Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mwijage Aipongeza Kampuni Ya Total Kwa Kuzindua Mafuta Ya Magari Rafiki Kwa Mazingira

$
0
0
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage ameipongeza kampuni ya mafuta ya TOTAL kwa kuwa mstari wa mbele kwenye kuhakikisha kuwa watanzania wanapata mafuta bora ya vyombo vya moto.

Mwijage alizungumza jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa mafuta ya vyombo vya moto aina ya TOTAL Excellium kutoka kampuni ya mafuta ya TOTAL. Mafuta hayo yaliyotengenezwa kwa teknolojia ya ubora wa juu ya kimataifa ya TOTAL EXCELLIUM, kwa bidhaa zinazotumia mafuta ya Petroli na Diesel katika soko la Tanzania.

“Uzinduzi wa mafuta haya umekuja wakati muafaka kwani sasa tuko kwenye wiki ya mazingira na mafuta haya yanapunguza uchafuzi wa hali ya hewa utokanao na vyombo vya moto, nawapongeza kampuni ya TOTAL kwa kuwaletea watanzania bidhaa bora, na mimi na utaalamu wangu wa mafuta nafahamu hii ni hatua kubwa sana kwenye teknolojia ya kuboresha mafuta,” alisema Mwijage.

Mafuta haya mapya yana uwezo wa kusafisha injini na kuwezesha injini kufanya kazi kwa kipindi kirefu, kuwezesha matumizi kidogo ya mafuta na kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa utokanao na moshi wa vyombo vya moto.

Mafuta ya TOTAL EXCELLIUM yanapatikana katika vituo vyote vya kuuza mafuta vya kampuni ya TOTAL kwa gharama ya bei ya kawaida ya mafuta kwenye soko.

Tarik Moufaddal, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya TOTAL nchini anasisitiza, “Kuzinduliwa kwa TOTAL EXCELLIUM, katika soko la Tanzania ni hatua mpya na muhimu kwetu nchini hususani katika kufanikisha dhamira yetu ya kuingiza bidhaa bora za nishati. Tunayo dhamira ya kuwapatia wateja wetu bidhaa zenye ubora wa hali ya juu, sambamba na huduma bora kupitia mtandao wetu ambao umeenea nchini kote, uzinduzi wa TOTAL EXCELLIUM, unadhihirisha kuwa tumejipanga kuleta mapinduzi yenye kuleta manufaa katika sekta ya mafuta nchini.”

“TOTAL EXCELLIUM imetengenezwa kwa teknolojia ya juu ya kisasa ambayo inawezesha kusafisha injini, kuwezesha injini kufanya kazi kwa kipindi kirefu bila kuchoka, matumizi kidogo ya mafuta kuendesha injini, kupunguza uchafuzi wa mazingira utokanao na moshi na ni mazuri kwa matumzi ya aina zote za magari kuanzia madogo mpaka makubwa,” aliongeza Tarik.

“Uzinduzi huu ni moja ya ubunifu mkubwa wa kampuni uliolenga kuhakikisha wateja wetu wanapata bidhaa bora na kuwawezesha matumizi kidogo ya mafuta yaliyotengenezwa kwa teknolojia ya kisasa ya Excellium. 

"TOTAL EXCELLIUM imetengenezwa kwa ubunifu wa teknolojia za kisasa zenye kuleta ubora. Timu yetu ya wataalamu wa utafiti wamefanikisha kutengeneza mafuta haya kukidhi mahitaji ya wateja wetu wanaotumia magari ya kisasa ambayo yanahitaji umakini mkubwa katika matunzo ya injini kwa matumizi yao ya kila siku”  Mkurugenzi wa Mtandao wa TOTAL wa Nikesh Mehta.

“Zaidi ya watafiti makini na wataalamu wenye uzoefu mbalimbali wanafanyia kazi suala la kuleta bidhaa za mafuta na vilainishi vya injini na mitambo zenye ubora mkubwa zaidi katika kituo chetu cha utafiti cha Solaize,nchini Ufaransa.Wataalamu hao wamekuwa wakifanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka miwili kuboresha mafuta ya TOTAL EXCELLIUM. 

"Zaidi ya kanuni za kisayansi 2,300 zimefanyiwa majaribio katika maabara kwa zaidi ya masaa 6,000 na mafuta haya yamefanyiwa majaribio ya awali barabarani kwa zaidi ya masaa 8,500 sawa na kilometa 300,000. 

"Haya yote yanathibitisha uhakika na ubora wa mafuta ya TOTAL EXCELLIUM na yanasafisha injini za magari na kupunguza uharibifu wa mazingira,” anasema Marsha Msuya, Mkurugenzi wa Masuala ya Ndani ya kampuni ya TOTAL.

Credit: Fullshangwe

Serikali Kuirudishia Ruzuku CCBRT

$
0
0
Serikali  inakusudia kukaa mezani na uongozi wa Hospitali ya CCBRT kujadili kwa kina ili ianze tena kuipatia ruzuku kama ilivyokuwa awali.

Hayo yalielezwa   na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alipozungumza mbele ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan aliyetembelea hospitali hiyo, Dares Salaam  jana.

“Serikali inatambua mchango mkubwa wa CCBRT katika kuhudumia wananchi tena huduma nyingine mnatoa bila malipo.

“Hii inamaanisha mnatoa huduma zaidi bila kujali faida, mnafanya vizuri katika huduma za tiba ya mifupa, macho na afya ya mama na mtoto.

“Mnasaidia mno kupunguza mrundikano wa wagonjwa katika hospitali zetu za serikali, ni kweli awali serikali ilikuwa inawapatia ruzuku lakini katika awamu hii ya tano ilisitishwa.

“Tunakusudia kukaa nanyi tena mezani tujadiliane na tukubaliane,  lengo letu tunataka ile ruzuku tutakapokuwa tunaileta iwafikie watumishi husika moja wa moja, tunataka kujua tunawalipa wauguzi au madaktari kiasi gani,” alisema.

Alisema   CCBRT imekuwa mdau mzuri katika sekta ya afya kwa kushirikiana na serikali ambako imekuwa ikiwajengea uwezo watumishi wake.

“Kwa mantiki hiyo tunakusudia kuipandisha hadhi CCBRT na kuifanya hospitali ya pekee inayoshirikiana na serikali katika kutoa matibabu dhidi ya tatizo la fistula,” alisema.

Awali, Ofisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Erwin Telemans aliiomba serikali kuipunguzia kodi hospitali hiyo  iweze kuendelea kutoa huduma bora kwa jamii.

“Hatua hiyo itatuwezesha kuendele kununua vifaa tiba vya kutosha na hata kuwalipa maslahi mazuri wafanyakazi wetu ikizingatiwa kwamba zipo huduma ambazo wagonjwa huhudumiwa bila malipo ikiwamo ya fistula,” alisema.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alisema serikali imepokea ombi hilo na   italifanyia kazi hasa kupitia meza hiyo ya majadiliano.

“Waziri amesema itaandaliwa meza ya majadiliano, hivyo ni imani yangu kwamba mtajieleza vizuri kwa kina kuhusu huduma mnazotoa na kuonyesha matokeo ya kazi mlizofanya.

“Sisi (serikali) tupo tayari kushirikiana nanyi ili tuendelee kuboresha huduma za afya nchini kwa pamoja.

“Mmenieleza kwa siku mnapokea wagonjwa wapatao 700, binafsi nimeguswa kwa jinsi mlivyoboresha afya ya mama na mtoto na namna mnavyowarejeshea furaha watu waliopoteza viungo.

“Hakika hii ni kazi ya kiungu na mnatoa sadaka kubwa kwa watanzania,” alisema.

Mrema Afichua Siri Jinsi Wapinzani Wanavyotunga Kashfa Feki Kuichafua Serikali

$
0
0
Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa Chama Cha Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema ameweka wazi jinsi timu yake ilivyowahi kufoji sakata la ufisadi dhidi ya Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Mheshimiwa Benjamin Mkapa, kwa lengo la kujipatia umaarufu.

Akizungumza leo kwenye mahojiano na kipindi cha Maisha Mseto cha Times FM, Mrema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, amesema kuwa kuna wakati vyama vya upinzani kwa lengo la kujipatia umaarufu, hutunga kashfa dhidi ya Serikali na viongozi wake kama yeye na timu yake walivyowahi kufanya miaka ya 1990.

Mwanasiasa huyo alisema kuwa anakumbuka mwaka mmoja baada ya kutoka kwenye uchaguzi, walifoji barua na kutunga dhidi ya Serikali kuwa viongozi wa juu na hadi kumtaja Mheshimiwa Mkapa kuwa  alifanya ufisadi wa sh.900 milioni.

“Lile tukio la Mh. Mkapa kwamba amekula Milioni 900, tulitengeneza sisi ili kumnyima sifa Mheshimiwa Mkapa na wananchi watuamini sisi watupe nafasi,” alisema.

Alifafanua kuwa timu yake kwa pamoja walikubaliana kuwa kwakuwa yeye ndiye aliyekuwa na ushawishi zaidi kwa wananchi alibebe sakata hilo ‘feki’ na alifanya hivyo; alisema “tulipanda kwenye majukwaa na barua ile ya kufoji na tukawa tunahoji kuhusu fedha zile.”

Mwanasiasa huyo ambaye miaka ya 1990 alikuwa kiongozi wa upinzani mwenye ushawishi mkubwa zaidi akigombea urais tangu mwaka 1995, alisema kuwa hadi sasa baadhi ya vyama vya upinzani vimekuwa vikitunga matukio ya kuichafua Serikali na hata Rais kwa lengo la kujipatia umaarufu wa kisiasa.

Wakati huo, Mrema alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, chama ambacho kilikuwa chama kikuu cha upinzani.

Katika hatua nyingine, Mrema alisifu kazi inayofanywa na Rais John Magufuli na kueleza kuwa ndani ya muda mfupi Serikali yake imefanikiwa kupambana na ufisadi kwa kiasi kikubwa.

Alisema alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alijaribu kupambana na ufisadi, hali iliyosababisha achukiwe na wengi, lakini hakufanikiwa kama alivyofanikiwa Rais Magufuli.

“Unajua ili ufanikiwe kwa baadhi ya mambo ya nchi ni lazima uwe Rais kwakuwa unakuwa wewe ndiye muamuzi wa mwisho. Mimi nilishindwa kwa sababu wakati mwingine unakuwa unafanya jambo lakini lisipoungwa mkono na walio juu yako huwezi kufanikiwa,” alisema.

“Sasa hivi mwenye nchi ndiye anayepambana na ufisadi. Atafanikiwa kwa sababu yeye ndiye anayesimamia kuliko wakati wangu mimi sikuwa na Serikali,”  Mrema aliongeza na kutoa wito kwa wananchi kuwa wavumilivu na kumsikiliza Rais John Magufuli.

Akizungumzia mpango wa kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo kwenye uchaguzi wa mwaka 2020, Mrema alisema atawasikiliza wananchi wa jimbo hilo ambao amedai wanalalamika kwa kukosa maendeleo baada ya kutomchagua.

Mrema alishindwa katika uchaguzi wa mwaka 2015 alipokuwa akitetea kiti chake cha ubunge wa Vunjo na nafasi yake ikachukuliwa na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia kupitia Ukawa.

Serikali Yaanza Uchunguzi Sakata La Mwanamke Aliyejifungulia Kituo Cha Polisi

$
0
0
Serikali imesema imefungua jalada la uchunguzi kuhusu mwanamke aliyejifungua sakafuni katika kituo cha polisi Mang’ula wilayani Kilombero katika Mkoa wa Morogoro,  Amina Mapunda.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Yusuph Hamad Masauni alipotakiwa na Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kutoa ufafanuzi wa Serikali kuhusiana na suala hilo.

“Tukio lililotokea huko Morogoro ni la ovyo kabisa na la kinyama na Serikali mnaweza kutoa kauli hapa na taifa likasikia,” amesema Chenge.

Akitoa kauli ya Serikali, Masauni amesema tayari jalada la uchunguzi limefunguliwa ili hatua kali za kisheria zichukuliwe.

“Tukio hilo lilimhusisha mume wa huyu mama ambaye alinunua kitanda cha wizi na polisi walipokwenda kwake wakakuta hicho kitanda cha wizi.

“Hivyo wakamkuta mke wake wakamchukua kwa ajili ya mahojiano, kitu ambacho hakikuwa sawa katika mazingira ya kawaida busara ingetumika.

“Hivyo serikali tumelichukulia kwa uzito suala hili na tunaendelea na uchunguzi halafu hatua kali zitachukuliwa,” amesema.

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo dawa na PETE za bahati zenye uwezo mkubwa wakuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.
 
Kutana na Sharif Al_noor. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. -SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA- Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na inje ya nchi.
 
Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.
 
Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudisha  alipotea(MSUKULE), kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, kutoa ndagu, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMA, GARI..), Kesi mahakamani, Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET) Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa nambari ya simu
 
+255 746 426 604

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

BREAKING: Serikali Yaikana Barua waliyoandikiwa KKKT Ikiwataka Wafute Waraka Wao wa Pasaka

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema barua iliyoandikwa na wizara hiyo ya kulitaka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) kuufuta waraka wa Pasaka ni batili.

Akizungumza leo Juni 8 katika mkutano na wanahabari, Dk Nchemba amesema taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ni batili na siyo maelekezo ya serikali au wizara.

“Tunawaomba viongozi wa dini waendelee na kazi zao, nasema jamii iwe macho na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya jamii na wasifanyie kazi taarifa hizo,” amesema.

Kadhalika, Dk Nchemba amesema amefuatilia barua hizo na kuona zina mkanganyiko wa anuani.

“Viongozi wa dini wasiwe na taharuki na taarifa hizo, hazina baraka za Serikali. Wasisite kuwasiliana na Serikali kujua uhalali wake.” Amesema.

Pia Dk Nchemba amesema waraka wa viongozi wa dini uliotolewa miezi iliyopita ni jambo lililopita na hivyo akawataka viongozi wa dini waendelee na kazi zao.

Dk Nchemba amewataka viongozi wa dini kuendelea na kazi zao. “Nchi yetu ni moja na tunaishi kwa taratibu tulizojiwekea na tuna madhehebu mengi.” Amesema na kuongeza: “Wengine wameliona jambo hilo kama ajenda. Wananchi wawe makini, wasiwafuate watu hao wanaotaka kuwagawa.”


Mbali na hato Waziri Nchemba ameonya wanasiasa wanaoingilia jambo hilo kisiasa kwa kusema kwamba kama umakini usipowekwa amani ya nchi itavurugika na ingawa bado wanaendelea na uchunguzi kuwabaini wahusika ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa.

Serikali yawataka wasioridhishwa na utendaji wa wakuu wa Wilaya na Mikoa kwenda mahakamani

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, UTUMISHI na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu), George Mkuchika amewataka wasioridhishwa na utendaji kazi wa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa kwenda mahakamani kutafsiri sheria.
 
Mkuchika ametoa kauli hiyo, leo Juni 8, 2018 wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum(CHADEMA), Ruth Mollel aliyeihoji serikali kuwa, Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wameteuliwa wengi wao walikuwa ni wana CCM walioshindwa katika kura za maoni na wao ndio wasimamizi wa uchaguzi kuna wengine kama huyu wa Ubungo anahudhuria vikao vya CCM, Swali langu ikiwa tutaleta orodha ya Wakurugenzi ambao tunajua ni wana CCM na walikuwa katika kura za maoni Je serikali itakuwa tayari kuwaondoa?

“Swali la pili tunao wakuu wa mikoa ambao wanalipwa kwa pesa za walipa kodi Watanzania wenye vyama na wasiokuwa na vyama lakini wengi wameonyesha itikadi za kisiasa ukiangalia mkuu wa mkoa Arusha, Mkuu wa Mkoa wa Manyara na wengine Je, serikali ina kauli gani kuhusu hilo?

Akijibu swali hilo, Mkuchika amesema kuwa “Mkurugenzi yoyote utakaye mchagua katika nchi hii lazima kuna Chama anachokipenda, huyu yuko pale baada ya kuteuliwa kuwa mkurugenzi na Waraka wa utumishi wa umma unasema Mtumishi wa umma anaeteuliwa na Rais endapo hata ridhia kufanya ile kazi ana ruksa ya kumuambia Mh. Rais naomba niendelee na kazi yangu , sasa hao wakurugenzi walipokuwa wanafanya kazi walishakoma kazi waliokuwa wanaifanya, kazi wanayoifanya ni Ukurugenzi wa Halmashauri nataka niseme Rais anapoingia madarakani anapanga safu yake.”

Ameongeza, “Yule wa Ubungo kuhudhuria vikao naomba nisema mkishakuwa mnachama tawala siku zote kazi yenu nikuihoji serikali , Mkurugenzi wa Ubungo sio Mjumbe wa CCM lakini anweza kutwa akaelezea utendaji wa ilani ya uchaguzi katika jimbo la Ubungo.”

Amesisitiza kuwa “Swali la pili kuhusu wakuu wa mikoa , nataka niseme Wakuu wa Mikoa wanamuwakilisha Rais, Mkuu wa Mkoa ndio Rais wa Mkoa ule , Rais ni neno la kiarabu maana yake kichwa kwahiyo kichwa cha mkoa ule ni Mkuu wa mkoa ule, huyu Mkuu wa Mkoa anamuwakilisha Rais , hutegemei huyu Mkuu wa mkoa afanya mambo tofauti anayofanya Rais, lakini mwisho nimalizie kusema kwamba nchi hii tunachombo kinaitwa mahakama muhimili wa mahakama kazi yake ni kutafsiri sheria , pale mtu anavyoona hakutendewa ndivyo sivyo basi tufuate mkondo wa sheria na baadhi yao mnaowasema walikuja hapa kwenye maadili wakasiliza wakawa cleared wakaonekana hawana makosa.”

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume, Maumbile Mdogo, Busha Bila Kupasua

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO : Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliohangaika sehemu mbalimbali bila mafanikio.

Mabula Clinic ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya jeshini. Je unaupungufu wa nguvu za kiume au uume wako mdogo na mwembamba? 

Mapro pawer no 2 ndio tiba, kwa sasa hutibu matatizo matatu kwa pamoja 1. itakufanya uchelewe kufika kileleni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2. Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa hasa kwa wale walio athirika na upigaji punyeto 3. itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya mara tatu :Kwa nini ujione mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo 

Makakanua mix ni dawa iliyochanganywa na miti shamba 9 na kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 kwa urefu na unene sentimita 1-5, dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona

 Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke kwa masaa matatu tu ,mvuto wa biashara, kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu.

Tunatibu ngiri, miguu, mgongo na kiuno kuumwa, kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa 

Tiba na ushauli muone Dr Mabula au piga simu no 0743362017.Huduma zangu utazipata popote ulipo kama uwezi kufika ofisini

Dr Shika Kaja Kivingine...Leo Kamtambulisha Msanii Wake Anayemsimamia

$
0
0
Dkt. Louis Shika ambaye amejipatia umaarufu baada ya kutangaza dau la kununua nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi, amefunguka na kutangaza nia ya kujihusisha na masuala ya muziki nchini Tanzania hasa upande wa kuwasimamia wasanii wachanga na wakubwa.

Dkt. Shika ametoa kauli hiyo leo Juni 08, 2018 wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema siku si nyingi atatangaza jina rasmi ya label yake ambayo itakuwa inajuhusisha na kusimamia kazi za wasanii wa BongoFleva huku akidai lengo lake kubwa ni kutaka kutimiza ndoto za kila mmoja kupitia sanaa.

"Sasa tutaelewana tu na kabla hatujaanza na masuala ya viwanda 30 nilivyo vitaja na 'different services', kwa sasa ninaanza na 'music industry' na tunaanzia kwa msanii mmoja ambaye anaitwa Godson anayetokea Songea na hili nina uhakika watanzania watafurahi na kufuta 'stress' mbalimbali zilizokuwa zinawasumbua", amesema Dkt. Shika.

Pamoja na hayo, Dkt. Shika ameendelea kwa kusema "nipo tayari kuwasimamia wasanii wengine watakaopenda lakini ninaanza na huyu mmoja na nina uhakika atawafunika wasanii wengi, kwa hiyo jaribuni kumfuatilia".

Kwa upande mwingine, Dkt. Louis Shika amesema ukimya wake wa kipindi kirefu umetokana na yeye kuhangaikia kuingiza fedha nchini kutokea nje ili aweze kutimiza azma yake aliyokuwa ameitangaza hapo awali.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0785687900

Mrema Ammwagia Sifa Diamond

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema amesema msanii wa Bongo Flava anayemfuatilia kwa sana ni Diamond Platnumz.

Ameeleza sababu ya kumfuatilia muimbaji huyo ni kutokana na kujituma kwake na muziki wake unavutia.

“Namfuatilia sana Diamond, ni kijana mdogo, muimbaji mahiri, yaani Diamond asaidiwe naona hatima yake katika maisha yake na nchi yetu atatufikisha mahali pazuri. Kwa muziki wake unakosha roho, hata sisi wazee, mimi naridhika sana,” Mrema ameiambia Times FM.

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa serikali kuwa karibu zaidi na wasanii, hata hivyo amesema anaziona jitihada za Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe za kukutana na wasanii kila mara hasa pale wanapopata matatizo na kuwasaidia.

Serikali: “Tutapandisha mishahara hali ikiruhusu”

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema kuwa serikali itaweza kuboresha maslahi ya watumishi wa umma nchini kwa kuongeza mishahara kulingana na uwezo wa Serikali.

Waziri Mkuchika, amesema hayo leo Juni 8, 2018 Bungeni, Jijini Dodoma akielezea ni kwa namna gani Serikali inawajali watumishi swali lililoulizwa Mbunge wa viti maalumu Catherine Magige na kuongeza kuwa Serikali inafanya jitihada za kuwajali watumishi kwa kuwapa mikopo, mafunzo na kudhamini masomo kwa baadhi ya watumishi wanaosoma taaaluma mbalimbali.

“Kujali mtumishi sio lazima fedha, hata ukimpeleka kwa mafunzo umemjali mtumishi, niseme tu kifupi kwamba tunaendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma lakini kwa upande wa mishahara, tutaipandisha hali ya nchi ikiruhusu”, amesema Mkuchika.

Waziri huyo ameongeza kuwa Serikali haitasubiri sikukuu ya wafanyakazi (Mei Mosi) ili itangaze kupanda kwa mishahara bali muda wowote amabapo itajiridhisha na hali ya mfuko wa serikali basi itapandisha mishahara.

Menejiment BOT Yahojiwa na PAC....Ripoti Kukabidhiwa kwa Spika Jumatatu

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imemaliza kazi ya kuwahoji Bodi na Menejimenti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) juu ya tuhuma zinazowakabili za kutumia bima binafsi ya afya badala ya Bima ya Taifa ya Afya (NHIF).

Bodi na Menejimenti ya BoT wamefika mbele ya kamati ya PAC kujibu tuhuma hizo ambazo ziliibuliwa bungeni Juni 4 na Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka amesema, wameshazungumza na Bodi na Menejimenti ya BoT pamoja na NHIF.

“Kwa kuwa ni agizo la Mheshimiwa Spika (Job Ndugai), tunakamilisha kuandaa taarifa na Jumatatu (Juni 11, 2018) tutamkabidhi,” ameongeza Kaboyoka ambaye pia ni Mbunge wa Same Mashariki (Chadema).

Bodi na Menejimenti ya BoT ikiongozwa na Gavana wa Benki hiyo, Profesa Florens Luoga pia wamehudhuria kikao cha 47, Mkutano wa 11 leo na kutambulishwa na Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge.

Vyuo 20 Vyafutiwa Usajili na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte)

$
0
0
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE)limetengaza kufuta usajili wa vyuo 20 baada ya kubaini vimeshindwa kufuata tararibu zinazoendana na matakwa ya usajili wa vyuo hivyo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Kaim Katibu Mtendaji wa NACTE Dk.Adolf Rutayunga amesema uamuzi huo umefikiwa kwa kuzingatia kifungu cha 20 cha kanuni za usajili wa vyuo vya ufundi 2001.

Amesema vyuo ambavyo vimefutiwa usajili tayari baraza limeshaviandikia barua vyuo husika kuvitaka vihakikishe kuwa wanafunzi waliko kwenye programu zinazotolewa na vyuo hivyo wanahamia kwenye vyuo vingine vilivyosajiliwa na baraza kutoa programu kama hizo.

Amevitaja vyuo vilivyofutiwa usajili ni Covenant College of Business Sdudies(Dar es Salaam), Mugerezi Spatial Technology College(Dar es Salaam),Techno Brain(Dar es Salaam), DACICO Institute of Business and Management(Sumbawanga) na Arusha Institute of Technology (Arusha).

Vyuo vingine ni Lisbon Business Collage(Dar es Salaam), PCTL Training Institute(Dar es Salaam), Royal College of Tanzania(Dar es Salam), Iringa RETCO Business College(Iringa) na Highlands Health Instutute(Njombe).

Vyuo vingine ni East African Institute of Entrepreneurship and Finacial Management(EAIEFM) (Arusha), Musoma Utali Collage (Shinyanga) na Mlimani School of Professional Studies(Dar es Salaam).

Pia kuna chuo cha Dinobb Institute of Science and Business Technology(Mbeya), Institute of Social Work(Mbeya), Regency School of Hygiene (Dar es Salaam), St.Peters College of Health Sciences(Dar es Salaam), Genesis Institute of Social Science(Dar es Salaam), Institute of Management and Information Technology(Dar es Salaam) na Boston City Campus of Business College(Dar es Salaam).

Pia Dk. Rutayunga amesema mbali ya kufuta usajili kwa vyuo hivyo wamesitisha program zisizoidhinishwa na baraza ambapo vyuo vitatu vimefutiwa programu.

Amefafanua kabla ya kuanza kuendesha mafunzo ya kozi yoyote ,chuo kinatakiwa kuhakikisha kuwa mtaala wa mafunzo hayo umepitishwa na baraza na idara itakayosimamia mafunzo hayo imekaguliwa na kuonekanwa kuendesha mafunzo hayo katika ngazi husika.

Amesema vyuo vitatu ambavyo ni Quality Development College (Masasi)kimefutiwa programu ya Medical Attendent, St.Glory Nursing School (Dar es salaam) wamefutiwa program ya Medical Attendant and Medical Labaratory Sciences na chuo cha Lake Victoria Disability Medical Training Centre(Mwanza) wamefutiwa program ya Nursing and Midwifery.

Wakati huohuo amesema jumla ya vyuo tisa vimesitishwa kudahili wanafunzi wapya kuanzia mwaka wa masomo 2018/2019.Uamuzi huo umefikiwa kwa kuzingatia kifungu cha 22(1) cha kanuni za usajili wa vyuo vya ufundi,2001.

Amesema wanafunzi waliopo waliodahiliwa kwenye vyuo hivyo wanaruhusiwa kuendelea na masomo kama kawaida mpaka watakapohitimu mafunzo yao.

Amevitaja vyuo ambavyo vimesimamishwa kudahili ni Montfort Business College (Dar es Salaam), Institute for Environment and Development Sustainability(Dar es Salaam) na Songea Clinical Assintant Training Centre(Songea).

Pia chuo cha Institute of Continuing and Professional Studies(Zanzibar),Tanzania Institute for Trade and Investment(Dar es Salaam), Institute of Research and Innovation Zanzibar(Zanzibar), Silva Business and Management(Dar es Salaam), Mbeya Polytechnic College(Tukuyu Campus) na Earth Science Institute of Shinyanga(Shinyanga).

Binti wa Kazi Amuua Bosi Wake Pamoja na Mwanae

$
0
0
Jeshi la Polisi katika eneo la Kisumu, nchini Kenya, linamtafuta msichana ambaye ni msaidizi wa kazi za nyumbani kwa tuhuma za kumuuwa muajiri wake na mtoto wa miezi mitatu ambaye ni wa muajiri huyo.

Kwa mujibu Citizen Kenya imeripoti leo Juni 8, 2018 na mashahidi katika eneo hilo, wamedai kwamba tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Alhamisi, Juni 7, 2018 na ilipofika saa 2:00 usiku waliamua kuvunja mlango wa nyumba ambao ulikuwa umefungwa kwa siku nzima ya jana jambo ambalo halikuwa la kawaida

Mwili wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Elizabeth Ojwang, ulikutwa umeviringishwa mfuko wa plastiki shingoni, kando na mwili wa mtoto wake uliokutwa na majeraha mbalimbali katika mwili yaliyosababishwa na kuchomwa na kitu chenye ncha kali.

Akithibitisha tukio hilo kamanda Jeshi la Polisi, kaunti ya Muhoroni, John Kamau amesema kwamba Jeshi hilo linaendelea kumtafuta binti wa kazi kwa mahojiano ambaye alitoweka baada tukio hilo na kuongeza kuwa msichana huyo anaweza kuwa mtuhumiwa wa kwanza wa mauji hayo.

Sababu kubwa ya mauaji hayo bado haijajulikana, Jeshi la Polisi ilichukua miili ya marehemu hao na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Kisumu kwa uchunguzi zaidi

Serikali yawashukia Maafisa Utumishi wanaochelewesha malipo ya wastaafu

$
0
0
Serikali imesema mtumishi wa umma anayestaafu anatakiwa kulipwa mafao yake ndani ya siku 60 kwa mujibu wa sheria na kinyume na hapo waajiri watawajibishwa.

Kauli hiyo ilitolewa leo Ijumaa Juni 9, 2018 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Kapteni mstaafu George Mkuchika wakati akizungumza na waandishi wa habari, kupiga marufuku wastaafu kufuatilia mafao yao kwa kuwa kazi hiyo inapaswa kufanywa na maofisa utumishi.

Amesema kumekuwa mateso na usumbufu kwa wastaafu ambao wanachukua muda mrefu kulipwa mafao yao licha ya kuwa ni haki yao.

Kauli ya Mkuchika imekuja huku kukiwa na idadi kubwa ya watumishi wanaosotea mafao yao na baadhi wakitumia muda mrefu na wengine kufariki dunia bila kupata fedha hizo.

"Utakuta mtu anaishi Bukoba lakini anafuata haki yake Dar es Salaam na kila siku analala na kula hivyo kujikuta akitumia gharama kubwa ambazo ni mateso kwake, tunasema sasa mambo kama hayo hayapaswi kuwepo tena,” amesema Mkuchika

Amewataka maofisa utumishi wote kutimiza wajibu wao wa kuwasaidia wastaafu kupata haki yao vinginevyo Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali.

Kuhusu hatua za kufuata ili kupata mafao, amesema zinaanzia kwa waajiriwa wenyewe ambao miezi sita kabla wanatakiwa kuandika barua za kueleza mwezi na tarehe za kustaafu kwao kabla ya mwajiri naye kuitaarifu mifuko.

Amesema hatua ya tatu ni kwa mifuko ya pensheni ambayo nayo inatakiwa kuandaa nyaraka muhimu ambazo zitamwezesha mstaafu kupata haki yake mapema.

Tanzania Kuendelea Kuimarisha Biashara Na Malawi

$
0
0
Na Fatma Salum-MAELEZO
Serikali ya Tanzania inaendelea na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na Serikali ya Malawi kupitia sekta ya biashara na uwekezaji ili wananchi waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika nchi zote mbili.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, leo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla alisema kuwa katika kuimarisha uhusiano huo, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Malawi zimeandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji litakalofanyika Julai 26 na 27 mwaka huu Jijini Mbeya.

Makalla alieleza kuwa lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji wan chi zote mbili ili kubaini fursa mbalimbali zitakazowezesha kuanzisha na kuendeleza miradi katika sekta za viwanda, usafirishaji, utalii, uvuvi, kilimo, madini, elimu, afya, benki, mawasiliano, Tehama na biashara kwa ujumla.

“Kongamano hili linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki wapatao 500 ikijumuisha wafanyabiashara, wawekezaji, Taasisi za Umma na sekta binafsi kutoka Tanzania na Malawi,” alisema Makala.

Sambamba na kongamano hilo, kutakuwepo mikutano ya wafanyabiashara (B2B), mikutano ya watendaji wa Serikali (G2G) na mikutano kati ya Serikali na wafanyabiashara (B2G) kutoka nchi zote mbili.

Makalla alisisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya uko tayari kuchangamkia fursa za kibiashara na Malawi kwa sababu miundombinu ipo ya kutosha ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, meli mbili za kubeba mizigo ambazo zimeshaanza kufanya kazi na meli moja ya abiria ambayo itakamilika Julai mwaka huu.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kuanza ujenzi wa kituo kimoja cha forodha (One Stop Boarder Post) katika mpaka wa Kasumulu na imetenga eneo la kujenga bandari kavu katika eneo la Inyala kwa lengo la kuwezesha upokeaji na uhifadhi wa bidhaa moja kwa moja kutoka bandari ya Dar es Salaam.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), John Mnali alisisitiza kuwa kongamano hilo ni muhimu kwa wafanyabiashara wa kitanzania hivyo wajitokeze kushiriki ili waweze kuibua fusra mpya na kujitangaza kwa wenzao wa Malawi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye alitoa wito kwa wafanyabiashara wote hasa sekta binafsi kujitokeza kwa wingi kuangalia fursa zilizopo Malawi na kubadilishana uzoefu wa kibiashara.

Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji (TIC), Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TanTrade) na Taasisi ya Biashara na Uwekezaji ya Malawi (MITC) wanaratibu kongamano hilo na mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan.

Mfumuko Wa Bei Nchini Waendelea Kupungua Toka Asilimia 3.8 Hadi Asilimia 3.6

$
0
0
Na. Eliphace Marwa – Maelezo
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo imetoa taarifa ya mfumuko wa bei kwa mwezi Mei mwaka huu ambao umepungua hadi kufikia asilimia 3.6 ikilinganishwa na asilimia 3.8 ilivyokuwa kwa mwezi Aprili mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo amesema kuwa kupungua kwa bei kumechangiwa sana na kupungua kwa mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula.

“ Baadhi ya bidhaa za chakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei ni pamoja na mahindi kwa asilimia 10.3, unga wa mahindi kwa asilimia 12.5, mtama kwa asilimia 13.8, unga wa mihogo kwa asilimia 15.2, viazi mviringo kwa asilimia 9.0 na mihogo mibichi kwa asilimia 12.6, alisema bwana Kwesigabo.

Aidha ameongeza kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2018 imepungua ikilinganishwa na kasi ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi Aprili 2018.

Hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya nchi za Afrika Mashariki kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2018 nchini Uganda umepungua hadi asilimia 1.7 kutoka asilimia 1.8 kwa mwaka ulioishia mwezi aprili 2018.

Aidha kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2018 umeongezeka kidogo hadi asilimia 3.95 kutoka asilimia 3.73 kwa mwaka ulioishia mwezi Aprili, 2018.

Mfumuko wa bei unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images