Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wabunge CCM Wammwagia Sifa Rais Magufuli Bungeni

$
0
0
Wabunge wa CCM wamempongeza Rais John Magufuli anavyoshughulikia sekta ya madini ikiwamo kuzuia usafirishaji wa mchanga wa madini ya dhahabu ‘makinikia’ nje ya nchi.

Wabunge hao Goodluck Mlinga (Ulanga) na Sixtus Mapunda (Mbinga Mjini) wamesema hayo leo Juni 1, 2018 bungeni wakati wakichangia bajeti ya madini ya mwaka 2018/19.

“Nampongeza Rais (Magufuli) kwa kuzuia makinikia kupeleka nje ya nchi, Tanzania ni nchi ya nne kwa uzalishaji wa dhahabu kwa nchi za Afrika na duniani. Katika nchi matajiri wa uzalishaji wa mali tupo lakini mafanikio ya wananchi na Serikali tuko chini,” amesema Mlinga.

Amesema anampongeza Rais kwa kujenga ukuta katika mgodi wa Mirerani kwani ni madini adhimu.

“Tanzania ni nchi ya nne kwa uzalishaji wa gesi katika bara la Afrika. Lakini katika nchi masikini tupo,” amesema.

Akiendelea kuchangia, Mlinga amesema, Rais anapaswa kufanya mabadiliko katika wizara ya madini kwani watendaji wake wamesababisha haya.

Naye Mapunda amesema alichokifanya Rais ni jambo kubwa kwani tuna madini mengi lakini yalikuwa hayatunufaishi.

“Tuko katika mpito kutengeneza mfumo bora wa kutunufaisha na yote yanahitaji ushirikiano na kupeana moyo. Biashara ya dhababu ni ya familia kubwa na jinsi ya kuiingia inahitaji kutumia ubongo mkubwa sana,” amesema Mapunda na kuongeza:

“Ili kuingia kupambana nao inahitaji kuwa na mfumo mzuri na Serikali inapoanza kutengeneza sheria, hawa hawawezi kukubali, lazima watatuhujumu.”

Waziri wa Elimu avurugwa na Kwaya ya Utupu ya Wanafunzi

$
0
0
Waziri wa Elimu Nchini Afrika Kusini, Angie Motshekga amesikitishwa na kwaya ya kundi moja la wanafunzi ambao wamekuwa wakiimba wakiwa watupu.

Amesema kuwa amesikitishwa sana baada ya kuona kanda ya video ya wasichana hao wa Xhosa wakicheza densi yao huku wakiwa wamevalia nguo inayojulikana kama “inkciyo”.

Aidha, Waziri huyo amesema kuwa ni ukosefu wa heshima kwenda kinyume na maadili ya tamaduni za taifa hilo hasa kwa watoto wa kike.

“Tabia hiyo mbaya sana inaenda kinyume na maadili ya tamaduni zetu, mtoto wa kike anafaa kuthaminiwa na si kufundishwa mila potofu,”amesema Waziri Motshekga

Hata hivyo, mkufunzi wa Kwaya hiyo ya wanafunzi amesema kuwa ni fahari kubwa kucheza densi ya kitamaduni ya Xhosa huku wasichana wakiwa watupu.

Hakimu Atoa Ahirisho la Mwisho Kesi ya Halima Mdee

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa ahirisho la mwisho katika kesi ya kutumia lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli  inayomkabili mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee.

Akizungumza leo Ijumaa Juni 1, 2018 Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ametoa ahirisho hilo la mwisho kwa upande wa mashtaka baada ya wakili wa Serikali mwandamizi, Patrick Mwita kudai kesi ilipangwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa, hawana shahidi ikiwa ni mara ya tatu.

Baada ya kutolewa maelezo hayo, hakimu Simba alitoa ahirisho la mwisho na kupanga kesi hiyo kusikilizwa tena Juni 29, 2018 kwa mashahidi wa upande wa mashtaka kuanza kutoa ushahidi.

Katika kesi hiyo Mdee anadaiwa kufanya kosa hilo Julai 3, 2017 Makao Makuu ya Chadema yaliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni.

Anadaiwa kutamka “anaongea hovyo hovyo, anatakiwa afungwe breki” kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Halima alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Julai 10, 2017. Katika kesi hiyo mbunge huyo  anatetewa na mawakili, Peter Kibatala, Jeremiah Mtobesya na Hekima Mwasipu.

Serikali yasema Tanzanite One imefanya malipo ya awali...Yazungumzia Pia Suala la Barrick

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kampuni ya madini ya Tanzanite One imeshailipa Serikali malipo ya awali ambayo hayatawekwa wazi.

Amesema mbali na malipo hayo, mazungumzo kati ya kampuni ya kuchimba madini ya Barrick na Serikali yanaendelea vizuri na katikati ya Juni na Julai, 2018 watakuwa wamefikia hatua za mwisho.

Profesa Kabudi ameeleza hayo leo Ijumaa Juni 1, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Madini ya mwaka wa fedha wa 2018/19.

Amesema mazungumzo kati ya Serikali na Tanzania One  yalikamilika Aprili 15, 2018.

“Wamekili na kulipa kodi na tozo zote na watatoa fidia na tayari malipo ya kwanza wamelipa. Tunaishi kwa kujifunza, tukitaja watajua wanaotudai watafungua kesi zingine,” amesema.

“Lakini ndani ya Serikali Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) atajua na zinasimamiwa na Katiba Mkuu Kiongozi na tumejifunza hatutatamka katika kadamnasi, ni upuuzi kusema na tukisema watafungua kesi nyingine.”

Kuhusu Barrick amesema mazungumzo hayo yaliyoanza Oktoba 19, 2017 yamekuwa na tija kwa madini hayo kunufaisha nchi kwa kizazi cha sasa na kijacho.

“Kuangalia Tanzania ya kesho ya madini, tumerithi mikataba iliyokuwa na matatizo, makubaliano yalikuwa ya msingi na yanaendelea vizuri kati ya Serikali na Barrick na mwisho wa Juni au Julai tutakuwa tumefikia hatua za mwisho,” amesema.

Amesema lengo ni Serikali kuzungumza na kampuni mbalimbali za uchimbaji madini ili nchi kunufaika na rasilimali hizo, kwamba utaratibu wa sasa leseni zitatolewa kwa masharti ya baraza la mawaziri na kusisitiza kuwa asiyetaka asije nchini kuwekeza.

Mahakama yawaachia huru Wakurugenzi Jamii Forums

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao wa Jamii Forums, Maxence Melo na Mwanahisa wa mtandao huo, Micke William kwa sababu hawana kesi ya kujibu.

Viongozi hao, wameachiwa huru na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi 6 wa upande wa mashtaka na kuona ushahidi uĺiotolewa una mashaka na kwamba hauna mashiko.

“Nawaachia huru washtakiwa kwa sababu ushahidi uliotolewa hauna mashiko,” amesema Mwambapa

Katika kesi hiyo namba 457 Melo na Mushi wanadaiwa kulizuia jeshi la polisi kufanya uchunguzi wake, kinyume na kifungu namba 22 (2) cha Sheria ya Makosa ya Mtandao Namba 14 ya mwaka 2015.

Watuhumiwa wanadaiwa kushindwa kutoa taarifa kuhusu mmiliki wa akaunti moja iliyosajiliwa JamiiForums huku wakijua kwamba jeshi hilo linafanya uchunguzi wa makosa ya jinai yaliyochapishwa kielektroniki kwenye tovuti hiyo.

Tazama Hapa Taarifa Muhimu Toka IKULU Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. John Magufuli amemteua Prof Andrew Barnabas Pembe kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi kupitia Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa imesema kuwa uteuzi wa Prof. Pembe umeanza siku ya leo.

Kabla ya uteuzi huo Prof. Pembe alikuwa Mhadhiri  na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia taaluma, utafiti na ushauri.

Waziri Mkuu: ”Nahitaji maelezo yenu mpaka saa 12 jioni ...Mkishindwa Ondokeni”

$
0
0
SERIKALI imesema hairidhiki na ubia unaoendeshwa kwenye Kiwanda cha Nguo cha Urafiki.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo jioni (Ijumaa, Juni mosi, 2018) wakati akizungumza na mamia ya wafanyakazi wa kiwanda hicho mara baada ya kukagua mitambo mbalimbali kwenye kiwanda hicho.

“Serikali haturidhiki na ubia huu, na huyu mbia aelewe kwamba Serikali haturidhishwi na ubia huu wala kinachoendelea hapa kiwandani,” amesema huku akishangiliwa kwa nguvu na wafanyakazi wa kiwanda hicho.

Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage aongoze kikao baina ya wabia hao na menejimenti ya kiwanda na apewe taarifa hiyo leo saa 12 jioni baada ya kufuturu.

“Ubia wenu hauna tija. Kwa hiyo wewe Msajili wa Hazina na huyo mwekezaji, nikitoka hapa, mbaki mfanye kikao na mnipe majibu leo saa 12 jioni. Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Mkuu wa Mkoa muongoze mjadala huo na nikitoka kufuturu mniambie maazimio yenu, na kama haiwezekani, mvunje kabisa ubia huo ili tujue hatuna mbia tutafute mbia,” amesema.

Waziri Mkuu amesema wabia wakuu wa kiwanda hicho ni Msajili wa Hazina na kampuni ya Changzhou State owned Textile Assets Operations kutoka China na kwamba Serikali ilipoamua kukaribisha uwekezaji ilitarajia kupata mtaji, teknolojia na ajira za kutosha lakini hali ya sasa ni kinyume kabisa.

“Hatuwezi kuvumilia, tunasema tuna mbia mwenye mtaji, hakuna mtaji; tulisema tunataka mbia mwenye kuleta teknolojia mpya, hakuna teknolojia; tulisema aendeshe shughuli hii kukiwa na ajira endelevu, hizo ajira hakuna; halafu tubaki tunamwangalia tu. Bora atuambie amekwama, aondoke, tutangaze vinginevyo,” amesema.

“Tulikopa mtaji lakini Tanzania hizo hela hazijaja, tunataka majibu ya fedha hizo; kama fedha iliyokopwa kwenye Benki ya Exim ya China ingeletwa nchini tungeweza kuziba mapengo na kusaidia kiwanda kiweze kufanya kazi. Sasa kwa sababu fedha hiyo haijaja nchini, tunataka maelezo fedha hiyo iko wapi?” amesisitiza.

“Mitambo iliyonunuliwa na mwekezaji miaka mitano au sita iliyopita haifanyi kazi tangu ilipoletwa nchini, nataka majibu, je mitambo hii ilinunuliwa ikiwa mizima au vipi; na tena mmeng’oa mashine kwenye ma-godown matatu, nimeambiwa mlikuwa na nia ya kuleta mashine mpya, lakini sasa ni miaka mitano, je mashine zile zote zimeenda wapi, na kama mmeuza ameuziwa nani? Mkae mjadili na leo hii mniletee majibu yote haya,” amesisitiza.

Waziri Mkuu amesema kiwanda hicho ni matokeo ya urafiki wa China na Tanzania na kina historia ndefu na mahusiano ya muda mrefu. “Asiingie mtu akatuharibia, na tunataka mahusiano yetu na China yaendelee. Amesema baada ya kupokea taarifa hiyo, Serikali itakaa na Balozi wa China ili itafutwe suluhisho.

Waziri Mkuu amewataka watumishi wa kiwanda hicho walioko likizo na wale waliopo kazini wawe wavumilivu wakati Serikali ikiendelea kutafuta dawa ya matatizo yao.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amemtaka Meneja Rasilmali Watu na Utawala wa kiwanda hicho, Bw. Edwin Nkwanga aandae orodha ya watumishi wote yenye kuonyesha kila mtumishi analipwa nini na aifikishe kwake haraka.

“Hapa kuna watu wanalipwa sh. milioni saba hadi 10 na wengine wanalipwa sh. 120,000. Niletee orodha yenye kuonyesha jina, cheo na kiwango cha mshahara, lakini pia uonyeshe anapata stahili zipi, kama ni posho ya nyumba, maji au umeme,” amesema.

Amesema nia ya Serikali ni kutaka kupanga upya mishahara yao ili waweze kupatikana watumishi wa kutosha.

Wakati akikagua kiwanda hicho, Waziri Mkuu alielezwa kwamba kuna mashine 88 ambazo ziling’olewa kwenye kiwanda hicho na hazijulikani zimepelekwa wapi.

Mapema, akitoa taarifa fupi ya kiwanda hicho, Naibu Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Shadrack Nkelebe alisema kiwanda hicho kimesimamisha uzalishaji tangu Desemba 2017 ili kufanya ukarabati na kimeshindwa kuendelea nao kwa sababu ya madeni.

“Kiwanda kilikuwa na watumishi 3,000 lakini sasa hivi wamebakia 726 baada ya wengine kupunguzwa na kulazimishwa kwenda likizo licha ya teknolojia kubakia ni ileile. Kiwanda kinakabiliwa na changamoto nyingi lakini kwa sehemu kubwa ni za kutengeneza. Tumepigana vita katika kujenga uchumi wa Taifa kupitia kiwanda hiki, lakini tumekwama. Tunahitaji nguvu ya ziada ili tutoke hapa,” alisema.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Wizara Yalaani Vitendo Vya Ukatili Wa Kijinsia Vinavyoshamiri Nchini

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalaani na kukemea matukio ya ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake yaliyotokea hivi karibuni katika Mkoa wa Dodoma  Pwani na Mwanza.

Wizara imepokea taarifa za ukatili kwa wanawake hao kwa mshituko makubwa, na ina kemea vitendo hivyo vya ukatili maana ni ukiukaji wa Haki za Msingi za binadamu.

Matukio hayo yaliyotokea Dodoma Pwani na Mwanza ni tukio la Mei 26 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) Rose Malfred (31), mkazi wa Swaswa aliyeuawa kikatili na mumewe ambaye inadaiwa kuwa ni Mchungaji wa Kanisa la TAG Bw. John Mwaisango, kwa kumchoma visu sehemu mbalimbali za mwili hadi kufa. 

Tukio linguine lilitokea Mei 25, mwaka huu, ambapo mwili wa Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Rosemary Mgombela, ulikutwa umefukiwa pembeni ya nyumba wanayoishi.

Aidha, tukio lingine lililoripotiwa Aprili 30, mwaka huu ni la mfanyabiashara wa samaki mkazi wa mtaa wa Mahakama wilayani Ilemela, Bw.Nicholas Light (25) ambaye alimuua mpenzi wake, Victoria Swai (26) kwa kumnyonga na kumkaba shingo kwa wivu wa mapenzi.

Matukio hayo yote ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,ya mwaka 1977 inayoeleza bayana haki ya kuishi kwa kila raia, Ibara ya 14 ya Katiba hiyo imeeleza kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa Sheria.

Wizara inapenda kuchukua fursa hii kuiasa jamii kutoa taarifa kwa vitendo vya ukatili kwa wanawake katika jamii ili kudhibiti matukio ya ukatili hususan mauaji ya wanawake ambao unafanywa na watu waovu na kusababisha hofu kubwa katika jamii.

Wizara inaikumbusha jamii kuwa udhibiti wa vitendo vya ukatili kwa wanawake na vitendo vingine viovu vinahitaji  juhudi za pamoja katika kuvitokomeza; ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushiriki wa wananchi katika kuripoti vitendo vya ukatili.

Tunaliamini Jeshi la Polisi kwa umakini wake na kwamba litahakikisha linasimamia Sheria ili iweze kuchukua mkondo wake kwa wale wote waliohusika na kufanya vitendo vya ukatili kwa wenza wao  ili iwe Aidha, fundisho kwa wengine.

Taarifa MUHIMU Toka Bungeni Dodoma Leo

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 2

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aiagiza Tamisemi Kutenga Maeneo Maalumu Ya Wamachinga

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya wafanyabiashara wadogowadogo (Wamachinga) ili waweze kufanya biashara zao bia bughdha yoyote.

Maagizo hayo yametolewa Jijini Dodoma kwa niaba yake na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Shirika la Umoja wa Machinga (SHIUMA) na kuongeza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa wafanyabiashara hao wanashiriki kukuza biashara zao na pato la Taifa.

Dkt. Kijaji alisema kuwa wamachinga na wajasiriamali wengine wanapokosa maeneo maalumu ya kufanyia biashara zao inakuwa vigumukupata mikopo kutokana na kutotambuliwa, hivyo Sekta za Fedha zikiwemo Benki kuwa na wasiwasi na urejeshwaji wa Fedha hizo hivyo hatua ya kuwatambua itasaidia kutatua changamoto hiyo.

 “Tanzania inatarajia kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda ifikapo mwaka 2025 na wafanyabiashara wakiwemo wamachinga ndio watakaowezesha kufikia lengo hilo kwa kulipa kodi, hivyo Serikali inachokifanya inaweka mazingira mazuri ya kazi kwa wafanya biashara”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa baada ya maombi ya muda mrefu ya Wamachinga kutaka kutambuliwa, Serikali katika Sheria ya fedha ya mwaka 2017/18 imeanza kutekeleza maombi hayo kwa kuhakikisha wanatambuliwa na kupewa vitambulisho vya Taifa kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kurahisha utendaji kazi wao hasa na Sekta ya Fedha kwa kupata mikopo.

Dkt. Kijaji ameipongeza Benki ya NMB ambayo imeendelea kukutana na kuwafadhili wafanyabiashara wadogo ukiwemo Mkutano huo wa SHIUMA kwa kuwa wanatekeleza kwa vitendo azma ya Sekta ya Fedha kuwafikia wananchi wa hali ya chini

Aidha, alirejea pongezi zake kwa baadhi ya benki hapa nchini ikiwemo NMB, CRDB na ABC kwa uamuzi wao wa kushusha riba za mikopo yao na kueleza matumaini yake kwamba wamachinga na wajasiriamali wengine watachangamkia fursa za mikopo hiyo.

Alisema Desemba, 2017 Serikali ilizindua Sera ya huduma ndogo za Fedha itakayowezesha kutambua Taasisi zote ndogo za Fedha zinazokopesha wananchi ili ziweze kuzingatia kanuni za utawala bora zitakazosaidia wafanyabiashara wadogo kukopa kwa kufuata sheria ili kuondoa kudhurumiwa.

Aidha amewapongeza wanachama wa SHIUMA kwa kuanzisha umoja wao utakaosaidia Serikali kupeleka huduma kwa urahisi na kwa usahihi kwa manufaa ya wafanyabiashara na Taifa kwa ujumla na akaahidi kuwa Serikali ipo pamoja nao kwa kuwa ni Serikali inayojali wanyonge.

Akizungumza kwaniaba ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Nchini-IGP Simon Sirro, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Kipolisi ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi-Lazaro Mambosasa, amewapiga marufuku watu wote wanaopora mali za wamachinga nchi nzima.

Alisema kuwa Jeshi lake litawachukulia hatua kali wale wote watakaojihusisha kwa namna moja au nyingine kunyang’anya ama kutaifisha bidhaa za wafanyabiashara wadogowadogo popote pale kwa kuwa vitendo hivyo havikubaliki.

 “Watu wote waliokuwa wanajipatia mali za wamachinga kwa kuwanyanganya bila kupeleka kwenye Mamlaka husika na badala yake wanauza na kutumia huoni unyang’anyi na atakayefanya hivyo atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Alisema Umoja huo wa wamachinga usikubali kushawishiwa kwa nia ovu na watu na baaada ya kujinufaisha binafsi wanawaacha wafanyabiashara hao bila chochote.

Mwenyekiti wa Shirika la Umoja wa Machinga Bw. Ernest Masanja alisema kuwa Wanaunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuwa imeonesha nia ya kuwajali wanyonge hasa wamachinga.

Bw. Masanja alisema katika Mkutano huo wameazimia kushirikiana na TRA wakati wa kutoa semina kuhusu namana ya kulipa kodi na pia wanachama wa vikundi vyote vya wamachinga vilivyo sajiliwa wapewe vitambulisho vya Taifa ili wasajiliwe na Mamlaka hiyo.

Naye Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dodoma Bw. Peter Kundy alieleza kuwa mpaka sasa kwa Wilaya ya Dodoma Mjini, zoezi la Uhakiki na uandikishaji kwa ajili ya vitambulisho vya Taifa imefanyika kwa kata 41 na zimesalia 6 pekee na zoezi lililobaki ni kutoa pingamizi kwa wasio stahili ili ifikapo Desemba zoezi hilo la utoaji vitambulisho litakuwa limekamilika.

Alisema  zaidi ya watumishi mia tano kutoka Idara ya Uhamiaji wamepelekwa nchi nzima ili kuharakisha zoezi la upatikanaji wa vitambulisho hivyo ili kusaidia katika upatikanaji wa mikopo katika sekta za fedha, elimu, afya na hata hati za kusafiria nje ya nchi kwa ajili ya shughuli za uchumi.

Shirika la Umoja wa Wamachinga (SHIUMA), limeanzishwa hivi karibuni likiwa na lengo la kuwaunganisha wafanyabishara wadogo wadogo nchini kote.

Rais Magufuli Kamteua Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini na Kamishna wa Madini

Rais Magufuli Ateua Majaji wa Mahakama ya Rufani

Tundu Lissu Ampinga Spika Ndugai Sakata la Ripoti ya Uvuvi na Gesi Asilia

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amefunguka na kuwataka Wabunge wenzake bila ya kujali itikadi ya vyama vyao kutoshiriki kwenye hafla ya kupokea na kukabidhi taarifa za kamati maalum za kuchunguza na kushauri sekta ya Uvuvi wa bahari kuu na Gesi asilia iliyopangwa kufanyika kesho.

Lissu ametoa kauli hiyo jana mchana kupitia ukurasa wake wa kijamii mara baada ya Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuutarifu umma kuwa Juni 2, 2018 Spika wa Bunge Job Ndugai atapokea ripoti hizo ambazo zimepangwa kufanyikia katika viwanja vya Bunge mbele ya lango kuu la kuingilia.

Kutokana na hilo, Lissu amedai kitendo hicho ni kinyume na zinaharibu taratibu za kisheria kwa kuwa taarifa za uchunguzi za Bunge huwa zinawasilishwa bungeni tena mbele ya wabunge wote na kujadiliwa endapo itahitajika kabla ya kukabidhiwa serikalini.

"Nawaomba Wabunge wasikubali kushiriki katika maziko haya ya mamlaka ya kikatiba na kikanuni ya Bunge. Wadai taarifa hizi ziwasilishwe kwanza bungeni na kujadiliwa na wabunge, kama Spika Ndugai na watu wake wasipokubali kufanya hivyo, basi nawashauri wabunge wote wasusie hafla hiyo", amesema Lissu.

Pamoja na hayo, Lissu ameendelea kwa kusema "wabunge watakaoshiriki hafla wajue, au waambiwe, kwamba wanashiriki kwa ushiriki au uwepo wao katika mazishi ya mamlaka ya kikatiba ya Bunge ya kuisimamia na kuishauri serikali kwa kupitia majadiliano bungeni. 

"Kwa utaratibu huu, Bunge halitajadili, na watanzania hawataona wala kusikia tena taarifa za kamati za uchunguzi za Bunge kama zile za Richmond wa Bunge la Spika Sitta na Operesheni Tokomeza na Tegeta Escrow wakati wa Bunge la Spika Anna Makinda". ​

Kwa upande mwingine, Lissu amesema hakuna kanuni ya Bunge inayoruhusu Kamati yoyote ya Bunge kupeleka taarifa yake serikalini moja kwa moja, bila kupitia bungeni na kujadiliwa na wabunge.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Iletiba Sahihi Ya Matatizo Haya Chanzo Chake Na Visababisho Vyake.

DALILI;mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu au gololi kama mavi ya mbuzi. misuli ya uume kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. miguu kuuma na kuwaka moto.

 TIBA YAKE; 4mix ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizo hayo inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kufanya urudie tendo la mara tatu bila kuchoka. 

LUKUBA 3 pump; ni dawa inayorefusha na kunenepesha uume hadi inchi 7 hadi 9 na kunenepesha kwa CM 2 na kukupa umbile la uhakika. ITUMIE TIBA HII KUOKOA NDOA YAKO NA KUOKOA KUKIMBIWA NA UMPENDAYE,

 ISABILO; Ni dawa itoayo mafanikio na utajili kwa watu walioshindwa kufanikiwa kimaisha, 

MWITE; Ni dawa ya mvuto kumvuta umpendaye na kumrudisha aliyembali na atakutimizia ahadi zote awe mwanamke au mwanaume. 

LUTA CD; Ni dawa inayotibu magonywa nyemelezi yanayopunguza kinga za mwili na kusababisha mwili kuzoofu na inaondoa miwasho na kuondoa kemikali na taka zinazozagaa mwilini. 

KISUKARI; Tunayo dawa ya DAYON inayotibu na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenye tatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari, kwani husababisha misuli ya mwili kutokufanya kazi vizuri

MPIGIE DR DAGOTIMAN NDIYE SULUHISHO LA MATATIZO YAKO 0754372325/  0658920640
 
HUDUMA HII INAWEZA KULETWA POPOTE ULIPO OFISI ZETU ZIPO MBAGALA ZAKHEM DAR ES SALAAM.

Robert Kaseko Mjumbe wa Kamati ya Siasa CCM Atembelea Kukagua Miradi Mbalimbali ya Chama Hicho Longido

$
0
0
Jana nimepata nafasi ya kutembelea na kujionea utekelezaji wa ilani ya CCM Wilayani Longido ambayo ni wilaya ninayoiwakilisha kama Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya  Halmashauri  Kuu ya CCM  Mkoa wa Arusha.Nilitembelea  baadhi ya Miradi inayotekelezwa na Serikali Wilayani humo;     

1.Mradi Mkubwa wa Maji Longido.
Mradi Huu Utaigharimu Serikali Kiasi cha Fedha TZS Bilioni 15.8 hadi kukamilika kwake. Chanzo chake ni Mto Simba huko Wilayani Siha Mkoa wa Kilimanjaro. 

Uzinduzi na uwekaji jiwe la msingi  ulifanywa na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa mwezi Septemba, 2017. Mradi huu unasimamiwa na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Arusha ( AUWSA ) na kwa hakika Maendeleo ya Utekelezaji wake ni Mazuri, inaridhisha. 

Kukamilika kwa Mradi huu Mkubwa wa Maji utaondoa Changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji kwa wanaLongido ambapo mradi huo utakuwa na uwezo wa kuzalisha Lita 2,160,000 za maji wakati mahitaji ya sasa ni Lita 1,462,000 tu. 

Nichukue nafasi hii kuipongeza sana Serikali ya Rais John Pombe Magufuli juhudi inazochukua ili kupunguza ama kuondoa Changamoto ya Upatikanaji wa Maji na kumtua mama wa kitanzania  ndoo ya maji kichwani.

 2. Mradi wa Ujenzi wa Kituo Kikubwa kipya cha Huduma za Afya  Eworendeke kata ya Namanga.
Nimetembelea  Mradi huu wa ujenzi wa  Kituo Kikubwa   cha afya  utakaogharimu Fedha za kitanzania zaidi ya  TZS Milioni 800 hadi kukamilika kwake na zaidi ya Milioni 450 zimekwisha tumika na ujenzi unaendelea.

Nimeridhishwa na maendeleo ya Utekelezaji wake na baada ya kukamilika kwake wananchi wa Namanga na maeneo ya jirani watapata huduma  zote muhimu ikiwamo Huduma kwa wakinamama wajawazito & watoto, huduma ya X- ray, Ipasuaji n.k  

Wananchi hawatakwenda tena umbali mrefu kutafuta huduma za afya ambapo hulazimika kwenda nchi jirani ya kenya na maeneo mengine umbali mrefu ili tu kupata huduma za afya. Hongera nyingi sana kwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuboresha huduma za afya.

3. Uboreshaji wa Huduma za Afya Kituo Cha Afya Longido Mjini.
Nikiwa na Katibu wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ( UVCCM) Wilaya ya Longido Comrade Isaya Mollel baada ya kupokelewa na Kaimu Mganga Mkuu Dr. Jisabo Ngasa  tumetembelea Kituo Cha Afya Longido na kujionea utoaji wa huduma za afya Pamoja na kujionea Jengo jipya la huduma  ya  X- Ray na tayari ujenzi umekamilika na Mashine ya X- Ray ipo kwenye jengo hilo ikisubiri kufungwa ( Installation )  tu na mara baada ya kufungwa itaanza kutoa Huduma mara moja na  kuondoa changamoto iliyokuwepo awali ambapo huduma hii ilikihitajika ilikuwa ni mpaka mgonjwa asafirishwe Arusha mjini au nchini jirani ya Kenya. 

Pia Niwapongeze sana wadau wa Maendeleo Nchini hususani " Ngorongoro Conservation Area" kwa kujitolea kununua Jenereta mpya kubwa kwa ajili ya kuondoa/Kupunguza tatizo la Umeme pindi unapokatika.  Naipongeza sana Serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais Magufuli kwa kuendelea kuboresha Huduma za afya kwa watanzania na hivyo kupunguza vifo vinavyoweza epukika.

HAPA KAZI TU,  TUKUTANE KAZINI.
 
Robert PJN Kaseko
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha.
Juni 01, 2018

Rais Magufuli awapandisha vyeo Maafisa 9 wa Magereza

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa 4 wa Jeshi la Magereza kutoka Naibu Kamishna wa Magereza (Deputy Commissioner of Prisons – DCP) hadi kuwa Kamishna wa Magereza (Commissioner of Prisons – CP).

Pia amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Magereza wengine 5 kutoka Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (Senior Assistant Commissioner of Prisons – SACP) hadi kuwa Naibu Kamishna wa Magereza (Deputy Commissioner of Prisons – DCP).

Maafisa waliopandishwa vyeo kutoka DCP na kuwa CP ni wafuatao
  •    Hamis Ngarama
  •     Tusekile Mwaisabila
  •     Augustine Sangalali Mboje
  •     Gideon Marco Nkana
Maafisa waliopandishwa vyeo kutoka SACP na kuwa DCP ni,
  •    Julius Mayenga Sang’udi
  •     Afwilile Mwakijungu
  •     John William Masunga
  •     Phaustine Marint Kasike
  •     Joram Yoram Katungi
j

Hamisa Kachoka......Kamtaka Diamond Awaambie Ndugu Zake Waache Dharau na Wamheshimu

$
0
0
Mwanamitindo Hamisa Mobetto ambaye ni mama mtoto wa Diamond Platinumz amefunguka kupitia ukuraasa wa Instagram wa Baba mtoto wake, Diamond Platinumz mara baada ndugu wa msanii huyo kuongea maneno yaliyoonesha kumkejeli.

Kufuatia maneno hayo ambayo yamezagaa katika mtandao wa Instagram Hamisa ameibuka na kuandika waraka mzito akimtaka Diamond Platinumz kuoa mwanamke ambaye ndugu, maneja na mashabiki wa Diamond wanamtaka aoe kwani katika andiko lake ameonesha kukerwa na baadhi ya maneno yaliyoongelewa katika mitandao ya kijamii kuhusu yeye mara baada ya wimbo wa Iyena kutoka.

Ambapo katika wimbo huo Diamond ameonekana akifunga ndoa na aliyekuwa mpenzi wake na mama watoto wake Zarinah Hassan.

Ndo uoe Huyo Mwanamke ambae anatakiwa na Ndugu zako … na manager zako bila kusahau mashabiki … sio kutwa mie mtoto wa watu naandamwa na kukaliwa mie kooni!!! Sijakuita wala kukufunga kamba ……

Kila siku maneno mimi Kwani alishindwa kukufata kukushauri ? Mpaka akimbilie kwenye MaTv na Mitandao ? Unapokaa hapajui , number ya simu yako pia hana? …. kwani mie hayo maTv hayaombi kuniombi kunihoji mbona nakaa kimya ? Tena saa ingine nakaa Kimya kuwastiri kwa mengi na pia dee akikua asione hii migogoro lakin ndugu zako hawabebeki its too much 🙌🏽 talk to Your familia maana wewe ni mwananume na uwezo wa kuyamaliza ……… 

Na pia waambie unahitaji Mke sio House girl wa Nyumba🤚🏽… Mwanamke kazi yake kukupikia Ule , au nlikua sikupikii tena sio wewe tu na Ndugu zako mkala na kusaza ? … leo imekua hamisa hajui kupika kusafisha nyumba kwahiyo chumba chako tukimaliza lalana huwa anasafisha nani ? 

Au walitaka niende kuwafulia vyupi vyao nikimaliza niwapigie deki mpaka chumbani kwao ? Wakishindwa kuniheshimu basi waambie waheshimu damu yako . The End !

Mobeto amefunguka hayo kufuatia post mbalimbali zilizokuwa zikitumwa na watu wa karibu wa Diamond Platinumz wakidai kuwa wamemkumbuka sana Zari hivyo wanataka arudi ili ndoa iweze kufungukika.

Wimbo wa Iyena pamoja na mistari yake umewaibua watu wengi na mashabiki wengi ambao wameonekana kumshambulia kwa maneno mwanadada Hamisa Mobetto.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images