Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Mbunge Chadema Airushia Tuhuma Nzito Wizara ya Fedha

0
0
Mbunge wa Momba (Chadema), David Salinde amesema Wizara ya Fedha na Mipango ndio adui namba moja wa maendeleo ya Taifa na kushauri Bunge liichukulie hatua ili kutekeleza maagizo yake.

Silinde akichangia bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango ya mwaka 2018/19, jana Juni 4, 2018 bungeni, alisema: “Kwa lugha nyepesi kabisa, adui namba moja ni Wizara ya Fedha na Mipango. Wizara ya fedha inashindwa kutoa fedha ambazo zipo kisheria.”

Silinde amesema ukiangalia ripoti za CAG, wizara imekusanya fedha lakini haipeleki sehemu husika.

“Leo watu wa korosho wanalalamika wamekusanya Sh91 bilioni, wamepelekewa Sh10 bilioni,”alisema na kuongeza; “Wana sababu moja tu, uhakiki na ndio kichaka cha kujifichia kupeleka fedha. Mawaziri wanakuja hapa wanalia. Wao wajibu wao kukusanya na kupeleka. Hivi hawa wanaitakia mema nchi hii”

Wabunge Wahoji Ahadi ya Milioni 50 Kwa Kila Kijiji Iliyotolewa Na Rais Magufuli

0
0
Ahadi ya Chama Cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 ya kutoa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji na kila mtaa kwa sehemu za mijini, ambayo haijatekelezwa kwa miaka miwili mfululizo huenda ikaanza kutekelezwa baada ya jana Bunge kuitaka serikali kutoa taarifa bungeni kuhusu utekelezaji wake.

Akiwasilisha bungeni jijini Dodoma jana taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka ujao wa fedha, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Jitu Soni, alisema pamoja na kwamba serikali iliahidi kutoa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji, hadi sasa hakuna fedha yoyote iliyotolewa.

Alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17, serikali ilitenga Sh. bilioni 60 (Fungu 21) na katika mwaka huu wa fedha ilitenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kufanya utafiti wa majaribio kwa baadhi ya mitaa, vijiji, kata na shehia kutekeleza mradi huo.

"Hata hivyo, fedha hizo zilizotengwa katika miaka yote, hakuna fedha yoyote iliyotolewa licha ya serikali kuahidi na kuweka utaratibu maalum kuhusu utoaji wa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji kupitia Tamisemi," alisema.

"Kamati ingependa Bunge lako tukufu lipewe taarifa ya utekelezaji wa mradi huu ikiwamo 'Pilot Study' (utafiti wa majaribio) iliyofanyika," alisema.

Kiongozi huyo wa kamati pia alisema tathmini ya jumla ya mwenendo wa utoaji wa fedha za utekelezaji bajeti ya mwaka 2017/18 si wa kuridhisha kwa baadhi ya mafungu.

"Hadi kufikia Machi, mwaka huu, kati ya mafungu nane yaliyo chini ya wizara, ni miwili tu yaliyokuwa yamepokea fedha zaidi ya asilimia 60 ya bajeti zilizoidhinishwa na Bunge," alisema na kueleza zaidi:

"Kati ya mafungu 47 ya wizara mbalimbali yanayostahili kupata fedha za maendeleo ni mafungu 16 tu yamepata fedha zaidi ya asilimia 50."

Pia alisema mapato yatokanayo na ushuru wa usafirishaji wa fedha na bidhaa zinazotozwa ushuru wa bidhaa kama pombe kali yameshuka kwa asilimia 30.

"Kamati inaendelea kuishauri serikali kuhakikisha kwamba sera zake za kikodi kwa sekta zinazokua ziwe zina lengo la kulea na kuendeleza sekta hizo na si kukusanya kodi kiasi ambacho kinaathiri hata ukuaji wa sekta husika,"alisema.

Jitu pia alisema pamoja na michezo ya kubahatisha kukua kwa kasi na kuipatia serikali mapato, kamati yake inashauri kupanda kwa ada, tozo na kodi mbalimbali kwa kuwa kimsingi michezo hiyo si ya kiuzalishaji na imekuwa na madhara makubwa kwa jamii.

"Katika nchi za Afrika Mashariki, Tanzania inaongoza kwa kutoza kiwango cha chini kwenye mapato ghafi ya michezo ya kubahatisha kuliko nchi nyingine," alisema.

Alitolea mfano Kenya kuwa inatoza asilimia 35, Rwanda asilimia 13 na Uganda inatoza asilimia 20 ya mapato ghafi.

Alisema kamati inaitaka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (GBT) kusimamia kikamilifu sheria ili kuhakikisha kwamba wanaoshiriki katika michezo hiyo wawe wanafikia umri wa miaka 18.

Jitu pia alisema kamati yake inaishauri serikali kuhakikisha inalipa madeni yote ya watumishi, makandarasi na wazabuni yaliyohakikiwa.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Spika Ndugai Aionya Serikali....Atishia Kuzuia Mkutano wa Bunge Mwezi Oktoba

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ameitaka serikali kuhakikisha inatekeleza agizo lake la mwishoni mwa mwaka jana kuhusu kuwasilisha bungeni muswada wa sheria ya kuitangaza Dodoma kuwa makao makuu ya nchi vinginevyo atazuia kufanyika kwa mkutano ujao wa Bunge.

Novemba 17, mwaka jana, Spika Ndugai aliitaka serikali kuhakikisha muswada huo unasomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano uliofuata uliofanyika kwa wiki mbili kuanzia Januari 30, lakini haikufanya hivyo.

Muda mfupi kabla ya kusitisha kwa muda kikao cha Bunge jijini Dodoma jana mchana, Spika Ndugai alikumbusha kuhusu agizo lake hilo na kumuonya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama kwamba hakuna muswada wowote wa serikali ambao utasomwa bungeni kabla ya kuwasilishwa kwa muswada wa kuitambua Dodoma kuwa makao makuu ya nchi.

"Hakuna muswada utakaosomwa hapa kwa mara ya kwanza kabla ya muswada huo. Na kwa maana hiyo, mkutano wa mwezi Oktoba hautafanyika," Spika Ndugai alisema.

Kiongozi huyo wa Bunge alitoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa Iringa Mjini, Mch. Peter Msigwa (Chadema) kueleza bungeni jana kuwa mpango wa serikali kuhamia Dodoma haumo kwenye Mpango wa Taifa wa Maendeleo ya Miaka mitano 2015/6-2020/21.

Akichangia mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka ujao wa fedha, mbunge huyo alisema kuna mipango mingi imekuwa ikiibuliwa na kutekelezwa kwa fedha ambazo hazikuidhinishwa na Bunge.

Alisema mpango wa serikali kuhamishia shughuli zake Dodoma ni mfano mzuri kwa mipango inayotekelezwa bila kuidhinishwa na Bunge na haumo kwenye mpango mkuu wa serikali.

"Ndiyo maana leo tunahangaika kupata ofisi hapa Dodoma. Hatupingi serikali kuhamia Dodoma, lakini mpango huu Mheshimiwa Spika, haumo kwenye mpango wa serikali wa miaka mitano," Mch. Msigwa alisema.

Kutokana na kauli hiyo ya mbunge huyo, Spika Ndugai alisimama na kueleza kuwa suala la serikali kuhamia Dodoma limekuwa likiwekwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mpainduzi (CCM) tangu mwaka 1973.

Alisema kuna haja suala hilo liwe la kisheria, hivyo akamtaka Waziri Mhagama kuhakikisha anatekeleza agizo lake la kuwasilisha muswada huo bungeni vingine hatakubali muswada mwingine wowote kusomwa kwa mara ya kwanza ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria.

Mapacha walioungana kuzikwa kaburi moja

0
0
Marehemu mapacha Maria na Consolata Mwakikuti (20) waliofariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita mjini hapa watazikwa katika kaburi moja kesho.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mapacha hao watazikwa pamoja japo kunatengenezwa majeneza mawili.

Alisema kwa kuwa wakati wa uhai wao mapacha hao walishakataa kutenganishwa, uongozi wa mkoa unatengeneza majeneza mawili kwa sababu ni watu wawili, lakini watazikwa kwenye jeneza moja lenye miili miwili.

Hata hivyo, misalaba itakuwa miwili kwa sababu ni watu wawili tofauti, alisema Kasesela.

Alisema familia za baba na mama wa mapacha hao kutoka Tukuyu, Mbeya na Bukoba, Kagera pamoja na waliokuwa walezi wa mapacha hao, Masista wa Consolata wa hapa Iringa wamekubaliana makaburi ya kuzikwa pia.

“Kwa pamoja tumekubaliana watoto hawa wazikwe katika makaburi ya viongozi wa dini Tosamaganga Iringa," alisema Kasesela. "Sista aliongea nao kabla ya kufariki wakampa nafasi na jukumu la kuhakikisha kwamba wanazikwa hapo.”

Aidha, kaimu mkuu wa mkoa huo alisema wameamua mazishi yafanyike kesho, ili kumsubiri Askofu Mkuu wa Jimbo la Njombe, na Rais wa Baraza la Maaskofu (Tec), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo la Iringa aliye jijini Dar es Salaam kikazi.

Alisema shughuli za kuaga miili hiyo zitaanza saa mbili asubuhi katika Chuo Kikuu cha Ruaha (Rucu).

Baada ya zoezi la kuaga msafara wa mazishi utapita barabara kuu kuelekea Tosamaganga, ili wananchi waweze kutoa heshima zao za mwisho kama watashindwa kufika Rucu.

Spika Ndugai Aibana BOT....Aitaka Ikajieleze PAC

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai ametoa wiki moja kwa Bodi ya Benki Kuu Tanzania (BoT) na menejimenti yake kufika mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kujieleza kuhusu matumizi ya bima binafsi ya matibabu.

Spika Ndugai ametoa agizo hilo lejana  bungeni Juni 4, 2018 mara baada ya Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga kusema BoT kuna ufisadi mkubwa wa watumishi wake kuendelea kutibiwa nje ya nchi.

Mlinga alisema wakati usalama wa Taifa, Bunge na taasisi nyingine zikitumia Bima ya Taifa ya Afya (NHIF), BoT ndiyo inayotumia fedha nyingi kuliko taasisi yoyote.

“BoT ukiumwa mafua unakwenda Uingereza. Matumizi yao yamepanda kutoka Sh1 bilioni wanatumia Sh12 bilioni kwa sababu watu wana maslahi binafsi,” alisema Mlinga.

Mlinga alisema hataunga mkono hoja ya Waziri Mpango (Philip) hadi atakapokuja na majibu ya maswali hayo.

Mara baada ya kumaliza kuchangia, Spika Ndugai aliagiza PAC, kuiita bodi ya BoT na menejimenti yake na wajieleze kwa nini wanafanya matumizi hayo na baada ya wiki moja waripoti kwake.

“Muwe mmekaa na Mlinga na mkae na NHIF, halafu sasa mnawaita hawa BoT, baada ya kufanya haraka sana mnipe na nimwandikie Rais ili aingilie kati,” alisema.

Tume Ya Utumishi Wa Walimu Yatengewa Bil.12

0
0
Tume ya Utumishi wa Walimu imetengewa Sh bilioni 12 kwa mwaka wa fedha 2018/19, ambapo kati ya hizo Sh bilioni 7.8 ni za mishahara na Sh bilioni 4.6 ni za matumizi mengineyo.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo na Naibu Waziri Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Joseph Kakunda wakati akijibu swali la Mbunge Singida Mjini, Mussa Sima.

Mbunge huyo alihoji Tamisemi haioni haja sasa ya kuziagiza rasmi Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwezesha Tume ya Utumishi ya Walimu kutekeleza baadhi ya majukumu yake ili walimu wapate huduma stahiki kwa wakati.

Akijibu swali hilo, Kakunda alisema: ” Katika mwaka wa fedha 2018/19 Bunge limeidhinishia tume hiyo fedha hizo ili ipate vitendea kazi kama magari, samani za ofisi na pia kugharamia vikao vya mashauri ya nidhamu na rufaa.”

Mnyika Aihoji Serikali Kuhusu Wafungwa Wanaobambikiziwa Kesi

0
0
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika (Chadema) ameitaka Serikali ieleze ni lini itaanza kutoa fidia kwa wafungwa waliobambikiziwa kesi.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni leo Juni 5, kwa niaba ya Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mnyika alidai kwamba katika gereza la Segerea wafungwa wengi wamekuwa wakibambikiziwa kesi.

“Je, Lini Serikali itaanza kutoa fidia kwa wale waliobambikiziwa kesi,” aliuliza Mnyika.

Akijibu swali hilo kwa niaba ya Wizara ya Sheria na Katiba, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde alisema utaratibu wa kimahakama upo wazi kwa wale wanaobambikiziwa kesi kufungua kesi ya madai.

Tazama Hapa Ratiba Nzima na Makundi Yote ya Kagame Cup 2018

0
0
Wakongwe wa soka Tanzania, Simba SC na Yanga SC wamepangwa Kundi C katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Kagame Cup inayotarajiwa kuanza Juni 28 hadi Julai 13 mwaka huu mjini Dar es Salaam.
 
Akitaja makundi ya michuano hiyo, Katibu wa kudumu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye alisema kwamba pamoja na Simba na Yanga, timu nyingine katika Kundi hilo ni Dakadaha ya Somalia na Saint George ya Ethiopia.
 
Musonye alisema kwamba Kundi A linaundwa na timu za Azam FC, KCCA ya Uganda, JKU ya Zanzibar na Kator FC wa Sudan Kusini, wakati Kundi B linaundwa na timu za Rayon Sport ya Rwanda, Gor Mahia ya Kenya, Lydia Ludic ya Burundi na Ports ya Djibouti. Musonye aliishukuru Tanzania kwa kukubali kuwa wenyeji wa michuano hiyo na akasema kwamba anatarajia itafana kwa sababu ya rekodi ya nchi hii kuandaa mashindano yaliyokuwa na msisimko mkubwa miaka ya nyuma.
 
Musonye ambaye alisema mashindano yatafanyika viwanja vya Taifa na Azam Complex, Chamazi – pia amewapongeza Rwanda na Rais wao, Paul Kagame kwa kuwa wadhamini wa mashindano haya kwa zaidi ya miongo miwili sasa.
 
Musonye amesema kwamba wamelazimika kufanya mashindano ya mwaka huu sambamba na Fainali za Kombe la Dunia nchini Urusi, kwa sababu wasipofanya mwezi huu hayatafanyika tena kwa mwaka wa tatu mfululizo. 
 
Hata hivyo, Musonye amesema kwamba watatoa ratiba nzuri ambayo haitaruhusu mashindano ya mwaka huu kuingiliana na mechi za Kombe la Dunia.  
 
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited, Tido Mhando alisema kwamba wataitumia michuano hiyo kukizindua kituo chao chao Redio, Uhai FM na akawahakikishia kwamba pamoja na mashindano hayo kufanyika sambamba na Kombe la Dunia, lakini yatafana 
 
FIFA imeridhia Kagame kufanyika mwezi huu tofauti na agizo lake la kutotaka katika mwezi wa Fainali za Kombe la Dunia yasifanyike mashindano mengine yoyote, kwa sababu washiriki watano wa michuano hiyo wapo kwenye hatua ya makundi ya michuano ya Afrika, ambayo kwa sasa imesimama kupisha Kombe la Dunia itarejea Julai baada ya kumalizika kwa michuano hiyo nchini Urusi.
 
Hao ni KCCA ya Uganda iliyopo Kundi A katika Ligi ya Mabingwa Afrika na nyingine nne kwenye Kombe la Shirikisho ambazo ni Gor Mahia ya Kenya, Rayon Sports ya Rwanda, Yanga ya Tanzania zilizopoi Kundi D zote na Al-Hilal ya Sudan iliyopo Kundi A.
 
Na kwa sababu hatua ya makundi ya michuano hiyo ya Afrika itakwenda hadi Agosti, mwezi ambao msimu mpya wa Ligi Kuu nyingi duniani huanza – michuano ya Kagame isipofanyika mwezi huu kuna hatari isifanyike tena na mwaka huu kwa mara ya tatu mfululizo.
 
Azam FC ndiyo mabingwa wa mwisho wa michuano hiyo ilipofanyika Tanzania, walipowafunga Gor Mahia 2-0 katika fainali Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam, mabao ya waliokuwa washambuliaji wake hatari, John Raphael Bocco dakika ya 17 na Muivory Coast, Kipre Herman Tchetche dakika ya 64.
 
Na hiyo ndiyo ilikuwa michuano iliyomtoa mshambuliaji Mkenya, Michael Olunga ambaye kwa sasa anachezea Girona FC ya Hispania kwa mkopo kutoka Guizhou Zhicheng ya China.
 
Baada ya kufungha mabao matano akiwa na Gor Mahia na kuibuka mfungaji bora akiwapiku , Osman Bilal Salaheldin wa Al-Khartoum ya Sudan aliyefunga mabao manne sawa na Tchetche wa Azam FC, Olunga akachukuliwa na Djurgardens IF ya Sweden mwaka 2016 iliyomuuza Guizhou Zhicheng mwaka 2017.
 
Na Tanzania itawakilishwa na Azam FC kama mabingwa watetezi wa mashindano na Yanga SC, kama mabingwa wa nchi.

Credit: Full Shangwe

Waziri Ataka Watoto Walioungana Kagera Wafikishwe Muhimbili Haraka

0
0
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Ummy Mwalimu amemwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera, kuhakikisha watoto waliozaliwa wakiwa wameungana wanafikishwa Muhimbili.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo leo bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo ambaye alihoji je serikali ina taarifa kuwa kuna watoto wamezaliwa Kagera wakiwa wameungana.

Akijibu swali hilo, Ummy amesema: “Wanaozaliwa wakiwa na maumbile ya ajabu wapelekwe hospitali.

“Na kuhusu watoto waliozaliwa wakiwa wameungana huko Kagera, namwagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera ahakikishe watoto hao wanafikishwa Muhimbili,”.

Spika Ndugai ‘ampokonya’ mwenyekiti uongozi baada ya wapinzani kuitwa mbwa

0
0
Spika Job Ndugai leo amelazimika kumpokonya Najma Giga uongozi wa kikao cha Bunge baada ya mzozo uliosababishwa na mbunge wa CCM aliyewafananisha wapinzani na mbwa.

Spika Ndugai alifanya kitendo hicho kisicho cha kawaida katika kikao cha 44 cha Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya mwaka 2018/19 ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Wakati akichangia, mbunge huyo wa Jang’ombe, Ali Omar alisema: “Ukiona majuha wanapongezana wakaona wamefanya la maana, kuna hawa mbwa kama tutawatoa itakuwa vizuri sana. Nasikia milio ya mbwa ukiwatoa itakuwa vizuri.”

Baada ya kauli hiyo, wabunge wawili kutoka Chadema, Joseph Selasini (Rombo) na Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini) walisimama kutaka utaratibu ufuatwe kwa mchangiaji kuomba radhi.

Hata hivyo, Giga hakuruhusu hilo na kusababisha wabunge wengine wa upinzani kupiga kelele wakimtaka mbunge huyo afute kauli hiyo.

Giga alitumia kama dakika mbili kuwazuia lakini hakuweza na kumtaka Omar aendelee kuchangia.

Hata hivyo hakuweza kuwazuia kutokana na wabunge hao wa upinzani kuendelea kupiga kelele wakisisitiza Omar ashinikizwe kufuta kauli yake.

Wakati kelele zikiendelea na utulivu bungeni ukitoweka, Spika Ndugai akaingia na kuchukua uongozi wa kikao na hivyo Giga, aliyeanza kuongoza kikao hicho tangu asubuhi, kulazimika kumuachia uongozi.

Credit: Mwananchi

Mbunge CUF ataka Maalim Seif ahojiwe TAKUKURU

0
0
Mbunge wa Konde (CUF), Khatib Ally amelitaka Bunge kuamuru, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ahojiwe na Taasisi ya Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa kutopeleka hesabu za fedha za chama kukaguliwa na CAG.

Khatib alitoa kauli hiyo leo bungeni wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka 2018/19.

“Hapa wote tumeng’ang’ania kwenye Sh trilioni 1.5 lakini mimi nataka zile Sh bilioni 200 zije Zanzibar. Leo nitakuwa tofauti kwa sababu nitapataje ujasiri wa kuhoji 1.5 trilioni wakati hesabu fedha za chama changu hazijapelekwa kwa CAG kukaguliwa?” amehoji.

Kutokana na hilo, amesema Katibu Mkuu wa Chama chake hajakitendea haki chama kwa kutopeleka mahesabu kwa CAG.

“Katibu Mkuu wangu ahojiwe na Takukuru kwanini hakupeleka hesabu za fedha zikaguliwe? Haya mambo yanataka ujasiri sana.

“Mheshimiwa Spika naomba kanuni inayomlinda mbunge inilinde maana isije ikaja kama ilivyowakuta wenzangu,” amesema.

Kutokana na hilo, Spika wa Bunge, Job Ndugai amemwmabia mbunge huyo kuwa katika jambo hilo wanamuunga mkono kwa kuwa ni la maana.

Waziri Mkuu Ampongeza Steven Masele

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele na kumuahidi kwamba Serikali itampa ushirikiano ili aweze kutimiza majukumu yake.

Ametoa ahadi hiyo leo (Jumanne, Juni 5, 2018) wakati akizungumza na Mheshimiwa Masele ofisini kwake Bungeni, Dodoma. Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuchaguliwa kushika wadhifa huo.

Amesema ushindi wake katika nafasi hiyo umelipa heshima kubwa Bunge na Serikali na kwamba wana matarajio makubwa kwa sababu uwepo wake, utaliongezea Taifa ushirikiano na nchi nyingine za Afrika.

"Matarajio kwa Bunge ni makubwa kwani kuna mambo ambayo tunataka ushirikiano na nchi nyingine za Afrika, hivyo uwepo wako ni muhimu katika kufanikisha utekelezaji wake."

Vilevile, Waziri Mkuu amewapongeza wabunge wengine wawili, Waheshimiwa David Silinde na Asha Abdullah Juma kwa ushirikiano wao uliochangia ushindi wa Mheshimiwa Masele.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Masele ambaye ni Mbunge wa Shinyanga Mjini, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano iliyompa na hatimaye kuibuka na ushindi huo.

Amesema ushindani ulikuwa mkali kutokana na uwepo wa mataifa mengi yaliyokuwa yakiwania nafasi hiyo. Aliahidi kutetea maslahi ya Taifa kwa muda wote atakaotumikia nafasi hiyo. “Nakuhakikishia Waziri Mkuu kwamba nitayalinda na kuyatetea maslahi ya Tanzania kwa muda wote ambao nitakuwa katika wadhifa huu,” alisema Mhe. Masele.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Jishindie Gari la Bure Toka Japan.....Kushiriki Ni Bure Kabisa


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya June 6

Atupwa Jela Mwaka Mmoja kwa Tuhuma za Kujiteka

0
0
Mahakama ya Mji wa Kampala nchini Uganda, imempata na hatia mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Amina Mirembe (23) baada ya kukiri kosa la kujiteka makusudi kwa lengo la kupima upendo kwa mume wake.

Gazeti la Daily Monitor, limeripoti kuwa mwanamke huyo amehukumiwa jana Juni 5, 2018 kwa kutoa taarifa za uongo kwa Polisi kuhusu kutekwa kwake na Hakimu wa Mahakama hiyo  Patrick Tulisana alimhukumu kwenda jela mwaka mmoja na kutoa kiasi cha shilingi za Uganda 300,000.

Mwendesha mashtaka wa serikali, Bi Lydia Batiibwe aliitaka Mahakama kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa Amina ili iwe fundisho kwa watu wanaotoa taarifa za uongo huku nchi hiyo ikikumbwa na matukio mengi ya kujiteka makusudi

Mei 26, 2018 mshtakiwa aliandika maelezo ya uongo kwa Askari Polisi ASP Moses Acaye, katika eneo la Ntinda na kudai alikuwa ametekwa na watekaji hao walikuwa wakitaka shilingi za Uganda 500,000

Nchini Uganda kumekuwa na matukio ya watu kujiteka na kudai fedha kutoka kwa watu wa karibu, mathalani Juni 4, 2018 makahama eneo la Kayunga, ilimpata na hatia Bi Rebecca Birabwa (32) kwa makosa ya kujiteka na alihukumiwa kifungo cha miezi sita jela .

Mkuu Wa Mkoa Mbeya Kuunda Tume Ya Kusimamia Na Kukagua Miradi Inayoendelea Mkoani Humo.

0
0
Mkuu wa mkoa wa Mbeya,Amos Makalla ameunda tume ya watu nane na kuipa jukumu la kutembelea na kukagua miradi yote ya maji iliyopo kwenye halmashauri za mkoani humo.
 
Lengo la kuundwa kwa tume hiyo ni kubaini ubora na mapungufu kwenye utekelezaji wa miradi ya maji kutokana na kile kinachotajwa kuwepo kwa miradi iliyojengwa chini ya kiwango.
 
Miongoni mwa miradi inayotarajiwa kukaguliwa ni pamoja na uliojengwa katika kijiji cha Kiwanja kata ya Mbugani wilayani Chunya ambao unalalamikiwa na wananchi kujengwa chini ya kiwango kwa ufadhili wa Benki ya Dunia(WB).
 
Akizungumza katika maeneo na nyakato tofauti wilayani Chunya,Makalla amesema tume hiyo itapitia na kukagua mradi mmoja baada ya mwingine na hakuna utakaoachwa katika halmashauri zote.
 
Aidha amewasihi wananchi kwenye maeneo yote ya mradi kutoa ushirikiano kwa Tume hiyo ili iweze kukamilisha kazi yake kwa ufasaha na kwa wakati na kuiwezesha Serikali kuchukua hatua baada ya kazi kumalizika.

Mkoa Wa Mbeya Umeagizwa Kutenga Mapato A Ndani Kwaajili Kuratibu Shughuli Zinazo Halmashauri Na Wilaya.

0
0
Halmashauri za wilaya mkoani Mbeya zimeagizwa kutenga bajeti kutoka vyanzo vya mapato vya ndani kwaajili ya Kuratibu shughuli za vyama vya ushirika na kuufanya ushirika kuwa agenda ya kudumu.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya,Amos Makalla ametoka agizo hilo kwenye Hotuba yake iliyosomwa na Kaimu katibu tawala wa mkoa,Costantine Mushi kwenye hafla ya kufunga Jukwaa la Vyama vya ushirika mwaka huu lililofanyika kwa siku mbili. 
 
Halmashauri zimetakiwa  kuhakikisha Elimu ya ushirika inatolewa kwa vyama vyote ili kuwezesha Ushirika kuwa endelevu sambamba na wananchi kutambua umuhimu
 
Pia kutoa agizo kwa kila Afisa ushirika kutekeleza majukumu kwa wakati hususani kwa kuwa karibu zaidi na vyama vya ushirika huku pia kwa watendaji wa vyama hivyo wakitakiwa kuwa waadirifu na wasioungana na viongozi wanaopenda kujinufaisha wao badala ya wanachama.

Kwa upande wa Mrajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika mkoa wa Mbeya,Bibi Angel Maganga amevitaka vyama vya ushirika kuandaa agenda za Kodi kwenye mikutano

Mashine Za EFD Zatengamaa

0
0
Wafanyabiashara wametakiwa kurejea kutumia mashine za kieletroniki (EFD) kwa kuwa hitilafu iliyokuwa imetokea imetatuliwa.

Kauli hiyo imetolewa bungeni jana jioni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango wakati akijibu hoja za wabunge waliochangia kwenye bajeti ya wizara yake.

“Baada ya kutokea hitilafu iliyosababisha kifaa kilichokuwa kinatunza na kuchakata taarifa za wafanyabiashara kuharibika tayari imetatuliwa na wataalamu wetu wa teknolojia na mawasiliano.

“Tangu Juni Mosi mwaka huu wataalamu walifanikiwa kurejesha kwenye hali ya kawaida na kufanya kazi kama awali.

“Tatizo lililotokea kwa kujua au kwa kusudi, hata baada ya mfumo kurudi katika hali ya kawaida baadhi ya wafanyabiashara walizima mashine zao.

“Wito wangu kwa wafanyabiashara warejee kutumia mashine za EFD na tangu jana nimetoa maagizo kwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) nchi nzima kuwatembelea wafanyabiashara wote kama mashine zao zinafanya kazi,” amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images