Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ukipoteza Passport utatozwa 500,000 hadi 700,000 kupata nyingine

$
0
0
Kamishna wa Uhamiaji, Uraia na Passport, Gerald Kihinga amesema Mtanzania atakayepoteza hati ya kielektroniki ya kusafiria inayopatikana kwa Shilingi 150,000 atalazimika kulipa Shilingi 500,000 kupata mpya.

Pia aliongeza kuwa iwapo ataipoteza tena hiyo aliyoipata kwa Tsh. 500,000 basi atalipa Tsh. 750,000 ili aweze kupata nyingine.

Ameyasema hayo jana katika uzinduzi wa utoaji wa hati hizo ambapo tayari hati 15,101 zimeshatolewa kwa Watanzania tangu kuanza kwa utoaji huo January mwaka huu.

Alisema zipo kesi nyingi za watu kupoteza hati zao za kusafiria na baadhi yake ni zile zinazotokea katika matukio yasiyohitaji uwapo wake.

“Utakuta mtu anakuja kuomba hati mpya, ukimuuliza mazingira (ilivyopotea) anasema alikuwa akielekea Kariakoo kutoka Buguruni, sasa huko Kariakoo hati hiyo unaenda nayo ya nini? Tuzitunze hati hizi kwa sababu ni nyaraka muhimu kwa nchi yetu,” alisema Kihinga.

Alifafanua kuwa hakuna haja ya kuzunguka na hati hiyo kila mahali isipokuwa yale maeneo muhimu yanayohitaji uwapo wake kuepuka gharama kubwa ya upatikanaji wake wakati inapopotea.

Pia, alieleza kuwa tangu kuanza kutolewa kwa hati hizo hakuna changamoto zilizojitokeza zaidi ya kuwapo baadhi ya watu wanaotumia mawakala kupata hati na hivyo kutozwa zaidi ya Sh300,000.

Download Upya Application Yetu Ya mpekuzi .....Ile Ya Zamani Tutaifuta

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya Mpekuzi Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Maboresho Mapya Yamefanyika ili kukufanya upate habari zetu kwa wepesi zaidi kama vile Magazeti kuliko ilivyo sasa.

App ya zamani ilikuwa na tatizo kubwa la kuchelewa kufunguka, kuchelewesha habari na muonekano wake haukuwa wa kiwango kinachostahili.

Chakufanya, Ingia PlayStore, Download Upya Application yetu  MPYA. Ukishaipakua hii Mpya, ya zamani ifute tu.

NB: App mpya ina Icon ya Njano

Tumekurahisishia; 

Ronaldinho Kufunga Ndoa na Wachumba Wake Wawili Mwaka Huu

$
0
0
Gwiji wa soka nchini Brazil, Ronaldinho anatarajia kufunga ndoa katikati ya mwaka huu mwezi Agosti na kufanya sherehe moja na wachumba zake wawili, Priscilla Coelho na Beatriz Souza.

Watatu ambao wamekuwa wakiishi pamoja kwa amani na furaha  kwenye jumba la kifahari la nyota huyo wa soka jijini Rio de Janeiro tangu Disemba mwaka jana.

Gazeti la O Dia la Brazil limeripoti kuwa Ronaldinho alianza mapenzi na Coelho miaka michache iliyopita kabla ya kumuona Souza mwaka 2016.

Hata hivyo imeripotiwa kuwa wachumba zake hao wanapokea posho ya dola 2000 za kimarekani sawa na Shilingi Milioni 4.5 na zaidi kwa pesa ya kitanzania kutoka kwa Ronaldinho na amekuwa akiwapa zawadi zinazolingana yakiwamo manukato yanayofanana.

Ronaldinho hajawahi kuthibitisha uhusiano wake na wapenzi hao wawili lakini husafiri nao karibu katika matukio yote anayoalikwa limesema gazeti la  O Dia.

Aidha ndoa za wanawake wengi haziruhusiwi kisheria nchini Brazil, hivyo haijajulikana kwa gwiji huyo wa soka kama atafanikisha swala hilo la kufunga ndoa na wanawake hao ambao wameonesha kukubaliana na uamuzi huo.

Kamanda Mambosasa Azungumzia 'Mabilioni ya Dr Shika'

$
0
0
Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema swala la Dk. shika kuingiza pesa zake Tanzania hana uhakika nalo na mtu kutumiwa hela kihalali si kosa 

Amesema kuwa kama taarifa hizo ni za uongo anaweza kupuuzwa ila endapo kauli yake italeta madhara basi hatua zitachukuliwa.

Mambosasa amezungumza hayo leo pindi alipokuwa anaongea na waandishi wa habari akitoa ripoti za jeshi la polisi kuwashikilia watuhumiwa mbambali kwa kufanya makosa ya unyang’anyi kwa kutumia silaha za moto.

”Mtu kutumiwa hela kama ni halali haziingii kwenye pesa ambazo zinatakatishwa au hela ambazo zinapatikana kwa njia isiyo halali si kosa lakini kama ni muongo tu anajisema basi kuna mawili anaweza kupuuzwa lakini kama kauli zake zitamwaathiri yeyote anaweza kuja kulalamika na jeshi la polisi likachukua hatua” amesema Mambosasa.

Mambosasa amezungumza hayo pindi alipokuwa anajibu swali la mmoja wa waandishi wa habari baada ya kuhoji juu ya uhalali wa pesa za Dk. Luis Shika ambaye hivi karibuni taarifa zimeeleza tayari ameingiza mabilioni yake ya fedha nchini Tanzania.

Siku chache zilizopita Dkt. Louis Shika alivieleza baadhi ya vyombo vya habari nchini juu ya ujio wa fedha zake na baadhi ya vipande vya dhahabu zilizokuwa nje ya nchi kuwa tayari zimewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JKNIA) na kupelekwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa ajili ya kuhakikiwa.

Taarifa hizo zilizua mjadala mkubwa mtandaoni ambapo watu walionesha kutokuamini kwa ujio huo wa pesa za  Dk. Shika wakidhani ni stori zisizo na ukweli ndani yake.

Hata hivyo Shika alithibitisha ujio wa mali hizo na kuonyesha baadhi ya nyaraka zinazothibitisha umiliki wa mali hizo.

Mbunge CHADEMA Afariki Dunia

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Buyungu Mkoani Kigoma kupitia CHADEMA, Mh. Kasuku Samson Bilago amefariki dunia leo mchana akiwa katika Hospitali ya Muhimbili akipatiwa matibabu

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe.

Kuhusu chanzo cha kifo chake, Mbowe amesema:"Kwa sasa si wakati wake, tunahangaika kuhamisha mwili kutoka wodini kwenda chumba cha kuhifadhia maiti.  Hayo mengine itakuwa baadae."

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Habari wa chama hicho, Tumaini Makene amesema taarifa zaidi zitatolewa baadaye na chama hicho.

Bilago alishiriki baadhi ya vikao vya Bunge la bajeti lililoanza Aprili 3, 2018 mjini Dodoma.

Mheshimiwa Bilago pia alikuwa ni Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Magharibi na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA.

Marais wa Korea Kaskazini na kusini wakutana kwa dharula

$
0
0
Viongozi wa Korea Kaskazini na Korea Kusini wamekutana eneo lenye ulinzi mkali kati ya nchi hizo mbili na kufanya mazungumzo ya siri.

Mkutano huo ni wa pili kufanyika kati ya viongozi hao kati ya rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.

Aidha, mkutano huo unafanyika wakati pande hizo zinaendelea na jitihada za kufanikisha mkutano wa kihistoria kati ya Korea Kaskazini na Marekani.

Alhamisi Rais wa Marekani, Donald Trump alifuta mkutano uliopangwa kufanyika tarehe 12 mwezi Juni lakini baadaye akasema kuwa unaweza kufanyika,

Hata hivyo, mazungumzo kati ya Trump na Kim kama yatafanyika huku yatajikita zaidi katika kuondolewa silaha za nyuklia kutoka rasi ya Korea na kumaliza misukosuko.

Mwili wa mbunge Bilago wa CHADEMA kuagwa Jumatatu Dodoma

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema mwili wa aliyekuwa mbunge wa Buyungu (Chadema), Kasuku Bilago utaagwa Jumatatu Mei 28, 2018 bungeni mjini Dodoma.

Taarifa iliyotolewa leo Mei 26, 2018 na kitengo cha habari, elimu na mawasiliano cha Bunge, imeeleza kuwa baada ya kuaga mwili huo utapelekwa Kakonko mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.

“Ofisi ya Bunge inaendelea na kuratibu taratibu za mazishi kwa kushirikiana na familia ya marehemu na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa,” inaeleza taarifa hiyo.

Bilago amefariki dunia leo saa tisa alasiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Alihamishiwa Muhimbili Mei 22, 2018 akitokea Hospitali ya DCMC iliyopo eneo la Ntyuka jijini Dodoma alikokuwa amelazwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 27


Mashine za Kisasa Kubaini Wenye Ugonjwa wa Ebola Zafungwa Uwanja wa Julias Kambarage Nyerere

$
0
0
Na WAMJW-DSM
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto imeridhika na maandalizi ya mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa ya milipuko ukiwemo ugonjwa wa Ebola katika mipaka yote na viwanja vya ndege nchini

Hayo yamesemwa jana  na Naibu Waziri Dkt.Faustine Ndugulile wakati wa ziara yake katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere

Dkt.Ndugulile amesema amefika hapo ili kuangalia hali ya maandalizi na ufungaji wa mashine za kisasa za utambuzi wa ugonjwa wa Ebola endapo itatokea mtu mwenye ugonjwa huo

Aidha, alisema wizara imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa nchini na kuweka mfumo wa kubaini watu wanaoingia kwa kubaini hali ya joto linaloongezeka kwa  mgeni anayeingia na kufanyiwa uchunguzi zaidi.

“tumeweka mfumo wa kuwafuatilia wale ambao watakua wamebainika na joto zaidi mahali watakapofikia na mawasiliano yao ili kujua hali zao na endapo atapata mabadiliko”

Naibu huyo aliongeza kuwa wamewafanyia mazoezi ya kutosha kwa watoa huduma wa mipakani na viwanja vya ndege na pia kuwapatia elimu jinsi ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Dkt.Ndugulile ameendekea kusisitiza na kuwatia hofu wananchi kwamba hadi sasa hakuna mtu alobainika kuwa na ugonjwa wa Ebola na hali ya mipaka ya Tanzania ni salama

Waziri Mkuu: Tujiepushe na Vitendo Vya Chuki

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka waumini wa dini ya Kiislamu wajiepushe na vitendo vinavyoweza kupandikiza chuki dhidi yao au kwa waumini wa dini nyingine.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Mei 26, 2018) wakati akizungumza na viongozi na mamia ya waumini wa dini ya Kiislamu walioshiriki mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu kwenye ukumbi wa Mwl. J. K. Nyerere jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Kiislamu ya Istiqaama Tanzania (Istiqaama Muslim Community of Tanzania), yalijumuisha washiriki 29 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Visiwani.

“Serikali inatambua na inathamini sana, mchango wa dini katika kuwalea waumini kiimani na kutunza amani ya nchi. Hivyo, tujiepushe na kauli au vitendo ambavyo vinaweza kupandikiza chuki na uhasama dhidi yetu au dhidi ya waumini wa imani nyingine,” amesema.

“Nitoe rai kwenu viongozi wangu na waumini wenzangu, tujenge misingi ya kuvumiliana na kustahamiliana. Hilo pekee ndilo linaloisimamisha nchi yetu kuwa ni mfano wa kuigwa na kimbilio la wale waliovurugikiwa na amani katika nchi zao. Kadhalika, amani inajenga na kutoa fursa ya kuweza kutekeleza majukumu yetu ya kiibada, kiuchumi na kijamii bila hofu,” amesema.

Waziri Mkuu amesema kwa mujibu wa Surah Al-Imraan Ayah 103, Allah Mtukufu alihimiza umuhimu wa umoja miongoni mwa Waislamu. “Katika umoja huo, Allah amesisitiza Waislamu kuwa wamoja na kutofarakana. Mafundisho na wasia wa Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam ni kuwa tupendane na tushikamane. Wakati wote Mtume wetu aliheshimu na kuwathamini watu wote hata ambao hawakuwa Waislamu,” ameongeza.

“Kwa msingi huo, kama Waislamu nasi ni vema tukajipamba na tabia njema za Mtume wetu Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam. Katika hili, mtakubaliana nami kuwa tabia njema ni miongoni mwa makusudio muhimu sana ya kuletwa Mtume Muhammad kwetu,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa kuwapa elimu watoto kama ambavyo imesisitizwa kwenye Quran tukufu na kama ambavyo imesisitizwa na mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW) kwamba suala la kutafuta elimu ni la lazima kwa muislamu, awe mwanaume au mwanamke.

“Kama mnavyofahamu, Uislamu umeweka mkazo mkubwa sambamba na kusisitiza umuhimu wa elimu. Hili linathibitishwa na aya ya kwanza kabisa ya Quran kuteremshwa kwa Bwana Mtume Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam (SAW) ambayo ilimuamrisha kusoma (Surah Al-’Alaq ayah 1).”

“Kwa msingi huo, kama ambavyo mnatoa msukumo kwa vijana wetu kusomeshwa Quran, msukumo huo huo muutoe pia katika kuhakikisha kuwa vijana hawa wanapatiwa mafunzo sahihi kuhusu tabia njema, utii na kuheshimu mamlaka za utawala zilizopo. Kwa kufanya hivyo, tutawasaidia vijana hawa kuwa raia wema na wazalendo kwa nchi yao,” amesema.

Amesema Quran licha ya kuwa ni kitabu cha dini lakini kimebeba masuala yote muhimu katika maisha ya muislamu ya kila siku. “Hivyo, ukitaka kuleta maendeleo ya uchumi ulio imara, ukitaka kujenga jamii inayoheshimu na kufuata misingi ya uadilifu, ukitaka kujenga Taifa lenye amani na utulivu, huna budi kuwekeza zaidi katika elimu. Kwa hiyo, uwekezaji katika elimu haumaanishi tu kuhakikisha watoto wetu wanasoma na kuhifadhi Quran pekee, bali pia wanapaswa kupewa fursa ya kujifunza elimu ya mazingira ili waweze kufikia hatua bora za kimaisha duniani na akhera,” amesema.

Kwa upande wake, Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubei alisema mashindano hayo yamefana na imeshangaza kuona mtoto anatajiwa namba tu ya aya na anaweza kuielezea kuwa iko kwenye sura fulani.

Kama ambavyo nabii Yahya aliamriwa kushika kitabu, nasi pia tushike kitabu na tuyashike yaliyo ndani yake, tusije kuishi katika ardhi yenye rutuba na yenye rasilmali madini halafu na sisi tushindwe kuvuna kile kilichomo,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiaya ya Istiqaama Tanzania, Sheikh Seif Ally Seif alisema jumuiya hiyo yenye matawi 20 Tanzania Bara na Visiwani, ilianzishwa mwaka 1993 kwa lengo la kutoa mafunzo ya kiroho na kuwajengea vijana maadili mema ili Taifa liwe na watu wenye kujali amani, wanaoheshimiana na kupendana kidugu.

Alisema jumuiya hiyo imejenga shule 14 za msingi na sekondari kwenye maeneo mbalimbali nchini na inatarajia kujenga shule kubwa ya kimataifa jijini Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kufungua shule ya ufundi.

Katika mashindano hayo, kijana Kombo Fakhi Hamad (19) kutoka Istiqaama Pemba aliibuka mshindi wa jumla kwa kuweza kuhifadhi juzuu 30 na kupewa zawadi ya sh. milioni nne. Kombo pia aliibuka mshindi wa kwanza kwenye kundi la kuhifadhi juzuu 30 (tahfidh) akifuatiwa na Ally Said Mohamad (18) aliyepata sh. milioni mbili. Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Mariam Nassor Said (14) aliyepata sh. milioni 1.5.

Katika kundi la kuhifadhi juzuu 30 (tashdia), Masoud Bakari Ally (18) alikuwa mshindi wa kwanza na alipewa zawadi ya sh. milioni moja akifuatiwa na Mustafa Abdallah Hamad (17) aliyepata sh. 700,000 na wa tatu alikuwa Jumaa Ally Othman (16) aliyepata sh. 500,000.

Katika kundi la kuhifadhi juzuu 20, mshindi wa kwanza alikuwa Hilal Khamis Hamad (14) aliyepata sh. milioni 2.5 akifuatiwa na Ally Suleiman Ally (15) aliyepata sh. milioni 1.3 na mshindi wa tatu alikuwa Salim Khamiis Juma (15) aliyepata sh. milioni moja.

Makatibu Tawala wa Mikoa Waagizwa Takwimu za Wazee Ifikapo 30 Juni, 2018

$
0
0
Na. Atley Kuni-OR TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa        Mhe. Selemani Jafo (Mb), amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa Tanzania Bara kuwasilisha taarifa za takwimu za wazee ifikapo      30, Juni 2018.

Waziri Jafo, alitoa kauli hiyo mapema jana alipokuwa akizindua  zoezi la kuwapatia vitambulisho maalum wazee wapatao 1,118 wa Jiji la Dodoma kutoka kata za Mkonze, Mnadani, Uhuru, Madukani, Makole na Majengo. Vitambulisho hivyo, pamoja na mambo mengine vitawawezesha wazee hao kupata huduma za afya bure na kwa wakati.

“Ifikapo tarehe 15 Juni, 2018 kila kata iwe imetambua wazee na ifikapo tarehe 22 Juni, 2018 kila Halmashauri iwe imeunganisha taarifa za wazee kutoka katika kata zake zote” alisema Waziri. Aidha Waziri Jafo aliagiza kuwa, “ifikapo Juni, 26, 2018 kila Mkoa uwe umeunganisha taarifa zote na kuzituma kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI”. Aliwaonyawale wote watakaoshindwa kutimiza agizo hilo kuchukuliwa hatua kulingana na miongozo, kwasababu watakuwa wameshindwa kutekeleza wajibu wao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Ndugu Godwin Kunambi akizungumza katika hafla hiyo alisema shabaha ni kuwafikia wazee wote kwenye Jiji hilo, na kubainisha kwamba, vitambulisho wanavyo vitoa kwa wazee hao vitatumika pia kuwapa kipaumbele wazee sehemu zote za kutolea huduma hususan ofisi za serikali.

“Mhe. Waziri tunataka vitambulisho hivi tunavyo wapatia wazee wetu leo viwasaidie pia kupata huduma kwa haraka na kwa wakati pindi wanapofika kwenye ofisi zingine za Serikali” alisema Kunambi.

Mbali na kutolea ufafanuzi wa matumizi ya vitambulisho hivyo, Mkurugenzi Kunambi alisema juu ya Jiji hilo lilivyo jipanga katika suala zima la makusanyo ya mapato ya ndani, ambayo ndio yamekuwa chachu ya kuboresha huduma za afya kwa makundi maalum hususan wazee.

“Mhe. Waziri, Jiji limepanga kukusanya Bil. 68 katika mwaka wa fedha ujao ikilinganishwa na mwaka huu wa fedha ambapo tulijiwekea lengo la kukusanya Bil. 20 nahadi kufikia mwezi Februari tulikuwa tumekusanya Bil. 14”. Kunambi ameongeza kuwa, katika mwaka ujao wa fedha wametenga kiasi cha Mil. 58 kwaajili yakuwezesha huduma za wazee kwenye Jiji hilo.

Naye Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deo Ndejembi, ametumia fursa hiyo kuwaonya baadhi ya watendaji wanao waambia wazee kwamba hakuna dawa.

“Kumekuwepo na malalamiko mengi siku za nyuma kutoka kwa wazee kuwa, baadhi ya watendaji wa afya wanawanyanyapaa wazee na kuwaambia hakuna dawa wafikapo vituoni, sasa Mhe Waziri, mimi niliseme kwa uwazi kabisa hatuta mvumilia mtu yeyote atakaye onekana ni kikwazo kwa wazee hawa kadi zimetoka wazee wahudumiwe, sio mnajiwekea vijiduka karibu na vituo halafu mnawaambia waende waka nunue” alionya Ndejembi

Awali akitoa taarifa ya uandaji wa vitambulisho Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Mohamed Nyembea, alisema utekelezaji wa zoezi hilo ulianza kwa hatua za awali kwa kuwatambua wazee katika Kata 41 za Jiji la Dodoma, ambapo jumla ya wazee 15,885 kutoka kata 33 miongoni mwa 41 wamekwisha tambuliwa  na miongoni mwao wanawake ni 9,132 na wanaume ni 6,753 ambapo ni sawa na asilimia 80.5 ya kata zote 41 za Jiji la hilo.

Utoaji wa vitambulisho kwa wazee ni utekelezaji wa sera ya Taifa ya wazee ya mwaka 2003 ambapo inazungumzia mambo muhimu ya wazee ikiwepo kutenga dirisha maalum katika vituo vya kutolea huduma za afya.  

Polisi Dar Wakusanya Milioni 972 Za Makosa Barabarani Ndani ya Wiki Mbili

$
0
0
Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekusanya Sh972.7 milioni za makosa ya usalama barabarani katika kipindi cha wiki mbili.

Katika operesheni hiyo ya ukamataji wa magari iliyofanyika kati ya Mei 11 hadi Mei 24, mwaka huu magari yaliyokamatwa ni 24,116, pikipiki 763 na daladala 10,301.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema, “Waendesha babodada waliofikishwa mahakamani kwa makosa ya kutovaa kofia ngumu na kupakia mishikaki (abiria zaidi ya mmoja) ni 59. Jumla ya makosa yaliyokamatwa ni 30,850 na fedha zilizopatikana ni Sh972 milioni.

“Madereva na wamiliki wa magari wanatakiwa kulipa faini zao ndani ya siku saba ili kuepuka faini kuongezeka na kusababisha kukamatwa tena kwa kulimbikiza madeni,” alisema Mambosasa.

Katika hatua nyingine; Mambosasa alisema polisi wanamshikilia mhudumu wa Hoteli ya Sleep Inn kwa tuhuma za kukutwa na sare za polisi, silaha, cheo cha koplo, pingu na nguo inayofanana na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

“Tulipata taarifa kutoka kwa msiri kuwa kuna mtu mmoja anatumia sare za polisi kuwakamata watu na kuwafunga pingu na kuwatishia bastola ili kufanikisha kupora mali maeneo mbalimbali ya Jiji. Baada ya kupata taarifa hizo tulianza ufuatiliaji na kuweka mtego. Mei 12 tulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa,” alisema Mambosasa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 28

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

PICHA: Rais Magufuli Alivyokutana na Kufanya Mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Mei, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo Mhe. Rais Magufuli alipokea salamu kutoka kwa viongozi wa chama na Serikali wa Afrika Kusini na Zimbabwe ambako hivi karibuni Ndg. Kinana aliongoza ujumbe wa viongozi wa CCM kutembelea nchi hizo na kukutana na viongozi wakuu wa vyama tawala vya ANC na ZANU-PF vinavyoongoza Serikali.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli na Ndg. Kinana wamezungumzia maandalizi ya vikao vya Kamati Kuu ya CCM (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) vitakavyofanyika  tarehe 28-29, Mei, 2018 Jijini Dar es Salaam.


Taarifa Kwa Umma Kuhusu Mazishi Ya Aliyekuwa Mbunge Wa Jimbo La Buyunga,marehemu Mwl.kasuku Samson Bilago

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Mtanzania Aibuka Kidedea Mashindano Ya Kuhifadhi Quran Afrika.....Waziri Mkuu amtaka Sheikh Kishki akaonane na Waziri wa Ardhi atoe maamuzi ya kiwanja

$
0
0
KIJANA wa Kitanzania, Shujaa Suleiman Shujaa ameibuka kidedea na kitita cha sh. milioni 15 katika mashindano ya 19 ya Afrika ya kuhifadhi Quran kwenye kundi la washiriki wa juzuu 30.

Shujaa mwenye miaka 23 ambaye ni mkazi wa Morogoro, amejishindia pia laptop, kiwanja chenye hati eneo la Kigamboni kilichotolewa na kampuni ya Property International ya jijini Dar es Salaam pamoja na dola za Marekani 500 kutoka kwa Bw. Ahmed Seif “Magari” aliyetoa dola 500 kwa washindi wote watano.

Akizungumza na maelfu ya waumini na Watanzania waliofurika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana  mchana (Jumapili, Mei 27, 2018), Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kuilinda amani iliyopo nchini kwani ikipotea hakuna atakayeweza kufanya ibada.

“Mtakubaliana nami kuwa amani ya nchi yetu, ndiyo inatufanya tutembee vifua mbele dhidi ya wenzetu, ni neema kubwa ambayo kila muumini anapaswa kuilinda kwani ikipotea hata mkusanyiko wetu huu wa leo si rahisi kufanyika mahali kama hapa,” alisema.

“Leo hii tuko hapa uwanjani kwa sababu tuna amani, kama Serikali isingekuwa inashirikisha Watanzania wote kulinda amani, basi tusingeweza kukutanika hapa. Kuna nchi 18 ziko hapa, na watu wake wamekuja hapa uwanjani kwa kuwa wana uhakika na amani tuliyonayo sisi Watanzania,” alisema.

Alisema katika nchi ambazo amani imetoweka, watu wanalazimika kufanya shughuli za ibada majumbani au kwa kujificha. 

“Wenzetu hao, hawapati fursa adhimu kama hii ya kujumuika pamoja na majirani, ndugu, jamaa na marafiki kusikiliza na kufurahia kisomo cha Quran au kufanya shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii,” aliongeza.

Aliwataka Watanzania waendelee kubeza na kupuuza kauli za walio wachache ambao kwao kuzungumzia amani ni kujipendekeza kwa Serikali. “Watu hao wamesahau kwamba tofauti katika Uislamu hazikuanza leo, lakini tofauti hizo hazikuwa sababu ya wema waliotangulia kuacha kuheshimiana na kushirikiana,” alisisitiza.

Mshindi wa pili kwenye kundi hilo la juzuu 30 ni Ahmed Noor wa Sudan ambaye ameshinda sh. 12,564,750 pamoja na laptop akifuatiwa na Muzamil Awadh Mohamed wa Sudan alijishindia sh. milion 7.5 pamoja na laptop zilizotolewa na kampuni ya Camara Education.

Mshindi wa nne ni Abdulally A. Mohammed wa Kenya aliyepata zawadi ya sh. 5,711,000 na wa tano ni Ibrahim Maazur kutoka Niger, aliyepata sh. 3,426,000. Washindi hao wote watano walipewa zawadi ya kwenda hijja na Waziri wa Mambo ya Dini wa Saudi Arabia, Dk. Saleh Ally Sheikh.

Washiriki wengine kwenye kundi la juzuu 30 walitoka nchi za Rwanda, Burundi, Msumbiji Djibouti, Kenya, Ethiopia, Congo DRC, Nigeria, Ghana na Afrika Kusini.

Washiriki wengine waliopewa zawadi ni wale walioweza kuhifadhi Juzuu tatu (washindi watatu), Juzuu tano (washindi watatu); Juzuu 10 (washindi watatu) na Juzuu 20 (washindi watatu).

Viongozi wengine waliohudhuria mashindano hayo ni Makamu wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Mohammed Gharib Billal, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania kutoka Saudi Arabia, Comoro, Oman, Uturuki, Kenya, Msumbiji na Nigeria, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally na Rais wa taasisi ya Al-Hikma, Sheikh Sharif Abdilkadir Al-Ahdal.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemtaka Sheikh Nurdin Mohammed Ahmad (maarufu kama Sheikh Kishki) akaonane na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. William Lukuvi ili atoe maamuzi ya kiwanja chao kilichopo eneo la Matumbi ambacho mwaka jana aliagiza kifuatiliwe taratibu zake na kisha wapatiwe.

“Kuhusiana na suala la kiwanja mlichosema, mamlaka ya awali ni Manispaa ya Temeke na ilishakamilisha taratibu zote za kisheria, ikapeleka kwa Afisa Ardhi wa Mkoa kuona kama limepita kwenye vikao vyote ndipo wanaenda wizarani kupata kibali. Hakuna sababu ya wizara kuikatalia manispaa huku eneo lenyewe likiwa kwenye ramani kuu ya manispaa yenyewe, nenda mumuone Waziri mwenye dhamana, awape ardhi,” alisema.

Waziri Mkuu amefikia hatua hiyo baada ya kupewa taarifa akiwa jukwaani kwamba taasisi ya Al-Hikma iliwasiliana na Manispaa ya Temeke, hadi mkoani wakapewa barua zinaonyesha eneo liko sawa lakini walipofika wizarani wamekwamishwa na Afisa mmoja aliyemtaja kwa jina moja la Mama Mpetula.

Juni 11, mwaka jana katika mashindanio ya 18, taasisi ya Al-Hikma waliomba wapatiwe kiwanja na.118 kwenye kitalu E kilichoshikamana na kiwanja na. 117 chenye shule yao ya Al-Hikma Girls iliyoko Temeke ili waweze kujenga zahanati.

Lema alipongeza Bunge, akomaa na Stahiki za Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka kuwa bado wanaendelea kutafakari suala la Mbunge wa Sigida Mashariki Tundu Lissu kuhangaika na kutafuta misaada ya matibabu kwa watu mbalimbali duniani, kwani Bunge bado linatafakari kuhusu stahiki zake, haki na gharama za matibabu.

Mhe. Lema amezungumzia hayo ikiwa ni siku moja tangu kutokea kwa kifo cha Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago aliyefariki wakati akipatiawa matibabu katika hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Lema amesema "Mwili wa Marehemu Mhe. Bilago umepata heshima, haki na stahiki ya Kibunge, tumefanya kikao tena Kati ya Bunge, Chama na Familia, wema wa Bunge kwa mwili wa marehemu umekuwa ni wa kifani".

Ameongeza "Wakati tunalishukuru Bunge kwa wema huu, bado tunaendelea kulitafakari la rafiki yetu Lissu aliyeko Ubeligiji".

Lissu ambaye anatibiwa nchini Ubelgiji alipigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 9, 2017 maeneo ya Area D akiwa anatokea katika majukumu yake ya kikazi bungeni Dodoma.

Sababu za Lissu kutotibiwa na Bunge ziliwekwa wazi na Spika wa Bunge, Job Ndugai  siku moja baada ya tukio hilo ambapo alisema kuwa utaratibu wa matibabu kwa mbunge ulikuwa umeshafuatwa lakini familia pamoja na chama  waliamua kumpeleka Nairobi, na siyo kama wao walishindwa kumpeleka nchini India.

Mwanafunzi Chuo cha SAUT Ajinyonga Baada ya Timu Yake ya Liverpol Kufungwa

$
0
0
Mwanafunzi wa mwaka wa pili Chuo kikuu cha ‘St. Augustine’ kampasi ya Mbeya Moses Mashaka amejinyonga mara baadaya timu yake ya Liverpol kushindwa kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani ulaya.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Jijini Mbeya Naibu Kamishna wa Polisi Mussa Taib amesema Moses (24) amejinyonga mara baadaya ‘kubet’ na timu yake kushindwa kutwaa ubingwa.

“Mwanafunzi wa chuo kikuu cha sauti mwaka wa pili anachukua shahada ya ualimu amefariki baada ya ‘kubet’ pesa ambazo hazijulikani ni kiasi gani na baadaya Liverpol kushindwa ndipo akachukua uamuzi huo”,amesema kamanda Taibu.

Aidha Kamanda Taibu amewataka wanafunzi kuacha kutumia fedha za wazazi kwa mambo yasiyohusiana na masuala mazima ya elimu, kwani matokeo yake ni hasara kwa wazazi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images