Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Taarifa Muhimu Toka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)


Sakata la KKKT Lamfukuzisha Kazi Msajili wa Jumuiya za Kidini na Vyama vya Kijamii

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk.Mwigulu Nchemba amesimamisha kazi Msajili wa Taasisi za Dini Maryline Komba huku akiwaomba viongozi wa dini kuendelea na shughuli zao za kutoa huduma za kiroho.
 
Waziri Mwigulu ameyasema hayo wizarani hapo wakati alipotangaza kumsimamisha kazi na  kupisha uchunguzi wa kina na iwapo atabainika kutohusika na matamko hayo au nyaraka ambazo zinasambaa mtandaoni basi atarudi kwenye majukumu yake.
 
Wizara yake inaendelea kuchunguza aliyeandika na kusambaza nyaraka katika mitandao ya kijamii ambayo imeibua sintofahamu kwa viongozi wa dini na Watanzania kwa ujumla ili sheria ichukue mkondo wake.
 
“Serikali na viongozi wa dini wamekuwa na ushirikiano mkubwa na hakuna mahali ambapo wanaonekana kutoaminiana.Hivyo aliyesambaza nyaraka hizo tunachunguza na kisha tutachukua hatua zinazostahili,”amesema Dk.Mwigulu.
 
Amesema viongozi wa dini na watanzania kwa ujumla wafahamu kuwa nyaraka na matamko ambayo yamesambazwa kwenye mitandao ya kijamii hazina baraka za Wizara yake wala Serikali na hivyo ni vema zikapuuzwa tu.
 
Amewaomba  viongozi wa dini kupuuza nyaraka  zinasambazwa kwenye mitandao na kusema “Endeleeni na shughuli zenu kama kawaida kwani nchi hii inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria hivyo hakuna sababu ya kuhofu.
 
Amesisitiza kuwa Serikali inaheshimu viongozi wa dini zote huku akionya wanaotaka kutumia dini kama kigezo cha kufanya siasa au kuigawa nchini.
 
“Wale ambao wanataka kutugawa kwa misingi ya kidini ni vema wakaacha kwani haitakuwa na tija kwao wala kwa Taifa letu .Hivyo tusiwe sehemu ya kushabikia mambo yanayohusu dini,”amesema.

Wabunge Kuosha Magari Kuchangia Ujenzi Wa Vyoo Nchini

$
0
0
Wabunge wakiongozwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai wanatarajia kuosha magari ili kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya mfano kwa watoto wa kike na wenye uhitaji maalumu.

Tukio hilo litakalofanyika kesho Jumamosi Juni 9, katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma, limeandaliwa na Spika Ndugai ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Umoja wa Wabunge Wanawake (TWPG), katika kampeni yao ya ujenzi wa vyoo hivyo, litahusisha uoshaji magari ya wabunge na watu mbalimbali.

Hata hivyo, tukio hili ni utangulizi wa harambee iliyoandaliwa na TWPG, itakayofanyika Juni 22 mwaka huu, jijini Dodoma ili kuchangisha fedha za kujenga vyoo vya kisasa katika majimbo yote nchi nzima ili kumkomboa mtoto wa kike apate mahitaji muhimu na kwa utulivu, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli.

Akizungumzia tukio la kesho, Spika Ndugai amewataka watu mbalimbali kujitokeza kuosha magari yao ili kuchangisha fedha za ujenzi wa vyoo hivyo.

“Natoa wito kwa wote wenye magari, wafike pale kwa wingi hata kama una gari lako umelipaki siku nyingi limechafuka sana na vumbi, lilete kazi hiyo ataifanya Spika pamoja na wenzake wote bungeni,” amesema.

Aidha, ametoa wito kwa wakazi wa Dodoma na mikoa jirani wafike kwa wingi uwanjani hapo kuosha magari yao.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Waziri wa Elimu: Serikali Haitavumilia Walimu Wanaoshiriki Vitendo Vya Udhalilishaji Kwa Wanafunzi

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako Ndalichako ameweka wazi kwamba serikali haiwezi kuvumilia vitendo vya udhalilishaji  ambavyo vimeonekana kufanywa na mwalimu wa shule St. Florence iliyopo jijini Dar es salaam.

Waziri Ndalichakoameyasema hayo  wakati akikabidhi zawadi kwa shule na wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha nne na sita jijini Dodoma  baada ya kufanya vizuri kwenye matokeo ya mwisho ya mitihani yao.

Akizungumzia suala hilo Ndalichako amewahakikishia wananchi kuwa mwalimu aliyewafanyia udhalilishaji wanafunzi wa kike wa shule ya Mt. Florence vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi lakini watahakikisha serikali inawamchukulia hatua kali.

Pamoja na hayo Waziri Ndalichako ameshauri walimu wa kike kusafiri na wanafunzi wa jinsia ya kike katika ziara mbalimbali za kishule badala ya wanaume ili kuepukana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kama ilivyowatokea wanafunzi wa shule St. Florence.

Hivi karibuni kuliibuka sintofahamu ndani ya jiji la Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla baada ya kuwepo na taarifa kwamba katika shule ya St. Florence mwalimu mmoja aliyetajwa kwa jina la Ayubu kudaiwa kuwanajisi watoto wanne wa darasa la saba.

Waziri Mkuu Afungua Mkutano Wa Mawaziri Wa Madini Na Kuzindua Maabara Ya Kisasa Ya Madini........Inauwezo wa kutambua aina za madini na yalikotoka

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua maabara ya kisasa ya na ya kwanza barani Afrika yenye uwezo wa kupima na kutambua aina mbalimbali za madini.

Amesema maabara hiyo itasaidia kupunguza migogoro ya umiliki wa madini na kudhibiti utoroshwaji wa madini mbalimbali kati ya nchi moja na nyingine.

Maabara hiyo imefunguliwa leo (Ijumaa, Juni 8, 2018) katika Kituo cha Madini na Jiosayansi  cha Afrika  (AMGC) kilichopo Kunduchi jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema uzinduzi wa maabara hiyo utawezesha wataalamu kutambua aina za madini na nchi yanakotoka, hivyo kuondoa migogoro ya umiliki wake.

“Maabara hii litatuweza kulinda madini yetu na kufanya biashara ya madini vizuri. Pia hii ni fursa nzuri kwa nchi za Afrika kutumia maabara hii kupima madini yao na kubaini yalikotoka,” amesema.

Hata hivyo Waziri Mkuu amewataka viongozi wa kituo hicho kuhakikisha wanaziwesha nchi wanachama kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu masuala ya madini pindi zinapohitaji.

Pia Waziri Mkuu ameishukuru Serikali ya Ujerumani kwa kusaidia katika ununuzi wa vifaa vya maabara hiyo pamoja na kutoa mafunzo kwa wataalamu watakaoiendesha.

Waziri Mkuu, pia ameiomba Serikali hiyo kutoa mafunzo hayo kwa Watanzania wengi zaidi ili kuongeza idadi ya wataalamu wa kuendesha maabara hiyo.

Pia, Waziri Mkuu amefungua Mkutano 38 wa Mawaziri wa Madini kutoka nchi Wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu unaofanyika katika kituo cha AMGC.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini ikiwa ni pamoja na Mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama zilizosheheni wanyama wa aina mbalimbali pamoja na fukwe za bahari.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 9

Waziri Mkuu Ataka Wanaotoa Taarifa Za Uongo Wadhibitiwe

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wawachukulie hatua kali wananchi wote wanaotumia vibaya namba za mawasiliano za jeshi hilo kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu matukio ya majanga ya moto.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameliagiza Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini kuendelea kutoa mafunzo kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na kupambana na majanga ya moto pindi yanapotokea katika maeneo yao.

Pia ameziagiza Halmashauri zote nchini kuwa na magari ya zimamoto pamoja na magari ya kubeba wagonjwa kwenye vituo vyote vya Zimamoto na Uokoaji katika maeneo yao.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Ijumaa, Juni 8, 2018) wakati alipofanya ziara katika Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura ya Maafa pamoja na Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha mkoa wa Ilala.

Amesema ili kudhibiti wananchi wanaopiga simu za kuomba msaada wa kutaka kuokolewa, huku kukiwa hakuna tukio lolote la janga la moto lililotokea kwenye maeneo yao, ni vema watu hao wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,  Thobias Andengenye kumweleza baadhi ya changamoto zinazolikabili jeshi hilo kuwa ni pamoja na wananchi kupiga simu wakidai kuna ajali ya moto imetokea katika maeneo yao na baada watu wa uokoaji kufika wanabaini ni uongo.

Hata hivyo, Waziri Mkuu aziagiza Halmashauri zote nchini kuwa na magari ya zimamoto pamoja na ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya kutoa huduma pindi majanga yanapotokea kwenye maeneo yao ili kuharakisha utoaji wa huduma za dharura.

Pia amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kila Mtanzania aweze kuwa na uelewa wa kutoa huduma za awali pindi majanga ya moto yanapotokea katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kutumia vifaa vya kuzima moto.

Waziri Mkuu ambaye alitembelea kituo cha Jeshi la Zimamoto cha Ilala amejionea magari ya kuzimia moto likiwemo la aina ya Bronto Sky Lift lenye uwezo wa kufika futi 54 na kuzunguka nyuzi 360.

Alielezwa kuwa katika Bara la Afrika, magari ya aina hiyo yapo matatu tu, ambayo yapo nchini Tanzania, Misri na Afrika Kusini. Kwa upande wa Tanzania, gari hilo lilinunuliwa miaka 10 iliyopita kwa sh. bilioni 1.5.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alitembelea Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura ya Maafa, ambapo aliwasisitiza viongozi wa kituo hicho kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara yatokanayo na kuishi kwenye maeneo hatarishi hususan mabondeni.

Waziri Mkuu alisema licha ya kuwapa elimu, pia wanatakiwa kuwashawishi wakazi wa maeneo hayo kuondoka kabla ya kutokea kwa maafa badala ya kusubiri majanga yatokee. Pia aliwataka wawe na mpango wa kuonesha eneo lenye maafa na kuujulisha umma.

Pia aliwataka watendaji wanaohusika na kamati za maafa waimarishe mawasiliano katika ngazi zote kuanzia ya kijiji hadi Taifa na wafanye kazi kwa ushirikiano ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi pindi maafa yanapotokea.

Awali, Waziri Mkuualitembelea Ofisi za Mpiga Chapa wa Serikali jijini Dar es salaam ambapo mbali na mambo mengine alijionea moja kati ya mitambo ya kwanza ya Mpiga  Chapa wa Serikali uitwao  Original Heidelberg wenye zaidi ya miaka 100 ambao bado unafanya kazi vizuri. 

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Yanga Yaiomba TFF Kujitoa Mashindano ya Kagame CUP

$
0
0
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limethibitisha kupokea barua ya Yanga yenye ombi la kujiondoa kwenye mashindano ya Kagame Cup yanayotarajia kuanza Juni 29 mpaka Julai 13 2018.

Kwa mujibu wa Ofisa wa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, amesema wamepokea barua hiyo inayoeleza kuwa Yanga ina nia ya kuwapa mapumziko wachezaji wake.

Barua hiyo iliyowasili katika makao makuu ya TFF, imesema Yanga inahitaji kuwapa muda wa kupumzika wachezaji wake kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga itakuwa ina kibarua kizito kitakachopigwa nchini Kenya dhidi ya mabingwa wa ligi nchini humo kwa msimu wa 2017/18, Gor Mahia FC Julai 18.

Kutokana na muingiliano wa ratiba hiyo ya Kagame na CAF, Yanga wameona ni vema zaidi kuwapa wachezaji wake mapumziko ili kujiandaa kuelekea mechi hiyo ya kimataifa.

Habarika Masaa 24......Pakua Upya Application Yetu Tukuhabarishe Usiku na Mchana

$
0
0
==>Pakua Upya Application yetu tukuhabarishe masaa 24 usiku na mchana.

Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia;

Maalim Seif aanza ziara Ya Siku Mbili Pemba

$
0
0
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad ameanza ziara ya siku mbili kisiwani Pemba leo.

Mkurugenzi wa habari wa chama hicho upande wa Maalim Seif, Salim Abdalla Bimani amesema   leo kuwa ziara hiyo ni ya kawaida kwa kiongozi huyo kila ifikapo mwezi wa Ramadhan.

Amesema ziara hiyo haihusiani na harakati za chama bali ni kuwajulia hali wagonjwa na kuwapa pole wafiwa kama ilivyo kawaida yake.

Katika ziara hiyo ya siku mbili anatarajiwa kutembelea mikoa yote miwili ya kisiwa hicho na kisha kurudi kisiwani Unguja kuendelea na ziara kama hiyo katika maeneo mbali mbali.

Bimani amewataka wananchi wa kisiwani hicho cha Pemba kutoa ushirikiano wao wa kina kwa kiongozi huyo wa chama chao .

Mameneja Masoko Sita Manispaa Ya Ubungo Watumbuliwa KwA Ubadhirifu wa Milioni 293

$
0
0
Kamati ya fedha ya Manispaa Ubungo jijini Dar es Salaam, imemwagiza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuwasimamisha kazi mameneja wa masoko sita na watumishi watatu kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha Sh milioni 293.

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam jana Ijumaa Juni 8, Meya wa Manispaa hiyo, Boniface Jacob, alisema hatua hiyo ni kutoka na ripoti ya Mkaguzi wa Manispaa ya uchunguzi wa ukusanyaji wa mapato katika  masoko 16 ya wilaya hiyo.

Aliwataja wanaotakiwa kusimamishwa na na masoko yao kwenye mabano kuwa ni Obote Etta (Soko la Ndizi Mabibo),  Grayson Sebastian (Simu  2000), Frida Michael (Shekilango), Edwin Mugila (Mabibo) na Bakari Mshanga (Sinza) kwa upande wa watumishi wa Manispaa ni Mweka Hazina, Ofisa Mapato na Msimamizi wa Mfumo.

“Baada kutoridhishwa na taarifa ya mapato yatokanayo na masoko, Mkaguzi wa Manispaa ilibidi akachunguze kilichosababisha makusanyo kushuka hadi milioni 716.

“Ripoti yake imebaini ubadhirifu wa zaidi Sh milioni 293 ambapo mapato halali yanayoonekana kwenye mfumo ni zaidi ya Sh bilioni moja lakini baada ya kuwabana wamerejesha kiasi cha Sh milioni 139,” alisema Jacob.

Rais TFF Aitaka Yanga Ijieleze

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ameutaka uongozi wa klabu ya Yanga kutoa jibu linaloeleweka hadi kabla ya Jumapili juu ya kujitoa kwao kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, (CECAFA KAGAME CUP).

Kauli hiyo ya Karia imekuja kufuatia Yanga kuiandikia barua TFF kuwaarifu kutoshiriki michuano hiyo kutokana na kubanwa na ratiba ya mashindano mengine.

Karia amesema kwamba amelazimika kutoa agizo hilo kutokana na kutoridhishwa na sababu walizozitoa Yanga kwani hata timu nyingine zinazoshiriki michuano hiyo zina ratiba ngumu pia.

“Kabla hata hatujalipeleka suala hili CECAFA, nauomba uongozi wa Yanga hadi kufika jumapili uwe umetoa jibu la kueleweka juu ya mashindano hayo,”amesema Karia.

Aidha karia ameongeza kuwa kweney CECAFA KAGAME CUP kuna timu za Gor Mahia na Simba ambazo pia bado ziko kwenye michuano ya SportsPesa Super Cup hivyo kama kulalamikia ratiba zenyewe zingekuwa za kwanza kufanya hivyo.

Trump atamualika Kim Marekani kama mkutano wao utaleta matunda

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump alisema alhamis kwamba atamualika kiongozi wa Korea kaskazini, Kim Jong Un kuja Marekani kama mkutano ujao wa kihistoria na kiongozi huyo utakuwa na mafanikio. Kwa upande mwingine, alisema yuko tayari kujiondoa kwenye mkutano ikiwa mambo hayatakua sawa.

Rais Trump alikutana kwa saa mbili na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe huko White House siku ya alhamis chini ya wiki moja kabla ya mkutano wake wa kilele na Kim Jong Un huko Singapore.

Mkutano huo na Korea kaskazini pia masuala ya biashara yalizingatiwa zaidi wakati wa majadiliano yao. Abe alitaka uhakikisho kutoka Marekani kwamba hatua zitafanywa kudhibiti mipango ya nyuklia na makombora ya masafa marefu ya Korea kaskazini. Pia alitaka Rais Trump kuzungumza na Kim suala la raia wa Japan waliotekwa nyara na Korea kaskazini wakati wa miaka ya 1970 na 1980.

Kwenye mkutano wa pamoja na waandishi wa habari, baada ya mazungumzo yao, Trump alimuahidi Abe kwamba atalizungumzia suala hilo wakati wa mkutano wake na Kim.

Rais Trump pia alisema yupo wazi kutia saini makubaliano ya Juni 12 na Korea kaskazini kumaliza rasmi vita vya Korea, lakini alitahadharisha kwamba hiyo ni hatua ya kwanza tu. Trump pia aliwaambia waandishi wa habari kwamba angependa kuona hatimaye uhusiano kati ya Marekani na Korea kaskazini unarudishwa tena.

Trump alipongeza ushirikiano kati ya Japan na Korea kusini katika miezi ya hivi karibun uliowezesha mkutano huo na vile vile kumshukuru Rais wa China, Xi Jinping kwa kusaidia katika utaratibu huo.

Mbunge auwawa kwa kupigwa risasi

$
0
0
Mbunge wa manispaa ya Arua, Ibrahim Abiriga ameuawa kwa kupigwa risasi kadhaa na watu wasiojulikana, karibu na nyumbani kwake, Kirinyabigo mtaa wa Kawanda,wilayani Wakiso, karibu na jiji la Kampala.

Mlinzi wake aliyekuwa amevalia sare za kijeshi naye amauawa baada ya gari lao kumiminiwa risasi kadhaa.

Kulingana na walioshuhudia tukio hilo,watu waliokuwa wamefunika nyuso zao, wakitumia usafiri wa pikipiki, wamemimina risasi kwenye gari la Abiriga kabla ya kutoroka.

Mara kadhaa, Abiriga amekuwa akisema kwamba usalama wake umekuwa hatarini. Amekuwa akisema kwamba watu wengi hawana furaha kwamba anamuunga mkonorais Museveni, hasa baada ya mabadiliko ya katiba.

Matamshi yake hata hivyo yamekuwa yakichukuliwa kama mzaha, kwani usemi wake umekuwa na ucheshi mwingi kila mara.

Wakati mmoja, aliwaeleza waandishi wa habari kwamba alikuwa ameamua kujinunulia pistol, kwa sababu anahofia maisha yake

Abiriga amekuwa mmoja wa wabunge wazalendo kwa rais Yoweri Museveni, kiasi cha kuvalia nguo za rangi ya manjano, kuendesha gari la rangi ya manjano na kila kitu chake ni cha rangi ya manjano, ambayo ni rangi ya chama tawala cha NRM, cha raisMuseveni.

Alikuwa miongoni mwa wabunge walioshinikiza mabadiliko ya katiba yaliyotoa fursa kwa rais Yoweri Museveni kuwania tena urais,kwa kuondoa kizuizi cha umri.

Abiriga ambaye alikuwa na umri wa miaka 62 amekuwa mbunge wa chama tawala cha NRM, alikuwa Kapteni katika jeshikabla ya kuingia katika siasa.

Waziri wa habari na mawasiliano Frank Tumwebaze, kupitia kwa mtandao wake wa Twitter, amekitaja kifo cha Abiriga kuwa cha kuumiza moyo huku msemaji wa rais Yoweri Museveni,Don Wanyama akisema kwamba wale ambao wamemuua Abiriga kwa kumwaga damu, nao damu yao itamwagika.

Credit:Voa

Mahakama ya ICC imemuachia huru aliyekuwa Makamu wa Rais wa DRC

$
0
0
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu (ICC) Ijumaa imefuta makosa ya uhalifu wa vita na adhabu ya kifungo cha miaka 18 jela kwa mwanasiasa wa Congo, Jean Pierre Bemba, ikiwa ni pigo kubwa kwa waendesha mashtaka na huenda ikawa na matokeo makubwa kwa siasa za Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Jaji Christine Van den Wijingaert amesema Bemba, ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Congo hawezi kuwajibishwa kwa uhalifu uliotendwa na wanajeshi waliokuwa chini ya udhibiti wake katika nchi jirani ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) mwaka 2002 mpaka 2003.

Kwa kuongezea amesema majaji katika kesi hiyo wameshindwa kuangalia juhudi zake za kusitisha uhalifu uliotendwa na Movement for the Liberation of Congo (MLC) mara tu alipofahamu kuhusu hayo na jinsi ilivyokuwa vigumu kwa yeye kuwadhibiti wanajeshi akiwa mbali nao.

Uhalifu wa MLC
“Bwana Bemba hawezi kuwajibishwa kwa uhalifu ulioendeshwa na wanajeshi wa MLC wakati wa operesheni huko Jamhuri ya Afrika ya Kati,” amesema, alipokuwa akisoma maamuzi ya jopo la majaji watano wa rufaa.

Van den Wijingaert amesema juhudi za Bemba kusitisha uhalifu “zimefuta wajibu wake kikamilifu.”

Kufutiwa makosa kwa Bemba ni pigo kubwa sana kwa waendesha mashaka, ambaye kukutwa na hatia kwake ilikuwa moja ya kesi chache ambazo wameshinda tangu mahakama hiyo iundwe mwaka 2002.

Bemba alikuwa mwanasiasa wa juu kukutwa na hatia na mahakama ya kudumu ya uhalifu wa vita, na kesi imeonekana kuweka mfano kwamba maafisa wa siasa na kijeshi huenda wakawajibika kwa vitendo vya wanajeshi waliokuwa chini ya uongozi wao.

Makamu wa rais
Bemba, makamu rais wa zamani huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, alikutwa nahatia ya mauaji, ubakaji na vitendo vya utekaji nyara vya wanajeshi wa MLC ambao aliwapeleka Jamhuri ya Afrika ya Kati kumsaidia rais wa wakati huo Ange-Felix Pattasse.

Bemba hakutolewa haraka Ijumaa licha ya kufutiwa makosa kwasababu alikutwa na hatia ya kuingilia kati ushahidi, na uamuzi wa mahakama ya rufaa katika kesi bado haijakamilika.

Uhusiano na Mobutu Sese Seko
Bemba, mtoto wa kiume wa mfanyabiashara, alikuwa tajiri kutokana na uhusiano wake na kiongozi wa zamani wa Congo, Mobutu Sese seko. Aliingia katika serikali chini ya utawala wa rais wa sasa Joseph Kabila mwaka 2003 kama seheu ya makubaliano ya kushirikiana madaraka ambayo yalimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Bemba bado ni mtu maarufu magharibi mwa Congo, ambako chama chake cha MLC ni moja ya harakati kubwa sana za upinzani kwa Kabila, ambaye anatarajiwa kuachia madaraka baada ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Desemba.


Credit: Voa

Spika Ndugai Aosha Magari Katika Kuhamasisha Uchangiaji Wa Fedha Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Vyoo

$
0
0
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiosha magari tofauti tofauti wakati wa shughui ya kuosha Magari kwa ajili ya kuchangia fedha za kujengea Vyoo vya mfano kwa ajili ya watoto wa Kike na wenye mahitaji maalum. Shughuli hiyo imefanyika katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
PICHA NA BUNGE

Wimbo Mpya wa Mbosso - Nadekezwa | Download /Watch

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images