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 18(I) cha sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa ya mwaka 1990 pamoja na marekebisho yake mwaka 2005, ametengua uteuzi wa mkurugenzi wa shirika hilo”, imesema Taarifa.

Awali katika taarifa iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi Disemba 16, 2017 ilimtaka mkurugenzi huyo kusimama majukumu yake ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabiri za utendaji mbovu.

Rais Shein Afanya Uteuzi Wa Mwenyekiti Wa Tume Ya Uchaguzi Ya Zanzibar

Rais Magufuli ateua msajili wa vyama vya siasa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amemteua Bw. Mohammed Ali Ahmed kuwa Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Bw. Mohammed Ali Ahmed umeanza leo tarehe 20 Juni, 2018.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Mohammed Ali Ahmed alikuwa mwanasheria na mtafiti katika Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar.

Bw. Mohammed Ali Ahmed amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Rajab Baraka Juma ambaye amestaafu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya June 21

Uruguay Yaichapa Saudi Arabia bao 1-0 Na Kutinga 16 Bora Kombe La Dunia

$
0
0
Bao pekee katika mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay dhidi ya Saudi Arabia, limehitimisha safari ya michuano hiyo kwa Misri inayoongozwa na Mohamed Salah.
 
Uruguay imeshinda kwa bao 1-0 dhidi ya Saudi Arabia, shujaa akiwa ni Luis Suarez aliyewahi kuichezea Liverpool akiwa shujaa wa klabu hiyo, wakati huo.

Salah na Misri watapanda ndege kurejea nyumbani baada ya mechi yao ya mwisho ya kundi ikiwa ni ya kukamilisha.

Ushindi wa jana umeipa Uruguay pointi sita na kujihakikishia kusonga hatua ya mtoano pamoja na wenyeji Urusi huku Misri na Saudi Arabia, wakitupwa nyumbani.

Diego Costa aipaisha Hispania.....Ni Baada ya Kuichapa bao 1-0 Iran

$
0
0
Hispania imefikisha pointi 4 baada ya ushindi wake wa kwanza wa bao 1-0 dhidi ya Iran jana na sasa inasubiri mechi yake ya mwisho dhidi ya Morocco.

Diego Costa ndiye aliyefunga bao pekee akigongeshewa mpira na beki wa Iran aliyekuwa akijaribu kuokoa.

Pointi 4 za Hispania zinawafanya kuwa na pointi sawa na Ureno na Iran inabaki kuwa na pointi zake 3.

Maana yake, kuvuka katika kundi timu tatu za Ureno, Hispania na Iran zina nafasi wakati Morocco tayari imefungashiwa virago.

Mechi za mwisho Ureno itakipiga na Iran huku Hispania ikicheza na Morocco ambayo tayari imeshaaga michuano hiyo. 

Iran ndio ipo kwenye wakati mgumu kwani inahitaji kushinda dhidi ya Ureno huku Ureno na Hispania zikihitaji ushindi au sare tu ili ziweze kutinga 16 bora.

Shamsa Ford Amkingia Kifua Irene Uwoya Baada Ya Picha Yake Ya Nusu Uchi Kusambaa

$
0
0
Muigizaji wa Bongo movie Shamsa Ford ameibuka na kumkingia kifua Msanii mwenzake Irene Uwoya baada ya picha yake ya utata kusambaa mtandaoni.

Siku ya jana Irene Uwoya alitengeneza headlines baada ya kuweka picha kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha maungo yake nje ndani ya nguo ya kuogelea.

Watu walimjia juu Uwoya baada ya picha ile kusambaa ingawa mwenyewe alijitetea kuwa alikuwa yuko Beach na lile ni vazi la kuogelea hivyo haoni tatizo.

Shamsa amemtetea Uwoya na kuweka wazi kuwa haoni kama kuna kosa yeye kuvaaa vile hasa ukiangalia alikua mazingira ya baharini hivyo kuvaa vazi la baharini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Shamsa aliandika ujumbe huu:

"Picture zako zote nzuri mama umependeza sana, mimi nachojua mtu unavaa kutokana na location unayoenda, sasa sidhani kama Ir.Kuna wengine wanavaa en anaweza akavaa hivi halafu akaenda ofisini. Sasa mtu yupo beach mlitaka avae dira.

"Mumewe amemsifia amependeza sasa nyie wapembeni mnasema amekosea mnajisumbua, kila mtu atahukumiwa kwa matendo yake binafsi na Mungu. Tusiishi kwa kuhukumiana maana wa peponi hawajulikani.

"Hadi dira beach lakini matendo yake ukiyashuhudia unaweza ukatoa mbio. Tatizo lako wewe dada Iren ni hilo umbo ndo limewakosesha amani watu.Ungekuwa na flatscreen maneno yasingewatoka hebu kafanye operation upunguze Gushepu“.

Zitto Kabwe Ajitosa Kuwapigania Wakulima wa Korosho Kwa Kupinga Marekebisho ya Sheria Mpya ya Zao Hilo

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amesema chama hicho kitashirikikiana na wabunge wa vyama vya upinzani kupinga marekebisho ya Sheria ya Sekta ya Korosho namba 203.

Jana Jumatano Juni 20, 2018, Zitto ametoa taarifa katika mitandao mbalimbali ya kijamii akipinga mabadiliko hayo, kutaka wananchi kukataa kile alichokiita dhuluma kwa wakulima wa korosho.

Zitto ametoa kauli hiyo wakati Serikali ikikusudia kuifanyia marekebisho sheria hiyo.

Kwa mujibu wa muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2018, inapendekezwa kufutwa mgawo wa fedha zinazotokana na ushuru wa kusafirisha korosho nje zilizokuwa zikitolewa kwa wakulima ili kuboresha zao hilo.

Badala yake, muswada unapendekeza fedha hizo kupelekwa mfuko mkuu wa Hazina kama fedha nyingine za Serikali.

Sheria ya sasa inataka asilimia 65 ya fedha zinazotokana na ushuru wa kusafirisha korosho nje kupelekwa kwa wakulima kupitia Bodi ya Korosho (CBT).

"Sisi ACT Wazalendo, kwa kushirikiana na wabunge wote wa upinzani, pamoja na wale wa CCM watakaokuwa tayari kuwatetea, tutajitahidi sana kuhakikisha mapendekezo haya hayapiti,” amesema Zitto katika taarifa yake hiyo, akiwaeleza wananchi kuhusu mabadiliko hayo.

"Lakini Kuna haja kubwa ya wananchi, wakulima wa korosho, hasa wa mikoa ya kusini, kupaza sauti kukataa. Tusikubali.”

Amesema katika marekebisho hayo Serikali inapendekeza kufuta mgao wa fedha zinazotokana na ushuru wa kusafirisha korosho nje, “katika mgao wa sasa wa fedha hizo Serikali huchukua asilimia35 ya fedha, na asilimia 65 inayobakia hupelekwa kwenye mfuko wa kuendeleza zao la korosho nchini.”

“Fedha hizo kuingizwa mfuko mkuu wa Hazina kama fedha nyingine za Serikali, na hivyo kutumika kwa asilimia 100 kwa mambo mengine na sio kwaajili ya kuendeleza zao la korosho.”

Amedai  Serikali imegoma kutoa asilimia 65 ya uendelezaji korosho na imeshazitumia fedha za Korosho Sh211bilioni  kinyume cha sheria ya sasa.

“Wameamua sasa kufuta hiyo sheria ya korosho kabisa ili wasibugudhiwe. Tutapambana bungeni kupinga dhuluma hii dhidi yenu, ikishindikana tutarudi kwenu,” amesema.

Nape Kuungana na Zito Kabwe Kupinga Sheria Mpya ya Korosho

$
0
0
Serikali inakusudia kuifanyia marekebisho Sheria ya Sekta ya Korosho namba 203.

Kwa mujibu wa muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2018, inapendekezwa kufutwa mgawo wa fedha zinazotokana na ushuru wa kusafirisha korosho nje zilizokuwa zikitolewa kwa wakulima ili kuboresha zao hilo.

Badala yake, muswada unapendekeza fedha hizo kupelekwa mfuko mkuu wa Hazina kama fedha nyingine za Serikali.

Sheria ya sasa inataka asilimia 65 ya fedha zinazotokana na ushuru wa kusafirisha korosho nje kupelekwa kwa wakulima kupitia Bodi ya Korosho (CBT).

Fedha hizo zilikuwa zikitumika kuendeleza kilimo cha korosho kama vile kuendesha Chuo cha Utafiti Naliendele, kufanya utafiti wa mbegu bora na kuzuia magonjwa ya mnyauko.

Muswada unapendekeza kifungu cha 17A kibadilishwe kwa kufuta kifungu kidogo cha (2) na kuingizwa kipengele kipya. 

Kifungu kipya kinachopendekezwa kinasomeka, “Mapato yote yatokanayo na ushuru wa kusafirisha korosho yatahifadhiwa katika mfuko mkuu.”

Hivi karibuni wabunge waliibana Serikali wakitaka kujua ziliko fedha zinazotokana na mapato ya ushuru wa usafirishaji wa korosho nje.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia alitaka majibu ya Serikali, akisema ripoti zinaonyesha fedha hizo zilizokusudiwa kuendeleza kilimo cha korosho zimetumika katika matumizi mengine.

“Kukubali mapendekezo haya ya mabadiliko ya sheria hii ni kuhujumu juhudi za miaka mingi za kufufua zao la korosho, ni kuwatoa kafara wakulima wa korosho nchini na kuhujumu mapato ya Serikali kwani korosho ndiyo zao lililofanya vizuri msimu uliopita. Nitayapinga," amesema Nape katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images