Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Maneno ya Rais Magufuli akimtakia Heri ya siku ya kuzaliwa TB Joshua

$
0
0
Rais John Magufuli jana  alimtumia salamu za heri ya siku ya kuzaliwa, mchungaji maarufu wa Nigeria, TB Joshua, aliyefikisha miaka 55.
 
Rais Magufuli alituma salamu hizo kwenye ukurasa wake wa twitter,  Juni 12 akisema:

“Kwa niaba ya familia yangu, ninatuma salamu zangu za dhati katika siku yako ya kuzaliwa unapotimiza miaka 55. Mungu aendeelee kukupa uongozi mkubwa ili uweze kuleta ukombozi kwa watu wengi na kueneza harufu yake katika mataifa yote.” Heri ya siku ya kuzaliwa.”


Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

Wanunuzi Wa Pamba Waishukuru Serikali

$
0
0
WANUNUZI wa zao la pamba wameishukuru Serikari kwa kuweka mfumo mzuri wa ununuzi wa zao hilo, ambalo kwa mwaka huu linauzwa kupitia katika minada inayosimamiwa na Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS).

Hata hivyo wanunuzi hao wameiomba Serikali kuziwezesha AMCOS kuwa na maghala makubwa na ya kisasa ya kuhifadhia pamba, lengo likiwa ni kuhakikisha pamba inahifadhiwa kwenye maeneo salama na kuifanya isipoteze ubora.

Kauli hiyo imetolewa jana (Jumanne, Juni 12, 2018) na mmoja wa wanunuzi hao ambaye ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya NGS Investment LTD, Bw. Emmanuel Dandu alipokuwa akizungumzia kuhusu kuanza kwa uchambuaji wa pamba kwa msimu wa mwaka huu.

Alisema awali kabla pamba haijaanza kuuzwa kupitia AMCOS suala la ubora lilikuwa halizingatiwi sana na wakulima kwani  pamba yake ikikataliwa na kampuni moja alikuwa na uhuru wa kuipeleka kwenye kampuni nyingine na, jambo ambalo lilichangia kuisha thamani.

Hata hivyo ameiomba Serikali kuwajengea uwezo viongozi wa Ushirika ili waweze kutekeleza majuku yao kikamilifu na pia isaidie kutoa elimu kwa wanachama juu ya umuhimu na faida za AMCOS ili wakulima wengi waweze kujiunga.

Bw. Dandu ambaye kampuni yao ya NGS Investment LTD, licha ya kujishughulisha na biashara nyingine, pia inamiliki kiwanda cha kuchambua pamba cha Majahida kilichopo wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, ambayo tayari imeshaanza zoezi ya uchambuaji pamba.

Alisema pamba inayochambuliwa katika kiwanda hicho wanainunua kupitia AMCOS walizopangiwa, ambapo alipongeza mfumo huo kwa sababu unawawezesha kupata malighafi kwa urahisi na kwa wakati.

“Wanunuzi wote tunanunua pamba kupitia AMCOS. Serikali imeweka mfumo mzuri unaotuweza wote kununua pamba kadiri ya uwezo wetu. AMCOS zimeagizwa kuuza pamba kwa wanunuzi wote bila ya ubaguzi, tofauti na miaka ya nyuma” alisema.

Akizungumzia kuhusu uwezo wa kiwanda hicho, alisema kina uwezo wa kuchambua tani 40,000 za pamba kwa mwaka, lakini wanalazimika kuchambua wastani wa tani tano  hadi 12 kutokana na changamoto ya upatikanaji wa pamba ya kutosha pamoja na changamoto ya umeme wa uhakika.

Pia aliiomba Serikali iwasaidie wakulima kwa kuwapatia pembejeo kwa wakati pamoja na kuwapa elimu ya mara kwa mara juu ya kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo cha zao la pamba, ikiwa ni pamoja na kupanda kwa wakati ili waweze kujiongezea tija.

Alisema kwa sasa kiwanda hicho kina jumla ya wafanyakazi 300, ambao kati yao 62 ni wa waajiriwa wa kudumu na waliosalia ni vibarua.

Bw. Dandu alisema marobota yanayotengenezwa kiwandani hapo yanakuwa na uzito wa kilo 200 hadi 220, huku wateja wao wakubwa ni Cotton Distributors Inc (CDI) ya nchini Uswisi, Saurashtra Cotton and Agro Product PVT LTD ya nchini India.

Wengine ni Awatac Impex PTE LTD ya nchini Singapore pamoja na viwanda vya nguo vya ndani ya nchi kikiwemo cha Mwatex cha jijini Mwanza. Alisema matarajio ya kampuni hiyo ni kuanzisha kiwanda cha kutengeza nyuzi ili kuongezea thamani ya pamba kabla ya kuiuza.

Aidha, Meneja huyo alisema mbegu zinazopatikana baada ya pamba hiyo kuchambuliwa pamba zinapelekwa moja kwa moja katika kiwanda cha kukamua mafuta ya kula na mashudu huuzwa kama chakula ya mifugo.

Kuhusu mabaki yanayopatikana baada ya mafuta kuchujwa, alisema yanatumia kwa kutengeneza sabuni za kufulia, ambazo wanaziuza kwa wananchi.

 -MWISHO-

MamboSasa: Dr Shika Hana Hela Yoyote, Ni Muongo

$
0
0
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa Dk. Shika anacheza na akili za watu na hana fedha yoyote aliyopeleka benki kama alivyodai.

Akizungumza na Redio Times Fm, leo Juni 13, 2018 amesema kuwa kwa mara ya mwisho alisema fedha zimeingia benki lakini hana fedha.

Kauli hiyo imekuja baada ya kuulizwa kuwa kuna taarifa kuwa Dk. Shika amepata fedha zake, hizi taarifa zikoje mmempa ulinzi wa kutosha wakati wa kupokea?

“Dk. Shika anaendelea kucheza na akili za watu , hana fedha amepata lini yule mzee wa madau anapiga dau kubwa lakini kwa madhumuni yake binafsi, kwa mara ya mwisho alisema fedha zimeingia benki, benki gani hamna chochote , hana fedha,” amesema Kamanda Mambosasa.

Umaarufu wa Dkt. Shika umekuja baada ya kujitokeza katika mnada wa kuuza nyumba za Lugumi ambapo Dk. Shika aliahidi kununua nyumba hizo kwa thamani ya Sh. bilioni 2.3 lakini alishindwa kulipia asilimia 25 ya fedha hizo ambazo ni shilingi milioni 800.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/  0658920640
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Waziri Nchemba: Ni Kosa Polisi Kumkamata Mtu Mwingine kwa Kosa la Mwingine

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema si sawa Jeshi la Polisi kumchukulia hatua mtu ambaye si mkosaji kwa kosa la mtu mwingine.

Dkt. Mwigulu amesema hayo bungeni leo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Devotha Minja lililohoji kumekuwa na tabia ya jeshi la polisi, wanapokwenda kumkamata mtu, wakimkosa wanamkamata mbadala, mke au mme, je jeshi la polisi wanatoa wapi mamlaka haya kwa kumkamata mtu na kumtesa?

Akijibu swali hilo, Waziri Mwigulu amesema Jeshi la polisi linafanya kazi kwa mujibu wa sheria, hakuna mtu anayeruhusiwa kuadhibiwa kwa mbadala.

“Kosa linabaki kwa muhusika na kama kuna mtu anaweza kusaidia afanye hivyo lakini si kuchukua adhabu kwa mtu mwingine”, amesema Mwigulu.

Mwenyekiti PAC akalia kuti kavu sakata la BoT

$
0
0
Mwenyekiti  wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka ameingia matatani baada ya kutoa majibu ya madai ya kuwepo kwa tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa vyombo vya habari kabla ya Spika.

Akijibu mwogozo ulioombwa na Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga (CCM), Mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga amesema kitendo cha Mwenyekiti huyo wa PAC kuzungumza na vyombo vya habari kabla ya Spika Job Ndugai ni kinyume cha taratibu za Bunge.

Alisema suala la Mwenyekiti wa PAC kukiuka utaratibu litashughulikiwa na Spika Ndugai ambaye ndiye aliyeiagiza Kamati hiyo kufuatilia suala la tuhuma za BoT.

Kaboyoka ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki (Chadema), alinukuliwa na vyombo vya habari akieleza kile walichokibaini baada ya kuwahoji Bodi, Menejimenti ya BoT na Mlinga ambaye ndiye aliyetoa hoja hiyo bungeni wakati wa kuchangia Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Maofisa wa BoT akiwemo Gavana, Profesa Florens Luoga, walifikishwa mbele ya kamati hiyo baada ya Mlinga, kudai wametumia Sh bilioni 12 kwa matibabu ya watumishi wa benki hiyo nje ya nchi.

Mlinga alidai BoT ndiyo taasisi ya serikali inayotumia fedha nyingi kugharamia matibabu ya watumishi wake huku ukitumia kampuni binafsi ya bima badala ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

"Mpaka mtu kwenda kutibiwa nje kuna utaratibu na kuwe kuna haja ya kwenda kutibiwa nje. Hivi ninavyoongea watumishi wa BoT ndio taasisi inayotumia fedha nyingi katika matibabu bila msingi wowote.

" Mfanyakazi akiwa na mafua anakwenda kutibiwa India wanatumia fedha nyingi na wamesahau kuwa fedha hizi ni za walipa kodi.

Alisema taasisi za serikali zimewekewa utaratibu kwa ajili ya kupata matibabu kwa kutumia NHIF, lakini BoT wao wanatumia kampuni binafsi kwa gharama kubwa.

Alisema gharama ambayo wanatumia kwa ajili ya matibabu ambayo kama wangeitumia NHIF wangetumia Sh bilioni moja lakini wanatumia Sh bilioni 12 kwa mwaka kupitia kampuni binafsi ya bima na kuongeza kuwa huo ni ufisadi na wahusika wanafanya hivyo kwa maslahi binafsi.

"Wanasema NHIF haina matibabu ya nje kwa sababu wao ni taasisi nyeti lakini Usalama wa Taifa, Bunge, Takukuru, wako NHIF, Mke wa Rais aliugua na alilazwa Muhimbili lakini hata wabunge tumepima tezi dume kwenye zahati ya Bunge."

Baada ya hoja hiyo, Ndugai aliiagiza PAC inayoongozwa na Kaboyoka kufuatilia suala hilo kwa kuanza kukutana na Mlinga, NHIF, kisha kuiita Bodi na Menejimeti ya BoT na kumfikishia taarifa Jumatatu ya Juni 11, mwaka huu.

Baada ya kamati hiyo kufanya mahojiano na wahusika, Kaboyoka alinukuliwa na vyombo vya habari akizungumzia suala hilo na kudai kuwa tuhuma dhidi ya BoT hazina ukweli wowote kabla ya ripoti kuifikishwa kwa spika, kitendo kilichodaiwa na Mlinga kuwa ni kinyume cha kanuni za Bunge.

Hali hiyo ilimfanya mbunge huyo jana, baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu bungeni, kuomba muongozo kwa Mwenyekiti wa Bunge, Giga.

"Mheshimiwa Mwenyekiti kamati zetu zinapoagizwa na Spika zifanye kazi, zinatakiwa zipeleke ripoti kwa Spika ndipo aitolee ufafanuzi.

"Mwishoni mwa wiki nilizungumza kuhusu BoT kutumia fedha nyingi kwa ajili ya matibabu kuliko taasisi nyingine za serikali ambazo zinafanya kazi ngumu. Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya PAC ikakaa na mimi, NHIF na BoT, taarifa nilizokuwa nazo hadi sasa Spika hajalitolea majibu suala hilo." Mlinga aliongeza:

"Lakini jana (juzi) nimeona kwenye taarifa ya habari Mwenyekiti wa Kamati ya PAC akitoa taarifa za kamati ambayo ni siri mpaka Spika atakapotolea majibu, akisema taarifa kuhusu BoT kutumia fedha nyingi kwenye matibabu si za kweli.

"Mheshimiwa Spika naomba kupatiwa utaratibu kama na mimi naweza kulizungumzia suala hilo kwenye vyombo vya habari, kwani hata mimi nilizongwa zongwa na vyombo vya habari, lakini niliheshimu kanuni," alisisitiza Mlinga.

Baada ya kuomba muongozo huo, Mwenyekiti Giga alisema suala hilo ni kinyume cha kanuni na Spika atalishughulikia. "Na wewe Mlinga usizungumze na vyombo vya habari kwani ukifanya hivyo, utakuwa umekiuka kanuni za Bunge."

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 Kusomwa Kesho Bungeni

$
0
0
Bajeti  Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 ambayo ni ya tatu kwa Serikali ya Rais John Magufuli, itasomwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kesho Alhamisi.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema "Juni 16 Waziri wa Fedha na Mipango atasoma Bajeti Kuu ya serikali. Baada ya hotuba hiyo ya Waziri wa Fedha tumewaandalia futari wageni wote waalikwa. Siku hiyo tutakuwa na wageni wengi wa serikali."

Ndugai alisisitiza kwamba wabunge wote wawepo siku hiyo, wakati bajeti itakaposomwa.

Alisema anajua bado kuna hati hati, kuwa huenda sikukuu ya Idd itakuwa Ijumaa, lakini jambo muhimu wabunge wawepo siku ya Alhamisi kwenye hotuba ya bajeti na kisha kwenye futari pamoja na wageni waalikwa.

Alieleza kuwa baada ya hotuba hiyo, kusomwa bungeni ndipo wabunge wanaweza kwenda kuungana na familia na ndugu zao, kusherehekea sikukuu hiyo kubwa, inayoashiria kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Akiwasilisha Mapendekezo ya Serikali ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2018/19 kwa wabunge Machi 13, mwaka huu mjini Dodoma, Dk Mpango alieleza kuwa katika bajeti hiyo Serikali inatarajia kukusanya na kutumia Sh trilioni 32.476, ikiwa ni ongezeko la Sh bilioni 764 ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2017/18.

Mpango alitaja vipaumbele vya bajeti hiyo kuwa ni mradi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Stiegler’s Gorge katika Mto Rufiji kitakachozalisha megawati 2,100, ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na Morogoro hadi Makutupora kilometa 336 na uboreshaji wa Shirika na Ndege Tanzania (TTCL).

Pia, ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga, uzalishaji wa makaa ya mawe na umeme Mchuchuma na Liganga, uendeshaji wa shamba la miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari Mkulazi mkoani Morogoro na uboreshaji wa bandari za Tanga, Dar es Salaam na Mtwara.

Bilioni 22.5 zatengwa kwaajili ya matumizi ya uzazi wa mpango

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019 imepanga kutumia shilingi 22.5 kwaajili ya matumizi ya uzazi wa mpango.

Akizungumza leo, Juni 13, 2018 Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Wizara hiyo, Ummy Mwalimu amesema kutoka katika vyanzo vya ndani kiwango hiki ni sawa na ongezeko la asilimia 60 kutoka mwaka 2017/2018.

“Kwa mwaka wa fedha 2018/2019 serikali imepanga kutumia jumla ya shilingi Bilioni 22.5 kwaajili ya uzazi wa mpango kutoka katika vyanzo vya ndani kiwango hiki ni cha fedha sawa na ongezeko la asilimia 60 kutoka mwaka 2017/2018,” amesema Ummy.

Hayo yameelezwa baada ya Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi kuihoji serikali kuwa “Mahitaji halisi ya fedha kwaajili ya uzazi wa mpango kwa mwaka kwasasa ni zaidi ya Sh. Bilioni 36 , Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha zaidi ili kufikia kiasi kinachohitajika kwaajili ya wakina mama na watoto?”

Wema Sepetu Kuanza Kujitetea June 19

$
0
0
Muigizaji wa filamu Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili wanaokabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wataanza kujitetea Juni 19, 2018.

Wema na wenzake walipaswa kuanza kujitetea leo Juni 13 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kwa upande wa mawakili ni Costantine Kakula wa Serikali na Wakili wa Utetezi Albert Msando.

Hata hivyo ilishindikana washtakiwa hao kuanza kujitetea kwa sababu Hakimu Simba alikuwa na kazi nyingine na kesi imeahirishwa hadi Juni 19, 2018 ambapo washtakiwa wataanza kujitetea.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Hakimu Simba kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi watano wa upande wa mashtaka waliokuwa wakiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula na kutoa uamuzi uliowaona washtakiwa hao wana kesi ya kujibu na hivyo wanapaswa kujitetea.

Mbali na Wema washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa na Matrida Seleman Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Kamishna Mkuu Wa TRA Awashukuru Wafanyabiashara Jijini Dodoma

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere amewashukuru wafanyabiashara jijini Dodoma kwa mchango wao wa kulipa kodi na kuiwezesha Serikali kutekeleza wajibu wake wa kukuza uchumi na kutoa huduma mbalimbali za jamii hapa nchini.

Akizungumza wakati akifuturisha wafanyabiashara na wafanyakazi wa TRA katika ukumbi wa LAPF jijini hapa, Kichere alisifia uhusiano mzuri uliopo kati ya wafanyabiashara hao na ofisi ya TRA Mkoa wa Dodoma.

"Nachukua nafasi hii kuwashukuru wafanyabiashara wa Dodoma kwa kuwa walipakodi wazuri na kuonyesha ushirikiano wa hali ya juu na ofisi yetu ya TRA hapa mkoani Dodoma ambapo kutokana na uhusiano huu uliopo, tunapata urahisi wa kutekeleza jukumu letu la kukusanya mapato ya Serikali kwa manufaa ya watanzania wote," alisema Kichere.

Kichere amewaahidi wafanyabiashara hao kuwa, TRA itaendelea kudumisha ushirikiano huo na kukaribisha mazungumzo ya pamoja na viongozi wa TRA mkoani hapa ili kufikia muafaka wa masuala mbalimbali yanayohusu kodi badala ya kulalamika mitaani bila kupata suluhisho.

Aidha, Kamishna Mkuu Kichere amewahimiza wafanyabiashara hao kuendelea kulipa kodi mbalimbali kwa wakati kwani kodi hizo hutumika katika kujenga uchumi wa nchi na kutoa huduma mbalimbali za jamii ikiwa ni pamoja na huduma za afya, maji safi na salama, elimu, kulipa mishahara ya watumishi wa Umma, miundombinu ya barabara na umeme.

"Nachukua fursa hii kutoa rai kwenu wafanyabiashara kuendelea kulipa kodi zote kwa wakati ikiwa ni pamoja na Kodi ya Majengo na  Kodi ya Mapato awamu ya pili ambapo mwisho wa kulipa kodi hizi ni tarehe 30 Juni, mwaka huu. Kodi nyingine ni Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo hulipwa tarehe 20 ya kila mwezi.  Hivyo, uhiari wenu wa kulipa kodi hizi kwa wakati ndio chachu ya kujenga uchumi wetu na kuharakisha kutoa huduma za jamii kwa watanzania wote", alisema Kichere.

Naye Katibu Mtendaji wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) mkoani Dodoma ambaye pia ni Katibu wa Sekta Binafsi mkoani hapa Idd Senge amesema kwamba, sekta binafsi itaendelea kushirikiana na TRA kwa ajili ya kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wanalipa kodi kwa wakati ili kuepuka faini ambazo zinarudisha nyuma maendeleo ya biashara zao.

"Sisi kama wafanyabiashara wa hapa mkoani Dodoma tutaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania na pale patakapotokea sintofahamu yoyote tutafanya mawasiliano na viongozi wa TRA ili kupata muafaka wa pamoja," alieleza Senge.

Mamlaka ya Mapato Tanzania imejiwekea utaratibu wa kufuturisha wafanyabiashara na wafanyakazi wake kila ifikapo Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa lengo la kumshukuru Mwenyezi Mungu katika shughuli mbalimbali wanazozifanya hususani za ukusanyaji mapato ya Serikali.

Mwisho.

Simbacxhawene Awasilisha Azimio la Kumpongeza Rais Magufuli Kwa Kuiendeleza Dodoma

$
0
0
Mbunge wa Kibakwe (CCM) George Simbachawene amewasilisha azimio la kuitaka Serikali kuharakisha  mchakato wa Muswada wa Sheria ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu na kuuleta bungeni.

Akiwasilisha azimio la kumpongeza Rais John Magufuli  kwa uamuzi wake wa kuendeleza mji wa Dodoma na kuupa hadhi ya jiji, leo Juni 12 bungeni, Simbachawene amesema  ikiwezekana Muswada huo usomwe mara ya kwanza katika mkutano wa 11 unaoendelea.

"Naiomba Serikali kuongeza raslimali fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali itakayoendana na hadhi ya makao makuu na jiji kama vile ujenzi wa Barabara zenye kiwango, miundombinu ya majisafi na majitaka, upimaji na upangaji mzuri wa jiji la Dodoma," amesema.

Simbachawene pia ameliomba Bunge kumpongeza kwa dhati Rais Magufuli na kumuunga mkono kwa uamuzi wake wa kuifanya Dodoma kuwa jiji na hivyo kuliandaa jiji la Dodoma kuendana na hadhi ya Makao Makuu ya Serikali.

Lembeli atangaza kuachana na siasa

$
0
0
Mbunge wa zamani wa Kahama, (CCM) James Lembeli, ametangaza kuachana na siasa akitaja sababu kuu mbili.

Lembeli amesema ameamua kuachana na siasa kwa sababu mashirika na taasisi anayofanya nayo kazi, yamemwambia achague moja kubaki kwenye siasa au kuendelea kushirikiana na taasisi hizo.

Lembeli ameyasema hayo leo Juni 13, nyumbani kwake katika kijiji cha Mseki, kata ya Bulungwa, Ushetu, Kahama .

“Hivyo hizi taasisi zimeniambia nichague moja nibaki kwenye siasa au tupige kazi, nimeamua kuacha siasa,” amesema.

Lembeli ambaye alijiunga na Chadema mwaka 2015, amesema sababu ya pili iliyomfanya aachane na siasa ni matatizo yanayoipata familia yake baada ya kujiunga na chama hicho.

“Hapa kwetu kuna kaburi la Mtemi baba yangu. Siku hizi watu wa CCM hawaji kuomba dua kwenye kaburi hivyo nimeamua nisiwe na chama ili watu waendelee kuomba,” amesema.

Ameongezeka: “Napumzika siasa ila mimi bado mchezaji mzuri naamini kila chama nitakachoenda namba yangu ipo tu.”

Jeshi la Polisi Kuwashughulikia Matapeli Wa Mitandaoni

$
0
0
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa Jeshi la Polisi kushirikiana na TCRA kuna watu wanaotapeli kwa njia ya mtandao wameshawakamata na jambo hilo bado linafanyiwa kazi.

Akizungumza na Redio Times Fm, leo Juni 13, 2018 amesema kuwa jeshi lake litahakikisha linafanya juhudi wananchi hawatapeliwi.

“Utapeli ambao umekithiri ni wa kimtandao, mtu unatumiwa meseji kwamba umeshinda kiasi fulani kwa hivyo unatakiwa kutuma kiasi fulani ili upatiwe kiasi hicho, Wananchi wengi wamelizwa na utapeli huo lakini Polisi sasa hivi tunafanyia kazi,” amesema Kamanda Mambosasa.

“Sisi tuna ushirikiano wa karibu sana na TCRA na mpaka sasa kuna baadhi ya watu wanaotapeli wananchi kwa njia ya mtandao tumeshawakamata na bado tunaendelea na juhudi za kuhakikisha wananchi hawatapeliwi,” ameongeza Mambosasa.

Wabunge Wagawanyika azimio la kumpongeza Rais Magufuli Lililotolewa na Simbachawene

$
0
0
Wabunge wamegawanyika wakati wa kujadili azimio la kumpongeza Rais John Magufuli kwa uamuzi wa kuendeleza mji wa Dodoma na kuupa hadhi ya Jiji.

Azimio hilo limewasilishwa na Mbunge wa Kibakwe (CCM) George Simbachawene leo Juni 13 2018, ambaye katika azimio hilo amewaomba wabunge kuitaka Serikali kukamilisha haraka mchakato wa kuuleta bungeni muswada wa sheria ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu.

Wakichangia azimio hilo wabunge wa upinzani walipinga azimio hilo wakiitaka Serikali kuandaa kwanza mazingira ya miundombinu kabla ya kutangaza kuleta muswada huo wa Sheria.

Akichangia azimio hilo, Mbunge wa Liwale (CUF) Zuberi Kuchauka amehoji Serikali nini kinachotangulia kati ya Sheria na vigezo.

"Hatupingi Dodoma kuwa makao makuu ama jiji. Lakini ni kipi kinatangulia kati ya Sheria na vigezo vya kuwa jiji," amesema.

Mbunge wa Temeke (CUF) Abdallah Mtolea amesema kuwa azimio hilo lilipaswa kutanguliwa na maombi ya fedha kwa ajili ya uboreshaji wa mji wa Dodoma.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mariam Ditopile ameunga mkono azimio hilo na kuahidi kuwa wakazi wa Dodoma watampa ushindi mkubwa Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao.

Hata hivyo, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleiman Jafo amesema Serikali imetenga Sh 35 bilioni kwa jiji la Dodoma ili zitumike katika ujenzi wa miundombinu.

Kwanini Saa Za Automatic Ni Maarufu Tanzania

$
0
0
Kwanini Saa Za Automatic Ni Maarufu Tanzania
saa za automatic ni saa ambazo miaka ya karibuni zimepata umaarufu hasa kwenye mambo ya fashion ya saa hasa za mtindo wa skeleton kama hiyo juu kwenye picha.. saa za automatic ni saa ambazo hazitumii battery zinajichaji zenyewe kila ukitikisa mkono
  • saa hizi zimekuwa maarufu kutoka na sifa zake ambazo ni kama zifuatazo hapo chini
  • HAZITUMII BATTERY
sifa kubwa ya saa hizi hazitumiii battery zenyewe ukivaa ..jinsi unavyotisa mkono ndivyo zinavyozidi kujichaji yaani ukiitisha yenyewe ndo chaji yake inaingia ..hakuna haja ya battery
  • HAZIINGII MAJI
saa hizi haziingii maji 3ATM maana yake ni kwamba saa hizi kwenye maji ya mvua haziwezi kuingia pia maji ya kumwagikiwa bahati mbaya (splash water)
  • ZINAJICHAJI ZENYEWE
Saa hizi zina system za kujichaji zenyewe kupitia gia zake ambapo kuna gia ambayo ukitisa mkono inahifadhi nguvu hizi huitwa gia kuu (main spring) ukiwa na saa hii sahau kununua battery
  • WAPI ZINAPATIKANA NA JINSI YA KUNUNUA
saa hizi zinauzwa na mtandao wa daresalamshop.com ..kwa hawa jamaa ukiagiza utalipa mzigo ukifika majiji yote Tanzania arusha, dar mwanza,tanga,mbeya,moshi ,zanzbar,na iringa bofya link hiii kuagizaa bofya
>>>> skeleton automatic watch for men<<<<< au bofya hapo chini kwenye SHOP NOW kuagiza jaza address yako dereva ataleta cash on delivery

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) yawatumbua vigogo sita

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewafukuza kazi wakurugenzi wake sita kwa tuhuma mbalimbali zinazowakabili ikiwamo uzembe kazini.

Akizungumza leo Juni 13, Mkurugenzi wa HESLB Abdul Razac Badru, amesema miongoni mwa tuhuma hizo ni kufanya uzembe na kuisababishia hasara ya mabilioni ya fedha bodi hiyo.

Badru amesema tuhuma nyngine ni kushindwa kutekeleza majukumu yao ya urejeshaji wa mikopo kwa mujibu wa kanuni na taratibu.

Taarifa za kufukuzwa kazi kwa vigogo hao imesainiwa na Mwenyekiti Profesa William Anangisye na imesomwa mbele ya waandishi wa habari leo na Badru.

Waliofukuzwa kazi ni pamoja na mkurugenzi wa urejeshaji mikopo, Hamid Chagonja, mkurugenzi wa upangaji na ugawaji mikopo, Onesmus Laizer na msaidizi wake, John Elias na mkurugenzi msaidizi urejeshaji mikopo, Robert Kibona.

Bodi hiyo imebainisha kuwa imefikia hatua ya kuwafukuza wakurugenzi hao ambao awali walisimamishwa kazi, baada ya kujiridhisha na taarifa ya kamati iliyopewa jukumu la kuwachunguza.

"Watumishi hao waandamizi walikuwa wanakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwamo uzembe uliokithiri, hivyo kusababisha hasara na upotevu wa fedha za Serikali, "amesema Badru.

Amesema bodi hiyo imemwagiza kuzitaarifu mamlaka nyingine za Serikali kwa hatua za ziada pale zitakapoona inafaa.

Mwanasheria wa bodi hiyo Abdul Mtibora amesema pamoja na uamuzi huo watu hao wana haki ya kukata rufaa Tume ya Utumishi wa Umma ndani ya siku 45, ikiwa wanaona hawakutendewa haki.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Tanzania

Moto Mkubwa Wateketeza Ghala La Kuhifadhia Bidhaa Kariakoo

$
0
0
Jengo la ghorofa mbili lililopo mtaa wa Agrey na Livingstone, Kariakoo limeteketea kwa moto.

Moto huo umeanza leo Juni 13 saa 4 asubuhi na kuteketeza mali zote zilizohifadhiwa kwenye jengo hilo.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara mtaa wa Agrey Deogratius Sanya amesema moto ulianza kidogokidogo kwenye moja ya stoo iliyokuwa juu baada ya kutokea shoti ya umeme na baadae moto huo ukasambaa.

Amesema baada ya saa mbili Jeshi la Zimamoto na uokoaji walifika na magari  yenye maji lakini hayakuwa na uwezo wa kuuzima.

" Magari yalifika lakini hayakuwa na uwezo wa kurusha maji lakini baada ya muda ilifika kampuni binafsi iliyoshirikiana na kikosi cha bandari"amesema Sanya.

Ameongeza kuwa kikosi cha bandari kiliweza kuudhibiti moto huo  usisambae na kuleta madhara zaidi.

Msemaji wa kikosi cha zimamoto na uokoaji Joseph Mwasabeja amesema kikosi cha zimamoto na uokoaji kilifika na kukuta moto umesambaa kwenye jengo zima lakini kutokana na jengo hilo kuwa nauzio maji yalishindwa kupenya kwa urahisi.

"Tumefika na kukuta moto umesambaa tulichofanya nikuanza kubomoa kingo zilizowekwa  kuzunguka jengo ili kuwezesha maji kupenya kirahisi" amesema Mwasabeja.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images