Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Rais Magufuli Aishukuru Saud Arabia Kwa Msaada wa Kujenga Chuo cha Kiislam Nchini

Mahakama Moshi yapokea hoja tisa kesi ya Bilionea Msuya

$
0
0
Mawakili  wa utetezi katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara tajiri wa madini ya tanzanite ‘Bilionea’ Erasto Msuya (43), jana walitumia saa nne na nusu kuwasilisha hoja tisa za majumuisho kwa lengo la kuonyesha mahakama kuwa wateja wao hawana hatia.

Hoja hizo zilizowasilishwa katika Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi chini ya Jaji Salma Maghimbi anayesikiliza shauri hilo namba 12 la mwaka 2014, zilijikita zaidi kuhoji utaratibu mzima wa ukamataji washtakiwa.

Jaji Maghimbi alianza kusikiliza hoja za upande wa utetezi jana saa 4:08 asubuhi hadi saa 7:32 mchana alipoahirisha kwa muda usikilizaji wake hadi saa 7:45.

Washtakiwa walioonekana wana kesi ya kujibu ni mshtakiwa wa kwanza Sharif Athuman (35), ambaye ni mfanyabiashara wa madini na mchimbaji mdogo, mkazi wa Kimandolu mkoani Arusha, mshtakiwa wa pili Shaibu Saidi maarufu kama Mredii (42), mkazi wa Songambele, Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara na mshtakiwa wa tatu Mussa Mangu (34), mkazi wa Shangarai kwa Mrefu.

Wengine ni mshtakiwa wa tano Kihundwa, mkazi wa Lawate, Wilaya ya Siha, mshtakiwa wa sita Sadiki Jabir a.k.a Msudani (36), mkazi wa Dar es Salaam na Lang’ata, Wilaya ya Hai, na mshtakiwa wa saba Alli Musa maarufu Majeshi, mkazi wa Babati, mkoani Manyara.

Aliyekuwa mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo iliyobaki na washtakiwa sita, Jalila Said (32) mkazi wa Babati aliachiwa huru Mei 14 baada ya Jaji Maghimbi kuona ushahidi uliotolewa dhidi yake haumgusi kiasi cha kufanya awe na kesi ya kujibu.

Msuya, aliuawa kwa kupigwa risasi 22, Agosti 7, 2013, majira ya saa 6:30 mchana katika eneo la Mijohoroni, kando ya barabara kuu ya Arusha-Moshi, karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Mawasilisho ya uchambuzi wa hoja hizo yaliyofanywa na Wakili Majura Magafu katika waraka wenye kurasa 34, ulijikita zaidi kwenye uchambuzi wa mkanganyiko wa tarehe halisi za ukamataji wa watuhumiwa, utata wa tarehe za kupatikana vielelezo muhimu vya ushahidi kama bunduki aina ya SMG, pikipiki mbili zinazodaiwa kutumiwa na wauaji, maelezo yanayodaiwa ni ya kukiri kosa na ripoti ya DNA.

Hoja nyingine ni mateso ya washtakiwa, umiliki wa namba ya simu iliyosajiliwa kwa jina la Motii Mongululu inayodaiwa kutumika kumvuta marehemu kwenda eneo la tukio na kama ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashtaka ni ushahidi wa moja kwa moja au ni wa ushahidi wa kimazingira.

Akichambua hoja hizo, Wakili Magafu alidai hakuna ubishi kwamba Msuya alikufa kifo ambacho si cha kawaida cha kupigwa risasi na kuvuja damu nyingi, lakini pia hakuna ubishi kwamba shahidi pekee aliyeshuhudia mauaji hayo ni kijana wa miaka 19, Noel Thomas, mkazi wa Kijiji cha Ormelili, Wilaya ya Siha aliyekuwa akichunga mifugo lakini hakuweza kumtambua aliyefyatua risasi kumuua.

“Mheshimiwa Jaji (Maghimbi), kumekuwa na utata kuhusu ukamataji wa watuhumiwa, washtakiwa waliopo mbele yako wanasema tarehe zilizotajwa katika maelezo yao sizo tarehe walizokamatwa," alidai wakili Magafu na kueleza zaidi:

"Swali la kujiuliza ni hili je, hiyo caution statement (maelezo ya onyo) iliyokuwa admitted (pokelewa) hapa mahakamani na kusajiliwa kama Exhibit P.II (kielelezo cha ushahidi wa upande wa mashtaka namba II) kina sifa ya kuitwa confession statement (maelezo ya kukiri kosa)?

"Ni lazima confession statement iweze kukutia kwanza wewe hatiani na vile vile tunasema haiwezi kutumika kuwatia wenzako hatiani. Hakuna ushahidi uliotolewa hapa mahakamani ukionyesha Musa Mangu alihusika kununua na kuchonga laini za simu zilizotumika katika mauaji hayo zaidi ya maelezo ya wapelelezi.

"Mtu pekee ambaye angeweza kuisaidia mahakama na hakuletwa mahakamani kutoa ushahidi wake ni Adam Leyani.”

Wakili Magafu aliendelea kudai kwamba mshtakiwa wa kwanza, Mussa Mangu anadaiwa alikamatwa kati ya Agosti 11 na 13, 2013 na mkanganyiko huo umeletwa na shahidi wa 27 wa upande wa Jamhuri ambaye anakinzana na shahidi wa 18 na wote ni maofisa wa polisi.

Aidha, aliendelea kudai kuwa katika ukamataji wa bunduki upande wa mashtaka umedai kuwa ilikamatwa Septemba 11, 2013 lakini ushahidi huo huo unaonyesha kwamba watuhumiwa walikamatwa Septemba 13, 2013.

“Swali tunalojiuliza na ambalo mahakama inapaswa ilizingatie ni kwamba ni nani kati ya washtakiwa waliopo mbele ya mahakama alitumia bunduki hiyo (SMG) kumfyatulia risasi marehemu Msuya? Ushahidi huo haupo," alidai Wakili Magafu.

"We submit the gun was planted by the police (tunasema bunduki ilibambikwa na polisi) kwa sababu ilipatikana kabla ya watuhumiwa kukamatwa. Kukosekana kwa chronological events (mtiririko wa matukio) kunaacha utata.”

Aidha, wakili huyo aliyekuwa akiwasilisha hoja hizo kwa niaba ya wenzake watatu alidai kwamba hakuna ushahidi wa kuonyesha kwamba miongoni mwa watuhumiwa hao alikuwapo anayemiliki pikipiki aina ya King Lion na kutumia SMG hiyo kumuua Bilionea Msuya na kwamba ni jukumu la upande wa mashtaka kuthibitisha kosa hilo pasipo kuacha shaka.

Wakili Magafu aliendelea kudai kuwa kwa mshtakiwa wa pili Athuman ushahidi wa Jamhuri una mkanganyiko kwa vile shahidi wa 27, Mkaguzi wa Polisi Damian Chilumba alidai alikamatwa Agosti 12, 2013 lakini shahidi wa tisa, Mkaguzi wa Polisi Samuel Maimu akaieleza mahakama kwamba alikamatwa Agosti 13 mwaka huo.

Zaidi aliendelea kudai kwamba kwa 'Mredii’ ushahidi wa shahidi wa upande wa mashtaka alidai mahakamani hapo kwamba Mredii alikamatwa Agosti 16,2013 lakini shahidi wa utetezi ambaye ni yeye Mredii alidai kwamba hakukamatwa na polisi isipokuwa aliitwa kwa wito na Mkuu wa Kituo cha Polisi Mirerani na alitii na kwenda siku ya Agosti 17, 2013.

Kuhusu ushahidi wa uchunguzi wa DNA, Wakili Magafu alidai kwamba ushahidi wa shahidi wa 25 wa upande wa mashtaka, Gloria Omari (55) aliyekuwa akifanya kazi za kemia na utafiti kwenye Maabara ya Idara ya Sayansi ya Jinai ya Vinasaba katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali mwaka 2013, ushahidi wake hauungi mkono ushahidi wa shahidi wa 26, Kaijunga Brassy (35) ambaye alikuwa Mkemia kutoka Makao Makuu ya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Kaskazini.

Wakati anahitimisha uwasilisha hoja hizo, Wakili Magafu aliieleza mahakama hiyo kwamba hakuna ushahidi wa moja kwa moja katika kesi hiyo na kwamba mahakama imebaki na ushahidi mmoja ambao ni wa kimazingira.

"Mheshimiwa Jaji na waungwana wazee wa mahakama ili ushahidi wa circumstantial uweze kutumika ni matakwa ya sheria kwamba mnyororo wa ushahidi haupaswi kukatika," alidai.

"Ushahidi wa prosecution (Jamhuri) unakatika mno na ushahidi huo wa kimazingira wanaojaribu kuuleta mnyororo wake umekatika. Mahakama inastahili iwaone washtakiwa hawana hatia, prosecution wameshindwa kuthibitisha kesi yao na washtakiwa waachiwe huru."

Upande wa mashtaka katika kesi hiyo ambayo ni gumzo katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini, unaongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Abdala Chavula, akisaidiwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Omari Kibwana na Wakili wa Serikali, Kassim Nassir.

Mawakili wanaounda jopo la utetezi katika kesi hiyo ni Hudson Ndusyepo anayemtetea mshtakiwa wa kwanza, Magafu anayemtetea mshtakiwa wa pili na wa tano, Emmanuel Safari anayemtetea mshtakiwa wa tatu na John Lundu anayemtetea mshtakiwa wa nne, sita na saba.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

TEMBELEA KATIKA BLOG YETU HAPA>>>;

Mahakama yaondoa zuio matumizi ya kanuni za maudhui ya kimtandao

$
0
0
Mahakama Kuu ya Mtwara imeondoa mahakamani shauri la kupinga  matumizi ya Kanuni za Maudhui ya Kimtandao (Online Content Regulation) lililofunguliwa na Kituo cha Sheria na  Haki za Binadamu (LHRC) na wenzake dhidi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mbali na LHRC wengine waliopeleka zuio hilo ni Tanzania Human Rights Defenders (THRD); Baraza la Habari Tanzania(MCT) na Jamii Media; Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa ); na Jukwaa la Wahariri (TEF).

Kanuni hizo zilipaswa zianze kutumika Mei 5 lakini mahakama hiyo ikaweka zuio la muda Mei 4, baada ya kuwasilishwa kwa shauri la kupinga mahakamani hapo.

Kesi hiyo namba 12/2018 ilisomwa jana Mei 28 mbele ya Jaji Mfawidhi, Dk Fauz Twaib na ilipangwa kutolewa  uamuzi juu ya mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na upande wa Serikali.

Akitoa uamuzi huo jana, Jaji Dk Twaib alisema mahakama hiyo imekubali pingamizi moja kati ya matatu yaliyowasilishwa; kwamba mashirika yaliyopeleka kesi mahakamani hapo hayana maslahi ya kutosha kwa maana ya kufungua shauri hilo na kwamba hawakuonyesha  namna moja kwa moja yatakavyoguswa na kanuni hizo.

Hivyo, mahakama iliondoa shauri hilo lakini inatoa nafasi kwa mashirika hayo kama yatahitaji kupeleka shauri lingine kama watajidhihirisha wana nafasi ya kufanya hivyo.

Credit: Mwananchi

Nuh Mziwanda Azungumzia Picha Zake Tata na Amber Lulu

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Nuh Mziwanda amaefunguka na kuzungumzia video tata iliyokuwa ikiwaonyesha yeye na msanii mwenzake wa kike Amber  lulu wakiwa sehemu faragha  wakiwa katika mapozi ya kimahaba.

Wawili hao wanasadikika kuwa wapenzi hasa baada ya kuonekana kwa vido hiyo ambayo ilisambaa kupitia snap chat ya Amber Lulu.

Kwa mujibu wa Nuh anasema kuwa hakuna chochote kinachoendelaa kimapenzi kati yao bali kuna project wameeianda kati yao na ile iliyovuja walikuwa location kwa ajili ya ku-shoot.

"Mimi na Amber tuna project na hakuna kitu chochote, ila mimi niko snap chat kwaio wakati tunashoot video kulikuwa na zile vibes za snapchat  za kucheka, ku-enjoy na kufanya mambo mengine mengi , yeye alikuwa akichukua kwenye sanap na mimi nilikuwa nachukua katika snap lakini haikuwa kwa ubaya, na wala sikumwambia aitoe maana pale ile ni snapchat yake."

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Mpoki apewa shavu na Alikiba

$
0
0
 Katika kuelekea mchezo maalumu wa hisani ya kuchangia elimu, msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba ametangaza kikosi cha wachezaji watakao kuwa upande wake kupambana dhidi ya  kikosi cha wachezaji watakaokuwa upande wa mshambuliaji wa timu ya Taifa na klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta.

Kwenye kikosi hicho, Alikiba amemchukua mshambuliaji hatari wa klabu ya Simba, Emmanuel Okwi na wachezaji wengine kama John Bocco, Msuva, Erasto Nyoni, Abdu Kiba na wengineo kama inavyoonesha hapa chini kwenye picha.

Kikubwa zaidi ni kwamba Alikiba amemchagua mchekeshaji maarufu nchini Tanania, Mpoki kuwa msemaji wa timu yake aliyoichagua.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mnamo Juni 9, 2018 .


Khadija Kopa : Wasanii Wengi Wamekuwa Jeuri, Muda Si Mrefu na Mimi Ntaacha Muziki

$
0
0
Msanii mkongwe wa taaarabu nchini Khadija Kopa amefunguka na kuzungumzia hali ya taarabu ilivyo sasa nchini na kusema kuwa wasanii wengi wamekuwa jeuri na kwamba hawajitunzi kama zamani hivyio wanajishusha thamani wao wenyewe na wala sio kitu kingine.

Khadija kopa anasema kuwa wasanii wa taarabu wamekuwa wakiimba katika ma bar kwa kiinglio cha bia wakati hiyo haikuwa kama zamani na ili kukomesha hilo waimbaji hao wanatakiwa wakifuatwa wasikubali kufanya hivyo  na kujiona wa thamani ili kupanda hadhi yao.

Hata hivyo akizungumzia swala la yeye kustaafu kama alivyofanya gwiji wa taarabu nchini, mzee Yusup, malkia huyo amesema kuwa alichokifanya mzee ni kutokana na imani yake ilivyomtuma na ni jambo zuri , hata yeye siku yoyote atastaafu na sio muda mrefu kutoka sasa kwa sababu anahitaji kutenga muda mwingi pia kwa ajili yake , dini na mungu wake kwa sababu hajuai siku wala saa ya kufa kwake.

Hata hivyo Khadija Kopa anasema kuwa kama ataamua kufanya hivyo atafanya kimya kimya bila kumwambia wala kutangaza kwa watu, bali watashangaa tu haingii tena studio wala haonekani tena katika maswala ya burudani.

"Sina muda mrefu sana nitaacha huu muziki na nitakapo acha wala sina haja ya kutangaza eti eeh ninaacha muziki, hapana  nitaacha tu na watu wataona kimya tu sitoi nyimbo."

Belle 9 Akana Tetesi za Kukimbia Mjini Baada Ya Kufulia

$
0
0
Msanii mkongwe wa Bongo fleva aliyewahi kutamba na kibao chake cha ‘Masogange’ Belle 9 amekana tetesi zinazodai kuwa amefulia.

Belle 9 alipata shavu la kusainiwa na label ya ‘Vitamin Music’ ambayo ilimuhamisha kutoka Morogoro na kumleta Dar kwa ajili ya kufanya Muziki lakini baada ya kuoa  Belle 9 alipotea kidogo.

Baadae zilizuka stori kuwa Belle 9 ameamua kurudi nyumbani Morogoro kutokana na kukosa shoo na kufulia hapa Dar kiasi ya kwamba ana kosa hata pesa ya kulipia kodi ya nyumba.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, Belle 9 amekana tetesi hizo za kufulia na kusema hajahama Dar bado yupo mjini:

"Dah Hapana muda mrefu sijafika Morogoro mi Nipo Dar, hizo ni rumors tu zinazosambazwa na watu Lakini pia naona wanasema hivyo kwa sababu sionekani Kwenye maeneo ya starehe mengi."

Belle 9 amerudi upya na kazi yake mpya aliyotoa siku chache zilizopita inayokwenda kwa jina la ‘Dada’.

Diamond Akana Kumpigia Magoti Zari ili Warudiane

$
0
0
Msanii wa bongo fleva maarufu  nchini , Diamond Platinumz kwa mara ya kwanza amefunguka na kuzungumzia swala lake la kuachana na Zari na kumuomba radhi mwanamama huyo ambapo taarifa za hapo awali ziliwahi kusema kuwa kwa sasa Diamond amekuwa akipiga safari nyingi za Afrika ya Kusini ili kuomba radhi  kwa mwanamke huyo.

Akizungumzia kuhusu vijembe vingi ambavyo diamond amekuwa akitupiwa na mwanamama huyo hasa vya hapa karibuni alipokuwa kenya, Diamond alisema ; "hayo ya kenya bwana tuachane nayo, mimi nadhani yameshapita naomba tuendelee na  haya yasasa itapendeza sana”

Hata hivyo, mwandishi hakuishia hapo ndipo alipoamua kumuuliza moja kwa moja kuhusu yeye kusafiri kwenda afrika ya kusini kwa ajili ya kuomba radhi kwa zari huku akienda kwa siri mara kwa mara na diamond alijjibu kuwa safari zake za afrika ya kusini hazihusiani na mambo hayo.

"N kweli ninaenda na so mara moja au mara mbili nimekuwa ninaenda,nakwenda kule sio kwa ajili ya kumuomba msamaha , hapana ila ninakwenda kule kwa ajili ya kuona wanangu tu,haiwezekani niwe ninatuma pesa za matumizi tu alafu ninafka mpaka afrika ya kusini na nisiende kuwaona wanangu.

"Hao wanaosema kuwa sijui nimekuwa nikimuangukia nadhani yatakuwa ni maoni yao tu wala sio yangu, ni maneno yasiyokuwa na msingi, zari ni mama wa watoto wangu na itabaki kuwa hivyo."

Bunduki Ya Kivita Yaokotwa Vichakani

$
0
0
Bunduki ya kivita aina ya AK 47, ikiwa na risasi nne ndani imeokotwa ndani ya vichaka katika Kijiji cha Naan, Wilaya ya Ngorongoro mjini Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 29, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng’anzi amethibitisha kuokotwa kwa silaha hiyo na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka mmiliki wake.

“Mbali na bunduki hiyo, pia tumekamata pikipiki saba zinazodhaniwa kuwa ni mali ya wizi na watuhumiwa saba kupitia msako tuliofanya hivi karibuni,” amesema.

Kamanda Ng’anzi amezitaja mali zilizokamatwa kuwa ni televisheni sita, camera tatu, lensi mbili za camera, fedha taslimu Sh 915,000 na vitu vingine vya ndani na vifaa ofisini.

Pamoja na mambo mengine, Kamanda Ng’anzi amewaomba wakazi wa Arusha waliowahi kuibiwa kufika kituoni hapo ili kukagua kama wanaweza kutambua mali zao.

Lukuvi Apiga Marufuku Kampuni Za Kupima Ardhi Kudai Wananchi Gharama za Upimaji

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amepiga marufuku makampuni yanayopima ardhi yasiwadai wananchi gharama za upimaji wa ardhi.

Amesema kila makampuni hayo yatakapokuwa yakipima ardhi yatatakiwa kulipwa fedha za upimaji kupitia kwenye vikundi vilivyochaguliwa na wananchi.

Lukuvi ameyasema hayo bungeni jijini Dodoma leo, alipokuwa akiwasilisha bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2018/19.

“Aidha, wapimaji hao wanatakiwa kutoa taarifa katika uongozi wa wilaya husika kuhusu uwepo wao katika maeneo wanayopima ardhi,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Lukuvi aliwahimiza wananchi kuwa na kawaida ya kulipa kodi ya ardhi kila mwaka kwa kuwa ni wajibu wao kisheria.

“Kwa upande wa wananchi wanaokabiliwa na migogoro ya ardhi, nawaomba wafike kwa maofisa wa wizara yangu ili migogoro yao iweze kutatuliwa haraka iwezekanavyo,” amesema Lukuvi.

Waziri Mahiga: Tanzania itaendelea kushiriki katika ulinzi wa amani duniani

$
0
0
Siku ya Walinda Amani Duniani huadhimishwa tarehe 29 Mei ya kila mwaka ambapo kaulimbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni “Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa: Miaka 70 ya huduma na kujitoa (UN Peacekeeping: 70 Years of Service and Sacrifice).

Katika hotuba yake, Mhe. Waziri Mahiga alieleza kuwa yapata miaka 12 tangu Tanzania ianze kushiriki katika ulinzi wa amani chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa. 
 
Pia akasisitiza Tanzania itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inasaidia kupatikana kwa amani katika mataifa mengine kwakuwa hakuna taifa linaloweza kufanikiwa katika maendeleo pasipo kuwepo na amani ya uhakika. 

"Sio jambo rahisi kukubali kutoa uhai wako kwa ajili ya mtu mwingine lakini Tanzania itaendelea kuungana na mataifa mengine duniani katika kusaidia kupatikana kwa amani ya mataifa hayo" alisema Mhe. Mahiga.
 
Aidha, Katika kuwakumbuka Walinda Amani wote Duniani waliopoteza maisha wakati wakitekeleza majukumu yao, pamoja na kutoa heshima kwa wale ambao bado wanaendelea na jukumu la kulinda amani, Tanzania imepoteza jumla ya askari wapatao 30 ndani ya miaka 10, pia dunia imepoteza zaidi ya askari 3500 na kwa sasa Tanzania inajivunia kuwa na jumla ya askari wapatao 2,600 wanaohudumu katika misheni sita (6) za ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa.

Kwa Nini Saa Hii Inaongoza kwa Mauzo

$
0
0
KWANINI SAA HII INAONGOZA KWA MAUZO
au kwa lugha ya wazungu why this watch is best selling ...hili swali nilijiuliza kwa siku tatu mfulizo kwanini saa ilikuwa best selling mwezi tatu na wapili kwenye website nyingi dunia ikiwemo na ya kwetu....

Nikasema ngoja niivae nione ilinichukua masaa 72 kuja kujua why is best of best kwenye saa za mshale..kwanza kabisa saa hii ina mkanda wa ngozi then uko.comfortable yaani ngozi flani ya kibabe...

Pili rangi yake ni mchanyiko mzuri yaaani saa ya silver n mikanda meusi unapata best mchanganyiko.. ebwana saa hii pia ni water resistant 30meter chini ya maji ..... 

Imetengenezwa na kampuni ya skmei...mmmh nilipofungua nilikuta imekuja na box lake original sio saa inakuja bila box...bila kusahau kasaa haka mishale yote inazunguka ina kalenda na stop watch...hapo nikajua kujua kwa matumizi haya Lazima iwe BEST SELLING TU HAKUNA NAMNA......unaweza kwenye kuona sifa nyingine ukibonyeza buy now hapo agiza na utalipia mzigo ukifika majiji yote tanzania

Mama Wema Sepetu Ajichanganya Mahakamani, Nyaraka Za Kusafiria Adai Ni Vyeti Vya Matibabu

$
0
0
Mama wa Msanii Wema Sepetu, Mariamu Sepetu, amebanwa mahakamani baada ya kuwasilisha nyaraka alizodai za matibabu ya msanii huyo India wakati ni nyaraka za kusafiria.

Tukio hilo limetokea leo Mei 29, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema, ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alidai mahakamani kwamba kesi ilitakiwa kusikilizwa ushahidi wa upande wa utetezi lakini mshtakiwa wa kwanza, Wema hayupo ambapo mama Wema alidai msanii huyo ni mgonjwa yuko nchini India kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji na akawasilisha nyaraka alizodai kwamba zinathibitisha kuwa mgonjwa yuko kwenye matibabu.

Nyaraka hizo alizikabidhi kwa Wakili wa Serikali, Kakula ambaye alizikagua na kudai kwamba ni nyaraka za kusafiria ambapo alidai zilikuwa ni nyaraka za kusafiria na kumuomba mama Wema amuonyeshe mahali ilikoeleza kuhusu matibabu.

Mama Wema alijibu kwamba taarifa hizo atakuja kuzielezea Wakili wake Albert Msando ambapo Hakimu Simba alimfahamisha kwamba mahakama haiwezi kumsubiri hadi wakili wake aje.

Hata hivyo, Hakimu Simba alizichukua nyaraka hizo na kuzisoma kisha akasema nyaraka hizo ni tiketi na viambatanisho vya tiketi.

“Kesi itaendelea Juni 13, mwaka huu mshtakiwa aje na uthibitisho wa matibabu na kama hakutakuwa na uthibitisho, mahakama itatoa amri nyingine yoyote inayofaa,” alisema Hakimu Simba.

Mbali na Wema washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Angelina Msigwa  na Matrida  Abbas wanakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya na kukutwa na kiwango kidogo cha dawa hizo.

Taarifa rasmi ya Serikali kuhusu kesi ya kupinga Kanuni za Mitandaoni na maelekezo mahsusi kuhusu usajili wa mitandao ya kijamii.

Sekta Ya Fedha Yatakiwa Kuongeza Ubunifu Katika Utoaji Wa Mikopo

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
SERIKALI imeitaka Sekta ndogo ya Benki kuongeza ubunifu kwa kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu ambayo itawezesha ukuaji wa sekta za viwanda na kilimo pamoja na wajasiriamali wadogo.

Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Florens Luoga, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, katika Mkutano wa wadau wa Sekta ya Fedha uliowashirikisha wabunge, washirika wa Maendeleo, wakuu wa Taasisi za fedha na Wizara ya Fedha na Mipango.

Prof. Luoga alitoa wito huo kufuatia kuwepo kwa changamoto katika Sekta hiyo ikiwemo  ukosefu wa uwekezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika viwanda, kilimo na miundombinu pia  ukosefu wa mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.

“Kuna kiwango cha chini cha upatikanaji wa huduma za bima za kilimo, gharama kubwa za huduma za fedha, mifumo hafifu ya kuwalinda  watumiaji wa huduma za fedha, ukosefu wa elimu ya fedha kwa wananchi na wananchi wengi kutofikiwa na huduma za fedha ambapo ni asilimia 8.6 tu ya nguvu kazi ya wananchi waishio vijijini wanapata huduma za benki ikilinganishwa na asilimia 32.1 ya nguvu kazi kwa wanaoishi mijini” alisisitiza Prof Luoga

Gavana huyo wa Benki Kuu alisema kuwa ili kukabiliana na changamoto hizo, Serikali ilifanya maboresho ya Sekta ya Fedha  katika eneo la ubinafsishaji wa benki za Serikali kurekebisha na kutunga sera na sheria mbalimbali hadi kufikia Desemba, 2017 ili kuweka misingi imara ya kuwezesha ukuaji, ushindani na ufanisi katika sekta ya fedha.

“Maboresho ya Sekta ya Fedha yamesaidia ongezeko la idadi ya benki na taasisi za fedha kufikia 54, kampuni za bima 31, kampuni zilizoorodheshwa kwenye soko la hisa 27, taasisi za huduma ndogo za fedha takriban 450, mifuko na program za Serikali 34, vikundi vya kifedha vya kijamii takribani 30,019 katika mikoa 18 ya Tanzania bara na uanzishwaji wa soko la bidhaa” alieleza Prof. Luoga.

Alisisitiza kuwa taasisi za fedha zikitimiza wajibu wake, sekta binafsi itakuwa na uwezo wa kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa viwanda, kuongeza uzalishaji wa bidhaa zitakazouzwa nje ya nchi na hatimaye kukuza uchumi wa Taifa na kupunguza umasikini wa kipato wa wananchi.

Aidha Serikali katika kupunguza umaskini na kukuza uchumi, inaandaa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha, unalenga kuongeza upatikanaji wa huduma jumuishi za fedha, kulinda watumiaji wa huduma za fedha, upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu, uthabiti wa sekta ya fedha, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa katika sekta ya fedha, kudhibiti utakasishaji wa fedha haramu na kuweka mazingira wezeshi ya sheria, kanuni na taratibu katika sekta hiyo.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu, akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Doto James, alisema kuwa  azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha uchumi wa nchi  unaongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025.

“Kuwepo kwa viwanda vingi italeta ongezeko la ajira kwa wananchi walio wengi pamoja na kuiongezea Serikali mapato” alieleza Dkt. Kazungu

Aidha, kwa lengo la kuwawezesha wananchi kuwekeza katika viwanda vidogo vidogo, ni lazima wapate rasilimali fedha kutoka kwenye taasisi  kama vile benki na masoko ya mitaji hivyo watoa huduma kwenye taasisi hizo wanapaswa kuongeza ubunifu kwenye utoaji wa huduma zinazokidhi mahitaji ya wapokeaji huduma kulingana na shughuli wanazofanya na kwa gharama nafuu.

Alizitaka taasisi za fedha kuwekeza katika kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kutumia taasisi hizo kwa kujiwekea akiba na kupata mitaji itakayowezesha kukuza biashara na shughuli zao za kiuchumi hivyo wadau wa sekta ya fedha wanapaswa kujiuliza ni kwa nini mikopo ya biashara kwenda kwenye sekta binafsi hairidhishi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu), Prof. Faustin Kamuzora aliwataka wadau wa sekta ya fedha kuzungumzia mafanikio ya Sekta ya fedha kwa njia ya miamala ya Simu za mkononi kwa kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa Duniani katika eneo hilo na hivyo kuwa mfano kwa mataifa mbalimbali.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka Sekta binafsi inayonufaika na mikopo inayotolewa na taasisi za fedha kuwekeza kwenye miradi yenye tija na kulipa mikopo yao kwa wakati pamoja na kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha na kuongeza kiwango cha mauzo ya bidhaa hizo nje ya nchi,

mwisho

Breaking News: Huyu ndo Katibu Mkuu Mpya wa CCM Taifa

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemteua Dk Bashiru Ali kuwa katibu mkuu wa chama hicho.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Mei 29,2018 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole imesema Dk Bashiru ambaye ni mhadhiri wa masuala ya Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ndiye mrithi wa Abdulrahman Kinana aliyestaafu jana.

Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli aliridhia ombi la Kinana kujiuzulu jana.

Dk Bashiru ndiye aliongoza tume ya kuchunguza mali za CCM.

Taarifa ya CCM imesema, Raymond Mangwala ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana (UVCCM) na Queen Mlozi, kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake (UWT).

Erasto Sima ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM.

Mahakama Yamzuia Msajili wa Vyama Kumpa Fedha za Ruzuku Profesa Lipumba

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imemzuia Jaji Francis Mutungi na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini au Wakala wake yeyote yule kutoa fedha za ruzuku za Chama cha Wananchi (CUF), na kumpa Prof. Ibrahim Lipumba mpaka hapo mashauri ya msingi yanayoendelea Mahakamani yatakaposikilizwa.

Zuio hilo limetangazwa leo Mei 29, 2018 na Jaji Wilfred Dyansobera katika Mahakama hiyo na kusisitiza kwamba, maombi ya CUF ya kulinda fedha hizo yana nguvu za kisheria.

Taarifa za chama zinaeleza kuwa hadi amri hiyo ya Mahakama inatolewa, Jaji Mutungi na Ofisi yake ya Msajili wa Vyama imeshamruhusu Prof. Lipumba kuchukua zaidi ya shilingi Bilioni 1.5 na fedha hizo zimekuwa zikiwekwa kwenye akaunti zisizotambuliwa na Bodi Halali ya Udhamini ya chama na kisha kuhamishiwa kwenye akaunti za watu binafsi akiwemo Prof. Lipumba Mwenyewe.

Shauri kuhusu uhalali wa Bodi ya Wadhamini linaendelea kusikilizwa na inatarajiwa kuwa shahidi wa tatu wa upande wa Chama ataanza kutoa ushahidi wake mwezi Juni mwaka huu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images