Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri wa Nishati Amuomba Mungu Ailaze Serikali Mahali Pema Peponi

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani amewavunja mbavu wabunge baada ya kuwaambia anamuomba Mwenyezi Mungu aiweke serikali mahala pema peponi.

Dk. Kalemani ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo Mei 25, alipokuwa akihitimisha mjadala wa Bajeti ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/19 aliyowasilisha jana.

Kabla ya kusema hayo Dk. Kalemani alikuwa akieleza jinsi serikali ilivyotekeleza miradi mbalimbali na kuwapelekea wananchi umeme katika maeneo mbalimbali nchini ambapo alijikuta akisema: “namuomba Mwenyezi Mungu aiweke serikali mahali pema peponi,”.

Hatua hiyo iliwafanya wabunge kuangua vicheko huku Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu akilazimika kuwatuliza wabunge na kuwataka waendelee kumsikiliza waziri badala ya kucheka.

Hata hivyo, baada ya dakika chache Dk. Kalemani alisema anamuomba Mwenyezi Mungu aibariki serikali na kuwafanya wabunge kucheka tena kwa sauti.

Waziri: Tutawafunga Jela Wabunge Watakaokwamisha mradi wa Stiggler’s Gorge.

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Kangi Lugora amesisitiza kwamba serikali iko tayari kuwafunga jela wabunge watakaokwamisha mradi wa Stiggler’s Gorge.

Akijibu hoja za wabunge zilizoelekezwa katika wizara yake katika bajeti ya Wizara ya Nishati bungeni jijini Dodoma leo, Kangi amesema pamoja na malalamiko yanayotolewa na baadhi ya wabunge kwamba mradi huo haujafanyiwa tathmini ya mazingira, serikali imeshafanya tathmini hiyo kwa kuwashirikisha wataalamu mbalimbali.
 
Hata hivyo, majibu hayo ya Kangi yalionekana kuwakera baadhi ya wabunge wa upinzani na kulazimika kupiga kelele za kuzomea.

"Piga ua Serikali itatekeleza mradi huu. Tunajua chura wanapiga kelele, ila kelele za chura hazimzuii ng’ombe kunywa maji,” amesema.

Amesema kazi ya wapinzani kuanzia Januari Mosi hadi Desemba, 2018 ni kuipinga Serikali, “Sisi kama Serikali hatutachoka kutoa elimu na kuelimisha wanaopinga mradi huu.

“Hapa lilipo jengo la Bunge kulikuwa na mazingira kama mengine, lakini tukaharibu mazingira, hawa wabunge wanapokaa (wanapoishi) hata kama ni eneo dogo waliharibu mazingira ili kupata nyumba.”

Mbunge huyo wa Mwibara (CCM) amesema tathimini ya mazingira ambayo imefanywa katika mradi huo taarifa yake ni ya kitaalamu, imesheheni wataalamu wa mazingira, wadudu, ikolojia na maji na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) walitoa ushauri kwa mshauri mwelekezi ambaye ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

“Masuala haya ni ya kitaalamu, Watanzania wasiwe na hofu. Hawa wanaopinga mradi huu ukiwatazama wanahitaji umeme ufike vijijini mwao, wengine ni wachum lakini wanapinga,” amesema.

“Maana yake ni kwamba mradi huu wanaona Serikali ikiutekeleza tutakuwa na umeme mwingi, tutakuwa na viwanda, sasa Zitto (Kabwe-mbunge wa Kigoma Mjini) wewe ni mchumi uliyebobea hebu isaidie Serikali kuelimisha wenzako, kwa kuwa ni mpinzani watakuelewa.”

Akimalizia kujibu hoja hizo Lugola amesema, “Serikali itaendelea kujenga mradi huu na wale wote wanaopinga na kama wanatumwa tutawachukulia hatua na kuwapekeka jela.”

Waziri Mkuu Apokea Wanachama Wapya 89 Kutoka kutoka CUF, CHADEMA na ACT .....Yumo aliyekuwa Katibu Mwenezi wa kata wa CHADEMA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea wanachama saba kutoka vyama vitatu vya upinzani ambao wameamua kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) na wengine 82 kutoka Chama cha Wananchi (CUF) ambao walikuwa wapiga debe.

Wanachama hao wamepokelewa jana mchana (Ijumaa, Mei 25, 2018) wakati akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua uwanja mpya wa michezo unaojengwa katika kijiji cha Dodoma, kata ya Nachingwea, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi.

Waziri Mkuu ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alipokea kadi nne za CUF, moja ya ACT na mbili za CHADEMA kutoka kwa wanachama hao saba kabla hajawakabidhi kadi za CCM. Wanachama hao saba waliokabidhiwa kadi mpya za CCM pamoja na wenzao 82, walikula kiapo cha uaminifu mbele ya Waziri Mkuu.

Shangwe zililipuka uwanjani hapo wakati aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CHADEMA kata ya Nachingwea, Bw. Ismail Hamisi alipokabidhi kadi yake kwa Waziri Mkuu.

Akisoma risala kwa niaba ya wanachama wenzake walioamua kujiunga na CCM, mkazi wa Ruangwa mjini, Bw. Fred Mnimbo alisema wameamua kurudi kwa sababu yale waliyotarajia yafanyike upinzani hayaonekani.

“Tumegundua upinzani wa sasa ni maslahi binafsi na si wa kuwatumikia wananchi; kinachosemwa sicho kinachotendwa na wapinzani na pia tumeamua kuunga mkono juhudi anazofanya Rais John Pombe Magufuli,” alisema Bw. Mnimbo katika risala hiyo.

Alisema wameamua kuhamia CCM kwa sababu Serikali iliyopo madarakani kwa sasa inatekeleza mahitaji ya Watanzania kwa asilimia 90 na pia wanataka kumuunga mkono mbunge wao wakiwa katika chombo kimoja ili waijenge vizuri Ruangwa na Tanzania kwa ujumla.

“Tunataka kuunga mkono usimamizi mzuri wa rasilmali zetu hasa mazao ya korosho na ufuta kutokana na jinsi unavyoyasimamia kikamilifu hasa mikoa ya Kusini. Kaulimbiu ya Ruangwa kwa maendeleo inawezekana, imedhihirika kwa vitendo kwa sababu kila mmoja anaona kwamba Ruangwa ya jana si Ruangwa ya leo, maendeleo yanaonekana kwa mafanikio makubwa,” alisema huku akishangiliwa.

Akitoa utambulisho wa wanachama hao wapya, Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Bw. Barnabas Essau alisema wanachama hao wameamua kujiunga na CCM kwa sababu wameridhishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano.

Novemba 5, mwaka jana, Waziri Mkuu alipokea wanachama 37 kutoka vyama vya CUF na CHADEMA kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Mbekenyera, wilayani Ruangwa. Pia Desemba 29, 2017, alipokea wanachama 60 kutoka CUF kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Nkowe kata ya Nkowe, wilayani Ruangwa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Ashiriki Ujenzi Wa Uwanja Mpya

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki kazi za ujenzi wa uwanja mpya wa michezo wilayani Ruangwa kwa kubeba zege na matofali pamoja na wananchi.

Waziri Mkuu ambaye pia ni mbunge wa Ruangwa, ameshiriki zoezi hilo jana (Ijumaa, Mei 25, 2018) kwenye uwanja huo unaojengwa katika kijiji cha Dodoma, kata ya Nachingwea, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi.

Akizungumza na wananchi na viongozi waliojitokeza kushiriki zoezi hilo, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na kazi ya ujenzi inayoendelea hadi sasa na akatumia fursa hiyo kuwashukuru wana-Ruangwa kwa kurejesha moyo wa kufanya kazi kwa kujitolea.

“Ninawashukuru sana wana-Ruangwa kwa sababu mmeanza kufanya kazi za kujitolea, haya matofali ni matokeo ya kazi yenu, hakuna hata mtu mmoja amelipwa kwa kazi hii. Nimeambiwa yanahitajika matofali 60,000 kwa ajili ya kujenga uzio lakini hadi sasa mmeshafyatua 57,000 na zaidi, ninawashukuru sana,” amesema.

“Nimeambiwa madiwani walipiga kambi ya wiki moja hapa, Umoja wa Vijana wa CCM nao walipiga kambi, UWT walikuja kusomba matofali, watumishi wa Halmashauri nao walipiga kambi, hongereni sana kwa kurejesha moyo wa kujitolea miongoni mwa wananchi,” amesema.

Katika zoezi la leo, walijitokeza wananchi wengi wakiwemo wazee, vijana na watoto. Baadhi ya watoto walikuwa wakibeba tofali moja kwa kushirikiana wawili wawili, watatu watatu hadi wanne.

Alisema ujenzi wa uwanja huo hadi sasa umeungwa mkono na wadau mbalimbali ambapo aliishukuru Benki ya CRDB ambayo imetoa sh. milioni 15 zilizotumika kununua mifuko ya saruji 1,200; Mbunge wa Kwimba, Bw. Mansoor Shanif Hiran mifuko 1,200 ya saruji; Mtibwa Sugar mifuko 2,000 ya saruji na TFF waliotoa mbegu za nyasi kwa ajili ya uwanja huo.

Akiwa uwanjani hapo, Waziri Mkuu alipokea ahadi ya tani nne za nondo zenye thamani ya sh. milioni 10, kutoka kwa Kampuni ya Hyseas International Investment (T) Limited ya China.

Mapema, akisoma taarifa ya ujenzi wa uwanja huo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Afisa Utamaduni wa Wilaya hiyo, Bw. Simon Mwambe alisema awamu ya kwanza ya ujenzi inatarajiwa kukamilika Juni 2019 na hadi kukamilika kwake, uwanja huo utagharimu sh. bilioni 4.64.

Alisema uwanja huo ambao unajengwa kwa kutumia vipimo vya kimataifa, ukikamilika utawezesha watazamaji 10,500 kuingia uwanjani. Pia utajumuisha michezo mingine kama mpira wa miguu, pete, wavu, mikono, kikapu na riadha.

Naye Architecture Khalid Yassin ambaye alikuwa akitoa maelezo ya ujenzi wa uwanja huo kwa Waziri Mkuu, alisema utakapokamilika, uwanja huo utakuwa na kumbi mbili za kukutania wachezaji na makocha wao, vyumba vya kubadilishia, vyoo na ofisi ya meneja wa uwanja.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Trump Kageuka Tena...Kasema Yupo Tayari Kwa Mazungumzo na Korea Kaskazini

$
0
0
Siku moja baada ya kusitisha mkutano wa ngazi ya juu na Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un Rais wa Marekani, Donald Trump amesema mkutano huo huenda ukafanyika kama ilivyopangwa awali.

Alhamisi Trump alitangaza kusitisha mkutano huo uliopangwa kufanyika June 12 huko Singapore akitaja kile alichokiita “hasira kubwa na uadui wa wazi” uliooneshwa hivi karibuni katika taarifa iliyotolewa na Korea Kaskazini.

Siku moja baadae, Trump ameonekana akilegeza msimamo. Ameandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa;

WHO yatoa tahadhari kuhusu watu kuumwa na nyoka

$
0
0
Nchi wanachama wa mkutano wa shirika la afya duniani wamepitisha azimio la kutambua kuumwa na nyoka kuwa ni suala linalohitaji kupewa kipaumbele katika kulishughulikia.

Maelfu ya watu hufa kila mwaka na wengine kuwa walemavu kutokana sumu inayotokana na shambulio la nyoka.

WHO inasema athari zinazotokana na kuumwa na nyoka zimeendelea kuwa moja kati ya magonjwa ya kitropiki ambayo hayatiliwi maanani.

Kufikiwa makubaliano hayo kwa nchi wanachama wa WHO , kuna nia ya kuhakikisha kuwa kunakuwa na mbinu za kuzuia, kutibu na kukabili mashambulizi ya nyoka.

Makundi ya mbalimbali ya wanaharakati wa masuala ya afya yamesifia azimio hilo na kusema kuwa hatua hiyo inafungua milango katika kupunguza vifo na ulemavu duniani kote.

Shirika la Afya duniani sasa lina jukumu la kuja na mpango wa pamoja kuimarisha programu za tiba, kuzuia na kurekebisha.

Hii itahusisha kutoa dawa za kupambana na sumu kwa bei rahisi, dawa ambazo ilikua gharama kupatikana kwenye nchi zilizo masikini hasa zilizo kusini mwa jangwa la Sahara.

Hali ya umaskini na kutokuwa na vituo vya afya vinavyokidhi mahitaji kumesababisha vifo vya maelfu ya watu huku wengine wakitafuta tiba kwa matabibu wa kienyeji ambao husababisha madhara zaidi.

Lakini mpango huu mpya utalenga kuwafundisha watoa huduma wa afya jinsi ya kushughulikia mtu aliyeumwa na nyoka na elimu ya huduma ya kwanza kwa jamii iliyo hatarini.

Kila mwaka zaidi ya watu laki moja hufa duniani kutokana na kuumwa na nyoka asilimia 20 kutoka barani Afrika.

Karibu watu nusu milioni wana ulemavu wa kutokuona, kukatwa viungo na ulemavu mwingine kutokana na mashambulizi ya nyoka.
 
 Ondoka eneo la hatari
Kama uko mwenyewe mbali na msaada, jambo la kwanza ni kwenda eneo lenye usalama.Tafuta eneo ambalo utaomba msaada.Kama uko na watu wengine wacha wakubebe kama inawezekana,ili kupunguza kiasi cha sumu kutembea mwilini,wataalam wanaeleza.

Usifyonze sumu kutoka kwenye jeraha
Sumu huingia ndani kabisa kwenye eneo la kati ya ngozi na misuli na husambaa mara moja (ndani ya dakika moja).Hivyo haiwezekani kuondoa sumu kwa kunyonya kwani itazidisha maumivu na uharibifu zaidi pasipo na ulazima.

 Ondoa vitu vilivyovaliwa sehemu iliyoathiriwa
Vua vitu kama pete au nguo zinazobana katika eneo ambalo madhara yametokea kama mkononi kwa sababu vinaweza kusababisha damu kutotembea vizuri.

Credit: BBC

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota, Mvuto wa Biashara na Mapenzi

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi 

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Heche Afunguka Suala la Ufisadi wa TANESCO

$
0
0
Mbunge wa Tarime Vijijini (CHADEMA) John Heche amesema Shirika la Umeme nchini TANESCO halitaweza kupata faida mpaka kuisha kwa dunia kutokana na mkataba wa kifisadi waliongia na kampuni ya uzalishaji umeme ya Songas.

Heche amesema hayo jana Mei 25, 2018 Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa akichangia hoja mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati katika mwaka wa fedha 2018/2019 na kuongeza kuwa kama mkataba huo utaendelea basi madeni ya TANESCO yatazidi kuongezeka maradufu.

“Mwenyekiti umesema hapa TANESCO wameanza kupata faida, kamwe mpaka dunia hii inaisha TANESCO hawatapata faida kwasababu mkataba walioingia na Songas ni mkataba wa kihuni na wizi ndiyo unasababisha shirika hili kuendelea kuwa na madeni na hata dunia hii inaisha kama mkataba na Songas utaendelea kuwepo madeni ya TANESCO yataendelea kuwa makubwa”, alisema Heche.

Mbunge huyo aliongeza kuwa kitendo cha TANESCO kuwa shirika pekee linalozalisha umeme nchini bila ya kuwa na mshindani imechangia kwa kiasi kikubwa kuwa na mzigo wa kutoa huduma pamoja na madeni ambapo mpaka kufikia sasa TANESCO inadaiwa zaidi ya bilioni 900.

Bunge limepitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo jumla ya shilingi trilioni 1.69 imeizinishwa kwa matumizi ya miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida.

Serikali Yatoa Bilioni 4 Kwa Watafiti Walioshinda Andiko la Miradi

$
0
0
Serikali  kupitia Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), imetoa Sh. bilioni 4.16 kwa ajili ya taasisi na watafiti walioshinda maandiko ya miradi ya utafiti yenye mchango wa uendelezaji na uimarishaji wa viwanda na kuifikia uchumi wa kati.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akikabidhi hundi ya kiasi hicho cha fedha kwa taasisi zilizoshindwa kupitia shindano lililoshindanisha zaidi ya maandiko 160.

Prof. Ndalichako alisema miradi hiyo iliyofadhiliwa imelenga kwenye nyanja za kusaidia kukuza viwanda vya dawa za binadamu na kuongeza ufanisi katika sekta ya mifugo kupitia uboreshaji wa mitambo na chanjo.

Alisema Costech ilishindanisha taasisi za utafiti na vyuo vikuu na kupata miradi nane ya uboreshaji wa miundombinu yenye thamani ya Sh. bilioni 3.2.

Pia alisema Costech kwa kushirikiana na Tume ya Mipango Zanzibar, ilishindanisha watafiti na kupokea maandiko ya miradi ya utafiti ikilenga kutafuta ufumbuzi wa matatizo maalumu ya visiwani humo.

“Maeneo ambayo yalilengwa ni utalii, endelevu, kilimo biashara, kilimo bahari na magonjwa yasiyoambukiza, miradi nane yenye thamani ya jumla ya Sh. milioni 960 ilipata ufadhili,” alisema.

Alisema jumla ya miradi yote iliyoshinda imepatiwa jumla ya Sh. bilioni 4.16.

Prof. Ndalichako aliwaasa watafiti na taasisi zilizopata fedha hizo za walipa kodi wazitumie kwa uadilifu na kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Fedha hizi ni za walipa kodi sio za sherehe bali kwa ajili ya kufanya utafiti, naomba zitumike kwa uadilifu mkubwa, serikali inadhamira ya kuimarisha viwanda na kuviendeleza vilivyopo, fanyeni utafiti ili tujue njia sahihi za kuimarisha uchumi wa viwanda,” alisema.

Mkurugenzi wa Costech, Dk. Amos Nungu, alisema jumla ya tungo 155 ziliwasilishwa mwezi Februari mwaka huu na baada ya mapitio, 86 zilikidhi vigezo na kupelekwa kwa wataalamu kwa mapitio na uchambuzi.

“Tungo 69 zilikosa sifa za awali na 41 zilishinda na kustahili ufadhili, lakini kwa sababu ya uhaba wa bajeti, miradi nane ilichaguliwa kwa kuzingatia mchango itakayotoa katika dira ya nchi ya uendelezaji wa viwanda,” alisema.

Mwenyekiti wa Costech, Prof. Makenya Maboko, alisema tume imejielekeza zaidi katika kufadhili miradi yenye tija na matokeo chanja yanayochangia moja kwa moja kwenye maendeleo ya Taifa ili kuinua maisha ya watu wengi.

Pia alisema tume imefadhili miundombinu ya utafiti wa udongo, uzalishaji wa mbegu bora za mimea hususan migomba na mizabibu na Imefadhili upanuzi wa maabara ya kuchakata mazao ya kilimo.

Makanga 3 Power; Dawa Bora Nguvu Za Kiume

$
0
0
MAKANGA 3 POWER; DAWA BORA NGUVU ZA KIUME
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.
Tupo dar es salam mbagala rangi tatu.
 
Mawasiliano simu namba: 0784 460 348. Au 0659 103 360.

Serikali Yasema Gharama ya Kuunganisha Umeme ni 27000 Pekee

$
0
0
SERIKALI  Kupitria kwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu imesema gharama ya kuunganishia umeme ni Sh27, 000  tu.

Mgalu  amesema hayo jana bungeni Mei 25, 2018 wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge walizozitoa wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka 2018/19 .

Mgalu ameagiza makandarasi na wasimamizi wa miradi ya umeme vijijini (Rea) kuwashirikisha viongozi wa maeneo wanaposambaza umeme ili kuainisha maeneno yenye kipaumbele.

Alisema wamepokea ushauri wote uliotolewa ikiwamo suala la baadhi ya vijiji na maeneo yenye taasisi nyeti kurukwa kutokana na kutokuwapo ushirikishwaji.

Makongoro Nyerere: Rais Magufuli Amenipa Heshima Kubwa Sana

$
0
0
Mtoto  wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Makongoro Nyerere, amesema ameshangazwa na uteuzi uliofanywa na Rais John Magufuli kumteua kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi CCM) kwa kuwa hakuwahi kuwaza kupata nafasi hiyo.

Makongoro ambaye ni mtoto wa nne kuzaliwa kwa Baba wa Taifa anakuwa wa kwanza katika familia hiyo kuwa mjumbe wa NEC.

Mwenyeti wa CCM, Rais Magufuli, jana alitangaza kuwateua Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda na Makongoro Nyerere kuwa wajumbe NEC.

Makongoro amesema: “Rais Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wangu wa chama amenishangaza kati ya nafasi zake zisizozidi saba za kuteua wajumbe wa NEC ameniteua na mimi.”

“Amenipa heshima kubwa sana kuniteua katika nafasi zake za kwanza tena na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda ambaye ni kiongozi ninayemheshimu sana,” alisema Makongoro.

Alisema Rais Magufuli mara kwa mara amekuwa akitoa ahadi kwa Watanzania kuwa hatawaangusha katika utendaji kazi wake na hivyo kumteua kwake ni heshima kubwa.

“Si tu kunipa heshima bali pia ameona ninafaa na mimi naahidi sitamuangusha kwa sababu ameona namimi naweza kutoa mchango wangu katika vikao vya juu vya chama,” alisema.

Kuhusu uteuzi huo, Makongoro alisema hakuwa anafahamu jambo lolote na wala hakutarajia kupatiwa nafasi hiyo ya juu.

Alisema amekuwa akijishughulisha na kazi zake binafsi katika kipindi cha mwaka mmoja tangu akose nafasi ya ubunge wa Afrika Mashariki, mwaka jana.

“Nimekaa benchi kwa muda mrefu sasa na nimekuwa nikiendelea na shughuli zangu binafsi mkoani Morogoro huku nikiendelea kujifua na mazoezi kwa ajili ya kuwa mchezaji wa akiba” alisema huku akicheka.

Makongoro pia alisema neema ya uteuzi huo imekuja wakati ambao ni msimu wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaowalazimu Waislam kote nchini kufunga ili kutimiza nguzo za dini hiyo.

“Kweli nimeamini mwezi Mtukufu wa Ramadhani upo, Nimeshuhudia Ramadhani nyingi wakati nasoma na hatua nyingine katika maisha yangu, lakini hii ya mwaka huu ni historia sitausahau mwezi huu mtukufu wa Ramadhani,” alisema Makongoro.

Kadhalika, Makongoro aliahidi kuwa mtumishi na mwanachama mwaminifu wa CCM na uadilifu mkubwa.

“Katika utumishi wangu kwa nafasi niliyoteuliwa ya mjumbe wa NEC nitakuwa mwadilifu kwa kuwasilisha matatizo ya wanachama na kuhakikisha yanasikilizwa na kufanyiwa kazi,” alisema Makongoro.

Aprili 24, mwaka huu, wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa benki ya NMB mkoani Dodoma, Makongoro alimwomba Rais Magufuli ampe kazi kwa sababu yeye ni mchezaji wa akiba akisubiri kuanza kazi.

Aliposimama kuzungumza kwenye tukio hilo, Rais Magufuli alisema Makongoro anastahili kuwa mchezaji wa nafasi ya kwanza na si mchezaji wa akiba.

Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari,

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,

KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Rais Magufuli Amteua Bi. Khadija Issa Said Kuwa Naibu Kamishna Wa Mamlaka Ya Bima (TIRA)


Mkataba TANESCO, SONGAS Kupitiwa Upya

$
0
0
Serikali  imesema imechukua hatua ya kufanya rejea ya mkataba kati yake na Kampuni ya Songas Limited inayozalisha umeme kwa kutumia gesi asilia ili kuhakikisha mkataba huo unanufaisha taifa.

Vilevile, imeweka wazi kwamba mkataba huo wenye mikataba mingine midogo 42 ndani yake, una utata, hivyo ni lazima ufanyiwe rejea kwa manufaa ya taifa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk. Adelardus Kilangi, ndiye aliyetoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma jana alipokuwa anajibu hoja iliyoibuliwa na Mbunge wa Viti Maalum, Jesca Kishoa (Chadema) kuhusu mkataba huo wakati wa mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka ujao wa fedha.

Juzi wakati wa mjadala huo, Kishoa alilieleza Bunge kuwa mkataba wa serikali na Songas umekuwa hauinufaishi nchi licha ya serikali kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika miradi inayotekelezwa na kampuni hiyo.

Katika majibu yake wa mbunge huyo jana, Dk. Kilangi alisema: “Mkataba wa Kampuni ya Songas Limited upo ndani ya ubia kati ya serikali na sekta binafsi (PPP) wenye mikataba midogo midogo ipatayo 42, hivyo uhalisia wa mkataba ni 'complex'.

“Sasa nataka kuliarifu Bunge kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, imechukua hatua kuhusiana na suala la Songas. Hatua iliyokwishachukuliwa ni kuitisha mikataba yote na kuifanyia rejea.”

Alisema rejea ya mikataba hiyo inafanywa chini ya sheria mpya mamlaka ya nchi kuhusiana na umiliki wa maliasili ya mwaka 2017.

“Kwa hiyo, matokeo yatakayotokana na rejea hiyo, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itaishauri serikali nini cha kufanya," Dk. Kilangi alisema.

"Sasa tuna nafasi ya kurekebisha baadhi ya mikataba hiyo au 'terms' (vipengele) vya mikataba na hili tunapewa uwezo na sheria mpya.”

Katika mjadala huo juzi, Kishoa alisema mradi wa Songas ulianza kutekelezwa mwaka 2004 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 392 na serikali iliwekeza asilimia 73 ambayo ni Dola za Marekani milioni 285 wakati Songas waliwekeza asilimia 27.

“Lakini pamoja na uwekezaji huo, unakuta serikali iliyowekeza asilimia 73 haipati chochote huku Tanesco (Shirika la Ugavi wa Umeme) ikiendelea kuilipa Songas Dola za Marekani milioni tano kila mwezi wakati serikali ilitakiwa kulipwa Dola za Marekani milioni 3.5, lakini hakuna kitu, hivi tumerogwa?" Kishoa alihoji.

Mbunge huyo aliongeza kuwa kwa miaka 14 Tanzania imepoteza Sh. trilioni 1.5 kutokana na mkataba huo na kuwa jambo hilo likipuuzwa bado kutakuwa na hasara ya zaidi ya Sh. trilioni mbili.

Kilichosababisha Babu Tale Aachiwe Huru na Mahakama

$
0
0
Mkurugenzi wa kampuni ya Tip Top Connection na Meneja wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale ameachiwa huru  baada ya kusota rumande kwa Siku kadhaa

Tale alifikishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar Jumatano Mei 23, 2018 kufuatia kesi yake anayodaiwa na Sheikh Hashim Mbonde kiasi cha Tsh. Milioni 250 ambapo kesi hiyo iliahirishwa baada ya hakimu aliyetoa amri ya kumkamata kutokuwepo mahakamani hapo.

Kipindi cha nyuma mahakama hiyo ilimwamuru Babu Tale alipe Sh. milioni 250 Mhadhiri wa Dini ya Kiislamu, Sheikh Hashim Mbonde, baada ya kupatikana na makosa ya ukiukwaji wa hakimiliki kwa kutumia masomo yake kibiashara bila ridhaa yake kinyume cha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki.

 
Juzi jioni, Jaji Edson Mkasimongwa alimuachia huru kwa muda kwa kile kinachoelezwa kuwa ni makosa ya amri hiyo ya kumkamata na kumtaka afike mahakamani jana na akamwelekeza wakili wake amtaarifu wakili wa mdai afike mahakamani ili kuzisikiliza pande zote.

Hata hivyo, usikilizwaji wa hoja ambazo ziliibuliwa na mahakama yenyewe kuhusiana na amri ya kuwakamata ulikwama kutokana na upande wa mdai kutofika mahakamani.

Badala yake, Jaji Mkasimongwa aliahirisha shauri hilo hadi Juni 8, 2018 na kuagiza upande wa mdai kupewa taarifa ya wito kwa ajili usikilizwaji wa hoja zilizoibulia na mahakama yenyewe. Pia jaji alisimamisha amri ya kuwakamata hadi Juni 8.

Cheo cha koplo, Pingu vyamtia mbaroni mhudumu wa hoteli

$
0
0
Kamanda wa Polisi kanda Maalumu ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema jeshi la polisi linamshikilia mhudumu wa Hoteli ya Sleep Inn na mkazi wa Mwananyamala kwa kopa baada ya kukutwa na sare za polisi, silaha, cheo cha koplo na pingu.

Mambosasa amesema kuwa jeshi la polisi lilipokea taarifa hizo toka kwa msiri kuwa mtu mmoja anatumia sare za jeshi la polisi kuwakamata watu na kuwafunga pingu kuwatishia bastola ili kufanikisha kupora mali maeneo mbalimbali ya jiji.

”Baada ya kupata taarifa hizo jeshi la polisi lilianza ufuatiliaji mara moja na kuweka mtego mnamo tarehe 21, Mei 2018 majira ya saa nne usiku huko Mwenge Bamaga Polisi walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo” amesema Mambosasa.

Mambosasa ameongezea kuwa baada ya kufanya nae mahojiano mtuhumiwa alikiri kumiliki sare na vifaa mablimbali vya jeshi la polisi na kukubali kuwapeleka askari hadi nyumba anayoishi.

Ambapo baada ya kufanya upekuzi kwenye nyumba anayoishi alikutwa na sare za jeshi la polisi, pingu, cheo cha koplo wa polisi, mfuko wa kuhifadhia bastola na bastola aina ya GLOCK 17 ambayo imefutwa namba zake za usajili ikiwa haina risasi.

Aidha mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Makamu Mwenyekiti Wa CCM-Zanzibar- Rais Wa Zanzibar Dk. Shein Ikulu Jijini Dar Es Salaam

Mhadhiri UDOM Auawa Kwa Kuchomwa Kisu na Mumewe

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo cha Biashara katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Rose Mdenye ameuawa kwa  kuchomwa kisu na mumewe usiku wa kuamkia leo Mei 26 kwa wivu wa mapenzi.

Ofisa Uhusiano wa Chuo hicho, Beatriece Mtenga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadaye. Mtenga amesema msiba upo Kisasa Sheli.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images